Wednesday, February 17, 2021

MAJIFUNZO KATIKA SHERIA Sehemu ya Tatu STUDIES IN LAW Part III

Photo by B Smith from Patio


 

 

MAJIFUNZO KATIKA SHERIA Sehemu ya Tatu 

STUDIES IN LAW Part III 

Pastor Henry F. Kulp 1976 



 

Waroma 5: 12 – 14 

“Hivi kama kwa mtu mmoja zambi iliingia ulimwenguni, na kufa kwa njia ya zambi; na hivi kufa kulikuja juu ya watu wote, kwa sababu wote wamefanya zambi: - maana mbele ya sheria zambi ilikuwa ulimwenguni; lakini zambi haihesabiwi wakati sheria isipokuwa. 

Lakini kufa kulitawala tangu Adamu mpaka Musa, hata juu ya watu wasiofanya zambi kama alivyofanya Adamu, aliye mfano wake yeye atakayekuja.” 

Tunapata hapa watu wawili: Adamu na Musa. 

Kwa aya ya kumi na mbili tunapata ulimwengu wa zambi(zambi kutawala wote ulimwenguni) na ulimwengu wa kufa(kufa kutawala wote ulimwenguni). 

“Kwa njia ya mtu mmoja zambi iliingia ulimwenguni na kwa njia ya zambi ya yule mtu mmoja watu wote walifanya zambi na watu wote wanakufa.” 

Tunafikia sasa kwa jambo la muhimu sana inalomupasa kila mtu kufahamu. 

Kwa sababu gani wewe ni mwenye zambi? 

Kwa sababu gani mimi ni mwenye zambi? 

Sababu gani inasemwa kwamba: 

“Wote wamefanya zambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu?” 

Yanayosemwa ndani ya Waroma 3: 23 

Hayahusu zambi ilizozifanya na mtu yeye peke binafsi, hapa inahusu  zambi ya asili. 

Yatupasa kufahamu kwamba: 

Kila mmoja wetu alifanya zambi wakati Adamu alipo anguka na kufanya zambi. 

Adamu aliangusha uzao wa wanadamu wote ndani ya zambi. 

Wakati alipofanya zambi, mimi na wewe tulifanya zambi. 

Yeye ni baba, kichwa cha uzao cha wanadamu wote. 

Tunaita haya Matunzaji ya uwakilishi

Sote tulifanya zambi ndani ya Adamu. 

Pale pale mmoja wetu anaweza kusema ya kwamba: 

“Nazani hiyo siyo halali, namna gani mimi naweza kuwa mwenye zambi kwa sababu Adamu alitenda zambi?” 

Ni hasara kubwa sababu yale unayokuwa nayo kama mawazo ni kupingana na Mwenyezi Mungu. 

Mwenyezi Mungu anasema kwamba sote tulifanya zambi ndani ya Adamu. 

Jameni, niwasomee tena Aya ya 12: 

“Hivi, kama kwa mtu mmoja(aliye baba wa uzao wa wanadamu wote) zambi iliingia ulimwenguni, na kufa kwa njia ya zambi; na hivi kufa kulikuja juu ya watu wote, kwa sababu wote wamefanya zambi:-“ 

Maandiko haya yatasomeka ifwatavyo: 

“Kwa maana wote wamefanya zambi” hii ndio utafsiri wa Kigriki, “wote wamefanya zambi”, siyo “wote walifanya zambi.” 

Hapa haihusu zambi kila mmoja wetu aliyoyafanya kwa binafsi, hii inahusu zambi ya asili. 

Wote wamefanya zambi wakati Adamu alifanya zambi. 

Zambi ya Adamu ilikuja juu yetu sisi sote, ni kwa sababu hiyo, sisi tunakufa.  

Kama ingaliwezekana wewe bado kutenda zambi, hata  tu zambi moja, fahamu kwamba hata hivyo wewe ni mwenye zambi tu. 

Wewe ni mwenye zambi kweli.

 Aya ya 13 ni ya muhimu sana kwetu: 

“maana mbele ya sheria zambi ilikuwa ulimwenguni ; lakini zambi haihesabiwi wakati sheria isipokuwa.” 

