Tuesday, July 28, 2020

JE UMEKWISHA KUKUTANA NA NEEMA? HAVE YOU MET GRACE?

Photo taken by B Smith from the Patio



  

 

JE UMEKWISHA KUKUTANA NA NEEMA? 

HAVE YOU MET GRACE? 

Januari 6, 1980

Pastor Henry F. KULP





 

Waroma 5: 20, 21 

“Lakini sheria iliingia, ili zambi ziwe kubwa sana; lakini pahali zambi zilipozidi, neema ilizidi zaidi sana: 

hata, kama vile zambi ilivyotawala katika kufa, hivi kwa njia ya haki neema itawale hata uzima wa milele kwa Yesu Kristo Bwana wetu.” 

Hapa kweli, tuna neno moja la muhimu sana.

Neno lile ni, neno “Neema”, inayomaanisha “vyote kwa bure pasipo malipo”. 

Lakini utunzaji huu wa neema unakuwa, kwa wengi wa watu, nguvu kufahamu, ni wachache sana wanawoishi maisha yao wakiwa chini ya neema ya Mungu. 


1/ Katika vitabu 39 ya Agano la Kale, tunakuta tu aya mbili inayozungumuza juu ya neema ya Mungu kwa wanadamu. 

Katika vitabu ine vya Injili, neno “neema”, haipatikane katika kitabu cha Matayo, ama Marko, neno neema inapatikana mara moja tu ndani ya kitabu cha Luka, mara tatu ndani ya sura ya kwanza ya kitabu cha Yoane. 

Mara mia moja makumi mawili na nane (128) katika Agano Jipya nzima, lakini Mutume Paulo, yeye mwenyewe, anatumia neno “neema”, mara mia moja na tatu (103); hii inamaanisha kwamba, inje ya Mutume Paulo, neno “neema” imetumikishwa tu mara makumi mbili na tano (25) katika Agano Jipya. 

 

2/ Eti wewe bado kutambua kwamba Vitabu vyote vilivyoandikwa na Mutume Paulo, vinaanzishwa vikitaja neno “neema”, kwa mwanzo wa kitabu,  na vinafungwa vilevile  vikitamka neno “neema”, kwa mwisho wa kitabu.

Tutizame kwanza katika kitabu maali tunaposoma maandiko yetu tunayo jifunza kwa sasa. 

Waroma 1: 7  

“kwa wote walio kwa Roma, wapenzi wa Mungu walioitwa kuwa watakatifu: 

Neema iwe kwenu na salama kutoka kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana yetu Yesu Kristo.” 

Kiisha pale tuone kwamba Waroma 16: 24 inasema: 

“Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe pamoja nanyi wote. Amina.” 

Kiisha, 

1Wakorinto 1: 3 

“Neema kwenu, na salama toka Mungu Baba wetu, na kwa Bwana Yesu Kristo.” 

1Wakorinto 16: 23 

“Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe pamoja nanyi.” 

Pia tuone kwamba, 

2Wakorinto 1: 2 

“Neema iwe kwenu na salama toka Mungu Baba wetu na Bwana Yesu Kristo.”  



2Wakorinto 13: 14 

“Neema ya Bwana Yesu Kristo, na mapendo ya Mungu, na ushirika wa Roho Mutakatifu ukae pamoja nanyi wote.” 

Na vivi hivi, ni katika hali hii ndiyo Vibarua vya Mutume Paulo vinavyo kuwa. 

Hii inanishuhudia kwa kweli kwamba ni Mutume Paulo aliye Mujumbe na muhubiri wa Neema ya Mungu. Ujumbe wake wote ni neema na neema mtupu katika yote. 


3/ 1Wakorinto 15: 10 

“Lakini kwa sababu ya neema ya Mungu nimekuwa sawasawa nilivyo: 

Na neema yake niliyopewa haikuwa bure; lakini nilizidi sana kufanya kazi kupita wao wote: wala si mimi, lakini neema ya Mungu iliyokuwa pamoja nami.” 

Hapa Mutume Paulo anatuelezea nini ilitukia katika maisha yake. 

Anasema kwamba: kwa sababu ya neema ya Mungu nimekuwa sawasawa nilivyo: na neema yake niliyopewa haikuwa bure. 

Ni neema ya Mungu iliyobadirisha namna alivyokuwa akiishi, pia ni neema iliyo musukuma kufanya kazi nyingi. 


4/ Waefeso 3: 1 – 3 

“Kwa sababu hii mimi Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu kwa ajili yenu ninyi Mataifa, 

Ikiwa mumesikia habari za uwakili ya neema ile ya Mungu niliyopewa kwa ajili yenu; 

Ya kwamba kwa ufunuo nilijulishwa siri hii, kama nilivyoandika mbele kwa maneno machache.”  

Hii ni Utunzaji wa Neema ya Mungu. 

Ni mafundisho ya Neema mtupu, neema tu. 


5/ Waroma 11: 6 

“Lakini ikiwa kwa neema yake, haiko kwa matendo tena, au neema isingekuwa neema; na ikiwa kwa matendo, haiko neema tena; au matendo yasingekuwa matendo.” 

Tunaona na kuhakikisha hapa kwamba Neema na matendo haitembee pamoja.  

Yote inayokuwa ya neema, haina matendo ndani yake. 

Ukajaribu kuongeza tu neno moja juu ya neema, hauna tena neema. 


6/ Basi niwaoneshe neno moja la muhimu sana kuhusu neema. 

2Wakorinto 8: 6 - 7  

“Hata tulionya Tito, ya kwamba kama alivyoanzisha hivi atimize ndani yenu neema hii vilevile. 

Basi kama munavyozidi katika mambo yote, kwa imani, kwa usemi, kwa elimu, kwa bidii yote na kwa mapendo yenu kwetu, basi muzidi katika neema hii vilevile.” 

Hapo Mwenyezi Mungu anasema: 

Wakati mtu anatoa toleo, ama sadaka kwa Mungu, ni kwa njia ya neema ndiyo watu wanatolea Mungu. 

Ni kusema kwambo, kinacho sukuma mtu kutowa sadaka, ni neema yake Mungu inayotenda kazi katika maisha ya mwenye kutoa na ni hii neema inayo musukuma kwa kutowa. 

Watu kwa desturi ya kimtu wanapenda tu kupokea. 

Kila saa na kila nyakati wanapenda tu wapate kitu kingine, lakini wao walio katika Yesu Kristo, wao wanakuwa na viumbe vipya, wao wanafurahia kutolea wengine, na wanapofanya hivi, tendo lile linaitwa neema. 

Ni kusema kwamba: 

Wao wanapotolea wengine, si kwamba wanangojea matukio ya kwamba nao vilevile wapewe sababu walitowa kwa wengine, ni kusema kwamba, vyote ni bure pasipo malipo. 

Lakini tena, wao wanapotelea Mungu, wanaifanya kwa kadiri ya mapato yao, kwa kufwatano na hayo wao wanauwezo ya kutolea Mwenyezi Mungu. 

