Sunday, May 24, 2020

MWISHO WA KISIRISIRI WA KIZAZI HIKI / THE SECRET CONCLUSION OF THIS AGE

View from my kitchen window







MWISHO WA KISIRISIRI WA KIZAZI HIKI 
THE SECRET CONCLUSION OF THIS AGE
December 30, 1973
Pastor Henry F. Kulp




1 Wakorinto 15: 51 – 58
“Tazameni, ninawaambia ninyi siri: Sisi sote hatutalala, lakini sisi sote tutabadilika, Kwa dakika moja, kwa kufunga na kufungua jicho, kwa baragumu ya mwisho: sababu baragumu italia, na wafu watafufuliwa wasiwe na kuoza, na tutabadilika.
Maana sharti ule wenye kuoza uvae kutokuoza, na huu wa mauti uvae kutokufa. Lakini wakati ule wa kuoza utakapovaa kutokuoza, na ule wa mauti utakapovaa kutokufa, wakati ule litakapotimiya neno lililoandikwa:
Mauti imemezwa kwa kushinda.
Ee mauti, kushinda kwako ni wapi?
Ee mauti, uchungu wako ni wapi?
Basi uchungu wa mauti ni zambi; nguvu ya zambi ni sheria.
Lakini asante kwa Mungu ambaye anatupa sisi kushinda kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Basi, ndugu zangu, wapenzi, musimame imara, musitikisike, mukizidi siku zote kutenda kazi ya Bwana kwa sababu munajua ya kuwa kazi yenu si bure katika Bwana.”
Sura hii ina uzuri wa mastaajabu sana.
Inaitwa Sura ya UFUFUKO Kwa sasa ingekuwa vema tuone aya mbili inayoonekana kama wazo mbili tofauti. 
Aya ya 19 “Kama katika maisha haya tu tuna tumaini katika Kristo, sisi ni masikini kuliko watu wote.”
Hii inataka linganisha maisha yetu kuwa sawa yenye kuelekea maneno ya hapohapo na kwa saa ileile.
Kwa kweli ni hayo mambo hawa wahubiri wa upotevu wenye kufundisha mambo isiyofaa na ya umbalimbali kweli, wanapenda watuaminishe hivyo.
Wanamtia Bwana wetu Yesu Kristo kama Mwalimu mukuu, mwenye kutuonesha njia tunayopashwa pita, wakituambia kwamba sisi tunapashwa tu kushurulika na maisha yetu ya sasa na ya siku kwa siku.
Siyo mushangazo kuona vijana wa siku za leo wakichanganyikiwa na maisha, sababu maisha ya siku hizi inakuwa mbovu na kujaa maovu zaidi ya miaka kumi zilizo pita hapo kale. Na kweli hiyo ni kinyume ya haina mbovu ya uovu, ni hapo Mutume Paulo anasema kwamba maisha yetu ya ukristo siyo ya Ulimwengu huu.
Hapa chini duniani tunaonja tu madogo ya faida yenye tutapata baadaye, sababu Tumaini letu kweli si hapa chini.

1/ Aya ama shairi lenye ningelipenda tuchunguze kwa makini sana ni
Aya ya 57
“Lakini asante kwa Mungu ambaye anatupa sisi kushinda kwa Bwana wetu Yesu Kristo.”
Neno kubwa hapa ni neno Kushinda
Maisha ya mukristo ina ushindi.
Wengi wanazungumuza juu ya maisha ya ushindi, lakini, ushindi huo siyo ushindi tunaopata kwa siku za leo kwa maisha yetu ya kila siku, lakini ni Ushindi utakao kuja. Kila mtoto wa Mungu wa kweli, ana Ahadi ya Ushindi.
Na hii njo neno tutakalo jifunza leo.
Maisha ya mukristo ina ushindi.
Wengi wanazungumuza juu ya maisha ya ushindi, lakini, ushindi huo siyo ushindi tunaopata kwa siku za leo kwa maisha yetu ya kila siku, lakini ni Ushindi utakao kuja. Kila mtoto wa Mungu wa kweli, ana Ahadi ya Ushindi.
Na hii njo neno tutakalo jifunza leo.

