Wednesday, February 17, 2021

MAJIFUNZO KATIKA SHERIA Sehemu ya Tatu STUDIES IN LAW Part III

Photo by B Smith from Patio


 

 

MAJIFUNZO KATIKA SHERIA Sehemu ya Tatu 

STUDIES IN LAW Part III 

Pastor Henry F. Kulp 1976 



 

Waroma 5: 12 – 14 

“Hivi kama kwa mtu mmoja zambi iliingia ulimwenguni, na kufa kwa njia ya zambi; na hivi kufa kulikuja juu ya watu wote, kwa sababu wote wamefanya zambi: - maana mbele ya sheria zambi ilikuwa ulimwenguni; lakini zambi haihesabiwi wakati sheria isipokuwa. 

Lakini kufa kulitawala tangu Adamu mpaka Musa, hata juu ya watu wasiofanya zambi kama alivyofanya Adamu, aliye mfano wake yeye atakayekuja.” 

Tunapata hapa watu wawili: Adamu na Musa. 

Kwa aya ya kumi na mbili tunapata ulimwengu wa zambi(zambi kutawala wote ulimwenguni) na ulimwengu wa kufa(kufa kutawala wote ulimwenguni). 

“Kwa njia ya mtu mmoja zambi iliingia ulimwenguni na kwa njia ya zambi ya yule mtu mmoja watu wote walifanya zambi na watu wote wanakufa.” 

Tunafikia sasa kwa jambo la muhimu sana inalomupasa kila mtu kufahamu. 

Kwa sababu gani wewe ni mwenye zambi? 

Kwa sababu gani mimi ni mwenye zambi? 

Sababu gani inasemwa kwamba: 

“Wote wamefanya zambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu?” 

Yanayosemwa ndani ya Waroma 3: 23 

Hayahusu zambi ilizozifanya na mtu yeye peke binafsi, hapa inahusu  zambi ya asili. 

Yatupasa kufahamu kwamba: 

Kila mmoja wetu alifanya zambi wakati Adamu alipo anguka na kufanya zambi. 

Adamu aliangusha uzao wa wanadamu wote ndani ya zambi. 

Wakati alipofanya zambi, mimi na wewe tulifanya zambi. 

Yeye ni baba, kichwa cha uzao cha wanadamu wote. 

Tunaita haya Matunzaji ya uwakilishi

Sote tulifanya zambi ndani ya Adamu. 

Pale pale mmoja wetu anaweza kusema ya kwamba: 

“Nazani hiyo siyo halali, namna gani mimi naweza kuwa mwenye zambi kwa sababu Adamu alitenda zambi?” 

Ni hasara kubwa sababu yale unayokuwa nayo kama mawazo ni kupingana na Mwenyezi Mungu. 

Mwenyezi Mungu anasema kwamba sote tulifanya zambi ndani ya Adamu. 

Jameni, niwasomee tena Aya ya 12: 

“Hivi, kama kwa mtu mmoja(aliye baba wa uzao wa wanadamu wote) zambi iliingia ulimwenguni, na kufa kwa njia ya zambi; na hivi kufa kulikuja juu ya watu wote, kwa sababu wote wamefanya zambi:-“ 

Maandiko haya yatasomeka ifwatavyo: 

“Kwa maana wote wamefanya zambi” hii ndio utafsiri wa Kigriki, “wote wamefanya zambi”, siyo “wote walifanya zambi.” 

Hapa haihusu zambi kila mmoja wetu aliyoyafanya kwa binafsi, hii inahusu zambi ya asili. 

Wote wamefanya zambi wakati Adamu alifanya zambi. 

Zambi ya Adamu ilikuja juu yetu sisi sote, ni kwa sababu hiyo, sisi tunakufa.  

Kama ingaliwezekana wewe bado kutenda zambi, hata  tu zambi moja, fahamu kwamba hata hivyo wewe ni mwenye zambi tu. 

Wewe ni mwenye zambi kweli.

 Aya ya 13 ni ya muhimu sana kwetu: 

“maana mbele ya sheria zambi ilikuwa ulimwenguni ; lakini zambi haihesabiwi wakati sheria isipokuwa.” 

Maana mbele ya sheria zambi ilikuwa ulimwenguni, hiyo inamaanisha nini? 

“Maana mbele ya sheria” 

Mtume Paulo anahitaji kusema nini? 

Anatuambia kuhusu Torati ama Sheria ya Musa, miaka 2500 tangu Adamu mpaka kufikia Musa. 

Kwa kufwatana na mpangilio ya nyakati, Tangu Adamu mpaka Musa “zambi ilikuwa ulimwenguni”, hapa inahusu zambi ya kila mtu binafsi. 

Wote wamefanya zambi ndani ya Adamu, bali “zambi ilikuwa ulimwenguni tangu Adamu mpaka Musa.” 

Tangu Adamu mpaka Abrahamu, hapa tunapata kikundi cha Mataifa wenye zambi. Tuna Taifa moja na luga moja. 

Miradi ya Kiyuda inazaliwa tangu Abrahamu hadi Musa. Taifa moja na luga moja. Hapo Mataifa mengine Wapagani walikuwa na lugha mbalimbali. 

Walisambazwa na wakapewa lugha mbalimbali. 

Kwa hiyo mwafahamu kwamba tangu Adamu hadi Musa, tulikuwa na eneo mbili tofauti: 

Kulikuwa Kundi la Mataifa wote Wapagani waliokuwa Taifa Moja wakiwa na lugha moja. 

Kwa ngambo ingine  tangu Adamu mpaka Musa, kulikuwa Taifa moja ikiwa na lugha moja iliyo ya Kihebrania. 

Katika muda wote wa nyakati hii hakukukuweko Torati ya Musa. 

Jameni, kuna kasoro moja watu wengi wanafanya wakitumbukia ndani ya kosa kwa sababu wao hawafahamu kwamba katika Biblia Takatifu kunapatikana sheria mbalimbali.  

Washika Sabato, wa Mormoni, wakati wanasema juu ya sheria, wao wanazania kwamba ni “Sheria ya Musa.” 

Hiyo siyo ukweli. 

Waraka wa Waroma inakuwa na aina tano ya sheria. 

Tusome kiatabu cha Waroma 8: 2 

“Kwa sababu sheria ya Roho ya Uzima ulio katika Yesu Kristo imenifanya huru kwa sheria ya zambi na kufa.” 

Jameni, muniruhusu niwafahamishe sheria gani ilikua ikitumika kwa nyakati ya kutoka tangu Adamu mpaka Musa.  

Kulikuwa sheria yenye ilikuwa ikitumika katika wakati  huo.

Tusome tena kwa makini sana Andiko hili la Waroma 8: 2  


Waroma 8: 2 

“Kwa sababu sheria ya Roho ya Uzima ulio katika Yesu Kristo ilinifanya namna gani? 

Imenifanya kuwa huru, huru kwa nini? Kwa sheria. Sheria gani? Sheria ya zambi na kufa.” 

Kulikuwa sheria yenye ilikuwa inatumika wakati huo na sheria hiyo ilikuwa mbalimbali na Torati ya Musa. 

Toka Adamu mpaka Musa, kulikuwa sheria iliyokuwa inatumika, ni sheria ya zambi na kufa. 

Ni wakati gani sheria hii ya zambi na kufa ilipoanza? 

Turudi katika Kitabu cha Mwanzo, wakati Mwenyezi Mungu alikuwa anazungumuza na Adamu. 

“kama utakula kwa muti wa kujua mema na mabaya, siku ile utakalokula utakufa.” 

Adamu alitwaa tunda la muti ule na kula na Adamu akakufa kiroho na nyuma ya miaka mia kenda, Adamu akakufa pia kimwili. 

Mwenyezi Mungu hakumuumba Adamu ili afe. 

Ni kwa saa ile ile lenye Adamu alikula tunda lile, ni kwa saa ile ile ndiyo sheria ya zambi na kufa ilianza kutenda kazi yake, watu wote wakafa, ila Enoki peke yake ndiye aliyenyakuliwa. 

Sheria ya zambi na kufa ilikuwa ikitenda kazi tangu Adamu mpaka Musa, na hata hivi, sheria hiyo inaendelea kutumika tangu Musa hadi siku za leo.    

Kila yule anayezaliwa hapa chini ya jua, anazaliwa ili siku moja afariki.

