Monday, November 23, 2020

KUZALIWA KWA KANISA / THE BIRTH OF A CHURCH

Photo by B Smith from the patio

 



KUZALIWA KWA KANISA 

THE BIRTH OF A CHURCH

January 6, 1963 

Pastor Henry F. KULP



 

1Watesalonika 1: 1 – 5 

“Paulo, na Silvano, na Timoteo, kwa kanisa la Watesalonika katika Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo: Neema iwe kwenu na salama toka Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo. 

Tunashukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu ninyi wote, tukiwataja ninyi katika maombi yetu; tukikumbuka pasipo kuacha kazi yenu ya imani, na taabu yenu ya mapendo, na saburi yenu ya tumaini katika Bwana wetu Yesu Kristo, mbele ya Mungu Baba yetu; tukijua, ndugu munaopendwa na Mungu, kuchaguliwa kwenu, sababu Habari Njema yetu haikufika kwenu katika neno tu, lakini vilevile katika uwezo na katika Roho Mtakatifu, na katika matumaini mengi; sawasawa munavyojuwa tulikuwa watu wa namna gani katikati yenu kwa ajili yetu.” 

Kama vile tunavyoanza majifunzo ya Waraka huu wa Mtume Paulo kwa Watesalonika, nilitamani mufahamu kwamba kuna sababu nyingi mbalimbali zinazosukuma wakristo kufurahia na kupendalea faida na manufaa nyingi ya kipekee wanayopata katika kitabu hiki cha Watesalonika.  

Sababu ya muhimu ya kwanza ni kwamba Waraka wa kwanza wa Mutume Paulo kwa Watesalonika ndiyo Barua ya kwanza Mtume Paulo alioandika kwa Maongozi ya Roho Mutakatifu. 

Tuone kwa kifupi yanayokuwa katika Waraka huu wa kwanza kwa Watesalonika: 

Waraka wa Kwanza kwa Watesalonika una sura tano: 

Sura ya kwanza inatuonesha namna gani kuja kwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo kunaambatana na wokovu wetu. 

Sura ya pili inasema juu ya Siku ya Bwana, ikiiambatanisha na huduma ya mwamini. 

Sura ya tatu inaambatanisha kuja kwa Mwokozi Yesu Kristo na utakaso. 

Sura ya ine inaambatanisha kuja kwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo na ufufuko wa wale waliokufa katika Bwana Yesu Kristo. 

Sura ya tano inahitimisha sura zote tano za Waraka wote nzima, na  inasema juu ya salama ya mwamini katika hizo siku za mwisho zenye zitakuwa za hatari, na hiyo hali ya mateso ndiyo itaonesha dalili za mwisho za kuja kwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo.

 1/ Kuna jambo la muhimu lenye tunapata katika Waraka wa Watesalonika.

 Ni kwamba, wengi wa watu waliokuwa wanamemba kwa mwanzo wa kanisa la Tesalonika walikuwa wakristo wachanga wenye bado kutimiza umri wa mwaka moja ndani ya maisha ya kikristo. 

Lakini hiyo haikuwazuiza kuwa na ufahamu, matendo, kanuni na tabia nzuri katika mwenendo wa imani ya kikristo. 

Nikusema: Utakaso, Amani ya milele, Utatu Mtakatifu, Ufufuko, Siku ya Bwana. 

Hii inatuonesha picha ya matunda ya yeyote yule anayejitoa kwa huduma ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo.

 2/ Ni halali kujuwa ya kwamba, Mtume Paulo alihesabu kanisa hili kuwa la muhimu sana.  

Mtume Paulo alihesabu kanisa lile sawasawa wazazi wanavyo hesabu mtoto wao mchanga. 

Mtume Paulo anajihesabu mwenyewe kama mchungaji wa watoto anayependa na kuchunga watoto wake mwenyewe. 

 3/ Waraka huu uliandikwa miaka makumi mawili nyuma ya kusulubiwa na kufufuka kwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 

4/ Mambo tunayoyaona kuhusu kanisa hili la Tesalonika yanatuonesha namna gani Mwenyezi Mungu anavyo anzisha na kuunda makanisa; namna gani kanisa linazaliwa na jina kanisa, inamaanisha mkusanyiko wa watu. 

