Monday, September 6, 2021

ETI NI WATU WOTE WATAKAO OKOLEWA? / WILL ALL MEN BE SAVED?

Photo by B Smith from the patio


 


ETI NI WATU WOTE WATAKAO OKOLEWA? 

WILL ALL MEN BE SAVED?

November 11, 1962

Pastor Henry F. Kulp 


 

1 Timoteo 2: 1 – 4 


“Basi ninaonya mbele ya maneno yote, kuomba, na kusihi, na kuombea, na kushukuru kufanyike kwa ajili ya watu wote; kwa wafalme na kwa wote wenye mamlaka, tuishi maisha ya kimya na salama, katika utawa wote na upole.

Kwa sababu hii ni nzuri na la kukubaliwa mbele ya Mungu Mwokozi wetu; anayetaka watu wote waokolewe na kupata kujua sana yaliyo kweli.” 

Kuna mafundisho yanayovuma katika ulimwengu kwa siku za leo,na ni udanganyifu ya kuhamakia ili kuhepuka kutupwa  kwenye shimu la jehenamu. 

Ninahuzunishwa sana na kushangaa namna gani watu wanavyoweza kusadiki mafundisho yale, sababu hakuna hata aya moja ya Maandiko Matakatifu ya Biblia inayo tetea mafundisho ya namna ile. 


1/ Ni mafundisho gani yanayosambazwa ulimwenguni kwa siku za leo? 

Ni upatanisho kwa watu wote, inayotambulikana kwa jina la 

Kilimwengu ama ulimwengu wote. 

Zehebu hilo linaitwa Kilimwengu ama ulimwengu wote na mwenye kushiriki zehebu hiyo anaitwa wakilimwengu ama waulimwenguni wote. 

Bali zehebu hiyo inajulikana kwa jina la Upatanisho wa ulimwengu wote.

 2/ 2 Wakorinto 11: 14 

“Wala si ajabu; kwa sababu Shetani mwenyewe anajigeuza awe malaika ya nuru” 

Shetani anatajwa hapa, kama mwenye kuchochea wakristo wazembe akiwaonyesha matarajio yasiyo ya kweli ili awagandamize na kuwatenga wasisikie na kufuata ukweli ulio ndani ya Kristo Yesu, kwa hiyo, kujigeuza kwake kama malaika wa nuru kwa siku za leo na katika siku zilizo pita, ni katika mafundisho hayo ya upatanisho ya ulimwenguni mwote, sababu mafundisho yale yanakuwa sawa yaliyo mazuri kwa kusikia na yenye kubembeleza hadi wengi wanayakumbatia na kuanguka ndani.  

Ila, yote ni udanganyifu mtupu wa shetani toka mwanzo hadi mwisho. 

3/ Watu wale wanatumia Maandiko kama: 

1 Timoteo 2: 4  

“anayetaka watu wote waokolewe na kupata kujua sana yaliyo kweli.” 


2 Petro 3: 9 

“Bwana hakawii kutimiza ahadi yake, kama wengine wanavyozania kukawia; lakini ni vu 


1 Yoane 2: 2 

“naye ni kipatanisho kwa zambi zetu; wala si kwa zambi zetu tu, lakini kwa zambi za ulimwengu wote.” 

Wakitumia Maandiko yale ile wafundishe kwamba kwa mwisho watu wote wataokolewa, na Kristo ni wa watu wote.  


Tutambuwe kwamba 1 Yoane 2: 2 inasema kwamba:

Yeye ni kipatanisho kwa zambi zetu; wala si kwa zambi zetu tu, lakini kwa zambi za ulimwengu wote.” 

Mwenyezi Mungu hapendi hata mtu mmoja kupotea na watu wale wanatumia kwa ujanja aya moja kwa moja. 


4/ Mwenyezi Mungu haja ahidia bado kwamba watu wote wataokolewa. 

  Muniruhusu niwafahamishe kanuni moja inayopatikana mahali mbalimbali katika Biblia:  


Matayo 7: 13, 14 

“Ingieni kwa mlango ulio mwembamba; kwani mlango ni mpana na njia ni pana inayokwenda hata upotevu, nao ni wengi wanaoingia kwa mlango huu. 

