Tuesday, May 18, 2021

MLEMAVU WA KIROHO / THE SPIRITUALLY HANDICAPPED

Photo by B Smith from the kitchen window


 


MLEMAVU WA KIROHO 

THE SPIRITUALLY HANDICAPPED

August 27, 1978 

Pastor Henry F. Kulp


 

Waefeso 4: 11 – 15 

“Naye alitoa wengine kuwa mitume; na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wahubiri wa Habari Njema; na wengine kuwa wachungaji na walimu; 

Kwa kusudi la kukamilisha watakatifu, kwa kazi ya utumishi hata Mwili wa Kristo ujengwe; hata sisi sote tufikie umoja wa Imani, na kujua sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mzima, hata kufika kipimo cha urefu wa utimilifu wa Kristo; hata tusiwe tena watoto, tukitupwa huku na huku na kuchukuliwa kwa kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, kwa udanganyifu mbaya; lakini tukisema kweli katika mapendo tupate kukua katika maneno yote ndani yake aliye Kichwa, ndiye Kristo.” 

Tunasoma hapa kwamba Mwenyezi Mungu alitugawia zawadi za uongozi kwa kusudi la kukamilisha watakatifu, kusahihisha watakatifu, kwa kusudi la kutengeneza upya watakatifu na kwa kuwaweka tayari kwa Huduma. 

Kwa watakatifu kuwa wenye mafaa na kuwa washujaa katika huduma yao, wanapashwa mara na mara kutengenezwa upya, ni hii inayopashwa kuwa miradi ya msingi wa kila kanisa la fasi. 

Kutengenezwa upya na kurejesha  watakatifu. 

Kila mmoja wetu ana mtu wake wa zamani, kwa hivyo inatupasa mara kwa mara  kusikiliza Neno la Mungu, na ni Neno la Mungu itakayotumika  rohoni mwetu kwa kututayarisha kwa kazi ndani ya Huduma zetu mbalimbali. 

 

1/ Kumbukeni kwamba kila mmoja wetu anatumika kwa kujitoa kwa saa zake zote ndani ya huduma,  na Mwenyezi Mungu anatarajia matunda ndani ya huduma hiyo; twapasha kazaa matunda.  


2/ 2Wakorinto 5: 18 

“Na maneno yote yanatoka kwa Mungu, ambaye alitupatanisha sisi naye Mwenyewe kwa Yesu Kristo, naye alitupa sisi utumishi wa upatanisho.” 

Tunaambiwa hapa ya kwamba tulipewa utumishi wa upatanisho.

 Sisi tunatumika kwa pahali pa Kristo Yesu, tukisihi wanaume na wanawake wapatanishwe na Mwenyezi Mungu. 

Hakuna mchungaji mwenye anaweza kufanya kazi hii binafsi, hata pia muinjilisti hataweza kutimiza kazi hii peke yake. 

Yafaa watakatifu wote wa Mungu. 

Wale wanaokaa kwenye mimbari, hii ndiyo kazi yao. 


3/ 2 Wakorinto 8: 5 

“tena walitenda hivi si kama tulivyotumainia, lakini kwanza walijitoa wenyewe, wakampa Bwana, na sisi vilevile kwa mapenzi ya Mungu.” 

Hii ndiyo aina ya kanisa niliyokuwa nikitarajia kuona muda wa miaka hii yote iliyopita. 

Sababu gani huyu Mwenye Mungu mwenye Nguvu zote alikuwa anapendelea kutumikisha makanisa ya Makedonia? 

Ninaweza kuwaambia sababu gani. 

Tumeiambiwa wazi wazi katika Maandiko haya. 

Ni kwa sababu walijitowa kwanza wao wenyewe kwa Mungu. 

Sasa tazameni maneno yanayosemwa katika aya ya ine

Aya ya 4: 

“wakitusihi sisi na kusihi sana wapate kushiriki neema hii ya kutumikia watakatifu:” 

Kutumikia watakatifu, sababu gani wao waliweza kutumikia watakatifu, kiisha kutolea Mwenyezi Mungu? 

Kwa sababu walijitowa kwanza wao wenyewe kwa Mungu. 

Mutatambuwa ya kwamba neno hili linaelekea mali. 

Hakuna kati yetu mukristo mwenye anaweza kuwa mwenye nguvu, hakuna kati yetu yeye anayeweza kufanya kazi ya Mungu na ushujaa wote, kama yeye hatowi mali yake kwa Mwenyezi Mungu. 

Wale wanaokuwa tu na juhudi ya kuleta ushuhuda mbalimbali lakini wao hawapendi kumtolea Mungu mali yao, sizani kweli kama mbegu wanazo panda zaweza kuwa na nguvu.   

Mara nyingi niliwaza kufanya angalisho na maneno ninayoyasema kuhusu mali, sababu makanisa mengi wanazidi kuzorota kupita kipimo kuhusu matoleo ya mali. 

Lakini, upande mwengine, yafaa mufahamu kwamba Mwenyezi Mungu anahitaji ninyi kumutumikia na mali zenu, na kwa njia hii ya matoleo yafaa mutambuwe kwamba kutowa ni ya muhimu sana kwa kila kanisa la fasi. 

Siwe sawa munakusudia kutowa kwa mipango ya namna yenu na hapo mufanye angalisho musimuibie Mwenyezi Mungu. 

Ni vigume wewe kujitoa mwenyewe kwa Mungu na kukataa kutowa mali yako. 


4/ 2 Wakorinto 9: 6, 7 

“Lakini ninasema neno hili: Yeye anayepanda kwa choyo atavuna kwa choyo; na yeye anayepanda kwa ukarimu atavuna kwa ukarimu.

Kila mtu afanye kama alivyokusudia katika moyo wake: Si kwa huzuni, wala si kwa lazima: kwa sababu Mungu anampenda yeye anayetoa kwa furaha.” 

Mara tena hapa inahusu mali. 

