Tuesday, June 29, 2021

SIRI YA UTAUWA / THE MYSTERY OF GODLINESS

Photo by B Smith from the kitchen door


 


SIRI YA UTAUWA 

THE MYSTERY OF GODLINESS

May 20, 1962 

Pastor Henry F. Kulp

 


1 Timoteo 3: 15, 16 

“Lakini kama nilikawia, upate kujua sana namna inavyokupasa kutenda katika nyumba ya Mungu, iliyo kanisa la Mungu aliye hai, nguzo na msingi wa kweli. 

Na pasipo shaka, siri ya utawa ni kubwa: 

Mungu alionekana katika mwili, 

Alihesabiwa kuwa na haki katika Roho, 

Alionekana na malaika, 

Alihubiriwa katika mataifa, 

Aliaminiwa katika ulimwengu, 

Alipokewa katika utukufu.”  

Juma lililopita tulizungumuza kuhusu kanisa na namna gani mwenendo wetu wastahili kuwa. 

Kwa kweli kunakuwa kasoro nyingi wakati watu wanapozungumuza kuhusu kanisa. 

Wanazani kwamba kanisa ni jingo kubwa ama muungano wa watu unaoonekana kwa mecho. 

Lakini mafasiriyo mafupi yataondoa kunguku hiyo ya utata  na kuweka wazi tofauti iliyo kati ya kanisa sawa jamii ya watu hapa chini ulimwenguni na kanisa sawa chama cha kiroho ama kusanyiko la waamini  wanaokusanywa kwa kushirikiana pamoja na Bwana Yesu Kristo. 

Tutwae mfano wa John Smith. 

Rafiki wake walimufahamu kama mtu murefu, mwembamba na mwenye nywele nyeusi, mecho ya rangi la kahawia, na mwenye michezo ya kuchekesha. 

Ni namna hiyo wanadamu wanaleta maelezo kuhusu maumbile ya mtu. 

Lakini, tupime kuchunguza. 

Kwa mfano, tuseme kwamba John Smith anafariki. 

Tunajielekeza kwa nafasi ya maombolezo kwenye kilio kimewekwa, tunatizama mwili wa marehemu wakati watu wanaposema, oh kweli anaonekana kuwa mrembo na mwenye sura nzuri.

Hapo hapo tunatambuwa kwamba tuko tukitizama mwili usio tena na maisha, siyo tena bwana John Smith, yeye hayuko tena katika mwili huo, na hapo twatambuwa kweli kwamba John Smith hakuwa mwili huo. 

John Smith alikuwa mtu yule asiyeonekana na mecho, aliyekuwa akiishi ndani ya huo mwili. 

Ni jambo tunalokuwa nalo hivyo hivyo wakati tuwazapo kuhusu kanisa sawa jengo ama chama. 

Kwa kweli, kanisa ni jengo la kiroho.

Ni muungano wa wale wote walioamini Bwana wetu Yesu Kristo na kuokolewa kweli. 

Ni Jengo la Kiroho na wale wote walioamini Bwana Yesu Kristo, Roho Mtakatifu anawaingiza humo na Roho Mtakatifu anawaweka  kuwa Makao ya Mungu. 

Ndani ya nyumba lile, Mungu anakuja kufanya makao na kuishi ndani yao waliookolewa. 

Kanisa yaonekana kwa mecho wakati Roho Mtakatifu anafanya kao lake katika miili ya maumbile ya waamini. 

Hii haimaanishi onesho zidi la muungano fulani, silo la kina Batisti, ama silo la wa Luteriani, ama la mazehebu fulani zilizo huru: 

Kila yule aaminiye Bwana Yesu Kristo ni mmoja wa muungano huo ulio kao na nyumba  lenye Mwenyezi Mungu anamoishi. 


1/ Nyumba hiyo ya Mungu inayokuwa muungano wa watu wa Mungu, ndiyo inayokuwa na wajibu wa kutangaza na kueneza Habari Njema ya Yesu Kristo mahali pote. 

Na hapo tunafikia lengo la neno linalosema: Mungu kuvaa mwili wa mtu ni Siri kuu. 

Kumbukeni kwamba Bwana wetu Yesu Kristo alionekana katika mwili.     

Neno ilifanyika kuwa Mwili  na ilionekana na watu. 

Kumbukeni wakati Bwana Yesu Kristo alisaidia yule mwanamuke musamaria.

Mungu katika uwepo wake Yeye ni Roho. 

Ni Mungu katika hali ya utu usioguswa, ni kusema bila maumbile, Yeye haonekane. 

Yoane 4:24 

“Mungu ni Roho; nao wenye kumuabudu sharti wamwabudu katika roho na kweli.”  Yoane 18 na Yoane 14.  


2/ Jameni tusome sasa:  

Matayo 11: 27 

“Nimepewa vitu vyote na Baba yangu, wala hakuna mtu anayejuwa Mwana, ila Baba, wala hakuna mtu anayejuwa Baba ila Mwana, naye Mwana anapendezwa kumfunulia kwake.” 

Hii inatusaidia kufahamu Siri hii ya Mungu kuonekana katika mwili. 

Mungu na mtu kuwa katika nafsi moja, hii ni jambo linalotambuka mafikiri ya mwanadamu.  

Mtu hawezi kamwe kufahamu jinsi Mungu Mwana anaonekana kuwa mtu na Yeye ni Mungu. 

Ni mara kwa mara mtu anakwaa akiwaza jambo lile. 

Bali mtu, kwa sababu anaamini Biblia Maandiko Matakatifu, anafikia kiwango cha kuamini Siri hii. 

Yaonesha namna gani yatupasa kutumia akili na busara wakati tunapo tamka yanayohusu Bwana na Mwokozi wetu, tukifahamu ya kwamba Yeye ni pamoja  na Baba kwa  utimilifu wote. 

Kwa mfano, mabishano ya hali ya upumbafu ya wale watu wasio na akili wanao sema:  

Mtuoneshe basi namna Yesu Kristo ni Mungu kweli na Mtu kweli, jameni mutuoneshe namna gani jambo lile linaweza kuwa sambamba. 

Wewe, kama mtu huwezi kuyafahamu, ni Mungu Baba pekee anayejuwa jambo hilo, sisi twaamini tu kwa njia ya imani.


