Friday, July 30, 2021

NIA GANI MWENYEZI MUNGU ANAYO KUHUSU KIBURI CHAKO CHA DINI / WHAT GOD THINKS OF YOUR RELIGIOUS PRIDE

Photo by B Smith from the kitchen door


 


NIA GANI MWENYEZI MUNGU ANAYO KUHUSU KIBURI CHAKO CHA DINI / 

WHAT GOD THINKS OF YOUR RELIGIOUS PRIDE 

October 14, 1962

Pastor Henry F. Kulp



 

Waroma 3: 23 – 27 

“kwa sababu wote wamefanya zambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu; wanahesabiwa haki bure kwa neema yake kwa njia ya ukombozi ulio katika Yesu Kristo: 

Naye Mungu amekwisha kumweka awe upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake, kusudi aonyeshe haki yake kwa sababu ya kuachilia zambi zilizofanywa zamani, katika uvumilivu wa Mungu: 

Apate kuonyesha haki yake katika wakati huu, ili awe mwenye haki na mwenye kuhesabia haki mtu anayeamini Yesu. 

Basi wapi tena kujisifu? Kumefungwa inje. Kwa sheria gani? Kwa matendo?

Hapana! Lakini kwa njia ya sheria ya imani.” 

Watu wa dini hawachoke kuwa na mawazo, na wakati mawazo yao yanazidi, wanafika kiwango cha kuzania kwamba Mungu hatendi haki. 

Wanafikia kuzania kwamba Habari Njema kwa watu wote, siyo Habari Njema ya haki. Inamufanya Mungu kuwa sawa mnyonge, asiyekuwa na nguvu ya kulitetea Jina lake. 

Maandiko haya tutakayo jifunza kwa asubui ya leo yatatuhakikisha ya kwamba wakati Mwenyezi Mungu anaokowa nafsi kwa njia ya Kufa na Ufufuko wa Bwana wetu Yesu Kristo, Mungu huyo ni Mungu Mwenye haki na mwenye kulitetea Jina lake kwa sababu anaokoa mwenye zambi. 


1/ Mtume Paulo anatupatia mfano wa watakatifu wa Agano la Kale, namna gani Mwenyezi Mungu alikuwa akitetea Jina lake kwa namna alivyo waokowa watu wa Agano la Kale, akiwahesabu watu wale kuwa wenye haki, ijapokuwa Bwana Yesu Kristo alikuwa bado hajamwanga Damu yake. 

Tukamate mfano wa Abrahamu. 


2/  Maandiko yanasema kwamba Abrahamu alikuwa mtu aliye hesabiwa haki na Mungu miaka elfu mbele Bwana Yesu Kristo kuja kumwanga Damu yake. 

Abrahamu alikuwa mtu wa aina gani? 

Twajuwa kwamba Abrahamu alikuwa mwoga. 


3/  Yeye alitaka kuharibu heshima ya muke wake Sarah kwa kujiepusha na kifo. 

Tayari Mwenyezi Mungu alikwisha kumtaja Abrahamu kama rafiki wa Mungu. 

Kwa kweli Mungu wa Biblia ni Mungu wa aina gani anayekuwa rafiki ya mtu asiye na heshima na mwenye haya? 


4/ Tutwae pia mfano wa Musa. 

Musa alikuwa muuaji, mtu aliyekimbia mahakama, wakati Mwenyezi Mungu alipojionesha kwake na kumutuma aende kumuwakilisha huko Misri. 

Mwenyezi Mungu alimupa Musa jina la “Mtumishi wangu” akimuweka kuwa kiongozi wa Taifa lake kubwa. 

Kiisha Mwenyezi Mungu aliweka vibao vya amri kumi, kwa mikono ya Musa inayojaa damu, na  kati ya amri hizo, amri moja ilisema: Usiuwe. 

Eti tendo lile ni unafiki? Ni Mungu gani awezaye kumusweka mtu muuwaji kutangaza habari hiyo?  


5/ Mwaweza kusema kwamba Abrahamu pamoja na Musa waliokolewa kwa umwangaji wa damu ya sadaka mbadala isiyo na hatia, wakati walipotwaa toleo kwa sadaka na kuichinja kwa kumwanga damu yake. 

Bali, tuchukue muda kidogo kwa kufikiri katika Maandiko ya Waebrania 10: 4 

“Maana haiwezekani kwa damu ya ngombe na mbuzi kuondoa zambi.” 

