Monday, February 17, 2020

PAHALI PATAKATIFU PA MWAMINI / THE BELIEVER'S SANCTUARY

Photo taken from B Smith's Kitchen Window







     PAHALI PATAKATIFU PA MWAMINI 
     THE BELIEVER’S SANCTUARY
     Pastor Henry F. Kulp
     January 3, 1965 


Waroma 8: 1 - 4 
“Sasa, basi hakuna hukumu ya azabu juu yao walio katika Yesu Kristo, wasiotembea kufuata maneno ya mwili, lakini kufuata maneno ya Roho. 
Kwa sababu sheria ya Roho ya Uzima ulio katika Yesu Kristo imenifanya huru kwa sheria ya zambi na kufa. 
Maana yale yasiyowezekana kufanywa kwa sheria, kwa sababu ilikuwa zaifu kwa sababu ya mwili, Mungu alituma Mwana wake mwenyewe katika mufano wa mwili ulio wa zambi, na kwa sababu ya zambi, alihukumu zambi katika mwili; 
Hata haki ya sheria itimizwe ndani yetu, tusiotembea kufuata maneno ya mwili, lakini kufuata maneno ya Roho.”  
         Hivi namna tunafikia sehemu hii kubwa ya maana na ya mafaa katika Maandiko Matakatifu inayoanza ama kufunguliwa na neno “hakuna hukumu ya azabu” na inafungwa na kukamilishwa na neno “Wala chochote kingine hakitaweza kunitenga na.”  
Katika haya yake ya kwanza kuna ukweli moja nzuri na ya samani kubwa na ningependa muifahamu katika umati na urembo wake wote.

1/ Nazani kwamba mugawanyo wa ma sura ya hii andiko ingekuwa nzuri tena zaidi kama ingetia hiyo ma haya yote ine ya sura nane pamoja na sura ya saba. Sasa hapo, tutumiye neno “mahakama” pa nafasi ya “hukumu ya azabu.” 
Sababu yote mbili ina musingi mmoja. Hivi musemwa huu utakuwa kama ifwatavyo: “Wenye wanaokuwa katika Yesu Kristo hawataenda tena mahakamani.” 
Ndugu eti wajuwa kama siku yako ya kwenda mahakamani imekwisha kupita? 
Hakuna tena siku yako ya kwenda mahakamani kama wewe umekwisha kuokolewa. 
Unajiuluza mara kwa mara, eti mimi sitaenda tena mahakamani? 
Kwa kweli hii haya inasema hivyo.
Waamini wenye waliookolewa hawata kuwa tena na siku ya kuhukumiwa kwa milele.  

2/ Jameni niwape ulizo. 
Itawezekanaje wao walio hesabiwa haki wapite tena kwa hukumu juu ya kuhukumiwa milele? 
Ninasema mara tena ili muweze kukumbuka HAYA: 
KUWA MWENYE HAKI NI TENDO LA MUNGU MWENYEWE KUHESABIA HAKI MUTU MWENYE ZAMBI NA KUMUONA KUWA MKAMILIFU WAKATI MUTU HUYU ANGALI BADO NA MAKOSA. 
Waroma 4: 5  
“Lakini kwa mtu asiyefanya kazi, lakini anamwamini yeye anayehesabia haki wasioogopa Mungu, Imani yake inahesabiwa kuwa haki.”
Waroma 4: 17 
“(Kama ilivyoandikwa: Nimekuweka baba ya mataifa mengi) mbele yake aliyeamini, Mungu anayewapa wafu uzima, na anayeita vitu visivyokuwa kama vimekuwa.” 
         Mungu anahesabia vitu visivyokuwa kama vimekuwa.
  