Lakini mlango ni mwembamba, na njia imesonga inayokwenda hata uzima, nao ni wachache ambao wanaiona.” 

Hapa, katika mahubiri juu ya mlima Bwana Yesu Kristo anasema: 

 Ingieni kwa mlango ulio mwembamba; kwani, mlango ni mpana na njia, fwateni vizuri hapa, ni pana inayokwenda hata upotevu, hapana hata wokovu. 

Kiisha anatumia neno: nao ni wengi wanaoingia kwa mlango huu. 

Tuchunguze sana neno: Wengi na Upotevu.  

Kiisha kwa aya ya 14 anasema: 

Lakini mlango ni mwembamba, na njia imesonga inayokwenda hata uzima, nao ni wachache ambao wanaiona.” 

  Namna gani twaweza kuzania jambo la upatanisho wa kiulimwengu katika aya hizi tunazo zisoma? 


5/ Naamini kwamba munajiuliza ni kitu gani kinachotuma mafundisho yao yawe mabaya sana na yenye laana? 

Ni kwa sababu yanamutwiga Mungu china ya zambi. 

Na ni hiyo msingi wa mafundisho yao. 

Katika mafikara yao wanaweka china la zambi ndani ya roho na mawazo ya Mwenyezi Mungu. 

Wanasema ya kwamba ni Mungu mwenyewe aliyoyaunda na kuyaleta kwa faida ya mtu na kwa sifa yake Mungu mwenyewe. 

 Wanasema kwamba zambi iliingia duniani kwa njia ya Mungu. 

Na Yeye aliileta kwa kusudi la kuboresha miradi yake ya neema, ili apate kuokowa watu wote. 

Bali, Mwenyezi Mungu Yeye mwenyewe husema nini kwa ajili ya mambo haya? 

Eti ni yeye aliyeleta zambi katika dunia? 

Eti ni yeye aliyeunda zambi katika mawazo yake, ili baadaye nyinyi muokolewe kwa njia ya neema yake? 


6/ Kuna Andiko moja ya Biblia inayoleta uvuguvugu kwa hawa watu wa Kilimwengu. 


Mwanzo 6: 5, 6   

“Bwana akaona ya kama uovu wa watu ulikuwa mkubwa duniani, na ya kama mawazo yote ya mafikiri ya mioyo yao yalikuwa mabaya tu siku zote.  

Fanya sasa angalisho hapa:

Na Bwana alijuta ya kwamba amefanya watu duniani, ikamhuzunisha moyoni mwake.” 

Eti neno hili yaambatana na mafikiri ya kusema ya kwamba ni Mwenyezi Mungu aliyeunda zambi, na kuiingiza duniani kwa niaba ya Neema yake? 

Ni nini hawa watu wa kilimwengu waweza kufanya na Andiko kama hili? 


7/  bKuna vile vile Andiko lingine la Biblia lenye kukoroga hawa watu wa Kilimwengu. 


Yeremia 32: 35 

“Tena walijenga pahali pa juu kwa Bali, palipo katika bonde la mwana wa Hinomu, ili kupitisha wana wao na binti zao katika moto kwa ajili ya Moleki, nisivyowaamuru, wala halikuingia katika moyo wangu kwamba watende chukizo hili; wapate kukosesha Yuda.” 

Anasema ya kwamba, pale Tafa, wao walijenga pahali pa juu, ili kupitisha wana wao na binti zao katika moto, jambo lenyi sikuwaamuru, wala halikuingia katika moyo wangu. 

Mwenyezi Mungu hakufurahia zambi kufika katika ulimwengu, Yeye hakuunda zambi katika mafikiri yake kwa niaba ya neema. 

8/ Watu wa Kilimwengu wanafundisha ya kwamba hukumu ya zambi haiko juu ya mtu na wanatia mzigo wote wa zambi kwa Mwenyezi Mungu.  

Wanafundisha kwamba Mwenyezi Mungu aliweka  kati bustani, mti wa kujua mema na mabaya kwa kusudi la kumjaribia mwanadamu kwa kumusukuma kwa kutenda zambi, ili baadaye,  Mungu aje na Neema yake kwa kuokoa mwanadamu.  


