Tuesday, December 22, 2020

UBATIZO HUU NI WA MUHIMU Sehemu ya Pili THIS BAPTISM IS NECESSARY Part II

Photo by B Smith from patio




 

UBATIZO HUU NI WA MUHIMU Sehemu ya Pili 

THIS BAPTISM IS NECESSARY Part II

March 27, 1960 

Pastor Henry F. Kulp

 

 


Waefeso 4: 1 – 6 

“Kwa hivi basi mimi, mfungwa katika Bwana, ninawasihi ninyi mutembee kama inavyostahili mwito mulioitwa, 

Kwa unyenyekevu wote na upole, kwa uvumilivu, mukichukuliana katika mapendo; 

Mukiangalia sana kuchunga umoja wa Roho katika kifungo cha salama. 

Mwili ni mmoja, na Roho mmoja kama vilevile mulivyoitwa katika tumaini moja la mwito wenu; 

Bwana mmoja, Imani moja, ubatizo mmoja, Mungu mmoja, naye ni Baba ya wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote.”

Kama vile tunavyoanza hotuba hii ya asubui ya leo, ningelihitaji mufahamu kwamba tarakimu “MOJA”, ni tarakimu ya hesabu yenye ionyeshayo Kanisa. 

Kuna, Mwili mmoja, Roho Mmoja, Tumaini moja, Bwana Mmoja, Imani moja, Ubatizo mmoja, Mungu Mmoja naye ni Baba wa wote. 

Tulijifunza sote kwamba katika Biblia Takatifu, tarakimu 12(kumi na miwili) inaonesha Taifa la Israeli, tena kwa hiyi tunaweza kusema kwamba tarakimu MOJA inaonesha Kanisa. 


1/ Kama mungelikuweko pamoja nasi wakati tulikuwa tukijifunza maana ya tarakimu mbalimbali katika Biblia Takatifu, mungeliweza kukumbuka kama MOJA ni tarakimu inayo onesha UMOJA.   

MOJA inatoa matengano ama tofauti yoyote. 

Mutakumbuka vile vile ya kwamba: 

              a. Tatu ni tarakimu inayoonesha ukamilifu wa kitu, kitu kamili. 

                 b.  Tano ni tarakimu inayoonesha neema 

                 c.   Sita ni tarakimu inayoonesha mtu. 

                 d.   Taba ni tarakimu Kamili. 

                 e.    Kumi na mbili inaonesha Israeli.       

2/ Tufahamu kwamba Waraka wa Waefeso katika Waefeso 5: 31, inatuambia kwamba: 

“Kwa sababu ya neno hili mume ataacha baba yake na mama yake, na atafungana na mke wake, nao wawili watakuwa mwili mmoja.” 

Na inasemwa ya kwamba Kristo na Kanisa ni Mwili Mmoja, na Yeye aliwafanya Wayuda na Mataifa wawe mtu MOJA katika Kristo. 

Waefeso 2: 14 – 15 

“Kwa maana yeye ni salama yetu, ambaye aliyetufanya sisi sote tuliokuwa wawili kuwa mmoja, na alibomoa kiambaza cha kati ambacho kilitutenga. 

Naye akikwisha kuondosha uadui katika mwili wake, ndiyo sheria za amri  zilizo katika maagizo; ili apate kufanya hawa wawili kuwa mtu mpya mmoja ndani yake, akafanya salama.”  

Kuna Mwili mmoja tu, lakini una viungo vingi. 

Masemi ya watu inaonesha sawa kuna miili mengi lakini siyo hivyo. 

Kuna Mwili Mmoja tu. 

Mtu anageuka kuwa kiungo cha Mwili huu kwa njia ya kuamini Yesu Kristo kama Bwana na Mwokozi, tunaombwa basi kuuchunga huo Umoja wenye Roho Mtakatifu aliotufanyia sisi katika Mwili huo. 


