Saturday, June 12, 2021

KWA WANAUME PEKEE / FOR MEN ONLY

Photo by B Smith from the patio


 


244 - KWA WANAUME PEKEE  /  FOR MEN ONLY

March 25, 1962 

Pastor Henry F. Kulp



 

1 Timoteo 2: 9 -15 


“Na vivyo hivyo wanawake wajipambe kwa mavazi yanayofaa, pamoja na adabu na moyo wa kiasi, si kwa kusuka nyole, wala kwa zahabu na lulu, wala kwa nguo za damani; 

Lakini kwa matendo mema, kama ilivyopasa wanawake wanaokiri kuogopa Mungu. 

Mwanamuke ajifundishe katika kimya akitii kwa kila namna. 

Lakini simpi mwanamke ruhusa kufundisha, wala kutawala mwanamume, lakini kukaa kimya. 

Kwa maana Adamu aliumbwa kwanza, halafu Hawa. 

Na Adamu hakudanganywa, lakini mwanamke akidanganywa, aliingia hali ya kukosa. 

Lakini ataokolewa kwa kuzaa mtoto, kama wakidumu katika imani na mapendo na utakatifu pamoja na moyo wa kiasi.” 

Mtume Paulo anatatua hapa mambo yanayoelekea wanawake katika makanisa, na  kuanza, anazungumuza kuhusu mavazi ya mwanamke, namna gani yampasa mwanamke kuvaa, baadaye analeta vizuizo viwili kuhusu mwanamke ndani ya makanisa. 

Kwanza, mwanamke hastaili kufundisha wanaume Biblia. 

Ya pili, mwanamke hastaili kutawala juu ya wanamume. 


1/ Tunapata sababu ya kwanza katika aya ya kumi na tatu. 

“Kwa maana Adamu aliumbwa kwanza, halafu Hawa.” 

Ni matatizo ya kujiuliza sababu yake Mwenyezi Mungu kuumba Adamu na Hawa, kuumba mwanaume na mwanamke, mwanaume aliumbwa wa kwanza kama malighafi, kama kitu kikuu, kama mambo kiongozi, mwanaume anapashwa kuwa kwa nafasi ya kichwa. 

Tuchunguze yanayosemwa katika: 


Mwanzo 2: 18 


“Bwana Mungu akasema: Si vema mtu awe peke yake; nitamfanyia msaidia anayefaa kwake.” 

Bwana Mungu akasema kwamba si vema mtu awe peke yake.

Atamfanyia msaidia anayefaa kwake. Hii inamaanisha kusema msaidizi. 

Nafasi ya mwanamke katika maisha ya siku zote ni kukamilisha sehemu iliyokosa kwa mwanamume, kwa hivyo haifai mwanamke kunungunika nungunika kwa kuwekwa kwa nafasi hiyo, kwa sababu ni nafasi hiyo ndiyo aliyopewa na Mwenyezi Mungu, na nikwa hiyo nafasi ndipo anakuwa na furaha. 


2/  Tutambuwe sababu ya pili yenye kueleza sababu gani Mwenyezi Mungu hamruhusi mwanamuke kufundisha mwanamume Biblia ama kuwa na uwezo juu ya mwanamume. 

Adamu hakudanganywa, bali ni mwanamke aliyedanganywa. 

Yaonekana kuwa sawa umbalimbali na kawaida. 

Adamu hakupotoshwa kwa kudanganywa? Biblia yasema HAPANA. 

Yeye alifanya zambi mecho yake yakiwa wazi kabisa. 

Shetani alimjaribu Hawa moja kwa moja, lakini hakuweza moja kwa moja kumjaribu Adamu. 

Kama vile tulivyosema mbele, Adamu alifanya zambi mecho yake yakiwa wazi kabisa. 

Adamu alijuwa ni nini aliyokuwa akitenda, lakini Hawa hakutambua. 

Hawa, yeye alipotoshwa. Aliamini yale shetani aliyokuwa akimwambia. 

Shetani, akija kwa sura ya nyoka alimwambia Hawa: “Kama ukila ya tunda ya mti huu utakuwa na hekima, utakuwa sawa Mungu, utakuwa Mungu.” 

Utakuwa na ufahamu juu ya mambo yote, na kama unavyojuwa, Hawa aliamini mambo yale Shetani aliyomuambia. 

Adamu hakumwamini Shetani, alikuwa akimjua vizuri. 

