Friday, January 31, 2020

MWILI WA UREMBO / THE BODY BEAUTIFUL

Photo taken from B Smith's kitchen Window







     MWILI WA UREMBO 
     THE BODY BEAUTIFUL 
     Pastor Henry F. Kulp
     January 10, 1960 







Waefeso 2: 17 - 22 
“Akakuja na kuhubiri salama kwenu muliokuwa mbali, na salama kwao waliokuwa karibu. 
Kwa maana kwa yeye sisi sote tumepata njia ya kukaribia Baba katika Roho mmoja. 
Basi tangu sasa ninyi si wageni na wasafiri tena, lakini wenyeji pamoja na watakatifu, na watu wa nyumba ya Mungu. 

Mumejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kubwa la pembeni. 

Katika yeye jengo zima linaunganishwa vizuri na kukua hata lipate kuwa hekalu takatifu katika Bwana. 

Katika yeye ninyi vilevile munajengwa pamoja kuwa kao la Mungu katika Roho.” 

Katika siku zilizo pita, tulikuwa tukiwaonesha tofauti iliyokuweko zamani katikati ya Muyuda na mutu wa Mataifa. 

Wakati Mungu alikuwa bado angali anashimamisha kiambaza cha uadui, maagizo na ma shurti. 

Kulikuweko taifa lenye lilikuwa likifugwa kwa upendelevu kama vile mfuga nyama anaweza kufuga nyama. Kulikuweko Taifa pendelevu. 

Taifa hiyo ilikuwa ikipendelewa sana na kuwa na faida mbalimbali za upekee na lilo Taifa lilikuwa Taifa la Israeli. 

Mataifa mengine ama wapagani hawakuwa na faida lolote, hawakuwa na maagizo, ma shurti, ama sheria, wao hawakukuwa na agizo la kuja kwa Mwokozi, hawakuwa hata na kitu chochote, walikuwa wakitiwa mbali sana wakati Israeli ilikuwa karibu na Mungu. 

1/ Mungu alibomoa  kiambaza ile ya uadui kwa njia ya Yesu Kristo, na kwa sasa hakuna tena Muyuda wala mutu wa Mataifa na faida kubwa tunalolipata ni kwamba, wakati tunaamini Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo tunakuwa kiungo cha ule Mutu Mupya hiyo maagizo yote ya zamani na shurti zote za zamani  zikitupwa inje na kuvunjwa na shurti moja inayokuwa kwetu kwa leo inapatikana katika haya ya kumi na nane 18 inayosema: Muyuda na Mutu wa Mataifa, kwa njia ya Yesu Kristo, sisi sote tumepata njia ya kukaribia Baba katika Roho mmoja. 

Kweli hii ni kitu kipya, tunaona kwamba katika siku za kale haikuwezekana kukaribia Mungu Baba kwa mara moja, hata Wayuda, hata vile walivyokuwa na faida nyingi na walikuwa wapendelewa lakini hawakuweza kukaribia Baba Mungu kwa mara moja, kwa urahisi. 

2/ Hapo tunaona ya kwamba kiongozi ni Roho Mutakatifu. 
Ni Yeye njo mwenye anatufikisha katika uwepo wa Baba Mungu. 
Neno kupewa njiya ni neno la kigeni inatokea katika neno pros-ag-o. 
Pros inamaanisha uso kwa uso, 

Ago inamaanisha kuonesha mwelekeo. Yeye anatuelekeza tuwe uso kwa uso na misemwa hii inatumikishwa kwa ku maanisha kwenda mbele ya mukubwa mwenye mamlaka na uwezo, kuelekezwa mbele ya Yule Mwenye Uwezo kwa njia ya Yesu Kristo. 
Mbele ya kubomolewa kwa hiyo kiambaza cha uadui, neno hili halikujulikana. 

3/ Haya ya kumi na kenda 19  
Hapa tunafika kwa Ukweli huu wa kushangaza. 
Haya hii inaanza na neno Basi sasa. 

Sasa inakuwa ya muhimu kabisa na inaonesha kwamba ni katika wakati huu. Nikusema sisi tunapata kitu chenye hakuna mutu mwengine mwenye alikipata mbele. 
Na neno Basi sasa inamaanisha kitu kinacho pata sasa nafasi. 

Sababu kwa sasa Muyuda na mutu wa Mataifa wote kwa njia ya Bwana Yesu Kristo, wanakuwa na njia wazi kwa Baba Mungu, Roho Mutakatifu anawaongoza na kuwaelekeza mbele ya Mungu. 

Hatuko tena wageni na wasafiri, lakini wenyeji pamoja na watakatifu, hiyo inamaanisha nini? 

Kwa kweli, je, sisi si watakatifu? 
Kila yeye aliyeokolewa, yeye ni mutakatifu. 
Tafsiri ya Biblia King James haiko wazi hapa. 
Sisi tunakuwa wenyeji pamoja na watakatifu 

KUJISIKIA KWANGU MWENYEWE KWENYE ARZI na kweli hii inamaanisha nini? 
Hapo tusoma katika kitabu cha mutume Paulo kwa Waebrania 9: 8  

“Roho Mutakatifu akionyesha neno hili ya kuwa njia ya kuingia Pahali Patakatifu haijafunguka wazi bado, hema ya kwanza ilipokuwa ingali kusimama” 

Nafasi inaposemwa Pahali patakatifu pa patakatifu kama inavyosemwa na neno lilo moja la kigriki. 

Ni nafasi gani katika mbingu zote ilio nafasi patakatifu pa patakatifu? 
Nafasi hiyo haina kunjo, ama ukorofi, nafsi yenye haikumbwi na zambi, ni uwepo tu wa Baba Mungu, nafasi hiyo tutaishi milele na milele. 

Mambo mengine sawa vile mbingu mupya na dunia mupya yote itapita, bali ni nafasi hiyo tu njo itadumu milele ni kusema Mbinguni. 

Basi, sisi hatuko tena wageni lakini wenyeji pamoja na watakatifu katika mahali pa takatifu pa patakatifu huko juu Mbinguni.

4/ Watu wengine wanasema kama hawana uhakika wa kwenda mbinguni lakini sisi sharti tuwe na uhakika wa kwenda mbinguni sababu sisi ni wenyeji wa mbinguni, Makao yetu ni kule. 

HII NJO INAPASHWA KUWA KWA MWANZO WA KILA NENO LETU, NENO GANI LA RAHA NA MUSHANGAZO KWA SISI WENYE HAPO KALE TULIKUWA WAFU SABABU YA MAKOSA YETU NA ZAMBI, MBALI NA MUNGU, BILA MUNGU KATIKA DUNIA HII NA KWA LEO TUWE NA UWEZO WA KUANGALIA MUNGU ANA KWA ANA NA KUZUNGUMUZA NAYE KAMA BABA. PICHA HII YA KUSHANGAZA TUNAIPATA KATIKA KITABU CHA MUTUME PAULO KWA 

WAROMA 8:16  
“Kwa maana hamukupokea tena roho ya utumwa inayoleta woga, lakini mulipokea roho ya kufanywa wana, kwa sababu hii tunalia: Aba, Baba.”

Hapa inasemwa kwamba kama kwa maongozi ya Roho tunalia Aba Baba. 
Wataalamu wamoja wanatuambia kwamba Aba ni sawa vile mutoto anaita Baba, kama watoto wa kihebrania walivyokuwa wanaita wababa zao, sawa vile vile watoto wetu wachanga wanaita baba. Ni jina yenye inamaanisha undugu wa karibu sana, hiyo siyo lalamiko la namna ya kidini ama namna wayuda walikuwa wanaita Mungu. 

5/ Wakati tunaangalia mambo haya yote makubwa, tunaona kwa kweli kwamba wakati tunakaribia kweli uwepo wa Baba Mungu, hatupashwe kuchanganyikiwa ama kuwa na woga, hatupashwe kuwa wanyonge sababu sisi ni wana wa Mungu. 

