Friday, October 29, 2021

NAMNA GANI SHETANI ANAPINGA UKWELI / HOW SATAN OPPOSES THE TRUTH

Photo by B Smith from the kitchen door



 


NAMNA GANI SHETANI ANAPINGA UKWELI 

HOW SATAN OPPOSES THE TRUTH

June 3, 1962 

Pastor Henry F. Kulp


 

1 Timoteo 4: 1 – 5

 

“Basi Roho anasema waziwazi ya kwamba katika nyakati za mwisho watu wengi watajitenga na imani, wakisikiliza roho za kudanganya, na mafundisho ya mashetani, 

Wakisema uongo kwa udanganyifu, wakichomwa moto zamiri zao wenyewe; 

Wakikataza watu kuoana, na wakiagiza watu wakatae vyakula Mungu alivyoumba kupokewa kwa kushukuru na walio na imani na kujua kweli, 

Kwa maana kila kiumbe cha Mungu ni kizuri, wala hakuna cha kukataliwa, kama kikipokewa kwa asante: 

Kwa sababu hivi kimetakaswa kwa Neno la Mungu na kwa kuomba.” 

Mtume Paulo anaonya kijana Timoteo kwamba Roho Mtakatifu anasema na kufundisha waziwazi. 

Hii ni jambo la muhimu linalopaswa kujulikana, na tunalopashwa kushika kwa makini sana. 

Je, ni jambo gani? 

Ya kwamba katika nyakati za mwisho watu wengi watakanusha Imani la kweli na watajitenga na imani. 

Neno kukana ama kukanusha ni tafsiri ya neno kuasi ama uasi. 


Ni kwamba, katika kanisa kutakuwa hidadi ya watu wenye kujitenga na imani itaongezeka zaidi, watakanusha imani safi, mbalimbali na vile inavyopaswa kukubaliwa katika Yesu Kristo. 


1/ Swali hili halihusu ulimwengu, kwa sababu tiyari ulimwengu ni adui wa Mwenyezi Mungu. 

Jambo hili linahusu wale walio watu wa dini, waamini wa desturi, katika kanisa la Yesu Kristo, sawa vile tunavyoliisha na kuyaona kwa nyakati za leo. 

Watu wanabeuwa na kuzarau Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo, na kwa nafasi yake wanatafutia dini maelekezo mengine. 

Dini yao inaweka musingi wake juu ya matendo mema, watu wanatafuta kwa nguvu zao wenyewe kujipendeza na kuwa wenye kustahili mbele ya macho ya Mungu. 

Na jumla mingi ya madini katika dunia inapigwa marufuku na jambo hili. 


2/ Ni kitu gani inayosababisha anguko hili katika maisha ya nyakati za leo kanisani? 

Watu wanapendelea roho ya kudanganya na mafundisho ya mashetani. 

Inamaanisha kwamba watu hawa wameanguka katika mtego, na mipango na miradi ya Shetani. 

Shetani hana uwezo wa kuwa pahali pote kwa kila dakika, bali anatumikisha mapepo wabaya ili watende kazi yake katika dunia. 

Ma pepo wake wabaya wanasukuma wale wakristu wa desturi katika kanisa la Yesu Kristo wajitowe kwa mazoezi ya kujielekeza kwenye kawaida ya mafundisho ya mashetani. 

Je, mashetani ama pepo wabaya wanafundisha nini? 

 

3/ Wanafundisha yafwatayo: 

Uwe mtu mzuri, tenda matendo mema, bali uzarau Damu ya Bwana Yesu Kristo. Usikubali kwamba njia ya wokovu ni katika Yesu Kristo pekee. 


4/ Tuchunguze sasa namna Shetani anatumika ndani ya watu, yeye mwenyewe ama kwa njia ya wapepo wake wachafu. 

Matendo ya Mitume 13: 6 - 7 

“Walipokwisha kupita katika kisanga chote, mpaka Pafo, wakaona mchawi, nabii la uwongo, Myuda, jina lake Bara Yesu. 

