Tuesday, June 30, 2020

NAMNA GANI KUJAZWA NA ROHO / HOW TO BE FILLED WITH THE SPIRIT

    Photo taken by B Smith from the patio



 

 

NAMNA GANI KUJAZWA NA ROHO

HOW TO BE FILLED WITH THE SPIRIT

September 25, 1960 

Pastor Henry. F. Kulp

 

 


 

Waefeso 5: 18 

“Wala musilewe kwa mvinyo, ndani yake ni makelele, lakini mujazwe Roho;” 

Kwa mahubiri yetu iliyopita, kwanza tuliwaambia sababu gani imewapasa kujazwa na Roho, sababu nyinyi  watu muna nafsi na roho  na yote inajaa ukorofi,  kwa sababu  ya hiyo  Mungu Baba aliwawezesha kuwa na mtu mupya, ili mupate kuwa  na mawasiliano katikati yenu na  Mungu. 

Pia, tuliwajulisha kwamba kuna umbalimbali kati ya mambo yanayoelekea Ujazi wa Roho, ama kujazwa na Roho mutakatifu katika nyakati hizi za Mwili wa Kristo, Kanisa leo, na katika Ufalme wa Mungu utakao kuwa duniani.  Katika hiyo nyakati ya Ufalme wa Mungu duniani, Roho Mutakatifu atatawala mutu, akimiliki umtu wake wote na kumuongoza kufanya tu mapenzi ya Mungu.  

Lakini, kwa nyakati hizi za Mwili wa Kristo, Roho Mutakatifu anakuja tu kufanya makao ndani yetu, na Yeye ni Msaidizi tu.

Kwa nyakati ya Ufalme wa Mungu, Roho Mutakatifu anaitwa: Kumwaga kwa Roho Mutakatifu. 

Umbalimbali kwa nyakati za sasa, tunapokea Roho Mutakatifu anayefanya makao na kuishi ndani yetu. 

Anaitwa tena : Ubatizo wa Roho Mutakatifu, wakati Bwana wetu Yesu Kristo atakapobatiza watu katika Roho Mutakatifu. Hiyo siyo kwa nyakati za leo, wala kwa siku za leo. 

Sasa, tuone kupitia Wagalatia 3: 26 – 27 

“maana ninyi wote ni wana wa Mungu, kwa Imani, katika Yesu Kristo. 

Maana ninyi wote muliobatizwa na kuingizwa katika Kristo, mumevaa Kristo.” 


1/ Tulibatizwa katika Kristo, na Waefeso 4: 5 

“Bwana mmoja, Imani mmoja, ubatizo mmoja.” 

Kwa siku za leo, hatuna ubatizo ndani ya Roho Mutakatifu, ubatizo tunao leo ni ubatizo katika Kristo Yesu. 


2/ Sasa, ulizo inayo tujia kichwani ni hili: 

Kujazwa na Roho Mutakatifu inamaanisha nini? 

Kila mutoto wa Mungu, kila aliye okolewa anakuwa na Roho Mutakatifu. Ni kwa hiyo njo Roho Mutakatifu anataka kufanya neno moja kwake. 

Haiko jambo linalotukia wakati mutu anajiangusha chini kwa udongo, wakati anapoomba. 

Bali ni kitu chenye Roho Mutakatifu mwenyewe anataka kufanya kwako. 


3/ Hatua ya kwanza ya kutimiza wakati mutu anataka kujazwa na Roho Mutakatifu, tunaipata katika Wakolosai 3: 16

“Neno la Kristo likae kwa wingi ndani yenu kwa hekima yote, mukifundishana na kuonyana kwa zaburi na nyimbo na tenzi za roho, mukiimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu." 

Tunaona hapo, jambo la Neno la Mungu kukaa kwa uwingi ndani ya nafsi zetu. Tu rudie tena katika Waefeso na tusome moja kwa moja maneno haya,  

Hatuvumbue kwamba aya hizi mbili zinaleta  matokeo sawasawa, wakati katika Wakolosayi, tunaombwa kwamba Neno la Mungu likae kwa wingi ndani yetu, na wakati katika Waefeso tunaombwa kujazwa na Roho Mutakatifu. 

Hii inamaanisha nini? 

Katika sayansi ya hesabu, kuna sheria moja ya zamani inayosema kwamba: Mambo inayokuwa sawasawa na nyingine, inakuwa sawasawa moja kwa moja. 

Matokeo ya kujazwa na Neno la Mungu ni sawa na matokeo ya kujazwa na  Roho Mutakatifu … 

Hii jambo inapashwa kuwa wazi na ni ya muhimu sana kujua kwamba: 

Neno la Mungu lijaapo mukristo ni sawa na Roho Mutakatifu ajaapo mukristo. 


4/ Unaweza kusonga juu zaidi na kuona hakikisho ya neno hili katika kitabu cha Waefeso 5: 18 

“Wala musilewe kwa mvinyo, ndani yake ni makelele, lakini mujazwe Roho;” 


  Kujazwa na Roho. 

Tendo kujazwa hapa, linakuwa tendo la kufanywa na, na linafwatana moja kwa moja na neno linaloonesha ni nani anaye tenda tendo la kujaza. 

Kama ingelikuwa tendo la kufanywa na ingefwatwa na jambo la kuwa na, hapo ingelimaanisha milki. 

Na hiyo ingeoneshwa kwamba mpokeaji anajazwa na nini, nikusema anajazwa na Roho Mutakatifu. 

Siyo tatizo sisi tujazwe na Roho Mutakatifu, linalotupasa kujua ni kwamba ni Roho Mutakatifu ndiye anaye tenda tendo lile. 

Ni Yeye anaye jaza, ni Yeye mtendakazi ya kutujaza sisi. 

Anatujaza na nini? 

Anatujaza na Neno la Mungu. 

Ni kusema kwamba kujazwa na Roho siyo jambo la fumbo, la hisia, ama jambo la zoezi la kupoteza mafikili, lakini ni jambo la kujifunza Neno la Mungu, na hapo Roho Mutakatifu anatwaa Neno hili na anatujaza nalo. 

Sisi hatuwezi kufahamu maandiko kama Roho Mutakatifu hatuangazie. 

Na wakati tunapojifunza Maandiko matakatifu, tunaifahamu chini ya uongozi wa Roho Mutakatifu, kiisha anatujaza na Neno lile. 


5/ Watu wananiambia: 

Mimi ninajuwa kwamba Roho Mutakatifu aliniambia nifanye hiki ama kile, kwa kweli, mambo yale yanajaa machafuko mengi. 

Roho Mutakatifu hatumike namna hiyo. 

Roho Mutakatifu hatufundishe kitu inje ya Neno la Mungu. 

Wakati tunapopatikana katika shida fulani na hapo tunaamua kuketi chini na kufikili vema juu ya jambo linalotukumba, tunakumbuka kwamba Biblia inatuambia kwamba tujiepushe na mambo yote ya ibilisi,  ili tusiwe chanjo cha kuangusha ndugu yetu, na kwa hiyo tunageukia kwa yale Maandiko Matakatifu yanasema. Na ni hivi Neno la Mungu linavyo sema. 

Sisi tunapashwa kuwa watu wa aina hii: 

Jambo hili linatoka kwa muovu ama linaweza kuangusha ndugu? 

Eti, katika jambo hili, mapenzi ya Kristo inaonekana ama hapana? 

Kiisha nitafahamu kwamba niko katika makosa, na Roho Mutakatifu itanifunulia hayo kupitia Maandiko Matakatifu, Neno la Mungu. 

Hii ndilo hitimisho kamili la muhimu lenye ninapashwa kufikia.  

Twende tena kuchunguza katika Maandiko mengine ili tuhakikishe kawaida hii: 


6/ 1Wakorinto 2: 15   

“Lakini mwenye kufuata Roho anatambua maneno yote, lakini yeye mwenyewe hatambuliwi na mtu.” 

