Tuesday, May 18, 2021

MLEMAVU WA KIROHO / THE SPIRITUALLY HANDICAPPED

Photo by B Smith from the kitchen window


 


MLEMAVU WA KIROHO 

THE SPIRITUALLY HANDICAPPED

August 27, 1978 

Pastor Henry F. Kulp


 

Waefeso 4: 11 – 15 

“Naye alitoa wengine kuwa mitume; na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wahubiri wa Habari Njema; na wengine kuwa wachungaji na walimu; 

Kwa kusudi la kukamilisha watakatifu, kwa kazi ya utumishi hata Mwili wa Kristo ujengwe; hata sisi sote tufikie umoja wa Imani, na kujua sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mzima, hata kufika kipimo cha urefu wa utimilifu wa Kristo; hata tusiwe tena watoto, tukitupwa huku na huku na kuchukuliwa kwa kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, kwa udanganyifu mbaya; lakini tukisema kweli katika mapendo tupate kukua katika maneno yote ndani yake aliye Kichwa, ndiye Kristo.” 

Tunasoma hapa kwamba Mwenyezi Mungu alitugawia zawadi za uongozi kwa kusudi la kukamilisha watakatifu, kusahihisha watakatifu, kwa kusudi la kutengeneza upya watakatifu na kwa kuwaweka tayari kwa Huduma. 

Kwa watakatifu kuwa wenye mafaa na kuwa washujaa katika huduma yao, wanapashwa mara na mara kutengenezwa upya, ni hii inayopashwa kuwa miradi ya msingi wa kila kanisa la fasi. 

Kutengenezwa upya na kurejesha  watakatifu. 

Kila mmoja wetu ana mtu wake wa zamani, kwa hivyo inatupasa mara kwa mara  kusikiliza Neno la Mungu, na ni Neno la Mungu itakayotumika  rohoni mwetu kwa kututayarisha kwa kazi ndani ya Huduma zetu mbalimbali. 

 

1/ Kumbukeni kwamba kila mmoja wetu anatumika kwa kujitoa kwa saa zake zote ndani ya huduma,  na Mwenyezi Mungu anatarajia matunda ndani ya huduma hiyo; twapasha kazaa matunda.  


2/ 2Wakorinto 5: 18 

“Na maneno yote yanatoka kwa Mungu, ambaye alitupatanisha sisi naye Mwenyewe kwa Yesu Kristo, naye alitupa sisi utumishi wa upatanisho.” 

Tunaambiwa hapa ya kwamba tulipewa utumishi wa upatanisho.

 Sisi tunatumika kwa pahali pa Kristo Yesu, tukisihi wanaume na wanawake wapatanishwe na Mwenyezi Mungu. 

Hakuna mchungaji mwenye anaweza kufanya kazi hii binafsi, hata pia muinjilisti hataweza kutimiza kazi hii peke yake. 

Yafaa watakatifu wote wa Mungu. 

Wale wanaokaa kwenye mimbari, hii ndiyo kazi yao. 


3/ 2 Wakorinto 8: 5 

“tena walitenda hivi si kama tulivyotumainia, lakini kwanza walijitoa wenyewe, wakampa Bwana, na sisi vilevile kwa mapenzi ya Mungu.” 

Hii ndiyo aina ya kanisa niliyokuwa nikitarajia kuona muda wa miaka hii yote iliyopita. 

Sababu gani huyu Mwenye Mungu mwenye Nguvu zote alikuwa anapendelea kutumikisha makanisa ya Makedonia? 

Ninaweza kuwaambia sababu gani. 

Tumeiambiwa wazi wazi katika Maandiko haya. 

Ni kwa sababu walijitowa kwanza wao wenyewe kwa Mungu. 

Sasa tazameni maneno yanayosemwa katika aya ya ine

Aya ya 4: 

“wakitusihi sisi na kusihi sana wapate kushiriki neema hii ya kutumikia watakatifu:” 

Kutumikia watakatifu, sababu gani wao waliweza kutumikia watakatifu, kiisha kutolea Mwenyezi Mungu? 

Kwa sababu walijitowa kwanza wao wenyewe kwa Mungu. 

Mutatambuwa ya kwamba neno hili linaelekea mali. 

Hakuna kati yetu mukristo mwenye anaweza kuwa mwenye nguvu, hakuna kati yetu yeye anayeweza kufanya kazi ya Mungu na ushujaa wote, kama yeye hatowi mali yake kwa Mwenyezi Mungu. 