 5/ Tuchunguze neno tunalopata katika 1Watesalonika 1: 5  

“Sababu Habari Njema yetu haikufika kwenu katika neno tu, lakini vilevile katika uwezo na katika Roho Mtakatifu, na katika matumaini mengi; sawasawa munavyojuwa tulikuwa watu wa namna gani katikati yenu kwa ajili yenu.” 

Habari Njema yetu haikufika kwenu katika neno tu, lakini vilevile katika uwezo na katika Roho Mtakatifu, na katika matumaini mengi  

Vinyume  na matunda ya kuhubiri na kutangaza Injili vilikuwa vya maajabu sana na baada ya majuma machache kanisa lilizaliwa na kuundwa na kuwa na mizani ya kuyashinda  mateso na mashambulio ya aina mbalimbali. 

 6/ Kwa miaka 315 (Mbele ya Yesu Kristo), Kasandra mmoja wa Wakubwa wa Jeshi ya Mfalme Alegzandro Mkubwa, aliujenga muji ule na akaupanga jina la mmoja wa wadada wa Mfalme Alegzandro, dada aliyefika kuwa muke wa Mkubwa wa majeshi Kasandra na muke huyo jina lake lilikuwa Tesalonika, sawa vile vile Vitabu vya Ruta na Esteri katika Agano la Kale vina majina ya wanawake; vilevile china ya jina la Kitabu ya Watesalonika ilitoka kwa Mwanamuke aliyejulikana sana. 

7/ Mtume Paulo alifika kwa muji huu katika safari yake ya pili ya Injili. 

Paulo na Sila walikuwa kwa Wafilipi na huduma yao ilikuwa ikikatwa na mapigo, vifungo, kuachiliwa toka kifingo, na kushurtishwa kutoka katika muji fulani. 

Wakati walipotoka kwa Filipi, wakaenda Tesalonika. 

Ningelipendelea mufwate kwa makini sana yale yanayosemwa katika Kitabu cha 1 Watesalonika 2: 2 

“lakini tukikwisha kuteswa mbele na kutendewa jeuri, kama munavyojua, katika Filipi, tulikuwa na uhodari katika Mungu wetu kuwaambia ninyi Habari Njema ya Mungu katika kuishindania sana.” 

Mtume Paulo iko anapana ushuhuda namna gani aliwahubiri Injili kwa uhodari katika kutendewa jeuri nyingi. 

Kwa kweli alikua angali bado na uchungu ya mapigo aliyopigwa katika Filipi. 

Alikua angali bado na vidonda na chapa za fimbo zilizo chubua mwili, navyo vilikuwa bado kupona kwa uso wake na kichwa nzima hata pia nguo zake zilikuwa zenye kupasuka kwa fimbo na nguo hizo zilipashwa kutengenezwa na kushonwa kwa nyuzi. 

Mtume Paulo hakuruhusu hiyo kutendewa jeuri na mapigo na matukio yote aliyoyapata iwe na mamlaka juu ya huduma yake ya kuhubiri Injili. 

Watu wengine wangaliweza kusema: 

“Sitaendeleya kumutumikia Mwokozi Yesu katika hali hii ngumu, nitaacha kwanza na kupumzika.” 

Tumshukuru Mwenyezi Mungu sababu Mtume Paulo yeye hakukusudia kukamata hatua hiyo, na hakukubali kubaki sawa mtu mvivu. 

Hata hakusema:”Mimi ni muzaifu wa mwili, sina nguvu mwilini ili nimuhudumie Bwana wetu Yesu Kristo, bali, katika yote alipata nguvu na kusonga mbele katika kumuhudumia Mwokozi.” 

 8/ Mutatambua mahali Mtume Paulo alipoenda mbele ya pahali pengine. 

