Tuesday, May 12, 2020

ETI MWILI WA KIMUTU WA BWANA YESU KRISTO ULIKUWA TOFAUTI? / WAS THE HUMAIN BODY OF JESUS CHRIST DIFFERENT?

Banana Leaf Artwork by Radio Kahuzi Club Members





     ETI MWILI WA KIMUTU WA BWANA YESU KRISTO ULIKUWA TOFAUTI? 
     WAS THE HUMAIN BODY OF JESUS CHRIST DIFFERENT?
       January 17, 1965   
       Pastor Henry F. Kulp 




Waroma 8: 1 – 4 
“Sasa, basi hakuna hukumu ya azabu juu yao walio katika Yesu Kristo, wasiotembea kufuata maneno ya mwili, lakini kufuata maneno ya Roho. 
Kwa sababu sheria ya Roho ya Uzima ulio katika Yesu Kristo imenifanya huru kwa sheria ya zambi na kufa. 
Maana yale yasiyowezekana kufanywa kwa sheria, kwa sababu ilikuwa zaifu kwa sababu ya mwili, Mungu alituma Mwana wake mwenyewe katika mfano wa mwili ulio wa zambi, na kwa sababu ya zambi, alihukumu zambi katika mwili; 
Hata haki ya sheria itimizwe ndani yetu, tusiotembea kufuata maneno ya mwili, lakini kufuata maneno ya Roho.”
Tulifunzwa siku zilizopita kwamba siku ya hukumu ya mwamini, ilifanyika tangu miaka iliyo pita elfu mbili na makumi mawili pale kwa Musalaba wa Kalivari.  
Hukumu ya zambi zetu ilikuwa juu ya Bwana Yesu Kristo, ni kwa sababu ya hiyo mwamini hawezi kuhukumiwa tena juu ya zambi, sababu tayari zambi zake zilikwisha kuhukumiwa. 

1/ Tulitambua na kuona kwamba kuna sheria mbili: 
Sheria ya Roho ya Uzima ulio katika Yesu Kristo na sheria ya zambi na kufa.  
Kila mwanadamu anayezaliwa hapa chini duniani, anazaliwa akiwa chini ya sheria ya zambi na kufa.
Sheria hiyo ilianzishwa na Adamu na iliendelea tangu hapo. 
Lakini, wakati mtu anapookolewa, sheria ya Roho ya Uzima inaanzisha kazi ya Roho Mutakatifu ndani ya roho ya mwamini, na kwa hiyo, Roho Mutakatifu anayekuwa Roho wa Uzima, anatupatia uzima na palepale anatuondosha toka mauti. 
Kwa hivyo, sheria ya Roho ya Uzima ulio katika Yesu Kristo unatufanya huru kwa sheria ya zambi na kufa. 

2/ Musingi gani unao hakikisha kutokuwa na hukumu, na kupokea Roho ya Uzima unaotuweka huru na sheria ya zambi na kufa?  
Aya ya tatu yasema hayo mambo yote? 
 Eti ni kwa njia hiyo ndio Mwenyezi Mungu alimutuma Mwana wake wa Pekee katika mufano wa Mwili ulio wa zambi, na kwa sababu ya zambi, ili ahukumu china  na nyama ya mwili. 
Uzaifu wa mwili unaomba tu Mungu atende. 
Uzaifu wa mwili unakuwa ukuta mkubwa ama kiambazi na nguzo kubwa la ajabu linalo zuiza kila nguvu na tendo njema ya mwanadamu, lakini iyo siyo kibambazi ama nguzo mbele ya Neema ya Mungu. 