Mwenye kupanda kwa choyo, atavuna kwa choyo, na kwa aya ya 7 inasema:

Kila mtu afanye kama alivyokusudia katika moyo wake: Si kwa huzuni, wala si kwa lazima, lakini sababu wewe mwenyewe ulikusudia   hivyo na unapenda kufanya hivyo. 


5/ Kuna jambo lingine lenye twapashwa kuchunguza: 

Siyo tu kwamba twapashwa kujitoa kwanza wenyewe kwa Mungu na kiisha kutoa mali zetu, lakini kuna aina ya ushirika yenye inapashwa kuwa katikati yetu sisi kwa sisi ndani ya Huduma yetu. 

Moja ya Maandiko yenye nafurahia na kuipenda sana ni katika: 

Kumbukumbu la Torati 20: 19 -20 

“Wakati unapozunguka mji siku nyingi, kwa kufanya vita juu yake upate kuukamata, usiharibu miti yake kwa kupeleka shoka juu yao; kwani utaweza kula matunda yao, wala usiikate; kwa maana mti wa shamba ni mtu hata uuzunguke kwa vita?

Miti unayojua si miti ya chakula utaharibu na kuikata; na utajenga maburuji juu ya mji unaopigana nawe hata uanguke.” 

Hii ni taswuira ya yale kila moja wetu angelihitaji kuona. 

Hata hivyo ni Maandiko yenye mara nyingi inasahauliwa ndani ya Neno la Mungu, bali hapa, Mwenyezi Mungu anazungumuzia Taifa la Israeli akiiambia kwamba: 

Wakati atapozunguka mji siku nyingi, kwa kufanya vita juu yake apate kuukamata, kuna miti fulani  tu ndiyo yenye anaruhusiwa kukata. 

Kwa miti hizo, watajenga maburuji na kuipiga juu ya mji wanaopigana nao ili uanguke, bali hatakata hata mti mmoja unaozaa matunda, miti hiyo ya chakula inapashwa kulindwa. 

Mwenendo wetu wapashwa kuwa namna hiyo mbele ya watakatifu, watu wenye wako sawa kaka na dada katika Kristo, wao wanaokuwa Viungo vya Mwili wa Kristo. 

Sote twahitaji kuwa miti ya kuzaa matunda kwa Bwana Yesu Kristo. 

Twapashwa kuzaa matunda, hatupashwi kuinua shoka yetu juu ya dada na kaka watakatifu, bali, twapashwa kutumika kwa umoja. 

Yamaanisha kwamba hatupashwi kutenda hata tendo moja linaloweza kuhuzunisha mmoja wetu katika Huduma. 

Haifai Huduma ilaumiwe, wala kuzarauliwa. 

Hatupashwi kuwa na masongano mmoja kwa mwengeni bali yatupasa kutumika kwa umoja na kuzaa matunda.  


6/ Matendo ya Mitume 18: 24 -26 

“Basi Myuda mmoja jina lake Apolo, mzalia wa Alesanduria, mtu wa elimu, akafika Efeso; naye alijua sana Maandiko. 

Mtu huyu alikuwa amefundisha njia ya Bwana; na kwa kuwa roho yake ilikuwa ikiwaka, alianza kusema na kufundisha kwa kweli Maneno ya Yesu, naye alijua  ubatizo wa Yoana tu. 

Akaanza kusema pasipo hofu katika sunagogi; lakini wakati Akila na Prisila walipomsikia, walimtwaa kwao, wakamfunulia zaidi njia ya Bwana, aijue kabisa.” 

Hapa twapata mufano wa namna gani yatupasa kutenda mbele ya miti ya Mwenyezi Mungu yenye kuzaa matunda, wale wanaokuwa ndani ya kuhudumia Bwana Yesu Kristo, na hiyo inahusu watakatifu wote. Watakatifu wote wanaohudumia saa kwa saa katika shamba la Bwana. 

Hapa tuna mfano wa Apolo, mwenye, kama munavyokumbuka alichapa kazi ya Mungu bila ziaka na alikuwa anapenda sana Maandiko Matakatifu yaani Neno la Mungu. Matumikio yake iligusa sana mioyo ya Akila na Prisila, bali, mpaka hivyo ufahamu wa Apolo ulikuwa ungali chini ya wenzake katika hudumu kwa siku zile. 

Yeye hakuwa na ufahamu zaidi ya kujuwa kuhusu ubatizo wa Yoane, ni hivyo Akila na muke wake Prisila walivumbuwa ukosefu huwo wa ufahamu na wao walikuwa na upendo kwake, walifahamu kwamba Apolo alikuwa anataka kujuwa Kweli ya Maneno ya Mungu, alikuwa akifanya yote iwezekanavyo ili awe na ufahamu kamili ya Kweli ya Neno la Mungu. 

Ni kwa hiyo Akila na muke wake Prisila, wakiwa watumishi wa Mungu, hawakupenda kumupa Apolo haya kwa kuonesha kutokufahamu kwake azarani mbele ya watu wote, kwa macho ya watu wote na kuonesha kwamba Apolo alikuwa mtu wa kuchunga desturi lakini anayekosa ufahamu kamili katika Neno la Mungu, bali walimuita nyumbani kwao na hapo katika mapendo ya kikristo, walimutwaa kwao, wakamfunulia zaidi njia ya Bwana, aijue kabisa. 

Yatupasa kutumia shoka zetu kwa kukata miti mikavu iliyokufa na zambi, makosa na kasoro mbalimbali pahali pa kujiumiza sisi kwa sisi. 

Yatupasa kutumika mkono mukononi sawa vile Akila na Prisila walivyotumika kwa kusaidia watakatifu wenye wanahitaji kujuwa kweli, hata kama  hadi hapo  hawajaifahamu bado kabisa katika ukamilifu wake. 

Twapashwa kutumika pamoja ndani ya umoja na maelewano.  


7/ Twende sasa kwa aya ya kumi na ine ya Kitabu cha Waefeso sura 4 

Waefeso 4: 14 

“hata tusiwe tena watoto, tukitupwa huku na huku na kuchukuliwa kwa kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, kwa udanganyifu mbaya;” 

Nilitaka kuonesha  taswira ya tofauti. 

