Tuesday, September 24, 2019

INJILI YA PASAKA / THE GOSPEL OF EASTER




Photo taken from B Smith's Kitchen Window




     52 The Gospel of Easter / INJILI YA PASAKA 
     April 2, 1961
     Pastor Henry F. Kulp


Wagalatia 1:1-12 
Paulo, Mutume, (si mutume wa wanadamu, wala kutumwa na mwanadamu, bali na Yesu Kristo, na Mungu Baba aliemufufua kutoka kwa wafu),
Na ndugu wote walio pamoja nami, kwa makanisa ya Galatia;
Neema na iwe kwenu, na Amani, zitokazo kwa Mungu Baba, na kwa Bwana wetu Yesu Kristo;
Ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili ya zambi zetu, ili atuokoe na dunia hii mbovu iliyopo sasa, kama alivyopenda Mungu, Baba yetu.
Utukufu una Yeye milele na milele, Amina.
Nastaajabu kwa kuwa mnamwacha upesi hivi Yeye aliye waita katika Neema ya Kristo, na kugeukia injili ya namna ingine.
Wala si ingine; lakini wako watu wawataabishao na kutaka kuigeuza Injili ya Kristo.
Lakini ijapokuwa sisi ao malaika wa mbinguni atawahubiri ingine injili yoyote isipo kuwa hiyo tuliyo wahubiri, na alaaniwe.
Kama tulivyo tangulia kusema na sasa, nasema tena, mutu awayeyote akiwahubiri ingine injili isipokuwa hiyo mulio ipokea, na alaaniwe.
Maana, sasa je!
Ni wanadamu ninaowashawishi, au Mungu?
Au nataka kuwapendeza wanadamu?
Kama ningekuwa ata sasa nawapendeza wanadamu, singekuwa mutumwa wa Kristo.
Kwa maana, ndugu zangu, injili iyo niliyo wahubiri, nawajulisha ya kuwa siyo ya namna ya kibinadamu.
Kwa kuwa sikuipokea kwa mwanadamu wala sikufundishwa na mwanadamu, bali kwa ufunuo wa Yesu Kristo”.
Sawa vile tulivyo jifunza katika kitabu ya Wagalatia, tuliona ya kuwa walimu wengi wa uongo walijiingiza ndani ya muji ya Galatia na katika makanisa mingi na walikuwa wanawaalika na kuwafundisha watu waheshimu mafundisho ya utamaduni pahali ya Neema ya Mungu.
Na kwa kweli, kwa kufanya hivyo, walikuwa wanapenda kuzorotesha mutume Paulo na Injili yenye aliyowafundisha.
Ya kwanza, walikuwa wanakana wakisema kama Paulo haiko mutume wa Mungu, na Paulo aliwaonesha  kwa kutumia hakikisho mbalimbali inao onesha kama kwa kweli yeye ni Mutume wa Mungu.
Yeye alikuwa mutume wa Mungu na alikuwa akitumwa na Mwenyezi Mungu na anasamani ya kuonesha kama yeye ni wa Mungu.
Kiisha Mutume Paulo aliendelea kuonesha kwa kweli kama Injili aliyokuwa akifundisha ni hiyo pekee inayo faa kufundishwa na inayo kuwa kamilifu na yenye kuenea. 

1/ Munaona kwamba Mutume Paulo alihukumu kwa kulaani na kulahini yeyote yule hataitika hii injili ama mutu yeyote mwenye atahubiri ingine injili tafauti na hii. 
Tuaangalie sana,
Hapa mutume Paulo anasema:  Alaaniwe,
kweli ni maneno magumu, bali ni hiyo  njo neno yenye Mungu anapenda tujuwe.
Tuone hapo kama ni kulaaniwa mara mbili sababu anarudilia kusema alaaniwe.
Ni lazima kwetu tujuwe kama haiko kuhukumu ao kukufuru yenye inatoka kwa masemi ya watu, lakini hiyo njo kutaka kwa Mungu.
Ni kulaaniwa yenye Mungu anapenda iwe juu ya ule mutu.
Basi, inakuwa muhimu sana na yenye mafaa sana kufikiri na kuwa na uhakika wa kila neno mbele ya kuitamka wakati tunapokuwa tukihubiri habari njema. Angalisho na kuwaambia mali ya Bwana: “Hii ni Neno linalotoka kwa Mungu!”
Tunapashwa kufanya angalisho na kuwa na ujuzi na uhakikisho ya maneno tunayo yatamka.

2/ NI INJILI GANI?
Tunapata maelezo juu ya hii Injili katika moja Wakorinto 15: 1- 8,
Ni Yesu Kristo aliye sulubiwa musalabani juu yetu, alizikwa na akafufuka siku ya tatu.
1 Wakorinto 15: 1 - 8 
"Basi, ndugu zangu, nawaarifu ile Injili niliyo wahubiri; ambayo ndiyo mulioipokea, na katika hiyo munasimama, na kwa hiyo munaokolewa; ikiwa munayasikia sana maneno niliyo wahubiri isipo kuwa muliamini bure.
Kwa maana naliwatolea ninyi hapo mwanzo yale niliyo yapokea mimi mwenyewe, yakuwa Kristo alikufa kwa ajili ya zambi zetu, kama yanenavyo maandiko; na yakuwa alizikwa; na yakuwa alifufuka siku ya tatu, kama yanenavyo maandiko; na yakuwa alimutokea Kefa; tena na wale Kumi na wawili, baadaye aliwatokea ndugu Zaidi ya mia tano pamoja; katika hao wengi wanaishi ata sasa; ila baadhi yawo wamelala;
Baadaye akamtokea Yakobo; tena na mitume wote; na mwisho wa watu wote, alinitokea mimi, kama ni mutu aliyezaliwa si kwa wakati wake. “

3/ Wagalatia 1: 11-12 
“Kwa maana ndugu zangu, injili hiyo niliyo wahubiri, nawajulisha kuwa siyo ya namna ya kibinadamu.
Kwa kuwa sikuipokea kwa mwanadamu wala sikuifundishwa na mwanadamu, bali kwa ufunuo wa Yesu Kristo.”
         Tunaona hapa kama siyo injili iliyotoka kwa mutu, ao kupewa ama kufundishwa na mutu lakini ni Ufunuo toka Yesu Kristo.
Injili iliyotoka kwa Mungu, mutume Paulo aliipata toka mbinguni.

4/ INJILI HIYO ILITUTENDEA NINI?  
Ni Habari njema ya muhimu sana.
Lakini, kwa kweli, hiyo injili ilitutendea nini?
Twende basi tukayaona katika Ufunuo 1:18
Ufunuo 1:18 “Na aliye hai; nami nilikuwa nime kufa, na tazama ni hai hata milele na milele.
Nami ninazo funguo za mauti na za kuzimu.”
         Kama vile unavyoona sasa ni Yesu Kristo anayekuwa akisema, na Yesu Kristo anasema, ni Yeye msemaji na anasema Yeye ni Yule aliye hai na Yule aliyekufa,  na tazama Yeye ni hai milele kwa milele.
Ninazo funguo za mauti na za milango za hadeze.
Katika maisha yetu kama  wasafiri hapa chini duniani, sisi ni watenda zambi na tunaelekea kufa, na kiisha kufa ni pahali pa mapumuziko kiisha kufa.
Kufa ina nguvu, kama vile hadeze vilevile, na Bwana wetu Yesu alikufa, na Yeye alitoka toka kufa na Yeye yu hai na alisema nina funguo ya Hadeze, Jehenama haitaogopesha tena wale wanaomufwata Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, wao wanaoliamini Kufa kwake na kufufuka kwake,
Bwana Yesu alisema, mimi ninao funguo ya kifo. Kufa haina tena nguvu, nguvu ya Jehenama inakwisha.