Wangapi katikati yetu wanaosema kwamba tangia wakati mimi nilianza kutolea Mungu, mimi sina tena shida yoyote. 

Hiyo siyo shabaa yetu kwa kutolea Mungu. 

Tunatolea Mungu wetu kwa njia ya neema. 


7/ Waroma 5: 20 

“lakini sheria iliingia, ili zambi ziwe kubwa sana; lakini pahali zambi zilipozidi, neema ilizidi zaidi sana:” 

Sasa, hiyo inasema kwamba: 

Mahali zambi zilipozidi, neema ilizidi zaidi sana. 

Neema inayozidi. 

Neema inayozidi zaidi sana. Neema inayotiririka. 

Mutume Paulo hasemi kwamba, mahali zambi inapokomaa, ama kuzidi, neema itatolewa kwa kadiri ya uwingi wa zambi. 

Yeye anasema kama kuna kiwango cha neema kubwa zaidi, neema inayozidi zaidi sana kupita hiyo zambi zote, sababu anatumia maneno karibuni kumi katika luga ya Kigriki ili amaanishe neno kuzidi. 


8/ SABABU GANI MWENYEZI MUNGU ANAKUWA NA NEEMA KWA WANADAMU WOTE? 

Eti Biblia inatufunulia shabaa ya Neema ya Mungu? 

Kweli kweli Biblia inatufunulia mambo yale. 

Tuangalie kwanza na tukamate neno mbili kubwa ya humimu tunayoyapata katika Biblia. 

Mapendo na Neema

Yoane 3: 16 

“Kwa maana Mungu alivyopenda ulimwengu, hata kutoa Mwana wake wa pekee, ili kila mutu akimwamini asipotee, lakini apate uzima wa milele.” 

Tuone namna Mungu alivyopenda ulimwengu.

Nikusema, Mungu aliupenda ulimwengu kwa namna ya kuzidi, akamtoa Mwana wake wa pekee, na hapo tunafundishwa kusudi la Mapendo ya kuzidi ya Mwenyezi Mungu.  

Ni ya ngambo mbili, inasehemu mbili. 

Kwanza mtu asihaibike, asipotee na pili, mtu apate uzima wa milele.

Ni kusema kwamba faida hizo ni kwa yule anayeokolewa, lakini vilevile inakuwa tayari kwa niaba ya yule mtu bado kuokolewa. Huyu mtu asihaibike, lakini awe na uzima wa milele.  

Mtu mwenye zambi anapokuja kwa Bwana wetu Yesu Kristo, akimuamini kama Bwana na Mwokozi wake, kiisha hapo anavumbua shabaa ya Neema ya Mungu, yeye atasema moyoni mwake: 

Mwenyezi Mungu hakupenda mimi nihaibike. 

Mwenyezi Mungu anapenda mimi niwe na Uzima wa milele. 

Na Mungu alitayarisha yote sababu ya jambo lile.

Alitayarisha wokovu kwa njia ya Neema yake. 


9/ Tuchunguze sasa shabaa ya pili ya neema ya Mungu inayozidi sana. 

Waefeso 2: 8 – 10 

“Kwa maana mumeokolewa kwa neema kwa njia ya imani, wala neno hili halikutoka ndani yenu wenyewe, ni zawadi ya Mungu, 

Si kwa matendo, asiwe mtu atakayejisifu,

Maana sisi ni kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu ili tutende matendo mema Mungu aliyotengeneza mbele ili tutembee ndani yao.” 

Hapo tunasoma ya kwamba: 

Kwa maana tumeokolewa kwa neema kwa njia ya imani, kiisha tunashuka kwa aya ya kumi inayosema: 

Tuliumbwa katika Kristo Yesu ili tutende matendo mema Mungu aliyoyatengeneza mbele ili tutembee ndani yao. 

Moja ya shabaa ya neema ya Mungu, ilikuwa kwa sababu Mwenyezi Mungu apate kuokoa nafsi zetu, pia shabaa ya pili ni kwamba kiisha kuokolewa tupate kutenda matendo mema yanayoweza kumutukuza Mungu. 

Hapo, tunataka kufunua neno moja la muhimu kuusu neema ya Mungu katika wokovu.  

Hakuna mutu mwenye anapokea neema ya Mungu, nyingi sana kupita mwengine. 

Sote tumeokolewa na kiwango kimoja cha neema ndani ya Bwana wetu Yesu Kristo. 

Mwenyezi Mungu haambie huyu mtu mutenda zambi sana na mukaidi na muzalimu kwamba namna wewe ni muovu sana, itanipasa nichukuwe sehemu kubwa ya chini ya pipa ya neema ili nikutibu. 

Pia haambie mutu mwengine anayekuwa na maisha ya kawaida, kwamba, wewe unaishi kawaida tu na kwa hiyo, kwa wewe nitachukuwa tu kiwango cha kawaida ya neema ili nikutibu. 

Na pia Mwenyezi Mungu haambie huyu mutu wa tatu kwamba wewe unazamiri safi sana, unaishi maisha ya kujizuiza kweli kwa hali ya juu, hata majirani wako wanakushuhudia vema, wenzako wa kazi na marafiki wote wanakushuhudia vizuri na sasa kwa niaba yako nitakamata tu kipimo ya neema inayo ingia katika kijiko moja ama koleo ili nikutibu. 

Neema ya Mungu haijali uwe mwenye zambi wa aina ya kwanza, aina ya pili, ama aina ya tatu, na zaidi ya hayo tunavumbua kwamba Mwenyezi Mungu anapatia mwamini neema zaidi. 

Mwenyezi Mungu anatupatia sote kiwango kimoja cha neema katika wokovu wetu, lakini anatupatia neema zaidi katika maisha yetu ya kila siku, katika kazi tunazozifanya, na katika huduma zetu. 

Yakobo 4: 6  

“Lakini anatupa sisi neema nyingi zaidi; basi maandiko yanasema: Mungu anashindana na wenye kiburi, lakini anawapa neema wanyenyekevu.” 

Basi mutii Mungu, 


Yakobo anasema: anatupa sisi neema nyingi zaidi.

Kuna neema inayotufanya kutenda matendo mazuri. 


10/ Tuchunguze vema neno “matendo” yenye inatamkwa mara mbili katika maandiko ya Waefeso 2: 9 

“Si kwa matendo, asiwe mtu atakayejisifu.” 

Matendo yamelaaniwa kwani yametendwa na uwezo wa mwili, yametimizwa na mtu wa zamani akiwa na kusudi ya kulipa malipo juu ya wokovu. 

Katika Waefeso 2: 10 

“Maana sisi ni kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu ili tutende matendo mema Mungu aliyotengeneza mbele ili tutembee ndani yao.” 

Na Mungu hapo anatufunulia kwamba, matendo mema inayotukia katika maisha yetu ni moja ya shabaa ya neema inayozidi, katika wokovu wa mwenye zambi. 


11/ Tutambue kwamba  aya ya kumi (10) inasema: 

 Sisi ni kazi yake. 