Lakini wao wanasahau Maandiko katika Biblia iliyo wazi kweli na inayosema:  


Yakobo 1: 13 

“Mtu akijaribiwa, asiseme: Ninajaribiwa na MUNGU: maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, wala yeye mwenyewe hajaribu mtu.” 

Mwenyezi Mungu anasema hapa kwamba: 

Mtu yeyote akijaribiwa, asiseme: Mimi ninajaribiwa na Mungu, maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, wala Yeye mwenyewe hajaribu mtu. 

Ni kweli kwamba ni Mwenyezi Mungu ndiye aliyetia mti wa kujua mema na mabaya katika bustani, na haikuwa kwa ajili ya kujaribu ili mtu ale tunda la mti huo, lakini ilikuwa kwa kuhimarisha uhusiliano kati ya Mungu na mtu, sawa na kiumbe na Muumba wake, ili mwanadamu atende tu yale Mungu anayomuomba kutenda. 


9/ Kama ingelikuwa kwamba ni Mwenyezi Mungu aliyesukuma mwanadamu kutenda zambi, basi Adamu angelikuwa na singizio kamilifu wakati alipohukumu muke wake na kusema kwamba ni yeye aliye chanjo na wajibu wa zambi Adamu alilofanya, akisema: “Mwanamuke ambaye ulinipa awe pamoja name.”  

Eti Mungu hakuwa na haki ya kumuhukumu? 

Hapana kweli, mwanadamu alikuwa na uhuru wa kuchagua. 

Na Mungu hakumtuma mtu kuchagua zambi. 


Mwanzo 3: 12 

“Mwanamume akasema: Mwanamuke ambaye ulinipa awe pamoja nami, yeye alinipa ya mti, na nilikula.” 

10/ Wakati unaposoma kawaida ya mafundisho yale, ama mtu yeyote kukuzungumuzia juu yake, pale pale kuna Maandiko ninayo kumbuka katika mafikiri yangu: 

Yobu 1: 22 

“Katika maneno haya yote Yobu hakukosa wala kushitaki Mungu kwa upumbafu.” 

Ndugu zangu, kumutwiga Mungu wajibu wa zambi iliyo ilimwenguni ni neno la upumbafu na lenye laana. 

Yobu hakufanya zambi wala kusingizia yeyote kwa upumbafu. 

Ni kwa upumbafu ndiyo mafundisho yale yanamuhukumu Mungu. 

Mwenyezi Mungu hana wajibu wowote juu ya zambi zetu. 

Mungu hajaribu wanadamu ili watende zambi. 

11/ Acheni tuwaoneshe Maandiko mbali mbali yenye watu wa kiulimwengu wanatumia ili wahakikishe kwamba siku moja watu wote wataokolewa, wakishuhudia kwamba Neno la Mwenyezi Mungu inatangaza uhusiano wa ulimwengu wote. 

Yoane 12: 32  

“Nami kama nikinyanyuliwa juu ya dunia, nitakokota watu wote kwangu.” 

Ya kwaza ni kwamba Maandiko haya hayasemi ya kwamba Bwana Yesu atakokota watu wote kwake kwa niaba ya wokovu. 

Watu hao wanamemba wanaotangaza habari za uhusiano wa kiulimwengu, wao hawaamini kwamba Yesu Kristo ni Mungu. 

Wanakanusha Umungu wa Yesu Kristo na ni jambo hili inayotia mafundisho yao yawe ya laana na lenyi kukufuru. 

Kama ungelikuwa na bahati mbaya ya kuwasikiliza utatambuwa kwamba wao wanasema kwamba katika Maandiko haya, Bwana Yesu ni mwenye  kujionyesha na hali  tukufu ya juu sana. 

Na kwamba kilichomukosa ni kusema ukweli. 

Wakati aliposema: Mimi ni Kweli. 

Akisema: Nami wakati nitanyanyuliwa juu ya dunia, nitakokota watu wote kwangu. 


12/ Tuchunguze kwanza sehemu hii: Nami kama nikinyanyuliwa.  

Ni nini anayozungumuzia hapa? 

Bwana Yesu anazungumuza kuhusu Kufa kwake kwa Musalaba wa Kalvari.  