Kwa aya ya kumi na tatu, inatuonesha wakristu wanaokomaa. 

Kwa aya ya kumi na ine, inazungumuza kuhusu watoto. 

Ili tusiwe kama watoto

Anamaanisha nini wakati anasema kwamba tunakuwa sawa watoto wadogo? 

Kwa kweli, neno inayotumiwa hapa siyo “mtoto mudogo” lakini “utoto”, kufanya mambo ya kitoto. 

Mutume Paulo yuko akisema kwamba wamoja wa wakristo wa Efeso walikuwa wakifanya mambo ya kitoto. 

Tuchunguze kwa makini jambo lile na tufikiri kuhusu maana yake. 


8/ Neno mtoto ni NAY – PEE – OSIS pia twapashwa kufanya tofauti ya neno linalotumikishwa kwa nyakati tumeokolewa na hiyo ni neno katika kigriki BREATH – OSIS inayosema kuhusu mtoto mchanga anayenyonya kwa maziwa ya mama yake, na wakati unapokomaa kama ipasavyo utageuka kuwa WEE – OSIS, mwamini anayekomaa, mtu mzima.   


9/ Maana ya neno NAP – PEE – OSIS? 

Ni mtu mwenye kwenda pembeni, mwenye kuambatana na njia ya huduma yenye iko umbalimbali na mapenzi ya Mungu. Ni mtu mwenye anaacha kutumika kwa maongozi ya Mungu. Ni mwamini MPUMBAFU KIROHO. Mtu mwenye kurudi tu nyuma, hana maendeleo yoyote.  


10/ Kuna mambo matatu yanayoelekea huyu Mpumbafu wa kiroho  

Maandiko katika aya hii yawaita kwanza wapumbavu, kiisha yawataja kuwa vimelea walemeao wengine, wabaradhuli, wenye kumumunya.  


11/ Tuchunguze sasa tabia tatu inayoambatana na mwamini wa kitoto, mwamini asiyekomaa.


(1 Ni misemwa na mawazo ya watu wanaozoeya maji katika maziwa makuu: TUKITUPWA HUKU NA HUKU NA KUCHUKULIWA hii inatamkwa kwa neno moja katika Kigriki CLUE – DOUGH – NEEDS – O – MY na kwa kweli neno hili linamaanisha nini? INATUMIKISHWA KWA MASHUWA YENYE HAIWEZI KUONGOZWA KAMWE ILA ZORUBA PEKEE NDIO INAIKUMBA MAHALI INAYOPENDA. Kumbukeni wakati mashuwa haikuwa na mashini ya kutembeza ama injini sawa na siku hizi. Yote ilifwatana na namna ya kutumia hema kubwa la hewa, nanga,  usukani(uongozi), hapa ni picha ya mashuwa yenye uongozi yake ilivunjika na mlingoti wa hema ukivunjika, ni kwa sababu hiyo mashuwa inakumbwa kumbwa na zoruba. Kichwa ya mashuwa kinabebwa katika ngambo yote iwezekanavyo na mashuwa iko katika hatari kubwa MASHUA INAYUMBA YUMBA.


(2 Tukumbuke ya kwamba tunazungumuza juu ya mwamini. Mwamini anaye yumba yumba, na kweli wewe wajiuliza eti mwamini anaweza yumba yumba? Mara kwa mara mwamini anaweza kuwa katika hali hiyo, na wakati anapita katika mapito haya, maisha yake ya kiroho inazorota sana, yeye iko anatafuta kitu moja na hakipati, yeye ni mwenye kutafuta kitu kigeni kwake chenye bado kujua. 


(3 Tunapata neno lingine lenye watu wanaotumika kwa mashuwa ya maziwa makuu wanatumia: NA KUCHUKULIWA KWA KILA UPEPO WA ELIMU, kuchukuliwa huku na huku katika tafsiri la Kigriki ni PERRY – FUR – O  NA HII HAIMAINISHE KWAMBA MASHUWA IKO YENYE HAIONGOZWI TENA ILA ZORUBA PEKEE NDIO INAYOIKUMBA KUHU NA HUKU, BALI INAMAANISHA KWAMBA MASHUWA INAKUMBWA TU NA UPEPO. Katika hewa kali yenye kuchafua maji inayotoka inje ya ziwa, kuna vitu viwili vinavyo sababisha kuleta woga ni: Zoruba na Upepo. Na hapo, ni upepo ndiyo unayoletea waamini shida. Hii inamaanisha nini? Ni upepo wa elimu na kusema kweli siyo elimu safi ya musingi. Mwatambuwa kwa kweli kwamba waamini wenye wako walemavu kiroho, wao hawakomae katika Elimu ya Biblia, wao wanadanganywa na kukumbwa na elimu ya mapepo wachafu. Yawezekana iwe mapepo ya kuishi kijamii ama kisosialismi, yaweza kuwa ya kukumba watu kunena kwa lugha mupya, yaweza kuwa ya uponyaji.                                 

1Timoteo 4 : 1 inasema “Basi, Roho anasema waziwazi ya kwamba katika nyakati za mwisho watu wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho za kudanganya, na mafundisho ya mashetani,”  sawa ginsi tulivyo wafundisha kila mangaribi ya siku ya Mungu, tukiwaambia kwamba mashetani hawawezi kamwe kuishi ndani ya mwamini, lakini wakiwa inje wanaweza kuchochea mafikiri na mawazo ya mwamini kwa njia ya elimu mbalimbali, wanaweza kumukumba katika mafundishi ya uharibifu. Na tabia ya mafundisho yale ni nini? Ni mafundisho yenye madara, yakuumiza. KUCHANGAMUSHA NA KIVUMBI TELE IKIWA NA CHUMVI NA RAHA NA UREMBO WA UDANGANYIFU. Hamuja ona bado namna gani shetani anachamusha hali hiyo, muangalie hayo makani madogo madogo ya uwongo yenye yanaota siku hizi kama uyoga, yote yanatabia moja yanajaa na kuchangamusha na kivumbi tele na chumvi na raha na urembo wa udanganyifu.


