Saturday, April 30, 2022

UTAFANANA NAMNA GANI KWA NYAKATI ITAKAO KUJA / HOW WILL YOU LOOK IN THE FUTURE




UTAFANANA NAMNA GANI KWA NYAKATI ITAKAO KUJA 

HOW WILL YOU LOOK IN THE FUTURE 

March 14, 1965

Pastor Henry F. Kulp 





 

Waroma 8: 17 – 19 

“na kama sisi, basi tu wariti: wariti wa Mungu na wariti pamoja na Kristo; kama tukiteswa pamoja naye, ili tutukuzwe pamoja naye vilevile. 

Kwa maana ninahesabu mateso ya wakati huu wa sasa kuwa si kitu tukiyafananisha na utukufu ule utakaofunuliwa kwetu. 

Kwa maana viumbe vyote vinangojea kwa hamu sana ufunuo wa wana wa Mungu.” 

         Hapa Mwenyezi Mungu anazungumuzia mwamini kama muriti pamoja na Kristo, sisi tutakuwa wariti pamoja na Kristo katika yote na ndani ya yote. 

Sisi si wariti tu, lakini sisi ni wariti pamoja na Kristo. 

Uriti wetu ndani ya Kristo hautagawanyika. 

Hauta gawanyika kamwe kwa sehemu mbalimbali na hii ni jambo maalum umbalimbali na kuwa mwanamemba wa ufalme wa hapa duniani kwenye urizi unagawanywa kwa sehemu.  


1/ Mwenyezi Mungu anasema tena kwamba:  

… kama tukiteswa pamoja naye, ili tutukuzwe pamoja naye vilevile. 

Kwa maana ninahesabu mateso ya wakati huu wa sasa kuwa si kitu tukiyafananisha na utukufu ule utakaofunuliwa kwetu.  

Kwa kweli kuna neno lisilo andikwa hapa, lakini lenye kufaa sana katika wazo hili, na  ni neno la muhimu sana katika maisha ya kikristo. 


2/ Mbele niwajulishe neno lile, nataka kwanza tufikiri kuhusu jambo moja. 

Kwa kweli, kuna wapagani kazaa wenye kutizama maisha ya wakristo na wanasema: 

Sina kitu cha kutamania zidi ya maisha ya wakristo, kwa sababu sioni jambo njema wanalo lenye mimi sina. 

Wao, wanakumbwa na shida na matatizo aina yote yenye inayonikumba, pia wao hupata ajali kama mimi. 

Ninafahamu wengi wa watoto wa Watumishi maalum wa Mungu, walioishi maisha ya kumucha Mungu na utawa, na watoto wao vilevile walisema maneno kama yale, sababu waliona kiwango gani wazazi wao walisumbuka, wakiwa na maisha ya tabu, kwa hiyo, sioni jambo la kutisha  na kuvutia katika maisha ya kikristo. 

Kwa hiyo, jameni muacheni mimi niende inje, nikijifurahishe, nile, ninywe na nipitishe saa katika anasa na raha. 


3/ Wengine wanaojitahidi kuwa marafiki wa Biblia, wakijiita wakristo  wanajitwika bidii ya  kupima kubadirisha hali hili. 

Wanasema kwamba kanisa ilishindwa kutumia zawadi zake za kiroho na yakuwa, kwa kupata baraka hizo, sharti wewe uwe yule mtu mwenye kuambatana na hali yenye Mwenyezi Mungu anataka wewe kuwa. 

Ukiheshimu mwenendo huo, wewe utakuwa na gari nzuri sana kwa mahali pako, utaishi katika gorofa nzuri, ndaa yako itajaa na pesa, utakuwa na kazi nzuri na afya ya mwili wako itakuwa nzuri. 

Lakini kwa wepesi, unapotizama watu wale, utatambua kwamba hakuna hata kitu moja kinacho timilika ndani ya maneno yote wanayoyasema. 

Hakuna kile kinacho timilika. 


4/ Neno hili fupi tunalopenda kuwafunulia, ni jambo ambalo twapasha kufahamu, ni neno “Subiri” 

Mungu hakutuahidi vifaa na hazina vya hapa chini duniani, lakini anatuahidi nyakati itakao kuja ya utukufu.   

