Friday, December 27, 2019

MWENYEZI WA KAZI AMEFUFUKA / OUR RISEN EXECUTOR

Photo taken from B Smith's Kitchen Window







     78 OUR RISEN EXECUTOR
     MWENYEZI WA KAZI AMEFUFUKA
    August 23, 1963  
      Pastor Henry Kulp 
                          




Waroma 5: 9 - 11 
“Basi zaidi sana tukihesabiwa haki sasa kwa damu yake, tutaokolewa katika gazabu kwa yeye. Kwa maana, kama wakati tulipokuwa adui, tulipatanishwa na Mungu kwa kufa kwa Mwana wake; Zaidi sana, nyuma ya kupatanishwa, tutaokolewa katika uzima wake. 
Wala si hivyo tu, lakini tunafurahi katika Mungu kwa Bwana wetu Yesu Kristo, kwa yeye sasa tumepokea upatanisho.”   
Kama vile tunavyoanza mahubiri hii kwa asubui ya leo, ningetamani sana mujuwe na kufahamu neno moja inayo husu Kifo cha Bwana na Mwokozi wetu Kristo Yesu. 
Neno hili mutaliona wazi katika haya yake ya kumi; inayosema kwamba tutaokolewa katika uzima wake. 
Ningetamani neno hili mulisikie kwa makini kwa asubui ya leo. 
Singelipenda mubaki katika uvuguvugu.  
Neno la kwanza nikujiuliza kama Injili ya Waroma inatuambia nini juu ya Damu ya Yesu, na sisi tumeshikamana na kushika nini? 
Ningetamani mujuwe faida na umuhimu wa Damu ya Yesu. 

Waroma 5: 9  
“Basi zaidi sana tukihesabiwa haki sasa kwa damu yake, tutaokolewa katika gazabu kwa yeye.” 
Neno la muhimu  la lazima na linalopaswa ni kuhesabiwa haki. 
Kuhesabiwa haki ni jambo la Mungu mwenyewe kukutafuta na kukuona wewe bila hata kosa lolote, hakuone katika hali ya mwana mupotevu, lakini Yeye Mwenyewe anakushuhudiya kama wewe ni mwenye haki ijapokuwa haustahili. 
Na amekuona kwamba umeokolewa sababu uliamini tu. 

1/ Yote tunayo katika maisha yetu ya kikristo iliuzwa na sina woga ama kushitashita juu ya kutumia neno kuuzwa; tumepewa. 
Matendo ya mitume 20: 28  
“Mujiangalie wenyewe, na kundi lote, ambalo Roho Mutakatifu aliwapa ninyi kuwa wasimamizi ndani yake, mupate kulisha kanisa la Mungu ambalo alinunua kwa Damu yake mwenyewe.” 
Hapa tunapata tendo hili (aliwapa), Kanisa la Mungu ambalo alinunua kwa Damu yake mwenyewe. 
Nikusema kwamba kuhesabiwa haki njoo neno kubwa la muhimu na neno hili lilipewa kwetu kwa Damu ya Mwokozi wetu Yesu Kristo.  
Tuone sasa katika Waroma sura  tatu na mustari wa makumi mbili na tano. 

Waroma 3: 25 
“naye Mungu amekwisha kumweka awe upatanisho kwa njia ya Imani katika damu yake, kusudi aoneshe haki yake kwa sababu ya kuachilia zambi zilizofanywa zamani, katika uvumilivu wa Mungu:” 
Hapo tunaona kama ni kwa Imani katika Damu yake. 
Watu wengi wananiuliza, eti mimi kama mwanadamu, ninapashwa kuamini nini ili niokolewe? 
Watu wanapashwa kuamini Damu ya Kristo Yesu na ni ili iliyo timilifu na inakuwa na Vyote. 

2/ Lakini, tusonge mbele katika mawazo tu hiyo mamoja. 

