Thursday, October 29, 2020

WALIO HODARI WALIANGUKA / THE MIGHTY HAVE FALLEN

Photo by B Smith from the kitchen door



 


WALIO HODARI WALIANGUKA 

THE MIGHTY HAVE FALLEN

August 15, 1965 

Pastor Henry F. Kulp 


 

Waroma 9: 1 – 5 

“Ninasema kweli katika Kristo, sisemi uwongo, zamiri yangu inanishuhudia katika Roho Mtakatifu, 

ya kwamba nina huzuni nyingi na uchungu usiokoma katika moyo wangu. 

Kwa sababu ningeweza kuomba mimi mwenyewe nikatazwe na kutengwa na Kristo kwa sababu ya ndugu zangu, jamaa zangu kwa namna ya mwili; 

walio Waisraeli, wenye kuwekwa kama wana, wenye utukufu na maagano, wenye kupewa sheria na utumishi kwa Mungu, na ahadi; 

ndio na baba ni wao, na katika hawa alitoka Kristo kwa namna ya mwili, aliye juu ya maneno yote, Mungu Mbarikiwa kwa milele. Amina.” 

 

Juma iliyopita tuliona kwamba katika Waraka wa Waroma, katikati ya sura ya nane na sura ya kenda kuna pumziko ama kizuizi, toka katika hali ya furaha na kuingia katika hali ya huzuni.  

Kwa mwisho wa sura ya nane kuna masemi ya furaha na uwepo wa juu sana, hali ya raha na shangwe katika  Yesu Kristo, ikituhakikisha  kwamba hakuna kitu chochote kinachoweza kututenga na mapendo ya Kristo, bali sura yake ya kenda, inatuonesha Mtume Paulo akikumbwa na huzuni nyingi na uchungu usiokoma katika moyo wake. 

Mtume Paulo alikuwa akiwapenda sana wandugu zake katika mwili na jamaa yake katika mwili na hali yao ya ukiwa, iliweka Mtume Paulo katika hali ya uchungu sana moyoni mwake.

 

1/ Kwa kweli, Mtume Paulo anajionyesha waziwazi kuhusu shambulizi iliyotokana na ndugu zake wa kimwili, jamaa yake ya kimwili. 

Yeye alikuwa akibeba mzigo wa kutojali. 

Ilikuwa vigumu kufahamu Toleo lililopewa kwa Mataifa.

Kusema kwamba mataifa wanaweza kuwa watoto wa Mwenyezi Mungu kwa njia ya Imani pekee katika Kristo Yesu. 


Kwa siku za zamani, Mataifa hawakuwa na toleo kama lile. 

Hata siku moja katika historia ya wanadamu, Mataifa hawakupewa toleo kama lile, ni kwa sababu hiyo,  Wayuda walipata wivu na kujisikia wenye kukwazika sana wakiuzunishwa kuona kwamba wao waliokuwa kwa muda wote kama Taifa iliyopendwa na Mungu, sasa wametiwa kando, na Mataifa wapagani wamekaribishwa ndani, sawa vile Mtume Paulo anavyo hubiri.

 

2/ Mtume Paulo anauchungu, siyo sababu ya anguko lao, bali kuona kwamba wao hawakupata faida ya nafasi ya juu waliokuwa nayo na upendeleo yote Mungu aliyowakabizi, pahali pa kufaidika, wao wanaanguka toka hali hiyo. 

Katika majifunzo ndani ya Sura hii, mutaona namna gani Mtume Paulo ana uchungu kubwa na huzuni ndani ya moyo wake kuona kwamba wandugu wake hawakufaidika na toleo na upendeleo wote Mwenyezi Mungu aliyo wakabizi.

 

3/ Neno hili linatukumba hadi kufikia jambo la muhimu sana linalo tafutikana na kukosekana katika makanisa yetu ya kikristo na katika maisha yetu ya siku za leo ni jambo la ukosefu wa mapendo kwa wakristo wenzetu na kwa wale wasiookoka. 

Nazani kwamba naweza kusema wazi wazi bila kuwa na shaka kwamba wakristo wengi wa siku hizi wanakosa mapendo kwa wandugu zao wa kimwili na hata kwa wandugu zao wa kiroho, yaani waamini. 

  

 Wao wanakuwa tu wenye kuhukumu wengine bila kujiangalia kwanza wenyewe na hii tabia inaleta kasoro na unyonge zaidi juu ya huduma kwa ajili ya Kristo.


Mtume Paulo angaliweza kusema namna hii:

 

“Kweli ninyi Wayuda munapokea malipo munayostahili, baba zenu waliwauwa mitume, na kwa mwisho walimusulubisha Mwokozi wetu Yesu Kristo, tena, sawasawa   na namna inavyosemwa katika kitabu cha Matendo ya Mitume, wayuda walitupilia ushuhuda wa Roho Mtakatifu na kwa mwisho, wao hawapendi Habari Njema ifikie Mataifa wapagani.  

Mtume Paulo angaliweza kuwaambia kwamba:

 

Ninyi mulifuga na kukomalisha chuki yenu na kwa sasa munapokea malipo  munayostahili, na mimi sijali na hali yenu kwa saa zote zenye nitahusika na mambo haya.

 

Lakini, Mtume Paulo hakutenda namna ile. 

Bali yeye alisema kwamba:

 

“Kwa sababu ningeweza kuomba mimi mwenyewe nikatazwe na kutengwa na Kristo kwa sababu ya ndugu zangu, jamaa zangu kwa namna ya mwili, ili wao waokolewe.”

 

Eti na wewe pia unatabia hii mbele ya watu wenye wanatenda zambi mbele ya macho yako ama wenye kuanguka zambini ukiwa umekuwa nafasi mambo yanayotukia?

  

Ama wewe unaigeuza kuwa shida lako binafsi na kiisha kujumulisha uharibifu wote, unasema: “Wao wanavuna kabisa mabaya waliyo fanya”  

Natumaini kwamba siyo vile kwenu; umbalimbali na wao, ninyi munayo tabia ya Mtume Paulo. 


4/ Tukumbuke kwamba Mtume Paulo ndiye Mfano wetu maalum wa kuiga. 


1 Timoteo 1: 15, 16 

“Neno hili ni aminifu, na linastahili kukubaliwa na watu wote, ya kwamba Kristo Yesu alikuja kwa dunia kuokoa wenye zambi; na mimi wa kwanza wao.

 

Lakini kwa sababu hii nilipokea rehema, ili katika mimi wa kwanza, Yesu Kristo aonyeshe uvumilivu wake wote, kwa mfano kwao ambao watamwamini nyuma wapate uzima wa milele.” 