(4 Tunafikia sasa fumbo la tatu, na hapo tunakuwa na mawazo kuhusu muchezo wa kura, yaani mchezo wa kubahatisha. Hakuna mpumbavu mkuu katika dunia hii kushinda yule mtu anayejitowa kucheza michezo ya kubahatisha na katika michezo yale, mtu mwengine ndiye anaye mupigia kura.  Mtu mwengeni ndiye anayeshika kete kwa kuimwanga kwenye meza ya michezo na yo ita zunguka kwenye saba ama kumi na moja na mtu huyu anayechaza hataweza kamwe kufaulu. Atapoteza hata shati yake. Ni vigumu sana kufahulu kama kwa michezo ya kura ni mtu mwengine anayeshika kete.


(5 Mwamini mwenye ni mlemavu kiroho hawezi kamwe kufaulu. Yeye ni mwenye kungojea tu miradi ya kuchangamusha na kivumbi tele na  vukuto ya chumvi na raha ya udanganyifu yenye mashetani wanaoleta, mtu huyu atakuwa mnyonge wa mwisho hapa chini duniani. Mtu asiiyeokaka siyo yeye aliye mnyonge wa mwishi hapa duniani, bali ni mwamini mwenye anayetembea inje ya Mapenzi ya Mwenyezi Mungu.  


12/ Kwa kweli mutajiuliza: Ni wapi nitowapo mambo haya yote? 

Neno udanganyifu katika Kigriki ni KOO – B – AH na inamaanisha mchezo wa kura na kete yenye inahusu kweli mchezo wa kura na kete inayochezwa na watu

Twaweza kujiuliza, eti watu hawa wanacheza mchezo gani? 

Kwa kweli ni mchezo gani wachezao? 

Shetani ni mdanyanyifu, ni mkorofi. 

Dini yake ni ukorofi na michezo anayoyacheza ni michezo ya kidunia, UDANGANYIFU, UKOROFI WA WATU. 

Tafsiri kwa Kigriki ya haya mambo ni PAN – OORG – EÉ – AH, inayomaanisha KUFANYA UKOROFI KATIKA MCHEZO WA KURA.

Ni kusema kwamba wapumbafu hawa wa kiroho wenye hawaguwi kamwe katika BWANA, hawategemee hata Elimu moja na mbio wanaanguka na kutegwa  nyara kwa Mafundishi na elimu ya mashetani, na hapa tunaambiwa kwamba dini yao yote ni mchanganyiko wa kete mtupu na Mchezo wa kura na kete. 

Kwa mchezo huo hautaweza kamwe kufaulu, wewe unatarajia tu kushindwa. 


13/ Tunafikia neno kwa njia ya, na huo ni rafiki wetu wa kale, rafiki wetu wa zamani SIFA NA MCHONGEZI na hii ni kusema ANA KWA ANA.


14/ Ana kwa ana na nini? 

Biblia Takatifu, tafsiri ya King James, yasema, 

Wakingojea na kusimama kwenye zamu wakichungana na, na msemwa huo ni msemwa wa wataalam, METH – O – DOS. Kwenye neno MBINU yotokea.  


15/ Kiisha kuna neno ujanja ni neno lenye katika Kigriki ina tafsiri la Ukorofi. 

Kwa hiyo, nini inayofikia mwamini mwenye kuishi inje ya Mapenzi ya Mwenyezi Mungu? 

Asiye jifunza Elimu ya Biblia na pia haiishi katika maishani mwake? 

Yeye anaangukia ana kwa ana kwa mbinu ya ukorofi inayo potosha, ni kusema kwamba anageuka tu mtu wa dini. 


AMINA 


N° Ref: 08/27/1978 / 438-2 THE SPIRITUALLY HANDICAPPED / 05/18/2021

Wednesday, May 5, 2021

NGUVU YA NIA NJEMA / THE POWER OF POSITIVE THINKING

Photo by B Smith from the patio
 

 


NGUVU YA NIA NJEMA 

THE POWER OF POSITIVE THINKING

June 19, 1960

Pastor Henry F. Kulp


 

Waefeso 4: 17 – 20 

“Basi ninasema neno hili na kushuhudu katika Bwana hata musitembee tena kama Mataifa wanavyotembea, katika ubatili wa nia zao, 

Ufahamu wao uliotiwa giza, waliotengwa mbali na uzima wa Mungu kwa sababu ya ujinga ulio ndani yao, sababu ya ugumu wa moyo wao; 

Waliokwisha kufa na kujitia wenyewe katika mambo ya uasherati, kutenda uchafu wote kwa choyo. 


Lakini ninyi hamukujifundisha Kristo hivi.” 

Juma juzi, baada ya mahubiri yetu ya siku ya Mungu, tulifundishwa hadi kufikia maandiko ya Waefeso 4: 16.  


“Katika yeye mwili wote ukiunganishwa na kushikwanishwa kwa kusaidia kwa kila kiungo, kwa kadiri ya utendaji wa kila sehemu moja moja unaongeza mwili upate kujijenga wenyewe katika mapendo.” 


Tunasoma hapa namna gani Mwili wa Kristo unafananishwa na mwili na namna gani kila kiungo cha mwili kinatumika na kufanya kazi pamoja ili mwili upate kujengwa. 


Kwa hivyo, pahali pa mapigano na magonvi katikati yetu, kila kiungo kinapashwa kujitia kwa kazi. 


Kwa kweli kila kiungo kinapashwa kutumika juu ya lengo la umoja, lile la kumu


1/ Kumbukumbu la Torati 20: 19 – 20 

“Wakati unapozunguka mji siku nyingi, kwa kufanya vita juu yake upate kuukamata, usiharibu miti yake kwa kupeleka shoka juu yao; kwani utaweza kula matunda yao, wala usiikate; kwa maana mti wa shamba ni mtu hata uuzunguke kwa vita? 


Miti unayojua si miti ya chakula utaharibu na kuikata; na utajenga maburuji juu ya mji unaopigana nawe hata uanguke.” 

