Thursday, April 23, 2020

TUMAINI LA BARAKA / BLESSED HOPE


Photo taken from B Smith's Kitchen Window









     289 - TUMAINI LA BARAKA / BLESSED HOPE
     March 7, 1965 
     Pastor Henry F. Kulp





Waroma 8:14 -17 
“Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hawa ndio wana wa Mungu.
Kwa maana hamukupokea tena roho ya utumwa inayo leta woga, lakini mulipokea roho ya kufanywa wana, kwa sababu hii tunalia: Aba, Baba. 
Roho mwenyewe anashuhudu pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu: 
Na kama sisi tu watoto, basi tu wariti: Wariti wa Mungu, na wariti pamoja na Kristo; kama tukiteswa pamoja naye, ili tutukuzwe pamoja naye vilevile.”

Katika magazeti iliotangazwa na kusomwa munamo tariki 24 Marchi, mwaka wa 1965, kulikuweko tangazo juu ya mabishano yenye yalikuwa yakitarajiwa kati ya makanisa ya ki protestanti mujini. 
Gazeti hiyo ilikuwa ikisimamiya juu ya maandiko na masemi ya makundi tatu mbalimbali ya kiteologia kuhusu yale wanao amini juu ya maisha ya wanamemba wao wa protestanti kwa siku zile. 
Ijapokuwa walikuwa na mapingano juu ya mambo kazaa, wote walikuwa wakiamini kwamba yafaa kupunguza maneno moja moja katika Biblia Takatifu, maneno yote yenye wao walizani kwamba hailingani na maisha ya kingwana (siku za sasa). 

Kuna maandiko katika Biblia yenye mutu wa siku za leo hakubali wala kuamini. Na kwa kweli hii ni maarifa ya Ibilisi. 
Mbele ya kutenda jambo lolote, ningewasihi muone na kutambua umuhimu na mafaa makuu ya Biblia. 
Kuna Mambo makuu ya muhimu na ya faida sana yenye tutachunguza katika sura ya nane ya Barua ya Mtume Paulo kwa Waroma, inawezekana kwamba wengine wanaweza kukamata maandiko haya kama kawaida, kama kwao Biblia haiko Neno la Mungu, yaani Maandiko Matakatifu. 

1/ Katika semina yetu tuliyofanya kwa miaka iliopita juu ya kanuni na kawaida ya Kiprotestanti, tulizungumuzia juu ya kanuni na kawaida ya ortodoksia mupya. 
Yawezekana wewe umeisha sikia juu ya kundi hili, ama kwako yaweza kuwa ni mara ya kwanza, lakini wale tuliokuwa nao kwa semina iliyopita walisikia mengi juu ya neno hili. 
Kanuni na kawaida hii inasema na kuamini kwamba: 
Maandiko Matakatifu yaani Neno la Mungu iko tofauti na Yesu Kristo. 
Wanasema kwamba eti unaweza kuamini Bwana Yesu Kristo bila kuamini Neno la Mungu. 
Wanatangaza kuwa Imani yetu inapashwa jengwa juu ya Yesu Kristo pekee hapana juu ya Neno la Mungu.
Jameni muniruhusu ni niwaulize swali moja: 
Namna gani utafikia kwa kiwango cha kumwamini Bwana wetu Yesu Kristo bila mwangaza wa imani unao kuja wakati unasikia Neno la Mungu? 
Watu wale wanatofautishi Neno iliyofanyika Mwili na Neno lililoandikwa. Ijapokuwa hakuna tofauti kati ya Neno lililo vaa Mwili na Neno lililoandikwa. 
Hakuna hata tofauti moja. 
Katika Yoane 1: 1, tunasoma: 
“Katika mwanzo alikuwa Neno, na Neno alikuwa pamoja na Mungu, na Neno alikuwa Mungu.” 
Yesu ni Neno.   Neno ni Mungu. 
Sasa tushuke hapo chini katika Yoane 1: 14 
“Na Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu, tukatazama utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee akitoka kwa Baba, amejaa neema na kweli.” 
Neno alifanyika mwili ni YESU. 
Neno lililo andikwa, kila andiko ni Yesu Kristo na ni Yeye Neno iliofanyika Mwili. 
Tunalofahamu ni kwamba Neno alifanyika Mwili, na tunajuwa hivyo kupitiya usomi wa Neno lililo andikwa, ama kupitiya maandiko Matakatifu. 
Waweza namna gani kuwa na ufahamu wowote juu ya Bwana Yesu bila kusoma Biblia? 
Namna gani kufikia kupata maelezo makubwa kuhusu Bwana YESU bila kusoma Neno lililoandikwa? 

