Monday, January 31, 2022

SHETANI ANAJISUMBUA NA KAZI BURE / THE DEVIL’S HOPELESS JOB

Photo by B Smith from the kitchen door




SHETANI ANAJISUMBUA NA KAZI BURE 

THE DEVIL’S HOPELESS JOB

July 4, 1965 

Pastor Henry F. Kulp




 

Waroma 8: 28 - 34  

“Na tunajua maneno yote yanafanya kazi pamoja kuwapatia mema wale wanaopenda Mungu, kwa wale walioitwa kwa kusudi lake. 

Kwa sababu wale ambao aliwajua tangu zamani, aliwachagua tangu zamani wafananishwe na sura ya Mwana wake, ili awe Mzaliwa wa kwanza katikati ya ndugu wengi. 

Na wale ambao aliwachagua tangu zamani, akawaita vilevile; na wale ambao aliwaita, akawahesabia haki: na wale ambao aliwahesabia haki, akawatukuza vilevile. 

Basi tutasema nini juu ya maneno haya? 

Kama Mungu akiwa upande wetu, ni nani aliye juu yetu? 

Yeye asiyeachilia Mwana wake, lakini alimtoa kwa ajili yetu yote, namna gani atakosa kutuletea vitu vyote pamoja naye? 

Ni nani atakayeshitaki wachaguliwa wa Mungu? Mungu ambaye anawahesabia haki; 

Ni nani anayehukumu? Ndiye Kristo aliyekufa, ndiyo, zaidi amefufuka, naye yuko kwa mkono wa kuume wa Mungu, tena ndiye anayetuombea.” 

         Katika sehemu hii ya Maandiko tunafika kwa nafasi yenye Mtume Paulo anauliza: Basi tutasema nini juu ya maneno haya? 

Na hapo anatutolea maelekezo ya mambo saba. 

Kama Mungu akiwa upande wetu, ni nani aliye juu yetu? 

Baadaye anasema: 

Yeye asiyeachilia Mwana wake, lakini alimtoa kwa ajili yetu yote, namna gani atakosa kutuletea vitu vyote pamoja naye?  

Neno tuliyopata kwa mwisho wa mafundisho yetu ya juma jana ilisemaka ifwatavyo: 

Yeye asiyeachilia Mwana wake, lakini alimtoa kwa ajili yetu yote. 

Mungu Baba alimtoa Yesu Kristo. 

Alimtoa kwa nguvu ya giza, nguvu ya Shetani, na hapo alimufanya kuwa zambi kwa ajili yetu. 

Mara tena yatupasa kufahamu kawaida ya mafundisho haya inayosema Mungu Baba kamtoa Mungu Mwana kwa ajili yetu sote.

Twende kusoma ndani ya Wagalatia 2: 20 inayosema hivi:

“Nimesulubiwa pamoja na Kristo, lakini ni hai; wala si mimi, lakini Kristo ni hai ndani yangu; na uzima nilio nao sasa katika mwili, ni uzima wa Imani iliyo ya Mwana wa Mungu ambaye alinipenda akajitoa nafsi yake kwa ajili yangu.” 

         Neno “kwa ajili ya” ingelipashwa kuwa pale na tungesoma: 

Aliyejitoa nafsi yake Yeye mwenyewe kwa ajili yangu. 

Hii misemwa ni sawasawa na yale tunayoyapata katika musingi wa maneno tunayo katika tafsiri ya neno “kutoa kwa ajili ya” tunayopata katika Waraka wa 

Waroma 8: 32: Mungu alimutoa kwa ajili ya. 

Aliingia kwa shamba la Gestemani, kwa shabaa ya mapenzi yake yote. 

Yeye alitamka mara tatu: Baba, Baba, Baba, mapenzi yako yafanyike. 

Kiisha akatoka na kujitowa mwenyewe kwa mikono ya watesi wake. 

Alifanya hivyo kwa ajili yetu. 

Hakuna hata mtu mmoja anayeweza kutafsiri, kama ipasavyo, mateso na uchungu wa kuzidi wenye Mwana wa Mungu alioupata katika mapito yale ya uchungu, na unyonge na mateso makali. 

