Sunday, May 24, 2020

MWISHO WA KISIRISIRI WA KIZAZI HIKI / THE SECRET CONCLUSION OF THIS AGE

View from my kitchen window







MWISHO WA KISIRISIRI WA KIZAZI HIKI 
THE SECRET CONCLUSION OF THIS AGE
December 30, 1973
Pastor Henry F. Kulp




1 Wakorinto 15: 51 – 58
“Tazameni, ninawaambia ninyi siri: Sisi sote hatutalala, lakini sisi sote tutabadilika, Kwa dakika moja, kwa kufunga na kufungua jicho, kwa baragumu ya mwisho: sababu baragumu italia, na wafu watafufuliwa wasiwe na kuoza, na tutabadilika.
Maana sharti ule wenye kuoza uvae kutokuoza, na huu wa mauti uvae kutokufa. Lakini wakati ule wa kuoza utakapovaa kutokuoza, na ule wa mauti utakapovaa kutokufa, wakati ule litakapotimiya neno lililoandikwa:
Mauti imemezwa kwa kushinda.
Ee mauti, kushinda kwako ni wapi?
Ee mauti, uchungu wako ni wapi?
Basi uchungu wa mauti ni zambi; nguvu ya zambi ni sheria.
Lakini asante kwa Mungu ambaye anatupa sisi kushinda kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Basi, ndugu zangu, wapenzi, musimame imara, musitikisike, mukizidi siku zote kutenda kazi ya Bwana kwa sababu munajua ya kuwa kazi yenu si bure katika Bwana.”
Sura hii ina uzuri wa mastaajabu sana.
Inaitwa Sura ya UFUFUKO Kwa sasa ingekuwa vema tuone aya mbili inayoonekana kama wazo mbili tofauti. 
Aya ya 19 “Kama katika maisha haya tu tuna tumaini katika Kristo, sisi ni masikini kuliko watu wote.”
Hii inataka linganisha maisha yetu kuwa sawa yenye kuelekea maneno ya hapohapo na kwa saa ileile.
Kwa kweli ni hayo mambo hawa wahubiri wa upotevu wenye kufundisha mambo isiyofaa na ya umbalimbali kweli, wanapenda watuaminishe hivyo.
Wanamtia Bwana wetu Yesu Kristo kama Mwalimu mukuu, mwenye kutuonesha njia tunayopashwa pita, wakituambia kwamba sisi tunapashwa tu kushurulika na maisha yetu ya sasa na ya siku kwa siku.
Siyo mushangazo kuona vijana wa siku za leo wakichanganyikiwa na maisha, sababu maisha ya siku hizi inakuwa mbovu na kujaa maovu zaidi ya miaka kumi zilizo pita hapo kale. Na kweli hiyo ni kinyume ya haina mbovu ya uovu, ni hapo Mutume Paulo anasema kwamba maisha yetu ya ukristo siyo ya Ulimwengu huu.
Hapa chini duniani tunaonja tu madogo ya faida yenye tutapata baadaye, sababu Tumaini letu kweli si hapa chini.

1/ Aya ama shairi lenye ningelipenda tuchunguze kwa makini sana ni
Aya ya 57
“Lakini asante kwa Mungu ambaye anatupa sisi kushinda kwa Bwana wetu Yesu Kristo.”
Neno kubwa hapa ni neno Kushinda
Maisha ya mukristo ina ushindi.
Wengi wanazungumuza juu ya maisha ya ushindi, lakini, ushindi huo siyo ushindi tunaopata kwa siku za leo kwa maisha yetu ya kila siku, lakini ni Ushindi utakao kuja. Kila mtoto wa Mungu wa kweli, ana Ahadi ya Ushindi.
Na hii njo neno tutakalo jifunza leo.
Maisha ya mukristo ina ushindi.
Wengi wanazungumuza juu ya maisha ya ushindi, lakini, ushindi huo siyo ushindi tunaopata kwa siku za leo kwa maisha yetu ya kila siku, lakini ni Ushindi utakao kuja. Kila mtoto wa Mungu wa kweli, ana Ahadi ya Ushindi.
Na hii njo neno tutakalo jifunza leo.

2/ Mwisho wa kizazi hiki itakuwa katika siri.
Kizazi hiki kilianza na siri na mwisho wake utakuwa katika siri.
Ilianza na ugumu wa Israeli. Waroma 11: 25 “Kwa maana sitaki, ndugu, musijue siri hii, ili musijione wenyewe kuwa wenye akili, ya kwamba kwa sehemu ugumu umepata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa umefika.”
Hatungeliweza kutamka Kanisa Mwili wa Kristo bila kwanza ugumu wa Israeli. Utanzaji wa Neema unaanzishwa na siri na utafika mwisho katika siri.

3/ Aya ya 51
SISI SOTE HATUTALALA 
SISI SOTE HATUTALALA “Tazameni, ninawaambia ninyi siri: Sisi sote hatutalala, lakini sisi sote tutabadilika,”
Neno la raha na maastaajabu linalo onesha hali ya waliokufa katika Bwana Yesu Kristo.
Tunaipata tena katika kitabu cha
1 Watesalonika 4: 14 
“Kwa sababu tukiamini ya kama Yesu alikufa na kufufuka, hivyo wao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja Naye.”
Na hapa inamaanisha kwamba ni Bwana wetu Yesu Kristo aliye watia katika kulala. Na kweli hii inaelekea mwili wetu wa maumbile.

4/ Ila pale tunaambiwa kwamba:
Sisi sote hatutalala.
Kutakuweko kizazi chenye kitaona mauti na kufa na kutakuwa kizazi chenye hakitakufa ama kuona mauti.