3/ Tuchunguze na kuona kwamba katika hii maandiko tunayoyasoma kuna jambo la nyakati. 
“SASA” 
Sasa, basi hakuna hukumu ya azabu. 
Tukijuwa na kutiya mioyoni mwetu kwamba kwa siku zijazo hakuta kuwa mahakama ama hukumu ya azabu kwetu sisi, ni jambo la furaha na shangwe. 
Lakini, ukweli wa haya hii tunayosoma inasema: Hakuna tena mahakama ama hukumu ya milele kwetu sisi leo, kwa sasa. 
Ndugu yangu, wewe wawaza kwamba Mwenyezi Mungu anaweza kuwa na uvuguvugu kwa hali ya kuhesabia haki kila mwenye anayeamini Bwana Yesu Kristo? 
Kama mutu mlevi sana anayeponeshwa kwa kifo mbele ya saa moja na anabaki na uhai sababu yeye alimuamini Bwana Yesu Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wake, hakuna hukumu ya azabu kwake kwa ile saa. 
Yeye anaweza kuwa ameumwa kichwa ama maumivu mengine kazaa,  kuumwa kwake kwa kichwa kunaweza kuendelea kwa ma saa machache, lakini kwa mutu huyu, hakuna hukumu ya azabu kwake kwa saa ile. 

Tukamate mfano wa huyo mlinzi wa gereza kwa Filipi. Kwa saa ile alipokubali Bwana Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wake, hakukukuwa tena  na hukumu ya azabu juu yake hata kama upanga aliopenda kujizuru na kujiuwa nawo  hapo mbele kidogo, ulikuwa ukishikwa  mukononi mwake.   
Matendo ya Mitume 16: 27  
“Mlinzi wa kifungo, akiamka na usingizi, aliona milango ilikuwa wazi, akatoa upanga wake, akataka kujiua mwenyewe, akizani ya kama wafungwa wametoroka.” 

4/ Wakati ungetambua na kuona umuhimu wa ukweli huu, ndugu yangu ungelipaza sauti ya shangwe na furaha.  
Jameni umekwisha kutazama kwenye televijeni sherehe ya watu wenye kuhusika na kuhudumia wengine kwa njia ya misaada mbalimbali na katika hiyo sherehe wanatayarisha mapambano ya mchezo wa mpira na kwa muda mrefu, hizo timu mbili zinazo pambana hata moja haijawai kutia mwenzake goli, umati wa wale wanaouzuria sherehe wakiwa maelfu ya watu, na kwa dakika makumi tatu za mwisho, timu hizi mbili zinaanza pambana kwa nguvu sana ili mmoja wao aingize hata goli moja tu. Shangwe gani na vigelegele kubwa katika kiwanza cha mpira wakati timu moja inaingiza goli.
Tazame shangwe hiyo kwa kitu kidogo kama mchezo wa mpira, sasa kwa kweli wakati unatambua umuhimu wa ukweli huu, ndugu, ingelikupasa kupaza sauti ya shangwe na furaha namna gani? 
Tena, kwa siku hizi magaribi, nyakati za uchaguzi, umekwisha kuangalia kwenye televijieni, namna watu wanakusanyika kwa kungojea matukio, umati wa watu wanaozunguuka ule aliyechaguliwa, watu wanapiga vigelegele na kushangilia kwa  sauti.  
Sasa kwetu sisi wachaguliwa wa Bwana, wakati tunafahamu kwamba hakuna tena hukumu ya azabu juu yetu, tunapaza sauti ya furaha namna gani?  
Mfano ungine, mimi binafsi sijawai kuhuzuria mchezo wa mbio ya ma farasi, lakini ninafikiri wakati farasi zinapiga mbio na wakati farasi moja inaanza tambuka mwenzake, kelele ya shangwe inasikilika toka wahuzuriaji ijapokuwa hiyo timu  itapata tu kiwango cha dolla makumi tano ama kupata kiwango fulani ya pesa yenye itatiwa katika hakiba yao. 
Neno hili inapashwa kuwa kwetu neno la kutupatia JUHUDI, kuona kwamba Hakuna hukumu ya azabu juu yao walio katika Yesu Kristo. 

