Saturday, April 30, 2022

UTAFANANA NAMNA GANI KWA NYAKATI ITAKAO KUJA / HOW WILL YOU LOOK IN THE FUTURE




UTAFANANA NAMNA GANI KWA NYAKATI ITAKAO KUJA 

HOW WILL YOU LOOK IN THE FUTURE 

March 14, 1965

Pastor Henry F. Kulp 





 

Waroma 8: 17 – 19 

“na kama sisi, basi tu wariti: wariti wa Mungu na wariti pamoja na Kristo; kama tukiteswa pamoja naye, ili tutukuzwe pamoja naye vilevile. 

Kwa maana ninahesabu mateso ya wakati huu wa sasa kuwa si kitu tukiyafananisha na utukufu ule utakaofunuliwa kwetu. 

Kwa maana viumbe vyote vinangojea kwa hamu sana ufunuo wa wana wa Mungu.” 

         Hapa Mwenyezi Mungu anazungumuzia mwamini kama muriti pamoja na Kristo, sisi tutakuwa wariti pamoja na Kristo katika yote na ndani ya yote. 

Sisi si wariti tu, lakini sisi ni wariti pamoja na Kristo. 

Uriti wetu ndani ya Kristo hautagawanyika. 

Hauta gawanyika kamwe kwa sehemu mbalimbali na hii ni jambo maalum umbalimbali na kuwa mwanamemba wa ufalme wa hapa duniani kwenye urizi unagawanywa kwa sehemu.  


1/ Mwenyezi Mungu anasema tena kwamba:  

… kama tukiteswa pamoja naye, ili tutukuzwe pamoja naye vilevile. 

Kwa maana ninahesabu mateso ya wakati huu wa sasa kuwa si kitu tukiyafananisha na utukufu ule utakaofunuliwa kwetu.  

Kwa kweli kuna neno lisilo andikwa hapa, lakini lenye kufaa sana katika wazo hili, na  ni neno la muhimu sana katika maisha ya kikristo. 


2/ Mbele niwajulishe neno lile, nataka kwanza tufikiri kuhusu jambo moja. 

Kwa kweli, kuna wapagani kazaa wenye kutizama maisha ya wakristo na wanasema: 

Sina kitu cha kutamania zidi ya maisha ya wakristo, kwa sababu sioni jambo njema wanalo lenye mimi sina. 

Wao, wanakumbwa na shida na matatizo aina yote yenye inayonikumba, pia wao hupata ajali kama mimi. 

Ninafahamu wengi wa watoto wa Watumishi maalum wa Mungu, walioishi maisha ya kumucha Mungu na utawa, na watoto wao vilevile walisema maneno kama yale, sababu waliona kiwango gani wazazi wao walisumbuka, wakiwa na maisha ya tabu, kwa hiyo, sioni jambo la kutisha  na kuvutia katika maisha ya kikristo. 

Kwa hiyo, jameni muacheni mimi niende inje, nikijifurahishe, nile, ninywe na nipitishe saa katika anasa na raha. 


3/ Wengine wanaojitahidi kuwa marafiki wa Biblia, wakijiita wakristo  wanajitwika bidii ya  kupima kubadirisha hali hili. 

Wanasema kwamba kanisa ilishindwa kutumia zawadi zake za kiroho na yakuwa, kwa kupata baraka hizo, sharti wewe uwe yule mtu mwenye kuambatana na hali yenye Mwenyezi Mungu anataka wewe kuwa. 

Ukiheshimu mwenendo huo, wewe utakuwa na gari nzuri sana kwa mahali pako, utaishi katika gorofa nzuri, ndaa yako itajaa na pesa, utakuwa na kazi nzuri na afya ya mwili wako itakuwa nzuri. 

Lakini kwa wepesi, unapotizama watu wale, utatambua kwamba hakuna hata kitu moja kinacho timilika ndani ya maneno yote wanayoyasema. 

Hakuna kile kinacho timilika. 


4/ Neno hili fupi tunalopenda kuwafunulia, ni jambo ambalo twapasha kufahamu, ni neno “Subiri” 

Mungu hakutuahidi vifaa na hazina vya hapa chini duniani, lakini anatuahidi nyakati itakao kuja ya utukufu.   

Kwa mfano, hapa kwa kanisa letu la fasi, tunatarajia majengo ya shule ya jumapili ama nyumba yenye watoto watatumia kwa ibada yao ya watoto, pia tunatarajia kuwa na kitengo cha elimu na maadibisho, hapa kwa kanisa letu la Altoona Bible Church. 

Sisi tuko kwenye changamoto ya kuendelesha na kutimiza miradi na mkakato wa yale majengo. 

Tuna mbunifu mjenzi ama mjengaji mkuu anayefanya taswira ya majengo haya yote, na mipango haya yote yataoneshwa kwenu, na kweli mutayaona. 

Mistari hii iliyochorwa kwenye kartasi, siyo nyumba, baadaye itafaa kuweko mkataba na masikilizano kuhusu kazi, na kwa mwisho wajengaji wataanza kuchapa kazi. 

