Sunday, July 18, 2021

SHULE LA HEKIMA / THE SCHOOL OF WISDOM

Photo by B Smith from the kitchen door (Rare Whistling Ducks)


 


SHULE LA HEKIMA 

THE SCHOOL OF WISDOM

June 1, 1980 

Pastor  Henry F. Kulp


 

Mezali 2: 1 - 5  

“Mwana wangu, kama ukikubali maneno yangu, Na kuweka akiba maagizo yangu ndani yako; Halafu utatega sikio lako kusikia hekima, Na kutia moyo wako kwa ufahamu; Ndiyo, kama ukiita akili, 

Na kupaza sauti yako kwa ufahamu; Kama ukiutafuta kama feza, Na kuutafutatafuta kama hazina zilizofichwa; Halafu utafahamu woga wa BWANA, Na kupata maarifa kwa Mungu.” 

Hapa, tunayo shule la hekima. 

Katika Sura ya mwisho, sehemu ya mwisho wake, twaona kwamba, inje ya desturi za dini nyakati zile, hekima inawasihi, kwa mkazo na sauti kubwa, vijana wa Taifa la Israeli. 

Hekima ikiwapa wote angalisho kuhusu vinyume vitakavyo tokeya kama wanatupilia mbali hekima. 

1/ Wakati mashindano na majaribu ya maisha yanatukia, yote yale hayawezi kukupatia hekima kwa muda huo muchache, kwa sababu hekima ni kumujuwa Mwenyezi Mungu, tokeo la Neno la Mungu pamoja na kumucha Mungu. 

Na kuwa na ufahamu kuhusu Mungu haipatikani kwa rafla. 

Hii ni jambo linalotukumba hatuwa kwa hatuwa, ni tunda la kukusanya. 

Kwa kweli, ufahamu bila kumucha Mungu ama woga wa Bwana, yaweza kuwa bila mafaa yeyote. 

Imetupasa kuwa na ufahamu na woga wa Bwana, yote miwili itembee pamoja ili tuwe na hekima. 


2/ Yobu 28: 12  

“Fezaluka wala bilau havitatajwa: Ndiyo, bei ya hekima inapita vito vyekundu vya damani.” 

Bei ya hekima inapita vito vyekundu vya damani. 

Nikusema kwamba vifaa na hazina tunayo hayawezi kamwe kukamata nafasi ya hekima. 

Haijali kiwango gani cha hazina unayo, hekima inasamani kupita na ni ya mafaa sana. 

Kwa hiyo, mtu anaweza kuwa na utajiri nyingi, lakini kama hana hekima, mtu huyu anaweza kupokonya mali yake kwa muda kitambo tu na baadaye kujikuta hana tena kitu. 

YATUPASA KUTAMANI SANA HEKIMA. 

Mezali 4: 7  

“Hekima ni kitu cha kwanza; basi  ujipatie hekima: 

Ndiyo, pamoja na yote uliyopata pata ufahamu.” 

Tunasoma hapa kwamba hekima ni kitu maalum sana na ni ya msingi, kwa hiyo pata hekima, na pamoja na yote uliyopata pata ufahamu. 

Twapashwa kutamani sana hekima, lakini ni waamini wachache tu wanayokuwa na hekima.  


3/ Zaburi 119: 98, 99  

“Maagizo yako yananitia hekima kuliko adui zangu; Maana ni pamoja nami siku zote. 

Nina ufahamu kupita walimu wangu wote; Maana shuhuda zako ninazifikiri.”  

Hapa mtu moja maarufu anatujulisha kwamba chemchemi ya hekima yake ni katika ufahamu wa Neno la Mungu. 

Kwa sababu kwa aya ya 98 anasema: 

Maagizo yako yananitia hekima kuliko adui zangu, na yeye ni mwenye kumcha Mungu. 

Na kwa aya ya 99, anasema: 

Nina ufahamu kupita walimu wangu wote; shuhuda zako ninazifikiri. 

Nikusema kwamba walimu wake walikuwa na ufahamu lakini hawakukuwa na hekima. 

Walichunga mambo mengi katika vichwa vyao, bali hawakuwa na woga wa Bwana. 


4/ Yakobo 1: 5 

“Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na akili, aombe Mungu, anayewapa wote kwa ukarimu, pasipo kuhamakia; naye atapewa.” 

Mtume Yakobo asema kwamba: 

Kama mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, sikiliza kwa makini inayosemwa hapa: Omba Mungu, usiombe kwa mtu. 

Usiombe kwa walimu. 