Maana mbele ya sheria zambi ilikuwa ulimwenguni, hiyo inamaanisha nini? 

“Maana mbele ya sheria” 

Mtume Paulo anahitaji kusema nini? 

Anatuambia kuhusu Torati ama Sheria ya Musa, miaka 2500 tangu Adamu mpaka kufikia Musa. 

Kwa kufwatana na mpangilio ya nyakati, Tangu Adamu mpaka Musa “zambi ilikuwa ulimwenguni”, hapa inahusu zambi ya kila mtu binafsi. 

Wote wamefanya zambi ndani ya Adamu, bali “zambi ilikuwa ulimwenguni tangu Adamu mpaka Musa.” 

Tangu Adamu mpaka Abrahamu, hapa tunapata kikundi cha Mataifa wenye zambi. Tuna Taifa moja na luga moja. 

Miradi ya Kiyuda inazaliwa tangu Abrahamu hadi Musa. Taifa moja na luga moja. Hapo Mataifa mengine Wapagani walikuwa na lugha mbalimbali. 

Walisambazwa na wakapewa lugha mbalimbali. 

Kwa hiyo mwafahamu kwamba tangu Adamu hadi Musa, tulikuwa na eneo mbili tofauti: 

Kulikuwa Kundi la Mataifa wote Wapagani waliokuwa Taifa Moja wakiwa na lugha moja. 

Kwa ngambo ingine  tangu Adamu mpaka Musa, kulikuwa Taifa moja ikiwa na lugha moja iliyo ya Kihebrania. 

Katika muda wote wa nyakati hii hakukukuweko Torati ya Musa. 

Jameni, kuna kasoro moja watu wengi wanafanya wakitumbukia ndani ya kosa kwa sababu wao hawafahamu kwamba katika Biblia Takatifu kunapatikana sheria mbalimbali.  

Washika Sabato, wa Mormoni, wakati wanasema juu ya sheria, wao wanazania kwamba ni “Sheria ya Musa.” 

Hiyo siyo ukweli. 

Waraka wa Waroma inakuwa na aina tano ya sheria. 

Tusome kiatabu cha Waroma 8: 2 

“Kwa sababu sheria ya Roho ya Uzima ulio katika Yesu Kristo imenifanya huru kwa sheria ya zambi na kufa.” 

Jameni, muniruhusu niwafahamishe sheria gani ilikua ikitumika kwa nyakati ya kutoka tangu Adamu mpaka Musa.  

Kulikuwa sheria yenye ilikuwa ikitumika katika wakati  huo.

Tusome tena kwa makini sana Andiko hili la Waroma 8: 2  


Waroma 8: 2 

“Kwa sababu sheria ya Roho ya Uzima ulio katika Yesu Kristo ilinifanya namna gani? 

Imenifanya kuwa huru, huru kwa nini? Kwa sheria. Sheria gani? Sheria ya zambi na kufa.” 

Kulikuwa sheria yenye ilikuwa inatumika wakati huo na sheria hiyo ilikuwa mbalimbali na Torati ya Musa. 

Toka Adamu mpaka Musa, kulikuwa sheria iliyokuwa inatumika, ni sheria ya zambi na kufa. 

Ni wakati gani sheria hii ya zambi na kufa ilipoanza? 

Turudi katika Kitabu cha Mwanzo, wakati Mwenyezi Mungu alikuwa anazungumuza na Adamu. 

“kama utakula kwa muti wa kujua mema na mabaya, siku ile utakalokula utakufa.” 

Adamu alitwaa tunda la muti ule na kula na Adamu akakufa kiroho na nyuma ya miaka mia kenda, Adamu akakufa pia kimwili. 

Mwenyezi Mungu hakumuumba Adamu ili afe. 

Ni kwa saa ile ile lenye Adamu alikula tunda lile, ni kwa saa ile ile ndiyo sheria ya zambi na kufa ilianza kutenda kazi yake, watu wote wakafa, ila Enoki peke yake ndiye aliyenyakuliwa. 

Sheria ya zambi na kufa ilikuwa ikitenda kazi tangu Adamu mpaka Musa, na hata hivi, sheria hiyo inaendelea kutumika tangu Musa hadi siku za leo.    

