Tuesday, September 29, 2020

WOKOVU NA SIKU YA BWANA / SALVATION AND THE LORD'S APPEARING


Photo taken by B Smith from the patio
 

 


WOKOVU NA SIKU YA BWANA 

SALVATION AND THE LORD'S APPEARING

January 13, 1963 

Pastor Henry F. Kulp



 

1 Watesalonika 1: 1 – 5 

“Paulo, na Silvano, na Timoteo, kwa kanisa la Watesalonika katika Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo: Neema iwe kwenu na salama toka Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo. 

Tunashukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu ninyi wote, tukiwataja ninyi katika maombi yetu; tukikumbuka pasipo kuacha kazi yenu ya imani, na taabu yenu ya mapendo, na saburi yenu ya tumaini katika Bwana wetu Yesu Kristo, mbele ya Mungu Baba yetu; tukijua, ndugu munaopendwa na Mungu, kuchaguliwa kwenu, sababu Habari Njema yetu haikufika kwenu katika neno tu, lakini vilevile katika uwezo na katika Roho Mtakatifu, na katika matumaini mengi; sawasawa munavyojuwa tulikuwa watu wa namna gani katikati yenu kwa ajili yetu.” 

Juma iliyopita tulijifunza na kuonesha mazingira ya kuzaliwa na kuanzishwa kwa kanisa la Tesalonika. Kanisa hili lilianzishwa katika hali ya upekee na maajabu, kwa jia ya maelekezo machache yaliyotolewa na Mtume Paulo. 

Kwa kweli ilikuwa hatua ya mwanzo kwa kazi kubwa ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 

Kama vile munavyokumbuka, sawasawa tulivyowaambia, hii ni mabarua ya kwanza yenye Mtume Paulo aliandika pale Korinto wakati alipotoka Beroya kwa sababu ya mateso na mashambulizi.

 Timoteo na Sila wao sawa vile walivyoagiza na Mtume Paulo, wao, walibaki nyuma na walikwenda Tesalonika na kiisha walirudi kumpa Mtume Paulo ripoti ya hali ya yale makanisa changa. 


1/ Wengi wa washiriki katika Kanisa lile walikuwa watu toka wapagani na watu wasiokuwa wayuda, lakini wengi wa washirika walikuwa wapagani, sawa vile tunaweza kuiona kwa aya ya 9

“Kwa sababu wao wenyewe wanatangaza habari zetu namna tulivyoingia katikati yenu; na namna gani mulivyogeuka kwa Mungu toka sanamu, kutumikia Mungu aliye hai, na Mungu wa kweli;” 

Mtume Paulo alikuwa saa zote akifikiri na  kujali sana kuhusu maisha ya kiroho ya  wale wakristo wachanga, kwa hiyo,  Mtume Paulo anatuambia kwamba moyo wake haukuwa na pumziko, alikuwa akingoja kwa hamu sana ujio wa Timoteo na Sila, akiwa na hofu kwamba shetani asije akawajaribu wale wakristo wachanga walioamini Yesu. 


1 Watesalonika 3: 5 

“Kwa sababu hii mimi, wakati nilipokuwa siwezi kuvumilia tena, nilituma mtu nipate kujua imani yenu, asiye mjaribu akawajaribu ninyi, na taabu yetu ikakuwa pasipo faida.” 

Bali kwa aya ya sita anatuambia kwamba habari zilimufikia na taarifa zilikuwa za kutia moyo. 

Na hiyo ndiyo iliyosukuma Mtume kuandika Waraka huu. 


2/ Ni vizuri sana kufahamu ya kwamba siku ya Bwana Yesu Kristo, ama siku ya kunyakuliwa kwa Kanisa inazungumuzwa mahali pote katika Sura zote za Waraka huu wa Watesalonika. 

Kumbukeni kwamba Waraka huu ulioandikwa kwa niaba ya Wakristo wachanga katika Yesu Kristo, inatuonesha umuhimu wa Siku ya Bwana, siku Bwana Yesu atakuja na kuonekana pale mawinguni, na hapo itakuwa kunyakuliwa kwa Kanisa.

Kiini ya jambo hili ni kutia mkazo kwamba hata watoto wachanga katika Kristo wanapashwa  kufahamu sana  kawaida ya mafundisho haya. 

Ni huruma kweli kusikia kwa siku ya leo watu wakituambia kwamba hiyo kawaida ya mafundisho siyo ya mahimu na haitupasi kushikamana nayo kwa kiwango namna sawa. 

Wangapi wale wasiohubiri juu ya kuja kwa Bwana Yesu.

Lakini majifunzo yetu ya leo yanatuonesha umuhimu wake. 


3/ Tuone sasa mambo makuu yanayokuwa katika Waraka wa Watesalonika. 

Waraka wote nzima unahusika na Siku ya Bwana Yesu Kristo. 

Sura ya kwanza inaonesha uhusiano unaokuwa kati ya Wokovu na Kuja na kuonekana kwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 

Sura ya pili inatufunulia wazi uhusiano unaokuwa kati ya kazi ya mwamini  na Kurudi kwa Bwana wetu Yesu Kristo. 

Sura ya tatu inahusu uhusiano kati ya maisha ya utakaso na siku ya Bwana. 

Sura ya ine inasema juu ya uhusiano  kati ya ufufuko na kuonekana na kuja kwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 

Na Sura ya tano inaonesha Salama ya mukristo na kuja na kuonekana kwa Bwana Yesu Kristo. 


4/ Tujifunze sasa Aya hii ya kwanza

Aya hii ya kwanza inatupatia salamu. 

Tunaona ya kwamba katika aya hii hakuna matumizi ya majina ya madaraka ya mitume.    

 Tunapata tu majina pekee sawa ya akina Paulo, Silvano( yeye ndiye Sila) na Timoteo. 

Kuachwa kwa matumizi ya jina ya madaraka kama akina “Mtume” bila kuitia mbele ya jina “Paulo” ni jambo la muhimu sana. 

Jambo hili Mtume Paulo alilifanya mara tena katika Vitabo tisa juu ya Vitabu kumi na tatu alivyo andika. 

Katika Kitabu cha Wafilipi, moja ya hayo yenye hakutumikisha jina “Mtume”, katika Kitabu kile alijiita “Mtumishi wa Yesu Kristo”. 