Mtume Paulo siyo tu mfano wetu wa kuiga kwa jambo linalohusu wokovu wetu, bali pia mfano wa kuiga kwa kuhusu mapendo kwa wengine. 


5/ Ningetamani muwe na picha la urefu wa anguko toka juu sana walioanguka wana wa Israeli. 

Hakujakuweko hata Taifa moja la kulinganisha na Taifa la wana wa Israeli. 


Taifa hili lilikuwa na Mapatano na Mungu. 

Wayuda walikuwa na ahadi zote na Mataifa mengine, yaani Wapagani hawakuwa na kitu chochote kile. 


Waefeso 2: 11 - 13  

“Kwa ajili ya maneno haya mukumbuke ya kwamba zamani ninyi, watu wa Mataifa kwa maneno ya mwili, munaoitwa Wasiotahiriwa na wale wanaoitwa Waliotahiriwa, tohara katika mwili iliyofanyika kwa mikono; 

Kwamba kwa wakati ule mulikuwa mbali na Kristo, mumetengwa mbali na jamaa ya Israeli, na wageni kwa maagano ya ahadi.

 

Mulikuwa hamuna tumaini wala Mungu duniani.

 

Lakini sasa, katika Kristo Yesu, ninyi muliokuwa mbali zamani mumekuwa karibu kwa Damu ya Kristo.”


Mataifa wapagani walikuwa bila Mungu duniani. 

Kumbukeni, tafazali, kwamba Wayuda walikuwa na nafasi yenye Mataifa mengine hawakuwa nayo.

 

Mataifa hawakuwa hata na agano moja, hata ahadi moja, walikuwa bila Mungu duniani hadi wakati Mtume Paulo alikuja kuwaletea Injili hii, Mahubiri hii mupya.

 

6/ Sifahamu kwamba ninyi mumekwisha  kutambua kwamba Mwenyezi Mungu alianza kubariki ulimwengu huu kupitia Abrahamu. 

Abrahamu aliishi kwa miaka 2000 kiisha anguko.

 

Sababu miaka 2000, mbele ya Abrahamu, Mwenyezi Mungu hakutenda chochote juu ya anguko la ulimwengu.

 

Kwa kweli Yeye aliahidi Mukombozi, na alitia upinde wa mvua katika mawingu ili aoneshe kwamba Yeye hatafunika tena dunia kwa garika. 

Yeye alihukumu dunia kwa maji ili alisafishe na machafu yaliyojaa hamo. 

Mutu moja alizungumuza kwamba Mwenyezi Mungu alizamisha ulimwengu chini ya maji na akaiacha humu ndani ya maji kwa muda wa siku nyingi ili alisafishe, bali, kwa ngambo ingine yeye alipana ahadi wakati alipoweka upinde wa mvua katika mawingu ili aoneshe ya kwamba Yeye hatahukumu tena ulimwengu kwa maji.

 

Pia kwa munara wa Babeli Mwenyezi Mungu zusha alivuruga luga yao na kuwasambaza wote.

 

Kwa Sodomo na Gomora Mwenyezi Mungu alituma nvua ya moto na kiberiti kunyesha juu ya muji.

 

Kwa muda huu wote, alikuwa anasubiri ujio wa Abrahamu. 

 

Kiisha hapo, Mwenyezi Mungu alimuita Abrahamu toka muji wa Kaldea na kumuongoza hata Palestina.

  

Mungu akamwambia Abrahamu: 


Mwanzo 12: 1 - 3 

“Basi Bwana akamwambia Abramu: Toka wewe katika inchi yako na katika ndugu zako, na nyumba ya baba yako hata inchi ambayo nitakuonyesha; na nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na nitakubariki, nitatukuza jina lako, nawe uwe Baraka; na nitawabariki ambao wanakubariki; naye ambaye anakulaani nitamlaani vilevile, na ndani yako jamaa zote za inchi watabarikiwa.”

Nitakubariki na kwa njia yako nitabariki mataifa. 

Na nitawabariki ambao wanakubariki.

 

Nazani wewe utasema kwamba: “Kwa siku za leo siyo vile.” 

Kwa upande moja ni kweli.

 

Unaweza sema: “Mibaraka yangu inatoka kwa Mwokozi wangu Yesu Kristo.”


Sasa kwa kweli, Mwokozi ni nani? 

Si Yeye aliyezaliwa kwa namna ya mwili toka Taifa la Wayuda? 

Si Yeye aliyekuwa Muyuda kwa namna ya mwili?

 

7/ Kwa upande mwengine, Mwenyezi Mungu hakutuahidia wewe na mimi baraka za namna ya kimwili.

 

Hapo kwa Mwanzo 12, tunaona mibaraka ya hapa duniani.   

Wewe na mimi ni wenyeji wa mbinguni, siyo hapa duniani. 

Waweza kuniuliza sababu gani tuna migogoro ya vita, mauwaji na mapinduzi, uasi hapo na pale kama vile tulivyoona juma iliyopita katika muji wa Los Angels, na Chicago katika mapingano na migogoro na tunajiuliza sababu gani dunia inapatikana katika msukosuko. 

Sababu gani Mwenyezi mungu habariki inchi kwa nyakati za leo? 

Inchi zote zinakuwa na kasirani. 

Kwa siku za leo Mwenyezi Mungu habariki tena inchi kama alivyofanya mbele kwa Taifa chaguliwa.

Kwa kweli hapo hapo utaniuliza nilete sababu. 

Ni kwa sababu Yeye alipendelea kubariki inchi kupitia Israƫl na kupitia Abraham.


Na kwa siku za leo, Taifa la Israeli bado ingali inasambazwa mahali nyingi duniani, Taifa haliko kwa nafasi yake. 

Kama bado wana wa Israeli wakingali wanasambazwa, Mwenyezi Mungu hatabariki mataifa mengine katika dunia. 

Mataifa hayatakubali kukabizi Israeli udongo wake, Inchi lake, mataifa wanakataa kukabizi Israeli udongo wa Palestina. 

Waliikabizi sehemu kidogo tu la eneo ya Palestina. 

Bali, wakati Taifa la Israeli itapewa udongo wake katika heri na salama, wakati Israeli itaishi na kuenea katika eneo lote la uwanja wake, hapo ndipo Mwenyezi Mungu atabariki Taifa la Israeli na Taifa lile litakuwa njia ya  Baraka ya Mungu  kwa Mataifa mengine duniani. 

Kwa sasa Mwenyezi Mungu hatendi kama vile, Yeye anasukuma na kutuma   wa Misionari kwenda duniani pote, ili wahubiri watu na kuwaongoza kuamini Bwana Yesu Kristo. 

Na waamini hawa watatoka toka mataifa yao na kuja sasa kuwa kiungo cha Kanisa Mwili wa Kristo. 


