Sunday, September 20, 2020

WOKOVU WAKO WAKUTEGEMEA WEWE? / DOES YOUR SALVATION DEPEND ON YOU?

Photo taken by B Smith from the kitchen door



 


WOKOVU WAKO WAKUTEGEMEA WEWE?

DOES YOUR SALVATION DEPEND ON YOU?

June 26, 1977 

Pastor Henry F. KULP



 

Wakolosayi 1: 20 – 23 

“na kwa yeye kupatanisha vitu vyote kwake, akiwa amefanya salama kwa njia ya damu ya msalaba wake; kwa yeye, kama ni vitu duniani au vitu mbinguni. 

Nanyi, muliotengwa mbali zamani na mulikuwa adui katika nia zenu, kwa matendo yenu mabaya, amewapatanisha ninyi sasa katika mwili wa nyama yake, kwa kufa kwake, ili awalete ninyi mbele yake, watakatifu na pasipo kilema, wala laumu; kama mukidumu katika imani, mukiwekwa juu ya msingi na kusimama imara, wala hamugeuzwi mbali na tumaini la Habari Njema muliosikia, iliyohubiriwa katika viumbe vyote chini ya mbingu; nami Paulo nilifanywa mtumishi wake.”  

Aya ya 22 inasema:

“Katika Mwili ya Nyama yake, kwa Kufa kwake, ili awalete ninyi mbele yake, watakatifu na pasipo kilema, wala laumu;”

Mungu anatuambia kwamba sisi tu watakatifu na pasipo kilema, wala laumu mbele yake. 

Sitambue ingine aya ya raha na utukufu kama hii katika Biblia, na mambo haya yote ni kweli sababu KRISTO alikufa kwa sababu yetu. 

Pia wakati tuendapo kwa aya ya 23, tunaona kwamba neno la kwanza linalokuwa kwa mwanzo wa aya hii ni “kama”, kiisha palepale inatushimamisha kwa gafla. 

“kama mukidumu katika imani, mukiwekwa juu ya msingi na kusimama imara, wala hamugeuzwi mbali na tumaini la Habari Njema muliosikia, iliyohubiriwa katika viumbe vyote chini ya mbingu; nami Paulo nilifanywa mtumishi wake.”   

Kuna wale wanaojidanganya wakizania kwamba aya hii inasema kwamba mtu aliyeokoka anaweza kutereza na kuanguka na kufikia kiwango cha kupotea.  Hii ni uwongo.

Hii siyo maana yenye Mutume Paulo analeta katika aya hii. 

Mutume Paulo hafundishi Kawaida ya Mafundisho mawili mbalimbali ya utunzaji yenye kubishana na kukanushana kabisa. 

Kama kwa upande moja anafundisha Amani ya milele na uhakika wa kuwa na Uzima wa milele, kwa upande ungine, hawezi kufundisha uwezekano wa kuanguka hadi kupoteza wokovu. 

Na tunafahamu bila shaka yoyote kwamba Biblia nzima inatufundisha kuhusu Amani ya Milele, Uhakika wa Wokovu ya milele,  Salama ya milele na ina ya fundisha wazi wazi. 

1/ TUFAFANUE AMANI YA MILELE AMA SALAMA YA MILELE AMA UHAKIKA WA WOKOVU YA MILELE. 

Wale ambao Baba Mungu aliwakaribisha na kuwakubali katika Mwana wake Mupendwa aliwaita na kuwatakasa katika ROHO MUTAKATIFU hawawezi kamwe kuanguka milele ama kuanguka kwa mwisho toka neema ya Mungu, wao watakaza mwendo mpaka mwisho wakiwa na wokovu wa milele.


2/ Huu ufafanuzi unakuwa na musingi wake katika aya mbalimbali za Biblia Takatifu.

Tuchunguze kwanza maandiko katika Waebrania 7: 25

Waebrania 7: 25 

“Naye, kwa sababu hii anaweza kuokoa kabisa wao wanaokuja kwake Mungu kwa njia yake; maana yeye ni hai siku zote apate kuwaombea.” 

Tambua kwamba aya hii haiseme tangu mwisho, lakini inasema mpaka mwisho hivi tutaisoma namna ifwatayo: 

NJIANI MWOTE SIKU ZOTE HADI MWISHO. 

