Tuesday, September 29, 2020

WOKOVU NA SIKU YA BWANA / SALVATION AND THE LORD'S APPEARING


Photo taken by B Smith from the patio
 

 


WOKOVU NA SIKU YA BWANA 

SALVATION AND THE LORD'S APPEARING

January 13, 1963 

Pastor Henry F. Kulp



 

1 Watesalonika 1: 1 – 5 

“Paulo, na Silvano, na Timoteo, kwa kanisa la Watesalonika katika Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo: Neema iwe kwenu na salama toka Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo. 

Tunashukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu ninyi wote, tukiwataja ninyi katika maombi yetu; tukikumbuka pasipo kuacha kazi yenu ya imani, na taabu yenu ya mapendo, na saburi yenu ya tumaini katika Bwana wetu Yesu Kristo, mbele ya Mungu Baba yetu; tukijua, ndugu munaopendwa na Mungu, kuchaguliwa kwenu, sababu Habari Njema yetu haikufika kwenu katika neno tu, lakini vilevile katika uwezo na katika Roho Mtakatifu, na katika matumaini mengi; sawasawa munavyojuwa tulikuwa watu wa namna gani katikati yenu kwa ajili yetu.” 

Juma iliyopita tulijifunza na kuonesha mazingira ya kuzaliwa na kuanzishwa kwa kanisa la Tesalonika. Kanisa hili lilianzishwa katika hali ya upekee na maajabu, kwa jia ya maelekezo machache yaliyotolewa na Mtume Paulo. 

Kwa kweli ilikuwa hatua ya mwanzo kwa kazi kubwa ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 

Kama vile munavyokumbuka, sawasawa tulivyowaambia, hii ni mabarua ya kwanza yenye Mtume Paulo aliandika pale Korinto wakati alipotoka Beroya kwa sababu ya mateso na mashambulizi.

 Timoteo na Sila wao sawa vile walivyoagiza na Mtume Paulo, wao, walibaki nyuma na walikwenda Tesalonika na kiisha walirudi kumpa Mtume Paulo ripoti ya hali ya yale makanisa changa. 


1/ Wengi wa washiriki katika Kanisa lile walikuwa watu toka wapagani na watu wasiokuwa wayuda, lakini wengi wa washirika walikuwa wapagani, sawa vile tunaweza kuiona kwa aya ya 9

“Kwa sababu wao wenyewe wanatangaza habari zetu namna tulivyoingia katikati yenu; na namna gani mulivyogeuka kwa Mungu toka sanamu, kutumikia Mungu aliye hai, na Mungu wa kweli;” 

Mtume Paulo alikuwa saa zote akifikiri na  kujali sana kuhusu maisha ya kiroho ya  wale wakristo wachanga, kwa hiyo,  Mtume Paulo anatuambia kwamba moyo wake haukuwa na pumziko, alikuwa akingoja kwa hamu sana ujio wa Timoteo na Sila, akiwa na hofu kwamba shetani asije akawajaribu wale wakristo wachanga walioamini Yesu. 


1 Watesalonika 3: 5 

“Kwa sababu hii mimi, wakati nilipokuwa siwezi kuvumilia tena, nilituma mtu nipate kujua imani yenu, asiye mjaribu akawajaribu ninyi, na taabu yetu ikakuwa pasipo faida.” 

Bali kwa aya ya sita anatuambia kwamba habari zilimufikia na taarifa zilikuwa za kutia moyo. 

Na hiyo ndiyo iliyosukuma Mtume kuandika Waraka huu. 


2/ Ni vizuri sana kufahamu ya kwamba siku ya Bwana Yesu Kristo, ama siku ya kunyakuliwa kwa Kanisa inazungumuzwa mahali pote katika Sura zote za Waraka huu wa Watesalonika. 

Kumbukeni kwamba Waraka huu ulioandikwa kwa niaba ya Wakristo wachanga katika Yesu Kristo, inatuonesha umuhimu wa Siku ya Bwana, siku Bwana Yesu atakuja na kuonekana pale mawinguni, na hapo itakuwa kunyakuliwa kwa Kanisa.