6/ Tuangalie kwanza hiyo namana ya kuitwa jina wenyeji wa, na jina Pahali Patakatifu pa patakatifu. 
Hiyo wazo haiko kigeni ndani ya Biblia, sababu katika kitabu cha mutume Paulo kwa 

Wafilipi 3: 20 
“Kwa maana sisi ni wenyeji wa mbinguni; kutoka pale tunangoja Mwokozi, Bwana Yesu Kristo”

Tunasoma hapo kama sisi ni wanainchi wa mbinguni ni kusema kwamba Mutume Paulo alikuwa anajuwa kwamba yeye ni mwanainchi wa mbinguni. 

Muji wa Filipi ulikuwa kikoloni ya wa Roma. 

Jina ukoloni kwa nyakati zile ilikuwa na maana na hali nyingine mbalimbali na sasa. 
Muji unaokuwa chini ya ukoloni wa waroma ni muji wenye ulikuwa na kujitoa na kufanya maneno ya ushujaa kwa faida ya utawala wa waroma na kwa namna ya malipo kwa  taifa na watu wa muji ule kwa kujitowa kwao na uaminifu wao, waroma walikuwa wanapatia muji ule jina ya ukoloni. 

Na ile kuitwa ukoloni wa waroma, ilikuwa unapatia palepale kila mukaaji wa muji ule anayekuwa huru, ilikuwa inamupatia kuwa mwanainchi wa Roma na yeye alipokea faida  na haki yote sawa sawa  na mwanaichi halali wa taifa la Roma. 

7/ Ilikuwa miaka michache mbele Mutume Paulo aandike waraka huu wa wafilipi njo taifa la wa Roma ilikuwa na ugonvi na taifa la ngambo ya Mashariki- Kaskazini.
Wakati vikosi vya askari wa roma walipofika Filipi, walikuta tayari wafilipi wamekwisha tayarisha vifaa na vikosi nyingi kwa niaba ya kuunga mukono na kusaidia askari waroma.  
Ma jemadari waroma walishangaa na kufurahi sana kwa tendo lile la ukarimu na kujitowa na walituma ripoti ya ajabu kwao Roma. 

Wabunge wakuu walikusanyika huko Roma na walipatia Filipi madaraka ya kuwa koloni ya Roma na kwa hiyo kila mukaaji wa Filipi angiweza kujiita kwamba yeye ni mukaaji wa Roma, yeye anakuwa sawa sawa na muroma na kuwa na haki yote yenye inajulikana kwa waroma. 

Kwa kweli wao walikuwa wakaaji wa Filipi na Filipi ilipatikana ndani ya Makedonia walikuwa basi na mapashwa yakutimiza juu ya serkali ya Makedonia, lakini Filipi ilikuwa chini ya uongozi wa gavernementi ya Roma na Wafilipi walikuwa na mujumbe wao ndani ya gavernementi ya Roma hii njo ilikuwa maana yake. 

Sisi vile vile tunaishi katika dunia hii ya zambi lakini sisi ni wenye zambi waliookolewa kwa Neema na sisi sote tunaungwa kwa Mwokozi wetu Yesu Kristo mwenyi enzi utukufu na mubarikiwa hata kama dunia inamukataa. 

Na Mungu anafurahia kujitowa kwetu kwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo katika nyakati hizi mbaya yenye watu hawamupendi Mwokozi Yesu Kristo. 

Na Mungu anapatia kila mutu anaye amini Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, kama Bwana na Mwokozi wake, huyu mutu Baba Mungu anamupa madaraka ya kuwa mukaaji na mwenyeji wa Mbinguni.

Watu hawa wanakuwa wenyeji wa mbinguni hata kama kwa sasa wao wangali wanaishi duniani.

Raha kubwa gani kuwa mukaaji wa Mbinguni. 
Mimi ninajuwa yakwamba nimeokoka. 
Mimi ninajuwa kwamba nimenunuliwa kwa bei ya damani. 
Mimi ninajuwa kwamba niko katika safari ya kwenda mbinguni sababu mimi ni mukaaji wa mbinguni. 

8/ Hapa tuna picha ya ajabu ya Roho Mutakatifu kama Mujengaji na tunakuwa na kweli ingine yenye ilikuwa hata wakati hiyo kiambaza cha uadui kilikuwa kingaliko. Na kweli hii tunaipata katika haya 21 na 22. 

“Katika yeye jengo zima linaunganishwa vizuri na kukua hata lipate kuwa hekalu takatifu katika Bwana. 
Katika yeye ninyi vilevile munajengwa pamoja kuwa kao la Mungu katika Roho” 

Kweli hiyo ni gani? 
Kweli hiyo ni kusema kwamba kwa siku za leo Mungu iko na Kao. 
Mungu ana kao lenye anaweza kuishi ndani yake. 
Kwa wakati huu wa Neema, kwa nyakati za sasa, kao lenye Mungu iko nalo ni Hai ama ni kao lililo hai. 

Hiyo kao la Mungu siyo kanisa kubwa yenye tunaona ya mawe, siyo hiyo kanisa nzuri ya kipresibiteriani lenye lilijengwa na ma milioni ya dolla, wala siyo hata moja ya makanisa ya gorofa kubwa lenye unafahamu, hakuna hata moja za hizo magorofa inayokuwa nyumba ya Mungu na watu wote wanafahamu hivyo. 

Mungu katika nyakati za Agano la kale alikuwa na nyumba lililo jengwa kwa vifaa mbalimali. 
Ndani ya nyumba hilo, hekalu kwa zamani, alikuwa akionesha utukufu wake mkubwa. 
Lakini kwa siku za leo, Mungu anaishi katika Kao lililo hai, hekalu lililo hai, siyo ya vitu ama vifaa mbalimbali. 

9/ Ni Kao la Mungu, Jengo la Mungu linalo undwa na mukusanyo wa watu, watu walio okolewa kwa kuamini Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 

1 Timoteo 3: 15 
“Lakini kama nikikawia, upate kujua sana namna inavyokupasa kutenda katika nyumba ya Mungu, iliyo kanisa la Mungu aliye hai, nguzo na msingi wa kweli.”

Inatuambia kwamba tunapashwa kuchunguza namna gani tunapaswa kutembea katika nyumba ya Mungu. 

Hii aimaanishe nyumba iliyojengwa kwa mikono ya watu lakini Nyumba yenye Mungu iko anajenga akitumikisha watu walio hai sawa viungo vya iyo jengo.  
Hii aisemi namna gani wewe kutembea katika kanisa lako la nafasi, (…) 
ama katika gorofa mulio jenga kama kanisa, lakini ukiwa sasa kiungo cha hiyo Kanisa lenye liko linajengwa unapashwa kujuwa namna gani inavyokupasa kutenda sababu tusilete magonvi katika Kao la Mungu. 

10/ Tuone musingi ya maneno haya katika haya ya 20. 
“Mumejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kubwa la pembeni.”

Tuona namna misemwa inapangwa mitume na manabii. 
Mutume Paulo hakusema mumejengwa juu ya msingi wa manabii na mitume. 
Anasema mitume na manabii. 

Niya muhimu sana kuangalia namna maneno haya mawili yanapangwa, sababu kwa siku za leo kuna wale wanaosema ya kwamba hakuna tofauti kati ya Kanisa na Ufalme wa Mungu. 
Na wanasema kwamba watakatifu wa Agano la Kale wako sawa na watakatifu wa siku za leo wanao okolewa katika utunzaji hii wa neema. Hiyo ni kutokujuwa kweli. 

Wanasema kwamba mitume wanaotajwa hapa ni wale mitume kumi na miwili wa Bwana Yesu na kwamba manabii wanao tajwa hapa ni wale manabii wa Agano la Kale. Si hivyo. 
Ingelikuwa ni hivyo, mutume Paulo angelisema Manabii na mitume, hiyo njo ingekuwa kupangwa iliyo halali. 

11/ Tukumbuke kwamba watakatifu wa Agano la Kale tunaowaita watu wa haki, wao hawako viungo vya hiyo Kanisa, hawako viungo vya iyo jengo hata kama kuwa wameokolewa. 