Wakati wa kuzaliwa kwa mtoto mchanga, anatoa sauti ya kulia, na ni pale pale anaanza safari yake ya kuelekea kufa. 

Sheria ya zambi na kufa.

Mtume anapenda kusema nini hapa? 

Turudi katika Maandiko yetu ya Waroma 5: 13 

“maana mbele ya sheria(Torati ya Musa) zambi ilikuwa(wapi?) ulimwenguni.” 

Tuchunguze yanayosemwa katika Aya ya 14 

“Lakini(nini?) kufa kulitawala tangu Adamu mpaka Musa” 

Kufa kulikuwa mfalme, mwatambua hiyo? 

Kufa kulikuwa kukitawala, kufa kulikaa katika kiti chake cha enzi. 

Wakati tutafika kwa sehemu za mwisho wa majifunzo yetu, nitawaonesha aina ine ya wafalme  tuyopata katika Waroma sura 5, mwawajuwa wale wafalme? 

Wafalme wane wanaomiliki. 

Hapo tunaona kufa inayomiliki. 

Kufa inatawala tangu Adamu mpaka Musa, kwa sababu sheria ya zambi na kufa ndiyo yenye ilikuwa inafanya kazi. 

Sasa turudi kwa aya ya 13 na tujaribu kufahamu nini Mwenyezi Mungu anayosema hapo. 

maana mbele ya sheria zambi ilikuwa ulimwenguni; lakini zambi haihesabiwi wakati sheria isipokuwa.”

Kumbukeni yale tuliyoyasema kuhusu maana ya neno “kuandikiwa juu ya mtu fulani, ama kuhesabiliwa juu ya mtu fulani.” 

“haikuwa inahesabiliwa juu yao”, sawa sawa na namna inavyosemwa katika Filemono : 18, wakati Mtume Paulo anasema: 

“na kama amekukosea, au kuwa na deni, uandike hii juu yangu.” Kwa kumaanisha kwamba, “usiihesabu juu yake,” 

Hiyo inamaanisha nini? 

Sheria ya zambi na kufa ilikua ikitawala, watu walikuwa wakitenda zambi ya upekee. 

Kaina alimuua Abeli. 

Vurugu ilikuwa duniani katika siku za Noa.

Sasa, ni nini analohitaji kutufahamisha? 

zambi haikuhesabiliwa, nikusema zambi za kila mtu binafsi hazikuwekwa juu yake” 

Nazani sasa hapo tuna Utunzaji wenye kila mmoja wetu anayofahamu. 

Wakati Bwana Yesu Kristo alipokufa, Yeye hakufa tu juu ya zambi zako za kibinafsi, angelifanya hivyo, haingelikuwa na manufaa yoyote, 

Bwana Yesu Kristo alikufa kwa ajili ya zambi zako za asili ulizoriti toka Adamu. 

Ni jambo hili ndilo wengi wa watu hawatambuwi.  

Utaona Mwinjilisti anahubiri dakika 50 juu ya zambi na anahubiri dakika 3 juu ya Yesu Kristo.  

Bila shaka, zambi iko, lakini kiini ya neno hapa siyo jambo la zambi za mtu binafsi,  sababu ni zambi ya asili ndiyo inayokuwa chemichemi ya zambi ya mtu binafsi. 

Ni nini inayo nisukuma mimi kufanya zambi? 

Ni kwa sababu ndani mwangu munamo chanjo ya mbegu ya zambi. 

Ni kwa hiyo, Mtume Paulo anasema ndani ya Waroma 7:15 

“Maana sijui ninalofanya, kwa sababu lile ninalopenda kufanya, silifanyi; lakini lile ninalochukia, ninalifanya.” 

Kuna kitu ndani mwangu: 

Nina utu wa zamani wenye asili ya zambi nilioriti toka Adamu

Adamu alifanya zambi, nami nilifanya zambi pamoja naye, na aliniachia asili yake ya zambi, Asili ya Adamu. Na mwafahamu ni nini iliotukia:  

Ilimupasa Bwana Yesu Kristo akufe kwa ajili ya zambi hiyo.

Kwa hivyo twafahamu nini? 

Hadi kuifikia Torati ya Musa, sheria ya zambi na kufa ilikuwa ikitumika na kila mtu alikua na asili ya Adamu, na sote tulikuwa tukifa kiroho na kimwili

Yeyote yule aliyezaliwa ulimwenguni, alikuwa mfu kiroho. 

Mushike sana yafwatayo: 

Hiyo haikuwa inamaanisha tu kifo ya kimwili, bali pia kifo ya kiroho. 

Sote tunazaliwa tukiwa wafu. 

Kaina na Abeli walizaliwa wakiwa wafu  kiroho. 

Seti alizaliwa akiwa mufu kiroho, Abrahamu, Musa, Yakobo walizaliwa wakiwa wafu kiroho, na walihitaji wokovu. 

Walipata wokovu wao kwa njia ya sadaka ya kuchinjwa. 

Waliweka imani yao ndani ya damu iliyomwangika toka sadaka ya kuchinjwa. 

Tunaambiwa hapa kwamba, hadi kufikia Torati ya Musa, Mwenyezi Mungu hakuwahesabia zambi walizozifanya kila mtu binafsi. 

Wao walikuwa wafu  kiroho na walifikia kufa vile vile kimwili sababu ya zambi walizoriti toka Adamu. 

Sababu gani Sheria ililetwa kwa watu? 

Ujiuluze sasa ulizo lile. 

Sababu gani Mwenyezi Mungu aliwapatia watu Torati za Musa? 

Tuchunguze hiyo kwa mwangaza wa Maandiko Matakatifu. 

Kwa kufahamu mafaa ya sheria, tusome Waroma 5: 20  

“Lakini sheria iliingia, ili zambi ziwe kubwa sana; lakini pahali zambi zilipozidi, neema ilizidi zaidi sana;” 

Sheria iliingia kusudi zambi za kila mtu zihukumiwe. Ni kwa sababu hiyo  njo maana Amri kumi ilipewa kwa watu. 

Amri kumi iwe kingo la kukuzuiza na kukuwezesha kuwa na kiasi katika matendo yako maishani mwote. 

 Kila mmoja wetu anayekuwa na zamiri safi anafahamu ya kwamba ni vigumu sana kutii Amri zote kumi kwa jumla, bila kuvunja hata moja. 

Amri kumi ilitolewa ili zambi za kila mmoja wetu ziwekwe wazi hazarani. 

Tusome Waroma 3: 19 

“Na tunajua ya kama maneno gani inayosema sheria, inasema kwa walio chini ya sheria; kusudi kila kinywa kifungwe, na ulimwengu wote uwe chini ya hukumu ya Mungu.”  

Kwa sababu gani Mwenyezi Mungu aliwapa wana wa Israeli Sheria? 

Ilikuwa tu kwa Israeli peke yake? HAPANA. 

Kusudi kila mtu awe chini ya hukumu mbele ya Mungu

Mwaona, Mwenyezi Mungu ni Mwenye Haki na Mukamilifu. 

Hakukukuweko sheria, Amri kumi za Mungu, Sabbato, wakati Mwenyezi Mungu aliwasiliana na watu kwa wakati wa tangu Adamu mpaka Musa, Mungu alisema:

“Kwa kweli mutakufa kimwili na kiroho, na mutakufa kimwili kufwatana na Adamu, na pendekezo, na matetezi ya watu hapa duniani haita badirisha, hata neno lolote.” 

Wote wanakufa ndani ya Adamu; 

Wote ni wafu wa kiroho ndani ya Adamu na walizaliwa katika hali hiyo. 

Bali, tangu Adamu mpaka Musa, Mwenyezi Mungu akasema: Sitawahesabia zambi zao za kibinafsi, nitahesabu tu zambi yao ya asili. 

Lakini wakati sheria ilipoingia, 

Sheria ilikuja kuonesha watu wote kwamba wao walikuwa wenye zambi. 

Kuonesha watu wote kwamba wanahitaji Neema ya Mungu. 

Kuonesha watu wote kwamba mbali na Yesu Kristo, hawana matumaini ingine. 

Yote ni kwa njia ya Neema kupitia imani ndani YAKE. 

Ndugu zangu, sheria iliingia ili wote wawe wenye kuhukumiwa. 