2/ Ninafahamu kwamba kitabu hiki ninachoshika mukononi kiliundwa toka kiwanda cha kuchapa vitabu. Hivi kita zeeka na kuchakaa siku moja. 
Kweli, kila miaka miwili, mimi ninalazimishwa kununua Biblia ingine mupya wakati ile ya kwanza inachakaa na kupasuka pasuka. 
Ninaacha ile ya zamani na ninakwenda kununua ingine mpya. 
Sababu vikartasi havishikamane na kuungana tena pamoja sababu kila wakati kitabu hicho kilikuwa kikitumikishwa mara kwa mara na siku kwa siku. 
Wakati unatia kando Biblia ya zamani inayo chakaa sana, wewe hautupilie Neno la Mungu sababu uliuza Biblia ingine mupya. 
Ni Maandiko inayoandikwa katika kitabu hiki njo iko ya mafaa kabisa.
Hapana makartasi, habani utonvi waliotumikisha kwa kuunganisha makartasi, cha Muhimu ni Neno pekee.  

3/ 2 Timoteo 3: 16 
“Kila andiko limepewa kwa maongozi ya Mungu, na linafaa kwa mafundisho, na kwa kuonya watu juu ya makosa yao, na kwa kuwaongoza na kwa mafundisho katika haki.” 
Kila mmoja wetu angelipashwa kuchunga aya hii kwa ufahamu katika moyo wake. 
Kila andiko limepewa kwa maongozi ya Mungu. 
Neno, andiko linamaanisha yale yaliyoandikwa. 
Nikusema kila andiko imepewa kwa maongozi toka kwa Mungu ama Pumzi ya Mungu. 
Tuchunguze sasa neno “Maongozi ama Pumzi.” 
Katika Kiswahili, pumzi ya, ni kusema kukokota hewa kwa kupumuwa.
Hii inaweza maanisha neno la Kigriki inayo patikana hapo. Sasa ikawa kukokota hewa inje ama ndani, hiyo siyo tatizo, lakini tunafahamu kwamba Mwenyezi Mungu alipuliza pumzi. 
Hatufahamu kama Mungu alipulizia ndani ama inje lakini inatuonesha kwamba Kila andiko limepewa kwa pumzi ya Mungu. 
Pumzi ya Mungu ni Neno la Mungu, haijali fasi tunapolikutana, ni Nafsi ya Pili katika Utatu Mtakatifu. 
Bwana Yesu Kristo, anayekuwa Neno, Yeye ni Pumzi ya Mungu. Neno ni Pumzi ya Mungu. 