Wale wanaokuwa tu na juhudi ya kuleta ushuhuda mbalimbali lakini wao hawapendi kumtolea Mungu mali yao, sizani kweli kama mbegu wanazo panda zaweza kuwa na nguvu.   

Mara nyingi niliwaza kufanya angalisho na maneno ninayoyasema kuhusu mali, sababu makanisa mengi wanazidi kuzorota kupita kipimo kuhusu matoleo ya mali. 

Lakini, upande mwengine, yafaa mufahamu kwamba Mwenyezi Mungu anahitaji ninyi kumutumikia na mali zenu, na kwa njia hii ya matoleo yafaa mutambuwe kwamba kutowa ni ya muhimu sana kwa kila kanisa la fasi. 

Siwe sawa munakusudia kutowa kwa mipango ya namna yenu na hapo mufanye angalisho musimuibie Mwenyezi Mungu. 

Ni vigume wewe kujitoa mwenyewe kwa Mungu na kukataa kutowa mali yako. 


4/ 2 Wakorinto 9: 6, 7 

“Lakini ninasema neno hili: Yeye anayepanda kwa choyo atavuna kwa choyo; na yeye anayepanda kwa ukarimu atavuna kwa ukarimu.

Kila mtu afanye kama alivyokusudia katika moyo wake: Si kwa huzuni, wala si kwa lazima: kwa sababu Mungu anampenda yeye anayetoa kwa furaha.” 

Mara tena hapa inahusu mali. 

Mwenye kupanda kwa choyo, atavuna kwa choyo, na kwa aya ya 7 inasema:

Kila mtu afanye kama alivyokusudia katika moyo wake: Si kwa huzuni, wala si kwa lazima, lakini sababu wewe mwenyewe ulikusudia   hivyo na unapenda kufanya hivyo. 


5/ Kuna jambo lingine lenye twapashwa kuchunguza: 

Siyo tu kwamba twapashwa kujitoa kwanza wenyewe kwa Mungu na kiisha kutoa mali zetu, lakini kuna aina ya ushirika yenye inapashwa kuwa katikati yetu sisi kwa sisi ndani ya Huduma yetu. 

Moja ya Maandiko yenye nafurahia na kuipenda sana ni katika: 

Kumbukumbu la Torati 20: 19 -20 

“Wakati unapozunguka mji siku nyingi, kwa kufanya vita juu yake upate kuukamata, usiharibu miti yake kwa kupeleka shoka juu yao; kwani utaweza kula matunda yao, wala usiikate; kwa maana mti wa shamba ni mtu hata uuzunguke kwa vita?

Miti unayojua si miti ya chakula utaharibu na kuikata; na utajenga maburuji juu ya mji unaopigana nawe hata uanguke.” 

Hii ni taswuira ya yale kila moja wetu angelihitaji kuona. 

Hata hivyo ni Maandiko yenye mara nyingi inasahauliwa ndani ya Neno la Mungu, bali hapa, Mwenyezi Mungu anazungumuzia Taifa la Israeli akiiambia kwamba: 

Wakati atapozunguka mji siku nyingi, kwa kufanya vita juu yake apate kuukamata, kuna miti fulani  tu ndiyo yenye anaruhusiwa kukata. 

Kwa miti hizo, watajenga maburuji na kuipiga juu ya mji wanaopigana nao ili uanguke, bali hatakata hata mti mmoja unaozaa matunda, miti hiyo ya chakula inapashwa kulindwa. 

Mwenendo wetu wapashwa kuwa namna hiyo mbele ya watakatifu, watu wenye wako sawa kaka na dada katika Kristo, wao wanaokuwa Viungo vya Mwili wa Kristo. 

Sote twahitaji kuwa miti ya kuzaa matunda kwa Bwana Yesu Kristo. 

Twapashwa kuzaa matunda, hatupashwi kuinua shoka yetu juu ya dada na kaka watakatifu, bali, twapashwa kutumika kwa umoja. 

Yamaanisha kwamba hatupashwi kutenda hata tendo moja linaloweza kuhuzunisha mmoja wetu katika Huduma. 

Haifai Huduma ilaumiwe, wala kuzarauliwa. 

Hatupashwi kuwa na masongano mmoja kwa mwengeni bali yatupasa kutumika kwa umoja na kuzaa matunda.  