Ni vema sana kutambua kwamba katika I na II Watesalonika, hakutumikisha jina la madaraka, lakini alitumia jina lake pekee “Paulo”. 

Hii inamaanisha kwamba mbele ya watu hawa Paulo hakuwa na haja ya kujitambulisha. 

Katika Waraka nyingine mbalimbali alizo andika, yeye alipashwa kujitambulisha kwa kuonesha huduma yake kama mtume. 

Bali, kwa kanisa la Watesalonika, walikuwa wakiheshimu neno lolote la Mtume Paulo, haikuwa budi kwake kujitambulisha kwamba yeye ni Mtume. 

 

5/ Kumbukeni kwamba jina, Paulo, inayomaanisha mdogo ama mfupi, ilikuwa jina alilopewa na mtu wa mataifa, mtu wa kwanza aliye hubiri na kumuleta kwa Yesu Kristo katika kisiwa cha Pafoti. 

Jina Timoteo ni mchango wa majina mawili toka Kigriki: 

Timao: inayomaanisha yeye anaye mucha Mungu. Na kulingana na hilo tunasema kwamba Timoteo alikuwa kijana aliye mucha Mungu maishani mwake. 


6/ Tuchunguze sasa kuhusu kanisa la Watesalonika. 

Mara kwa mara tulikuwa tukizungumuzia juu ya jina “Ecclesia” inayo maanisha kanisa ama mukusanyiko wa watu walioitwa. 

Katika Agano la Kale, Taifa la wana wa Israeli walitumia neno kanisa. 

Neno lile lilitumikishwa pia juu ya kutambulisha kundi la wapigakelele. 


Matendo ya Mitume 19: 32 – 41. 

“Basi wengine walikuwa wakilia neno moja, na wengine neno lingine, kwa sababu makutano yamechafuka, na zaidi yao hawakujuwa kwa maana gani wamekwisha kukutana. 

Walitoa Alesanduro katika makutano, Wayuda wakamweka mbele ya watu, Alesanduro akawapungia mkono, akitaka kujibu watu wake. 

Lakini wakati walipotambua ya kuwa yeye ni Myuda, wote pia kwa sauti moja walipiga kelele kwa kadiri ya saa mbili, wakilia: Diana wa Efeso ni mkubwa. 

Kisha mkubwa wa mji alituliza makutano, akasema: Wanaume wa Efeso, mtu gani asiyejuwa ya kuwa mji wa Efeso ni mlinzi wa hekalu la Diana, aliye mkubwa, na wa sanamu iliyoanguka toka mbingu? 

Basi, kwa sababu maneno haya hayawezi kukanwa, imewapasa ninyi kunyamaza, musifanye neno kwa haraka haraka. 

Kwa maana mumekwisha kuleta watu hawa wasio wizi wa hekalu, wala wenye kutukana mungu wetu.

Basi kama Dimetrio, na mafundi walio pamoja naye wana neno juu ya mtu, kuna baraza na wakubwa: washitakiane. 

Lakini mukitafuta neno katika maneno mengine, yatatengenezwa mbele ya wakubwa katika baraza. 

Kwa maana tuna hatari ya kushitakiwa kwa ajili ya matata haya ya leo; kwani hakuna maana moja tunayoweza kueleza kwa makelele haya. 

Alipokwisha kusema maneno haya, akasambaza makutano.” 

Hii inamaanisha kwamba makutano ya ibada ni mukusanyiko ya watu walioitwa na Mungu toka wale wanaoabudu sanamu na pepo chafu za mashetani, wale wanao tumikia na kuabudu miungu za sanamu na sasa wanakusudia kutumikia Mungu. 

Tesalonika ni mahali hayo makutano yalikusanyika. 

Mtume Paulo aliwakuta ndani ya Neema na Amani. 

Wagriki walikuwa wanatumia neno Neema kwa kusalimiana wao kwa wao.  

Wahebrania walikuwa wanatumia neno Amani kwa kusalimiana wao kwa wao. 

Neema ni zaidi kuliko huruma, kwa sababu hurumu inamaanisha Mungu hakupatie ile unayostahili. 

Kwa hiyo Neema ni zaidi ya huruma, zaidi sana kupita maelfu ya huruma. 

Neema ni Mungu Baba na Mungu Mwana wakikupatia vitu vyote bure pasipo malipo. 

Tutambue kwamba Neema inatoka kwa Mungu Baba na Bwana wetu Yesu Kristo. 

Neema haitoke kwa Mitume, haitoke kwa Makusanyiko, haitoke kwa kikundi cha watu kinacho ongozwa vema. Neema inatoka tu kwa Mungu Baba na Mungu Mwana. 


7/ Amani haiwezi kamwe kupatikana bila Neema. 

Neema ni chemchemu ya Amani. 


8/ Aya ya 2 

“Tunashukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu ninyi wote, tukiwataja ninyi katika maombi yetu;” 

Tambua uaminifu wa Mtume Paulo katika maombi.

Tunapashwa kuombeana sisi kwa sisi.

Mtume Paulo anahakikisha katika 1Timoteo 2, na hapa, Mtume Paulo aliheshimu maagizo yake mwenyewe. 

Alikuwa akiombea kanisa hili sababu alikuwa akijitaabisha moyoni kwa ajli yake. 

Hili kanisa lenye lilikuwa bado halija shimika mizizi mirefu chini sana, 

Kanisa lenye lilikuwa kitovero cha mashambulizi na ujanja wa watu wa dini.

Tutambue kwamba Mtume Paulo hakuomba kwa jumla na kwa juu juu, lakini maombi  yake ilikua yenye lengo, kusudi na shabaa, alijuwa nini kuombea na sababu gani na katika shida gani. 

Nina uhakika kwamba munapashwa kuwa na horoza ya mambo yote munayopenda kuombea, kuombea watu kamili wenye wanaokumbwa na tatizo fulani. 

Munapashwa kuombea mtu fulani anayekumbwa na shida fulani. 


9/ Tusisahau kwamba mtume Paulo alikuwa na amesongwa na kazi nyingi sana. 

Alikua akihubiri hazarani, pia akienda na kuingia nyumba kwa nyumba kwa kutangaza injili. 