4/ Twende sasa kwa Waroma 8: 17  
“na kama sisi tu watoto, basi tu wariti: Wariti wa Mungu, na wariti pamoja na Kristo; kama tukiteswa pamoja naye, ili tutukuzwe pamoja naye vilevile.” 
Kwa hiyo, hakika watu wengi hawapendi kusikia hivyo. 
Watu wengi wakati wanaposoma Biblia, wanakusudia kuruka na kutambuka maneno haya, wakiyapita juu juu bila kutiya mukazo. Kwa kweli hawangepashwa fanya hivyo. 
Sisi ni wariti pamoja na Kristo. 
Kuna tofauti kati ya kuwa muriti,  na kuwa muriti pamoja. 
Juma iliyopita, tuliwaonesha umbalimbali ulio katika maneno haya mawili. 
Tulisema kwamba: 
Kama mutu akifa na anaacha nyuma yake shamba kubwa kwa watoto wake wane, eneo ile itagawanywa kwa watoto wake wane. 
Na kila muriti atapata sehemu yake asili mia makumi mbili na tano: 25%. 
Lakini kama mutu nyuma ya kufa akiachia watoto wake shamba kubwa, na wote wakiwa kama Wariti pamoja; 
Kila mmoja wao anaruhusa ya kusema nyumba ni yangu, kibandaholi ni changu, shamba ni langu, eneo lote ni langu, mali inayokuwa kwenye Banki ni yangu. 
Kwa namna ya umutu wa leo mambo haya ni magumu.
Lakini ni hivi itakuwa mbinguni sababu tutafananishwa na Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. Ndiyo maana nilipendelea mufahamu tofauti hii kubwa. 

5/ Niliwapa moja ya ma shairi ama aya inayojaza roho yangu na furaha kubwa: 
 1 Wakorinto 3: 21 
“Basi, mutu ye yote asijisifie watu, kwa sababu vitu vyote ni vyenu;” 
Ni vitu ngapi vinavyo kuwa vyenu? 
Muniruhusu kuwauliza swali hilo. 
Jibu lenu inaweza kuwa gani? 
Vitu vyote ni vyenu. 
Ninyi ni watajiri sana kupita namna munavyo wazia, watajiri kupita mwisho wa mawazo ya kibinadamu. 
Tufahamu vema kwamba inasemwa hapa: Ulimwengu wote ni yangu. 
Na ni ya Yesu Kristo, na kwa kuwa sisi ni wariti pamoja na Yesu Kristo, chochote kile kinakuwa chake, kinakuwa vilevile changu. Uzima ni wangu na kufa ni yangu. 

6/ Tulikuwa tukizungumuzia juu ya Kufasiri vema Neno lililo kweli. 
2 Timiteo 2: 15 
“Dumu kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mfanya kazi asiyeona haya, ukifasiri vema neno la kweli.” 
Kuna umbalimbali kati ya maneno inayoelekea Taifa la wana wa Israeli, Ufalme wa Mungu na Kanisa Mwili wa Kristo. 
Kwa kufahamu vema Uriti unaokuwa ndani yetu, Uriti ambao sisi ni wariti pamoja na Bwana Yesu, yafaa kwetu tuchunguze hali yetu na uhusiano wetu na Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 
Mutume Paulo alituandikia Vitabu kumi na tatu na hapo hatuingize kitabu cha Wahebrania, sababu sisadiki kama ni Mutume Paulo aliyeandika kitabu hicho. 
Na katika Barua yote kumi na tatu Mutume Paulo aliyoandika, hakuna hata fasi moja aliposema kwamba Bwana ni Muchungaji wetu. 
Hii ni ukweli moja ya mizani sana, lakini tunaona kwamba Mutume Paulo aliiweka kando, sababu uhusiano yenye iko kati ya muchungaji na kundi lake siyo iyo inayopatikana kati ya KRISTO na KANISA MWILI WA KRISTO. 
Uhusiano unaopatikana kati ya KANISA MWILI WA KRISTO na KRISTO ni uhusiano wa kichwa na mwili. 
KRISTO ni Kichwa na Sisi ni Mwili. 
Ni sababu ya hiyo ndio maana katika Barua za Mutume Paulo, hakuna hata nafasi moja aliosema kwamba Bwana Yesu ni Muchungaji wetu na kwamba sisi ni Kondoo za Kundi lake, Mutume Paulo hakusema neno hili hata mara moja. 