3/ Kanisa la Korinto halikuweza kuuchunga huu Umoja wenye uliofanywa kwao. 

1Wakorinto 1: 10 

“Basi ninawasihi ninyi, ndugu, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, ya kwamba ninyi wote museme neno moja, na matengano yasiwe katikati yenu; lakini mwungane katika nia moja na shauri moja.” 

Mtume Paulo anatuambia hapa kwamba matengano yalikuwa katikati yao. 

1Wakorinto 3: 1 – 3 

“Na mimi, ndugu, sikuweza kusema na ninyi kama na watu wa Roho, lakini kama na watu wa mwili; kama na watoto wadogo katika Kristo. 

Nimewakunywesha ninyi maziwa wala si chakula; kwa sababu mulikuwa hamujakiweza, hata sasa hamukiwezi; 

Kwa sababu hata sasa ninyi ni watu wa mwili; kwa sababu kuna wivu na ugomvi katikati yenu, ninyi si watu wa mwili mukienda kwa namna ya watu?” 

Mtume Paulo alikuwa na huzuni ya kuona kwamba watakatifu wa Korinto walikuwa wakigawanyika kwa zehebu mbalimbali. 

Hawakuwa wanajitahidi na kujikaza kuuchunga huo Umoja wa Roho, walikuwa wakiishi umujao wa magawanyiko.

 

4/ Najuwa kwamba nanyi mwafahamu yakuwa ni wazi kwamba kwa nafasi penye kunakua wivu na ugomvi, pale kunajaa magawanyiko. 

Mahali kwenye tamaa mbaya, wivu na magomvi inatawala, watu hawawezi kuishi Umoja wa Roho. 

1 Wakorinto 3: 3 

“Kwa sababu hata sasa ninyi ni watu wa mwili; kwa sababu kuna wivu na ugomvi katikati yenu, ninyi si watu wa mwili mukienda kwa namna ya watu?” 


Kila mukristo anapashwa kujitahidi katika roho yake kuchunga Umoja wa Roho

Kila mwamini wa kiroho anapashwa kuwa na wajibu na mapashwa kuhusu hali hii. 

Maneno yote tunayo nena yanapashwa kuelekea kuchunga umoja tunaokuwa nawo katika Yesu Kristo. 

Mambo yote tutendayo yanapashwa kuambatana na namna Mwenyezi Mungu anavyopenda sisi tuchunge Umoja wa Roho. 


6/ 1 Wakorinto 12: 25, 26 

“ili matengo yasiwe katika mwili; lakini viungo vichungane. 

Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote vinaumia pamoja; au kiungo kimoja kikitukuzwa, viungo vyote vinafurahi pamoja.” 

Hapa tunasoma ya kwamba matengano yasiwe katika Mwili, lakini viungo vichungane, kwa sababu kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote vinaumia pamoja; au kama kiungo kimoja kikitukuzwa, viungo vyote vinafurahi pamoja. 

Hii ni wajibu wetu na jibu letu, tuishi na tuone huu umoja na tuubebe popote tuendapo. 


7/ Kuna neno lenye tunapashwa kukazisha hapa: 

Mwenyezi Mungu hakusema matengano yasiwe kuhusu mtu asiyeamini Maneno ya Mungu, kwa maana, wasioamini hawako viungo vya Mwili wa Kristo, ni kwa sababu hii kuna utengano kati yetu na wao. 

Tunapashwa kuepuka wale wasiotembea pamoja na Bwana wetu Yesu Kristo. 

Tunapashwa fanya angalisho sana kwa kuheshimu Neno la Mungu wetu katika kila hali na kila jambo. Hii ndiyo njia moja tu ya kuwa na umoja. 


8/ Tulijifunza kwamba kuna Mwili Mmoja, Roho Mmoja, Tumaini moja, na kwa mwisho wa majifunzo yetu ya juma jana, tulikua tukizungumuzia neno Bwana Mmoja. 

Bwana Yesu Kristo anahitaji awe zaidi ya Mwokozi wetu maishani mwetu. 

