Sunday, July 18, 2021

JE MAPENDO YA KWELI NI KIPOFU? / IS TRUE LOVE BLIND?

Photo by B Smith from the patio




JE MAPENDO YA KWELI NI KIPOFU? 

IS TRUE LOVE BLIND?

January 23, 1977 

Pastor Henry F. Kulp


 

Wakolosayi 1: 1 – 8 

“Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na Timoteo ndugu yetu, kwa watakatifu na ndugu waaminifu katika Kristo walio katika Kolosayi: Neema iwe kwenu na salama toka Mungu Baba yetu. 

Tunashukuru Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo, tukiwaombea ninyi siku zote, tukiwa tumesikia  habari za imani yenu katika Kristo Yesu, na za mapendo muliyo nayo kwa watakatifu wote, kwa sababu ya tumaini mulilowekewa akiba mbinguni, habari zake mulizosikia zamani katika neno la kweli ya Habari Njema, iliyofika kwenu; kama ni vile katika ulimwengu wote ikizaa matunda na kukua kama inavyokua ndani yenu vilevile, tangu siku muliposikia na kujua neema ya Mungu katika kweli; kama vile mulivyofundishwa na Epafra, mjoli wetu mpenzi, aliye mtumishi mwaminifu wa Kristo kwa ajili yetu, ambaye alituambia vilevile habari za mapendo yenu katika Roho.” 

Tunapewa salamu za Mtume Paulo katika aya ya 1 na ya 2

Anawasiliana nao kama watakatifu na ndugu waaminifu katika KRISTO. 

Neno kubwa katika Wakolosayi ni UTIMILIFU

Na sisi ni utimilifu wake. Tulipokea Utimilifu wake.   


1/ Tangu aya ya 3 mpaka aya ya 5, ni masemi ya shukrani ya Mtume Paulo. Mtume Paulo anashukuru. 

Tunashukuru Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo, tukiwaombea ninyi siku zote.  Mtume Paulo anashukuru kwa niaba yao. Anashukuru Mungu kwa ajili yao. 

Hapa, neno kuwaombea ni ya kuvutia sana. 

PROSS – U – KUH – MY, eti unafahamu kwamba neno PROSS inamaanisha uso kwa uso na Mwenyezi Mungu. 

Upendeleo gani tunayo, bado tukiwa hapa duniani, ijapokuwa hata hatumuoni Mwenyezi Mungu, lakini tunamukaribia uso kwa uso tukimuletea malalamiko yetu. 

U – KUH – WRIST – O na katikati ya neno hili, tunapata neno KAR – RIS inayomaanisha NEEMA.    

Kwa kumaanisha kwamba tunashukuru kwa hayo yote tunayopata bila kustahili. 


2/ Ni mafaa kwetu kujuwa kwamba maombi yetu twayaelekeza kwa Baba  Mungu. Hakuta kuwa kamwe kinyume ya hiyo. 

Wakati unaposikia mtu akiomba “Yesu wangu…”, bila shaka iyo unayosikiliza ni  uasi, na Mwenyezi Mungu hatajibu maombi yale. 

Vivyo hivyo, kama ukisikia mtu anaomba kwa Roho Mtakatifu, kweli hiyo  unayosikia ni uasi, Mwenyezi Mungu hata jibu maombi yale, mushike haya kwa makini sana, wakati muombapo, maombi yenu yaelekezwe kwa Mungu Baba.  


3/ Tupate mwangaza kwa mafikili yetu toka sura moja kubwa ya Biblia inayohusu maombi.  

Waroma 8: 26 

“Hivi Roho anasaidia uzaifu wetu: kwa maana hatujui kuomba kitu namna inavyotupasa, lakini Roho mwenyewe anatuombea kwa kuugua kusikoweza kusemwa;” 

Twaona hapa kwamba Roho Mtakatifu anayefanya makao ndani yetu anatuombea kwa Mungu Baba, akitusaidia katika maombi yetu. 

Pia Aya ya 34 inasema:  

“ni nani anayehukumu? Ndiye Kristo aliyekufa, ndiyo, zaidi, amefufuka, naye yuko kwa mkono wa kuume wa Mungu, tena ndiye anayetuombea.” 

Twaona hapa, Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, huko mbinguni akiomba kwa Mungu Baba kwa ajili yetu. Ni neno hili ndilo twapasha tarajia, hatuwezi fanya zaidi ya hayo. 


4/ Kwenu ninyi, PEAR – EE, inayomaanisha, yenye kuwahusu. 

Kumbukeni kwamba yeye alikuwa bado hajakutana nawo, ama haja waona bado, lakini alikuwa akiwaombea. 

Eti, yawezekana mimi niombee mtu mwenye sijaona bado? 

Kwa kweli yawezekana.  


5/ Tuhakikishe kwamba Mtume Paulo anasema ya kwamba watu hawa walikuwa na Neema ya kuwa na vitu tatu maalum: 

Mambo matatu: Imani, Mapendo, na Matumaini.