Tunavumbua hapa Maandiko yanayoonesha kwamba wakati wana wa Israeli walikuwa wanazunguuka mji kwa kuushambulia, hawakuruhusiwa kukata hata mti moja inayozaa matunda kwa mtu kula. 


Wao walipashwa kukata na kuharibu miti isiyo tumiwa kwa kupata chakula. 


ababu, baadaye, wangaliweza kutumia matunda ya miti yale katika mahitaji zao. 


2/ Maandiko mazuri yenye inayosema kuhusu miti ya matunda kulindwa na Mwenyezi Mungu, tunaipata katika Kitabu cha Matendo ya Mitume 

Wakati wanapozungumuzia kuhusu Apolo. 


Matendo ya Mitume 18: 24 – 26 

“Basi Myuda mmoja jina lake Apolo, mzaliwa wa Alesanduria, mtu wa elimu, akafika Efeso; naye alijuwa sana maandiko.


Mtu huyu alikuwa amefundisha njia ya Bwana; na kwa kuwa roho yake ilikuwa ikiwaka, alianza kusema na kufundisha kwa kweli maneno ya Yesu, naye alijua ubatizo wa Yoane tu. 


Akaanza kusema pasipo wofu katika sunagogi; lakini wakati Akila na Prisila walipomsikia, walimtwaa kwao, wakamfunulia zaidi njia ya Bwana, aijue kabisa.” 


Kumbukeni kwamba Apolo alikuwa mutaratibu sana na mwenye kupenda Neno la Mungu, kweli yeye alivuta sana roho ya Akila na Prisila. 

Apolo hakuwa na ufahamu unaotoshelea ya yale yenye ilimubidi kufahamu katika Maandiko. 


fahamu wake haukuwa zaidi ya ubatizo wa Yoane, na hawa watumishi wa Mungu wakiwa muke na mume walitambua hitaji ya ndugu Apolo.


Walitambua kwamba Apolo alikuwa anahitaji kujuwa kweli, na kwa nguvu zake zote alitamani kujuwa kweli la Mafundisho, sasa hawa Watumishi wa Bwana muke na mume hawakupenda kuonesha hitaji la Apolo hazarani, wakionesha kwa watu wote kwamba yeye ni mushika sheria asiye na ufahamu kamili ndani ya Habari Njema, bali walimuchukuwa yeye pekee kwa nyumba yao, katika upendo wa kindugu na katika ujamaa wa kikristo, walimtwaa kwao, wakamfunulia zaidi njia ya Bwana, Maandiko na sheria aijue kabisa. 


utumie shoka zetu kwa kupiga miti inayokauka na zambi, Habana kuumizani sisi kwa sisi kati yetu. 


Tunapasa kutumika sisi sote kwa umoja katika kupasha na kutangaza H


3/ Waefeso 5: 17   

“Kwa hivi musiwe wajinga, lakini wenye kufahamu mapenzi ya Bwana.” 

Mwatambua kwamba mtume Paulo anawasihi musitembee kama wapagani. 

Hii ni shurti iliyo waziwazi yenye kila mwamini anapashwa kufahamu. 

Mukristo anaondoshwa inje ya dunia. 


Maisha yake haipashwe kuwa sawa ya wale wanao kuwa kando kando yake wakimzunguuka. 


Watu wengi wanasema fumbo ya kwamba: 

Wakati mtu iko Roma, atende kama Waroma wanavyotenda, lakini hiyo siyo kwa maisha ya mukristo. 


Wao wasioamini mwenendo wa upekee na wakujitenganisha na wapagani, wao hawaamini sura hii ya 17


Kujitenga huko kunafundishwa katika Maandiko Matakatifu, Neno la Mungu. 


4/ Mwenendo na Masemi yetu yanapashwa kuwa mbalimbali sana na ya wapagani, kwa hiyo haturuhusiwe kuhudumia pamoja nao sababu wao hawamjui Mwenyezi Mungu. 

Katika mambo ya huduma ndani ya kanisa, twapasha kujitenga na wapagani. 


Ufunuo 18: 4 – 5 

“Nikasikia sauti nyingine toka mbinguni ikisema: Tokeni kwake, watu wangu, musishirikiane na zambi zake, wala musipokee mapigo yake. 

Kwa sababu zambi zake zimefika hata mbinguni, na Mungu amekumbuka maovu yake.”  


Hii ni kwa wakati wa mateso makuu, Mwenyezi Mungu anawashurtisha  Taifa lake wazi wazi kwa muda huo wa mateso makuu, akiwaomba watoke katika eneo lile, ili wasishirikiane na zambi zake, wala wasipokee mapigo yake. 


Nikusema, musifanye huduma pamoja nao, wala musiabudu pamoja nao. 

Musifuate njia zao musije mukapokee hukumu juu ya zambi hiyo.   

Ninaamini kweli kwamba hata kwa leo shurtisho hilo linatumika. 

Mwenendo wetu haipashwi kuwa sawa na ya wapagani, watu wasio amini. 

Hatupashwi kumuhudumia Mwenyezi Mungu wala kumuabudu pamoja na watu wale. 

Mungu anatuonyesha njia ya matengano na watu wale, tutoke kwao. 


5/ Mwenendo ya Wapagani ni namna gani? 

Wanatembea katika ubatili wa nia zao. 

Tafsiri ya neno “ubatili” hapa siyo kama ya kawaida.  

Mara nyingi wakati tunapotumia neno lile tunakuwa na wazo la kujivuna, lakini hapa inamaanisha mtu asiyeona sambamba, anayeona katika uvuguvugu mwingi, ukosefu wa kutokuona sawa inakumba mafikili, na inamtuma mtu kuzania tu kama katika ndoto, na mawazo yale hayako kamili ama timamu. 


6/ Kwa jumla tunaweza kusema ya kwamba, mawazo yao yalikuwa yakiwadanganya wao wenyewe, na kuwafanyizia michezo ya kubahatisha bila msingi. 

Nikusema kwamba wao ni katika uvuguvugu wa nia yao. 