Yeye anatamani kuwa BWANA wetu. 

Utatambua mara na mara katika Biblia Takatifu tuna msemwa “Ndio, Bwana”, sisi hatupashwe kamwe kusema hapana Bwana. 

Wakati Bwana wetu anaposema neno, yatupasa sisi kujibu tu “NDIO, BWANA.” 

Wakati tunaposema “HAPANA”, Yeye hayuko tena Bwana wetu. 

Tunapashwa kumpa Bwana wetu pekee, utii wote. 

Twapashwa kumtii Bwana wetu. 


9/ Kuna taswira ya maneno haya tunayozungumuzia na picha yake inapewa kwetu wakati Bwana Yesu Kristo alikua angali bado hapa duniani. 

Bwana Yesu aliwaambia kusanyiko kwamba Ufalme wa Mbingu ni katika mikono yake, wakati alipomaliza kuhubiri Mahubiri juu ya Mlima na neno kubwa la mafundisho yale tulipata katika: 

Matayo 7: 21 - 23  

“Si kila mtu ambaye ananiambia: Bwana, Bwana, atakayeingia ufalme wa mbinguni; lakini yeye anayefanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni. 

Wengi wataniambia siku ile: Bwana, Bwana, hatukutabiri kwa jina lako, na kwa jina lako tulitoa pepo wachafu, na kwa jina lako tulifanya matendo mengi ya uwezo? 

Halafu nitawaambia: Sikuwajua ninyi wakati wo wote; ondokeni kwangu, ninyi munaotenda maovu.” 

Bwana Yesu anasema: Kwa siku ile wengi watakuja mbele yake, watamwambia kwamba Bwana, Bwana hatukutabiri kwa jina lako? 

Na kwa jina lako tulifanya matendo mengi ya uwezo? Na Bwana Yesu atawaambia ondokeni kwangu, sikuwajua ninyi wo wote, ninyi mutendao maovu. 

Ni kusema kwamba, watu hawa wanasema: 

Tulitenda mambo haya yote kwa sababu tulifahamu kwamba wewe ndiwe Bwana wa maisha yetu, na Yeye atawaambia, Mimi sikuwa Bwana wa maisha yenu. 

Nyinyi hamukunitambua mimi kama BWANA. 

Ni uwongo mtupu. 

Ondokeni kwangu. 

Haitoshi sisi ku tamka kwa midomo yetu “Bwana”, kweli hiyo haitoshi. 

Kumtambuwa na kumuruhusu Bwana Yesu Kristo kama “BWANA wa maisha yetu” yawezekana tu kama sisi tunanyenyekea chini ya UBWANA wake. 


10/ Wafilipi 2: 11 

“hata kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni na vya dunia, na chini ya dunia, 

Na kila ulimi ukiri ya kuwa Yesu Kristo ni Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.”  

Hapa, tunaambia ya kwamba kila ulimi na kila goti lipigwe mbele ya Yesu Kristo. 

Hata ma milioni ya watu wanaopotea waliomsaliti Bwana Yesu Kristo. 

Wao waliofanya maapizi na viapo, waliokufuru Jina lake, wakitaja bure Jina lake, wote watakiri kama Yesu Kristo ni Bwana. 

Wapagani wote waliosaliti, watakiri kwamba Yesu Kristo ni Bwana. 

Hata sisi wakristo tuliomuamini kama Bwana na Mwokozi wetu tutamkiri kama Bwana wetu. Tafauti gani! 

Watu hawa watamkiri Bwana wetu Yesu Kristo kama Bwana, wakati itakuwa nyuma ya saa, kwa milele. 

Ni vema sana kumjua kama Bwana na Mwokozi wakati bado saa ingaliko, sababu siku yakuja na siku ile ni ya hatari wakati kutaka na kutokutaka utamtambua kama Bwana, na hapo ukiwa ndani ya ziwa la moto na kiberiti na hapo itakuwa nyuma sana. 

