Thursday, June 30, 2022

HATARI NDANI YA KANISA / DANGER IN THE CHURCH



 


HATARI NDANI YA KANISA

239 - DANGER IN THE CHURCH 

January 21, 1962

Pastor Henry F. Kulp



 

1 Timoteo 1: 1 – 11

“Paulo, mtume wa Kristo Yesu, kwa agizo la Mungu Mwokozi wetu na la Kristo Yesu taraja letu; kwa Timoteo, mwana wangu wa kweli, katika imani: Neema, na rehema, na salama, kutoka kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Bwana wetu.

Kama vile nilivyokusihi kukaa katika Efeso, wakati nilipokwenda Makedonia, uwakataze wengine wasifundishe mafundisho ya namna nyingine, wala wasiangalie hadizi na maneno ya vizazi pasipo mwisho, yanayoleta mabishano wala si kama kanuni ya Mungu iliyo katika imani; basi sasa ufanye vile.

Lakini kutimia kwa agizo ni mapendo kutoka kwa moyo safi na zamiri njema, na imani pasipo udanganyifu.

Wengine wakikosa kwa maneno haya wamegeuka kwa maneno bure ya kusemasema; Wakitaka kuwa walimu wa sheria, wasiofahamu ambayo wanayasema, wala maneno yale ambayo wanayasimamia na nguvu.

Lakini tunajua sheria ni njema, kama mtu akiitumia kwa njia ya sheria,

Na tukifahamu neno hili, ya kama sheria haifanywi kwa mtu wa haki, lakini kwa mwenye kuvunja sheria na waasi, na kwa wasioogopa Mungu na kwa wenye zambi, na wachafu na wasiomcha Mungu, na kwa wenye kupiga baba zao na kupiga mama zao, na wauaji, na washerati, na wafiraji, na wenye kuiba watu, na wawongo, na wenye kuapa uwongo, na kama neno lingine lisilopatana na mafundisho yenye uzima;

Kama vile ilivyosemwa katika Habari Njema ya utukufu wa Mungu Mbarikiwa, niliyowekewa akiba.”

Mtume Paulo alimuweka na kumusihi Timoteo abaki kwa Efeso na awakataze wengine wasifundishe mafundisho ya namna nyingine, wala wasiangalie hadizi na maneno ya vizazi pasipo mwisho.

1/ Wakati tunaposoma katika kitabu cha Ufunuo, tunatambua ya kwamba: Ufunuo 2: 1 – 7 inasema:
“Kwa malaika ya kanisa la Efeso, andika;
Maneno haya anayasema yeye anayeshika hizi nyota saba katika mkono wake wa kuume, naye anatembea katikati ya vile vinara saba ya zahabu,

“Kwa malaika ya kanisa la Efeso, andika;

Maneno haya anayasema yeye anayeshika hizi nyota saba katika mkono wake wa kuume, naye anatembea katikati ya vile vinara saba ya zahabu,

Ninajua matendo yako, na taabu yako, na uvumilivu wako, na ya kuwa huwezi kuchukuliana na watu wabaya; tena umejaribu wale wanaojiita mitume, nao hawako, ukawatambua kuwa wawongo;

Tena ulisubiri, na ulikuwa na uvumilivu, na kwa ajili ya jina langu ulijitaabisha, wala hukuchoka.

Lakini nina neno juu yako, kwani umeacha mapendo yako ya kwanza.

Kumbuka toka wapi ulipoanguka, ukatubu, ukafanye matendo ya kwanza.

Lakini kama usipofanya hivi, nitakuja kwako upesi, nitaondoa kinara chako katika pahali pake, usipotubu.

Lakini una neno hili, ya kuwa unachukia matendo ya Wanikolayi, ambayo mimi ninayachukia.

Yeye aliye na sikio, asikie neno ambalo Roho anayaambia makanisa; Yeye anayeshinda nitampa kula matunda ya mti wa uzima ulio katika shamba la Mungu.”

Timoteo aliweza kuongaza kanisa lake vema.