8/ Jameni tuone jambo moja inayoonesha kuwekwa kuwa juu na samani sana kwa Taifa lile tukufu.

 

2 Samueli 7: 23 

“Na taifa gani duniani ni kama watu wako, hata kama Israeli, ambao Mungu alikwenda kuwakomboa kwa yeye mwenyewe, wawe watu wake na kujifanyia jina na kufanya maneno makubwa kwa ajili yenu, na maneno ya kuogopesha kwa ajili ya inchi yako, mbele ya watu wako ambao uliwakomboa kwa wewe mwenyewe toka Misri, toka mataifa na miungu yao?”


Daudi anazungumuza na Mwenyezi Mungu. 

Daudi alipenda kumujengea Mwenyezi Mungu makao. Nyumba ya Bwana Mungu. 


Mungu akasema:

 

Hapana, wewe ulikuwa mtu wa kumwanga damu na mtu wa vita. 

Ninahitaji nyumba yangu ijengwe na mtu wa amani. 

Ni mwanawe Solomono ndiye atakaye nijengea Nyumba. 

Natambua kwamba, kwa kusoma Biblia, munafahamu ya kwamba Mufalme Solomono hakupigana hata vita moja katika ufalme wake. 

Mfalme Solomono alitawala na katika utawala wake alimjengea Mwenyezi Mungu hekalu lenye linakuwa mfano wa ule utawala wa miaka elfu, wakati Mwokozi Yesu Kristo atakuja kutawala kwa miaka elfu moja hapa duniani. 


Kumbukeni wakati wageni walikuja kumutembelea Mfalme Salomono, walimuambia kwamba: “Kuna nusu ya maneno yaliyobaki bila kusemwa”. 


9/ Mwenyezi Mungu alimwambia Daudi, wewe hauta nijengea nyumba, bali, mimi nitakujengea nyumba yenye itaitwa Nyumba ya Daudi, nitakupatiya Mwana atakayetawala juu ya Kiti cha Ufalme wa nyumba yako, na kwa kweli Mwana huyo ni Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 

Ni hiyo iliyosemwa na Daudi na mambo haya tunayapata katika aya ya 23. 


Hapo anaonesha ukubwa wa Taifa lile. 

Taifa lenye kujaa Agano la Kale nzima. 

Lakini sasa kitu moja kilitukia. 

Mwenyezi Mungu aligeuzia taifa pendelevu mgongo wake na aliamusha mtu moja jina lake Paulo ili aende kuhubiri Mataifa wapagani mafundisho yenye dunia nzima ilikuwa bado kuyasikia. 


10/ 2 Samueli 7: 23 

“Na taifa gani duniani ni kama watu wako, hata kama Israeli, ambao Mungu alikwenda kuwakomboa kwa yeye mwenyewe, wawe watu wake na kujifanyia jina na kufanya maneno makubwa kwa ajili yenu, na maneno ya kuogopesha kwa ajili ya inchi yako, mbele ya watu wako ambao uliwakomboa kwa wewe mwenyewe toka Misri, toka mataifa na miungu yao?”  

JE WATAMBUA MANENO DAUDI ANAYOYASEMA KUHUSU TAIFA LILE LA AJABU? 


Kumbukumbu la Torati 4: 7 


“Maana taifa gani kubwa lililo na Mungu karibu nao kama Bwana Mungu wetu kila mara tunapomwita?”

 

NA MUSA ALIPAZA SAUTI AKISEMA: 


Maana taifa gani kubwa

Tambua kwamba haiwezekane kulinganisha taifa lile ne taifa lingine duniani. 

Taifa lililo na Mugu karibu nao kama Bwana Mungu wetu kila mara tunapomwita

Mataifa mengine Wapagani, hawakuwa na namna ya kumlilia Mungu na kupaza sauti yao kwake ili awaokowe toka shida na matatizo. 

Ni Taifa ya Israeli pekee ndilo lilikuwa na Mungu kwa upande wao

Yeye Mungu alikuwa akiishi ndani ya Schekina juu ya hekalu na alikuwa akishuka chini na kuketi kwa kiti chake kilichokua kati ya tao ama mabawa mawili ya maagizo kwenye alikua anakutana na Kuhani Mkuu kiisha hapo, Kuhani Mkuu alikutana na wana wa Israeli. 

Hakuna hata Taifa moja lenye lingeliweza kulinganishwa na Taifa la Israeli. 


Agano la Kale nzima linajaa tu na Taifa lile. 


11/ Kwa sasa tutie mkazo wetu katika maneno Mtume Paulo anayo leta kwetu katika Kitabu cha Matendo ya Mitume 22: 21 


“Naye aliniambia: Ondoka, nitakutuma mbali kwa watu wa Mataifa.”

 

Hapa Mtume Paulo anatuzungumuzia historia ya wokovu wake. 

Hapo sasa yeye ni mufungwa atakaye tumwa kwa inchi ya Roma. 

Yeye anakuwa sasa kwa nafasi ya kujitetea na kujishuhudia mbele ya makutano ya Wayuda na anasema ya kwamba: “Hii ni maneno Mungu mwenyewe aliniambia.”

 

Wakati damu ya Stefano aliye uwawa, ilitiririka, nami vilevile nilikuwa hapo kati ya watu waliokuwa wauwaji na mimi niliwasukuma wao kumuuwa Stefano, nikusema ya kwamba mimi nilichamusha chuki ya yale makutano na kuwasukuma kumuuwa Stefano. 

Baadaye Mwenyezi Mungu aliniambia: “Nitakutuma mbali kwa watu wa Mataifa.”

 

Kwa siku za kale, hakuna siku Mwenyezi Mungu alinena kama sawa. 

Kwa nyakati za kale, Mwenyezi Mungu hakuruhusu mtu Muyuda kwenda kwa Mataifa, sawa vile anasema kwa sasa, kwa kweli Bwana wetu Yesu 


Kristo aliwaambia Wanafunzi wake:

 

Matayo 10: 5, 6  

“Hawa kumi na wawili Yesu aliwaagiza akisema: 

Musiende katika njia ya Mataifa, wala musiingie mji wo wote wa Wasamaria; lakini zaidi kwendeni kwa kondoo wapotevu za nyumba ya Israeli.” 


Musiende katika njia ya Mataifa. 

Munatambuwa kweli kama hiyo ni kitu kipya kyenye kiliongezeka. 


12/ Kwa sasa tutachipua aya mbili yenye itakayo tuonesha namna gani Taifa hili ni la kipekee na la kushangaza sana. 

Asubui ya leo ninaweza kuwahakikishia kwamba hakuna hata kitu moja cha manufaa chenye tunacho duniani, chenye hakikutoka toka Israeli. 