Hata katika maisha ya umilele wale wote waasi wanawoishi kufwatana na mila zao na mawazo yao, wataishi kufwatana na yale Yeye ataamuru wao waishi. 

Hata kama iwe katika ziwa la moto na kiberiti na mateso, wao wataishi kule wakitambua UBWANA wake. 


11/ Ifwatayo ni: Imani Moja. 

Nina uhakika kwamba ni Imani iliyotupatia wokovu. 

Imani iliyotuletea ukombozi. 


12/ Tunafika sasa kwa neno: Ubatizo Mmoja, na hii ni ya muhimu sana.

Kuna wao wanaozania na kusema kwamba ni ubatizo wa maji, lakini ningelitamani mutambue kwamba mambo yote mengine yaliyotajwa hapo mbele, yote ni mambo isiyo ya kawaida(na- chu –ral) tena yote ina china la kiMungu. 

Mwili, Tumaini, na Roho, na vilevile kwa Ubatizo, yote ina china la KiMungu. Kama ingelikuwa ubatizo wa maji, hiyo ingemaanisha kwamba ubatizo wa maji unahitajika kwa wokovu, bali tunafahamu kwamba sivyo. 

Tena, haiwezikane kuwa Ubatizo wa Roho Mtakatifu, kwa maana ubatizo huo umekwisha tayari kutajwa. 

Basi ni Ubatizo gani huo ulio wa muhimu kwa wokovu wetu na ambao tunaohitaji, wenye Mwenyezi Mungu anao katika mafikiri yake? 


13/ Luka 12: 50 

“Nina ubatizo kubatizwa nao, na ninasongwa namna gani hata utakapotimizwa!” 

Miaka mengi ilipita kiisha Bwana Yesu kubatizwa na ubatizo wa Yoane Mubatizaji, Bwana Yesu alisema kwamba ana ubatizo kubatizwa nao. 

Siyo budi kuwa na maulizo kuhusu ubatizo huu anaozungumuzia hapa. 

Bwana Yesu iko anazungumuzia Kufa kwake juu ya Musalaba.

Na anaita kifo chake juu ya Msalaba wa Kalvari, UBATIZO


14/ Tuna ubatizo wa maji, Ubatizo wa Roho Mtakatifu, na kwa kweli hakuna maulizo kichwani mwetu kuhusu ubatizo anayo zungumuzia hapa, ni Ubatizo wa kufa.  

Tunaingizwa katika Ubatizo huu mmoja ili tupate kuokolewa. 


15/ Tujifunze pamoja yale yenye Mwandishi Kenneth Wuest alikua anasema kuhusu swali hili, na nazani kweli yeye ndiye aliyepata mwelekeo muzuri zidi ya yale yote yenye nimekwisha kuona. 

Anatuambia kwamba neno “kubatiza” siyo utafsiri maalum wa neno lake la msingi tunalolipata katika Kigriki, bali ni nakala katika maandiko tafauti. 

Neno lililo kawaida limetumikishwa na Mwandishi SMITH kuhusu kuzamisha kipande cha chuma iliyo moto sana ndani ya maji ili kuitia baridi. 

Neno lile lilitumikishwa pia kwa askari Wagriki wakati walipoingiza songe la mupanga wao wa vita ndani ya kikombe cha damu, ama wa askari wa kabila la wa dharura wakati walipo ingiza songe la mukuki wao ndani ya kikombe cha damu; 

Hivyo, kwa kweli, inamaanisha tendo la kuingizwa na kutiwa ndani ya,   ni kusema kwamba Ubatizo Mmoja unaotajwa hapa ni tendo la mtu kuingizwa na kutiwa ndani ya

Ulizo sasa ni ndani ya nini?

Kifo cha Bwana Yesu Kristo

Pia inamaanisha kuingizwa ama kutiwa kwa mtu ndani ya mazingira mapya ama kutiwa pamoja na kitu kingine kwa kusudi la kubadili hali na uweko wa kitu kile na manzingira yake ya kwanza. 