 Tusome Wagalatia 3: 24 

“Vivyo torati ilikuwa mwalimu wa kutuleta(kutuleta ni neno moja la muhimu sana, kuleta wanani? Mataifa Wapagani? Hapana, Wayuda) kwa Kristo, tupewe haki(namna gani na kwa jia gani?) kwa imani.”  

Siyo kwa matendo ya watu, kutahiriwa si kitu. 

Kuweka kando matendo yote ya watu: kutahiriwa ikiwa tendo la kuondosha sehemu ya mwili na kuitupa inje. 

Ndugu yangu, yatupasa kufahamu kwamba sisi tuko ginsi tulivyo kwa sababu ya Adamu, na kama hauamini hivyo, wewe unakanusha Biblia, hausadiki Biblia. 

Tuko namna tulivyo kwa sababu ya Adamu. 

Sisi hatuko wenye zambi sababu tulifanya zambi, bali, tuko wenye zambi sababu sote tulifanya zambi ndani ya Adamu, na ni kwa hiyo ndiyo maana tunatenda zambi kwa sababu sisi ni wenye zambi. 

“Sote ndani ya Adamu tunakufa” 

Kwa siku za leo, Mwenyezi Mungu anahesabia kila zambi kila mtu anayotenda kwa binafsi. 

Sote, yawezekana kuna mara tulitenda zambi. 

Kwa sababu gani Kaina hakupata hukumu ya kifo? 

Sawa vile tulivyoona siku iliyopita, ni tangu agizo la Mwanzo 9, hadi siku za leo hukumu ya kufa inaendelea  KUTUMIKISHWA

Kila Inchi yenye haitumie hukumu ya kufa, nazani hukumu ya Mungu iko juu ya inchi ile. 

Kiini cha Inchi yetu kuwa kama vile munavyoiona leo, ni kwa sababu haitumie hukumu ya kufa. 

Tuchunguze na kuangalia inchi zenye zinatumia hukumu ya kufa. 

Tuangalie mambo iliyofikia Ungereza. 

Ungereza ulianza pata anguko kweli wakati ulizidi sana kutumia kupita kiasi hukumu ya kufa. 

Hiyo ni kuzarau na kuto kuheshimu Mungu: 

“Yeye anayemwanga damu ya mtu, kwa mtu vilevile damu yake itamwangwa; kwa sababu alifanya mtu kwa sura ya Mungu.” 

Tunayo sasa sheria yenye haikupewa kwetu sisi, bali, sharia iliingia ili ioneshe wazi zambi za kila mtu ili vinywa vyote vifungwe na sote tuhukumiwe mbele za Mungu. 

Sisi sote tuko wenye zambi. 

Inayotupasa kufanya ni kujiangalia ndani ya sheria kama kioo na kuweka ndani vichwa vyetu na kweli kwa mweisho tujikuta uchi na kupata haya, sababu hakuna kitu njema tunayofanya. 

Ni kwa hiyo imesemwa kwamba: 

“Haki yetu yote ni kama (kama nini?)  vipande vichafu vya vitambaa.” 

Sote, ndani ya Adamu tunakufa, na kwa siku za leo, zambi zetu za kila mmoja kwa binafsi zinahesabiwa. Zinawekwa juu yake. 

Bali zambi hizo hazihesabiwi tena kwetu baada ya nini? 

Baada ya kumwamini Bwana Yesu Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yetu.    

Tuisome tena kwa ushujaa wote. 

Tusome tena ndani ya Waroma 5. 

Mtume Paulo anayasema kwa utaratibu na kwa hali sambamba, sawa vile nilivyowaambia juma iliyopita kwamba kutaka kwangu ni kwamba ingelikuwa heri kila mmoja aketi na kushiriki kwa  muda wa saa tatu kila mara katika  majifunzo hii, kweli ni yenye kuleta mchoko bali ni furaha sana kufahamu mawazo ya Mungu katika maandiko haya. 

Waroma 5: 14 

“Lakini kufa kulitawala tangu Adamu mpaka Musa, hata juu ya watu wasiofanya zambi kama aliyofanya Adamu, aliye mfano wake yeye atakayekuja.”  

(Neno lile “yeye” ina maana nyingi sana, lakini kwa leo hatutakuwa na muda kwa mambo yale, ningelitamani kuya fafanua bali muda ni mdogo sana.) 

15. Lakini zawadi ya neema haikuwa kama lile kosa. 

Kwa maana kwa kosa la mtu mmoja wengi walikufa, zaidi sana neema ya Mungu, na zawadi kwa njia ya neema ya mtu mmoja, Yesu Kristo, imezidi kwa watu wengi.”   

Shangwe kubwa gani! 

Yesu Kristo ndiye Jibu, Adamu wa mwisho, Mtu wa pili. 

Yeye alikufa na kuweka kando laumu yetu. 

Asili ya zambi ilikufa kwa njia ya Kufa kwa Yesu Kristo, na ni kwa njia hiyo ndiyo analipa zambi za kila mmoja wetu binafsi, akizivuta zote na kuziondosha kweli, na tunafanywa kuwa wenye haki wa Mungu katika Mpendwa wetu.   

Acheni sasa niwaoneshe jambo moja katika Aya ya 14

Waroma 5: 14 

“Lakini kufa kulitawala tangu Adamu mpaka Musa, hata juu ya watu wasiofanya zambi kama alivyofanya Adamu, aliye mfano wake yeye atakayekuja.”  

Twende kwa aya ya 21 na tuvumbue aina ya wafalme wanao miliki na kutawala. 

Waroma 5: 21  

“hata, kama vile zambi ilivyotawala katika kufa, hivi kwa njia ya haki neema itawale hata uzima wa milele kwa Yesu Kristo Bwana wetu.”  

Kama vile (nini) zambi ilivyotawala, kufa kuko kunatawala (hayo mambo inasemwa katika nyakati zilizo pita), angalia namna inavyosemwa kwa aya ya 14: “Lakini kufa kulitawala.”(Nyakati iliyopita)  

Tushuke hapo chini kwa aya ya 21. 

“hata, kama vile zambi ilivyotawala katika kufa, hivi kwa njia ya haki (nini?) neema itawale hata uzima wa milele kwa Yesu Kristo Bwana wetu.”  

Tunapata kufa kunatawala, zambi inatawala na neema inatawala.

Turuke hadi aya ya 17. 

Waroma 5: 17 

“Kwa maana kama, kwa njia ya kosa la mtu mmoja, kufa kulitawala kwa ajili ya mtu mmoja, zaidi sana wao wanaopokea neema ya kuzidi sana na zawadi ya haki watatawala katika uzima kwa yule mmoja, Yesu Kristo.” 

Kwa maana kama, kwa njia ya kosa la mtu mmoja, kufa kulitawala(hapo tunapata tena tendo kutawala), kwa njia ya mtu mmoja, 

zaidi sana wao wanaopokea (nini) neema ya kuzidi sana na zawadi ya haki watatawala katika uzima kwa yule mmoja, Yesu Kristo. 

Hapa tunaona mwamini anatawala, kufa kunatawala, zambi inatawala, neema inatawala na mwamini anatawala. 

Wafalme wane: 

Kufa kulikuwa mfalme, zambi ilikuwa mfalme, kwa sasa neema ni mfalme na mukristo ni mfalme

Wote wanatawala kwa sababu kwa njia ya Mtu mmoja Yesu Kristo, kazi ya mtu mmoja Adamu ilibomolewa. 

Ni raha kubwa gani kumjua Yesu Kristo. 

Ndugu mpendwa haiwezikani tena wewe kutia Imani yako katika kitu fulani, ama kuamini mtu mwengine, amini tu Bwana YESU KRISTO. 

AMINA. 

N°Ref: 1976 / 005 - STUDIES IN LAW Part III / 02/17/2021

MAJIFUNZO KATIKA SHERIA Sehemu ya Pili / STUDIES IN LAW Part II

Photo by B Smith from the Patio


 


MAJIFUNZO KATIKA SHERIA 

Sehemu ya Pili 

STUDIES IN LAW Part II  

Pastor Henry F. Kulp (Summer of 1976) 

 


 

Maandiko haya ni ya muhimu na ya manufaa sana katika Biblia, na mimi  ninaamini kwamba imetupasa kufahamu maana ya maandiko haya, na kama sivyo, hatuwezi kuwa na ufahamu timamu ya yale yanayosemwa katika Biblia nzima. 