5/ TUNA MAADUI WAKUBWA WENYE NGUVU NA WANAO TUZUNGUUKA NA WENYE TUNAPASHWA KUSHINDA.    
Zambi, Kufa na Hadeze.
Ninakuambia wewe ndugu musikilizaji kwamba yapashwa upate Wokovu, ni Injili inayo kuokoa toka zambi, toka kufa na toka hadeze,
Kwa sababu hawo ndiyo maadui wako, na Biblia inatuonesha waziwazi namna gani Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo aliwasaga hawo maadui wako, na wakati alipotowa roho na kwenda Mbinguni, aliharibu nguvu ya kufa, nguvu ya zambi, nguvu ya Hadeze na sisi tunakuwa Huru.
 Ni hiyo njo Wokovu, hapana kitu kingine.  
Watu wanaweza kuunda madini mbalimbali, lakini dini haiwezi kuokowa.
Tufanye angalisho na dini,
Kitu cha maana kwetu sisi watenda zambi ni Ukombozi.

6/ NA UKOMBOZI NI KWETU
Ukombozi ni kwetu sasa, sawa vile kufa na hadeze vina tusonga, kwa sababu Yesu Kristo ana Funguo na Funguo ni alama ya Ukubwa na Mamlaka.
Hii inamaanisha kwamba Kristo ana Ukubwa usio kuwa na ubishi na Katika kufa kwa KRISTO, na ufufuko wake KRISTO ana Mamlaka juu ya kufa na hadeze, na kwa matafsiri ya musingi tunaona kama kufa njoo iko mbele ya maali pa mapumuziko ya wafu. Hivi njo mambo yafwatana.

7/ 1 WAKORINTO 15: 17 
“Na kama KRISTO hakufufuka, Imani yenu ni bure; mungalimo katika zambi zenu.”
Naomba musamaa juu ya hawo wahubiri wakarimu wa siku hizi wasiosadiki ufufuko wa Bwana Yesu Kristo, sababu, musingi wa maandiko hii inaonesha kama hata wahubiri wa namna hiyo wanaweza kuwa na imani ya namna gani, na kweli wanajizania wana Imani kubwa, ndugu musisahau hata siku moja, mujuwe kwamba Imani yao ni bure, haina musingi na wao wangali tu katika zambi zao.
Tena hapo tunaona kwamba kuamini katika kuamini za kidini ni hatari sana,
Inafaa tu kuamini Injili yenye Mutume Paulo anayo fundisha, kama sivyo, wewe unalaaniwa, na laana hii iko juu yako, Hii laana ya Mungu, sababu yatupasa kuamini UFUFUKO wa Bwana na Mwakozi wetu Yesu KRISTO.
WAROMA 10: 9 -10 
“Kwa Sababu Ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na Kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimufufua katika wafu, utaokoka.
Kwa maana kwa moyo mutu aamini hata kupata haki na kwa kinywa anakiri hata kupata wokovu.” Hakuna mutu awezaye kuokolewa kama hasipoamini waziwazi ufufuko wa KRISTO.

8/ SASA HIYO INJILI INAMAFAA GANI KWETU?  
Injili ya Kristo Yesu kusulubiwa na kufufuka toka wafu?
         Inatuokowa toka Kufa na Hadeze,
Lakini inakazi nyingi kuliko hiyo,
Tujuwe kwamba:
Katika Kitabu hiki kizuri tunayo jifunza, kitabu cha Wagalatia, tunapata mwangaza wa Ukweli wa samani kuu katika hii Habari njema,
Wagalatia 2:20 
“Nimesulubiwa pamoja na KRISTO; lakini ni hai; wala si mimi tena, bali Kristo yu hai ndani yangu; na uhai niliyo nao sasa katika mwili, ninao katika Imani ya Mwana wa Mungu, ambaye alinipenda, akajitowa nafsi yake kwa ajili yangu.”
         Ndiyo, ni hii ndiyo Mwamba, Maana kamilifu, Nguzo na Musingi wa KIKRISTO.
         Ukristo siyo mambo yenye wewe binafsi unaweza kutimiza ao kufanya, lakini ni Hiyo Bwana Yesu afanyalo akiishi ndani yako.
Hii njoo tofauti katikati ya Ukristo na Dini.  Sivyo?
Dini ni kitu chenye mutu anaumba na anafanya, ni kusema dini ni mutu afanyae kitu Fulani, lakini Ukristo ni Yesu afanyae vyote.

9/ WAKOLOSAYI 1:27  
“Ambao Mungu alipenda kuwajulisha jinsi ulivyo utajiri wa utukufu wa siri hii katika mataifa, nao ni KRISTO ndani yenu, tumaini la utukufu.”
         Hii andiko inasema namna moja sawa hiyo ya wagalatia inayo sema KRISTO ndani yenu, tumaini la utukufu.
Kristo Yesu yu hai, Kristo ndani ya mwamini.
Hii Habari njema Nzuri inatuonesha namna gani Kristo anaishi ndani yetu.
Ni jambo la mastaajabu sana na ya kufurahisha!!!  

10/ HII UKWELI WA KRISTO AKIISHI NDANI YENU NI KITU KIPYA CHENYE KUELEKEA HIZI SIKU TUNAZOISHI.
         Watakatifu wa hapo kale hawakuishi hii ukweli,
Tukiangalia katika kitabu cha Yoane, tutakuta hii Ukweli ya Utukufu.
YOANE 14:17 
“Ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kupokea, kwakuwa haumwoni wala haumutambue; bali nyinyi munamutambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu.”
         Daudi, kama vile munavyo juwa, aliifikia kiwango cha juu sana.
Huyu muhimbaji wamanufaa wa Agano la kale.
Lakini, wewe na mimi tunapashwa kujuwa Zaidi ya Daudi.
Sisi tunapashwa kuwa wazuri na wakupendeza Mungu kushindia Daudi.
Sisi tungelipashwa kupanda milima mirefu Zaidi ya vile Daudi alifanya.
Sisi tungepashwa kuona mambo makuu kushinda hiyo Daudi aliyoona.
Sababu Daudi hakukuwa na KRISTO akiishi ndani yake.
Tutazame katika hii aye, inasema
KRISTO alihaidia kama siku inakuja nayo ni tayari hapo ROHO Mutakatifu ataishi ndani yao, lakini,  katika hizo siku za kale ROHO Mutakatifu alikuwa tu juu yao.
Lakini kwa leo, tunakuwa na KRISTO ndani yetu,
Taifa la Izraeli itakuwa na KRISTO ndani yao katika siku zijazo.

11/ KATIKA HII WAKATI YENYE TUNGALI NAFAFANUA HII WAZO, ACHA NIWAONESHE ANDIKO MOJA NZURI KATIKA
WAEFESO 3: 19
“Na kuujuwa Upendo wake Kristo, upitao ufahamu kwa jinsi ulivyo mwingi, mupate kutimilika kwa utimilifu wote wa Mungu.”
         Ukristu siyo aina ya utupu, ya bila mafaa yoyote
Ukristu siyo kitu isiyo ya faida, ya bure.                                              
Kama ukikutana na Ukristo usio vutia, usio na mafia, unao kuwa bure, fahamu ya kuwa unakutana na kitu kingine mbalimbali na Ukristu, sababu
Ukristu ni Uwingi, ni Kujaa.
Mungu anataka kuondoa kitu kimoja maishani mwako.
Wengi wetu wanasema, kweli mimi siwezi…
Kwa kweli, Hauwezi hata kuondowa kitu kimoja ndani mwako ili uokolewe.
Lakini kama unapenda kujuwa na kuishi ujazi wa Mungu, Mungu anapenda aondoshe ile isiyo stahili kuwa ndani yako.
Anapenda kuondosha kitu kimoja ndani mwako ili atiye nyingine ndani mwako.
Anaondosha yale mambo machafu ili ajifanyie nafasi ya kukaa na kukupatia ujazi wake.