Alikuwa akijenga hema  kwa  kupata chakula chake cha kila siku, na zaidi ya hayo yote, yeye alikua akipata muda ya kuombea yale makanisa yote aliyofungua.   

Alikua akiombea wale washirika wote. 

Siyo vizuri kusema kwamba wewe unakuwa na shuguli nyingi. 

Najuwa kwamba wewe hauna kiasi cha shuguli nyingi zaidi kuliko yale   Mtume Paulo aliyokuwa nayo.  


10/ Aya ya 3  

“Tukikumbuka pasipo kuacha kazi yenu ya Imani, na taabu yenu ya mapendo na saburi yenu ya tumaini, katika Bwana wetu Yesu Kristo, mbele ya Mungu Baba yetu;” 

Kuna maneno matatu ya muhimu sana ndani ya aya hii. 

Imani, Tumaini na Mapendo. 

Mutafahamu ya kuwa hii maneno matatu ya musingi imeungwa pamoja katika Maandiko mengine ya Mtume Paulo katika vitabu vingine. 

1Wakorinto 13: 13 

“Basi, sasa inadumu imani, tumaini, mapendo, hizi tatu; lakini neno kubwa katikati ya maneno haya ni mapendo.” 

Mutume Paulo anatuambia ya kwamba mambo haya matatu: Imani, Tumaini na Mapendo, yanadumu. 

Neno la muhimu na kubwa hadi hapo ni neno: “Kudumu”. 

Ninafurahi kujuwa kwamba mambo haya matatu yanadumu. 

Maishani mwetu kuna mambo mengi yasiyo dumu. 

Kwa mfano ujana unapambazuka na kutoweka. 

Afya, hata ikiwa bora hadi miaka 70 ama 80, itatoweka punde kidogo. 

Nafasi ya bahati, upendeleo, rafiki na vifaa vya kimwili, hata moja ya mambo haya tunayotaja haitadumu, bali tushukuru Mungu wetu kuona kwamba Imani, Tumaini na Mapendo yanadumu.  


11/ Jambo lingine la muhimu ni kwamba, moja ya maneno haya inakuwa na utumizi kubwa kushinda mbili nyingine. 

Ijapokuwa kwamba haya mambo matatu yanadumu, lakini neno kubwa katikati ya haya ni Mapendo.


12/ Ninafahamu kwamba mumetambua kwamba Imani ni ya muhimu sana. 

Waebrania 11: 5 

“Kwa imani Enoka alihamishwa asije akaona mauti, wala hakuonekana kwa sababu Mungu alimhamisha; maana mbele ya kuhamishwa kwake alikuwa ameshuhudiwa ya kwamba amependeza Mungu.” 

Bila imani, haiwezekani kumupendeza Mungu, na tuliwafahamisha siku zilizopita kwamba imani ni sawa miwani ya njia mbili kwa Mwamini, miwani ya kuangalia nayo mbali sana zaidi, ikiwezesha mukristo kuona kwa mbali vitu vyenye haviwezi kamwe kuonekana kwa mecho yake matupu.  

Bali, hapo juu kidogo, Baba Mungu anatuambia kwamba  neno kubwa katikati ya hayo mambo matatu ni Mapendo. 

Mwenyezi Mungu anasema kwamba Mapendo ni kubwa kushinda Imani. 

Je mapendo yawezavyo kuwa kubwa kupita imani? 

Hakuna shaka lolote, ni imani iliyo niokoa. 

Nikusema kwamba Imani inanipatia kitu changu binafsi, changu mimi mwenyewe bali mapendo inanituma kutumikia wengine. 

Mapendo inanisukuma kutimiza matendo ya neema  kwa wengine.  

Sasa, namna gani mapendo ni kubwa kuliko tumaini? 

Tumaini inanitia moyo kushangilia, lakini mara tena mapendo inanisukuma ku hudumia wengine. 

Tumaini inaniweka katika hatua ya kusubiri neno moja kwangu mwenyewe, lakini mara tena mapendo inanisukuma kutenda matendo ya neema kwa wengine. 


13/ Tutambue kwamba katika aya ya tatu, kuna neno: 

Kazi ya Imani

Imani inatenda kazi kama ni Imani inayokuwa hai, halisi na ya muhimu. 

Tuweke mkazo katika maandiko yanayokuwa katika Waefeso 2: 8 - 10  

“Kwa maana mumeokolewa kwa Neema kwa njia ya Imani, wala neno hili halikutoka ndani yenu wenyewe, ni zawadi ya Mungu, si kwa matendo asiwe mtu atakayejisifu. 

Maana sisi ni kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu ili tutende matendo mema Mungu aliyotengeneza mbele ili tutembee ndani yao.” 

Tumeokolewa kwa Neema kwa njia ya Imani, si kwa matendo yetu.

Bali kwa aya ya kumi tunaambiwa ya kwamba: 

Maana sisi ni kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu ili tutende matendo mema Mungu aliyotengeneza mbele ili tutembee ndani yao. 

Imani inapashwa kusukuma mtu kutenda kazi. 

 14/ Tukirudi kidogo nyuma katika 1Watesalonika 1: 3

“tukikumbuka pasipo kuacha kazi yenu ya imani, na taabu yenu ya mapendo, na saburi yenu ya tumaini katika Bwana wetu Yesu Kristo, mbele ya Mungu Baba;” 

Tukihakikisha neno “kazi ya mapendo” 

Imani ya kweli inazaa matunda, bali, mapendo inanisukuma kuhudumia hadi huduma iyo ifikiye kuwa kazi. 

Neno kazi inamaanisha kutaabika, kutumia nguvu kamilifu, inamaanisha kuchoka, inamaanisha kutumika kazi kwa hali kamilifu. 


15/ Tutambue Mapendo ni nini? 


1Wakorinto 13: 4, 5 

“Mapendo yanavumilia, ni upole; mapendo hayajui wivu, mapendo hayajisifu; hayajivuni, 

Hayakosi kuwa na adabu, hayatafuti maneno yake, hayakasiriki mbio, hayahesabu mabaya;” 

Kwanza ni kwamba mapendo yanavumilia, ni upole; mapendo hayajui wivu, mapendo hayajisifu; hayajivuni, hayakosi kuwa na adabu, hayatafuti maneno yake. 