Kila yule anayezaliwa hapa chini ya jua, anazaliwa ili siku moja afariki.

Wakati wa kuzaliwa kwa mtoto mchanga, anatoa sauti ya kulia, na ni pale pale anaanza safari yake ya kuelekea kufa. 

Sheria ya zambi na kufa.

Mtume anapenda kusema nini hapa? 

Turudi katika Maandiko yetu ya Waroma 5: 13 

“maana mbele ya sheria(Torati ya Musa) zambi ilikuwa(wapi?) ulimwenguni.” 

Tuchunguze yanayosemwa katika Aya ya 14 

“Lakini(nini?) kufa kulitawala tangu Adamu mpaka Musa” 

Kufa kulikuwa mfalme, mwatambua hiyo? 

Kufa kulikuwa kukitawala, kufa kulikaa katika kiti chake cha enzi. 

Wakati tutafika kwa sehemu za mwisho wa majifunzo yetu, nitawaonesha aina ine ya wafalme  tuyopata katika Waroma sura 5, mwawajuwa wale wafalme? 

Wafalme wane wanaomiliki. 

Hapo tunaona kufa inayomiliki. 

Kufa inatawala tangu Adamu mpaka Musa, kwa sababu sheria ya zambi na kufa ndiyo yenye ilikuwa inafanya kazi. 

Sasa turudi kwa aya ya 13 na tujaribu kufahamu nini Mwenyezi Mungu anayosema hapo. 

maana mbele ya sheria zambi ilikuwa ulimwenguni; lakini zambi haihesabiwi wakati sheria isipokuwa.”

Kumbukeni yale tuliyoyasema kuhusu maana ya neno “kuandikiwa juu ya mtu fulani, ama kuhesabiliwa juu ya mtu fulani.” 

“haikuwa inahesabiliwa juu yao”, sawa sawa na namna inavyosemwa katika Filemono : 18, wakati Mtume Paulo anasema: 

“na kama amekukosea, au kuwa na deni, uandike hii juu yangu.” Kwa kumaanisha kwamba, “usiihesabu juu yake,” 

Hiyo inamaanisha nini? 

Sheria ya zambi na kufa ilikua ikitawala, watu walikuwa wakitenda zambi ya upekee. 

Kaina alimuua Abeli. 

Vurugu ilikuwa duniani katika siku za Noa.

Sasa, ni nini analohitaji kutufahamisha? 

zambi haikuhesabiliwa, nikusema zambi za kila mtu binafsi hazikuwekwa juu yake” 

Nazani sasa hapo tuna Utunzaji wenye kila mmoja wetu anayofahamu. 

Wakati Bwana Yesu Kristo alipokufa, Yeye hakufa tu juu ya zambi zako za kibinafsi, angelifanya hivyo, haingelikuwa na manufaa yoyote, 

Bwana Yesu Kristo alikufa kwa ajili ya zambi zako za asili ulizoriti toka Adamu. 

Ni jambo hili ndilo wengi wa watu hawatambuwi.  

Utaona Mwinjilisti anahubiri dakika 50 juu ya zambi na anahubiri dakika 3 juu ya Yesu Kristo.  

Bila shaka, zambi iko, lakini kiini ya neno hapa siyo jambo la zambi za mtu binafsi,  sababu ni zambi ya asili ndiyo inayokuwa chemichemi ya zambi ya mtu binafsi. 

Ni nini inayo nisukuma mimi kufanya zambi? 

Ni kwa sababu ndani mwangu munamo chanjo ya mbegu ya zambi. 

Ni kwa hiyo, Mtume Paulo anasema ndani ya Waroma 7:15 

“Maana sijui ninalofanya, kwa sababu lile ninalopenda kufanya, silifanyi; lakini lile ninalochukia, ninalifanya.” 

Kuna kitu ndani mwangu: 

Nina utu wa zamani wenye asili ya zambi nilioriti toka Adamu

Adamu alifanya zambi, nami nilifanya zambi pamoja naye, na aliniachia asili yake ya zambi, Asili ya Adamu. Na mwafahamu ni nini iliotukia:  

Ilimupasa Bwana Yesu Kristo akufe kwa ajili ya zambi hiyo.