Tutambue na kufahamu kwamba ni Mwenyezi Mungu njo mutenda kazi wa matendo mazuri ndani yetu kwa njia ya neema yake. 

Tendo hili ni kwa wale tu walioumbwa upya katika Kristo Yesu. 

Hatuokolewi sababu ya kuepuka uchungu na mateso ya mauti ya pili, ama jehenamu, ama kufa ya milele, lakini ili tutende matendo mema. 

Maneno haya tumeyafundishwa mara tena katika kitabu cha Tito 2: 14 

Tito 2: 14   

“ambaye alijitowa mwenyewe kwa ajili yetu atukomboe toka uovu wote, na kujisafishia watu wawe mali yake mwenyewe, wenye bidii sana katika kazi njema.” 

12/ Tuone sasa shabaa ya tatu ya neema ya Mungu inayozidi sana. 

Waefeso 3: 10  

“ili sasa, kwa njia ya kanisa, hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi ijulishwe na falme na mamlaka katika pahali pa mbingu;” 

Tunaweza semezana mengi sana na kwa muda murefu kuusu andiko hili, lakini kwa ufupi tuone kwamba inamaanisha nini: 

Mwenyezi Mungu katika muumbo wake wa kwanza, aliumba majeshi ya wa malaika. 

Wao ndio falme na mamlaka katika pahali pa mbingu kwa sasa. 

Kundi moja ya tatu ya ile jeshi ya wa malaika ilitomboka na kuzani kujiinua wafananishwe na Mwenyezi Mungu. 

Isaya 14: 14 

“Nitapanda juu kupita virefu vya mawingu, nitafanana na Mjuu Sana.” 

Alipenda ageuke kuwa Makerubi aliye juu kupita. 

Alipenda afikie kwa nafasi ya Bwana Yesu Kristo, na aliitafuta  kwa uwezo wake mwenyewe, kwa nguvu zake mwenyewe, lakini sasa Mwenyezi Mungu iko anawaondowa watu wenye zambi katika ulimwengu, watu wenye wako chini  sana ya malaika,  kanisa, mwili, na atawafanya kuwa kile Yeye Mwenyewa alikusudia wageuke kuwa kutoka jeshi lile lililo anguka na kutupwa chini duniani. Na siyo kwa uhuru wetu, ama kwa matendo yetu, lakini kwa utegemezi na kutegemea tu neema ya Mungu peke yake. 

Kwa kweli, yale majeshi ya malaika wenye hawakushushwa huku chini duniani, wale wamalaika waliobakia juu mbinguni wakiwa waaminifu kwa Mungu, wamalaika wale hawafahamu hata neno juu ya Neema ya Mungu, tangu kutangwazwa kwake na kuanza kutumishwa kwake,  na ni kwa sababu ile  wamalaika wanatutazama na kujifunza kwetu, na sisi tunakuwa walimu wao tukiwafundisha juu ya neema siku kwa siku. 


13/ Kwa hiyo, sababu ya tatu ya shabaa ya neema ya Mungu inayozidi sana ni kwa sababu tuoneshe wamalaika namna gani Mungu anatumika na mwanadamu kwa upekee. 


14/ Shabaa ya ine ya neema ya Mungu inayozidi sana tutaipata katika maandiko ya Waefeso 1: 23 

“lililo mwili wake, utimilifu wake anayetimiza vyote katika vyote.” 

Hii ni andiko kweli la kutushangaza sana. 

Inatumia msemwa, utimilifu ndani ya KRISTO, kweli wazo gani iko hapa? 

Mungu alimufanya KRISTO awe Kichwa cha Kanisa iliyo Mwili wake, utimilifu wake anayetimiza vyote katika vyote. 

Utimilifu wa KRISTO unamaanisha nini? 

Yeye Kristo, haiko Mungu kamili?  La!, Yeye ni MUNGU Kamili. 

Tufahamu kwamba Waefeso 1: 22, 23 



Waefeso 1: 22, 23 

“na ameweka vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe Kichwa juu ya vitu vyote kwa kanisa 

Lililo Mwili wake, utimilifu wake anayetimiza vyote katika vyote.” 

Kristo ndiye Kichwa cha Mwili. 

Sisi ni viungo vya huo Mwili; na kichwa pekee bila mwili, hakitimilike. 

Kitu cha mastaajabu ni kwamba Kanisa, Mwili wa Kristo ndilo Utimilifu wa KRISTO. 

Siku moja inayokuja Mwili itakuwa pamoja na Kichwa katika Utukufu; lakini kwa leo, Mwili iko hapa duniani na Kichwa iko mbinguni. 

Ni mambo ya ajabu sana kutambua kwamba KRISTO haiko timilifu bila sisi. 

Fikili kwanza ndugu yangu, hapo kale sisi tulikuwa wenye zambi, wapotevu, tukitengwa na Mwenyezi Mungu, hatukukuwa na tumaini lolote, tukiwa tu tunastahili hukumu ya Mungu, na sasa kupitia neema yake tuliokolewa, tukageuka kuwa viungo vya Mwili wake, Mwili wa KRISTO, na hilo ni Utimilifu wa KRISTO. 

Uwajibu gani tunalo lakutupasa kutenda matendo mema sababu sisi ni kiungo cha KRISTO. 


15/ SEHEMU HII INAPATIKANA CHINI YA SHABAA YA KWANZA YA NEEMA YA MUNGU INAYOZIDI.  

Waefeso 1: 6  

“na kwa sifa ya utukufu wa neema yake ambayo alitupa sisi katika huyu Mpendwa.” 

Mwanadamu hana aja kujisifu hata kidogo. 

Ni yeye mwenyewe aliyetupatia kukubaliwa ndani ya Mpendwa. 

Kumbukeni kwamba neema inamaanisha, yote kwa bure pasipo malipo, sisi alitupatia tukubaliwe kwa mecho ya Mungu Baba kwa Neema katika Kristo Yesu. 


16/ Jameni niwape mfano kuusu maneno ninayotaka kusema: 

Munakumbuka huyo mwanamuke aliye penda kuuwa Malkia Elizabeth 1. 

Huyo mwanamuke alijivika nguo za kinaume na kujificha ndani ya chumba cha mapumuziko cha Malkia akingojea saa Malkia itajiingiza humo ili amuchomeke kisu mpaka kumuua. 

Mwanamuke huyu hakukumbuka kwamba walinzi wa Malkia wanapashwa kwanza kujitahidi kupekua chumba nzima na nafasi yote na kuhakikisha kwamba hakuna hatari yoyote, mbele ya kuruhusu Malkia kuingia ndani. 

Akiwa akijificha nyuma ya kanzu la kuoga, na mavazi marefu, walinzi walimufichua, wakamnyanganya mupanga aliokuwa nawo mikononi na wakamubeba mbele ya Malkia. 

Alipofika, alitambua kwamba hakuna tena kitu cha kufanya ni malipizi makali tu analostahili. 