5/ Kunakuwa kusudi kubwa tatu inayotuma waamini wahitaji KUNYAKULIWA ama kuwasukuma waamini wapendelee hiyo siri ije upesi.
5.1 Hawa furahie tena maisha ya siku hizi hapa duniani.
Maisha yanakuwa muzigo muzito mpaka kuwakata hamu na kupendelea sasa siku hiyo ya Kunyakuliwa ije ili iwaepushe na kuwatowa katika hiyo muzigo wa shida ya maisha kali ya leo. Lakini mambo hayatatembea hivyo.
Mwamini hapashwe kuhitaji Kunyakuliwa kusudi ahepuke ugumu wa maisha. Mwenyezi Mungu alitupatia Biblia, alitupatia Matunzaji yanayo patikana katika Biblia, Ahadi mbalimbali inayoweza kuturuhusu sisi tuishi kwa furaha katika maisha yetu ya hapa chini.
5.2 Kuna wale wanaokuwa na woga wa kufa.
Kuna wale wanao kimbia mbonde la kivuli cha mauti.
Wengi wao wanajuta na kuogopa wakijiuliza kama kifo itawapata kwa njia gani.  
2 Wakorinto 5: 8 “lakini tunauhodari, nasi tunapenda zaidi kutoka katika mwili, na kukaa pamoja na Bwana.”
5.3 Kuna wale waohitaji Mwokozi nao wanapendelea sana kukaa pamoja na Mwokozi.  
5.3 Kuna wale waohitaji Mwokozi nao wanapendelea sana kukaa pamoja na Mwokozi.  
2 Timoteo 4: 8 “nyuma ya haya nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana mhukumu wa haki atanipa siku ile; wala si mimi tu, lakini watu wote pia wameopenda kuonekana kwake.”
Kupenda kuonekana kwake, inamaanisha kumpenda, nikusema mapendo yoa kwake yamefurika na wamejaa na mapendo Kwake.
Wanapenda wawe pamoja NAYE.
Mambo ya dunia hii inaendelea tu kuwa muchafu zaidi, mpaka wao wanapendelea Kuonekana Kwake, Kumlaki Hewani.

6/ Lakini, haijali hata tukiwa tukiisha, ama tayari tukiwa tumeisha kufa katika KRISTO, sote tutabadilishwa.
Haijali kwamba tuwe wafu ama hapana.
Tumefundishwa tena ukweli huu katika:
1 Watesalonika 4: 16 – 18
“Kwa sababu Bwana Mwenyewe atashuka toka mbinguni, na sauti kubwa, na sauti ya malaika mkubwa, na pamoja na baragumu ya Mungu: nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza;
kiisha sisi tulio hai, tuliobaki, tutanyanyuliwa pamoja nao katika mawingu, kukutana na Bwana katika hewa, na hivi tutakuwa pamoja na Bwana milele.
Basi mufarijiane kwa maneno haya.”
Inawezekana ni kizazi hiki ndicho chenye hakita kufa, hatujuwi kitu chochote
juu ya maneno haya.

7/ Kunakuwa ujanja moja wakupenda kujionesha kama wale wafanyao ushuru, ujanja huo unatumikishwa na watu wanaojionyesha kuwa eti wao wanapenda Biblia sana.
Na wao wanaogopesha wengi juu ya neno “kuishi kwa sababu ya Yesu”
Wanasema kwamba kama wewe uko nafanya kitu chochote chenye hakimupendezi Bwana Yesu na ile siku ya Kunyakuliwa inafika na inakukuta ndani ya neno hilo, wewe hauta Nyakuliwa ili ukutane na Mwokozi hewani.
Yafaa tu wewe uhishi kwa sababu ya Bwana Yesu, haijali kwamba uko pamoja naye ama hapana. Wewe kwa siku ile utanyakuliwa katika hewa.

8/ Na TUTABADILIKA katika kigriki ni AL-LAS’-SO inayo maanisha: kuwa umbalimbali, ndugu watambua hiyo, Tutabadilika.
Tutakuwa na mwili wa aina nyingine mbalimbali.
Ninao uhakika kwamba hiyo itakuwa USHINDI kwetu.
Tutakuwa na mwili wa aina nyingine mbalimbali.
Ninao uhakika kwamba hiyo itakuwa USHINDI kwetu.
Sababu pahali ya kuwa na mwili wa kibinadamu, tutakuwa na mwili wa kiroho.

9/ Kubadilika huko kwa mwili kutafanyika kwa muda gani?
Ni neno “dakika” kwa kigriki AT-OM-OS inayomaanisha sehemu kidogo sana(atomi) ya muda.
Inayokuwa mugawanyiko wa moja kwa milioni kumi ya sekondi (1/10.000.000 ya sekondi).
Eti, wewe wajuwa kipimo ya muda unaoweza kupima kiwango hicho cha muda?

10/ Kwa baragumu ya mwisho
Wengi wanasema kwamba hii inaonekana sawa tabiya ya kiyuda. Hapana.
Kwa nini kutumikishwa kwa jina hilo “baragumu ya mwisho”?
Kwa nyakati hizo, jina hilo lilikuwa likitumikishwa mingi na watu wa nyakati ile. Ilikuwa ikitumikishwa kwa majeshi la waaskari wa Roma.
Wakati kampi la jeshi ilikuwa tayari kuondoka, iwe muchana wala usiku. Walipiga baragumu. Na palepale, kitu cha kwanza kufanya ilikuwa kukunja hema zao na kuwa tayari kwa kuondoka.
Neno ya pili ilikuwa kujipanga kwa mustari na kwa mwisho ilikuwa ile walikuwa wanaita “baragumu ya mwisho” nayo ilimaanisha amri yakusema “mbele songa, twende”. Mutume anatumikisha musemwa sawa sawa kwa kumaanisha kwamba, wakati baragumu ya mwisho italia, kizazi hiki kitatoweka na kufika mwisho na sote tutaamuriwa kwenda kukutana na Bwana wetu hewani.

