Wednesday, October 14, 2020

SHERIA YA MBINGU YA KUTOA NA KUHITAJI / HEAVEN’S LAW OF SUPPLY AND DEMAND

Photo by B Smith from the patio




SHERIA YA MBINGU YA KUTOA NA KUHITAJI

HEAVEN’S LAW OF SUPPLY AND DEMAND

July 26, 1981 

Pastor Henry F. Kulp



 

Kwa kweli, mahubiri hii itaelekea utoaji. 

Mazungumuzo yote yataangalia pesa, na, nazani kwamba hamuta umwa moyo na kusema kwamba ninatia mkazo juu ya mahubiri kuusu pesa. 

Kwa kweli, mimi sihitaji kunyanyasa mkoba wenu, ama akiba ya mofukoni wenu, lakini, mimi kama Mtumishi mwaminifu wa Mwenyezi Mungu, ninakuwa na mapashwa ya kuwafahamisha yale yanayo husu   Utoaji tukifahamu kwamba: Mwenyezi Mungu anafurahia yeye anaye toa kwa furaha. 


1/ Mara kwa mara najiuliza kwamba eti ninyi munafahamu ya kuwa Biblia inasema mambo mengi sana kuusu Mwamini na utoaji sawa sawa na namna Biblia inazungumuzia kuhusu Kawaida ya Mafundisho mengine. 

Biblia inazungumuza sana kuusu utoaji ndani ya Agano la Kale na ndani ya Agano Jipya vilevile. 

Hata katika Vitabu vilivyo andikwa na Mutume Paulo navyo vilevile vinazungumuzia kuusu utoaji. 


2/ Ningelitamani muweke mafikili yenu juu ya msemwa huu: 

Mungu anafurahia yeye anayetoa kwa furaha

Eti, Mwenyezi Mungu hawapendi watu wote? 

Siye Yeye aliyesema katika Yoane 3:16 kwamba Mungu alivopenda Ulimwengu? 

Sasa msemwa inayosema ya kwamba Mungu anafurahia yeye anayetoa kwa furaha inamaanisha nini? 


3/ Mbele ya kuleta jibu ya ulizo hili, twende kwanza kufahamu kwamba Mwenyezi Mungu ni Mtoaji


Yoane 3: 16 inatuambia: 

“Kwa maana Mungu alivyopenda ulimwengu, hata kutoa Mwana wake wa pekee, ili kila mtu akimwamini asipotee, lakini apate uzima wa milele.” 

Mungu aliupenda hata kutoa. 

Uwingi wa mapendo na kutoa inaambatana na haiwezikane kuyatenganisha. 

Ni vigumu kwake anayependa ajizuize kutoa. 

Anayependa atatoa moja kwa moja bila mashito. 


4/ 1 Wakorinto 13: 3 inasema: 

“Na kama nikitoa mali zangu zote kulisha masikini, tena nikitoa mwili wangu niunguwe kwa moto, lakini sina mapendo, hainiletee mimi faida.” 

Katika maisha ya kiroho, kutoa bila mapendo ni bure na haifai kwa kitu.  

Na kama nikitoa mali zangu zote kulisha masikini, tena nikitoa mwili wangu niunguwe kwa moto, lakini sina mapendo. 

Tambua na utie mkazo sana kwa neno hili: Hainiletee mimi faida.  

Mungu anatupatia na kututolea vitu kazaa sababu anatupenda na kama sisi vilevile tunapenda kutoa, yatupasa kufahamu Mapendo.  


5/ NI MAPENDO INAYOKUWA CHINA YA UTOAJI 

MWENYEZI MUNGU HAHESABU UTOAJI UNAOFANYIKA BILA MAPENDO. 


6/ 1 Wakorinto 2: 12 

“Lakini hatukupokea roho ya dunia, lakini Roho anayetoka kwa Mungu; kusudi tupate kujua zawadi tulizopewa na Mungu.” 

Ni kwa sababu gani tulipokea Roho Mutakatifu? 

Kuna sababu nyingi, lakini ni kwa sababu gani Roho Mutakatifu alifanya Makao ndani ya miili yetu?  

Ona sasa moja ya sababu: 

Kusudi tupate kujua zawadi tulizopewa na Mungu. 

