Sunday, September 20, 2020

WOKOVU WAKO WAKUTEGEMEA WEWE? / DOES YOUR SALVATION DEPEND ON YOU?

Photo taken by B Smith from the kitchen door



 


WOKOVU WAKO WAKUTEGEMEA WEWE?

DOES YOUR SALVATION DEPEND ON YOU?

June 26, 1977 

Pastor Henry F. KULP



 

Wakolosayi 1: 20 – 23 

“na kwa yeye kupatanisha vitu vyote kwake, akiwa amefanya salama kwa njia ya damu ya msalaba wake; kwa yeye, kama ni vitu duniani au vitu mbinguni. 

Nanyi, muliotengwa mbali zamani na mulikuwa adui katika nia zenu, kwa matendo yenu mabaya, amewapatanisha ninyi sasa katika mwili wa nyama yake, kwa kufa kwake, ili awalete ninyi mbele yake, watakatifu na pasipo kilema, wala laumu; kama mukidumu katika imani, mukiwekwa juu ya msingi na kusimama imara, wala hamugeuzwi mbali na tumaini la Habari Njema muliosikia, iliyohubiriwa katika viumbe vyote chini ya mbingu; nami Paulo nilifanywa mtumishi wake.”  

Aya ya 22 inasema:

“Katika Mwili ya Nyama yake, kwa Kufa kwake, ili awalete ninyi mbele yake, watakatifu na pasipo kilema, wala laumu;”

Mungu anatuambia kwamba sisi tu watakatifu na pasipo kilema, wala laumu mbele yake. 

Sitambue ingine aya ya raha na utukufu kama hii katika Biblia, na mambo haya yote ni kweli sababu KRISTO alikufa kwa sababu yetu. 

Pia wakati tuendapo kwa aya ya 23, tunaona kwamba neno la kwanza linalokuwa kwa mwanzo wa aya hii ni “kama”, kiisha palepale inatushimamisha kwa gafla. 

“kama mukidumu katika imani, mukiwekwa juu ya msingi na kusimama imara, wala hamugeuzwi mbali na tumaini la Habari Njema muliosikia, iliyohubiriwa katika viumbe vyote chini ya mbingu; nami Paulo nilifanywa mtumishi wake.”   

Kuna wale wanaojidanganya wakizania kwamba aya hii inasema kwamba mtu aliyeokoka anaweza kutereza na kuanguka na kufikia kiwango cha kupotea.  Hii ni uwongo.

Hii siyo maana yenye Mutume Paulo analeta katika aya hii. 

Mutume Paulo hafundishi Kawaida ya Mafundisho mawili mbalimbali ya utunzaji yenye kubishana na kukanushana kabisa. 

Kama kwa upande moja anafundisha Amani ya milele na uhakika wa kuwa na Uzima wa milele, kwa upande ungine, hawezi kufundisha uwezekano wa kuanguka hadi kupoteza wokovu. 

Na tunafahamu bila shaka yoyote kwamba Biblia nzima inatufundisha kuhusu Amani ya Milele, Uhakika wa Wokovu ya milele,  Salama ya milele na ina ya fundisha wazi wazi. 

1/ TUFAFANUE AMANI YA MILELE AMA SALAMA YA MILELE AMA UHAKIKA WA WOKOVU YA MILELE. 

Wale ambao Baba Mungu aliwakaribisha na kuwakubali katika Mwana wake Mupendwa aliwaita na kuwatakasa katika ROHO MUTAKATIFU hawawezi kamwe kuanguka milele ama kuanguka kwa mwisho toka neema ya Mungu, wao watakaza mwendo mpaka mwisho wakiwa na wokovu wa milele.


2/ Huu ufafanuzi unakuwa na musingi wake katika aya mbalimbali za Biblia Takatifu.

Tuchunguze kwanza maandiko katika Waebrania 7: 25

Waebrania 7: 25 

“Naye, kwa sababu hii anaweza kuokoa kabisa wao wanaokuja kwake Mungu kwa njia yake; maana yeye ni hai siku zote apate kuwaombea.” 

Tambua kwamba aya hii haiseme tangu mwisho, lakini inasema mpaka mwisho hivi tutaisoma namna ifwatayo: 

NJIANI MWOTE SIKU ZOTE HADI MWISHO. 

Kuna wale wanaozania kwamba Amani ya Milele ama Salama ya milele ni hiyo kudumu ya watakatifu ama waamini, lakini hiyo si kweli.

Siyo waamini wanaoweza kudumu na kusubiri. 

Ni Mungu anayedumu na kusubiri ndani ya watakatifu.

 

Waroma 6: 23  

“Kwa maana mushahara wa zambi ni mauti, lakini zawadi ya Mungu ni uzima wa milele katika Yesu Kristo Bwana wetu.” 

Hapa tunasoma kwamba: lakini zawadi ya neema ya Mungu ni uzima wa milele. 

Kwanza: 

Mungu hakutupatia uzima wa milele sababu tulikuwa tunastahili. 

Tunayostahili ni kufa kwa milele na hukumu. 

Ya pili: 

Hatukupewa uzima wa milele kwa sababu ya matendo yetu na tena uzima wa milele hauwezi kuondolewa kwetu kwa sababu ya matendo yetu. 

Hatukupokea wokovu kwa sababu ya matendo yetu pia hatuwezi poteza wokovu kwa sababu ya matendo yetu. 

Matendo haina sehemu katika wokovu wetu, hata mbele ya wokovu, hata nyuma ya wokovu, wokovu ni zawadi ya Mungu mwenyewe.