Kwa mfano, hapa kwa kanisa letu la fasi, tunatarajia majengo ya shule ya jumapili ama nyumba yenye watoto watatumia kwa ibada yao ya watoto, pia tunatarajia kuwa na kitengo cha elimu na maadibisho, hapa kwa kanisa letu la Altoona Bible Church. 

Sisi tuko kwenye changamoto ya kuendelesha na kutimiza miradi na mkakato wa yale majengo. 

Tuna mbunifu mjenzi ama mjengaji mkuu anayefanya taswira ya majengo haya yote, na mipango haya yote yataoneshwa kwenu, na kweli mutayaona. 

Mistari hii iliyochorwa kwenye kartasi, siyo nyumba, baadaye itafaa kuweko mkataba na masikilizano kuhusu kazi, na kwa mwisho wajengaji wataanza kuchapa kazi. 

Wajengaji watapandisha ukuta ya sehemu zote wakifuata kwa makini sana picha iliyochapwa na mjengaji mkuu, sawa vile  alivyochora kwenye kartasi.

Nasi vilevile, Mjengaji wetu Mkuu ni Mwenyezi Mungu, Yeye anatupatia ahadi kuhusu nyakati zitakazokuja, anatuchorea mipango yake na miradi yake ndani ya Maandiko Matakatifu. 

Na siku moja wakati tutakapokwenda kukutana naye uso kwa uso, yote tuliyo tarajia tutayaona waziwazi kwa mecho yetu wenyewe. 

5/ Kila mara wakati ninaposoma maandiko ya Waroma 8, mafikiri yangu yanakwenda pale pale kwa Maandiko ya 2 Timoteo 4: 7 – 8, 

“Nimepiga vita vizuri, nimemaliza mwendo wangu, nimelinda imani; nyuma ya haya nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana mhukumu wa haki atanipa siku ile; wala si mimi tu, lakini watu wote pia wameopenda kuonekana kwake.” 

         Mtume Paulo amesema hapa kwamba amepiga vita vizuri, amemaliza mwendo wake, pia amelinda imani, kwa muda huu, kama mutakumbuka, Mtume Paulo alikuwa anangojea kuuwawa, tayari walijitayarisha kumukata kichwa na alikuwa tayari kukutana na Bwana Yesu Kristo. 

Tizama sasa neno la kwanza la aya ya nane. 

“Nyuma ya haya” neno la kuvutia na la muhimu. 

Wewe, maishani mwako, unayo neno la kufanana kama neno “nyuma ya haya”? 

Neno hili latuangazia kwamba nyakati itakao kuja itakuwa ya raha na heshima kubwa. 

Je, maishani mwako, neno unayo yafanana tu na “sasa hivi”, hapo hapo”,  ama unayo vilevile neno “nyuma ya haya”? 

Kwa kweli, mukristo  anaishi kwa kungojea  “nyuma ya pale nimewekewa”. 


6/ Tuchunguze sasa yanayosemwa kwa aya ya 18, (Waroma 8: 18) 

…utukufu ule utakaofunuliwa kwetu. 

Hapa tuna jambo maaulum sana kujifunza. 

Biblia inatuambia kuhusu utukufu yenye kuumbwa na utukufu usioumbwa. 

 

1 Wakorinto 15: 41 

“kuna utukufu mmoja wa jua, na utukufu mwengine wa mwezi, na utukufu mwengine wa nyota; kwa sababu nyota moja inautukufu mbalimbali na nyota nyingine.” 

         Hapa mtume Paulo anatuzungumuzia kuhusu Ulimwengu, anatueleza kwamba kuna utukufu ndani ya jua, kuna utukufu mwengine ndani ya mwezi, pia kuna utukufu mwengine ndani ya nyota. 

Na nyota moja inautukufu mbalimbali ya nyota nyingine. 

Haya yote yanakuwa na utukufu yenye siku moja itatoweka, siyo utukufu wa milele. 

2 Petro 3: 10 

“lakini siku ya Bwana itakuja kama mwizi; katika siku hii mbingu zitatoweka na sauti kubwa, na viumbe vya asili vitayeyushwa kwa moto mkali, na inchi na kazi zilizo ndani yake zitateketezwa.” 

         Hii siyo utukufu wenye tutakuwa nao. 


7/ Tukumbuke kwamba 1 Wakorinto 15: 43, inasema kwamba: 

“unapandwa katika haya; unafufuliwa katika utukufu: unapandwa katika uzaifu, unafufuliwa katika uwezo;” 

         Mwili wa ufufuko, ulipandwa katika kuoza, unafufuliwa katika kutokuharibika. 

unapandwa katika haya; unafufuliwa katika utukufu: unapandwa katika uzaifu, unafufuliwa katika uwezo. 