Waroma 8: 30   
“Na wale ambao aliwachagua tangu zamani, akawaita vilevile; na wale ambao aliwaita, akawahesabia haki, na wale ambao aliwahesabia haki, akawatukuza vilevile.” 
Tunaona hapa kwamba wale ambao aliwahesabia haki, aliwatukuza vilevile, hakukukuwa kitu cha kuchunga muda fulani ama jambo lolote, hakuna jambo ama neno lingine katikati ya kuhesabiwa haki na kutukuzwa. 
Kama wewe ulihesabiwa haki, juwa kwa kweli na uhakika wote kama wewe utatukuzwa. 
Munaona namna gani Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo ni ya Muhimu sana? 
Bila Damu ya Kristo Yesu ndugu yangu wewe hauwezi kupata kitu chochote. 
Haiko maisha ya Kristo Yesu njo inaokowa, ni kufa kwake kama vile tena tunavyo soma ndaini ya Waroma 5:10

Musemwa, inayosema kama tutaokolewa katika uzima wake, unamaanisha nini? 
Tuone kama tutaokolewa kwa uzima wake kweli, ni ule uzima wake nyuma ya kufa kwake. Mambo yote hii inamaanisha nini kwa kweli? 
Katika kufa kwa Yesu, alitununulia yote na alitupatia yote, na wakati tunaamini kufa kwa Bwana na Mwokozi wetu Kristo Yesu, mambo yote yanakuwa yetu. 
Lakini tujuwe kweli kama haina faida kuwa muriti wa uriti na mali hii yote kama isipokuwa kwamba mwenye aliye andika hiyo agano na kutayarisha mambo mengi mbele ya kufa kwake na baadaye afe. 

Waebrania 9: 16 - 17   
“Maana kama agano la uriti lilikuwa lazima mauti la mwenye kulifanya iwe vilevile. 
Kwa maana agano la uriti lina nguvu tu saa ya mauti; kwa sababu halina nguvu hata kidogo, angali mwenye kulifanya ni hai.” 
   Kwa maana mahali agano iko, ile agano ni kutaka kwa mutu. 
Ninajuwa wazi kama sawa desturi mumefahamu misemwa hii: 
Misemwa ya mwisho, ama kulaga na kuagiza matako ya marehemu, ndiyo maana hapo wanatuambia kwamba agano la uriti linaomba kifo cha yule aliye fanya agano. 
Agano la uriti ni mapenzi ya marehemu na hayo yote inapata nguvu kiisha tu kifo ya mwenye aliye fanya hiyo agano la uriti. 
Mutu huyu anapashwa pata kifo ili agano la uriti upate nguvu na uanze kutumikishwa. 
Agano lile linabaki bila nguvu yeyote mpaka kifo cha mwenye kulifanya na ni kiisha kifo cha mwenye kulifanya njo wariti wataanza kutumikisha  na kupata faida ndani yake sababu nguvu yake inajionesha sasa wazi. 
Hiyo tuione katika haya ya kumi na saba: 
“Kwa maana agano la uriti lina nguvu tu saa ya mauti; kwa sababu halina nguvu hata kidogo, angali mwenye kulifanya ni hai.”  

3/ Kwa sasa turudi nyuma kidogo kwa haya ya kumi na tano (15), 
“Kwa sababu hii, yeye ni mupatanishi wa agano jipya, kusudi wale walioitwa wapokee ahadi ya uriti wa milele, maana mauti imefanyika, kwa kukomboa makosa yaliyo fanyika chini la agano la kwanza.” 
Kwa haya ya kumi na sita (16) 
“Maana kama agano la uriti likiwa lazima mauti ya mwenye kulifanya iwe vilevile” 
Na kwa haya ya kumi na saba : 
“Kwa maana agano la uriti lina nguvu tu saa mauti…” nilipendelea kuwaonesha neno hili katika Injili ya Yoane, 

