Tuesday, March 3, 2020

WAKATI MUNGU ANAPENDEZWA NA SIFA / WHEN GOD LOVES BOASTING


Photo by B. Smith from our kitchen window




     WAKATI MUNGU ANAPENDEZWA NA SIFA 
     WHEN GOD LOVES BOASTING
     Pastor Henry F. Kulp 
     August 30, 1964 



Waroma 5:  11 - 14 
“Wala si hivyo tu, lakini tunafurahi katika Mungu kwa Bwana wetu Yesu Kristo, kwa yeye sasa tumepokea upatanisho. 
Hivi, kama kwa mutu mumoja zambi iliingia ulimwenguni, na kufa kwa njia ya zambi; na hivi kufa kulikuja juu ya watu wote, kwa sababu wote wamefanya zambi:- 
Maana mbele ya sheria zambi ilikuwa ulimwenguni; lakini zambi haihesabiwi wakati sheria isipokuwa. 
Lakini kufa kulitawala tangu Adamu mpaka Musa, hata juu ya watu wasiofanya zambi kama alivyofanya Adamu, aliye mfano wake yeye atakayekuja.” 
         Hapa tunaambiwa ya kwamba, “wala si hivyo tu, lakini tunafurahi katika Mungu kwa Bwana wetu Yesu Kristo.” 
Maana ya neno kufurahi katika ni nini? 
Jameni niwape neno moja la kigriki inayo fanana na hii na tunaipata ndani ya waraka wa Mutume Paulo kwa Waefeso 2: 8 - 9  
“Kwa maana mumeokolewa kwa neema kwa njia ya imani, wala neno hili halikutoka ndani yenu wenyewe, ni zawadi ya Mungu, 
Si kwa matendo, asiwe mutu atakayejisifu.” 
         Tunapata kabisa kabisa hiyo hiyo neno moja. 
Hapa Mungu anatuambia kwamba kusiwe mutu atakayejisifu. 
Lakini katika Waroma 5: 11, sisi vilevile tunajisifu katika Mungu, tunaambiwa kwamba tujisifu. Na hiyo inaonekana kuwa kama umbalimbali, sivyo? 
Lakini siyo vile kama tukichunguza kweli katika hali gani neno hili linasemwa. 
1/ Hii inatusukuma kweli kuwa na zoezi ya kujiuliza mara kwa mara kwamba Maandiko Matakatifu yameandikwa katika hali na nyakati gani.  
Acha niwahakikishie neno moja munalopaswa kufahamu leo. 
Mimi siko muhubiri anayependa kujitetea kwa kusambia Neno la Mungu. Mungu hakuniita ili niwe nasambia Neno lake, lakini ili nitangaze Neno lake. 
Neno lake ni Timilifu na Sambamba na lenye Uhaki. Haina haja ya mimi nifanye masambo juu yake. Kyenye anahitaji kwangu ni kuitangaza. 
Mimi ni mutu anayepashwe kufahamisha watu wasikie maneno ya Mungu na ile ni kwako wewe vilevile. 
Ndani ya Biblia hakuna neno linalopinga neno lingine. 
Mungu anaweza kuwa na mapangilio yake mbalimbali kwa nyakati mbalimbali na iyo inafahamishwa hapa, anaposema katika Waefeso 2: 8 - 9
“Kwa maana mumeokolewa kwa neema kwa njia ya imani, wala neno hili halikutoka ndani yenu wenyewe, ni zawadi ya Mungu, si kwa matendo asiwe mutu atakayejisifu.” 
         Hatunabudi kujisifu wenyewe, hatuwezi kujisifu kwamba sisi tulitimiza ama kufanya jambo fulani, lakini hapa inabidi tujisifu katika Mungu. Tujisifu kwa kazi Mungu alitimiza kwa ajili yetu. 