3/ Tazameni Kwanza  kuzaliwa kwake na Bikira, hadi wakati wa nyuso yake ilibadirika na kungaa kama juwa lenye utukufu na kuonekana pamoja na mitume wa kale, miujiza zote alizo zifanya, na  wakati alipozimia roho katika bustani wakati aliposema kwa sauti kubwa: “kama ingeliwezekana, kikombe hiki kinipitie.” 

Pia, hapo Msalabani, ukitazama namna alivyofikia kufa, na wakati usomapo Maandiko kuhusu kufa kwake utakuta ya kuwa imeandikwa kwamba Yeye aliamuru kutoa Roho yake. 

Kwa siku za kale, hakuna mtu aliyekufa namna sawa, hakuna yule aliyefikia mwisho wa namna ile. 

Kiisha alifufuka toka wafu, akakwenda mbinguni naye ameketi kwa Mkono wa kuume wa Mungu Baba. 

Hakuna kamwe yule aliyekuwa na maisha kama yale. 

Ni vigumu, hautaweza kufahamu neno lile, wewe amini tu. 

Ndio, amini tu. 


4/ Tusome sasa Maandiko mengine: 

 2 Watesalonika 2: 7 

“Maana siri ya uasi hata sasa inatenda kazi; lakini yeye anayezuiza sasa atazuiza hata atakapoondolewa.” 

Kwa ngambo moja tunayo siri inayoleta starehe, raha na salama na kwa upande nyingine tunayo siri ya unyonge na giza. Siri hiyo inaitwa siri ya uasi na uovu. 

Neno la msingi katika waraka wa Watesalonika, ni kurudi kwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 

Kwa kweli siyo safari yake ya kurudi ya mara ya pili bali ni hiyo ya kunyakuliwa. 

Mtume Paulo anatujulisha hapa ya kuwa siri ya uasi hata sasa inatenda kazi, katika ulimwengu huu. 

Sasa siri ya uasi inamaanisha  nini? 

Tupime kuilinganisha na siri ya utauwa. 

Ina maanisha kwamba shetani yeye mwenyewe anakuja kukaa ndani ya mwili wa mtu, mtu mwenye zambi, mwana mpotevu. 

Kwa hii twagunduwa hatari ya vita mbaya ya huyo mnyama mukubwa atakayekuja duniani. 

Kwa aya ya 8 tutatambuwa kwamba anaitwa    mwenye uasi, yeye atakuwa muasi.  

Tofauti hapa ni kwamba Shetani yeye mwenyewe anakuja kukaa ndani ya mwili wa mtu, na Siri ya utauwa kwa sasa ni Mungu kugeuka kuwa mtu. 

Haya ndiyo inayoitofautisha kabisa, na kwa kweli shetani ni mwenye kufananisha yote  ya Mungu. 


5/ Tuchunguze uhusiano unaokuwa kati ya shetani na huyo mtu. 

 Ezekieli 28: 1 – 4 

“Neno la Bwana lilikuja kwangu tena likasema: 

Mwana wa watu, sema na mkubwa wa Tiro, Bwana MUNGU anasema hivi: 

Kwa sababu moyo wako umenyanyuliwa na unasema: Mimi ni Mungu, ninakalia kiti cha mungu, katikati ya bahari; hata hivi wewe ni mtu, wala si Mungu, hata ukiweka moyo wako kama moyo wa Mungu. 

Tazama, una hekima kuliko Danieli; hawawezi kukufichia siri yo yote; 

Kwa hekima yako na kwa ufahamu wako umejipatia mali, na umepata zahabu na feza katika hazina yako;” 

Hapa ni mwana wa mtu anayezungumuza na mwana wa mfalme wa Tiro, na tunaposhuka hapo chini kwa aya ya kumi na mbili, utasoma kuhusu mfalme wa Tiro. 

Hapo katika maandiko tunakuwa na picha ya watu wawili. 

Mfalme wa Tiro, pia na Mwana wa Mfalme wa Tiro. 

Uhusiano gani unaokuwa kati ya mfalme na mwana wa mfalme? 

Ni uhusiano kati ya Baba na Mtoto. 

Wote tunakubali kwamba yule mfalme wa Tiro anayezungumuziwa kwa aya ya 12, ni Shetani. 

Mwana wa mfalme wa Tiro, ni Mupinga Kristo, aliye mtoto wa Shetani. 

Mutaona ya kwamba zambi ya mtoto ndiyo ile ile ya baba yake Shetani. 

Yeye anasema: Mimi ni Mungu, ninakaa katika kiti cha Mungu. 

Nikusema, anajifanya mwenyewe kuwa Mungu, na ni hiyo aliyofanya shetani. Isaya 14. 


6/ Tuone nini inayosemwa katika kitabu cha Yoane 8: 44. 

“Ninyi ni wa baba yenu shetani na tamaa ya baba yenu munataka kuzifanya. 

Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo, na hakukaa katika kweli; kwa sababu hakuna kweli ndani yake. 

Wakati anaposema uwongo, anasema yaliyo yake mwenyewe, kwa sababu yeye ni mwongo na baba ya wongo.” 

Twasoma hapa kwamba shetani ni mwongo, yeye alikuwa mwuaji, na wakati anaposema uwongo, anasema yaliyo yake mwenyewe, yeye ni mwongo na baba ya uwongo. 

Baba ya nini? Na Kwa sababu gani? Uwongo. 

Uwongo ni nini? 

Ni mwana wake Mupingakristo.  

 

7/ Tufahamu kwamba 2Watesalonika 2: 7 inasema: 

“Maana siri ya uasi hata sasa inatenda kazi; lakini yeye anayezuiza sasa atazuiza hata atakapoondolewa.”  

Inasemwa hapa kwamba siri ya uasi hata sasa inatenda kazi, lakini yeye anayezuiza sasa atazuiza hata atakapoondolewa. 

Katika Biblia Tafsiri la Swahili, neno kuzuiza, ama kutokuruhusu, inamaanisha kukataza kitu kitendeke.  

Inamaanisha kuto kuruhusu.  

Mtume Paulo alipenda kumaanisha yafwatayo: 

Munafahamu ni kitu gani kinachofunga huyo mnyama asijifahamishe kwa sasa? Ni Roho Mtakatifu ndiye angali anamuzuiza, anazuiza miradi yake isianze kwa sasa, bali mipango yake yeye Mpingakristo, tayari yako katika ulimwengu huu na ni miradi inayoelekea madini kazaa na kazaa. 