Mwenye kufuata Roho, ama mtu wa Kiroho. 

Kwa kuwa mtu wa Kiroho, yatupasa kujazwa na Roho Mutakatifu… 

Ninajuwa kwamba ninyi vilevile mumekubaliana nami. 

Mutu wa kiroho anahukumu, anatambua maneno yote. 

Ni kusema anafahamu maneno yote. 

Mutu wa kiroho anahukumu, anatambua na kufahamu maneno yote.

Namna gani anafikia kufanya hivyo? 

Kitabu cha 1Wakorinto sura mbili, kinasumulia tu juu ya Neno la Mungu.

Mtu fulani niwa Kiroho sababu anafahamu Neno la Mungu chini ya uongozi na msukumo wa Roho Mutakatifu. 

Tujuwe kwamba 1Wakorinto 2: 9 inasema:

“Lakini kama ilivyoandikwa: 

Jicho halikuona, wala sikio halikusikia, wala hayakuingia katika moyo wa mutu, Maneno Mungu aliyotengenezea wenye kumupenda.” 

Hapa inaonekana kwamba siyo maneno ya duniani. 

Mwenyezi Mungu anahitaji nini kwangu? 

Mwenyezi Mungu anapenda mimi nifanye nini?

Namna gani mimi nitafahamu kuusu Mungu? 

Hatutaweza kufahamu maneno haya kwa kiasili, sawa vile inavyosemwa kwa aya ya kumi kwamba, Mwenyezi Mungu aliyafunua kwetu kwa kupitia Roho Yake.  

Namna gani alifanya hivyo? 

Kupitia Neno la Mungu. 

Ni kusema kwa kuwa mutu wa kiroho ama mutu anayejazwa na Roho Mutakatifu inafaa Roho mutakatifu akamate Neno la Mungu na atujaze na ile Neno la Mungu. 


7/ Jambo lingine ni kuhusu mtoto mchanga wa kiroho. 

Haiwezikane mukristo mupya, huyo anayemupokea Bwana Yesu punde kidogo tu, haiwezekani huyo kujazwa na Roho Mtakatifu. 

Ni kugumu Roho Mutakatifu kujaza mutu huyo, sababu bado hajajua Neno la Mungu. 

Ni kwa sababu hiyo inaombwa kwa mtoto wa Mungu aliyepokea Bwana Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wake, anaombwa kujifunza Neno la Mungu na kulificha moyoni mwake. 

Mukristo mchanga hawezi hesabiwa kuwa wa kiroho. 

Yeye si tayari kwa kiroho ama kwa kimwili.

Kama yeye ameonekana kuwa tayari kwa kiroho, itamupasa yeye kujifunza maandiko, akiruhusu Roho Mutakatifu kumujaza na Neno la Mungu. 

Imeombwa kwa mukristo muchanga kujifunza Neno la Mungu. 


8/ Twende sasa kuona umbalimbali gani uko kati ya: 

Kuwa uwanja wa kiroho, kuwa kimwili, kujajwa na kutokujajwa. 

Maneno haya yalikuwa yanaleta shida mwingi kwenye kanisa la Korinto.  

1Wakorinto 3: 1 – 2 

“Na mimi, ndugu zangu, sikuweza kusema na nyinyi kama na watu wa Roho, lakini kama na watu wa mwili; kama na watoto wadogo katika Kristo. 

Nimewakunywesha ninyi maziwa wala si chakula; kwa sababu mulikuwa hamujakiweza, hata sasa hamukiwezi;” 

Mpaka hapo, ninyi ni kama watoto wadogo katika Kristo. 

Nimewakunywesha ninyi maziwa wala si chakula, kwa sababu mulikuwa hamujakiweza, na hata sasa hamukiwezi. 

Hauwezi kamwe kujazwa na Roho Mutakatifu kama wewe bado kujazwa na Neno la Mungu.Hiyo ndiyo ukweli. 

Tuone kwamba 2Timoteo 3: 16 - 17  

“Kila andiko limepewa kwa maongozi ya Mungu, na linafaa kwa mafundisho, na kwa kuonya watu juu ya makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa mafundisho katika haki; 

Ili mutu wa Mungu awe mukamilifu, ametengenezwa kabisa kwa kila tendo njema.” 

Hii inatokana na Neno la Mungu, ni hii ni kweli wakati Neno inafundishwa katika kiroho. 


9/ Sasa yote inakuwa sambamba 

Namna gani Mutume Paulo alifikia kiwango hiki? 

Eti Mutume Paulo anatuambia tulifanye? 

Roho Mutakatifu tuliepewa, kama Mutenda kazi, anakamata Neno la Mungu na kuitia katika nia na mafikili yetu. 

Siyo jambo ya mazoezi ya hisia, mazoezi ya furaha ya kupita kipimo yenye hauwezi tena kuongoza, ama upendo wa kilokole, mambo yote inaenda sambamba. 

Kuna jambo lingeni la muhimu lenye ningelipendelea kuongeza hapo na jambo hili tunalipata katika kitabu cha Waroma 8: 18, mahali Mutume Paulo anaposema: 

“Kwa maana ninahesabu…” 

Neno “kuhesabu”  inatoka kwa tendo la “kuhesabia”, ni hesabu kamilifu, ni matokeo ya majifunzo kamilifu kiisha kutazama na uakili wote. 

“Kwa maana ninahesabu mateso ya wakati huu wa sasa kuwa si kitu tukiyafananisha na utukufu ule utakaofunuliwa kwetu.” 

Mutume Paulo anasema: 

Nimetumikisha akili, nia na ujuzi wangu, na Roho Mutakatifu alinifunulia na ufunuo wake ulinituma nifikie kuhakikisha kwamba magumu na shida tunayo kumbwa nayo kwa sasa, si kitu tukiyafananisha na utukufu ule utakao funuliwa kwetu. Na hii ni kweli na ni sambamba. 


10/ Ni kwa sababu ya hiyo tuna mapashwa kazaa yenye tunapashwa kutimiza. 

2Timoteo 2: 15 

“Dumu kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mfanya kazi asiyeona haya, ukitafsiri vema neno la kweli.” 

Tunashurtishwa kujuwa Neno la kweli, na tunapashwa kulitafsiri vema. Hatupashwe kuwa sawa wafanyakazi walio jitaabisha bure. 

Sisi tunapashwa kujiwekea Neno la Mungu na kulichunga mioyoni mwetu na Roho Mutakatifu anaitafsiri kwetu. Na anaitafsiri ndani ya Mawazo na Ufahamu wetu. Hii inaonesha umuhimu wa Mawazo na ufahamu. 


11/ 2Wakorinto 10: 5  

“tukiangusha mawazo na kila kitu cha juu kinachonyanyuliwa juu ya elimu ya Mungu, tukitia kila wazo katika utumwa wa Kristo.” 

Tunaambiwa  kutia kila wazo katika utumwa wa Kristo, ili Neno la Mungu likae kwa wingi ndani yetu. 

Nikusema kwamba, kujazwa na Roho Mutakatifu, inamaanisha kujifunza Neno la Mungu, kuruhusu Roho Mutakatifu alitafsiri ndani yetu, na katika ufahamu wetu, turuhusu mawazo yetu ijae na Neno la Mungu.

 Maneno haya tumeyahakikishiwa tena katika kitabu cha

          Wakolosayi 3: 2. 

“Tieni mafikili yenu juu ya maneno ya juu, wala si juu ya maneno yaliyo duniani,” 

Mupende na mutiye mafikili yenu juu ya maneno ya juu. 

Itawezekana-je kufanya hivyo? 

Ni kupitia tu Neno la Mungu. 

Nikusema hivi: 

Muinue mafikili yenu juu ya vitu vya mbinguni kwa njia ya Neno la Mungu.