Yafaa kuhakikisha kweli kwamba tunafahamu yanayosemwa katika Maandiko ya Waroma 5: 12 – 14.

Muniruhusu sasa niwasomee Maandiko haya na urembo wake wote.

Waroma 5: 12 – 14

“Hivi kama kwa mtu mmoja zambi iliingia ulimwenguni, na kufa kwa njia ya zambi; na hivi kufa kulikuja juu ya watu wote, kwa sababu wote wamefanya zambi: - maana mbele ya sheria zambi ilikuwa ulimwenguni; lakini zambi haihesabiwi wakati sheria isipokuwa. 

Lakini kufa kulitawala tangu Adamu mpaka Musa, hata juu ya watu wasiofanya zambi kama alivyofanya Adamu, aliye mfano wake yeye atakayekuja.” 

Inatupasa kufahamu Maandiko haya. 

Mchana kutwa, nilikuwa nikiomba Mwenyezi Mungu ili anipe ujuzi. 

Ninatamani ninyi wote mushiriki hapa kwa saa tatu ama ine sawa vile Mungu atatuwezesha kujifunza maandiko yetu ya leo kwa mupululizo. 

Sababu shali ni kwamba, mara nyingi tunajifunza tu kwa dakika 35 ama 45 na baadaye tunapata pumziko, na wakati tunarudi toka mapumziko, wandugu wengine wenye hawakuwa kwa sehemu ya kwanza, nawo vilevile wanaingia. 

Tukumbushe majifunzo yetu ya kwamba kuna Taasisi ine iliyo simikwa na Mwenyezi Mungu, yenye ilitupasa kufahamu na ya kwanza ni nini? 

MAPENZI, ya mwisho ni UTAIFA. 

Hizo Taasisi ine ni za manufaa mengi katika miradi ya Mwenyezi Mungu. 

Kila mtu yeyote ana Mapenzi. 

Ya Pili, 

Kati Bustani la Edeni, Mwenyezi Mungu alimukabizi mtu Mapenzi, kiisha alimupa muke na pale pale ndoa ikaanzishwa katika Bustani la Edeni. 

Kiisha hapo, kukakuwa jamii. 

Mungu aliamuru jamii iwe kwa ajili ya kuwakinga watoto. 

Watoto wanapashwa kuwa na waangalizi, wanapashwa kuwa na wale wanaowalea, wao wanao walisha, na wanaolisha watoto ni baba na mama. 

Na kwa mwisho, tuna UTAIFA. 

Kwa sababu gani Mwenyezi Mungu aliumba Taifa mbalimbali? 

Katika Gazeti”Kioo ya Altoona Usiku”, waliandika kuhusu kikundi kimoja kinacho hitaji kuwa na lugha moja, kabila moja. Je mumeisha soma sehemu hiyo? 

Kuwa na Kabila moja na lugha moja, wao kweli wanapotoka, sivyo? 

Mungu aliamuru lugha mbalimbali ziwe na hali hiyo itadumu tu hivyo hadi Mungu Mwenyewe aamuru tena kwamba iwe moja. 

Lugha mbalimbali iliamuriwa kwa kiini fulani. 

Mungu anataka ziwe Taifa mbalimbali na kwa Mapenzi yake aliamuru eneo na mahali na nafasi gani Ujermani itapatikana, Ostralia, Inchi yetu, Kanada, ma Inchi za Amerika ya mangaribi, Meksiko, Afrika. 

Aliamuru Inchi zile ziwe na kuziweka kwa eneo na mahali kwenye Yeye Mwenyewe alipendenzwa ziwe hapo. 

Aliamuru mipaka yao, eneo na mahali pao pa kuishi, nyumba zao, sawasawa na Maandiko ya Matendo ya Mitume 17.  

Kuona kwamba tumekwisha fanya kumbukumbu ya Taasisi ine yenye Mwenyezi Mungu aliamuru, turudi sasa kwa Maandiko yetu katika    Waroma 5: 12 -14, mahali Mwenyezi Mungu anatuambia kwamba tuna Taasisi lingine moja lenye Mungu aliamuru lakini bado kuanzishwa. 

Ni mshangao: 

Taifa zina sheria mbali mbali tangu Adamu mpaka Garika, na tangu Garika hadi Musa. 

Sasa, wakati gani Taifa lilianzishwa? 

Ni wakati wa Munara ya Babeli

Serkali lilianzishwa wakati gani? 

Wakati wa Noa, kiisha Garika. 

Kwa kweli, kwa wakati huo mutatambua kwamba sheria ya wanadamu ilikuwa bado haijashimikwa.  

Hiyo ni sheria gani? 

Hiyo ni Sheria ya MUSA. 

Tujifunze sasa neno hili kwa makini sana ili tupate kujuwa mapatano gani sisi tunayo na Sheria ya MUSA. 

Vile vile tufahamu nini watu walikuwa wakizani kuhusu mapatano kati yetu na Sheria ya MUSA. 

Tusome Waroma 5: 12, tukitia mkazo katika neno hili.

“Hivi, kama kwa mtu mmoja zambi iliingia ulimwenguni, na kufa kwa njia ya zambi; na hivi kufa kulikuja juu ya watu wote, kwa sababu wote wamefanya zambi.” 

Hivi, kama kwa mtu mmoja, neno gani inayofwata? ZAMBI

Hapo hapo, tunajiuliza ulizo hili: 

ZAMBI ni nini? 

Zambi inaufafanuzi nyingi, sawa nilivyowafundisha katika mahubiri ya siku iliyopita. 

Zambi ni : - Uvunjaji / Makosa

    • -Ukosefu wa alama fulani, wa hali fulani.

Hivi ukajumulisha ufafanuzi wote wa neno zambi, utafikia kupata maneno mawili: Wajuwa maneno haya mawili ni gani? 

Kwanza: Kumuasi Mungu.

Zambi ni tendo la kumuasi Mungu. 

Ya Pili: Kumuchukia Mungu, uadui na Mungu. 

Wewe utasema ya kwamba watu siyo waadui wa Mungu. 

Kweli, watu wamchukia MUNGU wa BIBLIA TAKATIFU

Wao wampenda tu Mungu wa mawazo yao na mafikili yao. 

Wampenda Mungu wa kifalsafa. 

Zamani, nilisoma habari moja katika Gazati “Kioo ya Altoona”, ikizungumuza kuhusu kuwa na Kabila na lugha moja, masemi moja. 

Sipendi tupoteze muda hapo. 

Watu hawa wanazani kwamba wanamufahamu na kumsikia Mungu, bali sivyo, wao hawamtambuwi hata kidogo. 

Zambi ni kumuasi Mungu, kumuchukia Mungu. 

Sasa kuna ulizo linalotukia hapo: 

Zambi ilifika na kuingia je duniani? 

Ni muhimu sana kufahamu haya. 

Kwa kweli, siyo mapashwa yetu kujiuliza ulizo lile, bali ni ulizo lenye mafaa sana. 

Namna gani zambi iliingia katika dunia? 

Tusome Waroma 5 

“Hivi kama kwa mtu mmoja, neno gani inayofwata? 

Zambi iliingia

Tendo hili “iliingia” inaweza kupata tafsiri nzuri tunaposema “ilishambulia na kugandamiza”. 

Kushambulia na kugandamiza Inchi. 

Zambi ilishambulia na kugandamiza ulimwengu. 

Zambi ili nyanyasa na kubaka dunia na kujiingiza kwa nguvu ulimwenguni. 

Zambi haikukuweko kwa mwanzo. 

Mwenyezi Mungu aliuumba ulimwengu ukiwa kamilifu, barabara, na mtu akiwa kamili. 

Kwa sababu hii, kweli ni ujinga mtupu kuwa na mawazo ya kwamba Mungu aliuumba dunia ikiwa ukiwa na bila manufaa yoyote, ukiwa mtupu na isiyofaa kwa kazi yeyote. 

Mungu hakufanya kitu cha namna sawa. 

Kuna watu wengi wa zehebu ya “Wachungaji wa mila na asili ya kidini” wanaorudilia mambo iitwayo “Ukosefu wa nadharia” ama “Nadharia ya kando, ya tofauti”. Kwangu mimi mambo haya yote ni upumbafu. 

Mungu hangaliumba kitu cha namna sawa. 

Yote ile Mwenyezi Mungu aliyoumba ilikuwa mzuri na kamili. 