Makanisa hayo saba yalikuwa kweli katika nyakati zilizo pita.

Siyo tu utafsiri wa usomi, lakini yanatupatia mwangaza kuhusu jambo mbalimbali zenye zilitukia katika makanisa hayo.

Mambo yale yanaweza yakatukiye tena katika makanisa kwa siku zitakazokuja. Bali, kwa aya ya 4, Mwenyezi Mungu anasema:

“Lakini nina neno juu yako, kwani umeacha mapendo yako ya kwanza,”

Mufahamu ya kwamba jambo hili latukia kwa muda mfupi lenye halifikii hata miaka mia moja.

Hataivyo anasema kwa aya ya pili:

“...tena umejaribu wale wanaojiita mitume, nao hawako, ukawatambua kuwa wawongo;”

Umewatambua kama ni mitume wa uwongo. Hata kama ni hivyo, kulikuwa tu kungali kitu kimoja kinachokukosea.

Kanisa iliacha upendo wake wa kwanza.

Imetupasa kufanya angalisho tusizani kwamba mapendo haya ni mapendo katikati ya ndugu.

Hii ni kuhusu Mapendo yetu kwa Yesu Kristo.

Mpaka kwa kiwango hiki, matendo yao yalikuwa mazuri kwa mastaajabu, lakini Mungu wetu ni Mungu mwenye wivu, na Yesu Kristo ni Mungu mwenye wivu.

Mwenyezi Mungu anataka mapendo yetu yawe kwake kwanza, awe kwa nafasi ya kwanza, awe Muheshimiwa Mkuu.

Anapenda kuwa kwa nafasi ya kwanza miyoyoni mwetu.

Eti mwajua nini iliyotukia kwa kanisa lile la Efeso?

Miyoyoni mwao walikuwa wakiteswa humo ndani sababu walijitenga mbali na Kristo. Vitu vingine vilichukua nafasi ya kwanza, mahali Kristo pekee angepashwa miliki.

2/ Tufahamu kwamba jina “Efeso” maana yake “anayependwa”.
Ni jina lenye mtu mugriki alitumia kwa kutambulisha chaguo lake la kwanza. Mushangazo ni kwamba, yeye anayependwa anaachilia mapendo yake ya kwanza.
Ni kweli kwamba wao watabaki daima wenye kuokolewa, hawatapotea, walikuwa wangali na neno, walikuwa tu wakimtumikia Mwenyezi Mungu, bali, hawakuwa tena na

Ni jina lenye mtu mugriki alitumia kwa kutambulisha chaguo lake la kwanza. Mushangazo ni kwamba, yeye anayependwa anaachilia mapendo yake ya kwanza.

Ni kweli kwamba wao watabaki daima wenye kuokolewa, hawatapotea, walikuwa wangali na neno, walikuwa tu wakimtumikia Mwenyezi Mungu, bali, hawakuwa tena na

furaha lenye waliokuwa nalo kwa siku za zamani wakati walipokua wakimtumikia Bwana.

Huduma yao iligeuka kuwa mzigo mzito, kwa kweli kuna matendo yenye walikuwa wakitimiza, lakini mambo mengi ya huduma iligeuka kuwa machungu na mazito kwao, ijapokuwa kwa mwanzo walikuwa wakiyatenda kwa urahisi sana. Walipoteza mapendo yao ya kwanza kwa Yesu Kristo.

3/ Kila mara ninapokumbuka jambo la Efeso kupoteza upendo wake wa kwanza, mafikiri yangu yanakumbuka Yakobo.
Kumbukeni kwamba kwa sababu alikuwa akimpenda Rakeli, ilimupasa kutumika tena muda wa miaka saba ili amuowe.

Kumbukeni kwamba kwa sababu alikuwa akimpenda Rakeli, ilimupasa kutumika tena muda wa miaka saba ili amuowe.

Tukumbuke kwamba kitabu cha Mwanzo 29: 20, kinatuambia ya kwamba: Mwanzo 29: 20

“Yakobo akatumika miaka saba kwa Rakeli; na ilikuwa kwake kama siku chache kwa mapendo ambayo alimpenda nayo.”