Mapendo hayana uchoyo, unatafuta kila mara faida ya mwengine. 

Kama tukijaribu kupima uwingi wa mapendo yetu kufwatana na aya hii, si wengi kati yetu watakao onekana wanao ishi namna sawa. 

Jameni sisi tunakumbwa na mambo kazaa. 


16/ Neno la mshangazo pia na raha tele, ni kwamba katika maandiko haya, tukiondoa neno Mapendo na kulibadirisha na Jina la Bwana Yesu Kristo, tutasoma maandiko kama ifwatayo: 

Yesu Kristo aliteswa na kuvumilia sana, Yesu Kristo ni mupole, Yesu Kristo hajui wivu, Yesu Kristo hajisifu; Yesu Kristo hajivuni, 

Yesu Kristo hakosi kuwa na adabu, Yesu Kristo hatafuti maneno yake, Yesu Kristo hakasiriki mbio, Yesu Kristo hahesabu mabaya,  

Kwa sasa, weka jina lako mahali pote kwenye jina mapendo inapatikana, baadaye utizame nini utakayopata. 

Eti, mimi naweza kufaulu? 

Wewe unaweza kufaulu? 

Nazani kwamba kanisa la Watesalonika lilifaulu. 

Wao walikuwa na Mapendo wakitumika hadi mwili kuchoka, kazi kamilifu 


17/ kiwango cha upendo wako kwa Bwana Yesu Kristo ni gani? 

Ujichunguze na kuwa mwamuzi wako mwenyewe. 

Ni kama msemwa tunaokuwa tukitumia kuhusu kiwango cha mapendo tunayo mioyoni mwetu, kwa kupenda jirani wetu na mapendo tunayo kwa Bwana Yesu Kristo.  


Luka 7: 47 

“Kwa sababu ya maneno haya ninakuambia: Zambi zake zilizo nyingi zimesamehewa; kwa sababu alipenda sana. 

Naye aliyesamehewa kidogo anapenda kidogo.” 

Hapa ni mfano kuhusu mwanamuke aliyeshikwa katika zambi kubwa na maovu kubwa, kwa hivyo alimupenda sana Bwana Yesu Kristo, na kwa upande ungine tunakuwa na mufarisayo aliyejizania kwamba amempenda Mwenyezi Mungu, bali wakati alimukutana huyu mwanamuke akimuabudu Bwana Yesu, palepale alihuzunishwa hadi kufika kiwango cha kutokuheshimu Yesu Kristo. 

Na hapo, Bwana Yesu alipomutazama na kuvumbua maneno iliyokuwa ndani ya roho ya huyo mufarisayo, akampa mfano wa Mtu mwenye mali aliyewapa  watumishi wake wawili  mkopo wa pesa kwa sababu walihitaji pesa. 

Na Bwana Yesu  kuonesha waziwazi kwa njia ya mfano hule kwamba ni sawa mwanamuke huyu aliyempenda Bwana Yesu, alimupenda sana sababu yeye alijiona kwamba alikuwa akibeba muzigo mzito sana ya zambi na masamaha yake ilikuwa kubwa sana kwa hiyo alimupenda Bwana Yesu Kristo kwa mapendo makubwa sana kwa sababu yeye anatambua kwamba alisamehewa sana zaidi. 

Lakini mufarisayo aliyejiona kwamba zambi yake ni kidogo sana kupita kipimo yeye hakuzania kwamba anahitaji masamaha, ni kwa sababu hiyo yeye hangaliweza kupenda sana.   

Kiwango cha mapendo unayokuwa nayo kwa Mwenyezi Mungu una ambatana na kiwango cha makuu, maishara, maajabu na mibaraka yenye Mwenyezi Mungu amekwisha kukutendea. 


18/ Waroma 12: 9 

“Mapendo yawe pasipo udanganyifu; muchukie lililo uovu, mwambatane nalo lililo jema.” 

Biblia inatuambia hapa kwamba mapendo yawe pasipo udanganyifu. 

Ni kusema ya kwamba Mapendo yanapashwa kuwa ya kweli. 

Njia moja halali kwa mwamini kuwa na mapendo ya kweli, ni kujua kuhesabia mibaraka na makuu yote Mwenyezi Mungu aliyomufanyia na kumurudishia aksanti na shukurani. 


19/ Galates 2: 20  

“Nimesulubiwa pamoja na Kristo, lakini ni hai; wala si mimi, lakini Kristo ni hai ndani yangu; na uzima nilio nao sasa katika mwili, ni uzima wa imani iliyo ya Mwana wa Mungu ambaye alinipenda akajitoa nafsi yake kwa ajili yangu.”

Hii inatuonesha Mapendo inayokumbwa na shukrani. 

Mwana wa Mungu alinipenda na akajitoa mwenyewe kwa ajili yangu, ni kwa sababu ile mimi nampenda. 

Tena 1Yoane 4: 19 inasema: 

“Sisi tunapenda kwa maana yeye alitupenda sisi kwanza.” 

Hii ni mapendo inayokumbwa na shukrani. 


20/ Mwenyezi Mungu anahitaji tuwe na Mapendo inayotenda kazi, mapendo inayo mutumikia na kumuhudumia. 

 Unaweza kufahamu kwamba mapendo yako ni ya halisi, kama mapendo yako yakusukuma kutenda kazi ya Bwana wakati ungali bado unaishi duniani. 


21/ Kiisha tuone “tumaini katika Bwana wetu Yesu Kristo inayotokana na uvumilivu wetu.” 

Tumaini inanipa subira ya kitu ninacho ngojelea kwa niaba yangu binafsi. 

Na hii inaambatana na kuja na kuonekana mawinguni kwa Bwana na Mwokozi wangu Yesu Kristo. 

Kama vile tulivyoona juma jana katika Kitabu cha Waroma, kuonekana kwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo hapo kwa mawingu, kwa siku ile ya Bwana, itakuwa sherehe kubwa kwa mwamini, itakuwa saa ya kashifa kwa mwamini, yaani kuondolewa kwa kitambaa iliyo tufunika, itakuwa saa ya muzinduo wa mwamini. 

