Monday, April 20, 2020

MUNGU NA MDUDU / GOD AND THE WORM

Photo taken by from B Smith's Kitchen Window







299 - MUNGU NA MDUDU / GOD AND THE WORM
June 27, 1965 
Pastor Henry F. Kulp 





Waroma 8: 30 - 34 
“Na wale ambao aliwachagua tangu zamani, akawaita vilevile; na wale ambao aliwaita, akawahesabia haki: na wale ambao aliwahesabia haki, akawatukuza vilevile. 
Basi tutasema nini juu ya maneno haya? Kama Mungu akiwa upande wetu, ni nani aliye juu yetu? 
Yeye asiyeachilia Mwana wake, lakini alimtoa kwa ajili yetu yote, namna gani atakosa kutuletea vitu vyote pamoja naye? 
Ni nani atakayeshitaki wachaguliwa wa Mungu? Mungu ambaye anawahesabia haki; 
Ni nani anayehukumu? Ndiye Kristo aliyekufa, ndiyo, zaidi, amefufuka, naye yuko kwa mkono wa kuume wa Mungu, tena ndiye anatuombea.” 

 Juma jana tulipata maelezo zaidi juu ya kuonesha, kupitia Baruwa ya Mtume Paulo kwa Waroma kwa shairi yake ya nane, namna UMUNGU wa MUNGU unakuwa upande wetu. 
Huyo UTATU Mtakatifu, Mungu Roho Mtakatifu, Mungu Baba, Mungu Mwana, na kwa kweli,  namna UTATU MTAKATIFU uko kwa upande wetu, hakuna hata mmoja atakayepima kuwa juu yetu. 
Jameni ndugu waona mahali pa ajabu, raha na utukufu kwenye twapatikana sisi tulioamini Yesu Kristo. 
Kama kungelikuwa kitu chenye kingekusisimua unene “aleluya”, hii ndicho.

1/ Wakati nilipokuwa nikichunguza maandiko haya, mawazo yangu ikaelekea moja kwa moja katika kitabu cha Isaya. 

Isaya 41: 11 – 14 
“Tazama, wote waliokasirika juu yako watapata haya na kufazaika; wao wanaoshindana nawe watakuwa si kitu, na wataharibika. 
Utawatafuta wala hutawaona, hata wao wanaopigana nawe: 
Watakuwa kama si kitu, kama kitu kisichokuwa, wale wanaofanya vita juu yako. 
Kwa maana mimi, BWANA, Mungu wako nitashika mkono wako wa kuume, nikikuambia: Usiogope, nitakusaidia. 
Usiogope, wewe mdudu Yakobo, nanyi watu wa Israeli; nitakusaidia, Bwana anasema, na mkombozi wako, Mtakatifu wa Israeli.” 

Shairi hiyi inatuambia kwamba Mungu alikuwa upande wa Israeli, kwa kweli ni hivyo, Mungu alikuwa upande wa Israeli kama Inchi inayoonekana machoni mwa watu hapa duniani. 
Mungu aliambia Israeli: 
Tazama, wote waliokasirika juu yako watapata haya na kufazaika; wao wanaoshindana nawe watakuwa si kitu,  na wataharibika. 
Utawatafuta wala hutawaona, hata wao wanaopigana nawe: watakuwa kama si kitu, kama kitu kisichokuwa, wale wanaofanya vita juu yako. 
Mungu alijulisha Israeli kwamba: 
Utakuwa na maadui, utakuwa na wao watakao sirika juu yako, lakini nini itakayo wafikia? 
Nyuma ya mambo yote watapata haya na kufazaika, watakuwa kama sikitu  na wale wenye wanaoshindana nawe wajuwe kwamba wataharibika. 
Na wakati utawatafuta, hutawaona. 
Na kwa kweli, ni maneno haya ndiyo wana wa Israeli wangelipashwa kutamka wakati wowote ule wangeli pata adui. 
Kama Mungu iko pamoja nasi(Israeli), ni wanani wale wanaoweza kuwa juu yetu? 
Wanaweza kushindana na Israeli lakini nyuma ya maneno yote watashindwa.  