Miaka hiyo saba ikawa kama siku chache kwa sababu ya mapendo ambayo alimpenda Rakeli.

Tunaweza tukatumike kweli, bali huduma hiyo yaweza kuwa kama mzigo kwetu kama hairaishishwe na kumbembelezwa na mapendo.

Tunaweza tukashikamane kweli na huduma yetu kwa Bwana, hata kuibana na kuishika kwa mikono miwili, tukiwa kati shida na matatizo kweli bali tukikumbuka kwamba siku moja mambo yetu itarekibishwa, na huduma itakamilishwa, na kweli ni hivyo.

Bali Mwenyezi Mungu hatamani sisi kumutumikia hivyo.

Mwenyezi Mungu anatarajia kwetu huduma iliyo nguvu kweli, na bila shaka, upendo wetu kwake unarahisisha mambo yote.

Mfano wa Timoteo aliyezungukwa na mbwa mwitu wenye kunguruma, tukifahamu kwamba pale Efeso kulikuwa mabishano kuhusu kawaida ya mafundisho, lakini Mtume Paulo aliendelea kumusadikia Timoteo.

Yeye alimuacha Timoteo hapo, na kwa kweli, Timoteo alikuwa akitumikishwa na Mwenyezi Mungu katika kanisa hilo ama katika makanisha yale.

4/ Tukumbuke mapashwa na wajibu wa Timoteo katika miji yale.
Yeye alipashwa kuwaonesha maelekezo, siyo mambo yote, lakini maelekezo ya musingi, sawa: Wasifundishe mafundisho mengine mbalimbali na mafundisho waliopata toka Mtume Paulo, wasijitoe kwa kufundisha hadizi, ambazo kwa mwisho zaleta hadizi bila mwisho.
Neno moja tunayopashwa kushika vichwani mwetu ni kwamba, kwa nyakati ile ilikuwa rahisi kwa matatizo yale yafike kwa sababu, kwa nyakati zile hakukuwa Biblia nzima kama tunayo kwa siku za leo, sawa maandiko ya Agano Jipya.

Yeye alipashwa kuwaonesha maelekezo, siyo mambo yote, lakini maelekezo ya musingi, sawa: Wasifundishe mafundisho mengine mbalimbali na mafundisho waliopata toka Mtume Paulo, wasijitoe kwa kufundisha hadizi, ambazo kwa mwisho zaleta hadizi bila mwisho.

Neno moja tunayopashwa kushika vichwani mwetu ni kwamba, kwa nyakati ile ilikuwa rahisi kwa matatizo yale yafike kwa sababu, kwa nyakati zile hakukuwa Biblia nzima kama tunayo kwa siku za leo, sawa maandiko ya Agano Jipya.

Ilikuwa rahisi kwa watu wa uzushi kupata wale wenye watakao amini mafundisho yao wakitunga hadizi kuhusu Bwana Yesu Kristo. Hadizi zenyi walizotunga kwa mafikiri yao kuhusu ujana wa Bwana Yesu Kristo, na nyingi za hadizi zao zingali hata kwa siku za leo.

Neno hadizi za uzao, ilimaanisha hadizi za aina ya mashetani.

Hadizi izo zilimaanisha hadizi za kizushi, na kweli yote yalikuwa matokeo ya mawazo. Mtu wa inje alitamani kupenya na nia ya kuwapata wale watakao musikiliza anapotunga hadizi za uzushi kuhusu Bwana Yesu Kristo.

Tuone namna mtume Paulo anaita hadizi za namna sawa:

1 Timoteo 4: 7

“Lakini ukatae hadizi za bure na za wanawake wazee. Nawe ujizobeleze katika utawa:”

Yanaitwa hadizi za bure na za wanawake wazee.

Walimu wale wa uwongo, ama manabii wale wa uwongo ni wenye zoezi ya kuunda hadizi za bure wanazozitunga wenyewe na mwisho wanazitupa juu ya watu kwa kuwapoteza.

