Wednesday, March 24, 2021

JE MWENYEZI MUNGU ALITUAHIDI HADISI ZA MBINGU IZUNGUUKAO NA CHAKULA CHA RAHA / GOD HAS PROMISED YOU A PIE IN THE SKY

Photo by B Smith from the kitchen door


 


JE MWENYEZI MUNGU ALITUAHIDI HADISI ZA MBINGU IZUNGUUKAO NA CHAKULA CHA RAHA 

452 - 1 GOD HAS PROMISED YOU A PIE IN THE SKY

November 5, 1978

Pastor Henry F. Kulp



 

Waroma 8: 28 – 34 

“Na tunajua maneno yote yanafanya kazi pamoja kuwapatia mema wale wanaopenda Mungu, kwa wale walioitwa kwa kusudi lake. 

Kwa sababu wale ambao aliwajua tangu zamani, aliwachagua tangu zamani wafananishwe na sura ya Mwana wake, ili awe Mzaliwa wa kwanza katikati ya ndugu wengi. 

Na wale ambao aliwachagua tangu zamani, akawaita vilevile; na wale ambao aliwaita, akawahesabia haki: na wale ambao aliwahesabia haki, akawatukuza vilevile. 

Basi tutasema nini juu ya maneno haya? 

Kama Mungu akiwa upande wetu, ni nani aliye juu yetu? 

Yeye asiyeachilia Mwana wake, lakini alimtoa kwa ajili yetu sote, namna gani atakosa kutuletea vitu vyote pamoja naye? 

Ni nani atakayeshitaki wachaguliwa wa Mungu? Mungu ambaye anawahesabia haki; 

Ni nani anayehukumu? 

Ndiye Kristo aliyekufa, ndiyo, zaidi, amefufuka, naye yuko kwa mkono wa kuume wa Mungu, tena ndiye anayetuombea.” 

Sehemu hii ya Maandiko, inatajwa na kutamkwa na watu wengi, bali wanaofahamu maana yake ni wachache mno.

Asubui ya leo ningelipendelea sote tupate kufahamu Maandiko haya yaliyo bora na ya muhimi sana. 

Watu wengi wanawaambia kwamba  si kama Mwenyezi Mungu aliwaahidi mbingu zinazozunguukwa na chakula cha raha, na vivi hivi.

Lakini, kiisha kumaliza majifunzo yetu ya asubui ya leo, matakwa yetu ni ninyi mufikie  kiwango cha kufahamu kwamba Mwenyezi Mungu aliwaahidi mbingu zinazozunguukwa na chakula cha raha, sasa na tena siku za usoni na siku zitakazokuja.  

Tutafurahi wakati tunapochanga yote mbili pamoja. 


1/ Maisha yetu ya sasa na yale yatakayokuja yote mbili yanashikamana pamoja. 

  HUWEZI kuishi barabara kwa sasa kama mecho yako hayatazami kwa yale yatakayokuja. 


2/ Hapo Mwenyezi Mungu  anazungumuzia kuhusu mateso.

Mateso yenye Mungu anaona yakikumba mtoto wa Mungu, na hapo tuliona kwamba mtoto wa Mungu ana namna mbili ya kusitawi mbele ya mateso. 

Ya kwanza tunapata katika Waroma 8: 18 

“Kwa maana ninahesabu mateso ya wakati huu wa sasa kuwa si kitu tukiyafananisha na utukufu ule utakaofunuliwa kwetu.” 

Matatizo, mateso, kuvinjika moyo, na mashindano mbalimbali yote ni kwa muda kitambo tu hapa chini duniani bali utukufu utakuwa kwa milele

 

3/ Jambo la pili tunalipata kwa Aya ya 28, na hii inasema:  

Hii ni jambo twapashwa kufahamu kwa sasa. 

“Na tunajuwa maneno yote yanafanya kazi pamoja kuwapatia mema wale wanaopenda Mungu, kwa wale walioitwa kwa kusudi lake.” 

Kwa sasa, Mwenyezi Mungu anatwaa shida na matatizo yetu, akiyachanga pamoja na miradi yake, mipango yake na haya yote yanatuletea mema kwetu. Mema hakika


4/ 1Watesalonika 5: 18 

“Katika maneno yote mushukuru; maana maneno haya ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.” 

Hapa, tunashurtishwa, ni oda, ni aina ya umuhimu, na tunaombwa kwamba katika maneno yote tushukuru; maana maneno haya ni mapenzi ya Mungu kwetu katika Kristo Yesu. 