Kiini ya jambo hili ni kutia mkazo kwamba hata watoto wachanga katika Kristo wanapashwa  kufahamu sana  kawaida ya mafundisho haya. 

Ni huruma kweli kusikia kwa siku ya leo watu wakituambia kwamba hiyo kawaida ya mafundisho siyo ya mahimu na haitupasi kushikamana nayo kwa kiwango namna sawa. 

Wangapi wale wasiohubiri juu ya kuja kwa Bwana Yesu.

Lakini majifunzo yetu ya leo yanatuonesha umuhimu wake. 


3/ Tuone sasa mambo makuu yanayokuwa katika Waraka wa Watesalonika. 

Waraka wote nzima unahusika na Siku ya Bwana Yesu Kristo. 

Sura ya kwanza inaonesha uhusiano unaokuwa kati ya Wokovu na Kuja na kuonekana kwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 

Sura ya pili inatufunulia wazi uhusiano unaokuwa kati ya kazi ya mwamini  na Kurudi kwa Bwana wetu Yesu Kristo. 

Sura ya tatu inahusu uhusiano kati ya maisha ya utakaso na siku ya Bwana. 

Sura ya ine inasema juu ya uhusiano  kati ya ufufuko na kuonekana na kuja kwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 

Na Sura ya tano inaonesha Salama ya mukristo na kuja na kuonekana kwa Bwana Yesu Kristo. 


4/ Tujifunze sasa Aya hii ya kwanza

Aya hii ya kwanza inatupatia salamu. 

Tunaona ya kwamba katika aya hii hakuna matumizi ya majina ya madaraka ya mitume.    

 Tunapata tu majina pekee sawa ya akina Paulo, Silvano( yeye ndiye Sila) na Timoteo. 

Kuachwa kwa matumizi ya jina ya madaraka kama akina “Mtume” bila kuitia mbele ya jina “Paulo” ni jambo la muhimu sana. 

Jambo hili Mtume Paulo alilifanya mara tena katika Vitabo tisa juu ya Vitabu kumi na tatu alivyo andika. 

Katika Kitabu cha Wafilipi, moja ya hayo yenye hakutumikisha jina “Mtume”, katika Kitabu kile alijiita “Mtumishi wa Yesu Kristo”. 

Ni vema sana kutambua kwamba katika I na II Watesalonika, hakutumikisha jina la madaraka, lakini alitumia jina lake pekee “Paulo”. 

Hii inamaanisha kwamba mbele ya watu hawa Paulo hakuwa na haja ya kujitambulisha. 

Katika Waraka nyingine mbalimbali alizo andika, yeye alipashwa kujitambulisha kwa kuonesha huduma yake kama mtume. 

Bali, kwa kanisa la Watesalonika, walikuwa wakiheshimu neno lolote la Mtume Paulo, haikuwa budi kwake kujitambulisha kwamba yeye ni Mtume. 

 

5/ Kumbukeni kwamba jina, Paulo, inayomaanisha mdogo ama mfupi, ilikuwa jina alilopewa na mtu wa mataifa, mtu wa kwanza aliye hubiri na kumuleta kwa Yesu Kristo katika kisiwa cha Pafoti. 

Jina Timoteo ni mchango wa majina mawili toka Kigriki: 

Timao: inayomaanisha yeye anaye mucha Mungu. Na kulingana na hilo tunasema kwamba Timoteo alikuwa kijana aliye mucha Mungu maishani mwake. 


6/ Tuchunguze sasa kuhusu kanisa la Watesalonika. 

Mara kwa mara tulikuwa tukizungumuzia juu ya jina “Ecclesia” inayo maanisha kanisa ama mukusanyiko wa watu walioitwa. 

Katika Agano la Kale, Taifa la wana wa Israeli walitumia neno kanisa. 

Neno lile lilitumikishwa pia juu ya kutambulisha kundi la wapigakelele. 


Matendo ya Mitume 19: 32 – 41. 

“Basi wengine walikuwa wakilia neno moja, na wengine neno lingine, kwa sababu makutano yamechafuka, na zaidi yao hawakujuwa kwa maana gani wamekwisha kukutana. 

Walitoa Alesanduro katika makutano, Wayuda wakamweka mbele ya watu, Alesanduro akawapungia mkono, akitaka kujibu watu wake. 

