Wednesday, April 29, 2020

NEEMA NI JIBU / GRACE IS THE ANSWER

Lake Kivu at sunset








     NEEMA NI JIBU
     321 - GRACE IS THE ANSWER
     December 28, 1976 
     Pastor Henry F. Kulp 




Waefeso 2: 7 - 10 
“Hata katika nyakati za kuja aoneshe wingi wa kupita kiasi wa neema yake kwa wema wake kwetu katika Kristo Yesu; 
Kwa maana mumeokolewa kwa neema kwa njia ya Imani, wala neno hili halikutoka ndani yenu wenyewe, ni zawadi ya Mungu, 
Si kwa matendo, asiwe mutu atakayejisifu. 
Maana sisi ni kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu ili tutende mema Mungu aliyotengeneza mbele ili tutembee ndani yao.” 
Hapa tunapata maandiko matamu na marembo sana. 
Wengi wenu wanafahamu kwa moyo sura mbili ya hii maandiko na yawezekana  sura ine.  Kwa binafsi  ningewasihi mushike na kufahamu kwa moyo,  sura hizo zote ine na mupate kuvumbuwa ukweli  mukubwa sana na wa muhimu wenye  kuonyeshwa hapa. 

1/ Mwenyezi Mungu ana miradi ama mipango yake inayotendeka si kwa kubahatisha. 
Mungu ni Mukamilifu kweli, na anatenda kazi zake zote na kupanga miradi yake yote  katika ukamilifu. 

2/ Inatupasa  kufahamu ya kuwa maisha ya mwamini ina  sehemu kubwa tatu: 
a. Wokovu 
b. Maisha ya hapa chini duniani mbele ya kutoweka ama kunyakuliwa. 
c. Umilele, wakati yuko pamoja na Bwana na Mwokozi wetu. 
Aya ya saba inazungumuza juu ya sehemu hii ya tatu, inayohusu  maisha ya milele ya mwamini. 
Shairi la nane(8) , na la kenda(9), inahusu sehemu ya kwanza yaani Wokovu,  kutoka kwenye mauti na kuingia uzima, kutoka kuwa mwana wa shetani na kugeuka kuwa mwana wa Mungu. 
Aya ya kumi ni sehemu ya pili, yaani maisha yetu hapa duniani kiisha wakovu, mbele ya kuhamishwa kwetu ama kunyakuliwa kwetu.
Tuchunguze sasa sehemu hizo tatu na tuone ujumbe gani Mwenyezi Mungu anapenda tufahamu. 

3/ Aya ya saba(7), hata katika nyakati za kuja. 
Hii inakuwa msemwa unaofwata ungine na kutuonesha kwamba  kuna jambo Mungu atatutendea  katika nyakati za kuja. 
KATIKA NYAKATI ZINAZO KUJA MOJA NYUMA YA NYINGINE. 
Inamaanisha katika umilele unaokuja, Mwenyezi Mungu atatutendea  jambo fulani. 

4/ ILI AONYESHE 
Hii ni neno maalum katika kigriki N-DIKE-NEW-ME na inamaanisha kuonyesha, kutambulisha, kuhakikisha kwa wazi. 
 ILI KWA KUONYESHA KWA KUHAKIKISHA KWA WAZI. 

5/ Ni nini Mwenyezi Mungu atakayo tuonesha kwa wazi? 
Wingi wa kupita kiasi wa neema yake kwa wema wake. 
Neno “ wa kupita kiasi”  ni HOOP – PEAR – BAL – O. 
Balo,  inamaanisha kutupa huko mbele na HOOP inamaanisha kupita kiasi na hapa inamaanisha nzuri sana kupita kiasi, nzuri sana zaidi na inasemwa kwa wakati wa sasa. 
Inamaanisha kwamba Mungu ataendelea kuitimiza kwa milele na milele. 
Ona raha za nyakati zetu za kuja. 
Utajiri sana, Samani kubwa kupita kiasi ni hii atatuonesha, samani kubwa zaidi ya wingi wa kupita kiasi wa wema wa Neema yake. 
Waroma 5: 20  
  “Lakini sheria iliingia, ili zambi ziwe kubwa sana; lakini pahali zambi zilipozidi, neema ilizidi zaidi sana:” 

6/ Namna gani kutofautisha na kujuwa umbalimbali kati ya hayo na namna anavyotuonesha  Neema kwa sasa? 
Kwa siku za leo, tumeokolewa kwa neema na tunakingwa na kuchungwa kwa neema. 
Lakini kwa leo, haiwezekane Mungu atuoneshe wingi wa kupita kiasi wa neema yake kwa wema, sababu tungali tukivaa mutu wetu wa zamani. 
Ni kwa hiyo, kuna wakati Mungu anaruhusu mateso yatufikie, yeye anatufunza na kutuhimiza, kuturekibisha, na mara kwa mara anaruhusu tupate mibaraka katika maisha yetu. 
Katika nyakati itakayo kuja, katika maisha ya umilele, utu wa zamani utaondoshwa na Mungu atatufurika na mibaraka, mateso hayatakuweko, hatutarekibishwa tena. Tuna nyakati za kuja za Baraka sana. 
Yote tunayoishi leo ni maonjo tu kidogokidogo ya hizo mibaraka. 

7/ Ingelikuwa kwamba Mwenyezi Mungu aliruhusu tuishi tu katika Baraka, sisi hatungeliwezekana, tungelijazwa na kiburi, tungelikuwa na uchoyo kiasi na tungelitamani kujisifu pahali pa kurudishia Mwenyezi Mungu Sifa. 


8/ Maana ya Neema ni vyote kwa bure  
Mara ngapi Neema iko ndani ya wingi wa kupita Neema kuzidi sana? 
Waroma 5: 20 
“Lakini sheria iliingia, ili zambi ziwe kubwa sana; lakini pahali zambi zilipozidi, neema ilizidi zaidi sana:” 
Katika hii aya tuna kipimo cha kuzidi sana cha Neema. 
Ni kupita sana zaidi hiyo tunayoweza kufikili. Mwenyezi Mungu atatufunulia hayo katika nyakati za umilele zinazokuja. 

9/ KATIKA WEMA 
Wema ni CRAY – STOW –TACE ni hii inamaanisha Ukaribishaji. 
Ni Mwenyezi Mungu alie Mukaribishaji Mkamilifu. 
Tukamate mfano wa baba mmoja aliye na mwana wake mume asiye kuwa kwa nafasi anapohitajika kuwa kwa wakati, anayekuwa na tabia ya kutenda maovu mengi hata baba yake hana ile wakati wa kumuonesha ukaribishaji wake, sababu kila wakati yuko nafikilijuu ya namna gani kuhazibu mtoto, kumurekibisha, lakini nyakati itakuja yenye huyu mwana ataamua kuachana na maisha ile mbaya na kwa saa hiyo baba ataanza kumukaribisha. 
Ni huu mwana njo alikuwa akizuiza wema wa baba yake. 
Katika YESU KRISTO haya yote ni kweli sababu sisi tunaunganishwa na KRISTO. 

10/ Aya ya nane(8), ya kenda(9) inatupeleka kwa sehemu ya kwanza. 
TUMEOKOLEWA KWA NEEMA KWA NJIA YA IMANI  
Katika kigriki, maneno haya hameandikwa katika nyakati inayoonesha kwamba tendo inazidi tu kuendelea. 
Ni tendo iliyoanza kwa ziku zilizo pita na yenye inaendelea katika nyakati na siku zitakazokuja. 
NI MUSALABA. 

11/ Kwa njia ya IMANI   
Hii njo vifaa ya Wokovu. 
IMANI na NEEMA njo vitu muhimu sana juu ya Wokovu. 
NEEMA ni mchango  kutoka kwa Mungu 
IMANI ni mchango kutoka kwa mwanadamu. 
Unacho lazimishwa kufanya ni kuamini tu na hakuna kustahili yoyote inayokuja kwa kuamini. 
Ni zawadi ya MUNGU. 
Imeandikwa waziwazi na kusomwa waziwazi: 
Wala neno hili halikutoka ndani yenu wenyewe. 
Neno hili, ni neno lisilo na tegemeo ama upendeleo, inaweza tumikishwa ngambo zote, bila kubadili  aina ya Neema, sawa vile  aina ya Imani na haibadirishe kitu kwa Wokovu. 