Tufahamu kwamba kitabu cha Waroma 9: 4 kinasema: 

“Walio wa Israeli, wenye kuwekwa kama wana, wenye utukufu na maagano, wenye kupewa sheria na utumishi kwa Mungu, na ahadi;” 

Wana wa Israeli ni wanani? 

Hilo ndilo jina lao. 

Nazani itakuwa heri na maana kwetu tujuwe china la jina lilo “Israeli”. 


Mwanzo 32: 24  

“Naye Yakobo aliachwa pekee; mtu akashindana naye hata mapambazuko.” 

Hapa inahusu Yakobo, na ni hivyo Taifa lile lilipata hiyo jina. 

Naye Yakobo aliachwa pekee; mtu akashindana naye hata mapambazuko. 

Yakobo alimukabizi Bwana vyote na kuacha vyote katika mikono ya Mungu. 

Najuwa kwamba wengi wanasoma aya hii bila kufahamu kwa makini nini Yakobo aliyoyafanya. 

Watu wengi wanazani kwamba Yakobo alikuwa sawa vile tunaita katika Swahili ya siku hizi “mukorofi”.

 

Wanamtia Yakobo kuwa mtu wa tabia ya ranga ya chini sana katika Agano la Kale, lakini Mwenyezi Mungu hakusema ivyo. 

Biblia vile vile haiseme vile. 

Je mwatambua ya kwamba katika Biblia nzima hakuna nafasi Biblia inasema maneno mabaya juu ya Yakobo?

 

Yakobo alitumwa Siria mahali aliwapata wake wake wawili. 

Yakobo alifanya kazi nzito kwa Mjomba wake Labani ili awapate wake wake wawili. 

Mjomba wake Labani alikuwa kweli mukorofi, lakini siyo Yakobo. 

Labani alimunyanganya Yakobo mali yote, lakini Bwana Mungu alimuahidi Yakobo kwamba atakuwa pamoja naye kwa muda wake wote wa kazi pale. 

Alimwambia: “Nitakuwa pamoja nawe na nitakurudisha kwako.” 

Wakati ilipotimu Yakobo alipenda kufika pale Betheli. 

Betheli ilikuwa mahali pa Baraka.

 

Lakini kwa Yakobo kufika Betheli, kati ya Yakobo na Betheli, Esau alikuwa akimungoja kwa mashambulio njiani akiwa na waaskari 400 wenye silaha nzito, na yeye Esau alikania kumuuwa Yakobo.

 

Yakobo akasema moyoni mwake: Yanipasa mimi nifike Betheli, kwa hiyo akachukua mali yake yote aliyopata hapa duniani na akayatuma kwa ndugu yake Esau ili apate kupoleza hasira ya Esau, kwa kuruhusu Yakobo apate kufika Betheli. 

Yakobo alikubali apoteze mali yote aliyopata hapa chini duniani na alifanya hivyo kwa niaba ya Mwenyezi Mungu. 


13/ Tuangalie mafundisho inayokuwa katika aya ya 24.  

“Naye Yakobo aliachwa pekee; mtu akashindana naye hata mapambazuko.” 


Aya ya 26 

“Naye alisema: Uniache kwenda, ni mapambazuko. Akasema: Sitakuacha kwenda ila utanibariki.” 

Huyo malaika alikuwa Bwana Mungu Mwenyewe mwenye aliambia Yakobo: Uniache kwenda. 

Yakobo alisema: Nimemushika Bwana Mungu na nitaendelea tu kumushika. 

Hakupenda kumuacha aende. 

Na wakati alipoona ya kama hakumshinda, akagusa mvungu wa paja lake; mvungu wa paja la Yakobo ulishutushwa wakati aliposhindana naye. 

Naye akasema: Uniache kwenda, ni mapambazuko.  

Akasema: Sitakuacha kwenda ila utanibariki. 

Akamwambia: Jina lako nani? 

Naye alisema: Yakobo 

Akasema: Jina lako halitaitwa tena Yakobo, lakini Israeli kwa sababu unashindana na Mungu, na watu, nawe umeshinda.  

Maana ya jina Israeli ni nini? 

Tuone namna haya hii inasema: 

Kwa sababu unashindana na Mungu.  

Wakati unapoita Yakobo “mukorofi” kumbuka wewe unasema vibaya juu ya mkuu wa Mungu, unazungumuza kuhusu mtu mwenye Mwenyezi Mungu alimupa jina la Israeli. 

Majina “Israeli” na “Yakobo” inatajwa mara nyingi sana katika Biblia kupita majina yote ila tu ya Mwenyezi Mungu mwenyewe. 

Yeye ni mkuu wa watu wa Mungu na jina lake, ni Mwenyezi Mungu pekee aliye lipatia Taifa nzima.    

Taifa la wana wa Israeli. 


14/ Waroma 9: 4 

“Walio wa Israeli, wenye kuwekwa kama wana, wenye utukufu na maagano, wenye kupewa sheria na utumishi kwa Mungu, na ahadi;”

  Wenye utukufu, Israeli ilikuwa na utukufu wa Mwenyezi Mungu. 

Nasema: ILIKUWA 

Wakati Mwenyezi Mungu alipowakomboa wana wa Israeli toka Misri, wana wa Israeli walikuwa wakifunikwa na mawingu ya Utukufu wa Mungu, ulioitwa Schekinah. 

Utukufu huo hautaupata hata mahali nyingine hapa duniani. 

Hakuna hata Taifa nyingine hapa duniani yenye ililindwa na utukufu wa Mungu Mwenyewe, lakini tendo hili Mwenyezi Mungu alilitimiza kwa Taifa la Israeli. 

Mungu alishusha mawingu ya utukufu itenganishe na kuwa kati ya Israeli na Farao, na hapo Farao hakuweza kufanya hata neno moja. 

Hakuna taifa lingine lenye lilionekana hapa duniani lenye lilikuwa na utukufu wa Mungu. 

Iwe taifa hodari. 

Iwe mataifa yenye yalijenga hekalu kubwa mno.

Iwe mataifa yenye iliishi katika sifa na maabudu kwa Mungu, hakuna Taifa lenye lilikuwa na utukufu wa Mungu. 

Wakati Musa alimaliza kulijenga hekalu na mambo yote yalikuwa tayari, utukufu wa Bwana ulijaa hekalu nzima na hapo hakuna aliyeweza tena kuhudumia. 

Wakati Solomono alipojenga hekalu na wakati alipolizindua kwa Bwana Mungu, utukufu wa Mungu ukajaa hekalu nzima na hakuna mtu aliyeweza kutumika. 