Lakini wakati walipotambua ya kuwa yeye ni Myuda, wote pia kwa sauti moja walipiga kelele kwa kadiri ya saa mbili, wakilia: Diana wa Efeso ni mkubwa. 

Kisha mkubwa wa mji alituliza makutano, akasema: Wanaume wa Efeso, mtu gani asiyejuwa ya kuwa mji wa Efeso ni mlinzi wa hekalu la Diana, aliye mkubwa, na wa sanamu iliyoanguka toka mbingu? 

Basi, kwa sababu maneno haya hayawezi kukanwa, imewapasa ninyi kunyamaza, musifanye neno kwa haraka haraka. 

Kwa maana mumekwisha kuleta watu hawa wasio wizi wa hekalu, wala wenye kutukana mungu wetu.

Basi kama Dimetrio, na mafundi walio pamoja naye wana neno juu ya mtu, kuna baraza na wakubwa: washitakiane. 

Lakini mukitafuta neno katika maneno mengine, yatatengenezwa mbele ya wakubwa katika baraza. 

Kwa maana tuna hatari ya kushitakiwa kwa ajili ya matata haya ya leo; kwani hakuna maana moja tunayoweza kueleza kwa makelele haya. 

Alipokwisha kusema maneno haya, akasambaza makutano.” 

Hii inamaanisha kwamba makutano ya ibada ni mukusanyiko ya watu walioitwa na Mungu toka wale wanaoabudu sanamu na pepo chafu za mashetani, wale wanao tumikia na kuabudu miungu za sanamu na sasa wanakusudia kutumikia Mungu. 

Tesalonika ni mahali hayo makutano yalikusanyika. 

Mtume Paulo aliwakuta ndani ya Neema na Amani. 

Wagriki walikuwa wanatumia neno Neema kwa kusalimiana wao kwa wao.  

Wahebrania walikuwa wanatumia neno Amani kwa kusalimiana wao kwa wao. 

Neema ni zaidi kuliko huruma, kwa sababu hurumu inamaanisha Mungu hakupatie ile unayostahili. 

Kwa hiyo Neema ni zaidi ya huruma, zaidi sana kupita maelfu ya huruma. 

Neema ni Mungu Baba na Mungu Mwana wakikupatia vitu vyote bure pasipo malipo. 

Tutambue kwamba Neema inatoka kwa Mungu Baba na Bwana wetu Yesu Kristo. 

Neema haitoke kwa Mitume, haitoke kwa Makusanyiko, haitoke kwa kikundi cha watu kinacho ongozwa vema. Neema inatoka tu kwa Mungu Baba na Mungu Mwana. 


7/ Amani haiwezi kamwe kupatikana bila Neema. 

Neema ni chemchemu ya Amani. 


8/ Aya ya 2 

“Tunashukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu ninyi wote, tukiwataja ninyi katika maombi yetu;” 

Tambua uaminifu wa Mtume Paulo katika maombi.

Tunapashwa kuombeana sisi kwa sisi.

Mtume Paulo anahakikisha katika 1Timoteo 2, na hapa, Mtume Paulo aliheshimu maagizo yake mwenyewe. 

Alikuwa akiombea kanisa hili sababu alikuwa akijitaabisha moyoni kwa ajli yake. 

Hili kanisa lenye lilikuwa bado halija shimika mizizi mirefu chini sana, 

Kanisa lenye lilikuwa kitovero cha mashambulizi na ujanja wa watu wa dini.

Tutambue kwamba Mtume Paulo hakuomba kwa jumla na kwa juu juu, lakini maombi  yake ilikua yenye lengo, kusudi na shabaa, alijuwa nini kuombea na sababu gani na katika shida gani. 

Nina uhakika kwamba munapashwa kuwa na horoza ya mambo yote munayopenda kuombea, kuombea watu kamili wenye wanaokumbwa na tatizo fulani. 

Munapashwa kuombea mtu fulani anayekumbwa na shida fulani. 


9/ Tusisahau kwamba mtume Paulo alikuwa na amesongwa na kazi nyingi sana. 

Alikua akihubiri hazarani, pia akienda na kuingia nyumba kwa nyumba kwa kutangaza injili. 