Tieni kilaa wazo katika utumwa, ni hapo mutatambua maana ya kujazwa na Roho Mutakatifu. 


12/ HII INGELIPASHWA KUWA KATIKA MUUNDO WA KISARUFI YA   WAEFESO 5: 18. 

MUFANO KUUSU ROHO. 

MFANO KIKOMBE AMA KIKOMBE CHA KIOO KINACHO JAA MAJI

NI KWELI KWETU SOTE KWAMBA NI BOMBA LA MAJI NDIO LIMETIA MAJI KATIKA HIYO KIKOMBE NA KUFANYA IJAE. 

HAINA LAZIMA BOMBA KUINGIA NDANI YA KIKOMBE ILI KIKOMBE IJAE MAJI. 

LAKINI NI BOMBA INAYOFANYA KAZI YA KUJAZA MAJI. 

NI HIVYO HIVYO ROHO MUTAKATIFU ANATUMIKA SAWA NA AYA HII YENYE IKO MBELE YETU. 

ROHO MUTAKATIFU NDIYE MUTENDA KAZI ANAYE TUJAZA, SIYO NA MAJI, BALI NA NENO LA MUNGU. 


13/ Namna gani mawazo hii inapingana na mawazo ya mutu kawaida wa kiroho. 

Mutu wa kawaida anazani kwamba kuomba, kuomba tena kuomba sana hiyo ndiyo kuwa mutu wa kiroho, na anafanya hivi bila hata kuchukuwa muda kidogo ili ajifunze Neno la Mungu. 

Hii tendo inaonesha wazi wazi namna gani watu hawa hawatambui maana ya kujazwa na Roho Mutakatifu. 

Ama namna gani kujazwa na Roho Mutakatifu. 

Kwa kweli maombi ni ya lazima na maana kabisa katika maisha ya mukristo.

Saa zote tunapashwa kuwa katika hali ya maombi. 

Lakini sasa tujiulize, ni nini ya muhimu  kati ya maneno sisi tunapenda kuambia Mwenyezi Mungu, ama Maneno Mwenyezi Mungu anataka kutuambia? 

Kwa kweli, kwa ulizo lile, jibu la kweli ni moja tu. 

Bila ubishi wowote, ni Maneno Mwenyezi Mungu anataka kutuambia ndiyo iko ya muhimu sana zaidi kupita neno sisi tulitaka ambia Mungu.  


14/ Hii ni hoja moja lenye linashikamana na hayo yote: 

2Timoteo 3: 16, 17 

“Kila andiko limepewa kwa maongozi ya Mungu, na linafaa kwa mafundisho, na kwa kuonya watu juu ya makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa mafundisho katika haki; 

Ili mutu wa Mungu awe mukamilifu, ametengenezwa kabisa kwa kila tendo njema.”  

Imesemwa hapa kwamba: 

Kila andiko limepewa kwa maongozi ya Mungu, chunguza vema hapa “Maongozi ya Mungu” 

Ili mutu wa Mungu awe mukamilifu, ametengenezwa kabisa kwa kila tendo njema.  


15/ Hali ya kujazwa na Roho ina matokeo Fulani, na kitabu ya Waefeso inatuonesha wazi namna gani tutakuwa wakati tunajazwa na Roho Mutakatifu, ama tunajazwa na Neno la Mungu.  

Tujifunze sasa matokeo ya kujazwa na Roho Mutakatifu. 

Waefeso 5: 19 – 20 

“mukisemezana ninyi kwa ninyi kwa zaburi na tenzi na nyimbo za roho, mukiimba na kushangilia Bwana mioyoni mwenu; 

Mukishukuru Mungu ndiye Baba siku zote kwa mambo yote, katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo;” 

Hii ingelitafsiriwa ifwatavyo: 

Mukisemezana ninyi kwa ninyi kwa zaburi na tenzi na nyimbo za roho, pahali pa kujizungumuzia binafsi. 

Inatupasa kusemezana moja na mwengine kwa nyimbo za roho. 

Katika maisha ya mwamini, tenzi na nyimbo za roho zinapashwa kuwa na nafasi kubwa tena ya heshima. 

Katika Kanisa Mwili wa Kristo, katika mazehebu yetu hapa duniani, ninashangazwa na kubabaishwa sana na mutu mwenye hajali kuimbia Mungu. Huyo mwenye nyimbo kwake haimwambie kitu. 

Yawezekanavyo hana kipaji cha uimbaji, lakini angelipenda kuimba. 


16/ Sasa tupime kusema kwa ufupi ndani ya dakika moja, kitu gani Mutume Paulo iko anazungumuzia hapo: 

Wasikilizaji walipo musikia Mutume Paulo akifundisha, walitambua palepale kwamba haifai mukristo kulewa sawa mutu mupagani mpaka kufika kiwango cha  ulevi wa mupagani, mwenye  kiisha kulewa na mvinyo  anaanza kuimbia  Bacchus mungu wa pombe, ama Venus(mungu wa mapendo). 


17/ Yakobo 5: 13 

“Mtu wa kwenu ameteswa? Aombe. Mtu amefurahiwa? Aimbe nyimbo.” 

Mtu kati yenu amefurahiwa? Aimbe nyimbo.

Nina uhakikisho kwamba katika maongozi ya ibada ya makanisa za mwanzo, nyimbo ilichukuwa nafasi kubwa tena ya heshima. Vile vile, Bwana wetu Yesu Kristo pamoja na mitume wake kiisha kugawa meza ya Bwana, waliimba tenzi la nyimbo 

Matayo 26: 30 

“Na wakati walipokwisha kuimba, wakatoka inje kwenda mlima wa Mizeituni.” 

Wakwisha kutambua kwamba ni muziki tu wa kikristo ndiyo inachezwa kupitiya ufungo wa msingi wa kinanda? 

   Twawezaje namna gani kuonesha furaha, raha, uzima, , nyimbo za kiroho zinatutia katika raha, pahali pakuwa wenye kuzoufika, wenye huzuni,waliokata tamaa. 

Lakini unaposikiliza nyimbo za kimataifa za siku hizi, sawa hiyo ya upumbafu rock “n” roll inayojaa na vifungo vya sauti kama vya rambirambi na kifo. 

Nilisikia kwamba huko Ungereza, kuna wimbo uliokatazwa sababu ulikuwa umekumba wavijana katika ulevi na furaha za ubatili wa kimwili. 

wimbo ule ulikuwa juu ya kumbukumbu ya jambazi moja alie fariki ndani ya ajali kubwa ya gari. 

Nyimbo zetu za kiroho zingepashwa kujaza mioyo yetu na nyimbo hizo zingelipashwa kujaa na Maneno ya Mungu.  


18/ Tufahamu kwamba tunapashwa imba pia kuchezea Mwokozi wetu muziki wa vinanda katika roho zetu. 

Yawezekana, sisi hatujuwi kucheza vyombo vya muziki, ili vilete sauti nyororo. 

Wengine wetu, kama wakilazimishwa kutowa sauti nyororo kupitia tu vyombo vya muziki, wao watakumbwa na shida, sababu hawataweza lolote. 

Lakini tizama ndugu yangu, kila roho ya mukristo ni kama kinanda na Roho mutakatifu anapulizia singa za kinanda na zinatowa sauti nyororo sana na inafikia sikio la Mungu Baba. 

Tujuwe kwamba tunapashwa imba zaburi, na tenzi na nyimbo za roho. 

Umbalimbali ni nini basi? 

Tenzi ni kwa niaba ya Mungu mwenyewe. 