Wajengaji watapandisha ukuta ya sehemu zote wakifuata kwa makini sana picha iliyochapwa na mjengaji mkuu, sawa vile  alivyochora kwenye kartasi.

Nasi vilevile, Mjengaji wetu Mkuu ni Mwenyezi Mungu, Yeye anatupatia ahadi kuhusu nyakati zitakazokuja, anatuchorea mipango yake na miradi yake ndani ya Maandiko Matakatifu. 

Na siku moja wakati tutakapokwenda kukutana naye uso kwa uso, yote tuliyo tarajia tutayaona waziwazi kwa mecho yetu wenyewe. 

5/ Kila mara wakati ninaposoma maandiko ya Waroma 8, mafikiri yangu yanakwenda pale pale kwa Maandiko ya 2 Timoteo 4: 7 – 8, 

“Nimepiga vita vizuri, nimemaliza mwendo wangu, nimelinda imani; nyuma ya haya nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana mhukumu wa haki atanipa siku ile; wala si mimi tu, lakini watu wote pia wameopenda kuonekana kwake.” 

         Mtume Paulo amesema hapa kwamba amepiga vita vizuri, amemaliza mwendo wake, pia amelinda imani, kwa muda huu, kama mutakumbuka, Mtume Paulo alikuwa anangojea kuuwawa, tayari walijitayarisha kumukata kichwa na alikuwa tayari kukutana na Bwana Yesu Kristo. 

Tizama sasa neno la kwanza la aya ya nane. 

“Nyuma ya haya” neno la kuvutia na la muhimu. 

Wewe, maishani mwako, unayo neno la kufanana kama neno “nyuma ya haya”? 

Neno hili latuangazia kwamba nyakati itakao kuja itakuwa ya raha na heshima kubwa. 

Je, maishani mwako, neno unayo yafanana tu na “sasa hivi”, hapo hapo”,  ama unayo vilevile neno “nyuma ya haya”? 

Kwa kweli, mukristo  anaishi kwa kungojea  “nyuma ya pale nimewekewa”. 


6/ Tuchunguze sasa yanayosemwa kwa aya ya 18, (Waroma 8: 18) 

…utukufu ule utakaofunuliwa kwetu. 

Hapa tuna jambo maaulum sana kujifunza. 

Biblia inatuambia kuhusu utukufu yenye kuumbwa na utukufu usioumbwa. 

 

1 Wakorinto 15: 41 

“kuna utukufu mmoja wa jua, na utukufu mwengine wa mwezi, na utukufu mwengine wa nyota; kwa sababu nyota moja inautukufu mbalimbali na nyota nyingine.” 

         Hapa mtume Paulo anatuzungumuzia kuhusu Ulimwengu, anatueleza kwamba kuna utukufu ndani ya jua, kuna utukufu mwengine ndani ya mwezi, pia kuna utukufu mwengine ndani ya nyota. 

Na nyota moja inautukufu mbalimbali ya nyota nyingine. 

Haya yote yanakuwa na utukufu yenye siku moja itatoweka, siyo utukufu wa milele. 

2 Petro 3: 10 

“lakini siku ya Bwana itakuja kama mwizi; katika siku hii mbingu zitatoweka na sauti kubwa, na viumbe vya asili vitayeyushwa kwa moto mkali, na inchi na kazi zilizo ndani yake zitateketezwa.” 

         Hii siyo utukufu wenye tutakuwa nao. 


7/ Tukumbuke kwamba 1 Wakorinto 15: 43, inasema kwamba: 

“unapandwa katika haya; unafufuliwa katika utukufu: unapandwa katika uzaifu, unafufuliwa katika uwezo;” 

         Mwili wa ufufuko, ulipandwa katika kuoza, unafufuliwa katika kutokuharibika. 

unapandwa katika haya; unafufuliwa katika utukufu: unapandwa katika uzaifu, unafufuliwa katika uwezo. 

Tunaona hapa hali tatu mbalimbali sana yanayoonesha hali ya mwili.  

 

Kwanza wakati mwili unazikwa kwa udongo,   pia wakati wa ufufuko. 

Kwanza tunapandwa katika haya ya kuoza, tunafufuka katika hali ya kutokuharibika. 

Kuoza yaonekana wazi na mwili wa mufu unazikwa katika hali hii ya kuoza. 

Mwili unaoza. 

Na Watumishi wa Mungu wanasema: “Mavumbi wewe, utarudi kwa mavumbi.” 

Nazani ni vema turudishe mafikiri yetu katika Maandiko ya Yoane 11: 39  

Hapa Marata yuko mbele ya kaburi ya kaka yake na anasema:

“Yesu akasema: Mwondoshe jiwe. 

Marata, ndugu mke ya yule mtu aliyekufa, akamwambia: Bwana ananuka sasa; maana, amekuwa maiti siku ine.” 

