Thursday, January 16, 2020

KWA NINI MUTUME PAULO ALIKUWA GEREZANI / WHY WAS PAUL IN PRISON



Photo taken from our kitchen window










     KWA NINI MUTUME PAULO ALIKUWA GEREZANI 
     WHY WAS PAUL IN PRISON 
     Pastor Henry F. Kulp
     January 24, 1960






Waefeso 3: 1-10 

“Kwa sababu hii mimi Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu kwa ajili yenu ninyi mataifa, 
ikiwa mumesikia habari za uwakili wa neema ile ya Mungu niliyopewa kwa ajili yenu; 
ya kwamba kwa ufunuo nilijulishwa siri hii, kama nilivyoandika mbele kwa maneno machache. 

Kwa maneno haya, wakati munaposoma munaweza kutambuwa ufahamu wangu katika siri ya Kristo. 

Siri hii haikujulikana kwa wana wa watu katika vizazi vingine, kama ilivyofunuliwa sasa kwa mitume yake watakatifu na manabii katika Roho; ya kwamba Mataifa ni wariti pamoja nasi wa uriti mmoja, na wa mwili mmoja, na washiriki pamoja nasi wa ahadi hii katika Kristo Yesu kwa njia ya Habari Njema. 

Nilifanywa muhubiri wa Habari Njema hii, kwa kadiri ya zawadi ya neema ile ya Mungu niliyopewa kwa kadiri ya utendaji wa uwezo wake. 

Mimi, niliye mdogo kuliko yeye mdogo wa watakatifu wote nilipewa neema hii  ya kuhubiri Mataifa utajiri wa Kristo usiotafutikana; na kuangazia watu wote wajue habari za madaraka ya siri iliyofichwa tangu zamani ndani ya Mungu aliyeumba vitu vyote; 
ili sasa, kwa njia ya kanisa, hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi ijulishwe na falme na mamlaka katika pahali pa mbingu;”  
Hapa katika kitabu cha Waefeso, mutume Paulo iko anatuzungumuzia Jengo ambalo Mungu Baba iko anajenga. 

Hekalu lenye iko anajenga kwa kupitia kazi ya Roho Mutakatifu. 

Mutume Paulo alituambia ya kwamba katika siku za kale, Baba Mungu alichaguwa kutumika na taifa la wana wa Israeli na kulikuwa kibambazi ya uadui katikati yao na mataifa zingine walioitwa wapagani, wasiojuwa Mungu wala hawakuwa na Mungu. 
Wala hawakuwasiliana na Mungu kwa sababu Yeye alikuwa anawasiliana tu na taifa la Israeli. 

Kiisha Paulo aliwaambia ya kwamba Mungu alibomoa kiambaza hicho cha uadui na matengano, aliibomoa kupitia Yesu Kristo. 

Sasa kwa leo, paali ya kuwasiliana tu na taifa moja tu, kwa leo Baba Mungu anawasiliana na mataifa yote ya ulimwengu.  

Mungu anawasiliana na kila mutu anayekuja kwake kwa njia ya Kristo Yesu. 

Na huyo mutu anakuwa jiwe la uzima katika Jengo hilo Mupya linalokuwa Kao la Mungu. 

1/ Sasa ndani ya sura ya tatu ya kitabu cha Waefeso, Mutume Paulo anasema kwamba angelitamani mujuwe namna gani alifikia kupata na kujulishwa Injili hii. Namuna gani alifikia kujulishwa na kuwa na ufahamu ya kweli hii, ni hapo anasema kama yeye aliijulishwa katika ufunuo (haya yake ya tatu).   

Juma jana, tulijishurtisha na  tulichukuwa muda ya kuwaonesha ya kwamba Injili hii aliijulishwa katika ufunuo akiwa uso kwa uso, na ana kwa ana, akiijulishwa na Mwokozi wetu Yesu Kristo Yeye mwenyewe uso kwa uso. 

Mutume Paulo hakuipata toka mutume Petro, ama Yakobo ama mutume mwengine. Yeye hakuipata toka kwa mitume kumi na wawili wa Bwana Yesu, wala hakuijifundisha toka mafundisho ya Agano la Kale, hii Injili ni kitu kipya chenye Mutume Paulo alipashwa funulia wanaadamu. 

2/ Ni ya muhimu na samani sana tujuwe na kufahamu kwamba Injili hii iko umbalimbali na habari njema yoyote katika Biblia. 

3/ Injili hii ama Habari Njema hii ni gani? 

Waefeso 3: 6 inayosema 

“ya kwamba Wayuda na Mataifa  watakuwa sasa ndani ya Mwili Mumoja,” hakuta kuwa tena kundi moja yenye itakuwa inapendelewa, hii ni jambo kubwa inayo itwa Injili ya  wasio tahiriwa. 

Tungeliuliza kama hiyo ndiyo Habari Njema iliyo hubiriwa na mitume kumi na miwili wa Bwana Yesu, jibu ni hapana, hii ni Habari Njema tafauti ni ile. 

Tuangalie hakikisho ya neno ili. 

4/ Mbele ya yote tujuwe kwa makini kwamba hii Habari njema siyo habari njema yenye Bwana wetu Yesu Kristo alikuwa anahubiri. 

Waroma 15: 8 

“Kwa sababu ninasema ya kwamba Yesu Kristo alikuwa mtumishi wa tohara kwa sababu ya kweli ya Mungu, kusudi ashimamishe ahadi walizopewa baba zetu;” 
Hapa Mutume Paulo anasema ya kwamba Bwana Yesu alikuwa mtumishi wa tohara, mtumishi kwa wayuda tena yeye alikuwa mtumishi kwa sababu ahakikishe na kushimamisha ahadi walizopewa wababa wao. 

Ahadi lilewalilopewa wababa itatimilika wakati watafikia ule ufalme unaokuja wenye utakuwa hapa chini duniani. 

Na mutume Paulo haiko anahubiri juu ya ufalme wa ulimwenguni.  

Yeye anahubiri kwamba wayuda na mataifa wote wanakuwa kwa daraja moja na wote wanapashwa kukaribia Baba Mungu kwa njia ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo ili wawe viungo vya Mwili huu Mumoja, Jengo hii mupya, Kao hii ya Mungu Baba, inayojengwa na Mawe yaliyo hai. 

5/ Tuone sasa habari njema yenye Bwana wetu Yesu alikuwa nayo, tukisoma 

Matayo 10: 5 - 6 

“Hawa kumi na wawili Yesu aliwatuma, akawaagiza akisema: Musiende katika njia ya Mataifa, wala musiingie muji wowote wa wasamaria; Lakini Zaidi kwendeni kwa kondoo wapotevu wa nyumba ya Israeli.” 
Hapa Bwana wetu Yesu Kristo anaagiza mitume wake kumi na wawili wasiende katika njia ya Mataifa lakini waende kwao kondoo wapotevu wa nyumba ya Israeli. 

Bwana wetu Yesu Kristo hakufunuliya mitume wake kwamba wao walikua viungo ya Mwili wenye utajengwa kwa muungano wa wayuda na mataifa. 
Bwana Yesu aliwaambia waende tu kwa taifa la Israeli. 

6/ Tusome sasa kwa kitabu ya Matendo ya mitume 1: 1 - 3, 6 

“Katika kitabu cha kwanza, Teofilo, nilikuandikia mambo yote aliyoanza Yesu kufanya na kufundisha, hata siku ile alipochukuliwa juu nyuma ya kuagizwa kwa Roho Mutakatifu mitume ambao aliwachagua. Na nyuma ya kuteswa kwake aliwatokea, akawaonyesha kwa alama nyingi yakuwa yuko hai, akaonekana nao kwa muda wa siku makumi ine, na kusema nao maneno ya ufalme wa Mungu. … Wakati walipokutanika wakamwuliza, wakisema: Bwana, utarudishia Waisraeli ufalme wao tena wakati huu?” 
Turudi nyuma kidogo kwa nyakati ile ya Pentekoste nafasi mutume Luka alifunguwa kitabu cha Matendo ya mitume na kusema kwamba Bwana Yesu alikuwa pamoja nao muda wa siku makumi ine juu ya kuwafundisha maneno ya ufalme wa Mungu. 