Hivi akajitupa kwa magoti mbele ya Malkia na kuomboleza na kumlilia akisema: wewe kama mwanamuke, unihue razi na kunihurumia sana kwa kunipa neema kutoka kwako. 

Malkia akamwangalia vizuri tena akakamata muda wa kumutizama na kumuchunguza kwa makini sana, kiisha akumuuliza huyu mwanamuke mwenye alitaka kumuuwa, akisema: 

“kama nikakupatia neema, ahadi gani unalo niagiza utakalo fanya kwa siku za usoni?” 

Huyu mwanamuke akaangalia juu kiiasha akamjibu Malkia: 

“Neema inayokuwa na ma sharti, hiyo siyo neema, siyo neema hata kidogo.” 

Malkia akafahamu maana ya jibu ya mwanamuke huyo, kwa hiyo Malkia akamwambia: 

“Mwanamuke, wewe ni huru sasa” 

Historia inatuambia kwamba tangu siku ile Malkia Elizabrth 1, hakuwa na mtumishi mwaminifu, anayejitoa sana sawa yule mwanamuke mwenye alikuwa kwa mwanzo akijitayarisha ili aondoe uzima wa Malkia Elizabeth 1 kwa kumuua kwa upanga. 


17/ Tunafika sasa kwa shabaa ya tano ya neema ya Mungu inayozidi, tena kumbuka namba tano ndiyo namba ya neema.

   Waefeso 2: 6, 7 

“na alitufufua pamoja naye na kutukalisha pamoja naye katika pahali pa mbingu, katika Kristo Yesu; 

Hata katika nyakati za kuja aonyeshe wingi wa kupita kiasi wa neema yake kwa wema wake kwetu katika Kristo Yesu;”  

Tufahamu sana shabaa yenye iko katika aya ya nane (8) 

“kwa maana mumeokolewa kwa neema kwa njia ya imani, wala neno hili halikutoka ndani yenu wenyewe, ni zawadi ya Mungu,” 

Na unaweza kuanza kujisumbuasumbua wewe pekee na kusema iyo mambo inahusu tu wokovu. 

Kweli mumeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani, lakini kuna mazoezi kidogo inayoombwa kwenu, hiyo ya kutambua kwamba aya hii, inaanza na neno moja fupi na ndogo, ni neno “kwa maana”. 

Kwa maana mumeokolewa kwa neema, hiyo inarudisha mafikili yetu kwa aya 6 na 7. 

Hivi basi nitawasomea aya hizo nikipima kuyatafsiri kwa ajili yenu: 

NA AKITUFUFUA PAMOJA NA KUTAKALISHA NDANI YA YESU KATIKA MAHALI PA MBINGU. 

KATIKA NYAKATI ITAKAO KUJA ATATUONESHA UTAJIRI WA MAARUFU, UTAJIRI UNAOPITA KIASI SANA, UTAJIRI WA WINGI WAKUPITA KIASI WA NEEMA YAKE KATIKA WEMA WAKE KWETU NDANI YA YESU KRISTO KWA MAANA TUMEOKOLEWA KWA NEEMA. 


18/ Wazo hapa ni kwamba mumeokolewa ili muonyeshe utajiri wa maarufu, utajiri wa kupita kiasi sana wa neema ya Mungu kwa wale wakaaji wa mbinguni. 

Siyo tu kwamba tumeokolewa kwa neema, lakini kweli, hiyo ndiyo ukomo wa wokovu wetu. Ni hiyo shabaa ya tano tena ya mwisho ya neema ya Mungu inayozidi. 


19/ Sinawofu ya kwamba katika nyakati zijazo, inawezekana iwe miaka bilioni inayokuja, tukihesabu tangu leo, wamalaika wanao angalia wewe na mimi na woga, wakishangaa na kututamani, watazungumuza wao kwa wao wakijiuliza na kusema: hawa ni wawili wa watakatifu, walikuwa ndani ya dunia katika hali ya uasi, walikuwa katika muda wa machafuko na zambi. 

Wao walikuwa watendazambi, mbali na Mungu, walikuwa adui wa Mungu, lakini Yeye aliwapenda na wao wangali bado katika hali hiyo, na Mapendo yake iliwafikia kupitia Kifo cha Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo na walimuamini Yesu Kristo na kufanywa kuwa watakatifu. 

Alitimiza na kufanya haya yote kwa ajili yao. 

Na sisi tutajibu wamalaika tukiwaambia: 

Kweli mulimusujudu na kumuabudu kwa sababu anastahili kusujudiwa. 

Yeye pekee ni wa Mastaajabu sana. 

Yeye tu anajaa wingi wa Neema. 

Hakuna hata mumoja kama Yeye. 

Ndiyo maana kwenye zambi ilizidi, neema ilizidi sana.      

Amina 


N°Ref: 01/06/1980 / 526 (DOC 319) HAVE YOU MET GRACE / 07/28/2020

Monday, July 20, 2020

NI NANI ANAYEKUWA NA RUHUSA YA KUITA MUNGU, BABA? WHO HAS THE RIGHT TO CALL GOD FATHER?

Photo taken by B Smith from kitchen window



 


 

NI NANI ANAYEKUWA NA RUHUSA YA KUITA MUNGU, BABA? 

WHO HAS THE RIGHT TO CALL GOD FATHER?

August 20, 1961           

Pastor Henry F. Kulp

 


 

Wagalatia 4: 1 - 7  

“Lakini ninasema ya kuwa mriti, wakati alipokuwa mtoto, anaonekana kama mtumwa hata akiwa bwana wa wote; 

Lakini ndiye chini ya wasimamizi na mawakili hata wakati uliokwisha kuamuriwa na baba. 

Vile na sisi, tulipokuwa watoto, tulifungwa chini ya desturi za dunia; 

Lakini wakati ulipomalizwa, Mungu alituma Mwana wake, aliye zaliwa kwa mwanamuke, aliyezaliwa chini ya sheria ili awakomboe waliokuwa chini ya sheria tupate kupokea hali ya wana. 

Lakini kwa sababu ninyi ni wana, Mungu alituma Roho ya Mwana wake katika mioyo yetu, anayelia: Aba, Baba. 

Basi, wewe si mtumwa tena, lakini mwana; na kama mwana, basi mriti wa Mungu kwa Kristo.” 

Mutume Paulo, katika kitabu cha Wagalatia 3, iko anafasiria kwa nini sheria ililetwa kwa watu. 

Mbele ya neno lolote, tufahamu kwamba sheria ilikuwa tu ya Taifa la Israeli peke yake na kwa wana wa Israeli tu. 

Sheria ilikuwa chuo cha wana wa Israeli, na Mwalimu wao, ili iwalete kwa Bwana Yesu Kristo. 

Sasa kwa aya ya ine, Mutume Paulo iko anatufahamisha namna gani, Taifa la Israeli, Wayuda, walikuwa chini ya sheria kama watoto wachanga, wasioweza hata kutamka neno lolote. 

Kwa kweli Taifa hilo la wana wa Israeli ni mriti, lakini haija fikia kiwango cha kuriti uriti wake alioupewa na Mwenyezi Mungu. 

