Sunday, August 30, 2020

KRISTO ALISHUKA KUZIMU? (Sehemu ya pili) / DID CHRIST DESCENDED INTO HELL (Part II)

 

Volcano in Goma 100 miles north of  Bukavu, D R Congo






   KRISTO ALISHUKA KUZIMU? (Sehemu ya pili) 

    DID CHRIST DESCENDED INTO HELL (Part II)

    May 1, 1960 

    Pastor Henry F. Kulp



 

Waefeso 4: 7 – 11

“Lakini kila mtu katikati yetu alipewa neema kwa kadiri ya kipimo cha zawadi ya Kristo. 

Kwa hivi anasema: 

Wakati alipopanda juu, alifunga kifungo, 

Akawapa watu zawadi. 

(Basi neno hili: Alipanda, maana yake nini kama si kusema kwamba Yeye alishuka vilevile mpaka pande za chini za inchi? 

Yeye aliyeshuka ndiye aliyepanda vilevile juu sana kupita mbingu zote ili ajaze vitu vyote.) 

Naye alitoa wengine kuwa mitume; na wengine kuwa manabii, na wengine kuwa wahubiri wa Habari Njema; na wengine kuwa wachungaji na walimu;”  

Juma jana, wakati  tulipojifunza maandiko haya, tuliona yakwamba kuna wale wanaojizania kujuwa imani ao fundisho lenye mutume alileta hapa, na wengi wao wanasema kwamba KRISTO alishuka kwenye Hadeze, na mafundisho wanayo fundisha kwa mawazo yao ni kwamba:

  KRISTO alienda kukutana na watakatifu wa Agano la Kale, waliokuwa kule,   kwa sababu damu ilikuwa bado haija mwangika. 

Na kwamba, Kiisha tu  kumaliza kazi yake pale musalabani, alishuka huko chini kusudi la wokovu wa hiyo sehemu,  ni kusema wale waliokuwa katika Hadeze. 

Na kwamba aliwahubiri wale watakatifu waliokuwa kule, kiisha akawakomboa na akawachukua akapanda pamoja nawo mbinguni. 

Kwangu mimi,  kwa kweli, hayo mafundisho nayaona kwamba ni ya ujinga kweli. 

Kwa sababu mafundisho ya namna sawa hayapatikani katika Maandiko hii.  

Maandiko hii haizungumuze kuhusu kupanda ama kushuka ya namna ya kimwili, bali kuhusu Hali na Nafasi, Ranga, Uwezo na Mamlaka. 


1/ KRISTO alikuwa SAWASAWA na MUNGU. 

Alikuwa Mmoja wa Utatu Mtakatifu. 

Akajifanya Mwenyewe kuwa na hali na nafasi ya kupokeya amri na pendekezo kutoka kwa Mungu Baba, wakati Alikuja Yeye Mwenyewe kutimiza Mapenzi yake hapa duniani. 

Aligeuka kuwa mwenye kutii Serkali. 

Alikuwa mwenye kutii wazazi wake, akageuka mtumwa wa wanadamu, na akafa kifo cha msalaba na akafufuka toka wafu. 

Kwa kutimiza hivyo Biblia inatuambia kwamba Yeye atanyanyuliwa juu zaidi sana kupita mbingu zote. 

Na kwa kweli neno hili haliwezi maanisha hali na nafasi ya kimwili, kwamba mtu awe kwa hali ya juu sana zaidi kupita mbingu zote, kwa sababu kwa saa hii, KRISTO ameketi pale Mbingu ya Tatu, Akiwa kwa Mukono wa Kuume wa Mungu Baba. 

Ni kusema kwamba,  hii inamaanisha Hali na Nafasi, Ranga, hapana kupanda ya namna ya kimwili.

Na kwa hiyo, kushuka inayotajwa  hapa haimaanishi kushuka ya namna ya kimwili, lakini hali ya kujiyenyekeza Mwenyewe, kujitia kama hana utukufu, kukamata namna ya mtu, kugeuka mtumwa, kulaaniwa wakati zambi zote ziliwekwa juu yake, na kufa  juu ya msalaba pale Kalvari. 


2/ Wakati tunaambiwa: Kwamba Bwana Yesu alishuka katika sehemu za chini za nchi(dunia), hiyo inamaanisha kwamba: 

Bwana Yesu alishuka katika sehemu za chini, dunia. 

Sababu kwa kufanya hivyo aligeuka kuwa mtumwa wa wanadamu. 

Ranga, ama hali na nafasi hii, hakuijuwa tangu Umilele wake uliopita, na hatalijuwa katika Umilele wake kwa wakati wote utakaokuja. 


3/ Yoane 13: 4, 5  

“akaondoka kwa chakula, akaweka mavazi yake kando; akatwaa kitambaa, akafunga kiuno chake. 

Kiisha akatia maji kwa kibakuli, akaanza kunawa miguu ya wanafunzi wake na kuipanguza kwa kitambaa ambacho alijifunga kiuno chake.” 

Hapa tunakuwa na picha ya KRISTO akishuka kwa Ranga, hali na nafasi. 

Tunaona Bwana Yesu Kristo akinawa miguu ya wanafunzi wake kumi na miwili, kiisha kutembea safari ndefu ya miguu toka njia inayo jaa mavumbi mingi. 

Na alialikwa  kwa chakula, na wakati walipokuwa mbele ya chakula, mwenye kuwakaribisha kwa nyumba yake anakuwa na mtumwa wa kunawisha miguu ya mgeni, ili mugeni ajisikie katika hali nzuri na inayofaa wakati anaketi mezani kwa chakula. 

Hapa tunaona Bwana Yesu Kristo mwenyewe akitwaa kitambaa, akakifunga kiunoni mwake, akanawa miguu ya wanafunzi wake, kwa sababu hapa KRISTO ni Mtumwa anayenawa miguu ya Wanafunzi wake. 

Taswira hii inamuonesha Yeye kama mtumwa. 

Alifanya yoyote ile mtumwa angalipashwa kufanya, alitwaa kitambaa, akajifunga  kiunoni, hii inaonesha kazi za namna ya chini chini sana yenye inakuwa kwa watu wa ranga za chini zaidi,  watumwa. 

Na kwa kweli ni kazi hizo Bwana Yesu alizofanya wakati alipokamata namna ya mtu, Yeye aligeuka mtumwa na akakufa kwa Msalaba pale Kalvari kwa ajili yetu. 


4/ Kiisha Maandiko yanatuambia kwamba alifunga kifungo. 