Mutatambua kwamba haihusu huduma aliyohudumia watu, ama siyo mafundisho yake iliyokuwa na uwezo wa kuwavuta watu kama asmako, lakini ni Kufa kwake kunaokuwa na uwezo wa kuvuta watu kwake kama asmako. 


13/ Tuzungumuzie sasa neno: Kukokota.  

 Neno hili linatumiwa mara tano katika Kitabu cha Yoane, na mara moja katika kitabu cha Matendo ya Mitume. 

Na wakati wowote neno kukokota inatumikishwa, inamaanisha kukukota kwa kutumia nguvu, ni kusema uwezo unao gandamiza, neno hilo limetumikishwa katika Yoane 21: 11 

“Basi Simoni Petro akaingia chombo, akakokota wavu hata pwani, umejaa samaki wakubwa mia moja makumi tano na watatu; na hata walikuwa wengi hivi, wavu haukupasuka.” 

Hapa ni kwamba ndani ya wavu munaonekana samaki wakubwa mia moja makumi tano na watatu, na samaki hizi zapatikana ndani ya wavu wakati wavu inakokotwa pwani. 

Samaki walikuwa ndani bila musaada wowote. Walishikwa na kuletwa mpaka pwani katika wavu.


14/ Matendo ya Mitume 16: 19 

“Lakini wakati bwana zake walipoona ya kuwa tumaini la faida yao limewapotea, wakakamata Paulo na Sila, wakawakokota hata sokoni mbele ya wakubwa wa mji.” 

Maandiko hapa ni kuhusu Paulo na Sila wakiwa hazarini sokoni. 

Walikuwa pasipo mwenye kuwasaidia wakakokotwa kwa nguvu. 

Pia tunaikuta tena katika Matendo ya Mitume 21: 30  

“Mji wote wakafazaika, watu wakakutanika mbiombio, wakakamata Paulo, wakamkokota inje ya hekalu; mara moja milango ilifungwa.” 

Maandiko hapa ni kuhusu Paulo na Sila wakiwa inje hazarani. 

Walimukokota Paulo inje ya hekalu. 

Walikuwa pasipo musaada toka kwa watu, wakikokotwa kwa nguvu. 

Ndani ya Matendo ya Mitume 21:30, imeandikwa kwamba: wakimukokota Paulo inje ya hekalu. 

Turudi kwa Andiko tuliloanza nalo: Yoane 12: 32  

“Nami kama nikinyanyuliwa juu ya dunia, nitakokota watu wote kwangu.”  

  Yawezekana kwamba, kati ya wanaadamu kuna wale wanaoweza kusema: Umbalimbali na yale, mimi sitaki kujongea kwake, sitaki nimuone uso kwa uso, sitaki nimupe hata muda wa kukutana nami. 

Bali, fahamu ndugu yangu ya kuwa kwa siku ile, hakuna mwenye atakuuliza lile unalolitaka, bali, wewe utasimama mbele ya kiti chake cha hukumu na kusimama mbele yake kwa kumujibu. 

Surulisho moja na jibu kwa swali hilo, mbele muda ingaliki bado, ni kukokotwa ndani ya Mapendo Yake kwa njia ya Neema yake kwa sasa, pahali pa kungojea kuonekana mbele Yake kwa hukumiwa, wakati itakuwa haiwezekani tena kwako kuweza kuokolewa. 


15/ Tuchunguze moja ya Maandiko yenye wanafurahia sana, iliyo katika 


Wafilipi 2: 9 – 11 

“Kwa hivi Mungu vilevile alimtukuza sana, na kumpa Jina lililo juu ya kila jina; 

Hata kwa Jina la Yesu kila goti litapigwa, la vitu vya mbinguni na vya duniani, na chini ya dunia, na kila ulimi ukiri ya kuwa Yesu Kristo ni Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.” 

Neno “Kila” katika aya zote hizo yatoka kwa neno la Kigriki linalomaanisha “Yote”, sawa sawa na katika Maandiko mengine ya Biblia na ni hapo ndipo watu wa kilimwengu wote wanatoa mawazo ya kuhakikisha  kwamba Maandiko yale yanafundisha kwamba  kwa mwisho watu wote wataokolewa na hapo wanataja:  

Waroma 10: 9 

“Kwa sababu kama ukikiri kwa kinywa chako ya kuwa Yesu ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua toka wafu, utaokolewa:” 

Bali wao hawataji: 


Wafilipi 2: 11 

“na kila ulimi ukiri ya juwa Yesu Kristo ni Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.” 