8/ Tuoneshe wazi wazi kwamba ni Roho Mtakatifu ndiye anayezuiza Mpingakristo kuanza kazi zake katika ulimwengu huu. 

Ni nani mwenye anayesukuma zambi isitendeke? 

Jibu inapatikana ndani ya Biblia Takatifu. Ni Mwenyezi Mungu ndiye mwenye kuzuiza zambi. 

Mwanzo 6: 3 

“Bwana akasema: Roho yangu haitashindana na mtu milele, kwa sababu yeye vilevile ni mwili; hata hivi siku zake zitakuwa miaka mia moja na makumi mbili.” 

          Twafahamu wazi wazi kwamba ni Roho wa Mungu ndiye mwenye alikuwa akizuiza zambi kwa wakati wa Noa.  


Tusome sasa Isaya 59: 19 

“Na wataogopa Jina la BWANA toka mangaribi, na utukufu wake toka kuamka kwa jua; wakati adui atakapoingia kama garika, Roho ya BWANA atanyanyua bendera juu yake.” 

        Tumesikia hapa kwamba wakati adui atakapoingia kama garika, Roho wa BWANA atanyanyua bendera juu yake, nikusema kwamba: 

Roho wa Bwana atamuzuiza kutenda lolote lile, hata kwa zamani za kale kwa miaka iliyopita ni Yeye aliyekuwa akizuiza zambi. 

Ni Yeye aliyekuwa anasukuma  mtu asitende zambi, na kwa sasa, Roho wa Mungu anakaa ndani ya mwili wa mwamini, na ni Yeye anayefanya kuwa na kujizuiza kwa zambi. 


9/ Sasa twatambua   siri hizo wazi wazi: 

  Siri moja ni ya utauwa na siri lingine ni la uasi. 

Moja ni “Mungu kugeuka kuwa na mwili wa mtu.” 

Na lingine ni: “Shetani kuikaa ndani ya mtu.” 


10/ Tufahamu tena ya  kwamba: 

Alihesabiwa haki katika Roho. 

Neno kuhesabiwa haki inamaanisha kupewa usamani wake wa kweli na chochote kile kilicho chake, kuhakikisha, ushahidi wake wa kuvaa mwili ulionekana na mecho, bali Umungu wake haukuonekana kwa sababu ulikuwa unafunikwa na mwili. 

Na tena kwa nyakati ile, kuna michale michale ya UMungu wake yenye ilikuwa ikionekana, na Roho Mtakatifu kwa njia ya ushuhuda alikuwa anaonyesha kwamba Bwana Yesu Kristo alikuwa tu Mungu, Yeye hakuwa muzalimu.  

Yoana 1: 32 

“Yoane alishuhudia, alisema: Nimeona Roho akishuka kama hua kutoka mbinguni, akakaa juu yake.” 

      Huo ni ushuhuda wa Roho Mtakatifu, akionesha ushuhuda ya kwamba Bwana wetu Yesu Kristo ni Mungu. 


11/ Tutambue tena kwamba inasemwa ya kuwa: 

Alionekana na malaika; Bwana wetu Yesu Kristo alionekana na malaika. 

Kuvaa mwili kwa Bwana Yesu kulikuwa jambo lenye kushitusha na kushangaza wamalaika na ulimwengu wote pia wakati walipomtazama katika mwili wa mtu. 

Wamalaika walikuwa bado kumuona Mungu, isiyokuwa tu kwa wakati aliposhuka na kuvaa mwili wa maumbile la mtu. 

Ni lazima kufahamisha na mukazo wote kwamba Bwana Yesu Kristo alikuja kuvaa mwili wa maumbile na kubaki nao hata milele na milele, ni tamasha la kuvutia kweli kwa mecho ya wamalaika. 


12/ Twatambuwa kwamba neno “kuonekana na malaika”, siyo neno iliyotumikishwa kwa desturi katika Agano Jipya. 

Ikiwa kwa ngambo ya vitu, neno lile linamaanisha: 

Kutazama kitu kwa kukichunguza na kukitizama sana na angalisho na faida yote, kutazama kitu kilicho cha mafaa.  

Wamalaika walikuwa wakichunguza hatuwa zote alizofanya Bwana Yesu Kristo.  


13/ Pia twaona msemwa: 

Alihubiriwa kwa Mataifa. 

Waweza kusema kwamba jambo hili halina hata neno moja la kigeni

na kujiuliza kwa nini imetamkwa katika aya hii.  

Kuhubiri kwa Mataifa. 

Bali, kuna kweli jambo la muhimu tunalopaswa kuzungumuzia hapa, ya kwamba kwa muda wa zaidi ya miaka 4000, Mwenyezi Mungu hakuwasiliana na Mataifa, hata hakuwatumia ujumbe yeyote ile. 

Ufikiri kwanja kuhusu jambo lile. 

Kwa muda wa miaka 4000, Mwenyezi Mungu hakukaa na Mataifa wapagani, isipokuwa tu Taifa la wana wa Israeli. 

Wapagani ama Mataifa walikuwa kwa upande ungine ulio mbali na mbaya ngambo lingine la ukuta wa upatanisho. 

Waefeso 2: 11, 12 

“Kwa ajili ya maneno haya mukumbuke ya kwamba zamani ninyi, watu wa Mataifa kwa maneno ya mwili, munaoitwa Wasiotahiriwa na wale wale wanaoitwa Waliotahiriwa, tohara katika mwili iliyofanyika kwa mikono; 

Kwamba kwa wakati ule mulikuwa mbali na Kristo, mumetengwa mbali na jamaa ya Israeli, na wageni kwa maagano ya ahadi. 

Mulikuwa hamuna tumaini wala Mungu duniani.” 

     Walikuwa hawana Mungu duniani. 

Walikuwa wasioabudu Mungu tangu nyakati za Abrahamu, nikusema, zaidi ya miaka elfu ine mbele(miaka 4000).   


14/ Baadaye twatambuwa kwamba Kristo hakujipokea yeye mwenyewe. 

Ni kwa hiyo, Mwenyezi Mungu alimfunulia Mtume Paulo aliye Mtume wa Mataifa, Habari Njema, ili alifikishe na kulihubiri kwa Mataifa wapagani. 

Ingelikuwa mambo yabaki kama vile yalivyokuwa hapo kale, zamani za kale mbele ya miaka 4000, sisi Mataifa wapagani tungelikuwa bila tumaini, tungekuwa hatuna Mungu duniani, hatungelikuwa hata na kitu kimoja chakuwekea matumaini kwa faida yetu, kama haingelikuwa tu mwisho mbaya wa shida na gazabu katika tanuru ya moto wa jehenama. 