Ni mtoto asiyejuwa kwamba yeye ana uriti mkubwa, hajuwi kwamba kuna uriti mkubwa unaowekwa na kutayarishwa wake. 

Anakuwa akilinganishwa na mtoto anaye zania kwamba makuta ya kikoroti moja inayo angaa, inakuwa na samani kubwa kupita ma milioni kazaa ya pesa, sababu yeye hajuwe kama ma milioni kazaa ya pesa ina samani gani. 

Hii inakamilisha masomi tunayoyasoma kwa mwanzo wa aya ya ine, kwamba mtoto huyu anaonekana kama mtumwa, akiwa sawa mtumwa. 


1/ Wagalatia 4: 5  

 

“ili awakomboe waliokuwa chini ya sheria, tupate kupokea hali ya wana,” 

Lakini sisi kwa siku za leo, hatuko tena chini ya sheria, hatuko tena sawa watoto wachanga. 

Sisi tunao sasa uriti wetu, sawa watoto wenye kukomaa wanaopokea sasa hali ya wana. 

Maana yake ni nini? 

Wakati tunapofikili juu ya maana ya neno kupokea hali ya wana, mafikili yetu inaenda kwa jambo la kukamata mtoto wa mtu mwengine na kumushurulikia kwa vyote, lakini hiyo siyo maana ya swali hili katika Kigriki.

Katika Kigriki inamaanisha kupatia hali hii ya wana kwa mutoto wako binafsi uliyezaa. 

Katika maisha ya mtoto wakiume wa Kihebrania, yeye alikuwa anafikia umri ambao baba yake mzazi angelipashwa kutimiza mchakato na sherehe ya kumufanya kupokea hali ya wana. 

Ni badala ya mchakato na sherehe lile ndiyo, kijana mwanaume aliitwa sasa mwana wa baba yake mzazi. 

Mbele ya sherehe hilo, hata mtoto alizaliwa na huyo baba, yeye alikuwa bado anaonekana kama mtumwa, akiwa chini ya uongozi wa wasimamizi na mawakili wenye walikuwa wanamuonesha nini kufanya na nini hapana kufanya. 

Nini anayoweza kufanya na nini asiyoweza kufanya, hivyo hakukuwa tofauti kati yake na mtumwa. 

Lakini wakati muda kamili ulitimia, kwa kweli, kijana akiwa tayari anaisha komaa, hapo inaonekana kwamba kijana hana tena mafaa ya kuwa na musimamizi anaye mchunga saa zote.

 

Hapo sasa kunakuwa sherehe ama mchakato ya kumupokeza hali ya wana na inafanyika hazarani pa nafasi ya watu wote. 

Baba ataleta mtoto wake wakiume kwenye korti, mutoto wake mume aliye kuwa akionekana hadi pale kama mtoto mchanga, na hapo baba atajibia kwa maulizo mbalimbali yenye Muhukumu atamuuliza, na ni badala ya hapo ndiyo mtoto atajulikana na Serkali kwamba yeye anapokea hali ya wana kwa baba yake. 

Pale, baba anamupa mtoto wake hali ya wana mbele ya Serkali. 

Hii inatuonesha tofauti yenye ilikuwa kati ya Wayuda, chini ya sheria na sisi chini ya neema.  

Waamini wa Agano la Kale, namna walikuwa chini ya sheria, wao walikuwa wana wa Mwenyezi Mungu, lakini wao hawakuwa bado kukamilishwa kama wana wa Mungu. 

Lakini kwa nyakati hii ya utunzaji wa Neema, mambo ni tofauti. 

Watoto wote wa Mungu ni wana wake. 

Unaweza kujiuliza je, tofauti gani iko pale? 


2/ Chini ya sheria watoto hawakukomaa, walibaki tu wachanga, umbalimbali na leo, sisi ni wana wa Mungu. 


3/ Kumbukeni kwamba kitabu ya Yeremia 31: 32 inasema: 

“Si kwa mfano wa agano lile nililofanya na baba zao, katika siku ile nilipowashika mkono, ili kuwatoa katika inchi ya Misri, lile agano langu ambalo walilivunja, hata mimi nikiwa bwana wao, asema Bwana,” 

Mwenyezi Mungu anazungumuza juu ya Wayuda kwa siku ile alio washika mukono ili awatoshe katika inchi ya Misri. 

Kwa wakati ule wao hawakuwa bado na hali yakupokelewa sawa wana. 

Lakini sisi kwa leo tunahesabiwa kuwa wana wa Mungu. 


4/ Mbele ya kuchunguza kupokelewa kwetu kama wana, waliopokea Roho anayetupokea kama wana, tuangalie kwanza namna gani tunapokea hali hiyo yakupokelewa kama wana.  

Wagalatia 4: 4 

“lakini wakati ulipomalizwa, Mungu alituma Mwana wake, aliyezaliwa na mwanamke, aliyezaliwa chini ya sheria” 

Kunakuwa watu wanaotuammbia kwamba Bwana wetu Yesu Kristo haiko Mwana wa Mungu tangu milele. 

Wao wanasema kwamba, Bwana Yesu aligeuka kuwa Mwana wa Mungu wakati alipozaliwa hapa chini duniani. 

Aya hii ya ine, inakanusha na kupinga mafundisho yale. 

Mungu alituma Mwana wake, aliyezaliwa na mwanamuke. 

Yeye alikuwa Mwana tangu zamani mbele ya Yeye kuacha Enzi yake ya juu na kuja kuingia katika tumbo la Bikira. 


5/ Tunaona namna inavyosemwa ndani ya kifungu cha aya hii:

  Aliyezaliwa chini ya sheria ili awakomboe walio chini ya sheria. 

Kristo anatupatia sasa nafasi na hali yetu ya utukufu tunaokuwa nao kama wana wa Mungu, alijitoa mwenyewe chini ya wasimamizi na mawakili hadi wakati uliokwisha kuamuriwa na Baba. 

Yeye alitiwa na kushushwa kwa hali na nafasi ya mutoto na mutumwa. 

Alitiwa kwa nafasi ya utii. Wafilipi 2 

Wakati alipokuwa duniani, Yeye alikuwa kweli Mwana aliye pendwa na Mungu, lakini kutangazwa tamko la kuwa Mwana wa Mungu ilikuwa bado haijatimilika. 

Yeye alikuwa bado hajapokelewa kama Mwana. 


6/ Zaburi 2: 7  

“Nitahubiri amri: Bwana aliniambia: Wewe ni mwana wangu. Leo nimekuzaa.” 

Tufahamu vema kwamba Zaburi hii inatuambia: 

Nitahubiri amri: Bwana aliniambia: wewe ni mwana wangu. Leo nimekuzaa. 

Ulizo inayofika kichwani mwako ni: Jambo hili lilifanyika siku gani? 

Ama, wakati gani Bwana na Mwokozi wetu alitangazwa kuwa Mwana wa Mungu? 