Na matokeo ya hayo yalikuwa namna gani?

Yalileta maulizo mengi yenye hayawezi kuwa na jibu lolote.

Maulizo yenye yanayotoka ndani ya Neno la Mungu, ni maulizo mazuri, sababu tunakuwa na uwezo wa kuchunguza na kuchipua Maandiko Matakatifu na tutapata jibu kamili.

Bali, wakati tunapotembea inje ya Neno la Mungu, hatuwezi kupata jibu kwa maulizo yetu.

Bali kwa ulizo lote kuhusu neno lolote tukimbilie kuchunguza na kuchipua Neno la Mungu, ili tupate jibu.

Kwa kweli, ni wazi kwamba maulizo yanayotoka katika yale hadizi walizo ziunda, ni maulizo yenye hayawezi kamwe kuwa na jibu, sababu yako inje ya Neno la Mungu.

5/ Kwa kweli, Tito vilevile alikumbwa na misharabaka ya namna ile tusome

Tito 1: 10, 11

“Kwa sababu kuna wengi wasiotii, wenye maneno ya bure na wadanganyifu, zaidi wale wa tohara,

Imepasa kuziba vinywa vyao; wao wanaopindua nyumba nzima, wakifundisha maneno ambayo hayawapasi kwa ajili ya feza chafu.”

Hapa twawapata wale wasiotii, wenye maneno ya bure na wadanganyifu, zaidi wale wa tohara.

Wale waliojiingiza na maneno yasiyo na maana, maneno ya bure, wenye mafundisho isiyo na maana na inayopingana na mafundisho iliyopewa na mtume Paulo.

6/ Kwa aya ya tano, mtume Paulo anakumbusha Timoteo, ya kwamba kiini ya majukumu hayo ni mapendo.
Maelekezo zidi ya wajibu wote yapashwa kuleta mapendo.
Najuwa neno hili lina manufaa mengi kati ya wandugu.

Maelekezo zidi ya wajibu wote yapashwa kuleta mapendo.

Najuwa neno hili lina manufaa mengi kati ya wandugu.

Bali, hadizi zisizo na mwisho na za bure, kama vile aya ya sita inavyo tuambia, yanaleta mabishano, na magonyi, sivyo?

Kila mmoja wenu anapaswa kufahamu kanuni hili.

Mafundisho hayapaswi kuwa na matokeo ya magonvi, mabishano, bali matokeo yake yanapashwa kuwa mapendo.

Kumbukeni wakati tuliwafundisha kuhusu wale wanaoshika sheria, wale waliotajwa ndani ya majifunzo yetu kwa kitabu cha Wagalatia, watu wale wanaokuwa na kazi moja tu ya kuhukumu wenzao.

Hawafurahie mafundisho yao, kwa sababu hayaleti mapendo kwa wengine, bali matokeo yake ni mabishano ya bure, yakitokana kwa wale wenyi lengo tu la kutizama songe la pua la mwengine.

7/ Kanuni ya mafundisho, na mafundisho ya kweli, matokeo yake ni mapendo, hapana magonvi, hapana chuki.
Kama mafundisho yangu ni ya kweli, basi hayawezi kunisukuma kukataa wale wasionisadiki, bali yanapaswa kunisukuma kuwapenda wengine kama walivyo, kuwasaidia na kuwa mtu mzuri kwa macho yao, na kutokuendelea kuchunguza makosa ndani yao daima.

Kama mafundisho yangu ni ya kweli, basi hayawezi kunisukuma kukataa wale wasionisadiki, bali yanapaswa kunisukuma kuwapenda wengine kama walivyo, kuwasaidia na kuwa mtu mzuri kwa macho yao, na kutokuendelea kuchunguza makosa ndani yao daima.

8/ 1 Timoteo 1: 7

“Wakitaka kuwa walimu wa sheria, wasiofahamu ambayo wanayasema, wala maneno yale ambayo wanayasimamia na nguvu.”

Inasemwa hapa kwamba wanatamani kuwa walimu wa sheria.