Kwa kufahamu maandiko hii, tunapashwa kwanza kujuwa yakwamba tukichunguza  Waraka wote wa Mtume Paulo kwa waefeso, hatuta pata aya inayotupatia maelezo kamili ama tafsiri kuhusu aya hii

Katika Kigriki, maandiko haya yanamaanisha kwamba: 

YEYE ALIFUNGA KIFUNGO. 

Tena tuvumbue kutajwa kwa neno Neema katika Waefeso 4: 7


Waefeso 4: 7

“Lakini kila mtu katikati yetu alipewa neema kwa kadiri ya kipimo cha zawadi ya Kristo.” 

Kila mtu katikati yetu alipewa neema. 

Pia inasemwa “kwa hivi” na hii ingelikuwa “kwa sababu ya neno hili”   

Na inasemwa kwamba wakati alipopanda juu, alifunga kifungo.  

Wakati KRISTO alipandishwa na kutukuzwa juu sana zaidi kupita falme zote, na uwezo, akili zote na mamlaka, na juu ya kila jina linaloweza kuitwa, Alifunga kila kanuni iliyotia mwanaadamu katika utumwa.

Ilimubidi kwa kazi yake ya kiMungu, kuvunja na kuvuta  amri zile mbaya  za kutisha zilizoandikwa na zilizokuwa zikiwashitaki. 

Alizitundika kwa msalaba na hapo  alifunga kifungo na kuvunja nguvu zao zote. 

Na Alipopanda kwa Kiti Cha Ufalme wa Mungu, alizifanya kuwa hazina nguvu yoyote ile. 

Sheria inatoka kwa Kiti cha Ufalme wa Mungu, na kwa kupanda kwake juu, aliiweka kando kabisa na kwa sasa ni Neema tu ndiyo inayotenda kazi katika maisha yetu. 


5/ Kumbukeni kwamba mara kwa mara tunasisitiza na kutia mukazo kwamba sisi kwa leo tuko katika Utunzaji wa Neema, na vyote twavipata kwa Neema pekee. 

Katika matunzaji mengine watu walikuwa wakiokolewa kwa neema, lakini Yote hayakukuwa kwa Neema mtupu. 

Kwa sababu tunasoma katika Waraka wa Wagalatia kwamba sheria iliongezwa pembeni ya neema, na Mungu alivunja nguvu zote za sheria, alifunga kitu kilichokuwa kinatufunga kwa kifungo na kwa sasa ni Neema tu inayotumika maishani mwetu. 

Tumeokolewa kwa Neema tu, bila kuongeza kitu ama tendo lolote lenye mwanadamu anaweza kutarajia kufanya. 

Hakuna tena kanuni lolote juu yetu, ama sheria lolote juu yetu. 


6/ Wakolosayi 2: 4 

“akikwisha kuzima hati ile iliyoandikwa kwa kutushitaki kwa hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondosha na kuifunga kwa msalaba na misumari.” 

Kulikuwa vitu vilivyokuwa vinashika watu katika vifungo, na Bwana Yesu Kristo alivitundika kwa msalaba. 

Na wakati alipaa na kupanda mbinguni Alivunja vinyume vya hati na hukumu zote zilizokuwa na uadui kwetu. 

Ni Neema pekee tu sasa ndiyo inayotumika kati yetu. 


7/ Kiisha tunaona kwamba aliwapa watu zawadi mbalimbali. 

Aliwapa hizo zawadi, akiwa KRISTO aliye fufuka. 

Ni zawadi gani? 

Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wahubiri wa Habari Njema; na wengine kuwa wachungaji na walimu. 


8/ Muhubiri wa Habari Njema ama muinjilisti ni nani? 

Ni mwenye kubeba Habari Njema kwa wengine. 

Huduma ya muinjilisti inaelekea watu wa inje.

Wakati Mwenyezi Mungu anapatia mtu zawadi ya uinjilisti, huyu mtu anasikia ndani ya roho yake mapendo kwao wanaopotea, mapendo kwa wasioamini. 

Anamupa kipaji ya kupasha  Neno la Mungu na Nguvu  na usaafi wote. 

Ni zawadi ya mastaajabu kweli. 

Kuwa muinjilisti ni kuwa na zawadi ya mastaajabu kweli. 

Lakini sasa, siyo watu wote walio na kipaji hiki. 

Muinjilisti anatoa Neno linalokuwa na uaminifu wote ndani mwake.

Najuwa kwamba sote tayari tumekwisha kukutana na wao wanaoitwa wavuvi wa roho za watu. 

Nia yao nikushuhudia wababa na wamama kuhusu Yesu Kristo na wanakuwa na kipaji ya kuwaleta watu hawa kwake Bwana na Mwokozi Yesu Kristo.

Mimi binafsi nilikutana na watu wengi kama wale.

Ninakumbuka kijana mmoja Muhubiri katika muji wa Johnstown, mwenye nazani alikuwa na kipaji ya uinjilisti. 

Nilikuwa nikifurahia kuona namna alikuwa akileta roho za watu kwa Bwana Yesu. 

Yeye maisha yake yote ilizungukwa tu na hiyo kipaji. 

Munaweza kupatana  naye kwamba mutakutana kwa mahali fulani, lakini kama desturi yeye atafika nyuma ya saa moja ama saa moja na nusu, na ukapima kumuuliza kwa nini yeye amefika nyuma,  alikuwa tu  anakuambia umurehemu, kwa sababu yeye alikuwa na mazungumuzo na mtu moja aliyekutana naye kwa njia ama kwa nyumba ya kutengeneza nywele, ama kwa mgahawa(nyumba ya kuuzishia chakula chenye kupigwa),  na watu wenye alikua akikutana nao ni watu wenye ilikuwa tu kwa mara ya kwanza kukutana nao, alikua hajawai kukutana nao hata mara moja, lakini alikaa chini pamoja nao akiwashuhudia juu ya Kristo Yesu. 


9/ Baada ya ayo, tunasoma ya kwamba: 

Naye alitoa wengine kuwa wachungaji. 

Jina muchungaji inamaanisha mwenye kuchunga na mlinzi. 

Muchungaji mwema ni Mlinzi mwenye kutia roho yake yote juu ya kundi anayochunga katika zizi lake. 

Wakati Bwana Yesu alipo endelea mara na mara tena kuuliza Petro: “Wanipenda kuliko wote hawa?” 

Na nyuma ya haya yote Petro alikiri akisema: 

Najua kwamba upendo hauko ndani yangu. 