Ona tabia ya Mwenyezi Mungu wakati anapotoa: 

Kwa uhuru wote, bila sababu

Siyo kwa sababu tunastahili, lakini anatutolea kwa mapendo. 


7/ Waweza kukadirisha uwingi wa mapendo aliyonayo mtu kwako, kwa kufwatana na namna anavyokuhudumia ama kukutolea, siyo tu kwa kukupatia pesa.  

Unaweza kukadirisha Mapendo ya Mungu kwako kufwatana na yale Mwenyezi Mungu aliyokukabizi na vilevile kufwatana na yale anayoendelea kukupatia na kukubariki nayo. 


8/ 2 Wakorinto 9: 6 

“Lakini ninasema neno hili; yeye anayepanda kwa choyo atavuna kwa choyo; na yeye anayepanda kwa ukarimu atavuna kwa ukarimu.” 

Hapa tuna maneno mawili ya muhimu: 

Kwa choyo na kwa ukarimu. 

Kuna namna mbili ya wapandaji mbegu na kwa kweli kuna swali inayohitaji jibu: Wewe unakuwa upande gani? Ama ungelitamani kuwa kwa kundi gani? 

 

9/ Wagriki wanasema hivi: 

Yeye anayekuwa mupandaji wa mbegu saa zote. 

Ni sura ama picha hili ndilo Mutume Paulo anayokuwa nayo kwa huyu anayetoa. 

Hitaji la mupandaji wa mbegu ni kupanda mbegu, na kweli, kwa kila mukristo, kutoa ni kupanda mbegu. 

Kwa hivyo, sisi wote ni walimaji na shabaa yetu kuu ni kupanda na kuvuna.  

Je inakufikia kuzania na kuona sawa mwenye unapoteza wakati   unapopanda mbegu? 

Siyo kawaida kwa sababu kupanda mbegu kunaleta mavuno. 


10/ Tujiulize sasa swali hili: 

Ni mahali gani mupandaji wa mbegu, alipata yale mbegu alizopanda kwa mara ya kwanza? 

Yeye hangaliweza kuziunda, ni Mwenyezi Mungu aliye mukabizi yale mbegu. 

Yoyote ile unayo kwa namna ya kimwili ama kwa namna ya mapato, ni Mwenyezi Mungu aliye tangulia kukupatia yote unayo. 

 11/ Kuna namna tatu ya hali ya matumizi na mwenendo kufwatana na yale Mwenyezi Mungu aliyokukabizi.

1/  Mwenyezi Mungu alikukabizi mapato yote unayo, Yeye alikukabizi tu na Yeye hajali hata kukuomba chochote kile kwa kumuhudumia Yeye.

 2/  Sisi tulimuiba na kumunyanganya mali, kwa sasa ni pato letu binafsi, hatuna shida lolote juu yake na hatujali hata na neno atakalolisema.

 3/  Ni yeye alitukabizi pato lile kama deni na anapenda tuisimamie na utumizi uwe sawa sawa na mapenzi yake.  

Watu wengi wanaishi sawa vile pato yao ni yao wenyewe na ni kwa wao tu, kwa hivyo wanaamua kuishi sawa sawa na mapenzi yao na hawa jali hata pendekezo ama shauri kutoka kwa Mwenyezi Mungu. 


12/ Eti Mwenyezi Mungu ana lazima ya matoleo yetu? 

Kweli, hakika, ndio.

Siyo kwamba analazimishwa, lakini Yeye anamiliki yote na kuyaongoza hata kuwa mwenye kupendelea kuhitaji matoleo toka sisi walio wake. 

Angalia mufano wa kueneza Injili mahali pote. 

Mwenyezi Mungu hangalianza kuchapa Habari Njema toka huko mbinguni na kukabizi malaika vitabu ili washuke toka mbingu na kuja kupaza sauti katika mawingu, hapa duniani. Mwenyezi Mungu hakufanya hivyo.

Yeye alikua na uwezo wa kuchapa Habari Njema kule mbinguni, lakini Yeye hakufanya hivyo. 

Kupanua na kuenea kwa Injili duniani kutafanyika kwa musaada wetu, nafasi kote kule tutafikisha Injili na kulihubiri kwa mataifa tukiwapasha Injili na kuwaonesha maandiko. 

Mwenyezi Mungu alipendelea sisi tujitoe kwa kupasha na kupanua Injili na aliongoza yote ili itimilike namna sawa. 

