Thursday, January 14, 2021

BIBLIA YAFUNDISHA MATUNZAJI KUHUSU MIPANGO NA MATAKWA YASIYOWEZA BADILIKA? / DOES THE BIBLE TEACH FATALISM?

Photo by B Smith from the patio


 


BIBLIA YAFUNDISHA MATUNZAJI KUHUSU MIPANGO NA MATAKWA YASIYOWEZA BADILIKA?  

DOES THE BIBLE TEACH FATALISM?

May 30, 1965 

Pastor Henry F. Kulp 



 

Waroma 8: 28, 29 

“Na tunajuwa maneno yote yanafanya kazi pamoja kuwapatia mema wale wanaopenda Mungu, kwa wale walioitwa kwa kusudi lake. 

Kwa sababu wale ambao aliwajua tangu zamani, aliwachagua tangu zamani wafananishwe na sura ya Mwana wake, ili awe Mzaliwa wa kwanza katikati ya ndugu wengi.” 

Kwa muda huu tunao jifunza maandiko hii, majifunzo yetu inaingia sasa kwa juma ya tano katika tu andiko hili moja. 

Kwa hiyo, nilifahamu ya kwamba ni vigumu sana kuzani kwamba majifunzo ya maandiko haya yanaweza kukomeshwa ama kumalizika. 

Ni vigumu sana kuzani kwamba yawezekana kwa mtu kutwaa tu aya moja katika Biblia na kujaribu kumaliza kufafanua maana ya aya hiyo, ama Maandiko Matakatifu fulani. 

Biblia Takatifu inajaa Utajiri kubwa na mwingi mno, inajaa  na Mawazo mazuri ya ajabu sana yenye tunawaweza kuhubiri juma kwa juma tukiwa tunapata kwa kila wakati utajiri na mali mupya isiyoweza kumalizika, Mawazo ya utajiri na utukufu wa mastaajabu na mambo makuu ya kushangaza.

  

1/ Kwa asubui ya leo nilitamani tufikilie zaidi na kufafanua neno inayosemwa hapa: 

Maneno yote yanafanya kazi pamoja kuwapatia mema.”  

Juma nzima iliyopita nilikuwa nikifikilia na kujifunza andiko hili na mawazo na mafikara yangu iliguzwa sana na kujengwa sana na aya hii, na ni ya muhimu kukumbuka kwamba neno “maneno” , “maneno yote” inapatikana mara 1600 ndani ya Biblia Tafsiri ya King James. 

Ni ya maana pia kutambua kwamba katika Waraka na  Maandiko ya Mtume Paulo, msemwa “Maneno yote” inatumiwa mara 76. 

Nazani kwamba kwa sasa hatuwezi kutaja mahali popote kwenye Mtume Paulo anatumia msemwa huo hadi kiwango cha mara 76, na kumaliza kutaja mara hizo zote, bali, kuna mambo yenye ningelitamani tuyatambue na kuyafahamu  tukiyatoa toka msemwa “Maneno yote” ama “Vitu vyote.”


2/ Jamii zetu zinaishi kufwatana na vitu ama maneno. 

Siyo tu vifaa mbalimbali bali pia matukio na mazingira yoyote na vitu vinavyotukia. 

Maisha ya jamii zetu inajengwa juu ya jambo mbalimbali na mambo kazaa, raha na furaha yetu inaambatana na vitu tunavyo. 

Tutambue kwamba tunapojifunza neno “furaha” kati yake tunakuta ndani vifaa mbalimbali. 

Wakolosayi 1: 17 

“Naye ni mbele ya vitu vyote na ndani yake vitu vyote vinashikamana.”

  Tunasoma ya kwamba Yeye, KRISTO, ni mbele ya vitu vyote. 

Ni Yeye KRISTO peke yake ndiye aliyekuwa tangu Umilele. 

Yeye ni wa Muhimu kuliko vitu vyote sababu Yeye alikuwa mbele ya vitu vyote. 


3/ Turudi nyuma kidogo katika Wakolosayi 1: 16 

“Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo duniani, vitu vinavyoonekana na visivyo onekana, ikiwa ni viti vya wafalme au usultani au falme au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake na kwa ajili yake.” 