12/ SOLOMONO KATIKA MAOMBI YAKE ALISEMA HIVI ”MBINGU NA DUNIA YOTE MUNGU HAWEZI AKAIENEE AMO”  
Lakini sasa, hapa tulipo sasa, tunaweza jazwa na Ujazi wake.
Ona sasa ndugu yangu namna gani Mungu ni Mwema!
Ni Hii Habari Njema ya Mastaajabu yenye hii Injili inafanya kwetu.
Hii habari Njema Inaweza kutujaza na Ujazi wa Kristo Yesu.

13/ LAKINI HABARI NJEMA HII YA SALAMA INATUOKOWA NA INAFANYA MAMBO MENGI MAKUBWA KWETU.
Ufufuko wa Bwana wetu Yesu Kristo njoo vilevile ufufuko wetu.
Waroma 8:19 
Kwa maana viumbe vyote pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa  kwa wana wa Mungu.”
Tunaona kwamba Roho wa Mungu aliye mufufua Bwana na Mwokozi wetu toka wafu, Roho ule anakaa ndani yako, Yeye aliye mfufua Kristo Yesu toka wafu, atabadirisha, kwa kufunga macho na kufungua, mwili wako uliokuwa wa kufa kwa nguvu ya Roho anayeishi ndani yako.
Mwili wa mukristo, mwili wa mwamini ni mali ya Roho Mutakatifu, ni mawazo ya Raha kweli. Kwa njia ya ufufuko wa Bwana Yesu, Roho yule aliye mufufua Bwana wetu Yesu Kristo toka kufa, anashurulikia mwili wetu huu wa udongo.
Kama Mwamini Mukristo anakufa, na mwili wake unazikwa kaburini, huyu mwili unachungwa na Roho Mutakatifu.
Kama wewe umekwisha kuamini, Mungu amekwisha kukupatia Roho Mutakatifu naye anaishi katika miili yenu na miili yenu ni Hekalu ya Roho Mutakatifu.
Na kwa hiyo, kama umehamishwa, na mwili wako umetiwa udongoni, mwili huo una baki katika ukingo wa Roho Mutakatifu, na huyo mwili utabadirishwa tena upya.

14/ KWA HIVYO WATU WENGI WANAMAULIZO MBALIMBALI JUU YA UFUFUKO WA WAFU, WAKIJIULIZA KAMA MWILI YA UFUFUKO ITAKUWA ILE ILE ILIYOINGIZWA KABURINI?  
         Roho Mutakatifu anahusika na hiyo miili na ni Yeye pekee njoo atarudisha kwa upya hiyo miili kwa uzima, sababu ni miili yake, Anaiishi ndani ya miili hiyo na hiyo miili ilikuwa hekalu lake, na kwa hiyo anahusika nazo naye ataziweka tena upya wa uzima.
Kuna mufano moja yenye nilisikia siku nyingi zilizopita, na ninawaza kama inaweza wasaidia kidogo kwa kusikia mambo haya.
Kamata bahasha ya kartasi yenye tunatumikisha kwa kubebeya ndani vyakula, kunjakunja hayo mukononi mwako, na kwa mwisho saa utapuliza hamo hewa, utaona kama bahasha hiyo itarudiliya sura yake iliyo kuwa nayo. Itakuwa hivo hivyo kwa miili yetu.
Katika hizo miili zenye zilizo kunjwa na kuharibishwa, miili yenye iko chini ya udongo, kwa siku ya ufufuko, Roho Mutakatifu atapulizia pumzi mu miili hizo na miili hizo zitakamata sura yake.
Na ni hizohizo miili njo zitafufuka katika utukufu wa milele.

15/ UZURI NA RAHA GANI KUJUWA HIVYO!
Bwana Yesu Kristo atatubadirisha katika mwili wa utukufu unao fanana na mwili wake.
Ufufuko wake ni harabuni ya ufufuko wetu toka wafu.
KRISTO anaye ishi leo ndani ya mwamini, kwa njia ya kufa kwake na ufufuko wake.
Ni yakusikitisha sana kuona kama wengi hawafahamu Ukubwa wa Kazi ya Bwana wetu Kristo Yesu.
Siku moja nilikuwa nasoma maandiko ya Muganga Dr Tom Dooley, mwenye alikuwa muganga mukubwa naye alijulikana ulimwenguni pote na yeye alikuwa akipatikana katika Jungle ya LAOS.
Pa siku 02 Mwezi wa kumi na mbili wa mwaka wa elfu moja mia kenda makumi sita, nilipatikana nikiwa na uchungu na machozi nyingi rohoni mwangu wakati niliposoma maandiko yake ya mwisho wa maisha yake wakati ugonjwa wa kansa ulikuwa ukimusonga kweli, na yeye aliandikia Mwalimu moja mukubwa wa Yunivarsti akisema hivi:
“Wakati yoyote saa kansa yangu itanifikisha mwisho na kunibeba kwenye mauti, nilikuwa nawaza moyoni mwangu, nikiingia katika utu wangu wa ndani kwa muda pande,
Nikiona bila faida ao mafaa,  hospitali zangu kubwa zinazo patikana ulimwenguni pote,  na waganga wangu makumi kenda na ine wenye ujuzi wa juu sana kama mimi, na wenye kujulikana, na tena juu ya hiyo, nikajiuliza kama nilipima waza juu ya muganga moja toka mbinguni sababu ya vitu nyingi niliyotolea kwa makanisa, nilijiuliza kama haingiweza kutosha?
Ona hapa mufano wa mutu mwenye hakukuwa na tarajia maisha ya milele.
Huu ni mutu wa dini akiishi katika kujitoa kwa matoleo ya namna ya kibinadamu, akipana maisha yake kwa wengini.
Alikufa sababu alijitowa mwenyewe juu wengine wapate maisha mazuri hapa chini duniani.   
Lakini alikufa akiwa anahuzuni kubwa juu ya kifo yake mbaya na yenye uchungu yenye iko inamukaribia dakika kwa dakika.
 Yeye alikuwa mutu wa dini, mutu mwenye aliongeza matendo yake juu ya neema ya Mungu, hakuamini kama Kifo na Ufufuko wa Bwana na Mwokozi wetu Kristo Yesu tu njoo Yatosha juu ya wokovu wetu. Ni kwa njia hii njoo
ati Muganga Dr Dooley alifariki.
Yeye hakuandika juu ya Salama na Raha ndani ya Wokovu katika Kristo Yesu, lakini alikuwa akijiuliza kama matoleo yake nyingi na zaka zake nyingi hazikutoshelea?
Tunafahamu kwamba hata matoleo yetu yawe nyingi namna gani haiwezi hata kwa namna ya zamiri kukamilisha mwenye kuabudu, kutuokowa na kuponya roho yetu.
Ni Kazi tu Ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo njoo yatoshelea na kufaa kwa ukamilifu juu ya wokovu wetu.
Oh, sisi tuliokombolewa tunaweza fikia siku yetu ya kufa bila woga yoyote sababu tunajuwa kwamba Kristo anaishi ndani yetu, na ni kwa njia yake tutaishi milele.