Alijuwa kwamba ni uwongo mtupu. Hawa alipotoshwa. 

Alitwaa tunda na akampa Adamu, Adamu alichukuwa tunda toka mkono wa Hawa, na Adamu alikuwa mwenye kujuwa lile alilokuwa akitenda. 

Alifahamu, akiwa mecho wazi, kwamba alikuwa akimukosea Mwenyezi Mungu. 

Ni kweli, Adamu alikuwa mwenye makosa, lakini alikuwa anatenda haya yote kwa kumuokoa mke wake. 


Waroma 5: 14 

“Lakini kufa kulitawala tangu Adamu mpaka Musa, hata juu ya watu wote wasiofanya zambi kama alivyofanya Adamu, aliye mfano wake yeye atakayekuja.” 


3/ Adamu alijitoa peke yake ili aokowe mke wake, ni kwa hiyo Mwenyezi Mungu alimuweka mwanamke kwa nafasi ya kunyenyekeza.  


4/ Bali, tukumbuke kwamba mwanamke anaweza kuwa na huduma.

Siyo katika kusanyiko ya hazarani kanisani. 

Siyo kwa kufundisha wanaume Biblia ama kuwa na mamlaka juu ya wanaume, bali mwanamke anakuwa na wajibu wa kuizungumuzia katika mazungumuzo ya upekee. Acheni niwaletee mwangaza kuhusu jambo lile kwa mwangaza wa Maandiko Matakatifu ndani ya Kitabu cha 

Matendo ya Mitume 18: 24 – 26 

“Basi Myuda mmoja, jina lake Apolo, mzalia wa Alesanduria, mtu wa elimu, akafika Efeso; naye alijua sana maandiko. 

Mtu huyu alikuwa amefundisha njia ya Bwana; na kwa kuwa roho yake ilikuwa ikiwaka, alianza kusema na kufundisha kwa kweli maneno ya Yesu, naye alijua ubatizo wa Yoane tu.

Akaanza kusema pasipo hofu katika sunagogi; lakini wakati Akila na Prisila walipomsikia, walimtwaa kwao, wakamfunulia zaidi njia ya Bwana, aijue kabisa. ” 


5/ Inaonekana wazi kwamba Apolo hakupata mafundisho ya kuongeza elimu ya sayansi ya  Biblia katika Mashule Makuu ya kiteolojia, ama kwa njia ya mwongozi moja mkuu wa dini, wa nyakati zile, bali alipata mafunzo yake kwa njia ya wasani wawili, mmoja wao akiwa mwanamke. Hii ni yenye kuvutia sana. Yaonesha namna gani Mwenyezi Mungu anaweza kutumia mwanamke.  


6/ Mara tena kazi hii wasani wale wawili wa Mwenyezi Mungu, kazi  waliofanya kwa KRISTO, siyo tu kwa shairi lilo pekee ndipo inapotajwa. 


1 Wakorinto 16: 19 

“Makanisa ya Asia wanawasalimu ninyi. Akila na Prisila wana wasalimu ninyi sana katika Bwana, pamoja na kanisa linalokutana ndani ya nyumba yao.”

7/ Aina ya walimu mwenye Mutume Paulo alikuwa anafikiria katika Maandiko haya yanatajwa katika Kitabu cha 

Waefeso 4: 11 

“Naye alitoa wengine kuwa mitume; na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa Wahubiri wa Habari Njema; na wengine kuwa wachungaji na walimu,” 

Ni wanaume ndiwo wanao hudumia  ndani ya huduma hizo zote,  kuna vikwazo kazaa kuhusu wanawake wanaohudumia kwa nafasi hizo, hiyo siyo kwa ajili ya kuleta mazarau juu ya wanawake ama kuwafezeesha, hii haifanye mwanamuke kuwa mwenye hana faida, bali Mwenyezi Mungu anakuwa na nafasi alilotayarisha juu ya mwanamuke, na nafasi yake siyo ya kukamata ofisi za madaraka. 


8/ Mutatambuwa kwamba wanawake wanakuwa wakiwekwa katika hali hiyo, sababu Hawa alishindwa  kuchunga na kubaki imara kwa  zamu yake. 

Hiyo ndiyo sababu ya pili. 

Waweza kusema hiyo siyo haki, kitu gani kilicho fikia Hawa, eti yeye hangaliweza kukumbuka kuwaza kuhusi sisi? 

Lakini, ni  hivyo alivyotenda. 