Yeye ni mbele ya vitu vyote na vitu vyote viliumbwa kwa njia Yake na kwa ajili Yake

Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo duniani, vitu vinavyoonekana na visivyo onekana. 

KRISTO ndiye Muumba wa vitu vyote. 

Kiisha Wakolosayi 1: 17 inasema kwamba 

Yeye KRISTO ni mbele ya vitu yote na ndani yake vitu vyote vinashikamana.   

Vitu vyote vinashikamana pamoja katika hali sambamba ya umoja. 

 Eti yawezekana kweli kujiuliza tena kama kunaweza kuwa ulizo kuhusu jambo la kwamba vitu vyote vinafanya kazi kuwapatia mema wale wanaopenda Mungu?

 

4/ Wakolosayi 1: 18   

“Naye ni kichwa cha mwili, ulio kanisa; aliye mwanzo, mzaliwa wa kwanza kutoka katika wafu; ili apate kuwa wa kwanza katika yote.” 

Ili apate kuwa wa kwanza katika yote. 

Neno hili ni kwa muda huu wa sasa. 

Mwenyezi  Mungu anahitaji Yesu Kristo awe na nafasi ya kwanza katika vyote. 

Eti, wewe wampa nafasi ya kwanza maishani mwako? 

Hii inamaanisha ya kwamba yapasa Bwana Yesu Kristo awe kwa nafasi ya kwanza. 


5/ Waebrania 1: 2 

“katika siku hizi za mwisho amesema nasi katika Mwana, ambaye alimweka kuwa mriti wa vitu vyote, kwa yeye aliyefanya ulimwengu.” 

Kusema kwamba Mwenyezi Mungu, amesema nasi katika siku hizi za mwisho katika Mwana, ambaye alimweka kuwa Mriti wa vitu vyote. 

Tufahamu hapa kwamba neno Mriti siyo juu ya karibuni mambo yote ama karibuni vitu vingi, bali juu ya vitu vyote. 

Na kwa kweli, sisi ni wariti pamoja na Kristo, nikusema kwamba vyote ni vyetu. 

6/ Ni kwa ajili ya hii,“mambo yote”, njo sisi wakristo, tunapashwa kutii maandiko ya   Waefeso 5: 20 

“mukishukuru Mungu ndiye Baba siku zote kwa mambo yote, katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo;” 

Tukishukuru Mungu kwa mambo yote

Tuchunguze vizuri namna  msemwa huu tunao hapa umeundwa: 

Shukrani, kushukuru kwa mambo yote, maneno yote yanafanya kazi pamoja juu ya mema, kwa hivyo yatupasa sisi tuseme aksanti kwa mambo yote.

 Na hii inatokana kweli kwa kutii na kutimiza maandiko tunayopata katika  


Wafilipi 2: 14 

“Fanyeni maneno yote pasipo manunguniko wala mashindano;” 

Wakati tunatumbua kwamba maneno yote yanatumika pamoja kutupatia mema; na kwamba vitu vyote ni kwa ajili yetu, na kwamba Yesu Kristo anapashwa kukamata nafasi ya kwanza mbele ya vitu vyote, tutashukuru kwa ajili ya vitu vyote na ni hapo ndipo tunaweza fanya maneno yote pasipo manunguniko wala mabishano.  

Hii ni tukio tutakayotimiza kwa urahisi wote.

 

7/ kwa kweli haitatupasa sisi kuomba zaidi ya vitu vyote. 

Yatupasa kujua kushukuru kama inavyostahili kuhusu “maneno yote” 

na tukijikabizi maneno yote.


8/ Maneno yote yanafanya kazi pamoja kutupatia mema sababu sisi ni wamoja kati ya miradi yenye Mwenyezi Mungu alitayarisha tangu zamani za kale. 

Sawa vile tulivyo wafahamisha juma iliyo pita, kuchaguliwa toka asili, siyo jambo la kikatili, bali ni jambo nzuri. 

Siyo jambo la kuogopesha bali ni jambo lenye lingelipashwa kutusukuma sisi tuseme “haleluya” kwa sauti kubwa. 

