Thursday, July 14, 2022

RAFIKI KWENYE MIMBARI / A FRIEND ON THE BENCH




 


RAFIKI KWENYE MIMBARI 

A FRIEND ON THE BENCH

May 15, 1977 

Pastor Henry F. Kulp




 

Wakolosayi 1: 16 – 19 

“Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa vilivyo mbinguni na vilivyo duniani, vitu vinavyoonekana na visivyoonekana, ikiwa ni viti vya wafalme au usultani au falme au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake na kwa ajili yake. 

Naye ni mbele ya vitu vyote na ndani yake vitu vyote vinashikamana. 

Naye ni kichwa cha mwili, ulio kanisa; aliye mwanzo, mzaliwa wa kwanza kutoka katika wafu; ili apate kuwa wa kwanza katika yote. 

Kwa kuwa katika yeye ilipendeza utimilifu wote ukae;”  

         Ndani ya Maandiko haya, Mtume Paulo anaonesha kwamba Kristo ndiye Bwana wa vyote vilivyoumbwa. Kristo ndiye Bwana wa uumbaji. 

Katika uwepo wa uumbaji, Kristo hana mpinzani. 

YEYE NI KIONGOZI JUU YA YOTE ULIMWENGUNI. 

Tufahamu kwa makini neno inayosemwa kwa mwisho wa aya ya 16:

VITU VYOTE, viliumbwa kwa ajili yake na kwa njia yake.  

Kwa kweli tungaliweza kuyasoma kama ifwatavyo: 

YOTE YANAYOKUWA NA KUONEKANA, yaliumbwa naye na pia yaliumbwa kwa ajili yake. 

Ni aina ya sarufi ya asili ya neno Dee- a na hii inamaanisha kupitia yeye. 

Kwa hiyo, pahali pa kutumia “kwa yeye” ICE inachochea kabisa, na ingelitafsiriwa kuwa: “kwa matumizi yake” sawasawa na mapenzi yake. 

Hii inatuonesha namna gani yeye ni wa kwanza katika yote ulimwenguni.  

Popote pale unapokwenda, waweza kuweka muhuri isemao: “Iliumbwa na Kristo, kwa ajili ya matumizi yake na mapenzi yake.”  


1/ Namna unavyotumia mazingira, arzi na vitu vilivyo kando kando yako ni muhimu sana. 

Eti, wewe watumia vitu vilivyo ulimwenguni kwa utukufu wa Bwana, kwa utukufu wako binafsi, utukufu wa mtu fulani, ama wa mtu mwengine? 


2/ Aya ya 17, inasema: 

“Naye ni mbele ya vitu vyote.” 

Kwa kweli, kwa luga ya Kigriki, jambo hili lingelitafsiriwa kama ifwatavyo: 

NA DAIMA YEYE NI MBELE YA VITU VYOTE. 

Ni nini vitu vyote? Vitu vyote vilivyoumbwa. 

Yeye ni mbele ya viumbe vyote. 

Hii inamaanisha umilele wa Bwana Yesu Kristo. Yeye ni mbele ya vitu vyote. Yeye ni wa milele. 


3/ Kiisha tunasoma: 

“Na ndani yake vitu vyote vinashikamana.” 

Neno “kushikamana” inayokuwa SOON – AS – STAME inayomaanisha kuambatanishwa na kushikwa pamoja, kuendelea katika hali hiyo hiyo, inayokuwa kinyume ya Kuh – Teed – Zoe inayokuwa tendo linalomaanisha kuumba. 

Bali, hapo haimaanishe kuumba, bali kulinda siyo kuumba. 

Kwa kumaanisha kwamba ni yeye anayeumba, anayelinda pia. 

Ni kusema kwamba Yesu Kristo anashika dunia nzima katika kuambatana kikamilifu. 

Ni yeye anayefanya vitu vya mbinguni viwe kama vilivyo, na ni yeye anayevilinda visijikwae katika mzunguuko wao na viwe kwa mahali vinavyopatikana sasa. 