Muda ya siku hii makumi ine, Bwana Yesu alionekana na wale kumi na miwili wakati alipokuwa akiwafundisha. Tunaweza kujiuliza kama mafundisho aliowafundisha ni ile inayosema kwamba wayuda na Mataifa wanakuwa wote viungo vya Mwili mmoja? 
Tujiulize tena eti Bwana Yesu alikuwa anafundisha mitume kumi na wawili kwamba taifa la Israeli haita pata tena ufalme wake? 

Kwamba ufalme huo uliwekwa kando? 

Ama, Bwana Yesu alikuwa akiwafundisha habari aliyowaambia ndani ya kitabo cha Matayo sura 10? 

7/ Tunaweza kutambua kwamba nyuma ya Bwana Yesu kuwa nawo muda ya siku makumi ine akiwaambia maneno mazito ya ufalme wa Mungu, kuna ulizo tunayo pata katika aya yake ya 6, inayotuonesha kwamba: mitume kiisha siku makumi ine ya mafundisho, Bwana Yesu hakuwafunulia kuhusu siri hiyo, sababu alikuwa akiwafundisha juu ya taifa la Israeli. 

Mitume wake walimuuliza: (Matendo ya mitume 1: 6) Wakamwuliza, wakisema: Bwana, utaturudishia Waisraeli ufalme wao tena wakati huu? 

Ingelikuwa Ufalme wao umetiwa kando na kwamba Bwana Yesu angalikuwa anawafundisha kwamba ufalme wao umetiwa kando, munazani kwamba wangemuuliza ulizo la namna ile? 

Wao hawakuwa hata na wazo fulani kujuwa kwamba kwa sasa Baba Mungu iko sasa na kazi ya kujenga  Mwili Mupya ambayo ni jengo lenye litaunganisha na kuweka wayuda na mataifa kwa daraja moja.  

8/ Na inaonekana tena kwamba wao hawakujuwa kitu chochote juu ya maandiko ya 

Waroma 11: 11, 12, 15   

“Basi ninasema: Wamejikwaa waanguke kabisa? Hapana, hata kidogo; lakini kwa sababu ya kuanguka kwao wokovu umefikia Mataifa, ili wao watiwe wivu. 
Basi kama ikiwa kuanguka kwao kumekuwa mali ya dunia, na upungufu wao umekuwa mali ya Mataifa; si Zaidi sana utimilifu wao? 

Kwa sababu kama kutupwa kwao kumeleta upatanisho kwa dunia, kupokewa kwao kutakuwa nini kama si uzima toka wafu?” 
Hapa inaoneshwa ya kuwa kutupwa kwa taifa la wana wa Israeli kumeleta utajiri wa Neema kwa Mataifa, lakini wao hawakufahamu hivyo katika nyakati zile, Wangelifahamu hivyo, wangelikuwa hata na ulizo moja kwake. Wangelifahamu kwamba taifa la Israeli lilitiwa kando. 

9/ Kwa sasa twende kwanza siku kumi nyuma, hapo mutume Petro alikuwa akihubiri hiyo siku ya pentekoste. 

Matendo ya Mitume 2: 22   Yeye alisema ya kwamba: 
“Ninyi wanaume wa Israeli, sikieni maneno haya: Yesu wa Nazareti mtu aliyeoneshwa kwenu na Mungu kwa matendo ya uwezo, maajabu na alama alizofanya Mungu kwa mkono wake kati yenu, kama ninyi wenyewe munavyojua;” 
Alisema ya kwamba nyinyi wanaume wa Israeli, musikie maneno haya. Nikusema kwamba hawakujuwa kitu juu ya neno inayosema kama Israeli ilitiwa kando ya nini? 
Ya Siri iliyo letwa kwa mutume Paulo kwa njia ya ufunuo. 

10/ Muniruhusu niwaulize kwamba Mutume Paulo alijifunza hiyo siri wapi? Kama Yeye hakuijuwa nyuma ya ile siku makumi tano ya mafundisho iliyo fundishwa na Bwana wetu Yesu Kristo, ni fasi gani basi kwenye yeye alifundishwa hiyo Siri nyuma ya siku kumi? 

Hapana hata kidogo, 

Yeye hakuyafahamu na tena Habari Njema ya waliotahiriwa iko tofauti na Habari njema kwao wasiotahiriwa. 

11/ Hivyo sasa turudilie maandiko yetu katika Matendo ya mitume 1: 7. Jibu ya Bwana wetu Yesu Kristo ilikuwa gani? Na ni ile jibu njoo iko ya muhimu sana ndani ya majifunzo yetu.  

Matendo ya mitume 1: 7  

“Basi kama Mungu aliwapa zawadi namna alivyotupa sisi, wakati tulipoamini Bwana Yesu Kristo, mimi ni nani, niweze kuzuiza Mungu?” 
Ni nini Bwana Yesu aliwajibu? Eti aliwaambia kwamba ninyi hamuta pata ufalme wenu ama 

Aliwajibu kwamba ufalme wenu hautakuweko tena? 
Yeye hakuwajibu namna ile. 

Eti tujiulize kama Yeye aliwaambi kwamba nyinyi mumepoteza bahati yenu ama kwamba matabiri ya Agano la kale yamekomeshwa na kwamba Mungu ataanza kutumika na watu wote kwa namna moja, ama kwamba watu wote wayuda na mataifa wote watakuwa na samani moja na daraja namna sawa? 

Hapana hata kidogo, yeye hakufanya hivyo. 

Yeye hakuwafundisha Waroma 11

12/ Bwana na Mwokozi wetu hakuwaambia kama mawazo yao yalikuwa inje ya mustari; ama mawazo yao yalikuwa ya upotevu sababu Yeye alikuwa anazungumuza juu ya ufalme. 

Yeye aliwaambia tu kwamba siyo kwao kuuliza maulizo juu ya nyakati. 
Kwa kweli hapa, walikuwa wanauliza Bwana na Mwokozi wetu, kwamba kurudi kwake kutakuwa lini, ama nyakati gani yeye atarudi? Na ufalme utaanzishwa wakati gani? 
Hiyo iliambatana na Matayo 24: 36. 

Matayo 24: 36 

“Lakini hakuna mutu anayejuwa habari za siku ile na saa ile, hata malaika walio mbinguni wala Mwana, ila Baba peke yake.” 
Kwa kweli hakuna mutu anaye fahamu saa ama siku ya kuja kwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 

Wanafunzi walikuwa na ulizo juu ya iyo, lakini aliwajibu kwamba hawawezi kuifahamu. 
Aliwaambia kwamba wanaweza kuwa na ufahamu juu ya ufalme wa Mungu, lakini hapana juu ya kuja na kurudi kwa Bwana wetu Yesu Kristo, na hii siyo Habari yenye Mutume Paulo alikuwa anahubiri. 

13/ Sasa tuchunguze kidogo juu ya hii jambo, tujiulize sababu gani wanafunzi walikuwa wanazungumuzia juu ya Ufalme wa Mungu? 

Sababu gani walikuwa na maulizo mazito juu ya hiyo ufalme? 

Kwa kweli tukiangalia mitume waliuliza maulizo mengi sana, sasa sababu gani Bwana 

Yesu anatuzungumuzia juu ya hii ulizo moja tu?  

Kuna kweli sababu iliyo sababisha hiyo. 

Kiisha mafundisho aliyofanya Bwana Yesu Kwa muda wa siku makumi ine, wanafunzi walimuuliza juu ya ufalme wa Mungu, sababu gani? 

Kwa sababu kweli kweli Bwana Yesu alikuwa anawafundisha juu ya ufalme wa Mungu. 
Bwana Yesu angeliwazungumuzia juu ya Siri ya Habari njema, muda wa siku zile makumi ine, nina uhakika kama wamitume hawangeli kosa kumuuliza ulizo hata moja juu ya hiyo Siri. 

Kama unaweza kuketi hata tu kwa muda wa siku mbili ukifwata kwa makini mutu anaye kuzungumuzia juu ya neno fulani, kichwa chako kitajaa na hiyo maneno na hautakosa kuuliza hata swali moja inayoambatana na hayo maneno. 

Nikusema vichwa vya mitume vilikuwa vimejaa na maneno inayo elekeya mambo ya ufalme wa Mungu. 