12/ Ni zawadi ya Mungu 

13/ Si kwa matendo   
Hii inamanisha nini? 
Hii inamaana ya kusema kwamba, si kwa tabia nzuri ama kazi nzuri ya kimutu. 
Inatupaswa kufahamu kwamba tungali tunavaa utu wetu wa zamani. Na siyo zambi tu njo mutu wa zamani anaweza tenda, ila  mutu wa zamani anaweza vilevile kutenda matendo ama tabia nzuri za kimutu. 
Lakini yatupasa vile vile kufahamu kwamba tabia nzuri za mwanadamu ni kufa. 
Wahebrania 6: 1  
“Kwa sababu ile, tukiacha mafundisho ya kwanza ya Kristo, tuendelee hata utimilifu; tusiweke tena msingi wa kutubu kwa kazi za kufa, na ya Imani kwa Mungu.” 
Matendo yote mazuri na tabia yote muzuri ya mwanadamu ni matendo ya kufa. 
Tabia hizi ni za kufa kama tukilinganisha na kuwaza juu ya Mungu, lakini sivyo vile kama maelekezo ni kwa mutu. 
Na hapo yafaa tutambuwe kwamba matendo mazuri ya mwanadamu, ni matendo ya kufa mbele ya macho ya Mungu tena matendo yale hayakubaliwe na Mwenyezi Mungu. 
Isaya 64: 6 
“Lakini sisi sote tumekuwa kama kitu kichafu, na haki zetu zote ni kama vitambaa vya kupasukapasuka vya taka; sisi sote tunakauka kama jani, na maovu  yetu yametuondoa, kama upepo unavyoondoa,” 
Tabia zote nzuri tunazo na matendo yote mazuri tufanyayo ni kama taka. 

14/ Tabia na Matendo nzuri ya mwanadamu haiwezi kuokowa 
Waroma 11: 6 
“Lakini ikiwa kwa neema yake, haiko kwa matendo tena, au neema isingekuwa neema; na ikawa kwa matendo, haiko neema tena; au matendo yasingekuwa matendo.”  
2 Timoteo 1: 9 
“ambaye alituokoa akatuita kwa mwito mtakatifu, si kwa kadiri ya matendo yetu, lakini kwa kadiri ya kusudi lake mwenyewe na neema yake, tuliyopewa katika Kristo Yesu mbele ya nyakati za zamani,”  
Tito 3: 5, 7 
“Si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyoyafanya lakini kwa rehema yake alituokoa, kwa kuoshwa kwa kuzaliwa mpya na kufanywa upya na Roho Mtakatifu; 
7. tukihesabiwa haki kwa neema yake, tupate kufanywa wariti kwa tumaini la uzima wa milele.” 

15/ Tuchunguze hapa utu wa zamani na tabia na matendo mazuri ya mwanadamu. 
Wanadamu waliumbwa bila kuwa na zambi ya asili, ni kwa sababu hiyo walikuwa na ufahamu juu ya tabia na matendo mema. 
Lakini tangia siku mwanadamu alianguka, alipokea ule utu wa zambi, ule utu wa zamani na tendo la kwanza lenye mwanadamu alilolifanya kiisha kuanguka ni tendo nzuri ni hiyo Kazi ya kujijengea nguo ya majani. 
Kazi ya mwanadamu aliyo ifanya ya kwanza baada ya kuanguka, kazi hiyo haikuwa ya zambi lakini kazi nzuri ya kufunika uchi ama utupu wake.  

16/ Asiwe mutu atakaye jisifu 
Kujisifu inamaanisha nini? 
Ni kupata kusudi ama tendo katika maisha yako,  itakaokuonesha wewe kama mutu mwema. 
Ni hiyo mwanadamu anajikaza daima kutimiza  katika dini mbalimbali. 
1 Wakorinto 1: 30, 31 
“Lakini kwa yeye ninyi ni katika Yesu, aliyefanyizwa na Mungu kuwa kwetu akili, na haki, na utakaso na ukombozi; 
Hata sawasawa ilivyoandikwa: Yeye mwenye kujisifu, ajisifu katika Bwana.” 
1 Wakorinto 4: 7 
“Basi ni nani ambaye anakufanya kuwa mbalimbali? 
Nawe una kitu gani usichopokea? Lakini kama ulikipokea, kwa nini unajisifu sawasawa hukupokea?  

AMINA 


N°Ref: 12/26/1976 / 321 - GRACE IS THE ANSWER / 2020 

Thursday, April 23, 2020

TUMAINI LA BARAKA / BLESSED HOPE


Photo taken from B Smith's Kitchen Window









     289 - TUMAINI LA BARAKA / BLESSED HOPE
     March 7, 1965 
     Pastor Henry F. Kulp





Waroma 8:14 -17 
“Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hawa ndio wana wa Mungu.
Kwa maana hamukupokea tena roho ya utumwa inayo leta woga, lakini mulipokea roho ya kufanywa wana, kwa sababu hii tunalia: Aba, Baba. 
Roho mwenyewe anashuhudu pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu: 
Na kama sisi tu watoto, basi tu wariti: Wariti wa Mungu, na wariti pamoja na Kristo; kama tukiteswa pamoja naye, ili tutukuzwe pamoja naye vilevile.”

Katika magazeti iliotangazwa na kusomwa munamo tariki 24 Marchi, mwaka wa 1965, kulikuweko tangazo juu ya mabishano yenye yalikuwa yakitarajiwa kati ya makanisa ya ki protestanti mujini. 
Gazeti hiyo ilikuwa ikisimamiya juu ya maandiko na masemi ya makundi tatu mbalimbali ya kiteologia kuhusu yale wanao amini juu ya maisha ya wanamemba wao wa protestanti kwa siku zile. 
Ijapokuwa walikuwa na mapingano juu ya mambo kazaa, wote walikuwa wakiamini kwamba yafaa kupunguza maneno moja moja katika Biblia Takatifu, maneno yote yenye wao walizani kwamba hailingani na maisha ya kingwana (siku za sasa). 

Kuna maandiko katika Biblia yenye mutu wa siku za leo hakubali wala kuamini. Na kwa kweli hii ni maarifa ya Ibilisi. 
Mbele ya kutenda jambo lolote, ningewasihi muone na kutambua umuhimu na mafaa makuu ya Biblia. 
Kuna Mambo makuu ya muhimu na ya faida sana yenye tutachunguza katika sura ya nane ya Barua ya Mtume Paulo kwa Waroma, inawezekana kwamba wengine wanaweza kukamata maandiko haya kama kawaida, kama kwao Biblia haiko Neno la Mungu, yaani Maandiko Matakatifu. 

1/ Katika semina yetu tuliyofanya kwa miaka iliopita juu ya kanuni na kawaida ya Kiprotestanti, tulizungumuzia juu ya kanuni na kawaida ya ortodoksia mupya. 
Yawezekana wewe umeisha sikia juu ya kundi hili, ama kwako yaweza kuwa ni mara ya kwanza, lakini wale tuliokuwa nao kwa semina iliyopita walisikia mengi juu ya neno hili. 
Kanuni na kawaida hii inasema na kuamini kwamba: 
Maandiko Matakatifu yaani Neno la Mungu iko tofauti na Yesu Kristo. 
Wanasema kwamba eti unaweza kuamini Bwana Yesu Kristo bila kuamini Neno la Mungu. 
Wanatangaza kuwa Imani yetu inapashwa jengwa juu ya Yesu Kristo pekee hapana juu ya Neno la Mungu.
Jameni muniruhusu ni niwaulize swali moja: 
Namna gani utafikia kwa kiwango cha kumwamini Bwana wetu Yesu Kristo bila mwangaza wa imani unao kuja wakati unasikia Neno la Mungu? 
Watu wale wanatofautishi Neno iliyofanyika Mwili na Neno lililoandikwa. Ijapokuwa hakuna tofauti kati ya Neno lililo vaa Mwili na Neno lililoandikwa. 
Hakuna hata tofauti moja. 
Katika Yoane 1: 1, tunasoma: 
“Katika mwanzo alikuwa Neno, na Neno alikuwa pamoja na Mungu, na Neno alikuwa Mungu.” 
Yesu ni Neno.   Neno ni Mungu. 
Sasa tushuke hapo chini katika Yoane 1: 14 
“Na Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu, tukatazama utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee akitoka kwa Baba, amejaa neema na kweli.” 
Neno alifanyika mwili ni YESU. 
Neno lililo andikwa, kila andiko ni Yesu Kristo na ni Yeye Neno iliofanyika Mwili. 
Tunalofahamu ni kwamba Neno alifanyika Mwili, na tunajuwa hivyo kupitiya usomi wa Neno lililo andikwa, ama kupitiya maandiko Matakatifu. 
Waweza namna gani kuwa na ufahamu wowote juu ya Bwana Yesu bila kusoma Biblia? 
Namna gani kufikia kupata maelezo makubwa kuhusu Bwana YESU bila kusoma Neno lililoandikwa? 