Matendo ya Mitume 17: 23  

“Kwa sababu nilipokuwa nikipita nilitazama vitu vya kuabudu kwenu, niliona mazabau yenye maandiko haya: 

Kwa Mungu yule asiyejulikana. Basi yule ambaye munamwabudu pasipo kumjua, ndiye mimi ninawahubiri ninyi habari zake.” 

Kwa siku ya sabato, aliingia katika sinagogi. 

Kwanza, kuna jambo linalotupasa sisi tufahamu hapa. 

Alizungumuza pamoja nao kufwatana na maandiko. 

Kiongozi na msingi wa mazungumuzo yao ilikuwa tu Maandiko Matakatifu. 

Kuna watu wamoja wanaojiita wakristo, nao wanasema kwamba kwa nyakati zile, Biblia Takatifu ilikuwa bado haijakuweko. 

Kwamba hakukukuweko Biblia Takatifu hadi wakati kanisa iliwapa Biblia. 

Eti, nyinyi munaamini wazo lile? 

Chunguzeni mambo iliyofanyika kwa kanisa la Beroya. 

Matendo ya Mitume 17:11  

“Watu hawa walikuwa wema kuliko wale wa Tesalonika, kwa sababu walipokea Neno kwa nia iliyokuwa tayari kabisa, walitafuta Maandiko kila siku kujua hakika ya maneno yale.” 

Tunaona hapa kwamba wakristo wa kanisa la Beroya walikuwa wema kuliko wale wa Tesalonika, kwa sababu walipokea Neno kwa nia iliyokuwa tayari kabisa. Neno ni Maandiko inayokuwa  ndani ya Biblia Takatifu. 

Nikusema Neno ni Biblia Takatifu, na inasemwa kwamba wao walipokea Neno kwa nia iliyokuwa tayari kabisa, walitafuta Maandiko kila siku kujua hakika ya maneno yale.

Kanisa la fasi linapashwa kujengwa juu ya Maandiko, hapana juu ya desturi za watu, hapana juu ya kitu kingine isipokuwa Maandiko Matakatifu. 

 9/ Mahali tufikapo, kuna neno lingine la muhimu sana lenye tunapashwa kujuwa na kufahamu kwa makini yote. 

Waamini wa Tesalonika walikuwa Viumbe vya Kanisa Mwili wa Kristo.  

Kuna wale wanaokuwa na mafikili juu juu tu bila msingi na wanasema kwamba kanisa iliundwa kiisha Matendo 28: 28.  

“Basi ijulikane kwenu ya kuwa wokovu huu wa Mungu umepelekwa kwa Mataifa, nao watasikia.” 

Kusema namna wale watu wa juu juu wanavyosema ni upumbafu tu bila maana. 

Ninyi munazani Mtume Paulo alihubiri Injili gani kule Tesalonika? Ama kule Beroya? 

Eti munafikiri Mtume Paulo alihubiri Habari Njema ya Ufalme wa Mungu? Hapana hata kidogo. 

Biblia haitupatiye hata ushahidi moja ya kusema kwamba Mtume Paulo aliweza kuhubiri Injili ya Ufalme wa Mungu, iitwao tena Injili ya wenye kutahiriwa. Yeye hakufanya hivyo hata mara moja. 

Jameni niwasomee kitabu cha Wagalatia 2: 7 

“Lakini mbali na maneno haya, walipoona ya kuwa niliwekwa kwa Habari Njema ya wasiotahiriwa, kama vile Petro alivyowekwa kwa Habari Njema ya waliotahiriwa;” 

Mtume Paulo anaonesha tofauti na kutia umbalimbali kati ya Habari Njema hizi mbili mbalimbali.

Pale ni mwanzo wa huduma yake. 

Mutatambua ya kwamba hii siyo nyuma ya Matendo ya Mitume 28: 28. 

Habari Njema ya Waliotahiriwa ilipewa kwa Petro na Habari Njema ya Wasiotahiriwa ilipewa kwa Paulo

Siyo kusema kwamba Mtume Paulo alihubiri kwa muda Habari Njema ya Waliotahiriwa kiisha punde kidogo njo akaigeukia Habari Njema ya Wasiotahiriwa. 