Tukumbuke kwamba Waroma 5: 12  inasema:  

“Hivi, kama kwa mtu mmoja zambi iliingia ulimwengu.” 

Sisi sote ni watendazambi kwa leo, na zambi ilikuja juu yetu sisi sote kwa njia ya Adamu, na sote tunakufa kwa sababu ya zambi ya Adamu. 

Waweza kujiambia kwamba hiyo siyo haki. Mwenyezi Mungu hakukuuliza neno. 

Ni kwa namna hivi ndivyo Mwenyezi Mungu alivyotatua jambo lile, kwa njia ya Adamu sote tulifanya zambi na sote tunakufa. 

Tutambue ya kwanza kwamba: 

1 Wakorinto 15: 21 yasema: 

“Maana kwa kuwa kufa kuliletwa na mtu.” Na kwa Aya ya 22 twasoma:

“Kwa sababu kama katika Adamu wote wanakufa,”

Wanadamu wanaweza kuwa hawafurahiye jambo hili, bali hiyo ndiyo kweli na hakika kuleta mapinduzi juu yake haitabadirisha hata nugta moja. 

Ni vivyo hivyo kuhusu wanawake, mwanamke anaweza kujiletea mawazo ya mapinduzi na kusema kwamba yeye hawezi kamwe kugandamizwa kwa sababu Hawa alipoteza nafasi yake na kuanguka, lakini mwanamke atadumu tu katika hali hiyo na Mwenyezi Mungu ahakikisha kwamba ni hivyo. 

Na neno njema lipaswalo kufanya ni kuheshimu na kuitika hiyo nafasi iliyo mapenzi ya Mwenyezi Mungu na kuwa  mtu ambaye aliye sawasawa na mapenzi ya Mwenyezi Mungu na kuheshimu Maandiko yake Matakatifu na ni kwa njia hiyo ndipo utakapofanyikiwa. 


9/ 1 Timoteo 2: 15    

“Lakini ataokolewa kwa kuzaa mtoto, kama wakidumu katika imani na mapendo na utakatifu pamoja na moyo wa kiasi.” 

Hii haimaanishi kusema kwamba mwanamke fulani anaokolewa sababu alizaa mtoto, bali, ameokolewa kwa njia ya kuja kwa Mbegu la mwanamke. 

Mbegu hiyo ni Bwana wetu Yesu Kristo aliyeleta Wokovu.  


10/ Tutambue pia kwamba 1 Timoteo 3: 1 yasema: 

“Na neno hili ni la kweli: Kama mtu akitaka kazi ya mwangalizi, anataka kazi nzuri,” 

Jina Bishop inayomaanisha jina Mzee, ni jina Mwangalizi. 

Katika Agano Jipya hatuja jali kuona namna ya mamlaka watu wanaokabizi wa Bishop kwa siku za leo. 

Mtu anayekuwa na ranga fulani na nafasi ya heshima sana katika kanisa pia akiwa na mavazi maridadi ya namna ya kanzu. Kwa kweli hiyo haiambatani na Biblia. 

Jina Bishop inayo maanisha Mzee, inaonesha tu mtu anayetaka kujitoa mwenyewe kwa kazi ya kuhudumia maneno ya kanisa. 

Kwa kufahamu maneno haya, kwanza twapashwa kutambua kwamba mafundisho yanayoletwa kwa siku za leo kuhusu viongozi wa dini, kuhusu ranga na mamlaka katika makanisa ni machukizo kwa Mungu. 


11/ Jameni muniruhusu niwaoneshe jambo inayojulikana zidi ya Viongozi wa kanisa. 

Ndani ya hayo makanisa saba yanayotajwa katika Maandiko ya Kitabu cha Ufunuo wa Siri sura ya pili na sura ya tatu, na ndani yake tunachukuwa lile kanisa la tatu lililo kanisa la Pergamo(Aya ya 12). 

Tutambuwe kwamba Ufunuo wa Siri 2: 15 inasema kwamba: 

“Vivyo hivyo wewe una watu wanaoshika mafundisho ya Wanikolayi.” 

Jambo inayokuwa machukizo kwangu. 

Katika kanisa hili kuna Kawaida ya Mafundisho ya namna mbili inayofahamika: Mafundisho ya Baalama na Mafundisho ya Wanikolayi. 

Kawaida ya mafundisho ya Baalama inafundisha kuvumiliana.

Baalama alikuwa anatiya waisraeli moyo wachangane na mataifa mengine za wapagani na hii ilisukuma waisraeli wapoteze hali yao ya Taifa lililopendelewa.