2/ Sasa tuone kwamba katika hii kitabu cha Waroma 3: 27
“Basi wapi tena kujisifu? Kumefungwa inje. Kwa sheria gani? Kwa matendo? Hapana! Lakini kwa njia ya sheria ya imani.” 
         Jameni, mumekwisha kutizama kijana mutoto mdogo wakati anapovua viatu vyake vya namna ya godio ama boti? Anashika viatu vyake na kuvibulula kwa nguvu zote, anapiganisha kuvivua mpaka mishipa yote kichani mwake yanasimama na kuonekana kwamba yanavimba na kwa mwisho kweli, anashindwa na wewe unamwambia mtoto, haufahamu kwamba nguvu za arzi nazo pia zinabulula hii kiatu yako ngambo ya chini na nguvu kuliko ile unayotumia ngambo ya juu? 
Ni udanganyifu kweli na kutokufahamu wakati mtu anajaribu binafsi kupanda juu mbinguni kwa matendo yake na mambo yake na hali nzuri anayo kwa nguvu zake. 
Zaburi 40: 2, 3   
“Akanipandisha vilevile toka shimo ya uharibifu, toka udongo ulio mterezi, 
Akaweka miguu yangu juu ya mwamba na kushimamisha hatuwa zangu. 
Ameweka wimbo mpya kinywani mwangu, hata sifa kwa Mungu wetu; Watu wengi wataona na kuogopa, Na watawekea Bwana tumaini lao.” 


Waimbaji maalum wenye kujulikana na watu wote wanapendelea kuimba nyimbo kama SABABU YANGU, MIMI MWENYEWE, NIMEFIKA HAPO KWA NGUVU YANGU, NIMEJIINUA NA KUJIFANYA MKUU MIMI PEKE YANGU.
Mbinguni hakuta kuweko hata wimbo moja inayofanana na nyimbo zile. 
Wimbo wenye waliokombolewa wataimba, haitakuwa hata na kumbukumbu moja juu ya huduma na mambo tuliofanya, kazi na tabia nzuri tulizofanya duniani, lakini tutakuwa tu tukimutukuza na kumushangilia Mwenyezi Mungu na sifa tukimutukuza juu ya kazi aliotenda juu yetu sisi.  
3/ Katika Zaburi 40: 3, tunasoma: 
“Ameweka wimbo mupya kinywani mwangu, hata sifa kwa Mungu wetu; 

Watu wengi wataona na kuogopa, na watawekea Bwana tumaini lao.”
         Na ukakwenda tena kwa Zaburi 34: 2 utasoma:
“Nafsi yangu itajisifu katika BWANA, wapole watasikia na watafurahi.” 
         Neno kusifu na neno kutukuza ina shina moja katika kihebrania. 
Yote miwili ina maana moja. Kusifu ni kutukuza na sisi tunatukuzwa ndani ya Bwana, hapana ndani yetu binafsi. Kujisifu sisi wenyewe inatupwa mbali, lakini kujisifu ndani ya Bwani ni ile inaitajika. 

4/ Ningetamani musikilize wimbo wenye Musa alioimba, baada ya wana wa waisraeli kuvuka bahari nyekundu. 
Munatamani kuona jinsi ya kujisifu ndani ya Bwana?
Ni kama ifwatavyo: 
Kutoka 15: 11 
“Nani ni kama wewe, Ee Bwana, katikati ya miungu?
Nani ni kama wewe, mwenye utukufu kwa utakatifu? 
Mwenye kuogopwa katika sifa zake akifanya maajabu? 
         Sikilizeni sasa wimbo wa HANA baada ya Mungu kumuagiza kwamba atazaa Samweli. 
1 Samweli 2: 1 - 2 
“Hana akaomba, akasema: 
Moyo wangu unashangilia BWANA, 
Pembe yangu imetukuzwa katika BWANA;
Kinywa changu kimeongezeka juu ya adui zangu, kwa sababu ninafurahi katika wokovu wako. 
Hakuna mmoja Mtakatifu kama BWANA;
Hakuna mwingine ila wewe; 
Wala hakuna mwamba kama Mungu wetu.” 
         Musa anamsifu Mungu mwenye uwezo. Hana anashangilia ndani ya Mwenyezi Mungu na anatukuza faraja yake takatifu. 
Nasi vilevile tunapashwa kujisifu ndani ya Mungu wetu. 