16/ WAROMA 14: 9   
“Maana Kristo alikufa akawa hai tena kwa sababu hii, awamiliki walio kufa na walio hai pia.”
         Tuone kitu kingine hapa, inayoelekea kufa na kufufuka kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
Kwa siku hizi Kristo alikufa na alifufuka na kuhishi tena milele juu awe Bwana wa waliokufa na walio hai.
Hakuja onekana kabla mwana wa mwanadamu kwa miaka hii yote mwenye anaweza ongoza mambo ya dunia.
Magumu ya mwanadamu ni nini?
Magumu ya mwanadamu haiko tu vita, vita ni musiba katika historia ya mwanadamu.
Watu wanachukiana, watu wanatamani vyeo, kutawala na mamulaka juu ya wengini na hivyo njoo inawasukuma katika vita,  Na vita inakuwa musiba.
Nini inayo sumbuwa wanadamu? Wanasumbushwa na kifo.
Mutu hapande matungulu juu ioze udongoni na kupotea.
Mutu hapande mbegu ama milimo juu ibakie tu udongoni bila hata siku moja kupamba.
Mufurugano wa mwanadamu ni juu yeye anajuwa atakufa.
Atakufa katika zambi zake,  watu wanaonekana wakitembea duniani lakini wao kweli ni wafu katika zambi zao.
Hakuja patikana mwana wa mwanadamu hata mumoja, mwenye angeliweza kupiganisha kufa na kulipa zambi.
Hakuna hata mumoja mwenye angaliweza kufanya hivyo, ila MUNGU, asiye jua zambi, alijifanya kuwa zambi kwa ajili yetu akijifanya kuwa MUTU ili avunje Kufa na awe BWANA wa walio kufa na wenye walio hai.

AMEN
Ref:  04/02/1961 / njili ya Pasaka / 52 - The Gospel of Easter - 9/24/2019

Wednesday, September 11, 2019

NATHARIA YA SAYANSI YA MABADILIKO / THE THEORY OF EVOLUTION





Photo taken from B. Smith's Kitchen Window




     Natharia Ya Sayansi Ya Mabadiliko 
     Theory of Evolution
     Pasteur Henry F. Kulp 
     April 26, 1981



Jameni niwasomee Biblia Takatifu katika kitabu cha Mwanzo sura moja na haya yake ya kwanza. 


Mwanzo 1:1

“Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na inchi” 

Tuombe: 

Mungu wetu na Baba yetu uliye juu, tunakupigia aksanti kwa huu ulinzi wako wa upekee unawo onesha kwetu, na kwa makuu yako yote. 

Ingelikuwa razi utufanye sisi sote tusijiwaze ama kusema juu yetu wenyewe, ama kuwa na mawazo juu yetu wenyewe, lakini tufikiliye kujuwa kiwango cha hali tunayokuwamo, na tufikiye kusadikia na kuamini mambo haya tutakayo yaona pamoja, katika Jina tukufu Lenye Nguvu na Uwezo, Jina La Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo , tunaomba, Amina. 


Kwa sasa, tutazungumuza juu ya Natharia ya sayansi ya Mabadiliko, hii inaelekea watu wasioamini Elimu ya kuwa Muumbaji ni Mungu pekee. 

Kitu mbaya siku hizi ni kuona kwamba; hapana watu wote wa sayansi, lakini wamoja wao, na vilevile waadibishaji wengi wanatuambia kwamba hii Natharia ya sayansi ya mabadiriko ni elimu yenye haina maana, ya bure. 

Wao, hawana hata uhamuzi wowote unaotokea kwa miungu yenye wanaoamini. 

Ndugu zangu, tunafuha kubwa kuwaonesha leo kama hiyo Natharia ya sayansi ya mabadiliko ni ya bure ,bila maana yoyote. 

Ni filamu tu tunayo iona na kufwata kupitia televijene zetu. 

Niwaambie, 

Kulikuwa mutu moja wa elimu sana, mutu wa sayansi toka yunivarsti moja inayo julikana sana ulimwenguni, mwenyi presidenti wa zamani wa merikani, bwana Reagan alimualika kwake juu azungumuzie juu ya Natharia ya sayansi ya mabadiliko, lakini mwalimu huyu alifika na kusema kama yeye haamini kweli yale yanayo semeka katika natharia ya sayansi ya mabadiliko. 

Tunaona kamam kuna mengi ya kusema juu ya mabadiliko(Evolution katika kifransa), hii njoo tutasemea leo.




KWANZA TUNA WAO WASIO AMINI MUNGU  

Wao wasio amini Mungu wanasema kwamba, hawaamini Mungu yeyote, hawaamini nguvu yeyote ya kiMungu, 

Wao wanasema kama viumbe ilionekana tu na sisi watu tunakuwa pale, na tunakuwa na ulimwengu wote na anga lote na watu. 

Lakini sasa, kuna wao walio hatari sana ni male tunaweza kuita Watu wa mabadiliko na wasio amini Mungu. 

Wao ni wa hatari sana, 

Wao ni Mapadiri, Ma pastori wanaokuwa katika majifunzo katika YUnivasti za teologia na za bibilia katika ma seminari na wao wanatuzungumuzia yale wanao amini kupitia elimu na nazaria ya mabadiliko, na wanasema wanaamini Mungu muumbaji na wanatumia yanayosemwa katika sayansi ya mabadiliko ili watufasirie maumbaji. 

Wanasema hawana ufahamu kamilifu juu ya kuonesha jinsi mwanadamu aliumbwa, namana gani tunafikia siku zetu za leo, hatujuwe namna Mungu aliumba ulimwengu. 

Lakini ndugu zangu sikilizeni namna haya ya kwanza ya Biblia takatifu inasema, 

Katika mwanzo, wakati hakukukuwa kitu mbele, Mungu aliumba, 

Hii ni ya kwanza, ya mwisho nay a kuhakikisha yenye Mungu aliyuandikia ili atuonyesha namuna gani vyote viliumbwa naye. 

Hii aya ya kwanza inasema tu kwamba katika mwanzo Mungu aliumba 

Basi sasa mimi na wewe ni wajibu wetu kuamini hivyo ao kutokuamini hivyo. 

Sasa, sikilizeni, sababu ni ya manufaa kabisa, 

Wewe hauwezi sema kama umeokoka na wewe hausadiki Mwanzo sura ya kwanza na haya ya kwanza. 

Kama maandiko ya Mwanzo sura ya kwanza na haya ya kwanza haisimami basi Biblia inatikisika. 

Kama Mungu hakuumba kwa mwanzo, basi Biblia haina mafaa. 

Wewe kauwezi kuwa hauamini kitabu cha Mwanzo 1:1  na kusema tu hivi, 

Mutumishi wangu, ama Pastori wangu, kitu tunacho tu cha kufanya ni kuamini tu Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, 

Sasa ulizo, juu ya KUOKOKA, 

Ningelipendelea kuwauliza hivi: 


1/ Namana gani unajuwa kwamba ni Yesu Kristo aliye kuokoa? 

Hii hakikisho nah ii ukweli unaupata wapi? 

Jibu, tunaupata katika Biblia  

2/ Namana gani unajuwa kwamba wewe ni mutenda zambi? 

Ni Biblia inayo tufunuliya sisi mambo hayo. 

3/ Namana gani wafahamu kama Bwana Yesu Kristo alikufa juu ya zambi zako? 

Ni Biblia inayo tu onesha hayo. 

4/ Namana gani wajuwa kwamba Yesu Kristo alifufuka toka wafu juu ya ukombozi wako na Utakaso wako? 

Ni Biblia inayo tuambia neon hili. 

Basi kama wewe unaweza kusema kama Mwanzo1:1 ni hadisi tu yenye watu walijitungia, na unasema kwamba Mwanzo1:1 haisemi ukweli, ni hadisi, sasa 

Namna gani unasadiki kwamba kwa kweli Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo alikufa juu ya zambi zetu? Wajuwa hii kweli? 