5/ Haya hii inaanza na namna ya hakikisho katika luga ya kigriki. 
Kukanusha kwake kunaleta mkazo na maana zaidi. 
“hakuna” ama “hapana”  inaleta mkazo na  maana zaidi kama imetumikishwa mbele ya msemwa. 
Katika kigriki, mara kwa mara wanatumikisha neno hizi mbili juu ya kukanusha , wanatumikisha neno “our” na “me” 
Katika Biblia, utakuta mara moja moja haya maneno mawili yakitumikishwa pamoja. 
Katika vitabu vya injili utakuta kwa mara tano watu wanatumikisha namna hizi mbili za kukanusha kwa midomo yao, lakini watu ni wazaifu. 
Matayo 16: 22  
“Petro akamchukua, akaanza kumkemea akisema: Iwe mbali nawe, Bwana; neno hili halitatokea juu yako kamwe.”
         Hapa mutume Petro iko anaambia Bwana Yesu kwamba hatakufa, lakini Bwana Yesu alikufa. Tena Petro alitumikisha namna hizi mbili ya kukanusha wakati alipenda kuambia Bwana Yesu kwamba hatamusaliti kamwe.  
Matayo 26: 35 
“Petro akamwambia: Hata ikinipasa kufa pamoja nawe, sitakukana kabisa. Na wanafunzi wote walisema vivyo hivyo.” 
         Lakini Petro alimkana.
Lakini, tuangalie sasa wakati Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo alitumikisha hilo jambo ya kukanusha mara mbili, Katika Biblia Bwana Yesu alikanusha mara mbili kwa fasi makumi ine na sita (46), na tuwe na uhakika kwamba, wakati Yeye alikanusha mara mbili, ilikuwa ili ahakikishe kweli na tuwe na uhakika kwamba neno analolisema ni kweli. 
Kama Mungu anatuhakikishia kama neno ili ni Njema na Kweli, tuwe na uhakika kama ni hivyo. 
Matayo 24: 34, 35 
“Kweli ninawaambia ninyi, kizazi hiki hakitapita hata maneno haya yote yatakapotimia. 
Mbingu na dunia zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kabisa.” 
         Bwana Yesu alikuwa akisema: Maneno yangu hayatapita kamwe, na kweli maneno ya Bwana Yesu hayaja pita. 
Ubatili gani kwa watu ama kikundi cha watu wanaojikaza kutokufahamu na kutokutumikisha na kusadiki maneno ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, maneno aliyoyasema katika Waroma 8: 1 
“Sasa, basi hakuna hukumu ya azabu juu yao walio katika Yesu Kristo, wasiotembea kufuata maneno ya mwili, lakini kufuata maneno ya Roho.” 
         Haya ni masemi ya Bwana wetu Yesu Kristo Mwenyewe. 
6/ Tuone sababu gani hakuna hukumu ya azabu  kwa waamini
Kwa sababu sisi tuko ndani ya Bwana Yesu Kristo. 
Kama kwa sasa sisi tunapatikana ndani ya kanisa letu la fasi, jengo letu la fasi, ni nafasi kama desturi, vivyo hivyo, wote waliookolewa wako ndani ya KRISTO. 

7/ Hakuna hata kitu kimoja kinachoweza kufanya kama wewe uhukumiwe kwa hukumu ya azabu sababu zambi zako zote zilihukumiwa ndani ya KRISTO. 
Ndani ya KRISTO, uko katika nafasi kwenye hukumu imekwisha kufanyika na imeshindwa na kutupwa mbali haiwezi kufanyika tena, Mwenyezi Mungu amekwisha kuhukumu Bwana Yesu Kristo, alimuhukumu wakati Bwana wetu Yesu Kristo alifanyika kuwa kama zambi na Mwenyezi Mungu hata hukumu tena ile zambi kwa mara ya pili. 
Na kama wewe uko ndani ya KRISTO, wewe uko mahali penye hiyo hukumu ya azabu imeisha kufanyika kwa siku zilizo pita na wewe huwezi tena pata hiyo hukumu ya azabu. 