Omba kwa Mwenyezi Mungu kwa maana hekima ya kweli inatoka kwa Mungu. 

Wanadamu waweza kukupatia mashauri mazuri, kiisha punde kidogo wanashindwa kukushauri. 

Kama si wenye kuokolewa, mashauri yao yawezakuwa mabaya, lakini hata watu waliookoka wanaweza kuwa na mashauri mabaya vile vile, kwa sababu, mambo yote ya waamini hayakamiliki kwa kila hali, bali ni Neno la Mungu pekee lililo kamilifu na lenyi haki daima. 


5/ Mezali 3: 5    

“Tumainia Bwana kwa moyo wako wote, wala usitegemee ufahamu wako mwenyewe:” 

Twasoma hapa: Tumainia Bwana kwa moyo wako wote, wala usitegemee akili yako mwenyewe. 

Ni kusema: Umuombe Mungu, usijiombe mwenyewe, wala kutafuta kujua kiini ya mambo wewe mwenyewe. 

Umuombe Mwenyezi Mungu hekima, nikusema kimbilia kwenye Neno la Mungu. 


6/ Kwa kweli hii ndiyo maana ya maombi.  

Omba kwa Mungu. 

Katika mashauri mengi kuhusu maombi tunayoyapata katika kitabu cha Yakobo, 

Hili ndilo la kwanza. 

Bali, Maombi pekee yatosha? 

Kuomba Mungu bila jambo lingine? Hapana. 

Kwa njia gani Mwenyezi Mungu hujibu maombi yetu kama tukimuomba hekima? 

Ni kwa njia tu la Neno la Mungu. 

Mwenyezi Mungu hatumii njia nyingine kwa kuzungumuza nasi, kama siyo tu kwa njia ya Neno la Mungu. 

Waweza kujiuliza: Eti Mwenyezi Mungu hutumia pia mazingira na  matukio mbalimbali yanayotutokea maishani mwetu? 

Kwa kweli yanawezekana, bali yale mazingira na matukio yote yanapashwa kuambatana na Neno la Mungu, yakifuata Kawaida ya Mafundisho ya Biblia Takatifu. 


7/ Tufahamu ya kwamba Mwenyezi Mungu ni, mwenye kupenda kutoa. 

Yeye ni Mtoaji Mkubwa, na Toleo lake ni la bure bila malipo yoyote. 

Ni Yeye atupae chakula chetu cha kila siku, ni Yeye anaye tuvika na kutupatia manufaa yote yanayotufaa. 


8/ Siyo tu kwamba Mwenyezi Mungu anatoa, lakini Yeye utowa kwa ukarimu wote. 

Waefeso 1: 3 

“Abarikiwe Mungu na Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye alitubariki kwa baraka zote za roho katika pahali pa mbingu ndani ya Kristo;” 

Tutambue hapa: Mwenyezi Mungu anatoa kwa ukarimu. 

Alitubariki kwa baraka zote za roho, siyo kwa baraka nyingi, ama karibuni baraka nyingi, lakini baraka zote, na tunayapokea bure bila malipo wakati tunapo okoka.  


9/ Yakobo 3: 15  

“Akili hii haitoki juu, lakini ni ya dunia, na ya tamaa, na ya Shetani.”

Hii ni aya ingine ya manufaa sana katika majifunzo yetu kuhusu hekima. 

Aya hii inaanza na: 

Hekima hii haitoki juu.  

Siyo hekima toka kwa Mungu. Ni hekima isiyotoka kwa Mwenyezi Mungu. 

Tukiilinganisha na aya ya 17. Kuna jambo moja tofauti: 

Aya ya 17  

“Lakini akili inayotoka juu, kwanza ni safi, tena ni ya salama, na upole, tayari kusikiliza maneno ya watu, imejaa rehema na matunda mema, pasipo fitina, pasipo udanganyifu.” 

Twatambua hapo kwamba kuna aina tatu ya hekima. 

Kwanza kuna hekima itokayo juu. 

Kiisha kuna hekima isiyotoka juu, na kwa mwisho kuna hekima ya kimtu. 

Tuchunguze sasa aya ya 15. 

Aya ya 15 

“Akili hii haitoki juu, lakini ni ya dunia, na ya tamaa, na ya Shetani.” 

Hekima isiyo toka juu. Ni hekima ya kidunia, ya tamaa, ya Shetani.

 Ya kidunia ni yenye kufurahisha ulimwengu.

China lake katika Kigriki ni neno GHEY inayomaanisha dunia. 