Eti Andiko hili lafundisha kwamba kuna siku moja, kila ulimi utakiri kwamba Yesu Kristo ni Bwana? Hapana hata kidogo, jibu ni HAPANA.  


Waroma 10: 9 – 10 

“Kwa sababu kama ukikiri kwa kinywa chako ya kuwa Yesu ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua toka wafu, utaokolewa: 

Kwa maana kwa moyo mtu anaamini hata kupata haki; na kwa kinywa anakiri hata kupata wokovu.” 

Kukiri inatiwa pamoja na imani moyoni. 


Wafilipi 2: 9 – 11 

“Kwa hivi Mungu vilevile alimtukuza sana, na kumpa Jina lililo juu ya kila jina; 

Hata kwa Jina la Yesu kila goti litapigwa, la vitu vya mbinguni na vya duniani, na chini ya dunia, na kila ulimi ukiri ya kuwa Yesu Kristo ni Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.” 

Hapa haiambatane vile. 

Hapa inatiwa pamoja na jambo ambalo kila goti litapigwa, la watu wote bila ubaguzi. 

Tufahamu vizuri kwamba, wakati hali hiyo itatimilika, haitakuwa tena wakati wa kuamini moyoni mwetu ya kuwa Mungu alimfufua Kristo toka wafu, sababu, kwa wakati ule Ufufuko wake utakuwa wazi dhahiri. 

Andiko la Waroma 10: 9 – 10, yaonekana wazi kwamba ni shauri, pendekezo. 


Waroma 10: 9 – 10 

“Kwa sababu kama ukikiri kwa kinywa chako ya kuwa Yesu ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua toka wafu, utaokolewa: 

Kwa maana kwa moyo mtu anaamini hata kupata haki; na kwa kinywa anakiri hata kupata wokovu.”  


Wafilipi 2: 9 – 11 

“Kwa hivi Mungu vilevile alimtukuza sana, na kumpa Jina lililo juu ya kila jina; 

Hata kwa Jina la Yesu kila goti litapigwa, la vitu vya mbinguni na vya duniani, na chini ya dunia, na kila ulimi ukiri ya kuwa Yesu Kristo ni Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.”  

Amini sasa hivi Bwana Yesu, kama Bwana na Mwokozi wako, na utaokolewa. 

Kama unakataa ombi hili, kumbuka kwamba kufwatana na Maandiko ya Wafilipi 2: 9 - 11, upende ama usipopenda, siku moja itakuja ambalo utalazimishwa kumufahamu.  

Aya hii inatufundisha kugandamizwa ama kushushwa ya ulimwengu wote, 

bali halitufundishe ushirika wa ulimwengu wote. 

Mutatambuwa kwamba Mwenyezi Mungu alimupa Yesu Kristo Jina lililo juu ya majina yote. 

Ni Jina lenye litajaa duniani kwote, kama vile ninavyo amini, ni jina lenye munalolipenda. 

Jina hilo ni la ajabu sana. 

Jina nzuri kwa ulimi ya watu wote, nyimbo ya furaha sana kuliko. 

Naamini kwamba ni jina lenye ungelipendelea mtoto mchanga alitamke kwanza. 

Pendekezo lako ni kwamba mbele mtoto wako mchanga ajue kusema ama kutamka neno la kwanza, angelianza kutaja Jina Yesu Kristo, na pia kwa watu makamu, wazee, mbele watoe pumzi yao ya mwisho, ungelipendelea wataje jina la Yesu Kristo.  


16/ Goti na ulimi. 

Goti litapigwa mbele ya Kristo, hata magoti ya wa milioni ya watu wanaopotea, wakaidi wanao sengenya na kumuchekelea, vizazi vya laani wenye kucheza na Jina la Kristo bure, wote watamukiri kwamba Yeye ni Bwana. 

Kweli, Mungu anasema kwa wale watu wenye kiburi wenye wanakataa kupiga magoti mbele ya Yesu, Mungu atasema: Munapashwa piga magoti yenu mbele ya Jina la Yesu na ndimi zenu zinapashwa kumukiri, bali kwa wakati ule itakuwa jambo la kunyanyasa, la kutiishwa. 


