Sunday, August 30, 2020

KRISTO ALISHUKA KUZIMU? (Sehemu ya pili) / DID CHRIST DESCENDED INTO HELL (Part II)

 

Volcano in Goma 100 miles north of  Bukavu, D R Congo






   KRISTO ALISHUKA KUZIMU? (Sehemu ya pili) 

    DID CHRIST DESCENDED INTO HELL (Part II)

    May 1, 1960 

    Pastor Henry F. Kulp



 

Waefeso 4: 7 – 11

“Lakini kila mtu katikati yetu alipewa neema kwa kadiri ya kipimo cha zawadi ya Kristo. 

Kwa hivi anasema: 

Wakati alipopanda juu, alifunga kifungo, 

Akawapa watu zawadi. 

(Basi neno hili: Alipanda, maana yake nini kama si kusema kwamba Yeye alishuka vilevile mpaka pande za chini za inchi? 

Yeye aliyeshuka ndiye aliyepanda vilevile juu sana kupita mbingu zote ili ajaze vitu vyote.) 

Naye alitoa wengine kuwa mitume; na wengine kuwa manabii, na wengine kuwa wahubiri wa Habari Njema; na wengine kuwa wachungaji na walimu;”  

Juma jana, wakati  tulipojifunza maandiko haya, tuliona yakwamba kuna wale wanaojizania kujuwa imani ao fundisho lenye mutume alileta hapa, na wengi wao wanasema kwamba KRISTO alishuka kwenye Hadeze, na mafundisho wanayo fundisha kwa mawazo yao ni kwamba:

  KRISTO alienda kukutana na watakatifu wa Agano la Kale, waliokuwa kule,   kwa sababu damu ilikuwa bado haija mwangika. 

Na kwamba, Kiisha tu  kumaliza kazi yake pale musalabani, alishuka huko chini kusudi la wokovu wa hiyo sehemu,  ni kusema wale waliokuwa katika Hadeze. 

Na kwamba aliwahubiri wale watakatifu waliokuwa kule, kiisha akawakomboa na akawachukua akapanda pamoja nawo mbinguni. 

Kwangu mimi,  kwa kweli, hayo mafundisho nayaona kwamba ni ya ujinga kweli. 

Kwa sababu mafundisho ya namna sawa hayapatikani katika Maandiko hii.  

Maandiko hii haizungumuze kuhusu kupanda ama kushuka ya namna ya kimwili, bali kuhusu Hali na Nafasi, Ranga, Uwezo na Mamlaka. 


1/ KRISTO alikuwa SAWASAWA na MUNGU. 

Alikuwa Mmoja wa Utatu Mtakatifu. 

Akajifanya Mwenyewe kuwa na hali na nafasi ya kupokeya amri na pendekezo kutoka kwa Mungu Baba, wakati Alikuja Yeye Mwenyewe kutimiza Mapenzi yake hapa duniani. 

Aligeuka kuwa mwenye kutii Serkali. 

Alikuwa mwenye kutii wazazi wake, akageuka mtumwa wa wanadamu, na akafa kifo cha msalaba na akafufuka toka wafu. 

Kwa kutimiza hivyo Biblia inatuambia kwamba Yeye atanyanyuliwa juu zaidi sana kupita mbingu zote. 

Na kwa kweli neno hili haliwezi maanisha hali na nafasi ya kimwili, kwamba mtu awe kwa hali ya juu sana zaidi kupita mbingu zote, kwa sababu kwa saa hii, KRISTO ameketi pale Mbingu ya Tatu, Akiwa kwa Mukono wa Kuume wa Mungu Baba. 

Ni kusema kwamba,  hii inamaanisha Hali na Nafasi, Ranga, hapana kupanda ya namna ya kimwili.

Na kwa hiyo, kushuka inayotajwa  hapa haimaanishi kushuka ya namna ya kimwili, lakini hali ya kujiyenyekeza Mwenyewe, kujitia kama hana utukufu, kukamata namna ya mtu, kugeuka mtumwa, kulaaniwa wakati zambi zote ziliwekwa juu yake, na kufa  juu ya msalaba pale Kalvari. 