2/ Hapo, tunafika kwa aya ya kumi na ine(14),  wazo inataka kuwa sawa  ya ziaka na kuwa sawa umbalimbali na ya kwanza na kwa mwisho inatuonesha wazi utupu wa mwanadamu, pia inasema  kwamba mwanadamu  hana samani hata moja na kwa ngambo nyingine inatuonesha samani kubwa sana ya nguvu za ajabu za Mungu kupitia matendo yake. 
Tukumbuke kama Mungu aliambia taifa la Israeli kwamba: Adui wako hawatakushinda kamwe watakuwa kama sikitu. 
Kiisha Mungu  akasema: 

Usiogope wewe mdudu Yakobo, mimi nitakusaidiya… O Mungu mkuu. Patano gani hii! 
Mungu na mdudu. 
Mara kwa mara Israeli walikuwa wakianguka sababu hawakuwa wanatambua kwa kweli kama wao ni wanani. 
Wana wa Israeli walikuwa midudu. 
Wakati watu wanafanya patano la kazi, mmoja analeta mchango wa kipesa, mwengine analeta ujuzi wake ama mambo ingine kazaa ya kazi yao. 
Lakini wakati tunafanya patano na Mungu, 
Yeye anatuomba tu tuheshimu maagizo yake. 

Tunaleta mchango wa unyonge wetu na Yeye analeta mchango wa Nguvu zake. 
Sisi tunaleta zambi zetu na Yeye analeta Neema na Haki. 
Sisi ni washuhuda wa utupu yetu na Yeye anatujibu kwamba anavyo vitu vyote. 
Mungu na mdudu. 
Mungu anasema kwamba mutu yeyote asipime kupinga ama kubishana na patano hii. 
Ajali gani wana wa Israeli waliokuwa nalo wakati walishindwa kukubali upotevu, na anguko lao na kuitika uepo wa ujazi na utimilifu wa Mungu katika vyote. 

3/ Kwa kweli hii ndiyo mambo ya siku za leo.
Kumbukeni, sawa vile tulivyo jifunza katika masomo yetu ya saa ya usiku kwa siku zilizopita, Tuliona namna Mwenyezi Mungu alivyosema, kwa kutaja Mwenyezi Mungu, tunamwona  Bwana wetu Yesu Kristo, alisema kwamba mataifa ni imbwa na kiisha akalinganisha wayuda na nyoka na kizazi cha nyoka na hapa wanaitwa mdudu ama midudu. 
Hawakuwa kweli na kitu cha kutowa.
Patano yenye ilifanywa kati la taifa la wana wa Israeli na Mungu ilifanyika kwa namna hii: Mwenyezi Mungu akiwa mwenye kuleta vitu vyote. 
Kwa siku za leo tunajikuta tuko mikono mitupu, hatuna kitu hata kimoja chenye tunaweza kuleta kwa Mungu, lakini Yeye anatutolea vyote, tuangalie vema nini anayosema katika aya hii. 
Basi tuseme nini juu ya maneno haya? 
Kama Mungu akiwa upande wetu, ni nani aliye juu yetu? 
Yey asiyeachilia Mwana wake, lakini alimtoa kwa ajili yetu yote, namna gani atakosa kutuletea vitu vyote pamoja naye? 
 Ni nani atakayechitaki wachaguliwa wa Mungu? 
Mungu ambaye anawahesabia haki; 
(Ni nani anaye hukumu)? Ni Mungu, hakuna kitu kinacho fanyika na mwanadamu. Ni Mungu anaye fanya vyote.
Ndugu yangu shikamana na nafasi yako ya mdudu mbele ya Mwenyezi Mungu na umwache Yeye afanye vyote kwa faida yako. 

4/ Tutazame vema nini inayosemwa kwa sehemu ya kwanza ya aya ya makumi tatu na moja(31). 