Aya hii ni Andiko la muhimu sana tunalopashwa kufahamu. 

Mara kwa mara kuna hali nyingine linalo kuwa kwetu vigumu sisi tushukuru Mungu, katika maneno yote kama hatufahamu na kusikia yale          Waroma 8: 28 inayotuambia, kwa sababu aya hizi mbili zinashikamana mukono kwa mukono. 

Ni vigumu kwetu kushukuru Mwenyezi Mungu kwa yote yanayotufikia kama sisi hatuwezi kufahamu kwamba yote yanayotufikia ni katika mipango ya Mungu kwetu, matakwa ya Mungu kwetu na miradi ya Mungu kwetu, na mema  yabubujika kwetu kwa njia ya mambo yale yote. 


5/ Tayari wakwisha kumushukuru Mwenyezi Mungu wakati bado ungali ndani ya  mashindano na matatizo yanayokukumba.  

Wapashwa pia waweza kama ukifahamu Maandiko ya Waroma 8:28.   

 

Waroma 8: 28

“Na tunajua maneno yote yanafanya kazi pamoja kuwapatia mema wale wanaopenda Mungu, kwa wale walioitwa kwa kusudi lake”

  Wakati ufahamu wako unastarehe, ni kwepesi kumushukuru Mungu kwa mambo yote, matatizo, mashindano, na mateso yote, hiyo mambo yote yanayotukumba na kutuvunja moyo, yote yanaenda pamoja na miradi ya Mungu kwenu na yanatufikia kwa kutuletea sisi mema. 


6/ Ni ya muhimu na ya manufaa sana kutambua  neno hili: 

WALE WANAOPENDA MUNGU.

Hii ni jina na hali inayokuwa kwa upekee kwa waamini mtupu, kitambulisho ya waamini. 

Hii haileti tufauti kwa wale wanaompenda sana Mungu ama wale wasiompenda kwa lengo la juu, bali inasema tu kuhusu wale wanaompenda MUNGU

Haijali mapendo yako ni kiwango gani. 

Haijali kwamba wewe wampenda Mungu sana zaidi ama siyo sana zaidi.  

Ila tu wewe wampenda Mwenyezi Mungu. 

Hii ni tamko, pendekezo inayokuwa juu ya wote, na yenye kufahamika. 

1Wakorinto 16: 22 

“Kama mtu asipopenda Bwana Yesu Kristo, amelaaniwa. Maranatha.” 

Yapashwa kumpenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa sababu Yeye alitupenda wa kwanza. 

Yatupasa kufikili kuhusu mapendo yetu kwa Kristo na kufahamu ya kwamba upana na urefu chini  ya mapendo yetu yaambatana na namna tunayo fahamu Kawaida ya Mafundisho ya Biblia inayohusu Bwana Yesu Kristo. 

Kuna mara walewanaosema ya kwamba wanampenda Bwana Yesu Kristo, kwa kweli hawampendi, kwa sababu hawamjui. 

Hawajuwi Kawaida ya Mafundisho ya Biblia. 

Haiwezikani wewe kumpenda mtu usiyemjua. 


7/ KWA WALE WANAOMPENDA.

NENO HILI LINATAFSIRIWA NDANI YA NENO MOJA TU KATIKA UTAFSIRI WA KIGRIKI. 

Ni katika aina, sarufi inayoonesha uhusikatendea, ama faida. 

Ni faida kwetu kumpenda Mungu. 

Kiisha neno lile linaandikwa kwa uwingi kwa kumaanisha kwamba kuna umati wa watu katika ulimwengu wanaompenda Mungu. 

Kwa kweli, kila aliyeokoka anampenda Mungu. 


8/ Ni katika hali ya kutenda, ilikuonesha kutaka kwa mwamini. 

Ni kuhusiliana na Mungu


9/ KWA WALE WALIOITWA

Wale walioitwa, walichaguliwa. 

WALIO ni tendo lililotoka kwa tendo la KUWA DAIMA. 

Kwa hivyo tafsiri letu linakuwa: 

Kwa wao wanaokuwa daima WALIOITWA. 

Walioitwa inaweza tafsiriwa sawa “WALIO CHAGULIWA” 

Neno “WALIOCHAGULIWA” ni tendo la kazi linalomaanisha kwamba Sisi tumo katika miradi ya Mwenyezi Mungu

Tunageuka wachaguliwa kwa milele kwa wakati tunapomwamini na kumupokea Bwana wetu Yesu Kristo kama Mwokozi wetu. 