Kwa hiyo tu neno moja tunapata vile vile neno jiolojia inayoambatana na neno EPI katika Kigriki inayomaanisha YA KIDUNIA SANA ZAIDI, ni hekima inayopatikana katika Yakobo 3: 15. 

Hekima ya kidunia sana zaidi yatoka kwa mapepo ya mashetani. 

Neno la mwisho ni Shetani nalo linamaanisha yanayohusu mapepo wachafu. 

Ni hekima ya mapepo wachafu, na hii neno pepo wachafu inaandikwa kwa sarufi ya kuonesha uwingi. 

Kuna Shetani mmoja na wapepo wachafu wengi.

Wenye kujaa na mapepo wachafu ni wale wenye wanakuwa na hekima ya namna ile. 

Ebu tuchunguze kwanza neno EPI-GHEY. 

Tuangalie namna gani inatumikishwa nafasi nyingine.

Yoana 3: 12 

“Kama nimewaambia ninyi maneno ya dunia na hamuyaamini, mutaamini namna gani kama nikiwaambia ninyi maneno ya mbingu?” 

Bwana Yesu Kristo alimwambia Nikodemu, kwamba: nimekuambia kuhusu maneno ya dunia na haukuniamini, utaamini namna gani kama nikikuambia maneno ya mbinguni? 

Neno  katika Kigriki EPI-GHEY inamaanisha ya kidunia, ya kidunia zaidi, ya hali ya ufalme wa ulimwengu. 

Aliwaambia wawe na haki inayopita haki ya mafarisayo na waandishi, na akawaambia: kama ninawaamia ninyi maneno haya ya kidunia zaidi na ninyi hamuyaamini, mutaamini namna gani kama nikiwaambia ninyi maneno ya mbingu?  


10/ Twakuta mara tena neno hili katika Wafilipi 3: 17 – 19 

“Ndugu zangu, munifuate na mutazame wao wanaotembea kwa kufuata mfano tuliowapa ninyi. 

Maana watu wengi wanatembea, juu yao niliwaambia ninyi mara nyingi, na sasa ninawaambia ninyi hata kwa machozi, ya kuwa wao ni adui za musalaba wa Kristo; 

Mwisho wao ni uharibifu, mungu wao ni tumbo, utukufu wao ni haya yao, wanaofikiri maneno ya dunia.” 

Anasema kuhusu wale walio adui wa Musalaba wa Kristo, wale ambao mwisho wao ni uharibifu, mungu wao ni tumbo zao, na utukufu wao ni haya yao, wanaofikiri maneno ya kidunia zaidi. 

Wanapenda na kutafuta mambo yanayokuwa juu ya yale ya kawaida ya kidunia. 

Watu hawa, katika dunia hii ya sasa, hasa kwa upande wa watu wa dini, wanakuwa wengi sana. 


11/ 1 Wakorinto 1: 21 

“Kwa sababu katika akili ya Mungu, dunia katika akili yake yenyewe haikujua Mungu, ilipendeza Mungu kwa upumbavu wa neno linalohubiriwa kuwaokoa wanaoamini.” 

Twaona hapa hekima ya kimtu, tunasikia hapa kwamba dunia katika hekima yake yenyewe haikujua Mungu.  

1Wakorinto 3: 19  

“Kwa sababu akili ya dunia hii ni upumbavu mbele ya Mungu. 

Kwa sababu imeandikwa: Anakamata wenye akili katika hila yao;”  

Hakuna budi kutarajia  wingi wa hekima. 


12/ Hekima ya kweli yatoka juu. 

Yakobo 1: 17  

“Kila zawadi njema, na kila zawadi timilifu inatoka juu, inashuka kwa Baba ya nuru kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeukageuka.” 

Hekima hiyo siyo ya mtu kawaida, mwenye kuambatana na mtu wake wa zamani. Hekima hiyo inatoka kwa Mungu, inatoka juu.  


Kuna mfano mmoja tunaopata tukiangaziwa na Maandiko ya Matendo ya Mitume 6: 10 

“Lakini hawakuweza kushindana na hekima yake wala na Roho Mtakatifu aliyesema naye.” 

Hapa ni kuhusu Stefano. 

Hawakuweza kamwe kushindana na Hekima ya Roho aliyekuwa akiongoza Stefano kwa kuzungumuza.

Ikiwa nasi vile vile twatamani kuwa na hiyo hekima, twaweza kuipata kutoka kwenye Stefano alipoipata. Toka juu. 


13/ Hiyo hekima toka juu ina tabia nane. 

