Thursday, December 3, 2020

WAKATI MUNGU ALIPOWAAMBIA SIRI / WHEN GOD TOLD A SECRET

Photo by B Smith from Patio



 

WAKATI MUNGU ALIPOWAAMBIA SIRI 

WHEN GOD TOLD A SECRET

July 10, 1977

Pastor Henry F. Kulp

 

 

Wakolosayi 1: 24 – 29 

“Basi sasa ninafurahi katika mateso yangu kwa ajili yenu, na ninatimiza katika mwili wangu yale yaliyokosa ya mateso ya Kristo kwa ajili ya mwili wake, ndio kanisa lake. 

Nami nimefanywa mtumishi wake, sawasawa na uwakili wa Mungu niliopewa kwa faida yenu, nitimize Neno la Mungu, 

Siri iliyofichwa tangu nyakati na vizazi vyote; lakini sasa imefunuliwa kwa watakatifu wake, 

Kwao Mungu alipendezwa kuwafunulia utajiri wa utukufu wa siri hii katika Mataifa, iliyo Kristo ndani yenu, tumaini la utukufu; 

Ambaye tunamhubiri, tukionya kila mtu na kufundisha kila mtu na akili yote, ili tupate kuleta kila mtu mtimilifu katika Kristo. 

Kwa sababu hii ninajitaabisha, nikishindana na nguvu kwa kadiri ya kutenda kazi kwake anayetenda kazi ndani yangu kwa nguvu.” 

Tulikuwa tukijifunza upekee wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. Umtu wake na Kazi yake. 

Bali, kwa sasa tutaona upekee wa Mtume Paulo. 

Hii ni Kufwatana na namna Mtume Paulo anatuletea Mahubiri ya namna ya kipekee. 


1/ Mtume Paulo, kwa upande wa kimtu, hanachochote kile cha kumuweka kwa hali ya kipekee, bali ni Huduma yake ama wizara yake ndiyo ya kipekee.  

Hatuzungumuze kuhusu upekee wa mtu Paulo ama kazi yake, bali upekee wa Mahubiri na Habari njema aliyo hubiri na kutangaza.  


2/ Aya ya 24 

“Basi sasa ninafurahi katika mateso yangu kwa ajili yenu, na ninatimiza katika mwili wangu yale yaliyokosa ya mateso ya Kristo kwa ajili ya mwili wake, ndio kanisa lake.” 

Kwa kweli, watu wengi, wanaposoma Aya hii wanaanguka katika mawazo isiyo halali pia ya udanganyifu ya kuzania kwamba mateso ya Bwana na Mwokozi wetu YESU KRISTO hayakutimilika na kwamba ingeliwezakuwa Mtume Paulo ndiye aliyeweza kukamilisha yale yaliyobaki. 

Mawazo hii siyo ya kweli, ni umbalimbali sana na mafundisho yenye Aya hii inatufundisha hapa, Aya hii haisemi namna ile.  

Katika Maandiko haya Mtume alikua anazungumuzia huduma yake ya namna mbili, huduma yenye ilikuwa na ngambo mbili ama pande mbili. 

Tutajifunza na kuleta mwangaza zaidi juu ya upekee wa Huduma na  Wizara ya Mtume Paulo. 

Wakati mtu asomapo maandiko haya, mtu anazania kwamba mateso ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo juu ya musalaba pale Kalvari hayakukamilika na kwamba iliwezekana Mtume Paulo ndiye aliyeweza kuyakamilisha. 

Maandiko mengi na Aya nyingi mbalimbali katika Maandiko Matakatifu, Biblia Takatifu yanatuonesha kwamba KRISTO alikufa mara moja tu juu ya ondoleo la zambi zetu na hapana na kitu hata kimoja chenye Mtume Paulo angaliweza kufanya ili atimilize Kazi ya Bwana na Mwokozi YESU KRISTO. 


3/ Tufahamu sasa kwamba Aya hii haiseme juu ya Kusulubiwa ama hukumu ya KRISTO, hapana hata kidogo, bali inasema juu ya mateso ya KRISTO katika mwili wa Mtume Paulo.  

Hukumu aliyopata Bwana Yesu Kristo na kusulubiwa kwake haiwezi hata mara moja kuitwa sawa mateso ama mahangaiko. 