(1)  Imani katika KRISTO YESU. 

(2)  Mapendo tunayo kwa watakatifu wote. 

(3)  Matumaini tunayo kuhusu mbinguni. 


6/ Imani katika KRISTO YESU. 

Tusome Wakolosayi 2: 5  

“Maana hata nikiwa mbali katika mwili, mimi ni pamoja nanyi katika roho, nikifurahia na kutazama utaratibu wenu na uaminifu wa imani yenu katika Kristo.” 

Hapa inahusu uaminifu wa imani yao katika Kristo.

 Neno imani, inamaanisha uaminifu ya uhakika.  

Wao wanakuwa na uaminifu wa uhakika ya kumsadiki Bwana Yesu Kristo.

Waweza kuwa na imani kwa jambo fulani, ama hapana.

 Wengi wanamjua Bwana Yesu Kristo kama Mwokozi, kama Mwenye aliyechukuwa zambi zao, lakini hawana uhusiliano wa urafiki pamaoja naye, hawamjui kama rafiki wa kweli na wa ndani. 

Hawatembei na Bwana Yesu Kristo katika mwendo wao wa kila siku. 

Kwa kuwa na Salama, yafaa kumjua Bwana Yesu Kristo na kutembea naye daima siku zote. 


7/ Ni lazima kwetu tufahamu kwamba imani ni jambo la hatari sana katika ulimwengu. 

Kama imani yetu tukiiweka ndani ya kitu kibaya, jambo hili litazorotesha maisha yetu, litatuharibu hata kufikia kiwango cha kutuuwa. 

Kuna mwanamemba wa kanisa letu la fasi mwenye kwa siku za leo alisafiri mbali sana na nikule anaishi kwa sasa, bali, kwa wakati alipokuwa akiishi pamoja nasi, siku moja alipenda kuunguza majani katika kiwanza chake, na hapo mavazi yake yakapata moto na kuunguwa na yeye vilevile mwili wake uliunguwa vikali sana na hapo hapo akapelekwa kwa haraka kwenye hospitali, kule wakamutibu na peniceline yenye kwa siku za mbele haikuwa inatunza hata mwili wake na hiyo ilitaka kumupeleka kwa kifo. 

Yafaa kuwa na Imani katika jambo lililo aminifu. 


8/ Wagalatia 3: 26 

“maana ninyi wote ni wana wa Mungu, kwa imani, katika Yesu Kristo.” 

Ninyi wote mumekuwa watoto wa Mungu waliokomaa kwa imani katika Kristo Yesu

Tuone sasa neema ya pili waliokuwa nayo: Mapendo.  

Ni neno moja katika Swahili inayotumiwa kwa namna mbalimbali ya mapendo. 

Mapendo kwa Mwenyezi Mungu, mapendo kwa watoto, mapendo kwa wazazi, mapendo kwa marafiki. 

Watu wengi wanaita tendo la ndoa, kufanya mapendo, Neno la Kigriki ni mapendo kati ya ngono. Na kweli yaweza tu kuwa shauku. 

Ni mapendo ya uchoyo, mambo yote yakifwata tu njia moja. Haitumikishwi hata mara moja katika Agano Jipya. 


9/ Baadaye tuna neno la Kigriki PHIL - LET - O kwenye  tunapata undugu wa filadelfia, undugu,  na hii inamaanisha mapendano na hii njo maana ya msingi ya neno: urafiki


10/ Neno lililotumikishwa hapa ni AH - GOP – A, Mungu ni Pendo


(1) Ni neno linalotumikishwa kati ya Mungu Baba na Mwana wake. 

Yoane 17: 26 

“Nami niliwajulisha jina lako, nitalijulisha; hata mapendo ambayo ulinipenda mimi yawe ndani yao, nami ndani yao.”  


(2) Ni neno linalotumiwa kwa kuonesha Mapendo ya Mungu Baba kwa ulimwengu. 

Yoane 3: 16 

“Kwa maana Mungu alivyopenda ulimwengu, hata kutoa Mwana wake wa pekee, ili kila mtu akimwamini asipotee, lakini apate uzima wa milele.” 

Yoane 16: 27  

“Kwa maana Baba mwenyewe anawapenda ninyi, kwa sababu ninyi mumenipenda mimi, na kuamini ya kwamba nilitoka kwa Mungu.” 

Tunasoma ya kwamba: Baba mwenyewe anawapenda ninyi, kwa sababu ninyi mumenipenda mimi. 


11/ Kwa kufikia kiwango cha kupenda na haya mapendo, yafaa Roho Mtakatifu atawale na kuongoza maisha yako. 


12/ Kwa siku iliyopita, wengi wenu hawakunisadiki wakati niliposema kwamba yapashwa muwe na imani kwa Mungu, hapana kuwa na imani ndani ya watakatifu, bali yafaa kuwapenda. 