2/ Mwisho wa kizazi hiki itakuwa katika siri.
Kizazi hiki kilianza na siri na mwisho wake utakuwa katika siri.
Ilianza na ugumu wa Israeli. Waroma 11: 25 “Kwa maana sitaki, ndugu, musijue siri hii, ili musijione wenyewe kuwa wenye akili, ya kwamba kwa sehemu ugumu umepata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa umefika.”
Hatungeliweza kutamka Kanisa Mwili wa Kristo bila kwanza ugumu wa Israeli. Utanzaji wa Neema unaanzishwa na siri na utafika mwisho katika siri.

3/ Aya ya 51
SISI SOTE HATUTALALA 
SISI SOTE HATUTALALA “Tazameni, ninawaambia ninyi siri: Sisi sote hatutalala, lakini sisi sote tutabadilika,”
Neno la raha na maastaajabu linalo onesha hali ya waliokufa katika Bwana Yesu Kristo.
Tunaipata tena katika kitabu cha
1 Watesalonika 4: 14 
“Kwa sababu tukiamini ya kama Yesu alikufa na kufufuka, hivyo wao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja Naye.”
Na hapa inamaanisha kwamba ni Bwana wetu Yesu Kristo aliye watia katika kulala. Na kweli hii inaelekea mwili wetu wa maumbile.

4/ Ila pale tunaambiwa kwamba:
Sisi sote hatutalala.
Kutakuweko kizazi chenye kitaona mauti na kufa na kutakuwa kizazi chenye hakitakufa ama kuona mauti.

5/ Kunakuwa kusudi kubwa tatu inayotuma waamini wahitaji KUNYAKULIWA ama kuwasukuma waamini wapendelee hiyo siri ije upesi.
5.1 Hawa furahie tena maisha ya siku hizi hapa duniani.
Maisha yanakuwa muzigo muzito mpaka kuwakata hamu na kupendelea sasa siku hiyo ya Kunyakuliwa ije ili iwaepushe na kuwatowa katika hiyo muzigo wa shida ya maisha kali ya leo. Lakini mambo hayatatembea hivyo.
Mwamini hapashwe kuhitaji Kunyakuliwa kusudi ahepuke ugumu wa maisha. Mwenyezi Mungu alitupatia Biblia, alitupatia Matunzaji yanayo patikana katika Biblia, Ahadi mbalimbali inayoweza kuturuhusu sisi tuishi kwa furaha katika maisha yetu ya hapa chini.
5.2 Kuna wale wanaokuwa na woga wa kufa.
Kuna wale wanao kimbia mbonde la kivuli cha mauti.
Wengi wao wanajuta na kuogopa wakijiuliza kama kifo itawapata kwa njia gani.  
2 Wakorinto 5: 8 “lakini tunauhodari, nasi tunapenda zaidi kutoka katika mwili, na kukaa pamoja na Bwana.”
5.3 Kuna wale waohitaji Mwokozi nao wanapendelea sana kukaa pamoja na Mwokozi.  
5.3 Kuna wale waohitaji Mwokozi nao wanapendelea sana kukaa pamoja na Mwokozi.  
2 Timoteo 4: 8 “nyuma ya haya nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana mhukumu wa haki atanipa siku ile; wala si mimi tu, lakini watu wote pia wameopenda kuonekana kwake.”
Kupenda kuonekana kwake, inamaanisha kumpenda, nikusema mapendo yoa kwake yamefurika na wamejaa na mapendo Kwake.
Wanapenda wawe pamoja NAYE.
Mambo ya dunia hii inaendelea tu kuwa muchafu zaidi, mpaka wao wanapendelea Kuonekana Kwake, Kumlaki Hewani.

