Friday, July 30, 2021

NIA GANI MWENYEZI MUNGU ANAYO KUHUSU KIBURI CHAKO CHA DINI / WHAT GOD THINKS OF YOUR RELIGIOUS PRIDE

Photo by B Smith from the kitchen door


 


NIA GANI MWENYEZI MUNGU ANAYO KUHUSU KIBURI CHAKO CHA DINI / 

WHAT GOD THINKS OF YOUR RELIGIOUS PRIDE 

October 14, 1962

Pastor Henry F. Kulp



 

Waroma 3: 23 – 27 

“kwa sababu wote wamefanya zambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu; wanahesabiwa haki bure kwa neema yake kwa njia ya ukombozi ulio katika Yesu Kristo: 

Naye Mungu amekwisha kumweka awe upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake, kusudi aonyeshe haki yake kwa sababu ya kuachilia zambi zilizofanywa zamani, katika uvumilivu wa Mungu: 

Apate kuonyesha haki yake katika wakati huu, ili awe mwenye haki na mwenye kuhesabia haki mtu anayeamini Yesu. 

Basi wapi tena kujisifu? Kumefungwa inje. Kwa sheria gani? Kwa matendo?

Hapana! Lakini kwa njia ya sheria ya imani.” 

Watu wa dini hawachoke kuwa na mawazo, na wakati mawazo yao yanazidi, wanafika kiwango cha kuzania kwamba Mungu hatendi haki. 

Wanafikia kuzania kwamba Habari Njema kwa watu wote, siyo Habari Njema ya haki. Inamufanya Mungu kuwa sawa mnyonge, asiyekuwa na nguvu ya kulitetea Jina lake. 

Maandiko haya tutakayo jifunza kwa asubui ya leo yatatuhakikisha ya kwamba wakati Mwenyezi Mungu anaokowa nafsi kwa njia ya Kufa na Ufufuko wa Bwana wetu Yesu Kristo, Mungu huyo ni Mungu Mwenye haki na mwenye kulitetea Jina lake kwa sababu anaokoa mwenye zambi. 


1/ Mtume Paulo anatupatia mfano wa watakatifu wa Agano la Kale, namna gani Mwenyezi Mungu alikuwa akitetea Jina lake kwa namna alivyo waokowa watu wa Agano la Kale, akiwahesabu watu wale kuwa wenye haki, ijapokuwa Bwana Yesu Kristo alikuwa bado hajamwanga Damu yake. 

Tukamate mfano wa Abrahamu. 


2/  Maandiko yanasema kwamba Abrahamu alikuwa mtu aliye hesabiwa haki na Mungu miaka elfu mbele Bwana Yesu Kristo kuja kumwanga Damu yake. 

Abrahamu alikuwa mtu wa aina gani? 

Twajuwa kwamba Abrahamu alikuwa mwoga. 


3/  Yeye alitaka kuharibu heshima ya muke wake Sarah kwa kujiepusha na kifo. 

Tayari Mwenyezi Mungu alikwisha kumtaja Abrahamu kama rafiki wa Mungu. 

Kwa kweli Mungu wa Biblia ni Mungu wa aina gani anayekuwa rafiki ya mtu asiye na heshima na mwenye haya? 


4/ Tutwae pia mfano wa Musa. 

Musa alikuwa muuaji, mtu aliyekimbia mahakama, wakati Mwenyezi Mungu alipojionesha kwake na kumutuma aende kumuwakilisha huko Misri. 

Mwenyezi Mungu alimupa Musa jina la “Mtumishi wangu” akimuweka kuwa kiongozi wa Taifa lake kubwa. 

Kiisha Mwenyezi Mungu aliweka vibao vya amri kumi, kwa mikono ya Musa inayojaa damu, na  kati ya amri hizo, amri moja ilisema: Usiuwe. 

Eti tendo lile ni unafiki? Ni Mungu gani awezaye kumusweka mtu muuwaji kutangaza habari hiyo?  


5/ Mwaweza kusema kwamba Abrahamu pamoja na Musa waliokolewa kwa umwangaji wa damu ya sadaka mbadala isiyo na hatia, wakati walipotwaa toleo kwa sadaka na kuichinja kwa kumwanga damu yake. 

Bali, tuchukue muda kidogo kwa kufikiri katika Maandiko ya Waebrania 10: 4 

“Maana haiwezekani kwa damu ya ngombe na mbuzi kuondoa zambi.” 

Kwa mwangaza ya aya hii, jameni niwaulize: 

Namna gani, kwa muda wa miaka 4000, Mwenyezi Mungu alikuwa akitizama zambi kwa sababu  hazikuwa zimeondolewa ? 

Na hapo ningelitamani muweke mafikiri yenu juu ya neno “kuondolewa”.  

Katika Agano la Kale, damu ya ngombe na mbuzi haikuweza kuondoa zambi, kwa kumaanisha kwamba kwa wakati ule zambi hazikuondolewa. 


6/ Tuchunguze pia Maandiko ya Zaburi 32: 1 

“Heri yeye aliyesamehewa makosa yake na zambi yake imefunikwa.” 

Katika nyakati zile, wao walihesabiwa haki. 

Katika Agano la Kale, Mwenyezi Mungu alitenda nini kwa kuwahesabia haki? 

Tambuwa vema yasemavyo: Heri yeye aliyesamehewa makosa yake na zambi yake imefunikwa. 


7/ Tulinganishe sasa yale mawazo na yale tunayoyapata katika Maandiko ya Waebrania 10: 4.

 “Maana haiwezekani kwa damu ya ngombe na mbuzi kuondoa zambi.” 

Zambi hazikuondolewa, zambi zilifunikwa. 


8/ Tuyalinganishe vilevile na Maandiko ya Waebrania 9: 6 

“Basi vitu hivi vikikwisha kutengenezwa, makuhani waliingia katika hema ya kwanza siku zote, wakitimiza mambo ya kuabudu.” 

Yawezekana wengi katikati yenu wanasema: 

Tunatoka kwa kartasi hiki na kwenda kwa nyingine na vivi hivi tukibadili ukurasa mbalimbali za Biblia. 

Ninakubali jambo lile, bali ninawajulisha kwamba ni mazoezi mazuri kwani itawasaidia kupata haraka kitabu fulani cha Biblia, pia ni mazoezi mazuri katika Majifunzo ya Biblia. 

Tuchunguze yanayosemwa katika Maandiko ya Waebrania 9: 26  

“…, lakini sasa, mara moja tu, katika mwisho wa dunia, ameonekana aondoe zambi kwa kujitoa mwenyewe.” 

Siyo jambo la kufunika zambi. 

Katika Agano la Kale, zambi zilikuwa zikifunikwa tu.

Mwenyezi Mungu alikuwa akifunika zambi hadi kufika kwa Kristo, na ni hapo Mwenyezi Mungu aliondoa zambi. 

Aliondoa zambi kwa kujitoa mwenyewe. 


9/ Waroma 3: 26  

“apate kuonyesha haki yake katika wakati huu, ili awe mwenye haki na mwenye kuhesabia haki mtu anayeamini Yesu.” 

Wakati Mwenyezi Mungu anapohesabia mtu haki, anamufanya kuwa safi safi sana pasipo taka mbele ya Mungu, siyo mtu ambaye zambi zake zilisamehewa, siyo mtu ambaye zambi zake zilifunikwa, bali zambi ziliondolewa na mtu anafanywa kuwa mwenye haki sawasawa na haki ya Mwenyezi Mungu mwenye Nguvu zote. 

Mungu anafanya tendo lile katika haki yake, siyo pasipo kufahamu vinyume vyake, bali Mwenyezi Mungu anaona kwamba ni vizuri atende hivyo. 


10/ Mwenyezi Mungu ni mwenye uwezo wa kutenda jambo lenye baraza ya mahakama ya kimtu haiwezi kamwe kutenda. 