Hivyo hivyo kuusu utoaji, Mwenyezi Mungu ni mwenyezi wa mali yote, lakini anapendelea sisi tumutolee ili Huduma ya Injili na Kazi yake isonge mbele. 

Tungelijiuliza sababu gani Mwenyezi Mungu hakuchapa pesa toka kule mbinguni kiisha aigawe kwa watu wanaojitoa katika huduma ya Injili na Kazi ya Mungu, lakini Yeye hakufanya hivyo. 


13/ Luka 16: 1, 2 

“Tena aliwaambia wanafunzi wake: Kulikuwa mtu tajiri, naye alikuwa na mlinzi mali; huyu alishitakiwa kwake, ya kuwa amepoteza mali zake. 

Akamwita, akamwambia: Habari gani hizi ninazosikia juu yako? Toa hesabu ya uwakili wako, kwani huwezi tena kuwa mlinzi mali.” 

Hapa ni Bwana Yesu Kristo mwenyewe ndiye anazungumuzia wanafunzi wake, ya kwamba: Kulikuwa mtu tajiri, naye alikuwa na mlinzi mali; huyu alishitakiwa kwake, ya kuwa amepoteza mali zake. 

Mali ya nani? 

Mali ya bwana wake. 

Akamwita, akamwambia: Habari gani hizi ninazosikia juu yako? Toa hesabu ya uwakili wako, kwani huwezi tena kuwa mlinzi mali.

Tunafahamu ya kwamba haitupasi sisi kutumia ovyo na   kupoteza mali yenye Mwenyezi Mungu aliyotukabizi. 

Yeye anatutia mawakili na anatukabizi muzigo mkubwa wa madeni, namna gani sisi tunatumia mali aliyotukabizi.  


14/ Kanuni ni kwamba: Upandalo ndilo utakalovuna. Nikusema Tavuna ulichapanda. 

Kufwatana na namna na hali upandavyo mbegu, Mwenyezi Mungu anakuonesha picha ya mbele ya namna mavuno yako itakuwa. 

Kama wewe unapanda kwa choyo, ukitia tu mbegu kidogo ndani ya udongo, kwa kweli hauna budi kungojea kwamba kwa mavuno wewe utatarajia magunia kazaa na kazaa za mavuno. 

Wakati unapopanda mbegu, pale pale utakuwa na taswira ya aina ya mavuno, na uwingi wa mavuno utakao vuna. 


15/ Kwa mwangaza wa Maandiko, tuone namna gani utoaji ulikuwa unafanyika. 

Matayo 19: 21, 22 

“Yesu akamwambia: Kama ukitaka kuwa mtimilifu, kwenda zako, ukauze vitu ulivyo navyo, uwape masikini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; na kuja unifuate. 

Lakini wakati yule kijana aliposikia neno hili, akakwenda zake kwa huzuni, kwa sababu alikuwa mwenye mali mengi.” 

Hapa tunakuwa na kijani kiongozi mwenye mali mengi, na anaambiwa: kwenda uuzishe vitu ulivyo navyo. 

Pambanisha maandiko haya na yale tunayopata katika kitabu cha Injili ya Luka 12: 33  

“Uzeni vitu vyenu, toeni sadaka, mujifanyie mifuko isiyochakaa, na hazina isiyopunguka katika mbingu, pahali asipoweza wizi kukaribia, wala nondo kuharibu.” 

Uzicheni vitu vyenu vyote, kiisha toeni sadaka, tena kweli tuna ukweli huu tena katika Kitabu cha Matendo ya Mitume.

 Matendo ya Mitume 2: 45, 46 

“Wakiuza mali zao, na vitu vyao, wakagawia watu wote kama kila mtu alivyokuwa na uhitaji. 

Na siku kwa siku kwa nia moja waliingia hekaluni, wakivunja mkate nyumba kwa nyumba, na kupokea chakula chao kwa furaha, na kwa moyo mmoja.” 

Bali kwa leo Mwenyezi Mungu haitaji wewe kupanda mbegu na kutowa kwa namna ile. 


16/ 2 Wakorinto 8: 12 

“Kwa maana kama nia ni tayari, inakubaliwa kwa kadiri ya mali mtu aliyo nayo, si kwa kadiri asiyo nayo.” 