2/ Wakati tunaambiwa: Kwamba Bwana Yesu alishuka katika sehemu za chini za nchi(dunia), hiyo inamaanisha kwamba: 

Bwana Yesu alishuka katika sehemu za chini, dunia. 

Sababu kwa kufanya hivyo aligeuka kuwa mtumwa wa wanadamu. 

Ranga, ama hali na nafasi hii, hakuijuwa tangu Umilele wake uliopita, na hatalijuwa katika Umilele wake kwa wakati wote utakaokuja. 


3/ Yoane 13: 4, 5  

“akaondoka kwa chakula, akaweka mavazi yake kando; akatwaa kitambaa, akafunga kiuno chake. 

Kiisha akatia maji kwa kibakuli, akaanza kunawa miguu ya wanafunzi wake na kuipanguza kwa kitambaa ambacho alijifunga kiuno chake.” 

Hapa tunakuwa na picha ya KRISTO akishuka kwa Ranga, hali na nafasi. 

Tunaona Bwana Yesu Kristo akinawa miguu ya wanafunzi wake kumi na miwili, kiisha kutembea safari ndefu ya miguu toka njia inayo jaa mavumbi mingi. 

Na alialikwa  kwa chakula, na wakati walipokuwa mbele ya chakula, mwenye kuwakaribisha kwa nyumba yake anakuwa na mtumwa wa kunawisha miguu ya mgeni, ili mugeni ajisikie katika hali nzuri na inayofaa wakati anaketi mezani kwa chakula. 

Hapa tunaona Bwana Yesu Kristo mwenyewe akitwaa kitambaa, akakifunga kiunoni mwake, akanawa miguu ya wanafunzi wake, kwa sababu hapa KRISTO ni Mtumwa anayenawa miguu ya Wanafunzi wake. 

Taswira hii inamuonesha Yeye kama mtumwa. 

Alifanya yoyote ile mtumwa angalipashwa kufanya, alitwaa kitambaa, akajifunga  kiunoni, hii inaonesha kazi za namna ya chini chini sana yenye inakuwa kwa watu wa ranga za chini zaidi,  watumwa. 

Na kwa kweli ni kazi hizo Bwana Yesu alizofanya wakati alipokamata namna ya mtu, Yeye aligeuka mtumwa na akakufa kwa Msalaba pale Kalvari kwa ajili yetu. 


4/ Kiisha Maandiko yanatuambia kwamba alifunga kifungo. 

Kwa kufahamu maandiko hii, tunapashwa kwanza kujuwa yakwamba tukichunguza  Waraka wote wa Mtume Paulo kwa waefeso, hatuta pata aya inayotupatia maelezo kamili ama tafsiri kuhusu aya hii

Katika Kigriki, maandiko haya yanamaanisha kwamba: 

YEYE ALIFUNGA KIFUNGO. 

Tena tuvumbue kutajwa kwa neno Neema katika Waefeso 4: 7


Waefeso 4: 7

“Lakini kila mtu katikati yetu alipewa neema kwa kadiri ya kipimo cha zawadi ya Kristo.” 

Kila mtu katikati yetu alipewa neema. 

Pia inasemwa “kwa hivi” na hii ingelikuwa “kwa sababu ya neno hili”   

Na inasemwa kwamba wakati alipopanda juu, alifunga kifungo.  

Wakati KRISTO alipandishwa na kutukuzwa juu sana zaidi kupita falme zote, na uwezo, akili zote na mamlaka, na juu ya kila jina linaloweza kuitwa, Alifunga kila kanuni iliyotia mwanaadamu katika utumwa.

Ilimubidi kwa kazi yake ya kiMungu, kuvunja na kuvuta  amri zile mbaya  za kutisha zilizoandikwa na zilizokuwa zikiwashitaki. 

Alizitundika kwa msalaba na hapo  alifunga kifungo na kuvunja nguvu zao zote. 

Na Alipopanda kwa Kiti Cha Ufalme wa Mungu, alizifanya kuwa hazina nguvu yoyote ile. 