17/ 1 Timoteo 2: 4 - 6  

“anayetaka watu wote waokolewe na kupata kujua sana yaliyo kweli.

Kwa sababu Mungu ni mmoja tu, na mpatanishi katikati ya Mungu na watu ni mmoja, yule mtu Kristo Yesu, ambaye alijitoa mwenyewe kuwa ukombozi kwa ajili ya wote; utakaoshuhudiwa kwa wakati wake;” 

Kwa andiko hili wale watu wa zehebu ya kilimwengu wanasema kwamba: Kama Mungu anahitaji watu wote waokolewe na Yeye haitimize, ni kusema kama Yeye ayupo mahali pote, na Kristo alikufa kama mtu aliyechindwa. 

Masimi yao yanafanana kuwa sambamba lakini sivyo. 

Tulinganishe Maandiko haya na Maandiko yafwatao:  


Ezekieli 18: 20 -23 

“Nafsi inayofanya zambi itakufa, mwana hatabeba uovu wa baba, wala baba hatabeba uovu wa mwana; haki ya mwenye haki itakuwa juu yake, na uovu ya mwovu utakuwa juu yake. 

Lakini kama mwovu akigeuka toka zambi zake zote ambazo alizitenda, na kuchunga sheria zangu zote, na kutenda hukumu na haki, hakika ataishi, hatakufa. 

Zambi zake zote ambazo alizifanya hazitakumbukwa juu yake, kwa haki ambayo aliitenda ataishi. 

Mimi ninafurahi kwa kufa kwa mwovu? 

Bwana MUNGU anasema; na si zaidi ageuke toka njia yake, na kuishi?” 

Kwa aya ya 23 anasema:  

Eti mimi ninafurahi kwa kufa kwa mwovu? HAPANA 

Bali, tunajuwa kwamba aya ya 20, inatuambia kwamba mwovu atakufa. 


18/ Tunapashwa kuchunguza kwa makini kabisa masemi ya 


1 Timoteo 2: 4 -6  

“anayetaka watu wote waokolewe na kupata kujua sana yaliyo kweli.

Kwa sababu Mungu ni mmoja tu, na mpatanishi katikati ya Mungu na watu ni mmoja, yule mtu Kristo Yesu, ambaye alijitoa mwenyewe kuwa ukombozi kwa ajili ya wote; utakaoshuhudiwa kwa wakati wake;” 

  Maombi kwa wengine inafwatwa na musemwa unaosema kwamba Mungu anataka watu wote waokolewe, na kwamba Kristo alijitoa mwenyewe kuwa ukombozi kwa ajili ya watu wote, kwa hiyo, wazo ni kwamba Mungu anahitaji watu wote waokolewe, kwa sababu Kristo alijitoa mwenyewe kuwa ukombozi kwa ajili ya wote. 

Sisi tulio wake twapasa kuwa na nia hiyo na kutamani kuombea wengine. 

Nasi tunatamani watu wote waokolewe, lakini tunajuwa ya kwamba Mwenyezi Mungu hawezi kuokowa mtu asiyemjia kwa kupitiya njia ya Yesu Kristo. 


19/ Tuone sasa Maandiko mengine yenye wanapenda kuonesha. 


1 Timoteo 4: 10 

“Kwa sababu hii tunajitahabisha na kulaumiwa sana, kwa sababu tunatumainia Mungu aliye hai, aliye Mwokozi wa watu wote, zaidi wa hawa wanaoamini.” 

Mungu ni Mwokozi wa watu wote, zaidi sana wa hawa wanaoamini. 

Ni huzuni sana kuona watu wa zehebu ya Kiulimwengu kufikia kuzania kwamba wanaweza kutumia Andiko hili kwa kuonesha kwamba watu wote wataokolewa. 

Mutatambuwa kwamba neno “mwokozi” yaweza kumaanisha “Mlinzi”: Yeye ni Mlinzi wa wote wanaoamini. Hii aimaanishi kazi ya Kristo kuhusu wokovu. 

Ni picha tu ya Mungu kama Muumbaji na Mlinzi wa watu wote. 