Alikuwa akijenga hema  kwa  kupata chakula chake cha kila siku, na zaidi ya hayo yote, yeye alikua akipata muda ya kuombea yale makanisa yote aliyofungua.   

Alikua akiombea wale washirika wote. 

Siyo vizuri kusema kwamba wewe unakuwa na shuguli nyingi. 

Najuwa kwamba wewe hauna kiasi cha shuguli nyingi zaidi kuliko yale   Mtume Paulo aliyokuwa nayo.  


10/ Aya ya 3  

“Tukikumbuka pasipo kuacha kazi yenu ya Imani, na taabu yenu ya mapendo na saburi yenu ya tumaini, katika Bwana wetu Yesu Kristo, mbele ya Mungu Baba yetu;” 

Kuna maneno matatu ya muhimu sana ndani ya aya hii. 

Imani, Tumaini na Mapendo. 

Mutafahamu ya kuwa hii maneno matatu ya musingi imeungwa pamoja katika Maandiko mengine ya Mtume Paulo katika vitabu vingine. 

1Wakorinto 13: 13 

“Basi, sasa inadumu imani, tumaini, mapendo, hizi tatu; lakini neno kubwa katikati ya maneno haya ni mapendo.” 

Mutume Paulo anatuambia ya kwamba mambo haya matatu: Imani, Tumaini na Mapendo, yanadumu. 

Neno la muhimu na kubwa hadi hapo ni neno: “Kudumu”. 

Ninafurahi kujuwa kwamba mambo haya matatu yanadumu. 

Maishani mwetu kuna mambo mengi yasiyo dumu. 

Kwa mfano ujana unapambazuka na kutoweka. 

Afya, hata ikiwa bora hadi miaka 70 ama 80, itatoweka punde kidogo. 

Nafasi ya bahati, upendeleo, rafiki na vifaa vya kimwili, hata moja ya mambo haya tunayotaja haitadumu, bali tushukuru Mungu wetu kuona kwamba Imani, Tumaini na Mapendo yanadumu.  


11/ Jambo lingine la muhimu ni kwamba, moja ya maneno haya inakuwa na utumizi kubwa kushinda mbili nyingine. 

Ijapokuwa kwamba haya mambo matatu yanadumu, lakini neno kubwa katikati ya haya ni Mapendo.


12/ Ninafahamu kwamba mumetambua kwamba Imani ni ya muhimu sana. 

Waebrania 11: 5 

“Kwa imani Enoka alihamishwa asije akaona mauti, wala hakuonekana kwa sababu Mungu alimhamisha; maana mbele ya kuhamishwa kwake alikuwa ameshuhudiwa ya kwamba amependeza Mungu.” 

Bila imani, haiwezekani kumupendeza Mungu, na tuliwafahamisha siku zilizopita kwamba imani ni sawa miwani ya njia mbili kwa Mwamini, miwani ya kuangalia nayo mbali sana zaidi, ikiwezesha mukristo kuona kwa mbali vitu vyenye haviwezi kamwe kuonekana kwa mecho yake matupu.  

Bali, hapo juu kidogo, Baba Mungu anatuambia kwamba  neno kubwa katikati ya hayo mambo matatu ni Mapendo. 

Mwenyezi Mungu anasema kwamba Mapendo ni kubwa kushinda Imani. 

Je mapendo yawezavyo kuwa kubwa kupita imani? 

Hakuna shaka lolote, ni imani iliyo niokoa. 

Nikusema kwamba Imani inanipatia kitu changu binafsi, changu mimi mwenyewe bali mapendo inanituma kutumikia wengine. 

Mapendo inanisukuma kutimiza matendo ya neema  kwa wengine.  

Sasa, namna gani mapendo ni kubwa kuliko tumaini? 

Tumaini inanitia moyo kushangilia, lakini mara tena mapendo inanisukuma ku hudumia wengine. 

Tumaini inaniweka katika hatua ya kusubiri neno moja kwangu mwenyewe, lakini mara tena mapendo inanisukuma kutenda matendo ya neema kwa wengine. 


13/ Tutambue kwamba katika aya ya tatu, kuna neno: 

Kazi ya Imani

Imani inatenda kazi kama ni Imani inayokuwa hai, halisi na ya muhimu. 