Jameni niwaoneshe namna gani kujisifu kwa namna ile. 
Kuna neno moja nzuri na ya muhimu tunayoweza kupata katika waraka wa Waroma.

5/ Katika sura ya kwanza, ya pili na ya tatu ya kitabu cha Mtume Paulo kwa Waroma, Mwenyezi Mungu anatuonesha wazi kwamba sisi ni wenye zambi, tunapotea na hatuko wakamilifu, tukisoma katika Waroma 3: 19 
“Na tunajua ya kama maneno gani inayosema sheria, inasema kwao walio chini ya sheria; kusudi kila kinywa kifungwe, na ulimwengu wote uwe chini ya hukumu ya Mungu.” 
         Hapa tunaambiwa kwamba zambi ilitufunga sote vinywa. Zambi inatusukuma sote tukae kimya mbele ya uwepo wa Mungu. Zambi ilifunga kila kinywa cha mwanadamu, kinywa cha yeyote ule alieumbwa, kwa maana wote wamehukumiwa. 
Tukianza sasa na Waroma 3: 24  
“Wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Yesu Kristo:” 
         Tuna wokovu Mungu anayotupatia katika Bwana Yesu Kristo, na wakati tunamwamini Bwana Yesu Kristo kuwa Mwokozi wetu, anafunguwa vinywa vyetu na kila kinywa cha mwamini kinakuwa wazi na kinafunguliwa ili tuimbe kwa sauti kubwa nyimbo za shangwe na sifa kwa Bwana wetu Yesu Kristo, tukijisifu katika Yeye. 
Mwamini hakuzaliwa bubu. 
Hakuna hata mtoto moja alietupwa ndani ya jamaa ya Mungu. 
Tulikuwa zamani wapotevu, wenye kusongwa na wenye mizigo ya zambi, lakini Mungu aliweka wimbo mupya katika mioyo yetu. 
6/ Jameni niwaoneshe neno moja ambalo litatusukuma tuimbe. 
Mimi siweze kujifunga kumwimbia wakati wowote ninaposoma haya hii. 
Wakati ninaposoma aya hii, roho yangu inajaa na furaha na kushangilia kupita kipimo. 
Waroma 5: 20 
“Lakini sheria iliingia ili zambi ziwe kubwa sana; lakini pahali zambi zilipozidi, neema ilizidi zaidi sana:” 
         Ninauhakika kama mutanisadikia kwamba zambi ni neno ngumu. 
Kama Mwenyezi Mungu angiwapa hali ya maajabu ya kuwa na uwezo wa kutazama mambo yanayopitikana chini ya juwa katika dunia nzima, kwa nyakati fulani na awawezeshe kuona uwingi wa upotevu na zambi unaofanyika kwa wakati ule ndogo, najuwa kwamba utatowa sauti kubwa ya masikitiko na kusema: zambi na upotevu inajaa sana dunia, na kweli ni hivyo. 
Lakini, Mungu anasema sasa, kwa umbalimbali kulingana na kushangaa kwako na malalamiko yote, Mungu yeye anasema Neema inazidi zaidi sana. 
Mwenyezi Mungu hatumikishe hiyo neno lenye tunapata katika kigriki wakati tunataka kusema kwamba neema inazidi zaidi sana. 
Lakini musemwa, zaidi sana, hapo ndiyo neno la kigri inayo maanisha zaidi kuliko. Ni neno tunayopata katika sayansi ya hesabu kwa kuonesha jumla kubwa kupita jumla zote.    
Mungu anasema kwamba zambi inaanza kuwa nyingi , lakini Neema inazidi kuwa kubwa zaidi sana , na anatumikisha, neno zaidi  mbele ya kubwa,  ili kumaanisha neno lenye litakuwa kubwa mara na mara  kuliko lile linalotajwa  na kuendelea tena kupata muzunguuko unao endelea mara na mara. Nikusema wakati zambi zitazidi, Neema itazidi kuwa kubwa zaidi sana.
 Nikusema Mungu hajali na uwingi wa zambi unaozidi kuwa nyingi sana sababu Mungu alitayarisha Neema inayozidi kuwa kubwa zaidi sana kupita hiyo uwingi wa zambi. 
Utukufu na shangwe kwa Mwenyezi Mungu kwa sababu Neema yake inazidi kuwa kubwa zaidi kwa kiwango kinachotosha kwa zambi nilizokuwa nazo katika maisha yangu  na ni hii inanisukuma nijisifu katika Mungu wa Milele hapana katika mimi binafsi. 