2/ Ninafahamu kwamba kitabu hiki ninachoshika mukononi kiliundwa toka kiwanda cha kuchapa vitabu. Hivi kita zeeka na kuchakaa siku moja. 
Kweli, kila miaka miwili, mimi ninalazimishwa kununua Biblia ingine mupya wakati ile ya kwanza inachakaa na kupasuka pasuka. 
Ninaacha ile ya zamani na ninakwenda kununua ingine mpya. 
Sababu vikartasi havishikamane na kuungana tena pamoja sababu kila wakati kitabu hicho kilikuwa kikitumikishwa mara kwa mara na siku kwa siku. 
Wakati unatia kando Biblia ya zamani inayo chakaa sana, wewe hautupilie Neno la Mungu sababu uliuza Biblia ingine mupya. 
Ni Maandiko inayoandikwa katika kitabu hiki njo iko ya mafaa kabisa.
Hapana makartasi, habani utonvi waliotumikisha kwa kuunganisha makartasi, cha Muhimu ni Neno pekee.  

3/ 2 Timoteo 3: 16 
“Kila andiko limepewa kwa maongozi ya Mungu, na linafaa kwa mafundisho, na kwa kuonya watu juu ya makosa yao, na kwa kuwaongoza na kwa mafundisho katika haki.” 
Kila mmoja wetu angelipashwa kuchunga aya hii kwa ufahamu katika moyo wake. 
Kila andiko limepewa kwa maongozi ya Mungu. 
Neno, andiko linamaanisha yale yaliyoandikwa. 
Nikusema kila andiko imepewa kwa maongozi toka kwa Mungu ama Pumzi ya Mungu. 
Tuchunguze sasa neno “Maongozi ama Pumzi.” 
Katika Kiswahili, pumzi ya, ni kusema kukokota hewa kwa kupumuwa.
Hii inaweza maanisha neno la Kigriki inayo patikana hapo. Sasa ikawa kukokota hewa inje ama ndani, hiyo siyo tatizo, lakini tunafahamu kwamba Mwenyezi Mungu alipuliza pumzi. 
Hatufahamu kama Mungu alipulizia ndani ama inje lakini inatuonesha kwamba Kila andiko limepewa kwa pumzi ya Mungu. 
Pumzi ya Mungu ni Neno la Mungu, haijali fasi tunapolikutana, ni Nafsi ya Pili katika Utatu Mtakatifu. 
Bwana Yesu Kristo, anayekuwa Neno, Yeye ni Pumzi ya Mungu. Neno ni Pumzi ya Mungu. 

4/ Twende sasa kwa Waroma 8: 17  
“na kama sisi tu watoto, basi tu wariti: Wariti wa Mungu, na wariti pamoja na Kristo; kama tukiteswa pamoja naye, ili tutukuzwe pamoja naye vilevile.” 
Kwa hiyo, hakika watu wengi hawapendi kusikia hivyo. 
Watu wengi wakati wanaposoma Biblia, wanakusudia kuruka na kutambuka maneno haya, wakiyapita juu juu bila kutiya mukazo. Kwa kweli hawangepashwa fanya hivyo. 
Sisi ni wariti pamoja na Kristo. 
Kuna tofauti kati ya kuwa muriti,  na kuwa muriti pamoja. 
Juma iliyopita, tuliwaonesha umbalimbali ulio katika maneno haya mawili. 
Tulisema kwamba: 
Kama mutu akifa na anaacha nyuma yake shamba kubwa kwa watoto wake wane, eneo ile itagawanywa kwa watoto wake wane. 
Na kila muriti atapata sehemu yake asili mia makumi mbili na tano: 25%. 
Lakini kama mutu nyuma ya kufa akiachia watoto wake shamba kubwa, na wote wakiwa kama Wariti pamoja; 
Kila mmoja wao anaruhusa ya kusema nyumba ni yangu, kibandaholi ni changu, shamba ni langu, eneo lote ni langu, mali inayokuwa kwenye Banki ni yangu. 
Kwa namna ya umutu wa leo mambo haya ni magumu.
Lakini ni hivi itakuwa mbinguni sababu tutafananishwa na Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. Ndiyo maana nilipendelea mufahamu tofauti hii kubwa. 

5/ Niliwapa moja ya ma shairi ama aya inayojaza roho yangu na furaha kubwa: 
 1 Wakorinto 3: 21 
“Basi, mutu ye yote asijisifie watu, kwa sababu vitu vyote ni vyenu;” 
Ni vitu ngapi vinavyo kuwa vyenu? 
Muniruhusu kuwauliza swali hilo. 
Jibu lenu inaweza kuwa gani? 
Vitu vyote ni vyenu. 
Ninyi ni watajiri sana kupita namna munavyo wazia, watajiri kupita mwisho wa mawazo ya kibinadamu. 
Tufahamu vema kwamba inasemwa hapa: Ulimwengu wote ni yangu. 
Na ni ya Yesu Kristo, na kwa kuwa sisi ni wariti pamoja na Yesu Kristo, chochote kile kinakuwa chake, kinakuwa vilevile changu. Uzima ni wangu na kufa ni yangu. 

6/ Tulikuwa tukizungumuzia juu ya Kufasiri vema Neno lililo kweli. 
2 Timiteo 2: 15 
“Dumu kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mfanya kazi asiyeona haya, ukifasiri vema neno la kweli.” 
Kuna umbalimbali kati ya maneno inayoelekea Taifa la wana wa Israeli, Ufalme wa Mungu na Kanisa Mwili wa Kristo. 
Kwa kufahamu vema Uriti unaokuwa ndani yetu, Uriti ambao sisi ni wariti pamoja na Bwana Yesu, yafaa kwetu tuchunguze hali yetu na uhusiano wetu na Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 
Mutume Paulo alituandikia Vitabu kumi na tatu na hapo hatuingize kitabu cha Wahebrania, sababu sisadiki kama ni Mutume Paulo aliyeandika kitabu hicho. 
Na katika Barua yote kumi na tatu Mutume Paulo aliyoandika, hakuna hata fasi moja aliposema kwamba Bwana ni Muchungaji wetu. 
Hii ni ukweli moja ya mizani sana, lakini tunaona kwamba Mutume Paulo aliiweka kando, sababu uhusiano yenye iko kati ya muchungaji na kundi lake siyo iyo inayopatikana kati ya KRISTO na KANISA MWILI WA KRISTO. 
Uhusiano unaopatikana kati ya KANISA MWILI WA KRISTO na KRISTO ni uhusiano wa kichwa na mwili. 
KRISTO ni Kichwa na Sisi ni Mwili. 
Ni sababu ya hiyo ndio maana katika Barua za Mutume Paulo, hakuna hata nafasi moja aliosema kwamba Bwana Yesu ni Muchungaji wetu na kwamba sisi ni Kondoo za Kundi lake, Mutume Paulo hakusema neno hili hata mara moja. 

7/ Mutume Paulo haja tarajia kusema kwamba Bwana Yesu ni Mufalme wetu, anasema tu Yesu ni Mufalme wa wafalme na Bwana wa mabwana. Na Mutume Paulo haja tarajia kusema Bwana Yesu ni Mufalme wa Kanisa Mwili wa Kristo. 
Hapa duniani, kama  tuwatu wa mufalme wa inchi fulani, sisi wakaaji wote  katika huo ufalme tunakuwa na mapashwa na tunarizika namna sawa, na pia kuna hata watu wengine wenye hawana bahati ya kumwona mfalme uso kwa uso hata kwa mara moja maishani mwao. Wao hawazaliwe katika jamaa la kifalme ama hawana hata urafiki moja na mufalme kwa hivyo hawawezi hata kumuona ana kwa ana hata mpaka kufa kwao.  
Kwetu sisi wakristo hatuko namna sawa. 