Kwa mwangaza ya aya hii, jameni niwaulize: 

Namna gani, kwa muda wa miaka 4000, Mwenyezi Mungu alikuwa akitizama zambi kwa sababu  hazikuwa zimeondolewa ? 

Na hapo ningelitamani muweke mafikiri yenu juu ya neno “kuondolewa”.  

Katika Agano la Kale, damu ya ngombe na mbuzi haikuweza kuondoa zambi, kwa kumaanisha kwamba kwa wakati ule zambi hazikuondolewa. 


6/ Tuchunguze pia Maandiko ya Zaburi 32: 1 

“Heri yeye aliyesamehewa makosa yake na zambi yake imefunikwa.” 

Katika nyakati zile, wao walihesabiwa haki. 

Katika Agano la Kale, Mwenyezi Mungu alitenda nini kwa kuwahesabia haki? 

Tambuwa vema yasemavyo: Heri yeye aliyesamehewa makosa yake na zambi yake imefunikwa. 


7/ Tulinganishe sasa yale mawazo na yale tunayoyapata katika Maandiko ya Waebrania 10: 4.

 “Maana haiwezekani kwa damu ya ngombe na mbuzi kuondoa zambi.” 

Zambi hazikuondolewa, zambi zilifunikwa. 


8/ Tuyalinganishe vilevile na Maandiko ya Waebrania 9: 6 

“Basi vitu hivi vikikwisha kutengenezwa, makuhani waliingia katika hema ya kwanza siku zote, wakitimiza mambo ya kuabudu.” 

Yawezekana wengi katikati yenu wanasema: 

Tunatoka kwa kartasi hiki na kwenda kwa nyingine na vivi hivi tukibadili ukurasa mbalimbali za Biblia. 

Ninakubali jambo lile, bali ninawajulisha kwamba ni mazoezi mazuri kwani itawasaidia kupata haraka kitabu fulani cha Biblia, pia ni mazoezi mazuri katika Majifunzo ya Biblia. 

Tuchunguze yanayosemwa katika Maandiko ya Waebrania 9: 26  

“…, lakini sasa, mara moja tu, katika mwisho wa dunia, ameonekana aondoe zambi kwa kujitoa mwenyewe.” 

Siyo jambo la kufunika zambi. 

Katika Agano la Kale, zambi zilikuwa zikifunikwa tu.

Mwenyezi Mungu alikuwa akifunika zambi hadi kufika kwa Kristo, na ni hapo Mwenyezi Mungu aliondoa zambi. 

Aliondoa zambi kwa kujitoa mwenyewe. 


9/ Waroma 3: 26  

“apate kuonyesha haki yake katika wakati huu, ili awe mwenye haki na mwenye kuhesabia haki mtu anayeamini Yesu.” 

Wakati Mwenyezi Mungu anapohesabia mtu haki, anamufanya kuwa safi safi sana pasipo taka mbele ya Mungu, siyo mtu ambaye zambi zake zilisamehewa, siyo mtu ambaye zambi zake zilifunikwa, bali zambi ziliondolewa na mtu anafanywa kuwa mwenye haki sawasawa na haki ya Mwenyezi Mungu mwenye Nguvu zote. 

Mungu anafanya tendo lile katika haki yake, siyo pasipo kufahamu vinyume vyake, bali Mwenyezi Mungu anaona kwamba ni vizuri atende hivyo. 


10/ Mwenyezi Mungu ni mwenye uwezo wa kutenda jambo lenye baraza ya mahakama ya kimtu haiwezi kamwe kutenda. 

Jambo lenye hakimu wakili hawezi kamwe kutarajia kutenda.

Yaweza kuwa jambo la kushtusha na la mastaajabu kuona hakimu kumuachilia mtu aliyehukumiwa na kusema kwamba anakuwa mwenye haki. 

Ni Mungu pekee anayeweza kumgeuza mwenye zambi na kumuweka mwenye haki, na anafanya hiyo katika Kufa, Kuzikwa na Kufufuka kwa Bwana wetu Yesu Kristo. 


11/ Siku iliyopita, nilisoma maonyo makubwa katika Maandiko ya 2 Samweli na ingelikuwa heri tuyasome pamoja, ni hadisi inayojulikana sana katika Agano la Kale, lakini kuna jambo moja watu hawaweze kamwe kuvumbua.  

Ni historia ya Abusaloma mwana wa Daudi. 