7/ Tunafika sasa kwa maandiko ya Waroma 5: 12 - 14  
“Hivi, kama kwa mtu mmoja zambi iliingia ulimwenguni, na kufa kwa njia ya zambi; na hivi kufa kulikuja juu ya watu wote, kwa sababu wote wamefanya zambi:-
Maana mbele ya sheria zambi ilikuwa ulimwenguni; lakini zambi haihesabiwi wakati sheria isipokuwa. 
Lakini kufa kulitawala tangu Adamu mpaka Musa, hata juu ya watu wasiofanya zambi kama alivyofanya Adamu, aliye mfano wake yeye atakayekuja.” 
         Hapa Mtume Paulo anatuingiza sasa kwa ukweli ungine wa maana sana. 
Neno lile lilikuwa bado kujulikana hadi kufika kwa aya hii ya Waroma.
Tuone vema kwamba inasema: 
“Hivi, kama kwa mtu mmoja zambi iliingia ulimwenguni, na kufa kwa njia ya zambi; na hivi kufa kulikuja juu ya watu wote,” 
Kwa kweli hii ni ukweli wenye uko nguvu sana kuufahamu. 
Ni kwa sababu hiyo watu wanakufa si kwa sababu wamefanya zambi, lakini sababu Adamu alifanya zambi.
Kama watu wa maumbile ya kibinadamu wangelikuwa wanakufa kwa sababu ya zambi zao, basi, watoto wachanga hawange kuwa wanakufa, sababu mpaka hapo wao hawakufanya hata zambi moja. 
Hii njo tunayoita ukweli wa KUWA PAHALI PA. 
Wanadamu wote wanakuwa wakionekana ndani ya mtu mmoja. 
Ninajiuliza na kuwaza namna gani munajiuliza kwamba kama ni halali watu wote wawe ndani ya mtu mmoja alie Adamu?
Siyo haja kwangu na kwako kupenda kufanya mabishano na Mungu. 
Maneno Mungu anayoyasema yanasimama, ni ya kweli na yanabaki hivyo hivyo. 
8/ Sasa tuone jambo lingine mupya kwa hii tu sehemu ya maandiko katika haya ya 12. 
Hivi, kama kwa mutu mmoja zambi iliingia duniani, na kufa kwa njia ya zambi; na hivi kufa kulikuja juu ya watu wote, kwa sababu wote wamefanya zambi:-
Maana mbele ya sheria zambi ilikuwa ulimwenguni; lakini zambi haihesabiwi wakati sheria isipokuwa.  
         Tangu kuumbwa kwa dunia na vyote vilivyomo kufika mpaka wakati wa Musa, sheria haikukuweko.
Tangu kuumbwa kwa dunia mpaka wakati wa Musa, Mwenyezi Mungu hakuambia ulimwengu: usiuwe. 
Kiisha garika, Mungu alipatia Musa uwezo wa kushurtisha malipizi ya kipekee. Ni mambo haya tu njo wenyezi Mungu alipana toka nyakati za Adamu hadi nyakati za Musa. 
Mungu hakumwambia mwanadamu kwamba: usidanganye, usiibe, usitamani. Watu walitenda zambi, na walipotenda zambi, hakukukuwa bado malipo ama malipizi, Sababu Mwenyezi Mungu alikuwa hajatoa hukumu yeyote juu ya zambi. 
Sasa unaweza jiuliza, namna gani hawa watu wote walifariki basi? 
Walikufa sababu Adamu alitenda zambi. Sawa vile aya ya kumi na mbili inatuambia. 
“Hivi, kama kwa mutu mmoja zambi iliingia duniani, na kufa kwa njia ya zambi;” 
         Katika Adamu wote wanakufa hata kama hawakufanya zambi, sababu Adamu alikufa, sote tulipashwa kufa sababu Adamu alifanya zambi, sisi sote ni wenye zambi ni sababu ya iyo njo tunakufa. 