Na hii ni kweli kwa sababu hakuna hata moja kati ya wanaadamu aliye mkamilifu katika njia zake zote, ili mufikie kiwango cha kufahamu kwamba: MAPENDO SI KIPOFU. 

1Wakorinto 13: 6 

“hayafurahi kwa uzalimu, lakini yanafurahi pamoja  na kweli:” 

Mapendo yanafurahi pamoja na kweli. 

Eti upendo waweza kufwatana na namna mtu tunaye mpenda ni mkamilifu? 

Eti twaweza kukoma kupenda watu sababu walifanya makosa, ama walitenda uzalimu? 

Kama ingelikuwa namna sawa, hatungimpenda hata mtu mmoja. 

Sote tunaye kweli huyo mtu wa zamani anayetuvutia kutenda zambi na makosa, eti jambo lile lasukuma waamini wengine wasitupende? 

Mapendo yenye inaweza kukomeshwa na ukweli wa mambo siyo mapendo ya namna ya Mungu. 

Twapashwa kufanana Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, aliyetupenda si kwa ajili ya matunda ya matendo yetu mazuri, lakini hata ivyo alitupenda. 

Waroma 5: 8  

“Lakini Mungu anaonesha mapendo yake kwetu, wakati tulipokuwa tungali wenye zambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.” 

1Yoane 4: 19  

“Sisi tunapenda kwa maana yeye alitupenda sisi kwanza.” 


13/ Watu wengine wanakuwa sawa wenye wazimu, wao hawaoni hata kasoro yeyote ndani ya mtu wanao shuhudia  kumpenda. 

 Wababa na wamama wengine wanawapenda watoto wao hata kufika kiwango cha kufanya kuwa sawa hawaoni makosa na hisia za watoto wao na hii inawafanya watoto kuwa wakosa adabu na wenye wasio kuwa na maono sambamba kuhusu maisha ya kesho.  

Mapendo ya kweli kwa mwamini ni ile inayomuruhusu kujuwa ukweli wote kuhusu mtu anayempenda na hiyo ukweli haitamuvunja roho ama kumukata tamaa.  


14/ Tuchunguze sasa neema ya tatu: Tumaini 

Tumaini la baraka tunalowekewa akiba mbinguni.

Tumaini lilo tunalipata katika Tito 2: 13 

“tukitazamia tumaini la Baraka na kuonekana kwa utukufu wa Mungu mkubwa, Mwokozi wetu Yesu Kristo:” 

Waamini wote wangepewa tumaini hili la baraka toka Mungu wetu.


15/ Msingi wa huu tumaini tunaupata katika 1Timoteo 1: 1 

“Paulo mtume wa Kristo Yesu, kwa agizo la Mungu Mwokozi wetu na la Kristo Yesu taraja letu;”  

Yesu Kristo ni taraja letu. 


16/ Ndani ya Tumaini muna jambo tatu: 


(1) Hamu  

Hatuwezi kuwa na tumaini ikiwa hatutamani jambo tunalotumainia litimilike.

Tumaini siyo tu hamu, sababu tunaweza kuwa na hamu ya jambo lenye hatutarajie. 


(2) Matarajio 

Tena kabisa matarajio siyo kabisa tumaini, kwa sababu tunaweza kutakia jambo lenye hatupashwi kutakia. 

Yatupasa kuchanga hamu na matarajio. 


(3) Uvumilivu 

Twapashwa kuwa na uvumilivu kuhusu hamu na matarajio yetu. 


17/ Ni muhimu sana tufahamu kwamba kuna tofauti na umbalimbali kati ya Tumaini la wa Israeli na Tumaini la waamini wa siku za leo. 

Tuchunguze tofauti hizo kwa makini kabisa: 


(1) Tumaini la Israeli ni la Duniani. 


(2) Tumaini letu ni la Mbinguni


(3) Katika tumaini la Israeli, KRISTO ni Mwana wa Mtu, Mwana wa Daudi, na Mwana wa Abrahamu. 


(4) Katika tumaini letu KRISTO ni Mwana wa Mungu, KRISTO ni Kichwa cha Mwili. 


(5) Tumaini la Israeli ni kuhusu kuja kwa KRISTO hapa duniani. 


(6) Tumaini letu ni kuhusu kuchukuliwa kwetu na KRISTO na kumulaki hewani. 


(7) Tumaini la Israeli litatimilika kiisha hukumu mkubwa na mateso makuu hapa duniani. 


(8) Tumaini letu litatimilika mbele ya hukumu na mateso hapa duniani. 


18/ 1 Wakorinto 13: 13 

“Basi, sasa inadumu imani, tumaini, mapendo, hizi tatu; lakini neno kubwa katikati ya maneno haya ni mapendo.”  

Kati ya hizo neema tatu ni moja tu inayodumu nayo ni mapendo. 

Siku moja imani na tumaini zitakoma, bali mapendo itakuwa kwa milele. 


AMINA. 


N°Ref: 01/23/1977 / 335-2 IS TRUE LOVE BLIND / 07/18/2021

No comments:

Post a Comment