Mtu hakuwa wa umilele. 

Mtu alikuwa kiumbe Kamili, bali angaliweza kufanya zambi na kufa. 

Sasa Mwenyezi Mungu anasema: Zambi ilishambulia na kunyanyasa dunia. 

Na nini tena? 

“Na kufa kwa njia ya zambi”

Hapa Mwenyezi Mungu anazungumuza kuhusu nini? 

Kwanza Mungu anaonesha kwamba: 

Zambi inatawala na kuenea dunia nzima, “kilimwengu cha zambi” 

pia anazungumuza kuhusu kutawala na kuenea kwa mauti dunia nzima, “kilimwengu cha kufa” 

Swali ni kujuwa kama washika mambo haya katika mafikili yako?

Ni haya yanayosemwa katika Maandiko ya Waroma 5: 12 hadi 14. 

Kilimwengu cha zambi 

Kilimwengu cha mauti. 

Sababu gani inaenea duniani pote, na sababu gani mauti vile vile inaenea duniani pote? 

Sababu gani watu wanafariki? 

Sababu gani karibuni watu wote wanafariki? 

Ila, kwa siku za leo, kama wasikia yale wataalam wa sayansi wanayoyasema wakijizania kuwa na elimu ya juu sana na wenye masomo ya juu sana, wale wanaokuwa katika masomo ya juu sana, ma Univarsti na vivi hivi, wao wanazania kwamba umaridadi na maumbile ya mtu yanaendelea kusonga mbele na maisha yake ya kesho itakuwa muzuri zaidi, juma iliyopita tulizungumuza mengi juu ya jambo hilo, kwa hivyo, kwa siku ya leo, hatutaponda tena muda wetu. 

Lakini, ningelitamani sana mufahamu neno hili: 

Wao wanasema kwamba wanaendelea kusonga mbele na namna ya mabadiriko ya hali yao. 

Masemi yao yanamaanisha nini?   

Eti sisi ni viumbe vyenye kutokea kwa mabadiliko toka mnyama.

Ni kwa namna hii wanayotafsiri kiulimwengu cha zambi na kiulimwengu cha mauti.  

Wanaandika na kuchapa vitabu vingi wakisema kwamba sisi tunafanya zambi sababu aina yetu ni nusu nyama na nusu mtu. 

Sisi ni tukio la kubadirika tukikomaa toka hali ya yayi la msingi hadi kufikia kiwango cha kuwa mtu kamili wa siku za leo, kwa hiyo hatuja timilika, tunaendelea kubaki na tabia moja moja ya kinyama na kwa namna mabadiriko ya umbo letu yanaendelea mbele, tutaendelea kuacha  na kuangusha tabia moja moja sawa sawa vile sayansi itazidi kupata mambo mengine mapya na kusonga mbele ndani ya elimu ya kiganga na usafi na tutafikia kiwango cha kutokufa tena. 

Watu wataishi miaka 100, kiisha watafikia kiwango cha miaka 200, kiisha miaka 300 na kiisha hatutakufa tena. 

Haya yote ni ujinga na upumbafu mtupu. 

Hayo ndiyo watu wanavyosema kuhusu maendeleo yao, lakini Mwenyezi Mungu anasema umbalimbali na yale. 

Mwenyezi Mungu anasema ya kwamba kuna kiulimwengu cha zambi na kiulimwengu cha kufa. 

Sababu gani? 

Niwasomee mara tena aya yake ya 12

“Hivi, kama kwa mtu mmoja zambi iliingia ulimwenguni, na kufa kwa njia ya zambi; na hivi kufa kulikuja juu ya watu wote, kwa sababu wote wamefanya zambi…” 

Sasa, ninatamani munisikilize kwa makini sana. 

Kwa sababu gani kufa kulikuja juu ya watu wote, kiulimwengu cha kufa; 

Kwa sababu gani zambi iliingia juu ya watu wote, kiulimwengu cha zambi? 

Ni kwa sababu ya mtu mmoja. 

Watu wengi wanaosoma Teolojia hawafurahiye aya hii, wanachukia sana ukweli huu. 

Na wataalam wengi wanaokuwa na ufahamu wa juu katika dunia, wataalam wa siku za  leo akili yao mbovu inawabeba kwa mawazo yale yale. 

Wanajiuliza kama yawezekana je mtu moja afanye zambi zake na hiyo zambi inakuja juu ya wanadamu wote na kwa ajili ya zambi hiyo sisi sote tunafikia kwa hali ya kufariki, kufa? 

Wanasema kwamba hiyo ni upuuzi mtupu na haiwezi kamwe kuwezekana. 

Bali, neno lile ndilo Mtume Paulo analotuambia hapa. 

“Kwa mtu mmoja (Adamu) aliyefanya zambi, na kwa ajili ya zambi zake, zambi iliingia ulimwenguni, zambi ilishambulia na kubaka watu wote. 

Tusome sasa sehemu ya pili ya aya hii ya 12.” 

“Kama kwa mtu mmoja zambi iliingia ulimwenguni, na kufa kwa njia ya zambi; na hivi kufa kulikuja juu ya watu wote, kwa sababu wote wamefanya zambi:…”

Kwa sababu wote, kiisha neno wote tuna “wamefanya”. 

Tendo hili halingipashwa kuweko. 

Mwatambua namna gani tungelipashwa kusoma mahali hapo? 

“Wote ni wenye zambi” 

Hii inamaanisha nini?  

Ni kweli wewe hauja wai kutenda zambi? 

Hata kama wewe hauja wai kutenda hata zambi tu moja maishani mwako? 

Hata kama ingeliwezekana wewe bado kutenda zambi, wewe ni mwenye zambi. Watambua hiyo? 

Hata kama tangu kuzaliwa kwako mpaka kufa kwako wewe haukufanya zambi. Wewe ni mwenye zambi. 

Mtume Paulo anahitaji kutufahamisha nini hapa? 

Kwanza: 

Mtu mmoja Adamu aliye kichwa cha kizazi cha wanadamu wote alifanya zambi, na sote tuliriti zambi hiyo toka baba yetu Adamu, zambi ikatutawala sisi wanadamu wote tulio uzazi wake. 

Wote ni wenye zambi. 

Eti hiyo ni ya muhimu kweli?  

Kwa sababu gani watoto wachanga wanakufa? 

Kwa sababu gani hata watoto wanafariki kwa saa yao ya kuzaliwa? 

Kama ni kwa sababu ya zambi, ni zambi gani aliyefanya mtoto mwenye anakufa baada ya dakika chache ama saa chache kasha yeye kuzaliwa, zambi gani aliyofanya? 

Yeye hakutenda hata zambi moja. 

Sasa, sababu gani anafariki? Kufa ni mushahara wa zambi. 

Mwafahamu sasa? 

Wakati unafahamu kiulumwengu cha zambi, unatambua kwamba wote ni wenye zambi. Wote wamefanya zambi. 

Wakati Adamu alipofanya zambi, kizazi chote cha wanadamu kilifanya zambi. 

Mwenyezi Mungu aliuona ulimwengu wote, wanaume wote, wanawake wote, watoto wote ndani ya Adamu, wamefanya zambi. 

Na mimi na wewe tuko wenye zambi, siyo sababu tulikosa na kufanya zambi, bali sababu Adamu alifanya zambi. 

Sisi tunakuwa na aina yake na kwa sisi wenyewe hatuwezi kujitenga na zambi. 

Lakini zambi inatugonga na kutuvuruga vichwani mwetu hata kufikia kiwango cha kuzania kwamba kwa nguvu yetu sisi wenyewe tunaweza kufikia kiwango fulani cha utakaso na utakatifu hata tusifanye tena hata zambi moja. 

Hii kweli ni udanganyifu na upumbafu, sababu sote ni wenye zambi ndani ya Adamu. 

Na kama neno hili halingekuwa kweli, yaani kusema ya kwamba wakati Adamu alipofanya zambi mimi na wewe hatungelifanya zambi, sababu inasemwa kwamba wakati ule Adamu alipofanya zambi, wanadamu wote walifanya zambi, basi isingekuwa hivyo, Bwana Yesu ingelimupasa afe mara na mara kwa ajili ya kila mmoja wetu peke yake. 

Unaweza kweli kukubali Utunzaji huu? 

Ama ni mara yako ya kwanza kuusikia, lakini ingalikuwa hivyo. 