Basi tutasema nini juu ya maneno haya? 
Ni ulizo inayofwata mambo yote makuu na ya  ajabu Mungu anayo tufunulia hapo juu. 
Tunaona kwamba katika mistari ifwatayo, tunapata majibu mazuri Mwenyezi Mungu anazo patia kila aliye amini Bwana wetu Yesu Kristu, kwa kuweza kujibu. 
Kwanza: Mungu ni upande wetu. 
Ya pili, kwa aya ya makumi tatu na mbili (32):

Yeye asiyeachilia Mwana wake, lakini alimtoa kwa ajili yetu yote, namna gani atakosa kutuletea vitu vyote pamoja naye? 
Si fahamu vema kama tunajuwa kwa makini maana ya msemwa: 
Mungu Baba alimtoa Mwana wake. 
Sijuwe kama siku moja umeisha kaa kabisa na kuanza kujiuliza na kutafuta kufahamu hali gani inayoweza kuwa ndani ya nyumba maali mupendwa, mutu wa mafaa sana, mutu yule anayependwa sana katika ile nyumba, mutu yule aondoshwe katika ile nyumba. 
Nina waza na kujiuliza kama Mbingu ilikuwa katika hali gani na kufanana namna gani wakati Bwana wetu Yesu Kristo alipoacha mbingu na kuja hapa duniani. 
Aliacha vyote na kuja mikono mitupu.  
Nazani munakumbuka prezidenti moja wa inchi ya Marekani jina lake ilikuwa Calvin Coolidge. 
Wakati alipokuwa angali bado katika mamlaka, mtoto kijana wake alikufa. 
Nazani mtoto yule alikuwa na umri wa miaka 17. 
Yeye alikuwa akifanya mazoezi ya mchezo wa mbio ya miguu katika boma la michezo la masomo, na hapo katika mazoezi ya kwenda mbio, mguu wake ulijikwaa kwenye musumari ama kisiki, na damu chafu ilibaki mwilini bila kutiririka inje, na Muganga alipofika, hakuweza kumuokoa. 
Baada ya hayo, bwana Coolidge alipoteza na kukata tamaa yoyote ya kuishi. 
Tamaa yake hata yakufanya kazi ya Inchi ilipotea, ijapokuwa yeye alikuwa Prezidenti mwenye alikuwa anachapa kazi vizuri sana na kwa moyo wote kupita hata wa prezidenti walio mtangulia. 
Na wakati watu walipima kumsisimua ili awe tena kandideti katika mapambano ya kiti cha uraïsi wa Marekani, yeye alikataa na akasema hapana. 
Walipomuuliza kwa nini anakataa, akajibu kama Yeye hapendi. 
Lakini nyuma alipozungumuza na watu wake wa karibu, aliwaambia kwamba kukataa kwake kwa kugombea tena kiti cha uraïsi wa Marekani kunasababishwa na kifo cha kijana wake, kifu ile ilimuondowa hamu yote na sababu yote ya kuishi.  
Mungu Baba, yeye haiko wa hali, tabia na aina hii. 
Lakini nalinganisha na kutambua kwamba hata kwa Mungu Baba, ilikuwa huzuni sana kumutoa Mwana wake wa pekee kushuka hapa Duniani. 
Katika Injili ya Mutakatifu Yoane inaoneshwa wazi kwa mara makumi ine(40) kwamba Bwana Yesu alikuwa akipaza sauti akisema: “Mimi sikuja kwa shauri langu mimi pekee.” 
Mungu Baba ndiye aliye mtuma Bwana wetu Yesu Kristo. 
Mungu Baba aliona namna gani Mungu Mwana aliteswa, alikataliwa, na kuchukiwa, kutupiliwa na mwisho kuuwawa. 
Utakumbuka kama mbambo haya yote yalipitikana wakati alikuwa bado akifundisha na kutenda maishara hapa duniani na kwa muda huwo wote watu walikuwa wakitafuta kwa nguvu zao zote wamshike ili auwawe. 

5/ Hii ni Alama ya Mapendo. 

6/ Kitambo bado nilikuwa nikijiuliza kama katika Maandiko Matakatifu, yaani Biblia, neno Mapendo, ilitamkwa kwa mara ya kwanza nafasi gani. 
Sijuwi kama mumekwisha kusikia juu ya neno lenye watu wenye kujifunza teologia ama elimu ya Biblia na Kimungu, neno wanaloita Dalili na Masikilizano ya kwanza. 
Nikusema wakati wajuzi wa Biblia wanakuwa na haja ya kufahamu neno ama jambo fulani, wanatafuta katika Biblia kama, ni katika Kitabu gani, sura gani na aya gani neno hili lilitajwa kwa mara ya kwanza. Na kwa kweli shahiri ilo itapatikana. 
Neno Mapendo ilitajwa kwa mara ya kwanza katika Biblia ndani ya 

Mwanzo 22 : 2 
“Akasema: Twaa sasa mwana wako, mwana wako wa pekee ambaye unampenda, hata Isaka, uende zako hata inchi ya Moria; umtoe pale kwa sadaka ya kuteketezwa juu ya mmoja wa milima ambao nitakuambia.” 