Sheria inatoka kwa Kiti cha Ufalme wa Mungu, na kwa kupanda kwake juu, aliiweka kando kabisa na kwa sasa ni Neema tu ndiyo inayotenda kazi katika maisha yetu. 


5/ Kumbukeni kwamba mara kwa mara tunasisitiza na kutia mukazo kwamba sisi kwa leo tuko katika Utunzaji wa Neema, na vyote twavipata kwa Neema pekee. 

Katika matunzaji mengine watu walikuwa wakiokolewa kwa neema, lakini Yote hayakukuwa kwa Neema mtupu. 

Kwa sababu tunasoma katika Waraka wa Wagalatia kwamba sheria iliongezwa pembeni ya neema, na Mungu alivunja nguvu zote za sheria, alifunga kitu kilichokuwa kinatufunga kwa kifungo na kwa sasa ni Neema tu inayotumika maishani mwetu. 

Tumeokolewa kwa Neema tu, bila kuongeza kitu ama tendo lolote lenye mwanadamu anaweza kutarajia kufanya. 

Hakuna tena kanuni lolote juu yetu, ama sheria lolote juu yetu. 


6/ Wakolosayi 2: 4 

“akikwisha kuzima hati ile iliyoandikwa kwa kutushitaki kwa hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondosha na kuifunga kwa msalaba na misumari.” 

Kulikuwa vitu vilivyokuwa vinashika watu katika vifungo, na Bwana Yesu Kristo alivitundika kwa msalaba. 

Na wakati alipaa na kupanda mbinguni Alivunja vinyume vya hati na hukumu zote zilizokuwa na uadui kwetu. 

Ni Neema pekee tu sasa ndiyo inayotumika kati yetu. 


7/ Kiisha tunaona kwamba aliwapa watu zawadi mbalimbali. 

Aliwapa hizo zawadi, akiwa KRISTO aliye fufuka. 

Ni zawadi gani? 

Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wahubiri wa Habari Njema; na wengine kuwa wachungaji na walimu. 


8/ Muhubiri wa Habari Njema ama muinjilisti ni nani? 

Ni mwenye kubeba Habari Njema kwa wengine. 

Huduma ya muinjilisti inaelekea watu wa inje.

Wakati Mwenyezi Mungu anapatia mtu zawadi ya uinjilisti, huyu mtu anasikia ndani ya roho yake mapendo kwao wanaopotea, mapendo kwa wasioamini. 

Anamupa kipaji ya kupasha  Neno la Mungu na Nguvu  na usaafi wote. 

Ni zawadi ya mastaajabu kweli. 

Kuwa muinjilisti ni kuwa na zawadi ya mastaajabu kweli. 

Lakini sasa, siyo watu wote walio na kipaji hiki. 

Muinjilisti anatoa Neno linalokuwa na uaminifu wote ndani mwake.

Najuwa kwamba sote tayari tumekwisha kukutana na wao wanaoitwa wavuvi wa roho za watu. 

Nia yao nikushuhudia wababa na wamama kuhusu Yesu Kristo na wanakuwa na kipaji ya kuwaleta watu hawa kwake Bwana na Mwokozi Yesu Kristo.

Mimi binafsi nilikutana na watu wengi kama wale.

Ninakumbuka kijana mmoja Muhubiri katika muji wa Johnstown, mwenye nazani alikuwa na kipaji ya uinjilisti. 

Nilikuwa nikifurahia kuona namna alikuwa akileta roho za watu kwa Bwana Yesu. 

Yeye maisha yake yote ilizungukwa tu na hiyo kipaji. 

Munaweza kupatana  naye kwamba mutakutana kwa mahali fulani, lakini kama desturi yeye atafika nyuma ya saa moja ama saa moja na nusu, na ukapima kumuuliza kwa nini yeye amefika nyuma,  alikuwa tu  anakuambia umurehemu, kwa sababu yeye alikuwa na mazungumuzo na mtu moja aliyekutana naye kwa njia ama kwa nyumba ya kutengeneza nywele, ama kwa mgahawa(nyumba ya kuuzishia chakula chenye kupigwa),  na watu wenye alikua akikutana nao ni watu wenye ilikuwa tu kwa mara ya kwanza kukutana nao, alikua hajawai kukutana nao hata mara moja, lakini alikaa chini pamoja nao akiwashuhudia juu ya Kristo Yesu. 