4/ 2Timoteo 1: 9, 10 

“ambaye alituokowa akatuita kwa mwito mtakatifu, si kwa kadiri ya matendo yetu, lakini kwa kadiri ya kusudi lake mwenyewe na neema yake, tuliyopewa katika Kristo Yesu mbele ya nyakati za zamani, 

Na sasa imefunuliwa na kuonekana kwa Mwokozi wetu Yesu Kristo, aliyebatili kufa, na kufunua uzima na maisha yasiyokoma kwa njia ya Habari NJema.” 

Mwenyezi Mungu alituokowa na akatuita kwa mwito mutakatifu, si kwa kadiri ya matendo yetu. 

Matendo yetu haina muchango hata moja katika wokovu wetu. 

Kazi yenye Bwana Yesu aliyotimiza msalabani pa kalvari ndiyo iliyonunua wokovu wetu.

 

5/ Wokovu wetu siyo miradi yenye Mwenyezi Mungu alipanga ama kupata wazo wakati mtu alipoanguka zambini, bali ni ahadi ya Mungu aliyotayarisha tangu umilele uliopita. 

Tito 1: 2, 3 

“katika tumaini la uzima wa milele, Mungu asiyeweza kusema uwongo, aliuahidi mbele ya nyakati za milele; 

Lakini akafunua neno lake kwa nyakati zake katika mahubiri, niliyowekewa amana kama amri ya Mungu Mwokozi wetu;” 

Katika tumaini la uzima wa milele, Mungu asiyeweza kusema uwongo, aliuahidi mbele ya nyakati za milele.

 

6/ Kazi ya Roho Mutakatifu inakuwa  ushahidi ungine juu ya salama ya milele. 


Waefeso 1: 13 - 14  

“Ndani yake ninyi vilevile, wakati muliposikia neno la kweli, Habari Njema ya wokovu wenu, ndani yake mumekwisha kuamini vilevile na kutiwa mhuri wa Roho Mutakatifu ya ahadi. 

Ndiye aliye arabuni ya uriti wetu, ili kuleta ukombozi kwa mali yake mwenyewe, kuwa sifa ya utukufu wake.” 

Ndani yake ninyi vilevile, wakati muliposikia neno la kweli, Habari Njema ya wokovu wenu, ndani yake mumekwisha kuamini vilevile.

Ni hii utaratibu wa kawaida. 

Kiisha kuamini, tunatiwa muhuri ya Roho Mutakatifu. 

Mhuri wa Roho Mtakatifu, Yeye ndiye arabuni ya wokovu wetu. 

Waefeso 4: 30   

“Wala musihuzunishe Roho Mtakatifu ya Mungu, ndani yake mulitiwa mhuri hata siku ya ukombozi.” 

Tunasoma hapa kwamba hatupashwe huzunisha Roho Mtakatifu ndani yake tulitiwa mhuri hata siku ya ukombozi, hapana hata siku tutapoteza wokovu wetu.  

Siku ya ukombozi inamaanisha siku ya ukombozi wa miili yetu.

 Wakati Bwana Yesu atarudi kutuchukuwa, miili yetu ya haya itafananishwa na Mwili wake wa Utukufu, Mwili wa Ufufuko wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 

Wafilipi 3: 21 

“atakayebadilisha mwili wetu wa haya upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uwezo ule anaoweza kutiisha vitu vyote viwe chini yake.” 

7/ Waroma 3: 24  

“Wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Yesu Kristo:” 

Mwamini iko katika salama sababu yeye anahesabiwa haki. 

Sasa kuna neno kubwa iliyotafsiriwa na kasoro kidogo, ikituweka kama watu wenye bado kutenda zambi. 

Nikusema tungelikuwa kama wasio na hatia. 

Adamu, mbele ya kuanguka kwake katika zambi, alikuwa katika hali ile sawa asiye na hatia, lakini kuhesabiwa haki ni bora zaidi kupita hali ile. 

Kuhesabiwa haki ni kutangazwa kuwa mwenye haki sawasawa na Mwenyezi Mungu aliye MWENYE HAKI. 

Hapana kuwa sawa asiye na hatia.


8/ Waroma 4: 5 na Waroma 3: 24 inatuambiaya kwamba: 

“… kwa mtu asiyefanya kazi, lakini anamwamini yeye anayehesabia haki wasioogopa Mungu, imani yake inahesabiwa kuwa haki” kwani

“Wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Yesu Kristo:” 

Tufahamu kwamba kwa njia ya neema yake KRISTO, mtu muovu anahesabiya haki.

Hapana wale wanaoishi maisha ya usafi. 

Hapana wale walio wazuri kufwatana na mwenendo wao wenyewe.

 

9/ Twende sasa katika kitabu cha Wakolosayi 1: 23 

“kama mukidumu katika Imani, mukiwekwa juu ya msingi na kusimama imara, wala hamugeuzwi mbali na tumaini la Habari Njema muliyosikia, iliyohubiriwa katika viumbe vyote chini ya mbingu ; nami Paulo nilifanywa mtumishi wake.” 

Tuliwaonesha kupitiya Maandiko Matakatifu kwamba mwamini hawezi kujiokoa kwa njia ya matendo yake mema, na kwamba hawezi kupoteza wokovu wake kwa sababu ya matendo aliyofanya. 

Sasa, ni nini Mutume Paulo anataka maanisha wakati anaposema kwamba sisi tutakuwa watakatifu pasipo kilema, wala laumu mbele ya mecho ya Mungu, kama tukidumu katika imani. 

Neno “kama” inaonesha sharti ya hali, na inamaanisha “kama, na ni kweli kama”, 

Nikusema kama kweli, na ni kweli munaendelea katika imani. 