Kwa kweli katika Kigriki neno mateso ama mahangaiko ni THE-LIP-SIS inaonesha majukumu ya shida, na hiyo inasemwa kwa uwingi. 


4/ Inaonekana wazi kwamba Kusulubiwa na Hukumu ya Bwana wetu Yesu Kristo Musalabani haiwezekani yaitwe majukumu ya shida.  

Wakati mtu anaposambishwa mahakamani na kuhukumiwa, hiyo siyo majukumu ya shida, bali ni kuhukumiwa. 

Bwana wetu Yesu Kristo alibeba hukumu pale msalabani, na  ni kwa mahamuzi yake mwenyewe ndiyo alihamuru Mtume Paulo katika huduma yake apate mateso na majukumu mbali mbali ya shida katika mwili wake, na hiii inamaanisha kwamba hiyo mateso ilikuwa bado ingali inangojewa itendeke. 

Ni jambo gani Mtume Paulo anapenda kutufahamisha kwa masemi haya? 

Yafaa tufahamu kwamba maneno yaha yatutambulisha upekee wa Mtume Paulo. 

Hapa yeye anazungumuza juu yake yeye mwenyewe kwa  upekee, siyo kuhusu mtumishi mwengine, ama kuhusu mwalimu ama mchungaji mwengine atakayetokea  kwa  nyakati za kuja. 

Yeye haseme kuhusu wanamemba wa Kanisa Mwili wa Kristo, bali anazungumuza juu yake binafsi. 

Yeye anazungumuza kuhusu mzigo aliotwigwa na Mwenyezi Mungu kwa  kumubebesha hiyo huduma ama Wizara ya mateso. 


5/ Tuchunguze neno moja la muhimi sana lililotukia wakati Mtume Paulo alipo okolewa na kuitwa kwa huduma. 

Matendo ya Mitume 9: 15, 16 katika maandiko haya inasemwa wazi kwamba Huduma ama Wizara ya Mtume Paulo itakuwa ya kuteswa. Bwana Yesu mwenyewe ndiye  anayemwambia Anania ili naye aende kumwambia Paulo wakati alipokuwa bado akilazwa chini kwa pigo alilopigwa na Bwana katika njia yake ya kwenda Damasiki. Na Anania alipashwa kumuharifu juu ya mambo mangapi makubwa atakayoteswa kwa ajili ya JINA la KRISTO.  

Matendo ya Mitume 9: 15, 16

“Lakini Bwana akamwambia kwenda zako; kwa maana mtu huyu ni chombo kichagulifu kwangu, achukue Jina langu mbele ya Mataifa, na wafalme, na wana wa Israeli. 

Maana nitamwonesha mambo makubwa mangapi atakayoteswa kwa ajili ya Jina langu.”   

Eti munavumbua neno hili? 

Mtume Paulo alikua na Huduma ama Wizara ya Mateso. 

Tangu mwanzo wa mwito wake huduma yake ilikuwa ya mateso yasiyo ya kawaida. 


6/ Wagalatia 6: 17 

“Tangu sasa mtu asinisumbue, kwa maana ninachukua katika mwili wangu chapa zake Bwana Yesu.” 

Chapa zake Bwana Yesu ilimaanishanini ? 

Toka utafsiri wa Kigriki tunayo neno “unyanyapaa: alama ya uaribifu juu ya ngozi” ama tendo  kuchapa alama juu ya ngozi, kutia  chapa ama kovu. 

Inaonekana wazi kwamba Mtume Paulo anazungumuza juu ya kovu zilizokuwa juu ya mwili wake. 

Bila shaka yeye anazungumuza kuhusu kovu, vidonda na alama mbalimbali ya kuumia yenye aliyopata katika kumuhudumia Bwana Yesu Kristo. 

Vidonda, alama za mapigo na kovu zote alizokuwa nazo ziliharibu hata uso wake na haikuwa tena raisi kumutambua. 

Mtume Paulo anazungumuzia vidonda, alama za mapigo na kovu aliokuwa nayo kwa mwili wake. 

Tufahamu wazi hapa kwamba Mtume Paulo anatuonesha tofauti kati yake binafsi na wale walimu wa Wayaudi waliopinga huduma yake. 