 Mafundisho ya wanikokolayi inamaanisha kutawala juu ya Taifa fulani.

Ni sawasawa na viongozi wa makanisa wanajiweka kando, mbali na watu wengine wa kidunia. Ningelitamani mufahamu kwamba Mwenyezi Mungu anachukia mambo yale. Mawazo yale yanakuwa machukizo mbele ya Mungu. 

Usomapo Ufunuo wa Siri 2: 6 

“Lakini una neno hili, ya kuwa unachukia matendo ya Wanikolayi, ambayo mimi ninayachukia.” 


12/ Tujaribu kuambatanisha aina ya wa Bishop ama Waangalizi, katika makanisa zetu, kufwatana na Maandiko ya aya ya 2, ya 1Timoteo sura 3   (1 Timoteo 3: 2). 

“Basi imempasa mwangalizi asiwe na laumu, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi, mwenye akili, mtu wa utaratibu, mkaribishaji wageni, mwenye kujua kufundisha.” 

Maelezo haya yaonesha kwamba huyu mtu anayetajwa hapa ni mtu mwenye maadili ya juu sana. 

Ni maelezo yenye kwa kweli ni vigumu kuyatimiza.  

13/ Mutatambuwa kwanza kwamba ni hiyo ndiyo kiini cha matarajio bora. Kweli hatupashwi kungojea hali hiyo ijifanye yenyewe bila kujitowa kwetu sisi, bali yapashwa kujitoa na kuamuwa kupiga mwendo ulio bora.

Hiyo ndiyo inapashwa kuwa shauku la moyo wetu. 

Twapashwa kutarajia hali hiyo kwa roho yetu yote bila kuzubaa. 

 

Neno la kwanza ni kwamba mtu huyo anapashwa kuwa bila laumu. 

Inamaanisha  mtu asiye laumiwa. 

Huyu Mzee ama Mwangalizi anapashwa kuwa mtu mwenye hawezi kushotwa kidole cha mashitaka hata kwa mtu mmoja. 

Ni kweli kwamba watu watapendelea kumuchongea Mwangalizi, bali, mashitaka yao yanapashwa kuwa bule pasipo msingi yoyote, na bila ushahidi wowote. 

Watu watakushitaki wakikusingizia mambo kazaa na kazaa. 

Kila yule anayesimama imara katika njia ya Mungu atasingiziwa tu.

Lakini mashtaka haya ya watu mbalimbali yakasimama na kuwa kweli na kuwa na ushahidi, itabidi uangalizi wa huu mtu ukomeshwe, asiwe tena Mwangalizi. 

Bali imetupasa kukataa na moyo wetu wetu kusikiliza uvumi ama mambo ya aina ya kutetana. 

Twapashwa kujielekeza na kuvutwa na mambo yaliyo na ushahidi. 


14/ Mume wa mke mmoja. 

Tumefikia sasa jambo lenye linaleta shida na uvuguvugu nyingi kwa kanisa. 

Jambo hilo lamaanisha nini? 

Mume wa mke mmoja? 

Kuna wao wanaosema kwamba hapashwi kuwa na wanawake wengi pamoja. 

Wengine wanasema kwamba, kama mke wake akifariki, huyu mtu anapashwa baki bila kuowa mara tena. 

Wengine wanasema kwamba mtu mwenye hana bibi hapashwi kuwa Mwangalizi wa kanisa; na kwa kweli hiyo siyo kweli. 

Tafsiri lake kufwatana na namna inavyoandikwa nikusema: MWANAMUME WA MWANAMKE MMOJA, yenye tunaweza kutafsiri kama ifwatavyo: AINA YA BWANA MWENYE ANA MKE MOJA. 

Ni kama aina ya imbwa iitwao Mchungaji-Ujermani, inakuwa ya mtu mmoja tu peke yake(Bwana). 

Nina imbwa wangu anayeitwa Apache ni Mchungaji-Ujermani, wengi wanamuita Imbwa-Polisi. 

Ni umbwa wa mtu mmoja pekee, waweza kupenda kumulea, waweza kupenda kumushurulikia, mambo haya yote hayamwambiye kitu. 

Umbwa ule unatii tu mtu mmoja katika jamii nzima. 

Katika jamii nzima umbwa huu unatambuwa  na kuheshimu mamlaka ya mtu mmoja tu ndani ya jamaa nzima. 