Hiyo inatuonesha wazi umuhimu wa aya ya Waroma 8: 3  

3/ Wakati nilipofika kwa Altoona kwa mara ya kwanza, kwa miaka zilizo pita, kanisa nililokuwa naongoza kama Muchungaji, kanisa lilo lilikuwa na makusanyiko ya maombi kwa kila juma na makanisa mengine jirani. 
Kama desturi yetu ya mukusanyo wa maombi, ninakumbuka siku moja kwa saa za maombi yetu ya kila juma, wakati wa mukusanyo wetu wa usiku, tulikusanyika katika moja ya makanisa yale yaliyokuwa pana zaidi kuliko yengine, na hapo tulipokuwa tukizungumuza mawazo yakawaka sana na kuelekea Tabia ya madini yanayochunga desturi na nyengineo yanayofuata maendeleo ya mambo ya kisasa. 
Na Muchungaji wa lile kanisa lililotupokea kwa maombi ya usiku ule, yeye alikuwa wa tabia ya watu wanaoacha wengine huru kwa misemwa, tabia, hata matendo, naye akaleta wazo hili: Ku fwatana na kuzaliwa na bikira, eti munioneshe andiko fulani ya Mutume Paulo inayosema kama ilikuwa lazima Bwana wetu Yesu Kristo azaliwe na bikira. 
Maandiko tunayoyasoma leo haingelikuwa yakusikilika kama hakungelikuwa mwandishi aliyeshurulika kuonesha kwamba KRISTO ni MWANA wa Mungu aliyekuja duniani bila mchango wa baba wa hali ya kimitu. 
Ukweli ni kwamba Mutume Paulo hangeli waza umbalimbali na hayo, yeye aliamini tendo hili kwa roho yake yote. 
Yeye angelikuwa hakutumikisha musemwa: kuzaliwa na Bikira, lakini hata hivyo matunzaji yake ingelikuwa bila maana na ya watu wasio na busara na akili kama hangeliamini bila hata shaka yeyote kwamba Mwokozi wetu Yesu Kristo alizaliwa na Bikira. 

4/ Neno la kwanza ni kwamba Mungu Baba alimutuma Mwana wake Mwenyewe katika mufano wa Mwili ulio wa zambi  
Tufahamu kweli kwamba haisemwi: 
Alituma Mwana wake wa pekee katika Mwili ama katika mufano wa mwili, lakini katika mufano wa Mwili wa zambi. 
Mwili wake ulikuwa kweli mwili halali, mbele na kiisha Ufufuko wake, kama vile inavyosemwa kweli katika injili ya Yoane 1: 14  
Yoane 1: 14 
“Na Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu, tukatazama utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee akitoka kwa Baba, amejaa neema na kweli.” 
Neno likavaa Mwili, likakaa kwetu. 
Mwili wenye Bwana wetu Yesu Kristo alilokuwa nalo, lilikuwa  la nyama na maumbile ya kimutu, ikifanana kwa namna ya kuonekana kwake kama mwili wa kimutu, lakini haikufanywa katika mufano wa mwili wa zambi. 
Kulikuwa tofauti mkubwa kati ya Mwili wake na mwili wetu.   
Inatupasa sisi tujifunze hiyo tofauti ama umbalimbali.

5/ Tuchunguze Maandiko Matakatifu, na tuoneshe kwa mwangaza wa Biblia, kwamba Mwili wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo ulikuwa tofauti na mwili wetu
Matendo 2: 23, 24 
“huyu alitwaliwa nanyi kwa shauri lililokusudiwa, na kwa  kujua kwa Mungu tangu zamani, nanyi mulimsulibisha, mukamwua kwa mikono ya watu wabaya. 
Lakini Mungu alimfufua, akilegeza uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao.” 
Tuchunguze vema maandiko haya: 
Haikuwezekana ashikwe na mauti. 
Tujiulize kwanza, eti neno hili linaweza semeka kwa mwili wetu huu wa kibinadamu? Hapana hata kidogo! 
Kiisha anataja ufunuo wenye Bwana wetu Yesu Kristo anasema juu ya namna na hali ya Mwili wake katika aya ya makumi mbili na saba (27). 
“Kwa maana hutaniacha Roho yangu katika Hadeze, Wala hutatoa Mtakatifu wako aone uharibifu.” 
Ni mwili gani huo usingeliweza kuoza, ama kuona uharibifu? 
Ni kwa sababu ya hiyo Biblia inatufundisha kwamba nguvu zote za uwezo wa kufa unaokuwa ndani ya miili yetu, haikuwa ndani ya Mwili wa Bwana wetu Yesu Kristo. 