8/ Mutume Paulo hajawai kusema kwamba KRISTO ni Mwalimu wetu. 
Yeye hakumuita Bwana Yesu Rabbi. 
Usomapo Vitabu ine vya Injili, utaona kwamba kwa kumwita Bwana Yesu, wanatumia jina Rabbi, Mwalimu. 
Kama vile Barua za Mutume Paulo zinavyosema, kwetu sisi Bwana Yesu haiko Mwalimu. 
Ni ROHO MTAKATIFU ndiye Mwalimu wetu. 
Anatufundisha juu ya Yesu Kristo, anashuhudia Yesu Kristo, anatuongoza katika yote yaliyo kweli juu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 
Tunatambua kweli kwamba uhusiano unaokuwa kati ya mwalimu na mwanafunzi siyo ule unaokuwa kati ya KRISTO YESU na KANISA MWILI WA KRISTO.
Mwanafunzi anaweza akasikilize mwalimu wake na kushika yote anayofundisha na kupata faida ya mafundisho yote, lakini mwanafunzi huyu hampendi hata kidogo mwalimu wake.
Munajuwa wanafunzi wengi wanaoshuhudia kama mwalimu tunaye ni mzuri, anafundisha safi sana lakini sura na umbo wake haunipendezi hata kidogo.
Ni kwa sababu hiyo njo maana Mutume Paulo hakusema hata kidogo kwamba Bwana wetu Yesu Kristo ni Mwalimu wetu. 
Roho Mutakatifu anatufundisha na kutushuhudia juu ya Bwana wetu Yesu Kristo mpaka anatusukuma kumpenda Mwokozi wetu zaidi na zaidi tena.  

9/ Sisi ni viungo vya Mwili wake na KRISTO ndiye KICHWA.  

10/ Kama vile tunavyoendelea kuchimbua majifunzo haya,   itakuwa ya muhimu sana kufahamu tofauti inayo kuwa kati ya kuwa KIUNGO CHA MWILI WA KRISTO na kuwa MWANAMEMBA WA UFALME WA MUNGU. 
Uriti wetu haugawanyiki, sasa,   kuwa mwanamemba wa KANISA MWILI WA KRISTO, inamaanisha nini? 
Neno ngumu hapo ni “KUGAWA” uendapo sisi ni Wariti pamoja na KRISTO. 
Uriti wetu siyo wa kugawanya katikati yetu sababu sisi ni wariti pamoja na Kristo, tunariti yote kama vile Maandiko inatuambia katika                         
1 Wakorinto 3: 21 – 23 
“Basi, mutu ye yote asijisifie watu, kwa sababu vitu vyote ni vyenu; 
Kama Paulo, au Apolo, au Kefa, au dunia, au uzima,au kufa, au vitu vya sasa, au vitu vya kuja; vyote ni vyenu, 
Na ninyi ni wa Kristo na Kristo ni wa Mungu.”
YESU KRISTO hata gawanya nasi uriti kwa nusu. 
Ole kwao wanaotiya uvuguvugu katika ufahamu wao juu ya mambo inayo elekea UFALME WA MUNGU na KANISA MWILI WA KRISTO, Wayuda na Mwili wa Kristo, wenye kutiya uvuguvugu hawata tambua umbalimbali huu. 

11/ Luka 19: 11 – 19 
“Nao wakisikia maneno haya, aliendelea kusema mfano, kwa sababu alikuwa karibu na Yerusalema, nao walizania ya kama ufalme wa Mungu utaonekana mara moja. 
Basi alisema: Mtu mmoja mwenye heshima alisafiri kwenda inchi ya mbali kupokea kwake mwenyewe ufalme na kurudi. 
Akaita watumwa wake kumi, akawapa feza kumi, akawaambia: 
Fanyeni biashara hata wakati nitakaporudi. 
Lakini watu wake walimchukia, wakatuma wajumbe kumfuata, wakisema: 
Hatutaki mtu huyo kutawala juu yetu. 
Ilikuwa aliporudi, nyuma ya kupata ufalme, akatoa amri kuita wale watumwa ambao aliwapa feza, apate kujua namna ya biashara aliyofanya kila mtu. 
Wa kwanza alikuja, akasema: 
Bwana, feza yako imepata feza kumi. 
Akasema: Vema, mtumwa mzuri; kwa sababu umekuwa mwaminifu kwa neno dogo sana, uwe na mamlaka juu ya miji kumi. 
Na wa pili alikuja, akisema: 
Bwana, feza yako imepata feza tano. 
Akamwambia: Nawe uwe juu ya miji mitano.” 
Fahamu vema kwamba hii inahusika na Ufalme wa Mungu duniani, hapana Mwili wa Kristo, sababu kwenye aya yake ya kumi na moja Biblia inasema kwamba: Alisema hivyo sababu alikuwa pembeni ya Yerusalema, na kwamba nao walizania ya kama Ufalme wa Mungu utaonekana mara moja. 
Na aliwaambia fumbo ama mufano huo juu ya kuwaonesha kwamba haija timia bado nyakati ya Ufalme wa Mungu kuonekana mara moja. 
Na Yeye mwenyewe alijifananisha na yule Mutu moja mwenye heshima aliyeenda inchi ya mbali, - Yeye alienda Mbinguni. 
Alikwenda mbinguni kisha kufa kwake na kufufuka alipanda juu mbinguni.
Na Yeye atarudi tena ili apokee Ufalme wake, na inasemwa kwamba Yeye aliita watumishi wake kumi(10), akawapa feza kumi na akawaambia fanyeni biashara mpaka wakati nitakaporudi. 
Wakati gani na namna gani watumwa hawa watafanya biashara? Sasa hivi. 
Sisi hatuko watumwa, sisi ni Viungo vya Mwili wake Kristo. 
Kwa kweli, kurudi hii inayosemwa hapa, ni kurudi kwa mara ya pili kwa Mwokozi wetu Yesu Kristo, hii safari siyo ya kuchanganya na KUNYAKULIWA kwa KANISA, inayokuwa wakati Mwokozi wetu Yesu Kristo atakuja kuchukuwa Kanisa Mwili wa Kristo. 
Aliita watumishi wake na alipenda kupata ripoti ya viashara vyao. 
Wa kwanza alikuja, akasema: Bwana, feza yako imepata feza kumi. 
Akasema: Vema, mtumwa mzuri; kwa sababu umekuwa mwaminifu kwa neno dogo sana, uwe na mamlaka juu ya miji kumi. 
Na wa pili alikuja, akisema: Bwana, feza yako imepata feza tano. 
Akamwambia: Nawe uwe juu ya miji mitano.
Ni vema muvumbuwe kwamba hapa mufano huu hausemwi juu ya Kanisa Mwili wa Kristo. 
Mungu hakuahidi hii juu ya Kanisa, lakini ahadi hii ni juu ya Israeli. 
Uriti wetu pamoja na KRISTO hautagawanyika, sisi ni wariti pamoja na KRISTO. 
Yote inayokuwa ya Bwana wetu Yesu, yote yale ni yetu na tunayo pamoja naye. 
Mungu hatagawanya uriti wetu, ni kweli, ni ajabu na ni Baraka kubwa na ni hivyo. 

12/ Tukumbuke neno moja la muhimu.
Bwana wetu Yesu Kristo hatatuambia fanyeni biashara hata wakati nitakaporudi. 
Mwokozi wetu atatuambia: Vitu vyote ni vyetu, furahini pamoja NAMI. 
Hii ndiyo tofauti. 

13/ Matayo 19: 27 - 28  
“Halafu Petro akajibu, akamwambia: Tazama sisi tumeacha yote, na kukufuata, sisi tutapata nini basi? 
Yesu akamwambia: Kweli ninawaambia ninyi, ya kwamba ninyi ambao mulinifuata, katika ulimwengu mupya, wakati Mwana wa watu atakapoketi juu ya kiti cha utukufu wake, ninyi vilevile mutaketi juu ya viti vya ufalme kumi na viwili, mukihukumu makabila kumi na miwili ya Israeli.”
 Tunaona hapa Bwana Yesu anazungumuza kuhusu makabila kumi na miwili ya Israeli na hakusema chochote kuhusu Mataifa. 
Wao watakuwa wakimiliki chini ya uongozi wa ufalme wa Yesu wakati ataketi juu ya kiti cha utukufu wake. 
Kwetu sisi wariti pamoja na Yesu haitakuwa sawa vile. 
Kweli tutamiliki nazani sisi tutakuwa tunamiliki tukiwa huko mbinguni. 
Sisi hatutamiliki chini ya uongozi wa Bwana Yesu, lakini sisi tutamiliki pamoja na Bwana Yesu. 
Hii ndiyo tofauti kati ya Kanisa Mwili wa Kristo na Ufalme wa Mungu. 