         Hali ya kutokuharibika ni umbalimbali na kuoza. 

Kutokuharibika ni hali isiyo ya muda, ni ya milele, kamili, isiyo na kivuli ya kugeuka. 


8/ Pia anasema 

Unapandwa katika haya; unafufuliwa katika utukufu. 

Ni kweli kwamba tunafanya yote iwezekanayo kwa kuleta heshima kwa mwili wa marehemu wakati wa mazishi. 

Tunatafuta mavazi mazuri, sanduku nzuri, maua, tunajipanga kwa mustari mbele ya sanduku ya marehemu ili tumutazame kwa mwisho, kiisha tunaendelea na mazishi, na haya yote ni vema. 

Bali, kwa muda huohuo, mwili mwenyewe unaanza kuoza, hali ya haya, tunaanza kujiharakisha ili tuutowe kando yetu kwa woga wa kutokuvumilia matokeo ya mwili kuanza kuharibika na kuoza na hatutaki kufikia kiwango cha kutokuvumilia harufu mbaya ya mwili kuoza. 

Bali, mwili wenye tutakuwa nao kwa ufufuko, utakuwa mwili wa utukufu. 

Jameni, bila shaka, mwili huo utakuwa wa utukufu. 

Hii ni sehemu ya utukufu yenye itakuwa yetu.

Waroma 8, inatuambia kuhusu nyakati hiyo, miili yetu itakuwa ya utukufu. 

Na itafananishwa na nini?  

Tujikumbushe kwa muda muchache jambo la Bwana Yesu kugeuzwa sura juu ya mlima. 


Matayo 17: 1 – 2 

“Na nyuma ya siku sita Yesu akatwaa Petro, na Yakobo, na Yoane, ndugu yake pamoja naye, na kuwaleta juu ya mlima mrefu peke yao; 

Akageuzwa sura mbele yao; sura yake ikangaa kama jua, na mavazi yake yalikuwa meupe kama nuru.” 

         Inasemwa kwamba sura yake ikageuzwa na ikangaa kama jua, na mavazi yake yalikuwa meupe kama nuru.  

Miili yetu itakuwa sawa na ya Bwana Yesu, kama vile tusomavyo katika 

Wafilipi 3: 21 

“atakayebadilisha mwili wetu wa haya upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uwezo ule anaoweza kutiisha vitu vyote viwe chini yake.” 

         Kwa wewe uliyeokoka kweli utarajie jambo hili, kwa sababu utakuwa na mwili wa utukufu. 

Tafakari namna unavyotunza mwili wako kila siku. 

Lakini siku moja, mwili peke yake utakuwa mwili wenye utukufu. 

Mbele ya siku chache, nilisoma katika gazeti Altoona mirroir, kwa sehemu iitwayo Siku ya sita mangaribi, na ilikuwa kuhusu mchezaji moja mwanamuke aliyekuwa murembo sana, lakini uzee ulimushambulia na anapoteza kungaa kwa urembo wake. 

Lakini utukufu tutakayopata haitatoweka kamwe, itakuwa nasi siku zote kwa milele. 

Nashindwa namna ya kueleza aina ya utukufu huo, bali ni utukufu  tutakaokuwa nao.  

Ni wajibu wetu kuisubiri kweli. 


9/ Baadaye, mwili wa kufa wenye unazikwa katika haya, 

 Ushujaa wote unatoweka, hakuna hata nguvu kidogo ya kumruhusu kupumua hata donge moja la pumzi. 

Mwili inapoteza uwezo na nguvu ya kupiganisha mashambulio yote ya nje inayosababisha mwili kuoza. 

Mwili unalala hapo ukiwa bila uwezo wowote wa kujikinga na mashambulizi yote ya asili. 

Ni hiyo hiyo mwili itakayoonekana baadaye katika uwezo. 


10/ Baadaye, tupime kufahamu mambo machache kuhusu utukufu. 

Yoane 17: 5 

“Na sasa unitukuze, Baba, pamoja nawe mwenyewe, kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe mbele ya kuwa dunia.” 

         Bwana Yesu Kristo, katika maombi yake hapa kama Kuhani Mkuu, aliomba Baba Mungu amurudishie utukufu wake aliokuwa nao katika umilele uliopita, mbele Bwana Yesu ajifanye kuwa mtu, akiacha kando ule utukufu wake. 

Hii ni utukufu wenye hauwezi kuumbwa. 

Ni utukufu wa milele. 

Ni utukufu unaodumu milele daima, sawa vile Mungu ni wa milele daima. 

Utukufu huu ni wa milele daima, kwa hivyo aliomba Baba Mungu amurudishie ule utukufu wake, na kweli Utukufu wake ulirudishwa kwake. 


11/ Bali, wakati Bwana Yesu alipokuwa akitembea duniani, Yeye hakuonekana na huo utukufu. 


Marko 6: 1 – 3 

“Akatoka kule, akafika katika inchi yake mwenyewe; wanafunzi wake wakamfuata. 