Bwana Yesu akamwambia: Lisha zizi langu, lisha wanakondoo wangu, linda na kulisha zizi langu, nikusema, Aliweka Petro kuwa Mchungaji wa zizi hilo. 


10/ Hapo tunafikia kiwango cha kusema kwamba muinjilisti anakuta walewasioamini, anawaleta kwa Bwana Yesu, na kwa kweli anawaleta katika kikundi cha waamini, na ni hapo Mchungaji anajifunza namna ya kuwaongoza katika majani mabichi ya Neno la Mungu anayo wapa akiwaonesha namna gani kuishi maisha yao katika kutenda Neno la Mungu,  akiwasaidia kushindana na matatizo na migorogoro ya maisha. 


11/ Tunafikia sasa Walimu. 

Tofauti gani inayokuwa kati ya Muchungaji na Mwalimu? 

Mwalimu ni mtu ule anayeweza kufungua Neno la Mungu akilisoma na kulicheuwa na kuleta ufunuo na maana mbalimbali ya muhimu sana ya maneno yenye kuzama ndani ya andiko alilolisoma.

Mwalimu anakuwa na kipaji ya kuchimbua neno na kulifafanua kwa namna ya mtu yeyote apate kulifahamu na kulisikia kwa uraisi wote.

Watu wengi wanaweza kuwa na uwezo wa kuwa Wainjilisti ama Wachungaji ama Walimu, lakini kwa binafsi, mtu huyo atakuwa amefanyikiwa sana kwa huduma yake katika moja ya zawadi hizo tatu kuliko mbili nyingine,  na tena kipaji kimoja ndicho kitainuka zaidi na kuwa na matendo zaidi kupita zingine zote. 

Yeye anaweza kuwa Mwalimu zaidi kuliko Mchungaji ama Muinjilisti. 

Ama anaweza kuwa Muinjilisti wa manufaa kabisa kuliko kuwa Mchungaji ama Mwalimu. 

Tunahakikisha kwamba vikundi hivi vimepewa kwa kanisa. 

Tufahamu vilevile kwamba zawadi za Mitume na Manabii nazo vilevile ni zawadi za Kristo aliye fufuka.  

Angalisho kwa utaratibu kuhusu namna majina haya mawili yanapangana. 

Mitume na Manabii, Paulo hakusema Manabii na Mitume, huu ni utaratibu wa Agano la Kale. 

2 Petro 3: 2 

“mupate kukumbuka maneno yaliyosemwa zamani na manabii watakatifu, na amri ya Bwana na Mwokozi iliyoletwa na mitume yenu.” 

Mutume Petro anasema hapa juu ya Manabii na Mitume, wanaomaanisha watakatifu wa Agano la Kale.

Hii haimaanishe wale kumi na wawili na Manabii wa Agano la Kale. 

Hapana hata kidogo, haya ni kwa nyakati ya Mwili wa Kristo. 

Mutume inamaanisha, anayetumwa. 

Na Nabii inamaanisha, anayetangulia kusema, hapana yeye anaye tabiri mambo yatakayokuja kesho. 


12/ Kuna kusudi la muhimu na la musingi kwa watu hawa kuwa na zawadi hizi mbalimbali katika Mwili wa Kristo. 

Sawa vile watu wanavyojua: 

Katika Biblia Takatifu, uwekaji wa vituo vya uandishi haukupanwa kwa maongozi ya Mungu. 

Kwa mara yanasaidiya na mara hayasaidiye. 

Kwa kesi tunayo, haisaidiye.  

Tunapo ondoa “mkato” katika aya hii ya kumi na mbili, hapo tunapata maelezo na maana kamili. 

Naye alitowa wengine kuwa mitume; na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wahubiri wa Habari Njema; na wengine kuwa wachungaji na walimu; 

Kwa kusudi ya kukamilisha watakatifu kwa kazi ya utumishi hata Mwili wa Kristo ujengwe. 

Kuna kusudi la muhimu na la musingi kwa zawadi hizo kupewa kwa Kanisa Mwili wa Kristo. 

Neno kukamilisha haimaanishe kugeuka kuwa pasipo kosa lakini inamaanisha KUTAYARISHA ama KUPATIA VIFAA. 


13/ Zawadi hizo ni kwa ajili ya kupatia taifa la Bwana vifaa kwa kazi ya Bwana, taifa hilo ni mukusanyiko ya waamini wote wa kanisa la fasi, wale walioamini Bwana Yesu kama Bwana na Mwokozi wao. 


14/ Tunafahamu ya kwamba zawadi hizo zinatolewa kwa Kanisa Mwili wa Kristo kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu na kupanua kazi ya Bwana kwa kuhimiza na kujenga Mwili wa Kristo kwa kazi ya Bwana ili Kanisa lipanuke.  

Ni vizuri gani kama tungelikuwa na watakatifu wanaokaa kwa mimbari ama viti vya kanisa kwa kujiweka tayari kwa kazi ya Bwana.

Kama wasema kwamba umeamini Bwana Yesu na wewe haufanyi kazi yoyote kanisani, wewe unakuwa kikwazo kwa malaika wa Bwana,  na jambo la sifa na furaha kwa mapepo wa giza. 

Kwa sababu tulipokea zawadi mbalimbali ili sisi kwa nafasi ya KRISTO tupate kusihi watu ili kuwapatanisha na Mungu. 

2 Wakorinto 5: 17 

“Hivi kama mtu akiwa ndani ya Kristo, yeye ni kiumbe kipya; maneno ya zamani yamepita; tazama, maneno yote yamekuwa mapya.” 

15/ Zamani nilijuwa kijana moja aliyekuwa mwanamemba wa kanisa letu, lakini kwa sasa yeye anakuwa Mchungaji. 

Siku moja nilikuwa nikihubiri katika kanisa lake na wakati nilipofika mwisho wa mahubiri, alikuja kwangu na kuniuliza, je inaweza kuwa shida kwako kama mimi nikitumikisha mahubiri hii wakati ninapohubiri watu wengine? Nikamujibu, hapana hata kidogo, kwangu itakuwajambo la furaha kuona kwamba unatumia mahubiri hii. 

Naye akaongeza akisema:   kwa jumaa hii nitatoa Neno kwa mukusanyiko ya Watumishi. 

Pia akasema tena: Sioni sababu gani ninakuuliza, kwa sababu tayari nimekwisha kutumikisha mahubiri yako mara nyingi sana wakati ninatoa neno hapa kanisani.