Tunakuwa na namna mbaya ya kutumia neno “kama” toka Kigriki wakati inapotumiwa sawa sharti ya muhimu na inayohitajika. 

Ni sawa mtu anayesema: Nitakwenda kuogelea kwa bahari kama nvua hainyeshi. 

Bali, hii siyo maana tunayokuwa nayo hapa. 

Hapa, inamaana kusema, ni kweli. 

Siyo sharti. 


10/ Neno kuendelea, ama kudumu ni EPEE – MEN – O. 

Epee inamaanisha juu. 

Meno inamaanisha kukaa. 

Na kama tukichanga yote pamoja tunapata: 

Kuendelea kukaa, ama, kudumu katika kutenda jambo fulani. 

Na neno imani, PISS – TIS na ina  tanguliwa na makala kamili mbele yake, hivi itatafsiriwa kama ifwatavyo: 

KAMA UKIENDELEA NA KUDUMU KATIKA KUSADIKI MAFUNDISHO YA BIBLIA NA UKIYATENDA. 

Imani inamaanisha Kusadiki Mafundisho ya Biblia, na neno kuwekwa juu ya msingi inamaanisha KUTIYA MSINGI, na neno kusimama imara ni KUTOKUTIKISIKA.

Ni kusema wewe hauongeze kitu kwa mafundisho ya Biblia, bali unaamini yale Biblia inayofundisha kuhusu wewe na Bwana wetu Yesu Kristo.


11/ Wala hamugeuzwi mbali na tumaini la Habari Njema. 

Kwa halisi hiyo inamaanisha hapana kujitenga kando, na neno TUMAINI ni kuwa na uhakika AL –PUS. 

Kuwa na uhakika katika Habari Njema, hapana kujitenga kando ya Habari Njema. 

Habari Njema muliosikia na iliyohubiriwa kwenu. 

Neno kuhubiri KAY – RUE SO inamaanisha kutangaza hazarani. 

Pia angalia kwa makini maneno haya: 

Nami Paulo nilifanywa mtumishi wake. 

Ni nini Mtume Paulo anataka kutuambia hapo? 

Anapenda kutufahamisha kwamba tunapashwa kudumu katika kawaida ya  mafundisho yale aliyotufundisha, tutie msingi wetu katika kawaida ya mafundisho yale, na tusimame imara, tusitikisike, tuki weka tumaini letu ndani ya  Habari Njema. 

Habari Njema iliyofundishwa na Mutume Paulo. 

Waroma 2: 16 

“Katika siku ile Mungu atakapohukumu siri za watu, sawasawa na Habari Njema yangu, kwa Yesu Kristo.” 

Pia tufahamu kwamba Waroma 16:25 inasema:  

“Kwake yeye anayeweza kuwasimamisha ninyi sawasawa na Habari Njema yangu na kwa mahubiri ya Yesu Kristo, kama ufunuo wa siri iliyowekwa tangu nyakati za milele,” 

2 Timoteo 2: 8 

“Ukumbuke Yesu Kristo, aliyekufa toka wafu, wa uzao wa Daudi, kama inavyosema Habari Njema yangu.” 

Nikusema kwamba ni Habari Njema ya Mutume Paulo ndiyo inayo funua Kweli hii, kwamba nyinyi munakuwa sasa watakatifu, pasipo kilema wala laumu mbele ya Mungu.

Hakuna  sheria , wala amri ila tu Imani katika Yesu Kristo inayo tutiya katika hali hii. 


12/ Wakolosayi 1: 24 

“Basi sasa ninafurahi katika mateso yangu kwa ajili yenu, na ninatimiza katika mwili wangu yale yaliyokosa ya mateso ya Kristo kwa ajili ya mwili wake, ndio kanisa lake.” 

Hii ni aya moja ya upekee na yenye maana. 

Kuna wamoja wenye hawafikilie kuifahamu na wanapotosha misemwa hayo wakisema kwamba mateso ya Bwana wetu Yesu Kristo pale Msalabani hayakuwa kamili, na ya kwamba ni Mutume Paulo aliye musaidiya kwa kuitimiza. Hii siyo kweli, ni uongo mtupu na makosa. Na hii siyo maana inayokuwa katika aya hii.  

Aya hii haielekee Mateso ya KRISTO.

 

13/ Hapana Mateso ya KRISTO msalabani, bali maumivu  na manyonge ama  mateso  ya Kristo katika mwili wa Paulo. 

Mateso ya Kristo msalabani haiitwe maumivu na manyonge. 

Kama mtu anasambishwa kwenye Korti na anahukumiwa, hii siyo maumivu na manyonge lakini hii ni hukumu. 

Bwana Yesu Kristo alibeba Hukumu juu ya Musalaba. 

Basi, Mwokozi wetu Yesu Kristo aliamuru maumivu na manyonge ishike watu wake ili iwasaidia kukusanya kanisa, Mwili wa Kristo. 

Na Mutume Paulo alisema kwamba: 

Nitatimiza mapenzi ya Mungu kwangu, nipate maumivu, manyonge, na mateso katika mwili wangu kwa ajili ya Yesu Kristo ili kanisa likusanywe.

 

14/ Eti watambua? 

Kanisa la Kristo haikusanyiki kamwe bila mateso. 

Waweza kuchunguza ndani ya Biblia. 

Kweli Mutume Paulo hakustarehe katika mwili wake, yeye aliishi katika machungu na maumivu ya kila siku na kila saa. 

Wakati tunachunguza historia ya kanisa tutaona namna kanisa ilikusanywa kwa maumivu na mateso ya  watumishi wake Mungu. 