Tukamate muda kidogo katika kawaida ya mafundisho haya, na tufahamu namna gani watu walikuwa wanasaliti kawaida ya mafundisho haya. 


(1) Kizazi cha wanadamu walikuwa katika hali ya kuchaguliwa katika miradi ya Mwenyezi Mungu ya wokovu bila mpaka. 

2Timoteo 2: 10 

“Kwa ajili ya hili ninavumilia maneno yote kwa sababu ya wachaguliwa, wapate wokovu ulio katika Kristo Yesu, pamoja na utukufu wa milele.” 


(2) KRISTO alichaguliwa tangu zamani za kale za milele. 

Isaya 42: 1 

“Tazama Mtumishi wangu ambaye ninamshika, Mchaguliwa wangu, na Nafsi yangu inapendezwa naye, nimetia Roho yangu juu yake, Naye atatoa  hukumu kwa mataifa.” 

1Petro 2: 4 – 6 

“Na mukikuja kwake, Jiwe lenye hai, lililokataliwa na watu, lakini Chaguliwa kwa Mungu, Lenye heshima. 

Ninyi vilevile, kama mawe yaliyo hai, mumejengwa muwe nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu, kutoa zabihu za roho, za kupendeza Mungu kwa njia ya Yesu Kristo. 

Kwa kuwa imeandikwa katika Maandiko: 

Tazama ninaweka katika Sayuni Jiwe kubwa la pembeni, Chaguliwa , Lenye heshima; 

Naye ambaye anamwamini hataona haya.” 

Kwa kweli, ukijifunza Biblia yako nzima kwa makini sana utatambua kwamba ni Yeye pekee ndiye Mtu aliyechaguliwa. 

Miaka ma elfu ya ma milioni zamani za kale, Mungu Baba, Mungu Mwana na Mungu Roho Mtakatifu alifanya kikao. 

Ilikuwa miaka ma elfu ya ma milioni mbele ya kuumbwa kwa Adamu, Mwenyezi Mungu alijuwa na kufahamu yote, hata kuweko kwako na kuweko kwangu katika mwaka huu wa karne ya 21. 

Katika mazungumuzo yao, walipanga  miradi. 

Kiini ya miradi hiyo ilikuwa kuhusu Bwana Yesu Kristo. 

Mupango kuhusu Bwana Yesu Kristo. 


(3) Ni ya muhimu sana kujuwa kwamba mwamini wowote ni mchaguliwa katika kuchaguliwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo. 


(4) Katika Biblia Takatifu kuna Miradi miwili za msingi: 

Inchi ya Israeli inayokuwa Miradi ya Unabii, 

Mwili wa Kristo iliyo Miradi ya Siri iliyofichwa. 

Kila muyuda wa kweli ni mwanamemba katika kuchaguliwa kwa Bwana Yesu Kristo katika Ufalme, wakati Bwana Yesu Kristo atamiliki dunia yote na kuwa Mufalme wa wafalme wote, na yeye atakuwa pamoja na Kristo katika Ufalme huo. 

Katika Mwili wa Kristo, kila mwenye anayeamini Bwana Yesu Kristo, yeye anakuwa mmoja wa wanamemba katika kuchaguliwa kwa Bwana Yesu Kristo, akiwa kiungo cha Mwili wa Kristo. 

Ni ya muhimu sana kujitambua kuwa kama muchaguliwa, kuwa muchaguliwa wa Yesu, tunapashwa kuwa na uhusiano NAYE.  

Na kundi hizi zote mbili, ikiwa Taifa la Israeli, ama  ikiwa Kanisa Mwili wa Kristo, yote mbili ina uhusiano na Yesu Kristo. 


(5) Tunakuwa wanamemba ndani ya Kuchaguliwa kule kwa saa ile ile tunapookolewa. 

Ni kusema kwamba tunakuwa wanamemba wa kule kuchaguliwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo, wakati tunapomwamini kama Bwana na Mwokozi wetu, wakati wa wokovu wetu. 


10/ Waroma 8: 29 - 30  

“Kwa sababu wale ambao aliwajuwa tangu zamani, aliwachagua tangu zamani, wafananishwe na sura ya Mwana wake, ili awe Mzaliwa wa kwanza katikati ya ndugu wengi. 

Na wale ambao aliwachaguwa tangu zamani, akawaita vilevile; na wale ambao aliwaita, akawahesabia haki: na wale ambao aliwahesabia haki, akawatukuza vilevile.” 