Nikamujibu: Kama neno lolote linagonga sana moyo wako na kukuletea burudani na wewe pia unkusudia kuileta kwa mtu mwengine ili abarikiwe kiroho, sioni hata tatizo moja kwa tendo lile, bali nitamtukuza Bwana Mungu wetu. 

Na kwamba, kama kwa njia ya neno lile, mtu anakiri na kupokea Bwana Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wake, wewe utakuwa baba yake wa kiroho na mimi nitakuwa tate yake. 

Kama ingelikuwa kundi lote la waamini wanajiweka pamoja na kusimama ili kutenda kazi ya Mungu, kwani najua kwa kweli kwamba kanisa la nafasi inakuwa ya manufaa kabisa mbele ya mecho ya Mungu, nivizuri sana watu wote kujitoa kwa kuhudumia Mungu. 

Hakuna Mchungaji anaye weza kutimiza huduma huu pekeyake.

Hata kundi ya Wachungaji haiwezi lolote pekeyao. 

16/ 1Wakorinto 1: 10  

“Basi ninawasihi ninyi, ndugu, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, ya kwamba ninyi wote museme neno moja, na matengano yasiwe katikati yenu; lakini mwungane katika nia moja na shauri moja.” 

Hapa tunaona upumbafu wa kutokutumika pamoja. 

Ujinga wa kutokupanga kazi. 

Kanisa la Korinto lilikuwa katika mikorogano sababu kila mtu alikuwa akijifungia kwa upande wake, akisongana tu na kuangalia kazi yake mwenyewe pahali pa kujioa wote pamoja kwa kazi ya Bwana. 

Watakatifu wenye wanaojitoa kwa kazi ya Bwana hawana iyo saa ya kubaguwa wengine kwa kuwatia kando kwa kazi. 

Yawezekana unaweza kuchanganyikiwa na kuhuzunishwa kupitia mwamini moja anayekuwa sawa mutakatifu wa Mungu. 

Waweza kufwata mufano wa marehemu Mutumishi Billy Sunday. 

Yeye alikua aki kosolewa na kurejeshwa mara kwa mara na wale wanaokuwa sawa watakatifu kupita watu wote, juu ya namna yake ya kuhubiri. 

Hivi akawauliza wale watakatifu: 

“Kama hamufurahie namna yangu ya kuhubiri, muniambie ninyi munahubiri namna gani?” 

Na jibu ilikuwa: “Sisi hatujawai bado kuhubiri.” 

Hivyo Mchungaji Billy Sunday akawaambia: 

“Mimi ninafurahia namna yangu ya kuhubiri zaidi ya namna yenu.” 


17/ Ni vizuri kujitoa sana kwa yale Mwenyezi Mungu anatarajia kwako. 

Wajibu wako wa maana katika maisha yako ni kutangaza na kupanua kazi kwa kuhudumia katika Shamba la Bwana. 

Wewe hauko pale juu ya kununua manyumba, viwanja ama vifaa. 

Hauko pale ili ujaze mali kwenye banki yako. 

Mwizi wakati anakutokea anakuambia uchague kati ya pesa na uzima wako, 

Lakini Mungu anakuomba zaidi. 

Anasema: Mali yako Na Uzima yako. 

Kama Mungu hakutumie wewe, yawezekana ni wewe ndiwe hautapenda kumuruhusu. 

Sababu gani Mwenyezi Mungu alikuwa akitumikisha sana makanisa ya Makedonia? 

Nitawaambia sababu gani. 

Ni kwa sababu wao wenyewe walijitoa kwanza wenyewe kwake. 

1 Wakorinto 8: 5 

“Kwa maana hata wakiwa walioitwa miungu, ama katika mbingu au katika dunia, kama ni miungu mingi na bwana wengi.” 

18/ Neno hili litadumu hata lini? 

Ninaweza kuwajibu. 

Waefeso 4: 13 

“hata sisi sote tufikie umoja wa imani, na kujua sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mzima, hata kufika kipimo cha urefu wa utimilifu wa Kristo;” 

Hii inamaanisha nini? 

Inamaanisha wakati Kanisa Mwili wa Kristo itakusanyika pale Mbinguni ikizunguuka Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, hapo KRISTO atafunuliwa kwetu sisi wote. 

Kwa sababu hapa chini duniani bado tungali tunasemasema chini chini bila ufahamu kabisa kuhusu utimilifu wa Kristo. 

Ndani ya Waefeso 1: 23, tunasoma ya kwamba: 

“lililo Mwili wake, utimilifu wake  anayetimiza vyote katika vyote.” 

KRISTO ni Kichwa cha Mwili, akiwa kule juu mbinguni ndani ya Utukufu wake; na sisi Waaminifu ni Viungo vya Mwili wake, basi Yeye hatimiliki bila sisi, na sisi hatutimiliki bila YEYE.

Bali, tutafikia Utimilifu wa KRISTO wakati tutafika mbinguni tukiwa pamoja NAYE. 


AMINA

 

N°Ref: 05/01/1960  220 - DID CHRIST DESCENDED INTO HELL / 08/30/2020

Friday, August 21, 2020

KRISTO ALISHUKA KUZIMU? (Sehemu ya kwanza) / DID CHRIST DESCENDED INTO HELL (Part I)

Photo taken by B Smith from Patio




 

KRISTO ALISHUKA KUZIMU? (Sehemu ya kwanza) 

219 - DID CHRIST DESCENDED INTO HELL (Part I)

April 24, 1960 Pastor Henry F. Kulp 



 

Waefeso 4: 7 – 11

“Lakini kila mtu katikati yetu alipewa neema kwa kadiri ya kipimo cha zawadi ya Kristo. 

Kwa hivi anasema: 

Wakati alipopanda juu, alifunga kifungo, 

Akawapa watu zawadi. 

(Basi neno hili: Alipanda, maana yake nini kama si kusema kwamba Yeye alishuka vilevile mpaka pande za chini za inchi? 

Yeye aliyeshuka ndiye aliyepanda vilevile juu sana kupita mbingu zote ili ajaze vitu vyote.) 

Naye alitoa wengine kuwa mitume; na wengine kuwa manabii, na wengine kuwa wahubiri wa Habari Njema; na wengine kuwa wachungaji na walimu;”

Katika maandiko hii tunapata zawadi zenye KRISTO anatoa kwa Kanisa Mwili wake, na zawadi zile zinatokana na Ushindi wa Utukufu wa Bwana Yesu Kristo, sawa vile inavyo andikwa katika aya 8 hadi 10

Ni kwa hiyo imesemwa kwamba: 

Wakati alipopanda juu, alifunga kifungo, Akawapa watu zawadi.  