Tuzitaje moja kwa moja: 

Kwanza, hekima toka juu ni safi. 

Tukio la kwanza la hekima ni usafi, mtu mchafu hata awe na akili kwa mambo mengine, hawezi kuwa na hekima. 

Usafi unachina lake kwenye ufahamu  kichwani, hii ni jambo maalum kweli, ni kwa hiyo mawazo yetu yanapokuwa safi, mafikiri machafu hayapati mahali pa kukaa katika ufahamu wetu. 

Neno hili linatuhusu sote, hatupashwi kuweka mawazo machafu katika mafikiri yetu. 


14/ TABIA MCHAFU 

Wakristo wanapashwa kutupa mbali tabia za namna sawa. 

Kwa hiyo haifai kwa wakristo kuingia katika nyumba ya wageni ama bweni la vinywaji vya kuchacha, vyenye hawapashwi kutumia kwa uwingi ama kwa kukadirisha. Yafaa kujitenga mbali nayo. Nafasi hizo haziongeze hata neno moja kwa usafi.  

Wajibu wetu ni kujiacha wenyewe kuishi siku kwa siku katika utamaduni wa kikristo, hii ibebe sehemu kubwa sana ya maisha yetu. 


15/ LENGO NA MAKUSUDI SAFI. 

Hii ni kiini kinachotusukuma kutenda tendo. 

Tusisukumwe na makusudi ya kujipenda wenyewe, 

Hapana kwa sifa yetu wenyewe, ila kwa kumusifu na kumutukuza Bwana wetu Yesu Kristo. 

1 Timoteo 5: 25 

“Vivyo hivyo matendo mazuri yanaonekana wazi; na yale yasiyoonekana, hayawezi kufichwa.” 

Mtume Paulo, anapoandikia Timoteo, anamusihii kuwa na mwenedo mwema akijichunga katika usafi wa kiroho. 


16/ SALAMA 

Hii ni tabia ama hali ya pili ya hekima. 

Kama mtu mwanamume ama mwanamke ni mugonvi, huyu mtu haoneshi hekima kutoka juu. 

Watu wa namna hii walikuwa wengi katika makanisa ya Wayuda hapo kale, walikua na ushujaa na bidii mbaya, kila mtu akipendelea kujiweka wa kwanza na wa faida kuliko mwenzake, na hii ilileta machafuko na uvuguvugu pahali pa salama. 

Mtu wa salama atafanya yote iwezekanavyo ili avunje uadui, vikwazo, nakujitia mbali na vita na mabishano.  


17/ MPOLE 

2 Wakorinto 10: 1 

“Nami Paulo mwenyewe, ninawasihi ninyi kwa unyenyekevu na upole wa Kristo, mimi niliye mnyenyekevu wakati mimi ni pamoja nanyi, lakini nisipokuwa mimi ni mwenye uhodari kwenu:” 

Ninawasihi ninyi kwa unyenyekevu na upole wa Kristo. 

Ni upole wa namna gani, Bwana wetu Yesu Kristo alikuwa nawo mbele ya Nikodemu, na vile vile mbele ya mwanamuke musamaria mbele ya kisima. 

Bwana Yesu hakuwa mgumu kwa mtu yeyote, ila tu kwa wale mafarisayo katika dini. 

Mtume Paulo vile vile alikuwa mpole. 

1Watesalonika 2: 7 

“Lakini tulikuwa wapole katikati yenu kama mlezi anayetunza watoto wake mwenyewe;” 

Angaliweza kuandika: 

Tulikuwa wapole katikati yenu sawasawa vile mlezi anavyotunza watoto wake mwenyewe. 

2Timoteo 2: 24 

“Na haipasi mtumwa wa Bwana kugombana, lakini kuwa mpole kwa watu wote, anayeweza kufundisha, mvumilivu,”  


18/ MWENYE KUJAA HURUMA 

Ni vema sana kuwa mwenye kuhurumia, lakini, siyo rahisi kuwa mwenye huruma. 

Kuhurumia, sawa vile tunaweza kuwafahamisha, siyo kumurudishia mwengine yale aliyostahili kweli. 

Hii nikusema kwamba wajirani wanaotizama wanaweza kuhitaji wewe uwatendee wale watu kwa ukali na hasira sana ukiwarudishia kisasi, sawa vile wanavyostahili, lakini wewe huwatendei kama vile walivyostahili. 

Umejaa na huruma. 


19/ MATUNDA MEMA.

Neno kujaa inahusu matunda mema na vile vile huruma.  

Na kwa kweli ni mara moja. 