Jambo lenye hakimu wakili hawezi kamwe kutarajia kutenda.

Yaweza kuwa jambo la kushtusha na la mastaajabu kuona hakimu kumuachilia mtu aliyehukumiwa na kusema kwamba anakuwa mwenye haki. 

Ni Mungu pekee anayeweza kumgeuza mwenye zambi na kumuweka mwenye haki, na anafanya hiyo katika Kufa, Kuzikwa na Kufufuka kwa Bwana wetu Yesu Kristo. 


11/ Siku iliyopita, nilisoma maonyo makubwa katika Maandiko ya 2 Samweli na ingelikuwa heri tuyasome pamoja, ni hadisi inayojulikana sana katika Agano la Kale, lakini kuna jambo moja watu hawaweze kamwe kuvumbua.  

Ni historia ya Abusaloma mwana wa Daudi. 

Naamini kwamba munakumbuka historia ya Abusaloma aliye uwa mtu.

Uuaji ulitendeka katika jamaa ya Daudi. 

Abusaloma alimurukia ndugu yake na kumuuwa baadaye akakimbia. 

Abusaloma alikuwa mtoto mpendwa wa Daudi na Daudi alikuwa anamupenda sana. 

Abusaloma alikuwa mwenye sura nzuri na wana wa Israeli wote walikuwa wakimpenda, lakini aliishi katika ukimbizi, na Yoabu, mkubwa na kiongozi wa majeshi yeye alipenda Abusaloma arudi, lakini mfalme Daudi hakufanya chochote kile kiwezekanavyo ili Abusaloma arudi. 

Kwa hivi Yoabu alitumia mwanamuke mwenye hekima ili aende kumlilia mfalme Daudi, kusudi Abusaloma arudi nyumbani. 

Kwa hivyo mwanamke huyo alitunga hadisi. 

Naye akasema: 

Mimi ni mujane na nina watoto wanaume wawili.

Watoto hawa wangu wawili waligombana na mmoja akamuuwa ndugu yake. 

Kwa hiyo taifa nzima ikajiinuwa juu ya huyo aliyebaki mzima, wakimshambulia na kuniambia kwamba wanahitaji mimi nimuuwe. 

Magumu ni kwamba, wakimuuwa, mimi nitabaki peke yangu. 

Nitakuwa mujane bila mafaa yoyote. 

Mwanamke huyu alilia akimsihi sana mfalme hata ikafika kiwango mfalme akaamuwa kwamba huyo mtoto hatauwawa, atahepushwa kufa. 

Kusihi na kuomba kwa huyu mama kulikuwa namna hii na ningeliwaomba kuyachunguza: 

2 Samueli 14: 13, 14  

“Mwanamke akasema; kwa nini basi ulifikiri mambo ya namna hii juu ya watu wa Mungu? 

Kwa nini akisema neno hili, mfalme ni kama mmoja aliye na kosa, kwa kuwa mfalme harudishi tena mfukuzwa wake. 

Kwa kuwa ni sharti kwetu kufa, nasi ni kama maji yaliyomwangika juu ya udongo yasiyoweza kuokotwa tena; wala Mungu haondoi uzima, lakini anafanya shauri hata yeye aliyefukuzwa asiwe mkimbizi kwake.” 

Mwanamke huyo alimwambia mfalme Daudi: 

Daudi ulitenda makosa ndani ya maneno uliyoyasema. 

Ulisema kwamba mwanangu atahepushwa kufa sasa je kuhusu mwana wako?

 Yeye amelaaniwa, nawe hupendi kamwe arudi, siyo hayo tu, wewe umekosea watu wa Mungu na umemkosea pia Mungu, kwa sababu Mwenyezi Mungu anawarudisha wale waliomkosea na waliofukuzwa. 

Daudi akasema: Sawa, nitamrudisha Abusaloma. 

Lakini Abusaloma hakusamehewa zambi zake kamwe.

Yeye alikuwa muuaji na Daudi alikusudia kufanya yale Mwenyezi Mungu aliyofanya, na matukio yake yalikuwa gani? 

Abusaloma alirudishwa na kwa mwisho alimufukuza baba yake Daudi kwenye kiti cha ufalme. 

Daudi aligeuka mtu wa kuangaika angaika mbali na kiti cha ufalme na Abusaloma, kiisha kufukuza baba yake toka kiti cha ufalme, alitawala juu ya kiti cha ufalme na ni kiisha tu kufa cha Abusaloma ndiyo Daudi alirudi kwenye kiti chake cha ufalme. 

Ningelitamani muhakikishe na kukumbuka neno hili: 

Hakuna yule anayeweza kufanya yale Mwenyezi Mungu anayoyafanya. 

Ni Mungu pekee aliye Mwenye Haki. 

Daudi alizani kwamba anaweza kutenda yale Mwenyezi Mungu anayotenda, lakini matukio yake ni kwamba aliteseka. 

Wakati unapokusudia kutimiza yale Mwenyezi Mungu anayoyafanya, kwa  kukusudia kuongeza neno lolote kwa miradi ya wokovu, ili watu wawe wenye haki, utajikuta umekumbwa na matatizo kwa sababu wewe hauko Mungu, na huwezi kamwe kutenda yale Mwenyezi Mungu anayoyatenda.  


12/ Tuchunguze sasa Taifa la Israeli ilikuwa namna gani wakati ilipokuwa chini ya sheria, wakati Mwenyezi Mungu aliwahesabu kuwa wenye haki akifunika zambi zao kwa damu ya toleo ya sadaka.  

Tuone kiwango gani Mwenyezi Mungu aliwahesabu kuwa haki. 

 Mwenyezi Mungu aliwakombowa toka Misri, akawafungulia njia katika Bahari Nyekundu, katika safari yao walikuwa wakinungunika na kulaani Jina la Mungu, pia walikuwa wakichunga miungu katika masanduku zao, hata wakati walipokuwa wakila kondoo aliyechomwa kwa pasaka ya mapito. 

Wana wa Israeli walikuwa wakizunguukwa na Mataifa yenye ilikuwa ikiabudu Shetani na mapepo mengine mbalimbali. 

Siku moja, wana wa Israeli katika safari yao jangwani, walifika katika pwani la Moabu, kwa njia panda ya Yeriko na ya Yordani. 

 Na ilikuwa kiisha wana wa Israeli kupiga vita kali na wa Amori na kuwaangamiza sana, na habari  hiyo ilileta woga kwa wana wa Moabu. 

Na mawazo ya wana wa Moabu ilitiwa woga kuona namna wana wa Israeli watafika pale na kuwafwagia kwa mara moja. 

Katika siku zile mfalme wa Moabu jina lake lilikuwa Balaka, naye kwa woga na kuharikisha akakwenda kumwona mtu moja jina lake Balama. 

Mtu huyo Balama alikuwa akijulikana kama nabii katika eneo lile. 

Mfalme Balaka akakwenda kumwona Balama akimusifu akisema kwamba anaushuhuda wake kwamba yoyote yale Balama analaani yanalainiwa kweli na yoyote yale Balama anabariki, yanabarikiwa kweli. 

Mfalme Balaka akamtolea Balama heshima na mali mengi na kumuomba awalaani wana wa Mwenyezi Mungu. 

Mwenyezi Mungu akamtokea Balama na kumuagiza asifanye yale anayoombwa kufanya. 

Hatuta poteza wakati tukiwaambia namna ngamia ilizungumuza na Balama na mambo yote yaliyotendeka. 

Natamani niwapeleke pole pole kwa kiini ya historia hii. 

Kiini ya historia hii kwetu ni kwamba tutambuwe ya kuwa wana wa Israeli walikuwa wenye zambi na Mwenyezi Mungu aliwabariki katika neema yake pahali pa kuwalaani katika haki yake. 

Ni vigumu kutambuwa kwa nini ilimushinda Balama kupata maneno yanayoweza kulaani Israeli.  Hapa tuna hotuba ya Balama yeye pekee: Na anayesemwa hapa ni Mwenyezi Mungu.