Nyimbo sawa: “Yesu wangu ninakupenda”, ama, “Mungu wetu musaada wetu nyakati zote”, ama, “Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu Mungu Mwenye Uwezo”, ama “Mimi ni wako, O Mwokozi njia ni yako, Mwokozi wewe ni Mufinyazi, mimi ni udongo” 


Kiisha tuna zaburi:

Zaburi inasindikizwa na muziki wa nzenze, vinanda, na vyombo vyote vya muziki. 

Kiisha tuna nyimbo za roho: 

Nyimbo za sifa na Maabudu 

Mfano, wimbo wa ushuhuda, ninapenda shuhudia makuu Bwana aliyo nifanyia, “Mapendo ilinihimiza wakati sikuwa hata na musaada,…Mapendo ilinitowa kwenye shida,” ama “Mkombozi, nitakushuudia, nimeokolewa na Damu ya Mwana Kondoo.” 

Kiisha tena 

“Ole Damu ilitoka Mwokozi wangu, Mfalme wangu alikufa” 

Ama inaweza kuwa wimbo wa kufariji ama kupana angalisho.

“Amini na utii, sababu hakuna njia lingine” 

Kwa hiyo, mioyo yetu haingelipashwa kujazwa na nyimbo za kitamaduni, lakini ijazwe na nyimbo za roho. 

Ni Yeye anaye jazwa na Neno la Mungu, maana yake anayejazwa na Roho Mutakatifu ndiye anayekuwa akiimba nyimbo za sifa na maabudu kwa Mwokozi wetu Yesu Kristo. 


19/ Mwamini mwenye anajazwa na Roho, ni mwamini mwenye anakuwa mutu wa kushukuru. 

Akishukuru Mungu katika yote katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo. 

Nyakati zingine tunasema kwamba kuna mambo mengine ya shida zaidi inayo tukumba na tunashindwa kushukuru. 

Mambo mazito na magumu kweli. Mambo inayochoma roho zetu na kuvunja nafsi zetu. 

Sawa na mutu aliye pasuliwa mwili wake ili wanganga waondowe kitu kilichokuwa kikimuzoufisha, kumuuma na kumuregeza kwa hali isiyowezekanavyo. 

Mutu huyo atasikia kuumwa kwa visu vya waganga, lakini baadaye atakuwa na wajibu wa kusema asante sababu anakombolewa na hayo maumivu na mateso iliyo mukumba siku nyingi. 

Sasa inageuka kuwa Baraka, aksanti kwa Mungu kwa baraka hiyo. 


AMEN

 

N°Ref: 09/25/1960 / 22 - HOW TO BE FILLED WITH THE SPIRIT / 04/06/2020

Saturday, June 20, 2020

NATHARIA YA SAYANSI YA MABADILIKO Silaha ya Shetani / Theory of Evolution

Photo taken from B. Smith's kitchen window



 

NATHARIA YA SAYANSI YA MABADILIKO 

Silaha ya Shetani

605-2 Theory of Evolution

April 26, 1981

Pastor Henry Kulp





 

Jameni niwasomee Biblia Takatifu katika kitabu cha Mwanzo sura moja na haya yake ya kwanza. 


Mwanzo 1:1

“Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na inchi” 

Tuombe: 

Mungu wetu na Baba yetu uliye juu, tunakupigia aksanti kwa huu ulinzi wako wa upekee unawo onesha kwetu, na kwa makuu yako yote. 

Ingelikuwa razi utufanye sisi sote tusijiwaze ama kusema juu yetu wenyewe, ama kuwa na mawazo juu yetu wenyewe, lakini tufikiliye kujuwa kiwango cha hali tunayokuwamo, na tufikiye kusadikia na kuamini mambo haya tutakayo yaona pamoja, katika Jina tukufu Lenye Nguvu na Uwezo, Jina La Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo , tunaomba, Amina. 


Kwa sasa, tutazungumuza juu ya Natharia ya sayansi ya Mabadiliko, hii inaelekea watu wasioamini Elimu ya kuwa Muumbaji ni Mungu pekee. 

Kitu mbaya siku hizi ni kuona kwamba; hapana watu wote wa sayansi, lakini wamoja wao, na vilevile waadibishaji wengi wanatuambia kwamba hii Natharia ya sayansi ya mabadiriko ni elimu yenye haina maana, ya bure. 

Wao, hawana hata uhamuzi wowote unaotokea kwa miungu yenye wanaoamini. 

Ndugu zangu, tunafuha kubwa kuwaonesha leo kama hiyo Natharia ya sayansi ya mabadiliko ni ya bure ,bila maana yoyote. 

Ni filamu tu tunayo iona na kufwata kupitia televijene zetu. 

Niwaambie, 

Kulikuwa mutu moja wa elimu sana, mutu wa sayansi toka yunivarsti moja inayo julikana sana ulimwenguni, mwenyi presidenti wa zamani wa merikani, bwana Reagan alimualika kwake juu azungumuzie juu ya Natharia ya sayansi ya mabadiliko, lakini mwalimu huyu alifika na kusema kama yeye haamini kweli yale yanayo semeka katika natharia ya sayansi ya mabadiliko. 

Tunaona kamam kuna mengi ya kusema juu ya mabadiliko(Evolution katika kifransa), hii njoo tutasemea leo.



KWANZA TUNA WAO WASIO AMINI MUNGU  

Wao wasio amini Mungu wanasema kwamba, hawaamini Mungu yeyote, hawaamini nguvu yeyote ya kiMungu, 

Wao wanasema kama viumbe ilionekana tu na sisi watu tunakuwa pale, na tunakuwa na ulimwengu wote na anga lote na watu. 

Lakini sasa, kuna wao walio hatari sana ni male tunaweza kuita Watu wa mabadiliko na wasio amini Mungu. 

Wao ni wa hatari sana, 

Wao ni Mapadiri, Ma pastori wanaokuwa katika majifunzo katika YUnivasti za teologia na za bibilia katika ma seminari na wao wanatuzungumuzia yale wanao amini kupitia elimu na nazaria ya mabadiliko, na wanasema wanaamini Mungu muumbaji na wanatumia yanayosemwa katika sayansi ya mabadiliko ili watufasirie maumbaji. 

Wanasema hawana ufahamu kamilifu juu ya kuonesha jinsi mwanadamu aliumbwa, namana gani tunafikia siku zetu za leo, hatujuwe namna Mungu aliumba ulimwengu. 

Lakini ndugu zangu sikilizeni namna haya ya kwanza ya Biblia takatifu inasema, 

Katika mwanzo, wakati hakukukuwa kitu mbele, Mungu aliumba, 

Hii ni ya kwanza, ya mwisho nay a kuhakikisha yenye Mungu aliyuandikia ili atuonyesha namuna gani vyote viliumbwa naye. 

Hii aya ya kwanza inasema tu kwamba katika mwanzo Mungu aliumba 

Basi sasa mimi na wewe ni wajibu wetu kuamini hivyo ao kutokuamini hivyo. 

Sasa, sikilizeni, sababu ni ya manufaa kabisa, 

Wewe hauwezi sema kama umeokoka na wewe hausadiki Mwanzo sura ya kwanza na haya ya kwanza. 

Kama maandiko ya Mwanzo sura ya kwanza na haya ya kwanza haisimami basi Biblia inatikisika. 

Kama Mungu hakuumba kwa mwanzo, basi Biblia haina mafaa. 

Wewe kauwezi kuwa hauamini kitabu cha Mwanzo 1:1  na kusema tu hivi, 

Mutumishi wangu, ama Pastori wangu, kitu tunacho tu cha kufanya ni kuamini tu Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, 

Sasa ulizo, juu ya KUOKOKA, 

Ningelipendelea kuwauliza hivi: 


1/ Namana gani unajuwa kwamba ni Yesu Kristo aliye kuokoa? 

Hii hakikisho nah ii ukweli unaupata wapi? 

Jibu, tunaupata katika Biblia  

2/ Namana gani unajuwa kwamba wewe ni mutenda zambi? 