9/ Baada ya ayo, tunasoma ya kwamba: 

Naye alitoa wengine kuwa wachungaji. 

Jina muchungaji inamaanisha mwenye kuchunga na mlinzi. 

Muchungaji mwema ni Mlinzi mwenye kutia roho yake yote juu ya kundi anayochunga katika zizi lake. 

Wakati Bwana Yesu alipo endelea mara na mara tena kuuliza Petro: “Wanipenda kuliko wote hawa?” 

Na nyuma ya haya yote Petro alikiri akisema: 

Najua kwamba upendo hauko ndani yangu. 

Bwana Yesu akamwambia: Lisha zizi langu, lisha wanakondoo wangu, linda na kulisha zizi langu, nikusema, Aliweka Petro kuwa Mchungaji wa zizi hilo. 


10/ Hapo tunafikia kiwango cha kusema kwamba muinjilisti anakuta walewasioamini, anawaleta kwa Bwana Yesu, na kwa kweli anawaleta katika kikundi cha waamini, na ni hapo Mchungaji anajifunza namna ya kuwaongoza katika majani mabichi ya Neno la Mungu anayo wapa akiwaonesha namna gani kuishi maisha yao katika kutenda Neno la Mungu,  akiwasaidia kushindana na matatizo na migorogoro ya maisha. 


11/ Tunafikia sasa Walimu. 

Tofauti gani inayokuwa kati ya Muchungaji na Mwalimu? 

Mwalimu ni mtu ule anayeweza kufungua Neno la Mungu akilisoma na kulicheuwa na kuleta ufunuo na maana mbalimbali ya muhimu sana ya maneno yenye kuzama ndani ya andiko alilolisoma.

Mwalimu anakuwa na kipaji ya kuchimbua neno na kulifafanua kwa namna ya mtu yeyote apate kulifahamu na kulisikia kwa uraisi wote.

Watu wengi wanaweza kuwa na uwezo wa kuwa Wainjilisti ama Wachungaji ama Walimu, lakini kwa binafsi, mtu huyo atakuwa amefanyikiwa sana kwa huduma yake katika moja ya zawadi hizo tatu kuliko mbili nyingine,  na tena kipaji kimoja ndicho kitainuka zaidi na kuwa na matendo zaidi kupita zingine zote. 

Yeye anaweza kuwa Mwalimu zaidi kuliko Mchungaji ama Muinjilisti. 

Ama anaweza kuwa Muinjilisti wa manufaa kabisa kuliko kuwa Mchungaji ama Mwalimu. 

Tunahakikisha kwamba vikundi hivi vimepewa kwa kanisa. 

Tufahamu vilevile kwamba zawadi za Mitume na Manabii nazo vilevile ni zawadi za Kristo aliye fufuka.  

Angalisho kwa utaratibu kuhusu namna majina haya mawili yanapangana. 

Mitume na Manabii, Paulo hakusema Manabii na Mitume, huu ni utaratibu wa Agano la Kale. 

2 Petro 3: 2 

“mupate kukumbuka maneno yaliyosemwa zamani na manabii watakatifu, na amri ya Bwana na Mwokozi iliyoletwa na mitume yenu.” 

Mutume Petro anasema hapa juu ya Manabii na Mitume, wanaomaanisha watakatifu wa Agano la Kale.

Hii haimaanishe wale kumi na wawili na Manabii wa Agano la Kale. 

Hapana hata kidogo, haya ni kwa nyakati ya Mwili wa Kristo. 

Mutume inamaanisha, anayetumwa. 

Na Nabii inamaanisha, anayetangulia kusema, hapana yeye anaye tabiri mambo yatakayokuja kesho. 


12/ Kuna kusudi la muhimu na la musingi kwa watu hawa kuwa na zawadi hizi mbalimbali katika Mwili wa Kristo. 

Sawa vile watu wanavyojua: 

Katika Biblia Takatifu, uwekaji wa vituo vya uandishi haukupanwa kwa maongozi ya Mungu. 