11/ Hapa waliokufa na wafu, sote tunakwenda kukutana na Bwana. Nikusema hapo kuna kundi mbili: Waliohai na walio hai.

12/ Aya ya 53 Tunaposema “wenye kuoza”, tunamaanisha wale waliokufa.
Na “huu wa mauti” unamaanisha wale walio hai.
Huu wa mauti unaweza kufa, lakini ukivaa kutokufa, hauwezi tena kufa.
Na “huu wa mauti” unamaanisha wale walio hai.
Huu wa mauti unaweza kufa, lakini ukivaa kutokufa, hauwezi tena kufa.

13/ Aya ya 54 Hapa tunapata neno moja la manufaa.
Wakati ule litakapotimia neno lililoandikwa:
“Mauti imemezwa kwa kushinda”
Hii ni neno muhimu tunalopata katika: 
Wakati ule litakapotimia neno lililoandikwa:
“Mauti imemezwa kwa kushinda”
Hii ni neno muhimu tunalopata katika: Isaya 25: 8“Atazame kufa kusiwe tena milele. Na Bwana Mungu atapangusa machozi toka nyuso zote; na haya ya watu wake ataiondosha toka dunia yote, maana Bwana amesema maneno haya.”
Neno “Atameza” inamaanisha kumeza yote.
Kunakuwa misemwa inayo ambatana na hiyo sawa “KOPO YA MWISHO” inayomaanisha kwamba unameza kinywaji chote cha mwisho chenye kilikuwa katika kopo na hakubaki tena kitu ndani.
Nikusema kwamba kifo kinakomeshwa na tukio lile.

14/ Aya ya 55 “Ee mauti, uchungu wako ni wapi?
Ee mauti kushinda kwako ni wapi?” Hapo Mutume Pauloanaf ananisha na maandiko ya  
Ee mauti kushinda kwako ni wapi?” Hapo Mutume Pauloanaf ananisha na maandiko ya  
Hosea 13:14.
Hosea 13: 14 “Nitawakomboa toka nguvu za kaburi, nitawaokoa toka mauti; Ee mauti wapi mapigo yako? Ee kaburi, wapi kuharibu kwako? Toba itafichwa kwa macho yangu.”
Wakati kaburi inaomba mwili wa mwamini, kweli hapo kaburi inapata ushindi. Kuna uchungu katika kufa.
Eti, wewe umeisha poteza mupendwa wako?
Unakumbuka hiyo chozi la uchungu uliovuisha.
Hauliliye yeye aliye kufa, bali, unakumbuka wale walioachwa pia unaona picha ya namna mwili huo utaenda baki pekee kaburini.

15/ UPIME KWANZA KUFIKIRI, KAMA IKIWEZEKANA, KUSIWE TENA WALE WATAKAO HAMISHWA, HAKUNA TENA MAJISHI, KUFA KUMESHINDWA. Ukweli gani mtamu na faraja gani hii.

16/ Aya ya 56  “Basi uchungu wa mauti ni zambi; na nguvu ya zambi ni sheria.”
Uchungu wa mauti ni zambi, na hii ni zambi ya mutu wetu wa zamani.
Ni hiyo uchungu wa mauti, unaambatana na mutu wetu wa zamani anayekuwa na zambi hiyo ya asili.
Na nguvu ya zambi hiyo ya asili ni sheria.
Sababu sheria ndiyo inaonesha wazi kwamba tunayo zambi hiyo ya asili, lakini kuna kusudi lingine linalo tusukuma ili tuseme kwamba nguvu ya zambi ni sheria.
Lakini, ukijitahidi kuheshimu sheria, kwa muda kitambo, wewe unaheshimu sheria hizo kumi na tunda ya hiyo itaonekana sawa matendo mazuri ya kibinadamu, lakini kumbuka kwamba yote ni takataka ya uchafu, hata haki zetu zote tunazo zitimiza kwa nguvu yetu sisi wanadamu ni takataka mbele ya macho ya Mungu na Mungu hazikubali, anazitupa mbali.

17/ Aya ya 57 “Lakini asante kwa Mungu ambaye anatupa sisi kushinda kwa Bwana wetu Yesu Kristo.”
Shukrani kwa Mungu, inayosemwa: Asante kwa neema ya Mungu.
Neno lingine ya muhimu ni neno “anatupa”
Neno “Neema” na “anatupa” vyote viwili vinaambatana pamoja.
Kushinda kwetu tunaopata kwa njia ya Neema ya Mungu, si kwa namna tulio ama kwa kitu chochote tunalokuwa nalo, lakini kwa aina ya Mungu na kwa yale Mungu aliofanya kwetu.
Lakini mutu wetu wa zamani anaichukia sana Neema ya Mungu.