Yoane 14: 27 
“Salama ninawaachia ninyi: salama yangu ninawapa ninyi; nami ninawapa ninyi si kama dunia inavyotoa. Musifazaike mioyoni mwenu, wala musiwe na woga.” 
Hapo ni saa Bwana Yesu Kristo alikuwa analaga wanafunzi wake mbele ya kuwaacha. 
Kwa mwanzo wa sura hii, aliwaambia: roho yenu isifazaike, kiisha akawaambia kama mimi ninakwenda kwa Baba. 
Kiisha kwa haya yake ya makumi mbili na saba alisema: Salama ninawaachia. 
Sasa twende kwa Yoane 20: 19  
“Basi mangaribi ya siku ile ile, ikiwa siku ya kwanza ya juma, wakati milango ilipofungwa pahali walipokuwa wanafunzi kwa sababu ya kuogopa Wayuda, Yesu akakuja, akasimama katikati, akasema nao: Salama kwenu.” 
Hiyo ilikuwa siku ya ufufuko. 
Mangaribi ya siku ile ile, ikiwa siku ya kwanza, kwa maana milango ilikuwa ya kufungwa mahali wanafunzi walikuwa wakijifungia kwa kujificha sababu walikuwa wanaogopa wayuda. 
Bwana Yesu akakuja katikati yao na akawaambia: Salama kwenu. 
Unaona kwa kweli kama mbele ya kufa kwake alisema: Salama ninayo waachia, ile ilikuwa mapenzi yake kwa Mitume kumi na wawili, 
Sasa kiisha ufufuko alikuja sasa kama Mwenyezi wa kutimiza mapenzi yake na akasema ; Salama kwenu. 
Kwa sasa munaweza kuwa na hiyo Salama, sababu sasa Yeye ni Mwenyezi anaye timiza mapenzi yake. 
Ilimupasa Yeye kufa kwanza, bila hiyo hakuna mwenye angelipata salama kama Yeye hangali kufa.  
Hivi alisema salama kwenu, sasa tukiangalia kwa haya ya makumi mbili(20) 

Yoane 20: 20 
“Naye akikwisha kusema maneno haya, akawaonyesha mikono yake na mbavu zake.
Basi wanafunzi wakafurahi wakati walipoona Bwana.” 
Hata wakati alipokuwa katikati yao, aliwaonesha mikono yake na mbavu zake, nikusema mimi nilikufa ili muwe sasa na Salama. 
Mutakutana na vipingamizi na majaribu mengi, yinyi musimame imara, 
Mutakuwa katika dunia isiyo wapenda na inayo wachukia, inayochukia hapari njema yangu, na kwa hiyo nyinyi munaitaji Salama na mimi nilikufa ile niwape Salama. 

4/ Lakini katika Waebrania 9: 16 - 17 
“Maana kama agano la uriti lilikuwa lazima mauti la mwenye kulifanya iwe vilevile
Kwa maana agano la uriti lina nguvu tu saa ya mauti; kwa sababu halina nguvu hata kidogo, angali mwenye kulifanya ni hai.” 
Kwa sababu kwenye kuko mapatano ama agano, kuna mapenzi, vile vile kunapashwa kuwa lazima ya kifo cha mutu alie pana agano. 

Haya ya 18: 
“Kwa sababu hii, hata lile la kwanza halikuanzwa pasipo damu.” 
Damu ni alama ya kifo. 
Siku moja usiku niliingia kwa kiwanda ya kuuzisha mafuta ya gari, na hapo nikaona gari moja lililo jeruliwa, likiharibika na kuvunjikavunjika kwa ukali sana na lote likiwa limepakwa damu ngambo zote, hiyo damu inatuonesha kama watu walikufa wengi kupitiya hiyo aksidenti, sivyo? 
Mutu alikufa ndani ya gari lile. 
Sasa tuone yanayo fwata: Katika hiyo aya ya kumi na munane inayosema : kwa sababu hii, hata ile agano la kwanza  halikufanyika pasipo damu. 

Haya ya 19:  
“Maana wakati Musa alipokwisha kuwaambia watu kila amri kama sheria ilivyoamuru, alitwaa  damu ya makinda naya mbuzi, pamoja na maji na sufu nyekundu na hisopo, akanyunyizia kitabu chenyewe, na watu wote,”  
Turudi kwanza katika Agano la Kale 