Naamini kwamba munakumbuka historia ya Abusaloma aliye uwa mtu.

Uuaji ulitendeka katika jamaa ya Daudi. 

Abusaloma alimurukia ndugu yake na kumuuwa baadaye akakimbia. 

Abusaloma alikuwa mtoto mpendwa wa Daudi na Daudi alikuwa anamupenda sana. 

Abusaloma alikuwa mwenye sura nzuri na wana wa Israeli wote walikuwa wakimpenda, lakini aliishi katika ukimbizi, na Yoabu, mkubwa na kiongozi wa majeshi yeye alipenda Abusaloma arudi, lakini mfalme Daudi hakufanya chochote kile kiwezekanavyo ili Abusaloma arudi. 

Kwa hivi Yoabu alitumia mwanamuke mwenye hekima ili aende kumlilia mfalme Daudi, kusudi Abusaloma arudi nyumbani. 

Kwa hivyo mwanamke huyo alitunga hadisi. 

Naye akasema: 

Mimi ni mujane na nina watoto wanaume wawili.

Watoto hawa wangu wawili waligombana na mmoja akamuuwa ndugu yake. 

Kwa hiyo taifa nzima ikajiinuwa juu ya huyo aliyebaki mzima, wakimshambulia na kuniambia kwamba wanahitaji mimi nimuuwe. 

Magumu ni kwamba, wakimuuwa, mimi nitabaki peke yangu. 

Nitakuwa mujane bila mafaa yoyote. 

Mwanamke huyu alilia akimsihi sana mfalme hata ikafika kiwango mfalme akaamuwa kwamba huyo mtoto hatauwawa, atahepushwa kufa. 

Kusihi na kuomba kwa huyu mama kulikuwa namna hii na ningeliwaomba kuyachunguza: 

2 Samueli 14: 13, 14  

“Mwanamke akasema; kwa nini basi ulifikiri mambo ya namna hii juu ya watu wa Mungu? 

Kwa nini akisema neno hili, mfalme ni kama mmoja aliye na kosa, kwa kuwa mfalme harudishi tena mfukuzwa wake. 

Kwa kuwa ni sharti kwetu kufa, nasi ni kama maji yaliyomwangika juu ya udongo yasiyoweza kuokotwa tena; wala Mungu haondoi uzima, lakini anafanya shauri hata yeye aliyefukuzwa asiwe mkimbizi kwake.” 

Mwanamke huyo alimwambia mfalme Daudi: 

Daudi ulitenda makosa ndani ya maneno uliyoyasema. 

Ulisema kwamba mwanangu atahepushwa kufa sasa je kuhusu mwana wako?

 Yeye amelaaniwa, nawe hupendi kamwe arudi, siyo hayo tu, wewe umekosea watu wa Mungu na umemkosea pia Mungu, kwa sababu Mwenyezi Mungu anawarudisha wale waliomkosea na waliofukuzwa. 

Daudi akasema: Sawa, nitamrudisha Abusaloma. 

Lakini Abusaloma hakusamehewa zambi zake kamwe.

Yeye alikuwa muuaji na Daudi alikusudia kufanya yale Mwenyezi Mungu aliyofanya, na matukio yake yalikuwa gani? 

Abusaloma alirudishwa na kwa mwisho alimufukuza baba yake Daudi kwenye kiti cha ufalme. 

Daudi aligeuka mtu wa kuangaika angaika mbali na kiti cha ufalme na Abusaloma, kiisha kufukuza baba yake toka kiti cha ufalme, alitawala juu ya kiti cha ufalme na ni kiisha tu kufa cha Abusaloma ndiyo Daudi alirudi kwenye kiti chake cha ufalme. 

Ningelitamani muhakikishe na kukumbuka neno hili: 

Hakuna yule anayeweza kufanya yale Mwenyezi Mungu anayoyafanya. 

Ni Mungu pekee aliye Mwenye Haki. 

Daudi alizani kwamba anaweza kutenda yale Mwenyezi Mungu anayotenda, lakini matukio yake ni kwamba aliteseka. 

Wakati unapokusudia kutimiza yale Mwenyezi Mungu anayoyafanya, kwa  kukusudia kuongeza neno lolote kwa miradi ya wokovu, ili watu wawe wenye haki, utajikuta umekumbwa na matatizo kwa sababu wewe hauko Mungu, na huwezi kamwe kutenda yale Mwenyezi Mungu anayoyatenda.  