Hesabu 23: 21 

“Hakutazama uovu katika Yakobo, 

Wala hakuona ukaidi katika Israeli; 

Bwana Mungu wake ni pamoja naye, 

Na sauti kubwa ya mfalme ni katikati yao.” 

Aya hii ni ya ajabu na maalum sana.

Kwa kusema kweli, uovu ulikuwa katika Yakobo, lakini Mwenyezi Mungu alikataa kuyaona, na kweli  katika Israeli, wengi walikuwa katika njia ya upotevu, lakini Mwenyezi Mungu hakuyatazama. 

Kwa kweli hangaliweza kuyatazama, kwa sababu hangaliweza kufanya hivyo. 

Mwenyezi Mungu hatazami zambi za wale wenye wanaomwamini. 

Mwenyezi Mungu hatazami zambi za wale wenye anao wahesabia haki. 


13/ Hesabu 23: 19, 20 itatusaidiya kufikia kiwango cha neno hili.

“Mungu si mtu aseme uwongo; wala mwana wa mtu, ajute, 

Amesema naye hatalifanya? Au amenena naye hatalitimiza? 

Tazama, nimepewa amri kukubariki; 

Naye amebariki, na siwezi kuligeuza.”  

Mutambue kwamba mimi Balama nililazimishwa kubariki, hata nikiagizwa maneno toka kwa Mungu, maneno nitakayobariki nayo Taifa lile.  

Na kwa huyo mwenye Mungu anambariki, mimi sina la kufanya hata siwezi kuligeuza. 

Mwenyezi Mungu alibariki Israeli, Mwenyezi Mungu alihesabia Israeli kuwa yenye haki. 

Mshtuko gani wa raha unaotiwa na neno hili katika mioyo yetu. 

Ni Mwenyezi Mungu pekee aliye mwenye Haki na ni yeye pekee anayehesabia Haki wale wanaomuamini. 


14/ Tuchunguze sasa sehemu ya mwisho wa Aya hii ya Waroma 3: 26, 27 

Inayosema kwamba: 

“…Ni Mwenyezi Mungu ndiye anayehesabia haki mtu anayeamini Yesu.

Basi wapi tena kujisifu? Kumefungwa inje.”  

Lakini kama vile munavyo fahamu, watu wa dini, hawapendi kufahamu maneno haya, wao wanazania kufanya tendo fulani ili wawe wenye kustahili na kuwa wenye samani fulani kwa mecho ya Mwenyezi Mungu.        

Kuna wengine watu wanao ambia wenye zambi watolee Mwenyezi Mungu roho zao. 

Muniruhusu kuwapa swali moja: 

Faida gani Mwenyezi Mungu anaweza kupata na roho yenye kujaa uchafu? 

Roho ya mtu haikubali kusahihishwa, ni mkali sana na yenye kupotoka. 

Siyo lazima kumwambia mtu mwenye anapenda kugeuka mwamini kwamba amletee Mwenyezi Mungu roho yake. 

Kwa kweli ni nini inayompasa kufanya? 

Inayompasa kufanya ni kuamini Maandiko Matakatifu Neno la Mungu kuhusu Damu ya Msalaba, na kuhusu kufa kwa Bwana wetu Yesu Kristo.  

Ni kwa yule mwamini, mtu aliyeokoka anayekuwa sasa na roho iliyozaliwa na kufanywa upya, ni huyo anayeweza kuombwa kumtolea Mwenyezi Mungu roho yake. 

Tumeokoka kwa kuamini ushuhuda wa Mwenyezi Mungu kuhusu Mwana wake, Kufa kw


15/ Jameni tuwaoneshe kitu kingine cha lazima sana tunachokipata katika Waraka wa Yoane. 

Yoane 3: 14, 15, 16   Mwenye kuzungumuza ni Yesu Kristo.

“Na kama Musa alivyonyanyua nyoka jangwani, vivyo hivyo sharti Mwana wa watu anyanyuliwe, ili kila mtu akimwamini asipotee, lakini awe na uzima wa milele. 

Kwa maana Mungu alivyopenda ulimwengu, hata kutoa Mwana wake wa pekee, ili kila mtu akimwamini asipotee, lakini apate uzima wa milele.” 

Aya hii inatangulia aya inayojulikana na watu wote katika Biblia Yoane 3: 16 Mfano huu wa Musa akinyanyua nyoka jangwani inamaanisha  kawaida ya mafundisho juu ya wokovu kwa imani, kwa njia ya kuamini tu.  


16/ Wana wa Israeli walifanya safari ndefu toka Bahari Nyekundu hadi mpaka wa Edoni, njia hii ndefu iliwachokesha mno, wakaanza kunungunikia Musa na Mungu, Mwenyezi Mungu akawatumia nyoka wakali na wenye sumu mbaya, wakauma watu wengi na wengi kati ya watu wakafa. 

Watu katika hali ya kujuta na kutubu  na kutambuwa zambi na makosa yao wakamjia Musa  wakimuomba awaombee huruma kwa Mwenyezi Mungu, Musa akawaombea kwa Mungu, na Mwenyezi Mungu akajibu kwa njia yenye kuwa kweli kama ya mtu mwenye akili yake siyo timamu. 

Kwa sababu Mungu alimwambia Musa ajenge nyoka ya shaba, na aiinue kwa muti, na mambo yatatendeka kama ifwatao: 

Kila mtu atakaye umwa na nyoka, na atakaye inua mecho yake na kuangalia nyoka ya shaba, ataponyeshwa.  


17/ Tupate fundisho kwa jambo lile: 

Neno la kwanza ni kwamba hakuna mtu aliyeambiwa ajenge dawa. 

Hakuna yule aliyeombwa kutokotesha hata dawa fulani ya majani. 

Ama kujipakaa mafuta fulani. 

Hawakupashwa kupigwa hata shindano fulani. 

Hawakupashwa kufanya hata neno moja. 

Walipashwa kuacha mbali dawa yote itakayotoka nyumbani mwao na kutumainia tu kwa dawa kutoka kwa Mungu. 

Wanadamu waliumwa na nyoka ya zambi. 

Wataponeshwa namna gani na hiyo kidonda? 

Ni kifo tu kinachowangojea wakiwa na kidonda chao, isipokuwa Mwenyezi Mungu mwenyewe awape dawa. 


18/ Tena katika hiyo jangwa, watu hawakuambiwa wajisaidiye wao kwa wao, waliombwa tu kuinua macho yao kuangalia nyoka iliyonyanyuliwa juu ya muti. 

Kwa siku zetu za leo, kungeliundwa mashirika ya kibinadamu na kuandikisha watu wengi watakaojitowa kwa kusaidiya wale walioumwa na nyoka, lakini Mwenyezi Mungu hakuwaambia watu wasaidiane wao kwa wao. 

Hawakutumwa kuunda mashirika ya masaidio ya kijamii, HAPANA, waliambiwa tu kutazama nyoka ya shaba.  


19/ Neno la tatu ni kwamba: 

Haikuombwa kwa watu walioumwa na nyoka kupigana na nyoka. HAPANA. 

Iliwapasa tu kuinua mecho yao kutizama nyoka ya shaba. 


20/ Jambo la ine ni kwamba: 

Watu waliokuwa kwa mipaka ya Edoni, baada ya kuumwa na nyoka, wao hawakuombwa kuanza kuelekeza maombi yao kwa nyoka. 

Sisi hatuombwi kuomba tukielekeza maombi yetu kwa nyoka ya shaba iliyo inuliwa, tena kabisa haiombwi kwa mwenye zambi kuomba kuhusu wokovu wake. 

Kristo alikufa ili alete wokovu, yafaa tu kuamini, hapana kuomba kuhusu wokovu. 