9/ Unaweza jiuliza tena eti mambo yale ni halali? 
Kwa kweli ni hivyo, acheni niwaoneshe sehemu iliyo ya shangwe na utukufu katika miradi hiyo. 
Katika nyakati za kale Mwenyezi Mungu alikuwa na Mupango. 
Ilikuwa mapangilio ya utukufu. 
Mpango wenye tunapashwa kufahamu leo. 
Mpango wenye Mwenyezi Mungu alikuwa nao ni kwamba sisi sote tungepashwa kupotea ndani ya mtu moja, na pia sisi sote tungepashwa pata wokovu ndani ya mtu mmoja. Hapa ninataka maanisha nini? 
Tusome aya ya kumi na ine (14). 
“Lakini kufa kulitawala tangu Adamu mpaka Musa, hata juu ya watu wasiofanya zambi kama alivyofanya Adamu, aliye mfano wake yeye atakayekuja.”   
         Hamuoni ya kwamba kama kila mutu angelikufa juu ya zambi zake, ingelibidi Bwana Yesu akufe mara na mara kwa kila mutu moja binafsi ili kila mutu apate wokovu. 
Lakini, kuona ginsi ulimwengu mzima ulipotea katika mtu mmoja vivyo hivyo ulimwengu wote unaweza okolewa kwa njia ya mtu mmoja. 
Adamu ndiye yule tunaye ita kichwa chetu kikuu ama kichwa chetu cha musingi. 
Mwenyezi Mungu aliweka ulimwengu wote ndani ya Adamu, kwa hiyo, ulimwengu wote ulianguka na Mungu alikuwa na Mpango kwamba ulimwengu wote ungepata wokovu kwa njia ya mtu mmoja yule mutu KRISTO YESU. 

10/ Waroma 5: 19 Ingelikuwa heri mutambue kabisa uzuri wa sura hii ya Waroma. 
“Kwa sababu kama kwa kuasi kwa mtu mmoja watu wengi waliingizwa  katika hali ya wenye zambi, hivi kwa kutii kwake mtu mmoja, wengi wameingizwa katika hali ya wenye haki.” 
         Watu wote wameanguka katika Adamu, na watu wote wamekuwa watenda zambi. 
Hata watoto wachanga wanakufa na hiyo siyo sababu ya zambi zao binafsi. 
Watu wengi wanauliza ulizo hili, itakuwa namna gani mbinguni kuusu watoto wanaokufa wachanga? 
Watu wengi wamekwisha niuliza ulizo hili. 
Bwana Yesu alikufa juu ya ulimwengu wote mzima, watu wote wamepotea na neno itakayo onesha kwamba wamepotea milele ni kutokuwa pamoja na Bwana Yesu Kristo.

Hiyo ndiyo neno inayoonesha mtu asiye okoka. Huyu mtu anafika mbele ya kiti cha hukumu cha Mungu na baadaye anatupwa katika ziwa la moto. 
Hautatupwa motoni sababu ya wingi wa zambi zako lakini sababu la ulizo ili: Wewe ulifanya nini na mwito wa Yesu Kristo? 
Watoto wachanga hawawezi kupokea Bwana Yesu Kristo kama Bwana na Mwokozi wao. Na Bwana Yesu alikufa juu ya zambi zao na wakati wanafikia umri wa umutu wanaweza kukamata uhamuzi wa kumwamini Bwana Yesu Kristo kuwa Mwokozi wao. Ni kwa sababu ile ndiyo maana wakati mutoto anaanza fikisha hiyo umri wa umutu, sisi wazazi tuna wajibu wa kumuleta na kumuonesha njia ya Mungu na kumuleta kwa Yesu Kristo. 
Wataalamu wanasema kwamba jumla 51 kwa mia ya watoto wachanga wano zaliwa katika China, wanakufa kwa mwaka wao wa kwanza wa kuzaliwa. 
Katika inchi ya Haïti ni watoto 8 juu ya kumi njo wanafariki kwa mwaka wao wa kwanza kiisha kuzaliwa. 
Watoto hawa wanaenda mbinguni. Kwa kweli hawabaki kama watoto mbinguni, wanakuwa wakubwa. 