Ilipokuwa sabato, akaanza kufundisha katika sunagogi. 

Watu wengi wakisikia, wakashangaa, wakasema: 

Huyu amepata maneno haya wapi? 

Na akili gani aliyopewa huyu? Na nini matendo ya uwezo yaliyofanyiwa na mikono yake? 

Huyu si seremala, mwana wa Maria, na ndugu ya Yakobo na Yose na Yuda na Simini? Ndugu zake wanawake si hapa pamoja nasi? Wakachukizwa naye.” 

         Wakati alipokuwa akitembea hapa chini duniani, Bwana Yesu alikuwa sawa sawa na mtu kawaida, sawa mtu wa aina ya watu kama desturi, na wao walimjuwa kama musermala. 

Kwa muda huo hakuwa hata na sehemu ya Utukufu wake, 

Alifanya maishara mengi na matendo ya ishara bila kuwa mtu wa hali ya utukufu, sawasawa nasi kwa siku za leo. 

Wakati tunapotembea na kujielekeza huko na kule katika mitaa yetu, hatuoni watu kushimama kwa kushangaa wakisema: Tazameni mtoto wa Mungu yule anayeelekea huko, ama tazameni mtu wa utukufu anayetembea. 

Hakuna mambo sawa na yale ijapokuwa mchana na usiku wanatutizama tukiwa kama mashaidi kwao. 


12/ Wakolosayi 3: 4 

“Wakati Kristo aliye uzima wetu atakapofunuliwa, nanyi vilevile mutafunuliwa pamoja naye katika utukufu.” 

         Sisi tutafunuliwa pamoja Naye katika Utukufu wake, na utukufu ule hautakuwa utukufu ulioumbwa, ni utukufu ambao, baada ya sisi kuupata, utabaki kwetu milele daima. 


13/ Tunavumbua kawaida ya mafundisho ya aina mbili katika Maandiko ya Wakolosayi 3: 4, sababu inasema kwamba wakati Kristo aliye uzima wetu atakapofunuliwa, nanyi vilevile mutafunuliwa pamoja naye katika utukufu.  

Neno kuonekana inatafsiriwa mu kigriki kwa neno kufunuliwa, pia vilevile kwa neno kumfunua. 

Nikusema kwamba kawaida ya mafundisho ya kufunuliwa na ya utukufu yanatimilika kwa nyakati moja. 

Wakati tutafunuliwa, tutatukuzwa.  

 

AMINA.


N°Ref: 03/14/1965 / 290 - HOW WILL YOU LOOK IN THE FUTURE / 04/30/2022

Friday, April 1, 2022

JAMBO LA KUTUSISIMUA KWA NYIMBO / SOMETHING TO SING ABOUT






JAMBO LA KUTUSISIMUA KWA NYIMBO 

SOMETHING TO SING ABOUT 

November 23, 1977

Pastor Henry F. Kulp




 

2 Timoteo 2: 11 – 13 


“Neno hili ni neno la kweli: Maana kama tukikufa pamoja naye, tutaishi pamoja naye: 

Kama tukivumilia, tutamiliki pamoja naye: 

Kama tukimkana yeye, yeye atatukana sisi vilevile: 

Kama sisi hatuamini, yeye anakaa mwaminifu; maana hawezi kujikana mwenyewe.” 

         Tunayo hapa aya moja maaulum kweli toka Maandiko Matakatifu. 

Aya hizi tatu, zinahesabiwa kuwa sawa shairi ama pia wimbo wa taifa kwa Wasomi na maakili wenye ufahamu nyingi. 

Na yaonekana wazi kwamba, makanisa na makusanyiko ya hapo kale, tayari yalikuwa yakiyaimba.  

Nasi vilevile, kufwatana na namna tutaendelea na majifunzo yetu katika aya hizi, tutagunduwa kwamba kuna jambo maalum, njema na nzuri lenye laweza kutusisimua sisi kwa nyimbo.

 

1/ Hii ni neno muhimu sana na lenye manufaa kweli tunalopaswa kufahamu kwa mwanzo wa hutuba hili tunalo. 

Tuliwafahamisha kwamba kuna kanuni zinazo baki imara na kubaki daima katika kila Matunzaji, na hapo tunakuta jambo lenye kuonekana katika kila Utunzaji. 

Wao wanaofahamu Kawaida ya Mafundisho na kuyatumia katika mwenendo wao wa kila siku, wao watakuwa waamini wenye kuimba nyimbo. 


2/ Isaya 12: 2 

 

“Tazama, Mungu ndiye wokovu wangu, nitatumaini, na sitaogopa: maana BWANA YEHOVA ni nguvu zangu na wimbo wangu; naye amekuwa wokovu wangu.” 

         Nabii anatuambia hapa kwamba: 

Mungu ni wokovu wangu, nguvu yangu na wimbo wangu. 

Utatu wa namna gani! 

Ya kwanza, Mungu ni wokovu wangu. 

Hakungelikuwako uhusiano na Mungu kama mtu hangeliokolewa. 