Ni Biblia inayo tufunuliya sisi mambo hayo. 

3/ Namana gani wafahamu kama Bwana Yesu Kristo alikufa juu ya zambi zako? 

Ni Biblia inayo tu onesha hayo. 

4/ Namana gani wajuwa kwamba Yesu Kristo alifufuka toka wafu juu ya ukombozi wako na Utakaso wako? 

Ni Biblia inayo tuambia neon hili. 

Basi kama wewe unaweza kusema kama Mwanzo1:1 ni hadisi tu yenye watu walijitungia, na unasema kwamba Mwanzo1:1 haisemi ukweli, ni hadisi, sasa 

Namna gani unasadiki kwamba kwa kweli Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo alikufa juu ya zambi zetu? Wajuwa hii kweli? 

Hauwezi kukani sehemu hii na kukubali sehemu ingine. 

Sababu Biblia nzima inaamini katika umoja na ukweli wa Mwanzo 1:1. 

Acha niwafunuliye kitu kimoja: 

Katika mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia, sasa tuone namna gani wao wanao sema juu ya natharia ya sayansi ya mabadiliko wanasema. 

Mabadiliko inasungumuza ikisema kama kwa mwanzo kulikuwa seli moja na ikafwatana na kugawanywa inayo endelea yenye ina itwa Big Bang, 

Kulikuweko seli moja yenye haikukuwa na akili, ilikuabila mawazo yenye inayoenda sambamba, kiisha hiyo seli iligawanyika mara mbili, kiisha hizo vipande viwili katika vipande ine na izo ine katika munane makumi tatu na mbili, makumi sita na ine na vivyo hivyo na kufikia kwako wewe leo!!! 

Lakini kunaulizo yenye kutembea vichwani mwetu, 

Ulizo hili ni lakujuwa namna gani hivi vyote vilianza? 

Hiyo seli inayotajwa ya kwanza nayo vilevile ilitokea wapi? 

Hiyo seli iliundwa vipi na wakati gani? 

Seli hiyo ilionekana kuwa seli lini, na namna gani? 

Kwa mwisho kweli, hata uwaze je, utasema kama tu kulikuwa mwanzo wa vyote.  

Sasa watu wanaosadiki kama kuna mwanzo wa vyote watasema, sawa nani huyu alieumba mwanzo, jibu ni rahisi na inaonesha kama ni yeye MUNGU!!! 

Ile seli ya kwanza ilitokea wapi? 

Utasema kama kulikuwako na mwanzo juu hiyi seli ya kwanza ipate kuanza kujigawa. 

Kwa kweli kulikuwako na Mwanzo wa vitu vyote. 

Tuzungumuze sasa juu ya wakristo. 


WAKRISTO 

Wakristo wanajuwa kwa makini yote kama Mungu yu Hai na Yeye anaishi tangu milele na Yeye njoo Muumbaji wa vyote vinavyo onekana na visivyo onekana, 

Wakristo hawawezi amini hizo mawazo ya upumbafu isiyo na musingi kamili, wao wanaimani tu katika hiyo BIBILIA pekee inasema. 

Biblia inatuambia kwa urahisi na upole wote, Mungu aliumba. 

Kusema kama kiwiliwili kimoja kisiyo na akili, wala mawazo njoo kilijigawanya na kufanya leo hii ulimwengu tunaonawo leo ni mushangazo! 

Tazama kwanza vizuri  mwili wako murembo, Biblia inasema kwa uzuri na upole wote, ALIUMBA, wewe ni kiumbe kirembo kweli, 

Tazama mikono yako. 

Kumbuka wakati kiungo kimoja kinaumwa, ni mwili muzima njoo unausika. 

Biblia inatuambia kwa mustari wa pili, 

Nayo Dunia, Inchi ilikuwa  ukiwa tena utupu, 

Unazani kama hiyo kiwiliwil ikya zahabu, bila akili bila mawazo sambamba ingejigawa na kuunda huyu mutu murembo mwenye ni sisi leo? 

Tazameni mikono yenu, unazani kama kuna chombo cha wanadamu ama kitu kingine kyenye mwanadamu aliunda kyenye unaweza kulinganisha na mkono wako? 

Wewe unajuwa aina moja ya Kamera yenye unaweza kulinganisha na mecho yako? 

Angalia nywele yako, nafsi yako yote, Buongo yako kichwani, nina yapenda, niupumbafu mtupu unatuma watu kusema maneno hayo. 

Sasa, mbele ya kuzungumuza juu hayo yenye iko inje ya natharia ya sayansi ya mabadiliko, ingeliwa vema tusema madogo juu ya  sayansi ya mabadiliko kwa wale wasio amini. 


SAYANSI YA MABADILIKO KWA WALE WASIO AMINI

Tujiuliza eti Bibilia inasema ama inafundisha nafasi moja kama Mungu alitumikisha mabadiliko? 

Haiwezekani Mungu kuumba watu namna hii. 

Tukisoma kitabu cha 


MWANZO 2:3 “Na siku ya saba Mungu alimaliza kazi yake yote aliyoyafanya; akastarehe siku ya saba, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoifanya”

Hapo tunakuta  jinsi Mungu alitumika kazi ya kuumba katika siku saba, ni kusema,  

Mungu aliumba kwa muda wa siku saba.  Tusome sasa 


MWANZO 1:3

“Mungu akasema, iwe nuru; ikawa nuru” 

Tusome sasa haya yake ya sita, pale tunakuta siku ya pili, 

“ Mungu akasema, na liwe anga katikati ya maji, likayatenge maji na maji.

Mungu akalifanya anga, akayatenga yale maji yaliyo juu ya anga nay ale maji yaliyo chini ya anga; ikawa hivyo”. 


Tuone sasa siku ya tatu yenye iko hapa chini kidogo katika masomi: 

 “Mungu akasema , Maji yaliyo chini ya mbingu na yakusanyike mahali pamoja, ili pakavu paonekane; ikawa hivyo. 

Mungu akapaita pale pakavu Nchi; na makusanyiko ya  maji akayaita Bahari; Mungu akaona yakuwa ni vyema. 

Mungu akasema, Nchi na itoe majani, mche utoao mbegu, na muti wa matunda uzaao matunda kwa jinsi yake, ambao mbegu zake zimo ndani yake, juu ya Nchi; ikawa hivyo. 

Ikawa jioni ikawa asubui, siku ya tatu.” 


Sikilizeni kwa makini wandugu!!! 

Mungu akayaumba uoto wa asili, akaumba  miti, akaumba majani,  uoto, yote hii Mungu aliiumba kwa siku ya tatu, 

Sasa, ingelikuwa kama Mungu alikuwa anatumikisha mabadiliko, siku inayofwata ingezaa wa nyama, lakini haikuwa hivyo, 

Tuone basi nini ilipitikana siku ya ine. 

“Mungu akasema, Na iwe mianga katika anga la mbingu ili itenge kati ya mchana na usiku; nayo iwe ndiyo dalili na majira na siku na miaka; 


Munaona, MUNGU anajuwa vyote, ndugu, je unalisadiki? 

Mungu anajuwa yote, unaulizo juu ya hayo? 

Ningelitamani tuangalie pamoja namna gani Biblia ina fafanua maneno haya. 

Mungu alifahmu tangu kale kama watu watakuja na elimu yao ya upumbafu ya mabadiriko, alijuwa kwamba  waubiri wamoja na walimu wamoja wa Biblia wataamini hiyo mafundisho ya ujinga ya mabadiriko na wataanza kusema kama Mwenyezi Mungu alitumikisha mabadiliko. 

Mungu alijuwa hayo yote, 

Tutazame sasa siku ya ine 

Kwa siku ya ine Mungu alifanya nini? 

Tujiulize eti Mungu aliwaza kuumba kitu cha kutokea kwa majani, ama muti, ama uoto?  Hapana. 