Kwa kweli ni hiyo maana ya neno lile hapa. 

Sisi tulikuwa wenye kupotea na wenye kufa kwa sababu ya zambi zetu, tukiwa katika Adamu, na kwa sasa sisi tulitoshwa ndani ya Adamu na kutiwa katika Yesu Kristo kwa njia ya Kifo chake Msalabani. 


16/ Kwa kupana maana na mafasirio vizuri na waziwazi tena, kuna maandiko yanayoyasema wazi wazi: 

Waroma 6: 3, 4  

“Au hamufahamu, sisi sote tuliobatizwa katika Yesu Kristo, tulibatizwa katika kufa kwake? 

Hivi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika kufa: hata kama Kristo alivyofufuka toka wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo tutembee katika upya wa uzima vilevile.” 

Tunasoma hapa: Au hamufahamu, sisi sote tuliobatizwa katika Yesu Kristo.   

Tunapo tumia utafsiri wa “tendo la kuingizwa na kutiwa ndani ya”, hapa tunapata maana kamili. 

Au hamufahamu. Sisi sote tulioingizwa na kutiwa ndani ya Yesu Kristo, hatukubatizwa, bali tuliingizwa na kutiwa ndani ya kufa kwake. 

Ni kwa namna hii tu tunapata wokovu. 

Tunapata kuokolewa tu kwa njia hii pekee. 

Tukumbuke maandiko ya Wagalatia 2: 20  

“Nimesulubiwa pamoja na Kristo, lakini ni hai, wala si mimi, lakini Kristo ni hai ndani yangu, na uzima nilio nao katika mwili, ni uzima wa Imani iliyo ya Mwana wa Mungu ambaye alinipenda akajitoa nafsi yake kwa ajili yangu.” 

Sisi tuliingizwa na kutiwa ndani ya Kifo cha Yesu Kristo. 


17/ Waroma 6: 23  

“Kwa maana mshahara wa zambi ni mauti, lakini zawadi ya Mungu ni uzima wa milele katika Yesu Kristo Bwana wetu.” 

Kwa hivyo, sharti kila zambi ilipwe. 

Mungu haachiliye zambi ama kufunga mecho juu ya zambi. 

Mungu hazarau zambi, haliachi kupita bure. 

Mungu anasema sharti kila zambi lilipwe, na malipo yake ni mauti.

Wakati Bwana wetu Yesu Kristo alikufa kwa msalaba, alilipa malipizi na mshahara wa zambi. 

Yeye asiyejuwa zambi alimufanya kuwa zambi na alilipa malipo ya zambi kwa ajili yetu, malipo ya zambi ni kifo.

 Wakati tunapomwamini Bwana Yesu Kristo, tunaingizwa na kutiwa katika Kufa Kwake, na Ufufuko wake na ni hii UBATIZO MMOJA unaosemwa katika maandiko ya Waefeso 4: 5. 

“Bwana mmoja, Imani moja, ubatizo mmoja,” 


18/ Waroma 6: 4 

“Hivi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika kufa: hata kama Kristo alivyofufuka toka wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo tutembee katika upya wa uzima vilevile.” 

Hapa tunaambiwa kwamba tulizikwa pamoja naye kwa tendo la kuingizwa na kutiwa ndani ya kifo yake, hata kama Kristo alivyofufuka toka wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo tutembee katika upya wa uzima vilevile. 

Kwa kweli, ubatizo wa maji hauwezi kamwe kutenda kazi hii.  

Hapa Biblia haituambie kwamba ni mufano wa kitu kinacho fanyika kwa mwamini; hapa siyo jambo la mfano. 

Hapa ni tendo kamili lenye linafanyika. 

Sisi tuliingizwa na kutiwa katika kufa ya Bwana wetu Yesu Kristo, tulizikwa pamoja naye pia tena mwamini alifufuka pamoja na Yesu Kristo. 