Mwatambuwa vema kwamba Mungu ni wokovu. 

Sasa dini yajiwekea wokovu. 

Bali, bila wokovu, dini halingalifaa kwa kitu. 

Ya pili, Nabii anasema kwamba Mungu ndiye nguvu yake. 

Yamaanisha kwamba siku kwa siku twaishi kwa kumtwiga Bwana vyote. 

Ya tatu, anasema kwamba Mungu ni wimbo wake. 


3/ Waefeso 5: 18 - 19

 Hii ni jambo la ajabu sana lenye Mwenyezi Mungu analokabizi tu wale wenye kuamua kuhusiana na kutembea na Mungu. 

Hakuna yeye anayeweza kuhakikisha na kuzibitisha kwamba yafaa furaha iwe kwao wenye kuwa na wokovu. 

Mtu aweza kuwa mwamini bali bila kuwa na nyimbo. 

Kwa kweli, wengi kati ya wana wa Mungu wanaishi kati maisha inayo tembelewa na unyonge, kuna wanao kuwa na huzuni,  na hata manunguniko  katika hali namna sawa ni vigumu kuwa na  wimbo rohoni mwako; na kwa kweli  hii ni ungo la nyongezo. 


4/ Zaburi 40: 2, 3

 

“Akanipandisha vilevile toka shimo la uharibifu, toka udongo ulio mtelezi; 

Akaweka miguu yangu juu ya mwamba na kusimamisha hatua zangu.” 

Ameweka wimbo mupya kinywani mwangu, hata sifa kwa Mungu wetu, 

Watu wengi wataona na kuogopa, 

Na watawekea Bwana tumaini lao.”  

         Hapa tuna mzunguko wa tawasifu ya kiroho. 


(1) Akanipandisha vilevile toka shimo la uharibifu, toka udongo ulio mtelezi; hii ni neno la msingi. 


(2) Akasimamisha hatua zangu; hii ni jambo la kila siku, kila nyakati. 


(3) Ameweka wimbo mupya kinywani mwangu. 

Jambo nyingine la zaidi, siyo la muhimu kweli, lakini halali kuwa nalo. 


5/ Tena kwa mushangao mkubwa twasoma kwamba:  

Watu wengi wataona. 

Hapo hapo unasema kwamba: 

“Hii ni makosa, sababu, tafsiri lake lingepashwa kuwa, watu wengi watalisikia.” 

Siyo hilo, awali neno la asili linasema: watu wengi wataona. 

Siyo kosa, ni MATOKEO YANAYOONEKANA NA MECHO. 

Mtu anayeimba wimbo unaotoka humo ndani ya roho yake, anaionesha wazi kwa hali yake ya njee kwa kusisitiza na viungo vya maumbile yake. 

Kuonekana kwake kwa nje kunasema zaidi ya sauti analolitoa. 


6/ “Wala musilewe kwa mvinyo, ndani yake ni makelele, lakini mujaze Roho; 

Mukisemezana ninyi kwa ninyi kwa zaburi na tenzi na nyimbo za roho, mukiimba na kushangilia Bwana mioyoni mwenu;”  

         Katika waraka wa Mtume Paulo, tokeo la mwamini kujazwa na Roho Mtakatifu ni kuwa mwamini anayeimba. 

Jameni niwaonesha kwamba, hata Mtume Paulo naye vilevile alikuwa akiheshimu maagizo hayo. 

Yeye hatuambie neno ambalo lilikuwa kigeni kwake na lenye yeye mwenyewe hakutenda.  


7/ Matendo ya Mitume 16: 21 – 25 


“Tena wanafundisha desturi zisizo halali kwetu kupokea wala kuzifuata, kwa sababu sisi tuko waroma. 

Makutano yote wakaondoka, wakawakwendea kwa nguvu, watawala wakaondosha nguo zao, wakaamuru wapigwe kwa fimbo. 

Walipokwisha kuwapiga mapigo mengi, wakawatupa katika kifungo, wakaamuru mlinzi wa kifungo awalinde sana. 

Naye akipata amri hii akawatupa katika chumba cha ndani, akawafunga miguu kwa mikatale. 

Lakini katikati ya usiku Paulo na Sila walikuwa wakiomba kwa Mungu, na kumwimbia sifa, na wafungwa wengine walisikiliza.” 

         Hapo, Paulo ndani ya kifungo chenye uchafu na cha ndani, kiisha kuumia na mapigo ya fimbo na kuregea sana, amejazwa na Roho Mtakatifu na kuanza kuimba. 

Alipata kusudi la jambo la kumusisimua kwa nyimbo, hakujali magumu yaliyomukumba. 

Walimuweka ndani ya gereza ya ndani iliyokuwa chafu sana ikijaa harufu ya kuleta matapishi, bali mambo haya yote kazaa hayakumufazaisha na kupambazusha mafikili yake. 

Yeye alipokea jambo hilo la zaidi lenye kusemekana ndani ya Isaya na Zaburi. 