Bwana Yesu Kristo alikufa kwa ajili ya zambi ya Adamu na zambi zetu sisi wanadamu wote, sababu tulifanya zambi ndani ya Adamu. 

Kama ingelimupasa Bwana Yesu kufa msalabani mara kwa mara, kanisa ya kikatoliki ya Roma na umati wake wa waamini, ingelijikuta mbele ya swali kubwa,  kama Bwana Yesu angalikufa mara na mara kama sadaka ya zambi. 

Kweli, wote wamefanya zambi ndani ya Adamu na Bwana Yesu Kristo alikufa kwa ajili ya zambi za watu wote. 

Na kwa kweli, inatufikia sisi kuanguka katika zambi, na ni wachache wanaokuwa na ufahamu wa neno hili. 

Wewe na mimi tunafanya zambi, si kwa sababu hali yetu ni ya zambi, lakini sababu tulifanya zambi katika Adamu. 

Hili ndilo jibu. 

Hii ni jibu kweli la utukufu! 

Kwa hivi sasa, tunaweza kusoma na kujifunza Maandiko ya Waroma 5: 15  

“Lakini zawadi ya neema haikuwa kama lile la kosa. 

Kwa maana kwa kosa la mtu mmoja wengi walikufa, zaidi sana neema ya Mungu, na zawadi kwa njia ya neema ya mtu mmoja Yesu Kristo, imezidi kwa watu wengi.” 

16.”Wala kadiri ya yule mtu mmoja aliyefanya zambi, si kadiri ya ile zawadi; kwa maana hukumu ilikuja kwa njia ya mtu mmoja ikaleta azabu, lakini zawadi ya neema ilikuwa kwa ajili ya makosa mengi, ikaleta kuhesabiwa haki. 

17. Kwa maana kama, kwa njia ya kosa la mtu mmoja, kufa kulitawala kwa ajili ya mtu mmoja, zaidi sana wao wanaopokea neema ya kuzidi sana na zawadi ya haki watatawala katika uzima kwa yule mmoja, Yesu Kristo.” 

… la mtu mmoja, mtu mmoja, kwa njia ya kosa la mtu mmoja, kufa ya yule mmoja. 

Kwa hivi, tunayo sasa Maandiko haya katika mioyo yetu, tusome sasa    

Waroma 5: 13 

“maana mbele ya sheria zambi ilikuwa ulimwenguni: “ 

Maana mbele ya sheria, neno gani inayofuata? 

Zambi ilikuwa ulimenguni. 

Waamini sasa ukweli huu? 

Waamini sasa kwamba mbele sheria ije, kwa nyakati ile ya tangu Adamu mpaka Musa, zambi ilikuwa ulimwenguni? 

Ndiyo kabisa, zambi ilikuwa katika nyakati ile. 

Namna gani ninajuwa kwamba zambi ilikuwa ulimwenguni? 

Kwa nini yanipasa kufahamu kwamba zambi ilikuwa ulimwenguni tangu Adamu mpaka Musa? 

Tuchunguze kwa makini Waroma 5  

Namna gani ninaweza kufahamu kwamba zambi ilikuwa ulimwenguni katika nyakati hiyo ya tangu Adamu mpaka Musa na kwamba sheria ilikuwa bado kuwa?  

 Na kwa sababu gani sheria ilikuja?  

Ili zambi ionekane wazi. 

Ili ukubwa wa zambi uonekane wazi. 

Sasa kwa njia gani ninaweza kufahamu kwamba tangu Adamu mpaka Musa zambi ilikuwa ulimwenguni na ijapokuwa sheria inayoonesha na kufunua zambi na makosa ili yaonekane wazi ilikuwa haijakuwa bado? 

Namna gani nitafahamu maneno haya? 

Tusome Maandiko katika Kitabu cha Mwanzo sura yake ya tano, na muniruhusu niwaoneshe jambo lile. 

Mwanzo 5: 3 

“Adamu akaishi miaka mia moja makumi tatu, akazaa mwana kwa sura yake, kwa mfano wake mwenyewe; akaita jina lake Seti; 

4. Siku ya Adamu nyuma ya kuzaa Seti zilikuwa miaka mia nane; akazaa wana na binti. 

5. Na siku zote Adamu alizoishi zilikuwa miaka mia tisa makumi tatu; akakufa.” 

Akakufa, 

Yeye ni mwenye zambi, Adamu alifanya zambi. 

Sasa, tushuke hapo chini tusome yale yanayosemwa katika Maandiko ya Mwanzo 5: 8 

“Na siku zote za Seti zilikuwa miaka mia tisa kumi na miwili; akakufa.” 

Tusome sasa aya ya 11.

“Na siku zote za Kenani zilikuwa mia tisa na kumi; akakufa.” 

Hii siyo mshangazo kweli !!! 

Nawezaje namna gani kufahamu kwamba tangu Adamu hadi Noa, zambi zilikuwa ulimwenguni? Na tangu Adamu mpaka Musa? 

Sababu kila mara, zaidi ya mtu mmoja alikufa. 

Ni nani mwenye aliepuka kufariki? Enoke. 

Bali kuhusu wengine wote ni: “na akafa, na akakufa, na akakufa na vivi hivi. 

Katika Biblia Takatifu, sura hii (ya Mwanzo 5) inaitwa Sura ya kufa. 

Sababu gani alikufa? 

Sababu zambi ilikuwa ulimwenguni na kwamba tangu Adamu mpaka Noa, watu wote walikuwa wenye zambi, sababu wakati Adamu alipotenda zambi, sisi sote tulihesabiwa kuwa wenye zambi. 

Kwa njia gani tena naweza kufahamu kwamba zambi ilikuwa ulimwenguni tangu Adamu mpaka Noa na Toka Noa hadi Musa? 

Namna gani ninaweza kufahamu jambo hilo? 

Unipe sababu ingine inayoonesha kwamba zambi ilikuwa ulimwenguni. 

Namna gani naweza kujuwa? 

Waroma 5: 12 Zambi ilikuwa duniani?  

Namna gani naweza kujua? 

Siyo kwa kuleta jibu ya kubahatisha tu, ama kuzania, ama pendekezo la swali.

Neno hili ni la muhimu sana kufahamu. 

Tusome sasa Mwanzo 6: 5 

“Bwana akaona ya kama uovu wa watu ulikuwa mkubwa duniani, na ya kama mawazo yote ya mafikiri ya mioyo yao yalikuwa mabaya tu siku zote.” 

6. “Na BWANA alijuta ya kwamba amefanya watu duniani, ikamhuzunisha moyoni mwake.” 

7. “Bwana akasema: Nitaharibu mtu ambaye nilimwumba toka uso wa inchi; mtu wa nyama vilevile, na kitu kinachotambaa na ndege ya anga; kwani ninajuta ya kwamba nimewafanya.” 

Sasa, ni nini inayohakikisha kwamba zambi ilikuwa ulimwenguni tangu Adamu mpaka wakati wa Noa? 

Ni kwa kuona Garika. 

Garika: Sababu gani Mwenyezi Mungu aliangamiza ulimwengu nzima kwa maji na kuokowa tu wale waliokuwa ndani ya Safina? 

Kwa sababu zambi ilizidi duniani. 

Pia wajiuliza, kuwa na ufahamu katika mambo yote haya yanafaida gani? 

Sikiliza kwa makini, ndugu yangu. 

Kumbuka Maandiko ya Waroma 5: 13 

“maana mbele ya sheria zambi ilikuwa ulimwenguni; lakini zambi haihesabiwi wakati sheria isipokuwa.”

Sasa, kwa kuwa na ufahamu bora wa Maandiko haya, inatupasa kujua neno moja. 

Tuchunguze kwa upekee, wakati wa tangu Adamu mpaka Noa. 

Watu wote walifariki ila tu Enoke ndiye mwenye hakuona kufa. 

“Mushahara wa zambi ni mauti.” 

Sasa Garika ina maana gani kwangu? 

Garika inanijulisha kwamba Mwenyezi Mungu alihukumu zambi tangu Adamu mpaka Noa. 

Ni vigumu sana kufahamu Waroma 5, bila kuwa na ufahamu ndani ya maneno haya.  

Mungu alikuwa akiwaona watu wote namna walivyo fariki moja kwa moja, ila Enoke tu peke yake ndiye mwenye aliyechukuliwa na Mungu ili asione kufa. 