Tulisema kwamba neno hili linapata musingi wake toka maneno mawili: 

“toka asili” inayo maanisha “mbele”, ama “mbele ya wakati” 

Marudio ama kuchaguliwa toka, inayomaanisha kiini. 

Ni kusema kwamba kuchaguliwa toka asili inaambatana na jambo tukichunguza, mbele ya wakati na kiini chake. 

Kuchaguliwa toka asili haiambatane na maneno yenye inatukia katikati ya mwendo. 

Haiambatani na wokovu, bali inaambatana na kusudi la Mungu katika Utatu Mtakatifu, jinsi Mungu Baba, Mungu Mwana na Mungu Roho Mtakatifu alivyokusudia zamani katika umilele wake kuhusu mpango kuhusu wokovu, kwamba wokovu itatimilika na kutakuwa Mwili utakaoitwa Mwili wa Kristo, na siku moja Mwili huo utafanywa kwa Sura yake Yesu Kristo, na tukio lake litahakikishwa katika sura yake Mungu Mwana. 

9/ Mwenyezi Mungu hachaguwe kwa asili mtu binafsi lakini anachaguwa Shirika Nzima. 

Mtu anakuwa mwanamemba wa Mwili huu kwa njia ya kuamini Yesu Kristo kama Bwana na Mwokozi wake. 

Tukumbuke kwamba tendo la kuchaguliwa toka asili linahusu Mwili Mzima. 

Mwenyezi Mungu hakuchagua toka asili mtu binafsi kwa upekee, lakini alichagua toka asili Shirika nzima, Mwili wa Kristo uwe kwa sura yake Yesu Kristo. 

Bali, kwa sasa ndani ya Biblia Takatifu, kuna neno moja kwa upekee lililo mbalimbali  na hali hii. 

Mwenyezi Mungu, kwa namna ya kipekee na ya ajabu alichagua toka asili mtu mmoja apite katika hali mbili tofauti. 

1 Petro 1: 11 

“Walitafuta ni wakati wa namna gani Roho ya Kristo aliye ndani yao alioonyesha wakati aliposhuhudia mbele mateso yatakayopata Kristo, na utukufu ambao utayafuata.” 

Tutambue hapa kwamba Bwana Yesu Kristo alichaguliwa toka asili kwa mateso na utukufu ambao utayafuata.  

Katika neno la msingi la Kigriki neno utukufu unaandikwa kwa uwingi. 

Kwa kweli, Manabii wa Agano la Kale walisema kuhusu mateso ya Bwana Yesu na utukufu wa Bwana Yesu Kristo, kwa sababu Mungu Baba, Mungu Mwana na Mungu Roho Mtakatifu aliamua kuhusu miradi hiyo tangu umilele wa hapo zamani za kale. 

Kanisa Mwili wa Kristo ni Kundi lililochaguliwa toka asili kwa sababu Kristo Yesu alichaguliwa toka asili kumwanga Damu yakekufa juu ya musalaba, kuteswa na kutukuzwa kiisha kufufuka na kupaa kule mbinguni.

 

10/ Tufikiri sasa kuhusu jambo la kwamba Kristo alichagulia toka asili kuteswa, kufa na kutukuzwa. 

Tusome katika Ufunuo wa siri 13: 8 

“Na watu wote wanaokaa juu ya dunia watamwabudu, wale majina yao hayakuandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo, aliyechinjwa tangu kuwekwa misingi ya dunia.” 

KRISTO alichinjwa tangu kuwekwa misingi ya dunia. 

Kuna wale wanaokosa ufahamu kamilifu kuhusu wokovu. 

Wanazani kwamba Mwenyezi Mungu aliuumba ulimwengu, baadaye muovu shetani akaja kuliharibu, mwanadamu akaanguka na Mwenyezi Mungu alikuwa mwenye kuchanganyikiwa sana na akatafuta surulisho ya kupinga hiyo. 

Hiyo mimi ninaweza kuiita sawa mpango ya ovyo ovyo kuhusu wokovu. 

Bali wokovu siyo mpango wa ovyo ovyo ama wa hivi hivi ama wa muda. 