14/ Sasa tuangalie kwa makini sana neno la mwisho lenye linapatikana katika shairi ili: 
“kama tukiteswa pamoja naye, ili tutukuzwe pamoja naye vilevile.” 
Msemwa huu unamaanisha kama yatupasa kuteseka pamoja naye ili tutukuzwe pamoja naye.
Sawa vile tafsiri ya Kigriki inaonesha; 
Tunaona kwamba Maandiko hayasemi kuteswa kwa ajili ya Bwana Yesu, lakini Maandiko yanasema kuteseka pamoja na Bwana Yesu. 
Na kanuni kubwa lenye tuko tunajifunza katika shairi hii ya Waroma ni kanuni ya UTAMBULISHO YA KUUNGWA NDANI YA YESU
Tunateswa pamoja na Bwana Yesu, hapana kwa ajili ya Bwana Yesu. 

15/ Kama basi ni hivyo maneno yale tatu mu Kigriki ni A- PEAR, na kama unapenda kupata tafsiri nzuri ya neno –PEAR, tusome katika 
1 Watesalonika 1: 6 
“Mukakuwa wafuataji wetu, na wafuataji wa Bwana, mukikwisha kupokea neno katika mateso mengi, pamoja na furaha ya Roho Mtakatifu;” 
Yakuwa kwamba neno hili ni halali kwa Mungu.  Na neno yakuwa kwamba ndio tafsiri ya neno A-Pear ya kigriki. 
Sasa shairi hiyo ingelitafsiriwa ifwatavyo: 
Yakuwa kwamba tukiteswa pamoja naye, ili tutukuzwe pamoja naye vilevile. 

16/ Mateso haya siyo mateso ya maisha ya kawaida. 
Tangu wakati tuliungwa na KRISTO, ni halali tungojee yale yote aliyopata Mukombozi wetu Bwana Yesu Kristo. Hayo yasituuzunishe kwa maana tutatukuzwa pamoja naye vilevile na kuishi milele pamoja naye. 

17/ Kuna mateso yanayoambatana na wanaadamu na mateso haya mengi ni ya kimwili. 
Tunapata uchungu, unyonge na maumiwu, tunateseka na magonjwa, misiba mbalimbali, hata misiba ya arzi. 
Sisi sote siku moja tutakufa, miili yetu inazorota siku kwa siku na hiyo inatupatia mateso ya kimwili, lakini hayo yote siyo mateso Mungu anayo tuzungumuzia hapo.  

18/ Kunakuwa kuvunjika mioyo, na hii inafikia watu wote, waliookolewa kama wapagani wote wanateswa kwa kuvunjika mioyo.
Tunaneseka na magumu mbalimbali inayotuzunguuka, inayokumbwa na vita ya chinichini ya mataifa makuu duniani, magumu inayoletwa toka mahali petu pa kazi ya kila siku. 

19/ Kuna mateso hiyo ya kimutu inayotufikia wakati tunatambua kwamba ndugu yetu fulani iko anapitia katika kipindi cha shida na maangaiko makubwa, tunaweza tukiwa bila tatizo, lakini tunapoona ndugu katika shida na maangaiko hadi kufikia kufa, nasi tunashiriki yale mateso pamoja naye. 
Lakini Mungu hazungumuzie mateso kama hiyo hapa.

20/ Mungu anatuzungumuzia mateso yenye tunateswa pamoja naye. 
Kukataliwa, kuchukiliwa, kuzarauliwa. 
2 Wakorinto 4: 18 
“Kwa sababu hatuangalii vitu vinavyoonekana; lakini vitu visivyoonekana: Kwa sababu vitu vinavyoonekana ni vya saa kidogo tu, lakini vitu visivyoonekana ni vya milele.” 
Hapa tunazungumuziwa juu ya ile utukufu utakaokuja na ukubwa wa ajabu wa utukufu kubwa sana utakao uzunguuka.
Mara kwa mara inakuwa magumu kwetu kulinganisha namna utukufu ule utakuwa. 
Hatuweze kufahamu kukadirisha utukufu huo, sababu unashinda mafikili yetu kama watu wa dunia hii. 
Sisi tunatarajia utukufu na hakuna mateso yoyote inayotufikia tunayoweza kulinganisha na utukufu wenye tutapata yenye Mungu Baba anayo tayarishia wewe na mimi. 
Tazama Baba Mungu anasema hapa: 
Mateso ya sasa hayawezi linganishwa na utukufu yenye itafunuliwa ndani yetu.  
Hii inaburudisha nafsi yangu sana. 
Ninatamani sana wewe utukuzwe siku moja, sijuwe kama utafanana namna gani lakini utavaa utukufu na mimi vilevile pamoja nawe. 

21/ Tuone kwamba 2 Wakorinto 4: 17 inasema: 
“Kwa sababu mateso yetu mwepesi yaliyo kwa dakika tu, yanatufanyia utukufu wa milele unaozidi mwingi sana;” 
Hapa tuna nyakati mbili zinazopingana, nyakati ya muda na umilele. 
Mateso yetu hapa chini duniani ni ya muda kitambo. Yanadumu miaka kumi na miwili, sawa mfano iyo ya ndugu John Bunyan. 
Ama mateso inaweza kuwa ya maisha mzima, hiyo isikusumbue, si kitu, ni ya faida ndogo sana sababu siku moja tutapata utukufu wa milele unaozidi mwingi sana.  
Angalia umbalimbali kati ya mambo iliyo ya muda kitambo na utukufu wa milele unaozidi mwingi sana yenye tutariti. 
 
AMINA.

N°Ref: 03/07/1965 / 289 - BLESSED HOPE / 03/04/2020 

Monday, April 20, 2020

MUNGU NA MDUDU / GOD AND THE WORM

Photo taken by from B Smith's Kitchen Window







299 - MUNGU NA MDUDU / GOD AND THE WORM
June 27, 1965 
Pastor Henry F. Kulp 





Waroma 8: 30 - 34 
“Na wale ambao aliwachagua tangu zamani, akawaita vilevile; na wale ambao aliwaita, akawahesabia haki: na wale ambao aliwahesabia haki, akawatukuza vilevile. 
Basi tutasema nini juu ya maneno haya? Kama Mungu akiwa upande wetu, ni nani aliye juu yetu? 
Yeye asiyeachilia Mwana wake, lakini alimtoa kwa ajili yetu yote, namna gani atakosa kutuletea vitu vyote pamoja naye? 
Ni nani atakayeshitaki wachaguliwa wa Mungu? Mungu ambaye anawahesabia haki; 
Ni nani anayehukumu? Ndiye Kristo aliyekufa, ndiyo, zaidi, amefufuka, naye yuko kwa mkono wa kuume wa Mungu, tena ndiye anatuombea.” 

 Juma jana tulipata maelezo zaidi juu ya kuonesha, kupitia Baruwa ya Mtume Paulo kwa Waroma kwa shairi yake ya nane, namna UMUNGU wa MUNGU unakuwa upande wetu. 
Huyo UTATU Mtakatifu, Mungu Roho Mtakatifu, Mungu Baba, Mungu Mwana, na kwa kweli,  namna UTATU MTAKATIFU uko kwa upande wetu, hakuna hata mmoja atakayepima kuwa juu yetu. 
Jameni ndugu waona mahali pa ajabu, raha na utukufu kwenye twapatikana sisi tulioamini Yesu Kristo. 
Kama kungelikuwa kitu chenye kingekusisimua unene “aleluya”, hii ndicho.

1/ Wakati nilipokuwa nikichunguza maandiko haya, mawazo yangu ikaelekea moja kwa moja katika kitabu cha Isaya. 

Isaya 41: 11 – 14 
“Tazama, wote waliokasirika juu yako watapata haya na kufazaika; wao wanaoshindana nawe watakuwa si kitu, na wataharibika. 
Utawatafuta wala hutawaona, hata wao wanaopigana nawe: 
Watakuwa kama si kitu, kama kitu kisichokuwa, wale wanaofanya vita juu yako. 
Kwa maana mimi, BWANA, Mungu wako nitashika mkono wako wa kuume, nikikuambia: Usiogope, nitakusaidia. 
Usiogope, wewe mdudu Yakobo, nanyi watu wa Israeli; nitakusaidia, Bwana anasema, na mkombozi wako, Mtakatifu wa Israeli.” 