Ilikuwa jambo la mushangao na kutisha sana wakati alipojitoa Mwenyewe kwa ajili yako na mimi. 


1/ Tusome ndani ya waraka wa Waebrania 9: 14   

“basi si zaidi Damu ya Kristo, ndiye kwa Roho ya milele, alijitoa mwenyewe kwa Mungu, kuwa zabihu isiyo na alama, itasafisha zamiri zenu na matendo ya kufa, mupate kutumikia Mungu aliye hai?” 

         Damu inatajwa mara kumi na miwili katika Waraka huu. 

Inatuambia kuhusu kazi na umuhimu wa Damu na mambo gani Damu ilitimiza. 

Bila kumwanga Damu, hakuna ondoleo ya zambi.  

Kwa siku za leo, watu wanajaribu kuweka kando Damu ya Kristo, lakini hakuna yeyote atakayeweza kusadiki mafundisho ya Biblia na kuhepuka Damu ya Kristo. 

Damu ndiyo musingi wa wokovu wetu, na yakupasa kweli kweli kuamini Damu ile. 


2/ Sitaweza kusita kutangaza imara kwamba Wokovu ndiyo kazi ya muhimu na ya maalum sana ya Mwenyezi Mungu. 

Kama tunavyo fahamu, hakuna hata kazi moja katika uumbaji iliyo kuwa nzito na kuwa bei kali mbele ya Mungu. 

Hata hapa sasa, Mwenyezi Mungu anaweza kuamuwa kuumba ulimwengu ungine mupya na hiyo siyo shida kwake. 

Bali kuna jambo moja iliyofanya Mungu kuwa maskini, ni wakati Mungu Baba alimtoa Mungu Mwana aliyejitoa mwenyewe.

 

3/ Tuchunguze sasa yanayosemwa katika sura hii, tuendeleapo usomi: 

 Ndiye kwa Roho ya milele, alijitoa mwenyewe kwa Mungu 

Hili neno tunalipata tena kwa waraka wa Waroma 8: 32, pia ndani ya Wagalatia 2: 20. 

Tungelipashwa kusoma namna hii: 

Ndiye kwa Roho ya milele, alijitoa mwenyewe bila kilema wala alama. 

Mutafsiri alisahau neno “kwa ajili ya” 

Fundisho tunalopata hapa ni kwamba, kwa kujitoa Yeye mwenyewe kama Sadaka, Bwana wetu Yesu alikuwa na haja ya musaada wa Roho Mtakatifu; na hapo hapo tunamuona vile vile Mungu Baba, Mungu Mwana na Mungu Roho Mtakatifu akitumika pamoja ili Yesu Kristo atolewe kwa ajili ya zambi zetu.

  

4/ Waroma 8: 32  

“Yeye asiyeachilia Mwana wake, lakini alimtoa kwa ajili yetu yote, namna gani atakosa kutuletea vitu vyote pamoja naye?” 

         Tuangalie kwa makini sehemu ya pili ya aya hii: 

Namna gani atakosa kutuletea vitu vyote pamoja naye?   

Wakati Mungu Baba alimtoa Mungu Mwana wake kwa ajili yetu, Yeye alitupatia yote aliyokuwa nayo wakati alimutoa Mwana wake kwa ajili yetu. 

Katika utafuti wangu kuhusu china ya neno, niligunduwa kwamba msemwa: “kuletea vitu vyote” inatafsiriwa na neno: kutoa bila shaka ama shurti, ama bila malipo ama kutarajia kitu fulani baadaye. 

Yatupasa kufahamu haya mbele ya mambo yeyote. 

Mwenyezi Mungu hauzishi kitu. 

Mwenyezi Mungu si mwenye kutarajia masikilizano ya bei ya kitu fulani na wanadamu ili wapokee kitu toka kwake. 

Mwenyezi Mungu ni mwenye kututolea akitukabizi vyote. 

Mwenyezi Mungu yuko na zawadi kwa ulimwengu. 