Tunapashwa kutoa kwa kadiri ya mali tuliyo nayo, si kwa kadiri tusiyo nayo. 

Namna yetu ya kutoa inafwatana na ile yenye inafurika kwa yale tunayo, ile inayo baki. Ngapi tunayo tumia kwa niaba ya sisi wenyewe. 

Mwenyezi Mungu hapendi sisi tufikie kiwango cha kusema kwamba: 

“Kama ningelikuwa na dolla 25, ningelitoa kwa sadaka.” 

Utoaji hauhusike na yale mtu hana, lakini inahusika na yale mtu aliyo nayo.

Mwenyezi Mungu anapenda aone kiwango cha namna gani utatosha katika hakiba yako, hii ni tofauti kweli? 


17/ 1 Wakorinto 16: 1, 2  

“Basi juu ya sadaka kwa sababu ya watakatifu, kama nilivyoamuru makanisa ya Galatia, ninyi fanyeni hivi vilevile. 

Siku ya kwanza ya juma, kila mtu kwenu aweke akiba kwake, kwa kadiri ya mapato yake, ili sadaka zisifanyike wakati nitakapokuja.” 

Hapa Mwenyezi Mungu anasema kwamba, kwa siku ya kwanza ya juma, kila mmoja wetu aweke akiba kwa kadiri ya mapata Mungu aliyo mubariki nayo, ili wakati Mutume Paulo atafika sadaka zisifanyike tena. 

Hapo tena tunapata kanuni ingine: 

Kufwatana na ginsi Mwenyezi Mungu alikubariki

Eti, namna gani Mwenyezi Mungu alikubariki kwa asubui ya leo? 


Eti, wewe ulimtolea Mwenyezi Mungu kufwatana na namna alivyokubariki? 


18/ 2 Wakorinto 9: 7 

“Kila mtu afanye kama alivyokusudia katika moyo wake: Si kwa huzuni, wala si kwa lazima: Kwa sababu Mungu anampenda yeye anayetoa kwa furaha.” 

Mara tena hapa tuna kanuni kwetu: 

Kama alivyokusudia katika moyo wake.


19/  KWA UPEKEE, hapa tulisoma maneno mawili ya muhimu sana. 

Kila mtu, kila mwamini. Siyo lazima kwa asiye mwamini. 

Kila mwamini anaombwa kutoa. 

Roho Mutakatifu anazungumuzia kila mmoja anayetaja Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, hakuna yule anaye tiwa kando. 

Mwenyezi Mungu anahitaji kila mwamini atoe ili huduma ya kazi yake isonge mbele, haizuru kiwango cha pesa kubwa ama ndogo, haizuru awe mtoto sana ama mzee zaidi. 


20/ MWENYEZI MUNGU ANA HAKI GANI YA KUTUOMBA SISI TUMTOLEE? 

Hii ni kwa sababu sisi ni mali yake mwenyewe. 

Sisi ni watumwa wake, na kama watumwa, Yeye anaruhusa ya kutuamuru chochote kile anachopenda tulifanye. 

Sisi ni mali ya Mungu kwa hali mbili:


  1/  Zaburi 24: 1 

“Inchi na kujaa kwake ni mali ya Bwana; Dunia, nao wanaokaa ndani yake.”  

Hii inaonesha kwamba sisi ni mali ya Mungu kupitia muombo. Ni Yeye aliye tuumba na sisi ni mali yake mwenyewe na kwa hiyo anaruhusa ya kutuambia nini tufanye.


2/  Wakorinto 6: 19, 20 

“Hamujui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, muliyepewa na Mungu? 

Na ninyi si mali yenu wenyewe; 

Kwa sababu mulinunuliwa kwa bei; basi tukuzeni Mungu katika mwili wenu na katika roho yenu, maana ni ya Mungu.” 

Sisi ni mali ya Mungu kwa njia ya Ukombozi. 

Sisi tulikuwa zamani katika soko ya watumwa wa zambi na Yeye alitununua kwa Damu ya Damani sana na bei kali mno, kwa hivyo Yeye anaruhusa ya kutuambia tufanye nini na hasa kuusu mali yetu. 


21/ Twende sasa kwa neno linalofwata katika maandiko yetu. 

Neno lile ni msemwa: “Kama alivyokusudia.”  