21/ Neno la tano: 

Mwenyezi Mungu hakuwaambia wajitenge na yale nyoka ama wa wabebe inje na kuwauwa wote. Mungu hakuondosha yale nyoka. 

Mwenyezi Mungu aliwapa dawa katika hali ileile na Katika mtanziko huo, na dawa hiyo ilitolewa tu kwao, na ilikuwa kuinua mecho na kuangalia tu nyoka wa shaba aliyeinuliwa juu ya muti.  

Mwatambua, hakuna lengo la kujisifu. 

Wale watu wa wakati wa Musa, mbele ya hizo nyoka, hawakuwa na neno lenye linaloweza kuwasukuma kujisifu. 

Mungu anachukizwa na kiburi. 

Jameni basi wapi tena kujisifu? 

Mwenyezi Mungu hafurahishwi na neno kama yale.  


22/ Kuna aya moja ya manufaa kabisa ndani ya Maandiko ya Yeremia 9: 23 

“Bwana anasema hivi: Mwenye akili asijisifu kwa sababu ya akili yake, wala mwenye nguvu asijisifu kwa sababu ya nguvu zake, wala tajiri asijisifu kwa sababu ya utajiri wake;” 

Kama tunavyo tambuwa inasemwa hapa kwamba watu wasijisifu, lakini umbalimbali na ile, watu wanajisifu siku kwa siku. 

Mwenye hekima asijisifu juu ya hekima yake, kwa sababu hekima ya mwanadamu ni nini? 

Kitambo kidogo inatoweka nayo haikuleta hata surulisho ya mambo mengi. 

Mutu mwenye nguvu asijisifu kwa sababu ya nguvu zake, tumekwisha kuona mara nyingi watu wenye nguvu kupigwa sana. 

Hatupashwi kujisifu juu ya nguvu yetu. Hatupashwi pia kujisifu juu ya utajiri wetu, lakini kwa kweli watu wanajisifu lakini ningelipenda mukumbuke mwaka wa njaa ya 1923, ilikuwa mwaka mugumu sana, sasa hapo kujisifu kulikuwa wapi? Kuliondoshwa. 

Kazi yote ya wokovu ni kazi ya yeye mwenyewe Mwenyezi Mungu, ni Yeye pekee aliye Mwenye Haki na ni Yeye pekee anayehesabia Haki. 

 AMINA    

N°Ref: 10/14/1962/ 249 - WHAT GOD THINKS OF YOUR RELIGIOUS PRIDE / 07/30/2021       

Sunday, July 18, 2021

JE MAPENDO YA KWELI NI KIPOFU? / IS TRUE LOVE BLIND?

Photo by B Smith from the patio




JE MAPENDO YA KWELI NI KIPOFU? 

IS TRUE LOVE BLIND?

January 23, 1977 

Pastor Henry F. Kulp


 

Wakolosayi 1: 1 – 8 

“Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na Timoteo ndugu yetu, kwa watakatifu na ndugu waaminifu katika Kristo walio katika Kolosayi: Neema iwe kwenu na salama toka Mungu Baba yetu. 

Tunashukuru Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo, tukiwaombea ninyi siku zote, tukiwa tumesikia  habari za imani yenu katika Kristo Yesu, na za mapendo muliyo nayo kwa watakatifu wote, kwa sababu ya tumaini mulilowekewa akiba mbinguni, habari zake mulizosikia zamani katika neno la kweli ya Habari Njema, iliyofika kwenu; kama ni vile katika ulimwengu wote ikizaa matunda na kukua kama inavyokua ndani yenu vilevile, tangu siku muliposikia na kujua neema ya Mungu katika kweli; kama vile mulivyofundishwa na Epafra, mjoli wetu mpenzi, aliye mtumishi mwaminifu wa Kristo kwa ajili yetu, ambaye alituambia vilevile habari za mapendo yenu katika Roho.” 

Tunapewa salamu za Mtume Paulo katika aya ya 1 na ya 2

Anawasiliana nao kama watakatifu na ndugu waaminifu katika KRISTO. 

Neno kubwa katika Wakolosayi ni UTIMILIFU

Na sisi ni utimilifu wake. Tulipokea Utimilifu wake.   


1/ Tangu aya ya 3 mpaka aya ya 5, ni masemi ya shukrani ya Mtume Paulo. Mtume Paulo anashukuru. 

Tunashukuru Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo, tukiwaombea ninyi siku zote.  Mtume Paulo anashukuru kwa niaba yao. Anashukuru Mungu kwa ajili yao. 

Hapa, neno kuwaombea ni ya kuvutia sana. 

PROSS – U – KUH – MY, eti unafahamu kwamba neno PROSS inamaanisha uso kwa uso na Mwenyezi Mungu. 

Upendeleo gani tunayo, bado tukiwa hapa duniani, ijapokuwa hata hatumuoni Mwenyezi Mungu, lakini tunamukaribia uso kwa uso tukimuletea malalamiko yetu. 

U – KUH – WRIST – O na katikati ya neno hili, tunapata neno KAR – RIS inayomaanisha NEEMA.    

Kwa kumaanisha kwamba tunashukuru kwa hayo yote tunayopata bila kustahili. 


2/ Ni mafaa kwetu kujuwa kwamba maombi yetu twayaelekeza kwa Baba  Mungu. Hakuta kuwa kamwe kinyume ya hiyo. 

Wakati unaposikia mtu akiomba “Yesu wangu…”, bila shaka iyo unayosikiliza ni  uasi, na Mwenyezi Mungu hatajibu maombi yale. 

Vivyo hivyo, kama ukisikia mtu anaomba kwa Roho Mtakatifu, kweli hiyo  unayosikia ni uasi, Mwenyezi Mungu hata jibu maombi yale, mushike haya kwa makini sana, wakati muombapo, maombi yenu yaelekezwe kwa Mungu Baba.  


3/ Tupate mwangaza kwa mafikili yetu toka sura moja kubwa ya Biblia inayohusu maombi.  

Waroma 8: 26 

“Hivi Roho anasaidia uzaifu wetu: kwa maana hatujui kuomba kitu namna inavyotupasa, lakini Roho mwenyewe anatuombea kwa kuugua kusikoweza kusemwa;” 

Twaona hapa kwamba Roho Mtakatifu anayefanya makao ndani yetu anatuombea kwa Mungu Baba, akitusaidia katika maombi yetu. 

Pia Aya ya 34 inasema:  

“ni nani anayehukumu? Ndiye Kristo aliyekufa, ndiyo, zaidi, amefufuka, naye yuko kwa mkono wa kuume wa Mungu, tena ndiye anayetuombea.” 

Twaona hapa, Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, huko mbinguni akiomba kwa Mungu Baba kwa ajili yetu. Ni neno hili ndilo twapasha tarajia, hatuwezi fanya zaidi ya hayo. 


4/ Kwenu ninyi, PEAR – EE, inayomaanisha, yenye kuwahusu. 

Kumbukeni kwamba yeye alikuwa bado hajakutana nawo, ama haja waona bado, lakini alikuwa akiwaombea. 

Eti, yawezekana mimi niombee mtu mwenye sijaona bado? 

Kwa kweli yawezekana.  


5/ Tuhakikishe kwamba Mtume Paulo anasema ya kwamba watu hawa walikuwa na Neema ya kuwa na vitu tatu maalum: 

Mambo matatu: Imani, Mapendo, na Matumaini.


(1)  Imani katika KRISTO YESU. 

(2)  Mapendo tunayo kwa watakatifu wote. 

(3)  Matumaini tunayo kuhusu mbinguni. 


6/ Imani katika KRISTO YESU. 

Tusome Wakolosayi 2: 5  

“Maana hata nikiwa mbali katika mwili, mimi ni pamoja nanyi katika roho, nikifurahia na kutazama utaratibu wenu na uaminifu wa imani yenu katika Kristo.” 

Hapa inahusu uaminifu wa imani yao katika Kristo.