Yobu 1: 8 - 10  

“Bwana akamwambia shetani: Umeangalia mutumishi wangu Yobu? 
Maana hakuna mmoja kama yeye duniani, mutu mkamilifu na wa haki, mwenye kuogopa Mungu na kuepukana na uovu. Shetani akajibu Bwana, akisema: Yobu anaogopa Mungu bure? Wewe hukumzunguka yeye na nyumba, na vyote alivyo navyo, kwa boma pande zote? Umebariki kazi ya mikono yake, na mali yake imeongezeka inchini.” 
Hapa Shetani iko anazungumuza na Mungu juu ya Yobu. Wewe hukumzunguka yeye na nyumba yake, na vyote alivyo navyo, kwa boma la ukingo pande zote? 

Munafahamu kuna zehebu moja ya watu waliopenda ukristo Safi, wawe na ukristo usiokuwa na dowa ama uchafu. 

Hawa watu waliopenda kuishi ukristo usiokuwa na dowa ama uchafu wowote walikuwa wakifasiriya kwamba hiyo boma ya ukingo iliyozunguka Yobu na mali yake yote ilikuwa boma ya urefu wa kupanda juu sana hata ma pepo wa ibilisi wakuu hawakuweza kuruka hiyo boma na ilikuwa na upana wa zaidi sana hata ma pepo wa ibilisi wembamba sana na wadogo hawakuweza kujiingiza kama shindano ndani ya boma hiyo mpaka Mungu yeye mwenyewe awape ruhusa. Ni hii walifundisha watu. 

14/ Twende sasa kwa maandiko ya mutume Petro 

Kwa kweli Bwana Yesu hakumufunuliya juu ya SIRI hiyo. 

Lakini Bwana Yesu alifanya hivyo kwa mutume Paulo

Paulo alikuwa na Habari Njema tofauti. 

Sasa, Habari njema gani mutume Petro alihubiri siku ya pentekoste? 

Matendo ya Mitume 2: 39 

“Kwa sababu ahadi hii ni kwa ajili yenu, na watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu,” 
Hapa, tunaona kwamba wakati mutume Petro alikuwa anahubiri, alisema, kwa sababu ahadi hii ni kwenu na kwa watoto wenu, ni kwenu ninyi wayuda, na kwa watoto wa wayuda na kwa  watu wote walio mbali. 

Hakupenda kuzungumuza juu ya wayuda wengine wenye wiko katika inchi jirani, lakini alimaanisha kwa kweli waziwazi kama ni kwa sisi, sawa vile tunavyosoma katika kitabu cha Waefeso sura mbili, Waefeso 2 

“Nanyi mulikuwa wafu kwa sababu ya makosa yenu na zambi zenu,” 
Tunaona hapo watu wenye walikuwa sawa wakuzarauliwa, watu waliokuwa mbali. 
Katika Waefeso 2, Mutume Paulo anatufunuliya kwamba, wakati hiyo kiambaza cha uadui na matengano kilikuwa bado kingaliko, Mataifa mengine walikuwa sawa wakiwa mbali kwa muda wa siku zile. 

Sasa Mutume Petro wakati alipokuwa akihubiri akijazwa na Roho Mutakatifu alipata ufahamu juu ya hiyo ukuta na alizungumuza juu ya hiyo ukuta kama sawa bado ilikuwa ingaliko. 

15/ Mutume Petro hakukua anatambuwa kwamba hiyo ukuta imekwisha ku bomolewa na kutiwa mbali. 

Tusome Matendo ya Mitume 2: 39 

“Kwa sababu ahadi hii ni kwa ajili yenu, na watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu,” 
Unatambuwa hapa kama Mutume Petro anatumikisha nyakati za sasa akisema: “na kwa wote walio mbali”, wakati alipokuwa akisema yeye aliwaona kama wao bado wangali mbali na ijapokuwa wameisha kuwa karibu. 

Mutume Petro hakufahamu kama wao wameisha kuwa karibu, angelijuwa vile, angeliizungumuzia hiyo siku ya Pentekoste.

Nikusema mutume Petro hakuwa na habari njema sawa na hiyo iliyosemwa na mutume Paulo. 

16/ Matendo ya Mitume 10:28  

“Akawaambia: Nanyi munajuwa ya kuwa si halali kwa mutu wa Yuda kupatana na kabila lingine, wala kumkwendea, lakini Mungu amenionyesha nisiite mutu yeyote mnyonge wala mchafu.” 
Hapa tunaona Kornelio, mutu wa mataifa na kwake njoo Mungu alituma mtume Petro. 
Na kama mutume Petro alikuwa akiheshimia agizo iliyosema Nendeni ulimwenguni kwote, tunaona kwamba hainge faa tena kwa mutume Petro kungoja kwanza Mungu amutume tena kwa Kornelio, hivi ingelifaa Kornelio njo atumwe kwa mutume Petro. 
Na sasa tutazame namna mutume Petro anavyosema kwamba:

Nanyi munajuwa ya kuwa si halali kwa mutu wa Yuda kupatana na kabila lingine, wala kumkwendea, lakini Mungu amenionyesha nisiite mutu yeyote mnyonge wala mchafu. 
Hapo, mutume Petro, anajionyesha kwa hali yakuwa kama yeye ni mutu kweli aliye muyuda. 

Hakufahamu maneno inayosemwa katika Waroma 10: 12  
“Kwa maana hapana tofauti katikati ya Wayuda na Wayunani, maana yeye yule ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa watu wote ambao wanamwitia:” 

Mutume Petro, kwa kusema vile alikuwa anasema kama muyuda. Hakufahamu Siri ya siku za leo. 

17/ Kitu cha muhimu kujuwa  

Matendo ya mitume 10: 28 
Tujiuluze kama hii jambo ilikuwa nyuma ya mutume Petro kupata maonyo, na kiisha hiyo kuendelea kujitambuwa tu kama muyuda, hii ni neno kubwa linalopaswa watu kufahamu. 

18/ Twende sasa katika Waefeso 3: 1 

“Kwa sababu hii mimi Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu kwa ajili yenu ninyi Mataifa,” 
Mutume Paulo iko anatuambia kwamba ni kwa sababu ya SIRI hii Mupya njoo maana iko anajijulisha kwamba yeye ni mfungwa kwa ajili yetu sisi Mataifa. 

Yeye ni mfungwa wa Kristo Yesu kwa Mataifa, watu wasiojuwa Mungu. 

19/ Mutume Paulo anasema hapo kwamba yeye haiko mufungwa juu ya kosa lolote la binafsi, SIRI hii Mupya yenye Mwenyezi Mungu alimufunulia njo yenye watu wanachukia sana. 

Watu walichukia Habari Njema hii na Mutume Paulo alibaki tu mwaminifu kwa Habari Njema hii. 

20/ Pima kuwaza na kuchunguza neno hili: Mutume Paulo kwa kweli alitiwa katika gereza ya chini, ndani ya chimo katika gereza hizo za muji wa Roma zilizokuwa chini ya udongo na Mutume Paulo alitiwa huko kwa sababu alikuwa na ile hamu kubwa ya kutufahamisha SIRI HII KUBWA YA MUNGU katika utunzaji huu wa siku za leo na kwa kweli jambo hili lingelipashwa kuburudisha moyo wako. 

21/ Hakuna kitu kingeliweza kuwasha hasira na kasirani ya wayuda, taifa la kidini ya wakati ule, sawa Hahari njema yenye mutume Paulo alikuwa anatosha kwa mudomo wake, ni hii ilikuwa inaleta hasira nyingi na kasirani sababu mutume Paulo alikuwa anahubiri kwamba Mungu akuendelea kuishi tena ndani ya hekalu zilizojengwa na mikono ya watu na Mungu hakuendelea kutumika na Israeli kama taifa pendelevu kwa upekee kwa sababu Mungu aliwageukia vilevile Mataifa mengine za ulimwengu na kumupa ama kumuletea wokovu yeyote yule atakaye amini. Tuhakikishe maneno haya kwa kusoma kitabu ya Matendo ya mitume 22: 22 - 24   

“Walimusikiliza mpaka neno hili, wakapaza sauti zao, wakisema: Mwondoshe huyu katika inchi kwa maana haifai aishi. 
Walipokuwa wakipiga kelele na kuondoa mavazi yao na kutupa mavumbi juu, 
Yule mkubwa aliamuru aletwe ndani ya nyumba kubwa, akisema aulizwe kwa mapigo ya fimbo, apate kujuwa kwa maana gani walipiga kelele namna hii juu yake.”    
Hapa tunaona namna gani wandugu wa damu, wandugu wa kabila moja na mutume Paulo, walikuwa wakilalamika kwa sauti kubwa sababu mutume Paulo alipokuwa akihubiri,  wao walimusikiliza na kungojea tu saa atatamka neno Mataifa na ni hapo walipaza sauti zao, wakisema: Mwondoshe huyu mutu wa namna hii katika inchi, sababu yeye hastaili kuishi.