18/ Aya ya 58 “Basi, ndugu zangu, wapenzi, musimame imara, musitikisike, mukizidi siku zote kutenda kazi ya Bwana kwa sababu munajua ya kuwa kazi yenu si bure katika Bwana,”
Hapa tunatambuwa ya kwamba wakati tunakaza mecho yetu kwa kuangalia tu iyo kushinda kwetu, inatuletea nguvu katika huduma ama kazi ya Bwana.
18. 1 Musi... inamaanisha wazi: Muwe
Ni shurtisho ya muda huu wa saa hii na inamaanisha : Muwe wenye kusimama imara. 18. 2 Ndugu zangu, wapenzi, hii inamaanisha kwamba ni watu waliookolewa.
Ni wenye kimwili lakini waliokolewa.1 Wakorinto 3: 1 – 3“Na mimi, ndugu, sikuweza kusema na ninyi kama na watu wa Roho, lakini kama na watu wa mwili; kama na watoto wadogo katika Kristo.
Nimewakunywesha ninyi maziwa wala si chakula; kwa sababu mulikuwa hamujakiweza, hata sasa hamukiwezi;
Kwa sababu hata sasa ninyi ni watu wa mwili; kwa sababu kuna wivu na ugonvi katikati yenu, ninyi si watu wa mwili mukienda kwa namna ya watu?
18. 3 Kuna matumizi aina tatu ya Ushindi huo katika maisha ya mwamini.
Nimewakunywesha ninyi maziwa wala si chakula; kwa sababu mulikuwa hamujakiweza, hata sasa hamukiwezi;
Kwa sababu hata sasa ninyi ni watu wa mwili; kwa sababu kuna wivu na ugonvi katikati yenu, ninyi si watu wa mwili mukienda kwa namna ya watu?
18. 3 Kuna matumizi aina tatu ya Ushindi huo katika maisha ya mwamini.
18. 3. 1 Kushimamishwa imara kwa milele
Waroma 16: 25
“Kwake yeye anayeweza kuwasimamisha ninyi sawasawa na Habari Njema yangu na kwa mahubiri ya Yesu Kristo, kama ufunuo wa siri iliyowekwa tangu nyakati za milele,”
18. 3. 2 Kuzaa matunda kwa milele.
18.3.3 Utawa wa milele.

19/ Tunapashwa kusimama imara, tusitikisike,
Neno kusimama imara inamaanisha kuwa na mushimamo.
Neno tusitikisiki nikusema kubaki imara hata pepo mbalimbali zikivuma.
Tunapata tena hii wazo katika Waefeso 4: 14 “hata tusiwe tena watoto, tukitupwa huku na huku na kuchukuliwa kwa kila upepo wa elimu, kwa hila za watu, kwa ujanja, kwa udanganyifu mbaya;”

20/ Mukizidi siku zote kutenda kazi ya Bwana, inamaanisha kuzidisha mara na mara kazi ya Bwana.
Ni wengi wakristo wenye tayari wamekwisha kuregea.

21/ Tunapashwa kuwa na lengo, changamoto, na matumaini daima sababu tunajuwa ya kuwa kazi yetu si bure katika Bwana.
Huduma yetu siyo ya bure, isiyo kuwa kitu, ama isiyo na manufaa.


AMEN


N°Ref: KULP - 12/30/1973 / 333 - THE SECRET CONCLUSION OF THIS AGE / 05/24/2020

Tuesday, May 12, 2020

ETI MWILI WA KIMUTU WA BWANA YESU KRISTO ULIKUWA TOFAUTI? / WAS THE HUMAIN BODY OF JESUS CHRIST DIFFERENT?

Banana Leaf Artwork by Radio Kahuzi Club Members





     ETI MWILI WA KIMUTU WA BWANA YESU KRISTO ULIKUWA TOFAUTI? 
     WAS THE HUMAIN BODY OF JESUS CHRIST DIFFERENT?
       January 17, 1965   
       Pastor Henry F. Kulp 




Waroma 8: 1 – 4 
“Sasa, basi hakuna hukumu ya azabu juu yao walio katika Yesu Kristo, wasiotembea kufuata maneno ya mwili, lakini kufuata maneno ya Roho. 
Kwa sababu sheria ya Roho ya Uzima ulio katika Yesu Kristo imenifanya huru kwa sheria ya zambi na kufa. 
Maana yale yasiyowezekana kufanywa kwa sheria, kwa sababu ilikuwa zaifu kwa sababu ya mwili, Mungu alituma Mwana wake mwenyewe katika mfano wa mwili ulio wa zambi, na kwa sababu ya zambi, alihukumu zambi katika mwili; 
Hata haki ya sheria itimizwe ndani yetu, tusiotembea kufuata maneno ya mwili, lakini kufuata maneno ya Roho.”
Tulifunzwa siku zilizopita kwamba siku ya hukumu ya mwamini, ilifanyika tangu miaka iliyo pita elfu mbili na makumi mawili pale kwa Musalaba wa Kalivari.  
Hukumu ya zambi zetu ilikuwa juu ya Bwana Yesu Kristo, ni kwa sababu ya hiyo mwamini hawezi kuhukumiwa tena juu ya zambi, sababu tayari zambi zake zilikwisha kuhukumiwa. 

1/ Tulitambua na kuona kwamba kuna sheria mbili: 
Sheria ya Roho ya Uzima ulio katika Yesu Kristo na sheria ya zambi na kufa.  
Kila mwanadamu anayezaliwa hapa chini duniani, anazaliwa akiwa chini ya sheria ya zambi na kufa.
Sheria hiyo ilianzishwa na Adamu na iliendelea tangu hapo. 
Lakini, wakati mtu anapookolewa, sheria ya Roho ya Uzima inaanzisha kazi ya Roho Mutakatifu ndani ya roho ya mwamini, na kwa hiyo, Roho Mutakatifu anayekuwa Roho wa Uzima, anatupatia uzima na palepale anatuondosha toka mauti. 
Kwa hivyo, sheria ya Roho ya Uzima ulio katika Yesu Kristo unatufanya huru kwa sheria ya zambi na kufa. 