12/ Tusome kama tukitamani katika kitabu cha 2 Petro 3: 2  
“mupate kukumbuka maneno yaliyosemwa zamani na manabii watakatifu, na amri ya Bwana na Mwokozi iliyoletwa na mitume yenu.”

Nafasi hii Manabii wa Agano la kale wanatajwa na kapangwa mbele ya Mitume. 
Hii inaelekea habari ya kuja ama kurudi hapa duniani kwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo na inaonesha kwamba ni manabii wa Agano la kale njo walianza kwanza kutabiri juu ya neno hilo na kiisha hawa mitume kumi na miwili wa Bwana Yesu walisema tena kiisha juu ya jambo lilo. 

Manabii kiisha mitume ni hii mupango ulio kwa namna ya halali. 

13/ Lakini tukirudi katika Waefeso, tutaona kama pale haikupangwa namna hii. 
Katika Waefeso 4:11 tunasoma:

“Naye alitoa wengine kuwa mitume; na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wahubiri wa Habari Njema; na wengine kuwa wachungaji na walimu;”

Hapa inasemwa juu ya zawadi za kiroho yenye Bwana wetu Kristo Yesu aliipatia kanisa na hapo mutume Paulo anasema ya kwamba Kristo alitoa wengine kuwa mitume na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wahubiri wa Habari Njema; na wangine kuwa wachungaji na walimu. 

Tuchunguze namna misemwa inavyopangwa hapa, mitume kiisha manabii.
Hii aimaanishi wale kumi na wawili ama mitume wa Agano la kale. 

Mitume ni wanani? Kweli kwa siku zilizo pita tuliwakumbusha kwamba Mutume ni mutu aliyetumwa, Mutume Paulo alikuwa Mutume na alikuwa mutu aliye tumwa. Neno Mutume inamaanisha mutu aliye tumwa kwenda kuhubiri, naye ni mutume ndani ya Agano jipya. 
Alitumwa kuhubiri Maneno ya Mungu, siyo ya kutia uvuguvugu na hali ya kupana unabii wa mambo itakayo kuja. 

Yote ni zawadi ya Mungu kwa kanisa.

14/ Sasa, tukumbuke kwamba mitume na manabii wa Agano Jipya hawakuwa Msingi wa kanisa. 
Mutume Paulo hakusema yakwamba: mimi ni msingi, lakini alisema mimi ninatia msingi. 

1 Wakorinto 3: 11 
“Maana mtu hawezi kuweka msingi mwengine ila ule uliokwisha kuwekwa, yeye Yesu Kristo”

Walikuwa wakihubiri na kufundisha kwamba Yesu Kristo ndiye Msingi. Kanisa inajengwa juu ya Msingi ulio Imara hauwezi kutikisika. 

15/ Kiisha tuangalie neno “jengo linaunganishwa pamoja na kukua”, kugua inaonesha kukomaa, inamaanisha kuendelea mbele, kutimilika katika utimilivu. 

Kila mtu hagui kwa upekee, lakini jengo lote zima inakomaa ndani ya Hema takatifu ya Roho Mutakatifu katika Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 

Kweli hiyo ni raha kujuwa katika roho yako kwamba sisi ni mawe yaliyo hai katika jengo lile la utukufu. 

Nazani neno hili linasukuma nafsi yako kuona umuhimu wa kuishi maisha ya utakaso kwa kujuwa namna gani inatupasa kutembea katika nyumba ya Mungu, JENGO la Mungu, KANISA la Mungu, KAO la Mungu.” 

16/ Wakati wa Agano la Kale, wakati Hekalu la Solomono lilikuwa likijengwa, lilitiwa juu ya mulima wa moria, kwenye nafasi lililotengenezwa  
Kwenye chongo ya mulima. 
Mawe makuu yalikuwa yakichorewa na kutengenezwa na kupandishwa ili yatiwe kwa jengo la hekalu.  

Kiisha muda wa miaka saba, jengo lile lilikuwa kubwa sana na la mastaajabu na kupendeza kwa wakati ule katika daftari ya dunia zima. 

Na kulikuwa kitu kimoja cha upekee wakati hekalu lile lilikuwa likijengwa 
Majengo ya hekalu ilikuwa ikifanyika bila fujo yoyote, hata mulio wa hama haukuwa unasikilikana sababu mawe yote yalikuwa yakitengenezwa na kuchorewa huko chini  na kukatwa na kurandwa na kupewa umbo linalostahili, kiisha baadaye njo yanakwenda tiliwa katika jingo wakiunganisha jiwe moja pembeni ya jiwe lingine wakiyabananisha na simenti bila kutumikisha hama ya watumishi wajengaji. 
Ni kwa hiyo hapana mutu mwenye anastahili kusikia fujo ama mulio wowote katika Jengo la leo, kama kweli sisi ni Majiwe yaliyo na uhai, yanayo tiwa pamoja katika Hekalu ya Mungu, Kao la Mungu. 

Roho Mutakatifu njo mwenye kuchimba mawe yaliyo na uhai akayatosha  toka shimo la zambi, anayainua kwa Nguvu na Uwezo wake wa ajabu na kuyaingiza katika Jengo linalokuwa juu ya Msingi kubwa ndiye Mwokozi wetu Yesu Kristo. 

Kwa kweli, mawe haya yaliyo na uhai yanatokea katika bara la Afrika, yanatokea huko India, Chaina, katika visanga vyote vya ma bara, hii ni ukweli wa utukufu.

17/ Kama ungaliweza kuniuliza mawazo yangu kuhusu siku gani hayo majengo ya Hekalu lile yatamalizika na kutimizwa, nitakujibu kwamba inabaki tu kutiya Majiwe mamoja mamoja hapa na pale kwa ukuta wa juu na yote itatimilika. 
Nina uhakika kwamba tunakuwa ndani ya majira ya nyakati zenye majengo ya Hekalu tayari inaanza malizika. 

Inawezekana kwamba Jiwe la mwisho litatiwa leo hii na kazi yote itakwisha. 
Maombi yangu ni kwamba wewe vile vile uwe kiungo cha ile Hekalu la utukufu, Kao la Baba Mungu. 

Majengo ya Hekalu inaweza kwisha leo na itakuwa nyuma kwako hauta weza tena fanya kitu chochote kwa kuwa moja wa viungo vya lile jengo na itakuwa hasara sana. 

18/ Sasa twende ndani kabisa ya hii waraka. 
 Katika sura yake ya tatu Mutume Paulo anatuonesha namna gani alifikia kupewa Ufahamu wa Ukweli huu uliofunuliwa kwake. 

Anatuambia kwamba yeye aliupata kwa njia ya UFUNUO. 
Yeye hakupata ufunuo huu kwa Yakobo, ama kwa Yoane, ama kwa mumoja wa wale mitume kumi na miwili. 

Na sasa hii Ukweli yenye aliyo upata kwa ufunuo, inaita “SIRI KUU.” 

19/ Ni kwa sababu ya Ukweli huu njo alipatikana katika gereza wakati alikuwa akiandika Waraka kwa Waefeso.   

Mutume Paulo hakupatikana ndani ya gereza kwa makosa aliyo yafanya ama kwa sababu hakutii Baba Mungu, sivyo. 

Yeye alipatikana katika kifungo cha gereza sababu ya Ukweli huu wakusema kama hakuna tena Muyuda ama Mutu wa Mataifa, wote wanakuwa kwa daraja moja mbele ya Mungu Baba na wote watakuwa viungo vya Mwili Mumoja, hapana ufalme. 