Kwa kuzania kwangu, si sadiki kama kuna mwalimu mzuri wa sheria, hata mumoja. Sijuwe hata mmoja mwenye kiisha kufundisha sheria hakujikoroga mwenyewe.

Na vilevile wafuasi wake hawakuanguka katika uvuguvugu.

Mwenyezi Mungu hakuinua walimu wa sheria.

Sitambue kwa nini watu hawapendi kujitenga na sheria ijapokuwa Mwenyezi Mungu anatuomba kujitenga na sheria.

Najuwa kweli kuna wengi kati yenu ninyi munaonisikiliza sasa, munaosema na nguvu zote ndani yenu, kwamba ninyi munahitaji sheria, kwamba yawapasa kuwa na sheria. Mukisema ya kwamba munafahamu ya kwamba ni imani pekee inayookowa lakini munahitaji kuwa na sheria.

9/ Ninyi mumeokolewa kweli?
Kwa hivyo mumehesabiwa haki ndani ya Kristo.

Kwa hivyo mumehesabiwa haki ndani ya Kristo.

Sheria si juu yenu tena.

Sheria haikufanywa juu ya mtu mwenye haki, bali juu ya wale wenye kuvunja sheria, wakaidi, wasio tii.

Mufahamu kwamba ni nyinyi pekee, kwa kutaka kwenu mumeshikamana na sheria na kujiweka kama wavunja sheria na wakaidi.

Sheria haiko juu ya mtu wa haki.

Mwenyezi Mungu alitufanya kuwa haki ndani ya Kristo, kwa hivi sheria iliwekwa pembeni hatuna lolote lile twaweza kufanya na sheria.

10/ Tutambue vema maneno yanayotajwa hapa:
Kama wewe wajitambua kuwa mumoja wao basi shikamana na sheria, na ni vema ukumbuke ya kwamba sheria ililetwa ili ifunuwe uwovu wa zambi.
Eti, munaweza kunionesha maandiko yenye inasema kwamba sheria ni mwalimu? Hakuna.
Sheria ni kiongozi, mwalimu mkuu, ndio, kwa kumleta Izraeli kwa Kristo, bali kwetu sisi ni Neema ya Mungu inayotufundisha.

Kama wewe wajitambua kuwa mumoja wao basi shikamana na sheria, na ni vema ukumbuke ya kwamba sheria ililetwa ili ifunuwe uwovu wa zambi.

Eti, munaweza kunionesha maandiko yenye inasema kwamba sheria ni mwalimu? Hakuna.

Sheria ni kiongozi, mwalimu mkuu, ndio, kwa kumleta Izraeli kwa Kristo, bali kwetu sisi ni Neema ya Mungu inayotufundisha.

Tito 2: 11 – 12

“Kwa sababu neema ya Mungu inayoleta wokovu kwa watu wote, imeonekana, Ikitufundisha sisi kukataa ubaya na tamaa za dunia, na kuishi na kiasi kwa haki, na utawa, katika ulimwengu wa sasa,”

12/ Jibu kwa kushika sheria ni Habari Njema ya utukufu wa Mbarikiwa Mungu iliyowekewa akiba kwangu katika imani yangu.
Aya ya kumi na moja yatuonesha wazi kwamba ni:
Habari Njema ya utukufu wa Mungu Mbarikiwa, niliyowekewa akiba.

Aya ya kumi na moja yatuonesha wazi kwamba ni:

Habari Njema ya utukufu wa Mungu Mbarikiwa, niliyowekewa akiba.

Neno Mbarikiwa yaweza kutafsiriwa na neno Mwenye heri na furaha,

Siku moja nilikuwa nikisoma kitabu kilichoandikwa na ndugu G. Campbell Morgan, “Makadirio ya Neno”, na niligundua maana hii na ilinipa shangwe na raha.

“Mungu mwenye heri na furaha tele alitupatia Habari hii Njema ya utukufu.”