(Basi neno hili : Alipanda, maana yake nini kama si kusema kwamba Yeye alishuka vilevile mpaka pande za chini za inchi?  

Yeye aliyeshuka ndiye aliyepanda vilevile juu sana kupita mbingu zote ili ajaze vitu vyote.)

Akikwisha kushinda wapinzani wake, walio pia wapinzani wetu, aliwapa watu zawadi mbalimbali ili washiriki Ushindi wake, bali, mbele ya kutafakari juu ya zawadi zenyi KRISTO alizogawa kwa Kanisa Mwili wake, tutiye mafikili yetu kwanza juu ya Ushindi wake wa Utukufu unao oneshewa hapa. 

Ni Ukweli wa muhimu sana na wa ajabu utakoa furahisha mioyo yetu. 


1/ Sasa mbele ya yote, kuna jambo moja mbovu yenye tungelipendelea kujulisha hapa: 

Inakuwa vigumu kwa wakristo wengi kufahamu maandiko hii yenye Mwenyezi Mungu anatuonesha hapa. 

Katika kuamini kwa Mutume, wakristo wengi, kila siku ya yenga inayofika na hasa wakati wa kushiriki Meza ya Bwana, wanasemezana juu ya kushuka kwa Bwana Yesu kule kuzimu. 

Na wengi wanasema kwa juhudi yote kwamba hiyo inahakikisha kwamba KRISTO alishuka kule chini ya inchi, ama kuzimu, akahubiri watu waliokuwa kule na kukomboa watakatifu wa Agano la Kale, na akawapandisha mbinguni, wakiwa pamoja naye.  

Mawazo na mafikili ya namna hii ni kigeni na kinyume na Maandiko Matakatifu. 

Hii siyo mafundisho inayopatikana ndani ya Waefeso 4: 7 – 11. 


2/ Ni muhimu sana kujulisha ya kwamba, kuna wale wanaoamini mambo yanayokuwa mbali sana na ukweli, wanaanguka  ndani  ya mutego  huohuo  kwa kufwata umati wa watu wenye kusadiki vile. 

Siyo kwamba neno lisilokuwa kweli litageuka kuwa kweli kwa sababu umati wa watu unawaza namna sawa. 

Neno lolote kwa kuwa sambamba na kusimama imara, linapashwa kuwa na msingi wake katika Maandiko Matakatifu.  

Tusijali kwamba umati wa watu unaamini neno fulani, ama kufundisha jambo fulani, inatubidi sisi kujiuliza: Maandiko Matakatifu yanatuhubiri nini juu ya jambo hili? 

Tuoneshe utafiti kamili kuusu Ushindi wa Bwana Yesu Kristo, kama inavyooneshwa kwetu katika aya ya 8 hadi 10 kuusu jambo la kwamba anapana zawadi kwa Kanisa. 


3/ Tutumie taswira wanayotuonesha hapa. 

Mbele ya yote inasemwa kwamba: 

Wakati alipopanda juu, alifunga kifungo, Akawapa watu zawadi. 

Sasa, Bwana Yesu Kristo, aliye panda, ndiye vilevile aliye shuka katika pande za chini za inchi.  

Na Yeye aliye shuka ndiye vilevile Yeye aliye panda juu kuliko mbingu zote. 

Sasa hiyo inamaanisha nini?  


4/ Maandiko yanatuambia kwamba Yeye alishuka, mbele ya kushuka, alipanda kwanza juu. 

Hio inamaanisha nini?  

Wakati tunaambiwa kwamba alishuka kwa pande za chini za inchi, 

Hii haimaanishe yale yanayosomeka kwa juu juu tu ndani ya tafsiri ya Biblia ya King James. 

Wakati inasemwa kwamba Yeye alishuka katika pande za chini ya inchi, inamaanisha tu ya kwamba Yeye alishuka katika dunia. 

Sababu ukitazama dunia ukiwa mbinguni, utaona ya kwamba dunia inapatikana kwa pande za chini. 

Mutume Paulo haiko anazungumuza juu ya kushuka ama kupanda ya namna ya kimwili na hii iko mbali sana na tofauti na maana ya maandiko hii. 

Namna gani iwezekanavyo kwa sasa Bwana Yesu Kristu kupanda juu sana kuliko mbinguni? Kwa saa hii Yeye anapatikana kwa Mukono wa Kuume wa Mungu pale mbinguni. 


5/ Utatambua kwamba aya ya kumi inasema kwamba Yeye alipenda juu sana kupita mbinguni, hii inamaanisha kwamba hapa hawazungumuzie juu ya kupanda ya namna ya kimwili. 

Neno “mbali sana”, katika Kigriki inamaanisha HOOP – ER – ONNA na iyo si kwamba ni kupanda ya kimwili. 

Ayo ina maana ya Jamii ya, ama Cheo, ama Nafasi katika jamii, Uwezo ama Mamlaka.  


6/ Kama iyo kupanda haiko kupanda ya kimwili, sababu gani kuzania kwamba wakati inaposemwa: Alishuka, kushuka huko kuwe kwa namna ya kimwili? Hiyo ni mambo yasiyo na msingi.

Hapo, wanazungumuzia juu ya Bwana Yesu kama Mungu, Akiacha makao yake ya Utukufu huko mbinguni na kuja hapa chini zaidi, hapa pa dunia akijitia Yeye mwenyewe katika hali ya kutiishwa. 

Akijifanya Yeye mwenyewe kuwa mutumwa wa mtu. 


7/ Tutafakari kwanza kidogo juu ya msemwa tuliopata katika Waefeso

“alipanda juu sana kupita mbingu zote” 

Tulinganishe hii musemwa kwa yale yanayokuwa ndani ya maandiko ya  

Waebrania 7: 26 

“Maana kuhani mkubwa wa namna hii alitufaa sisi sana, aliye mtakatifu, pasipo uovu, wala alama ya uchafu, aliyetengwa na wenye zambi, aliye kuwa juu kuliko mbingu;” 

Tunatambua kwamba hapa inasemwa kwamba: Aliye kuwa juu kuliko mbingu. 

Neno la kwanza ni kusema kwamba “Aliye pandishwa”, hiyo inamaanisha kwamba, kwa saa ile hakuwa tena katika ngazi yake ya Utukufu ndiyo maana alipandishwa. 