Katika Aya hizi mbili tunapata hatuwa tano inayoelekea hadi utukufu.

Hatua tano zinazotutosha toka chimo la Jehenamu la uchafu na kutuchukuwa hadi utukufu wa mbinguni. 

Kwa kweli, hatua hizo tano zinatuhusu sisi, sababu kuna maneno tano yenye Mwenyezi Mungu anafanya ndani yetu. 

Yote ni kazi ya Mungu, ni kwa hiyo twasema YOTE NI KWA NEEMA


11/ HATUA YA KWANZA 

Kujuwa tangu zamani

Hatua ya kwanza ni kwamba, mamilioni maelfu ya miaka hapo zamani za kale, Mwenyezi Mungu alikuwa na mawazo kuhusu wewe hapo tangu zamani, wewe bado kuwa. 

Kujuwa tangu zamani inafuatana ta aina ya Mungu Baba ya Kujuwa yote, kwa kweli Yeye alikuwa anajuwa yote tangu zamani kuhusu kila mmoja wetu. 

Tangu zamani za kale, Mwenyezi Mungu alikuwa anamjuwa kila mmoja wetu binafsi kwa upekee, alikuwa anamjuwa kwa upekee kila mmoja atakaye zaliwa hapa duniani, kama haingelikuwa hivyo, basi yeye hangalikuwa Mungu. 

Miradi na Mipango yake ilianza katika UFAHAMU wake(MAWAZO yake).  

MAWAZO ya Mungu ni Kamilifu, ni kwa hiyo, Mipango yake yote ni kamilifu.  


12/ Hakuna hata mmoja atakayeweza kunongona ama kulialia kwamba yenye anaachiliwa ama anatupiliwa na wote. 

Je waweza kutaja jina la mtu mmoja aliyekufahamu kabla wewe bado haujazaliwa? 

Ni nani huyo angaliweza hata kuwa na mawazo juu yako? 

Je wazani kwamba mapepo ama mashetani wangaliweza kuwa hata na mawazo kuhusu wewe? Hapana hata kidogo. 

Kwa kweli sheteni ni mwerevu kiasi, lakini hangaliweza kuwa hata na wazo moja juu yako. 

Hakuna hata malaika ama mizimu yenye ingeliweza kuwa na mawazo juu yako kabla wewe bado kuzaliwa, ni Mwenyezi Mungu peke yake anayeweza. 


13/ Tena Mwenyezi Mungu alifahamu tangu kale kwamba wewe utaokolewa. 

 Neno hili lisiwasumbue. Hii inaambatana na hali ya Mungu ya kufahamu neno tangu zamani za kale. 

Ufahamu wa Mungu juu yako na Mawazo ya kwanza aliyokuwa nayo tangu zamani za kale kuhusu wewe, yote yalikuwa katika MAPENDO


14/ HATUWA YA PILI 

KUCHAGUWA TANGU ASILI 

Kuchagua tangu asili ni moja ya maneno yenye watu hawafahamu wazi wazi katika Biblia. 

Watu wengi wanazani kwamba kuna sehemu ya watu waliochaguliwa tangu asili ili wao waende mbinguni, na wengine walichaguliwa tangu asili ili waende katika Jehenamu, lakini hiyo siyo kweli. 

Hakuna hata mmoja aliye chaguliwa tangu asili ili aende Jehenamu. 

KRISTO alikufa kwa ajili ya watu wote ulimwenguni. 


15/ Utafsiri katika Kigriki wa neno KUCHAGULIWA TANGU ASILI ni “Kuweka mipaka”

Mutatambuwa kwamba katika Swahili tamko “tangu asili” inamaanisha mbele ya mambo yote, na kuchaguwa inamaanisha kufikia kiwango: kituo cha mwisho. 

Kwa kuendelea sasa tunasoma: “Alituchaguwa tangu asili, ona neno linalofuata,   tufananishwe na sura ya Mwana wake” 

Tunatambua kwamba kuchaguliwa tangu asili kunaambatana na hali ya Mungu ya Kujua tangu zamani na hii inamaanisha kwamba siku moja mwamini atariti pamoja na Yesu Kristo yale yatakayokuwa kwa ajili ya Yesu Kristo na mwamini atakuwa kama YEYE.  

Muniruhusu niwaulize swali. 

Jambo hili ni vizuri ama vibaya?  

Kwa kweli ni vizuri kupita kipimo. 

Matendo yangu ni ya namna gani wakati wa mateso?