 Mungu aliruka hayo yote na kujitegemeza tu na anga, na hapo akaumba Jua, akaumba Mwezi, na Nyota juu ifanya majira na dalili. 

Mbele ya kuumba Nyakati, hakukukuweko nyakati, 

Saa, haikukuwa, na hivyo tunaona Mungu hakuguza tena dunia. 

Unazani kwamba Mungu aliumba JUA na MWEZI juu ya uoto? 

Hapana, ni upumbafu!!! 

Mwenyezi Mungu kwa siku ya ine aliacha kuumba mambo inayo elekea udongo. 

Sasa tuone nini Mungu aliumba kwa siku ya tano. 

Na Mungu akasema: 

“Mungu akasema, Maji na yajawe kwa wingi na kitu kiendacho chenye uhai, na ndege waruke juu ya Inchi katika anga la mbingu. 

Mungu akawaumba nyangumi wakubwa, na kila  kiumbe chenye uhai kiendacho, ambavyo maji yalijawa navyo kwa wingi kwa jinsi zao, na kila ndege arukaye, kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema. 


Sikiliza sasa ndugu yangu, 

“Mungu akavibarikia, akisema, Zaeni, mkaongezeke, mkajaze maji ya baharini, ndege na wazidi katika nchi. 

Ikawa jioni ikawa asubui, siku ya tano. 


Sasa, twende kwa haya ya makumi mbili na ine: 

“Mungu akasema, Nchi na izae kiumbe hai kwa jinsi zake, mnyama wa kufugwa, nacho kitambaacho, na wanyama wa mwitu kwa jinsi zake; ikawa hivyo.

Mungu akafanya mnyama wa mwitu kwa jinsi zake, na mnyama wa kufugwa kwa jinsi zake, na kila kitu kitambaacho juu ya nchi kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema. 

Ndugu zangu, munaona Mungu iko anafanya angalisho kwa vyote anavyo umba, Biblia inasema kwa JINSI ZAKE, KWA JINSI YAKE, KWA JINSI YAKE, hatuoni hapa mugawanyiko ama mugawanyo, hakuna kutoka kwa hii aina na kwenda kwa aina nyingine. 

Sasa ni nini inasemwa juu ya kuumbwa kwa Mutu? 

Tusome sasa haya yake ya makumi mbili na sita, inasema: 


Tusikilize kwa makini sana na angalisho yote  na Mungu akasema tuumbe nini MUTU, tujiulize kwa hiyo Mungu alitumikisha magawanyiko? Hapana 


“Mungu  akasema, na tumfanye mutu kwa mufano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, nan chi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.” 

Tusikilize yenye inasemwa hapa, 

Mungu akasema, Mutu akatawale dunia, 

Kutawala, sawa vile tunavyoona ni kuongoza, kumiliki, 

Mutu aongoze na kumiliki samaki, nyama, mtambaazi  na viumbe vyote vykutambaa. 

Sasa ninaulizo la kuwauliza: 

Ningelipenda kujuwa kama mutu ni mabadiliko ya kutokea kwa kitu kimoja kyenye tayari kilikuwa kiishi ama kupatikana katika dunia? 

Juu ya yenye kuelekea uvuvi wa samaki, sawa vile wengi wanapenda kuwua samaki, ni kama mimi siku moja nikiwa narudi kutokea kwenye shule la Biblia, wengi wenye tuliokuwa nawo pamoja walipendelea kwamba ingelikuwa saa ya kufanya mazoezi ya kimwili, ama gymnastics na tulienda kwenye pwani ili tulowe samaki. 

Sisi sote tulikuw na ndoano, mcheche na tukashuka kwa maji kwenye pwani, ilikuwa ikiitwa “Paradizo” 

Na hapo, kulikuwa tu samaki nyembamba  sana. 

Samaki ilikua nyembamba sana kupita wembamba wenye nilikua nalo. 

Na tulipo fika hapo, tukaona kwamba wale wavuvi va samaki kwa siku nyingi wenye walikuwa pale tangu saa nyingi wenye kusimama, mpaka hivyo walikuwa hawaja pata kitu chochote. 

Mara kwa mara wakati nilikuwa nasafiri niki pita kwa barabara yenye kuwa juu ya ile pwani kwenye walikuwa wanalowa samaki, wakati nilikuwa naona wale wavuvi wakisimama tu wima, ilikuwa inanipa shida sana. 

Nilikuwa nikijiuliza, “Watu hawa wata pata kweli samaki ngapi?” 

Kwa hiyo tujiulize eti watu wanatawala juu ya samaki? 

Aksanti hivi Maandiko inatuambia juu ya wavuvi wa watu! 

Hakuja patikanako mufalme wa dunia nzima, na hivyo vivyo, hakuna mufalme wa samaki kama vile najuwa! 

Wandege vile vile wanatajwa, nini inasemwa juu ya samaki? 

Namna gani munatawala juu ya ndege? 

Namna gani munawanasa? 

Munatumia  singa ya mitego, sivyo, 

Mimi, kwa kweli naogopa nyoka sana, sipende kuiona, heri kweli nikutane na simba, ndege, kitu chochote mbalimbali na nyoka! 

Dada yangu, mutoto wa mujomba alikuwa akitumika katika chamba kubwa la mjomba, na ndani yake kulikuweko miwa, na mara kwa mara wakati alikuwa anatumika amo, alikua anaacha milango wazi 

Vitu nyingi vilikuwa amo na mimi nilikuwa tu nachukuwa kwa mukono wangu fimbo ya kujikinga na nyoka, sababu nyoka iko hatari. 

Na ninajuwa kwamba wengine watu wenye woga walikuwa wanafanya hivyo. 

Sasa tujiulize, munawaza kama watu wanakuwa na mamlaka juu ya nyoka wanaokuwa katika pori? 

Sasa tuangalie yanayo elekea uoto, watu wanapendelea kufikilia sana kwa vitu vinavyo waletea utajiri … 

Tuone sasa anga, angahewa, hali ya hewa, hatuna mamlaka juu ya hali ya hewa, kama kunanyesha mingi, hiyo inaweza hata kutuzuia kukusanyika pamoja juu ya kuabudu Mungu wetu. 

Munajuwa mutu mwenye anamiliki hali ya hewa? 

Siku moja wakati nilikuwa najitayarisha kupokea wageni na mukristo moja aliniuluza kama nilijiandaa juu ya hali ya hewa nili mujibu hapana, na wakati tu lilimukumbusha kama inawezekana nisafiri kesho, hapohapo nvua ikaanza kunyesha. Na vilevile siku ifwatayo kuliendelea kunyesha kweli. Unaweza kuwaza kama ilikuwa tu ya kubahatisha, hapana, ni nvua. 

Nikajona kama sina mamulaka juu ya hali ya hewa. 

Munaona, watu hawana mamulaka yote juu ya ulimwengu, 

Pahali ya kuendelea mbele, watu wanarudi nyuma kweli, nyuma hata ya kwenye walianzia. 

Tusome sasa kwa kitabu ya  Mwanzo sura mbili, 

Kweli Mungu aliumba mutu sawa mutu, musikilize kwa makini maandiko haya, Mungu akaumba nani, mutu, sasa eti hapa Mungu alitumikisha mabadiliko ama magawanyiko, hapana!!!


MWANZO 2:7 

“Bwana Mungu akamfanya mutu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mutu akawa nafsi hai.” 

 Ndugu zangu sikilizeni kwa makini, 

Mungu aliukamata mavumbi na kwa hiyo akamufanya mutu na akapulizia katika pua yake pumzi ya uzima. 

Tuzungumuzie kidogo juu ya hiyo sayansi ya mabadiliko, 

Tukiangalia hiyo magawanyiko ya kufwatana, mugawanyo unao jifwta kwa muda Fulani, 

Mungu alimuumba mutu kwa mavumbi, 

Sasa tujiulize, 

Eti Mungu aliukamata yale mavumbi na akaanza kuugawanya? 