Katika Zaburi 36: 6 

“Haki yako ni kama milima ya Mungu; Hukumu yako ni vilindi vikubwa; 

Ee Bwana, unaokoa mtu na nyama.” 

Ni namna hivyo tu ndivyo afanyavyo. 

Kumbukeni asemavyo katika Matayo 5: 45 

“Mupate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni, sababu Yeye anaangazia jua lake waovu na wema, naye ananyeshea mvua wenye haki na wasio haki.” 

Zawadi yote nzuri na kamilifu inatoka kwake Mungu, na watu wote wanaoamini na wasioamini kwao wote pamoja Mungu ni mlinzi wa maisha yao wote.  

Ni yeye aliyeumba ulimwengu na kuweka nguvu zinazoongoza ulimwengu, siyo tu juu ya watu, lakini pia juu ya wanyama, na zaidi sana juu ya wale wanaoamini. 

Anatushurulikia kwa sababu vitu vyote vinatumika pamoja juu ya mema yetu. 


20/ Muniruhusu niwape mfano wa jambo Mwenyezi Mungu alilolifanya juu ya Mtume Paulo. 


2 Wakorinto 11: 32 – 33 

“Katika Damasiki mtawala wa mfalme Areta alilinda mji wa Wadamasiki apate kunikamata: 

Na kutoka dirisha nilishushwa kwa ukuta ndani ya kitunga, na nikaponyoka toka mikono yake.” 

Hapa kwa namna ya upekee, Mwenyezi Mungu Mwenyewe alikuwa mlinzi wa Paulo. 


21/ Tuchunguze sasa Maandiko mengine moja moja. 

Eti, Maandiko yale yanatuambia kwamba kuna siku moja watu wote wataokolewa?  

Wafilipi 3: 19 

“mwisho wao ni uharibifu, mungu wao ni tumbo, utukufu wao ni haya yao, wanaofikiri maneno ya dunia.” 

Tambueni yanayosemwa hapa: Wao ni adui za Msalaba wa Kristo, na nini iliyo mwisho wa wale walio maadui za Musalaba wa Kristo? 

  Ni upotevu, ni uharibifu, ni laana. 

Eti jambo hili linaambatana na mawazo ya kwamba mwisho wao ni wokovu? Hapana, mwisho wao ni upotevu, ni laana.  


22/ Tupime kusonga mbele na mawazo haya: 

Kama katika Waroma 8: 33 tunaulizwa:  

“Ni nani atakayeshitaki wachaguliwa wa Mungu?” 

Kama ingelikuwa kwamba mawazo inayosemwa na watu wa zehebu ya kilimwengu ni ya kweli, tungelipashwa kusoma namna hii: 

Ni nani atakayeshitaki mtu yeyote ule? Sababu watu wote wataokolewa, Hapana hii Andiko ingeligeuka isiyo na maana. 

Tutwae sasa Waroma 8: 28 

“Na tunajua maneno yote yanafanya kazi pamoja kuwapatia mema wale wanaopenda Mungu, kwa wale walioitwa kwa kusudi lake.” 

Sababu gani haikusemwa: 

Mwenyezi Mungu anafanya maneno yote yafanye kazi pamoja kuwapatia mema watu wote? 

Kwa sababu gani ni kwa wale wanao mpenda Mungu peke yake? 


23/ Hata tunafikia kiwango wanapowaza kwamba hata Shetani siku moja ataokolewa. 

Mapepo wachafu wote wataokolewa, hii ni mafundisho ya upumbafu. 

Tuchunguze tena Maandiko yafwatao:  


2 Wakorinto 11: 13 – 15 

“Maana hawa ni mitume ya uongo, wenye kutenda kazi kwa hila, wakijigeuza wenyewe kuwa kama mitume ya Kristo. 

Wala si ajabu; kwa sababu Shetani mwenyewe anajigeuza awe malaika ya nuru. 

Basi si neno kubwa kama watumishi wake vilevile wanajigeuza wawe watumishi wa haki; mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao.” 

Tambueni kwamba inasemwa hapa ya kwamba: 

Wenye mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao.  

Hawastahili wokovu. 

Mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao. 


AMINA


N°Ref: 11/11/1962/ 252 - WILL ALL MEN BE SAVED /9/6/2021

No comments:

Post a Comment