Mwaweza kusikia wakisema kwamba: 

“Musiamini mambo ya Jehenama, sababu gani niamini neno lile

Kwa kweli, wewe kama mzazi waweza kumtupa mtoto wako katika ziwa la moto ili achomwe na kuunguwa ndani milele na milele?” 

Na wanaongeza wakisema: 

“Kama wewe hauwezi kutenda hivyo, namna gani Mwenyezi Mungu wa Uzuri na Mapendo anaweza kutenda jambo kama lile?” 

Mawazo yao inafika mwisho na kukwama hapo. 

Mawazo yao, inakuwa mazuri na yenye maana kwao wenyewe, wao wenyewe wanajidanganya wakizani kwamba wanawaza sambamba, lakini wao ni katika uvuguvugu wa nia zo. 

Na sasa kuhusu UTATU MTAKATIFU, wanasema: 

“Mutuoneshe hiyo Utatu Mtakatifu, mutupatie mafasiriyo yake. 

Namna gani Mungu Mmoja anaweza kuwa Mungu Baba, Mungu Mwana na Mungu Roho Mtakatifu?” 

Na watakuambia: 

“Hiyo siyo busara” 

 Wao hawawezi kufikia kiwango cha kuwa na mawazo kama yale sababu wanakuwa katika uvuguvugu wa nia yao. 


7/ Munaweza mukaniulize: 

“Sababu gani wapagani hawafike kwa kiwango cha kufahamu mambo haya katika nia zao?” 

Kuna jambo mbili ya muhimu munayopasa kutambua kuhusu nia na akili ya Wapagani. 


Waroma 1: 28 

“Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika ufahamu wao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa; wafanye maneno yasiyowapasa” 


8/ Tuchunguze kwa makini sana. 

Katika Aya hii ya Waroma 1:28, neno “kukataa kuwa na ufahamu”, inaonesha wazo la kumuweka mtu katika mutiano wa kupana uamuzi wake, ni kwa namna hiyo ndiyo mwenendo wao ulikuwa mbele ya Mungu. 

Kizazi cha wanadamu kiisha kumuweka Mungu katika mizani, waliamuwa ya kwamba Yeye hastahili na walimutupilia. 

Wazo lenye linaoneshwa hapa ni kwamba watu, kwa nyakati fulani walipata habari kuhusu Mungu, wao hawakutaka kufahamu hata neno moja juu yake, walimuweka katika mizani na walikamata uamuzi wa kusema kwamba Yeye hastahili kuabudiwa, wala hastahili kutumikiwa na waliamuwa kwamba kumujuwa ni neno bila maana, na kwa hiyo hawakuwa na faida ya kumujua kwa hiyo hawakulinda ufahamu huo. 

Kiisha Mwenyezi Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizo faa.


9/ Tunatambua ya kwamba, bila musaada unaotoka inje, mawazo ya mwanadamu ni mbaya na chafu, ni mawazo ya uuaji mtupu. 

Kwa hiyo, mawazo ya kuzani kuwa na nia njema ni mawazo isiyo na msingi, isiyo halali, ni maneno isiyo ya haki ni kama mchezo wa kitoto tu. 

Mwenyezi Mungu anatusihi tusitembee kama Wapagani wanavyotembea. 


10/ Kuna musaada moja yenye iliyokuja kusaidia mawazo ya mwanadamu. 


 2 Wakorinto 4: 3 – 4 

“Lakini kama ikiwa Habari Njema yetu imefichwa, imefichwa kwao wanaopotea; 

Ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha mafikiri yao wasioamini, ili nuru ya Habari Njema ya utukufu wa Kristo, aliye sura ya Mungu isiwaangazie.” 

Wale wasioamini watatambuwa kwamba Habari Njema imefichwa kwao, na kwa kweli Habari Njema imefichwa kwao sababu Shetani mungu wa dunia hii, amefunika mafikiri ya wale wasio amini, ili wasije wakaokolewe. 

 Muovu shetani ameshika nyara mfikili yao na inaitia giza. 

Anafunika mafikiri yao ili wamama na wababa wale wasije kuvumbuwa kweli. 

Mwatambua sasa sababu gani haitupase kutembea katika ubatili wa nia sawa wale wasiookolewa, Wapagani. 

Ni kosa sana kuwa na mwenendo wa namna ile, ni mwenedo pasipo kuona kama kipofu, Shetani anafunika nia ya watu wale.   


11/ Kwa kweli dunia haijitambuwi kwamba iko katika hali lile. 

Nia na mafikiri yake ya wakati huu inatiwa giza na kufunikwa. 

Ni vema mufahamu namna gani dunia inaendelea kuchafuka siku kwa siku na kuwa mbaya sana kuliko, dunia haifahamu inatoka wapi na inaenda wapi. 

Uliza dunia katika maarifa yake, haitapata jibu kwa maswali zifwatazo: 

Pahali pa kuleta jibu, dunia itakubeba katika sayanzi ya mabadiliko bila kujibu hata swali moja ikikukumba katika mizaa yenye haina maana yeyote. 


12/ Mtu inje ya Bwana Yesu ni kama ule kijana masikini wa Inchi ya Wagerase mwenye wazimu na mwenye kujaa pepo wachafu (Luka 8: 26), 

Nafahamu kwa kweli kwamba watu wa dini wengi, wapagani hawatafurai kuona ninawalinganisha mtu wa wazimu mwenye kujaa pepo tele, wakilinganishwa na huyo kijana masikini mwenye wazimu na mwenye kujaa mapepo.

Bali ni vile wapagani walivyo katika asili yao ya ukali wa kyenyeji na umasikini na unyonge wao. 

Kijana masikini huyo alikuwa akiachiliwa yeye mwenyewe ndani ya mateso yale makali, tangu utoto wake, bila mlezi na lililo mbaya kabisa, ni kwamba yeye aligeuka kuwa hatari kwake yeye mwenyewe. 

Baadaye, siku moja Bwana Yesu alikuja kwake akamkutana na hapo hapo kitu moja kilitukia maishani mwake. 