Shairi hiyi inatuambia kwamba Mungu alikuwa upande wa Israeli, kwa kweli ni hivyo, Mungu alikuwa upande wa Israeli kama Inchi inayoonekana machoni mwa watu hapa duniani. 
Mungu aliambia Israeli: 
Tazama, wote waliokasirika juu yako watapata haya na kufazaika; wao wanaoshindana nawe watakuwa si kitu,  na wataharibika. 
Utawatafuta wala hutawaona, hata wao wanaopigana nawe: watakuwa kama si kitu, kama kitu kisichokuwa, wale wanaofanya vita juu yako. 
Mungu alijulisha Israeli kwamba: 
Utakuwa na maadui, utakuwa na wao watakao sirika juu yako, lakini nini itakayo wafikia? 
Nyuma ya mambo yote watapata haya na kufazaika, watakuwa kama sikitu  na wale wenye wanaoshindana nawe wajuwe kwamba wataharibika. 
Na wakati utawatafuta, hutawaona. 
Na kwa kweli, ni maneno haya ndiyo wana wa Israeli wangelipashwa kutamka wakati wowote ule wangeli pata adui. 
Kama Mungu iko pamoja nasi(Israeli), ni wanani wale wanaoweza kuwa juu yetu? 
Wanaweza kushindana na Israeli lakini nyuma ya maneno yote watashindwa.  

2/ Hapo, tunafika kwa aya ya kumi na ine(14),  wazo inataka kuwa sawa  ya ziaka na kuwa sawa umbalimbali na ya kwanza na kwa mwisho inatuonesha wazi utupu wa mwanadamu, pia inasema  kwamba mwanadamu  hana samani hata moja na kwa ngambo nyingine inatuonesha samani kubwa sana ya nguvu za ajabu za Mungu kupitia matendo yake. 
Tukumbuke kama Mungu aliambia taifa la Israeli kwamba: Adui wako hawatakushinda kamwe watakuwa kama sikitu. 
Kiisha Mungu  akasema: 

Usiogope wewe mdudu Yakobo, mimi nitakusaidiya… O Mungu mkuu. Patano gani hii! 
Mungu na mdudu. 
Mara kwa mara Israeli walikuwa wakianguka sababu hawakuwa wanatambua kwa kweli kama wao ni wanani. 
Wana wa Israeli walikuwa midudu. 
Wakati watu wanafanya patano la kazi, mmoja analeta mchango wa kipesa, mwengine analeta ujuzi wake ama mambo ingine kazaa ya kazi yao. 
Lakini wakati tunafanya patano na Mungu, 
Yeye anatuomba tu tuheshimu maagizo yake. 

Tunaleta mchango wa unyonge wetu na Yeye analeta mchango wa Nguvu zake. 
Sisi tunaleta zambi zetu na Yeye analeta Neema na Haki. 
Sisi ni washuhuda wa utupu yetu na Yeye anatujibu kwamba anavyo vitu vyote. 
Mungu na mdudu. 
Mungu anasema kwamba mutu yeyote asipime kupinga ama kubishana na patano hii. 
Ajali gani wana wa Israeli waliokuwa nalo wakati walishindwa kukubali upotevu, na anguko lao na kuitika uepo wa ujazi na utimilifu wa Mungu katika vyote. 

3/ Kwa kweli hii ndiyo mambo ya siku za leo.
Kumbukeni, sawa vile tulivyo jifunza katika masomo yetu ya saa ya usiku kwa siku zilizopita, Tuliona namna Mwenyezi Mungu alivyosema, kwa kutaja Mwenyezi Mungu, tunamwona  Bwana wetu Yesu Kristo, alisema kwamba mataifa ni imbwa na kiisha akalinganisha wayuda na nyoka na kizazi cha nyoka na hapa wanaitwa mdudu ama midudu. 
Hawakuwa kweli na kitu cha kutowa.
Patano yenye ilifanywa kati la taifa la wana wa Israeli na Mungu ilifanyika kwa namna hii: Mwenyezi Mungu akiwa mwenye kuleta vitu vyote. 
Kwa siku za leo tunajikuta tuko mikono mitupu, hatuna kitu hata kimoja chenye tunaweza kuleta kwa Mungu, lakini Yeye anatutolea vyote, tuangalie vema nini anayosema katika aya hii. 
Basi tuseme nini juu ya maneno haya? 
Kama Mungu akiwa upande wetu, ni nani aliye juu yetu? 
Yey asiyeachilia Mwana wake, lakini alimtoa kwa ajili yetu yote, namna gani atakosa kutuletea vitu vyote pamoja naye? 
 Ni nani atakayechitaki wachaguliwa wa Mungu? 
Mungu ambaye anawahesabia haki; 
(Ni nani anaye hukumu)? Ni Mungu, hakuna kitu kinacho fanyika na mwanadamu. Ni Mungu anaye fanya vyote.
Ndugu yangu shikamana na nafasi yako ya mdudu mbele ya Mwenyezi Mungu na umwache Yeye afanye vyote kwa faida yako. 

4/ Tutazame vema nini inayosemwa kwa sehemu ya kwanza ya aya ya makumi tatu na moja(31). 

Basi tutasema nini juu ya maneno haya? 
Ni ulizo inayofwata mambo yote makuu na ya  ajabu Mungu anayo tufunulia hapo juu. 
Tunaona kwamba katika mistari ifwatayo, tunapata majibu mazuri Mwenyezi Mungu anazo patia kila aliye amini Bwana wetu Yesu Kristu, kwa kuweza kujibu. 
Kwanza: Mungu ni upande wetu. 
Ya pili, kwa aya ya makumi tatu na mbili (32):

Yeye asiyeachilia Mwana wake, lakini alimtoa kwa ajili yetu yote, namna gani atakosa kutuletea vitu vyote pamoja naye? 
Si fahamu vema kama tunajuwa kwa makini maana ya msemwa: 
Mungu Baba alimtoa Mwana wake. 
Sijuwe kama siku moja umeisha kaa kabisa na kuanza kujiuliza na kutafuta kufahamu hali gani inayoweza kuwa ndani ya nyumba maali mupendwa, mutu wa mafaa sana, mutu yule anayependwa sana katika ile nyumba, mutu yule aondoshwe katika ile nyumba. 
Nina waza na kujiuliza kama Mbingu ilikuwa katika hali gani na kufanana namna gani wakati Bwana wetu Yesu Kristo alipoacha mbingu na kuja hapa duniani. 
Aliacha vyote na kuja mikono mitupu.  
Nazani munakumbuka prezidenti moja wa inchi ya Marekani jina lake ilikuwa Calvin Coolidge. 
Wakati alipokuwa angali bado katika mamlaka, mtoto kijana wake alikufa. 
Nazani mtoto yule alikuwa na umri wa miaka 17. 
Yeye alikuwa akifanya mazoezi ya mchezo wa mbio ya miguu katika boma la michezo la masomo, na hapo katika mazoezi ya kwenda mbio, mguu wake ulijikwaa kwenye musumari ama kisiki, na damu chafu ilibaki mwilini bila kutiririka inje, na Muganga alipofika, hakuweza kumuokoa. 
Baada ya hayo, bwana Coolidge alipoteza na kukata tamaa yoyote ya kuishi. 
Tamaa yake hata yakufanya kazi ya Inchi ilipotea, ijapokuwa yeye alikuwa Prezidenti mwenye alikuwa anachapa kazi vizuri sana na kwa moyo wote kupita hata wa prezidenti walio mtangulia. 
Na wakati watu walipima kumsisimua ili awe tena kandideti katika mapambano ya kiti cha uraïsi wa Marekani, yeye alikataa na akasema hapana. 
Walipomuuliza kwa nini anakataa, akajibu kama Yeye hapendi. 
Lakini nyuma alipozungumuza na watu wake wa karibu, aliwaambia kwamba kukataa kwake kwa kugombea tena kiti cha uraïsi wa Marekani kunasababishwa na kifo cha kijana wake, kifu ile ilimuondowa hamu yote na sababu yote ya kuishi.  
Mungu Baba, yeye haiko wa hali, tabia na aina hii. 
Lakini nalinganisha na kutambua kwamba hata kwa Mungu Baba, ilikuwa huzuni sana kumutoa Mwana wake wa pekee kushuka hapa Duniani. 
Katika Injili ya Mutakatifu Yoane inaoneshwa wazi kwa mara makumi ine(40) kwamba Bwana Yesu alikuwa akipaza sauti akisema: “Mimi sikuja kwa shauri langu mimi pekee.” 
Mungu Baba ndiye aliye mtuma Bwana wetu Yesu Kristo. 
Mungu Baba aliona namna gani Mungu Mwana aliteswa, alikataliwa, na kuchukiwa, kutupiliwa na mwisho kuuwawa. 
Utakumbuka kama mbambo haya yote yalipitikana wakati alikuwa bado akifundisha na kutenda maishara hapa duniani na kwa muda huwo wote watu walikuwa wakitafuta kwa nguvu zao zote wamshike ili auwawe. 

5/ Hii ni Alama ya Mapendo. 