Kuna wale wanaozania kwamba Amani ya Milele ama Salama ya milele ni hiyo kudumu ya watakatifu ama waamini, lakini hiyo si kweli.

Siyo waamini wanaoweza kudumu na kusubiri. 

Ni Mungu anayedumu na kusubiri ndani ya watakatifu.

 

Waroma 6: 23  

“Kwa maana mushahara wa zambi ni mauti, lakini zawadi ya Mungu ni uzima wa milele katika Yesu Kristo Bwana wetu.” 

Hapa tunasoma kwamba: lakini zawadi ya neema ya Mungu ni uzima wa milele. 

Kwanza: 

Mungu hakutupatia uzima wa milele sababu tulikuwa tunastahili. 

Tunayostahili ni kufa kwa milele na hukumu. 

Ya pili: 

Hatukupewa uzima wa milele kwa sababu ya matendo yetu na tena uzima wa milele hauwezi kuondolewa kwetu kwa sababu ya matendo yetu. 

Hatukupokea wokovu kwa sababu ya matendo yetu pia hatuwezi poteza wokovu kwa sababu ya matendo yetu. 

Matendo haina sehemu katika wokovu wetu, hata mbele ya wokovu, hata nyuma ya wokovu, wokovu ni zawadi ya Mungu mwenyewe.


4/ 2Timoteo 1: 9, 10 

“ambaye alituokowa akatuita kwa mwito mtakatifu, si kwa kadiri ya matendo yetu, lakini kwa kadiri ya kusudi lake mwenyewe na neema yake, tuliyopewa katika Kristo Yesu mbele ya nyakati za zamani, 

Na sasa imefunuliwa na kuonekana kwa Mwokozi wetu Yesu Kristo, aliyebatili kufa, na kufunua uzima na maisha yasiyokoma kwa njia ya Habari NJema.” 

Mwenyezi Mungu alituokowa na akatuita kwa mwito mutakatifu, si kwa kadiri ya matendo yetu. 

Matendo yetu haina muchango hata moja katika wokovu wetu. 

Kazi yenye Bwana Yesu aliyotimiza msalabani pa kalvari ndiyo iliyonunua wokovu wetu.

 

5/ Wokovu wetu siyo miradi yenye Mwenyezi Mungu alipanga ama kupata wazo wakati mtu alipoanguka zambini, bali ni ahadi ya Mungu aliyotayarisha tangu umilele uliopita. 

Tito 1: 2, 3 

“katika tumaini la uzima wa milele, Mungu asiyeweza kusema uwongo, aliuahidi mbele ya nyakati za milele; 

Lakini akafunua neno lake kwa nyakati zake katika mahubiri, niliyowekewa amana kama amri ya Mungu Mwokozi wetu;” 

Katika tumaini la uzima wa milele, Mungu asiyeweza kusema uwongo, aliuahidi mbele ya nyakati za milele.

 

6/ Kazi ya Roho Mutakatifu inakuwa  ushahidi ungine juu ya salama ya milele. 


Waefeso 1: 13 - 14  

“Ndani yake ninyi vilevile, wakati muliposikia neno la kweli, Habari Njema ya wokovu wenu, ndani yake mumekwisha kuamini vilevile na kutiwa mhuri wa Roho Mutakatifu ya ahadi. 

Ndiye aliye arabuni ya uriti wetu, ili kuleta ukombozi kwa mali yake mwenyewe, kuwa sifa ya utukufu wake.” 

Ndani yake ninyi vilevile, wakati muliposikia neno la kweli, Habari Njema ya wokovu wenu, ndani yake mumekwisha kuamini vilevile.

Ni hii utaratibu wa kawaida. 

Kiisha kuamini, tunatiwa muhuri ya Roho Mutakatifu. 

Mhuri wa Roho Mtakatifu, Yeye ndiye arabuni ya wokovu wetu. 

Waefeso 4: 30   

“Wala musihuzunishe Roho Mtakatifu ya Mungu, ndani yake mulitiwa mhuri hata siku ya ukombozi.” 