Hapana hata kidogo, Mtume Petro pamoja na Mitume wengine walifahamu wazi wazi kwamba Mtume Paulo ni muhubiri wa Habari Njema ya Wasiotahiriwa. 

Yeye hakuhubiri Habari Njema ya Ufalme wa Mungu, alihubiri tu Yesu Kristo, namna gani Alikufa kwa ajili ya zambi zao, na kwamba wokovu unapatikana kwa njia ya kuamini tu Yeye Kristo Yesu. 

10/ Jameni muniruhusu niwahakikishie kwamba Mtume Paulo hakujaribu kuhubiri maneno mawili ambao Mtume Petro alikuwa na zoezi ya kuhubiri. 

 Pia ni muhimu mutambue tofauti kati ya Huduma ya Mtume Petro Katika Habari Njema ya Ufalme wa Mungu na Huduma ya Mtume Paulo katika Habari Njema ya Neema ya Mungu. 

Neno la kwanza ni kwamba Mtume Paulo hakuwa anaalika Wayuda kusema kwamba Mataifa hawana sehemu katika Kufa kwa Bwana wetu Yesu Kristo, kama vile Mtume Petro alikuwa na zoezi ya kufanya.  


Tufahamu kwamba Neno la Mungu katika Matendo ya Mitume 2: 23 -36, 38  

“Huyu alitwaliwa nanyi kwa shauri lililokusudiwa, na kwa kujua kwa Mungu tangu zamani, nanyi mulimsulibisha, mukamwua kwa mikono ya watu wabaya. 

Lakini Mungu alimfufua, akilegeza uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao. 

Maana Daudi anasema juu yake: 

Niliona Bwana mbele yangu siku zote, kwa kuwa yuko kwa mkono wangu wa kuume, nisitikisike. 

Kwa hili, moyo wangu ulipendezwa, ulimi wangu ukafurahi: 

Tena mwili wangu nao utakaa katika matumaini. 

Kwa maana hutaniacha roho yangu katika Hadeze. 

Wala hutatoa Mtakatifu wako aone uharibifu. 

Umenijulisha njia ya Uzima; 

Utanijaza furaha kwa uso wako. 

Ndugu, muniruhusu niseme pasipo woga mbele yenu habari za baba yetu mkubwa, Daudi, ya kuwa alikufa, akazikwa, na kaburi lake ni kwetu hata leo. 

Basi kwa sababu alikuwa nabii, akajua ya kuwa Mungu alimwapia kwa kiapo, ya kwamba toka uzao wake, kwa namna ya mwili, atanyanyua Kristo akae katika kiti cha ufalme. 

Akitangulia kuona maneno haya, alisema habari za ufufuko wake Kristo, ya kama nafsi yake haikuachwa katika Hadeze wala mwili wake haukuona uharibifu. 

Huyu Yesu, Mungu alimfufua, na sisi sote tuko washuhuda wake. 

Basi akikwisha kupandishwa hata Mkono wa kuume wa Mungu, na kupokea kwa Baba ahadi ile ya Roho Mtakatifu, amemwanga hili munaloona sasa, na kulisikia. 

Maana Daudi hakupanda katika mbingu, lakini yeye mwenyewe alisema: 

Bwana alimwambia Bwana wangu, keti kwa mkono wangu wa kuume, 

Hata niweke adui zako chini ya miguu yako. 

Basi kila nyumba yote ya Israeli ijuwe kwa kweli, Mungu amefanya huyu Yesu ambaye mulimsulibisha kuwa Bwana na Kristo. 

38: Petro akamwambia: Tubuni mukabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mupate ondoleo la zambi zenu, nanyi mutapokea zawadi ya Roho Mtakatifu.” 

Munatambua kwamba Mtume Paulo hajahubiri hata mara moja maneno kama yale. 

Yapili ni kwamba, haizuru hapa ama nafasi nyingine Mtume Paulo hakuhubiri juu ya habari ya kuja kwa Bwana Yesu na kushimikwa kwa Ufalme kwa namna inavyosemwa hapa na Mtume Petro. 