Kiisha hapo, alitukuzwa na kupandishwa juu sana kupita mbingu zote, mara tena tunafahamu kwamba kupandishwa tunayozungumuzia siyo kupandishwa kwa mahali ama nafasi ya kimwili.  


Lakini inamaanisha ranga aliyokuweko, sababu Bwana Yesu Kristo aliamuwa binafsi kujishusha na kunyenyekea akikamata sura ya mtu, akija huku chini duniani na kufa musalabani pale pa Kalvari kwa ajili yetu. 

Na Yeye alitukuzwa baada ya kufufuka alitukuzwa kwa Ranga yake ya Ajabu na Utukufu katika ulimwengu wote.

 8/ Kama vile inavyokuwa wazi ndani ya kitabu cha   Wafilipi 2: 5 – 11  

“Muwe na nia hii ndani yenu iliyokuwa ndani ya Kristo Yesu vilevile; ndiye aliyekuwa na namna ya Mungu, hakuona kuwa sawa na Mungu kuwa kitu kushikamana nacho, 

Lakini alijifanya mwenyewe kuwa hana utukufu, akitwaa namna ya mtumwa, akakuwa na mfano wa mtu 

Na akionekana na sura ya mtu, alijinyenyekeza mwenyewe, akakuwa mwenye kutii hata mauti, ndiyo mauti ya msalaba. 

Kwa hivi Mungu vilevile alimtukuza sana, na kumpa Jina lililo juu ya kila jina; 

Hata kwa Jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni na vya duniani, na chini ya dunia, 

Na kila ulimi ukiri ya kuwa Yesu Kristo ni Bwana kwa utukufu wa Mungu Baba.” 

Mbele ya yote, ningelipendelea tutafakari zaidi, aya ya 7,  

Alijifanya mwenyewe kuwa hana heshima yoyote ile, nikusema kwamba alikamata nafasi ya kujinyenyekeza, Aliuacha nafasi yake ya utukufu, Aliiacha Ranga aliyokuwa nayo. 

Kumbuka kwamba alikamata fasi ya mutumwa, akajifanya kuwa sawa na mtu, ijapokuwa hapo mbele alikuwa sawasawa na Mungu Baba na Mungu Roho Mutakatifu. 

Hakuna yule aliye muamuru kutenda hivyo, hakuna yeyote aliye muambia nini kufanya. 

Tangu milele alikuwa bado hajapima kuwa katika nafasi hiyo ya kujinyenyekeza, lakini kwa gafla Yeye Mwenyewe akanyenyekea. 

Akakamata hali na nafasi hiyo. 

Alikuwa na namna ya mtu, na kwa kuwa na namna ya mutu akajifanya kuwa mtumwa. 


9/ Sawa vile tunafika kwa kiwango hiki, tuchunguze na kuonesha umbalimbali unaokuwa kati ya aya ya 6 na aya ya 7. 

Aya ya sita inasema: Ndiye aliyekuwa na namna ya MUNGU. 

Kulinganisha na Aya ya saba inayosema: akitwaa namna ya mtumwa. 

Katika umilele uliopita, Bwana Yesu alikuwa na namna ya Mungu

Hakuna yeyote aliyeweza kumuamuru, hakuna yeyote aliyeweza kumuambia nini afanye, Yeye ndiye Muumbaji wa Ulimwengu, ni Yeye ndiye aliyefanya Ulimwengu iwe, sasa, siyo tu kwamba anatwa namna ya mtu, lakini jambo mbovu zaidi ni kwamba, anatwaa namna ya mtumwa. 

Sheria ya nyakati zile ilikuwa ikimukabizi yoyote yule anayekuwa na mtumwa kumutendea chochote kile anachotaka, hata kufika kiwango cha kumuuwa, bila kuwa na ajali yeyote na Serkali ama kuwa na swali ama shida na mtu yeyote yule.  

Serkali haingaliweza kuhesabiya kosa lile sawa uuwaji, sababu mtumwa hakuwa na haki hata moja.  

Wakati Bwana Yesu Kristo alishuka na kuja duniani aliacha kando, Haki yake, Ranga yake, Nafasi yake ya Utukufu. 

Yeye alijishusha na kuwa na hali ya unyonge wa kujinyenyekeza. 


10/ Tufahamu kwamba katika maisha yake hapa chini duniani alikuwa chini ya uamzi wa wazazi wake, alikuwa akitenda chochote kile walimuambia kufanya. 

Alikuwa mtu wa Serkali. 

Wakati Serkali ilimuambia alipe kodi, alikuwa akitii. 

Kuna mara alitumia samaki, akiifunguwa kinywa chake na ndani yake alipata pesa ya kulipa kodi. 

Walimuuambia kuibeba musalaba wake, aliunyanyua na kuubeba, o alijushusha na kujinyenyekeza kwa kila hali: Mamlaka, ranga, hata hali na nafasi yake. 


11/ Kama unataka kupata taswira ya Bwana Yesu Kristo kama mtumwa, akiweka kando Mamlaka yake, Utukufu wake, Ranga yake, taswira hiyo utaiona waziwazi katika Maandiko Matakatifu. 

Yoane 13: 4, 5 

“akaondoka kwa chakula, akaweka mavazi yake kando; akatwaa kitambaa, akafunga kiuno chake. 

Kiisha akatia maji kwa kibakuli, akaanza kunawa miguu ya wanafunzi wake na kuipanguza kwa kitambaa ambacho alijifunga kiuno chake.” 

Hapa tunaona Bwana Yesu Kristo akinawisha miguu ya wanafunzi wake. 

Tunaambiwa kwamba alitwaa kitambaa na kuanza kunawa miguu ya wanafunzi wake. 

Picha tunayo hapa ni ile ya mtu mwenye anatoka kwa safari ndefu kwa miguu katika njia inayojaa mavumbi. 

Na sasa kama msafiri huyu alikuwa mgeni kwa chakula katika yumba fulani, mwenyeji wa nyumba alipashwa kuwa na mtumwa mwenye angelipashwa kunawa miguu ya mgeni huyu. 

Ni nini iliyofanyika siku ile? 

Kwa karamu ya mwisho, Yesu Kristo kama mtumwa, alinawa miguu ya wanafunzi wake. 

Hii ilionesha hali yake kama mtumwa. 


12/ Alifanya mapashwa ya mtumwa. 

Alitwaa kitambaa, akafunga kiuno chake, hii inaonesha kazi za ranga ya chini zaidi na ni hizi kazi za chini alizotwaa wakati alikuwa na mufano wa mutu. 

