Tuesday, July 28, 2020

JE UMEKWISHA KUKUTANA NA NEEMA? HAVE YOU MET GRACE?

Photo taken by B Smith from the Patio



  

 

JE UMEKWISHA KUKUTANA NA NEEMA? 

HAVE YOU MET GRACE? 

Januari 6, 1980

Pastor Henry F. KULP





 

Waroma 5: 20, 21 

“Lakini sheria iliingia, ili zambi ziwe kubwa sana; lakini pahali zambi zilipozidi, neema ilizidi zaidi sana: 

hata, kama vile zambi ilivyotawala katika kufa, hivi kwa njia ya haki neema itawale hata uzima wa milele kwa Yesu Kristo Bwana wetu.” 

Hapa kweli, tuna neno moja la muhimu sana.

Neno lile ni, neno “Neema”, inayomaanisha “vyote kwa bure pasipo malipo”. 

Lakini utunzaji huu wa neema unakuwa, kwa wengi wa watu, nguvu kufahamu, ni wachache sana wanawoishi maisha yao wakiwa chini ya neema ya Mungu. 


1/ Katika vitabu 39 ya Agano la Kale, tunakuta tu aya mbili inayozungumuza juu ya neema ya Mungu kwa wanadamu. 

Katika vitabu ine vya Injili, neno “neema”, haipatikane katika kitabu cha Matayo, ama Marko, neno neema inapatikana mara moja tu ndani ya kitabu cha Luka, mara tatu ndani ya sura ya kwanza ya kitabu cha Yoane. 

Mara mia moja makumi mawili na nane (128) katika Agano Jipya nzima, lakini Mutume Paulo, yeye mwenyewe, anatumia neno “neema”, mara mia moja na tatu (103); hii inamaanisha kwamba, inje ya Mutume Paulo, neno “neema” imetumikishwa tu mara makumi mbili na tano (25) katika Agano Jipya. 

 

2/ Eti wewe bado kutambua kwamba Vitabu vyote vilivyoandikwa na Mutume Paulo, vinaanzishwa vikitaja neno “neema”, kwa mwanzo wa kitabu,  na vinafungwa vilevile  vikitamka neno “neema”, kwa mwisho wa kitabu.

Tutizame kwanza katika kitabu maali tunaposoma maandiko yetu tunayo jifunza kwa sasa. 

Waroma 1: 7  

“kwa wote walio kwa Roma, wapenzi wa Mungu walioitwa kuwa watakatifu: 

Neema iwe kwenu na salama kutoka kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana yetu Yesu Kristo.” 

Kiisha pale tuone kwamba Waroma 16: 24 inasema: 

“Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe pamoja nanyi wote. Amina.” 

Kiisha, 

1Wakorinto 1: 3 

“Neema kwenu, na salama toka Mungu Baba wetu, na kwa Bwana Yesu Kristo.” 

1Wakorinto 16: 23 

“Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe pamoja nanyi.” 

Pia tuone kwamba, 

2Wakorinto 1: 2 

“Neema iwe kwenu na salama toka Mungu Baba wetu na Bwana Yesu Kristo.”  



2Wakorinto 13: 14 

“Neema ya Bwana Yesu Kristo, na mapendo ya Mungu, na ushirika wa Roho Mutakatifu ukae pamoja nanyi wote.” 

Na vivi hivi, ni katika hali hii ndiyo Vibarua vya Mutume Paulo vinavyo kuwa. 

Hii inanishuhudia kwa kweli kwamba ni Mutume Paulo aliye Mujumbe na muhubiri wa Neema ya Mungu. Ujumbe wake wote ni neema na neema mtupu katika yote. 


3/ 1Wakorinto 15: 10 

“Lakini kwa sababu ya neema ya Mungu nimekuwa sawasawa nilivyo: 

Na neema yake niliyopewa haikuwa bure; lakini nilizidi sana kufanya kazi kupita wao wote: wala si mimi, lakini neema ya Mungu iliyokuwa pamoja nami.” 

Hapa Mutume Paulo anatuelezea nini ilitukia katika maisha yake. 

Anasema kwamba: kwa sababu ya neema ya Mungu nimekuwa sawasawa nilivyo: na neema yake niliyopewa haikuwa bure. 

Ni neema ya Mungu iliyobadirisha namna alivyokuwa akiishi, pia ni neema iliyo musukuma kufanya kazi nyingi. 