Matendo ya Mitume 3: 19 – 21 

“Tubuni basi, mugeuke, ili zambi zenu ziondoshwe, zipate kuja nyakati za ufufuko toka uso wa Bwana, 

Apate kutuma Kristo aliyehubiriwa kwenu, tangu zamani; ndiye ilimpasa kupokewa mbinguni hata wakati wa kutengenezwa kwa maneno yote, ambayo aliyasema Mungu kwa vinywa vya manabii yake watakatifu tangu mwanzo wa ulimwengu.”  


11/ Hiyo ilikuwa mahubiri ya mastaajabu. 

Ni kwepesi sana kufikili namna makusanyiko ya watu yangefanya umate wa watu katika masinagogi, uvuguvugu ulioletwa na kawaida hii mupya ya mafundisho. 

Matokeo ya huduma hiyo ni kwamba Wayuda wengi waliacha njia zao na kumufwata Yesu, waliamini, na kweli katika masinagogi haya yote kulikuwa wanafiki wapagani wengi.  

Umati wa watu wengi ulipokea hiyo ushuhuda na kulikuwa wanawake wengi wenye kujulikana sana wenye waliamua kupokea Bwana Yesu Kristo kama Bwana na Mwokozi. 

Kwa mwangaza wa Waraka wa Mtume Paulo kwa Watesalonika, tunavumbua ya kwamba, kanisa lile kwa mwanzo liliundwa na watu wenye walikuwa wakiabudu miungu na wachache wao walikuwa wakitoka kwa dini ya Kiyuda, ili wageuke kuwa Wakristo. 

Kwa hiyo tusome 1 Watesalonika 1: 9  

“Kwa sababu wao wenyewe wanatangaza habari zetu, namna tulivyoingia katikati yenu; na namna gani mulivyogeuka kwa Mungu toka sanamu, kutumainia Mungu aliye hai, na Mungu wa kweli.”

12/ Kuna viongozi vya makanisa wenye wanakua wazito kuamini.                    Na ni viongozi wa dini ndio waliokuwa wanakataa kuamini, wakiongozwa na nia yao mbaya, walishawishi watu wa ngazi za chini, wasiokuwa na akili timamu. Watu wa aina ile, wasiokuwa na kazi kamili, wanaponda muda wao wakizunguka zunguka ndani ya soko na wao ni wepesi kwa kuleta ugonvi na fujo na kelele.

Na hawa watu walikumba mji mzima kwa kelele sana na hata walishambulia nyumba ya Jasoni mahali Paulo na Sila walikuwa wakikaa. 

Aya ya sita inatuambia namna walifanya kivumbi na jasho. 

Vinyume na matunda ya huduma ya Paulo ilionesha chapa ya mataajabu. 

Ningelitamani hata sisi kwa siku za leo kazi yetu iwe na ushuhuda wa namna ile.  

Kwa siku za leo dunia inakuwa ya kusumbuka, kuangaika na kuyumbayumba.

Masingizio na machongezi walio singizia Paulo na Sila hayakuwa na msingi, hata hivyo, Paulo na Sila walikusudia kutoka Tesalonika na kwenda zao Beroya. Wakiacha tayari kanisa ya maastajabu na tukufu imekwisha kuzaliwa katika muji ule. 

13/ Waraka huu wa kwanza Mtume Paulo kwa kanisa la Tesalonika, aliuandika bado akiwa pa Korinto.

 Ilikuwa kwa mwisho wa safari yake ya pili ya Injili. 

Timoteo alikuwa akija toka safari ya maonyo na mafundisho na kuletea kanisa lile changa moyo, na alimletea Mtume Paulo ripoti kuhusu kanisa lile. 