6/ Kitambo bado nilikuwa nikijiuliza kama katika Maandiko Matakatifu, yaani Biblia, neno Mapendo, ilitamkwa kwa mara ya kwanza nafasi gani. 
Sijuwi kama mumekwisha kusikia juu ya neno lenye watu wenye kujifunza teologia ama elimu ya Biblia na Kimungu, neno wanaloita Dalili na Masikilizano ya kwanza. 
Nikusema wakati wajuzi wa Biblia wanakuwa na haja ya kufahamu neno ama jambo fulani, wanatafuta katika Biblia kama, ni katika Kitabu gani, sura gani na aya gani neno hili lilitajwa kwa mara ya kwanza. Na kwa kweli shahiri ilo itapatikana. 
Neno Mapendo ilitajwa kwa mara ya kwanza katika Biblia ndani ya 

Mwanzo 22 : 2 
“Akasema: Twaa sasa mwana wako, mwana wako wa pekee ambaye unampenda, hata Isaka, uende zako hata inchi ya Moria; umtoe pale kwa sadaka ya kuteketezwa juu ya mmoja wa milima ambao nitakuambia.” 

 Ni kusema jameni, namna gani na kwa hali gani upendo ulitajwa? 
Ni namna gani upendo unatumikishwa katika maandiko haya? 
Mungu alisema: 

Twaa sasa mwana wako, mwana wako  wa pekee ambaye unampenda na kwa kweli, umtoe kwa sadaka ya kuteketezwa. 
Hii njo mwanzo wa Mapendo katika Biblia.   
Na ni mapendo gani? 
Ni mapendo ya baba kwa mtoto wake mume.  
Ni mapendo ya baba kwa mtoto wake mume ambaye alipashwa kumtoa kama sadaka. 
Kwa kusema kweli, hii ni mfano maalum ya picha ya Musalaba wa Kalvari, ni mfano kamili wa Kalvari. 
Katika Biblia Takatifu, ni Abrahamu pekee anaye kuwa mfano wa Baba anayemtoa mtoto wake mume kama sadaka ya kuteketezwa. 
Mungu aliambia Abrahamu: Twaa sasa mwana wako, mwana wako wa pekee ambaye unampenda. 
Abrahamu alikuwa na mtoto mwengine, Ismaeli, lakini Mungu alisema simutambue  na simjui. 
Twaa mwana wako wa pekee, Isaka, unayempenda, umtoe kwangu kama sadaka ya kuteketezwa. 
Ni hapo mwanzo wa mapendo katika Biblia.  

7/ Ni heri sana nyinyi mujuwe kwamba: 

Misumari waliopigilia katika mikono ya Mwokozi wetu, hiyo misumari ilipenya ndani ya Roho ya Mungu Baba. 
Mukuki iliyochomwa kwa ubavu wa Mwokozi wetu, mukuki huyo uliacha alama ndani ya mapendezi ya Baba.
Mungu Baba aliteswa pamoja na ndani ya Mungu Mwana. 

8/ Neno hili linakamatana na picha hii ya Mungu na Mdudu. 
Wakati nilikuwa nikifikiri juu ya taifa la wana wa Israeli, nilifikiri juu ya picha ingine inayokuwa kati ya Mungu na Taifa lile, 

Yeremia 20: 11 
“Lakini Bwana yuko pamoja nami, kama mpiga vita mwenye kuogopesha; kwa hivi wenye kunitesa watajikwaa, wala hawatashinda; wataona haya kubwa. Kwa sababu hawakutenda kwa akili, wataona haya ya milele, isiyoweza kusahauliwa kamwe.”  
Utafsiri maalum wa aya hii ni: 

MWOKOZI WANGU YUKO PAMOJA NAMI KAMA SHUJAA MKUBWA MWENYE UWEZO, NANI ANAYE WOGA?  
Na ninawaza kweli kwamba hiyo ndiyo tafsiri bora inayo maanisha shairi hilo. 
Shairi hilo inaonesha picha ya kijana mdogo mwanaume mwenye alikuwa anasumbuliwa sana na kuteswa vibaya akigombanishwa na jirani kijana mwengine mukubwa kuliko yeye. Huyo kijana mdogo akawa mwenye woga kiasi na kutetemeka mara kwa mara mpaka kuwa na woga wa kutoka nyumbani na kwenda kucheza inje, sababu kila wakati na dakika alikuwa na woga asije akapigwe vikali na wale vijana jirani wakubwa. 
Sasa, siku moja, baba yake mzazi akaja mbele yake na kumwambia, mwana wangu twende pamoja kwa hiyo duka inayo kuwa pale kwa lukumba ya njia. Na kweli, kwenda kwa ile duka ni kupita katika ile njia kwenye wale vijana wanaume wakubwa kwake wanaomuogopesha na kumutetemesha wanazoezi ya kungoja na kusimama.  
Lakini kwa sasa kijana huu mdogo hana woga yoyote hata kidogo. Anakwenda njiani akitelemuka pamoja na baba yake anaye mushika kwa mukono wake. Kwa sasa yeye hana woga wowote, anawatizama washambulizi wake wakisimama kwa nafasi zao za kawaida, anawaona moja kwa moja lakini yeye haogopi kitu, sababu sasa yeye yuko pamoja na mutu anayeweza kumulinda na kumukinga, mutu mukubwa sana na shujaa, mwenye nguvu na nwenye uwezo kupita wale washambulizi na wachokozi wote na ni hii picha ndiyo tunayo katika hiyo shairi. 
Nabii Yeremia anasema: Lakini Bwana yuko pamoja nami kama Shujaa Muhodari Mukuu Mwenye nguvu. Mungu akiwa upande wangu, nani aliye juu yangu. 
Hakuna hata mchokozi mumoja mwenye anaweza simama mbele ya Shujaa Muhodari Mkuu Mwenye nguvu.  


9/ Ningelipendelea tuchikamane na maana ya maneno haya: 
Yeye asiyeachilia Mwana wake” 
Hii maneno ni ya muhimu sana kutambuwa na kuchunguza. 
Wengi wetu hawafikilie kutambuwa kwamba Mungu ni Mwenye haki na Mutakatifu kwa hiyo anapashwa kuhukumu zambi. 
Wanazani kama wanaweza ishi hapa ulimwenguni namna wanaotaka na hata ivyo Mungu anaweza akawaponye kwa kuwatupa kwa jehanamu. 
Shairi hili litatuonesha kwamba hiyo mawazo ni ya upumbafu. 
Kweli, nyinyi hamuja kuta musemwa ama neno “hakuachilia” katika Biblia Takatifu? 
Tusome 2 Petro 2: 4  
“Kwa maana ikiwa Mungu hakuachilia malaika wakati walipokosa, lakini aliwatupa shimoni, na kuwatia katika vifungo vya giza walindwe hata hukumu.”  
 Sawa sawa jinsi Mwenyezi Mungu hakuachilia malaika wake wakati walifanya zambi ndivyo vile Mwenyezi Mungu hata achilia hata mufanya zambi mmoja sababu yeye iko kiumbe kamilifu na kizuri kweli. 
Malaika wanakuwa na nguvu zaidi kuliko sisi, wanakuwa warembo zaidi kupita sisi, lakini wakati walipokosa Mungu aliwahukumu palepale bila kungojea, kwa hivyo tusipime kuzubaa na kuzania sababu wewe ni murembo, mukamilifu, mwenye nguvu za kimwili ama wewe unakuwa na nafasi nzuri mbele ya macho ya Mungu na uzubae kuwaza kwamba sababu ya hayo, Mungu atakuachilia hata ufanyapo zambi, kwa kweli Mungu hatakuachilia. 
Zambi inaleta laana, ni hivyo, ni laana tu njo zambi inaleta.  
Unaweza kuwa mutu wa neno, mfalme, unaweza kuwa raïsi, mutu wa serkali, mutu wa ma kampuni mbalimbali, mutu wa sayansi, hakuna hata kitu kinaweza sukuma Mungu aachilie  mutu atendae zambi asipite kwenye hukumu, sababu zambi inapashwa kuhukumiwa. 