20/ Tuone namna inavyosemwa: 
Mimi Paulo, mufungwa wa Yesu Kristo kwa ajili yenu nyinyi Mataifa. 
Mutakumbuka ya kuwa ni wakati Mutume Paulo alikuwa akishuka toka mulango wa Hekalu ya Yerusalemu ndiyo wakati alio anza kutangaza hazarani kwamba yeye alitumwa na Bwana Yesu Kristo. Na kwamba Bwana Yesu Kristo alimutuma kwa Mataifa, ili aende kuhubiri Mataifa, wapagani na saa wayuda walisikia maneno haya walichanganyikiwa na kuwa na hasira kubwa sana zaidi na walilalamika na kupaza sauti wakisema “Ondocheni mutu wa namna hii katika dunia, sababu hastahili kuishi”  

Matendo ya Mitume 22: 22  
“Walimusikiliza mpaka neno hili, wakapaza sauti zao, wakisema: Mwondoshe huyu katika inchi kwa maana haifai aishi”

Ni kwa sababu ya hii, sisi Mataifa tunao kuwa wapagani kwa kuzaliwa kwetu, tuna  sababu kweli ya kuleta shukrani kubwa zaidi na  ya upekee na ya sifa kwa uhodari, ukamilifu na kustawi  na kustahimili kwa Mutume Paulo katika kutangaza na kuhubiri Mapenzi na Mupango wa Mungu katika Utunzaji wake huu mupya. 

Siyo miradi ya Ufalme lakini ni miradi ya Mwili wa Kristo.  
Ni kwa sababu ya Miradi hii ya Mwili wa Kristo njo maana mutume Paulo alishindana na kuvumilia haya na zarau na kupitisha siku nyingi katika mateso na uchungu kubwa, katika unyonge wa gereza na aliitika hayo yote pahali ya yeye kukosa kutangaza hata nugta moja ya Ukweli  na mwito na kujitoa yenye Baba Mungu aliutia ndani mwake. 

21/ Turuke haya zimoja za hii sura ya tatu ya Waefeso na twende kwa haya ya kenda: 
Waefeso 3: 9  
“na kuangazia watu wote wajue habari za madaraka ya siri iliyofichwa tangu zamani ndani ya Mungu aliyeumba vitu vyote;” katika Yesu Kristo.

Hii maneno ilikuwa inafichwa ndani ya MUNGU. 
Haisemwe tu kwamba hii siri ilikuwa tu inafichwa ndani ya Biblia, haiko kusema kwamba hii siri ilikuwa inapatikana katika Agano la Kale, na kwamba ilitupasa sisi kucheuwa na kuchimba na kuchunguza ili tuipate. Sivyo vile. 

Hii siri ilikuwa ikificha tangu zamani ndani ya Mungu na haikuwezekana hata mutu yeyote kuigundua kama haingelikuwa yeye Mwenyezi Mungu mwenyewe aifunulie mutu kwa ufunuo wa kimungu. 

Ni kwa ufunuo wa Mungu Mwenyewe njo siri hii ilifunuliwa kwa ufunuo kwa Mutume Paulo kwa njia ya Ufunuo toka Mungu yeye mwenyewe akimufunulia uso kwa uso. 

22/ Hata wamalaika wema sana na wabaya hakuna mwenye alikuwa na ufahamu wowote juu ya siri hii ya Mwili wa Kristo, mpaka ikamupendeza Mungu amufunulie kiumbe chake Paulo aliyekuwa akiishi ndani ya dunia, na kwa njia ya kutangaza kwa Mutume Paulo, wengine vile vile wapate kufunuliwa na wao vile vile wafunulie wengine, hii njo maana ya haya hiyo ya kumi. 

Waefeso 3: 10  
“ili sasa, kwa njia ya kanisa, hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi ijulishwe na falme na mamlaka katika pahali pa mbingu;”

Hii ni Ukweli mkubwa na ya manufaa yenye wengi wetu hawaelewe kwa siku za leo kwa sababu haiwezekane kuupapasa kwa namna ya kimutu, haiwezekane kuuona na mecho ya kibinadamu, na haiwezekane kuikadirisha na akili ya kimutu. 
 
AMEN

 
Ref: 01/10/1960 / 209 - THE BODY BEAUTIFUL / 1/31/2020

Thursday, January 16, 2020

KWA NINI MUTUME PAULO ALIKUWA GEREZANI / WHY WAS PAUL IN PRISON



Photo taken from our kitchen window










     KWA NINI MUTUME PAULO ALIKUWA GEREZANI 
     WHY WAS PAUL IN PRISON 
     Pastor Henry F. Kulp
     January 24, 1960






Waefeso 3: 1-10 

“Kwa sababu hii mimi Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu kwa ajili yenu ninyi mataifa, 
ikiwa mumesikia habari za uwakili wa neema ile ya Mungu niliyopewa kwa ajili yenu; 
ya kwamba kwa ufunuo nilijulishwa siri hii, kama nilivyoandika mbele kwa maneno machache. 

Kwa maneno haya, wakati munaposoma munaweza kutambuwa ufahamu wangu katika siri ya Kristo. 

Siri hii haikujulikana kwa wana wa watu katika vizazi vingine, kama ilivyofunuliwa sasa kwa mitume yake watakatifu na manabii katika Roho; ya kwamba Mataifa ni wariti pamoja nasi wa uriti mmoja, na wa mwili mmoja, na washiriki pamoja nasi wa ahadi hii katika Kristo Yesu kwa njia ya Habari Njema. 

Nilifanywa muhubiri wa Habari Njema hii, kwa kadiri ya zawadi ya neema ile ya Mungu niliyopewa kwa kadiri ya utendaji wa uwezo wake. 

Mimi, niliye mdogo kuliko yeye mdogo wa watakatifu wote nilipewa neema hii  ya kuhubiri Mataifa utajiri wa Kristo usiotafutikana; na kuangazia watu wote wajue habari za madaraka ya siri iliyofichwa tangu zamani ndani ya Mungu aliyeumba vitu vyote; 
ili sasa, kwa njia ya kanisa, hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi ijulishwe na falme na mamlaka katika pahali pa mbingu;”  
Hapa katika kitabu cha Waefeso, mutume Paulo iko anatuzungumuzia Jengo ambalo Mungu Baba iko anajenga. 

Hekalu lenye iko anajenga kwa kupitia kazi ya Roho Mutakatifu. 

Mutume Paulo alituambia ya kwamba katika siku za kale, Baba Mungu alichaguwa kutumika na taifa la wana wa Israeli na kulikuwa kibambazi ya uadui katikati yao na mataifa zingine walioitwa wapagani, wasiojuwa Mungu wala hawakuwa na Mungu. 
Wala hawakuwasiliana na Mungu kwa sababu Yeye alikuwa anawasiliana tu na taifa la Israeli. 

Kiisha Paulo aliwaambia ya kwamba Mungu alibomoa kiambaza hicho cha uadui na matengano, aliibomoa kupitia Yesu Kristo. 

Sasa kwa leo, paali ya kuwasiliana tu na taifa moja tu, kwa leo Baba Mungu anawasiliana na mataifa yote ya ulimwengu.  

Mungu anawasiliana na kila mutu anayekuja kwake kwa njia ya Kristo Yesu. 

Na huyo mutu anakuwa jiwe la uzima katika Jengo hilo Mupya linalokuwa Kao la Mungu. 

1/ Sasa ndani ya sura ya tatu ya kitabu cha Waefeso, Mutume Paulo anasema kwamba angelitamani mujuwe namna gani alifikia kupata na kujulishwa Injili hii. Namuna gani alifikia kujulishwa na kuwa na ufahamu ya kweli hii, ni hapo anasema kama yeye aliijulishwa katika ufunuo (haya yake ya tatu).   

Juma jana, tulijishurtisha na  tulichukuwa muda ya kuwaonesha ya kwamba Injili hii aliijulishwa katika ufunuo akiwa uso kwa uso, na ana kwa ana, akiijulishwa na Mwokozi wetu Yesu Kristo Yeye mwenyewe uso kwa uso. 

Mutume Paulo hakuipata toka mutume Petro, ama Yakobo ama mutume mwengine. Yeye hakuipata toka kwa mitume kumi na wawili wa Bwana Yesu, wala hakuijifundisha toka mafundisho ya Agano la Kale, hii Injili ni kitu kipya chenye Mutume Paulo alipashwa funulia wanaadamu. 