Hauwezi kukani sehemu hii na kukubali sehemu ingine. 

Sababu Biblia nzima inaamini katika umoja na ukweli wa Mwanzo 1:1. 

Acha niwafunuliye kitu kimoja: 

Katika mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia, sasa tuone namna gani wao wanao sema juu ya natharia ya sayansi ya mabadiliko wanasema. 

Mabadiliko inasungumuza ikisema kama kwa mwanzo kulikuwa seli moja na ikafwatana na kugawanywa inayo endelea yenye ina itwa Big Bang, 

Kulikuweko seli moja yenye haikukuwa na akili, ilikuabila mawazo yenye inayoenda sambamba, kiisha hiyo seli iligawanyika mara mbili, kiisha hizo vipande viwili katika vipande ine na izo ine katika munane makumi tatu na mbili, makumi sita na ine na vivyo hivyo na kufikia kwako wewe leo!!! 

Lakini kunaulizo yenye kutembea vichwani mwetu, 

Ulizo hili ni lakujuwa namna gani hivi vyote vilianza? 

Hiyo seli inayotajwa ya kwanza nayo vilevile ilitokea wapi? 

Hiyo seli iliundwa vipi na wakati gani? 

Seli hiyo ilionekana kuwa seli lini, na namna gani? 

Kwa mwisho kweli, hata uwaze je, utasema kama tu kulikuwa mwanzo wa vyote.  

Sasa watu wanaosadiki kama kuna mwanzo wa vyote watasema, sawa nani huyu alieumba mwanzo, jibu ni rahisi na inaonesha kama ni yeye MUNGU!!! 

Ile seli ya kwanza ilitokea wapi? 

Utasema kama kulikuwako na mwanzo juu hiyi seli ya kwanza ipate kuanza kujigawa. 

Kwa kweli kulikuwako na Mwanzo wa vitu vyote. 

Tuzungumuze sasa juu ya wakristo. 


WAKRISTO 

Wakristo wanajuwa kwa makini yote kama Mungu yu Hai na Yeye anaishi tangu milele na Yeye njoo Muumbaji wa vyote vinavyo onekana na visivyo onekana, 

Wakristo hawawezi amini hizo mawazo ya upumbafu isiyo na musingi kamili, wao wanaimani tu katika hiyo BIBILIA pekee inasema. 

Biblia inatuambia kwa urahisi na upole wote, Mungu aliumba. 

Kusema kama kiwiliwili kimoja kisiyo na akili, wala mawazo njoo kilijigawanya na kufanya leo hii ulimwengu tunaonawo leo ni mushangazo! 

Tazama kwanza vizuri  mwili wako murembo, Biblia inasema kwa uzuri na upole wote, ALIUMBA, wewe ni kiumbe kirembo kweli, 

Tazama mikono yako. 

Kumbuka wakati kiungo kimoja kinaumwa, ni mwili muzima njoo unausika. 

Biblia inatuambia kwa mustari wa pili, 

Nayo Dunia, Inchi ilikuwa  ukiwa tena utupu, 

Unazani kama hiyo kiwiliwil ikya zahabu, bila akili bila mawazo sambamba ingejigawa na kuunda huyu mutu murembo mwenye ni sisi leo? 

Tazameni mikono yenu, unazani kama kuna chombo cha wanadamu ama kitu kingine kyenye mwanadamu aliunda kyenye unaweza kulinganisha na mkono wako? 

Wewe unajuwa aina moja ya Kamera yenye unaweza kulinganisha na mecho yako? 

Angalia nywele yako, nafsi yako yote, Buongo yako kichwani, nina yapenda, niupumbafu mtupu unatuma watu kusema maneno hayo. 

Sasa, mbele ya kuzungumuza juu hayo yenye iko inje ya natharia ya sayansi ya mabadiliko, ingeliwa vema tusema madogo juu ya  sayansi ya mabadiliko kwa wale wasio amini. 


SAYANSI YA MABADILIKO KWA WALE WASIO AMINI

Tujiuliza eti Bibilia inasema ama inafundisha nafasi moja kama Mungu alitumikisha mabadiliko? 

Haiwezekani Mungu kuumba watu namna hii. 

Tukisoma kitabu cha 


MWANZO 2:3 “Na siku ya saba Mungu alimaliza kazi yake yote aliyoyafanya; akastarehe siku ya saba, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoifanya”

Hapo tunakuta  jinsi Mungu alitumika kazi ya kuumba katika siku saba, ni kusema,  

Mungu aliumba kwa muda wa siku saba.  Tusome sasa 


MWANZO 1:3

“Mungu akasema, iwe nuru; ikawa nuru” 

Tusome sasa haya yake ya sita, pale tunakuta siku ya pili, 

“ Mungu akasema, na liwe anga katikati ya maji, likayatenge maji na maji.

Mungu akalifanya anga, akayatenga yale maji yaliyo juu ya anga nay ale maji yaliyo chini ya anga; ikawa hivyo”. 


Tuone sasa siku ya tatu yenye iko hapa chini kidogo katika masomi: 

 “Mungu akasema , Maji yaliyo chini ya mbingu na yakusanyike mahali pamoja, ili pakavu paonekane; ikawa hivyo. 

Mungu akapaita pale pakavu Nchi; na makusanyiko ya  maji akayaita Bahari; Mungu akaona yakuwa ni vyema. 

Mungu akasema, Nchi na itoe majani, mche utoao mbegu, na muti wa matunda uzaao matunda kwa jinsi yake, ambao mbegu zake zimo ndani yake, juu ya Nchi; ikawa hivyo. 

Ikawa jioni ikawa asubui, siku ya tatu.” 


Sikilizeni kwa makini wandugu!!! 

Mungu akayaumba uoto wa asili, akaumba  miti, akaumba majani,  uoto, yote hii Mungu aliiumba kwa siku ya tatu, 

Sasa, ingelikuwa kama Mungu alikuwa anatumikisha mabadiliko, siku inayofwata ingezaa wa nyama, lakini haikuwa hivyo, 

Tuone basi nini ilipitikana siku ya ine. 

“Mungu akasema, Na iwe mianga katika anga la mbingu ili itenge kati ya mchana na usiku; nayo iwe ndiyo dalili na majira na siku na miaka; 


Munaona, MUNGU anajuwa vyote, ndugu, je unalisadiki? 

Mungu anajuwa yote, unaulizo juu ya hayo? 

Ningelitamani tuangalie pamoja namna gani Biblia ina fafanua maneno haya. 

Mungu alifahmu tangu kale kama watu watakuja na elimu yao ya upumbafu ya mabadiriko, alijuwa kwamba  waubiri wamoja na walimu wamoja wa Biblia wataamini hiyo mafundisho ya ujinga ya mabadiriko na wataanza kusema kama Mwenyezi Mungu alitumikisha mabadiliko. 

Mungu alijuwa hayo yote, 

Tutazame sasa siku ya ine 

Kwa siku ya ine Mungu alifanya nini? 

Tujiulize eti Mungu aliwaza kuumba kitu cha kutokea kwa majani, ama muti, ama uoto?  Hapana. 

 Mungu aliruka hayo yote na kujitegemeza tu na anga, na hapo akaumba Jua, akaumba Mwezi, na Nyota juu ifanya majira na dalili. 

Mbele ya kuumba Nyakati, hakukukuweko nyakati, 

Saa, haikukuwa, na hivyo tunaona Mungu hakuguza tena dunia. 

Unazani kwamba Mungu aliumba JUA na MWEZI juu ya uoto? 