Ninafahamu ya kuwa Mwenyezi Mungu alikuwa na mawazo kuhusu mimi tangu zamani za kale mbele ya miaka ma elfu ya ma milioni; Yeye alifahamu ya kwamba nitaokolewa, na Yeye alikuwa na Miradi iliyokuwa na mipango kamili juu yangu kwamba siku moja nitakuwa sawa sawa na Bwana wangu Yesu Kristo. 


16/ Kuna jambo zaidi kuliko hilo lenye Mwenyezi Mungu angeliweza kufanya kwa ajili yako? 

Waweza kupima kuwaza kuhusu jambo lingine nzuri lenye Mwenyezi Mungu angeliweza kufanya kwa ajili yako, jambo nzuri kuliko wewe kufananishwa na Bwana Yesu Kristo?  

Waamini wengi tayari wamekwisha kuja kwangu kuniambia: 

“Uniombee ili nifanane kweli na Bwana Yesu Kristo” 

Kila yule anayekuwa na maisha ya kiroho, maisha ya utawa anakuwa na hamu sana ndani mwake ya kufanana na Bwana Yesu Kristo. 

Mwenyezi Mungu alikuchaguwa tangu zamani uwe sawa na MWANA wake; 

Je hii siyo Jambo la Mshangao Kweli na Kitu chema kuliko? 

Kwa kweli hii ni Neno kubwa la raha lenye Mwenyezi Mungu alifanya. 

Mwenyezi Mungu angelikungojea wewe ujikaze ufanane na Yesu Kristo, neno hili halingeliwezekana hata kidogo. Wewe hungeliweza hata mara moja kufanana na Bwana Yesu Kristo. 

Wewe huna hata njia moja binafsi ya kufikia kufanana na Bwana Yesu Kristo.  


17/ Namna gani mimi nina salama ya milele? 

Mimi niko ndani ya Miradi na Mipango ya Mwenyezi Mungu na Yeye , tangu milele alifahamu mwelekezo wangu utakuwa wa njia gani, na hii siyo kwa nguvu yangu, ni mpango wa Mwenyezi Mungu kwa ajili yangu, kwa sababu mimi ni mwamini anaye amini Bwana Yesu Kristo. 


18/ Mutatambua ya kwamba maneno yote yanasemwa katika nyakati iliyopita. 

Kwa sababu wale ambao aliwajuwa tangu zamani, aliwachagua tangu zamani, aliwaita vilevile, na wale ambao alioita akawahesabia haki, na wale ambao akawahesabia haki, akawatukuza vilevile. 

Wewe unaweza kutizama hali hii ya mwisho “kutukuzwa” na unajiuliza, kwa kweli sisi kwa leo tunatukuzwa? 

Kwa kweli katika Mafikili ya Mwenyezi Mungu, sisi ni wenye kutukuzwa, sawa sawa na kama neno lile linakwisha fanyika. 


19/ HATUWA YA TATU   

      KUCHAGULIWA 

Kila mwamini yeyote ni Miradi ya Mwenyezi Mungu, neno kuitwa INAHUSU MARINGO, KUPEWA KAZI FULANI. 

Mwenyezi Mungu alituwekea nyakati katika maisha yetu. Alitutia katika karne ya makumi mawili na moja.  


20/ HATUWA YA INE 

     KUHESABIWA HAKI. 

Wenye haki?  Ndiyo kwa kweli sisi ni wenye haki kama Mwenyezi Mungu, sisi tumevaa haki ya Mungu. 

Mwanadamu mwenye mpaka leo anatereza katika zambi, lakini mbele ya mecho ya Mwenyezi Mungu, yeye ni Mtakatifu. 


21/ HATUWA YA TANO 

     KUTUKUZWA

 Siku moja sisi tutatukuzwa. 

Tutakuwa na mwili wa utukufu. 

Wafilipi 3: 20, 21 

“Kwa maana sisi ni wenyeji wa mbinguni; kutoka pale tunangoja Mwokozi, Bwana Yesu Kristo; 

Atakayebadilisha mwili wetu wa haya upate kufanana na Mwili wake wa utukufu, kwa uwezo ule anaoweza kutiisha vitu vyote viwe chini Yake.” 

Hapa chini duniani, hakuna utukufu, kuna tu namna ya utukufu wa muda kitambo, lakini kutakuwa utukufu wa milele, na sisi sote tutabadirishwa. HALELUYA! 


AMINA 


N°Ref: 11/05/1978 / 452-1 GOD HAS PROMISED YOU A PIE IN THE SKY / 03/24/2021