2/ Ni ya muhimu na samani sana tujuwe na kufahamu kwamba Injili hii iko umbalimbali na habari njema yoyote katika Biblia. 

3/ Injili hii ama Habari Njema hii ni gani? 

Waefeso 3: 6 inayosema 

“ya kwamba Wayuda na Mataifa  watakuwa sasa ndani ya Mwili Mumoja,” hakuta kuwa tena kundi moja yenye itakuwa inapendelewa, hii ni jambo kubwa inayo itwa Injili ya  wasio tahiriwa. 

Tungeliuliza kama hiyo ndiyo Habari Njema iliyo hubiriwa na mitume kumi na miwili wa Bwana Yesu, jibu ni hapana, hii ni Habari Njema tafauti ni ile. 

Tuangalie hakikisho ya neno ili. 

4/ Mbele ya yote tujuwe kwa makini kwamba hii Habari njema siyo habari njema yenye Bwana wetu Yesu Kristo alikuwa anahubiri. 

Waroma 15: 8 

“Kwa sababu ninasema ya kwamba Yesu Kristo alikuwa mtumishi wa tohara kwa sababu ya kweli ya Mungu, kusudi ashimamishe ahadi walizopewa baba zetu;” 
Hapa Mutume Paulo anasema ya kwamba Bwana Yesu alikuwa mtumishi wa tohara, mtumishi kwa wayuda tena yeye alikuwa mtumishi kwa sababu ahakikishe na kushimamisha ahadi walizopewa wababa wao. 

Ahadi lilewalilopewa wababa itatimilika wakati watafikia ule ufalme unaokuja wenye utakuwa hapa chini duniani. 

Na mutume Paulo haiko anahubiri juu ya ufalme wa ulimwenguni.  

Yeye anahubiri kwamba wayuda na mataifa wote wanakuwa kwa daraja moja na wote wanapashwa kukaribia Baba Mungu kwa njia ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo ili wawe viungo vya Mwili huu Mumoja, Jengo hii mupya, Kao hii ya Mungu Baba, inayojengwa na Mawe yaliyo hai. 

5/ Tuone sasa habari njema yenye Bwana wetu Yesu alikuwa nayo, tukisoma 

Matayo 10: 5 - 6 

“Hawa kumi na wawili Yesu aliwatuma, akawaagiza akisema: Musiende katika njia ya Mataifa, wala musiingie muji wowote wa wasamaria; Lakini Zaidi kwendeni kwa kondoo wapotevu wa nyumba ya Israeli.” 
Hapa Bwana wetu Yesu Kristo anaagiza mitume wake kumi na wawili wasiende katika njia ya Mataifa lakini waende kwao kondoo wapotevu wa nyumba ya Israeli. 

Bwana wetu Yesu Kristo hakufunuliya mitume wake kwamba wao walikua viungo ya Mwili wenye utajengwa kwa muungano wa wayuda na mataifa. 
Bwana Yesu aliwaambia waende tu kwa taifa la Israeli. 

6/ Tusome sasa kwa kitabu ya Matendo ya mitume 1: 1 - 3, 6 

“Katika kitabu cha kwanza, Teofilo, nilikuandikia mambo yote aliyoanza Yesu kufanya na kufundisha, hata siku ile alipochukuliwa juu nyuma ya kuagizwa kwa Roho Mutakatifu mitume ambao aliwachagua. Na nyuma ya kuteswa kwake aliwatokea, akawaonyesha kwa alama nyingi yakuwa yuko hai, akaonekana nao kwa muda wa siku makumi ine, na kusema nao maneno ya ufalme wa Mungu. … Wakati walipokutanika wakamwuliza, wakisema: Bwana, utarudishia Waisraeli ufalme wao tena wakati huu?” 
Turudi nyuma kidogo kwa nyakati ile ya Pentekoste nafasi mutume Luka alifunguwa kitabu cha Matendo ya mitume na kusema kwamba Bwana Yesu alikuwa pamoja nao muda wa siku makumi ine juu ya kuwafundisha maneno ya ufalme wa Mungu. 

Muda ya siku hii makumi ine, Bwana Yesu alionekana na wale kumi na miwili wakati alipokuwa akiwafundisha. Tunaweza kujiuliza kama mafundisho aliowafundisha ni ile inayosema kwamba wayuda na Mataifa wanakuwa wote viungo vya Mwili mmoja? 
Tujiulize tena eti Bwana Yesu alikuwa anafundisha mitume kumi na wawili kwamba taifa la Israeli haita pata tena ufalme wake? 

Kwamba ufalme huo uliwekwa kando? 

Ama, Bwana Yesu alikuwa akiwafundisha habari aliyowaambia ndani ya kitabo cha Matayo sura 10? 

7/ Tunaweza kutambua kwamba nyuma ya Bwana Yesu kuwa nawo muda ya siku makumi ine akiwaambia maneno mazito ya ufalme wa Mungu, kuna ulizo tunayo pata katika aya yake ya 6, inayotuonesha kwamba: mitume kiisha siku makumi ine ya mafundisho, Bwana Yesu hakuwafunulia kuhusu siri hiyo, sababu alikuwa akiwafundisha juu ya taifa la Israeli. 

Mitume wake walimuuliza: (Matendo ya mitume 1: 6) Wakamwuliza, wakisema: Bwana, utaturudishia Waisraeli ufalme wao tena wakati huu? 

Ingelikuwa Ufalme wao umetiwa kando na kwamba Bwana Yesu angalikuwa anawafundisha kwamba ufalme wao umetiwa kando, munazani kwamba wangemuuliza ulizo la namna ile? 

Wao hawakuwa hata na wazo fulani kujuwa kwamba kwa sasa Baba Mungu iko sasa na kazi ya kujenga  Mwili Mupya ambayo ni jengo lenye litaunganisha na kuweka wayuda na mataifa kwa daraja moja.  

8/ Na inaonekana tena kwamba wao hawakujuwa kitu chochote juu ya maandiko ya 

Waroma 11: 11, 12, 15   

“Basi ninasema: Wamejikwaa waanguke kabisa? Hapana, hata kidogo; lakini kwa sababu ya kuanguka kwao wokovu umefikia Mataifa, ili wao watiwe wivu. 
Basi kama ikiwa kuanguka kwao kumekuwa mali ya dunia, na upungufu wao umekuwa mali ya Mataifa; si Zaidi sana utimilifu wao? 

Kwa sababu kama kutupwa kwao kumeleta upatanisho kwa dunia, kupokewa kwao kutakuwa nini kama si uzima toka wafu?” 
Hapa inaoneshwa ya kuwa kutupwa kwa taifa la wana wa Israeli kumeleta utajiri wa Neema kwa Mataifa, lakini wao hawakufahamu hivyo katika nyakati zile, Wangelifahamu hivyo, wangelikuwa hata na ulizo moja kwake. Wangelifahamu kwamba taifa la Israeli lilitiwa kando. 

9/ Kwa sasa twende kwanza siku kumi nyuma, hapo mutume Petro alikuwa akihubiri hiyo siku ya pentekoste. 

Matendo ya Mitume 2: 22   Yeye alisema ya kwamba: 
“Ninyi wanaume wa Israeli, sikieni maneno haya: Yesu wa Nazareti mtu aliyeoneshwa kwenu na Mungu kwa matendo ya uwezo, maajabu na alama alizofanya Mungu kwa mkono wake kati yenu, kama ninyi wenyewe munavyojua;” 
Alisema ya kwamba nyinyi wanaume wa Israeli, musikie maneno haya. Nikusema kwamba hawakujuwa kitu juu ya neno inayosema kama Israeli ilitiwa kando ya nini? 
Ya Siri iliyo letwa kwa mutume Paulo kwa njia ya ufunuo. 