Ni jambo la muhimu kwetu kufikia lengo la kufahamu na kugundua ukweli unaokuwa ndani ya Maandiko ya 


2 Timoteo 2: 11 – 13 


“Neno hili ni neno la kweli: Maana kama tukikufa pamoja naye, tutaishi pamoja naye: 

Kama tukivumilia, tutamiliki pamoja naye: 

Kama tukimkana yeye, yeye atatukana sisi vilevile: 

Kama sisi hatuamini, yeye anakaa mwaminifu; maana hawezi kujikana mwenyewe.” 

 8/ Tufikili sasa kuhusu wimbo huo na tugundue jambo moja la muhimu sana. 

Katika aya ya kumi, Mwenyezi Mungu anazungumuza kuhusu wokovu na utukufu wa milele, ama utukufu wa kudumu. 

Wokovu ni kwa waamini wote, bali wokovu yenye utukufu wa kudumu haipewi kwa kila mwamini. 

Hili ndilo neno la msingi tunalolipata katika tenzi tupatalo katika aya 11 hadi 13.  

 

9/ Kuna namna mbili mbalimbali ya kawaida ya mafundisho tunayoweza kuona katika tenzi hili. 

Katika aya ya 11: kwa maana kama tulikufa pamoja naye, jambo hili linahusu maisha.  

Ya pili kuna jambo kuhusu kumiliki. 

10/ Jambo la kuhusu kuishi pamoja na Kristo, haliambatani na uaminifu wa mutakatifu, lakini linaambatana na uaminifu wa Bwana Yesu Kristo Musalabani. 

Hii ndiyo Musingi wa Mafundisho ya Waroma. 

Sasa twapaswa kusoma namna hii: 

SISI TULIKUFA PAMOJA NAYE. 


11/ Waroma 6: 3, 4 


“Au hamufahamu, sisi sote tulio batizwa katika Yesu Kristo, tulibatizwa katika kufa kwake? 

Hivi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika kufa kwake: hata kama Kristo alivyofufuka toka wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo tutembee katika upya wa uzima vilevile,” 

         Tufahamu kwamba wote waliobatizwa katika Kristo, walibatizwa katika kufa kwake, na ubatizo huu hauwezi kamwe kulinganishwa na ubatizo wa maji, jambo hili haliwezi kamwe kuwa vile, sababu haiwezekani. 

Tupate mwangaza wa ufahamu kwa njia ya Maandiko ya Wagalatia 3: 27 

“Maana ninyi wote muliobatizwa na kuingizwa katika Kristo, mumevaa Kristo.” 

         Nikusema kwamba, kama wewe haujapata ubatizo huu, wewe hauja vaa Kristo. 

Inaonekana wazi wazi kwamba ni upumbafu mtupu kuzani kwamba maji yanaweza kufanya kazi hii. 


TUTAISHI PAMOJA NAYE VILE VILE. 

Yamaanisha kwamba kifo hicho siyo mwisho ya maneno bali ni mwanzo. 


13/ Aya ya 12. 

“Kama tukivumilia, tutamiliki pamoja naye,…” 

         Tunafikia sasa: 

Kama tukivumilia, tutamiliki pamoja naye: kama tukimkana yeye, yeye atatukana sisi vilevile.  

Jina la sarufi “Sisi” yaonesha kwamba ni waamini wanao tenda tendo. 

Hali hii ni kwa wakristo pekee, bali siyo kila mukristo ndiye anayeweza kuvumilia mateso. 

Wengine kwepesi wanamukana. 

Kumbukeni Maandiko ya 2 Timoteo 1: 8 – 12 – 16 

“Basi usione haya kwa ushuhuda wa Bwana wetu, wala kwa mimi mfungwa wake: lakini uvumilie taabu pamoja na Habari Njema kwa nguvu za Mungu; 

Ambaye alituokoa  akatuita kwa mwito mtakatifu, si kwa kadiri ya matendo yetu, lakini kwa kadiri ya kusudi lake mwenyewe na neema yake, tuliyopewa katika Kristo Yesu mbele ya nyakati za zamani na sasa imefunuliwa na kuonekana kwa Mwokozi wetu Yesu Kristo, aliyebatili kufa, na kufunua uzima na maisha yasiyokoma kwa njia ya Habari Njema. 

Kwa Habari Njema hii niliyowekwa mhubiri, na mtume, na mwalimu wa Mataifa. 

Na kwa sababu yake ninapata mateso haya vilevile; lakini sioni haya; maana ninamjua yeye ambaye nilimwamini, na ninajua kabisa ya kwamba anaweza kulinda ile niliyoweka kwake hata siku ile. 

Shika mfano wa maneno ya kweli uliosikia kwangu, katika imani na mapendo yaliyo katika Kristo Yesu. 

Ulinde kitu kile kizuri kilichowekwa kwako kwa Roho Mtakatifu anayekaa ndani yetu. 