Tafsiri maalum yenye ninaweza kuwa nayo kwa msemwa “kuletea vitu vyote” ni “kutoa kwa kukabizi yote bila mashito yoyote”. 

Tukirudi nyuma kidogo katika historia ya Inchi yetu, wakati Serkali iligawanyia watu viwanja kwa bure, shurti moja lenye kila aliyepata udongo alilopashwa kufanya, ni kwenda tu kwa udongo aliyopewa kushurulika nalo na kulimiliki na kulifanya kuwa mali yako binafsi.  

Ni hiyo tu ilimupasa kufanya, hakukulazimishwa hata malipo fulani, hakukukuwa hata mabishano, hakukukuwa kamba yenye iliyokuwa ikifungwa kwa zawadi ile, jambo lilikuwa tu la toleo ya zawadi ya sehemu ya ardhi bila malipo toka kwa Serkali.  

Hii ndiyo aina ya misemwa inayotumiwa hapa: 

Kuletea vitu vyote. 

Mwenyezi Mungu alitutolea bila malipo zawadi kubwa na yote aliyokuwa nayo wakati alipotutolea Mwana wake. 

Kwa sababu hiyo imeandikwa: 

Mambo yote ni yetu.

Nikifahamu kwamba Mwokozi Yesu Kristo ni wangu, mimi ninahaki ya kusema hivyo, ninaweza kusema kwa urahisi wote kwamba: Muumba wa ulimwengu wote, Yeye ni wangu. 

Yeye ni mali yangu, na vilevile wapashwa kufahamu kwamba wewe vilevile ni mali yake.  

Wakati Mwenyezi Mungu alitutolea Bwana Yesu Kristo, hapo alitupatia zawadi bila malipo ya ulimwengu wote kwa wale wenye kumuamini Bwana Yesu Kristo. 

Jambo hili ni la muhimu sana, unapashwa kumuamini Yesu Kristo. 


5/ Kuna hadisi lenye napenda kuwahadisia: 

Tayari mumekwisha kulisikia hapo mbele, lakini nazani kwamba haitakuwa mauzi kwenu kama ninawaadisia mara tena.   

Ni hadisi ya mtu moja aliyekuwa na mali mingi sana. 

Mke wake alifariki na akamuachia mtoto kijana mwanamume. 

Mtoto yule ndiye alikuwa yote kwa mtu yule. 

Na yeye aliweka kijakazi mwenye atakuwa akihusika na kulea mtoto huyo na kushurulika na haja zote za yule mtoto, na kijana huyu aligeuka kuwa sawa mtoto wa huu kijakazi, na kwa kweli ni hivyo tu njo ingepashwa kutukia. 

Huyu mtoto kijana mwanamume alikomaa na akafikisha umri wa miaka makumi mawili kiisha kwa gafla, akafariki. 

Mtu yule mutajiri akavunjika moyo sana, roho yake ikaumizwa sana kupita kiasi. 

Akajikuta kwamba dunia haifai kitu tena kwake na kwa kweli yeye hakugawa tena na kutoweka. 

Hakuna mtu aliyefahamu maelekezo gani iliyopangwa kuhusu hazina ya mtu huyu. 

Walitafuta huku na kule wakiangalia kila kartasi waliokuta, lakini hawakupata agano la mapenzi ya mwisho ya aliyefariki, hata kufika kiwango cha Serkali kushurulika na mambo haya, na kuchukuwa mali yote sababu hakukukuweko murizi, ama habari kuusu maandiko ya mapenzi ya mwisho ya marehemu. 

Ushuru ulifaanyika, vifaa vyote vya nyumbani hata na vitu vyote vya samani, vyote viliwekwa kwa bei ili kuuzishwa. 

Huyu kijakazi mama mlezi wa huyo kijana, naye alifika hapo, na kushimama wima kwa pembe moja la ukuta, naye hakuwa na pesa ila tu kiwango ndogo sana, yeye hangaliweza kujiuzia vitu vile vya samani, kwa hivyo, kwa ukuta, kulikuwa kungali picha ya kijana huyo na mecho ya kijakazi huyo ilikuwa tu ikielekea kwa picha ile aliyotamani na kuhitaji kwa moyo wake wote. 