10/ Muniruhusu niwaulize kwamba Mutume Paulo alijifunza hiyo siri wapi? Kama Yeye hakuijuwa nyuma ya ile siku makumi tano ya mafundisho iliyo fundishwa na Bwana wetu Yesu Kristo, ni fasi gani basi kwenye yeye alifundishwa hiyo Siri nyuma ya siku kumi? 

Hapana hata kidogo, 

Yeye hakuyafahamu na tena Habari Njema ya waliotahiriwa iko tofauti na Habari njema kwao wasiotahiriwa. 

11/ Hivyo sasa turudilie maandiko yetu katika Matendo ya mitume 1: 7. Jibu ya Bwana wetu Yesu Kristo ilikuwa gani? Na ni ile jibu njoo iko ya muhimu sana ndani ya majifunzo yetu.  

Matendo ya mitume 1: 7  

“Basi kama Mungu aliwapa zawadi namna alivyotupa sisi, wakati tulipoamini Bwana Yesu Kristo, mimi ni nani, niweze kuzuiza Mungu?” 
Ni nini Bwana Yesu aliwajibu? Eti aliwaambia kwamba ninyi hamuta pata ufalme wenu ama 

Aliwajibu kwamba ufalme wenu hautakuweko tena? 
Yeye hakuwajibu namna ile. 

Eti tujiulize kama Yeye aliwaambi kwamba nyinyi mumepoteza bahati yenu ama kwamba matabiri ya Agano la kale yamekomeshwa na kwamba Mungu ataanza kutumika na watu wote kwa namna moja, ama kwamba watu wote wayuda na mataifa wote watakuwa na samani moja na daraja namna sawa? 

Hapana hata kidogo, yeye hakufanya hivyo. 

Yeye hakuwafundisha Waroma 11

12/ Bwana na Mwokozi wetu hakuwaambia kama mawazo yao yalikuwa inje ya mustari; ama mawazo yao yalikuwa ya upotevu sababu Yeye alikuwa anazungumuza juu ya ufalme. 

Yeye aliwaambia tu kwamba siyo kwao kuuliza maulizo juu ya nyakati. 
Kwa kweli hapa, walikuwa wanauliza Bwana na Mwokozi wetu, kwamba kurudi kwake kutakuwa lini, ama nyakati gani yeye atarudi? Na ufalme utaanzishwa wakati gani? 
Hiyo iliambatana na Matayo 24: 36. 

Matayo 24: 36 

“Lakini hakuna mutu anayejuwa habari za siku ile na saa ile, hata malaika walio mbinguni wala Mwana, ila Baba peke yake.” 
Kwa kweli hakuna mutu anaye fahamu saa ama siku ya kuja kwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 

Wanafunzi walikuwa na ulizo juu ya iyo, lakini aliwajibu kwamba hawawezi kuifahamu. 
Aliwaambia kwamba wanaweza kuwa na ufahamu juu ya ufalme wa Mungu, lakini hapana juu ya kuja na kurudi kwa Bwana wetu Yesu Kristo, na hii siyo Habari yenye Mutume Paulo alikuwa anahubiri. 

13/ Sasa tuchunguze kidogo juu ya hii jambo, tujiulize sababu gani wanafunzi walikuwa wanazungumuzia juu ya Ufalme wa Mungu? 

Sababu gani walikuwa na maulizo mazito juu ya hiyo ufalme? 

Kwa kweli tukiangalia mitume waliuliza maulizo mengi sana, sasa sababu gani Bwana 

Yesu anatuzungumuzia juu ya hii ulizo moja tu?  

Kuna kweli sababu iliyo sababisha hiyo. 

Kiisha mafundisho aliyofanya Bwana Yesu Kwa muda wa siku makumi ine, wanafunzi walimuuliza juu ya ufalme wa Mungu, sababu gani? 

Kwa sababu kweli kweli Bwana Yesu alikuwa anawafundisha juu ya ufalme wa Mungu. 
Bwana Yesu angeliwazungumuzia juu ya Siri ya Habari njema, muda wa siku zile makumi ine, nina uhakika kama wamitume hawangeli kosa kumuuliza ulizo hata moja juu ya hiyo Siri. 

Kama unaweza kuketi hata tu kwa muda wa siku mbili ukifwata kwa makini mutu anaye kuzungumuzia juu ya neno fulani, kichwa chako kitajaa na hiyo maneno na hautakosa kuuliza hata swali moja inayoambatana na hayo maneno. 

Nikusema vichwa vya mitume vilikuwa vimejaa na maneno inayo elekeya mambo ya ufalme wa Mungu. 

Yobu 1: 8 - 10  

“Bwana akamwambia shetani: Umeangalia mutumishi wangu Yobu? 
Maana hakuna mmoja kama yeye duniani, mutu mkamilifu na wa haki, mwenye kuogopa Mungu na kuepukana na uovu. Shetani akajibu Bwana, akisema: Yobu anaogopa Mungu bure? Wewe hukumzunguka yeye na nyumba, na vyote alivyo navyo, kwa boma pande zote? Umebariki kazi ya mikono yake, na mali yake imeongezeka inchini.” 
Hapa Shetani iko anazungumuza na Mungu juu ya Yobu. Wewe hukumzunguka yeye na nyumba yake, na vyote alivyo navyo, kwa boma la ukingo pande zote? 

Munafahamu kuna zehebu moja ya watu waliopenda ukristo Safi, wawe na ukristo usiokuwa na dowa ama uchafu. 

Hawa watu waliopenda kuishi ukristo usiokuwa na dowa ama uchafu wowote walikuwa wakifasiriya kwamba hiyo boma ya ukingo iliyozunguka Yobu na mali yake yote ilikuwa boma ya urefu wa kupanda juu sana hata ma pepo wa ibilisi wakuu hawakuweza kuruka hiyo boma na ilikuwa na upana wa zaidi sana hata ma pepo wa ibilisi wembamba sana na wadogo hawakuweza kujiingiza kama shindano ndani ya boma hiyo mpaka Mungu yeye mwenyewe awape ruhusa. Ni hii walifundisha watu. 

14/ Twende sasa kwa maandiko ya mutume Petro 

Kwa kweli Bwana Yesu hakumufunuliya juu ya SIRI hiyo. 

Lakini Bwana Yesu alifanya hivyo kwa mutume Paulo

Paulo alikuwa na Habari Njema tofauti. 

Sasa, Habari njema gani mutume Petro alihubiri siku ya pentekoste? 

Matendo ya Mitume 2: 39 

“Kwa sababu ahadi hii ni kwa ajili yenu, na watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu,” 
Hapa, tunaona kwamba wakati mutume Petro alikuwa anahubiri, alisema, kwa sababu ahadi hii ni kwenu na kwa watoto wenu, ni kwenu ninyi wayuda, na kwa watoto wa wayuda na kwa  watu wote walio mbali. 

Hakupenda kuzungumuza juu ya wayuda wengine wenye wiko katika inchi jirani, lakini alimaanisha kwa kweli waziwazi kama ni kwa sisi, sawa vile tunavyosoma katika kitabu cha Waefeso sura mbili, Waefeso 2 

“Nanyi mulikuwa wafu kwa sababu ya makosa yenu na zambi zenu,” 
Tunaona hapo watu wenye walikuwa sawa wakuzarauliwa, watu waliokuwa mbali. 
Katika Waefeso 2, Mutume Paulo anatufunuliya kwamba, wakati hiyo kiambaza cha uadui na matengano kilikuwa bado kingaliko, Mataifa mengine walikuwa sawa wakiwa mbali kwa muda wa siku zile. 

Sasa Mutume Petro wakati alipokuwa akihubiri akijazwa na Roho Mutakatifu alipata ufahamu juu ya hiyo ukuta na alizungumuza juu ya hiyo ukuta kama sawa bado ilikuwa ingaliko. 

15/ Mutume Petro hakukua anatambuwa kwamba hiyo ukuta imekwisha ku bomolewa na kutiwa mbali. 