Walipiga kelele na kuondosha mavazi yao na kutupa mavumbi juu, wakatia mutume Paulo gerezani wakamutia katika kifungo cha chini ya udongo. 

Ni kwa sababu ya mahubiri ya maneno yale aliyo yahubiri mbele ya mulango wa hekalu, maneno yaliyo  kuwa magumu na nguvu kwao na kuvuruga akili yao, maneno yale  yalichanganyikisha  ufahamu wa wale watu wa dini, kwa sababu ya hiyo ushuhuda njo mutume Paulo alitiwa gerezani.  

22/ Ni hii njo inahakikisha sababu gani mutume Paulo alikuwa mara na mara akileta ushuhuda na hakikisho ya huduma aliyopewa. Ni kwa sababu ya hiyo njo mara kwa mara mutume Paulo alikuwa anatiya mukazo wa kusema kwamba yeye ni mutume wa Bwana Yesu Kristo, siyo kwa mapenzi ya mutu lakini kwa Yesu Kristo pekee. 

Watu wamoja wanasema kwamba mutume Paulo angepashwa tu kusema hivyo sababu mutume Matiasi vilevile alikuwa anapenda kukamata nafasi ya Yuda Eskariote na ni kwa hiyo walizani kwamba mutume Paulo vilevile alikuwa anapenda apate hiyo nafasi ya Yuda, lakini maandiko matakatifu hayaleti mawazo ama neno lolote juu ya misemwa hiyo, ni umbalimbali kweli na yale Maandiko Matakatifu yanasema. 

Mutume Paulo alihakikisha huduma yake sababu yeye alikuwa akihubiri Habari Njema mupya, Habari Njema tofauti, Habari Njema ya Siri aliyo ipata kwa ufunuo yeye pekee akiioneshwa na Mungu.  

23/ Tufahamu ya kuwa namna ya kuishi gerezani kwa mutume Paulo inakuwa inaambatanishwa sawa sawa na vile Yosefu vilevile alivyokuwa gerezani. 
Tusome 

Mwanzo 45: 4, 5 

“Yosefu akawaambia ndugu zake: Karibieni kwangu, ninawaomba ninyi. Wakakaribia. Akasema: Mimi ni Yosefu ndugu yenu ambaye mulimwuza kwenda kwa Misri. 
Basi sasa musihuzunishwe, wala isiwe hasira kwa macho yenu ya kwamba muliniuza hapa; kwa sababu Mungu alinituma mbele yenu kwa kuponyesha maisha ya watu.” 
Kwa namna nyingine nikusema kwamba ilikuwa mapenzi ya Mungu nikuwe gerezani, ingelinipasa niuzishwe, kulikuwa kusudi juu ya hayo yote. 
Kuponyesha maisha ya vizazi. 

Mutume Paulo anasema sioni kwangu kuwa hasara mimi kupatikana gerezani. Ni mapenzi ya Mwenyezi Mungu mimi niwe hapo. 

Najuwa kwamba Habari njema hii ya Siri inakuwa na sababu yake na mimi ni mufungwa kwa sababu ya Habari Njema hii na Mungu aliona kwamba ni vema mimi nipatikane gerezani kwa sababu ya Habari Njema hii ya Siri. 

24/ Tufahamu kwamba mutume Paulo hakusema kwamba mimi ni mufungwa wa mufalme NERO, ama mufungwa wa taifa la Roma, lakini mufungwa wa Kristo Yesu. 

25/ Vifungo vya nyakati za hapo kale vilikuwa tofauti na ma gereza za nyakati ya sasa. 
Kwa nyakati za kale vyumba vya vifungu havikukuwa na vifaa yoyote kwa ajili ya mfungwa, kulikuwa tu taa ndogo sana, hewa haikuwa bora, chakula kilikuwa kidogo sana.

Mufungwa alikuwa anatiwa munyororo akifungwa kwa mwili wa askari moja wa Roma saa makumi mbili na ine kwa siku. 

Gereza ya leo ni umbalimbali kweli na hiyo mutume Paulo alikuwa ndani. 
Mutume Paulo alivumilia shida hii yote sababu yeye alikuwa na Habari njema ya Siri yenye alipashwa kuhubiri na kutangaza. 

26/ Wakati mutume Paulo alikuwa akisema kwamba yeye ni mufungwa wa Kristo Yesu, alikuwa na uhakika na hakikisho kwamba falme zote za ulimwenguni hazina mamlaka yoyote juu yake isipokuwa Mungu yeye mwenyewe kwa mapenzi yake aruhusu neno lolote, 

Tukumbuke historia ya Yobu. 

Mungu alitiya mupaka. 

Shetani hangaliweza kufanyia Yobu chochote kama Mungu hangeliliruhusu. 
Mpaka vile Mungu aliruhusu shetani aguse vifaa vya Yobu bila kunyoosha mukono wake kwa umutu wa Yobu.

Na mutume Paulo vilevile iko anasema maneno yale vilevile. 

Mimi siko mufungwa wa mufalme Nero. 

Mimi siko mufungwa wa taifa la waroma. 

Mimi niko mufungwa wa Yesu Kristo, ni yeye njo aliona kwamba ni vema nipatikane hapo. 

27/ Inawezekana ndugu yangu kwamba wewe uko unapitiya majaribu kazaa. 
Inawezekana Mwenyezi Mungu aliruhusu boma lako la ukingo ibomolewe sawa vile alivyofanya kwa Yobu na kwa mutume Paulo. 

Ninakuhakikishia kwamba Mwenyezi Mungu atakutendea na kukushimamisha sawa vile alivyotendea Yobu, sawa tu vile alivyo shindia mutume Paulo wakati wote walipokuwa wakipitia saa hizo za majaribu. 

28/ Mutume Paulo alionesha na kuzungumuzia juu ya SIRI hii katika vitabu vingine, lakini umbalimbali na hii tunayoipata katika kitabu cha waefeso, hapo tunaona ya kwamba Ukweli wa Siri hii unaonyeshwa kwa ukubwa na upana na uzito wake. 
Hapo Ukweli wa Siri hii unaonyeshwa wazi sana tofauti na nafasi kwenye inasemwa kwa jumla tu. 

Katika kitabu cha Waefeso ni hapo tunaona na kupata kujuwa sana Siri hii kwa Umuhimu wake wote, siyo tu mimi ninaeona hivyo, nakumbuka  kama alivyosema vilevile mutumushi wa Mungu Pastori Talbot wa kanisa la Fundamental church pa Los Angeles. 

29/ Katika haya ya 5 mpaka 9, mutume Paulo ana tuonesha wazi wazi na bila fumbo lolote kwamba watu wa vizazi vilivyo pita hawakufahamu hata neno moja juu ya ufunuo wa Siri hii. 

Maneno ya mafundisho ya manabii wa Agano la Kale kuhusu Kusulubishwa kwa Kristo na Utukufu unaofwata kusulubishwa kwake ni hiyo Utawala wa Utukufu wa Kristo. 
Tukijifunza kwa makini sana maandiko ya Agano la kale inatufunuliya ya kwamba Utawala wa miaka elfu wa Kristo hapa duniani unakuja nyuma ya kusulubiwa kwake musalabani. 

30/ Tuendelee na majifunzo yetu ya kutangaza SIRI hii kuu ya Mungu. 
Mutume anatuonesha nafasi yenye Mataifa wanapata katika huduma na utunzaji huu mupya. 