6/ Lakini, haijali hata tukiwa tukiisha, ama tayari tukiwa tumeisha kufa katika KRISTO, sote tutabadilishwa.
Haijali kwamba tuwe wafu ama hapana.
Tumefundishwa tena ukweli huu katika:
1 Watesalonika 4: 16 – 18
“Kwa sababu Bwana Mwenyewe atashuka toka mbinguni, na sauti kubwa, na sauti ya malaika mkubwa, na pamoja na baragumu ya Mungu: nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza;
kiisha sisi tulio hai, tuliobaki, tutanyanyuliwa pamoja nao katika mawingu, kukutana na Bwana katika hewa, na hivi tutakuwa pamoja na Bwana milele.
Basi mufarijiane kwa maneno haya.”
Inawezekana ni kizazi hiki ndicho chenye hakita kufa, hatujuwi kitu chochote
juu ya maneno haya.

7/ Kunakuwa ujanja moja wakupenda kujionesha kama wale wafanyao ushuru, ujanja huo unatumikishwa na watu wanaojionyesha kuwa eti wao wanapenda Biblia sana.
Na wao wanaogopesha wengi juu ya neno “kuishi kwa sababu ya Yesu”
Wanasema kwamba kama wewe uko nafanya kitu chochote chenye hakimupendezi Bwana Yesu na ile siku ya Kunyakuliwa inafika na inakukuta ndani ya neno hilo, wewe hauta Nyakuliwa ili ukutane na Mwokozi hewani.
Yafaa tu wewe uhishi kwa sababu ya Bwana Yesu, haijali kwamba uko pamoja naye ama hapana. Wewe kwa siku ile utanyakuliwa katika hewa.

8/ Na TUTABADILIKA katika kigriki ni AL-LAS’-SO inayo maanisha: kuwa umbalimbali, ndugu watambua hiyo, Tutabadilika.
Tutakuwa na mwili wa aina nyingine mbalimbali.
Ninao uhakika kwamba hiyo itakuwa USHINDI kwetu.
Tutakuwa na mwili wa aina nyingine mbalimbali.
Ninao uhakika kwamba hiyo itakuwa USHINDI kwetu.
Sababu pahali ya kuwa na mwili wa kibinadamu, tutakuwa na mwili wa kiroho.

9/ Kubadilika huko kwa mwili kutafanyika kwa muda gani?
Ni neno “dakika” kwa kigriki AT-OM-OS inayomaanisha sehemu kidogo sana(atomi) ya muda.
Inayokuwa mugawanyiko wa moja kwa milioni kumi ya sekondi (1/10.000.000 ya sekondi).
Eti, wewe wajuwa kipimo ya muda unaoweza kupima kiwango hicho cha muda?

10/ Kwa baragumu ya mwisho
Wengi wanasema kwamba hii inaonekana sawa tabiya ya kiyuda. Hapana.
Kwa nini kutumikishwa kwa jina hilo “baragumu ya mwisho”?
Kwa nyakati hizo, jina hilo lilikuwa likitumikishwa mingi na watu wa nyakati ile. Ilikuwa ikitumikishwa kwa majeshi la waaskari wa Roma.
Wakati kampi la jeshi ilikuwa tayari kuondoka, iwe muchana wala usiku. Walipiga baragumu. Na palepale, kitu cha kwanza kufanya ilikuwa kukunja hema zao na kuwa tayari kwa kuondoka.
Neno ya pili ilikuwa kujipanga kwa mustari na kwa mwisho ilikuwa ile walikuwa wanaita “baragumu ya mwisho” nayo ilimaanisha amri yakusema “mbele songa, twende”. Mutume anatumikisha musemwa sawa sawa kwa kumaanisha kwamba, wakati baragumu ya mwisho italia, kizazi hiki kitatoweka na kufika mwisho na sote tutaamuriwa kwenda kukutana na Bwana wetu hewani.

11/ Hapa waliokufa na wafu, sote tunakwenda kukutana na Bwana. Nikusema hapo kuna kundi mbili: Waliohai na walio hai.