7/ 2 Wakorinto 11: 24 – 26 

“Kwa wayuda mara tano nilipata mapigo makumi ine ila moja. 

Mara tatu nilipigwa kwa fimbo, mara moja nilipigwa kwa mawe, mara tatu nilipata kuvunjika kwa merekebu, mchana na usiku nimekaa katika bahari: 

Katika safari mara nyingi, katika hatari za mito, katika hatari za wanyanganyi, katika hatari za taifa langu, katika hatari za Mataifa, katika hatari za muji, katika hatari za jangwa, katika hatari za bahari, katika hatari za ndugu za uwongo;” 

Mtume Paulo alipigwa kwa fimbo, alifungwa vifungo, alipata kuvunjika kwa merekebu, mateso gani aliopata Mtume Paulo kwa upekee na kama vile munavyoona mateso haya mazito mno hayawezi kutiwa juu yetu.  


8/ Tatambue ya kwamba Mtume Paulo alifurahia mateso yale. Yeye alikua mwenye furaha katika mateso yale. 

Mateso yale hayakumusukuma kupoteza lengo alilokuwa nalo, wala hayakumgeuza munyonge, bali, yalimupa furaha katika yote. 

Sisi tunayo bahati ya kuingia na kupenya moyo wa mtume Paulo na kuona na kupenya katika mafikili yaliyokuwa kichwani mwake na kutambua hali ya huyu mtu mtume Paulo aliyeitwa katika huduma ya ngambo mbili.  

Upande wa kwanza ni Huduma ama Wizara ya mateso kwa niaba ya waamini, Mwili wa Kristo, huduma ambao haukumutia ndani ya hasira ama kumugeuza munyonge na asiye na furaha bali ilimutia moyo na kumupa furaha. 

Hii inaonesha namna gani Mtume Paulo alikuwa tofauti sana na wengi kati yetu. 


9/ Mtume Paulo alivumilia haya mateso mazito kwa niaba ya Mwili wa Kristo iliyo KANISA. 

Kanisa ni nini? 

Katika Biblia, wakati wowote tunapotafakari Maandiko Matakatifu, tukikuta neno Kanisa, yafaa tufikiri sana na kujiuliza eti ni kanisa gani? 

Siyo tu kanisa inayosemwa hivi hivi tu, siyo Taifa la Wana wa Israeli, siyo kanisa ya ufalme wa Utawala wa miaka elfu moja utakaokuja, Utawala wa Kristo, bali Kanisa iliyo Mwili wa Kristo, Huyo Mutu Mupya Mmoja anayesemwa katika Kitabu cha 


Waefeso 2: 15 

“Naye akikwisha kuondosha uadui katika mwili wake, ndiyo sheria ya amri zilizo katika maagizo; ili apate kufanya hawa wawili kuwa mtu mpya mmoja ndani yake, akafanya salama.” 


10/ Neno la kwanza ni kwamba Mtume Paulo alifanya Huduma ama Wizara ya Mateso na Neno la pili ni kwamba alifanya Huduma ama Wizara yake katika Mwili wa Kristo.  


11/ Hapo tunafika sasa kwa neno: Matunzaji (Mpango

Hiyo siyo neno ngumu kufahamu. 

Yawezekana siku moja ulikuwa kwenye Kambi ama umekwisha kutumika kwenye Wiwanda mbalimbali, unaweza kuwa na ufahamu ya kitu wanachoita Zahanati. 

Hapo ni mahali wanapo toa mpango, kuleta mashauri mbalimbali kuhusu afya na magonjwa, pia kuleta dawa kwa wagonjwa, ama kuwatunza. 

Matunzaji ni wakati ule muhimu wa kuleta ama kupana mpango ama kutoa.  

Ni tendo la Mwenyezi Mungu Baba wetu kuleta ama kupana, kugawa ama kushiriki kwa nyakati fulani. 


12/ Anayoyasema Mtume Paulo ni kwamba Mwenyezi Mungu amenikabizi maneno yenye nami vile vile kwa upande wangu napashwa kuwakabizi ninyi vile vile. 