6/ Kama ingelikufikia kwenda kwa Kalvari kama Muganga wa kufanya utafiti na kushusha miili yote tatu, hiyo wa Bwana Yesu na yale miwili ya wale wajambazi waliosulubishwa pembeni ya Bwana wetu Yesu Kristo, na hapo wakuambie uandike Kitambulisho cha kiini ya kifo cha hawa watu tatu, miili yote tatu inafanana kwa namna ya inje, sababu wote watatu walipata malipizi ya kifo ya namna sawa. 
Wangelikuambia ulete na kuandika kiini cha kifo chao, utapata matukio mbalimbali kwa sababu, majambazi hawa wawili waliokufa pembeni ya Bwana wetu Yesu Kristo walipata kufa kwa sababu ya vidonda na ukosefu wa damu. 
Lakini Bwana wetu Yesu Kristo, wakati alipoona kwamba yote yametimia na kwamba sasa Yeye yuko tiyari, na saa imefika, akotowa Roho yake.  
Yoane 10: 18 
“Hakuna mutu anaye uondoa kwangu, lakini mimi mwenyewe ninautoa. Nina uwezo kuutoa, na ninauwezo kuutwaa tena. Agizo hili nililipokea kwa Baba yangu.”  
Wakati hawa wajambazi walikuwa wakienda kufa polepole, Bwana wetu Yesu Kristo alikuwa na mamlaka juu ya Uzima wake. 
Tujuwe kwamba Yeye hakuweza kuwa na mamlaka juu ya uchungu na mateso aliyoyapata hapo msalabani kwa wakati ule wa uzaifu na mateso makali. Lakini kwa saa ya mwisho aliinama kichwa chake na kutowa Roho. 
Yeye hakutoweka katika uzaifu mkubwa hata kufikia kiwango cha kutokuweza kusema neno, kwa sababu baada ya saa sita kwa Musalaba Yeye alipaza sauti kubwa.
Mwili wake haukukufa kwa namna ya kawaida. Tusome Luka 23: 46 
“Yesu alipolia kwa sauti kubwa, akisema: Baba, katika mikono yako ninaweka Roho yangu; na alipokwisha kusema maneno haya akatoa Roho.” 
Tuone pia 
Yoane 19: 30 
“Basi wakati Yesu alipopokea ziki, akasema: Imekwisha; akainama kichwa chake, akatoa Roho yake.” 
Kichwa chake haikuwa ya kuinama na kusegemea ubavuni saa zile zote kama ya mutu muzaifu sana.  
Hapana Bwana Yesu alikuwa akiongoza uzima wake hata saa alipo toa Roho. 

7/ Sehemu hii ingestahili kuwa kwa nafasi ya mwanzo, wakati tulikuwa tukizungumuzia jambo la kuwa huru kwa sheria hili ama lile. 
Jameni tutwae mfano moja muzuri: 
Twa tazama kinakidudu kwa udongo, nayo ni ndogo na yenye kutambaa, watu wengi wanakachukia na kukazarahu, lakini kidudu hiki kina uhuru wake wa kutambaa. 
Kidudu hiki kina uwezo wa kutambaa na kupanda kwenye muti, kutambaa kwenye udongo, lakini hakiwezi kujiondosha kwenye udongo ili kiende angani, wala hakiwezi kuruka hewani. 
Kinabana kwenye udongo sababu ya uwezo na kuvutiwa kwa nguvu za sheria za arzi. 
Lakini kiisha muda kitambo, hii kidudu kinajificha katika bahasha lake na kutoka kule kiisha punde kidogo, tayari kinatoka kule kikiwa sasa kipepeo kirembo 
Kwa sasa kina mabawa na kuweza sasa kupinga kuvutwa na nguvu za arzi.
Hakibaki tena tu kwa udongo, lakini kwa sasa kinaweza kutoka kwenye udongo na kuruka hewani. 
Sheria ya kuvutwa kwa arzi haikuondolewa, lakini kuna sheria mupya inayoumbwa ndani. Ni sheria ya kuruka juu na mabawa yakibinafsi.
Ni sawasawa mambo inayo tufikia: 
Sheria ya zambi na kufa inavunjwa na Sheria ya Roho na Uzima ulio katika Yesu Kristo. 
Tumewekwa huru kwa sheria ya zambi na kufa na ni kwa sababu ya hii ndio maana hakuna tena hukumu ya gazabu juu yetu sisi tulio katika Yesu Kristo. 