Hapana, ni upumbafu!!! 

Mwenyezi Mungu kwa siku ya ine aliacha kuumba mambo inayo elekea udongo. 

Sasa tuone nini Mungu aliumba kwa siku ya tano. 

Na Mungu akasema: 

“Mungu akasema, Maji na yajawe kwa wingi na kitu kiendacho chenye uhai, na ndege waruke juu ya Inchi katika anga la mbingu. 

Mungu akawaumba nyangumi wakubwa, na kila  kiumbe chenye uhai kiendacho, ambavyo maji yalijawa navyo kwa wingi kwa jinsi zao, na kila ndege arukaye, kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema. 


Sikiliza sasa ndugu yangu, 

“Mungu akavibarikia, akisema, Zaeni, mkaongezeke, mkajaze maji ya baharini, ndege na wazidi katika nchi. 

Ikawa jioni ikawa asubui, siku ya tano. 


Sasa, twende kwa haya ya makumi mbili na ine: 

“Mungu akasema, Nchi na izae kiumbe hai kwa jinsi zake, mnyama wa kufugwa, nacho kitambaacho, na wanyama wa mwitu kwa jinsi zake; ikawa hivyo.

Mungu akafanya mnyama wa mwitu kwa jinsi zake, na mnyama wa kufugwa kwa jinsi zake, na kila kitu kitambaacho juu ya nchi kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema. 

Ndugu zangu, munaona Mungu iko anafanya angalisho kwa vyote anavyo umba, Biblia inasema kwa JINSI ZAKE, KWA JINSI YAKE, KWA JINSI YAKE, hatuoni hapa mugawanyiko ama mugawanyo, hakuna kutoka kwa hii aina na kwenda kwa aina nyingine. 

Sasa ni nini inasemwa juu ya kuumbwa kwa Mutu? 

Tusome sasa haya yake ya makumi mbili na sita, inasema: 


Tusikilize kwa makini sana na angalisho yote  na Mungu akasema tuumbe nini MUTU, tujiulize kwa hiyo Mungu alitumikisha magawanyiko? Hapana 


“Mungu  akasema, na tumfanye mutu kwa mufano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, nan chi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.” 

Tusikilize yenye inasemwa hapa, 

Mungu akasema, Mutu akatawale dunia, 

Kutawala, sawa vile tunavyoona ni kuongoza, kumiliki, 

Mutu aongoze na kumiliki samaki, nyama, mtambaazi  na viumbe vyote vykutambaa. 

Sasa ninaulizo la kuwauliza: 

Ningelipenda kujuwa kama mutu ni mabadiliko ya kutokea kwa kitu kimoja kyenye tayari kilikuwa kiishi ama kupatikana katika dunia? 

Juu ya yenye kuelekea uvuvi wa samaki, sawa vile wengi wanapenda kuwua samaki, ni kama mimi siku moja nikiwa narudi kutokea kwenye shule la Biblia, wengi wenye tuliokuwa nawo pamoja walipendelea kwamba ingelikuwa saa ya kufanya mazoezi ya kimwili, ama gymnastics na tulienda kwenye pwani ili tulowe samaki. 

Sisi sote tulikuw na ndoano, mcheche na tukashuka kwa maji kwenye pwani, ilikuwa ikiitwa “Paradizo” 

Na hapo, kulikuwa tu samaki nyembamba  sana. 

Samaki ilikua nyembamba sana kupita wembamba wenye nilikua nalo. 

Na tulipo fika hapo, tukaona kwamba wale wavuvi va samaki kwa siku nyingi wenye walikuwa pale tangu saa nyingi wenye kusimama, mpaka hivyo walikuwa hawaja pata kitu chochote. 

Mara kwa mara wakati nilikuwa nasafiri niki pita kwa barabara yenye kuwa juu ya ile pwani kwenye walikuwa wanalowa samaki, wakati nilikuwa naona wale wavuvi wakisimama tu wima, ilikuwa inanipa shida sana. 

Nilikuwa nikijiuliza, “Watu hawa wata pata kweli samaki ngapi?” 

Kwa hiyo tujiulize eti watu wanatawala juu ya samaki? 

Aksanti hivi Maandiko inatuambia juu ya wavuvi wa watu! 

Hakuja patikanako mufalme wa dunia nzima, na hivyo vivyo, hakuna mufalme wa samaki kama vile najuwa! 

Wandege vile vile wanatajwa, nini inasemwa juu ya samaki? 

Namna gani munatawala juu ya ndege? 

Namna gani munawanasa? 

Munatumia  singa ya mitego, sivyo, 

Mimi, kwa kweli naogopa nyoka sana, sipende kuiona, heri kweli nikutane na simba, ndege, kitu chochote mbalimbali na nyoka! 

Dada yangu, mutoto wa mujomba alikuwa akitumika katika chamba kubwa la mjomba, na ndani yake kulikuweko miwa, na mara kwa mara wakati alikuwa anatumika amo, alikua anaacha milango wazi 

Vitu nyingi vilikuwa amo na mimi nilikuwa tu nachukuwa kwa mukono wangu fimbo ya kujikinga na nyoka, sababu nyoka iko hatari. 

Na ninajuwa kwamba wengine watu wenye woga walikuwa wanafanya hivyo. 

Sasa tujiulize, munawaza kama watu wanakuwa na mamlaka juu ya nyoka wanaokuwa katika pori? 

Sasa tuangalie yanayo elekea uoto, watu wanapendelea kufikilia sana kwa vitu vinavyo waletea utajiri … 

Tuone sasa anga, angahewa, hali ya hewa, hatuna mamlaka juu ya hali ya hewa, kama kunanyesha mingi, hiyo inaweza hata kutuzuia kukusanyika pamoja juu ya kuabudu Mungu wetu. 

Munajuwa mutu mwenye anamiliki hali ya hewa? 

Siku moja wakati nilikuwa najitayarisha kupokea wageni na mukristo moja aliniuluza kama nilijiandaa juu ya hali ya hewa nili mujibu hapana, na wakati tu lilimukumbusha kama inawezekana nisafiri kesho, hapohapo nvua ikaanza kunyesha. Na vilevile siku ifwatayo kuliendelea kunyesha kweli. Unaweza kuwaza kama ilikuwa tu ya kubahatisha, hapana, ni nvua. 

Nikajona kama sina mamulaka juu ya hali ya hewa. 

Munaona, watu hawana mamulaka yote juu ya ulimwengu, 

Pahali ya kuendelea mbele, watu wanarudi nyuma kweli, nyuma hata ya kwenye walianzia. 

Tusome sasa kwa kitabu ya  Mwanzo sura mbili, 

Kweli Mungu aliumba mutu sawa mutu, musikilize kwa makini maandiko haya, Mungu akaumba nani, mutu, sasa eti hapa Mungu alitumikisha mabadiliko ama magawanyiko, hapana!!!


MWANZO 2:7 

“Bwana Mungu akamfanya mutu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mutu akawa nafsi hai.” 

 Ndugu zangu sikilizeni kwa makini, 

Mungu aliukamata mavumbi na kwa hiyo akamufanya mutu na akapulizia katika pua yake pumzi ya uzima. 

Tuzungumuzie kidogo juu ya hiyo sayansi ya mabadiliko, 

Tukiangalia hiyo magawanyiko ya kufwatana, mugawanyo unao jifwta kwa muda Fulani, 

Mungu alimuumba mutu kwa mavumbi, 

Sasa tujiulize, 

Eti Mungu aliukamata yale mavumbi na akaanza kuugawanya? 

Akafanya mugawanyo unao jifwata kwa kiasi Fulani ili afikie kupata mutu? 

