Wednesday, February 17, 2021

MAJIFUNZO KATIKA SHERIA Sehemu ya Kwanza / STUDIES IN LAW Part I

Photo by B Smith from the Patio


 


MAJIFUNZO KATIKA SHERIA 

Sehemu ya Kwanza 

STUDIES IN LAW Part I  

Pastor Henry F. Kulp (1976) 



 

Waroma 5: 12 – 13 

“Hivi kama kwa mtu mmoja zambi iliingia ulimwenguni, na kufa kwa njia ya zambi; na hivi kufa kulikuja juu ya watu wote, kwa sababu wote wamefanya zambi: - maana mbele ya sheria zambi ilikuwa ulimwenguni; lakini zambi haihesabiwi wakati sheria isipokuwa.” 

Tujuwe kwamba majifunzo yetu kuhusu neno hili sharti itachukua muda wa kutosha na kwa kweli, tutahesabu ma jumaa kazaa. 

Mumesikia namna msemwa huu unatamkwa katika maandiko yafwatayo: 

“maana mbele ya sheria zambi ilikuwa ulimwenguni; lakini zambi haihesabiwi wakati sheria isipokuwa.” 

Kwa sasa, nitawafahamisha neno moja. 

Mimi binafsi, nilijitahidi kwa nguvu zangu zote kwa miaka mengi sana kujaribu kuelewa Maandiko haya. 

Maandiko haya, yana maana gani? 

Tangu Adamu mpaka Musa kuna kiwango cha miaka 2500. 

Na wakati huu unagawanyika katika sehemu mbili: 

Sehemu ya kwanza ya nyakati hili ni tangu Adamu mpaka Noa, na hapo tunafika kwanye Garika. 

Sehemu ya pili ya nyakati hili ni tangu Noa mpaka Musa. 

Sehemu hizi mbili zinagawanywa kwa pande mbili na Garika, moja ikiwa mbele ya garika na lingine likiwa kiisha garika. 

Na hapo, Mwenyezi Mungu anasema ya kwamba kwa muda huu wote wakati sheria haikukuweko, yaani hakukukuwa bado sheria yoyote, bali kwa nyakati ile kulikuwa utaratibu ama kanuni ya zambi na kufa, lakini Torati ya Musa, ama Sheria Kumi haikukuweko bado. 

Na Mwenyezi Mungu anasema hapa ya kwamba: “Zambi haihesabiwi wakati hakuna sheria.” 

Sasa, munisikilize kwa makini sana. 

Tangu Adamu mpaka Noa na tangu Noa mpaka Musa, Mwenyezi Mungu alikua bado hajapana sheria, kwa muda huu sheria ilikua bado haijaingia na kweli hata kwa mimi binafsi, ilikua vigume kuhakikisha muda huo. 

Biblia nzima inagawanyika katika Nyakati mbili kubwa: 

Wakati wa SHERIA na Wakati wa NEEMA. 

Miradi ya kidunia na Miradi ya MUNGU. 

Sasa, muda huo tuliotaja hapo juu, twaweza kuutia katika nyakati gani? 

Tangu Adamu mpaka Noa na tangu Noa mpaka Musa. 

Watu walioishi kwa nyakati hiyo hawakuwa chini ya Sheria pia hawakuwa wanamemba wa Kanisa Mwili wa Kristo, hivi sasa yafaa tuwaweke katika nafasi gani? 

Kwa kusema kweli pasipo kuficha neno kwenu, swali hili lilinisumbua kwa muda wa miaka mingi. 

Kama unatamani kufanya utafiti katika vitabu mbalimbali vilivyoandikwa kuhusu swali hili, utapata tu majibu madogo madogo sana. 

Mimi binafsi nilinunua Kamusi za Biblia nyingi sana, lakini, kwa mwisho, niliziacha zote. 

Wakati ninapoongoza mikutano ya majifunzo na maulizo na majibu juu ya Biblia,   watu wengi wana kuja kwangu ili niwafahamishe ni gani Kamusi  la Biblia iliyo nzuri kutumia? 

Mimi sijawayi kupata Kamusi yenye kuleta musaada na lenye kuwa nzuri, sababu wakati unapo yachunguza yote utatambua ya kwamba, kila mara wanapofikia swali lililo ngumu; kitu wanachofanya ni kufunga macho na kuhepuka swali lile na kufanya sawa swali lile haliko. 

Ni shida kweli, kuna Kamusi  za Biblia chache tu zinazo jitahidi kuleta jibu ama maelezo  mafupi kwa maulizo yaliyo magumu.  

Sasa, Maandiko tuliyosoma hapo juu yanamaana gani? 

Jameni ni chamche mafikiri yenu kidogo. 

Tuchunguze sisi sote pamoja. 

“Zambi haiisabiwe pahali pasipo sheria” 

 Ulizo ni kwamba, watu wote walioishi tangu Adamu mpaka Musa, watu hawa je hawakupata hukumu ama malipizi ya makosa na zambi walizozitenda? 

Ni kusema kwamba wale watu wote walioishi kwa wakati ule waliokolewa? 

Na kwamba kiisha kufa kwa wale watu wote, eti hivi wanakaa mbinguni? 

Eti kunakuwa upatanisho wa kijamii kuhusu watu hawa? Wao hawakupata gazabu ya zambi walizozifanya? 