Bali sasa, tumusifu Mwenyezi Mungu kwa maana Mtume wa Mungu kwa Mataifa, Mtume Paulo alitufunulia na kutufahamisha sisi Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 

Kwa nyakati ya leo, Mwenyezi Mungu anayo sasa Habari Njema ya kupasha kwa Mataifa Wapagani. 

 

15/ Matendo ya Mitume 13: 44 – 46 

“Hata sabato ya pili, watu wengi, karibu mji mzima walikusanyika wasikie Neno la Mungu. 

Lakini wakati Wayuda walipoona makutano, wakajaa uwivu, wakabisha maneno yaliyosemwa na Paulo na kutukana. 

Paulo na Barnaba walisema pasipo woga: 

Ilikuwa lazima Neno la Mungu liambiwe kwenu kwanza; lakini kwa sababu munalisukuma mbali na kujihesabu wenyewe wasiostahili wa uzima wa milele, tazameni tunageuka kwa Mataifa.” 

     Tunafahamu hapa kwamba Wayuda hawakupenda kusikiliza Maneno ya Mungu, na ya kwamba Mataifa wao, walipenda kusikiliza Maneno ya Mungu pamoja na Wayuda, na jambo hili liliwapa Wayuda uwivu, walikuwa na wivu kuhusu ranga yao na nafasi pendelefu waliokuwa nayo mbele ya Mwenyezi Mungu, na walitaka kutenga Mataifa na kuwazuia wasisikie Maneno ya Mungu.  

Mutatambua kwamba inasemwa kwamba: 

Hata sabato ya pili, watu wengi, karibu mji mzima walikusanyika wasikie Neno la Mungu iliyohubiriwa na Mtume Paulo.  

Hapa tunaye Mtume Paulo anayepaza sauti kwa kusanyiko, akiwashambulia na kusema pasipo woga kwa Mataifa, na hapo wayuda hawakupenda Mataifa nao pia wahuzurie hiyo mkutano wa kusikiliza Neno la Mungu, walitaka wawaepushe kusikia na watiwe pembeni, wawe inje ya imani, kwa hiyo, Wayuda walianza kubisha na kupinga maneno yaliyosemwa na Mtume Paulo kwa wale Mataifa, walikanusha na kupinga yale maneno na kuyalaani Maelekezo  sawa na  historia ya Bwana Yesu Kristo inayopatikana katika sehemu ya kwanza ya Matendo ya Mitume sura 13. 


16/ Jambo lao la kupinga kukanusha na kulaani ilikuwa jambo nzito. 

Sawa Maandiko iliyosemwa na Bwana Yesu Kristo akisema: 

Yeyote yule atakaye toa matukano juu ya Mwana wa watu, atasamehewa, lakini, yeyote yule atakaye laani ama kutukana Roho wa Mungu, yeye hata samehewa kamwa wala katika ulimwengu huu wa sasa wala katika ulimwengu utakaokuja. 

Matayo 12: 31, 32 

“Kwa hivi ninawaambia ninyi, kila zambi na kila tukano watu watasamehewa; lakini kwa kutukana Roho hawatasamehewa. 

Na kila mtu atakayesema neno juu ya Mwana wa watu atasamehewa; lakini mtu ye yote anayesema juu ya Roho Mtakatifu hatasamehewa, wala katika ulimwengu wa sasa, wala katika ule unaokuja.” 

     Bwana wetu Yesu Kristu alisema hapo kale ili watu wafanye angalisho sana. 

Niliwatumia Roho Mtakatifu. 

Kama wewe unakufuru Roho Mtakatifu, ama unamupinga, wewe hautasamehewa kwa tendo lile. 

Ni kwa kufuana na tendo lile ndiyo maana Mtume Paulo alisema ya kuwa yeye anageukia sasa kwenye Mataifa Wapagani. 

Hii ni jambo la manufaa sana, jambo la furaha na raha, jambo nzuri kuliko. 

Neno la Mwenyezi Mungu linahubiriwa sasa kwa Mataifa Wapagani. 

Mataifa Wapagani wanageuka sasa nafasi lenye Habari Njema ya Yesu Kristo linatangazwa na kuelekezwa. 

Na kwa kweli, tendo hili linafanyika na kukamilika sasa kwa njia ya anguko la Wana wa Israeli. 


17/ Waroma 11: 11 – 12 

“Basi ninasema: Wamejikwaa waanguke kabisa? Hapana hata kidogo: 

Lakini kwa sababu ya kuanguka kwao wokovu umefikia Mataifa, ili wao watiwe wivu. 

Basi kama ikiwa kuanguka kwao kumekuwa mali ya dunia, na upungufu wao umekuwa mali ya Mataifa; si zaidi sana utimilifu wao?” 

     Mwenyezi Mungu anatuambia hapa kwamba, kwa njia ya kuanguka kwao, anguko la wana wa Israeli, ndiyo maana wokovu ulifikia Mataifa, ili uwaletee wana wa Israeli wivu. 

Mwenyezi Mungu anasema kwamba Habari Njema ya Yesu Kristo itahubiriwa sasa kwa Mataifa wapagani ili ichochee wana wa Israeli kwa wivu, na anguko lao limekuwa mali ya dunia, Mataifa wapagani, na upungufu wao umekuwa mali ya Mataifa, sawa vile Mtume Paulo alivyosema: 

Kwa maana ninasema kwenu Mataifa, mimi kama vile Mtume wa Mataifa Wapagani, mutambue neno hili: 

Habari Njema ya Yesu Kristo aliye Mungu, Mungu aliyevaa mwili wa mwanadamu, Habari Njema hiyo inatumwa sasa kwa Mataifa wapagani. 


18/ Baadaye muchunguze vema yanayosemwa hapa: 

     Aliaminiwa ulimwenguni 

Hii siyo jambo rahisi, sivyo? 

Siri kuu la ajabu na tukufu, Mungu kuvaa mwili wa mwanadamu inaaminiwa. 

Ni kweli siri hii haliaminiwi mahali pote duniani, tunatambua jambo lile; dunia hii inazidi kupinga, kukanusha, dunia inajaa na wale wanaopinga chochote kile hakifahamiki na akili ya kimtu, pahali pa kujaa na wakristo, dunia hii imejaa na dini mbali mbali.              