Kwa mara yanasaidiya na mara hayasaidiye. 

Kwa kesi tunayo, haisaidiye.  

Tunapo ondoa “mkato” katika aya hii ya kumi na mbili, hapo tunapata maelezo na maana kamili. 

Naye alitowa wengine kuwa mitume; na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wahubiri wa Habari Njema; na wengine kuwa wachungaji na walimu; 

Kwa kusudi ya kukamilisha watakatifu kwa kazi ya utumishi hata Mwili wa Kristo ujengwe. 

Kuna kusudi la muhimu na la musingi kwa zawadi hizo kupewa kwa Kanisa Mwili wa Kristo. 

Neno kukamilisha haimaanishe kugeuka kuwa pasipo kosa lakini inamaanisha KUTAYARISHA ama KUPATIA VIFAA. 


13/ Zawadi hizo ni kwa ajili ya kupatia taifa la Bwana vifaa kwa kazi ya Bwana, taifa hilo ni mukusanyiko ya waamini wote wa kanisa la fasi, wale walioamini Bwana Yesu kama Bwana na Mwokozi wao. 


14/ Tunafahamu ya kwamba zawadi hizo zinatolewa kwa Kanisa Mwili wa Kristo kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu na kupanua kazi ya Bwana kwa kuhimiza na kujenga Mwili wa Kristo kwa kazi ya Bwana ili Kanisa lipanuke.  

Ni vizuri gani kama tungelikuwa na watakatifu wanaokaa kwa mimbari ama viti vya kanisa kwa kujiweka tayari kwa kazi ya Bwana.

Kama wasema kwamba umeamini Bwana Yesu na wewe haufanyi kazi yoyote kanisani, wewe unakuwa kikwazo kwa malaika wa Bwana,  na jambo la sifa na furaha kwa mapepo wa giza. 

Kwa sababu tulipokea zawadi mbalimbali ili sisi kwa nafasi ya KRISTO tupate kusihi watu ili kuwapatanisha na Mungu. 

2 Wakorinto 5: 17 

“Hivi kama mtu akiwa ndani ya Kristo, yeye ni kiumbe kipya; maneno ya zamani yamepita; tazama, maneno yote yamekuwa mapya.” 

15/ Zamani nilijuwa kijana moja aliyekuwa mwanamemba wa kanisa letu, lakini kwa sasa yeye anakuwa Mchungaji. 

Siku moja nilikuwa nikihubiri katika kanisa lake na wakati nilipofika mwisho wa mahubiri, alikuja kwangu na kuniuliza, je inaweza kuwa shida kwako kama mimi nikitumikisha mahubiri hii wakati ninapohubiri watu wengine? Nikamujibu, hapana hata kidogo, kwangu itakuwajambo la furaha kuona kwamba unatumia mahubiri hii. 

Naye akaongeza akisema:   kwa jumaa hii nitatoa Neno kwa mukusanyiko ya Watumishi. 

Pia akasema tena: Sioni sababu gani ninakuuliza, kwa sababu tayari nimekwisha kutumikisha mahubiri yako mara nyingi sana wakati ninatoa neno hapa kanisani.

Nikamujibu: Kama neno lolote linagonga sana moyo wako na kukuletea burudani na wewe pia unkusudia kuileta kwa mtu mwengine ili abarikiwe kiroho, sioni hata tatizo moja kwa tendo lile, bali nitamtukuza Bwana Mungu wetu. 

Na kwamba, kama kwa njia ya neno lile, mtu anakiri na kupokea Bwana Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wake, wewe utakuwa baba yake wa kiroho na mimi nitakuwa tate yake. 

Kama ingelikuwa kundi lote la waamini wanajiweka pamoja na kusimama ili kutenda kazi ya Mungu, kwani najua kwa kweli kwamba kanisa la nafasi inakuwa ya manufaa kabisa mbele ya mecho ya Mungu, nivizuri sana watu wote kujitoa kwa kuhudumia Mungu. 

Hakuna Mchungaji anaye weza kutimiza huduma huu pekeyake.

Hata kundi ya Wachungaji haiwezi lolote pekeyao. 