KUSHIKAMANA inamaanisha kuendelea kuwa. 


4/ Tunapashwa kufahamu kwamba Yesu Kristo ni Nafsi katika Utatu Mtakatifu anaye linda ulimwengu na katika Yeye ulimwengu wote unashikamana. 

Tukumbuke kwamba wakati alipokuwa mtoto mchanga katika sanduku ya kulisha ngombe, Yeye daima alikuwa Mungu, ulimwengu wote ukishikamana pamoja katika Yeye. 

Wakati alipokuwa akitundikwa kwa msalaba, daima alikuwa Mungu, ulimwengu wote ukishikamana pamoja katika Yeye. 

Ni Yeye anayelinda na kushika yote. 

Ingawaje watu wanaweza kutaja Jina lake bure, kukana Umungu wake, bali kila saa na dakika uzima wao unashikwa naye. 


5/ Sheria zenye wanadamu wanazania kuwa sheria za kisayansi, kwa kweli siyo za kisayansi. 

Sheria hizo ni za Kimungu, siyo za kisayansi. 

Sayansi haina jinsi ya kuziamuria kawaida na namna ya kutawala. 

Sayansi haiweze kuakikisha kwamba sheria hizo zitaendelea kuwa kama zilivyo kwa siku ya leo. 

Haina hata budi ya kusema lini litakalokuwa kwa siku za usoni. 

Waebrania 1: 3 

“Yeye akiwa kungaa kwa utukufu wake, na chapa ya nafsi yake mwenyewe, akichukua vitu vyote kwa Neno la uwezo wake, akikwisha kufanya katika yeye utakaso wa zambi zetu, aliketi mkono wa kuume wa Mwenye Ukuu;” 

         Waraka wa Waebrania watuambia kwamba: 

KWA NENO LA UWEZO WAKE YESU KRISTO ANASHIKA NA KUAMBATANISHA ULIMWENGU WOTE PAMOJA. 

Yamaanisha kwamba ni Yesu Kristo anayeleta harabuni kwa sheria hizo. 

Kwa kweli, hii ni kwa wakati wa sasa. 

Kwa sasa, sheria hizi zinatumika sawa kawaida kufuatana na uaminifu wa Bwana Yesu Kristo. Kwa hiyo, katika neno imani, twaona imani ilivo sawa na mawazo ya kibinafsi. 

2 Timoteo 2: 12 

“Kama tukivumilia, tutamiliki pamoja naye: Kama tukimkana yeye, yeye atatukana sisi vilevile.” 

         Yesu Kristo ni Mwaminifu. 

Waroma 3: 3 

“Ni nini basi, kama wengine hawakuamini? Kutokuamini kwao kutafanyiza uaminifu wa Mungu kuwa bure?” 

         Eti ni jambo gani kama wengine hawakuamini? 

Eti, kutukuamini kwao kutafanyiza uaminifu wa Mungu kuwa bure? 

Kwa kweli, hapana hata kidogo. 

Sawa vile jua litaamka asubui mapema, vivyo hivyo dunia itaendelea kuwa jinsi ilivyo, na hii inamaanisha ya kuwa uaminifu wa Mwenyezi Mungu hautabadirishwa kamwe na wasioamini.

Tusome tena katika kitabu cha 2 Timoteo 2: 13 

“kama sisi hatuamini, yeye anakaa mwaminifu; maana hawezi kujikana mwenyewe.” 


6/ Hatavile sayansi yaweza kusema: Tunafahamu kwamba sheria hizo ni kamilifu na zitatumikishwa kwa miaka na miaka, hata hivyo hawasemi kweli, hawana sheria sababu kwa gafla mabadiriko yanaweza kutukia.  


7/ 2 Petro 3: 10 – 12 

“Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwizi; katika siku hii mbingu zitatoweka na sauti kubwa, na viumbe vya asili vitayeyushwa kwa moto mkali, na inchi na kazi zilizo ndani yake zitateketezwa. 

Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitayeyushwa hivi, ingewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utawa, 

Mukitazamia na kutaka sana, kuja kwa siku ya Mungu, kwa sababu yake, mbingu zikiungua, zitayeyushwa, na viumbe vya asili vitayeyuka kwa moto mkali?” 

         Jameni, ningelipashwa kusema: 

Kama haingelikuwa uaminifu wa Bwana Yesu Kristo kushika vitu vyote hivi kushikamana pamoja, ulimwengu wote ungelipambazuka na kugawanyika na kusagika kama mavumbi na kupeperuka. 

Uaminifu wake unaendelea daima hata kwa punje ya dakika chache. 

Haingelikuwa uaminifu wa Bwana Yesu Kristo, Miradi yetu ya utafiti na  kwenda angani kufika kwenye mwezi na kuendelea, miradi hiyo haingeli wezekana.

Katika ulimwengu huu, kama haingalikuwa Bwana Yesu Kristo na uaminifu wake, haingeliwezekana kutuma ndege ya kusafiri kati anga na kufika kwa mwezi na kuruhusu mtu aweke mguu wake kwenye mwezi. 

Watu wa sayansi, walitumia tu kwa makini sana sheria za kimungu, zilizo shimikwa na Mwenyezi Mungu, na kufikia kiwango cha kutuma mtu kukanyaga juu ya mwezi. 

Hatungeliweza kufanya ujumbe wa utafiti kwa sayari za kidunia, kama sayari Marci na Venuchi, kama haingelikuwa Bwana Yesu Kristo na Uaminifu wake katika sheria za Kimungu. 


8/ Ni kusema kwamba, na twasema haya na heshima na pongezi yote kwa Bwana Yesu, kwamba Bwana Yesu ndiye Gundi inayo gandisha ulimwengu wote kushikamana na kubanana pamoja. 


9/ Bila shaka siku inakuja yenye ulimwengu haitakuwako tena. 

Yesu Kristo ataiachilia, na ataifanya isishikamane tena pamoja. 

2 Petro 3: 10, 11 

“Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwizi; katika siku hii mbingu zitatoweka na sauti kubwa, na viumbe vya asili vitayeyushwa kwa moto mkali, na inchi na kazi zilizo ndani yake zitateketezwa. 

Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitayeyushwa hivi, ingewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utawa, 

Mukitazamia na kutaka sana, kuja kwa siku ya Mungu, kwa sababu yake, mbingu zikiungua, zitayeyushwa, na viumbe vya asili vitayeyuka kwa moto mkali?” 

         Kwa aya ya 11 anasema: 

Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitayeyushwa hivi. 

Neno “kuyeyushwa” ni ya manufaa nyingi katika Kigriki.  

  

Neno hili linatumikishwa ndani ya kitabu cha Luka 3: 16 

“Yoane akajibu akiwaambia wote: 

Mimi ninawabatiza ninyi kwa maji, lakini mmoja anakuja, mwenye uhodari kuliko mimi, sistahili kufungua kamba ya viatu vyake; Yeye atawabatiza ninyi kwa Roho Mtakatifu, na kwa moto.” 

         Yoane Mbatizaji alisema hapa kwamba: 

Yeye aliye mwenye uhodari kuliko mimi, hata sistahili kufungua kamba ya viatu vyake. 

“Kufungua”, alitumia msemwa “kufungua kiato”, ni picha hili twapasha kuweka kwa ulimwengu, utakuwa wenye kufunguliwa, usiojikusanya pamoja. 

Dunia itakuwa yenye kufunguliwa. 


10/ Sisi watu wa siku za leo tunafahamu nini inayotukia kama chembe ndogo la maumbile linagawanywa, kama atomu inagawanyika. 

Jambo ambalo linatukia kama atomu haishikamane pamoja, inagawanywa na kuvunjwa. 

Kweli, umbalimbali na watu walioishi mbele yetu, sisi watu wa siku za leo,  kufwatana na mifano kazaa, tunayo urahisi wa kusikia kwa makini sura hii na hata Waraka wa Wakolosayi sura ya kwanza. 