Kutoka 24: 6 - 8 
“Musa akatwaa nusu ya damu, akaiweka ndani ya mabakuli, na nusu ya damu akanyunyiza juu ya mazabahu. 
Akatwaa kitabu cha agano, akakisoma masikioni mwa watu; wakasema: Yote ambayo Bwana aliyasema tutafanya na kutii. 
Musa akatwaa damu, akainyunyiza juu ya watu, akasema: Tazameni damu ya agano Bwana alilofanya pamoja nanyi juu ya maneno haya yote.” 
Wao walisema, yote ambayo Bwana aliyasema tutafanya na tutatii na kwa kweli Musa alijuwa kweli kwamba inawezekana washindwe kuyafanya na kwa vile wawe chini ya laana kwa kutokutimiza ahadi walioleta na kwa hiyo aliwa mimia wote damu ni damu ya wokovu. 
Ndugu, wewe hauwezifika kwa Mungu kwa matendo yako, 
angalia, siku ile alipowanyunyizia damu, hakuangalia ama kujiuliza kama walivaa manguo muzuri ama ya bei, hatuwezi kuhesabu kati yao watu wenye walikuwa wakivaa manguo mazuri, wengi wao walikuja kwa mukutano wakivaa kweli vizuri lakini wote walitoka pale manguo yao ikijaa damu na lile jambo halikuambia Musa neno. 
Musa aliwasomea Amri na aliwaambia juu ya Sheria lakini hapana juu ya Neema. 
Nazani kwamba leo munafafanua umbalimbali. 
Bwana wetu Yesu Kristo halombi kitu ama hana aja ya kitu katika Habari hii Njema ya Neema, anaitaji tu wewe ukuje kwake na umwachilie Yeye akuokoe. 

5/ Habari Njema hailombi malipo, inafaa kujuwa hiyo, Habari njema haikushurtishe kitu, Habari Njema inakupa tu bure, Neema inakupa tu bure na haijakoma bado 
Sheria inakuwa na shurti, sheria inapenda nawe utende neno, nawe ulete kitu toka kwako, lakini Neema ni umbalimbali na hiyo. 
Watu wale walijitia wao wenyewe chini ya laana wakati walihaidi wao wenyewe kama wataheshimu Mungu ni kwa sababu ya hiyo njoo Mungu aliwamimia damu ili iwalinde na laana yenye ingetokea kwa mambo yenye walikuwa wanaahidi bila kufanya. 

6/ Walawi 17: 11 
“Kwa kuwa uhai wa mwili ni katika damu; na nime wapa ninyi damu hii juu ya mazabahu ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu; kwa maana ni damu inayofanya upatanisho kwa ajili ya nafsi.” 
Mara kwa mara niliwapa na kuwasomea haya hii na kwa kweli wakati wote wenye nitaendelea kuwa Muhubiri na muchungaji wenu hapa nitaendelea tu kuwapa hayo mara na mara. 
Sababu iko na faida sana na iko muhimi na vizuri kila mmoja wenu aitie mustari kwa kalamu katika Biblia yake na kila mumoja wenu ahakikishe kama anaifahamu na kuijuwa. 
Hiyo ni Musingi wa mafundisho juu ya Damu. 
Kwa kuwa uhai wa mwili ni katika damu, 
Ni hapo tu nyuma nyuma ndiyo wana sayansi  wanaoitwa wa doktari walikuja sasa kufahamu hivyo. 
Maisha ni damu. 
Ma daktari wa zamani walikuwa wanaitwa wa “Kuchuja” sababu walikuwa na tabia ya kutosha damu ya  mutu ili wamuponeshe. 
Kwa sasa hawafanyi tena hivyo. 
Kwa sasa wana ingiza mutu damu kwa njia ya serumu ili mutu ajisikie vizuri na kupona. 
Musa alisema hayo mambo miaka elfu tatu mia tano mbele, lakini wana sayansi na ma daktari wanakuja kuigunduwa tu hapo jana jana. 
Kuna watu wanaozani kama Biblia ni mambo yaliyopita. 
Lakini Biblia tangia hiyo miaka yote ilikuwa inangojea tu ujinga na kutokujuwa kwa wanadamu ili wafikie kujuwa kweli hilo. 
Biblia inakuwa tayari kwa mambo yote na tayari kwa kila dakika  nyakati na wakati na ayo ni juu ya elimu zote na kazi zote za vinadamu. 
Musingi ya yote ni Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 
Kwa mwisho tunaona kwamba Bwana wetu Kristo Yesu alikufa na kwa njia ya kufa kwake aligeuka kuwa Mwenyezi wa kazi yake na kutimiza mapenzi yake kwa ufufuko wake.  
Mungu Baba alitupatia ahadi nyingi, lakini ahadi zote zile za Mungu zilibaki bila nguvu na faida mpaka Kifo cha Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo ili agano zile zipewe nguvu na faida na zianze kufanya kazi.  
Na sasa Mwokozi wetu anatutazama akiangalia kama sisi tuko na uhakika wa kuwa na Faida yote na Baraka zote alizotupatia. 
Bwana Yesu alituachia Utajiri mkuu, lakini namna gani tutatumikisha utajiri huu? 
Yaweza kuwezekana kama hiyo utajiri wote na ahadi zote zipambazushwe? 
Siyo Mwokozi wetu Yesu Kristo njo anaweza penda hivyo, Yeye alifufuka kutoka wafu, na alipanda mbinguni akikaa kuume kwa Baba Mungu, Yeye alinyanyuliwa juu ya mbingu zote na kuwa na mamlaka yote, Mwenyezi wa kutimiza kazi zote na agano na utajiri wote. 
Yeye alijishusha na kuishi katika mahali panapo ongozwa na zambi, akakuwa na kufanyizwa kuwa zambi kwa ajili yetu ili sisi tuwe haki kwa Mungu katika Yeye, na Yeye alikufa ili hiyo utajiri wote wa Mungu tuuriti sasa. 
Tena, tuzidi sana kujiuliza kama tuna uhakika kweli wa uriti wetu sababu Mwokozi wetu alifufuka toka wafu ili atuongozee kazi zetu. 
Hii njo habari yenye tumepata katika Waroma 8: 34 
“Ni nani anayehukumu? Ndiye Kristo aliyekufa, ndiyo, Zaidi, amefufuka, naye yuko kwa mkono wa kuume wa Mungu, tena ndiye anayetuombea.” 