Yeye aligeuka kuwa mtumwa. 

Yeye alijishusha mbele ya mecho ya ulimwengu. 


13/ Kushuka kwa Bwana Yesu Kristo inaonesha kweli kweli mfano wa kupoteza heshima yoyote na Mungu Mwenye Nguvu zote kujinyenyekeza. 

Inatushinda kufahamu namna gani Mungu alijinyenyekeza wakati alipotwaa mfano wa mtu.  

Sababu tunajidanganya kwa kuwa na namna yetu binafsi ya kuona heshima ya kizazi cha wanadamu. 

Hatutambui na kuona kizazi cha wanadamu katika umbo lake la kweli, katika asili yake ya kweli, wamiliki, potofu na kinyume, kichefuchefu, kichafu katika kila hali, na Mwenyezi Mungu aliweza kujishusha, siyo tu hadi kukamata mfano wa mtu, lakini zaidi sana kukamata sura ya mtumwa kwa ajili ya kumkomboa mtu. 


14/ Mara kwa mara ninatafakari juu ya Ukweli unaokuwa katika Waefeso sura 4,   na Wafilipi sura 2

Katika miaka iliyopita, nilisoma ndani ya gazeti za habari “Pittsburg Post”, huko nilipata habari ya mtu mmoja aliyekuwa prezidenti wa Banki. 

Yeye alikuwa akiishi maisha ya raha, akizunguukwa na vifaa vya samani kubwa katika ofisi yake na alikuwa akiisha ndani ya Gorofa kubwa na jamaa lake lilikuwa na kila kile kizuri juu ya maisha yao. 

Lakini, siku moja alianguka katika kosa. 

Munganga moja mwenye alikuwa na aja ya kukopesha dolla 15.000$ alikuja kwake kumuambia hiyo ombi. 

Akamwambia, nitafanya yote iwezekanayo ili upate mkopo huo wa hiyo pesa, lakini kwa shurti moja, inafaa wewe unipe chini ya meza kituliro cha 2000$, na mambo yote yalitendeka vile. 

Prezidenti wa Banki akatupwa kwenye jela. 

Je waweza kufikili mtu huyu iko anaisha katika mateso gani, ijapokuwa jamaa lake wanaishi maisha ya anasa na raha. 

Jamaa lake wanaishi ndani ya gorofa kubwa ya samani sana ijapokuwa yeye anaishi katika mateso, ndani ya chumba ndogo yenye baridi na unyevu. 

Wanasikia raha ya kuwa huru wakati yeye anaishi pamoja na wahalifu. 

Yeye alishushwa sana na kupatishwa haya. 

Kwa kweli picha hii siyo kitu ukilinganisha na namna KRISTO alijinyenyekeza wakati alipotwaa namna ya mtu. 

O, nafurahia sana tendo hili, ni katika kujinyenyekeza kwake ndio sisi tunapata wokovu.


15/ Tuseme kwa mfano kwamba wewe unakuja kushiriki kwenye mchezo wa mbio pamoja na wa Wazalendo wa Mbilikimo, wao ni wafupi sana kwa kimo, wamaskini, kwa hali yao ya maisha, wao ni wachafu katika yote, utu wao una matatizo sana, ni hasara kweli. 

Yote ya maisha yao ni hivihivi tu, wanauwa na kuchinja watu wengine. 

Wana lugha isiyofahamika na wengine. 

Tuseme sasa kwamba wewe vilevile wanakupunguza kimo unakuwa mfupi mno ili uweze kufanana na kuingia katika mashindano, unaanza kuwahubiri juu ya Mungu, na unakufa kwa ajili yao, ukiwa na kimo hicho cha mtu mfupi sana, na unasema nitakufa kwa ajili yenu. 

Ni hivi kweli njo KRISTO alifanya. 

Yeye alishuka katikati ya watu, akiacha mapambo makubwa na Utukufu wake, akijishusha na kujinyenyekeza kwa hali ya mtumwa wa watu.


16/ Kujiangusha chini kwa poromoko ya maajabu sana na kuanguka kwa mwendo mrefu gani huo, Bwana Yesu Kristo alishuka mpaka hapa duniani? 

Wafilipi 2: 8  

“na akionekana na sura ya mtu, alijinyenyekeza mwenyewe, akakuwa mwenye kutii hata mauti, ndiyo mauti ya msalaba.” 

Tafakari kwanza Yesu Kristo Mungu kuuwawa. 

  Kikwazo ni kwamba hakufa kifo cha kawaida. 

Alikufa kifo cha laana. 

Hakufa kwa uraisi katikati ya walio wake, hakufa kwa kifo ya wachujaa ndani ya kiwanza cha vita. 

Yeye alitundikwa tu. 

Kwa nyakati zile, kifo cha musalaba ilikuwa kifo cha malipizi, sawa vile kiti cha umeme. 

Msalaba ilikuwa kifo cha haya. 

Turudie nyuma kidogo katika kitabu cha Kumbukumbu la Torati 21: 23 

“maiti yake haita baki usiku mzima juu ya mti, lakini lazima utamzika siku ile ile; maana yeye aliyetundikwa amelaaniwa na Mungu; usichafue inchi yako ambayo BWANA Mungu wako anakupa wewe iwe uriti wako.” 

Hapa wanazungumuza juu ya mwana anayeasi naye anapashwa kupigwa kwa mawe na kutundikwa kwenye muti, na kutundikwa kwenye muti ni kuwa chini ya laana ya Mungu. Ama kulaaniwa na Mungu.

Ni hivyo kifo cha Bwana Yesu Kristo kilikuwa. 

Na kwa namna hii ndiyo alishuka na kuporomoka kwa ngazi za chini sana zaidi. 

Wagalatia 3: 13 

“Kristo alitukomboa kwa laana ya torati, ikiwa alifanywa laana kwa ajili yetu, kama ilivyoandikwa: Amelaaniwa kila mtu aliyetundikwa juu ya mti;” 

Waraka wa Wagalatia inatuambia mambo yaleyale tu, mambo sawasawa.  

Kweli Bwana Yesu alishuka toka Ranga ya Mamlaka hadi ranga ya mtumwa pamoja na kifo cha majambazi. 

 

17/ Lakini Mungu Baba alimutukuza sana, 

Pia kitabu cha Waefeso 4: 10, kinasema: 

“Yeye aliyeshuka ndiye aliyepanda vilevile juu sana kupita mbingu zote ili ajaze vitu vyote.)” 