13/ Waweza kuwa haufahamu kwa makini sana maana ya neno “Heri na Furaha”
Kuna watu wanaosema: Tunakutakia mwaka mpya wa heri.
Eti wewe ni mtu mwenye heri. Ama mtu yule ni mwenye heri?
Wakati dunia inatumia neno furaha na heri, vichwani mwao kuna wazo lingine, sababu neno “furaha na heri” inamsingi wake toka neno haphazard, nikusema kwamba ni mambo yanayotukia kwa ghafla, kubahatisha bila mpango, nikusema kwamba waweza kufurahi kwa sababu jambo moja nzuri ilitukia katika maisha yako.

Kuna watu wanaosema: Tunakutakia mwaka mpya wa heri.

Eti wewe ni mtu mwenye heri. Ama mtu yule ni mwenye heri?

Wakati dunia inatumia neno furaha na heri, vichwani mwao kuna wazo lingine, sababu neno “furaha na heri” inamsingi wake toka neno haphazard, nikusema kwamba ni mambo yanayotukia kwa ghafla, kubahatisha bila mpango, nikusema kwamba waweza kufurahi kwa sababu jambo moja nzuri ilitukia katika maisha yako.

Inamaanisha kwamba kama unatukiwa na vitu vizuri, wewe ni mwenye heri, na kama ni jambo la huzuni na mbaya, wewe si mwenye heri.

Bali Mtume Paulo hakumwandikia Timoteo akitumia maana yale.

14/ Biblia mara kwa mara inazungumuza kuhusu neno “Heri na Furaha” na mara inamaanisha “Mbarikiwa”, bali kwa kweli maana yake ni Heri na Furaha.
Tufauti ninayopenda kuonesha twaipata katika luga ya Kigriki.
Tujuwe kwamba kuna maneno mawili katika kigriki yenye kuwa na maana tofauti. Na maneno yale mawili tafsiri yao ni “Mbarikiwa” ama “Heri”

Tufauti ninayopenda kuonesha twaipata katika luga ya Kigriki.

Tujuwe kwamba kuna maneno mawili katika kigriki yenye kuwa na maana tofauti. Na maneno yale mawili tafsiri yao ni “Mbarikiwa” ama “Heri”

Ya kwanza ni MUCK – KAR – EE – OS neno hili lilitumiwa na waandishi wagriki kwa kuonesha furaha na heri inayotoka kwa miungu.

Neno lingine waliotumia ni U – DIE – MON, neno lenye waandishi wagriki walitumia kwa kumaanisha heri na furaha ya kibinaadamu.

Mutatambua wazi kwamba neno U – die - mon ni china la neno DIE – MON – E – OWN yenye inaleta jina DEMON katika Kingereza na kwa Swahili ni Shetani/Pepo. Jina Shetani ndilo linalomaanisha Udiemon.

Nikusema kwamba wagriki waliamini kwamba bahati nzuri na utajiri nzuri wa mali unatoka kwa mashetani.

Wakati unatambua mtu akisema mimi/yeye nina/ana bahati, ama ana bahati nzuri, kwa wakati ule wagriki walikuwa wakisadiki kwamba bahati nzuri ama utajiri nzuri wa mali unatoka kwa mashetani.

15/ Heri na raha inatoka kwa Mungu.

1 Timoteo 6: 15

“Kwa maana katika nyakati zake hii itaonyeshwa na yeye mwenyewe, mwenye kubarikiwa na uwezo wote peke yake, Mfalme wa wafalme, na Bwana wa wabwana;”

Hapa inasema: Yeye Mwenyewe mwenye kubarikiwa na uwezo wote peke yake. Heri wema na furaha ya kweli inatoka kwa Mwenyezi Mungu na ni Yeye anayeyakabizi kwa wale wanaomwamini.

16/ Taifa la Mungu linapashwa ishi ndani ya heri na furaha. Kumbukumbu la Torati 33: 29

“Wewe ni heri,Ee Israeli:

Nani aliye kama wewe, taifa lililookolewa na Bwana,

Ngabo ya kusaidia kwako,

Aliye upanga wa utukufu wako!

Na adui zako watajitiisha chini yako; Nawe utakanyaga pahali pao pa juu.”