Huyu alikuwa pamoja na mtawala Sergio Paulo, mtu mwenye akili. 

Yeye aliita Barnaba na Saulo wafike kwake, akataka kusikia Neno la Mungu.” 

Hapa ni Saulo na Barnaba wakijielekeza na kupenya hadi ndani ya kisanga cha Seleukia, wakafika Pafo iliyokuwa muji mkuuu wa Serkali ya Kisanga hicho, mahali kulikopatikana mchawi mmoja aliyekuwa nabii la uwongo , myuda na jina lake lilikuwa Bara Yesu. 

Bara ayesu alikuwa muyuda mwenye aliyejiingiza kwao Mataifa, akijiweka kuwa mtu wa kutenda miujiza na maishara, na zaidi ya yote alikuwa akijifanya kuwa nabii. 

Alijipanga jina la Bara Yesu, neno Bara inamaanisha “mtoto wa”, nikusema Bara Yesu maana yake “mtoto wa Yesu”. 

Yeye alikuwa akisikiliza kwa makini ili ajitayarishe kwa kiini chake, akigeuza kweli yote na kujionyesha mbele ya watu akiwaambia kwamba yeye ni mtoto wa Yesu, na kwamba yeye anauwezo wa kutenda miujiza yote kama Yesu. 

Naye alikwenda katika hali hiyo, mbele ya Mtawala Sergio Paulo. 


Ni yeye aliyekuwa Liwali wa kisanga hicho, huyo mtu mupagani Sergio Paulo alikuwa mtu mwenye busara, na jambo lile lilionekana kwa sababu yeye aliwaita Paulo na Barnaba wafike kwake ili asikilize Maneno ya Mungu. 

Bali, Elima ama Bara Yesu, alitambua kwamba anaanza kupoteza mamlaka yake juu ya Sergio Paulo, ikiwa Sergio Paulo atafikia lengo la kuhubiriwa neno la kweli. 

Na hii ingesababisha hali yake kama mtu mubaya ijulikane waziwazi. 

Alijuwa kwamba uwezo wake juu ya Sergio Paulo unapambazuka na kupotea. 

Yeye aliwafahamu Paulo na Barnaba, kwa hiyo alitaka kumugeuza mtu huyo Sergio Paulo awe mbali na imani. 

Aya ya 8. 

“Lakini Elema;(kwani hii ni maana ya jina lake) alishindana nao, akitaka kugeuza yule mtawala aache imani.” 


5/ Lakini, Mtume Paulo, akijaa na Roho Mtakatifu, akamkazia macho akasema: Wewe mwenye kujaa hila na uovu wote, mwana(mtoto wa) wa Shetani, na hapa maana ya neno mwana siyo ile tunayo kwa kawaida, yeye ni mtoto wa Shetani kwa kumaanisha kwamba yale anayoyatenda, anayatenda kama mujumbe wa Shetani aliyetumwa kutimiza kazi za Shetani, akijaribu uerevu mbalimbali ili amugeuze huyu mtawala toka imani. 

Ni kwa hiyo Mtume Paulo alimwambia:

Wewe adui ya haki yote, huachi kupotoa njia za Bwana zenye kunyoloka? 

Twatambuawa sasa, mtu huyu, mwana wa Shetani alitaka kupotoa njia za Bwana zenye kunyoloka. 

 

Yeye alikuwa mtu wa dini, na kwa hiyo alitaka kumufundisha mtawala Sergio dini, hakutaka afahamu kweli kuhusu Yesu Kristo. 

Alikuwa akipotosha njia za Mungu zenye kunyoloka.

Na ni hii ndiyo miradi ya Ibilisi kwa kila wakati.

Yeye ni malaika wa jambo linaloonekana kuwa kama sheria ya haki. 

Wajumbe wao, mapepo wabaya wanawapeleka wanaume na wanawake watende matendo mazuri, wafikie matelekezo mema, wawe watu wa dini, lakini wazarau na kubeuwa Yesu Kristo, na Damu yake iliyotiririka. 