 Neno imani, inamaanisha uaminifu ya uhakika.  

Wao wanakuwa na uaminifu wa uhakika ya kumsadiki Bwana Yesu Kristo.

Waweza kuwa na imani kwa jambo fulani, ama hapana.

 Wengi wanamjua Bwana Yesu Kristo kama Mwokozi, kama Mwenye aliyechukuwa zambi zao, lakini hawana uhusiliano wa urafiki pamaoja naye, hawamjui kama rafiki wa kweli na wa ndani. 

Hawatembei na Bwana Yesu Kristo katika mwendo wao wa kila siku. 

Kwa kuwa na Salama, yafaa kumjua Bwana Yesu Kristo na kutembea naye daima siku zote. 


7/ Ni lazima kwetu tufahamu kwamba imani ni jambo la hatari sana katika ulimwengu. 

Kama imani yetu tukiiweka ndani ya kitu kibaya, jambo hili litazorotesha maisha yetu, litatuharibu hata kufikia kiwango cha kutuuwa. 

Kuna mwanamemba wa kanisa letu la fasi mwenye kwa siku za leo alisafiri mbali sana na nikule anaishi kwa sasa, bali, kwa wakati alipokuwa akiishi pamoja nasi, siku moja alipenda kuunguza majani katika kiwanza chake, na hapo mavazi yake yakapata moto na kuunguwa na yeye vilevile mwili wake uliunguwa vikali sana na hapo hapo akapelekwa kwa haraka kwenye hospitali, kule wakamutibu na peniceline yenye kwa siku za mbele haikuwa inatunza hata mwili wake na hiyo ilitaka kumupeleka kwa kifo. 

Yafaa kuwa na Imani katika jambo lililo aminifu. 


8/ Wagalatia 3: 26 

“maana ninyi wote ni wana wa Mungu, kwa imani, katika Yesu Kristo.” 

Ninyi wote mumekuwa watoto wa Mungu waliokomaa kwa imani katika Kristo Yesu

Tuone sasa neema ya pili waliokuwa nayo: Mapendo.  

Ni neno moja katika Swahili inayotumiwa kwa namna mbalimbali ya mapendo. 

Mapendo kwa Mwenyezi Mungu, mapendo kwa watoto, mapendo kwa wazazi, mapendo kwa marafiki. 

Watu wengi wanaita tendo la ndoa, kufanya mapendo, Neno la Kigriki ni mapendo kati ya ngono. Na kweli yaweza tu kuwa shauku. 

Ni mapendo ya uchoyo, mambo yote yakifwata tu njia moja. Haitumikishwi hata mara moja katika Agano Jipya. 


9/ Baadaye tuna neno la Kigriki PHIL - LET - O kwenye  tunapata undugu wa filadelfia, undugu,  na hii inamaanisha mapendano na hii njo maana ya msingi ya neno: urafiki


10/ Neno lililotumikishwa hapa ni AH - GOP – A, Mungu ni Pendo


(1) Ni neno linalotumikishwa kati ya Mungu Baba na Mwana wake. 

Yoane 17: 26 

“Nami niliwajulisha jina lako, nitalijulisha; hata mapendo ambayo ulinipenda mimi yawe ndani yao, nami ndani yao.”  


(2) Ni neno linalotumiwa kwa kuonesha Mapendo ya Mungu Baba kwa ulimwengu. 

Yoane 3: 16 

“Kwa maana Mungu alivyopenda ulimwengu, hata kutoa Mwana wake wa pekee, ili kila mtu akimwamini asipotee, lakini apate uzima wa milele.” 

Yoane 16: 27  

“Kwa maana Baba mwenyewe anawapenda ninyi, kwa sababu ninyi mumenipenda mimi, na kuamini ya kwamba nilitoka kwa Mungu.” 

Tunasoma ya kwamba: Baba mwenyewe anawapenda ninyi, kwa sababu ninyi mumenipenda mimi. 


11/ Kwa kufikia kiwango cha kupenda na haya mapendo, yafaa Roho Mtakatifu atawale na kuongoza maisha yako. 


12/ Kwa siku iliyopita, wengi wenu hawakunisadiki wakati niliposema kwamba yapashwa muwe na imani kwa Mungu, hapana kuwa na imani ndani ya watakatifu, bali yafaa kuwapenda. 

Na hii ni kweli kwa sababu hakuna hata moja kati ya wanaadamu aliye mkamilifu katika njia zake zote, ili mufikie kiwango cha kufahamu kwamba: MAPENDO SI KIPOFU. 

1Wakorinto 13: 6 

“hayafurahi kwa uzalimu, lakini yanafurahi pamoja  na kweli:” 

Mapendo yanafurahi pamoja na kweli. 

Eti upendo waweza kufwatana na namna mtu tunaye mpenda ni mkamilifu? 

Eti twaweza kukoma kupenda watu sababu walifanya makosa, ama walitenda uzalimu? 

Kama ingelikuwa namna sawa, hatungimpenda hata mtu mmoja. 

Sote tunaye kweli huyo mtu wa zamani anayetuvutia kutenda zambi na makosa, eti jambo lile lasukuma waamini wengine wasitupende? 

Mapendo yenye inaweza kukomeshwa na ukweli wa mambo siyo mapendo ya namna ya Mungu. 

Twapashwa kufanana Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, aliyetupenda si kwa ajili ya matunda ya matendo yetu mazuri, lakini hata ivyo alitupenda. 

Waroma 5: 8  

“Lakini Mungu anaonesha mapendo yake kwetu, wakati tulipokuwa tungali wenye zambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.” 

1Yoane 4: 19  

“Sisi tunapenda kwa maana yeye alitupenda sisi kwanza.” 


13/ Watu wengine wanakuwa sawa wenye wazimu, wao hawaoni hata kasoro yeyote ndani ya mtu wanao shuhudia  kumpenda. 

 Wababa na wamama wengine wanawapenda watoto wao hata kufika kiwango cha kufanya kuwa sawa hawaoni makosa na hisia za watoto wao na hii inawafanya watoto kuwa wakosa adabu na wenye wasio kuwa na maono sambamba kuhusu maisha ya kesho.  

Mapendo ya kweli kwa mwamini ni ile inayomuruhusu kujuwa ukweli wote kuhusu mtu anayempenda na hiyo ukweli haitamuvunja roho ama kumukata tamaa.  


14/ Tuchunguze sasa neema ya tatu: Tumaini 

Tumaini la baraka tunalowekewa akiba mbinguni.

Tumaini lilo tunalipata katika Tito 2: 13 

“tukitazamia tumaini la Baraka na kuonekana kwa utukufu wa Mungu mkubwa, Mwokozi wetu Yesu Kristo:” 

Waamini wote wangepewa tumaini hili la baraka toka Mungu wetu.


15/ Msingi wa huu tumaini tunaupata katika 1Timoteo 1: 1 

“Paulo mtume wa Kristo Yesu, kwa agizo la Mungu Mwokozi wetu na la Kristo Yesu taraja letu;”  

Yesu Kristo ni taraja letu. 


16/ Ndani ya Tumaini muna jambo tatu: 


(1) Hamu  

Hatuwezi kuwa na tumaini ikiwa hatutamani jambo tunalotumainia litimilike.

Tumaini siyo tu hamu, sababu tunaweza kuwa na hamu ya jambo lenye hatutarajie. 


(2) Matarajio 

Tena kabisa matarajio siyo kabisa tumaini, kwa sababu tunaweza kutakia jambo lenye hatupashwi kutakia. 

Yatupasa kuchanga hamu na matarajio. 


(3) Uvumilivu 

Twapashwa kuwa na uvumilivu kuhusu hamu na matarajio yetu. 


17/ Ni muhimu sana tufahamu kwamba kuna tofauti na umbalimbali kati ya Tumaini la wa Israeli na Tumaini la waamini wa siku za leo. 