7/ Tuone pamoja kama Walawi 17: 11 
“Kwa kuwa uhai wa mwili ni katika damu; na nime wapa ninyi damu hii juu ya mazabahu ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu; kwa maana ni damu inayofanya upatanisho kwa ajili ya nafsi.” 
Damu hii haikupewa katika mishipa ya nyama, lakini juu ya mazabahu. 

8/ Sasa tuchunguze kitabu ya Waebrania 9: 20 
“Akisema: Hii ni Damu ya agano muliloamuriwa na Mungu”  
Neno kuamuriwa inamaanisha kwamba Mungu ameiomba. 
Hakuna kufanya mabishano na Mungu. 
Hakuna kupima kuwaza kama Mungu anaweza rizika na maisha yetu yenye tunazani kuwa bora na safi, ama Cheti yetu ya ubatizo ama cheti yenye kanisa ilitupatia. Hapana tena hapana, Mungu alisema ninahitaji Damu, ninataka Damu, ninawaamuru munipe Damu. 
Sababu gani wengi wanapenda kubishana na Mungu? 
Sababu gani kupenda kutafuta uelewa na maelezo ya namna ingine mbalimbali na ile Mungu anaamuru? 

9/ Waroma 5: 11  
“Wala si hivyo tu, lakini tunafurahi katika Mungu kwa Bwana wetu Yesu Kristo, kwa yeye sasa tumepokea upatanisho” 
Haya hii kwa kweli inaenda pamoja na hiyo ya pili. Tuangalie vema neno “tunafurahia”, inaweza tafsiriwa na neno ” kujivunia”. Nafurahi sana wakati sisi tunajivunia Mungu. 
Hakuna kitu chenye tunaweza jivunia. Siyo sisi kujivuna kwa nafsi yetu wenyewe, lakini sisi kujivuna katika Mungu. 
Siwezi kuelewa kwa sababu gani tunakuwa na haya ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 
Sababu gani tunakuwa na haya ya wokovu? 
Tunapashwa ijivunia.  

10/ Namna gani unaonesha majigambo yetu ama kiburi yetu katika Mungu? 
Tujiingize pamoja ndani ya maandiko matakatifu na tuone watu wenye walikuwa wakijivunia Mungu. 