Picha hiyo ilimufanana kweli kijana huyo marehemu aliyemupenda kwa moyo wake wote. 

Na ikafika wakati ya kuuzisha picha hiyo, hakuna hata mwenye alishurulika nayo. 

Mama mlezi huyo akanunua picha hiyo kwa bei ya chini mno, senti kama ngapi. 

Na alibeba picha hiyo nyumbani kwake. 

Akaipanguza na angalisho yote kwa saa za kutosha na baadaye akaiweka kwenye ukuta na hapo ikafanya miaka mengi. 

Na siku moja wakati alipokusudia kufungua kada ya nyuma, gafula, vikartasi kazaa vikaanguka chini, na kweli kwa mecho yake, vikartasi vile vilionesha sura ya kuwa vyenye mafaa na umuhimu sana. 

Baadaye, akakusudia kubeba vikartasi hivyo kwa Mwanasheria. 

Huyo Mwanasheria akamwambia, mwanamke, kwa sasa mana imekuangukia toka mbinguni na imeanguka kwa miguu yako, sababu huyo bwana marehemu mutajiri aliacha urizi wa mali yake yote kwa mtu ambaye alimpenda sana mtoto wake, hata kufika kiwango cha kununua hii picha iliyomfanana sana mtoto wake mwanaume. 

Yeye aliachia huyo mtu azina na mali yake yote. 

Mwenyezi Mungu anakutolea VYOTE kama wewe ukimupenda Mwana wake. 

Anakupatia vyote bila malipo yeyote, kama ZAWADI BILA MALIPO.


6/ Waroma 8: 33 – 34 

“Ni nani atakayeshitaki wachaguliwa wa Mungu? Mungu ambaye anawahesabia haki; 

Ni nani anayehukumu? Ndiye Kristo aliyekufa, ndiyo, zaidi amefufuka, naye yuko kwa mkono wa kuume wa Mungu, tena ndiye anayetuombea.” 

     Jambo muhimu la kutiya mkazo ni, kukumbuka neno lililokuwa kwa mwanzo wa Waraka huu wa Waroma sura ya nane, mara tena ni neno lilelile linalotumikishwa hapa. 

Kwa aya ya kwanza tunasoma:  

“Sasa, basi hakuna hukumu ya azabu juu yao walio katika Yesu Kristo, wasiotembea kufuata maneno ya mwili, lakini kufuata maneno ya Roho.” 

Na hapa kwa aya ya 33, tunapata hakikisho ya neno lile kwa sababu anatuambia kwamba, usipo amini, wewe wajiweka mwenyewe kwa nafasi ya hukumu. 

Nina swali la kuwauliza: 

Ni nani atakaye hukumu sisi? 

Ama ni nani kweli anayeweza kutuhukumu? 

Kama ni Mungu anayetuhesabia haki, ni nani basi anayeweza kujitia kwa nafasi ya kutuhukumu? 

Mungu ni muhukumu wa wote, 

Mungu ndiye Mahakama kuu. 

Wakati Mahakama kuu inaleta hukumu ya jambo lako, jambo lile limekomeshwa. 

Tayari Mahakama kuu imekwisha kutatua jambo lako, na Mahakama kuu ni Mungu na ni Yeye aliyesema: 

Ni Mungu ndiye anayehesabia haki. 

Kwa kumaanisha kwamba, anakukomboa toka migogoro yote, kukuweka huru toka migogoro yote, na kama Muhukumu anakuweka huru, ni nani yule atakayekuhukumu tena? Ni nani atakaye hukumu sisi? 


7/ Tuchunguze kwanza aya hii ya ajabu: 

Matendo 13: 39   

“na kwa yeye kila mtu anayeamini amekwisha kuhesabiwa haki katika maneno yote asiyoweza kuhesabiwa haki kwa torati ya Musa.” 

         Na kwa Yeye, Yeye ni KRISTO, kwa yeye kila anayeamini. 

Hii haimaanishi wale watu wanaozania kujiweka wenyewe kuwa wenye utawa kwa matendo yao wenyewe. 