12/ Tuchunguze sasa Taifa la Israeli ilikuwa namna gani wakati ilipokuwa chini ya sheria, wakati Mwenyezi Mungu aliwahesabu kuwa wenye haki akifunika zambi zao kwa damu ya toleo ya sadaka.  

Tuone kiwango gani Mwenyezi Mungu aliwahesabu kuwa haki. 

 Mwenyezi Mungu aliwakombowa toka Misri, akawafungulia njia katika Bahari Nyekundu, katika safari yao walikuwa wakinungunika na kulaani Jina la Mungu, pia walikuwa wakichunga miungu katika masanduku zao, hata wakati walipokuwa wakila kondoo aliyechomwa kwa pasaka ya mapito. 

Wana wa Israeli walikuwa wakizunguukwa na Mataifa yenye ilikuwa ikiabudu Shetani na mapepo mengine mbalimbali. 

Siku moja, wana wa Israeli katika safari yao jangwani, walifika katika pwani la Moabu, kwa njia panda ya Yeriko na ya Yordani. 

 Na ilikuwa kiisha wana wa Israeli kupiga vita kali na wa Amori na kuwaangamiza sana, na habari  hiyo ilileta woga kwa wana wa Moabu. 

Na mawazo ya wana wa Moabu ilitiwa woga kuona namna wana wa Israeli watafika pale na kuwafwagia kwa mara moja. 

Katika siku zile mfalme wa Moabu jina lake lilikuwa Balaka, naye kwa woga na kuharikisha akakwenda kumwona mtu moja jina lake Balama. 

Mtu huyo Balama alikuwa akijulikana kama nabii katika eneo lile. 

Mfalme Balaka akakwenda kumwona Balama akimusifu akisema kwamba anaushuhuda wake kwamba yoyote yale Balama analaani yanalainiwa kweli na yoyote yale Balama anabariki, yanabarikiwa kweli. 

Mfalme Balaka akamtolea Balama heshima na mali mengi na kumuomba awalaani wana wa Mwenyezi Mungu. 

Mwenyezi Mungu akamtokea Balama na kumuagiza asifanye yale anayoombwa kufanya. 

Hatuta poteza wakati tukiwaambia namna ngamia ilizungumuza na Balama na mambo yote yaliyotendeka. 

Natamani niwapeleke pole pole kwa kiini ya historia hii. 

Kiini ya historia hii kwetu ni kwamba tutambuwe ya kuwa wana wa Israeli walikuwa wenye zambi na Mwenyezi Mungu aliwabariki katika neema yake pahali pa kuwalaani katika haki yake. 

Ni vigumu kutambuwa kwa nini ilimushinda Balama kupata maneno yanayoweza kulaani Israeli.  Hapa tuna hotuba ya Balama yeye pekee: Na anayesemwa hapa ni Mwenyezi Mungu.

Hesabu 23: 21 

“Hakutazama uovu katika Yakobo, 

Wala hakuona ukaidi katika Israeli; 

Bwana Mungu wake ni pamoja naye, 

Na sauti kubwa ya mfalme ni katikati yao.” 

Aya hii ni ya ajabu na maalum sana.

Kwa kusema kweli, uovu ulikuwa katika Yakobo, lakini Mwenyezi Mungu alikataa kuyaona, na kweli  katika Israeli, wengi walikuwa katika njia ya upotevu, lakini Mwenyezi Mungu hakuyatazama. 

Kwa kweli hangaliweza kuyatazama, kwa sababu hangaliweza kufanya hivyo. 

Mwenyezi Mungu hatazami zambi za wale wenye wanaomwamini. 

Mwenyezi Mungu hatazami zambi za wale wenye anao wahesabia haki. 


13/ Hesabu 23: 19, 20 itatusaidiya kufikia kiwango cha neno hili.

“Mungu si mtu aseme uwongo; wala mwana wa mtu, ajute, 

Amesema naye hatalifanya? Au amenena naye hatalitimiza? 

Tazama, nimepewa amri kukubariki; 

Naye amebariki, na siwezi kuligeuza.”  

Mutambue kwamba mimi Balama nililazimishwa kubariki, hata nikiagizwa maneno toka kwa Mungu, maneno nitakayobariki nayo Taifa lile.  

Na kwa huyo mwenye Mungu anambariki, mimi sina la kufanya hata siwezi kuligeuza. 