 Ni kusema jameni, namna gani na kwa hali gani upendo ulitajwa? 
Ni namna gani upendo unatumikishwa katika maandiko haya? 
Mungu alisema: 

Twaa sasa mwana wako, mwana wako  wa pekee ambaye unampenda na kwa kweli, umtoe kwa sadaka ya kuteketezwa. 
Hii njo mwanzo wa Mapendo katika Biblia.   
Na ni mapendo gani? 
Ni mapendo ya baba kwa mtoto wake mume.  
Ni mapendo ya baba kwa mtoto wake mume ambaye alipashwa kumtoa kama sadaka. 
Kwa kusema kweli, hii ni mfano maalum ya picha ya Musalaba wa Kalvari, ni mfano kamili wa Kalvari. 
Katika Biblia Takatifu, ni Abrahamu pekee anaye kuwa mfano wa Baba anayemtoa mtoto wake mume kama sadaka ya kuteketezwa. 
Mungu aliambia Abrahamu: Twaa sasa mwana wako, mwana wako wa pekee ambaye unampenda. 
Abrahamu alikuwa na mtoto mwengine, Ismaeli, lakini Mungu alisema simutambue  na simjui. 
Twaa mwana wako wa pekee, Isaka, unayempenda, umtoe kwangu kama sadaka ya kuteketezwa. 
Ni hapo mwanzo wa mapendo katika Biblia.  

7/ Ni heri sana nyinyi mujuwe kwamba: 

Misumari waliopigilia katika mikono ya Mwokozi wetu, hiyo misumari ilipenya ndani ya Roho ya Mungu Baba. 
Mukuki iliyochomwa kwa ubavu wa Mwokozi wetu, mukuki huyo uliacha alama ndani ya mapendezi ya Baba.
Mungu Baba aliteswa pamoja na ndani ya Mungu Mwana. 

8/ Neno hili linakamatana na picha hii ya Mungu na Mdudu. 
Wakati nilikuwa nikifikiri juu ya taifa la wana wa Israeli, nilifikiri juu ya picha ingine inayokuwa kati ya Mungu na Taifa lile, 

Yeremia 20: 11 
“Lakini Bwana yuko pamoja nami, kama mpiga vita mwenye kuogopesha; kwa hivi wenye kunitesa watajikwaa, wala hawatashinda; wataona haya kubwa. Kwa sababu hawakutenda kwa akili, wataona haya ya milele, isiyoweza kusahauliwa kamwe.”  
Utafsiri maalum wa aya hii ni: 

MWOKOZI WANGU YUKO PAMOJA NAMI KAMA SHUJAA MKUBWA MWENYE UWEZO, NANI ANAYE WOGA?  
Na ninawaza kweli kwamba hiyo ndiyo tafsiri bora inayo maanisha shairi hilo. 
Shairi hilo inaonesha picha ya kijana mdogo mwanaume mwenye alikuwa anasumbuliwa sana na kuteswa vibaya akigombanishwa na jirani kijana mwengine mukubwa kuliko yeye. Huyo kijana mdogo akawa mwenye woga kiasi na kutetemeka mara kwa mara mpaka kuwa na woga wa kutoka nyumbani na kwenda kucheza inje, sababu kila wakati na dakika alikuwa na woga asije akapigwe vikali na wale vijana jirani wakubwa. 
Sasa, siku moja, baba yake mzazi akaja mbele yake na kumwambia, mwana wangu twende pamoja kwa hiyo duka inayo kuwa pale kwa lukumba ya njia. Na kweli, kwenda kwa ile duka ni kupita katika ile njia kwenye wale vijana wanaume wakubwa kwake wanaomuogopesha na kumutetemesha wanazoezi ya kungoja na kusimama.  
Lakini kwa sasa kijana huu mdogo hana woga yoyote hata kidogo. Anakwenda njiani akitelemuka pamoja na baba yake anaye mushika kwa mukono wake. Kwa sasa yeye hana woga wowote, anawatizama washambulizi wake wakisimama kwa nafasi zao za kawaida, anawaona moja kwa moja lakini yeye haogopi kitu, sababu sasa yeye yuko pamoja na mutu anayeweza kumulinda na kumukinga, mutu mukubwa sana na shujaa, mwenye nguvu na nwenye uwezo kupita wale washambulizi na wachokozi wote na ni hii picha ndiyo tunayo katika hiyo shairi. 
Nabii Yeremia anasema: Lakini Bwana yuko pamoja nami kama Shujaa Muhodari Mukuu Mwenye nguvu. Mungu akiwa upande wangu, nani aliye juu yangu. 
Hakuna hata mchokozi mumoja mwenye anaweza simama mbele ya Shujaa Muhodari Mkuu Mwenye nguvu.  