Haimaanishi kuwa mushirika wa kanisa fulani, bali kuamini, kila mtu anayeamini. 

Ni pale twapashwa kuweka msingi wetu, hakuna jambo la kukadirisha. 

Kama ukileta swali kwa watu kumi, ukiwauliza kama tiyari wao ni wakristo, kenda juu ya kumi watakujibu kwamba: “Wako wanajikaza kutenda mema kwa kadiri wanavyoweza.” 

Mwenyezi Mungu haokowe kwa njia ile. Bali, kila mtu anayeamini anahesabiwa haki. Kwa mambo ngapi? Mambo yote. 

Kama wewe unahesabiwa haki kwa mambo yote, sasa ni nani atakayepata jambo la kuleta hukumu juu yako?

 

8/ Turudi nyuma kidogo kwa Waraka moja yenye watu wengi wanapendelea kutumia. 

Ufunuo 12: 10 

“Nikasikia sauti kubwa katika mbingu ikisema: Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye ambaye anawashitaki mbele ya Mungu wetu, mchana na usiku.” 

         Hii ni kwa nyakati ya Mateso Makuu, Shetani anakuwa akishitaki, wale wenye kuhubiri habari njema, wale 144000. 

Na hapo, kwa mwisho wa nyakati ya Mateso Makuu, Shetani mshitaki atatupwa chini toka eneo iliyokuwa yake. 

Kwa kweli, naamini kwamba hata kwa siku za leo kazi yake ni ile ile na anatumika namna sawa. 

Kumbukeni yale aliyofanya kwa Yobu. 

Yobu 1: 8 - 11  

“Bwana akamwambia Shetani: Umeangalia mtumishi wangu Yobu?

Maana hakuna mmoja kama yeye duniani, mtu mkamilifu na wa haki, mwenye kuogopa Mungu na kuepuka na uovu. 

Shetani akajibu BWANA akisema: Yobu anaogopa Mungu bure? Wewe hukumzunguka yeye na nyumba yake, na vyote aliyo navyo, kwa boma pande zote? 

Umebariki kazi ya mikono yake, na mali yake imeongezeka inchini. 

Lakini nyosha sasa mkono wako, na gusa vyote alivyo navyo, na yeye atakukufuru mbele ya uso wako.”  

         Hapa Shetani anaamua kumshitaki Yobu kwa Mungu. 

Ni baada ya Mungu kumtaja Yobu ndiyo Shetani baadaye alipata uwezo wa kumtaja. 

Shetani hangejaribu hata kidogo, bali ni Mwenyezi Mungu aliye muuliza eti umemwona Yobu? 

Ni kweli, wewe umemuzunguusha na boma la ukingo hata mimi siwezi kumutatiza, siwezi kumgusa Yobu. 

Na Shetani akaongeza akisema kwamba; uniruhusu nimunyanganye vitu vyote alivyonavyo, yeye atakukufuru mbele ya uso wako. 

Aya ya 12 

“Bwana akamwambia Shetani: Tazama, vyote alivyo navyo ni mkononi mwako; lakini usinyoshe mkono wako juu yake mwenyewe, Basi Shetani akatoka mbele ya uso wa Bwana.” 

         Shetani alitwaa mali yote yenye Yobu alikuwa nayo katika dunia hii. 

Yobu alisema kwa aya ya 21: 

“akasema: Mtupu nilitoka tumboni mwa mama yangu, na mtupu nitarudi tena kule; Bwana ametoa, na Bwana ametwaa; abarikiwejina la BWANA.” 

         Mwatambua namna gani Shetani anapata haya, imeonekana wazi kwamba yeye ni mudanganyi. 

Shetani alikuwa akisema: Yobu atakukufuru mbele ya uso wako, bali Yobu hakutenda hivyo. 

Fundisho, tunalolipata katika Kitabu cha Yobu, kuhusu Shetani,  ni kwamba Shetani ni musema uongo, na wakati anapo washitaki watu, yeye anatumia uwongo.