Tupate jibu katika kitabu ya Matendo 13: 33 

“Mungu ametutimizia sisi watoto wa ahadi hii, kwa kufufua Yesu; kama ilivyo andikwa katika Zaburi ya pili: Wewe ndiwe Mwana wangu, siku hii ya leo nimekuzaa.” 

Ni kwa wakati wa ufufuko ndiwo Tamko lilitangazwa kwamba Yesu Kristo alitangazwa na kuamuriwa kwamba Yeye ni Mwana wa Mungu aliye zaliwa leo. 


7/ Hiyo hiyo wazo tunaipata katika kitabu cha Waroma 1: 3 – 4 

“habari za Mwana wake, aliyezaliwa katika jamaa ya Daudi kwa namna ya mwili, na kuonyeshwa kuwa Mwana wa Mungu kwa uwezo, kwa namna ya Roho ya utakatifu, kwa ufufuko katika wafu; Yesu Kristo Bwana Wetu.” 

Mchakato ama mipango ya kumupopea na kumutangaza Mwokozi Yesu kama Mwana imekwisha kamilishwa.

Ni kwa siku ya Ufufuko wake ndilo jambo lile lilifanyika, Yeye alilotangazwa na kuamuriwa kwamba Yeye ni Mwana wa Mungu. 

Kristo Yesu, alitii na kunyenyekea mwenyewe, na alikubaliwa na kutangazwa na Mungu Baba, kuwa Mwana, wakati alipofufuka, na ni kwa wakati ule ndipo sisi vilevile tulipata kukubaliwa kuwa wana. 


8/ Waefeso 1: 3 - 6  

“Abarikiwe Mungu na Baba ya Bwana wetu Yesu, ambaye alitubariki kwa Baraka zote za roho katika pahali pa mbingu ndani ya Kristo; 

Kama vile alivyotuchagua ndani yake mbele ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, ili tuwe watakatifu na pasipo kilema mbele yake katika mapendo. 

Kwa kuwa alitangulia kutuchagua ili tufanywe wana wake kwa njia ya Yesu Kristo sawasawa ilivyopendeza mapenzi yake, 

Na kwa sifa ya utukufu wa neema yake ambayo alitupa sisi katika huyu Mpendwa.” 

Tufahamu sasa neno inalosemwa hapa: 

Kwa mambo inayotuangalia sisi, imeonekana kwamba, si kwa sababu ya uwingi wa matendo yetu mema, ama hali yetu nzuri, ama kujitowa kwetu kwa kazi ya Bwana, lakini sawasawa ilivyopendeza mapenzi yake, 

Alivyotuchagua ndani yake mbele ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, ili tufanywe wana wake kwa njia ya Yesu Kristo. 

Sasa, namna gani Yeye awezaje kutupeleka mbele ya Baba tukiwa pasipo kilema ama alama, tukiwa na hali na nafasi ya wana? 

Kuna jibu moja tu na ni Maandiko Matakatifu yanayo tupatiya jibu hilo, ni kwa njia ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 


9/ Tufahamu ya kuwa ndani ya Yesu Kristo, sisi tumepokelewa kama wana wanaokwisha tayari kukomaa na kuwa watu wazima, hata kama ukombozi wetu hauja kamilika katika Kristo Yesu, Mwana wa Mungu, Mungu anaye pendezwa na ye na anayekaa kwa Mukono wa kuume wa Mungu, kwenye sisi tunayo njia wazi kwa wingi wa utajiri wa Baba Mungu unaokuwa katika mahali pa mbingu. 

Kwa kweli, wakati wana wa Israeli walikuwa chini ya sheria, wana wa Israeli walikuwa sawa watoto wachanga, kama watoto wadogo wakiwa chini ya uongozi wa wasimamizi na maliwali, wakiwa na maelfu ya amri na maagizo mbalimbali, siyo tu amri kumi iliyo waambia nini wanapaswa kufanya. 

Kwa leo, sisi si chini ya sheria tena, kwa maana, ndani ya Bwana wetu Yesu Kristo, sisi ni watu wenye kukomaa, watu wazima. 

Katika Yesu Kristo, sisi ni watu wazima. 

Je, kwa sasa ni sharti sisi kurejea kushikamana na sheria?

Hapana hata kidogo! 

Hali yetu ni nzuri zaidi sana kupita wale awali chini ya sheria.  

Chini ya neema sisi ni wenye raha kweli.  


10/ Kwa sasa tumepokea Roho ya kufanywa wana, sisi tunakuwa wana walio komaa na kuwa watu wazima, wana wa Mungu wanaokuwa watu wazima, kwa njia ya kufa na ufufuko wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo na ni hii inatufanya sisi kuwa na hali yetu ya wana, lakini itakamilishwa hiyo siku ya ufufuko toka wafu, na ni kwa njia ya ufufuko ndiyo tuta miliki sasa hali yetu kwa ukamilifu.   

 

Waroma 8: 15 

“Kwa maana hamukupokea tena roho ya utumwa inayoleta woga, lakini mulipokea Roho ya kufanywa wana, kwa sababu hii tunalia Aba Baba.” 

Ni kwa njia ya Roho Mutakatifu, anayetupatia hali ya kufanywa wana wa Mungu, ndio tunalia Aba Baba. 

Ni wakati tu tunaye Roho Mutakatifu ndiyo tunaweza kuita Mwenyezi Mungu Baba. 

Kwa kweli, hapo tunapata jibu ya swali yenye inapatikana kwa kichwa cha mahubiri hii: Ni nani anayekuwa na ruhusa ya kuita Mungu, Baba?  

Tunakuwa na hiyo ruhusa, sisi wana wa Mungu tunaokuwa watu tayari wamekomaa, kwa sasa, tunakamilika na kuwa watu wazima katika Kristo Yesu. 


11/ Basi tuseme nini? Eti hali hiyo inatupatia ruhusa ya kudumu katika zambi na kuishi kama tunavyotaka, sababu sisi hatuko tena watoto wadogo wanaoishi maisha ya kujaribu jaribu, wanaokuwa katika kifungo, bila uhuru, wakiwa na wasimamizi, lakini sisi ni wana wanaokuwa watu wenye tayari wamekomaa wakati tunamwamini Bwana Yesu kama Bwana na Mwokozi wetu. 

Eti, hali hii inatupatia ruhusa ya kutenda zambi? Hapana hata kidogo. 

Kumbukeni wana wa Israeli, wakati walipokuwa pekee chini ya sheria wao walikuwa sawa watoto wachanga, wakiwa chini ya uongozi ya wasimamizi na maliwali, walio waambia nini kusema, ama nini kufanya. 

Mungu aliwaambia katika kitabu ya Kutoka 20: 7   

“Usitaje jina la Bwana Mungu wako bure; maana Bwana hatamhesabu ya kuwa hana kosa mwenye kutaja jina lake bure.” 

Wengi wanazani kwamba tunafanya hivyo wakati tunapofanya kiapo, ama laana. 

Siyo ile inayosemwa hapa.