Twasoma hapa: Wewe ni heri, Ee Israeli, haya ni masemi ya mwisho ya Musa, mbele ya kupanda kwenda kufa kwa mlima Nebo.

Taifa la Mungu ni la heri na linapashwa kuwa taifa la heri, likimufuata Mungu.

Heri na raha ya kweli si ya dunia hii.

Dunia haitambui kitu kuhusu heri na raha, bali Taifa la Mungu lapashwa kuwa Taifa la heri.

Hapa twaona kwamba Israeli ilikuwa taifa chaguliwa la Mungu na lilipashwa kuwa na heri.

17/ Ni kwa njia gani?
Ni nini chanjo chenyi kitafanya wana wa Israeli wawe taifa la heri?
Tupate mwangaza wa neno hili tunaposoma 

Ni nini chanjo chenyi kitafanya wana wa Israeli wawe taifa la heri?

Tupate mwangaza wa neno hili tunaposoma Waroma 4: 6

“Kama Daudi vile anavyoonyesha heri ya mtu yule ambaye Mungu anamhesabia haki pasipo matendo.”

Hapa mtume Paulo anatumia masemi ya mtu wa Agano la Kale, aliyeishi chini ya sheria, na hapa anaonyesha heri ya mtu ambaye Mungu anamhesabia haki pasipo matendo.

Mutatambua kwamba wana wa Israeli walikuwa na heri sababu heri hiyo waliipata toka ndani ya Mungu.

18/ Luka 11: 28

“Lakini yeye alisema: Afazali heri wale wenye kusikia Neno la Mungu na kulishika.” Hii ni kanuni linaloheshimiwa ndani ya Biblia nzima.

Heri wao wenye kusikia Neno la Mungu na kulishika.

Na neno heri linakuja mara nyingine, na tungelisoma :

Furaha na Raha kwao wenye kusikia Neno la Mungu na kulishika. Twatambua kwamba maana ya neno lile yasemwa wazi.

Tutwae kwa upesi, mfano mwengine:

Ufunuo 1: 3

“Heri anayesoma nao wanaosikia maneno ya unabii huu, na kushika maneno yaliyoandikwa ndani yake; kwa maana wakati ni karibu.”

Sisi ni wenye heri na furaha wakati tunachunguza neno la Mungu kwa makini sana.

Hatuta ponda wakati kwa kuchipua jambo hili, bali kwa kweli ni hivyo.

Mtu mwenye aliyesamehewa zambi, mtu mwenye alifanywa kuwa haki ni mwenye furaha kama akijitambua na kujua hali yake ya sasa.

Mtu mwenye kufanya angalisho na Neno la Mungu, ni mtu wa heri.

19/ Tito 2: 13

“tukitazamia tumaini la baraka, na kuonekana kwa utukufu wa Mungu mkubwa, Mwokozi wetu Yesu Kristo:”

Tunapata hapa: Tumaini la baraka.

Tumaini la heri na furaha wakati Bwana Yesu ataonekana pale kwa mawingu kwa kutuchukua.

Wakati tunapotazamia tumaini hili la Baraka, kwa njia hii mwenyezi Mungu anatujaza na furaha na raha kila siku. Kwa njia ya Neno lake anatuweka ndani ya furaha. Wakati unapokamata muda kuchunguza Neno la Mungu, unapogundua swali moja nzuri na palepale roho yako inajaa na furaha sana, na raha na amani rohoni na hasa wakati unapoinua mecho yako juu ukitazamia lile tumaini la Baraka, wakati Bwana Yesu atakapoonekana kwa kuja kutuchukua, utasikia raha na amani na furaha, haijali lile unalopitia kama mapito, hata iwe jaribu nzito na misharabaka na majaribu, bali mawazo yako yanafikia kutambua kwamba Bwana Yesu anaweza kutokea kwa saa hiyo hiyo na kukuchukua kwake mbinguni, akikuondoa toka dunia hii ya shida, kweli hii ni jambo la heri, na raha , na furaha.