Ni hapo tunasoma masemi hizi za raha: 


Luka 8: 35 

“Wakatoka kuona maneno yaliyotokea, wakakuja kwake Yesu, wakaona yule mtu pepo wachafu walikwisha kutoka kwake, akiketi karibu na miguu ya Yesu, amevaa nguo, na mwenye roho nzuri; wakaogopa.” 

  Kweli kweli, wakati Bwana Yesu anapoingia maishani mwako, kuna kitu kinachoingia katika nia na mafikiri yako. 

Huyo mtu wa mapepo chafu alirudi na kugeuka mtu mwenye akili timamu na mwenye roho nzuri. 

Dunia bila Bwana Yesu inayumbayumba kama mtu wa wazimu. 


Waroma 12: 2 

“Na musifananishwe kwa namna ya dunia hii; lakini mugeuzwe kwa kufanya upya nia zenu, mupate kujua sana mapenzi ya Mungu, yaliyo mema, ya kumpendeza na ukamilifu.” 

Hapa mtume Paulo anatuambia ya kwamba: 

Mtu asijiwazie mwenyewe kuwa na kiasi kupita kipimo, bali awe na utawa, akijizuiza mwenyewe katika kila jambo

Neno utawa katika Kigriki ni SO – FRON - EH – O inayomaanisha nia na akili iliyopona

Wakati mtu anapookoka, Mwenyezi Mungu anamupa nia na akili iliyopona, kwa hivi mtu huyo hapashwe tena kutembea akiwa na nia mbovu na yenye kupotoshwa na ulimwengu huu, lakini katika nia na akili iliyopona aliyopewa na Mwenyezi Mungu. 

Mapendekezo hayo hayo tunayapata tena katika Tito 2: 11 -12.  



Tito 2: 11 -12 

“Kwa sababu neema ya Mungu inayoleta wokovu kwa watu wote, inaonekana, 

Ikitufundisha sisi kukataa ubaya na tamaa za dunia, na kuishi na kiasi kwa haki, na utawa, katika ulimwengu wa sasa,” 

Neema ya Mungu inatufundisha sisi kukataa ubaya na tamaa za dunia, na kuishi na kiasi kwa haki, na utawaa, ni hiyo hiyo neno la kigriki, tunapashwa kuishi kwa nia na akili iliyopona

Mwenendo wetu haupashwi kuwa sawa na ya wapagani wanaotembea katika ubatili wa nia zao, bali sisi tunapashwa kutembea katika nia na akili iliyoponeshwa, tukiweza kufahamu Neno la Mungu. 


13/ Tugundue tena tabia hii ifwatayo: 


Waefeso 4: 18 

“Ufahamu wao uliotiwa giza, waliotengwa mbali na uzima wa Mungu kwa sababu ya ujinga ulio ndani yao, sababu ya ugumu wa moyo wao;” 

Wanatengwa mbali na uzima wa Mungu na kweli hii ni katika hali ya kiroho. 

Mafikiri na nia yao ni katika ubatili na giza, na kwa hali ya kiroho hawana  uzima. 

Kweli wana uzima wa maumbile, lakini kwa hali ya kiroho wao wamekufa, hawana uzima wa kiroho. 

Mutasikia wengine wakisemasema kwa sauti kubwa ya kwamba kuna mshale wa moto wa kimungu katika kila mtu, lakini hiyo siyo ukweli. 

Hiyo ni masemi  na hitimisho inayotoka kwa kichwa na mafikiri ya mtu mwenye nia na mafikiri yake imetiwa giza na anayeishi tu katika ubatili wa nia yake akichanganyikiwa katika yote. 

Kwa hali ya mafikara na nia mtu yuko ndani ya ubatili na kwa hali ya kiroho yeye ni maiti. 


14/ Katika Aya ya 18, mtume Paulo anakaza akisema, siyo tu kuhusu hali yao ya kiroho, akihakikisha kwamba hawana uzima, lakini pia wana ujinga ndani yao, roho yao ikiwa mbaya zaidi, wakiwa vipofu, na wao wenyewe hawajitambue katika hali walimo, kwa hiyo neno wakiwa vipofu, inafanana kuwa na maana ya nguvu sana, lakini kwa kweli haituonesha katika hali gani dunia yapatikana. 

Ni kusema roho yenye inalewa na dawa ya kulevya, inayomupa usingizi mnono, yeye hasikie tena kitu kwa ngozi yake, anakuwa chini ya dawa ya kulalisha ya nusukaputi. 

Mtu mzima anayeishi akiwa na akili yake yote sambamba, anaweza kupiganisha machungu ya maumivu inayozidi mno, hata kufikia kiwango cha kuanza kutetemeka na maumivu, lakini wakimtwanga dawa ya nusukaputi, huyo mtu hatajuwa tena mambo yanayopita, hafahamu tena vitu viko vinaendelea namna gani. 

Wanaume na wanawake wanaokumbwa chini ya uwezo wa kufa na uharibifu wa zambi, wao wanakuwa vipofu, na hawana mawazo zidi ya vitu vinavyotendeka kwa kweli. 

Hawana ufahamu kuhusu hali yao, yenye kwanza hawatambue, hawajuwi hali yao ya sasa, hawafahamu kwamba wao ni wafu mbele ya Mwenyezi Mungu. 

Ni kwa sababu hii, tunamapashwa ya kuombea watu wale wa kike ama wa kiume nakuwasihi: Muwe wenye kupatanishwa na Mwenyezi Mungu

Ni kwa hiyo wakati tunapopasha Habari Njema, tunapashwa kuonesha wanaume na wanawake wale hali yao mbaya, hali ya upotevu na uchafu na kutengwa mbali na Mungu. Wakaidi katika zambi. 


15/ Waefeso 4: 19 

“Waliokwisha kufa na kujitia wenyewe katika mambo ya uasherati, kutenda uchafu wote kwa choyo.” 

  Twavumbua sasa nini Mwenyezi Mungu anasema kuhusu mtu kuhusu nia na akili yake na kuhusu kiroho yake, pia kuhusu maadili yake.  

Mwenendo yao ya maadili ni machukizo mtupu, wanajitia katika mambo ya uasherati wakitenda uchafu wote kwa choyo. 