8/ Tuchepuwe na kufahamu kwa makini kabisa hii jambo la kusema yakuwa KRISTO alihukumiwa kwa ajili ya zambi zetu. 
Mutume Paulo ni Mutume wa Musalaba. 
Sijuwe kama wewe umekwisha kweli kufahamu neno hili, yakwamba  neno ama jina Musalaba haitumikishwe katika Baruwa  ama Waraka zingine zinazopatikana katika Biblia, isipokuwa tu ndani ya Baruwa za Mutume Paulo. 

Wakati mutume Petro alizungumuza juu ya kusulubiwa kwa Bwana Yesu Kristo, alisema, Alibeba zambi zetu katika Mwili wake juu ya muti. 
1 Petro 2: 24  
“Yeye mwenyewe alichukuwa zambi zetu katika mwili wake juu ya muti, hata sisi, tukiwa wafu kwa maneno ya zambi, tuwe hai kwa maneno ya haki; na kwa kupigwa kwake muliponyeshwa.” 
         Tuone tena ndani ya kitabu cha Matendo ya Mitume 
Matendo ya Mitume 5: 30 
“Mungu wa baba zetu alifufua Yesu, ambaye ninyi mulimuuwa mukamtundika juu ya mti.” 
         Kiisha twende kwa Matendo 10:39, 
Matendo ya Mitume 10: 39  
“Na sisi tuko washuhuda wa maneno yote aliyotenda katika inchi ya wayuda, na katika Yerusalema, ndiye walimwua, wakamtundika mtini.” 
Matendo ya Mitume 13: 29 pahali maandiko yanayosema kwamba: wakamshusha toka mti. 
Matendo ya Mitume 13: 29 
“Nao wakati walipokwisha kutimiza yote yaliyoandikwa juu yake, wakamshusha toka mti, wakamweka kaburini.” 
         Lakini Mutume Paulo alitumikisha jina ama neno MUSALABA, na kinachoshangaza ni kwamba Mutume Paulo hakusema maneno mengine ya kipekee juu ya neno hilo musalaba. 
Ni musalaba kama inavyoandikwa. 
Mutume Paulo hatuambie namna gani maneno yalipitika na kufwatana moja nyuma ya ingine pale kwa kalvari. 
Hatuadisie juu ya vidonda kubwa tano vya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 
Hatupashe juu ya taji la miiba, juu ya maneno saba ya mwisho yenye Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo alitamka pale musalabani, maneno yenye yanahubiriwa Zaidi wakati wa pasaka, Mutume Paulo hajawai kusemezana juu ya maneno yale. 
Wokovu wa yule mwizi juu ya musalaba, Mutume Paulo hakuzungumuza juu yake. 
Hakutuambia hata juu ya mambo yote kazaa na kazaa yenye ilipitikana, lakini yeye anahubiri MUSALABA. 
Yeye ni Mutume wa MUSALABA. 
Sababu MUSALABA, kwa Mutume Paulo, haimaanishe chombo kimoja cha mbao, ama mbao yenye walijenga nayo musalaba. 
MUSALABA kwa Mutume Paulo ni Kazi yenye Bwana Yesu alitimiza katika kufa kwake, ni hii Mutume Paulo iko anazungumuza juu yake. 

9/ Kwa sasa tuna neno la muhimu. 
Kwa kweli, Mutume Paulo anatuambia kazi gani Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo alifanya musalabani. 
Vitabu ine vya injili vinatuelezea historia yote ya maneno yaliyo pitikana wakati Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo alisulubiwa musalabani, lakini hakuna hata kitabu cha injili kimoja kinacho tuaambia maana ya Musalaba. 
Ni Mutume Paulo anayetuambia maana ya MUSALABA na kwa Mutume Paulo, MUSALABA ni Kazi yenye Bwana wetu Yesu Kristo alitimiza wakati alipokufa. Siyo musalaba kama vile jina ama namna ya kuandika.  