2/ Musingi gani unao hakikisha kutokuwa na hukumu, na kupokea Roho ya Uzima unaotuweka huru na sheria ya zambi na kufa?  
Aya ya tatu yasema hayo mambo yote? 
 Eti ni kwa njia hiyo ndio Mwenyezi Mungu alimutuma Mwana wake wa Pekee katika mufano wa Mwili ulio wa zambi, na kwa sababu ya zambi, ili ahukumu china  na nyama ya mwili. 
Uzaifu wa mwili unaomba tu Mungu atende. 
Uzaifu wa mwili unakuwa ukuta mkubwa ama kiambazi na nguzo kubwa la ajabu linalo zuiza kila nguvu na tendo njema ya mwanadamu, lakini iyo siyo kibambazi ama nguzo mbele ya Neema ya Mungu. 

Hiyo inatuonesha wazi umuhimu wa aya ya Waroma 8: 3  

3/ Wakati nilipofika kwa Altoona kwa mara ya kwanza, kwa miaka zilizo pita, kanisa nililokuwa naongoza kama Muchungaji, kanisa lilo lilikuwa na makusanyiko ya maombi kwa kila juma na makanisa mengine jirani. 
Kama desturi yetu ya mukusanyo wa maombi, ninakumbuka siku moja kwa saa za maombi yetu ya kila juma, wakati wa mukusanyo wetu wa usiku, tulikusanyika katika moja ya makanisa yale yaliyokuwa pana zaidi kuliko yengine, na hapo tulipokuwa tukizungumuza mawazo yakawaka sana na kuelekea Tabia ya madini yanayochunga desturi na nyengineo yanayofuata maendeleo ya mambo ya kisasa. 
Na Muchungaji wa lile kanisa lililotupokea kwa maombi ya usiku ule, yeye alikuwa wa tabia ya watu wanaoacha wengine huru kwa misemwa, tabia, hata matendo, naye akaleta wazo hili: Ku fwatana na kuzaliwa na bikira, eti munioneshe andiko fulani ya Mutume Paulo inayosema kama ilikuwa lazima Bwana wetu Yesu Kristo azaliwe na bikira. 
Maandiko tunayoyasoma leo haingelikuwa yakusikilika kama hakungelikuwa mwandishi aliyeshurulika kuonesha kwamba KRISTO ni MWANA wa Mungu aliyekuja duniani bila mchango wa baba wa hali ya kimitu. 
Ukweli ni kwamba Mutume Paulo hangeli waza umbalimbali na hayo, yeye aliamini tendo hili kwa roho yake yote. 
Yeye angelikuwa hakutumikisha musemwa: kuzaliwa na Bikira, lakini hata hivyo matunzaji yake ingelikuwa bila maana na ya watu wasio na busara na akili kama hangeliamini bila hata shaka yeyote kwamba Mwokozi wetu Yesu Kristo alizaliwa na Bikira. 

4/ Neno la kwanza ni kwamba Mungu Baba alimutuma Mwana wake Mwenyewe katika mufano wa Mwili ulio wa zambi  
Tufahamu kweli kwamba haisemwi: 
Alituma Mwana wake wa pekee katika Mwili ama katika mufano wa mwili, lakini katika mufano wa Mwili wa zambi. 
Mwili wake ulikuwa kweli mwili halali, mbele na kiisha Ufufuko wake, kama vile inavyosemwa kweli katika injili ya Yoane 1: 14  
Yoane 1: 14 
“Na Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu, tukatazama utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee akitoka kwa Baba, amejaa neema na kweli.” 
Neno likavaa Mwili, likakaa kwetu. 
Mwili wenye Bwana wetu Yesu Kristo alilokuwa nalo, lilikuwa  la nyama na maumbile ya kimutu, ikifanana kwa namna ya kuonekana kwake kama mwili wa kimutu, lakini haikufanywa katika mufano wa mwili wa zambi. 
Kulikuwa tofauti mkubwa kati ya Mwili wake na mwili wetu.   
Inatupasa sisi tujifunze hiyo tofauti ama umbalimbali.

5/ Tuchunguze Maandiko Matakatifu, na tuoneshe kwa mwangaza wa Biblia, kwamba Mwili wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo ulikuwa tofauti na mwili wetu
Matendo 2: 23, 24 
“huyu alitwaliwa nanyi kwa shauri lililokusudiwa, na kwa  kujua kwa Mungu tangu zamani, nanyi mulimsulibisha, mukamwua kwa mikono ya watu wabaya. 
Lakini Mungu alimfufua, akilegeza uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao.” 
Tuchunguze vema maandiko haya: 
Haikuwezekana ashikwe na mauti. 
Tujiulize kwanza, eti neno hili linaweza semeka kwa mwili wetu huu wa kibinadamu? Hapana hata kidogo! 
Kiisha anataja ufunuo wenye Bwana wetu Yesu Kristo anasema juu ya namna na hali ya Mwili wake katika aya ya makumi mbili na saba (27). 
“Kwa maana hutaniacha Roho yangu katika Hadeze, Wala hutatoa Mtakatifu wako aone uharibifu.” 
Ni mwili gani huo usingeliweza kuoza, ama kuona uharibifu? 
Ni kwa sababu ya hiyo Biblia inatufundisha kwamba nguvu zote za uwezo wa kufa unaokuwa ndani ya miili yetu, haikuwa ndani ya Mwili wa Bwana wetu Yesu Kristo. 