10/ 2 Petro 2: 5  
“Wala hakuachilia ulimwengu wa kale, lakini alilinda Noa pamoja na wengine saba, mhubiri wa haki, wakati alipoleta garika juu ya ulimwengu wa wale wasioogopa Mungu;” 
 Hapo tunakuta tena msemwa huo: “hakuachilia” 
Tunajifunza hapo kuusu wao waliotenda zambi mbele ya wakati wa garika ya Noa.  
Tujiulize miyoyo ngapi iliangamia na garika? 
Ni vigumu kujuwa idadi ama jumla ya mioyo ya watu iliyo angamia na garika, lakini neno moja ya kweli ni kwamba watu wengi walipoteza maisha yao na garika kwa wakati ule. 
Kwa kweli fundisho maalum tunalopata hapa ni kwamba umati kubwa ama jumla kubwa la watu haukutuma Mwenyezi Mungu awaepushe na garika, 
Unaweza kupambazushwa na kudanganywa na umati kubwa wa watu wenye bado kumwamini Bwana Yesu; na kujiuliza: umati huo hauambie Mungu kitu? 
Umati mkubwa wa watu na idadi yao haitatuma Mwenyezi Mungu kuepusha hukumu juu ya zambi. 

11/ Pia  kwa aya ya sita(6) 
“Tena akahukumu miji ya Sodomo na Gomora akiipindua na kuifanya majivu, akaifanya iwe mfano kwao watakaokaa pasipo kuogopa Mungu.” 
 Hapo Mungu anataja na kuzungumuzia uharibifu wa Sodomo na Gomora. 
Hata kama Mtume Petro hakutumikisha msemwa “hakuachilia”, sawa na namna tuliona hapo juu, wazo inabaki tu ya namna moja. 
Hata moja ya miji hii miwili haikuachiliwa, Mungu aliponyesha tu Loti na mabinti zake wawili.  
Miji hii mbili ilipeperushwa na kupinduliwa sababu wakaaji walifanya zambi. 

12/ Katika Waroma 8: 32  
“Yeye asiyeachilia Mwana Wake, lakini alimtoa kwa ajili yetu yote, namna gani atakosa kutuletea vitu vyote pamoja naye? 
 Zambi ni tendo la kuhatarisha sana ni kwa hiyo, mbele ya zambi yoyote kutafuta kusamehewa ama mutenda zambi kusamehewa ili ahesabiwe mwenye haki, ilimupasa Bwana Yesu Kristo kufa Musalabani ili alipe malipo ya zambi na afe kwa nafasi ya huyo mutenda zambi. 

13/ Tuangalie namna sehemu ya pili ya aya hii inavyosema. 
Waroma 8: 32 
“…lakini alimtoa kwa ajili yetu yote.” 
Sasa unatambua msemwa: “alimtoa kwa” 
Nikusema kulikuwa na muda ambao Mungu Baba alimtoa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo.  
Alimtoa kwa. 
Alimwachilia sababu ya neno fulani. 
Aya hii haiseme kama Mungu Baba alitupatia Mungu Mwana.
Lakini Mungu Baba alimtoa kwetu. 
Na ninafahamu kwamba kama tukijikaza kujuwa, tutafahamu kwamba Mungu Baba alimtoa kwa kitu fulani, kwa ajili yetu,  na ni kwa njia hiyo ndiyo tutasikia na kufahamu aya hii. 
Kulikuwa na muda ambao Bwana Yesu Kristo alitolewa kwa MATESO

14/ Tupime kujifunza mambo yaliyo pitikana kunako Bustani ya Gethsemani. 
Nazani kwamba imetupasa kusoma na kufahamu historia hiyo, tusijali mara ngapi tumekwisha kulisoma. 
Ninauhakika kwamba kila wakati mutakalo isoma lazima mutapata kitu kipya kingine. 

Luka 22: 53  
“Kila siku nilipokuwa pamoja nanyi katika hekalu hamukunyosha mikono yenu juu yangu; lakini saa hii ni yenu, na mamlaka ya giza.” 
 Pale Gethsemane, Bwana wetu Yesu Kristo alikuwa katika uchungu sana, na alitetemeka kwa uchungu, nazani hiyo msemwa ndiyo   namna nzuri ninalo weza kupima kueleza nalo. 
Na kwa uchungu ule kubwa alipaza sauti akisema: Baba hakuna njia nyingine la kunywa kikombe hiki? 

Luka 22: 42 – 44 
“akasema: Baba, ukipenda, uniondolee kikombe hiki; lakini si mapenzi yangu yafanyike, ila mapenzi yako. 
Malaika toka mbingu alitokea, akampa nguvu. 
Naye alikuwa katika uchungu sana, akazidi kuomba kwa bidii; na jasho yake ilikuwa kama matone ya damu yanayoanguka kwa udongo.” 
 Kiisha alikuja kwa wanafunzi wake, akija kwa bustani ya Gethsemane na alianguka kifulifuli akitia uso chini na akaomba tena. 
Lakini hakukuwa tena jibu kutoka mbinguni kwa ajili ya maombi yale. 
Hii ndilo jambo nilikuwa napenda tuchunguze.   
Hakukukuwa tena jibu kutoka mbinguni juu ya maombi yale.
Alipoomba mara mbele ya hapo na hata akachoka kabisa, Malaika toka mbinguni alitokea akampa nguvu. 
Hakuwa tena na nguvu za kimutu ili aone hayo mapito katika hali ya kimwili. Ni kwa sababu ya hiyo njo Baba Mungu alimutumia Malaika toka mbinguni ili amutie nguvu, lakini hakukuwa jibu toka mbinguni juu ya ombi aliloomba. Kiisha akatoka kwenye bustani. 

Na Luka 22: 53 
“Kila siku nilipokuwa pamoja nanyi katika hekalu hamukunyosha mikono yenu juu yangu; lakini saa hii ni yenu, na mamlaka ya giza.” 
 Bwana Yesu alikutana na Yuda aliyekuwa akisindikizwa na waaskari, waandishi, mafarisayo na makuhani wote wakiwa na silaha za fimbo. 
Walikuwa wanashika silaha ili wamushike na kumufunga Bwana Yesu Kristo.
Bwana wetu Yesu Kristo aliwaambia kila siku nilipokuwa pamoja nanyi katika hekalu hamukunyosha mikono yenu juu yangu; lakini saa hii ni yenu, na mamlaka ya giza. 
Chunguza vema hii misemwa ifwatayo. 
Mamlaka ya giza  
Ni hapo Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo alitolewa kwa Mamlaka ya giza. 
Tangu hapo hakuwa hata na neno moja la musaada toka juu mbinguni. 
Juu ya Musalaba Yesu alilia: Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha? 
Kumbuka kwamba hapakuwako mutu yeyote aliyekuwa akimshika, lakini palikuwako nguvu za giza. 
Mbele ya hapo, malaika alikuja kumupa nguvu, lakini kwa Msalaba hapakukuwa msaada yoyote. 
Hakuna malaika aliye msaidiya pale kwa kalvari, hakuna malaika alie msaidia wakati alipokuwa katika mikono ya watesi wake.
Walimupiga makofi usoni, walimutemea mate. Na kwa kutemea mutu mate, yafaa uwe kabisa pembeni yake na kumusogelea sana. Walimukokota nywele kichwani wakati walipomupiga makofi. 
Walimufunga kipande cha nguo machoni na kumufungilia kwa nguzo na kumupiga mijereti. 

15/ Ni sawa ukipita katika njia ndogo kati ya pori kubwa yenye miti mikubwa na majani ya kufungana, na kwa gafla, mutu mwenye wazimu anarukaa mbele yako na silaha mikononi akikugeuzia silaha hizo.
Waweza kufahamu woga wa aina gani utakao kushika wakati utashituka na mtetemeko gani wa woga utalipuka na kukujaa? Ni hiyo hali ndiyo tunapata hapa. 

16/ Tuangalie namna misemwa iliundwa hapo katika shairi hii: 
Haikusemwa: 

Yeye atapashwa kutupatia vitu vyote bure. 
Lakini imesemwa: 
Namna gani atakosa kutuletea vitu vyote. 
Yeye alitupatia vyote. 
Namna gani yawezekanavyo sisi kufikiri kwamba Mwenyezi Mungu aliyefanya hivyo kwa kututolea Mwana wake, namna gani yawezekanavyo Yeye tena atuombe kitu chochote kile? 
Neno hili haliwezekani hata kidogo. 
Haiwezekani kwa Mungu kuwa na hitaji ya kitu kutoka kwetu, sababu Yeye alitutolea Mwana wake, Alitupatia VYOTE Alivyokuwa navyo. 
ALITOA VYOTE VYAKE.   

17/ Tuchunguze sasa kwa makini neno KWA BURE 
Kwa Kigriki, inatoka kwa neno DOE-RAY-ON. 
Inamaanisha Bila neno lolote, Bila malipo. 

Yoane 15: 25 
“Lakini litimie neno lililoandikwa katika torati yao: Walinichukia bure.” 

AMEN
 
N°Ref:  06/27/1965 / 299 - GOD AND THE WORM / 2020