Tuweke mkazo katika maandiko yanayokuwa katika Waefeso 2: 8 - 10  

“Kwa maana mumeokolewa kwa Neema kwa njia ya Imani, wala neno hili halikutoka ndani yenu wenyewe, ni zawadi ya Mungu, si kwa matendo asiwe mtu atakayejisifu. 

Maana sisi ni kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu ili tutende matendo mema Mungu aliyotengeneza mbele ili tutembee ndani yao.” 

Tumeokolewa kwa Neema kwa njia ya Imani, si kwa matendo yetu.

Bali kwa aya ya kumi tunaambiwa ya kwamba: 

Maana sisi ni kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu ili tutende matendo mema Mungu aliyotengeneza mbele ili tutembee ndani yao. 

Imani inapashwa kusukuma mtu kutenda kazi. 

 14/ Tukirudi kidogo nyuma katika 1Watesalonika 1: 3

“tukikumbuka pasipo kuacha kazi yenu ya imani, na taabu yenu ya mapendo, na saburi yenu ya tumaini katika Bwana wetu Yesu Kristo, mbele ya Mungu Baba;” 

Tukihakikisha neno “kazi ya mapendo” 

Imani ya kweli inazaa matunda, bali, mapendo inanisukuma kuhudumia hadi huduma iyo ifikiye kuwa kazi. 

Neno kazi inamaanisha kutaabika, kutumia nguvu kamilifu, inamaanisha kuchoka, inamaanisha kutumika kazi kwa hali kamilifu. 


15/ Tutambue Mapendo ni nini? 


1Wakorinto 13: 4, 5 

“Mapendo yanavumilia, ni upole; mapendo hayajui wivu, mapendo hayajisifu; hayajivuni, 

Hayakosi kuwa na adabu, hayatafuti maneno yake, hayakasiriki mbio, hayahesabu mabaya;” 

Kwanza ni kwamba mapendo yanavumilia, ni upole; mapendo hayajui wivu, mapendo hayajisifu; hayajivuni, hayakosi kuwa na adabu, hayatafuti maneno yake. 

Mapendo hayana uchoyo, unatafuta kila mara faida ya mwengine. 

Kama tukijaribu kupima uwingi wa mapendo yetu kufwatana na aya hii, si wengi kati yetu watakao onekana wanao ishi namna sawa. 

Jameni sisi tunakumbwa na mambo kazaa. 


16/ Neno la mshangazo pia na raha tele, ni kwamba katika maandiko haya, tukiondoa neno Mapendo na kulibadirisha na Jina la Bwana Yesu Kristo, tutasoma maandiko kama ifwatayo: 

Yesu Kristo aliteswa na kuvumilia sana, Yesu Kristo ni mupole, Yesu Kristo hajui wivu, Yesu Kristo hajisifu; Yesu Kristo hajivuni, 

Yesu Kristo hakosi kuwa na adabu, Yesu Kristo hatafuti maneno yake, Yesu Kristo hakasiriki mbio, Yesu Kristo hahesabu mabaya,  

Kwa sasa, weka jina lako mahali pote kwenye jina mapendo inapatikana, baadaye utizame nini utakayopata. 

Eti, mimi naweza kufaulu? 

Wewe unaweza kufaulu? 

Nazani kwamba kanisa la Watesalonika lilifaulu. 

Wao walikuwa na Mapendo wakitumika hadi mwili kuchoka, kazi kamilifu 


17/ kiwango cha upendo wako kwa Bwana Yesu Kristo ni gani? 

Ujichunguze na kuwa mwamuzi wako mwenyewe. 

Ni kama msemwa tunaokuwa tukitumia kuhusu kiwango cha mapendo tunayo mioyoni mwetu, kwa kupenda jirani wetu na mapendo tunayo kwa Bwana Yesu Kristo.  


Luka 7: 47 

“Kwa sababu ya maneno haya ninakuambia: Zambi zake zilizo nyingi zimesamehewa; kwa sababu alipenda sana. 

Naye aliyesamehewa kidogo anapenda kidogo.” 