Waefeso 3: 6    

“ya kwamba Mataifa ni wariti pamoja nasi wa uriti mmoja, na wa mwili mmoja, na washiriki pamoja nasi wa ahadi hii katika Kristo Yesu kwa ajili ya Habari Njema.” 
Tunapashwa kweli kufahamu katika akili na mioyo yetu kwamba Baraka hii ni mbalimbali na mibaraka nyingine iliyo patikane wakati wa mwisho ya historia ya Agano la Kale wakati wa ile utawala wa miaka elfu moja wakati kutakuwa uwingi wa mataifa mengine yaliyo okolewa na wao vilevile watabarikiwa na mibaraka ya hapa chini ulimwenguni na hakuna siri katika Agano la Kale linalosema juu ya utabiri wa utukufu huo wenye mataifa ile iliyo okoka itapata. Na hii haiko sawa sawa na Mwili huo Mumoja unaopatikana katika kitabu cha Waefeso.  

Tuchunguze nusu ya maandiko ya Agano la Kale ili tufahamu maneno tunayoyasema. 

31/ Isaya 62: 2 

“Na mataifa wataona haki yako, na wafalme wote wataona utukufu wako; na utaitwa kwa jina jipya, litakalotajwa na kinywa cha Bwana.” 

32/ Isaya 11: 10 

“Na itakuwa katika siku ile, shina la Yese linalosimama kuwa kama bendera kwa makabila ya watu, kwake mataifa watatafuta; na pahali pake pa kupumzika patakuwa na utukufu.” 

33/ Isaya 66: 12  

“Maana Bwana anasema hivi: Tazama, nitamnyoshea salama kama mto, na utukufu wa mataifa kama maji yanayofurika; na mutanyonya na mutabebwa kwa nyonga; na mutabembelezwa juu ya magoti.” 

34/ Malaki 1: 11 

“Kwa maana tangu kucha kwa juwa hata kushuka kwake jina langu ni kubwa katikati ya Mataifa, na kwa kila pahali wanatolea uvumba kwa jina langu, na toleo safi; kwa maana jina langu ni kubwa katikati ya Mataifa; Bwana wa majeshi anasema.” 
Kwa kuchunguza kila moja ya ma haya hizo tunatoka kuzisoma, tunatambua ya kwamba mibaraka inayosemwa hapo ni mibaraka yenye ina aina ya ulimwengu. 
Lakini Mibaraka yenye tunasoma katika Waefeso 3: 6 ni mibaraka tofauti sababu hayo ni mibaraka ya Mbinguni. 

35/ Sasa ndani ya kitabu cha Waefeso 3: 9 tunaona ombi na aliko la siku za leo hapo tunaona mawazo ya utukufu. 

Hapa tunayatofautisha na nyingine na kuonesha watu wote na kuonesha ahadi hii na kuangazia watu wote wajuwe habari za madaraka ya siri iliyofichwa tangu zamani ndani ya Mungu aliyeumba vitu vyote. 

Tunapashwa kafanya yote iwezekanavyo ili watu wote waangaziwe na wajuwe SiRi hii. 

AMEN

N°Ref: 01/24/1960 / 211 - WHY WAS PAUL IN PRISON / 2020

Tuesday, January 7, 2020

KWA JUHUDI NA UJASIRI KUPITIA DAMU / BOLDLY, THROUGH THE BLOOD



Photo taken from B Smith's Kitchen Window








     KWA JUHUDI NA UJASIRI KUPITIA DAMU 
     203 BOLDLY THROUGH THE BLOOD 
     Pastor Henry Kulp 
     January 3,1960 







Waefeso 2: 14 - 22 

“Kwa maana yeye ni salama yetu, ambaye alitufanya sisi sote tuliokuwa wawili kuwa mmoja, na alibomoa kiambaza cha kati ambacho kilitutenga. Naye akikwisha kuondosha uadui katika mwili wake, ndiyo sheria ya amri zilizo katika  maagizo; ili apate kufanya hawa wawili kuwa mtu mpya mmoja ndani yake, akafanya salama. Akapatanisha wote wawili na Mungu katika mwili mmoja, kwa njia ya musalaba wake, akikwisha kuuua ule uadui kwa njia yake. Akakuja na kuhubiri salama kwenu muliokuwa mbali, na salama kwao waliokuwa karibu. Kwa maana kwa yeye sisi sote tumepata njia ya kukaribia Baba katika Roho mmoja. 

Basi tangu sasa ninyi si wageni na wasafiri tena, lakini wenyeji pamoja na watakatifu, na watu wa nyumba ya Mungu. Mumejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo mwenyewe ni jiwe kubwa la pembeni. Katika yeye jengo zima linaunganishwa vizuri na kukua hata lipate kuwa hekalu takatifu katika Bwana. Katika yeye ninyi vilevile munajengwa pamoja kuwa kao la Mungu katika Roho.” 

Katika hii maandiko matakatifu, Mutume Paulo alitamani kutuonesha wazi kwamba kwa siku za kale wayuda na mataifa zingine walikuwa tofauti. Mungu aliweka na kusimamisha ukuta ama kibambazi katikati yetu. Alitia umbalimbali kati ya wayuda na mataifa mengine. 

Lakini sasa kupitiya Bwana Yesu Kristo, hiyo kiambaza ilibomolewa ilivunjwa nkuondoshwa na sasa hakuna tofauti kati ya muyuda na mutu wa mataifa. Wote wanakuwa hali na daraja moja hakuna aliye pendelewa. Mungu anaona sasa tu mutu mupya mmoja, hakuna tena ule aliekuwa akipendelewa. Kuwa muyuda ama mutu wa mataifa hiyi siyo tena tatizo, ya muhimu ni kuwa chini ya Mwamba Yesu Kristo na kumuamini, na kuwa mutu mupya mumoja, siyo tena taifa, lakini Mutu mupya mumoja. 
   
1/ Yote inahusu huyu mutu mupya     

Wakati tunalinganisha hii neno kupitiya andiko la 2 Wakorinto 5: 17

“Hivi kama mutu akiwa ndani ya Kristo, yeye ni kiumbe kipya; maneno ya zamani yamepita; tazama, maneno yote yamekuwa mapya”

Tunatambuwa ya kuwa ndani ya kiumbe hiki kipya, katika huu mutu mupya, tunaona ya kwamba mambo yote ya zamani yamekwisha, tazama yote yanakuwa mapya. Kwa sasa, mambo yote yaliyo pita, sawa maagizo na shurti iliyo kuwa katika siku za kale, imepita, na yote yanakuwa mapya. 

2/ Tuchunguze maneno mojamoja ya maandiko ya agano lililo pita, maagizo na shurti za musingi ya taifa la wana waizraeli. Mimi kwa binafsi namushukuru Mungu kuona kama mimi siko tena chini ya hiyo utumwa kwa leo. Hii ni kwa njia ya kiroho. 

Wagalatia 6: 15 

“Kwa sababu katika Kristo Yesu kutahiriwa si kitu, wala kutokutahiriwa, lakini kiumbe kipya.” 

Hapo ni katika Kristo Yesu, katika kiumbe hicho kipya, katika huyu mutu mupya kutahiriwa ama kutokutahiriwa si kitu, lakini tu kiumbe kipya. Sasa kumbukeni kwamba kwa siku za kale, hiyo tendo ilikuwa yenye maana na yenye mafaa sana.  

Mwanzo 17: 11 - 12 

“Nanyi mutatahiriwa kwa nyama ya ngovi, na itakuwa alama ya agano katikati yangu nanyi.  Naye aliye na siku nane atatahiriwa katikati yenu, kila mwanaume kwa vizazi vyenu anayezaliwa nyumbani, ao anayenunuliwa kwa feza kwa mugeni asiye wa uzao wako.” 

Hapa inasemwa kwamba, mwanaume wote wa siku nane katikati yenu atatahiriwa. Hiyo njo itakuwa alama ya agano katikati yangu nanyi. Ni kwa sababu ya hiyo njo Abrahamu mwenye aliitwa mbele Abramu, wakati alipata kutahiriwa saa alikuwa na umri wa miaka makumi kenda na kenda, jina lake likageuka kuwa sasa Abrahamu. Kutahiriwa ilikuwa ya maana sana, na ilikuwa musingi wa agano lenye Mungu alilofanya na Baba wa taifa la wana wa Izraeli. Katika nyakati yenye hiyo ukuta ama kiambaza ilikuwako, kutahiriwa ilikuwa na maana sana na ilikuwa shurti. 

3/ Mwanzo 17: 14, hapa inasema ya kuwa: 

“Na mwanamume asiye tahiriwa kwa nyama ya ngovi, nafsi ile itakatiliwa mbali na watu wake; amevunja agano langu.” 