Tuchunguze tofauti hizo kwa makini kabisa: 


(1) Tumaini la Israeli ni la Duniani. 


(2) Tumaini letu ni la Mbinguni


(3) Katika tumaini la Israeli, KRISTO ni Mwana wa Mtu, Mwana wa Daudi, na Mwana wa Abrahamu. 


(4) Katika tumaini letu KRISTO ni Mwana wa Mungu, KRISTO ni Kichwa cha Mwili. 


(5) Tumaini la Israeli ni kuhusu kuja kwa KRISTO hapa duniani. 


(6) Tumaini letu ni kuhusu kuchukuliwa kwetu na KRISTO na kumulaki hewani. 


(7) Tumaini la Israeli litatimilika kiisha hukumu mkubwa na mateso makuu hapa duniani. 


(8) Tumaini letu litatimilika mbele ya hukumu na mateso hapa duniani. 


18/ 1 Wakorinto 13: 13 

“Basi, sasa inadumu imani, tumaini, mapendo, hizi tatu; lakini neno kubwa katikati ya maneno haya ni mapendo.”  

Kati ya hizo neema tatu ni moja tu inayodumu nayo ni mapendo. 

Siku moja imani na tumaini zitakoma, bali mapendo itakuwa kwa milele. 


AMINA. 


N°Ref: 01/23/1977 / 335-2 IS TRUE LOVE BLIND / 07/18/2021

SHULE LA HEKIMA / THE SCHOOL OF WISDOM

Photo by B Smith from the kitchen door (Rare Whistling Ducks)


 


SHULE LA HEKIMA 

THE SCHOOL OF WISDOM

June 1, 1980 

Pastor  Henry F. Kulp


 

Mezali 2: 1 - 5  

“Mwana wangu, kama ukikubali maneno yangu, Na kuweka akiba maagizo yangu ndani yako; Halafu utatega sikio lako kusikia hekima, Na kutia moyo wako kwa ufahamu; Ndiyo, kama ukiita akili, 

Na kupaza sauti yako kwa ufahamu; Kama ukiutafuta kama feza, Na kuutafutatafuta kama hazina zilizofichwa; Halafu utafahamu woga wa BWANA, Na kupata maarifa kwa Mungu.” 

Hapa, tunayo shule la hekima. 

Katika Sura ya mwisho, sehemu ya mwisho wake, twaona kwamba, inje ya desturi za dini nyakati zile, hekima inawasihi, kwa mkazo na sauti kubwa, vijana wa Taifa la Israeli. 

Hekima ikiwapa wote angalisho kuhusu vinyume vitakavyo tokeya kama wanatupilia mbali hekima. 

1/ Wakati mashindano na majaribu ya maisha yanatukia, yote yale hayawezi kukupatia hekima kwa muda huo muchache, kwa sababu hekima ni kumujuwa Mwenyezi Mungu, tokeo la Neno la Mungu pamoja na kumucha Mungu. 

Na kuwa na ufahamu kuhusu Mungu haipatikani kwa rafla. 

Hii ni jambo linalotukumba hatuwa kwa hatuwa, ni tunda la kukusanya. 

Kwa kweli, ufahamu bila kumucha Mungu ama woga wa Bwana, yaweza kuwa bila mafaa yeyote. 

Imetupasa kuwa na ufahamu na woga wa Bwana, yote miwili itembee pamoja ili tuwe na hekima. 


2/ Yobu 28: 12  

“Fezaluka wala bilau havitatajwa: Ndiyo, bei ya hekima inapita vito vyekundu vya damani.” 

Bei ya hekima inapita vito vyekundu vya damani. 

Nikusema kwamba vifaa na hazina tunayo hayawezi kamwe kukamata nafasi ya hekima. 

Haijali kiwango gani cha hazina unayo, hekima inasamani kupita na ni ya mafaa sana. 

Kwa hiyo, mtu anaweza kuwa na utajiri nyingi, lakini kama hana hekima, mtu huyu anaweza kupokonya mali yake kwa muda kitambo tu na baadaye kujikuta hana tena kitu. 

YATUPASA KUTAMANI SANA HEKIMA. 

Mezali 4: 7  

“Hekima ni kitu cha kwanza; basi  ujipatie hekima: 

Ndiyo, pamoja na yote uliyopata pata ufahamu.” 

Tunasoma hapa kwamba hekima ni kitu maalum sana na ni ya msingi, kwa hiyo pata hekima, na pamoja na yote uliyopata pata ufahamu. 

Twapashwa kutamani sana hekima, lakini ni waamini wachache tu wanayokuwa na hekima.  


3/ Zaburi 119: 98, 99  

“Maagizo yako yananitia hekima kuliko adui zangu; Maana ni pamoja nami siku zote. 

Nina ufahamu kupita walimu wangu wote; Maana shuhuda zako ninazifikiri.”  

Hapa mtu moja maarufu anatujulisha kwamba chemchemi ya hekima yake ni katika ufahamu wa Neno la Mungu. 

Kwa sababu kwa aya ya 98 anasema: 

Maagizo yako yananitia hekima kuliko adui zangu, na yeye ni mwenye kumcha Mungu. 

Na kwa aya ya 99, anasema: 

Nina ufahamu kupita walimu wangu wote; shuhuda zako ninazifikiri. 

Nikusema kwamba walimu wake walikuwa na ufahamu lakini hawakukuwa na hekima. 

Walichunga mambo mengi katika vichwa vyao, bali hawakuwa na woga wa Bwana. 


4/ Yakobo 1: 5 

“Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na akili, aombe Mungu, anayewapa wote kwa ukarimu, pasipo kuhamakia; naye atapewa.” 

Mtume Yakobo asema kwamba: 

Kama mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, sikiliza kwa makini inayosemwa hapa: Omba Mungu, usiombe kwa mtu. 

Usiombe kwa walimu. 

Omba kwa Mwenyezi Mungu kwa maana hekima ya kweli inatoka kwa Mungu. 

Wanadamu waweza kukupatia mashauri mazuri, kiisha punde kidogo wanashindwa kukushauri. 

Kama si wenye kuokolewa, mashauri yao yawezakuwa mabaya, lakini hata watu waliookoka wanaweza kuwa na mashauri mabaya vile vile, kwa sababu, mambo yote ya waamini hayakamiliki kwa kila hali, bali ni Neno la Mungu pekee lililo kamilifu na lenyi haki daima. 


5/ Mezali 3: 5    

“Tumainia Bwana kwa moyo wako wote, wala usitegemee ufahamu wako mwenyewe:” 

Twasoma hapa: Tumainia Bwana kwa moyo wako wote, wala usitegemee akili yako mwenyewe. 

Ni kusema: Umuombe Mungu, usijiombe mwenyewe, wala kutafuta kujua kiini ya mambo wewe mwenyewe. 

Umuombe Mwenyezi Mungu hekima, nikusema kimbilia kwenye Neno la Mungu. 


6/ Kwa kweli hii ndiyo maana ya maombi.  

Omba kwa Mungu. 

Katika mashauri mengi kuhusu maombi tunayoyapata katika kitabu cha Yakobo, 

Hili ndilo la kwanza. 

Bali, Maombi pekee yatosha? 

Kuomba Mungu bila jambo lingine? Hapana. 

Kwa njia gani Mwenyezi Mungu hujibu maombi yetu kama tukimuomba hekima? 

Ni kwa njia tu la Neno la Mungu. 

Mwenyezi Mungu hatumii njia nyingine kwa kuzungumuza nasi, kama siyo tu kwa njia ya Neno la Mungu. 

Waweza kujiuliza: Eti Mwenyezi Mungu hutumia pia mazingira na  matukio mbalimbali yanayotutokea maishani mwetu? 

Kwa kweli yanawezekana, bali yale mazingira na matukio yote yanapashwa kuambatana na Neno la Mungu, yakifuata Kawaida ya Mafundisho ya Biblia Takatifu. 