Wote wale wanaosema: Sisi hatuamini Biblia, hatusadiki kwamba Kweli ni katika Yesu Kristo peke yake. Bali, tumshukuru na kumutukuza Mwenyezi Mungu kwa kuwa kuna vile vile umati wa watu wenye kuamini Siri hii. 

Waweza vile vile kwa asubui ya leo kumushukuru Mwenyezi Mungu kwa kuwa wewe pia ni mmoja wa wale wenye kuamini Siri hii. 


19/ Tusome sasa Waraka wa: 

2 Watesalonika 1: 8 - 9  

“Katika moto wa kuwaka akiwalipa kisasi wao wasiojua Mungu, na wao wasiotii Habari Njema ya Bwana wetu Yesu Kristo; 

Watakaoazibiwa kwa uharibifu wa milele, kutengwa na uso wa Bwana na utukufu wa nguvu zake,”  

     Hapa Mtume Paulo anatuonesha kuhusu malipo yao, akisema kwamba itakuwa katika moto wa kuwaka akiwalipa kisasi wao wasiojua Mungu, na wao wasiotii Habari Njema ya Bwana wetu Yesu Kristo; 

Watakaoazibiwa kwa uharibifu wa milele, kutengwa na uso wa Bwana na utukufu wa nguvu zake. 

Hapa Mwenyezi Mungu anaonesha wazi kwamba atahazibu wale wenye hawapendi kuamini Mungu Mwema wa  Ajabu na Mtukufu. 


20/ Tufahamu mara tena kwamba inasemwa: 

Alipokelewa katika utukufu. 

Ni nani aliyemupokea? Mtu anapokelewa wakati kuna yule anayemupokea. 

Wakati unakwenda kumutembelea mtu nyumbani kwake na kwa bahati mbaya anamkuta hayuko, ametoka, na kweli wote wametoka, utasema: hakukukuweko yule ambaye angeliweza kunipokea. 

Neno kunipokea inaonesha Mapokezi. 

Ni nani yule aliyekuwa hapo ili amupokee Mwana wa Mungu? 

Eti kulikuweko mapokezi? Kwa kweli yalikuweko. 

Yeye alishikwa Mbinguni akipokelewa na Mungu Baba. 


21/ Mapokezi yale yalikuwa ya Ajabu. 

Wahebrania 7: 26 

“Maana kuhani mkubwa wa namna hii alitufaa sisi sana, aliye Mtakatifu, pasipo uovu, wala alama ya uchafu, aliyetengwa na zambi, aliyekuwa juu kuliko mbingu;” 

     Yeye aliyepandishwa juu sana kuliko mbingu.   


Wafilipi 2: 9 

“Kwa hivi Mungu vile vile alimtukuza sana, na kumpa Jina lililo juu ya kila jina;” 

     Mungu alimtukuza sana na kumpa Jina lililo juu ya kila jina. 

Ranga na Nafasi yake ni Mutawala. 

Mapokezi ya Bwana Yesu Kristo yalikuwa ya ajabu wakati alipopaa kwenda Mbinguni. 

Alitukuzwa na kunyanyuliwa juu sana kuliko. 

Alitukuzwa na kupandishwa juu sana kuliko mbingu zote kwa sababu yeye alijishusha chini sana, akiwa chini ya mutumwa wakati alipochukuwa mwili wa mtu, na yeye alipata mateso na uchungu na laana wakati alipotundikwa msalabani, tumtukuze Mwenyezi Mungu kwa sababu sasa ameketi kwa Mkono wa kuume wa Mungu Baba katika mahali pa kutukuzwa. 


AMINA. 

      

N°Ref: 05/20/1962 / 246 - THE MYSTERY OF GODLINESS/ 06/29/2021

Saturday, June 12, 2021

KWA WANAUME PEKEE / FOR MEN ONLY

Photo by B Smith from the patio


 


244 - KWA WANAUME PEKEE  /  FOR MEN ONLY

March 25, 1962 

Pastor Henry F. Kulp



 

1 Timoteo 2: 9 -15 


“Na vivyo hivyo wanawake wajipambe kwa mavazi yanayofaa, pamoja na adabu na moyo wa kiasi, si kwa kusuka nyole, wala kwa zahabu na lulu, wala kwa nguo za damani; 

Lakini kwa matendo mema, kama ilivyopasa wanawake wanaokiri kuogopa Mungu. 

Mwanamuke ajifundishe katika kimya akitii kwa kila namna. 

Lakini simpi mwanamke ruhusa kufundisha, wala kutawala mwanamume, lakini kukaa kimya. 

Kwa maana Adamu aliumbwa kwanza, halafu Hawa. 

Na Adamu hakudanganywa, lakini mwanamke akidanganywa, aliingia hali ya kukosa. 

Lakini ataokolewa kwa kuzaa mtoto, kama wakidumu katika imani na mapendo na utakatifu pamoja na moyo wa kiasi.” 

Mtume Paulo anatatua hapa mambo yanayoelekea wanawake katika makanisa, na  kuanza, anazungumuza kuhusu mavazi ya mwanamke, namna gani yampasa mwanamke kuvaa, baadaye analeta vizuizo viwili kuhusu mwanamke ndani ya makanisa. 

Kwanza, mwanamke hastaili kufundisha wanaume Biblia. 

Ya pili, mwanamke hastaili kutawala juu ya wanamume. 


1/ Tunapata sababu ya kwanza katika aya ya kumi na tatu. 

“Kwa maana Adamu aliumbwa kwanza, halafu Hawa.” 

Ni matatizo ya kujiuliza sababu yake Mwenyezi Mungu kuumba Adamu na Hawa, kuumba mwanaume na mwanamke, mwanaume aliumbwa wa kwanza kama malighafi, kama kitu kikuu, kama mambo kiongozi, mwanaume anapashwa kuwa kwa nafasi ya kichwa. 

Tuchunguze yanayosemwa katika: 


Mwanzo 2: 18 


“Bwana Mungu akasema: Si vema mtu awe peke yake; nitamfanyia msaidia anayefaa kwake.” 

Bwana Mungu akasema kwamba si vema mtu awe peke yake.

Atamfanyia msaidia anayefaa kwake. Hii inamaanisha kusema msaidizi. 