Wakati Mwenyezi Mungu anapotumikisha mtu, kunakuwa mpito wa machungu. 

Mutume Paulo anasema kwa namna halisi kwamba yeye anafurahi kuteseka kwa ajili ya Yesu Kristo. Oh, kweli aliteseka sana. 

2 Wakorinto 11: 23 - 25  

“Wao ni watumishi wa Kristo? (Ninasema sawasawa mwenye wazimu) mimi zaidi; katika taabu kuzidi sana, katika mapigo kuzidi sana, katika vifungo kuzidi sana, katika mauti mara nyingi.Kwa wayuda nilipata mapigo makumi ine ila moja. Mara tatu nilipigwa kwa fimbo, mara moja nilipigwa kwa mawe, mara tatu nilipata kuvunjika kwa merekebu, mchana na usiku nimekaa katika bahari:” 


15/ Wewe tayari umeisha soma Vitabu vya hadisi ya Shahidi? 

Wesley na Whitefield, Morrison na Carey na wahubiri wakuu waliopima kuonesha kwa wazi hadisi na vitumba vya miili ya Shaidi Wangreza? 

Mbele ya nyakati za Uinjilisti, mbele wamisionari waende India, Afrika na Chaina, kulikuweko  nyakati za mauaji na wengi walipoteza maisha yao.

 

16/ Wakolosayi 1: 25  

“Nami nimefanywa mtumishi wake, sawasawa na uwakili wa Mungu niliyopewa kwa faida yenu, nitimize Neno la Mungu.” 

Hapa tunaona aya moja ya muhimu na manufaa kabisa, ila watu wengi wanapendelea kuiruka ama kuisoma bila faida, ama kuisahau. 

Mutume Paulo alitiwa Mtumishi sawasawa na uwakili wa Mungu. 

Mungu alimupa ruhusa ya kutimiza Neno la Mungu. 

Mutume Paulo alitimiza Neno la Mungu, siyo Kitabu cha Ufunuo wa siri.

 

17/ Maneno ambayo Mutume Paulo anatuambia katika Biblia Takatifu, ni Ufunuo Mkubwa katika Biblia tangu Kitabu cha Mwanzo hadi Kitabu cha Ufunuo wa siri. 

Katika Kitabu cha Ufunuo wa Siri, hakuna jambo mupya kwa upekee. 

Kitabu cha Ufunuo wa Siri kinajaa na misemwa yenye inapatikana katika sehemu za Vitabu vingine katika Biblia. 

Ukweli wote tunaopata katika Kitabu cha Ufunuo wa Siri, ukweli huo tumeupata katika Vitabu vingine vya Biblia.

Bali, Kitabu cha Ufunuo wa siri umeyakusanyisha yote katika Kitabu kubwa ya mambo ya mwisho. 

Ni Mutume Paulo ndiye aliyepokea UFUNUO ya kwamba KRISTO alikua anaunganisha watu wote katika Kanisa unaoitwa KANISA MWILI WA KRISTO.  

Waefeso 1: 7 inatuambia kwamba: 

“Katika yeye tuna ukombozi wetu kwa njia ya Damu yake, usamehe wa zambi zetu, sawasawa na wingi wa neema yake,” 

Mutume Paulo anatumikisha neno “utajiri”, “wingi” neno hili linatumikishwa na Paulo pekee. 

Utajiri wa neema yake, wingi wa neema yake. 

Tena katika Kitabu cha Waefeso 2: 7, tunasoma ya kwamba: 

“hata katika nyakati za kuja aonyeshe wingi wa kupita kiasi wa neema yake kwa wema wake kwetu katika Kristo Yesu.” 

Wingi wa utajiri ya neema yake. Wingi wa kupita kiasi wa neema yake. 

Wewe unafikiri juu ya wingi wa kupita kiasi wa neema yake? 

Wingi wa utajiri wa neema yake unapita kiasi. 


AMINA 


N°Ref: 06/26/1977/ 395-2 DOES YOUR SALVATION DEPEND ON YOU? / 09/20/2020 

Thursday, September 10, 2020

TOKA MBINGUNI NA MAPENDO / FROM HEAVEN WITH LOVE

Photo taken by B Smith from the Kitchen Door



 

TOKA MBINGUNI NA MAPENDO 

 FROM HEAVEN WITH LOVE

 December 23, 1979

 Pastor Henry F. Kulp 


Asubui ya leo tunataka kuchunguza kwa makini sana aya moja ya muhimu na ya manufaa kweli, ni aya ya kumi na ine ya Yoane 1.  Kwa njia ya aya hii tutafahamu makusudi, shabaa na umuhimu wa sherehe ya Noeli. 

Katika aya hii, mambo yote yanaoneshwa wazi wazi.  

Watu wengi wanasherekea siku kuu ya Noeli bila kufahamu maana ya siku kuu hiyo na kwa nini kuisherekea. 

Yoane 1: 11 - 14  

“Alikuja kwake, nao walio wake hawakumpokea; 

Lakini wote ambao walimpokea aliwapa uwezo wa kuwa watoto wa Mungu, ndio wale walioamini Jina lake. 

Waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili; wala si kwa mapenzi ya mtu, lakini kwa Mungu. 

Na Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu, tukatazama utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee akitoka kwa Baba, amejaa neema na kweli.” 


1/ Katika Aya hii ya 14, tunapata Tamko tatu.

Ujumbe tatu tofauti kuhusu Bwana Yesu KRISTO katika hali yake ya mtu kweli, hapa chini duniani.

Ya kwanza ni: 

UKWELI WA JAMBO LA KUVAA MWILI: 

Na Neno alifanyika mwili.    