7/ Mutume Paulo haja tarajia kusema kwamba Bwana Yesu ni Mufalme wetu, anasema tu Yesu ni Mufalme wa wafalme na Bwana wa mabwana. Na Mutume Paulo haja tarajia kusema Bwana Yesu ni Mufalme wa Kanisa Mwili wa Kristo. 
Hapa duniani, kama  tuwatu wa mufalme wa inchi fulani, sisi wakaaji wote  katika huo ufalme tunakuwa na mapashwa na tunarizika namna sawa, na pia kuna hata watu wengine wenye hawana bahati ya kumwona mfalme uso kwa uso hata kwa mara moja maishani mwao. Wao hawazaliwe katika jamaa la kifalme ama hawana hata urafiki moja na mufalme kwa hivyo hawawezi hata kumuona ana kwa ana hata mpaka kufa kwao.  
Kwetu sisi wakristo hatuko namna sawa. 

8/ Mutume Paulo hajawai kusema kwamba KRISTO ni Mwalimu wetu. 
Yeye hakumuita Bwana Yesu Rabbi. 
Usomapo Vitabu ine vya Injili, utaona kwamba kwa kumwita Bwana Yesu, wanatumia jina Rabbi, Mwalimu. 
Kama vile Barua za Mutume Paulo zinavyosema, kwetu sisi Bwana Yesu haiko Mwalimu. 
Ni ROHO MTAKATIFU ndiye Mwalimu wetu. 
Anatufundisha juu ya Yesu Kristo, anashuhudia Yesu Kristo, anatuongoza katika yote yaliyo kweli juu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 
Tunatambua kweli kwamba uhusiano unaokuwa kati ya mwalimu na mwanafunzi siyo ule unaokuwa kati ya KRISTO YESU na KANISA MWILI WA KRISTO.
Mwanafunzi anaweza akasikilize mwalimu wake na kushika yote anayofundisha na kupata faida ya mafundisho yote, lakini mwanafunzi huyu hampendi hata kidogo mwalimu wake.
Munajuwa wanafunzi wengi wanaoshuhudia kama mwalimu tunaye ni mzuri, anafundisha safi sana lakini sura na umbo wake haunipendezi hata kidogo.
Ni kwa sababu hiyo njo maana Mutume Paulo hakusema hata kidogo kwamba Bwana wetu Yesu Kristo ni Mwalimu wetu. 
Roho Mutakatifu anatufundisha na kutushuhudia juu ya Bwana wetu Yesu Kristo mpaka anatusukuma kumpenda Mwokozi wetu zaidi na zaidi tena.  

9/ Sisi ni viungo vya Mwili wake na KRISTO ndiye KICHWA.  

10/ Kama vile tunavyoendelea kuchimbua majifunzo haya,   itakuwa ya muhimu sana kufahamu tofauti inayo kuwa kati ya kuwa KIUNGO CHA MWILI WA KRISTO na kuwa MWANAMEMBA WA UFALME WA MUNGU. 
Uriti wetu haugawanyiki, sasa,   kuwa mwanamemba wa KANISA MWILI WA KRISTO, inamaanisha nini? 
Neno ngumu hapo ni “KUGAWA” uendapo sisi ni Wariti pamoja na KRISTO. 
Uriti wetu siyo wa kugawanya katikati yetu sababu sisi ni wariti pamoja na Kristo, tunariti yote kama vile Maandiko inatuambia katika                         
1 Wakorinto 3: 21 – 23 
“Basi, mutu ye yote asijisifie watu, kwa sababu vitu vyote ni vyenu; 
Kama Paulo, au Apolo, au Kefa, au dunia, au uzima,au kufa, au vitu vya sasa, au vitu vya kuja; vyote ni vyenu, 
Na ninyi ni wa Kristo na Kristo ni wa Mungu.”
YESU KRISTO hata gawanya nasi uriti kwa nusu. 
Ole kwao wanaotiya uvuguvugu katika ufahamu wao juu ya mambo inayo elekea UFALME WA MUNGU na KANISA MWILI WA KRISTO, Wayuda na Mwili wa Kristo, wenye kutiya uvuguvugu hawata tambua umbalimbali huu. 