4/ Munakumbuka historia ya Musa katika Kutoka 4: 24 - 26 

“Na ilikuwa njiani kwa pahali pa kupanga, Bwana akakutana naye akitaka kumwua. Halafu Sipora akatwaa jiwe, akakata ngovi ya mwana wake, akaitupa chini kwa miguu yake, akasema: Hakika wewe ni bwana-arusi ya damu kwangu. Hivi akamwacha.  Halafu akasema: Bwana arusi ya damu wewe kwa sababu ya tohara.” 

Musa alikuwa bado kutahiri mwana wake, na ijapokuwa ni yeye ndiye alikuwa mukombozi wa Taifa Lake. Mungu akakuja akifwata mutoto wa musa na nia ya kumuuwa. Sababu gani? Sababu musingi wa maagizo la agano ilikuwa bado haijafanyika! Kutahiriwa ilikuwa ya manufaa kabisa katika hiyo nyakati. Lakini katika Wagalatia inasemwa kama kutahiriwa si kitu, lakini ya lazima ni kuwa mwanamemba wa hiyo kiumbe kipya kwenye maagizo hizo zote za zamani zimetupwa kando na mambo yote yanakuwa mapya. 

5/ Tena tuone hapa ya kuwa Taifa la Israeli ilikuwa taifa pendelevu ya Mungu. 

Kutoka 19: 5 - 6 
“Kwa hivi basi kama kweli mutasikia sauti yangu, na kuchunga agano langu, halafu mutakuwa mali yangu mwenyewe kuliko mataifa yote; maana dunia nzima ni yangu; na mutakuwa kwangu ufalme wa makuhani, na taifa takatifu. Haya ni maneno ambayo utawaambia wana wa Israeli.” 

Mungu anatia ma shurti ya kusema “kama” mbele ya hiyo maagizo yote. Kama kweli mutasikia sauti yangu, na kwa njia hiyo njo nyinyi mutakuwa maliyangu mwenyewe. Lakini tushukuru Mungu, kwa sababu ndani ya huyo mutu mupya, hiyo shurti ya kusema “kama” imetupwa, yote ni kwa Neema. Kwa kweli sisi leo tuko wazuri zaidi sana kwa sababu ya ginsi Mungu aliuvunja huo kibambazi ama ukuta uliokuwa katikati yetu na faida tunayo inatambuka namna Israeli walikuwa naiishi wakati kibambazi hiyo ilikuwa bado ingali. 

6/ Tuzungumuze sasa juu ya Siku ya sabato 

Kutoka 31: 16 - 17 

“Kwa hivi wana wa Israeli watachunga siku ya sabato, kuangalia sana sabato katika vizazi vyao vyote, ni agano la milele. Ni alama katikati yangu na wana wa Israeli milele; kwa kuwa kwa siku sita Bwana alifanya mbingu na dunia, akastarehe siku ya saba na kupumzika.”

Hapa inasemwa kwamba wana wa Israeli wanapashwa kuheshimia siku ya sabato. Wanapashwa heshimu siku ya sabato vizazi na vizazi kama alama ya milele. Ni alama katikati yangu mimi Mungu na wana wa Israeli kwa milele. Siku ya sabato haiko tena leo sababu taifa la Israeli imeachwa kando na Mungu anatembea na Israeli na mataifa yote mengine pamoja na kwa daraja na namna moja.  Kama tu wanaamini Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, wanakuwa viungo vya huu mutu mupya, ni kwa maana hiyo na kwa ukweli hii njo maana siku ya sabato haiko tena leo, ilitiwa kando. Ninashukuru Mungu sana kwa maana mimi leo silazimishwe kuheshimu siku ya sabato leo, mimi ninakuwa na kitu cha muhimu sana ndani ya Kristo Yesu. 

7/ Tumefanywa wote kuwa mumoja ndani ya Kristo Yesu maana tumefanywa kuwa huyu mutu mupya mumoja. Ni kwa sababu hii njo maana neno kutengenezwa haipatikani ndani ya maandiko ya mutume Paulo. Leo tunasema juu ya kutengenezwa, lakini tunalo neno la muhimu Zaidi ya kutengenezwa. Ni neno lililo tumikishwa zamani katika agano la kale, ni neno lililokuwa na mafaa wakati hiyo kibambazi ilikuwa ingali bado katikati yetu, Hii neno haitumikishwe kwa wakati wa leo sababu hii ukuta wa kututenga umeishwa ondoshwa. 
Sababu kutengenezwa inamaanisha kufunika. Tunapashwa kusema kama ilivyo katika 

Waroma 5: 11 

“Wala si hivyo tu, lakini tunafurahi katika Mungu kwa Bwana wetu Yesu Kristo, kwa Yeye sasa tumepokea upatanisho.”

Hapa, neno kutengenezwa ingelionekana, lakini utafsiri wa kweli unatumikisha neno upatanisho. Na kwa hiyo, tunakuwa sote viungo vya huyu mutu mupya. Kwa mara tena tunakaza tena kwa kusema kwamba, kwa njia ya kubomoa hiyo ukuta ulioleta matengano katikati yetu, tunakuwa sasa na faida Zaidi. Sababu inayo onesha kama kwa leo sisi tunakuwa sasa na faida Zaidi ni kwamba sisi tunakuwa sasa viungo vya Yesu Kristo. 
Zambi zetu hazifunikwe tena kwa leo, lakini zimevutwa, zimesahauliwa na kutupwa mbali sana nasi, na sisi tunakuwa wenye haki kama vile Yesu Kristo iko mwenye haki kwa sababu sasa sisi ni viungo vya Kristo Yesu.

Tuangalie kwanza kwa muda kidogo Adamu. Adamu aliumbwa kwanza mbele apewe muke wake. Mungu alimutia Adamu katika usingizi nzito kiisha akatosha ubavu moja wa mwanaume, na kwa hiyo ubavu akamuumba mwanamuke kiisha akamuleta mwanamuke akamupa kwa mwanaume ili wajenge mwili mumoja  pamoja naye Adamu. 
Na akawaita wote wawili Adamu. 

Mwanzo 5: 2 

“aliwaumba mume na muke, akawabariki, akaita jina lao Adamu, kwa siku walipoumbwa.”

Ni kwa namna hiyo moja tu njo Yesu Kristo alikuja duniani na kwa kupitia Damu yake na Ufufuko wake njo sote tumekuwa viungo vya Mwili  wake, tunakuwa Mwili mumoja pamoja naye, kama sawa tunavyoona kwa Ewa(muke wa Adamu), jina lake Yesu limetukusanya sote. Wakati tunapozungumuzia juu ya Mwili wa Kristo, mutume Paulo katika 

1 Wakorinto 12: 12 anasema

“Kwa sababu kama mwili ni mumoja, na una viungo vingi, na viungo vyote vya mwili ule mumoja, vilivyo vingi ni mwili mumoja, vivyo hivyo na Kristo.”

Jina letu ni Kristo, sisi ni viungo vya huyo mutu mupya na hii ina mafaa zaidi kupita vitu vyote vilivyo kuwa katika nyakati za kale.  


8/ Waefeso 2: 16 

“Akapatanisha wote wawili na Mungu katika mwili mmoja, kwa njia ya musalaba wake, akikwisha kuua ule uadui kwa njia yake.” 

Maandiko hii inatuambia kama Bwana wetu Kristo Yesu alipatanisha wa Israeli na mataifa wawe mwili mumoja kwa njia ya Musalaba wake. Mungu alifanya neno lingine kubwa hapa, alifanya upatanisho. Jina upatanisho ni nzuri sana. 

Katika Kiswahili, wakati tunazungumuza juu ya neno upatanisho, pale tunaona kundi mbili waliokuwa na ugonvi, uadui, na waliokuwa kweli na chuki ya ndani moja kwa mwengine, na kwa njia hii ya upatanisho wanakuwa sasa na salama moja kwa mwengine. 

Lakini siyo maana ya upatanisho tunayopata hapa, wataalamu wanaonesha maana  ya neno upatanisho sawa MABADIRIKO NDANI YA VIUNGO VYA KIUMBE KIMOJA: kutoka kutokupendana na uadui kati ya Mungu na watu yote imevunjwa kwa sababu ni Mungu anayehusika na tendo hili. Uadui yenye inaweza kuwa leo ni hiyo tu yenye inaweza kuwa ndani ya roho ya mutu yeye peke binafsi. 