Ya pili: 

KUSUDI LA KUVAA MWILI: 

Akakaa kwetu, tukatazama utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee akitoka kwa Baba,  

Ya tatu: 

TABIA YA UMTU WAKE: 

Amejaa neema na kweli. 

Tutajifunza kwa makini sana hizo Tamko tatu ili tuvumbue ufunuo unaokuwa ndani. 


2/ Sisi tumebarikiwa na kweli, tunabahati nzuri kufahamu maneno haya ya muhimu na ya musingi inayo tufundisha kusudi ya Bwana wetu Yesu Kristo kuchukuwa mwili na nyama ya kibinadamu.

Wakati watu bado wangali mbali hawaja onja Yesu, wengi wao hawapendi kusikia hata neno moja kuhusu KRISTO, lakini baadaye wao wanageuka wenye kupendelea kushirikiana naye.  

Jambo hili halifurahishi Bwana Yesu, tena jambo hili ni mbovu sana kwa watu wale. 

Mhadhiri mmoja mupagani alipo maliza kutoa hutuba yake mbele ya umati wa watu, akafanya mwito akisema: yeyote ule anayekuwa na ulizo apite mbele kwa jukwaa na aulize ulizo lake. Watu wakabaki kimya kwa muda fulani. 

Kiisha punde kidogo, mtu mmoja anayejulikana mlevi wa hali ya juu kwa watu wote wa eneo lile, lakini aliyeokoka baadaye, akashimama na kujielekeza mbele, kiisha akapanda kwenye majukwaa, akatwaa machungwa iliokuwa katika mufoko wake wa suruali akaanza kuumenya. Hasira ikamshika huyo Mhadhiri,   akamuhamakia akisema: ndugu leta ulizo lako kwa haraka. 

Huyu mtu mlevi hakumujibu neno, wala kujali naye, akaendelea kumenya machungwa yake.

Alipo maliza kuondoa maganda, akala machungwa yake, alipomaliza yote nzima akageuka sasa upande wa huyu Mhadhiri mupagani akamwuliza eti: “machungwa hii ilikuwa sukari sana?”  

Huyu Mhadhiri akakasirika akamwambia, “wewe mupumbafu, ulizo gani lile la ujinga mno, namna gani ninaweza kutambuwa kama machungwa yako ilikuwa sukari ama chungu na mimi sikuonja hata kidogo?” 

Kwa hayo matusi, huyu mlevi naye akajibu huyo mtu aliyekuwa anatoa hutuba akimwambia: 

Ewe Mhadhiri, “namna gani wewe waweza kufahamu neno lolote juu ya KRISTO na wewe bado kumuonja?” 


3/ Tuchunguze sasa Tamko la kwanza:

NA NENO ALIFANYIKA MWILI. 

Hakuna msemwa ulioandikwa kwa namna ya mushangazo na maajabu kama hii msemwa inayokuwa kwa mwanzo ya Aya hii ya kumi na ine, sawa vile tunaweza pia kusoma kwa aya ya kwanza na aya ya kumi na ine

Tunaweza kuisoma kama ifwatavyo: 

Katika mwanzo alikuwa Neno, na tunaruka hapo chini, na Neno alifanyika mwili.

Na hapo tuna mabano inayojifungua kwa aya ya 2 na kujifunga kwa aya ya 13. 


4/ Neno ni katika Swahili kwa Kigriki ni LOGOS, na inamaanisha:  HOTUBA YENYE KUSEMWA NA KINYWA. 

Ni aina ya mazungumuzo kati ya watu wawili. 

Tunatambua ya kwamba, tunapozungumuza kuhusu    LOGOS, inamaanisha kwamba tunazungumuza kuhusu YESU KRISTO anayekuwa Hotuba ya Mungu ama mjadala kwa watu. 

Tunaweza kumbuka maandiko ya Ufunuo 22: 13, inayosema: 

“Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.” 

Alpha ni herufi ya kwanza katika alfabeti ya Kigriki na Omega ni herufi ya mwisho. 

Ni kusema YESU KRISTO ni HOTUBA ya MUNGU. 


5/ Na Mungu anajifunua MWENYEWE kwetu kwa njia ya YESU KRISTO. 


6/ KRISTO ni Hotuba ya mwisho ya Mwenyezi Mungu kwa Wanadamu.

Hakutakuwa tena ingine Hotuba toka kwa Mungu. Haitawezekana. 


7/ Tufafanue Yoane 1: 1  

Katika mwanzo alikuwa Neno. 

Tunaona hapa kwamba tendo “alikuwa” ni katika Mifano ya nyakati: Wakati Uliopita. Inamaanisha siku za nyuma za Wakati wa Mazoea. 

Hiyo inamaanisha nini? 

Katika Mifano ya Nyakati katika Swahili, tendo kamili lililo fanyika siku zilizopita kwa namna ya Mazoea katika Nyakati za nyuma, ndio nyakati inayo tumikishwa hapa, lakini linalo hitajika zaidi ni namna ya kuonesha nyakati za nyuma zinazoendelea katika lugha ya Kigriki.  

Na ni tendo la Kigriki lenye kuwa sawa china ya tendo “alikuwa” ndilo linaloleta mwangaza na maana kamili ya tendo lenye Mutume Yoane alitumikisha hapa. 

Na inamaanisha nyakati yenye ilikuwa mbele ya viumbe yote.

Nikusema, hiyo LOGOS, ama hiyo NENO ilikuweko mbele Mwenyezi Mungu hajaumba chochote kile. 

Na hii ingetafsiriwa hivi: 

Na katika mwanzo wakati hakujakuweko mwanzo yoyote.