11/ Luka 19: 11 – 19 
“Nao wakisikia maneno haya, aliendelea kusema mfano, kwa sababu alikuwa karibu na Yerusalema, nao walizania ya kama ufalme wa Mungu utaonekana mara moja. 
Basi alisema: Mtu mmoja mwenye heshima alisafiri kwenda inchi ya mbali kupokea kwake mwenyewe ufalme na kurudi. 
Akaita watumwa wake kumi, akawapa feza kumi, akawaambia: 
Fanyeni biashara hata wakati nitakaporudi. 
Lakini watu wake walimchukia, wakatuma wajumbe kumfuata, wakisema: 
Hatutaki mtu huyo kutawala juu yetu. 
Ilikuwa aliporudi, nyuma ya kupata ufalme, akatoa amri kuita wale watumwa ambao aliwapa feza, apate kujua namna ya biashara aliyofanya kila mtu. 
Wa kwanza alikuja, akasema: 
Bwana, feza yako imepata feza kumi. 
Akasema: Vema, mtumwa mzuri; kwa sababu umekuwa mwaminifu kwa neno dogo sana, uwe na mamlaka juu ya miji kumi. 
Na wa pili alikuja, akisema: 
Bwana, feza yako imepata feza tano. 
Akamwambia: Nawe uwe juu ya miji mitano.” 
Fahamu vema kwamba hii inahusika na Ufalme wa Mungu duniani, hapana Mwili wa Kristo, sababu kwenye aya yake ya kumi na moja Biblia inasema kwamba: Alisema hivyo sababu alikuwa pembeni ya Yerusalema, na kwamba nao walizania ya kama Ufalme wa Mungu utaonekana mara moja. 
Na aliwaambia fumbo ama mufano huo juu ya kuwaonesha kwamba haija timia bado nyakati ya Ufalme wa Mungu kuonekana mara moja. 
Na Yeye mwenyewe alijifananisha na yule Mutu moja mwenye heshima aliyeenda inchi ya mbali, - Yeye alienda Mbinguni. 
Alikwenda mbinguni kisha kufa kwake na kufufuka alipanda juu mbinguni.
Na Yeye atarudi tena ili apokee Ufalme wake, na inasemwa kwamba Yeye aliita watumishi wake kumi(10), akawapa feza kumi na akawaambia fanyeni biashara mpaka wakati nitakaporudi. 
Wakati gani na namna gani watumwa hawa watafanya biashara? Sasa hivi. 
Sisi hatuko watumwa, sisi ni Viungo vya Mwili wake Kristo. 
Kwa kweli, kurudi hii inayosemwa hapa, ni kurudi kwa mara ya pili kwa Mwokozi wetu Yesu Kristo, hii safari siyo ya kuchanganya na KUNYAKULIWA kwa KANISA, inayokuwa wakati Mwokozi wetu Yesu Kristo atakuja kuchukuwa Kanisa Mwili wa Kristo. 
Aliita watumishi wake na alipenda kupata ripoti ya viashara vyao. 
Wa kwanza alikuja, akasema: Bwana, feza yako imepata feza kumi. 
Akasema: Vema, mtumwa mzuri; kwa sababu umekuwa mwaminifu kwa neno dogo sana, uwe na mamlaka juu ya miji kumi. 
Na wa pili alikuja, akisema: Bwana, feza yako imepata feza tano. 
Akamwambia: Nawe uwe juu ya miji mitano.
Ni vema muvumbuwe kwamba hapa mufano huu hausemwi juu ya Kanisa Mwili wa Kristo. 
Mungu hakuahidi hii juu ya Kanisa, lakini ahadi hii ni juu ya Israeli. 
Uriti wetu pamoja na KRISTO hautagawanyika, sisi ni wariti pamoja na KRISTO. 
Yote inayokuwa ya Bwana wetu Yesu, yote yale ni yetu na tunayo pamoja naye. 
Mungu hatagawanya uriti wetu, ni kweli, ni ajabu na ni Baraka kubwa na ni hivyo. 