12/ Aya ya 53 Tunaposema “wenye kuoza”, tunamaanisha wale waliokufa.
Na “huu wa mauti” unamaanisha wale walio hai.
Huu wa mauti unaweza kufa, lakini ukivaa kutokufa, hauwezi tena kufa.
Na “huu wa mauti” unamaanisha wale walio hai.
Huu wa mauti unaweza kufa, lakini ukivaa kutokufa, hauwezi tena kufa.

13/ Aya ya 54 Hapa tunapata neno moja la manufaa.
Wakati ule litakapotimia neno lililoandikwa:
“Mauti imemezwa kwa kushinda”
Hii ni neno muhimu tunalopata katika: 
Wakati ule litakapotimia neno lililoandikwa:
“Mauti imemezwa kwa kushinda”
Hii ni neno muhimu tunalopata katika: Isaya 25: 8“Atazame kufa kusiwe tena milele. Na Bwana Mungu atapangusa machozi toka nyuso zote; na haya ya watu wake ataiondosha toka dunia yote, maana Bwana amesema maneno haya.”
Neno “Atameza” inamaanisha kumeza yote.
Kunakuwa misemwa inayo ambatana na hiyo sawa “KOPO YA MWISHO” inayomaanisha kwamba unameza kinywaji chote cha mwisho chenye kilikuwa katika kopo na hakubaki tena kitu ndani.
Nikusema kwamba kifo kinakomeshwa na tukio lile.

14/ Aya ya 55 “Ee mauti, uchungu wako ni wapi?
Ee mauti kushinda kwako ni wapi?” Hapo Mutume Pauloanaf ananisha na maandiko ya  
Ee mauti kushinda kwako ni wapi?” Hapo Mutume Pauloanaf ananisha na maandiko ya  
Hosea 13:14.
Hosea 13: 14 “Nitawakomboa toka nguvu za kaburi, nitawaokoa toka mauti; Ee mauti wapi mapigo yako? Ee kaburi, wapi kuharibu kwako? Toba itafichwa kwa macho yangu.”
Wakati kaburi inaomba mwili wa mwamini, kweli hapo kaburi inapata ushindi. Kuna uchungu katika kufa.
Eti, wewe umeisha poteza mupendwa wako?
Unakumbuka hiyo chozi la uchungu uliovuisha.
Hauliliye yeye aliye kufa, bali, unakumbuka wale walioachwa pia unaona picha ya namna mwili huo utaenda baki pekee kaburini.

15/ UPIME KWANZA KUFIKIRI, KAMA IKIWEZEKANA, KUSIWE TENA WALE WATAKAO HAMISHWA, HAKUNA TENA MAJISHI, KUFA KUMESHINDWA. Ukweli gani mtamu na faraja gani hii.

16/ Aya ya 56  “Basi uchungu wa mauti ni zambi; na nguvu ya zambi ni sheria.”
Uchungu wa mauti ni zambi, na hii ni zambi ya mutu wetu wa zamani.
Ni hiyo uchungu wa mauti, unaambatana na mutu wetu wa zamani anayekuwa na zambi hiyo ya asili.
Na nguvu ya zambi hiyo ya asili ni sheria.
Sababu sheria ndiyo inaonesha wazi kwamba tunayo zambi hiyo ya asili, lakini kuna kusudi lingine linalo tusukuma ili tuseme kwamba nguvu ya zambi ni sheria.
Lakini, ukijitahidi kuheshimu sheria, kwa muda kitambo, wewe unaheshimu sheria hizo kumi na tunda ya hiyo itaonekana sawa matendo mazuri ya kibinadamu, lakini kumbuka kwamba yote ni takataka ya uchafu, hata haki zetu zote tunazo zitimiza kwa nguvu yetu sisi wanadamu ni takataka mbele ya macho ya Mungu na Mungu hazikubali, anazitupa mbali.