Tusome Matendo ya Mitume 2: 39 

“Kwa sababu ahadi hii ni kwa ajili yenu, na watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu,” 
Unatambuwa hapa kama Mutume Petro anatumikisha nyakati za sasa akisema: “na kwa wote walio mbali”, wakati alipokuwa akisema yeye aliwaona kama wao bado wangali mbali na ijapokuwa wameisha kuwa karibu. 

Mutume Petro hakufahamu kama wao wameisha kuwa karibu, angelijuwa vile, angeliizungumuzia hiyo siku ya Pentekoste.

Nikusema mutume Petro hakuwa na habari njema sawa na hiyo iliyosemwa na mutume Paulo. 

16/ Matendo ya Mitume 10:28  

“Akawaambia: Nanyi munajuwa ya kuwa si halali kwa mutu wa Yuda kupatana na kabila lingine, wala kumkwendea, lakini Mungu amenionyesha nisiite mutu yeyote mnyonge wala mchafu.” 
Hapa tunaona Kornelio, mutu wa mataifa na kwake njoo Mungu alituma mtume Petro. 
Na kama mutume Petro alikuwa akiheshimia agizo iliyosema Nendeni ulimwenguni kwote, tunaona kwamba hainge faa tena kwa mutume Petro kungoja kwanza Mungu amutume tena kwa Kornelio, hivi ingelifaa Kornelio njo atumwe kwa mutume Petro. 
Na sasa tutazame namna mutume Petro anavyosema kwamba:

Nanyi munajuwa ya kuwa si halali kwa mutu wa Yuda kupatana na kabila lingine, wala kumkwendea, lakini Mungu amenionyesha nisiite mutu yeyote mnyonge wala mchafu. 
Hapo, mutume Petro, anajionyesha kwa hali yakuwa kama yeye ni mutu kweli aliye muyuda. 

Hakufahamu maneno inayosemwa katika Waroma 10: 12  
“Kwa maana hapana tofauti katikati ya Wayuda na Wayunani, maana yeye yule ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa watu wote ambao wanamwitia:” 

Mutume Petro, kwa kusema vile alikuwa anasema kama muyuda. Hakufahamu Siri ya siku za leo. 

17/ Kitu cha muhimu kujuwa  

Matendo ya mitume 10: 28 
Tujiuluze kama hii jambo ilikuwa nyuma ya mutume Petro kupata maonyo, na kiisha hiyo kuendelea kujitambuwa tu kama muyuda, hii ni neno kubwa linalopaswa watu kufahamu. 

18/ Twende sasa katika Waefeso 3: 1 

“Kwa sababu hii mimi Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu kwa ajili yenu ninyi Mataifa,” 
Mutume Paulo iko anatuambia kwamba ni kwa sababu ya SIRI hii Mupya njoo maana iko anajijulisha kwamba yeye ni mfungwa kwa ajili yetu sisi Mataifa. 

Yeye ni mfungwa wa Kristo Yesu kwa Mataifa, watu wasiojuwa Mungu. 

19/ Mutume Paulo anasema hapo kwamba yeye haiko mufungwa juu ya kosa lolote la binafsi, SIRI hii Mupya yenye Mwenyezi Mungu alimufunulia njo yenye watu wanachukia sana. 

Watu walichukia Habari Njema hii na Mutume Paulo alibaki tu mwaminifu kwa Habari Njema hii. 

20/ Pima kuwaza na kuchunguza neno hili: Mutume Paulo kwa kweli alitiwa katika gereza ya chini, ndani ya chimo katika gereza hizo za muji wa Roma zilizokuwa chini ya udongo na Mutume Paulo alitiwa huko kwa sababu alikuwa na ile hamu kubwa ya kutufahamisha SIRI HII KUBWA YA MUNGU katika utunzaji huu wa siku za leo na kwa kweli jambo hili lingelipashwa kuburudisha moyo wako. 

21/ Hakuna kitu kingeliweza kuwasha hasira na kasirani ya wayuda, taifa la kidini ya wakati ule, sawa Hahari njema yenye mutume Paulo alikuwa anatosha kwa mudomo wake, ni hii ilikuwa inaleta hasira nyingi na kasirani sababu mutume Paulo alikuwa anahubiri kwamba Mungu akuendelea kuishi tena ndani ya hekalu zilizojengwa na mikono ya watu na Mungu hakuendelea kutumika na Israeli kama taifa pendelevu kwa upekee kwa sababu Mungu aliwageukia vilevile Mataifa mengine za ulimwengu na kumupa ama kumuletea wokovu yeyote yule atakaye amini. Tuhakikishe maneno haya kwa kusoma kitabu ya Matendo ya mitume 22: 22 - 24   

“Walimusikiliza mpaka neno hili, wakapaza sauti zao, wakisema: Mwondoshe huyu katika inchi kwa maana haifai aishi. 
Walipokuwa wakipiga kelele na kuondoa mavazi yao na kutupa mavumbi juu, 
Yule mkubwa aliamuru aletwe ndani ya nyumba kubwa, akisema aulizwe kwa mapigo ya fimbo, apate kujuwa kwa maana gani walipiga kelele namna hii juu yake.”    
Hapa tunaona namna gani wandugu wa damu, wandugu wa kabila moja na mutume Paulo, walikuwa wakilalamika kwa sauti kubwa sababu mutume Paulo alipokuwa akihubiri,  wao walimusikiliza na kungojea tu saa atatamka neno Mataifa na ni hapo walipaza sauti zao, wakisema: Mwondoshe huyu mutu wa namna hii katika inchi, sababu yeye hastaili kuishi.

Walipiga kelele na kuondosha mavazi yao na kutupa mavumbi juu, wakatia mutume Paulo gerezani wakamutia katika kifungo cha chini ya udongo. 

Ni kwa sababu ya mahubiri ya maneno yale aliyo yahubiri mbele ya mulango wa hekalu, maneno yaliyo  kuwa magumu na nguvu kwao na kuvuruga akili yao, maneno yale  yalichanganyikisha  ufahamu wa wale watu wa dini, kwa sababu ya hiyo ushuhuda njo mutume Paulo alitiwa gerezani.  

22/ Ni hii njo inahakikisha sababu gani mutume Paulo alikuwa mara na mara akileta ushuhuda na hakikisho ya huduma aliyopewa. Ni kwa sababu ya hiyo njo mara kwa mara mutume Paulo alikuwa anatiya mukazo wa kusema kwamba yeye ni mutume wa Bwana Yesu Kristo, siyo kwa mapenzi ya mutu lakini kwa Yesu Kristo pekee. 

Watu wamoja wanasema kwamba mutume Paulo angepashwa tu kusema hivyo sababu mutume Matiasi vilevile alikuwa anapenda kukamata nafasi ya Yuda Eskariote na ni kwa hiyo walizani kwamba mutume Paulo vilevile alikuwa anapenda apate hiyo nafasi ya Yuda, lakini maandiko matakatifu hayaleti mawazo ama neno lolote juu ya misemwa hiyo, ni umbalimbali kweli na yale Maandiko Matakatifu yanasema. 

Mutume Paulo alihakikisha huduma yake sababu yeye alikuwa akihubiri Habari Njema mupya, Habari Njema tofauti, Habari Njema ya Siri aliyo ipata kwa ufunuo yeye pekee akiioneshwa na Mungu.  

23/ Tufahamu ya kuwa namna ya kuishi gerezani kwa mutume Paulo inakuwa inaambatanishwa sawa sawa na vile Yosefu vilevile alivyokuwa gerezani. 
Tusome 

Mwanzo 45: 4, 5 

“Yosefu akawaambia ndugu zake: Karibieni kwangu, ninawaomba ninyi. Wakakaribia. Akasema: Mimi ni Yosefu ndugu yenu ambaye mulimwuza kwenda kwa Misri. 
Basi sasa musihuzunishwe, wala isiwe hasira kwa macho yenu ya kwamba muliniuza hapa; kwa sababu Mungu alinituma mbele yenu kwa kuponyesha maisha ya watu.” 
Kwa namna nyingine nikusema kwamba ilikuwa mapenzi ya Mungu nikuwe gerezani, ingelinipasa niuzishwe, kulikuwa kusudi juu ya hayo yote. 
Kuponyesha maisha ya vizazi. 