Akafanya mugawanyo unao jifwata kwa kiasi Fulani ili afikie kupata mutu? 

Tusome kwanza ZABURI 103:14 

Sikilizeni ni wasomee, Tusome katika Jina la Yesu: 


ZABURI 103:14 

“Kwa maana Yeye anatujua umbo letu, Na kukumbuka yakuwa sisi tu mavumbi.” 

Mungu anajuwa sisi ni nini na anajuwa kama sisi ni mavumbi, 

Eti, sisi tunatokea kwa mugawanyo? Acheni mawazo hiyo ya upumbafu. 

Kiisha kufa kwetu, wakati wandugu zetu wanachukuwa mwili wetu, wanau ili wampake, wanautengeneza matumbo na kuumwangia malashi, na kuuvika nguo na kwa mwisho nini inakuja? 

Wanaukamata na inaenda mara moja kwa mavumbi. 

Hiyo imeetwa rushwa, utoaji hongo, 

Kumbukeni kwamba wakati Bwana Yesu alienda kaburini kwa rafiki yake mpendwa, 


YOANE 11 

Wakati Bwana Yesu alikuwa akizungumuza na wa dada wawili wa marehemu, wao walimusii na kumwambia kama ndugu yao alikufa tangu siku nyingi na hivi ananuka  harufu mbaya sana. 

Wakati Mungu alipoumba mutu, alimuumba kutoka mavumbi na ni kwa mavumbi anarudi wakati anapokufa. 

Mutu anarudi kwenye alipotoka. 

Sasa tusikilize neno lingine. 

MWANZO 2:7, acheni nowasomee tena neno moja: 

“Mungu akamuumba mutu kwa mavumbi na aka… 

Sikiliza muzuri ngugu yangu, 

Akampulizia wapi, 

Kwa pua yake, pumzi ya uzima na mutu akakuwa nafsi inayokuwa na uhai. 


Mungu aliukamata mavumbi, mavumbi, akamufanya mutu, na mbele ya kupulizia ndani yam utu pumzi ya uzima, alimutia kwanza pua. 

Sasa hapo eti munaona hadisi zao za mabadiliko kutokea mutu? 

Eti Mungu alitumikisha aina Fulani ya mabadiliko? 

Mutu aliumbwa mutu na akiwa na pua yake vilevile. 

Na Mungu alimupumuzia katika pua lake pumzi ya uzima. 

Sasa tusome katika ISAYA 2:22 

“Mwacheni mwanadamu ambaye pumzi yake I katika mianzi ya pua; kwa maana hudhaniwaje kuwa ni kitu?” 

Tuisome tena katika WAEBRANIA. 

Sasa tupime kuingiza pumzi tuki ingiza kwa ujazi pumzi mara moja, 

Uiingize ijae mbavuni, na mbele yakuiondosha uingize tena ingine mara moja, eti yawezekana? Jibu ni hapana. 

Haiwezekane sababu mutu ana uwezo ya kuingiza  pumzi kwa kujaza mbavu yake kwa mara moja tu. 

Unaona namna gani uzima wetu unategemea iyo? 

 

Mungu akapumuzia ndani ya pua la mutu pumzi ya uzima na mutu akageuka kuwa nafsi ya uzima.

Alimuumba mutu mzima, hakufanya magawanyiko ama kufanya kwanza kazi moja mbele. 

Napenda kujuwa kama kuliisha acha kutumikisha pua zetu? 

Munajuwa namna gani pua ni ya lazima kabisa, sivyo? 

Mungu alimuumba mutu kama mutu na akampatia pumzi ya uzima na mutu akaendelea kutegemea pua yake inayomupa pumzi ya uzima. 


Ninaulizo lingine lakuwauliza. 

Eti umbo la mutu uliendelea kubadilika kuachana na vile ulikuwa mbele? 

Tusome 


MWANZO 6:5  

“Bwana akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoni mwake ni baya siku zote.

Bwana akaghairi kwa kuwa amemfanya mwanadamu duniani, akahuzunika moyo.

Bwana akasema, Nitamfutilia mbali mwanadamu niliye muumba usoni pa nchi; mwanadamu na nyama, na kitambaacho, na ndege wa angani, kwa maana naghairi ya kwamba nimewafanya.” 

Tupime kufikili, 

Hii njoo umutu wa mwanadamu unafanya. 

Mungu alimuumba mutu, sawa mutu, akamuita Adamu. 

Na muzaliwa wa kwanza kwa dunia hii alikuwa nani? 

Alikuwa muuaji njoo maana kiisha vizazi vichache, hapo tunafika kwa nyakati za Nowa, 

Mungu alihuzunika na akaghairi juu ya nini alimufanya mutu, nikusema mutu aligeuka kuwa muchafu sana rohoni,  mubaya saana kuputiya mwanzo waki, aligeuka kuwa mutenda zambi Zaidi ya vile alikuwa mutenda zambi wakati wa Adamu, 

Adamu aliye fanya zambi. 

Sasa tujiulize, ingelikuwa mutu anaendeleaka katiko mabadiliko, jee hangalikuwa muzuri Zaidi? 

Mutu anakuwa mubaya sana na muchafu sana tangia siku nyingi. 



Tusome

 

2 TIMOTHEO 3: 1  

“Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. 

Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, 

Wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, … 

Wenye mfano wa utawa, lakini wakikana nguvu zake; “


Tujiulize, eti mutu anasonga mbele? 

Katika 2 TIMOTHEO. Mungu anatuzungumuzia juu ya watu walioamini, watu wenye wiko wanamemba wa Mwili wa Kristo. 

Nazani kama Kanisa Mwili wa Kristo, inapoteza samani yake kweli. 

Na hapo kweli, 

Hakuna mwenye kuendelea mbele, 

Lakini kuna huyo mwenye kurudia nyuma. 

Mutu anageuka kuwa mubaya sana kupita jinsi alivyokuwa mbele. 

Mutu wa leo ana vifaa vingi,  ana Gazeti, Redio, Televijieni, anakuwa na urahisi wa kupasha habari na kuzungumuza, simu, anakuwa na uwezo ya kuenda angani, kuruku kama ndege hewani, tena Zaidi kwenda kwa mwezi ama angani nzima Zaidi ya saa makumi mbili na ine. 

Lakini mafaa ya hiyo? Yeye anapoteza!!! 

Tusome 


MWANZO 5:1, hapo, nitawaonesha kitu kingine kinao onesha kama Mwenyezi Mungu hakutumikisha mabadiliko. 


MWANZO 5:1  

“Hiki ndicho kitabu cha vizazi vya Adamu. 

Siku ile Mungu alipoumba mutu, kwa sura ya Mungu alimfanya; 

Mwanamume na mwanamuke aliwaumba; akawabariki akawaita jina lao Adamu, siku ile walipoumbwa. 

Adamu akaishi miaka mia na thelathini, akazaa mwana wake kwa sura yake, kwa mfano wake, akamwita jina lake Sethi, 

Siku za Adamu baada ya kumzaa Sethi zilikuwa miaka mia nane, akazaa wana, waume na wake. 

Siku zote az Adamu alizoishi ni miaka mia kenda na thelathini, naye akafa. 

 

Sasa munifwate kwa makini sana, 

Hapa tunaona mutu wa kwanza aliye umbwa sawa Adamu, aliishi miaka mia kenda makumi tatu, 

Munamujua mutu moja anye fikisha umri huo leo? 

Sasa tutasema kama mutu anabadirika na kuenda mbele ama ? 

Sasa tusome haya ya sita, 


Sethi akaishimiaka mia na mitano, akamzaa Enoshi. 