Mwenyezi Mungu alifahamu yote kuhusu wokovu tangu umilele, mbele sana ya Yeye kuumba ulimwengu, mbele sana Yeye hajaumba dunia hii mbele ya kuweka Adamu na Awa katika shamba la Edeni. 

Miradi yote ilipangwa toka hapo umilele wa  zamani za kale. 

Wokovu ulianza zamani za kale mbele ulimwengu huu uundwe na shetani hana uwezo juu wa kusimamisha mpango huu.  

Ibilisi hana nguvu sawa vile wanadamu wanavyozani. 

Hapa tunaona kwamba tangu hapo kale katika umilele wa kale Bwana Yesu alichaguliwa toka asili ili aje hapa duniani, afe, na anunue wokovu wetu.

Hii ndiyo utimilifu wa wokovu, wokovu kamili na hakuna chochote cha kuongeza ama kufanya juu ya wokovu wetu. 

Yeye alilipa deni ya zambi zetu kwa msalaba, ni kwa hiyo sasa ameketi kwa sababu Yeye tayari amekwisha kumaliza kazi yake.

 

11/ Tuone sasa ya kwamba mambo haya yote siyo matunzaji kuhusu matakwa bila mabadiliko, kwa sababu iyo kundi iliyochaguliwa toka misingi ni Mwili, Kanisa Mwili wa Kristo. 

Kuna kundi lingine lenye Mwenyezi Mungu alilochagua toka misingi, ni Taifa la Israeli. 

Bali hakuna hata moja kati yao iliyo ya matunzaji kuhusu matakwa bila mabadiliko. 

Kama unahitaji uwe mmoja wa miradi hii, inakupasa kuchukua uamzi bora kuhusu Yesu Kristo. Inakupasa  kuamini Bwana Yesu Kristo.

 

9/ Tuchunguze sasa maneno yanayofwata katika Waroma 8: 29    

“Kwa sababu wale ambao aliwajua tangu zamani, aliwachagua tangu zamani wafananishwe na sura ya Mwana wake, ili awe Mzaliwa wa kwanza katikati ya ndugu wengi.” 

Sababu gani aliwachagua toka misingi wafananishwe na sura ya Mwana wake? 

Ili KRISTO awe Mzaliwa wa Kwanza katikati ya ndugu wengi. 

Yeye ndiye Lengo, Kusudi la Mwisho la Miradi na Mpango wa milele wake  Mwenyezi Mungu. 

Maneno yote yanafanya kazi pamoja kwa kuwapa mema. 

Tunajua ya kwamba alituita sisi tangu zamani sawasawa na kusudi lake, na kusudi lake ni kwamba Bwana Yesu Kristo awe Mzaliwa wa kwanza katikati ya ndugu wengi.  

Kuna wale watu wanaokuja kupiga hodi milangoni kwenu na wao wanajiteea kwa namna ya maarifa na ujuzi wote wakiwaambia kwamba hakuna jehenamu na ya kwamba hakuna Utatu Mtakatifu. 

Wanajaribu kuwaambia kwamba Bwana Yesu Kristo ni Mzaliwa wa kwanza wa Mungu wakisema kwamba hiyo inamaanisha kwamba Yesu Kristo anakuwa na mwanzo. 

Kwa kweli hiyo ni udanganyifu mtupu na maana yake ni mbali sana na masemi yale ya upumbafu. 

Tupime kujifunza maana ya msemwa:

Mzaliwa wa kwanza katikati ya ndugu wengi.

 

13/ KRISTO hakuzaliwa kamwe mbele ya kuja kwake hapa chini duniani,  

Yeye alizaliwa tu hapa kwa dunia, kwa hivyo Yeye si muzaliwa wa kwanza wa Mwenyezi Mungu. 

Yeye alizaliwa na mtu. 

Wakati Yeye aligeuka kuwa Mzaliwa wa Kwanza wa Mungu ni kwa nyakati ingine tofauti sana.

 

14/ Tujifunze kwa makini sana Wakolosayi 1: 18. 

“Naye ni kichwa cha mwili, ulio kanisa; aliye mwanzo, mzaliwa wa kwanza kutoka katika wafu; ili apate kuwa wa kwanza katika yote.” 