7/ Tufahamu ya kwamba Mwenyezi Mungu ni, mwenye kupenda kutoa. 

Yeye ni Mtoaji Mkubwa, na Toleo lake ni la bure bila malipo yoyote. 

Ni Yeye atupae chakula chetu cha kila siku, ni Yeye anaye tuvika na kutupatia manufaa yote yanayotufaa. 


8/ Siyo tu kwamba Mwenyezi Mungu anatoa, lakini Yeye utowa kwa ukarimu wote. 

Waefeso 1: 3 

“Abarikiwe Mungu na Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye alitubariki kwa baraka zote za roho katika pahali pa mbingu ndani ya Kristo;” 

Tutambue hapa: Mwenyezi Mungu anatoa kwa ukarimu. 

Alitubariki kwa baraka zote za roho, siyo kwa baraka nyingi, ama karibuni baraka nyingi, lakini baraka zote, na tunayapokea bure bila malipo wakati tunapo okoka.  


9/ Yakobo 3: 15  

“Akili hii haitoki juu, lakini ni ya dunia, na ya tamaa, na ya Shetani.”

Hii ni aya ingine ya manufaa sana katika majifunzo yetu kuhusu hekima. 

Aya hii inaanza na: 

Hekima hii haitoki juu.  

Siyo hekima toka kwa Mungu. Ni hekima isiyotoka kwa Mwenyezi Mungu. 

Tukiilinganisha na aya ya 17. Kuna jambo moja tofauti: 

Aya ya 17  

“Lakini akili inayotoka juu, kwanza ni safi, tena ni ya salama, na upole, tayari kusikiliza maneno ya watu, imejaa rehema na matunda mema, pasipo fitina, pasipo udanganyifu.” 

Twatambua hapo kwamba kuna aina tatu ya hekima. 

Kwanza kuna hekima itokayo juu. 

Kiisha kuna hekima isiyotoka juu, na kwa mwisho kuna hekima ya kimtu. 

Tuchunguze sasa aya ya 15. 

Aya ya 15 

“Akili hii haitoki juu, lakini ni ya dunia, na ya tamaa, na ya Shetani.” 

Hekima isiyo toka juu. Ni hekima ya kidunia, ya tamaa, ya Shetani.

 Ya kidunia ni yenye kufurahisha ulimwengu.

China lake katika Kigriki ni neno GHEY inayomaanisha dunia. 

Kwa hiyo tu neno moja tunapata vile vile neno jiolojia inayoambatana na neno EPI katika Kigriki inayomaanisha YA KIDUNIA SANA ZAIDI, ni hekima inayopatikana katika Yakobo 3: 15. 

Hekima ya kidunia sana zaidi yatoka kwa mapepo ya mashetani. 

Neno la mwisho ni Shetani nalo linamaanisha yanayohusu mapepo wachafu. 

Ni hekima ya mapepo wachafu, na hii neno pepo wachafu inaandikwa kwa sarufi ya kuonesha uwingi. 

Kuna Shetani mmoja na wapepo wachafu wengi.

Wenye kujaa na mapepo wachafu ni wale wenye wanakuwa na hekima ya namna ile. 

Ebu tuchunguze kwanza neno EPI-GHEY. 

Tuangalie namna gani inatumikishwa nafasi nyingine.

Yoana 3: 12 

“Kama nimewaambia ninyi maneno ya dunia na hamuyaamini, mutaamini namna gani kama nikiwaambia ninyi maneno ya mbingu?” 

Bwana Yesu Kristo alimwambia Nikodemu, kwamba: nimekuambia kuhusu maneno ya dunia na haukuniamini, utaamini namna gani kama nikikuambia maneno ya mbinguni? 

Neno  katika Kigriki EPI-GHEY inamaanisha ya kidunia, ya kidunia zaidi, ya hali ya ufalme wa ulimwengu. 

Aliwaambia wawe na haki inayopita haki ya mafarisayo na waandishi, na akawaambia: kama ninawaamia ninyi maneno haya ya kidunia zaidi na ninyi hamuyaamini, mutaamini namna gani kama nikiwaambia ninyi maneno ya mbingu?  


10/ Twakuta mara tena neno hili katika Wafilipi 3: 17 – 19 

“Ndugu zangu, munifuate na mutazame wao wanaotembea kwa kufuata mfano tuliowapa ninyi. 

Maana watu wengi wanatembea, juu yao niliwaambia ninyi mara nyingi, na sasa ninawaambia ninyi hata kwa machozi, ya kuwa wao ni adui za musalaba wa Kristo; 

Mwisho wao ni uharibifu, mungu wao ni tumbo, utukufu wao ni haya yao, wanaofikiri maneno ya dunia.” 

Anasema kuhusu wale walio adui wa Musalaba wa Kristo, wale ambao mwisho wao ni uharibifu, mungu wao ni tumbo zao, na utukufu wao ni haya yao, wanaofikiri maneno ya kidunia zaidi. 

Wanapenda na kutafuta mambo yanayokuwa juu ya yale ya kawaida ya kidunia. 

Watu hawa, katika dunia hii ya sasa, hasa kwa upande wa watu wa dini, wanakuwa wengi sana. 


11/ 1 Wakorinto 1: 21 

“Kwa sababu katika akili ya Mungu, dunia katika akili yake yenyewe haikujua Mungu, ilipendeza Mungu kwa upumbavu wa neno linalohubiriwa kuwaokoa wanaoamini.” 

Twaona hapa hekima ya kimtu, tunasikia hapa kwamba dunia katika hekima yake yenyewe haikujua Mungu.  

1Wakorinto 3: 19  

“Kwa sababu akili ya dunia hii ni upumbavu mbele ya Mungu. 

Kwa sababu imeandikwa: Anakamata wenye akili katika hila yao;”  

Hakuna budi kutarajia  wingi wa hekima. 


12/ Hekima ya kweli yatoka juu. 

Yakobo 1: 17  

“Kila zawadi njema, na kila zawadi timilifu inatoka juu, inashuka kwa Baba ya nuru kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeukageuka.” 

Hekima hiyo siyo ya mtu kawaida, mwenye kuambatana na mtu wake wa zamani. Hekima hiyo inatoka kwa Mungu, inatoka juu.  


Kuna mfano mmoja tunaopata tukiangaziwa na Maandiko ya Matendo ya Mitume 6: 10 

“Lakini hawakuweza kushindana na hekima yake wala na Roho Mtakatifu aliyesema naye.” 

Hapa ni kuhusu Stefano. 

Hawakuweza kamwe kushindana na Hekima ya Roho aliyekuwa akiongoza Stefano kwa kuzungumuza.

Ikiwa nasi vile vile twatamani kuwa na hiyo hekima, twaweza kuipata kutoka kwenye Stefano alipoipata. Toka juu. 


13/ Hiyo hekima toka juu ina tabia nane. 

Tuzitaje moja kwa moja: 

Kwanza, hekima toka juu ni safi. 

Tukio la kwanza la hekima ni usafi, mtu mchafu hata awe na akili kwa mambo mengine, hawezi kuwa na hekima. 

Usafi unachina lake kwenye ufahamu  kichwani, hii ni jambo maalum kweli, ni kwa hiyo mawazo yetu yanapokuwa safi, mafikiri machafu hayapati mahali pa kukaa katika ufahamu wetu. 

Neno hili linatuhusu sote, hatupashwi kuweka mawazo machafu katika mafikiri yetu. 


14/ TABIA MCHAFU 

Wakristo wanapashwa kutupa mbali tabia za namna sawa. 

Kwa hiyo haifai kwa wakristo kuingia katika nyumba ya wageni ama bweni la vinywaji vya kuchacha, vyenye hawapashwi kutumia kwa uwingi ama kwa kukadirisha. Yafaa kujitenga mbali nayo. Nafasi hizo haziongeze hata neno moja kwa usafi.  