16/ 1Wakorinto 1: 10  

“Basi ninawasihi ninyi, ndugu, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, ya kwamba ninyi wote museme neno moja, na matengano yasiwe katikati yenu; lakini mwungane katika nia moja na shauri moja.” 

Hapa tunaona upumbafu wa kutokutumika pamoja. 

Ujinga wa kutokupanga kazi. 

Kanisa la Korinto lilikuwa katika mikorogano sababu kila mtu alikuwa akijifungia kwa upande wake, akisongana tu na kuangalia kazi yake mwenyewe pahali pa kujioa wote pamoja kwa kazi ya Bwana. 

Watakatifu wenye wanaojitoa kwa kazi ya Bwana hawana iyo saa ya kubaguwa wengine kwa kuwatia kando kwa kazi. 

Yawezekana unaweza kuchanganyikiwa na kuhuzunishwa kupitia mwamini moja anayekuwa sawa mutakatifu wa Mungu. 

Waweza kufwata mufano wa marehemu Mutumishi Billy Sunday. 

Yeye alikua aki kosolewa na kurejeshwa mara kwa mara na wale wanaokuwa sawa watakatifu kupita watu wote, juu ya namna yake ya kuhubiri. 

Hivi akawauliza wale watakatifu: 

“Kama hamufurahie namna yangu ya kuhubiri, muniambie ninyi munahubiri namna gani?” 

Na jibu ilikuwa: “Sisi hatujawai bado kuhubiri.” 

Hivyo Mchungaji Billy Sunday akawaambia: 

“Mimi ninafurahia namna yangu ya kuhubiri zaidi ya namna yenu.” 


17/ Ni vizuri kujitoa sana kwa yale Mwenyezi Mungu anatarajia kwako. 

Wajibu wako wa maana katika maisha yako ni kutangaza na kupanua kazi kwa kuhudumia katika Shamba la Bwana. 

Wewe hauko pale juu ya kununua manyumba, viwanja ama vifaa. 

Hauko pale ili ujaze mali kwenye banki yako. 

Mwizi wakati anakutokea anakuambia uchague kati ya pesa na uzima wako, 

Lakini Mungu anakuomba zaidi. 

Anasema: Mali yako Na Uzima yako. 

Kama Mungu hakutumie wewe, yawezekana ni wewe ndiwe hautapenda kumuruhusu. 

Sababu gani Mwenyezi Mungu alikuwa akitumikisha sana makanisa ya Makedonia? 

Nitawaambia sababu gani. 

Ni kwa sababu wao wenyewe walijitoa kwanza wenyewe kwake. 

1 Wakorinto 8: 5 

“Kwa maana hata wakiwa walioitwa miungu, ama katika mbingu au katika dunia, kama ni miungu mingi na bwana wengi.” 

18/ Neno hili litadumu hata lini? 

Ninaweza kuwajibu. 

Waefeso 4: 13 

“hata sisi sote tufikie umoja wa imani, na kujua sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mzima, hata kufika kipimo cha urefu wa utimilifu wa Kristo;” 

Hii inamaanisha nini? 

Inamaanisha wakati Kanisa Mwili wa Kristo itakusanyika pale Mbinguni ikizunguuka Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, hapo KRISTO atafunuliwa kwetu sisi wote. 

Kwa sababu hapa chini duniani bado tungali tunasemasema chini chini bila ufahamu kabisa kuhusu utimilifu wa Kristo. 

Ndani ya Waefeso 1: 23, tunasoma ya kwamba: 

“lililo Mwili wake, utimilifu wake  anayetimiza vyote katika vyote.” 

KRISTO ni Kichwa cha Mwili, akiwa kule juu mbinguni ndani ya Utukufu wake; na sisi Waaminifu ni Viungo vya Mwili wake, basi Yeye hatimiliki bila sisi, na sisi hatutimiliki bila YEYE.

Bali, tutafikia Utimilifu wa KRISTO wakati tutafika mbinguni tukiwa pamoja NAYE. 


AMINA

 

N°Ref: 05/01/1960  220 - DID CHRIST DESCENDED INTO HELL / 08/30/2020

No comments:

Post a Comment