Mwenyezi Mungu alibariki Israeli, Mwenyezi Mungu alihesabia Israeli kuwa yenye haki. 

Mshtuko gani wa raha unaotiwa na neno hili katika mioyo yetu. 

Ni Mwenyezi Mungu pekee aliye mwenye Haki na ni yeye pekee anayehesabia Haki wale wanaomuamini. 


14/ Tuchunguze sasa sehemu ya mwisho wa Aya hii ya Waroma 3: 26, 27 

Inayosema kwamba: 

“…Ni Mwenyezi Mungu ndiye anayehesabia haki mtu anayeamini Yesu.

Basi wapi tena kujisifu? Kumefungwa inje.”  

Lakini kama vile munavyo fahamu, watu wa dini, hawapendi kufahamu maneno haya, wao wanazania kufanya tendo fulani ili wawe wenye kustahili na kuwa wenye samani fulani kwa mecho ya Mwenyezi Mungu.        

Kuna wengine watu wanao ambia wenye zambi watolee Mwenyezi Mungu roho zao. 

Muniruhusu kuwapa swali moja: 

Faida gani Mwenyezi Mungu anaweza kupata na roho yenye kujaa uchafu? 

Roho ya mtu haikubali kusahihishwa, ni mkali sana na yenye kupotoka. 

Siyo lazima kumwambia mtu mwenye anapenda kugeuka mwamini kwamba amletee Mwenyezi Mungu roho yake. 

Kwa kweli ni nini inayompasa kufanya? 

Inayompasa kufanya ni kuamini Maandiko Matakatifu Neno la Mungu kuhusu Damu ya Msalaba, na kuhusu kufa kwa Bwana wetu Yesu Kristo.  

Ni kwa yule mwamini, mtu aliyeokoka anayekuwa sasa na roho iliyozaliwa na kufanywa upya, ni huyo anayeweza kuombwa kumtolea Mwenyezi Mungu roho yake. 

Tumeokoka kwa kuamini ushuhuda wa Mwenyezi Mungu kuhusu Mwana wake, Kufa kw


15/ Jameni tuwaoneshe kitu kingine cha lazima sana tunachokipata katika Waraka wa Yoane. 

Yoane 3: 14, 15, 16   Mwenye kuzungumuza ni Yesu Kristo.

“Na kama Musa alivyonyanyua nyoka jangwani, vivyo hivyo sharti Mwana wa watu anyanyuliwe, ili kila mtu akimwamini asipotee, lakini awe na uzima wa milele. 

Kwa maana Mungu alivyopenda ulimwengu, hata kutoa Mwana wake wa pekee, ili kila mtu akimwamini asipotee, lakini apate uzima wa milele.” 

Aya hii inatangulia aya inayojulikana na watu wote katika Biblia Yoane 3: 16 Mfano huu wa Musa akinyanyua nyoka jangwani inamaanisha  kawaida ya mafundisho juu ya wokovu kwa imani, kwa njia ya kuamini tu.  


16/ Wana wa Israeli walifanya safari ndefu toka Bahari Nyekundu hadi mpaka wa Edoni, njia hii ndefu iliwachokesha mno, wakaanza kunungunikia Musa na Mungu, Mwenyezi Mungu akawatumia nyoka wakali na wenye sumu mbaya, wakauma watu wengi na wengi kati ya watu wakafa. 

Watu katika hali ya kujuta na kutubu  na kutambuwa zambi na makosa yao wakamjia Musa  wakimuomba awaombee huruma kwa Mwenyezi Mungu, Musa akawaombea kwa Mungu, na Mwenyezi Mungu akajibu kwa njia yenye kuwa kweli kama ya mtu mwenye akili yake siyo timamu. 

Kwa sababu Mungu alimwambia Musa ajenge nyoka ya shaba, na aiinue kwa muti, na mambo yatatendeka kama ifwatao: 

Kila mtu atakaye umwa na nyoka, na atakaye inua mecho yake na kuangalia nyoka ya shaba, ataponyeshwa.  


17/ Tupate fundisho kwa jambo lile: 

Neno la kwanza ni kwamba hakuna mtu aliyeambiwa ajenge dawa. 

Hakuna yule aliyeombwa kutokotesha hata dawa fulani ya majani. 

Ama kujipakaa mafuta fulani. 

Hawakupashwa kupigwa hata shindano fulani. 

Hawakupashwa kufanya hata neno moja. 