Katika Kigriki neno hili linakuwa na maana sana. Msemwa huo una maana ya kufanya uamuzi wa kutenda neno kiisha kuchunguza na kukusudia


22/ Kama alivyokusudia katika moyo wake. 

Hii ni msemwa wa musingi wenye hatuwezi pita kwa juu juu. 

Musingi wa utoaji wowote katika Biblia unapatikana katika Kitabu cha Kutoka 25: 2 

“Sema na wana wa Israeli wanitwalie sadaka; toka kila mtu aliye tayari moyoni mwake mutatwaa sadaka yangu.” 

Yafaa tufahamu kwamba kutoa siyo rahisi. 

Mungu alipenda kuisha katika ya wana wa Israeli. Alipenda kupata mahali pa kukaa, hekalu, na kwa kupata hekalu lile Yeye alijitia kwa hali ya kusema kwamba ni wanadamu watakao mtolea vifaa na vitu vyote kwa kujenga hekalu, watakusanyisha vitu vyote pamoja kiisha watamujengea Mungu nyumba. 

Sawa vile munavyo fahamu, Mwenyezi Mungu angaliweza kuamuru hekalu liwe na kwa mahali pasipokuwa kitu, hekalu lingelionekana, lakini Mungu hakupenda kutenda kwa namna ile. 

Yeye alipatia Musa aina, hali na kipimo cha nyumba yake, na alipatia Roho Mtakatifu kwa wanaume na wanawake wa Taifa la Israeli, wenye walipashwa kuhusika na kukusanyisha  vifaa vyote vinavyo hitajika kwa majengo, ni kwa hivyo Mwenyezi Mungu alisema: 

Munitwalie sadaka; toka kila mtu aliye tayari moyoni mwake. 

Siyo halali kutoa kwa moyo wa kushitashita na huzuni, maandiko yafwatayo yanatushauri: 


2 Wakorinto 9: 7  

“Kila mtu afanye kama alivyokusudia katika moyo wake: Si kwa huzuni, wala si kwa lazima: Kwa sababu Mungu anampenda yeye anayetoa kwa furaha.”  

Kwa kweli hii inamaanisha hali ya huzuni. 

Kusiwe hata mtu yeyote atakaye huzunika wakati anapomtolea Bwana. 

Siyo vizuri kusema: Pole kwangu sababu nimetoa zaidi ya vile nilikuwa napendelea kutoa. 

Ingelikuwa heri kusema: Nashukuru Mungu kuona nimetowa kwa kiwango niliyotoa. Na ningelitamani kutoa zaidi ya yale. 

Ni hofu tena zaidi, Matoleo hayapashwi kuwa ya mkazo, mtu kujisikia sawa anasukumwa kutoa, anasukumwa kwa kinguvu, watu wanapenda wapate faida juu yake. 

23/ Nilipata habari kuhusu kanisa moja, na kanisa lile siyo mbali na hapa, katika hiyo kanisa, wakati wa sadaka wao wanatumia “Matoleo ya maandamano.” 

Na wanafanya namna hii: 

Mtu moja anashimama hapo mbele ya wote, na kila mmoja wakati wa kutoa sadaka anashimama toka mahali alipokaa na kuja akitembea akijeelekeza mbele na kutoa sadaka yake huko. 

Mimi sina maandamano ya namna sawa na siamini mambo yale. 

Hii ni kutoa ya mkazo, tena kusifu yeye anaye toa na pia sadaka yenye mtu anaenda kutoa huko mbele inaonekana na watu wote kanisani. 

Kama mmoja anatoa sadaka musiyofurahia, hapo hapo munamuambia kwamba asitoe na Mungu hafurahie sadaka yake.

Musingi wa utoaji ni mapendo na roho yenye kuwa tayari kwa kutoa. 


24/ KWA UHURU WOTE

Mwenyezi Mungu anatutolea kwa uhuru wote na anahitaji nasi vilevile  tumtolee kwa hali hiyo. 

Uhuru unachina lake katika Kigriki kwa neno DOE RAY ON, na inamaanisha bila sababu, bila nia lolote.  


Waroma 8: 32 inasema:    

“Yeye asiyeachilia Mwana wake, lakini alimtoa kwa ajili yetu yote, namna gani atakosa kutuletea vitu vyote pamoja naye?”  