Katika umilele uliopita, Neno lilikuweko. 

Hii inaonesha Umilele wa Yesu Kristo. 

Yesu Kristo anaishi Milele. 


8/ Tushuke sasa chini ili tucheue aya ya 14, tunasoma: 

Na Neno alifanyika mwili, 

Mwili ni kitu chenye umbo unaokuwa na mipaka yake, lakini hapa mastaajabu  ni kwamba kitu kisichokuwa na mipaka ama umbo, kinakuwa na umbo lenye mipaka na kona zake na ni hii inayoshinda ufahamu wetu.

Tunashindwa kufahamu namna gani tendo hili liliweza kufanyika. 

Bali tunaiamini na kuisadiki sababu ni Mwenyezi Mungu anayesema. 

Mara kwa mara ninajiuliza kama kwa kweli watu wanafahamu kwamba hapa chini duniani tunayo maswali mengi yasiyokuwa na majibu na horoza yake ni zaidi sana kupita maswali yenye ufahamu wetu unaweza kupata jibu ama kutafakari.  

 

9/ Tuchunguze pamoja tendo: “alifanyika” 

Mara tena tunapata matatizo kidogo na Mifano ya Nyakati.

Itakuwa vigumu kupana tafsiri kamili ya tendo hii katika Swahili. 

Kwa sababu tendo “alifanyika” liko katika sarufi ya usemi ya sentensi yenye kumaanisha kwamba kuna yule anayetenda tendo na pia kuna watazamaji ama tendo la kufanyika kuwa na, umalimbali na hayo, katika kigriki china la tendo lile ni katika nyakati ya katikati. 

Kama ingelikuwa katika nyakati na hali ya kufanyika kuwa na, ingemaanisha kwamba huyu anayefanyika kuwa na, hana nguvu yeyote ya kibinafsi kwa kukamilisha tendo lile.

Ni nguvu ya ufungaji. 

Lakani nyakati ama hali ya katikati, inamaanisha kwamba huyu Neno naye vilevile aliona mafaa ya kufanyika kwa tendo lile, kwa kutoka kwa hali ya Neno na kufanyika kuwa Mwili. 

Tendo hili lilifanyika kwa kutaka kwa Neno, kwa Nguvu na Uwezo wa Neno na kwa Nguvu ya Ufungaji wa Neno. 

Inamaanisha: KUGEUKA KUWA, ama KUANZA KUWA, yaani:  kugeuka mwili.  

Logos yenye haina Mwili, inavaa nyama.

YEYE mwenye hapo kale alikuwa haonekane na mecho, sasa anaweza kuonekana na mecho ya watu. 


10/ Tendo lenye kuwa kwa china ya tendo “alifanyika” halipashwi kukamatwa katika maana ya musingi tu yenye kumaanisha kama Neno alivaa mwili kama vile sisi tunavyokamata nguo na kuivaa. 

Hapa ni mfano wa kuundwa kwa. 

Siyo kuvaa nguo yenye hakuwa nayo mbele. 

Bali YEYE MWENYEWE alijiumba kwa hali lenye hakuwa mbele. 

Ni hiyo sababisha kuzaliwa kwake na Bikira. 

Tunafahamu ya kwamba YEYE MUUMBAJI wa Vyote Alijiumbia Mwili wa kufanana na huu wetu, lakini pasipo zambi. 

Sisi hatuwezi kuumba hata seli moja ndogo yenye uhai na uwezo wa kuishi bila musaada wa kulelewa. 


11/ Sababu gani Mutume Yoane alitumia neno “mwili” pahali pa neno lingine? 

Sababu gani hakutumia kwa mfano neno maumbile? 

Ni kwa sababu KRISTO alikuja kufa na kwa kufa Alipashwa kumwanga Damu yake kama vile uzima wa nyama unaokuwa ndani ya damu. 


Walawi 17: 11  

“Kwa kuwa uhai wa mwili  ni katika damu; na nimewapa ninyi damu hii juu ya mazabahu ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu; kwa maana ni damu inayofanya upatanisho kwa ajili ya nafsi.” 

KRISTO alikuja ili afe, lakini kumbuka kwa kupata mwili wa nyama, Alijiumbia YEYE MWENYEWE Mwili. Na Yeye aliendelea kuwa Mungu kweli na Mutu kweli. 


1 Yoane 5: 20  

“Nasi tunajua kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupa sisi akili ili tumjue yeye aliye wa kweli, nasi tuko ndani yake yeye aliye wa kweli, ndani ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyo ndiye Mungu wa Kweli, na Uzima wa milele.” 

Hapa Mutume Yoane anazungumuza kuhusu Mwana, yule LOGOS. 

Na alisema: 

Huyo ndiye MUNGU wa Kweli, na Uzima wa Milele


12/ Tuchunguze sasa Tamko la pili. 

Akakaa kwetu

Ili ndilo kusudi la kujiumbia mwili. 

Kitu cha mastaajabu sana na cha kigeni ni kwamba hata kufikia kiwango chake cha kujiumba mwili, viumbe alivyoviumba vinaendelea tu kumuchukia. 



Ingelikuwa heri tutambue ya kwamba: 

Yeye alikuja kuishi katikati ya maadui wake, na hii ndiyo inaonesha kweli UMUNGU wake, sababu hakuna mwanadamu mwenye anaweza kuwa hata na wazo ya kuishi katikati ya maadui wake.

Bali ni hiyo Bwana Yesu Kristo alilolifanya. 


13/ Tuchunguze neno “Kukaa”  

Ni neno la muhimu sana katika Kigriki. 