Tunasoma hapa kwamba hatupashwe huzunisha Roho Mtakatifu ndani yake tulitiwa mhuri hata siku ya ukombozi, hapana hata siku tutapoteza wokovu wetu.  

Siku ya ukombozi inamaanisha siku ya ukombozi wa miili yetu.

 Wakati Bwana Yesu atarudi kutuchukuwa, miili yetu ya haya itafananishwa na Mwili wake wa Utukufu, Mwili wa Ufufuko wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 

Wafilipi 3: 21 

“atakayebadilisha mwili wetu wa haya upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uwezo ule anaoweza kutiisha vitu vyote viwe chini yake.” 

7/ Waroma 3: 24  

“Wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Yesu Kristo:” 

Mwamini iko katika salama sababu yeye anahesabiwa haki. 

Sasa kuna neno kubwa iliyotafsiriwa na kasoro kidogo, ikituweka kama watu wenye bado kutenda zambi. 

Nikusema tungelikuwa kama wasio na hatia. 

Adamu, mbele ya kuanguka kwake katika zambi, alikuwa katika hali ile sawa asiye na hatia, lakini kuhesabiwa haki ni bora zaidi kupita hali ile. 

Kuhesabiwa haki ni kutangazwa kuwa mwenye haki sawasawa na Mwenyezi Mungu aliye MWENYE HAKI. 

Hapana kuwa sawa asiye na hatia.


8/ Waroma 4: 5 na Waroma 3: 24 inatuambiaya kwamba: 

“… kwa mtu asiyefanya kazi, lakini anamwamini yeye anayehesabia haki wasioogopa Mungu, imani yake inahesabiwa kuwa haki” kwani

“Wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Yesu Kristo:” 

Tufahamu kwamba kwa njia ya neema yake KRISTO, mtu muovu anahesabiya haki.

Hapana wale wanaoishi maisha ya usafi. 

Hapana wale walio wazuri kufwatana na mwenendo wao wenyewe.

 

9/ Twende sasa katika kitabu cha Wakolosayi 1: 23 

“kama mukidumu katika Imani, mukiwekwa juu ya msingi na kusimama imara, wala hamugeuzwi mbali na tumaini la Habari Njema muliyosikia, iliyohubiriwa katika viumbe vyote chini ya mbingu ; nami Paulo nilifanywa mtumishi wake.” 

Tuliwaonesha kupitiya Maandiko Matakatifu kwamba mwamini hawezi kujiokoa kwa njia ya matendo yake mema, na kwamba hawezi kupoteza wokovu wake kwa sababu ya matendo aliyofanya. 

Sasa, ni nini Mutume Paulo anataka maanisha wakati anaposema kwamba sisi tutakuwa watakatifu pasipo kilema, wala laumu mbele ya mecho ya Mungu, kama tukidumu katika imani. 

Neno “kama” inaonesha sharti ya hali, na inamaanisha “kama, na ni kweli kama”, 

Nikusema kama kweli, na ni kweli munaendelea katika imani. 

Tunakuwa na namna mbaya ya kutumia neno “kama” toka Kigriki wakati inapotumiwa sawa sharti ya muhimu na inayohitajika. 

Ni sawa mtu anayesema: Nitakwenda kuogelea kwa bahari kama nvua hainyeshi. 

Bali, hii siyo maana tunayokuwa nayo hapa. 

Hapa, inamaana kusema, ni kweli. 

Siyo sharti. 


10/ Neno kuendelea, ama kudumu ni EPEE – MEN – O. 

Epee inamaanisha juu. 

Meno inamaanisha kukaa. 

Na kama tukichanga yote pamoja tunapata: 

Kuendelea kukaa, ama, kudumu katika kutenda jambo fulani. 

Na neno imani, PISS – TIS na ina  tanguliwa na makala kamili mbele yake, hivi itatafsiriwa kama ifwatavyo: 

KAMA UKIENDELEA NA KUDUMU KATIKA KUSADIKI MAFUNDISHO YA BIBLIA NA UKIYATENDA. 

Imani inamaanisha Kusadiki Mafundisho ya Biblia, na neno kuwekwa juu ya msingi inamaanisha KUTIYA MSINGI, na neno kusimama imara ni KUTOKUTIKISIKA.