Umejua habari hizi ya kuwa wote walio katika Azia wameniacha, katika hawa ni Figelo na Hermogene. 

Bwana awape rehema walio wa nyumba ya Onesiforo; kwa mara nyingi aliniburudisha, wala hakuona haya kwa sababu ya mnyororo wangu.” 

         Twapata hapa waamini wanaosikia haya ya kumushuhudia Bwana Yesu na haya ya Mtume wake Paulo.  

Wao hawapendi maisha yao yaambatane na Maandiko ya Mtume Paulo, sababu yanasamani fulani na namna wao wanatenda namna sawa, yeye vilevile atawakana. Si kwamba watapoteza wokovu. 


14/ Aya ya 13 

“Kama sisi hatuamini, yeye anakaa mwaminifu; maana hawezi kujikana mwenyewe.” 

         Aya hii inatuonesha kwa makini sana kwamba neno hili lamaanisha kwamba siyo jambo la kupoteza wokovu. 

Kama sisi hatuamini, yenye kujitafsiri kwamba, kama sisi hatustahili kuheshimu imani, yenye inamaanisha kwamba kama sisi hatusadiki, nikusema kwamba tunajizuiza kuonesha ni nini tunaloamini kuhusu ukweli wa neno lake, yeye anabaki mwaminifu. Yeye hata watupilia. 

Jambo ni kwamba yeye hatawapa zawabu, bali watapata uzima. Wao ni wenye kuokolewa. 


15/ Tuchunguze kwa makini maneno mane ya mwisho wa aya ya 13. 

Yeye hawezi kujikana mwenyewe. 

Utafsiri wa kigriki ungelikua: kwa kujikana mwenyewe, kwake haiwezekane, Yeye hawezi kamwe kufanya hivyo. 

Hiyo inamaanisha nini? 

Sisi ni kipande cha Mwili wake. 

Sisi tunaungana naye, sisi ni viungo vya Mwili wake, na kutuondowa kwa kututupa mbali inamaanisha kwamba anajikana mwenyewe, na jambo hili haliwezekane kwake. 

Hii ni moja ya aya kubwa katika Biblia inayozungumuza kuhusu Amani ya milele. 

Aya hizi tatu zinaelekea jambo la zawabu. 

Waweza kupoteza zawabu yako, lakini hauwezi kupoteza wokovu wako. 


16/ Turudi nyuma kidogo na tuchunguze yale yanayoelekea Ufalme wa Mungu, tufahamu maana yake. 

Juma iliyopita,tulitumia aya ya Luka 19: 17 – 19 

“Akasema: Vema, mtumwa mzuri; kwa sababu unakuwa mwaminifu kwa neno ndogo sana, uwe na mamlaka juu ya miji kumi. 

Na wa pili alikuja, akisema: Bwana, feza yako imepata feza tano. 

Akamwambia: Nawe uwe juu ya miji mitano.” 

         Twapashwa kufahamu kweli kwamba hapo anazungumuzia kuhusu Ufalme wa Mungu, siyo kuhusu Kanisa Mwili wa Kristo. 

 Katika aya ya 11, katika mufano huo tunakuta vikundi vitatu. 

“Nao wakisikia maneno haya, aliendelea kusema mfano, kwa sababu alikuwa karibu na Yerusalema, nao walizania ya kama ufalme wa Mungu utaonekana mara moja.” 

         -Wanainchi walikuwa sawa wenyi kuwakilisha Taifa la Izraeli kwa nyakati ya muda fulani, kwa mwanzo wa huduma na hasa kwa mwanzo wa Matendo ya Mitume. 

 - Pia watumishi ni kweli wao walikuwa watumwa wa Mungu na hiyo yaonekana, wao ni watumishi wake na anawaagiza wafanye biashara hata wakati atakapo kuja. 

Luka 19: 13 

“Akaita watumwa wake kumi, akawapa feza kumi, akawaambia: Fanyeni biashara hata wakati nitakaporudi.” 

-Watumishi wale wawili wa kwanza walikuwa waaminifu na wao walipata zawabu. 

Lakini sasa kwa aya 22 – 24,  

“Akamwambia: kwa kinywa chako nitakuhukumu, wewe mtumwa mbaya. 

Ulijua mimi ni mtu mkali, nikiondoa ile nisiyoweka, nikivuna nisiyopanda; 

Kwa sababu gani hukuweka feza yangu kwa wale wanaolinda feza, ninaporudi, niipate pamoja na faida? 

Akawaambia wale waliosimama karibu: Ondosha feza kwake, mukampe yule wa feza kumi.” 

         Hapa tuna mtumishi mubaya, 

Kumbukeni kwamba mtu huyu ni mtumishi. 

Hapa hawazungumuzie wokovu, bali ni jambo la zawabu. 

Na Bwana akamuondosha hiyo feza na kuikabizi kwa yule mwenye tayari alikuwa na kumi nyingine. 