2 Mambo ya siku 7: 1 - 3  

“Basi Solomono wakati alipomaliza maombi haya, moto ukashuka kutoka mbinguni, ukateketeza sadaka ya kuteketezwa na zabihu; utukufu wa Bwana ukajaa nyumba. 

Wala makuhani hawakuweza kuingia katika nyumba ya Bwana, kwa kuwa utukufu wa Bwana umejaa nyumba ya Bwana. 

Wana wa Israeli wote waliona wakati moto uliposhuka, na utukufu wa Bwana ulipokuwa juu ya nyumba; wakaanguka kifudifudi hata inchi juu ya sakafu, wakaabudu, wakashukuru Bwana, wakasema: Kwa sababu Yeye ni Mwema; na rehema zake ni za milele.” 

Mambo kama sawa hamutaipata katika historia ya wanadamu. 

Hakuna ingine Taifa duniani iliyobarikiwa na utukufu wa Mungu. 

Kweli Taifa hili ilipanda juu sana katika yote, bali walio hodari walianguka.

Kwa sasa, Mwenyezi Mungu anatumika na watu wote katika dunia akiweka watu wote katika msingi mmoja. Wote wamefanya zambi na wanahitaji Kristo


AMINA. 

N°Ref: 08/15/1965/ 33 - THE MIGHTY HAVE FALLEN / 10/29/2020

Wednesday, October 14, 2020

SHERIA YA MBINGU YA KUTOA NA KUHITAJI / HEAVEN’S LAW OF SUPPLY AND DEMAND

Photo by B Smith from the patio




SHERIA YA MBINGU YA KUTOA NA KUHITAJI

HEAVEN’S LAW OF SUPPLY AND DEMAND

July 26, 1981 

Pastor Henry F. Kulp



 

Kwa kweli, mahubiri hii itaelekea utoaji. 

Mazungumuzo yote yataangalia pesa, na, nazani kwamba hamuta umwa moyo na kusema kwamba ninatia mkazo juu ya mahubiri kuusu pesa. 

Kwa kweli, mimi sihitaji kunyanyasa mkoba wenu, ama akiba ya mofukoni wenu, lakini, mimi kama Mtumishi mwaminifu wa Mwenyezi Mungu, ninakuwa na mapashwa ya kuwafahamisha yale yanayo husu   Utoaji tukifahamu kwamba: Mwenyezi Mungu anafurahia yeye anaye toa kwa furaha. 


1/ Mara kwa mara najiuliza kwamba eti ninyi munafahamu ya kuwa Biblia inasema mambo mengi sana kuusu Mwamini na utoaji sawa sawa na namna Biblia inazungumuzia kuhusu Kawaida ya Mafundisho mengine. 

Biblia inazungumuza sana kuusu utoaji ndani ya Agano la Kale na ndani ya Agano Jipya vilevile. 

Hata katika Vitabu vilivyo andikwa na Mutume Paulo navyo vilevile vinazungumuzia kuusu utoaji. 


2/ Ningelitamani muweke mafikili yenu juu ya msemwa huu: 

Mungu anafurahia yeye anayetoa kwa furaha

Eti, Mwenyezi Mungu hawapendi watu wote? 

Siye Yeye aliyesema katika Yoane 3:16 kwamba Mungu alivopenda Ulimwengu? 

Sasa msemwa inayosema ya kwamba Mungu anafurahia yeye anayetoa kwa furaha inamaanisha nini? 


3/ Mbele ya kuleta jibu ya ulizo hili, twende kwanza kufahamu kwamba Mwenyezi Mungu ni Mtoaji


Yoane 3: 16 inatuambia: 

“Kwa maana Mungu alivyopenda ulimwengu, hata kutoa Mwana wake wa pekee, ili kila mtu akimwamini asipotee, lakini apate uzima wa milele.” 

Mungu aliupenda hata kutoa. 

Uwingi wa mapendo na kutoa inaambatana na haiwezikane kuyatenganisha. 

Ni vigumu kwake anayependa ajizuize kutoa. 

Anayependa atatoa moja kwa moja bila mashito. 


4/ 1 Wakorinto 13: 3 inasema: 

“Na kama nikitoa mali zangu zote kulisha masikini, tena nikitoa mwili wangu niunguwe kwa moto, lakini sina mapendo, hainiletee mimi faida.” 

Katika maisha ya kiroho, kutoa bila mapendo ni bure na haifai kwa kitu.  

Na kama nikitoa mali zangu zote kulisha masikini, tena nikitoa mwili wangu niunguwe kwa moto, lakini sina mapendo. 

Tambua na utie mkazo sana kwa neno hili: Hainiletee mimi faida.  

Mungu anatupatia na kututolea vitu kazaa sababu anatupenda na kama sisi vilevile tunapenda kutoa, yatupasa kufahamu Mapendo.  


5/ NI MAPENDO INAYOKUWA CHINA YA UTOAJI 

MWENYEZI MUNGU HAHESABU UTOAJI UNAOFANYIKA BILA MAPENDO. 


6/ 1 Wakorinto 2: 12 

“Lakini hatukupokea roho ya dunia, lakini Roho anayetoka kwa Mungu; kusudi tupate kujua zawadi tulizopewa na Mungu.” 

Ni kwa sababu gani tulipokea Roho Mutakatifu? 

Kuna sababu nyingi, lakini ni kwa sababu gani Roho Mutakatifu alifanya Makao ndani ya miili yetu?  

Ona sasa moja ya sababu: 

Kusudi tupate kujua zawadi tulizopewa na Mungu. 

Ona tabia ya Mwenyezi Mungu wakati anapotoa: 

Kwa uhuru wote, bila sababu

Siyo kwa sababu tunastahili, lakini anatutolea kwa mapendo. 


7/ Waweza kukadirisha uwingi wa mapendo aliyonayo mtu kwako, kwa kufwatana na namna anavyokuhudumia ama kukutolea, siyo tu kwa kukupatia pesa.  

Unaweza kukadirisha Mapendo ya Mungu kwako kufwatana na yale Mwenyezi Mungu aliyokukabizi na vilevile kufwatana na yale anayoendelea kukupatia na kukubariki nayo. 


8/ 2 Wakorinto 9: 6 

“Lakini ninasema neno hili; yeye anayepanda kwa choyo atavuna kwa choyo; na yeye anayepanda kwa ukarimu atavuna kwa ukarimu.” 

Hapa tuna maneno mawili ya muhimu: 

Kwa choyo na kwa ukarimu. 

Kuna namna mbili ya wapandaji mbegu na kwa kweli kuna swali inayohitaji jibu: Wewe unakuwa upande gani? Ama ungelitamani kuwa kwa kundi gani? 

 

9/ Wagriki wanasema hivi: 

Yeye anayekuwa mupandaji wa mbegu saa zote. 