Kwa hivyo twafahamu nini? 

Hadi kuifikia Torati ya Musa, sheria ya zambi na kufa ilikuwa ikitumika na kila mtu alikua na asili ya Adamu, na sote tulikuwa tukifa kiroho na kimwili

Yeyote yule aliyezaliwa ulimwenguni, alikuwa mfu kiroho. 

Mushike sana yafwatayo: 

Hiyo haikuwa inamaanisha tu kifo ya kimwili, bali pia kifo ya kiroho. 

Sote tunazaliwa tukiwa wafu. 

Kaina na Abeli walizaliwa wakiwa wafu  kiroho. 

Seti alizaliwa akiwa mufu kiroho, Abrahamu, Musa, Yakobo walizaliwa wakiwa wafu kiroho, na walihitaji wokovu. 

Walipata wokovu wao kwa njia ya sadaka ya kuchinjwa. 

Waliweka imani yao ndani ya damu iliyomwangika toka sadaka ya kuchinjwa. 

Tunaambiwa hapa kwamba, hadi kufikia Torati ya Musa, Mwenyezi Mungu hakuwahesabia zambi walizozifanya kila mtu binafsi. 

Wao walikuwa wafu  kiroho na walifikia kufa vile vile kimwili sababu ya zambi walizoriti toka Adamu. 

Sababu gani Sheria ililetwa kwa watu? 

Ujiuluze sasa ulizo lile. 

Sababu gani Mwenyezi Mungu aliwapatia watu Torati za Musa? 

Tuchunguze hiyo kwa mwangaza wa Maandiko Matakatifu. 

Kwa kufahamu mafaa ya sheria, tusome Waroma 5: 20  

“Lakini sheria iliingia, ili zambi ziwe kubwa sana; lakini pahali zambi zilipozidi, neema ilizidi zaidi sana;” 

Sheria iliingia kusudi zambi za kila mtu zihukumiwe. Ni kwa sababu hiyo  njo maana Amri kumi ilipewa kwa watu. 

Amri kumi iwe kingo la kukuzuiza na kukuwezesha kuwa na kiasi katika matendo yako maishani mwote. 

 Kila mmoja wetu anayekuwa na zamiri safi anafahamu ya kwamba ni vigumu sana kutii Amri zote kumi kwa jumla, bila kuvunja hata moja. 

Amri kumi ilitolewa ili zambi za kila mmoja wetu ziwekwe wazi hazarani. 

Tusome Waroma 3: 19 

“Na tunajua ya kama maneno gani inayosema sheria, inasema kwa walio chini ya sheria; kusudi kila kinywa kifungwe, na ulimwengu wote uwe chini ya hukumu ya Mungu.”  

Kwa sababu gani Mwenyezi Mungu aliwapa wana wa Israeli Sheria? 

Ilikuwa tu kwa Israeli peke yake? HAPANA. 

Kusudi kila mtu awe chini ya hukumu mbele ya Mungu

Mwaona, Mwenyezi Mungu ni Mwenye Haki na Mukamilifu. 

Hakukukuweko sheria, Amri kumi za Mungu, Sabbato, wakati Mwenyezi Mungu aliwasiliana na watu kwa wakati wa tangu Adamu mpaka Musa, Mungu alisema:

“Kwa kweli mutakufa kimwili na kiroho, na mutakufa kimwili kufwatana na Adamu, na pendekezo, na matetezi ya watu hapa duniani haita badirisha, hata neno lolote.” 

Wote wanakufa ndani ya Adamu; 

Wote ni wafu wa kiroho ndani ya Adamu na walizaliwa katika hali hiyo. 

Bali, tangu Adamu mpaka Musa, Mwenyezi Mungu akasema: Sitawahesabia zambi zao za kibinafsi, nitahesabu tu zambi yao ya asili. 

Lakini wakati sheria ilipoingia, 

Sheria ilikuja kuonesha watu wote kwamba wao walikuwa wenye zambi. 