4/ Waefeso 3: 1 – 3 

“Kwa sababu hii mimi Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu kwa ajili yenu ninyi Mataifa, 

Ikiwa mumesikia habari za uwakili ya neema ile ya Mungu niliyopewa kwa ajili yenu; 

Ya kwamba kwa ufunuo nilijulishwa siri hii, kama nilivyoandika mbele kwa maneno machache.”  

Hii ni Utunzaji wa Neema ya Mungu. 

Ni mafundisho ya Neema mtupu, neema tu. 


5/ Waroma 11: 6 

“Lakini ikiwa kwa neema yake, haiko kwa matendo tena, au neema isingekuwa neema; na ikiwa kwa matendo, haiko neema tena; au matendo yasingekuwa matendo.” 

Tunaona na kuhakikisha hapa kwamba Neema na matendo haitembee pamoja.  

Yote inayokuwa ya neema, haina matendo ndani yake. 

Ukajaribu kuongeza tu neno moja juu ya neema, hauna tena neema. 


6/ Basi niwaoneshe neno moja la muhimu sana kuhusu neema. 

2Wakorinto 8: 6 - 7  

“Hata tulionya Tito, ya kwamba kama alivyoanzisha hivi atimize ndani yenu neema hii vilevile. 

Basi kama munavyozidi katika mambo yote, kwa imani, kwa usemi, kwa elimu, kwa bidii yote na kwa mapendo yenu kwetu, basi muzidi katika neema hii vilevile.” 

Hapo Mwenyezi Mungu anasema: 

Wakati mtu anatoa toleo, ama sadaka kwa Mungu, ni kwa njia ya neema ndiyo watu wanatolea Mungu. 

Ni kusema kwambo, kinacho sukuma mtu kutowa sadaka, ni neema yake Mungu inayotenda kazi katika maisha ya mwenye kutoa na ni hii neema inayo musukuma kwa kutowa. 

Watu kwa desturi ya kimtu wanapenda tu kupokea. 

Kila saa na kila nyakati wanapenda tu wapate kitu kingine, lakini wao walio katika Yesu Kristo, wao wanakuwa na viumbe vipya, wao wanafurahia kutolea wengine, na wanapofanya hivi, tendo lile linaitwa neema. 

Ni kusema kwamba: 

Wao wanapotolea wengine, si kwamba wanangojea matukio ya kwamba nao vilevile wapewe sababu walitowa kwa wengine, ni kusema kwamba, vyote ni bure pasipo malipo. 

Lakini tena, wao wanapotelea Mungu, wanaifanya kwa kadiri ya mapato yao, kwa kufwatano na hayo wao wanauwezo ya kutolea Mwenyezi Mungu. 

Wangapi katikati yetu wanaosema kwamba tangia wakati mimi nilianza kutolea Mungu, mimi sina tena shida yoyote. 

Hiyo siyo shabaa yetu kwa kutolea Mungu. 

Tunatolea Mungu wetu kwa njia ya neema. 


7/ Waroma 5: 20 

“lakini sheria iliingia, ili zambi ziwe kubwa sana; lakini pahali zambi zilipozidi, neema ilizidi zaidi sana:” 

Sasa, hiyo inasema kwamba: 

Mahali zambi zilipozidi, neema ilizidi zaidi sana. 

Neema inayozidi. 

Neema inayozidi zaidi sana. Neema inayotiririka. 

Mutume Paulo hasemi kwamba, mahali zambi inapokomaa, ama kuzidi, neema itatolewa kwa kadiri ya uwingi wa zambi. 

Yeye anasema kama kuna kiwango cha neema kubwa zaidi, neema inayozidi zaidi sana kupita hiyo zambi zote, sababu anatumia maneno karibuni kumi katika luga ya Kigriki ili amaanishe neno kuzidi. 


8/ SABABU GANI MWENYEZI MUNGU ANAKUWA NA NEEMA KWA WANADAMU WOTE? 

Eti Biblia inatufunulia shabaa ya Neema ya Mungu? 

Kweli kweli Biblia inatufunulia mambo yale. 

Tuangalie kwanza na tukamate neno mbili kubwa ya humimu tunayoyapata katika Biblia. 

Mapendo na Neema

Yoane 3: 16 

“Kwa maana Mungu alivyopenda ulimwengu, hata kutoa Mwana wake wa pekee, ili kila mutu akimwamini asipotee, lakini apate uzima wa milele.” 