1Watesalonika 3: 6 – 7 

“Lakini wakati Timoteo alipokuja kwetu sasa toka kwenu, alituletea sisi habari njema ya imani yenu na mapendo yenu, na ya kwamba munatukumbuka vema siku zote, mukitamani kutuona sisi, kama sisi kuwaona ninyi; 

Kwa sababu hii, ndugu, tulifarijiwa kwa habari zenu katika taabu yetu yote na mateso yetu kwa sababu ya imani yenu;” 

Walikuwa wakitamani kumuona Mtume Paulo na yeye pia vile vile kwa upande wake alifurahi  kuona wanashimama imara  hata katika mateso na taabu  wakikumbwa na shida na matatizo na kupitia mambo mazito sana. 

Walikuwa wakipita katika taabu sababu ya imani yao kwa Mwokozi Yesu Kristo.  

14/ 1Watesalonika 1: 1 

“Paulo na Silvano, na Timoteo, kwa kanisa la Watesalonika katika Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo: Neema iwe kwenu na salama toka Mungu Baba yetu, na Bwana Yesu Kristo.” 

Hapa tuna desturi ya salamu ya Mtume Paulo na kwa njia ya salamu yake anabariki na kuomba Neema juu ya kanisa lile changa la Watesalonika. 

Neema ni zaidi kuliko huruma, neema ni zaidi kuliko huruma ya zabuni. 

Neema ni zaidi kuliko wingi wa zabuni ya huruma. 

Neema ni zaidi kuliko mapendo. 

Neema ni Mwenyezi Mungu kutupatia vyote pasipo malipo. 

Tutambue kwamba Neema inatoka kwa Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo. 

Neema haitoke kwa Mitume, ama kwa njia yoyote ile ya kidunia, ama kwa namna gani yoyote ingine. 

Baadaye tunayo Amani. 

Amani haiwezi kudumu kati ya watu ama ndani ya roho za watu kama siyo kwa njia ya Neema. 

Tufahamu pia namna maneno haya mawili yanayopangwa. 

15/ Aya ya 2 (1Watesalonika 1: 2)   

“Tunashukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu ninyi wote, tukiwataja ninyi katika maombi yetu;” 

Mwatambua namna gani Mtume Paulo iko mwaminifu katika maombi? 

Ninajiuliza kama sisi tunazidi kuombeana sisi kwa sisi, kuombea mahitaji yetu na kuombea majirani wetu wanao tuzunguuka. 

Sababu hapa tunayo kanisa yenye inayokuwa katika upungufu wa kukosa walimu. 

Kanisa iliyozaliwa katika muji ya watu wasioabudu Mungu, muji unaokuwa katika desturi na tabia nyingi chafu. 

Kanisa lililopata tu juma chache ya mafundisho na maadibisho mbele ya kuachwa pekee katika nafasi inayojaa watu wasio mucha Mungu na wenye kuchukia Habari Njema. 

16/ Tutambue ya kwamba Mtume Paulo hakuombea vitu kwa jumla, sababu kuomba tu kwa jumla bila kutaja neno kwa neno ama ya horoza ya neno ya kuombea, hiyo siyo kuomba hata kidogo.  

Mtume Paulo alifahamu kwa makini nini anayo ombea na shida gani anayoombea. Yeye aliombea kanisa la Watesalonika na yawezekana alikuwa na horoza ya maneno aliyoyaweka katika maombi yake. 

17/ Kwa mwisho tutambue neno hili: 

Tunashukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu.  

Mtu mwenye anaombea wengine na kushukuru Mwenyezi Mungu kwa makuu na wema anayotendea watu wengine, siyo mtu mchoyo ama mwenye kujipenda binafsi. 

Mtu mchoyo ama mwenye kujipenda binafsi hana muda katika maisha yake kwa kuombea wengine ama kushukuru kwa mema Mwenyezi Mungu anayotendea wengine.  


18/ Aya ya 3 inasema: 

“tukikumbuka pasipo kuacha kazi yenu ya imani, na taabu yenu ya mapendo, na saburi yenu ya tumaini katika Bwana wetu Yesu Kristo, mbele ya Mungu Baba yetu;” 

Kuna mambo matatu ya muhimu katika Andiko hili: Imani, Tumaini, Mapendo. 