Wao kama watoto wa Mungu, walikuwa wanaitwa kwa jina la Mungu, kwa hivyo, iliwapasa wao kuheshimisha kwa njia ya ukujazi, Jina la Mungu. 

Kila wakati walipokuwa wakifanya neno lolote lililokuwa likizaraulisha Jina la Mwenyezi Mungu, kwa wakati ule, wao walikuwa wakitaja bure Jina la Mungu, fahamu hapo tunasema Mungu. 

Kumbukeni maneno Mutume Paulo alikuwa akisema juu yao: 

Kwa njia yenu, wapagani wanalaani na kutukana Jina la Mwenyezi Mungu. 

Waroma 2: 24  

“Kwa maana Jina la Mungu linatukanwa katikati ya Mataifa kwa sababu yenu, kama ilivyo andikwa.” 

Ni kusema kwamba: 

Mataifa waliona namna gani mwenendo ya wana wa Mungu ilikuwa mbaya sana na ya ukorofi hata kufika kiwango wapagani waanze kusema, basi kama watu hawa wanafanana na Mungu wao, nikusema Mungu wao hawezi kuwa mutakatifu. 

Basi kama ilikuwa hivyo kwa watoto wachanga waliokuwa chini ya sheria, 

Je yapasa kuwa kwetu sisi tunaoitwa wana wa Mungu, watoto wa Mungu wanaokuwa sasa watu wenye tayari wamekwisha kukomaa? 

Twapasha kweli kufanya angalisho tusitukanishe Jina lake Mungu. 


12/ Turudi kwa neno linalousika kufanywa kuwa wana. 

Tayari sisi tuna hali hilo, lakini tutaumiliki na ukamilifu wote wakati wa ufufuko wetu.  

Waroma 8: 23 

“Wala si hivyo tu, lakini sisi wenyewe tulio na malimbuko ya Roho, sisi vilevile tunaugua ndani ya roho zetu, tukitazamia kuwekwa kama wana, ndiyo ukombozi wa mwili wetu.” 

Siku moja tutapata ukombozi wa mwili wetu. Nani awezaje kujua kama siku hiyo ni karibu sana na leo? 

Waza sasa wakati tutafikilia kwa hali hilo linalosemwa katika Waroma 8: 23, ukombozi wa mwili wetu.


13/ Neno la kwanza tupaswalo kufahamu ni kwamba ufufuko wa miili yetu inaambatana na Ufufuko wa Mwili wa Bwana wetu Yesu Kristo. 

Kwa kweli ufufuko wa miili yetu unaungana na Bwana wetu Yesu Kristo. 

Wafilipi 3: 20 – 21 

“Kwa maana sisi ni wenyeji wa mbinguni; kutoka pale tunangoja Mwokozi, Bwana Yesu Kristo; 

Atakayebadilisha mwili wetu wa haya upate kufanana na Mwili wake wa Utukufu, kwa uwezo ule unaoweza kutiisha vitu vyote viwe chini yake.” 

Hapa kuna mawazo inayo nifurahisha na kunipa raha sana moyoni mwangu, na kwa asubui ya leo nitawapasha wazo lile. 

Badala ya alama za vidonda vilivyokuwa kwenyi Mwili wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, sijuwe kitu gani kingine kinachoweza kweli kuvuta mafikili yetu, na kweli wakati wa ufufuko wetu hakutakuwa hata jambo moja la kulinganisha na alama hizo. 

Hii ni wazo la muhimu kweli! 


14/ Miili zetu, kwa kweli zitakuwa zenye kuwezekana kupapaswa. 

Tuchunguze sasa Ufufuko wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, ili tufahamu nini inayofunuliwa kwetu juu ya Mwili wa Bwana wetu Yesu kristo alipo fufuka. 

Ilikuwa Mwili unaowezekana kupapaswa, mwili kweli wa kawaida, na tena ilikuwa mwili usiokuwa chini ya sharia na nguvu ya arzi inayokumba na kutawala vifaa vya kimwili. 

Tunajuwa kwamba Mwili wake ulionekana na mecho ya kibinadamu. 

Yoane 20: 20 

“Naye akikwisha kusema maneno haya, akawaonyesha mikono yake na mbavu zake. Basi wanafunzi wakafurahi wakati walipoona Bwana.”

Wanafunzi walifurahi wakati walipoona Bwana. 

1Wakorinto 15: 5 - 7  

“akaonekana na Kefa, tena na kumi na wawili; 

Kiisha alionekana na ndugu zaidi ya mia tano pamoja, katikati ya hao wengi wanaishi hata sasa, lakini wengine wamelala. 

Kiisha alionekana na Yakobo; tena na mitume yote.” 

Walimuona Bwana Yesu Kristo, wakahakikisha kwamba ni Yeye Bwana wetu Yesu Kristo. 


15/ Ilikuwa Mwili wenye mikono ya kibinadamu iliweza kugusa.

Ma mitume walishikwa na wago wakati Bwana Yesu alipo jitokeza na kuoneka katikati yao, walizania wanaona pepo. 

Luka 24: 39 Lakini Bwana Yesu Kristo aliwaambia: 

“Tazameni mikono yangu na miguu yangu ya kuwa ni mimi mwenyewe. 

Munipapase, mutazame: kwani roho haina mwili na mifupa, kama munavyoniona mimi kuwa nayo,” 

Ilikuwa Mwili iliyoweza kupapaswa na mikono ya watu. 


16/ Hiyo hiyo aya inatuonesha kwamba mwili huo ulikuwa na sauti inayoweza kusikilika na masikio ya wanadamu. 


17/ Wakati Bwana Yesu alionekana kwa mara ya tatu kwa wanafunzi wake, kiisha ufufuko wake; wanafunzi walikuwa wakirudia pwani kiisha kutumika usiku kutwa bila kupata hata samaki moja. 

Yoane 21: 12 

“Yesu akawaambia: Kujeni kwa chakula. Na hapana mmoja wa wale wanafunzi aliyesubutu kumwuliza: Wewe ni nani? Wakijua ya kama alikuwa Bwana.” 

Bwana Yesu aliwaamuri watupe ndoani zao kwa mukono wa kuume, na kwa gafla walinasa samaki nyingi sana. 

Na wakati walipofika pwani, walikuta Bwana Yesu anawasha moto, na juu ya moto samaki ilikuwa ikichomwa, na aliwakaribisha waje wale.

Ni kwa hiyo tunapashwa kufahamu ya kuwa Mwili wenye Bwana Yesu alikuwa nawo kwa ufufuko ni mwili wenye uliweza kula chakula, na Yeye kweli alikula chakula na Mwili huo.  


18/ Kuna umbalimbali mwingine kati ya Mwili wenye Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo aliokuwa nawo pa ufufuko na mwili tunao siku hizi.

Tunaweza kuhakikisha neno hili kupitia maandiko mbalimbali tunayopata katika Agano Jipya. 