Ni kusema wewe hauongeze kitu kwa mafundisho ya Biblia, bali unaamini yale Biblia inayofundisha kuhusu wewe na Bwana wetu Yesu Kristo.


11/ Wala hamugeuzwi mbali na tumaini la Habari Njema. 

Kwa halisi hiyo inamaanisha hapana kujitenga kando, na neno TUMAINI ni kuwa na uhakika AL –PUS. 

Kuwa na uhakika katika Habari Njema, hapana kujitenga kando ya Habari Njema. 

Habari Njema muliosikia na iliyohubiriwa kwenu. 

Neno kuhubiri KAY – RUE SO inamaanisha kutangaza hazarani. 

Pia angalia kwa makini maneno haya: 

Nami Paulo nilifanywa mtumishi wake. 

Ni nini Mtume Paulo anataka kutuambia hapo? 

Anapenda kutufahamisha kwamba tunapashwa kudumu katika kawaida ya  mafundisho yale aliyotufundisha, tutie msingi wetu katika kawaida ya mafundisho yale, na tusimame imara, tusitikisike, tuki weka tumaini letu ndani ya  Habari Njema. 

Habari Njema iliyofundishwa na Mutume Paulo. 

Waroma 2: 16 

“Katika siku ile Mungu atakapohukumu siri za watu, sawasawa na Habari Njema yangu, kwa Yesu Kristo.” 

Pia tufahamu kwamba Waroma 16:25 inasema:  

“Kwake yeye anayeweza kuwasimamisha ninyi sawasawa na Habari Njema yangu na kwa mahubiri ya Yesu Kristo, kama ufunuo wa siri iliyowekwa tangu nyakati za milele,” 

2 Timoteo 2: 8 

“Ukumbuke Yesu Kristo, aliyekufa toka wafu, wa uzao wa Daudi, kama inavyosema Habari Njema yangu.” 

Nikusema kwamba ni Habari Njema ya Mutume Paulo ndiyo inayo funua Kweli hii, kwamba nyinyi munakuwa sasa watakatifu, pasipo kilema wala laumu mbele ya Mungu.

Hakuna  sheria , wala amri ila tu Imani katika Yesu Kristo inayo tutiya katika hali hii. 


12/ Wakolosayi 1: 24 

“Basi sasa ninafurahi katika mateso yangu kwa ajili yenu, na ninatimiza katika mwili wangu yale yaliyokosa ya mateso ya Kristo kwa ajili ya mwili wake, ndio kanisa lake.” 

Hii ni aya moja ya upekee na yenye maana. 

Kuna wamoja wenye hawafikilie kuifahamu na wanapotosha misemwa hayo wakisema kwamba mateso ya Bwana wetu Yesu Kristo pale Msalabani hayakuwa kamili, na ya kwamba ni Mutume Paulo aliye musaidiya kwa kuitimiza. Hii siyo kweli, ni uongo mtupu na makosa. Na hii siyo maana inayokuwa katika aya hii.  

Aya hii haielekee Mateso ya KRISTO.

 

13/ Hapana Mateso ya KRISTO msalabani, bali maumivu  na manyonge ama  mateso  ya Kristo katika mwili wa Paulo. 

Mateso ya Kristo msalabani haiitwe maumivu na manyonge. 

Kama mtu anasambishwa kwenye Korti na anahukumiwa, hii siyo maumivu na manyonge lakini hii ni hukumu. 

Bwana Yesu Kristo alibeba Hukumu juu ya Musalaba. 

Basi, Mwokozi wetu Yesu Kristo aliamuru maumivu na manyonge ishike watu wake ili iwasaidia kukusanya kanisa, Mwili wa Kristo. 

Na Mutume Paulo alisema kwamba: 

Nitatimiza mapenzi ya Mungu kwangu, nipate maumivu, manyonge, na mateso katika mwili wangu kwa ajili ya Yesu Kristo ili kanisa likusanywe.

 

14/ Eti watambua? 

Kanisa la Kristo haikusanyiki kamwe bila mateso. 

Waweza kuchunguza ndani ya Biblia. 

Kweli Mutume Paulo hakustarehe katika mwili wake, yeye aliishi katika machungu na maumivu ya kila siku na kila saa. 