6/ Matendo ya Mitume 18: 24 -26 

“Basi Myuda mmoja jina lake Apolo, mzalia wa Alesanduria, mtu wa elimu, akafika Efeso; naye alijua sana Maandiko. 

Mtu huyu alikuwa amefundisha njia ya Bwana; na kwa kuwa roho yake ilikuwa ikiwaka, alianza kusema na kufundisha kwa kweli Maneno ya Yesu, naye alijua  ubatizo wa Yoana tu. 

Akaanza kusema pasipo hofu katika sunagogi; lakini wakati Akila na Prisila walipomsikia, walimtwaa kwao, wakamfunulia zaidi njia ya Bwana, aijue kabisa.” 

Hapa twapata mufano wa namna gani yatupasa kutenda mbele ya miti ya Mwenyezi Mungu yenye kuzaa matunda, wale wanaokuwa ndani ya kuhudumia Bwana Yesu Kristo, na hiyo inahusu watakatifu wote. Watakatifu wote wanaohudumia saa kwa saa katika shamba la Bwana. 

Hapa tuna mfano wa Apolo, mwenye, kama munavyokumbuka alichapa kazi ya Mungu bila ziaka na alikuwa anapenda sana Maandiko Matakatifu yaani Neno la Mungu. Matumikio yake iligusa sana mioyo ya Akila na Prisila, bali, mpaka hivyo ufahamu wa Apolo ulikuwa ungali chini ya wenzake katika hudumu kwa siku zile. 

Yeye hakuwa na ufahamu zaidi ya kujuwa kuhusu ubatizo wa Yoane, ni hivyo Akila na muke wake Prisila walivumbuwa ukosefu huwo wa ufahamu na wao walikuwa na upendo kwake, walifahamu kwamba Apolo alikuwa anataka kujuwa Kweli ya Maneno ya Mungu, alikuwa akifanya yote iwezekanavyo ili awe na ufahamu kamili ya Kweli ya Neno la Mungu. 

Ni kwa hiyo Akila na muke wake Prisila, wakiwa watumishi wa Mungu, hawakupenda kumupa Apolo haya kwa kuonesha kutokufahamu kwake azarani mbele ya watu wote, kwa macho ya watu wote na kuonesha kwamba Apolo alikuwa mtu wa kuchunga desturi lakini anayekosa ufahamu kamili katika Neno la Mungu, bali walimuita nyumbani kwao na hapo katika mapendo ya kikristo, walimutwaa kwao, wakamfunulia zaidi njia ya Bwana, aijue kabisa. 

Yatupasa kutumia shoka zetu kwa kukata miti mikavu iliyokufa na zambi, makosa na kasoro mbalimbali pahali pa kujiumiza sisi kwa sisi. 

Yatupasa kutumika mkono mukononi sawa vile Akila na Prisila walivyotumika kwa kusaidia watakatifu wenye wanahitaji kujuwa kweli, hata kama  hadi hapo  hawajaifahamu bado kabisa katika ukamilifu wake. 

Twapashwa kutumika pamoja ndani ya umoja na maelewano.  


7/ Twende sasa kwa aya ya kumi na ine ya Kitabu cha Waefeso sura 4 

Waefeso 4: 14 

“hata tusiwe tena watoto, tukitupwa huku na huku na kuchukuliwa kwa kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, kwa udanganyifu mbaya;” 

Nilitaka kuonesha  taswira ya tofauti. 

Kwa aya ya kumi na tatu, inatuonesha wakristu wanaokomaa. 

Kwa aya ya kumi na ine, inazungumuza kuhusu watoto. 

Ili tusiwe kama watoto

Anamaanisha nini wakati anasema kwamba tunakuwa sawa watoto wadogo? 

Kwa kweli, neno inayotumiwa hapa siyo “mtoto mudogo” lakini “utoto”, kufanya mambo ya kitoto. 

Mutume Paulo yuko akisema kwamba wamoja wa wakristo wa Efeso walikuwa wakifanya mambo ya kitoto. 

Tuchunguze kwa makini jambo lile na tufikiri kuhusu maana yake. 


8/ Neno mtoto ni NAY – PEE – OSIS pia twapashwa kufanya tofauti ya neno linalotumikishwa kwa nyakati tumeokolewa na hiyo ni neno katika kigriki BREATH – OSIS inayosema kuhusu mtoto mchanga anayenyonya kwa maziwa ya mama yake, na wakati unapokomaa kama ipasavyo utageuka kuwa WEE – OSIS, mwamini anayekomaa, mtu mzima.   