9/ Ningelipendelea tuchikamane na maana ya maneno haya: 
Yeye asiyeachilia Mwana wake” 
Hii maneno ni ya muhimu sana kutambuwa na kuchunguza. 
Wengi wetu hawafikilie kutambuwa kwamba Mungu ni Mwenye haki na Mutakatifu kwa hiyo anapashwa kuhukumu zambi. 
Wanazani kama wanaweza ishi hapa ulimwenguni namna wanaotaka na hata ivyo Mungu anaweza akawaponye kwa kuwatupa kwa jehanamu. 
Shairi hili litatuonesha kwamba hiyo mawazo ni ya upumbafu. 
Kweli, nyinyi hamuja kuta musemwa ama neno “hakuachilia” katika Biblia Takatifu? 
Tusome 2 Petro 2: 4  
“Kwa maana ikiwa Mungu hakuachilia malaika wakati walipokosa, lakini aliwatupa shimoni, na kuwatia katika vifungo vya giza walindwe hata hukumu.”  
 Sawa sawa jinsi Mwenyezi Mungu hakuachilia malaika wake wakati walifanya zambi ndivyo vile Mwenyezi Mungu hata achilia hata mufanya zambi mmoja sababu yeye iko kiumbe kamilifu na kizuri kweli. 
Malaika wanakuwa na nguvu zaidi kuliko sisi, wanakuwa warembo zaidi kupita sisi, lakini wakati walipokosa Mungu aliwahukumu palepale bila kungojea, kwa hivyo tusipime kuzubaa na kuzania sababu wewe ni murembo, mukamilifu, mwenye nguvu za kimwili ama wewe unakuwa na nafasi nzuri mbele ya macho ya Mungu na uzubae kuwaza kwamba sababu ya hayo, Mungu atakuachilia hata ufanyapo zambi, kwa kweli Mungu hatakuachilia. 
Zambi inaleta laana, ni hivyo, ni laana tu njo zambi inaleta.  
Unaweza kuwa mutu wa neno, mfalme, unaweza kuwa raïsi, mutu wa serkali, mutu wa ma kampuni mbalimbali, mutu wa sayansi, hakuna hata kitu kinaweza sukuma Mungu aachilie  mutu atendae zambi asipite kwenye hukumu, sababu zambi inapashwa kuhukumiwa. 

10/ 2 Petro 2: 5  
“Wala hakuachilia ulimwengu wa kale, lakini alilinda Noa pamoja na wengine saba, mhubiri wa haki, wakati alipoleta garika juu ya ulimwengu wa wale wasioogopa Mungu;” 
 Hapo tunakuta tena msemwa huo: “hakuachilia” 
Tunajifunza hapo kuusu wao waliotenda zambi mbele ya wakati wa garika ya Noa.  
Tujiulize miyoyo ngapi iliangamia na garika? 
Ni vigumu kujuwa idadi ama jumla ya mioyo ya watu iliyo angamia na garika, lakini neno moja ya kweli ni kwamba watu wengi walipoteza maisha yao na garika kwa wakati ule. 
Kwa kweli fundisho maalum tunalopata hapa ni kwamba umati kubwa ama jumla kubwa la watu haukutuma Mwenyezi Mungu awaepushe na garika, 
Unaweza kupambazushwa na kudanganywa na umati kubwa wa watu wenye bado kumwamini Bwana Yesu; na kujiuliza: umati huo hauambie Mungu kitu? 
Umati mkubwa wa watu na idadi yao haitatuma Mwenyezi Mungu kuepusha hukumu juu ya zambi. 