12/ Tukumbuke neno moja la muhimu.
Bwana wetu Yesu Kristo hatatuambia fanyeni biashara hata wakati nitakaporudi. 
Mwokozi wetu atatuambia: Vitu vyote ni vyetu, furahini pamoja NAMI. 
Hii ndiyo tofauti. 

13/ Matayo 19: 27 - 28  
“Halafu Petro akajibu, akamwambia: Tazama sisi tumeacha yote, na kukufuata, sisi tutapata nini basi? 
Yesu akamwambia: Kweli ninawaambia ninyi, ya kwamba ninyi ambao mulinifuata, katika ulimwengu mupya, wakati Mwana wa watu atakapoketi juu ya kiti cha utukufu wake, ninyi vilevile mutaketi juu ya viti vya ufalme kumi na viwili, mukihukumu makabila kumi na miwili ya Israeli.”
 Tunaona hapa Bwana Yesu anazungumuza kuhusu makabila kumi na miwili ya Israeli na hakusema chochote kuhusu Mataifa. 
Wao watakuwa wakimiliki chini ya uongozi wa ufalme wa Yesu wakati ataketi juu ya kiti cha utukufu wake. 
Kwetu sisi wariti pamoja na Yesu haitakuwa sawa vile. 
Kweli tutamiliki nazani sisi tutakuwa tunamiliki tukiwa huko mbinguni. 
Sisi hatutamiliki chini ya uongozi wa Bwana Yesu, lakini sisi tutamiliki pamoja na Bwana Yesu. 
Hii ndiyo tofauti kati ya Kanisa Mwili wa Kristo na Ufalme wa Mungu. 

14/ Sasa tuangalie kwa makini sana neno la mwisho lenye linapatikana katika shairi ili: 
“kama tukiteswa pamoja naye, ili tutukuzwe pamoja naye vilevile.” 
Msemwa huu unamaanisha kama yatupasa kuteseka pamoja naye ili tutukuzwe pamoja naye.
Sawa vile tafsiri ya Kigriki inaonesha; 
Tunaona kwamba Maandiko hayasemi kuteswa kwa ajili ya Bwana Yesu, lakini Maandiko yanasema kuteseka pamoja na Bwana Yesu. 
Na kanuni kubwa lenye tuko tunajifunza katika shairi hii ya Waroma ni kanuni ya UTAMBULISHO YA KUUNGWA NDANI YA YESU
Tunateswa pamoja na Bwana Yesu, hapana kwa ajili ya Bwana Yesu. 

15/ Kama basi ni hivyo maneno yale tatu mu Kigriki ni A- PEAR, na kama unapenda kupata tafsiri nzuri ya neno –PEAR, tusome katika 
1 Watesalonika 1: 6 
“Mukakuwa wafuataji wetu, na wafuataji wa Bwana, mukikwisha kupokea neno katika mateso mengi, pamoja na furaha ya Roho Mtakatifu;” 
Yakuwa kwamba neno hili ni halali kwa Mungu.  Na neno yakuwa kwamba ndio tafsiri ya neno A-Pear ya kigriki. 
Sasa shairi hiyo ingelitafsiriwa ifwatavyo: 
Yakuwa kwamba tukiteswa pamoja naye, ili tutukuzwe pamoja naye vilevile. 

16/ Mateso haya siyo mateso ya maisha ya kawaida. 
Tangu wakati tuliungwa na KRISTO, ni halali tungojee yale yote aliyopata Mukombozi wetu Bwana Yesu Kristo. Hayo yasituuzunishe kwa maana tutatukuzwa pamoja naye vilevile na kuishi milele pamoja naye. 