Hapa ni mfano kuhusu mwanamuke aliyeshikwa katika zambi kubwa na maovu kubwa, kwa hivyo alimupenda sana Bwana Yesu Kristo, na kwa upande ungine tunakuwa na mufarisayo aliyejizania kwamba amempenda Mwenyezi Mungu, bali wakati alimukutana huyu mwanamuke akimuabudu Bwana Yesu, palepale alihuzunishwa hadi kufika kiwango cha kutokuheshimu Yesu Kristo. 

Na hapo, Bwana Yesu alipomutazama na kuvumbua maneno iliyokuwa ndani ya roho ya huyo mufarisayo, akampa mfano wa Mtu mwenye mali aliyewapa  watumishi wake wawili  mkopo wa pesa kwa sababu walihitaji pesa. 

Na Bwana Yesu  kuonesha waziwazi kwa njia ya mfano hule kwamba ni sawa mwanamuke huyu aliyempenda Bwana Yesu, alimupenda sana sababu yeye alijiona kwamba alikuwa akibeba muzigo mzito sana ya zambi na masamaha yake ilikuwa kubwa sana kwa hiyo alimupenda Bwana Yesu Kristo kwa mapendo makubwa sana kwa sababu yeye anatambua kwamba alisamehewa sana zaidi. 

Lakini mufarisayo aliyejiona kwamba zambi yake ni kidogo sana kupita kipimo yeye hakuzania kwamba anahitaji masamaha, ni kwa sababu hiyo yeye hangaliweza kupenda sana.   

Kiwango cha mapendo unayokuwa nayo kwa Mwenyezi Mungu una ambatana na kiwango cha makuu, maishara, maajabu na mibaraka yenye Mwenyezi Mungu amekwisha kukutendea. 


18/ Waroma 12: 9 

“Mapendo yawe pasipo udanganyifu; muchukie lililo uovu, mwambatane nalo lililo jema.” 

Biblia inatuambia hapa kwamba mapendo yawe pasipo udanganyifu. 

Ni kusema ya kwamba Mapendo yanapashwa kuwa ya kweli. 

Njia moja halali kwa mwamini kuwa na mapendo ya kweli, ni kujua kuhesabia mibaraka na makuu yote Mwenyezi Mungu aliyomufanyia na kumurudishia aksanti na shukurani. 


19/ Galates 2: 20  

“Nimesulubiwa pamoja na Kristo, lakini ni hai; wala si mimi, lakini Kristo ni hai ndani yangu; na uzima nilio nao sasa katika mwili, ni uzima wa imani iliyo ya Mwana wa Mungu ambaye alinipenda akajitoa nafsi yake kwa ajili yangu.”

Hii inatuonesha Mapendo inayokumbwa na shukrani. 

Mwana wa Mungu alinipenda na akajitoa mwenyewe kwa ajili yangu, ni kwa sababu ile mimi nampenda. 

Tena 1Yoane 4: 19 inasema: 

“Sisi tunapenda kwa maana yeye alitupenda sisi kwanza.” 

Hii ni mapendo inayokumbwa na shukrani. 


20/ Mwenyezi Mungu anahitaji tuwe na Mapendo inayotenda kazi, mapendo inayo mutumikia na kumuhudumia. 

 Unaweza kufahamu kwamba mapendo yako ni ya halisi, kama mapendo yako yakusukuma kutenda kazi ya Bwana wakati ungali bado unaishi duniani. 


21/ Kiisha tuone “tumaini katika Bwana wetu Yesu Kristo inayotokana na uvumilivu wetu.” 

Tumaini inanipa subira ya kitu ninacho ngojelea kwa niaba yangu binafsi. 

Na hii inaambatana na kuja na kuonekana mawinguni kwa Bwana na Mwokozi wangu Yesu Kristo. 

Kama vile tulivyoona juma jana katika Kitabu cha Waroma, kuonekana kwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo hapo kwa mawingu, kwa siku ile ya Bwana, itakuwa sherehe kubwa kwa mwamini, itakuwa saa ya kashifa kwa mwamini, yaani kuondolewa kwa kitambaa iliyo tufunika, itakuwa saa ya muzinduo wa mwamini. 