Kwanza, wakati wamalaika wawili walipo zunguusha hiyo jiwe kubwa iliyowekwa kwa kaburi kwenye Mwili wa Bwana Yesu Kristo ulipolazwa, haikukuwa kwa kwa kuruhusu Bwana Yesu atoke toka kaburi, lakini ilikuwa kwa kuruhusu mitume wapate kuingia na kuona ndani ya kaburi. 

Bwana Yesu alifufuka na hakuna hata sheria moja ya nguvu za azri iliyoweza kuzuia Mwili wake. Yeye alipita kati ya ukuta na alionekana mwenye kutambulikana. 

Mwili wake ulikuwa ukizunguushwa ndani ya nguo ya kitambaa ya bei kali yenye madoamadoa yenye aliovikwa saa ya kuzikwa.

Lakini alipofufuka alipita ndani ya nguo hiyo ya kitambaa, na nguo hiyo ilibaki pale na umbo ileile, lakini ndani yake mulikuwa utupu, hakukukuwa tena mwili ndani yake. 

Kiisha kupita kati ya hiyo nguo na kupita kati ya ukuta ya kaburi, Bwana Yesu alienda kutokea wanafunzi katika chumba cha juu, mahali walipokuwa wakikusanyika kwa kujificha kwa woga ya wayuda. 

Yoane 20: 19 

“Basi mangaribi ya siku ile ile, ikiwa siku ya kwanza ya juma, wakati milango ilipofungwa pahali walipokuwa wanafunzi kwa sababu ya kuogopa Wayuda, Yesu akakuja, akisimama katikati, akasema nao: Salama kwenu.” 

 

19/ Umbalimbali mwingine kati ya Mwili Bwana Yesu aliokuwa nao pa ufufuko na miili tulio nazo sasa, tunaupata kwa kulinganisha aya mbili ya maandiko katika Agano Jipya. 

Katika sura inayozungumuza juu ya ufufuko, Mutume Paulo anaandika katika   1Wakorinto 15: 49 - 50 

“Na kama tulivyochukua sura ya yule wa udongo, vivyo hivyo tutachukua sura ya yule wa mbinguni. 

Basi ninasema hili, ndugu zangu, ya kwamba, nyama na damu haziwezi kuriti ufalme wa Mungu; wala kuoza kuriti kutokuoza.” 

Katika kufa, 

DAMU YA BWANA NA MWOKOZI WETU YESU KRISTO ILIONDOSHWA NDANI YA MWILI WAKE. 

Wakati alipofufuka toka wafu, aliambia wanafunzi wake waliokuwa na ubishi: 

Muniguse na muone kwamba roho haiweze kuwa na nyama na mifupa kama mimi ninao. 

Luka 24: 39 

“Tazameni mikono yangu na miguu yangu ya kuwa ni mimi mwenyewe. 

Munipapase, mutazame,; kwani roho haina mwili na mifupa, kama munavyoniona mimi kuwa nayo,” 

Furaha gani kuona namna maneno inayosemwa katika aya hizi mbili na kuambatana kabisa, ikionyesha namna ufunuo yenye Baba Mungu anatufunulia juu ya Mwana wake yote inaenda sawa bila kukanushana. 


20/ Umbalimbali mwingine kati ya Mwili wenye Bwana Yesu alikua nao pa ufufuko na miili tunazo kwa siku za leo ni kwamba Mwili wake haukuwa tena na hali ya kuharibika na kuoza, sawa vile miili yetu iko leo. 


21/ Umbalimbali wa mwisho kati ya Mwili wenye Bwana Yesu Kristo alikuwa nao pa ufufuko na miili tunazo kwa siku za leo, ni kwamba YEYE ALIKUWA AKITEMBEA NA KUTOKA HAPA NA PALE BILA KUSHIKWA NA NGUVU ZA AZRI NA AKIWA NA KASI AMA UPESI WA MAWAZO. 

Yoane 20: 17 

“Yesu akamwambia: Usiniguse kwa sababu sijapanda kwa Baba yangu; lakini kwenda kwa ndugu zangu, ukawaambie: Ninapanda kwa Baba yangu na Baba yenu; na kwa Mungu wangu na Mungu wenu.” 

Asubui mapema ya siku ya ufufuko wake Yeye alikutana na Maria na alimwambia: Usiniguse kwa sababu sijapanda kwa Baba yangu. 

Kiisha magaribi ya hiyo hiyo siku alitokea wanafunzi wake na aliwaambia: Muniguse. 

Luka 24: 39 

“Tazameni mikono yangu na miguu yangu ya kuwa ni mimi mwenyewe. 

Munipapase, mutazame,; kwani roho haina mwili na mifupa, kama munavyoniona mimi kuwa nayo,” 

  Inataka kusema ya kwamba: 

Punde tu alipoambia Maria: Usiniguse na wakati alipoambia mitume: munipapase. Yeye alipaa juu mbinguni na kurudi. 


Tunafahamu ya kuwa katika kitabu cha Matendo 1: 10, 11 Yeye alichukuliwa toka macho ya mitume, 

“Walipokuwa wakikaza macho mbinguni, Yeye alipokuwa akikwenda zake, tazama, watu wawili wenye nguo nyeupe wakasimama karibu nao, 

Wakisema: Ninyi watu wa Galilaya, kwa sababu gani mumesimama mukitazama mbinguni? 

Huyu Yesu aliyechukuliwa toka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja namna hii sawasawa mulivyomwona akikwenda zake mbinguni.” 

Tunafahamu kwamba kwa nyakati yakupokelewa sawa wana tutakuwa na mwili wa ufufuko, unaofanana na Mwili wake ambao unaweza kuonekana na mecho, unaweza kupapaswa, hata kusikilikana na wenye unaweza kutumia chakula, mwili unaokuwa na nyama na mifupa. 

Mwili unaoweza kupita ndani ya vitu vinavyokuwa hali ya vifaa, na wenye uwezo wa kutoka hapa na kwenda pale kwa haraka na mbio ya mawazo. 


22/ 1Wakorinto 15: 43 

“Unapandwa katika haya; unafufuliwa katika utukufu: Unapandwa katika uzaifu, unafufuliwa katika uwezo;” 

Mutume Paulo anasema kwamba mwili unapandwa katika uzaifu, na unafufuliwa katika uwezo. 

Hakuna mabishano inayoweza kuwa kuhusu uzaifu wa maiti: 

Hata kama mwili fulani ulikuwa wa mwanamichezo mkubwa, hauwezi tena kushindana kwa mbio, ama kushindana, ama kucheza muchezo wa ngumi, ama kucheza mupira. 

Lakini ufufuko utakuwa katika mwili wa uwezo, hata kama mutu huyo alikuwa kilema asiye hata na tegemeo lolote, mwili utakuwa na nguvu zote inayoweza kufanya kila lile lenye mtu kamili anaweza kufanya. 

Itakuwa sawa Mwili wa Mwana wa Milele wa Mungu. 


Amina. 


N°Réf: 08/20/1961 / 312 - WHO HAS THE RIGHT TO CALL GOD FATHER / July 20, 2020