6/ Muturuhusu tuwaoneshe Andiko katika Agano la Kale lenye kutufahamisha makosa na upumbafu unao kumba mtu mwenye anategemea dini na mafundisho ya mashetani. 

Isaya 19: 1 

“Mzigo wa Misri. Tazama, Bwana anapanda juu ya wingu la upesi, na anafika Misri, na sanamu za Misri zinatikisika mbele ya uwezo wake, na moyo wa Misri unayeyuka katikati yake.” 

Nabii Isaya anazungumuza kuhusu wana wa Misri na miungu yao. Huyo mungu wao aliitwa mungu wa hasira, kisasi na uhakiki kwa kuchekelea maovu ya watu. 

Hii ndiyo iliyokuwa hali ya wana wa Misri na miungu zao. 

Neno “miungu” kwa kutumia, maana yake ya asili ni “asiyefaa kwa neno lolote.” 

Inayotafsiriwa kama “isiyo na samani yoyote” tafsiri hili twalipata katika kitabu cha Yobu 19: 4, 

Maandiko yale yangelisomeka kama ifwatavyo: 

 

Wasiofaa kwa neno wa Misri wao walio kuwa sawa wa mastaajabu, walikuwa wakijikongoja na wenye kushuka wakiwa wakitetemeka mbele ya uso wake. 

Inamaanisha ubatili wa kutegemea wale mapepo wabaya wakali pamoja na mafundisho yao ya mashetani. 


7/ Ni muhimu kwetu kujua kwamba Mwenyezi Mungu hataruhusu hali hii kudumu, na kuendelea, siku moja Yeye atarudi kwa kuhukumu wale waliokumbwa chini ya mamlaka ya mafundisho yale ya mapepo, wote waliojitoa kutangaza na kueneza popote kawaida ya mafundisho yale ya mashetani. 

Hesabu 33: 4 

“Wakati Wamisri walipokuwa wakizika wazaliwa wa kwanza wao wote, ambao BWANA alipiga katikati yao; BWANA akafanya hukumu juu ya miungu yao vilevile.” 

Ni ya muhimu kwetu kuchunguza kwa makini sana aya hii ya Hesabu 33: 4, wakati Mwenyezi Mungu aliruhusu Musa na Farao wapingane kwa kushindana kuonesha kila mtu uwezo wake, na kweli hadi hapo haikuwa bado hukumu ya Mungu juu ya Wamisri, bali Mungu alishusha hukumu juu ya miungu ya Wamisri. 

Wamisri walikuwa taifa ya dini, walikuwa na mazoezi ya mafundisho ya mashetani na wao walikuwa wakiabudu miungu mingi. 

Miungu yao kwa kweli yalikuwa mashetani na wakati Mwenyezi Mungu alishusha hukumu juu ya miungu yao ya mashetani, ilionekana wazi kwamba hukumu hizo zilishuka vilevile juu ya Wamisri. 

Kwa sababu tukichunguza yanayosemwa katika Aya hii ya Hesabu 33: 4, 

 

“Wakati Wamisri walipokuwa wakizika wazaliwa wa kwanza wao wote, ambao BWANA alipiga katikati yao; BWANA akafanya hukumu juu ya miungu yao vilevile.” 

Mwenyezi Mungu alishusha hukumu juu yao. 

Ni kwa sababu ya jambo hili ndilo maana twapaswa kujuwa kuhukumu na kuwatowa inje ya mashirika na zehebu zetu, wale wote wenye hawasadiki ukweli. 

Hatupashwi kuwaachilia wadumu katika njia mbaya. 


8/ Jambo lifwatalo tunalopenda kujifunza hapa ni kwamba: 

Watu hawa waliokuwa wakihubiri na kufundisha mafundisho ya mashetani, na kusikiliza roho za kudanganya walikuwa wakisema uwongo kwa udanganyifu, wakichoma moto zamiri zao wenyewe. 

Walijuwa kwa uhakika kwamba hawasemi kweli, walisema uwongo kwa udanganyifu, wakichoma moto zamiri zao wenyewe, kama roho iliyotiwa chapa kwa chuma yenye moto iliyo nyekundu; ikimaanisha kwamba hawa watu hawakuwa tena na zamiri safi. 