Hii tumaini ya Baraka, hii subira ya Baraka ya kwenda kukaa pamoja na Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, tukiwa tumebadirishwa mwili ufanane na Mwili wake wa utukufu, na kuzinduliwa kama watoto wa Mungu, hayo mambo yote yananitia moyo ili nisubiri nikishindana na dunia. 

Na hii inahimiza mwendo wangu ili niishi kwa kutazama siku zitakazo kuja siyo kuishi kwa sababu ya siku za leo. 

Ni kwa sababu hii twatambua ya kwamba tumaini linazaa subira. 

Kwa hiyo nina haja ya kusubiri hata nikumbwe na chochote kile katika maisha yangu ya kila siku. 


22/ Jameni niwape mfano: 

Kwa mfano mimi ninamjua mtu moja wa mali nyingi na mbele ya kufa kwake yeye ananiweka kuwa mrizi wa maliyake yaliyo kiasi nyingi sana. 

Na kwa kweli, mali haya yatakuwa yangu punde kidogo tu. 

Kwa muda wote ule agano lile litachungwa salama, pesa inaweza kuingia kwenye akiba yangu saa ni saa. 

Kama nikipungukiwa na pesa leo ama kwa majuma mawili ijayo, hii siyo shida kwangu na haiwezi kamwe kuniangaisha sababu kwa sasa mimi ni mbali sana na hali yangu ya kale ya umaskini yenye inakuwa sasa hadisi, siyo kweli tena, sababu kwa leo mimi ni mutajiri. 

Na ni hii ndiyo hali yetu kwa sasa. 

Hili kanisa la Watesalonika lilikua linahudumia katika Imani, Tumaini na Mapendo. 


23/ Tujifunze sasa aya ya 3. 

“Tukikumbuka pasipo kuacha kazi yenu ya imani, na taabu yenu ya mapendo, na saburi yenu ya tumaini katika Bwana wetu Yesu Kristo, mbele ya Mungu Baba yetu;” 

Anamaliza msemwa na neno moja la muhimu sana. 

Siyo kusema kwamba Mtume Paulo aliona mambo aya: Imani, tumaini na mapendo ndani ya watu wa Tesalonika, bali mambo yale yalionekana mbele ya Mungu Baba yetu. 

Neno hili linatubeba kwa ulizo moja maalum yenye kila moja wetu anaweza kujiuliza. 

Kitu gani Mwenyezi Mungu anaona katika roho yangu? 

Kuamini na imani halisi katika Yeye? 

Mapendo halisi kwa kumtumikia? 

Tumaini halisi inayoleta uvumilivu maishani mwangu? 

Kwa kweli, Mwenyezi Mungu anaangalia roho zetu, lakini pia anarekodi yote tunayosema, tunayo zania na tunayofanya. 


24/ Mawazo yangu inarudi nyuma kidogo ndani ya Kitabu cha 

Kutoka 32: 9  

“Bwana akamwambia Musa: Nimeona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu.” 

Hapa tunaona wana wa Israeli wakati walifika mwisho wa uvumilivu wao. 

Musa alipopanda juu ya mulima iliachukue Amri kumi ya Mungu, na wakati alipokuwa angali mulimani, wana wa Israeli walichoka kungojea Musa, wakafika mwisho wa uvumilivu wao, na wakasema kwamba kuna jambo fulani lililo fikia mtu yule Musa. 

Yeye hatarudi tena. 

Wakamwambia Haruni awajengee miungu ya sanamu yenye itawaongoza sasa.

Na wakati Mwenyezi Mungu aliposhuka toka mlima pamoja na Musa, 

Mungu akamwambia Musa: Nimeona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu. 

Tufahamu kwamba Mwenyezi Mungu aliwaona, alijua roho zao. 

Mungu alifahamu kile kilicho waongoza kwa kuabudu miungu. 

Ni muhimu sana tufahamu ya kwamba Mwenyezi Mungu anatujua na macho yake inatutazama. 

Yafaa tuchunguze sana maandiko haya na tuone kama maneno haya hayafanyike katika maisha yetu. 


AMINA


N°Ref: 01/13/1963 / 256 - SALVATION AND THE LORD’S APPEARING / 09/29/2020

No comments:

Post a Comment