Tuone namna Mungu alivyopenda ulimwengu.

Nikusema, Mungu aliupenda ulimwengu kwa namna ya kuzidi, akamtoa Mwana wake wa pekee, na hapo tunafundishwa kusudi la Mapendo ya kuzidi ya Mwenyezi Mungu.  

Ni ya ngambo mbili, inasehemu mbili. 

Kwanza mtu asihaibike, asipotee na pili, mtu apate uzima wa milele.

Ni kusema kwamba faida hizo ni kwa yule anayeokolewa, lakini vilevile inakuwa tayari kwa niaba ya yule mtu bado kuokolewa. Huyu mtu asihaibike, lakini awe na uzima wa milele.  

Mtu mwenye zambi anapokuja kwa Bwana wetu Yesu Kristo, akimuamini kama Bwana na Mwokozi wake, kiisha hapo anavumbua shabaa ya Neema ya Mungu, yeye atasema moyoni mwake: 

Mwenyezi Mungu hakupenda mimi nihaibike. 

Mwenyezi Mungu anapenda mimi niwe na Uzima wa milele. 

Na Mungu alitayarisha yote sababu ya jambo lile.

Alitayarisha wokovu kwa njia ya Neema yake. 


9/ Tuchunguze sasa shabaa ya pili ya neema ya Mungu inayozidi sana. 

Waefeso 2: 8 – 10 

“Kwa maana mumeokolewa kwa neema kwa njia ya imani, wala neno hili halikutoka ndani yenu wenyewe, ni zawadi ya Mungu, 

Si kwa matendo, asiwe mtu atakayejisifu,

Maana sisi ni kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu ili tutende matendo mema Mungu aliyotengeneza mbele ili tutembee ndani yao.” 

Hapo tunasoma ya kwamba: 

Kwa maana tumeokolewa kwa neema kwa njia ya imani, kiisha tunashuka kwa aya ya kumi inayosema: 

Tuliumbwa katika Kristo Yesu ili tutende matendo mema Mungu aliyoyatengeneza mbele ili tutembee ndani yao. 

Moja ya shabaa ya neema ya Mungu, ilikuwa kwa sababu Mwenyezi Mungu apate kuokoa nafsi zetu, pia shabaa ya pili ni kwamba kiisha kuokolewa tupate kutenda matendo mema yanayoweza kumutukuza Mungu. 

Hapo, tunataka kufunua neno moja la muhimu kuusu neema ya Mungu katika wokovu.  

Hakuna mutu mwenye anapokea neema ya Mungu, nyingi sana kupita mwengine. 

Sote tumeokolewa na kiwango kimoja cha neema ndani ya Bwana wetu Yesu Kristo. 

Mwenyezi Mungu haambie huyu mtu mutenda zambi sana na mukaidi na muzalimu kwamba namna wewe ni muovu sana, itanipasa nichukuwe sehemu kubwa ya chini ya pipa ya neema ili nikutibu. 

Pia haambie mutu mwengine anayekuwa na maisha ya kawaida, kwamba, wewe unaishi kawaida tu na kwa hiyo, kwa wewe nitachukuwa tu kiwango cha kawaida ya neema ili nikutibu. 

Na pia Mwenyezi Mungu haambie huyu mutu wa tatu kwamba wewe unazamiri safi sana, unaishi maisha ya kujizuiza kweli kwa hali ya juu, hata majirani wako wanakushuhudia vema, wenzako wa kazi na marafiki wote wanakushuhudia vizuri na sasa kwa niaba yako nitakamata tu kipimo ya neema inayo ingia katika kijiko moja ama koleo ili nikutibu. 

Neema ya Mungu haijali uwe mwenye zambi wa aina ya kwanza, aina ya pili, ama aina ya tatu, na zaidi ya hayo tunavumbua kwamba Mwenyezi Mungu anapatia mwamini neema zaidi. 

Mwenyezi Mungu anatupatia sote kiwango kimoja cha neema katika wokovu wetu, lakini anatupatia neema zaidi katika maisha yetu ya kila siku, katika kazi tunazozifanya, na katika huduma zetu. 

Yakobo 4: 6  

“Lakini anatupa sisi neema nyingi zaidi; basi maandiko yanasema: Mungu anashindana na wenye kiburi, lakini anawapa neema wanyenyekevu.” 