6/ Kama ingelikufikia kwenda kwa Kalvari kama Muganga wa kufanya utafiti na kushusha miili yote tatu, hiyo wa Bwana Yesu na yale miwili ya wale wajambazi waliosulubishwa pembeni ya Bwana wetu Yesu Kristo, na hapo wakuambie uandike Kitambulisho cha kiini ya kifo cha hawa watu tatu, miili yote tatu inafanana kwa namna ya inje, sababu wote watatu walipata malipizi ya kifo ya namna sawa. 
Wangelikuambia ulete na kuandika kiini cha kifo chao, utapata matukio mbalimbali kwa sababu, majambazi hawa wawili waliokufa pembeni ya Bwana wetu Yesu Kristo walipata kufa kwa sababu ya vidonda na ukosefu wa damu. 
Lakini Bwana wetu Yesu Kristo, wakati alipoona kwamba yote yametimia na kwamba sasa Yeye yuko tiyari, na saa imefika, akotowa Roho yake.  
Yoane 10: 18 
“Hakuna mutu anaye uondoa kwangu, lakini mimi mwenyewe ninautoa. Nina uwezo kuutoa, na ninauwezo kuutwaa tena. Agizo hili nililipokea kwa Baba yangu.”  
Wakati hawa wajambazi walikuwa wakienda kufa polepole, Bwana wetu Yesu Kristo alikuwa na mamlaka juu ya Uzima wake. 
Tujuwe kwamba Yeye hakuweza kuwa na mamlaka juu ya uchungu na mateso aliyoyapata hapo msalabani kwa wakati ule wa uzaifu na mateso makali. Lakini kwa saa ya mwisho aliinama kichwa chake na kutowa Roho. 
Yeye hakutoweka katika uzaifu mkubwa hata kufikia kiwango cha kutokuweza kusema neno, kwa sababu baada ya saa sita kwa Musalaba Yeye alipaza sauti kubwa.
Mwili wake haukukufa kwa namna ya kawaida. Tusome Luka 23: 46 
“Yesu alipolia kwa sauti kubwa, akisema: Baba, katika mikono yako ninaweka Roho yangu; na alipokwisha kusema maneno haya akatoa Roho.” 
Tuone pia 
Yoane 19: 30 
“Basi wakati Yesu alipopokea ziki, akasema: Imekwisha; akainama kichwa chake, akatoa Roho yake.” 
Kichwa chake haikuwa ya kuinama na kusegemea ubavuni saa zile zote kama ya mutu muzaifu sana.  
Hapana Bwana Yesu alikuwa akiongoza uzima wake hata saa alipo toa Roho. 

7/ Sehemu hii ingestahili kuwa kwa nafasi ya mwanzo, wakati tulikuwa tukizungumuzia jambo la kuwa huru kwa sheria hili ama lile. 
Jameni tutwae mfano moja muzuri: 
Twa tazama kinakidudu kwa udongo, nayo ni ndogo na yenye kutambaa, watu wengi wanakachukia na kukazarahu, lakini kidudu hiki kina uhuru wake wa kutambaa. 
Kidudu hiki kina uwezo wa kutambaa na kupanda kwenye muti, kutambaa kwenye udongo, lakini hakiwezi kujiondosha kwenye udongo ili kiende angani, wala hakiwezi kuruka hewani. 
Kinabana kwenye udongo sababu ya uwezo na kuvutiwa kwa nguvu za sheria za arzi. 
Lakini kiisha muda kitambo, hii kidudu kinajificha katika bahasha lake na kutoka kule kiisha punde kidogo, tayari kinatoka kule kikiwa sasa kipepeo kirembo 
Kwa sasa kina mabawa na kuweza sasa kupinga kuvutwa na nguvu za arzi.
Hakibaki tena tu kwa udongo, lakini kwa sasa kinaweza kutoka kwenye udongo na kuruka hewani. 
Sheria ya kuvutwa kwa arzi haikuondolewa, lakini kuna sheria mupya inayoumbwa ndani. Ni sheria ya kuruka juu na mabawa yakibinafsi.
Ni sawasawa mambo inayo tufikia: 
Sheria ya zambi na kufa inavunjwa na Sheria ya Roho na Uzima ulio katika Yesu Kristo. 
Tumewekwa huru kwa sheria ya zambi na kufa na ni kwa sababu ya hii ndio maana hakuna tena hukumu ya gazabu juu yetu sisi tulio katika Yesu Kristo. 

8/ Turudiliye majifunzo yetu kuhusu Mwili wa Bwana wetu Yesu Kristo, nyama ya mwili wake
Imesemwa kweli kwamba Yeye hakutenda zambi.  
Luka 1: 35
“Malaika akamujibu akamwambia: Roho Mutakatifu atakuja juu yako, na nguvu zake Mungu aliye juu zitakutulia kivuli; kwani kile kitu ambacho kitazaliwa nawe, kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu.” 
Tuchukuwe katika aya hii, msemwa unaosema: kwani kitu kile ambacho kitazaliwa nawe, kitaitwa kitakatifu, hapo inaoneshwa kile kitu kitakatifu kilichozaliwa. Ni kitu kitakatifu, ni kitakatifu cha umilele.   
Mwili wake haukuwa hata na alama moja ya zambi. 
Kuna kundi ya wateologia wamoja wa siku zilizo pita walikuwa wakizungumuzia juu ya neno ya kwamba ilikuwa ingeliwezekana Bwana Yesu Kufanya zambi. Hapana tena hapana hata kidogo, jambo hili haliwezekani. 
Kwa Yeye kupata kutenda zambi, ilikuwa sharti ndani yake mupatikane sheria ya zambi na kufa ili apate kutenda zambi. 
Lakini hakukuwa ginsi mambo haya yawezekane, sababu hakukuwa zambi ndani yake. 