Tusome kwanza ZABURI 103:14 

Sikilizeni ni wasomee, Tusome katika Jina la Yesu: 


ZABURI 103:14 

“Kwa maana Yeye anatujua umbo letu, Na kukumbuka yakuwa sisi tu mavumbi.” 

Mungu anajuwa sisi ni nini na anajuwa kama sisi ni mavumbi, 

Eti, sisi tunatokea kwa mugawanyo? Acheni mawazo hiyo ya upumbafu. 

Kiisha kufa kwetu, wakati wandugu zetu wanachukuwa mwili wetu, wanau ili wampake, wanautengeneza matumbo na kuumwangia malashi, na kuuvika nguo na kwa mwisho nini inakuja? 

Wanaukamata na inaenda mara moja kwa mavumbi. 

Hiyo imeetwa rushwa, utoaji hongo, 

Kumbukeni kwamba wakati Bwana Yesu alienda kaburini kwa rafiki yake mpendwa, 


YOANE 11 

Wakati Bwana Yesu alikuwa akizungumuza na wa dada wawili wa marehemu, wao walimusii na kumwambia kama ndugu yao alikufa tangu siku nyingi na hivi ananuka  harufu mbaya sana. 

Wakati Mungu alipoumba mutu, alimuumba kutoka mavumbi na ni kwa mavumbi anarudi wakati anapokufa. 

Mutu anarudi kwenye alipotoka. 

Sasa tusikilize neno lingine. 

MWANZO 2:7, acheni nowasomee tena neno moja: 

“Mungu akamuumba mutu kwa mavumbi na aka… 

Sikiliza muzuri ngugu yangu, 

Akampulizia wapi, 

Kwa pua yake, pumzi ya uzima na mutu akakuwa nafsi inayokuwa na uhai. 


Mungu aliukamata mavumbi, mavumbi, akamufanya mutu, na mbele ya kupulizia ndani yam utu pumzi ya uzima, alimutia kwanza pua. 

Sasa hapo eti munaona hadisi zao za mabadiliko kutokea mutu? 

Eti Mungu alitumikisha aina Fulani ya mabadiliko? 

Mutu aliumbwa mutu na akiwa na pua yake vilevile. 

Na Mungu alimupumuzia katika pua lake pumzi ya uzima. 

Sasa tusome katika ISAYA 2:22 

“Mwacheni mwanadamu ambaye pumzi yake I katika mianzi ya pua; kwa maana hudhaniwaje kuwa ni kitu?” 

Tuisome tena katika WAEBRANIA. 

Sasa tupime kuingiza pumzi tuki ingiza kwa ujazi pumzi mara moja, 

Uiingize ijae mbavuni, na mbele yakuiondosha uingize tena ingine mara moja, eti yawezekana? Jibu ni hapana. 

Haiwezekane sababu mutu ana uwezo ya kuingiza  pumzi kwa kujaza mbavu yake kwa mara moja tu. 

Unaona namna gani uzima wetu unategemea iyo? 

 

Mungu akapumuzia ndani ya pua la mutu pumzi ya uzima na mutu akageuka kuwa nafsi ya uzima.

Alimuumba mutu mzima, hakufanya magawanyiko ama kufanya kwanza kazi moja mbele. 

Napenda kujuwa kama kuliisha acha kutumikisha pua zetu? 

Munajuwa namna gani pua ni ya lazima kabisa, sivyo? 

Mungu alimuumba mutu kama mutu na akampatia pumzi ya uzima na mutu akaendelea kutegemea pua yake inayomupa pumzi ya uzima. 


Ninaulizo lingine lakuwauliza. 

Eti umbo la mutu uliendelea kubadilika kuachana na vile ulikuwa mbele? 

Tusome 


MWANZO 6:5  

“Bwana akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoni mwake ni baya siku zote.

Bwana akaghairi kwa kuwa amemfanya mwanadamu duniani, akahuzunika moyo.

Bwana akasema, Nitamfutilia mbali mwanadamu niliye muumba usoni pa nchi; mwanadamu na nyama, na kitambaacho, na ndege wa angani, kwa maana naghairi ya kwamba nimewafanya.” 

Tupime kufikili, 

Hii njoo umutu wa mwanadamu unafanya. 

Mungu alimuumba mutu, sawa mutu, akamuita Adamu. 

Na muzaliwa wa kwanza kwa dunia hii alikuwa nani? 

Alikuwa muuaji njoo maana kiisha vizazi vichache, hapo tunafika kwa nyakati za Nowa, 

Mungu alihuzunika na akaghairi juu ya nini alimufanya mutu, nikusema mutu aligeuka kuwa muchafu sana rohoni,  mubaya saana kuputiya mwanzo waki, aligeuka kuwa mutenda zambi Zaidi ya vile alikuwa mutenda zambi wakati wa Adamu, 

Adamu aliye fanya zambi. 

Sasa tujiulize, ingelikuwa mutu anaendeleaka katiko mabadiliko, jee hangalikuwa muzuri Zaidi? 

Mutu anakuwa mubaya sana na muchafu sana tangia siku nyingi. 



Tusome

 

2 TIMOTHEO 3: 1  

“Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. 

Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, 

Wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, … 

Wenye mfano wa utawa, lakini wakikana nguvu zake; “


Tujiulize, eti mutu anasonga mbele? 

Katika 2 TIMOTHEO. Mungu anatuzungumuzia juu ya watu walioamini, watu wenye wiko wanamemba wa Mwili wa Kristo. 

Nazani kama Kanisa Mwili wa Kristo, inapoteza samani yake kweli. 

Na hapo kweli, 

Hakuna mwenye kuendelea mbele, 

Lakini kuna huyo mwenye kurudia nyuma. 

Mutu anageuka kuwa mubaya sana kupita jinsi alivyokuwa mbele. 

Mutu wa leo ana vifaa vingi,  ana Gazeti, Redio, Televijieni, anakuwa na urahisi wa kupasha habari na kuzungumuza, simu, anakuwa na uwezo ya kuenda angani, kuruku kama ndege hewani, tena Zaidi kwenda kwa mwezi ama angani nzima Zaidi ya saa makumi mbili na ine. 

Lakini mafaa ya hiyo? Yeye anapoteza!!! 

Tusome 


MWANZO 5:1, hapo, nitawaonesha kitu kingine kinao onesha kama Mwenyezi Mungu hakutumikisha mabadiliko. 


MWANZO 5:1

“Hiki ndicho kitabu cha vizazi vya Adamu. 

Siku ile Mungu alipoumba mutu, kwa sura ya Mungu alimfanya; 

Mwanamume na mwanamuke aliwaumba; akawabariki akawaita jina lao Adamu, siku ile walipoumbwa. 

Adamu akaishi miaka mia na thelathini, akazaa mwana wake kwa sura yake, kwa mfano wake, akamwita jina lake Sethi, 

Siku za Adamu baada ya kumzaa Sethi zilikuwa miaka mia nane, akazaa wana, waume na wake. 

Siku zote az Adamu alizoishi ni miaka mia kenda na thelathini, naye akafa. 

 

Sasa munifwate kwa makini sana, 

Hapa tunaona mutu wa kwanza aliye umbwa sawa Adamu, aliishi miaka mia kenda makumi tatu, 

Munamujua mutu moja anye fikisha umri huo leo? 

Sasa tutasema kama mutu anabadirika na kuenda mbele ama ? 

Sasa tusome haya ya sita, 


Sethi akaishimiaka mia na mitano, akamzaa Enoshi. 

Sethi akaishi baada ya kumzaa Enoshi miaka mia nane na saba, akazaa wana, waume na wake. 

Siku zote za Sethi ni miaka mia kenda na kumi na miwili, akafa.