Hii tumaini ya Baraka, hii subira ya Baraka ya kwenda kukaa pamoja na Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, tukiwa tumebadirishwa mwili ufanane na Mwili wake wa utukufu, na kuzinduliwa kama watoto wa Mungu, hayo mambo yote yananitia moyo ili nisubiri nikishindana na dunia. 

Na hii inahimiza mwendo wangu ili niishi kwa kutazama siku zitakazo kuja siyo kuishi kwa sababu ya siku za leo. 

Ni kwa sababu hii twatambua ya kwamba tumaini linazaa subira. 

Kwa hiyo nina haja ya kusubiri hata nikumbwe na chochote kile katika maisha yangu ya kila siku. 


22/ Jameni niwape mfano: 

Kwa mfano mimi ninamjua mtu moja wa mali nyingi na mbele ya kufa kwake yeye ananiweka kuwa mrizi wa maliyake yaliyo kiasi nyingi sana. 

Na kwa kweli, mali haya yatakuwa yangu punde kidogo tu. 

Kwa muda wote ule agano lile litachungwa salama, pesa inaweza kuingia kwenye akiba yangu saa ni saa. 

Kama nikipungukiwa na pesa leo ama kwa majuma mawili ijayo, hii siyo shida kwangu na haiwezi kamwe kuniangaisha sababu kwa sasa mimi ni mbali sana na hali yangu ya kale ya umaskini yenye inakuwa sasa hadisi, siyo kweli tena, sababu kwa leo mimi ni mutajiri. 

Na ni hii ndiyo hali yetu kwa sasa. 

Hili kanisa la Watesalonika lilikua linahudumia katika Imani, Tumaini na Mapendo. 


23/ Tujifunze sasa aya ya 3. 

“Tukikumbuka pasipo kuacha kazi yenu ya imani, na taabu yenu ya mapendo, na saburi yenu ya tumaini katika Bwana wetu Yesu Kristo, mbele ya Mungu Baba yetu;” 

Anamaliza msemwa na neno moja la muhimu sana. 

Siyo kusema kwamba Mtume Paulo aliona mambo aya: Imani, tumaini na mapendo ndani ya watu wa Tesalonika, bali mambo yale yalionekana mbele ya Mungu Baba yetu. 

Neno hili linatubeba kwa ulizo moja maalum yenye kila moja wetu anaweza kujiuliza. 

Kitu gani Mwenyezi Mungu anaona katika roho yangu? 

Kuamini na imani halisi katika Yeye? 

Mapendo halisi kwa kumtumikia? 

Tumaini halisi inayoleta uvumilivu maishani mwangu? 

Kwa kweli, Mwenyezi Mungu anaangalia roho zetu, lakini pia anarekodi yote tunayosema, tunayo zania na tunayofanya. 


24/ Mawazo yangu inarudi nyuma kidogo ndani ya Kitabu cha 

Kutoka 32: 9  

“Bwana akamwambia Musa: Nimeona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu.” 

Hapa tunaona wana wa Israeli wakati walifika mwisho wa uvumilivu wao. 

Musa alipopanda juu ya mulima iliachukue Amri kumi ya Mungu, na wakati alipokuwa angali mulimani, wana wa Israeli walichoka kungojea Musa, wakafika mwisho wa uvumilivu wao, na wakasema kwamba kuna jambo fulani lililo fikia mtu yule Musa. 

Yeye hatarudi tena. 

Wakamwambia Haruni awajengee miungu ya sanamu yenye itawaongoza sasa.

Na wakati Mwenyezi Mungu aliposhuka toka mlima pamoja na Musa, 

Mungu akamwambia Musa: Nimeona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu. 

Tufahamu kwamba Mwenyezi Mungu aliwaona, alijua roho zao. 

Mungu alifahamu kile kilicho waongoza kwa kuabudu miungu. 

Ni muhimu sana tufahamu ya kwamba Mwenyezi Mungu anatujua na macho yake inatutazama. 

Yafaa tuchunguze sana maandiko haya na tuone kama maneno haya hayafanyike katika maisha yetu. 


AMINA


N°Ref: 01/13/1963 / 256 - SALVATION AND THE LORD’S APPEARING / 09/29/2020

Sunday, September 20, 2020

WOKOVU WAKO WAKUTEGEMEA WEWE? / DOES YOUR SALVATION DEPEND ON YOU?

Photo taken by B Smith from the kitchen door



 


WOKOVU WAKO WAKUTEGEMEA WEWE?

DOES YOUR SALVATION DEPEND ON YOU?

June 26, 1977 

Pastor Henry F. KULP



 

Wakolosayi 1: 20 – 23 

“na kwa yeye kupatanisha vitu vyote kwake, akiwa amefanya salama kwa njia ya damu ya msalaba wake; kwa yeye, kama ni vitu duniani au vitu mbinguni. 

Nanyi, muliotengwa mbali zamani na mulikuwa adui katika nia zenu, kwa matendo yenu mabaya, amewapatanisha ninyi sasa katika mwili wa nyama yake, kwa kufa kwake, ili awalete ninyi mbele yake, watakatifu na pasipo kilema, wala laumu; kama mukidumu katika imani, mukiwekwa juu ya msingi na kusimama imara, wala hamugeuzwi mbali na tumaini la Habari Njema muliosikia, iliyohubiriwa katika viumbe vyote chini ya mbingu; nami Paulo nilifanywa mtumishi wake.”  

Aya ya 22 inasema:

“Katika Mwili ya Nyama yake, kwa Kufa kwake, ili awalete ninyi mbele yake, watakatifu na pasipo kilema, wala laumu;”

Mungu anatuambia kwamba sisi tu watakatifu na pasipo kilema, wala laumu mbele yake. 

Sitambue ingine aya ya raha na utukufu kama hii katika Biblia, na mambo haya yote ni kweli sababu KRISTO alikufa kwa sababu yetu. 

Pia wakati tuendapo kwa aya ya 23, tunaona kwamba neno la kwanza linalokuwa kwa mwanzo wa aya hii ni “kama”, kiisha palepale inatushimamisha kwa gafla. 

“kama mukidumu katika imani, mukiwekwa juu ya msingi na kusimama imara, wala hamugeuzwi mbali na tumaini la Habari Njema muliosikia, iliyohubiriwa katika viumbe vyote chini ya mbingu; nami Paulo nilifanywa mtumishi wake.”   