19/ Tukamate sehemu nyingine ya Maandiko Matakatifu inayoonesha ukweli huu. 

Wagalatia 3: 27 

“Maana ninyi wote mulio batizwa na kuingizwa katika Kristo, mumevaa Kristo.” 

Maana ninyi wote mulio batizwa na kuingizwa katika Kristo, mumevaa Kristo. 

Wakati mtu anapobatizwa, kuingizwa na kutiwa ndani ya Bwana Yesu, mtu huyo anakuwa ndani ya Yesu. 

Kwa kweli ubatizo wa maji haufanyi kazi hii. 

Ni wazimu mtupu kuwaza namna ile. 


20/ Waroma 3: 4  

“Hapana, hata kidogo; lakini 

Mungu akae kweli, na kila mtu mwongo: kama ilivyoandikwa: 

Uhesabiwe kuwa na haki katika maneno yako, 

Na ushinde wakati unapohukumiwa.” 

Tunasoma Maandiko inayosema: 

Hapana hata kidogo; lakini 

Mungu akae kweli, na kila mtu mwongo.  

Tujifunze neno moja kwa moja na tupime kufahamu nini Mwenyezi Mungu anapenda kutuambia kwa neno hili. 


22/ Baadaye anasema: 

Mungu ni Mmoja na ye ni Baba ya wote, alie juu ya yote na katika yote na ndani ya yote. 

Hii siyo maneno ya kawaida ya siku hizi namna tunavyoona Mungu kama Baba, ama ushirika ulimwenguni wa watu, lakini hii inamaanisha kwamba Mwenyezi Mungu ndiye aliyeumba kila mtu. 

Ukweli huu tunaupata katika Kitabu cha Matendo ya Mitume 17: 26

“Naye alifanya kila taifa la watu kuwa wa damu moja, wakae juu ya uso wa dunia yote, akaandika nyakati ambazo aliwaamuru tangu zamani, na mipaka na makao yao,”  

Hapo Mwenyezi Mungu anatuambia ya kwamba Yeye alifanya kila taifa la watu kwa damu moja. 

Ni kusema kwamba ni Yeye ndiye aliyeumba watu wote.

Ni kwa sababu ya hiyo ndiyo maana anaitwa Baba wa watu wote. 

Na Yeye anauhusiano na watu wote, siyo tu wale wakristo walioamini Mwana wake, bali Yeye anakua na uhusiano na kila mwanadamu anayeishi pia anauhusiano pia hata na wale waliomukana KRISTO. 

 

22/ Tutambue tena kwamba Mwenyezi Mungu iko juu ya wote. 

Tuchunguze vema tofauti anayoonesha hapa: 

Mungu ni juu ya watu wote, bali anakaa ndani yako.  Ndani ya wale waliomwamini Bwana Yesu Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wao. 

Ni kwa sababu ya hayo ndiyo maana tuliweka mbele yetu tofauti kati ya mtazamo wa Mwenyezi Mungu kwa ulimwengu mzima na kwa wale waliozaliwa mara ya pili kwa njia ya Roho wa Mungu. 

Kweli sisi tunayo hali kubwa na tukufu la kupandishwa. 

Wakani tunapotembea katika barabara za mtaa wetu, Mwenyezi Mungu anatamani sisi tuwe waangalifu, tukifahamu ya kuwa Yeye Mungu anakaa ndani yetu. 

Kwa mwanzo wa mahubiri na neno letu hili, tuliufungua na maonyo, na tulionya ya kwamba: 

Tutembee kama inavyostahili mwito tulioitwa. 

Kutembea kama inavyostahili Yesu Kristo kufwatana na mwito tunaokuwa nao katika Yesu Kristo. 


AMINA 


N°Ref: 03/27/1960/ 218 - THIS BAPTISM IS NECESSARY Part II / 12/22/20

No comments:

Post a Comment