Sethi akaishi baada ya kumzaa Enoshi miaka mia nane na saba, akazaa wana, waume na wake. 

Siku zote za Sethi ni miaka mia kenda na kumi na miwili, akafa.


Tusome haya ya makumi mbili na saba, 

Siku zote za Methusela ni miaka mia kenda na sitini na Kenda, akafa.

Tusome haya makumi tatu na moja.

Siku zote za Lameki ni miaka mia saba na sabini na saba, akafa.  


Watu wanasema kama Mungu alitumikisha mabadiliko, lakini sasa tazameni, watu kiisha kuumbwa kwao na Mungu walikuwa wanaishi mw miaka ma mia, 

Lakini kwa sasa, wanatudanganya wakisema kama sisi tuliendelea mbele katika mabadiliko…. 

Hiyo sayansi ya mabadiliko, eti ilifanyika katika siku nyingi sawa vile wasemavyo,  

Lakini hiyo haiambatane hata mara moja na Biblia tena haiangalie Biblia. 


Sasa naamini na ninajuwa kwamba haiwezekani mutukuamini Biblia na kuwa na mawazo ama mafikili ya kuamini hata chanjo moja ya hiyo sayansi ya mabadiliko.

Kama munasikia mutu ambaye yeyote iko anahubiri juu ya sayansi ya mabadiliko ya wasioamini, usijali kumufwata katika mambo asemaye, wewe umubebe tu kunako maandiko matakatifu, Neno la Mungu.  

Hiyo yao ni mawazo mtupe, sababu Biblia haiseme kitu juu ya hayo. 

Sasa tuone yanayo elekea hii sayansi ya mabadiliko kama SILAHA YA SHETANI,  

Eti kuna mumoja katikati yenu mwenye kufikili juu ya mambo yanayo tukia sasa katika inchi yetu? 

Tuache kwanza dunia nzima na tuangalie inchi yetu kwa upekee, 

Eti munajuwa ya kuwa tumetawaliwa na watu wenye miili ya kuharibika? 

Mutu moja mwenye akili jina lake DARWIN aliye zungumuza juu ya hiyo  sayansi ya mabadiliko ya upumbafu. 

Mfumo wetu wa kielimu, namna yetu ya kufunza watoto wetu,  eti munajuwa mwanzo wake? 

Mutu gani aliye uunda? 

Eti mwajuwa juu ya nini tuna hesabu miezi na masiku? 

Nani alie anzisha hiyo kutamka? 

Nani alieanza kijeli hiyo, muzaa huo? 

Ni ndugu Segman FROY 

Ni mutu gani aliyeunda msingi wa mfumo wa kiuchumi? 

Ni mutu anayeitwa John MELDREID KASE, na mbele ya kufa kwake, alikanusha hayo yote. 

Ni nini inayokumba wanadamu? 

Mwanadamu anafikia kwa kiwango ya kutafuta majibu ya maulizo yake yote kwa watu. 

Wakati Prezidenti GEORGES alileta sheria yake juu ya umaskini, yeye alikanusha Mungu. 

Mungu alitukumbusha kwamba ni uchovu wenye tunapendelea ndio uta  tunatumikia. 

Mungu hakuomba wanadamu waponesho magumu yote ya dunia. 

Ni vigumu sababu zambi iko hapo. 

Taabu, shida, kutafuta uhuru, yote ni vigumu sana sababu zambi iko hapo. 

Lakini watu walijizania kufika kusema kama mutu binafsi anaweza akapate surulisho kwa tabu zake,  na hiyo ni inaambatana na maadibisho na elimu tunayoipata. 

Na maadibisho hiyo inasema na kufundisha nini, eti munayafahamu? 

Tusome Biblia katika kitabu cha Wakorinto wa pili sura 11 na haya 13, 

Sababu gani tunahakikisha kwamba Shetani iko anatumika katika hiyo miradi? 

Nitawaonesha sababu hiyo… 


2 WAKORINTO 11: 13, sasa tusikilize kwanza, 

“Maana watu kama hao ni mitume wa uongo, watendao kazi kwa hila, wanajigeuza wawe mfano wa mitume wa Kristo. 

Wala si ajabu. 

Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru. 

Basi si neno kubwa watumishi wake nao wakijigeuza wawe mfano wa watumishi wa haki, ambao mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao.” 


Sasa, eti munafahamu mambo gani Shetani aliyomuambia Adamu? 

Alimuambia kama Mwenyezi Mungu anafahamu ya kwamba siku mutakula tunda la muti wa uliokataliwa, mutajuwa wazi, 

Shetani alitaka kuwaambia kama, mutakuwa sawa na Mungu. 

Kweli munasadiki hiyo? 

Mutakuwa na uwezo ya kupata jibu kwa malalamiko na taabu yenu, mutakuwa mukiziweza na kujitegemea, mutakuwa huru, hiyo njoo miradi hiyo. 

Wanadamu wanajaribu kushurulikia wanadamu wenzao. 

Wanadamu wanakuwa na ndoto na kujizania, watu wanaokuwa na uhuru juu ya mali zao, hawa hawaja onekana kamwe duniani. 

Sasa YESU KRISTO, MWANA KONDOO WA MUNGU, MKOMBOZI WETU, MWOKOZI WETU, alikuja hapa duniani akijinyenyekeza, akiacha kwa muda UFALME wake juu yako na yangu, juu ya zambi zako na zangu, Z.A.M.B.I. 

Haipashwi kutegemea tu elimu ya dunia hii na kusahau ukubwa wa Mkono wa Bwana aliye juu, na kuzarahu kusikiliza yasemayo Biblia, 

Kweli watu wanaonesha maendeleo, kunakuwa miradi na uundo wenye kufanikiwa na matumizi yao haiku ya kimungu. 

Namna gani watu wanajitememea? 

Namna gani wanaharibu mazingira, wewe una furahia hivyo? 

Miradi hizo zote zinaonesha kushindwa kwa shetani, sababu hii njoo ile miradi ya “HUMANISME” “UTU” 

Ni hali na falsafa ya kumutia mutu awe musingi wa vitu vyake vyote. 

Mutu akitafuta surulisho juu ya maulizo na taabu yake, mutu akija na ndoto yake na hiyo inamupa mutu kiburi na kumurudisha nyuma Zaidi, 

Mutu anakuwa mwenye kujipenda binafsi, mwenye matukano, asiye na maadibisho na kujizuiza. 

Kwa siku ijayo tutaona wale wa sayansi ya mabadiliko wenye wiko na wazimu. 

Maombi ya mwisho 

Tuombe: 

Mwenyezi Mungu na Baba yetu, 

Tunakushukuru kwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, 

Tunakushukuru hayo ya kadiri uliotupatia kupitia mahubiri tuliyopata leo, 

Yenye inatokea ndani ya Maandiko yako Matakatifu. 

Baba yetu tunakupigia aksanti mara dufu, 

Twafahamu kwamba tunapashwa kukutegemea katika njia zetu zote, 

Tukikutwiga mizigo yetu yote tunayo wazia, 

Wewe unamajibu yote yenye inaweza kutupatia mwangaza tena inaweza kututuliza, kutuongoza, na yenye mafaa kwetu. 

Na tungependelea kwamba uwe pia pamoja na wenye kukukana sababu hawajuwi kwamba kuna Yeye aliyewapenda na kutowa maisha yake na kufa kwa ajili yao, Yeye Yesu Kristo. 

Uwafunguwe macho yao ili wamuone na kumufahamu Bwana Yesu sawa vile Biblia inatuonesha. 

Tunakushuru katika Jima la Bwana na Mwokozi wetu YESU KRISTO. 


Amen. 


Ref: 04/26/1981 / 605-2 NATHARIA YA SAYANSI YA MABADILIKO / Silaha ya Shetani / Theory of Evolution / 04/16/2020