Kuna wale wanaojidanganya wakizania kwamba aya hii inasema kwamba mtu aliyeokoka anaweza kutereza na kuanguka na kufikia kiwango cha kupotea.  Hii ni uwongo.

Hii siyo maana yenye Mutume Paulo analeta katika aya hii. 

Mutume Paulo hafundishi Kawaida ya Mafundisho mawili mbalimbali ya utunzaji yenye kubishana na kukanushana kabisa. 

Kama kwa upande moja anafundisha Amani ya milele na uhakika wa kuwa na Uzima wa milele, kwa upande ungine, hawezi kufundisha uwezekano wa kuanguka hadi kupoteza wokovu. 

Na tunafahamu bila shaka yoyote kwamba Biblia nzima inatufundisha kuhusu Amani ya Milele, Uhakika wa Wokovu ya milele,  Salama ya milele na ina ya fundisha wazi wazi. 

1/ TUFAFANUE AMANI YA MILELE AMA SALAMA YA MILELE AMA UHAKIKA WA WOKOVU YA MILELE. 

Wale ambao Baba Mungu aliwakaribisha na kuwakubali katika Mwana wake Mupendwa aliwaita na kuwatakasa katika ROHO MUTAKATIFU hawawezi kamwe kuanguka milele ama kuanguka kwa mwisho toka neema ya Mungu, wao watakaza mwendo mpaka mwisho wakiwa na wokovu wa milele.


2/ Huu ufafanuzi unakuwa na musingi wake katika aya mbalimbali za Biblia Takatifu.

Tuchunguze kwanza maandiko katika Waebrania 7: 25

Waebrania 7: 25 

“Naye, kwa sababu hii anaweza kuokoa kabisa wao wanaokuja kwake Mungu kwa njia yake; maana yeye ni hai siku zote apate kuwaombea.” 

Tambua kwamba aya hii haiseme tangu mwisho, lakini inasema mpaka mwisho hivi tutaisoma namna ifwatayo: 

NJIANI MWOTE SIKU ZOTE HADI MWISHO. 

Kuna wale wanaozania kwamba Amani ya Milele ama Salama ya milele ni hiyo kudumu ya watakatifu ama waamini, lakini hiyo si kweli.

Siyo waamini wanaoweza kudumu na kusubiri. 

Ni Mungu anayedumu na kusubiri ndani ya watakatifu.

 

Waroma 6: 23  

“Kwa maana mushahara wa zambi ni mauti, lakini zawadi ya Mungu ni uzima wa milele katika Yesu Kristo Bwana wetu.” 

Hapa tunasoma kwamba: lakini zawadi ya neema ya Mungu ni uzima wa milele. 

Kwanza: 

Mungu hakutupatia uzima wa milele sababu tulikuwa tunastahili. 

Tunayostahili ni kufa kwa milele na hukumu. 

Ya pili: 

Hatukupewa uzima wa milele kwa sababu ya matendo yetu na tena uzima wa milele hauwezi kuondolewa kwetu kwa sababu ya matendo yetu. 

Hatukupokea wokovu kwa sababu ya matendo yetu pia hatuwezi poteza wokovu kwa sababu ya matendo yetu. 

Matendo haina sehemu katika wokovu wetu, hata mbele ya wokovu, hata nyuma ya wokovu, wokovu ni zawadi ya Mungu mwenyewe.


4/ 2Timoteo 1: 9, 10 

“ambaye alituokowa akatuita kwa mwito mtakatifu, si kwa kadiri ya matendo yetu, lakini kwa kadiri ya kusudi lake mwenyewe na neema yake, tuliyopewa katika Kristo Yesu mbele ya nyakati za zamani, 

Na sasa imefunuliwa na kuonekana kwa Mwokozi wetu Yesu Kristo, aliyebatili kufa, na kufunua uzima na maisha yasiyokoma kwa njia ya Habari NJema.” 

Mwenyezi Mungu alituokowa na akatuita kwa mwito mutakatifu, si kwa kadiri ya matendo yetu. 

Matendo yetu haina muchango hata moja katika wokovu wetu. 

Kazi yenye Bwana Yesu aliyotimiza msalabani pa kalvari ndiyo iliyonunua wokovu wetu.

 

5/ Wokovu wetu siyo miradi yenye Mwenyezi Mungu alipanga ama kupata wazo wakati mtu alipoanguka zambini, bali ni ahadi ya Mungu aliyotayarisha tangu umilele uliopita. 

Tito 1: 2, 3 

“katika tumaini la uzima wa milele, Mungu asiyeweza kusema uwongo, aliuahidi mbele ya nyakati za milele; 

Lakini akafunua neno lake kwa nyakati zake katika mahubiri, niliyowekewa amana kama amri ya Mungu Mwokozi wetu;” 

Katika tumaini la uzima wa milele, Mungu asiyeweza kusema uwongo, aliuahidi mbele ya nyakati za milele.

 

6/ Kazi ya Roho Mutakatifu inakuwa  ushahidi ungine juu ya salama ya milele. 


Waefeso 1: 13 - 14  

“Ndani yake ninyi vilevile, wakati muliposikia neno la kweli, Habari Njema ya wokovu wenu, ndani yake mumekwisha kuamini vilevile na kutiwa mhuri wa Roho Mutakatifu ya ahadi. 

Ndiye aliye arabuni ya uriti wetu, ili kuleta ukombozi kwa mali yake mwenyewe, kuwa sifa ya utukufu wake.” 

Ndani yake ninyi vilevile, wakati muliposikia neno la kweli, Habari Njema ya wokovu wenu, ndani yake mumekwisha kuamini vilevile.

Ni hii utaratibu wa kawaida. 

Kiisha kuamini, tunatiwa muhuri ya Roho Mutakatifu. 

Mhuri wa Roho Mtakatifu, Yeye ndiye arabuni ya wokovu wetu. 

Waefeso 4: 30   

“Wala musihuzunishe Roho Mtakatifu ya Mungu, ndani yake mulitiwa mhuri hata siku ya ukombozi.” 