17/ Kuna mateso yanayoambatana na wanaadamu na mateso haya mengi ni ya kimwili. 
Tunapata uchungu, unyonge na maumiwu, tunateseka na magonjwa, misiba mbalimbali, hata misiba ya arzi. 
Sisi sote siku moja tutakufa, miili yetu inazorota siku kwa siku na hiyo inatupatia mateso ya kimwili, lakini hayo yote siyo mateso Mungu anayo tuzungumuzia hapo.  

18/ Kunakuwa kuvunjika mioyo, na hii inafikia watu wote, waliookolewa kama wapagani wote wanateswa kwa kuvunjika mioyo.
Tunaneseka na magumu mbalimbali inayotuzunguuka, inayokumbwa na vita ya chinichini ya mataifa makuu duniani, magumu inayoletwa toka mahali petu pa kazi ya kila siku. 

19/ Kuna mateso hiyo ya kimutu inayotufikia wakati tunatambua kwamba ndugu yetu fulani iko anapitia katika kipindi cha shida na maangaiko makubwa, tunaweza tukiwa bila tatizo, lakini tunapoona ndugu katika shida na maangaiko hadi kufikia kufa, nasi tunashiriki yale mateso pamoja naye. 
Lakini Mungu hazungumuzie mateso kama hiyo hapa.

20/ Mungu anatuzungumuzia mateso yenye tunateswa pamoja naye. 
Kukataliwa, kuchukiliwa, kuzarauliwa. 
2 Wakorinto 4: 18 
“Kwa sababu hatuangalii vitu vinavyoonekana; lakini vitu visivyoonekana: Kwa sababu vitu vinavyoonekana ni vya saa kidogo tu, lakini vitu visivyoonekana ni vya milele.” 
Hapa tunazungumuziwa juu ya ile utukufu utakaokuja na ukubwa wa ajabu wa utukufu kubwa sana utakao uzunguuka.
Mara kwa mara inakuwa magumu kwetu kulinganisha namna utukufu ule utakuwa. 
Hatuweze kufahamu kukadirisha utukufu huo, sababu unashinda mafikili yetu kama watu wa dunia hii. 
Sisi tunatarajia utukufu na hakuna mateso yoyote inayotufikia tunayoweza kulinganisha na utukufu wenye tutapata yenye Mungu Baba anayo tayarishia wewe na mimi. 
Tazama Baba Mungu anasema hapa: 
Mateso ya sasa hayawezi linganishwa na utukufu yenye itafunuliwa ndani yetu.  
Hii inaburudisha nafsi yangu sana. 
Ninatamani sana wewe utukuzwe siku moja, sijuwe kama utafanana namna gani lakini utavaa utukufu na mimi vilevile pamoja nawe. 

21/ Tuone kwamba 2 Wakorinto 4: 17 inasema: 
“Kwa sababu mateso yetu mwepesi yaliyo kwa dakika tu, yanatufanyia utukufu wa milele unaozidi mwingi sana;” 
Hapa tuna nyakati mbili zinazopingana, nyakati ya muda na umilele. 
Mateso yetu hapa chini duniani ni ya muda kitambo. Yanadumu miaka kumi na miwili, sawa mfano iyo ya ndugu John Bunyan. 
Ama mateso inaweza kuwa ya maisha mzima, hiyo isikusumbue, si kitu, ni ya faida ndogo sana sababu siku moja tutapata utukufu wa milele unaozidi mwingi sana.  
Angalia umbalimbali kati ya mambo iliyo ya muda kitambo na utukufu wa milele unaozidi mwingi sana yenye tutariti. 
 
AMINA.

N°Ref: 03/07/1965 / 289 - BLESSED HOPE / 03/04/2020 

No comments:

Post a Comment