Kuonesha watu wote kwamba wanahitaji Neema ya Mungu. 

Kuonesha watu wote kwamba mbali na Yesu Kristo, hawana matumaini ingine. 

Yote ni kwa njia ya Neema kupitia imani ndani YAKE. 

Ndugu zangu, sheria iliingia ili wote wawe wenye kuhukumiwa. 

 Tusome Wagalatia 3: 24 

“Vivyo torati ilikuwa mwalimu wa kutuleta(kutuleta ni neno moja la muhimu sana, kuleta wanani? Mataifa Wapagani? Hapana, Wayuda) kwa Kristo, tupewe haki(namna gani na kwa jia gani?) kwa imani.”  

Siyo kwa matendo ya watu, kutahiriwa si kitu. 

Kuweka kando matendo yote ya watu: kutahiriwa ikiwa tendo la kuondosha sehemu ya mwili na kuitupa inje. 

Ndugu yangu, yatupasa kufahamu kwamba sisi tuko ginsi tulivyo kwa sababu ya Adamu, na kama hauamini hivyo, wewe unakanusha Biblia, hausadiki Biblia. 

Tuko namna tulivyo kwa sababu ya Adamu. 

Sisi hatuko wenye zambi sababu tulifanya zambi, bali, tuko wenye zambi sababu sote tulifanya zambi ndani ya Adamu, na ni kwa hiyo ndiyo maana tunatenda zambi kwa sababu sisi ni wenye zambi. 

“Sote ndani ya Adamu tunakufa” 

Kwa siku za leo, Mwenyezi Mungu anahesabia kila zambi kila mtu anayotenda kwa binafsi. 

Sote, yawezekana kuna mara tulitenda zambi. 

Kwa sababu gani Kaina hakupata hukumu ya kifo? 

Sawa vile tulivyoona siku iliyopita, ni tangu agizo la Mwanzo 9, hadi siku za leo hukumu ya kufa inaendelea  KUTUMIKISHWA

Kila Inchi yenye haitumie hukumu ya kufa, nazani hukumu ya Mungu iko juu ya inchi ile. 

Kiini cha Inchi yetu kuwa kama vile munavyoiona leo, ni kwa sababu haitumie hukumu ya kufa. 

Tuchunguze na kuangalia inchi zenye zinatumia hukumu ya kufa. 

Tuangalie mambo iliyofikia Ungereza. 

Ungereza ulianza pata anguko kweli wakati ulizidi sana kutumia kupita kiasi hukumu ya kufa. 

Hiyo ni kuzarau na kuto kuheshimu Mungu: 

“Yeye anayemwanga damu ya mtu, kwa mtu vilevile damu yake itamwangwa; kwa sababu alifanya mtu kwa sura ya Mungu.” 

Tunayo sasa sheria yenye haikupewa kwetu sisi, bali, sharia iliingia ili ioneshe wazi zambi za kila mtu ili vinywa vyote vifungwe na sote tuhukumiwe mbele za Mungu. 

Sisi sote tuko wenye zambi. 

Inayotupasa kufanya ni kujiangalia ndani ya sheria kama kioo na kuweka ndani vichwa vyetu na kweli kwa mweisho tujikuta uchi na kupata haya, sababu hakuna kitu njema tunayofanya. 

Ni kwa hiyo imesemwa kwamba: 

“Haki yetu yote ni kama (kama nini?)  vipande vichafu vya vitambaa.” 

Sote, ndani ya Adamu tunakufa, na kwa siku za leo, zambi zetu za kila mmoja kwa binafsi zinahesabiwa. Zinawekwa juu yake. 

Bali zambi hizo hazihesabiwi tena kwetu baada ya nini? 

Baada ya kumwamini Bwana Yesu Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yetu.    

Tuisome tena kwa ushujaa wote. 

Tusome tena ndani ya Waroma 5. 

Mtume Paulo anayasema kwa utaratibu na kwa hali sambamba, sawa vile nilivyowaambia juma iliyopita kwamba kutaka kwangu ni kwamba ingelikuwa heri kila mmoja aketi na kushiriki kwa  muda wa saa tatu kila mara katika  majifunzo hii, kweli ni yenye kuleta mchoko bali ni furaha sana kufahamu mawazo ya Mungu katika maandiko haya. 