Tunasoma hapa kwamba hatupashwe huzunisha Roho Mtakatifu ndani yake tulitiwa mhuri hata siku ya ukombozi, hapana hata siku tutapoteza wokovu wetu.  

Siku ya ukombozi inamaanisha siku ya ukombozi wa miili yetu.

 Wakati Bwana Yesu atarudi kutuchukuwa, miili yetu ya haya itafananishwa na Mwili wake wa Utukufu, Mwili wa Ufufuko wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 

Wafilipi 3: 21 

“atakayebadilisha mwili wetu wa haya upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uwezo ule anaoweza kutiisha vitu vyote viwe chini yake.” 

7/ Waroma 3: 24  

“Wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Yesu Kristo:” 

Mwamini iko katika salama sababu yeye anahesabiwa haki. 

Sasa kuna neno kubwa iliyotafsiriwa na kasoro kidogo, ikituweka kama watu wenye bado kutenda zambi. 

Nikusema tungelikuwa kama wasio na hatia. 

Adamu, mbele ya kuanguka kwake katika zambi, alikuwa katika hali ile sawa asiye na hatia, lakini kuhesabiwa haki ni bora zaidi kupita hali ile. 

Kuhesabiwa haki ni kutangazwa kuwa mwenye haki sawasawa na Mwenyezi Mungu aliye MWENYE HAKI. 

Hapana kuwa sawa asiye na hatia.


8/ Waroma 4: 5 na Waroma 3: 24 inatuambiaya kwamba: 

“… kwa mtu asiyefanya kazi, lakini anamwamini yeye anayehesabia haki wasioogopa Mungu, imani yake inahesabiwa kuwa haki” kwani

“Wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Yesu Kristo:” 

Tufahamu kwamba kwa njia ya neema yake KRISTO, mtu muovu anahesabiya haki.

Hapana wale wanaoishi maisha ya usafi. 

Hapana wale walio wazuri kufwatana na mwenendo wao wenyewe.

 

9/ Twende sasa katika kitabu cha Wakolosayi 1: 23 

“kama mukidumu katika Imani, mukiwekwa juu ya msingi na kusimama imara, wala hamugeuzwi mbali na tumaini la Habari Njema muliyosikia, iliyohubiriwa katika viumbe vyote chini ya mbingu ; nami Paulo nilifanywa mtumishi wake.” 

Tuliwaonesha kupitiya Maandiko Matakatifu kwamba mwamini hawezi kujiokoa kwa njia ya matendo yake mema, na kwamba hawezi kupoteza wokovu wake kwa sababu ya matendo aliyofanya. 

Sasa, ni nini Mutume Paulo anataka maanisha wakati anaposema kwamba sisi tutakuwa watakatifu pasipo kilema, wala laumu mbele ya mecho ya Mungu, kama tukidumu katika imani. 

Neno “kama” inaonesha sharti ya hali, na inamaanisha “kama, na ni kweli kama”, 

Nikusema kama kweli, na ni kweli munaendelea katika imani. 

Tunakuwa na namna mbaya ya kutumia neno “kama” toka Kigriki wakati inapotumiwa sawa sharti ya muhimu na inayohitajika. 

Ni sawa mtu anayesema: Nitakwenda kuogelea kwa bahari kama nvua hainyeshi. 

Bali, hii siyo maana tunayokuwa nayo hapa. 

Hapa, inamaana kusema, ni kweli. 

Siyo sharti. 


10/ Neno kuendelea, ama kudumu ni EPEE – MEN – O. 

Epee inamaanisha juu. 

Meno inamaanisha kukaa. 

Na kama tukichanga yote pamoja tunapata: 

Kuendelea kukaa, ama, kudumu katika kutenda jambo fulani. 

Na neno imani, PISS – TIS na ina  tanguliwa na makala kamili mbele yake, hivi itatafsiriwa kama ifwatavyo: 

KAMA UKIENDELEA NA KUDUMU KATIKA KUSADIKI MAFUNDISHO YA BIBLIA NA UKIYATENDA. 

Imani inamaanisha Kusadiki Mafundisho ya Biblia, na neno kuwekwa juu ya msingi inamaanisha KUTIYA MSINGI, na neno kusimama imara ni KUTOKUTIKISIKA.

Ni kusema wewe hauongeze kitu kwa mafundisho ya Biblia, bali unaamini yale Biblia inayofundisha kuhusu wewe na Bwana wetu Yesu Kristo.


11/ Wala hamugeuzwi mbali na tumaini la Habari Njema. 

Kwa halisi hiyo inamaanisha hapana kujitenga kando, na neno TUMAINI ni kuwa na uhakika AL –PUS. 

Kuwa na uhakika katika Habari Njema, hapana kujitenga kando ya Habari Njema. 

Habari Njema muliosikia na iliyohubiriwa kwenu. 

Neno kuhubiri KAY – RUE SO inamaanisha kutangaza hazarani. 

Pia angalia kwa makini maneno haya: 

Nami Paulo nilifanywa mtumishi wake. 

Ni nini Mtume Paulo anataka kutuambia hapo? 

Anapenda kutufahamisha kwamba tunapashwa kudumu katika kawaida ya  mafundisho yale aliyotufundisha, tutie msingi wetu katika kawaida ya mafundisho yale, na tusimame imara, tusitikisike, tuki weka tumaini letu ndani ya  Habari Njema. 

Habari Njema iliyofundishwa na Mutume Paulo. 

Waroma 2: 16 

“Katika siku ile Mungu atakapohukumu siri za watu, sawasawa na Habari Njema yangu, kwa Yesu Kristo.” 

Pia tufahamu kwamba Waroma 16:25 inasema:  

“Kwake yeye anayeweza kuwasimamisha ninyi sawasawa na Habari Njema yangu na kwa mahubiri ya Yesu Kristo, kama ufunuo wa siri iliyowekwa tangu nyakati za milele,” 

2 Timoteo 2: 8 

“Ukumbuke Yesu Kristo, aliyekufa toka wafu, wa uzao wa Daudi, kama inavyosema Habari Njema yangu.” 

Nikusema kwamba ni Habari Njema ya Mutume Paulo ndiyo inayo funua Kweli hii, kwamba nyinyi munakuwa sasa watakatifu, pasipo kilema wala laumu mbele ya Mungu.