8/ Turudiliye majifunzo yetu kuhusu Mwili wa Bwana wetu Yesu Kristo, nyama ya mwili wake
Imesemwa kweli kwamba Yeye hakutenda zambi.  
Luka 1: 35
“Malaika akamujibu akamwambia: Roho Mutakatifu atakuja juu yako, na nguvu zake Mungu aliye juu zitakutulia kivuli; kwani kile kitu ambacho kitazaliwa nawe, kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu.” 
Tuchukuwe katika aya hii, msemwa unaosema: kwani kitu kile ambacho kitazaliwa nawe, kitaitwa kitakatifu, hapo inaoneshwa kile kitu kitakatifu kilichozaliwa. Ni kitu kitakatifu, ni kitakatifu cha umilele.   
Mwili wake haukuwa hata na alama moja ya zambi. 
Kuna kundi ya wateologia wamoja wa siku zilizo pita walikuwa wakizungumuzia juu ya neno ya kwamba ilikuwa ingeliwezekana Bwana Yesu Kufanya zambi. Hapana tena hapana hata kidogo, jambo hili haliwezekani. 
Kwa Yeye kupata kutenda zambi, ilikuwa sharti ndani yake mupatikane sheria ya zambi na kufa ili apate kutenda zambi. 
Lakini hakukuwa ginsi mambo haya yawezekane, sababu hakukuwa zambi ndani yake. 

9/ Sababu gani tunalo juhudi na kujitowa sana kuonesha kwamba Mwili wa Bwana wetu Yesu Kristo, na nyama ya Mwili wake haukuwa na sheria ya zambi na kufa? 
Sababu gani tunapenda kusema kwamba Yeye hakuwa na Mwili wa zambi? 

Tupate maelezo maalum katika Waroma 8: 3 
“Maana yale yasiyowezekana kufanywa kwa sheria, kwa sababu ilikuwa zaifu kwa sababu ya mwili, Mungu alituma Mwana wake Mwenyewe katika mufano wa mwili ulio wa zambi, na kwa sababu ya zambi, alihukumu zambi katika mwili;” 
Kwa sababu ya zambi, alihukumu zambi katika mwili. 
Hiyo inamaanisha nini? 
Neno kwa sababu, ama kwa fasi na nafasi ya kitu fulani” inamaanisha kwamba: 
Yeye alifanywa zabihu juu ya zambi zetu. 
Na Yeye alihukumu zambi, alihukumu gazabu ya zambi.
Nafasi gani alihukumu gazabu ya zambi? 
Katika Mwili wake. 
Yeye alikuwa na Mwili pasipo zambi. 
Sisi tuna mwili wa zambi. 
Na wakati Mungu anahukumu zambi, anaihukumu katika mwili.
Lakini Mwenyezi Mungu angelihukumu zambi katika mwili sisi tungelipotea milele. 
Kwa hiyo, Mungu alifanya nini kwa kutuokowa? 
Mungu alikamata zambi inayokuwa katika miili zetu na kuitia katika mwili wake, Mwili wake takatifu na Yeye alikufa ili alipe malipo ya zambi. 

10/ 1 Petro 2: 24   
“Yeye mwenyewe alichukua zambi zetu katika mwili wake juu ya mti, hata sisi, tukiwa wafu kwa maneno ya zambi, tuwe hai kwa maneno ya haki; na kwa kupigwa kwake muliponyeshwa,” 
Tufahamu hapa kwamba siyo neno “juu” iliyo tumikishwa hapa lakini ni neno “katika”.
Yeye mwenyewe alichukuwa zambi zetu ndani ya Mwili wake. 
Alichukuwa zambi iliyokuwa ndani ya miili yetu.
Mungu alimupatia Mwili, Yeye angelipashwa tu kupata Mwili, mwili ulio takatifu, na Mungu alitia miili yetu ndani ya Mwili wake ili ateswe kwa ajili yetu.  