Aliyepanda vilevile juu sana kupita mbingu zote, hiyo inamaanisha nini? 

Mara tena Maandiko hii inatafsiriwa ndani ya Wafilipi 2. 

Wafilipi 2: 9 

“Kwa hivi Mungu vilevile alimtukuza sana, na kumpa Jina lililo juu ya kila jina;” 

Wafilipi inatupatia historia. 

Mungu alimuinua sana na hapa kwa Wafilipi 2: 9, inasema: 

“Kwa hivi” inayoweza kutafsiriwa kwamba: “Ni kwa sababu hii.”  

Sababu gani Mwana wa Watu alitukuzwa sana? 

Sababu aliitika kushuka na kujinyenyekeza na kutwaa mfano wa mtumwa.    


18/ Sababu gani Mungu anatukuzwa sana? 

Sababu Yeye ni Muumba wa vitu vyote? 

Hapana, sababu ni Yeye anashika vitu vyote? 

Hapana hata kidogo. 

Aliinuliwa na kutukuzwa sana kwa sababu Yeye aliitika kujishusha na kijinyenyekeza chini sana zaidi, sababu alipendelea wengine wapande juu yake. 


19/ Tendo hili la kuinuliwa na kutukuzwa sana kuliko mbingu zote, ni jibu kweli la maombi la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 

Yoane 17: 5 

“Na sasa unitukuze, Baba, pamoja nawe mwenyewe, kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe mbele ya kuwa dunia.” 

Anasema: unitukuze, Baba, pamoja nawe mwenyewe, kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe mbele ya kuwa dunia. 

Hali yake ya mbele, Ranga aliyokuwa nayo mbele. 


20/ Hii ingelipashwa kuwa mbele ya aya ya 8 

Tunafikia kiwango cha: 

Wakati alipoinuliwa juu sana alifunga kifungo na kuwapa watu zawadi. 

Mutakatifu na Mubarikiwa Mwokozi wetu Yesu Kristo aliwachaguwa mitumi wakati alipokuwa bado hapa chini duniani. 

Na kwa wakati wa kuzaliwa upya unaokuwa wakati wa utawala wa miaka elfu, wataikala juu ya kiti cha Falme kumi na Miwili, wakihukumu ma kabila kumi na miwili ya wana wa Waisraeli. 

Kwa KRISTO aliye inuliwa, alijichagulia Mitume na Manabii kwa Kanisa lake, na anawasimika hivyo akiwa huko mbinguni. 


21/ Tuchumguze sasa msemwa: 

Alifunga Kifungo  

Sasa, hiyo inamaanisha nini? 

Tunaweza kupata mwangaza katika Agano la Kale. 

Waamuzi 5: 12 

“Amka, amka Debora, 

Amka, amka, toa wimbo, 

Simama, Baraka, funga kifungo chako, wewe mwana wa Abinoamu.” 

Hapa tunapata huo huo msemwa moja, Debora iko anashukuru Mwenyezi Mungu kwa ajili ya ushindi wake mukubwa juu ya wana Wakanana; na hapa kwa aya ya 12 tunasoma: 

Amka, amka Debora, Amka, amka, toa wimbo, Simama, Baraka, funga kifungo chako,  


22/ Kiisha tunasoma katika Isaya 14: 2, ya kwamba: 

“Na wale makabila ya watu watawatwaa na kuwaleta pahali pao; na nyumba ya Israeli watawariti katika inchi ya BWANA kuwa watumishi na vijakazi; na watawakamata wafungwa, wao ambao waliwafunga, na watatawala watu wale ambao waliwaonea.” 

Hapa tunapata msemwa huo huo na wakufanana kweli, unaoleta utafsiri unaosikilika kweli wa maandiko tuliyosoma katika kitabu cha Waefeso, na hapa inasemwa ya kwamba: 

Na wale makabila ya watu watawatwaa na kuwaleta pahali pao; na nyumba ya Israeli watawariti katika inchi ya BWANA kuwa watumishi na vijakazi; na watawakamata wafungwa, wao ambao waliwafunga, na watatawala watu wale ambao waliwaonea.   

Kwa kweli, tunapata hapo utafsiri muzuri na wenye kusema waziwazi, na maandiko hii inamaanisha kwamba: 

Mutakatifu na Mubarikiwa Bwana wetu katika Ushindi wake juu ya kufa, alimuleta katika kifungo yeye aliyekuwa hadi hapo na nguvu za mauti, ili Yeye akomboe wale waliokuwa chini ya kifungo na woga ya mauti na waliokuwa watumwa maisha yao yote

Waebrania 2: 15 

“na kuwafunguwa wale wote waliokuwa maisha yao yote katika hali ya utumwa, kwa woga wa mauti.” 

Ni kusema kwamba adui wetu Shetani mwenye nguvu anakuwa mupambanaji wetu tayari ameisha shindwa. 

Analetwa akiwa mfungwa ndani ya garini ya KRISTO. 


23/ Sasa kiisha kuchambua na kuchehua maandiko haya,

Tunakuwa na wazo la ajabu. 

Kila saa na dakika yenye ninaposoma maandika haya, sitachoka kukumbuka mara kwa mara  kwamba Yeye, Bwana na Mwokozi Yesu Kristo alipanda juu sana zaidi kuliko ginsi hata mtu mmoja hajapima kufanya, na kwa kutukomboa, alishuka chini sana zaidi kuliko namna hata mutu mmoja hajawayi kushuka. 

Aliacha Mapambo yote aliyokuwa nayo huko juu na akaja kuwa mtumwa wa mtu, na kwa sasa ametukuzwa na kunyanyuliwa juu sana, anakuwa mtu wa Ulimwengu wote.  


24/ Mara ninajiuliza kwamba eti ufahamu wetu na roho zetu, zinatambua  kweli kwamba Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo ni kweli Mtu sawasawa na sisi, bali, kwa kweli Yeye anatukuzwa, Ni Mutukufu, Mutakatifu, pasipo zambi, na Anakaa na kumiliki katika Kiti cha Ufalme cha Mungu. 

Na Kwa kiti kile Cha Ufalme wa Mungu, anaombea Taifa lake kila saa na kila dakika muchana na usiku, sababu taifa lake bado lingali katika mahitaji, sababu wangali bado katika majira ya hapa chini dunia. 


AMINA. 


N°Ref: 04/24/1960/ 219 - DID CHRIST DESCENDED INTO HELL (Part I) 08/21/202