Mwenyezi Mungu ananipa na kuniletea kitu chenye mimi vile vile napashwa kuwaletea ama kuwapa ninyi vile vile na hapo anamaanisha  sana Mataifa, walioitwa Wapagani, Mataifa nyingine isiyokuwa Taifa la Israeli. 

Hii ni Ufunuo mkubwa kuliko ufunuo mbalimbali tunayokuwa nayo ndani ya Biblia Takatifu toka Kitabu cha Mwanzo hadi Ufunuo wa Yoane. 

Katika Kitabu cha Ufunuo ya Yoane hamuna kitu kipya chenye hakipatikane katika Vitabu vingine ndani ya Biblia Takatifu. 

Hakuna jambo kigeni. 

Kitabu cha Ufunuo kimejaa maonyesho ama ufunuo yenye tumepata nafasi mbalimbali ndani ya Vitabu vingine kati ya Biblia.  

Ufunuo wote tunaopata katika Kitabu cha Ufunuo, tumeupata ndani ya Vitabu mbalimbali za Biblia bali Kitabu cha Ufunuo kimeyakusanya kwa  nafasi moja maneno yote ya siku za mwisho. 

Bali Ufunuo wa Siri anayofunua Mtume Paulo ni Siri yenye haikujulikana kwa nyakati za mbele.  

Ufunuo huo haukujulikana kwa Mitume kumi na miwili, bali kwake yeye Mtume Paulo pekee sawa vile Mtume wa Matunzaji mapya. 

Kanisa Mwili wa Kristo haikufahamika katika Agano la Kale. 


13/ Siri hii haikujulikana hata kwa muda wa mapito ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo hapa chini duniani. 

Tunafahamu wazi kwamba siri hii ilikuwa ikifichwa  tangu  zamani za kale, tangu vizazi na vizazi lakini kwa sasa imefunuliwa kwa watakatifu  wake.  


14/ Tuchunguze msemwa: “niliopewa kwa faida yenu” yenu inamaanisha Mataifa, Wapagani. 

Mtume Paulo hakuwa mmoja wa wale kumi na miwili. 

Yeye hakuwa wa kumi na miwili, bali yeye alikuwa wa kumi na tatu, namba ya kuanzishwa upya. Yeye alikuwa Mtume wa kuongezwa. 

Yeye hakupangwa kwa Kabila kumi na miwili ya Israeli. 

Mwenyezi Mungu alipatia wa mitume kumi na miwili yale yenye walipashwa kuwapa kabila kumi na miwili ya wana wa Israeli. 

Pia kufwatana na mpango ule Mwenyezi Mungu alipatia Mtume Paulo yale yenye alipashwa kuwapa Mataifa. Ni hiyo inayoitwa UKWELI WA MWILI. 

 15/ Tuzingatie neno hili: Nitimize Neno la Mungu.  

Neno kutimiza inakuwa na china lake toka  neno la Kigriki PLAY- ROW – O na inamaana ya Kukamilisha, kutimiza. 

Mtume Paulo alitimiza Neno la Mungu, hii inamaanisha kwamba Mwenyezi Mungu alifunulia Ulimwengu mambo yenye aliyokuwa bado hajafunulia  vizazi  vingine vya tangu kale. 

Na aliwafunulia yale yaliyotoshelea kuwa na faida kwa watakatifu wake wa sasa. 

Wewe hauna budi ya kupata neno lingine zaidi ya yale, siri yote tayari imekwisha kufunuliwa kwenu, hakuna nyingine iliyobaki, hakuna mafumbo na miradi mengine ya Mwenyezi Mungu yenye anatarajia kufunuwa tena. Hii inatimiza Neno la Mungu. 

Inaigeuza kuwa yenye kuenea, yenye kukamilishwa na kutimilika. 

Hakuna tena budi kungojea waandishi maalum, iwe wa kiume ama wa kike kama vile wa kina SMITH ama WHITE, ama waandishi wengine wale. 

Hakuna tena mwandishi hata mmoja atakayeweza kutuandikia kuhusu mafumbo ama miradi yingine zitakazo kuja   toka Mwenyezi Mungu. 

Mara tena tufahamu ya kwamba tukisema kwamba Maandiko ya Mtume Paulo ilitimiza Neno la Mungu ni kusema ya kwamba Maandiko yale ndiyo Ufunuo wa mwisho wenye Mwenyezi Mungu angelipashwa kutufunulia. 