11/ Pia  kwa aya ya sita(6) 
“Tena akahukumu miji ya Sodomo na Gomora akiipindua na kuifanya majivu, akaifanya iwe mfano kwao watakaokaa pasipo kuogopa Mungu.” 
 Hapo Mungu anataja na kuzungumuzia uharibifu wa Sodomo na Gomora. 
Hata kama Mtume Petro hakutumikisha msemwa “hakuachilia”, sawa na namna tuliona hapo juu, wazo inabaki tu ya namna moja. 
Hata moja ya miji hii miwili haikuachiliwa, Mungu aliponyesha tu Loti na mabinti zake wawili.  
Miji hii mbili ilipeperushwa na kupinduliwa sababu wakaaji walifanya zambi. 

12/ Katika Waroma 8: 32  
“Yeye asiyeachilia Mwana Wake, lakini alimtoa kwa ajili yetu yote, namna gani atakosa kutuletea vitu vyote pamoja naye? 
 Zambi ni tendo la kuhatarisha sana ni kwa hiyo, mbele ya zambi yoyote kutafuta kusamehewa ama mutenda zambi kusamehewa ili ahesabiwe mwenye haki, ilimupasa Bwana Yesu Kristo kufa Musalabani ili alipe malipo ya zambi na afe kwa nafasi ya huyo mutenda zambi. 

13/ Tuangalie namna sehemu ya pili ya aya hii inavyosema. 
Waroma 8: 32 
“…lakini alimtoa kwa ajili yetu yote.” 
Sasa unatambua msemwa: “alimtoa kwa” 
Nikusema kulikuwa na muda ambao Mungu Baba alimtoa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo.  
Alimtoa kwa. 
Alimwachilia sababu ya neno fulani. 
Aya hii haiseme kama Mungu Baba alitupatia Mungu Mwana.
Lakini Mungu Baba alimtoa kwetu. 
Na ninafahamu kwamba kama tukijikaza kujuwa, tutafahamu kwamba Mungu Baba alimtoa kwa kitu fulani, kwa ajili yetu,  na ni kwa njia hiyo ndiyo tutasikia na kufahamu aya hii. 
Kulikuwa na muda ambao Bwana Yesu Kristo alitolewa kwa MATESO

14/ Tupime kujifunza mambo yaliyo pitikana kunako Bustani ya Gethsemani. 
Nazani kwamba imetupasa kusoma na kufahamu historia hiyo, tusijali mara ngapi tumekwisha kulisoma. 
Ninauhakika kwamba kila wakati mutakalo isoma lazima mutapata kitu kipya kingine. 

Luka 22: 53  
“Kila siku nilipokuwa pamoja nanyi katika hekalu hamukunyosha mikono yenu juu yangu; lakini saa hii ni yenu, na mamlaka ya giza.” 
 Pale Gethsemane, Bwana wetu Yesu Kristo alikuwa katika uchungu sana, na alitetemeka kwa uchungu, nazani hiyo msemwa ndiyo   namna nzuri ninalo weza kupima kueleza nalo. 
Na kwa uchungu ule kubwa alipaza sauti akisema: Baba hakuna njia nyingine la kunywa kikombe hiki? 

Luka 22: 42 – 44 
“akasema: Baba, ukipenda, uniondolee kikombe hiki; lakini si mapenzi yangu yafanyike, ila mapenzi yako. 
Malaika toka mbingu alitokea, akampa nguvu. 
Naye alikuwa katika uchungu sana, akazidi kuomba kwa bidii; na jasho yake ilikuwa kama matone ya damu yanayoanguka kwa udongo.” 
 Kiisha alikuja kwa wanafunzi wake, akija kwa bustani ya Gethsemane na alianguka kifulifuli akitia uso chini na akaomba tena. 
Lakini hakukuwa tena jibu kutoka mbinguni kwa ajili ya maombi yale. 
Hii ndilo jambo nilikuwa napenda tuchunguze.   
Hakukukuwa tena jibu kutoka mbinguni juu ya maombi yale.
Alipoomba mara mbele ya hapo na hata akachoka kabisa, Malaika toka mbinguni alitokea akampa nguvu. 
Hakuwa tena na nguvu za kimutu ili aone hayo mapito katika hali ya kimwili. Ni kwa sababu ya hiyo njo Baba Mungu alimutumia Malaika toka mbinguni ili amutie nguvu, lakini hakukuwa jibu toka mbinguni juu ya ombi aliloomba. Kiisha akatoka kwenye bustani. 