Ni sura ama picha hili ndilo Mutume Paulo anayokuwa nayo kwa huyu anayetoa. 

Hitaji la mupandaji wa mbegu ni kupanda mbegu, na kweli, kwa kila mukristo, kutoa ni kupanda mbegu. 

Kwa hivyo, sisi wote ni walimaji na shabaa yetu kuu ni kupanda na kuvuna.  

Je inakufikia kuzania na kuona sawa mwenye unapoteza wakati   unapopanda mbegu? 

Siyo kawaida kwa sababu kupanda mbegu kunaleta mavuno. 


10/ Tujiulize sasa swali hili: 

Ni mahali gani mupandaji wa mbegu, alipata yale mbegu alizopanda kwa mara ya kwanza? 

Yeye hangaliweza kuziunda, ni Mwenyezi Mungu aliye mukabizi yale mbegu. 

Yoyote ile unayo kwa namna ya kimwili ama kwa namna ya mapato, ni Mwenyezi Mungu aliye tangulia kukupatia yote unayo. 

 11/ Kuna namna tatu ya hali ya matumizi na mwenendo kufwatana na yale Mwenyezi Mungu aliyokukabizi.

1/  Mwenyezi Mungu alikukabizi mapato yote unayo, Yeye alikukabizi tu na Yeye hajali hata kukuomba chochote kile kwa kumuhudumia Yeye.

 2/  Sisi tulimuiba na kumunyanganya mali, kwa sasa ni pato letu binafsi, hatuna shida lolote juu yake na hatujali hata na neno atakalolisema.

 3/  Ni yeye alitukabizi pato lile kama deni na anapenda tuisimamie na utumizi uwe sawa sawa na mapenzi yake.  

Watu wengi wanaishi sawa vile pato yao ni yao wenyewe na ni kwa wao tu, kwa hivyo wanaamua kuishi sawa sawa na mapenzi yao na hawa jali hata pendekezo ama shauri kutoka kwa Mwenyezi Mungu. 


12/ Eti Mwenyezi Mungu ana lazima ya matoleo yetu? 

Kweli, hakika, ndio.

Siyo kwamba analazimishwa, lakini Yeye anamiliki yote na kuyaongoza hata kuwa mwenye kupendelea kuhitaji matoleo toka sisi walio wake. 

Angalia mufano wa kueneza Injili mahali pote. 

Mwenyezi Mungu hangalianza kuchapa Habari Njema toka huko mbinguni na kukabizi malaika vitabu ili washuke toka mbingu na kuja kupaza sauti katika mawingu, hapa duniani. Mwenyezi Mungu hakufanya hivyo.

Yeye alikua na uwezo wa kuchapa Habari Njema kule mbinguni, lakini Yeye hakufanya hivyo. 

Kupanua na kuenea kwa Injili duniani kutafanyika kwa musaada wetu, nafasi kote kule tutafikisha Injili na kulihubiri kwa mataifa tukiwapasha Injili na kuwaonesha maandiko. 

Mwenyezi Mungu alipendelea sisi tujitoe kwa kupasha na kupanua Injili na aliongoza yote ili itimilike namna sawa. 

Hivyo hivyo kuusu utoaji, Mwenyezi Mungu ni mwenyezi wa mali yote, lakini anapendelea sisi tumutolee ili Huduma ya Injili na Kazi yake isonge mbele. 

Tungelijiuliza sababu gani Mwenyezi Mungu hakuchapa pesa toka kule mbinguni kiisha aigawe kwa watu wanaojitoa katika huduma ya Injili na Kazi ya Mungu, lakini Yeye hakufanya hivyo. 


13/ Luka 16: 1, 2 

“Tena aliwaambia wanafunzi wake: Kulikuwa mtu tajiri, naye alikuwa na mlinzi mali; huyu alishitakiwa kwake, ya kuwa amepoteza mali zake. 

Akamwita, akamwambia: Habari gani hizi ninazosikia juu yako? Toa hesabu ya uwakili wako, kwani huwezi tena kuwa mlinzi mali.” 

Hapa ni Bwana Yesu Kristo mwenyewe ndiye anazungumuzia wanafunzi wake, ya kwamba: Kulikuwa mtu tajiri, naye alikuwa na mlinzi mali; huyu alishitakiwa kwake, ya kuwa amepoteza mali zake. 

Mali ya nani? 

Mali ya bwana wake. 

Akamwita, akamwambia: Habari gani hizi ninazosikia juu yako? Toa hesabu ya uwakili wako, kwani huwezi tena kuwa mlinzi mali.

Tunafahamu ya kwamba haitupasi sisi kutumia ovyo na   kupoteza mali yenye Mwenyezi Mungu aliyotukabizi. 

Yeye anatutia mawakili na anatukabizi muzigo mkubwa wa madeni, namna gani sisi tunatumia mali aliyotukabizi.  


14/ Kanuni ni kwamba: Upandalo ndilo utakalovuna. Nikusema Tavuna ulichapanda. 

Kufwatana na namna na hali upandavyo mbegu, Mwenyezi Mungu anakuonesha picha ya mbele ya namna mavuno yako itakuwa. 

Kama wewe unapanda kwa choyo, ukitia tu mbegu kidogo ndani ya udongo, kwa kweli hauna budi kungojea kwamba kwa mavuno wewe utatarajia magunia kazaa na kazaa za mavuno. 

Wakati unapopanda mbegu, pale pale utakuwa na taswira ya aina ya mavuno, na uwingi wa mavuno utakao vuna. 


15/ Kwa mwangaza wa Maandiko, tuone namna gani utoaji ulikuwa unafanyika. 

Matayo 19: 21, 22 

“Yesu akamwambia: Kama ukitaka kuwa mtimilifu, kwenda zako, ukauze vitu ulivyo navyo, uwape masikini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; na kuja unifuate. 

Lakini wakati yule kijana aliposikia neno hili, akakwenda zake kwa huzuni, kwa sababu alikuwa mwenye mali mengi.” 

Hapa tunakuwa na kijani kiongozi mwenye mali mengi, na anaambiwa: kwenda uuzishe vitu ulivyo navyo. 

Pambanisha maandiko haya na yale tunayopata katika kitabu cha Injili ya Luka 12: 33  

“Uzeni vitu vyenu, toeni sadaka, mujifanyie mifuko isiyochakaa, na hazina isiyopunguka katika mbingu, pahali asipoweza wizi kukaribia, wala nondo kuharibu.” 

Uzicheni vitu vyenu vyote, kiisha toeni sadaka, tena kweli tuna ukweli huu tena katika Kitabu cha Matendo ya Mitume.

 Matendo ya Mitume 2: 45, 46 

“Wakiuza mali zao, na vitu vyao, wakagawia watu wote kama kila mtu alivyokuwa na uhitaji. 