9/ Maana ya neno NAP – PEE – OSIS? 

Ni mtu mwenye kwenda pembeni, mwenye kuambatana na njia ya huduma yenye iko umbalimbali na mapenzi ya Mungu. Ni mtu mwenye anaacha kutumika kwa maongozi ya Mungu. Ni mwamini MPUMBAFU KIROHO. Mtu mwenye kurudi tu nyuma, hana maendeleo yoyote.  


10/ Kuna mambo matatu yanayoelekea huyu Mpumbafu wa kiroho  

Maandiko katika aya hii yawaita kwanza wapumbavu, kiisha yawataja kuwa vimelea walemeao wengine, wabaradhuli, wenye kumumunya.  


11/ Tuchunguze sasa tabia tatu inayoambatana na mwamini wa kitoto, mwamini asiyekomaa.


(1 Ni misemwa na mawazo ya watu wanaozoeya maji katika maziwa makuu: TUKITUPWA HUKU NA HUKU NA KUCHUKULIWA hii inatamkwa kwa neno moja katika Kigriki CLUE – DOUGH – NEEDS – O – MY na kwa kweli neno hili linamaanisha nini? INATUMIKISHWA KWA MASHUWA YENYE HAIWEZI KUONGOZWA KAMWE ILA ZORUBA PEKEE NDIO INAIKUMBA MAHALI INAYOPENDA. Kumbukeni wakati mashuwa haikuwa na mashini ya kutembeza ama injini sawa na siku hizi. Yote ilifwatana na namna ya kutumia hema kubwa la hewa, nanga,  usukani(uongozi), hapa ni picha ya mashuwa yenye uongozi yake ilivunjika na mlingoti wa hema ukivunjika, ni kwa sababu hiyo mashuwa inakumbwa kumbwa na zoruba. Kichwa ya mashuwa kinabebwa katika ngambo yote iwezekanavyo na mashuwa iko katika hatari kubwa MASHUA INAYUMBA YUMBA.


(2 Tukumbuke ya kwamba tunazungumuza juu ya mwamini. Mwamini anaye yumba yumba, na kweli wewe wajiuliza eti mwamini anaweza yumba yumba? Mara kwa mara mwamini anaweza kuwa katika hali hiyo, na wakati anapita katika mapito haya, maisha yake ya kiroho inazorota sana, yeye iko anatafuta kitu moja na hakipati, yeye ni mwenye kutafuta kitu kigeni kwake chenye bado kujua. 


(3 Tunapata neno lingine lenye watu wanaotumika kwa mashuwa ya maziwa makuu wanatumia: NA KUCHUKULIWA KWA KILA UPEPO WA ELIMU, kuchukuliwa huku na huku katika tafsiri la Kigriki ni PERRY – FUR – O  NA HII HAIMAINISHE KWAMBA MASHUWA IKO YENYE HAIONGOZWI TENA ILA ZORUBA PEKEE NDIO INAYOIKUMBA KUHU NA HUKU, BALI INAMAANISHA KWAMBA MASHUWA INAKUMBWA TU NA UPEPO. Katika hewa kali yenye kuchafua maji inayotoka inje ya ziwa, kuna vitu viwili vinavyo sababisha kuleta woga ni: Zoruba na Upepo. Na hapo, ni upepo ndiyo unayoletea waamini shida. Hii inamaanisha nini? Ni upepo wa elimu na kusema kweli siyo elimu safi ya musingi. Mwatambuwa kwa kweli kwamba waamini wenye wako walemavu kiroho, wao hawakomae katika Elimu ya Biblia, wao wanadanganywa na kukumbwa na elimu ya mapepo wachafu. Yawezekana iwe mapepo ya kuishi kijamii ama kisosialismi, yaweza kuwa ya kukumba watu kunena kwa lugha mupya, yaweza kuwa ya uponyaji.                                 