Ni jambo mbaya na la hatari sana kwetu kuamini zamiri zetu, kama isipokuwa tu zamiri inayoongozwa na Roho Mtakatifu. 

Watu wale hawakuwa tena na zamiri safi. 

Watu wanaokumbana na mafundisho yale, wao wenyewe hawayaamini, bali mafundisho yale yanaleta pesa na mali mengi. 

Kuna wafuasi wengi wanaopenda kufwata mafundisho yale na wanatoa pesa nyingi, na mchango ya mali yao yanakuwa ya hidadi kubwa kwa kuwaruhusu waendelee kuwa wanamemba wa mashirika yale. 


9/ Na kwa aya ya 3, Mtume Paulo anaonesha mifano miwili ya mafundisho wanaofundisha. 

 

Neno la kwanza ni kwamba wanakataza watu kuoana, na wanawaagiza watu wakatae vyakula Mungu alivyoumba. 

Mwatambuwa mara tena nini inayosuma mambo haya: 

Watu hawa wanafikia kiwango ya kujihesabu wenyewe kuwa wenye haki na kustahili kwa njia ya matendo wanayo yafanya. 

Kwa nyakati za sheria, kulikuwa chakula iliyokuwa ikikatazwa watu kula, lakini kwa sasa siyo vile. 


10/ Mutakumbuka na kufahamu ya kwamba kila kitu ni cha kupokea na asante. 

Mwenyezi Mungu anatamani sisi tuwe watu wa kushukuru kwa yote tunayo. Tukumbuke kwamba aya ya 4 inasema kwamba: 

“Kwa maana kila kiumbe cha Mungu ni kizuri, wala hakuna cha kukataliwa, kama kikipokewa kwa asante:” 

Kushukuru Mungu mbele ya kutumia chakula, ilikuwa desturi kwa siku zile. 

Bwana wetu Yesu Kristo alibariki hidadi chache ya mikate. 

Matayo 14: 19, Mtume Paulo alibariki na kuombea chakula katika merekebu. 

Matendo ya Mitume 27: 35 

“Alipokwisha kusema hivi, akatwaa mkate, akashukuru Mungu mbele yao yote, akauvunja, akaanza kula.” 

Yatupasa kuwa watu wa kushukuru, bali nazani kwamba hayatoshi tu kushukuru mbele ya kutumia chakula. 

Ni vema kuwa na nia ya kushukuru lakini yatupasa kusonga mbele zaidi. 

 

Twapaswa kushukuru katika miyoyo yetu kwa yale yote Mwenyezi Mungu aliyotutendea. 


11/ Kwa aya ya 7, twaona:

“Lakini ukatae hadizi za bure na za wanawake wazee. Nawe ujizobeleze 

katika utawa:”

Timoteo anaombwa kukataa hadizi za bure na za wanawake wazee. 

Kwa kweli hii inamaanisha neno za hadisi za kizushi ama uvumi, inamaanisha, desturi za kabila ama mila zetu. 

Tunaombwa kufanya angalisho na desturi za kabila ama mila zetu. 

Mara kwa mara mapepo wachafu wapitia katika mila zetu, desturi zenye kwa mara, watu waliunda wakiongozwa na mapepo wabaya. 

Watu wengi kwa nyakati hizo, walikuwa wakitembea na kuzunguuka zunguuka katika soko wakiandaa mikutano yenye ya kuteka nyara watu na kupotosha watu, kwa mitego na mila ni ni katika maandamano haya ndiyo walipata namna ya kuishi, bali maneno haya yalihigwa na waongozi wa makanisa na kuanza kufanyika hata ndani ya makanisa, ni kwa sababu hii, Timoteo anaombwa kujizobeleza utawa. 

Neno “kuzobelea” inatumiwa katika aya ya 7 na katika aya ya 8 pia. Aya ya 7 inasema: Nawe ujizobeleze katika utawa. 