Na Luka 22: 53 
“Kila siku nilipokuwa pamoja nanyi katika hekalu hamukunyosha mikono yenu juu yangu; lakini saa hii ni yenu, na mamlaka ya giza.” 
 Bwana Yesu alikutana na Yuda aliyekuwa akisindikizwa na waaskari, waandishi, mafarisayo na makuhani wote wakiwa na silaha za fimbo. 
Walikuwa wanashika silaha ili wamushike na kumufunga Bwana Yesu Kristo.
Bwana wetu Yesu Kristo aliwaambia kila siku nilipokuwa pamoja nanyi katika hekalu hamukunyosha mikono yenu juu yangu; lakini saa hii ni yenu, na mamlaka ya giza. 
Chunguza vema hii misemwa ifwatayo. 
Mamlaka ya giza  
Ni hapo Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo alitolewa kwa Mamlaka ya giza. 
Tangu hapo hakuwa hata na neno moja la musaada toka juu mbinguni. 
Juu ya Musalaba Yesu alilia: Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha? 
Kumbuka kwamba hapakuwako mutu yeyote aliyekuwa akimshika, lakini palikuwako nguvu za giza. 
Mbele ya hapo, malaika alikuja kumupa nguvu, lakini kwa Msalaba hapakukuwa msaada yoyote. 
Hakuna malaika aliye msaidiya pale kwa kalvari, hakuna malaika alie msaidia wakati alipokuwa katika mikono ya watesi wake.
Walimupiga makofi usoni, walimutemea mate. Na kwa kutemea mutu mate, yafaa uwe kabisa pembeni yake na kumusogelea sana. Walimukokota nywele kichwani wakati walipomupiga makofi. 
Walimufunga kipande cha nguo machoni na kumufungilia kwa nguzo na kumupiga mijereti. 

15/ Ni sawa ukipita katika njia ndogo kati ya pori kubwa yenye miti mikubwa na majani ya kufungana, na kwa gafla, mutu mwenye wazimu anarukaa mbele yako na silaha mikononi akikugeuzia silaha hizo.
Waweza kufahamu woga wa aina gani utakao kushika wakati utashituka na mtetemeko gani wa woga utalipuka na kukujaa? Ni hiyo hali ndiyo tunapata hapa. 

16/ Tuangalie namna misemwa iliundwa hapo katika shairi hii: 
Haikusemwa: 

Yeye atapashwa kutupatia vitu vyote bure. 
Lakini imesemwa: 
Namna gani atakosa kutuletea vitu vyote. 
Yeye alitupatia vyote. 
Namna gani yawezekanavyo sisi kufikiri kwamba Mwenyezi Mungu aliyefanya hivyo kwa kututolea Mwana wake, namna gani yawezekanavyo Yeye tena atuombe kitu chochote kile? 
Neno hili haliwezekani hata kidogo. 
Haiwezekani kwa Mungu kuwa na hitaji ya kitu kutoka kwetu, sababu Yeye alitutolea Mwana wake, Alitupatia VYOTE Alivyokuwa navyo. 
ALITOA VYOTE VYAKE.   

17/ Tuchunguze sasa kwa makini neno KWA BURE 
Kwa Kigriki, inatoka kwa neno DOE-RAY-ON. 
Inamaanisha Bila neno lolote, Bila malipo. 

Yoane 15: 25 
“Lakini litimie neno lililoandikwa katika torati yao: Walinichukia bure.” 

AMEN
 
N°Ref:  06/27/1965 / 299 - GOD AND THE WORM / 2020 

No comments:

Post a Comment