Basi mutii Mungu, 


Yakobo anasema: anatupa sisi neema nyingi zaidi.

Kuna neema inayotufanya kutenda matendo mazuri. 


10/ Tuchunguze vema neno “matendo” yenye inatamkwa mara mbili katika maandiko ya Waefeso 2: 9 

“Si kwa matendo, asiwe mtu atakayejisifu.” 

Matendo yamelaaniwa kwani yametendwa na uwezo wa mwili, yametimizwa na mtu wa zamani akiwa na kusudi ya kulipa malipo juu ya wokovu. 

Katika Waefeso 2: 10 

“Maana sisi ni kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu ili tutende matendo mema Mungu aliyotengeneza mbele ili tutembee ndani yao.” 

Na Mungu hapo anatufunulia kwamba, matendo mema inayotukia katika maisha yetu ni moja ya shabaa ya neema inayozidi, katika wokovu wa mwenye zambi. 


11/ Tutambue kwamba  aya ya kumi (10) inasema: 

 Sisi ni kazi yake. 

Tutambue na kufahamu kwamba ni Mwenyezi Mungu njo mutenda kazi wa matendo mazuri ndani yetu kwa njia ya neema yake. 

Tendo hili ni kwa wale tu walioumbwa upya katika Kristo Yesu. 

Hatuokolewi sababu ya kuepuka uchungu na mateso ya mauti ya pili, ama jehenamu, ama kufa ya milele, lakini ili tutende matendo mema. 

Maneno haya tumeyafundishwa mara tena katika kitabu cha Tito 2: 14 

Tito 2: 14   

“ambaye alijitowa mwenyewe kwa ajili yetu atukomboe toka uovu wote, na kujisafishia watu wawe mali yake mwenyewe, wenye bidii sana katika kazi njema.” 

12/ Tuone sasa shabaa ya tatu ya neema ya Mungu inayozidi sana. 

Waefeso 3: 10  

“ili sasa, kwa njia ya kanisa, hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi ijulishwe na falme na mamlaka katika pahali pa mbingu;” 

Tunaweza semezana mengi sana na kwa muda murefu kuusu andiko hili, lakini kwa ufupi tuone kwamba inamaanisha nini: 

Mwenyezi Mungu katika muumbo wake wa kwanza, aliumba majeshi ya wa malaika. 

Wao ndio falme na mamlaka katika pahali pa mbingu kwa sasa. 

Kundi moja ya tatu ya ile jeshi ya wa malaika ilitomboka na kuzani kujiinua wafananishwe na Mwenyezi Mungu. 

Isaya 14: 14 

“Nitapanda juu kupita virefu vya mawingu, nitafanana na Mjuu Sana.” 

Alipenda ageuke kuwa Makerubi aliye juu kupita. 

Alipenda afikie kwa nafasi ya Bwana Yesu Kristo, na aliitafuta  kwa uwezo wake mwenyewe, kwa nguvu zake mwenyewe, lakini sasa Mwenyezi Mungu iko anawaondowa watu wenye zambi katika ulimwengu, watu wenye wako chini  sana ya malaika,  kanisa, mwili, na atawafanya kuwa kile Yeye Mwenyewa alikusudia wageuke kuwa kutoka jeshi lile lililo anguka na kutupwa chini duniani. Na siyo kwa uhuru wetu, ama kwa matendo yetu, lakini kwa utegemezi na kutegemea tu neema ya Mungu peke yake. 

Kwa kweli, yale majeshi ya malaika wenye hawakushushwa huku chini duniani, wale wamalaika waliobakia juu mbinguni wakiwa waaminifu kwa Mungu, wamalaika wale hawafahamu hata neno juu ya Neema ya Mungu, tangu kutangwazwa kwake na kuanza kutumishwa kwake,  na ni kwa sababu ile  wamalaika wanatutazama na kujifunza kwetu, na sisi tunakuwa walimu wao tukiwafundisha juu ya neema siku kwa siku. 


13/ Kwa hiyo, sababu ya tatu ya shabaa ya neema ya Mungu inayozidi sana ni kwa sababu tuoneshe wamalaika namna gani Mungu anatumika na mwanadamu kwa upekee. 