Walipashwa kuacha mbali dawa yote itakayotoka nyumbani mwao na kutumainia tu kwa dawa kutoka kwa Mungu. 

Wanadamu waliumwa na nyoka ya zambi. 

Wataponeshwa namna gani na hiyo kidonda? 

Ni kifo tu kinachowangojea wakiwa na kidonda chao, isipokuwa Mwenyezi Mungu mwenyewe awape dawa. 


18/ Tena katika hiyo jangwa, watu hawakuambiwa wajisaidiye wao kwa wao, waliombwa tu kuinua macho yao kuangalia nyoka iliyonyanyuliwa juu ya muti. 

Kwa siku zetu za leo, kungeliundwa mashirika ya kibinadamu na kuandikisha watu wengi watakaojitowa kwa kusaidiya wale walioumwa na nyoka, lakini Mwenyezi Mungu hakuwaambia watu wasaidiane wao kwa wao. 

Hawakutumwa kuunda mashirika ya masaidio ya kijamii, HAPANA, waliambiwa tu kutazama nyoka ya shaba.  


19/ Neno la tatu ni kwamba: 

Haikuombwa kwa watu walioumwa na nyoka kupigana na nyoka. HAPANA. 

Iliwapasa tu kuinua mecho yao kutizama nyoka ya shaba. 


20/ Jambo la ine ni kwamba: 

Watu waliokuwa kwa mipaka ya Edoni, baada ya kuumwa na nyoka, wao hawakuombwa kuanza kuelekeza maombi yao kwa nyoka. 

Sisi hatuombwi kuomba tukielekeza maombi yetu kwa nyoka ya shaba iliyo inuliwa, tena kabisa haiombwi kwa mwenye zambi kuomba kuhusu wokovu wake. 

Kristo alikufa ili alete wokovu, yafaa tu kuamini, hapana kuomba kuhusu wokovu. 


21/ Neno la tano: 

Mwenyezi Mungu hakuwaambia wajitenge na yale nyoka ama wa wabebe inje na kuwauwa wote. Mungu hakuondosha yale nyoka. 

Mwenyezi Mungu aliwapa dawa katika hali ileile na Katika mtanziko huo, na dawa hiyo ilitolewa tu kwao, na ilikuwa kuinua mecho na kuangalia tu nyoka wa shaba aliyeinuliwa juu ya muti.  

Mwatambua, hakuna lengo la kujisifu. 

Wale watu wa wakati wa Musa, mbele ya hizo nyoka, hawakuwa na neno lenye linaloweza kuwasukuma kujisifu. 

Mungu anachukizwa na kiburi. 

Jameni basi wapi tena kujisifu? 

Mwenyezi Mungu hafurahishwi na neno kama yale.  


22/ Kuna aya moja ya manufaa kabisa ndani ya Maandiko ya Yeremia 9: 23 

“Bwana anasema hivi: Mwenye akili asijisifu kwa sababu ya akili yake, wala mwenye nguvu asijisifu kwa sababu ya nguvu zake, wala tajiri asijisifu kwa sababu ya utajiri wake;” 

Kama tunavyo tambuwa inasemwa hapa kwamba watu wasijisifu, lakini umbalimbali na ile, watu wanajisifu siku kwa siku. 

Mwenye hekima asijisifu juu ya hekima yake, kwa sababu hekima ya mwanadamu ni nini? 

Kitambo kidogo inatoweka nayo haikuleta hata surulisho ya mambo mengi. 

Mutu mwenye nguvu asijisifu kwa sababu ya nguvu zake, tumekwisha kuona mara nyingi watu wenye nguvu kupigwa sana. 

Hatupashwi kujisifu juu ya nguvu yetu. Hatupashwi pia kujisifu juu ya utajiri wetu, lakini kwa kweli watu wanajisifu lakini ningelipenda mukumbuke mwaka wa njaa ya 1923, ilikuwa mwaka mugumu sana, sasa hapo kujisifu kulikuwa wapi? Kuliondoshwa. 

Kazi yote ya wokovu ni kazi ya yeye mwenyewe Mwenyezi Mungu, ni Yeye pekee aliye Mwenye Haki na ni Yeye pekee anayehesabia Haki. 

 AMINA    

N°Ref: 10/14/1962/ 249 - WHAT GOD THINKS OF YOUR RELIGIOUS PRIDE / 07/30/2021       

No comments:

Post a Comment