Ni furaha na raha ya namna sawa ndiyo Mwenyezi Mungu anapenda tufurahi ndani yake, na heri na furaha hii inatoka kwake Mungu mwenyewe.

20/ Kwa aya ya 11,
Mtume Paulo anatamka neno moja lenye hakuna yule aliyeweza kulisema hadi hapo. “kama vile ilivyosemwa katika Habari Njema ya utukufu wa Mungu Mbarikiwa, niliyowekewa akiba.”
Habari Njema niliyowekewa akiba.
Bila mabishano yoyote, Habari Njema hii ya Neema ya Mungu, Siri hii kuu ya Mungu ilipewa kwa Mtume Paulo pekee, haikutolewa kwa mitume wengine.

Mtume Paulo anatamka neno moja lenye hakuna yule aliyeweza kulisema hadi hapo. “kama vile ilivyosemwa katika Habari Njema ya utukufu wa Mungu Mbarikiwa, niliyowekewa akiba.”

Habari Njema niliyowekewa akiba.

Bila mabishano yoyote, Habari Njema hii ya Neema ya Mungu, Siri hii kuu ya Mungu ilipewa kwa Mtume Paulo pekee, haikutolewa kwa mitume wengine.

21/ Nilitaka kuleta nuru kwa masemi ya watu wengine,
Wengi wanasikia tunataja mara kwa mara jina la Mtume Paulo kwa kiasi sana na hata wanafikia kuwaza kwamba sisi tumemuweka mtume Paulo juu sana kwa nafasi inayostahili Kristo.
Bali sivyo;
Hapo tu jana jana haijapita siku nyingi, kulikuwa chama kinachoitwa “Tumrudilie Kristo”, ama “Turudi kwa Kristo”, waliounda chama hii ni wale waliokuwa wanasema kwamba namna tunataja sana Mtume Paulo, jambo lile linatubeba mbali na Kristo. Kwa kweli, jambo hili ni udanganyifu mtupu.
Tunataja mara kwa mara mtume Paulo, sababu Mwenyezi Mungu alimuwekea akiba ya Habari Njema ya kweli iliyo tofauti na inayokuwa kwetu sisi Mataifa wa siku za leo.

Wengi wanasikia tunataja mara kwa mara jina la Mtume Paulo kwa kiasi sana na hata wanafikia kuwaza kwamba sisi tumemuweka mtume Paulo juu sana kwa nafasi inayostahili Kristo.

Bali sivyo;

Hapo tu jana jana haijapita siku nyingi, kulikuwa chama kinachoitwa “Tumrudilie Kristo”, ama “Turudi kwa Kristo”, waliounda chama hii ni wale waliokuwa wanasema kwamba namna tunataja sana Mtume Paulo, jambo lile linatubeba mbali na Kristo. Kwa kweli, jambo hili ni udanganyifu mtupu.

Tunataja mara kwa mara mtume Paulo, sababu Mwenyezi Mungu alimuwekea akiba ya Habari Njema ya kweli iliyo tofauti na inayokuwa kwetu sisi Mataifa wa siku za leo.

22/ Kuna uvuguvugu mwingi kwa wala wenye kusoma Biblia bila kutambua utunzaji wa Mungu, bila kutambua kwamba Biblia nzima siyo yote kwa kanisa.
Ninaamini bila shaka kwamba Biblia nzima ilitolewa kwa maongozi ya Mungu na kuandikwa kwa kanisa, lakini Biblia nzima siyo kwa kanisa.

Ninaamini bila shaka kwamba Biblia nzima ilitolewa kwa maongozi ya Mungu na kuandikwa kwa kanisa, lakini Biblia nzima siyo kwa kanisa.

Maandiko mengine mengi ya Biblia ilikuwa kwa Wayuda, na kuna sehemu la upekee la Biblia lenye linaelekea Kanisa la Yesu Kristo, na ni sehemu ile ambayo Mwenye Mungu alimuangazia mtume Paulo.

AMINA.

N°Ref: 01/21/1962 / 239 - DANGER IN THE CHURCH / 06/31/2022

No comments:

Post a Comment