Tusome haya ya makumi mbili na saba, 

Siku zote za Methusela ni miaka mia kenda na sitini na Kenda, akafa.

Tusome haya makumi tatu na moja.

Siku zote za Lameki ni miaka mia saba na sabini na saba, akafa.  


Watu wanasema kama Mungu alitumikisha mabadiliko, lakini sasa tazameni, watu kiisha kuumbwa kwao na Mungu walikuwa wanaishi mw miaka ma mia, 

Lakini kwa sasa, wanatudanganya wakisema kama sisi tuliendelea mbele katika mabadiliko…. 

Hiyo sayansi ya mabadiliko, eti ilifanyika katika siku nyingi sawa vile wasemavyo,  

Lakini hiyo haiambatane hata mara moja na Biblia tena haiangalie Biblia. 


Sasa naamini na ninajuwa kwamba haiwezekani mutukuamini Biblia na kuwa na mawazo ama mafikili ya kuamini hata chanjo moja ya hiyo sayansi ya mabadiliko.

Kama munasikia mutu ambaye yeyote iko anahubiri juu ya sayansi ya mabadiliko ya wasioamini, usijali kumufwata katika mambo asemaye, wewe umubebe tu kunako maandiko matakatifu, Neno la Mungu.  

Hiyo yao ni mawazo mtupe, sababu Biblia haiseme kitu juu ya hayo. 

Sasa tuone yanayo elekea hii sayansi ya mabadiliko kama SILAHA YA SHETANI,  

Eti kuna mumoja katikati yenu mwenye kufikili juu ya mambo yanayo tukia sasa katika inchi yetu? 

Tuache kwanza dunia nzima na tuangalie inchi yetu kwa upekee, 

Eti munajuwa ya kuwa tumetawaliwa na watu wenye miili ya kuharibika? 

Mutu moja mwenye akili jina lake DARWIN aliye zungumuza juu ya hiyo  sayansi ya mabadiliko ya upumbafu. 

Mfumo wetu wa kielimu, namna yetu ya kufunza watoto wetu,  eti munajuwa mwanzo wake? 

Mutu gani aliye uunda? 

Eti mwajuwa juu ya nini tuna hesabu miezi na masiku? 

Nani alie anzisha hiyo kutamka? 

Nani alieanza kijeli hiyo, muzaa huo? 

Ni ndugu Segman FROY 

Ni mutu gani aliyeunda msingi wa mfumo wa kiuchumi? 

Ni mutu anayeitwa John MELDREID KASE, na mbele ya kufa kwake, alikanusha hayo yote. 

Ni nini inayokumba wanadamu? 

Mwanadamu anafikia kwa kiwango ya kutafuta majibu ya maulizo yake yote kwa watu. 

Wakati Prezidenti GEORGES alileta sheria yake juu ya umaskini, yeye alikanusha Mungu. 

Mungu alitukumbusha kwamba ni uchovu wenye tunapendelea ndio uta  tunatumikia. 

Mungu hakuomba wanadamu waponesho magumu yote ya dunia. 

Ni vigumu sababu zambi iko hapo. 

Taabu, shida, kutafuta uhuru, yote ni vigumu sana sababu zambi iko hapo. 

Lakini watu walijizania kufika kusema kama mutu binafsi anaweza akapate surulisho kwa tabu zake,  na hiyo ni inaambatana na maadibisho na elimu tunayoipata. 

Na maadibisho hiyo inasema na kufundisha nini, eti munayafahamu? 

Tusome Biblia katika kitabu cha Wakorinto wa pili sura 11 na haya 13, 

Sababu gani tunahakikisha kwamba Shetani iko anatumika katika hiyo miradi? 

Nitawaonesha sababu hiyo… 


2 WAKORINTO 11: 13, sasa tusikilize kwanza, 

“Maana watu kama hao ni mitume wa uongo, watendao kazi kwa hila, wanajigeuza wawe mfano wa mitume wa Kristo. 

Wala si ajabu. 

Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru. 

Basi si neno kubwa watumishi wake nao wakijigeuza wawe mfano wa watumishi wa haki, ambao mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao.” 


Sasa, eti munafahamu mambo gani Shetani aliyomuambia Adamu? 

Alimuambia kama Mwenyezi Mungu anafahamu ya kwamba siku mutakula tunda la muti wa uliokataliwa, mutajuwa wazi, 

Shetani alitaka kuwaambia kama, mutakuwa sawa na Mungu. 

Kweli munasadiki hiyo? 

Mutakuwa na uwezo ya kupata jibu kwa malalamiko na taabu yenu, mutakuwa mukiziweza na kujitegemea, mutakuwa huru, hiyo njoo miradi hiyo. 

Wanadamu wanajaribu kushurulikia wanadamu wenzao. 

Wanadamu wanakuwa na ndoto na kujizania, watu wanaokuwa na uhuru juu ya mali zao, hawa hawaja onekana kamwe duniani. 

Sasa YESU KRISTO, MWANA KONDOO WA MUNGU, MKOMBOZI WETU, MWOKOZI WETU, alikuja hapa duniani akijinyenyekeza, akiacha kwa muda UFALME wake juu yako na yangu, juu ya zambi zako na zangu, Z.A.M.B.I. 

Haipashwi kutegemea tu elimu ya dunia hii na kusahau ukubwa wa Mkono wa Bwana aliye juu, na kuzarahu kusikiliza yasemayo Biblia, 

Kweli watu wanaonesha maendeleo, kunakuwa miradi na uundo wenye kufanikiwa na matumizi yao haiku ya kimungu. 

Namna gani watu wanajitememea? 

Namna gani wanaharibu mazingira, wewe una furahia hivyo? 

Miradi hizo zote zinaonesha kushindwa kwa shetani, sababu hii njoo ile miradi ya “HUMANISME” “UTU” 

Ni hali na falsafa ya kumutia mutu awe musingi wa vitu vyake vyote. 

Mutu akitafuta surulisho juu ya maulizo na taabu yake, mutu akija na ndoto yake na hiyo inamupa mutu kiburi na kumurudisha nyuma Zaidi, 

Mutu anakuwa mwenye kujipenda binafsi, mwenye matukano, asiye na maadibisho na kujizuiza. 

Kwa siku ijayo tutaona wale wa sayansi ya mabadiliko wenye wiko na wazimu. 

Maombi ya mwisho 

Tuombe: 

Mwenyezi Mungu na Baba yetu, 

Tunakushukuru kwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, 

Tunakushukuru hayo ya kadiri uliotupatia kupitia mahubiri tuliyopata leo, 

Yenye inatokea ndani ya Maandiko yako Matakatifu. 

Baba yetu tunakupigia aksanti mara dufu, 

Twafahamu kwamba tunapashwa kukutegemea katika njia zetu zote, 

Tukikutwiga mizigo yetu yote tunayo wazia, 

Wewe unamajibu yote yenye inaweza kutupatia mwangaza tena inaweza kututuliza, kutuongoza, na yenye mafaa kwetu. 

Na tungependelea kwamba uwe pia pamoja na wenye kukukana sababu hawajuwi kwamba kuna Yeye aliyewapenda na kutowa maisha yake na kufa kwa ajili yao, Yeye Yesu Kristo. 

Uwafunguwe macho yao ili wamuone na kumufahamu Bwana Yesu sawa vile Biblia inatuonesha. 

Tunakushuru katika Jima la Bwana na Mwokozi wetu YESU KRISTO. 


Amen

Ref: 04/26/1981 / 605-2 NATHARIA YA SAYANSI YA MABADILIKO / Silaha ya Shetani / Theory of Evolution / 04/16/2019