Na siku kwa siku kwa nia moja waliingia hekaluni, wakivunja mkate nyumba kwa nyumba, na kupokea chakula chao kwa furaha, na kwa moyo mmoja.” 

Bali kwa leo Mwenyezi Mungu haitaji wewe kupanda mbegu na kutowa kwa namna ile. 


16/ 2 Wakorinto 8: 12 

“Kwa maana kama nia ni tayari, inakubaliwa kwa kadiri ya mali mtu aliyo nayo, si kwa kadiri asiyo nayo.” 

Tunapashwa kutoa kwa kadiri ya mali tuliyo nayo, si kwa kadiri tusiyo nayo. 

Namna yetu ya kutoa inafwatana na ile yenye inafurika kwa yale tunayo, ile inayo baki. Ngapi tunayo tumia kwa niaba ya sisi wenyewe. 

Mwenyezi Mungu hapendi sisi tufikie kiwango cha kusema kwamba: 

“Kama ningelikuwa na dolla 25, ningelitoa kwa sadaka.” 

Utoaji hauhusike na yale mtu hana, lakini inahusika na yale mtu aliyo nayo.

Mwenyezi Mungu anapenda aone kiwango cha namna gani utatosha katika hakiba yako, hii ni tofauti kweli? 


17/ 1 Wakorinto 16: 1, 2  

“Basi juu ya sadaka kwa sababu ya watakatifu, kama nilivyoamuru makanisa ya Galatia, ninyi fanyeni hivi vilevile. 

Siku ya kwanza ya juma, kila mtu kwenu aweke akiba kwake, kwa kadiri ya mapato yake, ili sadaka zisifanyike wakati nitakapokuja.” 

Hapa Mwenyezi Mungu anasema kwamba, kwa siku ya kwanza ya juma, kila mmoja wetu aweke akiba kwa kadiri ya mapata Mungu aliyo mubariki nayo, ili wakati Mutume Paulo atafika sadaka zisifanyike tena. 

Hapo tena tunapata kanuni ingine: 

Kufwatana na ginsi Mwenyezi Mungu alikubariki

Eti, namna gani Mwenyezi Mungu alikubariki kwa asubui ya leo? 


Eti, wewe ulimtolea Mwenyezi Mungu kufwatana na namna alivyokubariki? 


18/ 2 Wakorinto 9: 7 

“Kila mtu afanye kama alivyokusudia katika moyo wake: Si kwa huzuni, wala si kwa lazima: Kwa sababu Mungu anampenda yeye anayetoa kwa furaha.” 

Mara tena hapa tuna kanuni kwetu: 

Kama alivyokusudia katika moyo wake.


19/  KWA UPEKEE, hapa tulisoma maneno mawili ya muhimu sana. 

Kila mtu, kila mwamini. Siyo lazima kwa asiye mwamini. 

Kila mwamini anaombwa kutoa. 

Roho Mutakatifu anazungumuzia kila mmoja anayetaja Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, hakuna yule anaye tiwa kando. 

Mwenyezi Mungu anahitaji kila mwamini atoe ili huduma ya kazi yake isonge mbele, haizuru kiwango cha pesa kubwa ama ndogo, haizuru awe mtoto sana ama mzee zaidi. 


20/ MWENYEZI MUNGU ANA HAKI GANI YA KUTUOMBA SISI TUMTOLEE? 

Hii ni kwa sababu sisi ni mali yake mwenyewe. 

Sisi ni watumwa wake, na kama watumwa, Yeye anaruhusa ya kutuamuru chochote kile anachopenda tulifanye. 

Sisi ni mali ya Mungu kwa hali mbili:


  1/  Zaburi 24: 1 

“Inchi na kujaa kwake ni mali ya Bwana; Dunia, nao wanaokaa ndani yake.”  

Hii inaonesha kwamba sisi ni mali ya Mungu kupitia muombo. Ni Yeye aliye tuumba na sisi ni mali yake mwenyewe na kwa hiyo anaruhusa ya kutuambia nini tufanye.


2/  Wakorinto 6: 19, 20 

“Hamujui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, muliyepewa na Mungu? 

Na ninyi si mali yenu wenyewe; 

Kwa sababu mulinunuliwa kwa bei; basi tukuzeni Mungu katika mwili wenu na katika roho yenu, maana ni ya Mungu.” 

Sisi ni mali ya Mungu kwa njia ya Ukombozi. 

Sisi tulikuwa zamani katika soko ya watumwa wa zambi na Yeye alitununua kwa Damu ya Damani sana na bei kali mno, kwa hivyo Yeye anaruhusa ya kutuambia tufanye nini na hasa kuusu mali yetu. 


21/ Twende sasa kwa neno linalofwata katika maandiko yetu. 

Neno lile ni msemwa: “Kama alivyokusudia.”  

Katika Kigriki neno hili linakuwa na maana sana. Msemwa huo una maana ya kufanya uamuzi wa kutenda neno kiisha kuchunguza na kukusudia


22/ Kama alivyokusudia katika moyo wake. 

Hii ni msemwa wa musingi wenye hatuwezi pita kwa juu juu. 

Musingi wa utoaji wowote katika Biblia unapatikana katika Kitabu cha Kutoka 25: 2 

“Sema na wana wa Israeli wanitwalie sadaka; toka kila mtu aliye tayari moyoni mwake mutatwaa sadaka yangu.” 

Yafaa tufahamu kwamba kutoa siyo rahisi. 

Mungu alipenda kuisha katika ya wana wa Israeli. Alipenda kupata mahali pa kukaa, hekalu, na kwa kupata hekalu lile Yeye alijitia kwa hali ya kusema kwamba ni wanadamu watakao mtolea vifaa na vitu vyote kwa kujenga hekalu, watakusanyisha vitu vyote pamoja kiisha watamujengea Mungu nyumba. 

Sawa vile munavyo fahamu, Mwenyezi Mungu angaliweza kuamuru hekalu liwe na kwa mahali pasipokuwa kitu, hekalu lingelionekana, lakini Mungu hakupenda kutenda kwa namna ile. 

Yeye alipatia Musa aina, hali na kipimo cha nyumba yake, na alipatia Roho Mtakatifu kwa wanaume na wanawake wa Taifa la Israeli, wenye walipashwa kuhusika na kukusanyisha  vifaa vyote vinavyo hitajika kwa majengo, ni kwa hivyo Mwenyezi Mungu alisema: 

Munitwalie sadaka; toka kila mtu aliye tayari moyoni mwake. 