14/ Shabaa ya ine ya neema ya Mungu inayozidi sana tutaipata katika maandiko ya Waefeso 1: 23 

“lililo mwili wake, utimilifu wake anayetimiza vyote katika vyote.” 

Hii ni andiko kweli la kutushangaza sana. 

Inatumia msemwa, utimilifu ndani ya KRISTO, kweli wazo gani iko hapa? 

Mungu alimufanya KRISTO awe Kichwa cha Kanisa iliyo Mwili wake, utimilifu wake anayetimiza vyote katika vyote. 

Utimilifu wa KRISTO unamaanisha nini? 

Yeye Kristo, haiko Mungu kamili?  La!, Yeye ni MUNGU Kamili. 

Tufahamu kwamba Waefeso 1: 22, 23 



Waefeso 1: 22, 23 

“na ameweka vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe Kichwa juu ya vitu vyote kwa kanisa 

Lililo Mwili wake, utimilifu wake anayetimiza vyote katika vyote.” 

Kristo ndiye Kichwa cha Mwili. 

Sisi ni viungo vya huo Mwili; na kichwa pekee bila mwili, hakitimilike. 

Kitu cha mastaajabu ni kwamba Kanisa, Mwili wa Kristo ndilo Utimilifu wa KRISTO. 

Siku moja inayokuja Mwili itakuwa pamoja na Kichwa katika Utukufu; lakini kwa leo, Mwili iko hapa duniani na Kichwa iko mbinguni. 

Ni mambo ya ajabu sana kutambua kwamba KRISTO haiko timilifu bila sisi. 

Fikili kwanza ndugu yangu, hapo kale sisi tulikuwa wenye zambi, wapotevu, tukitengwa na Mwenyezi Mungu, hatukukuwa na tumaini lolote, tukiwa tu tunastahili hukumu ya Mungu, na sasa kupitia neema yake tuliokolewa, tukageuka kuwa viungo vya Mwili wake, Mwili wa KRISTO, na hilo ni Utimilifu wa KRISTO. 

Uwajibu gani tunalo lakutupasa kutenda matendo mema sababu sisi ni kiungo cha KRISTO. 


15/ SEHEMU HII INAPATIKANA CHINI YA SHABAA YA KWANZA YA NEEMA YA MUNGU INAYOZIDI.  

Waefeso 1: 6  

“na kwa sifa ya utukufu wa neema yake ambayo alitupa sisi katika huyu Mpendwa.” 

Mwanadamu hana aja kujisifu hata kidogo. 

Ni yeye mwenyewe aliyetupatia kukubaliwa ndani ya Mpendwa. 

Kumbukeni kwamba neema inamaanisha, yote kwa bure pasipo malipo, sisi alitupatia tukubaliwe kwa mecho ya Mungu Baba kwa Neema katika Kristo Yesu. 


16/ Jameni niwape mfano kuusu maneno ninayotaka kusema: 

Munakumbuka huyo mwanamuke aliye penda kuuwa Malkia Elizabeth 1. 

Huyo mwanamuke alijivika nguo za kinaume na kujificha ndani ya chumba cha mapumuziko cha Malkia akingojea saa Malkia itajiingiza humo ili amuchomeke kisu mpaka kumuua. 

Mwanamuke huyu hakukumbuka kwamba walinzi wa Malkia wanapashwa kwanza kujitahidi kupekua chumba nzima na nafasi yote na kuhakikisha kwamba hakuna hatari yoyote, mbele ya kuruhusu Malkia kuingia ndani. 

Akiwa akijificha nyuma ya kanzu la kuoga, na mavazi marefu, walinzi walimufichua, wakamnyanganya mupanga aliokuwa nawo mikononi na wakamubeba mbele ya Malkia. 

Alipofika, alitambua kwamba hakuna tena kitu cha kufanya ni malipizi makali tu analostahili. 

Hivi akajitupa kwa magoti mbele ya Malkia na kuomboleza na kumlilia akisema: wewe kama mwanamuke, unihue razi na kunihurumia sana kwa kunipa neema kutoka kwako. 

Malkia akamwangalia vizuri tena akakamata muda wa kumutizama na kumuchunguza kwa makini sana, kiisha akumuuliza huyu mwanamuke mwenye alitaka kumuuwa, akisema: 

“kama nikakupatia neema, ahadi gani unalo niagiza utakalo fanya kwa siku za usoni?” 