9/ Sababu gani tunalo juhudi na kujitowa sana kuonesha kwamba Mwili wa Bwana wetu Yesu Kristo, na nyama ya Mwili wake haukuwa na sheria ya zambi na kufa? 
Sababu gani tunapenda kusema kwamba Yeye hakuwa na Mwili wa zambi? 

Tupate maelezo maalum katika Waroma 8: 3 
“Maana yale yasiyowezekana kufanywa kwa sheria, kwa sababu ilikuwa zaifu kwa sababu ya mwili, Mungu alituma Mwana wake Mwenyewe katika mufano wa mwili ulio wa zambi, na kwa sababu ya zambi, alihukumu zambi katika mwili;” 
Kwa sababu ya zambi, alihukumu zambi katika mwili. 
Hiyo inamaanisha nini? 
Neno kwa sababu, ama kwa fasi na nafasi ya kitu fulani” inamaanisha kwamba: 
Yeye alifanywa zabihu juu ya zambi zetu. 
Na Yeye alihukumu zambi, alihukumu gazabu ya zambi.
Nafasi gani alihukumu gazabu ya zambi? 
Katika Mwili wake. 
Yeye alikuwa na Mwili pasipo zambi. 
Sisi tuna mwili wa zambi. 
Na wakati Mungu anahukumu zambi, anaihukumu katika mwili.
Lakini Mwenyezi Mungu angelihukumu zambi katika mwili sisi tungelipotea milele. 
Kwa hiyo, Mungu alifanya nini kwa kutuokowa? 
Mungu alikamata zambi inayokuwa katika miili zetu na kuitia katika mwili wake, Mwili wake takatifu na Yeye alikufa ili alipe malipo ya zambi. 

10/ 1 Petro 2: 24   
“Yeye mwenyewe alichukua zambi zetu katika mwili wake juu ya mti, hata sisi, tukiwa wafu kwa maneno ya zambi, tuwe hai kwa maneno ya haki; na kwa kupigwa kwake muliponyeshwa,” 
Tufahamu hapa kwamba siyo neno “juu” iliyo tumikishwa hapa lakini ni neno “katika”.
Yeye mwenyewe alichukuwa zambi zetu ndani ya Mwili wake. 
Alichukuwa zambi iliyokuwa ndani ya miili yetu.
Mungu alimupatia Mwili, Yeye angelipashwa tu kupata Mwili, mwili ulio takatifu, na Mungu alitia miili yetu ndani ya Mwili wake ili ateswe kwa ajili yetu.  

11/ Wagalatia 3: 13   
“Kristo alitukomboa kwa laana ya torati, akiwa alifanywa laana kwa ajili yetu, kama ilivyoandikwa: Amelaaniwa kila mtu aliyetundikwa juu ya mti;”
Ni neno hili ndilo Bwana Yesu alifanya kwa ajili yako na kwa ajili yangu. Na yote ilikuwa katika Mwili wake. 
Kwa kasikia vema hii andiko, yatupasa kusoma kitabu cha 
Kumbukumbu la Torati 21: 22 
“Na mtu akiwa ametenda zambi inayopasa mauti, naye anauawa, nawe utamtundika juu ya mti; 
Maiti yake haitabaki usiku mzima juu ya mti, lakini lazima utamzika siku ile ile; maana yeye aliyetundikwa amelaaniwa na Mungu; usichafue inchi yako ambayo BWANA Mungu wako anakupa wewe iwe uriti wako.” 
Yesu Kristo alitundikwa kwenye mti, laana ya Mungu. 
Na hapa inasemwa kwamba: 
Kama mtu akitenda zambi inayopasa mauti, nikusema hakuna malipizi na mateso nyingine yenye huu mtu anastahili kupata, isipokuwa auwawe. 
Zambi yake italipwa tu na kifo na yeye anapashwa atundikwe juu ya mti. 
Na yeye anapashwa azikwe siku ile ile, kama sivyo kutakuwa laana itakayotoka kwa Mungu. 
Kwa kweli ni hii Bwana Yesu Kristo aliyobeba.
Sisi sote tulikuwa tunastahili kifo katika miili zetu, sababu sisi sote ni wenye zambi, lakini Bwana wetu Yesu Kristo alichukuwa zambi zetu katika Mwili wake na alituweka huru kwa sheria ya zambi na kufa. 

12/ Sisi pekee hatukuweza kujiweka huru kwa sheria hiyo ya zambi na kufa ni Bwana Yesu Kristo peke yake anayekuwa na uwezo wa kuiondoa. 
Ni Yeye pekee anaye uwezo wa kufanywa zambi kwa ajili yetu. 

13/ Wakolosayi 1: 21, 22
“Nanyi, muliotengwa mbali zamani na mulikuwa adui katika nia zenu, kwa matendo yenu mabaya, amewapatanisha ninyi sasa
Katika Mwili wa nyama yake, kwa kufa kwake, ili awalete ninyi mbele yake, watakatifu na pasipo kilema, wala laumu;” 
Aya hii, inatuambia kwamba sisi tulikuwa wanani, hali yetu ilikuwa lini. 
Sisi kama wakristo inatubidi kila mara tuwe tunakumbuka nafasi gani Bwana Yesu alitutosha na kutuokowa.
Mara kwa mara, wakati tunatenda matendo mazuri kama wakristo katika maisha yetu ya kikristo,  hapo tunakuwa na mawazo na kuzania kwamba sisi ni watu wazuri, tunasahau kwamba Mwenyezi Mungu alituokowa kututosha toka yalala ya zambi, chimo ya uchafu na  zambi na mauti, alituokowa na kutupa zambi zetu mbali sana, ni vizuri  mara kwa mara, tukuwe tunakumbuka hiyo. 