Nafasi ya mwanamke katika maisha ya siku zote ni kukamilisha sehemu iliyokosa kwa mwanamume, kwa hivyo haifai mwanamke kunungunika nungunika kwa kuwekwa kwa nafasi hiyo, kwa sababu ni nafasi hiyo ndiyo aliyopewa na Mwenyezi Mungu, na nikwa hiyo nafasi ndipo anakuwa na furaha. 


2/  Tutambuwe sababu ya pili yenye kueleza sababu gani Mwenyezi Mungu hamruhusi mwanamuke kufundisha mwanamume Biblia ama kuwa na uwezo juu ya mwanamume. 

Adamu hakudanganywa, bali ni mwanamke aliyedanganywa. 

Yaonekana kuwa sawa umbalimbali na kawaida. 

Adamu hakupotoshwa kwa kudanganywa? Biblia yasema HAPANA. 

Yeye alifanya zambi mecho yake yakiwa wazi kabisa. 

Shetani alimjaribu Hawa moja kwa moja, lakini hakuweza moja kwa moja kumjaribu Adamu. 

Kama vile tulivyosema mbele, Adamu alifanya zambi mecho yake yakiwa wazi kabisa. 

Adamu alijuwa ni nini aliyokuwa akitenda, lakini Hawa hakutambua. 

Hawa, yeye alipotoshwa. Aliamini yale shetani aliyokuwa akimwambia. 

Shetani, akija kwa sura ya nyoka alimwambia Hawa: “Kama ukila ya tunda ya mti huu utakuwa na hekima, utakuwa sawa Mungu, utakuwa Mungu.” 

Utakuwa na ufahamu juu ya mambo yote, na kama unavyojuwa, Hawa aliamini mambo yale Shetani aliyomuambia. 

Adamu hakumwamini Shetani, alikuwa akimjua vizuri. 

Alijuwa kwamba ni uwongo mtupu. Hawa alipotoshwa. 

Alitwaa tunda na akampa Adamu, Adamu alichukuwa tunda toka mkono wa Hawa, na Adamu alikuwa mwenye kujuwa lile alilokuwa akitenda. 

Alifahamu, akiwa mecho wazi, kwamba alikuwa akimukosea Mwenyezi Mungu. 

Ni kweli, Adamu alikuwa mwenye makosa, lakini alikuwa anatenda haya yote kwa kumuokoa mke wake. 


Waroma 5: 14 

“Lakini kufa kulitawala tangu Adamu mpaka Musa, hata juu ya watu wote wasiofanya zambi kama alivyofanya Adamu, aliye mfano wake yeye atakayekuja.” 


3/ Adamu alijitoa peke yake ili aokowe mke wake, ni kwa hiyo Mwenyezi Mungu alimuweka mwanamke kwa nafasi ya kunyenyekeza.  


4/ Bali, tukumbuke kwamba mwanamke anaweza kuwa na huduma.

Siyo katika kusanyiko ya hazarani kanisani. 

Siyo kwa kufundisha wanaume Biblia ama kuwa na mamlaka juu ya wanaume, bali mwanamke anakuwa na wajibu wa kuizungumuzia katika mazungumuzo ya upekee. Acheni niwaletee mwangaza kuhusu jambo lile kwa mwangaza wa Maandiko Matakatifu ndani ya Kitabu cha 

Matendo ya Mitume 18: 24 – 26 

“Basi Myuda mmoja, jina lake Apolo, mzalia wa Alesanduria, mtu wa elimu, akafika Efeso; naye alijua sana maandiko. 

Mtu huyu alikuwa amefundisha njia ya Bwana; na kwa kuwa roho yake ilikuwa ikiwaka, alianza kusema na kufundisha kwa kweli maneno ya Yesu, naye alijua ubatizo wa Yoane tu.

Akaanza kusema pasipo hofu katika sunagogi; lakini wakati Akila na Prisila walipomsikia, walimtwaa kwao, wakamfunulia zaidi njia ya Bwana, aijue kabisa. ” 


5/ Inaonekana wazi kwamba Apolo hakupata mafundisho ya kuongeza elimu ya sayansi ya  Biblia katika Mashule Makuu ya kiteolojia, ama kwa njia ya mwongozi moja mkuu wa dini, wa nyakati zile, bali alipata mafunzo yake kwa njia ya wasani wawili, mmoja wao akiwa mwanamke. Hii ni yenye kuvutia sana. Yaonesha namna gani Mwenyezi Mungu anaweza kutumia mwanamke.  


6/ Mara tena kazi hii wasani wale wawili wa Mwenyezi Mungu, kazi  waliofanya kwa KRISTO, siyo tu kwa shairi lilo pekee ndipo inapotajwa. 


1 Wakorinto 16: 19 

“Makanisa ya Asia wanawasalimu ninyi. Akila na Prisila wana wasalimu ninyi sana katika Bwana, pamoja na kanisa linalokutana ndani ya nyumba yao.”

7/ Aina ya walimu mwenye Mutume Paulo alikuwa anafikiria katika Maandiko haya yanatajwa katika Kitabu cha 

Waefeso 4: 11 

“Naye alitoa wengine kuwa mitume; na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa Wahubiri wa Habari Njema; na wengine kuwa wachungaji na walimu,” 

Ni wanaume ndiwo wanao hudumia  ndani ya huduma hizo zote,  kuna vikwazo kazaa kuhusu wanawake wanaohudumia kwa nafasi hizo, hiyo siyo kwa ajili ya kuleta mazarau juu ya wanawake ama kuwafezeesha, hii haifanye mwanamuke kuwa mwenye hana faida, bali Mwenyezi Mungu anakuwa na nafasi alilotayarisha juu ya mwanamuke, na nafasi yake siyo ya kukamata ofisi za madaraka. 


8/ Mutatambuwa kwamba wanawake wanakuwa wakiwekwa katika hali hiyo, sababu Hawa alishindwa  kuchunga na kubaki imara kwa  zamu yake. 

Hiyo ndiyo sababu ya pili. 

Waweza kusema hiyo siyo haki, kitu gani kilicho fikia Hawa, eti yeye hangaliweza kukumbuka kuwaza kuhusi sisi? 

Lakini, ni  hivyo alivyotenda. 

Tukumbuke kwamba Waroma 5: 12  inasema:  

“Hivi, kama kwa mtu mmoja zambi iliingia ulimwengu.” 

Sisi sote ni watendazambi kwa leo, na zambi ilikuja juu yetu sisi sote kwa njia ya Adamu, na sote tunakufa kwa sababu ya zambi ya Adamu. 