Mutume Paulo anasema sioni kwangu kuwa hasara mimi kupatikana gerezani. Ni mapenzi ya Mwenyezi Mungu mimi niwe hapo. 

Najuwa kwamba Habari njema hii ya Siri inakuwa na sababu yake na mimi ni mufungwa kwa sababu ya Habari Njema hii na Mungu aliona kwamba ni vema mimi nipatikane gerezani kwa sababu ya Habari Njema hii ya Siri. 

24/ Tufahamu kwamba mutume Paulo hakusema kwamba mimi ni mufungwa wa mufalme NERO, ama mufungwa wa taifa la Roma, lakini mufungwa wa Kristo Yesu. 

25/ Vifungo vya nyakati za hapo kale vilikuwa tofauti na ma gereza za nyakati ya sasa. 
Kwa nyakati za kale vyumba vya vifungu havikukuwa na vifaa yoyote kwa ajili ya mfungwa, kulikuwa tu taa ndogo sana, hewa haikuwa bora, chakula kilikuwa kidogo sana.

Mufungwa alikuwa anatiwa munyororo akifungwa kwa mwili wa askari moja wa Roma saa makumi mbili na ine kwa siku. 

Gereza ya leo ni umbalimbali kweli na hiyo mutume Paulo alikuwa ndani. 
Mutume Paulo alivumilia shida hii yote sababu yeye alikuwa na Habari njema ya Siri yenye alipashwa kuhubiri na kutangaza. 

26/ Wakati mutume Paulo alikuwa akisema kwamba yeye ni mufungwa wa Kristo Yesu, alikuwa na uhakika na hakikisho kwamba falme zote za ulimwenguni hazina mamlaka yoyote juu yake isipokuwa Mungu yeye mwenyewe kwa mapenzi yake aruhusu neno lolote, 

Tukumbuke historia ya Yobu. 

Mungu alitiya mupaka. 

Shetani hangaliweza kufanyia Yobu chochote kama Mungu hangeliliruhusu. 
Mpaka vile Mungu aliruhusu shetani aguse vifaa vya Yobu bila kunyoosha mukono wake kwa umutu wa Yobu.

Na mutume Paulo vilevile iko anasema maneno yale vilevile. 

Mimi siko mufungwa wa mufalme Nero. 

Mimi siko mufungwa wa taifa la waroma. 

Mimi niko mufungwa wa Yesu Kristo, ni yeye njo aliona kwamba ni vema nipatikane hapo. 

27/ Inawezekana ndugu yangu kwamba wewe uko unapitiya majaribu kazaa. 
Inawezekana Mwenyezi Mungu aliruhusu boma lako la ukingo ibomolewe sawa vile alivyofanya kwa Yobu na kwa mutume Paulo. 

Ninakuhakikishia kwamba Mwenyezi Mungu atakutendea na kukushimamisha sawa vile alivyotendea Yobu, sawa tu vile alivyo shindia mutume Paulo wakati wote walipokuwa wakipitia saa hizo za majaribu. 

28/ Mutume Paulo alionesha na kuzungumuzia juu ya SIRI hii katika vitabu vingine, lakini umbalimbali na hii tunayoipata katika kitabu cha waefeso, hapo tunaona ya kwamba Ukweli wa Siri hii unaonyeshwa kwa ukubwa na upana na uzito wake. 
Hapo Ukweli wa Siri hii unaonyeshwa wazi sana tofauti na nafasi kwenye inasemwa kwa jumla tu. 

Katika kitabu cha Waefeso ni hapo tunaona na kupata kujuwa sana Siri hii kwa Umuhimu wake wote, siyo tu mimi ninaeona hivyo, nakumbuka  kama alivyosema vilevile mutumushi wa Mungu Pastori Talbot wa kanisa la Fundamental church pa Los Angeles. 

29/ Katika haya ya 5 mpaka 9, mutume Paulo ana tuonesha wazi wazi na bila fumbo lolote kwamba watu wa vizazi vilivyo pita hawakufahamu hata neno moja juu ya ufunuo wa Siri hii. 

Maneno ya mafundisho ya manabii wa Agano la Kale kuhusu Kusulubishwa kwa Kristo na Utukufu unaofwata kusulubishwa kwake ni hiyo Utawala wa Utukufu wa Kristo. 
Tukijifunza kwa makini sana maandiko ya Agano la kale inatufunuliya ya kwamba Utawala wa miaka elfu wa Kristo hapa duniani unakuja nyuma ya kusulubiwa kwake musalabani. 

30/ Tuendelee na majifunzo yetu ya kutangaza SIRI hii kuu ya Mungu. 
Mutume anatuonesha nafasi yenye Mataifa wanapata katika huduma na utunzaji huu mupya. 

Waefeso 3: 6    

“ya kwamba Mataifa ni wariti pamoja nasi wa uriti mmoja, na wa mwili mmoja, na washiriki pamoja nasi wa ahadi hii katika Kristo Yesu kwa ajili ya Habari Njema.” 
Tunapashwa kweli kufahamu katika akili na mioyo yetu kwamba Baraka hii ni mbalimbali na mibaraka nyingine iliyo patikane wakati wa mwisho ya historia ya Agano la Kale wakati wa ile utawala wa miaka elfu moja wakati kutakuwa uwingi wa mataifa mengine yaliyo okolewa na wao vilevile watabarikiwa na mibaraka ya hapa chini ulimwenguni na hakuna siri katika Agano la Kale linalosema juu ya utabiri wa utukufu huo wenye mataifa ile iliyo okoka itapata. Na hii haiko sawa sawa na Mwili huo Mumoja unaopatikana katika kitabu cha Waefeso.  

Tuchunguze nusu ya maandiko ya Agano la Kale ili tufahamu maneno tunayoyasema. 

31/ Isaya 62: 2 

“Na mataifa wataona haki yako, na wafalme wote wataona utukufu wako; na utaitwa kwa jina jipya, litakalotajwa na kinywa cha Bwana.” 

32/ Isaya 11: 10 

“Na itakuwa katika siku ile, shina la Yese linalosimama kuwa kama bendera kwa makabila ya watu, kwake mataifa watatafuta; na pahali pake pa kupumzika patakuwa na utukufu.” 

33/ Isaya 66: 12  

“Maana Bwana anasema hivi: Tazama, nitamnyoshea salama kama mto, na utukufu wa mataifa kama maji yanayofurika; na mutanyonya na mutabebwa kwa nyonga; na mutabembelezwa juu ya magoti.” 

34/ Malaki 1: 11 

“Kwa maana tangu kucha kwa juwa hata kushuka kwake jina langu ni kubwa katikati ya Mataifa, na kwa kila pahali wanatolea uvumba kwa jina langu, na toleo safi; kwa maana jina langu ni kubwa katikati ya Mataifa; Bwana wa majeshi anasema.” 
Kwa kuchunguza kila moja ya ma haya hizo tunatoka kuzisoma, tunatambua ya kwamba mibaraka inayosemwa hapo ni mibaraka yenye ina aina ya ulimwengu. 
Lakini Mibaraka yenye tunasoma katika Waefeso 3: 6 ni mibaraka tofauti sababu hayo ni mibaraka ya Mbinguni. 

35/ Sasa ndani ya kitabu cha Waefeso 3: 9 tunaona ombi na aliko la siku za leo hapo tunaona mawazo ya utukufu. 

Hapa tunayatofautisha na nyingine na kuonesha watu wote na kuonesha ahadi hii na kuangazia watu wote wajuwe habari za madaraka ya siri iliyofichwa tangu zamani ndani ya Mungu aliyeumba vitu vyote. 

Tunapashwa kafanya yote iwezekanavyo ili watu wote waangaziwe na wajuwe SiRi hii. 

AMEN

N°Ref: 01/24/1960 / 211 - WHY WAS PAUL IN PRISON / 2020