Tunaona hapa hali tatu mbalimbali sana yanayoonesha hali ya mwili.  

 

Kwanza wakati mwili unazikwa kwa udongo,   pia wakati wa ufufuko. 

Kwanza tunapandwa katika haya ya kuoza, tunafufuka katika hali ya kutokuharibika. 

Kuoza yaonekana wazi na mwili wa mufu unazikwa katika hali hii ya kuoza. 

Mwili unaoza. 

Na Watumishi wa Mungu wanasema: “Mavumbi wewe, utarudi kwa mavumbi.” 

Nazani ni vema turudishe mafikiri yetu katika Maandiko ya Yoane 11: 39  

Hapa Marata yuko mbele ya kaburi ya kaka yake na anasema:

“Yesu akasema: Mwondoshe jiwe. 

Marata, ndugu mke ya yule mtu aliyekufa, akamwambia: Bwana ananuka sasa; maana, amekuwa maiti siku ine.” 

         Hali ya kutokuharibika ni umbalimbali na kuoza. 

Kutokuharibika ni hali isiyo ya muda, ni ya milele, kamili, isiyo na kivuli ya kugeuka. 


8/ Pia anasema 

Unapandwa katika haya; unafufuliwa katika utukufu. 

Ni kweli kwamba tunafanya yote iwezekanayo kwa kuleta heshima kwa mwili wa marehemu wakati wa mazishi. 

Tunatafuta mavazi mazuri, sanduku nzuri, maua, tunajipanga kwa mustari mbele ya sanduku ya marehemu ili tumutazame kwa mwisho, kiisha tunaendelea na mazishi, na haya yote ni vema. 

Bali, kwa muda huohuo, mwili mwenyewe unaanza kuoza, hali ya haya, tunaanza kujiharakisha ili tuutowe kando yetu kwa woga wa kutokuvumilia matokeo ya mwili kuanza kuharibika na kuoza na hatutaki kufikia kiwango cha kutokuvumilia harufu mbaya ya mwili kuoza. 

Bali, mwili wenye tutakuwa nao kwa ufufuko, utakuwa mwili wa utukufu. 

Jameni, bila shaka, mwili huo utakuwa wa utukufu. 

Hii ni sehemu ya utukufu yenye itakuwa yetu.

Waroma 8, inatuambia kuhusu nyakati hiyo, miili yetu itakuwa ya utukufu. 

Na itafananishwa na nini?  

Tujikumbushe kwa muda muchache jambo la Bwana Yesu kugeuzwa sura juu ya mlima. 


Matayo 17: 1 – 2 

“Na nyuma ya siku sita Yesu akatwaa Petro, na Yakobo, na Yoane, ndugu yake pamoja naye, na kuwaleta juu ya mlima mrefu peke yao; 

Akageuzwa sura mbele yao; sura yake ikangaa kama jua, na mavazi yake yalikuwa meupe kama nuru.” 

         Inasemwa kwamba sura yake ikageuzwa na ikangaa kama jua, na mavazi yake yalikuwa meupe kama nuru.  

Miili yetu itakuwa sawa na ya Bwana Yesu, kama vile tusomavyo katika 

Wafilipi 3: 21 

“atakayebadilisha mwili wetu wa haya upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uwezo ule anaoweza kutiisha vitu vyote viwe chini yake.” 

         Kwa wewe uliyeokoka kweli utarajie jambo hili, kwa sababu utakuwa na mwili wa utukufu. 

Tafakari namna unavyotunza mwili wako kila siku. 

Lakini siku moja, mwili peke yake utakuwa mwili wenye utukufu. 

Mbele ya siku chache, nilisoma katika gazeti Altoona mirroir, kwa sehemu iitwayo Siku ya sita mangaribi, na ilikuwa kuhusu mchezaji moja mwanamuke aliyekuwa murembo sana, lakini uzee ulimushambulia na anapoteza kungaa kwa urembo wake. 

Lakini utukufu tutakayopata haitatoweka kamwe, itakuwa nasi siku zote kwa milele. 

Nashindwa namna ya kueleza aina ya utukufu huo, bali ni utukufu  tutakaokuwa nao.  