Waweza kujiambia kwamba hiyo siyo haki. Mwenyezi Mungu hakukuuliza neno. 

Ni kwa namna hivi ndivyo Mwenyezi Mungu alivyotatua jambo lile, kwa njia ya Adamu sote tulifanya zambi na sote tunakufa. 

Tutambue ya kwanza kwamba: 

1 Wakorinto 15: 21 yasema: 

“Maana kwa kuwa kufa kuliletwa na mtu.” Na kwa Aya ya 22 twasoma:

“Kwa sababu kama katika Adamu wote wanakufa,”

Wanadamu wanaweza kuwa hawafurahiye jambo hili, bali hiyo ndiyo kweli na hakika kuleta mapinduzi juu yake haitabadirisha hata nugta moja. 

Ni vivyo hivyo kuhusu wanawake, mwanamke anaweza kujiletea mawazo ya mapinduzi na kusema kwamba yeye hawezi kamwe kugandamizwa kwa sababu Hawa alipoteza nafasi yake na kuanguka, lakini mwanamke atadumu tu katika hali hiyo na Mwenyezi Mungu ahakikisha kwamba ni hivyo. 

Na neno njema lipaswalo kufanya ni kuheshimu na kuitika hiyo nafasi iliyo mapenzi ya Mwenyezi Mungu na kuwa  mtu ambaye aliye sawasawa na mapenzi ya Mwenyezi Mungu na kuheshimu Maandiko yake Matakatifu na ni kwa njia hiyo ndipo utakapofanyikiwa. 


9/ 1 Timoteo 2: 15    

“Lakini ataokolewa kwa kuzaa mtoto, kama wakidumu katika imani na mapendo na utakatifu pamoja na moyo wa kiasi.” 

Hii haimaanishi kusema kwamba mwanamke fulani anaokolewa sababu alizaa mtoto, bali, ameokolewa kwa njia ya kuja kwa Mbegu la mwanamke. 

Mbegu hiyo ni Bwana wetu Yesu Kristo aliyeleta Wokovu.  


10/ Tutambue pia kwamba 1 Timoteo 3: 1 yasema: 

“Na neno hili ni la kweli: Kama mtu akitaka kazi ya mwangalizi, anataka kazi nzuri,” 

Jina Bishop inayomaanisha jina Mzee, ni jina Mwangalizi. 

Katika Agano Jipya hatuja jali kuona namna ya mamlaka watu wanaokabizi wa Bishop kwa siku za leo. 

Mtu anayekuwa na ranga fulani na nafasi ya heshima sana katika kanisa pia akiwa na mavazi maridadi ya namna ya kanzu. Kwa kweli hiyo haiambatani na Biblia. 

Jina Bishop inayo maanisha Mzee, inaonesha tu mtu anayetaka kujitoa mwenyewe kwa kazi ya kuhudumia maneno ya kanisa. 

Kwa kufahamu maneno haya, kwanza twapashwa kutambua kwamba mafundisho yanayoletwa kwa siku za leo kuhusu viongozi wa dini, kuhusu ranga na mamlaka katika makanisa ni machukizo kwa Mungu. 


11/ Jameni muniruhusu niwaoneshe jambo inayojulikana zidi ya Viongozi wa kanisa. 

Ndani ya hayo makanisa saba yanayotajwa katika Maandiko ya Kitabu cha Ufunuo wa Siri sura ya pili na sura ya tatu, na ndani yake tunachukuwa lile kanisa la tatu lililo kanisa la Pergamo(Aya ya 12). 

Tutambuwe kwamba Ufunuo wa Siri 2: 15 inasema kwamba: 

“Vivyo hivyo wewe una watu wanaoshika mafundisho ya Wanikolayi.” 

Jambo inayokuwa machukizo kwangu. 

Katika kanisa hili kuna Kawaida ya Mafundisho ya namna mbili inayofahamika: Mafundisho ya Baalama na Mafundisho ya Wanikolayi. 

Kawaida ya mafundisho ya Baalama inafundisha kuvumiliana.

Baalama alikuwa anatiya waisraeli moyo wachangane na mataifa mengine za wapagani na hii ilisukuma waisraeli wapoteze hali yao ya Taifa lililopendelewa.

 Mafundisho ya wanikokolayi inamaanisha kutawala juu ya Taifa fulani.

Ni sawasawa na viongozi wa makanisa wanajiweka kando, mbali na watu wengine wa kidunia. Ningelitamani mufahamu kwamba Mwenyezi Mungu anachukia mambo yale. Mawazo yale yanakuwa machukizo mbele ya Mungu. 

Usomapo Ufunuo wa Siri 2: 6 

“Lakini una neno hili, ya kuwa unachukia matendo ya Wanikolayi, ambayo mimi ninayachukia.” 


12/ Tujaribu kuambatanisha aina ya wa Bishop ama Waangalizi, katika makanisa zetu, kufwatana na Maandiko ya aya ya 2, ya 1Timoteo sura 3   (1 Timoteo 3: 2). 

“Basi imempasa mwangalizi asiwe na laumu, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi, mwenye akili, mtu wa utaratibu, mkaribishaji wageni, mwenye kujua kufundisha.” 

Maelezo haya yaonesha kwamba huyu mtu anayetajwa hapa ni mtu mwenye maadili ya juu sana. 

Ni maelezo yenye kwa kweli ni vigumu kuyatimiza.  

13/ Mutatambuwa kwanza kwamba ni hiyo ndiyo kiini cha matarajio bora. Kweli hatupashwi kungojea hali hiyo ijifanye yenyewe bila kujitowa kwetu sisi, bali yapashwa kujitoa na kuamuwa kupiga mwendo ulio bora.

Hiyo ndiyo inapashwa kuwa shauku la moyo wetu. 

Twapashwa kutarajia hali hiyo kwa roho yetu yote bila kuzubaa. 

 

Neno la kwanza ni kwamba mtu huyo anapashwa kuwa bila laumu. 

Inamaanisha  mtu asiye laumiwa. 

Huyu Mzee ama Mwangalizi anapashwa kuwa mtu mwenye hawezi kushotwa kidole cha mashitaka hata kwa mtu mmoja. 

Ni kweli kwamba watu watapendelea kumuchongea Mwangalizi, bali, mashitaka yao yanapashwa kuwa bule pasipo msingi yoyote, na bila ushahidi wowote. 

Watu watakushitaki wakikusingizia mambo kazaa na kazaa. 