Huyu mwanamuke akaangalia juu kiiasha akamjibu Malkia: 

“Neema inayokuwa na ma sharti, hiyo siyo neema, siyo neema hata kidogo.” 

Malkia akafahamu maana ya jibu ya mwanamuke huyo, kwa hiyo Malkia akamwambia: 

“Mwanamuke, wewe ni huru sasa” 

Historia inatuambia kwamba tangu siku ile Malkia Elizabrth 1, hakuwa na mtumishi mwaminifu, anayejitoa sana sawa yule mwanamuke mwenye alikuwa kwa mwanzo akijitayarisha ili aondoe uzima wa Malkia Elizabeth 1 kwa kumuua kwa upanga. 


17/ Tunafika sasa kwa shabaa ya tano ya neema ya Mungu inayozidi, tena kumbuka namba tano ndiyo namba ya neema.

   Waefeso 2: 6, 7 

“na alitufufua pamoja naye na kutukalisha pamoja naye katika pahali pa mbingu, katika Kristo Yesu; 

Hata katika nyakati za kuja aonyeshe wingi wa kupita kiasi wa neema yake kwa wema wake kwetu katika Kristo Yesu;”  

Tufahamu sana shabaa yenye iko katika aya ya nane (8) 

“kwa maana mumeokolewa kwa neema kwa njia ya imani, wala neno hili halikutoka ndani yenu wenyewe, ni zawadi ya Mungu,” 

Na unaweza kuanza kujisumbuasumbua wewe pekee na kusema iyo mambo inahusu tu wokovu. 

Kweli mumeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani, lakini kuna mazoezi kidogo inayoombwa kwenu, hiyo ya kutambua kwamba aya hii, inaanza na neno moja fupi na ndogo, ni neno “kwa maana”. 

Kwa maana mumeokolewa kwa neema, hiyo inarudisha mafikili yetu kwa aya 6 na 7. 

Hivi basi nitawasomea aya hizo nikipima kuyatafsiri kwa ajili yenu: 

NA AKITUFUFUA PAMOJA NA KUTAKALISHA NDANI YA YESU KATIKA MAHALI PA MBINGU. 

KATIKA NYAKATI ITAKAO KUJA ATATUONESHA UTAJIRI WA MAARUFU, UTAJIRI UNAOPITA KIASI SANA, UTAJIRI WA WINGI WAKUPITA KIASI WA NEEMA YAKE KATIKA WEMA WAKE KWETU NDANI YA YESU KRISTO KWA MAANA TUMEOKOLEWA KWA NEEMA. 


18/ Wazo hapa ni kwamba mumeokolewa ili muonyeshe utajiri wa maarufu, utajiri wa kupita kiasi sana wa neema ya Mungu kwa wale wakaaji wa mbinguni. 

Siyo tu kwamba tumeokolewa kwa neema, lakini kweli, hiyo ndiyo ukomo wa wokovu wetu. Ni hiyo shabaa ya tano tena ya mwisho ya neema ya Mungu inayozidi. 


19/ Sinawofu ya kwamba katika nyakati zijazo, inawezekana iwe miaka bilioni inayokuja, tukihesabu tangu leo, wamalaika wanao angalia wewe na mimi na woga, wakishangaa na kututamani, watazungumuza wao kwa wao wakijiuliza na kusema: hawa ni wawili wa watakatifu, walikuwa ndani ya dunia katika hali ya uasi, walikuwa katika muda wa machafuko na zambi. 

Wao walikuwa watendazambi, mbali na Mungu, walikuwa adui wa Mungu, lakini Yeye aliwapenda na wao wangali bado katika hali hiyo, na Mapendo yake iliwafikia kupitia Kifo cha Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo na walimuamini Yesu Kristo na kufanywa kuwa watakatifu. 

Alitimiza na kufanya haya yote kwa ajili yao. 

Na sisi tutajibu wamalaika tukiwaambia: 

Kweli mulimusujudu na kumuabudu kwa sababu anastahili kusujudiwa. 

Yeye pekee ni wa Mastaajabu sana. 

Yeye tu anajaa wingi wa Neema. 

Hakuna hata mumoja kama Yeye. 

Ndiyo maana kwenye zambi ilizidi, neema ilizidi sana.      

Amina 


N°Ref: 01/06/1980 / 526 (DOC 319) HAVE YOU MET GRACE / 07/28/2020

No comments:

Post a Comment