11/ Wagalatia 3: 13   
“Kristo alitukomboa kwa laana ya torati, akiwa alifanywa laana kwa ajili yetu, kama ilivyoandikwa: Amelaaniwa kila mtu aliyetundikwa juu ya mti;”
Ni neno hili ndilo Bwana Yesu alifanya kwa ajili yako na kwa ajili yangu. Na yote ilikuwa katika Mwili wake. 
Kwa kasikia vema hii andiko, yatupasa kusoma kitabu cha 
Kumbukumbu la Torati 21: 22 
“Na mtu akiwa ametenda zambi inayopasa mauti, naye anauawa, nawe utamtundika juu ya mti; 
Maiti yake haitabaki usiku mzima juu ya mti, lakini lazima utamzika siku ile ile; maana yeye aliyetundikwa amelaaniwa na Mungu; usichafue inchi yako ambayo BWANA Mungu wako anakupa wewe iwe uriti wako.” 
Yesu Kristo alitundikwa kwenye mti, laana ya Mungu. 
Na hapa inasemwa kwamba: 
Kama mtu akitenda zambi inayopasa mauti, nikusema hakuna malipizi na mateso nyingine yenye huu mtu anastahili kupata, isipokuwa auwawe. 
Zambi yake italipwa tu na kifo na yeye anapashwa atundikwe juu ya mti. 
Na yeye anapashwa azikwe siku ile ile, kama sivyo kutakuwa laana itakayotoka kwa Mungu. 
Kwa kweli ni hii Bwana Yesu Kristo aliyobeba.
Sisi sote tulikuwa tunastahili kifo katika miili zetu, sababu sisi sote ni wenye zambi, lakini Bwana wetu Yesu Kristo alichukuwa zambi zetu katika Mwili wake na alituweka huru kwa sheria ya zambi na kufa. 

12/ Sisi pekee hatukuweza kujiweka huru kwa sheria hiyo ya zambi na kufa ni Bwana Yesu Kristo peke yake anayekuwa na uwezo wa kuiondoa. 
Ni Yeye pekee anaye uwezo wa kufanywa zambi kwa ajili yetu. 

13/ Wakolosayi 1: 21, 22
“Nanyi, muliotengwa mbali zamani na mulikuwa adui katika nia zenu, kwa matendo yenu mabaya, amewapatanisha ninyi sasa
Katika Mwili wa nyama yake, kwa kufa kwake, ili awalete ninyi mbele yake, watakatifu na pasipo kilema, wala laumu;” 
Aya hii, inatuambia kwamba sisi tulikuwa wanani, hali yetu ilikuwa lini. 
Sisi kama wakristo inatubidi kila mara tuwe tunakumbuka nafasi gani Bwana Yesu alitutosha na kutuokowa.
Mara kwa mara, wakati tunatenda matendo mazuri kama wakristo katika maisha yetu ya kikristo,  hapo tunakuwa na mawazo na kuzania kwamba sisi ni watu wazuri, tunasahau kwamba Mwenyezi Mungu alituokowa kututosha toka yalala ya zambi, chimo ya uchafu na  zambi na mauti, alituokowa na kutupa zambi zetu mbali sana, ni vizuri  mara kwa mara, tukuwe tunakumbuka hiyo. 

14/ Tuchunguze yanayosemwa kwa aya ya makumi mbili na mbili (22):
Katika Mwili wa Nyama yake kwa kufa kwake. 
Ingelikuwa vema mutambuwe kwamba mwisho wa aya ya makumi mbili na moja kwa kuingia makumi mbili na mbili, kiisha neno “amewapatanisha ninyi sasa”, hakuna mukato ama nugta. 
Hivyo hapo tungelisoma: 
Kwa sasa amewapatanisha katika Mwili wa Nyama yake  
Kwa Musalaba tulipatanishwa katika Mwili wa Nyama yake kwa kufa kwake. 
Njia moja inayo unganisha na kupatanisha Mungu na Mwanadamu ni kwamba Bwana wetu Yesu Kristo kuja duniani na kutwaa mwili wa mutu, na hii inatuonesha kwa makini kwamba Bwana Yesu Kristo angelipashwa tu kuchukuwa mwili wa mutu na kuwa mutu kweli. 
Angelipashwa kuwa na Mwili wa nyama. 
Maandiko matakatifu ni wazi na Mutume Paulo iko wazi kwa neno hili. 
Ni katika nyama ya Mwili wake ndio alilipa lipo kubwa la zambi zetu. 