Karne yetu inaitwa “Karne ya anga” 

Sisi tunafahamu kwamba bomu la atomu ni matokeo ya kugawanywa kwa atomu. 

Bomu la atomu linakuwa na mungurumo na mulipuko kubwa sana, tunakumbuka yaliyo pita huko Hiroshima na Nagasaki na hiyo ni picha tu ndogo ya majira yenye yatatukia katika 2 Petro 3: 10 – 11, wakati Mwenyezi Mungu atafungua ulimwengu. 

Tusome tena yanayoandikwa katika Kitabu cha : 

Ufunuo 21: 1 

“Nikaona mbingu mpya na dunia mpya; kwa maana mbingu za kwanza na dunia ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana habari tena.” 

Bomu la atomu. 

Isaya 66: 22 

“Kama vile mbingu mpya na inchi mpya, ambazo nitazifanya zitabaki  mbele yangu, Bwana anasema, ndivyo uzao wenu na jina lenu litabaki.” 


11/ Musihofu hata munavyosikia kwamba kuna yule mwenye kuwa na kifungo ndogo cha amri kwenye anaweza kufinya na kuunguza na kuharibu na kubomoa dunia mara moja, iwe Mosku, iwe Washingtoni, hakuna kati yao mwenye uwezo wa kuharibu dunia. Siyo wao watakaoharibu dunia. 

Ni Bwana Yesu Kristo Mwenyewe anaye ile uwezo, ni Yeye atakayearibu dunia. 

Hakuna yule atakayeanzisha vita vya kutumia ma bomu ya atomu kama dunia nzima haijapokea Injili, Habari Njema. 

Aya ya 17 - 18 

“Naye ni mbele ya vitu vyote na ndani yake vitu vyote vinashikamana.

Naye ni kichwa cha mwili, ulio kanisa; aliye mwanzo, mzaliwa wa kwanza kutoka katika wafu; ili apate kuwa wa kwanza katika yote.” 

         Kichwa cha Mwili, Mwili mmoja. 

Wakwanza aliyefufuka toka wafu. 

Yeye ni Kichwa cha Mwili, Kanisa.

Yeye si kichwa hapa duniani, lakini Kichwa katika pahali pa Mbingu. 

Matendo 7: 8 

“Yeye ndiye aliyekuwa katika kanisa jangwani pamoja na yule malaika aliyesema naye katika mlima Sinai, tena pamoja na baba zetu; ndiye aliyepokea maneno ya uzima atupe sisi.” 

Waebrania 2: 12 

“akisema: Nitahubiri jina lako kwa ndugu zangu; 

Katikati ya kanisa nitakuimbia sifa.” 

Zaburi 22: 22

“Nitahubiri jina lako kwa ndugu zangu; 

Katikati ya kusanyiko nitakusifu.” 

1 Timoteo 3: 15 – 16 

“lakini kama nikikawia, upate kujua sana namna inavyokupasa kutenda katika nyumba ya Mungu, iliyo kanisa la Mungu aliye hai, nguzo na msingi wa kweli. 

Na pasipo shaka, siri ya utawa ni kubwa: 

Mungu alionekana katika mwili, 

Alihesabiwa kuwa na haki katika Roho, 

Alionekana na malaika, 

Aliubiriwa katika mataifa, 

Aliaminiwa katika ulimwengu, 

Alipokewa katika utukufu.”   

  

Yeremia 32: 37 – 38 

“Tazama, nitawakusanya, na kuwatoa katika inchi zote ambazo niliwafukuza, katika hasira yangu, na uchungu wangu, na gazabu yangu nyingi; nami nitawaleta tena hata pahali hapa, nami nitawakalisha salama; 

Nao watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao.” 

Waebrania 10: 7 

“Halafu nilisema: Tazama, nimekuja(katika gombo la kitabu nimeandikiwa)

Nifanye mapenzi yako, Mungu.” 

 

AMINA.    

 

N°Ref: 05/15/1977/ 353-1 - A FRIEND ON THE BENCH / 07/14/2022