Kwa aya ya 26, hapo anaonesha kanuni: 

“Kwani ninawaambia ninyi: Kila mtu aliye na kitu, atapewa; lakini yeye asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitaondolewa kwake.” 

Kukosa zawabu. 


17/ Aya ya 27 

“Lakini adui zangu hawa, wale wasiotaka nitawale juu yao, muwalete hapa, mukawaue mbele yangu.” 

         Hapa tuna maadui wa Bwana, wale wasiotaka Bwana atawale juu yao, Bwana aliamuru wawalete pale na kuwauwa mbele yake. 

Hawa watu hawakuokolewa. 

Wale sio watumishi, bali ni maadui. 


18/ 1 Wakorinto 3: 10 – 14 

“Kwa kadiri ya neema ya Mungu, niliyopewa, sawasawa mjenga mkubwa mwenye akili, niliweka msingi; na mtu mwengine anajenga juu yake. 

Lakini kila mtu aangalie namna gani anavyojenga juu yake. 

Maana mtu hawezi kuweka msingi mwengine ila ule uliokwisha kuwekwa, yeye Yesu Kristo. 

Lakini kama mtu akijenga juu ya msingi huu zahabu au feza, au mawe ya bei kubwa, au miti au nyasi au majani; 

Kazi ya kila mtu itaonekana wazi: Kwa sababu siku ile itaionyesha, kwa sababu itafunuliwa na moto; na moto utajaribu kazi ya kila mtu, ni ya namna gani.” 

         Tunasikia hapa kwamba kwa mtu kupata zawabu, yafaa mtu huyu kujenga juu ya Msingi Yesu Kristo, ni Msingi uliokwisha kuwekwa na Mtume Paulo. 

Kama wewe siyo mufuasi wa mafundisho ya Mtume Paulo, wewe hutapokea zawabu. 

Tufahamu sana yanayosemwa kwa aya ya 15.

“Kama kazi ya mtu ikichomwa, atapata hasara: lakini yeye mwenyewe ataokolewa; lakini ni kama kwa moto.” 


19/ 1 Wakorinto 9: 27 

“Lakini ninatesa mwili wangu, na kuutumikisha, isiwe, nikikwisha kuwahubiri wengine, mimi mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa.” 

         Hapa anaonekana kama mtu aliepona ajali ya kufa, aliepona kuangamia majini kwa kuzama, hii haioneshi kwamba alipoteza wokovu wake, lakini, anakataliwa kwa kupewa zawabu, na tukiendelea mbali na usomi hata kufika kwa aya ya 24, 25, tutatambuwa wazi kwamba inazungumuzia kuhusu zawabu.   

“Hamujuwi ya kuwa wale wanaopiga mbio katika mashindano, wote wanapiga mbio, lakini mmoja anapokea zawadi? 

Pigeni mbio namna hii; ili mupate. 

Na kila mtu anayeshindana, ana kiasi katika maneno yote. 

Basi wanafanya hivi kusudi wapate taji ya kuharibika: lakini sisi tupate taji isiyoharibika.”  

 

20/ Kutawala pamoja na KRISTO 

Waefeso 2: 6 

“na alitufufua pamoja naye na kutukalisha pamoja naye katika pahali pa mbingu, katika Kristo Yesu.” 

         Hapa inahusu  uwezo wetu na kiti chetu cha utawala katika pahali pa mbingu. 


21/ Sawa sawa na Taifa la Izraeli itakao miliki na kutawala kwa dunia kwa niaba ya Yesu Kristo, na wao watakuwa wajumbe wa Bwana Yesu Kristo (Ufunuo na wale watu 144.000) 

Sisi tutatawala kule mbinguni na tutakuwa wajumbe kwa viumbe vya mbingu. 

Isaya 61: 5, 6 

“Na wageni watasimama na watakulisha makundi yenu, na watu wa kabila lingine watakuwa walimaji wenu, na wenye kuchunga mizabibu yenu. 

Lakini ninyi mutaitwa makuhani wa BWANA; watu watawaita ninyi watumishi wa Mungu wetu; mutakula utajiri wa mataifa, na mutajisifu katika utukufu wao.” 

         Bali sisi tutakuwa makuhani wa Bwana kwa viumbe vya mbinguni, wao hawataweza kufahamu Neema, hawataweza kuitafakali. 

Wanatutazama kwa nyakati hizi nao hawana uwezo wa kufahamu Neema, ni wajibu wetu kwa wakati ule kuwafahamisha Neema ni nini. 

1 Wakorinto 4: 9 

“Kwani ninazania ya kwamba Mungu ametutoa sisi mitume katika mwisho kama watu waliohukumiwa wauawe: kwa sababu tumekuwa matazamo kwa dunia, na kwa malaika, na kwa watu.” 

Waefeso 3: 10 

“ili sasa, kwa njia ya kanisa, hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi ijulishwe na falme na mamlaka katika pahali pa mbingu;” 

 

AMINA 

 

N°Ref: 11/223/1975 / 261-2 SOMETHING TO SING ABOUT / 03/31/2022