Kila yule anayesimama imara katika njia ya Mungu atasingiziwa tu.

Lakini mashtaka haya ya watu mbalimbali yakasimama na kuwa kweli na kuwa na ushahidi, itabidi uangalizi wa huu mtu ukomeshwe, asiwe tena Mwangalizi. 

Bali imetupasa kukataa na moyo wetu wetu kusikiliza uvumi ama mambo ya aina ya kutetana. 

Twapashwa kujielekeza na kuvutwa na mambo yaliyo na ushahidi. 


14/ Mume wa mke mmoja. 

Tumefikia sasa jambo lenye linaleta shida na uvuguvugu nyingi kwa kanisa. 

Jambo hilo lamaanisha nini? 

Mume wa mke mmoja? 

Kuna wao wanaosema kwamba hapashwi kuwa na wanawake wengi pamoja. 

Wengine wanasema kwamba, kama mke wake akifariki, huyu mtu anapashwa baki bila kuowa mara tena. 

Wengine wanasema kwamba mtu mwenye hana bibi hapashwi kuwa Mwangalizi wa kanisa; na kwa kweli hiyo siyo kweli. 

Tafsiri lake kufwatana na namna inavyoandikwa nikusema: MWANAMUME WA MWANAMKE MMOJA, yenye tunaweza kutafsiri kama ifwatavyo: AINA YA BWANA MWENYE ANA MKE MOJA. 

Ni kama aina ya imbwa iitwao Mchungaji-Ujermani, inakuwa ya mtu mmoja tu peke yake(Bwana). 

Nina imbwa wangu anayeitwa Apache ni Mchungaji-Ujermani, wengi wanamuita Imbwa-Polisi. 

Ni umbwa wa mtu mmoja pekee, waweza kupenda kumulea, waweza kupenda kumushurulikia, mambo haya yote hayamwambiye kitu. 

Umbwa ule unatii tu mtu mmoja katika jamii nzima. 

Katika jamii nzima umbwa huu unatambuwa  na kuheshimu mamlaka ya mtu mmoja tu ndani ya jamaa nzima. 

Hiyo ndiyo maana ya yale yasemwayo hapa. 

Ni mwanaume anayekuwa na mwanamke moja tu kama bibi yake. 

Eti haya yote yamaanisha nini? 

Hii aimaanishi kwamba mtu mwenye bado kuowa hawezi kuwa Mzee wa kanisa ama Mwangalizi. 

Neno lenye twapashwa kukumbuka ni kwamba, kama tukijaribu kurudi nyuma kidogo, wakati Mtume Paulo alikua akiandika Waraka huu, watu hawa walikuwa wakitokea moja kwa moja kwa maisha ya Kipagani, kwenye zambi ya uzinzi ilikuwa ikivuma sana. 

Kitu watu waliona kufanya ilikuwa kusoma tu Agano Jipya ili wapatekujuwa maagizo kuhusu uzinzi, pepo ya uzinzi ilikuwa kwa eneo zote. Ilikuwa jambo la muhimu sana kukataza kuwa na wake wengi.

Kama mtu mwenye kuwa na wake wengi alifikia kubadilika na kuokoka, mtu huyu hakuruhusiwa  kuwa Mzee ama  Mwangalizi. 

Na ninafahamu vilevile kwamba mtu hakuwa mwaminifu kabisa kwa mke wake, mtu huyu hakustahili kuwa Mzee ama Mwangalizi. 


15/ Anapashwa kuwa macho wazi, maana yake mwenye asiye zorota, mwenye kiasi maana yake akiwa na umakini, mwenye akili, Mzee wa kanisa ama Mwangalizi anapashwa kuwa mtu wa mwenendo safi, siyo tu kwamba anapashwa kuwa na usemi ulio bora, lakini zaidi mwenendo wake unapashwa kuwa bora zaidi. 

Mzee wa kanisa ni mtu anayeishi siku kwa siku akiambatana na mahubiri anayofundisha, mtu wa utaratibu, mkaribishaji wageni, neno mukaribishaji wageni inamaanisha kuwa mufurahifu na roho nzuri na wageni. Inamaanisha kukaribisha wageni nyumbani mwake, yaani nyumba yenye inakuwa mlango wazi kwenye wageni wakaribishwa. 


16/ Mwenye kujua kufundisha.

 Mzee wa kanisa anapashwa kuwa mwalimu. 

Mwenye kujua kufundisha inamaanisha, siyo mwenye kujitoa kufundisha, ama mwenye kujaribu kufundisha, bali mwenye kuzama katika Maandiko Matakatifu, mwenye kuwa na werevu wa kufundisha. 

Pia, Mzee wa kanisa hapashwi kupenda vinywaji vya pombe, si mtu wa kulewa na mvinyo, si mpigaji. 

Si mtu wa ugonvi, wazo tunalo hapa ni mtu mkali mwenye fujo ya ugonvi, mwenye machokozi na vikwazo iwe kwa mikono yake ama kwa ulimi ama masemo yake. 

Ulime wa watu wengine una sumu ya kuuwa, unaweza kuumiza na kusambaza. 

Kuna watu wengi wanaweza kuwa watenda maovu, wenye kukwazisha wengine kwa njia ya ulimi wao. 

Mwangalizi anapashwa kuwa mtu anayefanya angalisho kwa matumizi ya ulimi wake. 


Watu wanaoweza kumiliki vinywa vyao, wapole, watu wanaochunga vema nyumba zao, wenye hawahubiri kufwatana na tamaa yao ya feza ama mwenye kutamani. 


Feza siyo kabisa mbaya. 

Kuna watu wengi wenye mali, lakini wao ni watu wa Mungu. 

Abrahamu wa Agano la Kale alikuwa mtu mwenye mali sana, lakini pia alikuwa mtu wa Mungu. 

Inakuwa shida sana kama muhubiri anakuwa tu akitia mkazo kwa maisha ya kila siku, akitia mkazo tu kwa feza. 


Hiyo inakuwa sawa anasa ya kupenda feza, na kuwa huduma yenye Bwana hawezi kamwe kubariki. 

Kweli mahamatisho ni yenye maana katika kupanga miradi. 

Lakini yafaa kuchunguza kama makusudi yetu ni bora na nzuri katika mipango za njia zenu zote na hasa huko mbele kwa mazabau. 


AMINA. 


N°Ref: 03/25/1962 / 244 - FOR MEN ONLY / 06/12/2021