  

9/ Mara tena Mungu alimuuliza kama alimwona Yobu, naye alijibu ndiyo 

Yobu 2: 4 – 6 

“Shetani akajibu Bwana, akasema: Ngozi kwa ngozi, ndiyo, yote mtu aliyo nayo atatoa kwa ajili ya uzima wake. 

Lakini nyosha sasa mkono wako, na gusa mifupa yake na nyama yake, naye atakukufuru mbele ya uso wako. 

Bwana akamwambia Shetani: Tazama, yeye ni mkononi mwako; acha uzima wake tu.” 

         Bali wewe uguse mwili wa Yobu naye atakukufuru, ngozi kwa ngozi, Shetani akasema uniruhusu niguse mwili wake, Mwenyezi Mungu akamwambia gusa mwili wake lakini usiguse uzima wake. 

Mungu akamwachilia Shetani kucheza na mwili wa Yobu hadi kiwango cha kwenda kukuna vidonda vyake katika majifu, mwili wote ukijaa majipu, vidonda na makovu. 

Naamini kwamba Shetani aliona kwamba hiyo njo machungu ya aina ya juu sana kuliko katika dunia hii. 

Alimuweka Yobu kuwa katika uharibifu wa kupita kiasi, uvunjaji wa hali ya ajabu, mwili kuharibiwa mno. 

Hata kama mambo haya yote yalitukia Yobu hakukufuru Mungu, hata hakumubebesha Mungu hukumu yeyote. 

Mara tena Shetani anaonekana kuwa mwenye uongo mno, yeye ni mwongo mkubwa sana. Wakati anaposhitaki watoto wa Mungu kuhusu mambo fulani, yeye anatumia uwongo mtupu. Yeye ni mwongo.

 

10/ Ni nini inayotukia wakati Shetani anatushitaki mbele ya Mungu Baba? 

   Ni nini inatukia wakati Shetani anageuza macho yake na kumuambia Mwenyezi Mungu eti tizama kwanza huko chini duniani na uone mambo wanayoyafanya wakristo.  

Kufa kwa Bwana Yesu ni kwa manufaa na muhimu sana kwetu, na pia tena Bwana wetu Yesu Kristo anatuombea akiketi kwa Mkono wa kuume wa Mungu Baba. 

Ni nini inayotukia wakati Shetani anafika mbele ya Mungu Baba na kumwambia tizama mtu yule Mary Smith ama John Tomes pale chini duniani, 

Wao ni wakristo, wao walimwamini Bwana Yesu Kristo, lakini tizama maovu wanayoyafanya. 

Tizama machafuko na machukizo na maovu wanayoyatenda, bali Bwana Yesu Kristo anasema: 

Ninayajuwa hayo yote, wao ni mali yangu na niko hapa kwa ajili ya kuwaombea. Mimi nilikufa kwa ajili yao. 

Nililipa malipo ya zambi zile, na zambi zile ziliwekwa juu yangu. 

Shetani anajaribu kukusanya mambo mengine mapya na kuyaleta mbele ya Mwenyezi Mungu, lakini Mungu anamwambia, yote imekwisha lipwa, na kunakuwa harabuni ya hayo yote. 

Eti wafahamu kwamba ni vigumu na haiwezekani Shetani awe na ushahidi ya kwamba wewe unastahili hukumu? 

O kweli ninafahamu kwamba Shetani anajisumbua na kazi bure, kazi ya punda, kazi yenye haitamufikisha kwa lengo fulani. 

Anafahamu kwamba Biblia inasema kwamba zambi zetu zilitupwa mbali sana. 

Kwamba Mwenyezi Mungu alitukomboa na uzalimu wowote. 

Wewe binafsi waweza kujihukumu na kusema kweli Shetani anaweza akanishitaki kwa jambo hili na lile, hapana sivyo, Shetani hawezi kuleta ushahidi hata moja kwa sababu Bwana Yesu Kristo alibeba muzigo wako wote wa zambi na kuvaa hukumu iliyokuwa yako. 

Eti si Bwana Yesu alifanywa kuwa zambi? 

Kwa kweli, ni vigumu kwangu kusema zaidi ya hayo.