Ni wajibu wetu kuisubiri kweli. 


9/ Baadaye, mwili wa kufa wenye unazikwa katika haya, 

 Ushujaa wote unatoweka, hakuna hata nguvu kidogo ya kumruhusu kupumua hata donge moja la pumzi. 

Mwili inapoteza uwezo na nguvu ya kupiganisha mashambulio yote ya nje inayosababisha mwili kuoza. 

Mwili unalala hapo ukiwa bila uwezo wowote wa kujikinga na mashambulizi yote ya asili. 

Ni hiyo hiyo mwili itakayoonekana baadaye katika uwezo. 


10/ Baadaye, tupime kufahamu mambo machache kuhusu utukufu. 

Yoane 17: 5 

“Na sasa unitukuze, Baba, pamoja nawe mwenyewe, kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe mbele ya kuwa dunia.” 

         Bwana Yesu Kristo, katika maombi yake hapa kama Kuhani Mkuu, aliomba Baba Mungu amurudishie utukufu wake aliokuwa nao katika umilele uliopita, mbele Bwana Yesu ajifanye kuwa mtu, akiacha kando ule utukufu wake. 

Hii ni utukufu wenye hauwezi kuumbwa. 

Ni utukufu wa milele. 

Ni utukufu unaodumu milele daima, sawa vile Mungu ni wa milele daima. 

Utukufu huu ni wa milele daima, kwa hivyo aliomba Baba Mungu amurudishie ule utukufu wake, na kweli Utukufu wake ulirudishwa kwake. 


11/ Bali, wakati Bwana Yesu alipokuwa akitembea duniani, Yeye hakuonekana na huo utukufu. 


Marko 6: 1 – 3 

“Akatoka kule, akafika katika inchi yake mwenyewe; wanafunzi wake wakamfuata. 

Ilipokuwa sabato, akaanza kufundisha katika sunagogi. 

Watu wengi wakisikia, wakashangaa, wakasema: 

Huyu amepata maneno haya wapi? 

Na akili gani aliyopewa huyu? Na nini matendo ya uwezo yaliyofanyiwa na mikono yake? 

Huyu si seremala, mwana wa Maria, na ndugu ya Yakobo na Yose na Yuda na Simini? Ndugu zake wanawake si hapa pamoja nasi? Wakachukizwa naye.” 

         Wakati alipokuwa akitembea hapa chini duniani, Bwana Yesu alikuwa sawa sawa na mtu kawaida, sawa mtu wa aina ya watu kama desturi, na wao walimjuwa kama musermala. 

Kwa muda huo hakuwa hata na sehemu ya Utukufu wake, 

Alifanya maishara mengi na matendo ya ishara bila kuwa mtu wa hali ya utukufu, sawasawa nasi kwa siku za leo. 

Wakati tunapotembea na kujielekeza huko na kule katika mitaa yetu, hatuoni watu kushimama kwa kushangaa wakisema: Tazameni mtoto wa Mungu yule anayeelekea huko, ama tazameni mtu wa utukufu anayetembea. 

Hakuna mambo sawa na yale ijapokuwa mchana na usiku wanatutizama tukiwa kama mashaidi kwao. 


12/ Wakolosayi 3: 4 

“Wakati Kristo aliye uzima wetu atakapofunuliwa, nanyi vilevile mutafunuliwa pamoja naye katika utukufu.” 

         Sisi tutafunuliwa pamoja Naye katika Utukufu wake, na utukufu ule hautakuwa utukufu ulioumbwa, ni utukufu ambao, baada ya sisi kuupata, utabaki kwetu milele daima. 


13/ Tunavumbua kawaida ya mafundisho ya aina mbili katika Maandiko ya Wakolosayi 3: 4, sababu inasema kwamba wakati Kristo aliye uzima wetu atakapofunuliwa, nanyi vilevile mutafunuliwa pamoja naye katika utukufu.  

Neno kuonekana inatafsiriwa mu kigriki kwa neno kufunuliwa, pia vilevile kwa neno kumfunua. 

Nikusema kwamba kawaida ya mafundisho ya kufunuliwa na ya utukufu yanatimilika kwa nyakati moja. 

Wakati tutafunuliwa, tutatukuzwa.  

 

AMINA.


N°Ref: 03/14/1965 / 290 - HOW WILL YOU LOOK IN THE FUTURE / 04/30/2022

No comments:

Post a Comment