Siyo tu kwamba Mtume Paulo anashukuru Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo kwa niaba ya waamini hawa kwa ajili ya Imani, Tumaini na Mapendo, lakini zaidi anashukuru Mwenyezi Mungu kwa ajili ya matukio na matunda ya kazi ya mambo haya matatu Imani, Tumaini na Mapendo. 

Matokeo ya kazi inayosukumwa na maneno haya matatu yanafanya sasa maneno haya yapate kupapaswa. 

Imani, Tumaini na Mapendo yanapapaswa na kuonekana na mecho,kupitiya kazi mbalimbali inayotendeka kwa njia ya maneno haya matatu. 

Mambo haya matatu kwa kweli hayana maumbile, lakini matunda ya kazi yanayo timiza yanapapaswa kwa namna ya kimwili. 

Tutambue tena ya kwamba maneno haya matatu yanadumu. 

1Wakorinto 13: 13 

“Basi sasa inadumu Imani, tumaini, mapendo, hizi tatu; lakini neno kubwa katikati ya maneno haya ni mapendo.” 

Mambo mengi ni kwa muda kitambo tu. 

Ujana, afya, bahati za maisha, marafiki, watu maalum wanaokuwa na faida nyingi na manufaa sana kwetu. 

Wamoja wanapotea moja kwa moja na kusahaulika, na wengine wanapeperuka kwa haraka sana kama mvuke. 

Bali, tutambue kwamba haya maneno matatu ni ya kudumu na moja kati ya haya ni kubwa kuliko wenzake na ni Mapendo. 

Tupate mwangaza kwa Aya ya 8 ya 1Wakorinto 13, kwa kuchunguza maneno haya matatu. 

“Mapendo hayapunguki hata kidogo: Lakini kama ukiwa unabii, utaondoshwa, kama zikiwa lugha, zitakoma, kama yakiwa maarifa, yataondoshwa.”

Unabii utaondoshwa, lugha zitakoma, maarifa yataondoshwa. 

Kwa kweli, maneno haya matatu yanaweza kutenda kazi kubwa ya kuonekana katika maisha ya mwamini. 

Imani inazaa matunda kama vile muti wa tunda la tufaha linazaa matunda. 

Muti wa tufaha kama linachungwa vizuri, lina mimiwa maji, liko na afya njema na kupandwa kwa udongo nzuri wenye mboleo, muti huo unazaa matunda mengi. 

Ni namna sawa njo Imani inazaa matendo mazuri. 

Na hapo Mtume Paulo iko anashukuru Mwenyezi Mungu kwa sababu Imani yao ilizaa matunda. 

Baada ya hayo, tunaona kazi ya nguvu na kujitoa ya Mapendo.  

Neno kazi la nguvu linamaanisha kazi ya taabu na yenye kuchokesha, kazi inayoleta uregevu mno. 

Mapendo inatimiza makuu sana zaidi  kuliko Imani inayozaa matunda. 

Mapendo inatusukuma kutumika kwa nguvu yetu yote hadi kufikia kiwango cha kuvunjika viungo na kutoweka. 

Wakristo wengi hawaja jaribu kujitoa na kutumika namna ile. 


Hawapendi kujitoa na kutumikia Mwokozi wetu hadi kiwango cha kuvunjika viungo na kutoka pumzi. Na kama wakitumika namna sawa wanaanza kunungunika wakisema: Kwa kuendelea kutumika namna hii tutafikia hatua ya kupoteza viungo moja moja vya miili yetu. Bali, kwa hawa waamini wa Watesalonika, Mapendo iliwasukuma wawe na hamu zaidi na nguvu ya kujitoa zaidi tena katika kazi ya Bwana na Mwokozi Yesu Kristo. 

Pia tuna Tumaini, siyo tu Tumaini, lakini tumaini inayo zaa saburi, uvumilivu. 

Nina uhakika kwamba neno hili linahitajika katika maisha ya kila mwamini. 

Kwa siku za leo na kwa maisha yetu ya siku hizi, uvumilivu unakuwa neno inalokosekana kabisa. 

Lakini Mwenyezi Mungu anahitaji sote tuwe na Uvumilivu. 