11/ Zaburi 71: 17 -1 9 
“Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu; Na kufika sasa nimetangaza kazi zako za ajabu. 
Ndiyo, hata nikiwa mzee na mwenye nyole nyeupe, Ee Mungu, usiniache
Hata nitangaze nguvu yako kwa kizazi cha nyuma, Na uwezo wako kwa kila atakayekuja. 
Haki yako vilevile, Ee Mungu, ni juu sana; 
Wewe ulifanya maneno makubwa, Ee Mungu ni nani aliye kama wewe?” 
Tutazame Daudi anayesema Ee Mungu umenifundisha tangu ujana wangu; na kufika sasa nimetangaza kazi zako za ajabu. Ndiyo, hata nikiwa mzee na mwenye nywele nyeupe, Ee Mungu, usiniache Hata nitangaze nguvu yako kwa kizazi cha nyuma, Na uwezo wako kwa kila atakayekuja. 
Daudi anaonesha kama ushujaa wa kutangaza kazi ya Mungu, haiko tu  kwa vijana na wao wa umri wa katikati lakini iko pia kwa  watu wazee, katika uzee wao. 
Tena kwa haya ya kumi na kenda, “Haki yako” ninajisifu juu ya haki yako. 
Ndiyo kwa kweli Daudi alifahamu namna ya kujisifu juu ya Mungu wakati wa ujana wake hata saa alipo kuwa mzee.  

12/ Zaburi 86: 6 - 8  
“Sikia, Ee Bwana, maombi yangu; Na sikiliza sauti ya kuomba kwangu 
Kwa siku ya taabu yangu nitaomba kwako, Kwani utanijibu. 
Hakuna mwingine katika miungu kama wewe, Ee Bwana, wala hakuna kazi kama kazi zako.”  
Hapa Daudi haiko tu kuona vile alikuwa anajivunia Mungu katika ujana wake, lakini hata katika siku ya taabu yake, Daudi aliendelea tu kujivunia Mungu. 
Sababu Daudi alitambua kwamba hakuna mwengine katika miungu aliye kama Mungu. 
Na Daudi aliimba akisema Ee Mungu Sikia, Ee Bwana maombi yangu; Na sikiliza sauti ya kuomba kwangu. 
Kwa siku ya taabu yangu nitaomba kwako, kwani utanijibu. 

13/ Umekwisha kusikia jinsi Musa alijivunia Mungu?  
Musa mwenye alikuwa mutu wa sheria mkuu? 

Kutoka 15:11 
“Nani ni kama wewe, Ee Bwana, katikati ya miungu? 
Nani ni kama wewe, mwenye utukufu kwa utakatifu? 
Mwenye kuogopwa katika sifa zake akifanya maajabu?”  
Ndiyo kwa kweli Musa alikuwa anajivunia Mungu na ni hivyo njo tunapashwa kuwa. 

14/ Ninajiuliza kama mumekwisha tambua kwamba tukianza tu na sura ya kwanza ya Kitabu ya Mutume Paulo kwa Waroma na kuendelea mpaka sura ya kumi na tano, safari hii ndefu ya kusoma haya izi zote tutaona kwamba katika sura ya kwanza, ya pili na ya tatu inaonesha kama watu wote wametenda zambi. 
Alionesha hiyo katika  

Waroma 3: 23 inayosema: 
“Kwa sababu wote wamefanya zambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu” 
Lakini mambo inabadilika mu haya hii tu ya tatu na ni vizuri tuione katika 

Waroma 3: 19 
“Na tunajuwa ya kama maneno gani inayosema sheria, inasema kwao walio chini ya sheria; kusudi kila kinywa kifungwe, na ulimwengu wote uwe chini ya hukumu ya Mungu.” 
Inasema kwamba Kila kinywa kifungwe katika zambi 
Zambi ilifunga kinywa cha kila mutu aliye mwanadamu. 
Wote wamehukumiwa wote. 

AMEN

Réf: 08/23/1964 / Mwenyezi wa kazi amefufuka / 78 Risen Executor / 12/27/2019