Tendo lile lina msingi wake toka neno la Kigriki: SKAY’ – NOS maana yake: Alijenga hema lake,na hii inaonesha kukaa kwa muda kitambo, siyo makao ya kudumu. 

Tutafute katika Biblia na tuangalie mahali pengine tunapoweza kupata neno lilelile. 

2 Wakorinto 5: 1 

“Kwa maana tunajuwa ya kama nyumba ya dunia ya hema yetu ikibomolewa, tuna jengo linalotoka kwa Mungu, nyumba isiyofanywa kwa mikono, iliyo ya milele katika mbingu.” 

Neno tunalo hapa ni hema ama kibanda. 

Makao ya muda, na kwa kweli mwili wetu ni kao la muda, na mwili huu hautosheki kwa muda wote wa maisha yetu. 


14/ Neno hili la Kigriki, hema ama kibanda, linatumikishwa sawa makao kwa watu wa kuhamahama, ama wa nomad, na kwa waaskari. 

Shabaa ya Bwana Yesu Kristo haikuwa kuja hapa chini duniani na kuishi kwa muda murefu sawasawa na mapenzi yake,ama kuja kubaki hapa na kudumu. 

Kama angelitaka, Angeliishi muda murefu zaidi ya hiyo kipande fupi cha miaka 33, lakini Yeye hakufanya hivyo. 

Yeye alikuwa hapa kwa muda mfupi tu kama vile inavyokuwa maana ya tendo kukaa katika Kigriki.

Hiyo ndiyo ilikuwa kusudi la KRISTO. 


15/ Wakati Bwana Yesu alifufuka toka kaburi, Alijiumbia na Kujivalisha Mwili ungine Mupya wa Ufufuko na Mwili huo ulikuwa wa Kipekee na Usioharibika ama Usioweza kufa. 

Ni muhimu sana kufahamu vile.  

Mwili aliyokamata Yeye peke wakati alipozaliwa na Bikira, ulikuwa mwili wa kufa, haukuwa mwili usioweza kufa. 

Angaliweza kufa katika huo mwili, na kwa kweli Alikufa. 

 Tusome maandiko inayo patikana katika aya hizi mbili za muhimu: 

2 Timoteo 1: 8, 10 

“Basi usione haya kwa ushuhuda wa Bwana wetu, wala kwa mimi mfungwa wake: lakini uvumilie taabu pamoja na Habari Njema kwa nguvu ya Mungu; 

Na sasa imefunuliwa na kuonekana kwa Mwokozi wetu Yesu Kristo, aliyebatili kufa, na kufunua uzima na maisha yasiyokoma kwa njia ya Habari Njema.”  


Hapa inasemwa kwamba: 

Yesu Kristo, aliyebatili kufa, na kufunua uzima na maisha yasiyokoma kwa njia ya Habari Njema

Ni Bwana Yesu Kristo Pekee anayekuwa na Mwili Usiyokufa. 

Hiyo Mwili iliyotoka toka kaburi haiwezi kamwe kufa tena.

Ni Mwili wa Utukufu, ni Mwili Usiyokufa. 


16/ Wakati Bwana Yesu alikuwa bado angali duniani, mwili wake ulikuwa bado hauja pata ule Utukufu. 

Wakati alipokuwa akitembea hapa chini duniani, kichwa chake hakikuwa kimezunguukwa na mbaramwezi ya muviringo kama vile wachapaji wengi wanao chapa katika taswira zao. 


17/ Yeye hatarudi tena katika mwili huo aliokuwanao wakati wa kujinyenyekeza na kuzizaraulisha, bali Yeye atarudi katika Mwili wake wa Ufufuko, Mwili wa Utukufu. 


18/ Msemwa “akakaa katika hema” ama “akakaa” iko katika Mifano ya Nyakati katika Kigriki, iitwao AORISTI. 

Ni Mifano za Nyakati katika Kigriki inayoonesha nyakati zilizo pita na kwamba, neno lile lilipita na kubaki tu kule na haliwezi kamwe kuonekana ama kufanyika tena.  

Inamaanisha kwamba: 

Hizo ni makao zenye hazitafanyika tena, hata kidogo katika lile umbo moja ama maumbile sawasawa ama kwa kusudi lile moja

Bwana Yesu hatarejea tena hapa duniani kama Mtu mnyenyekevu, ama mnyonge, ama mtumwa, ama mtu munyenyekevu sana na mwenye kiasi. 

Atarudi kama Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana. 

Ni Yeye Pekee JABARI mwenye NGUVU. 


19/ Tuchunguze sasa neno “Sisi”  

Ni nani ambaye Mutume Yoane anapenda kutaja wakati anapotumia kiwakilishi nomino “sisi” ama “tu-”? 

Mbele ya yote tunafahamu kwamba Mutume Yoane yeye pia anapatikati kati ya wale walioona KRISTO kuvaa mwili, wakimuona na mecho yao wenyewe. 

Mutume Yoana hakuwa yeye pekee kama mushuhuda aliye ona na mecho yake binafsi Mungu kuvaa mwili wa nyama hapa chini duniani. 

Tukumbuke ushuhuda wa vinywa vya watu wawili ama watatu ili neno lishimamishwe kuwa kweli. 

2 Wakorinto 13: 1  

“Mara hii ni mara ya tatu ninakuja kwenu, katika vinywa vya washuhuda wawili au watatu kila neno litasimamishwa.” 

Neno hili ni hakika sababu kulikuwa washuhuda wengi walioona Bwana Yesu Kristo kuvaa Mwili wa nyama.  

Tambua kwamba Mutume Yoane hakusema: Nikatazama, lakini alisema: tukatazama. 