Jambo la pili lenye ningelitamani mufahamu ni kwamba, 

Mbele ya Garika, Mwenyezi Mungu aliona namna uovu wa watu ulizidi kuongezeka katika dunia, mawazo ya ukaidi na uchafu sana ulizidi kuendelea kuwa mbaya zaidi sana katika mioyo ya wanadamu, kwa hiyo, Mwenyezi Mungu aliyafungua madirisha ya mbingu na kuangamiza wote kwa kuwazamisha katika maji, ila tu Noa na wale waliokuwa katika Safina ndiwo waliopona. 

Mungu alihukumu zambi! 

Hii siyo mastaajabu kweli. 

Hata hivyo hakumuhesabia mtu zambi kwa binafsi sababu sheria ilikuwa bado kuingizwa.

Hivi ni mushangazo kweli. 

Tusome sasa Mwanzo 11: 1  

“Na dunia nzima ilikuwa na lugha moja na usemi mmoja.

Na ilikuwa wakati waliposafiri kwa mashariki, wakakuta inchi sawa katika inchi ya Sinari; wakakaa pale. 

Wakasemezana: Tufanye matafali na kuyachoma vizuri kwa moto. 

Wakakuwa na matafali kwa mawe, na lami kwa chokaa. 

Wakasema: Tujijengee wenyewe mji na mnara, kichwa chake kifike mbinguni na tujifanyie jina; hata tusisambazwe juu ya uso wa dunia. 

Bwana akashuka kuona mji na munara, ambao wana wa watu walijenga. 

Bwana akasema: Tazama, wao ni taifa moja, nao wote wana lugha moja; na maneno haya wanaanza kuyafanya; basi sasa hakuna kitu ambacho kitawazuiza wanachokusudi kufanya.” 

Sasa ingelikuwa heri munisikilize kwa makini sana. 

Ni nini iliyofanyika kwa Munara wa Babeli? 

Kwa munara wa Babeli, watu walianzisha dini yao. 

Mwenyezi Mugu aliwaambia: 

Nendeni na mukajaze dunia” 

Bali wao walisema: “Tutabaki na KUKAA HAPA” 

Na walijenga DINI YA BABILONI, dini yao ya mshangazo inatajwa tangu Mwanzo sura 10 mpaka Ufunuo 17 na 18

Na nini mwenyezi Mungu aliyowatendea? 

Mungu aliwaacha wajihukumu. 

Mwenyezi Mungu aliwatupilia kweli. 

Wakajichafua sana, wakafanya uzinzi wa haya na machafuko, mume na mume na muke na muke, wakazama sana ndani ya ahibu na machafuko ya zambi yenye kushangaza  eti  Mwenyezi Mungu aliwahukumu? 

Sawa sawa ginsi Mwenyezi Mungu alivyohukumu na Garika, wao pia vilevile Mwenyezi Mungu aliwahukumu kwa kuwapa mioyo migumu na kuwasambaza sambaza na kuwatupilia mbali na hapo akaanza upya na mtu mmoja jina lake ABRAM.  Baadaye jina la mtu huyu lilibadirishwa hata kuwa ABRAHAMU. 

Mwatambua kwamba Waroma 5, yaonesha kwamba kulikuwa zambi duniani mbele sheria haijakuwa, na Mungu alihukumu zambi. Kila mtu alifariki, ila tu Enoke ndiye aliyechukuliwa juu. 

Kufa kulifikia kila mtu kwa ajili ya zambi, sababu watu wote wamefanya zambi katika Adamu. 

Nafahamu kwamba wengi wanauzunishwa na neno hili. 

Mimi ninakuwa mwenye zambi kwa sababu Adamu alifanya zambi. 

Kwa hiyo, wewe utake wala usitake hiyo, wewe hauta badirisha hata nugta moja katika ukweli huu. 

Unaweza kuzania kwamba wewe ni mtu wa mila nzuri, Kweli yawezekana ndivyo ulivyo, lakini kumbuka wakati Adamu alipo anguka, na kufanya zambi, Mwenyezi Mungu alikuhesabia zambi ndani ya Adamu. 

Mwenyezi Mungu alikuona ndani ya Adamu. 

Wewe ulifanya zambi wakati Adamu alipofanya zambi; kwa hivyo wajidanganya tu kwa kuzania ya kwamba una mila nzuri. 

Wewe unafanya zambi kila saa na kila dakika, kutaka na kuto kutaka. 

Mimi ninakumbuka kwamba Mwenyezi Mungu anahukumu zambi. 

“Mushahara wa zambi ni mauti.” 

Tusome sasa katika Waebrania 11: 4 

“Kwa Imani Abeli alitolea Mungu zabihu nzuri zaidi kupita Kaina; kwa hii alishuhudiwa kuwa mwenye haki, Mungu akishuhudia sadaka zake; naye hata amekufa, angali akisema.” 

Hii ni wakati wa tangu Adamu mpaka wakati wa Noa, mpaka Musa, wakati sheria ilikuwa bado kuingia.

Mwenyezi Mungu hakuhesabia zambi juu ya mtu. 

Mume ama muke, musichana ama mufulana, wote wangeliweza kuokolewa. 

Abeli aliokolewa na Kaina hakuokolewa. 

Abeli aliokolewa namna gani? 

Kwa njia ya sadaka yake. 

Zambi ilkuwa duniani na Mwenyezi Mungu alihukumu zambi, lakini wanaume na wanawake walipata kuokolewa. 

Tusome Mwanzo sura yake ya ine

Mwanzo 4: 6 

“Bwana akamwambia Kaina: Kwa nini unakasirika? 

Na kwa nini uso wako unakunjamana? 

Kama ukitenda vema, hutakubaliwa? 

Na kama hutendi vema, zambi inakaa kwa mlango wako na inakutamani wewe, lakini sharti uishinde.” 

Kwa kweli, ni nini iliyomufikia baadaye? 

Kaina na Abeli walifika mbele za Mungu. 

Kwa wakati ule, wao wawili waligeuka kwa muda huo kuwa sawa Makuhani wa Mungu kwa namna yao. 

Katika kila jamii, Kichwa cha kila jamii, kwa umri wa miaka makumi tatu, waligeuka kuwa Makuhani. 

Kila mtoto mume mwenye anaeneza umri wa miaka makumi tatu, alikuwa akigeuka kuwa kuhani na alipashwa kwenda mbele ya Mwenyezi Mungu ili atowe zabihu ya sadaka ya kuchinjwa. 

Sadaka ya Abeli ilikubaliwa na Mungu. Kaina alitupiliwa na Kaina alipotea. Abeli aliokolewa. 

Sasa, kwa sababu gani iliwapasa Kaina na Abeli watolee Mungu zabihu? 

Tunapata jibu katika kitabu cha Waroma 5, inayosema wote walikuwa “wenye zambi”, wote wamefanya zambi ndani ya Adamu. 

Sasa, ni nini ambalo Mwenyezi Mungu anamuambia Kaina? 

Anamwambia Kaina: 

Una uwezo wa kujirekebisha (Mwenyezi Mungu anapenda kuona mapenzi yake.) 

“Zambi inakaa kwa mlango wako” 

Msemwa huu unamaanisha tena nini? 

Kaina alikuwa angali na uwezo wa kutoa zabihu ya sadaka la kuchinjwa kama angaliamuru hivyo, sababu toleo lile lilikuwa bado ingali linapatikana hapo karibu ya Kaina, toleo kwa ajili ya zambi, Mungu alikuwa nalo, akiweka hapo hapo pembeni ya Kaina mwana kondoo kwa ajili ya sadaka la kuchinjwa kwa niaba ya Kaina, ili naye vilevile awe na nafasi ya kupata wokovu. 

Kaina alifanya kosa, pahali pa kutolea Mungu damu, zabihu ama sadaka ya kuchinjwa isiyo na laumu, yeye alimutolea Mwenyezi Mungu matunda ya shamba. 

Na Mwenyezi Mungu alimuambia Kaina: 

“kungali uwezekano ya kutumia mapenzi yako ili uchague kutenda vema, nafasi ingali kwako kwa kuamuwa kutoa toleo nzuri ili uokolewe, nafasi ni wazi kwako kwa kutoa toleo la kuchinjwa.” 

Wafahamu namna gani maneno haya yaweza kusomwa katika Maandiko Matakatifu?  