Kumbuka kwamba Maandiko Matakatifu, Biblia, yanatuambia: “Waliokwisha kufa, hawasikie tena majuto yoyote” hii yatuonesha kwamba watu wale hawasikie uchungu ama majuto yoyote, hawajali na kitu wala hakiwaumi kamwe. 

Neno hili linatukumba kwa wazo moja la muhimu lenye watu wengi wananiuliza: 

“Kama ninasadiki kwamba kila kizazi kinacho ongezeka kinaendelea kuwa kiovu zaidi sana, na kwa kweli ni hivyo. 

Watu wanaendelea kuwa wenye kupenda sana zambi na kuukumbatia zaidi, siku kwa siku, zambi haiwakwazi tena, wala haiwaletee tena bughudha. 

Zambi iliyokuwa ya kutisha, miaka kumi iliyopita, kwa siku za leo watu wanaitenda bila majuto yoyote, na watu wanaitenda kama kawaida.

Umutu unaanza zimika polepole, kizazi cha mwanadamu hakitishwi tena na zambi za aibu. 

Zambi haliwahuzunishi kamwe.  

Mambo yote yale yanaweza vile vile kumufikia mwamini. 

Mwamini , kwa mwanzo anaweza kutenda kosa ama zambi na kweli hiyo zambi itamuhuzunisha, bali akiendelea kuitenda, atajikuta uchungu ya iyo zambi unaanza kupunguka polepole na kwa mwishi  hiyo zambi inaanza kuwa kama desturi na haimupi wofu wowote, na zamiri zake hazimuambie tena hata neno moja. 

Hajikute hata tena katika hali ya kuwaza kutubu zambi hiyo. 

Kama hali hiyo inaweza kufikia mukristo, jiulize sasa namna gani mutu kawaida awezavyo kuwa wakati anapita katika hiyo hiyo mapito, huyu mtu mwenye akiwa katika ubatili wa nia na akili na ambaye mbele ya Mungu, yeye ni maiti kwa hali ya kiriho. 

Kila siku iongezekayo katika maisha yake, yeye anazidi tu kutenda maovu zaidi. 

Sihitaji kamwe kupima kutia mafikiri yangu kuhusu picha ya namna watu wataishi baada ya miaka mia moja kama Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo hajakuja bado. 


16/ Wazo la kutokusikia uchungu wowote unatafsiriwa vizuri na Louis Talbot, yeye alisema ya kuwa: 

Wakati alipokuwa akiishi huko Australia, mara kwa mara alikuwa akipitisha mafungo yake katika mahali walipokuwa wanafuga ngombe. 

Naye alikuwa anahuzuria na kutizama na macho yake mwenyewe sherehe hiyo ya kutia chapa wakitumia chuma ya moto na kutia chapa kwa ngombe wachanga. 

Alikuwa anachunguza namna wanyama walikuwa wakitiwa chapa na chuma ya moto sana. Hiyo chuma ya moto wakiishoshea moto hadi kungaa nyekundu, baadaye kuitia chapa kwa kila nyama. 

Anakumbuka namna gani nyuso za wanyama zilikuwa zikijaa uchungu mkali, na anakumbuka hadi leo kilio kwa sauti kali ya wanyama wale na hata leo anaona picha ya mecho ya wanyama wale yenye ilikuwa inageuka nyekundu sababu ya uchungu. 

Kiisha kuwatia chapa, walikuwa wanawaachilia wakikimbia na kujilemba kidonda chao kwa ulimi. 

Bali, aliongeza kwa kusema kwamba: 

Lakini sasa kama unarudi mahali pale baada ya juma tatu na unajaribu kuumiza mnyama moja kwa kisu kwa ile nafasi alipotiwa chapa, utatambua ya kwamba nyama yule hasikie hata uchungu wowote. 

Hidadi kubwa ya ukali wa moto uliotiwa kwa nafasi ile, uliunguza hata mishipa iliyokuwa pale mpaka kiwango cha huyo mnyama hasikii tena uchungu, ngozi yake inakuwa isiyojali tena na maumivu. Utu wote wa maumivu unapotea.   

 Ni katika hali hiyo dunia inayokuwa kwa sasa. 

Wao walitiwa chapa na zambi na walipoteza utu wa uchungu na maumivu yote ya zambi, na kwa chochote kile kinachoangalia zambi, wao hawasikie tena hata majuto yoyote. 


17/ kuna neno moja la muhimu lenye nilitamani kuonesha hapa: 

Watu wenye wanakuwa na bahati yakusikia Habari njema mara kwa mara, lakini kiisha kuisikiliza, wanaikataa na kuitupa mbali. 

Kuna mara hotuba inawagusa, wanazani kwamba ni vizuri waokoke lakini hawafikie kiwango cha kuamuwa kukamata uamuzi wa kuokoka, wanaendelea kuwa wakaidi na kwa mara hata namna ya kuwafikia tena na Injili inaanza kuwa vigumu, kwa sababu wao wanafikia kiwango cha kutokusikia tena maumivu. 


18/ Waefeso 4: 20 

“Lakini ninyi hamukujifunza Kristo vile,” 

Mtume Paulo anajumulisha yote na kuyafunga tu kwa maneno tano.

Kwa kuonesha kwamba historia ya maisha ya mwamini ni tofauti. 

Hamukujifunza KRISTO kwa namna hiyo

Mtume Paulo anapenda kumaanisha nini na msemwa huo? 

Mwajuwa jibu? 

Waefeso 4: 21 – 23 

“Ikiwa mulimsikia na kufundishwa katika yeye, kama kweli iliyo katika Yesu, 

Mwondoshe, kwa maneno ya mwenendo wenu wa mbele, yule mtu wa zamani, anayeharibika kwa kufuata tamaa za udanganyifu; 

Na mufanywe wapya katika roho ya nia zenu;” 

Muruhusu Roho Mtakatifu abadirishe roho ya nia yenu. 


AMINA.


N°Ref: 06/19/1960/ 222 - THE POWER OF POSITIVE THINKING / 05/04/2021