Tunaambiwa hapa kwamba Yeye KRISTO ni Kichwa cha Mwili, Kanisa, Yeye aliye Mwanzo, Mzaliwa wa kwanza kutoka katika wafu. 

Watu wengine walikuwa wakizania na kusema kwamba   Kristo kama Mzaliwa wa kwanza, inamaanisha kwamba yeye anakua na mwanzo. 

Kwa kweli mzaliwa wa kwanza wa jamaa ni mutoto aliyekuwa wa kwanza kwa kuzaliwa, na hapa KRISTO anaitwa Mzaliwa wa kwanza. 

Wengine wanazania kwamba kunapashwa kuwa nyakati fulani yenye yeye kweli alikua Mwana wa pekee, sababu anaitwa tena Mwana wa pekee. 

Hapa katika Wakolosayi 1: 18, tunasoma ya kwamba: Yeye Kristo ni Mzaliwa wa kwanza kutoka katika wafu. 

Kulikuwa nyakati yenye Mungu alitoa Mwana wake kwa Kufa. 

Tangu zamani za kale za milele  na hata milele,  Mwenyezi Mugu anakua na Mwana Moja tu, na Alimtoa Mwana wake ili afe, Alikufa, Akazikwa, Akafanya siku tatu, mchana tatu na usiku tatu ndani ya kaburi, sasa kwa nini aliitwa Mzaliwa wa kwanza wa Mungu kutoka katika wafu? 

Ni kwa saa hiyo Yeye alitoshwa kutoka mauti ndipo Anakuwa Mzaliwa wa kwanza kutoka katika wafu.

 

15/ Matendo ya Mitume 13: 33 

“Mungu ametutimizia sisi watoto wao ahadi hii, kwa kufufua Yesu; kama ilivyoandikwa katika Zaburi ya pili: Wewe ndiwe Mwana wangu, siku hii ya leo nimekuzaa.” 

Hapa twasoma: 

Kama ilivyoandikwa katika Zaburi ya pili:

Wewe ndiwe Mwana wangu, siku hii ya leo nimekuzaa.

Hiyo siku ilikuwa siku gani? 

Aya hii inatuambia wakati alipomufufua Yesu Kristo. 

Bwana Yesu Kristo ndiye Mzaliwa wa Kwanza kutoka wafu, Yeye ndiye Mzaliwa wa Kwanza wa Viumbe vipya. 

Ninyi ni wanamemba wa Muumbo ule Mpya, munakuwa wanamemba wa Muumbo ule wakati munapoamini. 

Kwa njia ya Ufufuko Mwenyezi Mungu alianzisha kitu kingine kipya, Kiumbe Kipya.

 

16/ Hadi kufikia kwenye Ufufuko, mbele ya hapo hakukukuweko hata mtu mmoja aliefufuka na mwili wa utukufu, mwili tukufu, ni Bwana Yesu Kristo peke yake aliyefufuka na Mwili wa Utukufu, na Mwenyezi Mungu kwa njia ya Kristo Yesu ikoanaumba Kiumbe kingine. Yeye ni Mzaliwa wa kwanza kutoka wafu.

 

17/ Kumbukeni ya kwamba tangu milele hata milele Bwana Yesu ni Mwana wa Mungu, bali, wakati alipokuja hapa chini dunia, Yeye alifanywa kuwa zambi, akaacha na kutia pembeni, kwa muda hali yake ya Kipekee ya utukufu, na ilimpasa Mwenyezi Mungu kumuacha sababu Yeye alibeba zambi na kufanywa kuwa zambi. 

Bali, ndani ya Ufufuko Mwenyezi Mungu alimutetea kuwa Mwana wake wa Pekee.  

Kwa sasa Anakaa kwa Mukono wa Kuume wa Mungu, na Yeye ni Mzaliwa wa kwanza wa kile kiumbe. 

Kiumbe kipya kile  ni Kanisa Mwili wa Kristo

Ni kile Kitu kipya chenye Mwenyezi Mungu anachounda kwa siku za leo. 

Mwili huo uliochaguliwa toka zamani kuwa sawa Kristo Yesu.

 

AMINA


N°Ref: 05/30/1965 / 295 - DOES THE BIBLE TEACH FATALISM / 01/13/2021