1Timoteo 4 : 1 inasema “Basi, Roho anasema waziwazi ya kwamba katika nyakati za mwisho watu wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho za kudanganya, na mafundisho ya mashetani,”  sawa ginsi tulivyo wafundisha kila mangaribi ya siku ya Mungu, tukiwaambia kwamba mashetani hawawezi kamwe kuishi ndani ya mwamini, lakini wakiwa inje wanaweza kuchochea mafikiri na mawazo ya mwamini kwa njia ya elimu mbalimbali, wanaweza kumukumba katika mafundishi ya uharibifu. Na tabia ya mafundisho yale ni nini? Ni mafundisho yenye madara, yakuumiza. KUCHANGAMUSHA NA KIVUMBI TELE IKIWA NA CHUMVI NA RAHA NA UREMBO WA UDANGANYIFU. Hamuja ona bado namna gani shetani anachamusha hali hiyo, muangalie hayo makani madogo madogo ya uwongo yenye yanaota siku hizi kama uyoga, yote yanatabia moja yanajaa na kuchangamusha na kivumbi tele na chumvi na raha na urembo wa udanganyifu.


(4 Tunafikia sasa fumbo la tatu, na hapo tunakuwa na mawazo kuhusu muchezo wa kura, yaani mchezo wa kubahatisha. Hakuna mpumbavu mkuu katika dunia hii kushinda yule mtu anayejitowa kucheza michezo ya kubahatisha na katika michezo yale, mtu mwengine ndiye anaye mupigia kura.  Mtu mwengeni ndiye anayeshika kete kwa kuimwanga kwenye meza ya michezo na yo ita zunguka kwenye saba ama kumi na moja na mtu huyu anayechaza hataweza kamwe kufaulu. Atapoteza hata shati yake. Ni vigumu sana kufahulu kama kwa michezo ya kura ni mtu mwengine anayeshika kete.


(5 Mwamini mwenye ni mlemavu kiroho hawezi kamwe kufaulu. Yeye ni mwenye kungojea tu miradi ya kuchangamusha na kivumbi tele na  vukuto ya chumvi na raha ya udanganyifu yenye mashetani wanaoleta, mtu huyu atakuwa mnyonge wa mwisho hapa chini duniani. Mtu asiiyeokaka siyo yeye aliye mnyonge wa mwishi hapa duniani, bali ni mwamini mwenye anayetembea inje ya Mapenzi ya Mwenyezi Mungu.  


12/ Kwa kweli mutajiuliza: Ni wapi nitowapo mambo haya yote? 

Neno udanganyifu katika Kigriki ni KOO – B – AH na inamaanisha mchezo wa kura na kete yenye inahusu kweli mchezo wa kura na kete inayochezwa na watu

Twaweza kujiuliza, eti watu hawa wanacheza mchezo gani? 

Kwa kweli ni mchezo gani wachezao? 

Shetani ni mdanyanyifu, ni mkorofi. 

Dini yake ni ukorofi na michezo anayoyacheza ni michezo ya kidunia, UDANGANYIFU, UKOROFI WA WATU. 

Tafsiri kwa Kigriki ya haya mambo ni PAN – OORG – EÉ – AH, inayomaanisha KUFANYA UKOROFI KATIKA MCHEZO WA KURA.

Ni kusema kwamba wapumbafu hawa wa kiroho wenye hawaguwi kamwe katika BWANA, hawategemee hata Elimu moja na mbio wanaanguka na kutegwa  nyara kwa Mafundishi na elimu ya mashetani, na hapa tunaambiwa kwamba dini yao yote ni mchanganyiko wa kete mtupu na Mchezo wa kura na kete. 

Kwa mchezo huo hautaweza kamwe kufaulu, wewe unatarajia tu kushindwa. 


13/ Tunafikia neno kwa njia ya, na huo ni rafiki wetu wa kale, rafiki wetu wa zamani SIFA NA MCHONGEZI na hii ni kusema ANA KWA ANA.


14/ Ana kwa ana na nini? 

Biblia Takatifu, tafsiri ya King James, yasema, 

Wakingojea na kusimama kwenye zamu wakichungana na, na msemwa huo ni msemwa wa wataalam, METH – O – DOS. Kwenye neno MBINU yotokea.  


15/ Kiisha kuna neno ujanja ni neno lenye katika Kigriki ina tafsiri la Ukorofi. 

Kwa hiyo, nini inayofikia mwamini mwenye kuishi inje ya Mapenzi ya Mwenyezi Mungu? 

Asiye jifunza Elimu ya Biblia na pia haiishi katika maishani mwake? 

Yeye anaangukia ana kwa ana kwa mbinu ya ukorofi inayo potosha, ni kusema kwamba anageuka tu mtu wa dini. 


AMINA 


N° Ref: 08/27/1978 / 438-2 THE SPIRITUALLY HANDICAPPED / 05/18/2021

No comments:

Post a Comment