Hiyo ndiyo maana ya yale yasemwayo hapa. 

Ni mwanaume anayekuwa na mwanamke moja tu kama bibi yake. 

Eti haya yote yamaanisha nini? 

Hii aimaanishi kwamba mtu mwenye bado kuowa hawezi kuwa Mzee wa kanisa ama Mwangalizi. 

Neno lenye twapashwa kukumbuka ni kwamba, kama tukijaribu kurudi nyuma kidogo, wakati Mtume Paulo alikua akiandika Waraka huu, watu hawa walikuwa wakitokea moja kwa moja kwa maisha ya Kipagani, kwenye zambi ya uzinzi ilikuwa ikivuma sana. 

Kitu watu waliona kufanya ilikuwa kusoma tu Agano Jipya ili wapatekujuwa maagizo kuhusu uzinzi, pepo ya uzinzi ilikuwa kwa eneo zote. Ilikuwa jambo la muhimu sana kukataza kuwa na wake wengi.

Kama mtu mwenye kuwa na wake wengi alifikia kubadilika na kuokoka, mtu huyu hakuruhusiwa  kuwa Mzee ama  Mwangalizi. 

Na ninafahamu vilevile kwamba mtu hakuwa mwaminifu kabisa kwa mke wake, mtu huyu hakustahili kuwa Mzee ama Mwangalizi. 


15/ Anapashwa kuwa macho wazi, maana yake mwenye asiye zorota, mwenye kiasi maana yake akiwa na umakini, mwenye akili, Mzee wa kanisa ama Mwangalizi anapashwa kuwa mtu wa mwenendo safi, siyo tu kwamba anapashwa kuwa na usemi ulio bora, lakini zaidi mwenendo wake unapashwa kuwa bora zaidi. 

Mzee wa kanisa ni mtu anayeishi siku kwa siku akiambatana na mahubiri anayofundisha, mtu wa utaratibu, mkaribishaji wageni, neno mukaribishaji wageni inamaanisha kuwa mufurahifu na roho nzuri na wageni. Inamaanisha kukaribisha wageni nyumbani mwake, yaani nyumba yenye inakuwa mlango wazi kwenye wageni wakaribishwa. 


16/ Mwenye kujua kufundisha.

 Mzee wa kanisa anapashwa kuwa mwalimu. 

Mwenye kujua kufundisha inamaanisha, siyo mwenye kujitoa kufundisha, ama mwenye kujaribu kufundisha, bali mwenye kuzama katika Maandiko Matakatifu, mwenye kuwa na werevu wa kufundisha. 

Pia, Mzee wa kanisa hapashwi kupenda vinywaji vya pombe, si mtu wa kulewa na mvinyo, si mpigaji. 

Si mtu wa ugonvi, wazo tunalo hapa ni mtu mkali mwenye fujo ya ugonvi, mwenye machokozi na vikwazo iwe kwa mikono yake ama kwa ulimi ama masemo yake. 

Ulime wa watu wengine una sumu ya kuuwa, unaweza kuumiza na kusambaza. 

Kuna watu wengi wanaweza kuwa watenda maovu, wenye kukwazisha wengine kwa njia ya ulimi wao. 

Mwangalizi anapashwa kuwa mtu anayefanya angalisho kwa matumizi ya ulimi wake. 


Watu wanaoweza kumiliki vinywa vyao, wapole, watu wanaochunga vema nyumba zao, wenye hawahubiri kufwatana na tamaa yao ya feza ama mwenye kutamani. 


Feza siyo kabisa mbaya. 

Kuna watu wengi wenye mali, lakini wao ni watu wa Mungu. 

Abrahamu wa Agano la Kale alikuwa mtu mwenye mali sana, lakini pia alikuwa mtu wa Mungu. 

Inakuwa shida sana kama muhubiri anakuwa tu akitia mkazo kwa maisha ya kila siku, akitia mkazo tu kwa feza. 


Hiyo inakuwa sawa anasa ya kupenda feza, na kuwa huduma yenye Bwana hawezi kamwe kubariki. 

Kweli mahamatisho ni yenye maana katika kupanga miradi. 

Lakini yafaa kuchunguza kama makusudi yetu ni bora na nzuri katika mipango za njia zenu zote na hasa huko mbele kwa mazabau. 


AMINA. 


N°Ref: 03/25/1962 / 244 - FOR MEN ONLY / 06/12/2021  

No comments:

Post a Comment