Mwanzo 4: 7  

“Na kama hutendi vema, zambi inakaa kwa mlango wako na inakutamani wewe, lakini sharti uishinde.” 

Kama ukitenda vema, hutakubaliwa? 

Kutenda vema ni kutowa toleo nzuri, kuwa na zamiri safi ya kuona tofauti kati ya toleo mbaya na toleo nzuri. 

Kuepuka kushindwa kutokujuwa ni nini toleo mbaya. 

Kama wewe unashindwa kutofautisha yaliyo mema kwa yaliyo mabaya, hutendi zambi? 

Amuwa na tenda yaliyo mema. 

Amua na tenda mema, bali umeshindwa. 

Mwenyezi Mungu alimkumbusha Kaina kwamba kuna toleo la kuchinjwa lenye lingali bado linapumuwa kwa mlango wa kaina. Uamuwe tu kwenda kwa mulango, ukaichukuwe uichinje na kumwanga damu yake kwa sadaka. 

Lakini Kaina hakukupali na kuitaji kwenda mlangoni mwake ili achukue toleo lile . 

Mwafahamu neno lile? Pale pale kulipatikana wokovu, zambi, na pia kulikua pia hukumu ya zambi. 

Hii inamaanisha kwamba Maandiko ya Waroma 5: 13. Itatafsiriwa na kufafanuliwa kwamba zambi yalikuwa duniani na pia hayasemi kwamba Mwenyezi Mungu hakuwa anahukumu zambi; pia hayasemi kwamba Mwenyezi Mungu hakuwa anaokowa, Mwenyezi Mungu alikuwa anaokowa. 

 Neno lifwatalo ni kwamba, 

Tangu Adamu mpaka wakati wa Noa, tunampata mtu aliyeitwa Kaina, naye aliuwa mtu. 

Yeye alikuwa wa kwanza kuuwa na mtu wa kwanza aliye uwawa ni Abeli. 

 Kaina alimuuwa namna gani? 

Kaina aliangalia na kutazama namna Abeli alikuwa anatolea Mwenyezi Mungu zabihu la sadaka ya kuchinjwa. 

Abeli alikamata toleo lake, na akakamata kisu na kuchinja toleo lake, ili atowe sadaka la kuchinjwa, akalikata shingo la mwana kondoo na damu ikamwangika. 

Chuki na hasira ikajaa ndani ya roho ya Kaina kwa sababu Mungu alikubali toleo la Abeli na kukataa lile la Kaina. 

Naye Kaina alitwaa lilelile kissu lenye lilichinja kondoo ya sadaka na kukata shingo la ndugu yake Abeli. 

Mawazo yenu yanaweza kwenda mbali na kuzania kwamba ni mimi wenyewe ninayeunda wazo lile, bali siyo hivyo, tupate mwangaza ndani ya Maandiko katika Kitabu cha 1Yoane 3:12  

“Tusiwe kama Kaina aliyekuwa wa yule mwovu, akaua ndugu yake. 

Naye alimwua kwa sababu gani? 

Kwa sababu matendo yake yalikuwa mabaya, na ya ndugu yake yalikuwa ya haki>” 

Mwatambua tafsiri katika Kigriki la tendo hili “kuua”? 

Inamaanisha kuuwa nyama iliyotolewa kwa sadaka ya kuchinjwa. 

Kwa kweli, tafsiri nyingi zingine zinasomwa kama ifwatayo: 

“Kutumia kisu kilichotumiwa ili kukata nalo shingo la mwenye kuuwawa” 

Hilo ndilo, kwa kweli, tafsiri ya tendo lile katika Kigriki. 

Inamaanisha kutwaa kisu kilichotumikishwa kwa sadaka la kuchinjwa na kutumia hiyo hiyo kisu ili kukata nayo shingo la mwenye kuuwawa. 

Na kwa kweli, kitu gani kilicho fanyika? 

Kaina alitwaa hiyo kisu yemye Abeli aliyotumikisha kwa kuchinja zabihu ya toleo (Kaina angalitupilia mbali hiyo kisu, yeye angaliepuka kuuwa). 

Kaina akamwambia Mwenyezi Mungu: 

Tazama matunda mazuri ya shamba ninayokuletea kwa toleo. 

Mwenyezi Mungu akajibu: 

“Siyataki” 

Mwafahamu namna gani Abeli alijuwa kwamba Zabihu yake imekubaliwa na Mungu? 

Ni kwa njia ya moto. 

Mwenyezi Mungu alituma moto toka mbinguni na moto ile iliteketeza sadaka ya Abeli, lakini haikuteketeza sadaka ya Kaina. 

Kaina akatwaa kisu kilichotumikishwa kwa sadaka ya kuchinjwa na akakata shingo la Abeli na hiyo hiyo kisu. 

Sasa, kwa nini alifanya hivyo? 

Kanuni ya ine iliyoshimikwa na Mwenyezi Mungu dhidi ya Serkali ya Mungu, ilikuwa bado kushimikwa. 

Tusome Maandiko katika Mwanzo 9: 3  

“Kila kitu kinachotambaa kilicho hai kitakuwa chakula kwenu, sawasawa nilivyowapa ninyi mboga za majani, hivi ninawapa ninyi vitu vyote;” 

Kuna jambo iliyobadirika? 

Ni jambo gani kweli? 

Mpaka wakati ule, hawakuwa wanakula nyama, hivi sasa waliruhusiwa kula nyama. Kanuni ya kushimikwa ya Serkali ya Mungu ilibadirika.

Inatubidi sasa kuchunguza maneno yanayosemwa kwa aya ya ine.

Mwanzo 9:4  

“Lakini nyama na uzima wake, ndiyo damu yake, hamutakula.” 

5. Na hakika nitataka damu yenu, damu ya uzima wenu kwa mkono wa kila nyama. Na kwa mkono wa kila mtu, hata kwa mkono wa ndugu ya kila mtu nitataka uzima wa mtu. 

6. Yeye anayemwanga damu ya mtu, kwa mtu vilevile damu yake itamwangwa; kwa sababu alifanya mtu kwa sura ya Mungu.” 

Sasa kuna mabadiriko ya Kanuni ya ine ya Mungu hadi kufikia Garika. 

Kiisha Garika kupita, Mwenyezi Mungu alishimika sasa Serkali ya wanadamu yenye uwezo wa kutwaa pia maisha ya muuaji. 

Tupime kwanza kuweka mafikiri yetu kuhusu nini iliyotukia juu ya Kaina? 

Ni nani aliyehukumu Kaina? 

Kaina muyuda, Kaina muuwaji. 

Hapo mbele tulisema kwamba kwa wakati huo zambi ilikuwa duniani na Mwenyezi Mungu alikuwa anahukumu zambi. 

Sasa, ni nani aliyehukumu zambi hiyo ya Kaina, sababu Serkali ya wanadamu ilikuwa bado kushimikwa? 

Ni Mungu, Muhukumu mkuu wa mahakama ya Mbinguni. 

Tutafurahi kufundishwa mambo haya kwa juma ijayo na tutafafanua mengi.  

Maneno haya ni ya manufaa kweli na  ni yenye hisa. 

Zambi ilikuwa ulimwenguni na Mwenyezi Mungu alikuwa akihukumu zambi. 

Kwa sasa, twatambua zambi Kaina aliyofanya. 

Ulizo ni kujuwa kwamba nini ilitukia juu ya Kaina? 

Eti Kaina aliachiliwa bila malipizi ama kuhukumiwa? 

Tangu wakati ule mpaka kufika kwa wakati wa Garika, Mwenyezi Mungu aliamuwa kwamba: 

“Yeye anayemwanga damu ya mtu, kwa mtu vilevile damu yake itamwangwa; kwa sababu alifanya mtu kwa sura ya Mungu.” 

  Kitu gani kilichotukia kwa wakati ule wa tangu Adamu mpaka wakati wa Noa na ni nini iliyotukia kwa wakati wa tangu wakati wa Noa mpaka wakati wa Musa, wakati Sheria ilikuwa bado haija ingia? 

Ningelitamani ujuwe ya kwamba wewe ni mwenye zambi na mushahara wa zambi ni mauti na kila mtu anafariki, lakini katika KRISTO tuna UZIMA. 

AMEN

N°Ref:  1976 / 004 - STUDIES IN LAW Part II / 02/17/2021