1 Yoane 4:17 

“Hivi mapendo yamekamilishwa kwetu, ili tuwe na uhodari katika siku ya hukumu; kwa sababu kama yeye alivyo, ndivyo tulivyo sisi katika ulimwengu huu.” 

Kwa kweli, Wakolosai 2: 10 inasema: 

“Na ninyi mumetimilika katika yeye aliye Kichwa cha falme zote na mamlaka.” 


11/ Katika Kigriki: 

NI NANI ATAKAYEJARIBU KUTUHUKUMU? 

MUHUKUMU MKUU YEYE MWENYEWE ALITUHESABIA HAKI BILA ZAMBI. 

Kama kuna yeyote yule anayependa kukushota zambi zako kidole, yafaa kwake kushota kidole chake kwake YEYE, na ni nani atakayejaribu kumshota?  

1 Petro 2: 24  

“Yeye mwenyewe alichukua zambi zetu katika mwili wake juu ya mti, hata sisi, tukiwa wafu kwa maneno ya zambi, tuwe hai kwa maneno ya haki, na kwa kupigwa kwake muliponyeshwa.” 

         Nani atakayejaribu kumshitaki? 

Ni Yeye anayeshitaki. 

Ni Yeye aliyechukuwa zambi zetu. 

Aliteswa kwa ajili ya zambi zetu.

 

12/ Waebrania 10: 11, 12 

“Na kila kuhani anasimama kila siku akitumikia, na kutoa zabihu zile zile mara nyingi, nazo haziwezi kabisa kuondoa zambi. 

Lakini yeye wakati alipokwisha kutoa zabihu moja kwa zambi hata milele, akiketi mkono wa kuume wa Mungu;” 

         Waraka wa Waebrania unalinganisha huduma ya Bwana Yesu Kristo na ya wale Makuhani wa Agano la Kale. 

Na kila kuhani anasimama kila siku akitumikia, na kutoa zabihu zile zile mara nyingi, nazo haziwezi kabisa kuondoa zambi. 

Lakini yeye wakati alipokwisha kutoa zabihu moja kwa zambi hata milele, akiketi mkono wa kuume wa Mungu; 

Tufahamu kwamba wakati Bwana Yesu Kristo alirudi mbinguni, Yeye aliketi sababu alitimiza na kumaliza kazi yake. 

Najua siku moja umekwisha kutenda kazi ya nguvu sana na baadaye unarudi nyumbani ukiwa tu na uwezo wa kuketi na kupumzika. 

Ilikuwa muhimu Bwana Yesu Kristu afanywe zambi kwa ajili yetu. 

Yeye alisulubishwa, na kufufuka toka wafu na kiisha alipaa kwenda mbinguni. 

Alirudi KWAKE. 

Anaketi kwa sababu kazi yote imekwisha. 

 Kwa hiyo, kumshitaki mwamini yeyote kwa jambo fulani alilolifanya, ingelimaanisha kusema kwamba kazi hii ya Bwana Yesu Kristo haikutimilika. Kwamba kazi hii haitoshi. 

Bali kwa uhakika na kweli kazi yake yote ilitimizwa, ni kwa hiyo, kama unahitaji kushitaki yeyote ule, unyooshe kidole chako na kushota Mwokozi wetu Kristo Yesu. Umshitaki tu Yeye. 

Usijaribu kushitaki hata moja ya watoto wake. 

13/ Tukumbuke pia kwamba Yeye anatuombea, akiketi, na kutuombea. 

Yeye hajajali kamwe kuwa na hali ya kasirani, Yeye hana haja ya kuwa na haraka haraka kama kuna mashitaki juu yetu, kwa sababu alitimiza kazi yote, yote imekwisha na anaendelea tu kusema: 

Mimi nilikufa kwa ajili ya mtu huyu. 

Nilikufa na kulipa malipo ya zambi zake. 

Sisi tumewekwa huru, sisi ni huru. 

 

AMINA.  

 

 N°Ref: 07/04/1965 / 30 - THE DEVIL’S HOPELESS JOB / 01/29/2022