Waroma 5: 14 

“Lakini kufa kulitawala tangu Adamu mpaka Musa, hata juu ya watu wasiofanya zambi kama aliyofanya Adamu, aliye mfano wake yeye atakayekuja.”  

(Neno lile “yeye” ina maana nyingi sana, lakini kwa leo hatutakuwa na muda kwa mambo yale, ningelitamani kuya fafanua bali muda ni mdogo sana.) 

15. Lakini zawadi ya neema haikuwa kama lile kosa. 

Kwa maana kwa kosa la mtu mmoja wengi walikufa, zaidi sana neema ya Mungu, na zawadi kwa njia ya neema ya mtu mmoja, Yesu Kristo, imezidi kwa watu wengi.”   

Shangwe kubwa gani! 

Yesu Kristo ndiye Jibu, Adamu wa mwisho, Mtu wa pili. 

Yeye alikufa na kuweka kando laumu yetu. 

Asili ya zambi ilikufa kwa njia ya Kufa kwa Yesu Kristo, na ni kwa njia hiyo ndiyo analipa zambi za kila mmoja wetu binafsi, akizivuta zote na kuziondosha kweli, na tunafanywa kuwa wenye haki wa Mungu katika Mpendwa wetu.   

Acheni sasa niwaoneshe jambo moja katika Aya ya 14

Waroma 5: 14 

“Lakini kufa kulitawala tangu Adamu mpaka Musa, hata juu ya watu wasiofanya zambi kama alivyofanya Adamu, aliye mfano wake yeye atakayekuja.”  

Twende kwa aya ya 21 na tuvumbue aina ya wafalme wanao miliki na kutawala. 

Waroma 5: 21  

“hata, kama vile zambi ilivyotawala katika kufa, hivi kwa njia ya haki neema itawale hata uzima wa milele kwa Yesu Kristo Bwana wetu.”  

Kama vile (nini) zambi ilivyotawala, kufa kuko kunatawala (hayo mambo inasemwa katika nyakati zilizo pita), angalia namna inavyosemwa kwa aya ya 14: “Lakini kufa kulitawala.”(Nyakati iliyopita)  

Tushuke hapo chini kwa aya ya 21. 

“hata, kama vile zambi ilivyotawala katika kufa, hivi kwa njia ya haki (nini?) neema itawale hata uzima wa milele kwa Yesu Kristo Bwana wetu.”  

Tunapata kufa kunatawala, zambi inatawala na neema inatawala.

Turuke hadi aya ya 17. 

Waroma 5: 17 

“Kwa maana kama, kwa njia ya kosa la mtu mmoja, kufa kulitawala kwa ajili ya mtu mmoja, zaidi sana wao wanaopokea neema ya kuzidi sana na zawadi ya haki watatawala katika uzima kwa yule mmoja, Yesu Kristo.” 

Kwa maana kama, kwa njia ya kosa la mtu mmoja, kufa kulitawala(hapo tunapata tena tendo kutawala), kwa njia ya mtu mmoja, 

zaidi sana wao wanaopokea (nini) neema ya kuzidi sana na zawadi ya haki watatawala katika uzima kwa yule mmoja, Yesu Kristo. 

Hapa tunaona mwamini anatawala, kufa kunatawala, zambi inatawala, neema inatawala na mwamini anatawala. 

Wafalme wane: 

Kufa kulikuwa mfalme, zambi ilikuwa mfalme, kwa sasa neema ni mfalme na mukristo ni mfalme

Wote wanatawala kwa sababu kwa njia ya Mtu mmoja Yesu Kristo, kazi ya mtu mmoja Adamu ilibomolewa. 

Ni raha kubwa gani kumjua Yesu Kristo. 

Ndugu mpendwa haiwezikani tena wewe kutia Imani yako katika kitu fulani, ama kuamini mtu mwengine, amini tu Bwana YESU KRISTO. 

AMINA. 

N°Ref: 1976 / 005 - STUDIES IN LAW Part III / 02/17/2021

No comments:

Post a Comment