9/ Waefeso 2: 18   
  
“Kwa maana kwa yeye sisi sote tumepata njia ya kukaribia Baba katika Roho mmoja.” 

Maandiko yanatuambia kama sisi sote tumepata ruhusa na njia ya kukaribia Baba kwa Roho mmoja. 
Kwa kubowolewa kwa hiyo ukuta ama kibambazi ya matengano, tumepata njia ya kukaribia Baba. 
Hii ni jambo mupya. 
Sijuwe kama mumekumbuka kwamba katika siku za kale hakukukuwa njia ya kukaribia Baba kwa uraisi. 
Hamuone kama neno hili inausika pia wayuda ama wana wa Israeli wote kwa jumla? Hata kama wao ni wana wa Israeli. 
Wao hawakupata faida hii ya upekee yenye tunakuwa nayo kwa leo. 

Kumbukeni Hema ya kusanyiko, kulikuwa mahali takatifu, maali takatifu pa patakatifu maali palipokuwa sanduku ya upatanisho, ndani yake kukiweko ma amri yenye iliyovunjwa na watu, mahali pa rehema palipo juu ya pahali pote, pahali damu ilinyonyezwa juu ya yote, na kwa kuingia ndani ya chumba ile nafasi ya kukutana na Mungu, huyo kuani aliye ingia ili akutane na Mungu alipashwa kutoa kwanza viatu vyake, na kwa desturi alikuwa akiingia katika hema hii ya kusanyiko mara moja tu kwa mwaka na ni kuani mukubwa tu njo alikuwa na ruhusa ya  kuingia na kubeba damu ya kondoo na kwa kuingia alipashwa kutoa nguo yake ili akutane na Mungu na humo ndani ya hema ya kusanyiko kulikuwa giza kali, hakukukuwa dirisha kwa chumba hilo, ndani kulikuwa giza kali, giza kali wakati alipashwa kukutana na Mungu, na hapo, alikuwa anapaingia mara moja tu kwa mwaka. Kwa leo hatuna tena mazoezi hiyo.Tunakuwa tunakaribia Baba Mungu mwenye Enzi na Nguvu zote, tukimukaribia kwa uraisi wote. 

10/ Tuchunguze pamoja hali gani huyo kuhani mkuu aliyokuwa amo wakati alipoingia kwa siku hii moja ya upekee akibeba damu ndani ya hema ya kusanyiko ama hema ya ushuhuda, ndani ya nafasi ya rehema, katika pahali patakatifu ya patakatifu kwenye Mungu alikutana na kuhani mkuu katika giza kali, Mungu akija na utukufu wake ndani ya shekinah. 

Huyo kuani Mukuu alikuwa akiingia yeye peke yake ndani ya Hema hiyo ya kusanyiko ama ya ushuhuda.  

Makuani wengine na watumishi wote na wana wote wa israeli walibaki inje ya hema wakibaki kandokando yake wakiwa pamoja na wana wote wa Israeli. 

Na hapo, kiisha kuingia ndani ya hema la kusanyiko, huyu kuani mkuu alivua nguo yake yenye ilikuwa nzuri, yakupendeza na yenyi marangi nyingi, na kuvaa kanzu ya nguo nyepesi yenye ilimufunika toka kichwa mpaka kwa miguu na kanzu hii alikua akiivaa mbali na watu wengine, akiwa peke yake ndani ya hiyo hema ya kusanyiko na ni katika vazi hii inayo mufunika mwili muzima njo alitwaa sasa damu na kuipeleka kwenye mazabau kuuchoma zabiu na kuipeleka katika mahali patakatifu pa patakatifu mahali sanduku ya agano ilikuwa ikiweko akiikaribia bila kelele yoyote, kimia ikitawala vyote, naye hakusema hata neno lolote, naye alimimia damu pa mahali pa wema wa Bwana, na wakati Mungu alipofurahishwa, hapo kuhani mkuu angeliweza kurudia na kuvaa sasa hiyo nguo yake ya marangirangi. 

Ilikuwa nguo nzuri sana yenye marangimarangi na kwa pande za pembe   ya nguo huko chini kulikuwa ma kengele ndogondogo ya zaabu, yenye ilikuwa ikipiga kengele wakati kuhani mkuu alipokuwa akitembea katika hema la kusanyiko.  

Wakati kuhani mkuu alipokuwa akiingia ndani ya hema takatifu la kusanyiko, alikuwa akivua hiyo vazi yake nzuri ya bei na kuvaa hiyo kanzu ya nguo nyepesi iliomufunika toka kichwa chake hadi miguu yake na baada ya hiyo njo aliweza kugusa sadaka na alipomaliza kazi ya ukuhani alivua nguo ile ya huduma na kuvaa sasa nguo yake ya bei ya marangirangi iliyo fungwa kengele ndogo ndogo kwa pande za pembe za chini na wakati kuhani mukuu alifanya tu hatuwa ya kwanza hiyo makengele madogo madogo ilianza kupiga kengele na watu wote waliokuwa wakingojea inje kwa woga kubwa na kwa kutokujuwa kama Mungu atakubali sadaka ama hapana walibaki kwa huzuni kubwa inje wakiwa wote kimya sana. 

Kama kitu kimoja katika mambo yote yenye kuani alikuwa anatimiza, kama kitu hata kimoja hakikufanyika sawa na mapenzi ya Mungu, kama kuhani mukuu kwa bahati mbaya kitu moja kilizorota, Mwenyezi Mungu hakukuwa anakubali hiyo sadaka ya damu, na kwa gafla huyu kuhani mukuu aliuwawa. 

Ni sawa vile wana wawili wa Aruni walivyo poteza maisha yao na kufa kwa gafla. 
Hivyo makuani wengine na wana wote wa waisraeli walikuwa wakingoja matukio yenye itatokea kwa huduma ya kuani mkuu kwa ile siku  kwa shaka kubwa na woga na ukimya kubwa.  

Na wakati waliposikia makengele hizo madogo yakipiga kengele walifahamu kwamba mambo yote yamepita sawa na kuani mkuu hakuuwawa na kiisha punde kidogo atarudia kukutana nao. 

Mungu alikubali damu ya matengenezo na ya kufunika zambi na kwa mara hiyo watu walifahamu yakuwa wana uhusiano tena na Mungu, wanaweza kumukaribia mara tena. 
Hata kama kuani mukuu alibaki tena kwa muda murefu mbali ya macho ya watu, kwa kusikia tu mulio ya makengele hayo madogo madogo, watu walijuwa kama huduma imetimizwa. 

Na watu walipiga kelele kubwa ya shangwe na furaha kuona kwamba milima ya zambi na makosa yao imefunikwa.  

Kwa siku za leo, sisi tunayo kitu kikubwa sana na kyenye maana makubwa sana. 
Katika Yesu Kristo, hiyo kibambazi ya uadui ilivunjwa na kubomolewa na sisi tunakaribia Baba kwa uraisi wote kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo. 

Sisi tuna Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo anayekuwa wetu kwa sasa na yeye ni sadaka kamilifu tukikumbuka namna gani wana wa Israeli walisumbuka kwa siku za kale. 

11/ Tukumbushane tena maandiko matakatifu katika 

Walawi 10: 1 - 2   

“Na Nadabu na Abihu, wana wa Haruni wakatwaa kila mutu chetezo chake, wakatia moto ndani yake, na kutia uvumba juu yake, wakatowa moto mugeni mbele ya Bwana, ambao hakuwaagiza. 
Kiisha moto ukatoka kwa Bwana, ukawakula, wakakufa mbele ya Bwana.” 
Hii kweli ni hadisi mbovu ya makuhani hawa wawili Nadabu na Abihu waliotowa moto mgeni mbele ya Bwana na kwa hiyo wote waliunguzwa na kuteketezwa na moto ulioshuka toka mbinguni kwa Mungu. 

Wao hawakupata kuingia na kuhusiana maramoja na Mungu kama   faida ya upekee na njia tunayo sisi wakristo wa siku za leo. 

Moto yao ya kigeni haikuwapa wakati ya kuhusiliana na kukaribia Mungu. 
Sisi tunafaida ya upekee zaidi ya ile Nadabu na Abihu walikuwa nayo. 