11/ Ulizo kwako leo, jameni wawaza je juu ya hali yako ya mwenye zambi, eti wasadiki kwamba Bwana Yesu ni jibu kwa hali yako ya zambi? 
Wote wamefanya zambi katika Adamu, lakini katika Yesu Kristo wote wamevunja hali hiyo na wote wanakuwa walio HAI. 

12/ Yoane 16: 7 - 11  
“Lakini mimi ninawaambia ninyi kweli, Ni kwa faida yenu niondoke; kwa sababu kama siondoki, Msaidizi hata kuja kwenu; lakini kama nikikwenda, nitamtuma kwenu. 
Na wakati anapokuja, atahakikisha dunia maneno ya zambi, na maneno ya haki, na maneno ya hukumu; 
Kwa maneno ya zambi, kwa sababu hawaniamini mimi; 
Kwa maneno ya haki, kwa sababu ninakwenda kwa Baba na hamunioni tena; 
Kwa maneno ya hukumu, kwa sababu mkubwa wa dunia hii amehukumiwa.” 
         Hii ni zambi ya asili. Unajiuliza eti itakuwa namna gani kwa umati ma milioni ya watu wenye bado kusikia habari ya Yesu Kristo? 
Ni kwa ajili ya hii ndiyo maana tunakuwa na watu wanaojitoa kupasha habari njema kwa mainchi zingine. 
Ni kwa sababu hii ndiyo maana tunapashwa kuwa na huduma ya kubebea wengine Habari Njema ili watu wasikie Habari hii Njema Bora, ya Manufaa nay a Injili. 

13/ Ndugu, umeisha pata hamu ya kusoma barua ya Mutume Paulo kwa Waefeso, nenda kaone namna gani Mutume Paulo inasema juu ya jambo la kuwa ndani ya KRISTO. 
Tulizaliwa katika Adamu, lakini wakati tunaokoka tunakuwa ndani ya KRISTO. 
Waefeso 1: 3 
“Abarikiwe Mungu na Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye alitubariki kwa Baraka zote za roho katika pahali pa mbingu ndani ya Kristo;” 
         Inasemwa Baraka zote za roho ndani ya Kristo. 
Nini uliokuja nayo wakati ulipozaliwa? 
Nini uliriti toka Adamu wakati ulipozaliwa katika zambi? 
Na tena kwamba siku moja utakufa.
Hakuna kitu kingine ulichorizi kwa Adamu zidi ya zambi na kufa.
Ulizo ni kujuwa kama tayari umeishatoshwa ndani ya Adamu na kuwekwa ndani ya Yesu? 
Wakolosayi 3: 1 - 3 hapa wanatuambia ya kwamba:
“Basi mukiwa mumefufuliwa pamoja na Kristo, tafuteni maneno yaliyo juu, pahali Kristo yuko, akiketi kwa mkuno wa kuume wa Mungu. 
Tieni mafikiri yenu juu ya maneno ya juu, wala si juu ya maneno yaliyo dunuani. 
Kwa maana mulikufa, na maisha yenu yamefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.”  
         Tofauti kati ya mtu aliepotea na sisi tulio okolewa ni kwamba sisi tuko ndani ya KRISTO. 
Hakuna haja ikiwa sisi tunajisifu ndani ya Bwana Yesu. Tuna jambo la kujivunia ni Kazi Bwana na Mwokozi wetu alifanya juu ya Musalaba wakati alipolipa deni kubwa yetu ya zambi zetu pale Golgota.
Hatuna cha kujiuliza, wala hakuna shaka yoyote. Na hiyo inakanusha sisi kujisifu sababu ya utu wetu ama neno, desturi, tabia, kazi ama tendo lolote tulilofanya. 

AMEN 
N° Ref: 08/30/1964 / 278 - WHEN GOD LOVES BOASTING / 3/3/2020