Hakuna  sheria , wala amri ila tu Imani katika Yesu Kristo inayo tutiya katika hali hii. 


12/ Wakolosayi 1: 24 

“Basi sasa ninafurahi katika mateso yangu kwa ajili yenu, na ninatimiza katika mwili wangu yale yaliyokosa ya mateso ya Kristo kwa ajili ya mwili wake, ndio kanisa lake.” 

Hii ni aya moja ya upekee na yenye maana. 

Kuna wamoja wenye hawafikilie kuifahamu na wanapotosha misemwa hayo wakisema kwamba mateso ya Bwana wetu Yesu Kristo pale Msalabani hayakuwa kamili, na ya kwamba ni Mutume Paulo aliye musaidiya kwa kuitimiza. Hii siyo kweli, ni uongo mtupu na makosa. Na hii siyo maana inayokuwa katika aya hii.  

Aya hii haielekee Mateso ya KRISTO.

 

13/ Hapana Mateso ya KRISTO msalabani, bali maumivu  na manyonge ama  mateso  ya Kristo katika mwili wa Paulo. 

Mateso ya Kristo msalabani haiitwe maumivu na manyonge. 

Kama mtu anasambishwa kwenye Korti na anahukumiwa, hii siyo maumivu na manyonge lakini hii ni hukumu. 

Bwana Yesu Kristo alibeba Hukumu juu ya Musalaba. 

Basi, Mwokozi wetu Yesu Kristo aliamuru maumivu na manyonge ishike watu wake ili iwasaidia kukusanya kanisa, Mwili wa Kristo. 

Na Mutume Paulo alisema kwamba: 

Nitatimiza mapenzi ya Mungu kwangu, nipate maumivu, manyonge, na mateso katika mwili wangu kwa ajili ya Yesu Kristo ili kanisa likusanywe.

 

14/ Eti watambua? 

Kanisa la Kristo haikusanyiki kamwe bila mateso. 

Waweza kuchunguza ndani ya Biblia. 

Kweli Mutume Paulo hakustarehe katika mwili wake, yeye aliishi katika machungu na maumivu ya kila siku na kila saa. 

Wakati tunachunguza historia ya kanisa tutaona namna kanisa ilikusanywa kwa maumivu na mateso ya  watumishi wake Mungu. 

Wakati Mwenyezi Mungu anapotumikisha mtu, kunakuwa mpito wa machungu. 

Mutume Paulo anasema kwa namna halisi kwamba yeye anafurahi kuteseka kwa ajili ya Yesu Kristo. Oh, kweli aliteseka sana. 

2 Wakorinto 11: 23 - 25  

“Wao ni watumishi wa Kristo? (Ninasema sawasawa mwenye wazimu) mimi zaidi; katika taabu kuzidi sana, katika mapigo kuzidi sana, katika vifungo kuzidi sana, katika mauti mara nyingi.Kwa wayuda nilipata mapigo makumi ine ila moja. Mara tatu nilipigwa kwa fimbo, mara moja nilipigwa kwa mawe, mara tatu nilipata kuvunjika kwa merekebu, mchana na usiku nimekaa katika bahari:” 


15/ Wewe tayari umeisha soma Vitabu vya hadisi ya Shahidi? 

Wesley na Whitefield, Morrison na Carey na wahubiri wakuu waliopima kuonesha kwa wazi hadisi na vitumba vya miili ya Shaidi Wangreza? 

Mbele ya nyakati za Uinjilisti, mbele wamisionari waende India, Afrika na Chaina, kulikuweko  nyakati za mauaji na wengi walipoteza maisha yao.

 

16/ Wakolosayi 1: 25  

“Nami nimefanywa mtumishi wake, sawasawa na uwakili wa Mungu niliyopewa kwa faida yenu, nitimize Neno la Mungu.” 

Hapa tunaona aya moja ya muhimu na manufaa kabisa, ila watu wengi wanapendelea kuiruka ama kuisoma bila faida, ama kuisahau. 

Mutume Paulo alitiwa Mtumishi sawasawa na uwakili wa Mungu. 

Mungu alimupa ruhusa ya kutimiza Neno la Mungu. 

Mutume Paulo alitimiza Neno la Mungu, siyo Kitabu cha Ufunuo wa siri.

 

17/ Maneno ambayo Mutume Paulo anatuambia katika Biblia Takatifu, ni Ufunuo Mkubwa katika Biblia tangu Kitabu cha Mwanzo hadi Kitabu cha Ufunuo wa siri. 

Katika Kitabu cha Ufunuo wa Siri, hakuna jambo mupya kwa upekee. 

Kitabu cha Ufunuo wa Siri kinajaa na misemwa yenye inapatikana katika sehemu za Vitabu vingine katika Biblia. 

Ukweli wote tunaopata katika Kitabu cha Ufunuo wa Siri, ukweli huo tumeupata katika Vitabu vingine vya Biblia.

Bali, Kitabu cha Ufunuo wa siri umeyakusanyisha yote katika Kitabu kubwa ya mambo ya mwisho. 

Ni Mutume Paulo ndiye aliyepokea UFUNUO ya kwamba KRISTO alikua anaunganisha watu wote katika Kanisa unaoitwa KANISA MWILI WA KRISTO.  

Waefeso 1: 7 inatuambia kwamba: 

“Katika yeye tuna ukombozi wetu kwa njia ya Damu yake, usamehe wa zambi zetu, sawasawa na wingi wa neema yake,” 

Mutume Paulo anatumikisha neno “utajiri”, “wingi” neno hili linatumikishwa na Paulo pekee. 

Utajiri wa neema yake, wingi wa neema yake. 

Tena katika Kitabu cha Waefeso 2: 7, tunasoma ya kwamba: 

“hata katika nyakati za kuja aonyeshe wingi wa kupita kiasi wa neema yake kwa wema wake kwetu katika Kristo Yesu.” 

Wingi wa utajiri ya neema yake. Wingi wa kupita kiasi wa neema yake. 

Wewe unafikiri juu ya wingi wa kupita kiasi wa neema yake? 

Wingi wa utajiri wa neema yake unapita kiasi. 


AMINA 


N°Ref: 06/26/1977/ 395-2 DOES YOUR SALVATION DEPEND ON YOU? / 09/20/2020