Yeye alitupatia vitu vyote kwa uhuru wote, kwa hivyo ingelitupasa kusema: Bwana sisi hatutarajiye wewe uturudishie kitu.

Tunafahamu kweli ya kwamba utayafanya, ila tulipendelea kukutolea kwa uhuru wote. 


25/ kiisha yafaa tutoe KWA FURAHA

Wakati Mwenyezi Mungu alipotutolea Mwana wake, hakumutoa akiwa akifunga nyuso. 

Bali alimutoa kwa FURAHA na UHURU wote, na Roho Mtakatifu ni Zawadi kutoka kwa Mungu na Wokovu vilevile ni Zawadi kutoka kwa Mungu na haya yote Mungu alitukabizi kwa FURAHA toka kwake. 

Kwa sasa tunahitajika kusema: Leo nimepata nafasi na bahati nzuri ya kumtolea Mungu wangu ili Huduma na Kazi yake isonge mbele. 


26/ Sawa vile tulivyosema kwa mwanzo: 

MUNGU ANAMPENDA YEYE ANAYETOA KWA FURAHA

Tujiulize sasa swali hili: 

Eti, Mwenyezi Mungu anawapenda watu wote? 

Hata wao waliookolewa na wale wasiookolewa? 

Kwa kweli, Mungu anawapenda watu wote. 

Eti Mungu anampenda kila mwamini bila kujali kwamba huyu ananitolea ama hapana? 

Bila shaka ni hivyo. 

Mungu anasema, Yeye Mungu anampenda yeye anayetoa kwa furaha. 

Kila mtu, kila mwamini ni kazi ya mikono na Mapendo yake. 

Bali wakati mtu anafungua mufuko wake wa akiba kwa kubeba kazi ya Mwenyezi Mungu, kwa kueneza na kutangaza Injeli, mtu huyo anakuwa kipendeleo cha Mapendo ya Mungu. 

Hiyo ndiyo njia ya kupata Baraka ya kipekee toka Mwenyezi Mungu. 

 

27/ Kutoka 35: 21   

“Wakakuja kila mtu aliyesukumwa kwa moyo wake, kila mtu roho yake ilimfanya kuwa mwenye kutaka, wakaleta sadaka kwa BWANA kwa kazi ya hema ya kusanyiko, na kwa utumishi wake, na kwa yale mavazi matakatifu.” 

Namna gani Taifa la Israeli ilipokea na kujiandaa juu ya mwito wa Mungu kwa kumjengea Mungu Hekalu? 

Kila mtu aliyesukumwa kwa moyo wake na kila mtu roho yake ilimufanya kuwa mwenye kutaka. 

Matoleo yao ikawa nyingi kupita kiasi hata ikamulazimisha Musa aamuru watu kuacha kuendelea kuleta matoleo. 


Kutoka 36: 6 

“Musa katoa amri, wakaitangaza katika kambi, kusema: Mwanamume wala mwanamke wasifanye tena kazi nyingine kwa sadaka ya pahali patakatifu. 

Hivi watu wakazuizwa wasilete tena.” 

Watu wa Taifa la Israeli wakazuizwa kuendelea kuleta sadaka. 

Maandiko Matakatifu yanatuonesha wazi kwamba watu walikatazwa wasilete tena sadaka. 

Naamini ya kuwa watu wa Taifa la Israeli hawakumaliza yale   waliotayarisha na waliokusudia kutoa. 


28/ 2 Wakorinto 9: 15 

“Mungu ashukuriwe kwa sababu ya zawadi yake tusiyoweza kuisifu kama inavyopasa.” 

Hapa Mwenyezi Mungu anatuambia kwamba anastahili kushukuriwa kwa sababu ya zawadi yake tusiyoweza kuisifu kama inavyopasa. 

Hii ni chanjo na sababu kamili inayopashwa kutusukuma sisi kumutolea. 

Wakati mtu anapokutolea ama kukupatia kitu fulani, roho yako na mafikili yako inajaa na hamu sana na kukusukuma   wewe vilevile upate kumutendea vivyo hivyo kwa kumtolea ama kumukabizi kitu kingine. 

Mungu anampenda yeye anayetoa kwa furaha. 


AMEN 


N°Ref: 07/26/20 / 621-2 HEAVEN’S LAW OF SUPPLY AND DEMAND / 10/14/2020


No comments:

Post a Comment