Musalaba kama jina yenye watu waliunda, musalaba kama namna tunayoijenga kwa mbao mbili; kwa siku hizi watu wengi wanaipatia mafaa sana. 
Watu wanatia misalaba ndogo ndogo katika makanisa, wengine wanajijengea musalaba wa zahabu na wanawake wanaivaa shingoni mwao kama ushanga, lakini hiyo musalaba siyo wokovu. 
Wokovu ni Kazi ya Mwokozi Yesu pale kwa Kalvari. Kazi aliyotimiza. 
Ni hasara sana na vibaya kuabudu musalaba kama kitu kilichoundwa, hiyo ni kuabudu miungu. 

10/ Katika Agano la Kale, wakati wana wa Israeli walikuwa wakifa kwa uwingi ndani ya ma kambi pale Israeli, 
Mungu alimuambia  Musa ajenge nyoka ya shaba na aiinuwe mutini na wowote ule aliinua macho yake na kutazama nyoka ile ya shaba aliponeshwa pale pale. 
Hesabu 21: 4, 5, 6.  
“Wakasafiri toka mlima Hori kwa njia ya Bahari Nyekundu ili kuzunguka inchi ya Edomu; na roho za watu zilitiwa  mashaka sana kwa sababu ya njia. 
Watu wakanungunikia Mungu na Musa: Kwa nini mumetuleta sisi toka Misri ili tufe katika jangwa? Maana hapana mkate na hapana maji; na nafsi yetu inachukia chakula hiki bure. 
Na Bwana alituma nyoka za moto kati ya watu, wakauma watu; watu wengi katika Israeli wakakufa.” 
         Watu walihuzunikia Mungu, na Mungu akatuma nyoka za moto kati ya watu, wakauma watu; watu wengi katika Israeli wakakufa. 
Ni baada ya hapo njo Mungu akamwambia Musa kufanya nyoka ya shaba na kumweka juu ya mti; na ilikuwa nyoka akiuma mtu ye yote, wakati alipoangalia nyoka ya shaba, akaishi.  
Hesabu 21: 8 
“Bwana akamwambia Musa: Ujifanyie nyoka ya moto na kumweka juu ya   mti; na itakuwa kila mtu aliyeumwa, wakati anapomwona ataishi.” 
         Na wana wa Israeli wakachunga ile nyoka muda wa miaka mia nane, 800, wakaanza hata kuabudu hiyo nyoka na hakukukuweko hata mutu mmoja aliyewaambia kwamba neno wanaolifanya ni kuabudu Miungu. 
Mpaka wakati Hezekia alipofika. 
Hezekia akatwaa hiyo nyoka ya shaba na akaisagasaga mpaka mavumbi na akatupa hayo mavumbi katika maji na akasema kwamba ni NE – HUSH – TAN, maana yake ni ubatili, ni bure na haina maana. 
11/  2 Wafalme 18: 4  
“Aliondoka pahali pa juu, na kubomoa nguzo, na kukata Ashera; akavunja vipande vipande ile nyoka ya shaba aliyofanya Musa; kwa maana hata siku zile wana wa Israeli walikuwa wakichoma uvumba kwayo; naye akaita jina lake Nehustani.” 
         Haifai kujaribu kujitafutia neno kati yako na Mungu, hata iwe kati jaribu ama hasira gani.
Jambo tunalopashwa kufahamu kwa makini sana ni Kazi ya Ukombozi yenye Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo alifanya kwa ajili yetu. 
Bwana Yesu alibeba hukumu na malipizi yetu, Yeye alilipa bei ya zambi zetu, Yeye alitimiza kazi yote na kupata hukumu kwa sababu ya zambi zetu ili sisi tusipate tena hukumu ya azabu. Hakuna tena hukumu juu Yetu.

AMEN
 
N°Ref: 01/03/1965 / 283 - THE BELIEVER’S SANCTUARY/ 2/17/2020