Siyo halali kutoa kwa moyo wa kushitashita na huzuni, maandiko yafwatayo yanatushauri: 


2 Wakorinto 9: 7  

“Kila mtu afanye kama alivyokusudia katika moyo wake: Si kwa huzuni, wala si kwa lazima: Kwa sababu Mungu anampenda yeye anayetoa kwa furaha.”  

Kwa kweli hii inamaanisha hali ya huzuni. 

Kusiwe hata mtu yeyote atakaye huzunika wakati anapomtolea Bwana. 

Siyo vizuri kusema: Pole kwangu sababu nimetoa zaidi ya vile nilikuwa napendelea kutoa. 

Ingelikuwa heri kusema: Nashukuru Mungu kuona nimetowa kwa kiwango niliyotoa. Na ningelitamani kutoa zaidi ya yale. 

Ni hofu tena zaidi, Matoleo hayapashwi kuwa ya mkazo, mtu kujisikia sawa anasukumwa kutoa, anasukumwa kwa kinguvu, watu wanapenda wapate faida juu yake. 

23/ Nilipata habari kuhusu kanisa moja, na kanisa lile siyo mbali na hapa, katika hiyo kanisa, wakati wa sadaka wao wanatumia “Matoleo ya maandamano.” 

Na wanafanya namna hii: 

Mtu moja anashimama hapo mbele ya wote, na kila mmoja wakati wa kutoa sadaka anashimama toka mahali alipokaa na kuja akitembea akijeelekeza mbele na kutoa sadaka yake huko. 

Mimi sina maandamano ya namna sawa na siamini mambo yale. 

Hii ni kutoa ya mkazo, tena kusifu yeye anaye toa na pia sadaka yenye mtu anaenda kutoa huko mbele inaonekana na watu wote kanisani. 

Kama mmoja anatoa sadaka musiyofurahia, hapo hapo munamuambia kwamba asitoe na Mungu hafurahie sadaka yake.

Musingi wa utoaji ni mapendo na roho yenye kuwa tayari kwa kutoa. 


24/ KWA UHURU WOTE

Mwenyezi Mungu anatutolea kwa uhuru wote na anahitaji nasi vilevile  tumtolee kwa hali hiyo. 

Uhuru unachina lake katika Kigriki kwa neno DOE RAY ON, na inamaanisha bila sababu, bila nia lolote.  


Waroma 8: 32 inasema:    

“Yeye asiyeachilia Mwana wake, lakini alimtoa kwa ajili yetu yote, namna gani atakosa kutuletea vitu vyote pamoja naye?”  

Yeye alitupatia vitu vyote kwa uhuru wote, kwa hivyo ingelitupasa kusema: Bwana sisi hatutarajiye wewe uturudishie kitu.

Tunafahamu kweli ya kwamba utayafanya, ila tulipendelea kukutolea kwa uhuru wote. 


25/ kiisha yafaa tutoe KWA FURAHA

Wakati Mwenyezi Mungu alipotutolea Mwana wake, hakumutoa akiwa akifunga nyuso. 

Bali alimutoa kwa FURAHA na UHURU wote, na Roho Mtakatifu ni Zawadi kutoka kwa Mungu na Wokovu vilevile ni Zawadi kutoka kwa Mungu na haya yote Mungu alitukabizi kwa FURAHA toka kwake. 

Kwa sasa tunahitajika kusema: Leo nimepata nafasi na bahati nzuri ya kumtolea Mungu wangu ili Huduma na Kazi yake isonge mbele. 


26/ Sawa vile tulivyosema kwa mwanzo: 

MUNGU ANAMPENDA YEYE ANAYETOA KWA FURAHA

Tujiulize sasa swali hili: 

Eti, Mwenyezi Mungu anawapenda watu wote? 

Hata wao waliookolewa na wale wasiookolewa? 

Kwa kweli, Mungu anawapenda watu wote. 

Eti Mungu anampenda kila mwamini bila kujali kwamba huyu ananitolea ama hapana? 

Bila shaka ni hivyo. 

Mungu anasema, Yeye Mungu anampenda yeye anayetoa kwa furaha. 

Kila mtu, kila mwamini ni kazi ya mikono na Mapendo yake. 

Bali wakati mtu anafungua mufuko wake wa akiba kwa kubeba kazi ya Mwenyezi Mungu, kwa kueneza na kutangaza Injeli, mtu huyo anakuwa kipendeleo cha Mapendo ya Mungu. 

Hiyo ndiyo njia ya kupata Baraka ya kipekee toka Mwenyezi Mungu. 

 

27/ Kutoka 35: 21   

“Wakakuja kila mtu aliyesukumwa kwa moyo wake, kila mtu roho yake ilimfanya kuwa mwenye kutaka, wakaleta sadaka kwa BWANA kwa kazi ya hema ya kusanyiko, na kwa utumishi wake, na kwa yale mavazi matakatifu.” 

Namna gani Taifa la Israeli ilipokea na kujiandaa juu ya mwito wa Mungu kwa kumjengea Mungu Hekalu? 

Kila mtu aliyesukumwa kwa moyo wake na kila mtu roho yake ilimufanya kuwa mwenye kutaka. 

Matoleo yao ikawa nyingi kupita kiasi hata ikamulazimisha Musa aamuru watu kuacha kuendelea kuleta matoleo. 


Kutoka 36: 6 

“Musa katoa amri, wakaitangaza katika kambi, kusema: Mwanamume wala mwanamke wasifanye tena kazi nyingine kwa sadaka ya pahali patakatifu. 

Hivi watu wakazuizwa wasilete tena.” 

Watu wa Taifa la Israeli wakazuizwa kuendelea kuleta sadaka. 

Maandiko Matakatifu yanatuonesha wazi kwamba watu walikatazwa wasilete tena sadaka. 

Naamini ya kuwa watu wa Taifa la Israeli hawakumaliza yale   waliotayarisha na waliokusudia kutoa. 


28/ 2 Wakorinto 9: 15 

“Mungu ashukuriwe kwa sababu ya zawadi yake tusiyoweza kuisifu kama inavyopasa.” 

Hapa Mwenyezi Mungu anatuambia kwamba anastahili kushukuriwa kwa sababu ya zawadi yake tusiyoweza kuisifu kama inavyopasa. 

Hii ni chanjo na sababu kamili inayopashwa kutusukuma sisi kumutolea. 

Wakati mtu anapokutolea ama kukupatia kitu fulani, roho yako na mafikili yako inajaa na hamu sana na kukusukuma   wewe vilevile upate kumutendea vivyo hivyo kwa kumtolea ama kumukabizi kitu kingine. 

Mungu anampenda yeye anayetoa kwa furaha. 


AMEN 


N°Ref: 07/26/20 / 621-2 HEAVEN’S LAW OF SUPPLY AND DEMAND / 10/14/2020