17/ Aya ya 57 “Lakini asante kwa Mungu ambaye anatupa sisi kushinda kwa Bwana wetu Yesu Kristo.”
Shukrani kwa Mungu, inayosemwa: Asante kwa neema ya Mungu.
Neno lingine ya muhimu ni neno “anatupa”
Neno “Neema” na “anatupa” vyote viwili vinaambatana pamoja.
Kushinda kwetu tunaopata kwa njia ya Neema ya Mungu, si kwa namna tulio ama kwa kitu chochote tunalokuwa nalo, lakini kwa aina ya Mungu na kwa yale Mungu aliofanya kwetu.
Lakini mutu wetu wa zamani anaichukia sana Neema ya Mungu.

18/ Aya ya 58 “Basi, ndugu zangu, wapenzi, musimame imara, musitikisike, mukizidi siku zote kutenda kazi ya Bwana kwa sababu munajua ya kuwa kazi yenu si bure katika Bwana,”
Hapa tunatambuwa ya kwamba wakati tunakaza mecho yetu kwa kuangalia tu iyo kushinda kwetu, inatuletea nguvu katika huduma ama kazi ya Bwana.
18. 1 Musi... inamaanisha wazi: Muwe
Ni shurtisho ya muda huu wa saa hii na inamaanisha : Muwe wenye kusimama imara. 18. 2 Ndugu zangu, wapenzi, hii inamaanisha kwamba ni watu waliookolewa.
Ni wenye kimwili lakini waliokolewa.1 Wakorinto 3: 1 – 3“Na mimi, ndugu, sikuweza kusema na ninyi kama na watu wa Roho, lakini kama na watu wa mwili; kama na watoto wadogo katika Kristo.
Nimewakunywesha ninyi maziwa wala si chakula; kwa sababu mulikuwa hamujakiweza, hata sasa hamukiwezi;
Kwa sababu hata sasa ninyi ni watu wa mwili; kwa sababu kuna wivu na ugonvi katikati yenu, ninyi si watu wa mwili mukienda kwa namna ya watu?
18. 3 Kuna matumizi aina tatu ya Ushindi huo katika maisha ya mwamini.
Nimewakunywesha ninyi maziwa wala si chakula; kwa sababu mulikuwa hamujakiweza, hata sasa hamukiwezi;
Kwa sababu hata sasa ninyi ni watu wa mwili; kwa sababu kuna wivu na ugonvi katikati yenu, ninyi si watu wa mwili mukienda kwa namna ya watu?
18. 3 Kuna matumizi aina tatu ya Ushindi huo katika maisha ya mwamini.
18. 3. 1 Kushimamishwa imara kwa milele
Waroma 16: 25
“Kwake yeye anayeweza kuwasimamisha ninyi sawasawa na Habari Njema yangu na kwa mahubiri ya Yesu Kristo, kama ufunuo wa siri iliyowekwa tangu nyakati za milele,”
18. 3. 2 Kuzaa matunda kwa milele.
18.3.3 Utawa wa milele.

19/ Tunapashwa kusimama imara, tusitikisike,
Neno kusimama imara inamaanisha kuwa na mushimamo.
Neno tusitikisiki nikusema kubaki imara hata pepo mbalimbali zikivuma.
Tunapata tena hii wazo katika Waefeso 4: 14 “hata tusiwe tena watoto, tukitupwa huku na huku na kuchukuliwa kwa kila upepo wa elimu, kwa hila za watu, kwa ujanja, kwa udanganyifu mbaya;”

20/ Mukizidi siku zote kutenda kazi ya Bwana, inamaanisha kuzidisha mara na mara kazi ya Bwana.
Ni wengi wakristo wenye tayari wamekwisha kuregea.

21/ Tunapashwa kuwa na lengo, changamoto, na matumaini daima sababu tunajuwa ya kuwa kazi yetu si bure katika Bwana.
Huduma yetu siyo ya bure, isiyo kuwa kitu, ama isiyo na manufaa.


AMEN


N°Ref: KULP - 12/30/1973 / 333 - THE SECRET CONCLUSION OF THIS AGE / 05/24/2020

No comments:

Post a Comment