15/ Tuchunguze sasa misemwa: 
Katika Mwili wa Nyama yake, kwa kufa kwake ili awalete ninyi mbele yake, kwa hali gani? Watakatifu. 
Hii ndilo kazi Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo iko anafanya kwa kila mwamini, kila anaye amini Kufa ya Mwana.  
Kwa njia ya kufa kwake aliondowa makosa na zambi zetu na kutuleta mbele yake tukiwa Watakatifu. 
Tuchunguze neno la mwisho katika aya hii: 
Mbele yake
Mungu Mwana atatuleta mbele ya Mungu Baba, na katika uwepo wa Mungu Baba sisi ni watakatifu, pasipo kilema, wala laumu.
O jameni, tutakuwa Viumbe vya namna gani, wakati Mungu Mwana atatupeleka mbele ya Mungu Baba. 
Hakutakuweko hata alama moja ya zambi juu yetu, hakuta kuwa laumu. 
Zambi zote zimetoweka, hakuna tena siku ya hukumu ya gazabu juu yetu. 
Mara tena hapa tunatambua kwamba hakuna tena siku ya hukumu ya gazabu juu yetu. 
Siku yetu ya hukumu imekwisha toweka. 
Hii ni mambo ya muhimi sana, wakati tunapelekwa mbele ya Mungu Baba, sisi ni WATAKATIFU, PASIPO KILEMA, WALA LAUMU,   namna gani kuwe siku ya hukumu ya gazabu kwa waamini wanaokuwa katika hali hii? 

16/ Katika Miradi ya Mwenyezi Mungu, hakuna kitu kingine chenye kinangojewa kuonekana ndani ya hii muda hadi KUNYAKULIWA KWETU. 
Hakuna miradi nyingine iliyo pangwa. 
Kazi hii nzuri na ya manufaa inaendelea, tendo la kukusanya waamini na kuwageuza kuwa watakatifu, kazi hii kubwa ya Mungu inafanya kila mwamini anaye amini kifo cha Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo anafanywa kuwa Mutakatifu na watu hawa wote wanaonyeshwa kuwa watakatifu, kwa siku hiyo ya kupelekwa mbele ya Mungu Baba. 
Siku Nzuri ya shangwe na Ajabu na Tukufu.  

17/ Tufahamu kwamba Wakolosayi 2: 9 
“Maana katika Yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu kwa mwili.” 
Katika Bwana Yesu Kristo unakaa utimilifu wote wa Mungu kwa Mwili, utimilifu wote wa Utatu Mutakatifu. 
Tuchunguze neno Kwa mwili” 
Siku zilizo pita nilipata kuona tafsiri ama kufafanua iliyonipendeza sana: 
UTIMILIFU WOTE WA MUNGU UNAKAA NDANI YAKE KATIKA MWILI. 
Hii ndiyo ukweli wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo anaye kaa sasa kule mbinguni kwa mukono wa kuume wa Mungu Baba. 
Na Mwili wake wa kimutu, Mwili wenye Mungu Baba aliomutayarishia,
Mwili aliyo pewa wakati alizaliwa Bethleemu. 
Utimilifu wote wa Mungu unaikaa ndani ya mwili wa kimutu. 
Ni tendo la Mastaajabu ya shangwe naya kushangaza kweli.  
Mpaka kwa siku ya leo Yeye ana Mwili ule, Nyama ile. 
Nafsi ya Pili katika Utatu Mtakatifu ni Mutu kweli sawa vile ni MUNGU kweli. Yeye ni Mutu kweli. 
Tuchunguze sasa aya ya kumi (10) 
“Na ninyi mumetimilika katika Yeye aliye Kichwa cha falme zote na mamlaka.” 
Ninyi muko na vyote katika Yeye, mumetimilika katika Yeye. 
Kuwa wakutimilika nikusema hakuna kitu kilicho achwa, hakuna kitu kilicho sahaulika, hakuna kitu kinachokosa. 
Wazo gani nzuri katika KRISTO. 
Yeye anaye ishi Mbinguni. 
Aliye kufa katika NYAMA yake na NYAMA yake njo ilibeba zambi zetu. 
Sisi tunatimilika, hatukose kitu chochote, tumetimilika katika Yeye. 
Ukweli nzuri, tamu na ya ajabu. 


AMEN
 
N°Ref: 01/17/1965 / 285 - WAS THE HUMAN BODY OF JESUS CHRIST DIFFERENT / 05/12/2020

No comments:

Post a Comment