Wagalatia 5: 22, 23 

“Lakini matunda ya Roho ni mapendo, furaha, salama, uvumilivu, neema, wema, uaminifu, 

Upole, kujizuiza; hakuna sheria juu ya maneno ya namna hii.” 

Matunda ya Roho ni mapendo. 


20/ BILA UPENDELEO 

Mtu anayekuwa na hekima toka juu, makusudi yake ni safi, na bila ubaguzi.  

Hatafanya ubaguzi wa kupendelea  mtu moja kati ya kundi. 

Hata baguwa wengine na kupendelea tu wale walio na mali, ama wale walio na ranga ya maisha ya juu kuliko, ama wale wanaojulikana. 

Mtu wa hekima hatakuwa yule anayefanya ubaguzi wa majina akiyaita moja moja kufwatana na wale anaowajuwa kwamba ni wenye kujulikana, akihusika na kuzungumuza tu na wale.  


21/ BILA UNAFIKI 

Mara nyingi tunazani kwamba munafiki ni mtu yule anayejifanya kuwa mukristo na japo yeye hayupo mukristo. 

Yeye anafanya unafiki kwa ajili ya biashara yake ama ranga anayopenda kuwa nayo ili aheshimiwe na kujulikana. 

Ama ili awe mbele ya wengine, katika mambo kazaa.

Lakini, hata waamini wanaweza kuwa wanafiki. 

Kuna wakati waamini wanaweza hata kuhudumia kwa unafiki. 

Tukiwa hazarani, mbele ya watu wote, tunajifanya sawa tunampenda ndugu fulani ijapokuwa kwa kweli ndani ya roho yetu tunamuchukia kupita kiasi, hiyo ni unafiki. 

Tusiwe kama Yuda aliyemubusu Bwana Yesu Kristo na baadaye akamusaliti.  

Kuna wengine wanatenda na kusema sawa watu wakarimu ijapokuwa wao ni wachoyo wakijipenda wenyewe. 

Mtu mwenye hatendi kwa unafiki hawezi kujifanya kuwa mtu mwingine wa tabia isiyokuwa yake.

Unaweza kumwamini sababu anayoyasema ni kweli inayotoka rohoni mwake na hasemi uwongo. 


22/ Twatambua kwamba yatupasa kuwa na hekima toka juu.

Tutaipata kwa njia  ya Neno la Mungu pamoja na woga wa Bwana.  


23/ Neno lingine la muhimu lenye twapashwa kuona lapatikana ndani ya Sura ya pili.  

Mezali 2: 4, 5 

“Kama ukiutafuta kama feza, na kuutafutatafuta kama hazina zilizofichwa; 

Halafu utafahamu woga wa BWANA, na kupata maarifa kwa Mungu.” 

Ni kusema, ni jambo nguvu mno. Siyo rahisi, siye mambo ya wavivu. 

Siyo jambo la watu wanaokumbwa kwa urahisi. 

Kama unatamani kupata hekima, na kwa kweli ni jambo linalotamaniwa na watu wote, yakupasa kujitahidi kweli na kutoa jasho. 

Siyo jambo inayokuja kwa rafla. 

Siyo jambo wanaloweza kukukabizi kwa bure bila kazi yoyote. 

Wapashwa kuitafuta kwa njia ya Neno la Mungu kama mtu anayetafuta hazina zilizofichwa. 


24/ Aya ya 5  

“Halafu utafahamu woga wa BWANA, na kupata maarifa kwa Mungu.” 

Twatambua tena kwamba woga wa BWANA unakuja mbele ya kupata maarifa kwa Mungu. 

Kumjua Mungu haina mafaa kama mtu hamchi Mungu, kama mtu hatembei katika woga wa Bwana. Kumujua Mungu na kumcha Mungu yapashwa kutembea pamoja.   


25/ Tuchunguze yanayosemwa kwa aya ya 6. 

Aya ya 6 

“Maana BWANA anawapa watu hekima; 

Kinywani mwake zinatoka maarifa na ufahamu: “

Ni Mwenyezi Mungu anayetupa hekima tukiwa pia na woga wa Bwana, Kwa kumujua Mwenyezi Mungu kwa njia ya ufahamu tunayopata kwa kujikaza kuchunguza Maandiko Matakatifu kila mara kwa ufahamu, na kwa kufanya yote iwezekanao ili tulipokee Neno la Mungu. 


AMINA. 


N°Ref: 06/01/1980 / 548-2 THE SCHOOL OF WISDOM / 07/18/2021

No comments:

Post a Comment