Ufunuo ule unakuja kukamilisha nyingine yenye ilifunuliwa mbele ya hapo. 


16/ Katika mazingira ya kwamba mtu mmoja angelizuka na kuwa na ndoto ya kuwaza ya kwamba yeye ana yongezo ya kuongeza kwa Ufunuo wa Biblia Takatifu, mtu huyu ni mudanganyifu kweli na ni huzuni sana kusikia mambo kama yale sababu Biblia ilikamilishwa na Mtume Paulo. 

Hakuna tena hata wakati wa Nabii mupya kuja na neno lingine mupya. 


17/ Ukweli alioandika Mtume Paulo ni Jiwe la Musingi katika Biblia. 

Na tumesoma ya kwamba hiyo ni Siri Kuu ya Mungu, ni Siri iliyofishwa, inayovumbuliwa sasa kwa mtu.  


18/ Siri hiyo ni nini? 

   Kristo ndani yenu, Tumaini la utukufu. 

Hii ni kitu kipya kweli. 

Kusema kwamba Bwana wetu Kristo Yesu anaishi ndani ya  mtu wa Mataifa. 

Neno hili halingiwezekana wakati wa Pentekoste. 

Kwa siku ile Roho Mtakatifu alikuja kuishi ndani ya Wayaudi. 

Munakumbuka yale aliyoyasema: 

Yoane 16: 7, 8 

“Lakinni mimi ninawaambia ninyi kweli, Ni kwa faida yenu niondoke; kwa sababu kama siondoki, Msaidizi hatakuja kwenu; lakini kama nikikwenda, nitamtuma kwenu. 

Na wakati anapokuja, atahakikisha dunia maneno ya zambi, na maneno ya haki, na maneno ya hukumu;” 

Wakati nitaondoka, atakuja kwenu na kuishi kwenu

Ilimupasa Bwana Yesu Kristo kuondoka ili Roho Mtakatifu aje kuikaa kwao, na kwa siku ile ya Pentekoste, Roho Mtakatifu alikuja kuikaa ndani ya Wayaudi, Wayuda walio okoka; lakini kwa siku za leo, Bwana wetu Yesu Kristo anakuja kufanya makao yake ndani yenu, siyo tu Roho Mtakatifu peke yake, na kweli Yeye Yesu ni pale, na kweli Bwana Yesu Mwenyewe anaikaa sasa ndani ya Watu wa Mataifa, na hii ni Ukweli  mpya

Ni hii inafahamisha kwamba Kanisa Mwili wa Kristo  haiwezekane tena iwe Bibi arusi, sababu sisi ni kipande ama nafasi ya Yesu Kristo. 

Sisi tunakuwa ule Mtu Mpya Mmoja na Kristo anaishi ndani yetu.

Wayuda walikuwa tu na Roho Mtakatifu ndiye aliyeishi ndani yao, hapana Bwana Yesu Kristo, wao wanaweza kuwa Bibi arusi. 


19/ Tendo la kusema Kristo anaishi ndani yenu ni Ukweli Mkubwa wa Maandiko ya Mtume Paulo. 

Wagalatia 2: 20 

“Nimesulubiwa pamoja na Kristo, lakini ni hai; wala si mimi, lakini Kristo ni hai ndani yangu; na uzima nilio nao sasa katika mwili, ni uzima wa Imani iliyo ya Mwana wa Mungu ambaye alinipenda akajitoa nafsi yake kwa ajili yangu.” 


20/ Aya ya 28 (Wakolosayi 1: 28) 

“ambaye tunamhubiri, tukionya kila mtu na kufundisha kila mtu na akili yote, ili tupate kuleta kila mtu mtimilifu katika Kristo.” 

Ambaye tunamhubiri, tambua hapa kwamba sisi tunahubiri Mtu. 

Kubadilisha neno “Ambaye” na kuigeuza na neno “ndicho” ni kosa kubwa sana. 

Ukristo una Msingi wake juu ya Mtu na ule Mtu anaishi ndani ya mwamini. 


AMINA 


N°Ref: 07/10/1977 / 363-1 WHEN GOD TOLD A SECRET / 12/03/2020

No comments:

Post a Comment