Njia ya kuwa na uvumilivu ni katika Matumaini ama Tumaini. 

19/ Tutambue kwamba Aya ya tatu ya 1Watesalonika 1 inakamilisha masemo na neno moja la muhimu sana: 

“Tukikumbuka pasipo kuacha kazi yenu ya imani, na taabu yenu ya mapendo, na saburi yenu ya tumaini katika Bwana wetu Yesu Kristo, mbele ya Mungu Baba yetu;” 

Siyo tu kwamba Mtume Paulo aliona maneno haya matatu Imani, Tumaini na Mapendo, lakini ni hivyo alivyoona Mungu Baba wetu. 

Hii inatufikisha kwenye ulizo moja kubwa na la maana lenye kila mmoja wetu angelipashwa kujiuliza binafsi. 

Ni kitu gani Mwenyezi Mungu Baba yetu anayoona katika roho zetu? 

Matumaini ya kweli ndani Yake? 

Mapendo ya kweli kwa kumuhudumia na kumutumikia? 

Tumaini ya kweli inayozaa saburi maishani mwetu? 

Ni kweli kwamba Mwenyezi Mungu anatizama roho zetu, pia anarikodi yote yanayopita katika roho yetu. 

Watu wanazania kwamba ni yale wenzao wanayowaza juu yao ndiyo ya muhimu, lakini siyo vile. 

Kwa nyuso yako unaweza kuonesha furaha na hali nzuri, bali Mwenyezi Mungu anatambua kama wewe kwa kuongozwa na mapendo kwa kumuhudumia, wewe unatumika hadi viungo vyako vinachoka kufika mwisho wa kiwango. 

Mwenyezi Mungu anajua kama katika maisha yako uko na Tumaini inayokutuma kuvumilia wengine na kuwa na saburi kwa watu wengine na waamini wengine.  

Mawazo yangu inarudi kidogo nyuma kwa kitabu cha Kutoka 32: 9

 “Bwana akamwambia Musa: Nimeona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu.” 

Hapa tunakuwa na wana wa Israeli wakati walifika mwisho ya uvumilivu wao. 

Musa alipanda kwa mlima ili achukuwe Amri za Mungu. 

Alipokuwa angali kule juu ya mlima, wana wa Israeli wakashindwa kuvumilia na wakasemezana katikati yao kwamba kuna neno linalofikia mtu yule Musa sababu yeye hadi sasa hashuke kwa mlima na kurudi. 

Wakamwambia Haruni, utujengee miungu yenye itatuongoza. 

Na wakati Musa aliposhuka toka mlima, Mwenyezi Mungu akamwambia: 

Nimeona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu. 

Mwenyezi Mungu aliwaona, Mwenyezi Mungu alifahamu roho zao.  

Mungu alifahamu kitu gani kiliwasukuma kufika kiwango kile katika maisha ya uhusiano wao na Mungu. 

Kitu ya muhimu kwetu ni yale Mwenyezi Mungu anayoyaona na Mawazo ya Mwenyezi Mungu ndiyo ya muhimu. 

Eti Mwenyezi Mungu anaona ndani yako Imani, Tumaini na Mapendo? 

20/ Tunafahamu kwamba ni muhimu kuwapenda wengine na kuwa na Tumaini. 

Nikusema Tudumu katika saburi na kuvumilia maana Mwokozi ni karibu kuja. 

Ataonekana mawinguni wakati atakuja kutuchukua, ni mawazo ya kuchunga  matumaini  na  hii ndiyo inatusukuma kuendelea katika huduma na kuvumilia na  kuwa na saburi.  

Mawazo na mpango huo uwe tayari siku zote mbele yetu kama bendera ya ushindi wetu. 

1Watesalonika 1: 10  

“Na kungojea Mwana wake kutoka mbingu, ambaye alimfufua toka wafu, hata Yesu, mwenye kutuokoa toka gazabu itakayokuja.” 


AMINA 


N°Ref:01/06/1963 / 10-2 THE BIRTH OF A CHURCH / 11/23/2020