Katika Aya ya 8 twasoma kwamba: “Kwa sababu kuzobelea kupata nguvu ya mwili ni faida ndogo.” 

Neno mazoezi ni china ya jina Ukumbi wa michezo ama mazoezi ya viungo, na yote hii inaambatana na mazoezi. 

Mtume Paulo hasemi kwamba kufanya mazoezi ya viungo vya mwili ni vibaya na kwamba haina faida yeyote. 

 

Mazoezi ya mwili inafaida ndogo tukiyalinganisha na mazoezi ya utawa. 

Mazoezi ya viungo inafaida iliyo na mipaka, lakini mazoezi ya utawa inafaida ya milele. 


12/ Tunaishi katika nyakati ambapo utamaduni wa mazoezi ya viungo vya mwili inavuma pande zote na inaonekana kwamba ni ya muhimu. 

Naamini vilevile kwamba mwili inayojengwa vema kupitia mazoezi ni kitu njema, bali, kama mukristo anajizoeza mwenyewe katika mazoezi ya kimwili (kandanda na michezo mbalimbali), zaidi ya namna anavyo jizobeleza katika mazoezi ya utawa, hii inakuwa na vinyume katika maisha yake ya utawa, na kwa mwisho atakwaa katika uvuguvugu. 

Na wazo hapa ni kwamba itafikia siku moja mwili wako wa maumbile utakufa, na uwekaji wote ulioufanya juu yake utakwenda kaburini. 

Haitakuwa na mafaa yeyote wewe uishi miaka 50 ama miaka 70 na kwa muda huu wote wewe haukupata saa ya kumutukuza Bwana Yesu Kristo. 

Itamufalia mtu nini kuishi hadi miaka 80 na kwamba katika muda huu wote yale aliyoyafanya na kuhudumia Bwana Yesu Kristo ni machache sana. 

Mawazo yake yote na shuguli zake zote zilikuwa tu kuhusu mwili wake akizani kwamba ni hivyo atafikia lengo la kuishi miaka mingi. 

Mtume Paulo hakuishi hadi uzee, kama tunavyowaza, lakini huduma yake ilikuwa ya kutosha na alitenda mambo kazaa kwa utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo. 


13/ Mwili unaojengwa na mazoezi pia unao kuwa na afya njema nijambo bora. 

Bali, iliyo ya muhimu na manufaa sana ni nafsi inayo afya njema. 


14/ Kuna miradi inayopangwa na Raïsi wa Inchi yetu(Amerika) kuhusu mazoezi ya mwili kwa vijana, na vijana wote wanaalikwa kwa sababu hidadi kubwa ya vijana miili yao inakuwa hafifu sana kwa kokosa mazoezi ya mwili, kwa hiyo kwa kweli miradi hii ni jambo njema kwa vijana. Mimi si kanushe jambo hili. 

Lakini, kwa kuruhusu Inchi yetu ishimame imara na yenye nguvu mbele za Inchi adui, Inchi yetu inahitaji mengi zaidi kuliko afya ya maumbile. 

Tunapashwa kuwa na mafikara yenye afya bora, ili tupambane na mambo yatakayokuja, yafaa kweli Inchi yetu iwe na afya njema ya kiroho, tusiwe viozo vya maovu na mabaya yote, na dini zenye kujaa hadizi zilizotungwa, bali tumuamini Bwana na Mwokozi Yesu Kristo. 

Hatuwezi kuogopa Serkali ya ukomunisti, Serkali ya ujamii, hata kuwaza kwamba yaweza kuwa na mamlaka juu yetu, kama makanisa Inchini mwetu yako na nguvu za kiroho katika mahubiri na mafundisho ya msingi wa kweli, 

Bali kuona kwamba tuko wavivu kiroho, miili ya vijana wetu yatapata faida ndogo kupitia mazoezi yale mwili. 

Oh, kama viongozi wa Taifa letu wangelifahamu ukweli huu. 


AMINA 


N°Ref: 06/03/1962 / 29 - HOW SATAN OPPOSES THE TRUTH / 10/29/2021