Wakati tunachunguza historia ya kanisa tutaona namna kanisa ilikusanywa kwa maumivu na mateso ya  watumishi wake Mungu. 

Wakati Mwenyezi Mungu anapotumikisha mtu, kunakuwa mpito wa machungu. 

Mutume Paulo anasema kwa namna halisi kwamba yeye anafurahi kuteseka kwa ajili ya Yesu Kristo. Oh, kweli aliteseka sana. 

2 Wakorinto 11: 23 - 25  

“Wao ni watumishi wa Kristo? (Ninasema sawasawa mwenye wazimu) mimi zaidi; katika taabu kuzidi sana, katika mapigo kuzidi sana, katika vifungo kuzidi sana, katika mauti mara nyingi.Kwa wayuda nilipata mapigo makumi ine ila moja. Mara tatu nilipigwa kwa fimbo, mara moja nilipigwa kwa mawe, mara tatu nilipata kuvunjika kwa merekebu, mchana na usiku nimekaa katika bahari:” 


15/ Wewe tayari umeisha soma Vitabu vya hadisi ya Shahidi? 

Wesley na Whitefield, Morrison na Carey na wahubiri wakuu waliopima kuonesha kwa wazi hadisi na vitumba vya miili ya Shaidi Wangreza? 

Mbele ya nyakati za Uinjilisti, mbele wamisionari waende India, Afrika na Chaina, kulikuweko  nyakati za mauaji na wengi walipoteza maisha yao.

 

16/ Wakolosayi 1: 25  

“Nami nimefanywa mtumishi wake, sawasawa na uwakili wa Mungu niliyopewa kwa faida yenu, nitimize Neno la Mungu.” 

Hapa tunaona aya moja ya muhimu na manufaa kabisa, ila watu wengi wanapendelea kuiruka ama kuisoma bila faida, ama kuisahau. 

Mutume Paulo alitiwa Mtumishi sawasawa na uwakili wa Mungu. 

Mungu alimupa ruhusa ya kutimiza Neno la Mungu. 

Mutume Paulo alitimiza Neno la Mungu, siyo Kitabu cha Ufunuo wa siri.

 

17/ Maneno ambayo Mutume Paulo anatuambia katika Biblia Takatifu, ni Ufunuo Mkubwa katika Biblia tangu Kitabu cha Mwanzo hadi Kitabu cha Ufunuo wa siri. 

Katika Kitabu cha Ufunuo wa Siri, hakuna jambo mupya kwa upekee. 

Kitabu cha Ufunuo wa Siri kinajaa na misemwa yenye inapatikana katika sehemu za Vitabu vingine katika Biblia. 

Ukweli wote tunaopata katika Kitabu cha Ufunuo wa Siri, ukweli huo tumeupata katika Vitabu vingine vya Biblia.

Bali, Kitabu cha Ufunuo wa siri umeyakusanyisha yote katika Kitabu kubwa ya mambo ya mwisho. 

Ni Mutume Paulo ndiye aliyepokea UFUNUO ya kwamba KRISTO alikua anaunganisha watu wote katika Kanisa unaoitwa KANISA MWILI WA KRISTO.  

Waefeso 1: 7 inatuambia kwamba: 

“Katika yeye tuna ukombozi wetu kwa njia ya Damu yake, usamehe wa zambi zetu, sawasawa na wingi wa neema yake,” 

Mutume Paulo anatumikisha neno “utajiri”, “wingi” neno hili linatumikishwa na Paulo pekee. 

Utajiri wa neema yake, wingi wa neema yake. 

Tena katika Kitabu cha Waefeso 2: 7, tunasoma ya kwamba: 

“hata katika nyakati za kuja aonyeshe wingi wa kupita kiasi wa neema yake kwa wema wake kwetu katika Kristo Yesu.” 

Wingi wa utajiri ya neema yake. Wingi wa kupita kiasi wa neema yake. 

Wewe unafikiri juu ya wingi wa kupita kiasi wa neema yake? 

Wingi wa utajiri wa neema yake unapita kiasi. 


AMINA 


N°Ref: 06/26/1977/ 395-2 DOES YOUR SALVATION DEPEND ON YOU? / 09/20/2020 

No comments:

Post a Comment