20/ Tuchunguze sasa tendo “tukatazama”, ni mushangao kweli. 

Inamaanisha: 

KUONA KWA KIMTU KWA MECHO YA KIBINADAMU KUONA KITU KINACHOWEZA KUPAPASWA NA MUTU ANAYETIZAMA

(MTAZAMAJI). 

Nazani Mwenyezi Mungu alitumia neno lile ili kuonesha wazi aina ya Mwili wa nyama aliyo vaa Yesu Kristo. 

Katika kanisa la mwanzo, kulikuwa mafundisho ya uongo, Uzushi uliozaliwa na kuinuka nao ulikua unaitwa DOCETISMU, na ulikuwa unafundisha kwamba KRISTO hakuwa na mwili wa maumbile ya kibinadamu na kwamba Yeye hakuwa na hali ya kimutu. 

Wakiendelea kusema kwamba hata jinsi alikuwa akila ama akinywa maji ama alizaliwa, na kufa yote yale yalikuwa tu udanganyifu ama njozi. 

Neno lile tulisoma inaonesha kama njozi lile halikuwa kweli. 

Ni uwongo. 

Mwili wa nyama wa Bwana wetu Yesu Kristo wakati wa maisha yake hapa chini duniani ilikuwa mwili wa maumbile na aina ya kimutu, iliyoweza kuonekana na mecho ya wanadamu. 


21/ Neno “kutazama” inamaanisha: 

KUANGALIA KITU, KUTAZAMA KITU, MARA TUKIWA WENYE KUSHANGAA NA KUZUBAA. 

Kila mtu anaweza kushangaa wakati anaangalia YESU KRISTO. 


22/ Na tukatazama utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee akitoka kwa Baba.

Tunataka kuvumbua maneno mamoja mamoja ya Maombi ya Kuhani Mukuu wakati alikuwa akitazamia Musalaba. Anasema katika kitabu cha 

Yoane 17: 5 

Na sasa unitukuze, Baba, pamoja nawe mwenyewe, kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe mbele ya kuwa dunia.” 

Kitu gani kilishotukia wakati Bwana Yesu Kristo alipovaa mwili na kuwa mtu? 

Aliweka kando Utukufu wake; lakini kitu moja kinatushitusha katika hii aya: 

Yoane 1: 14  

“Na Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu, tukatazama utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee akitoka kwa Baba, amejaa neema na kweli.” 

Mutume Yoane anatuonesha hapa kwamba Bwana wetu Yesu Kristo ingawa vile, alikuwa na namna ya utukufu. 

Yeye alikuwa umbalimbali na watu wengine, mwenendo wake ulikuwa tofauti na ya watu wengine. Alikuwa na utukufu hapa duniani lakini utukufu ule haukukuwa sawa na Utukufu wake wa Mbinguni.  


23/ Tunafikia sasa Tamko la tatu: 

Neema na Kweli.  

Hii njo hali ya utu wake. 

Mbele ya yote Yeye ni Neema, na Yeye ni Kweli. 

Hii inaonekana katika maisha yake ya kimutu hapa duniani. 

Tabia hizo mbili zilikuwa zikitambulikana kweli katika maisha yake hapa duniani. 

Tuchunguze sasa neno “amejaa”. 

Kama nyama ya mwili, Alikuwa akijaa neema na kweli. 


24/ Katika Agano Jipya hatuwezi kupata ukurasa ungine kwenye neema na kweli zinaunganishwa na kusemwa pamoja kama vile tunavyoona hapa, ama katika hali na utaratibu kama tunavyo hapa. 

Tufahamu kwamba aya ya 17, inasema: 

Kwa kuwa torati ilitolewa kwa mkono wa Musa, neema na kweli zilikuja kwa mkono wa Yesu Kristo.” 


25/ Neema inatambulikana kwa kuja kwa Bwana Yesu hapa chini duniani.

Alikuja kujitoa kama Ulipaji(kununua wafungwa), Malimbuko juu ya zambi zetu. 

Tutazame tena katika hii Injili ya Yoane: 

Yoane 3: 17 

“Maana Mungu hakutuma Mwana wake ulimwenguni kuhukumu ulimwengu, lakini ulimwengu uokolewe naye.” 

Yeye alikuja duniani, hapa chini dunia, si kwa kuhukumu ulimwengu, lakini kusudi ulimwengu uokolewe NAYE. 

Ni sawa tunavyo sema mara kwa mara, Neema: Ni kupokea kitu usicho stahili. 

Yote bila malipo. 

Maisha ya hapa chini duniani ya Bwana wetu Yesu Kristo, inatuonesha Neema ya Mungu. 

Mara kwa mara mwenendo na tabia ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo mbele ya wana wa kuasi, watu wenye zambi, inaonesha Neema ya Mungu. 


26/ Na zaidi ya hayo, Yeye tena ni Kweli

Bwana Yesu Kristo alikuja kutuonesha kwamba Mungu amejaa Neema na Kweli, na bila shaka, Yesu Kristo ni Kweli.  


27/ Waroma 5: 20 

“Lakini sheria iliingia, ili zambi ziwe kubwa sana, lakini pahali zambi zilipozidi, neema ilizidi zaidi sana.” 

Hapa tuna neno ya  kwamba: 

Pahali zambi zilipozidi, neema ilizidi zaidi sana. 

Neema ilizidi juu yetu kwa njia ya mtu Yesu Kristo, na kwa sababu Alikufa ili alipe malipo ya zambi zetu.  


AMEN  


N°Ref: 12/23/1979/ 523-1 FROM HEAVEN WITH LOVE / 09/10/2020