14/ Tuchunguze yanayosemwa kwa aya ya makumi mbili na mbili (22):
Katika Mwili wa Nyama yake kwa kufa kwake. 
Ingelikuwa vema mutambuwe kwamba mwisho wa aya ya makumi mbili na moja kwa kuingia makumi mbili na mbili, kiisha neno “amewapatanisha ninyi sasa”, hakuna mukato ama nugta. 
Hivyo hapo tungelisoma: 
Kwa sasa amewapatanisha katika Mwili wa Nyama yake  
Kwa Musalaba tulipatanishwa katika Mwili wa Nyama yake kwa kufa kwake. 
Njia moja inayo unganisha na kupatanisha Mungu na Mwanadamu ni kwamba Bwana wetu Yesu Kristo kuja duniani na kutwaa mwili wa mutu, na hii inatuonesha kwa makini kwamba Bwana Yesu Kristo angelipashwa tu kuchukuwa mwili wa mutu na kuwa mutu kweli. 
Angelipashwa kuwa na Mwili wa nyama. 
Maandiko matakatifu ni wazi na Mutume Paulo iko wazi kwa neno hili. 
Ni katika nyama ya Mwili wake ndio alilipa lipo kubwa la zambi zetu. 

15/ Tuchunguze sasa misemwa: 
Katika Mwili wa Nyama yake, kwa kufa kwake ili awalete ninyi mbele yake, kwa hali gani? Watakatifu. 
Hii ndilo kazi Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo iko anafanya kwa kila mwamini, kila anaye amini Kufa ya Mwana.  
Kwa njia ya kufa kwake aliondowa makosa na zambi zetu na kutuleta mbele yake tukiwa Watakatifu. 
Tuchunguze neno la mwisho katika aya hii: 
Mbele yake
Mungu Mwana atatuleta mbele ya Mungu Baba, na katika uwepo wa Mungu Baba sisi ni watakatifu, pasipo kilema, wala laumu.
O jameni, tutakuwa Viumbe vya namna gani, wakati Mungu Mwana atatupeleka mbele ya Mungu Baba. 
Hakutakuweko hata alama moja ya zambi juu yetu, hakuta kuwa laumu. 
Zambi zote zimetoweka, hakuna tena siku ya hukumu ya gazabu juu yetu. 
Mara tena hapa tunatambua kwamba hakuna tena siku ya hukumu ya gazabu juu yetu. 
Siku yetu ya hukumu imekwisha toweka. 
Hii ni mambo ya muhimi sana, wakati tunapelekwa mbele ya Mungu Baba, sisi ni WATAKATIFU, PASIPO KILEMA, WALA LAUMU,   namna gani kuwe siku ya hukumu ya gazabu kwa waamini wanaokuwa katika hali hii? 

16/ Katika Miradi ya Mwenyezi Mungu, hakuna kitu kingine chenye kinangojewa kuonekana ndani ya hii muda hadi KUNYAKULIWA KWETU. 
Hakuna miradi nyingine iliyo pangwa. 
Kazi hii nzuri na ya manufaa inaendelea, tendo la kukusanya waamini na kuwageuza kuwa watakatifu, kazi hii kubwa ya Mungu inafanya kila mwamini anaye amini kifo cha Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo anafanywa kuwa Mutakatifu na watu hawa wote wanaonyeshwa kuwa watakatifu, kwa siku hiyo ya kupelekwa mbele ya Mungu Baba. 
Siku Nzuri ya shangwe na Ajabu na Tukufu.  

17/ Tufahamu kwamba Wakolosayi 2: 9 
“Maana katika Yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu kwa mwili.” 
Katika Bwana Yesu Kristo unakaa utimilifu wote wa Mungu kwa Mwili, utimilifu wote wa Utatu Mutakatifu. 
Tuchunguze neno Kwa mwili” 
Siku zilizo pita nilipata kuona tafsiri ama kufafanua iliyonipendeza sana: 
UTIMILIFU WOTE WA MUNGU UNAKAA NDANI YAKE KATIKA MWILI. 
Hii ndiyo ukweli wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo anaye kaa sasa kule mbinguni kwa mukono wa kuume wa Mungu Baba. 
Na Mwili wake wa kimutu, Mwili wenye Mungu Baba aliomutayarishia,
Mwili aliyo pewa wakati alizaliwa Bethleemu. 
Utimilifu wote wa Mungu unaikaa ndani ya mwili wa kimutu. 
Ni tendo la Mastaajabu ya shangwe naya kushangaza kweli.  
Mpaka kwa siku ya leo Yeye ana Mwili ule, Nyama ile. 
Nafsi ya Pili katika Utatu Mtakatifu ni Mutu kweli sawa vile ni MUNGU kweli. Yeye ni Mutu kweli. 
Tuchunguze sasa aya ya kumi (10) 
“Na ninyi mumetimilika katika Yeye aliye Kichwa cha falme zote na mamlaka.” 
Ninyi muko na vyote katika Yeye, mumetimilika katika Yeye. 
Kuwa wakutimilika nikusema hakuna kitu kilicho achwa, hakuna kitu kilicho sahaulika, hakuna kitu kinachokosa. 
Wazo gani nzuri katika KRISTO. 
Yeye anaye ishi Mbinguni. 
Aliye kufa katika NYAMA yake na NYAMA yake njo ilibeba zambi zetu. 
Sisi tunatimilika, hatukose kitu chochote, tumetimilika katika Yeye. 
Ukweli nzuri, tamu na ya ajabu. 


AMEN
 
N°Ref: 01/17/1965 / 285 - WAS THE HUMAN BODY OF JESUS CHRIST DIFFERENT / 05/12/2020