12/ Sasa tuone mambo mazitomazito katika Walawi 16   

Kiisha ajali hiyo, Mungu aliamuru Musa aoneshe ndugu yake Haruni namana gani anapashwa fanya hiyo huduma yake ya sadaka na toleo kwa zambi, mara moja kwa mwaka juu ya kufunika zambi ya wana waisraeli.  

Na sadaka hiyo juu ya zambi inapashwa kuwa kwanza kwa yeye kuhani, juu ya zambi zake kama kuhani na kiisha kwa wana wa israeli wote. 
Hii sadaka inapashwa kuwa ya damu na ifanywe na angalisho kubwa na kama sivyo, Haruni anaweza kufa. 

Haruni angaliweza kufa. 
Nikusema kwamba kuhani mukuu, alikuwa akiingia katika Hema la kusanyiko na kuingia pa mahali patakatifu pa patakatifu kwa kutowa sadaka ya matengenezo akiwa mwenye woga nyingi na mwenye kutetemeka.   

Lakini sisi waliokombolewa kwa siku za leo tunakaribia Baba Mungu kwa juhudi na ujasiri, bila woga na shaka lolote sababu tuna uhusiano na Mungu Baba bila mpaka. 

13/ Tufahamu kweli kama hapa kiongozi wetu ni Roho Mutakatifu 
Na ni Yeye analeta muyuda na mutu wa mataifa, wote wawili anawaleta mbele ya macho ya Mungu Baba. 

Neno njia ya kuhusiliana ni kweli neno ya kigeni. 
Katika utafsiri wake wa musingi inamaanisha kuingia maramoja, kusimama mbele ya Mufalme. 

Hapo tunayo neno la kuonesha kwamba ni Roho Mutakatifu yeye pekee njo anayo hii uwezo ya kutuingiza na kutushimamisha mbele ya Mufalme na Muumbaji wa mbingu na dunia yote, Mungu Baba. 

14/ Tuangalia kwa haya ya kumi na saba, Waefeso 2: 17 

Kwa siku za kale faida hii ya upekee haikuweko, lakini kwa sasa sisi tunayo. 
Twende sasa kwa haya ya kumi na kenda, 19 tuna jambo lingine la mafaa lenye tunaona hapo. 

Basi tangu sasa ninyi si wageni na wasafiri tena, lakini wenyeji pamoja na watakatifu, na watu wa nyumba ya Mungu. 

Hii neno haingeli wezekana kwa siku za kale. Wana wa Israeli hawakuionja. 
Wana wa Israeli hawakuishi hii tumaini la Baraka na hawangi kuwa hata na wazo lolote lakuzania kama neno hili ingekuwa kweli kwao. 

15/ Kunakuwa watu wanao tuambia kama hatutaenda mbingini, wanasema sisi tuko tu taifa la wana wa Israeli kwa Imani. Kwa kweli wewe unaamini hiyo? Hii siyo kweli kama tukichunguza maandiko matakatifu Kuna maneno mawili yenye iko kwetu ya muhimu na ya mafaa sana ni: 

“Basi” na “tangu sasa”. 

Kwa kusadiki na kutia maneno haya kuwa ya musingi, sisi sasa ni wenyeji pamoja na watakatifu na wenyeji wa mbinguni. 
Neno “pamoja na watakatifu” 

Ni TONE – HOG – GEE- OWN, inamaanisha KUJISIKIA NA KUJIPATIA UTU NA MANUFAA YA UZITO WAKO. 

Inamaanisha tena mutakatifu kuliko watakatifu wote. Sisi ni wenyeji wa mahali patakatifu kuliko utakatifu wote. Na tutajisikia tumekumbwa na hii hali wakati tunaposoma 

Waebrania 9: 8   

“Roho Mtakatifu akionyesha neno hili ya kuwa njia ya kuingia Pahali Patakatifu haijafunguka wazi bado, hema ya kwanza ilipokuwa ingali kusimama.” 

Pahali tunapo soma kwamba Roho Mtakatifu…, nikusema njia yenye kutuongoza kuingia pahali patakatifu pa patakatifu ni kusema pahali patakatifu sana na hapo tunafahamu kwamba ni mbinguni. Ni pahali pa takatifu kupita ulimwengu wote. Ni pahali pasipo kuwa taka, ama viozo, pahali mambo, tabia, na hali chafu haikuweko, pahali pasipo zambi. 

Ni pahali Mungu anapokaa. Ni kwa hiyo, sisi ni wenyeji wa mahali patakatifu nikusema sisi ni wenyeji wa mbinguni. 

16/ Tusome sasa haya ya makumi mawili. 

“Sisi tumejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kubwa la pembeni.” 
  
Kuna watu wanaofundisha kwamba manabii wanaotajwa hapa ni wale wa Agano la kale na mitume wanaotajwa hapa ni wale mitume kumi na wawili  wa Bwana Yesu Kristo. 
Kwa kweli haiwezikane iwe hivyo sababu tuko tunazungumuzia Siri yenye haikujulikana kwa wakati wa kale. 

Neno linaloweza kuwa la mafaa hapa ni kuangalia kwanza katika hii neno mbili gani inapangwa ya kwanza kiisha ingine. 
Kwa namna ya desturi ingelikuwa kwanza manabii, kiisha njo mitume wangelitajwa. 

Tusome 2 Petro 3: 2 

“mupate kukumbuka maneno yaliyosemwa zamani na manabii watakatifu, na amri ya Bwana na Mwokozi iliyoletwa na mitume yenu.” 

Hapo tunakuta namna hayo majina mawili yanapashwa kupangwa, kwanza manabii wa Agano la kale njo wanakuja kwanza, kiisha mitume wanafwata. Ona utaratibu ule wa kupanga hiyo maneno mawili. 

Tusome sasa Waefeso 4: 11 

“Naye alitowa wengine kuwa mitume; na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wahubiri wa habari njema; na wengine kuwa wachungaji na walimu;" 

Hii ni zawadi ya karama tu inayo tuonesha wazi wazi kama Kristo anamiliki Mwili wake, Kanisa lake. 

17/ Waefeso 2: 21 - 22  

“Katika yeye jengo nzima linaunganishwa vizuri na kukua hata lipate kuwa hekalu takatifu katika Bwana. Katika yeye ninyi vilevile munajengwa pamoja kuwa kao la Mungu katika Roho.” 

Hapa tunapata neno moja nzuri inayo tuonesha “sura ama picha” yenye watu wa Efeso walianza fananisha. Na mawazo yao iliona picha ya hiyo hekalu kubwa iliyo kuwa katika muji wao sababu ilikuwa hekalu kubwa waliojenga kwa mawe na ni fasi walikuwa wanaabudu mungu wao Diana kwa miaka mingi iliyopita na wao walikuwa na abudu huyo mungu wao Diana na walizani kwamba yeye alitokea inje ya dunia kwa jupiter. Sasa waliposikia neno lile la hekalu mawazo yao ilipata picha hiyo na walizani kwamba hiyo Hekalu ni hiyo inayopatikana kule kwao Efeso.   

Ni kwa hiyo mutume Paulo alitumikisha hiyo mfano na kweli aliona Roho Mutakatifu akiwa akijenga Hekalu hili likijengwa na mawe yaliyo hai na mawe haya ni kila mwamini aliye okolewa akiwa akiunganishwa kwenye jengo kama jiwe linalojengwa na Roho Mutakatifu, yeye pekee akiwa mujengaji mkuu akijenga Hekalu hili kubwa na watu wakristo kutoka inchi mbalimbali, Marekani(USA), Canada, Mexiko, … inchi mbalimbali kutoka dunia nzima na kujenga Nyumba na kao ya Mungu, Hekalu hiyo kubwa. 

18/ Raha gani kuwa kiungo cha Hekalu hili la Mungu, kao na Nyumba ya Mungu hapa duniani. 

Hii ni neno kubwa lenye kwa siku za kale haikuwa lenye linaweza kufikiriwa kama ni kweli, lakini kwa siku ya leo hiyo ni ukweli. 

Tushukuru Mungu kwa kubomoa hiyo kiambaza ama ukuta wa uadui na matengano.  

AMEN

N°Ref: 01/3/1960 / #203 BOLDLY, THROUGH THE BLOOD / KWA JUHUDI NA UJASIRI KUPITIA DAMU / 1/7/2020