Wajibu wetu ni kujiacha wenyewe kuishi siku kwa siku katika utamaduni wa kikristo, hii ibebe sehemu kubwa sana ya maisha yetu. 


15/ LENGO NA MAKUSUDI SAFI. 

Hii ni kiini kinachotusukuma kutenda tendo. 

Tusisukumwe na makusudi ya kujipenda wenyewe, 

Hapana kwa sifa yetu wenyewe, ila kwa kumusifu na kumutukuza Bwana wetu Yesu Kristo. 

1 Timoteo 5: 25 

“Vivyo hivyo matendo mazuri yanaonekana wazi; na yale yasiyoonekana, hayawezi kufichwa.” 

Mtume Paulo, anapoandikia Timoteo, anamusihii kuwa na mwenedo mwema akijichunga katika usafi wa kiroho. 


16/ SALAMA 

Hii ni tabia ama hali ya pili ya hekima. 

Kama mtu mwanamume ama mwanamke ni mugonvi, huyu mtu haoneshi hekima kutoka juu. 

Watu wa namna hii walikuwa wengi katika makanisa ya Wayuda hapo kale, walikua na ushujaa na bidii mbaya, kila mtu akipendelea kujiweka wa kwanza na wa faida kuliko mwenzake, na hii ilileta machafuko na uvuguvugu pahali pa salama. 

Mtu wa salama atafanya yote iwezekanavyo ili avunje uadui, vikwazo, nakujitia mbali na vita na mabishano.  


17/ MPOLE 

2 Wakorinto 10: 1 

“Nami Paulo mwenyewe, ninawasihi ninyi kwa unyenyekevu na upole wa Kristo, mimi niliye mnyenyekevu wakati mimi ni pamoja nanyi, lakini nisipokuwa mimi ni mwenye uhodari kwenu:” 

Ninawasihi ninyi kwa unyenyekevu na upole wa Kristo. 

Ni upole wa namna gani, Bwana wetu Yesu Kristo alikuwa nawo mbele ya Nikodemu, na vile vile mbele ya mwanamuke musamaria mbele ya kisima. 

Bwana Yesu hakuwa mgumu kwa mtu yeyote, ila tu kwa wale mafarisayo katika dini. 

Mtume Paulo vile vile alikuwa mpole. 

1Watesalonika 2: 7 

“Lakini tulikuwa wapole katikati yenu kama mlezi anayetunza watoto wake mwenyewe;” 

Angaliweza kuandika: 

Tulikuwa wapole katikati yenu sawasawa vile mlezi anavyotunza watoto wake mwenyewe. 

2Timoteo 2: 24 

“Na haipasi mtumwa wa Bwana kugombana, lakini kuwa mpole kwa watu wote, anayeweza kufundisha, mvumilivu,”  


18/ MWENYE KUJAA HURUMA 

Ni vema sana kuwa mwenye kuhurumia, lakini, siyo rahisi kuwa mwenye huruma. 

Kuhurumia, sawa vile tunaweza kuwafahamisha, siyo kumurudishia mwengine yale aliyostahili kweli. 

Hii nikusema kwamba wajirani wanaotizama wanaweza kuhitaji wewe uwatendee wale watu kwa ukali na hasira sana ukiwarudishia kisasi, sawa vile wanavyostahili, lakini wewe huwatendei kama vile walivyostahili. 

Umejaa na huruma. 


19/ MATUNDA MEMA.

Neno kujaa inahusu matunda mema na vile vile huruma.  

Na kwa kweli ni mara moja. 

Wagalatia 5: 22, 23 

“Lakini matunda ya Roho ni mapendo, furaha, salama, uvumilivu, neema, wema, uaminifu, 

Upole, kujizuiza; hakuna sheria juu ya maneno ya namna hii.” 

Matunda ya Roho ni mapendo. 


20/ BILA UPENDELEO 

Mtu anayekuwa na hekima toka juu, makusudi yake ni safi, na bila ubaguzi.  

Hatafanya ubaguzi wa kupendelea  mtu moja kati ya kundi. 

Hata baguwa wengine na kupendelea tu wale walio na mali, ama wale walio na ranga ya maisha ya juu kuliko, ama wale wanaojulikana. 

Mtu wa hekima hatakuwa yule anayefanya ubaguzi wa majina akiyaita moja moja kufwatana na wale anaowajuwa kwamba ni wenye kujulikana, akihusika na kuzungumuza tu na wale.  


21/ BILA UNAFIKI 

Mara nyingi tunazani kwamba munafiki ni mtu yule anayejifanya kuwa mukristo na japo yeye hayupo mukristo. 

Yeye anafanya unafiki kwa ajili ya biashara yake ama ranga anayopenda kuwa nayo ili aheshimiwe na kujulikana. 

Ama ili awe mbele ya wengine, katika mambo kazaa.

Lakini, hata waamini wanaweza kuwa wanafiki. 

Kuna wakati waamini wanaweza hata kuhudumia kwa unafiki. 

Tukiwa hazarani, mbele ya watu wote, tunajifanya sawa tunampenda ndugu fulani ijapokuwa kwa kweli ndani ya roho yetu tunamuchukia kupita kiasi, hiyo ni unafiki. 

Tusiwe kama Yuda aliyemubusu Bwana Yesu Kristo na baadaye akamusaliti.  

Kuna wengine wanatenda na kusema sawa watu wakarimu ijapokuwa wao ni wachoyo wakijipenda wenyewe. 

Mtu mwenye hatendi kwa unafiki hawezi kujifanya kuwa mtu mwingine wa tabia isiyokuwa yake.

Unaweza kumwamini sababu anayoyasema ni kweli inayotoka rohoni mwake na hasemi uwongo. 


22/ Twatambua kwamba yatupasa kuwa na hekima toka juu.

Tutaipata kwa njia  ya Neno la Mungu pamoja na woga wa Bwana.  


23/ Neno lingine la muhimu lenye twapashwa kuona lapatikana ndani ya Sura ya pili.  

Mezali 2: 4, 5 

“Kama ukiutafuta kama feza, na kuutafutatafuta kama hazina zilizofichwa; 

Halafu utafahamu woga wa BWANA, na kupata maarifa kwa Mungu.” 

Ni kusema, ni jambo nguvu mno. Siyo rahisi, siye mambo ya wavivu. 

Siyo jambo la watu wanaokumbwa kwa urahisi. 

Kama unatamani kupata hekima, na kwa kweli ni jambo linalotamaniwa na watu wote, yakupasa kujitahidi kweli na kutoa jasho. 

Siyo jambo inayokuja kwa rafla. 

Siyo jambo wanaloweza kukukabizi kwa bure bila kazi yoyote. 

Wapashwa kuitafuta kwa njia ya Neno la Mungu kama mtu anayetafuta hazina zilizofichwa. 


24/ Aya ya 5  

“Halafu utafahamu woga wa BWANA, na kupata maarifa kwa Mungu.” 

Twatambua tena kwamba woga wa BWANA unakuja mbele ya kupata maarifa kwa Mungu. 

Kumjua Mungu haina mafaa kama mtu hamchi Mungu, kama mtu hatembei katika woga wa Bwana. Kumujua Mungu na kumcha Mungu yapashwa kutembea pamoja.   


25/ Tuchunguze yanayosemwa kwa aya ya 6. 

Aya ya 6 

“Maana BWANA anawapa watu hekima; 

Kinywani mwake zinatoka maarifa na ufahamu: “

Ni Mwenyezi Mungu anayetupa hekima tukiwa pia na woga wa Bwana, Kwa kumujua Mwenyezi Mungu kwa njia ya ufahamu tunayopata kwa kujikaza kuchunguza Maandiko Matakatifu kila mara kwa ufahamu, na kwa kufanya yote iwezekanao ili tulipokee Neno la Mungu. 


AMINA. 


N°Ref: 06/01/1980 / 548-2 THE SCHOOL OF WISDOM / 07/18/2021