Nini twaweza kusema kuhusu jambari muuaji aliyeishi wakati ule?

Muuaji wa kwanza ni Kaina, nini iliyotukia kwa mtu huyu? 

Eti alipata kisasi cha tendo lake mbaya maishani mwake? 

Tuchunguze Maandiko haya: 

Tuyatafakari kwa makini na ujuzi wote na ningewasihi wote musikilize vema na kufuata na angalisho yote na mufanye yote iwezekanavyo ili musikose ama kuchelewa kwa muda huu wote wa juma tatu ama ine  ya Majifunzo haya tunayo

Sababu ningelitamani kila mmoja wetu apate kufikia kiwango ya kufahamu na kuelewa nyakati hizi mbele mimi nifike mwisho ya majifunzo haya. 

Ninaweza kuwahakikishia kwamba, walimu wengi kweli wanaruka na kuhepuka mafundisho haya. 

Turudi sasa kwa majifunzo yetu tukisoma aya yetu ya Waroma 5: 12

Waroma 5: 12 

“Hivi, kama kwa mtu mmoja zambi iliingia ulimwenguni, na kufa kwa njia ya zambi; na hivi kufa kulikuja juu ya watu wote, kwa sababu wote wamefanya zambi:-“ 

Maandiko haya ina maana gani? 

Jameni, tunaisha nyakati ambapo watu wengi hawatambui ni nini inayopitikana. 

Wale wanaoishi maisha ya “wataalam wa msingi na asili” wengi wao wanasema kwamba maisha inazidi kuharibika na kuzorota zaidi, ni maajabu kweli. 

Ya kushangaza ni kwamba, kitu ambacho hawatambuwi ni kwamba hawaelewi yanayofanyika ndani ya ufahamu wa watu katika ukweli wa kusadikia Maandiko Matakatifu yanayopatikana ndani ya Biblia Takatifu. 

Katika makanisa wanaojidayi kuwa Wachungaji wa mila za asili ya kidini, kuna mambo mawili yanayo tukia:  

Kwanza kuna wale wanaoitwa Wainjilisti Mamboleo. 

Watu wengi wenye hapo kale walikuwa wakisimama imara katika ukweli wa Biblia, kwa siku za leo, wamepotoshwa na kupotosha wengi wao. 

Nilisoma kitabu cha mwandishi moja maalum aliyekuwa hapo zamani akiheshimu na kuchunga mila na asili ya dini(sita taja jina lake sababu 95% ya watu wanaweza wakamutambua). 

Nilisoma kitabu chake kuhusu uumbaji, namna Mwenyezi Mungu alivyo umba vitu vyote.  

Baadaye, miaka kidogo mbele yake kuacha dunia alipotoshwa na kuandika kwamba yawezekana viumbe vilifanyika kwa njia ya nadharia ya mabadiliko.  

Mwafahamu sasa kwamba kuna wale  tayari wamekwisha  kupotoka na watu wa namna hii wamejaa katika makanisa mengi yenye hapo kale yalikuwa na msimamo wao ndani ya kuheshimu Biblia Takatifu, wakijidayi kuwa wanaochunga mila na asili ya dini na Biblia, lakini sasa wao kwa kweli, wamekwisha enda mbali na Maandiko Matakatifu.  

Kwa nini hivyo? 

Jibu ni kwamba watu hawa, pahali pa kuweka msingi safi wa imani yao ndani ya Maandiko Matakatifu, wao wanageuka na kuangalia na kusikiliza yale inayosemwa na wataalam wa dini na teologia. 

Wataalam wa vyuo vikuu, na ma yunivarsti wanawachekelea wakisema: 

“Wale ni wajinga, washenji, hawana elimu wala ufahamu wowote, hawana maadibisho…” 

Kwa yale matusi, wale wanaopotoshwa, hawafurahi kusikia matusi yale na wanaamua wao pia waonekane watu wa maana katika jamii na wanapotoshwa. 

Acheni niwape shauri: 

“Wakati watu wa dunia wanapotuhamakia na mazarau yote, ni ya muhimu kweli kuwatizama tu na macho na kubeuwa mambo yale yote. 

Kama tukitarajia kutukuzwa na wanadamu katika dunia hii ya leo, tutachanganyikiwa na kupotoshwa. 

Hali hii imewakokota wengi wa makanisa ya Wainjilisti mamboleo, wakishikamana na wazo la kuunda Chama cha umoja ya makanisa, ama kanisa la ushirika na umoja, kanisa la muungano wa makanisa katika kuchukuliana ndani ya  mila zote.   

Ya pili ni kwamba: 

Wandugu wale wa makanisa la ushirika na umoja, wanapendelea sana maombi ya usiku na waamini wengi wanakumbwa na desturi hiyo. 

Siku iliyopita nilikutana na Mume moja akiwa na mke wake, na wao, walinisimamisha njiani ili niwape jibu kwa swali lao. 

Waliniuliza, eti ni wewe Mchungaji KULP? 

Kwa zaidi ya miaka makumi mawili, tunafwata mahubiri yako kwa njia ya mitandao. 

Ulizo letu ni kwamba tunatamani kujuwa kama nawe vilevile, kwa juma jana ulifika pale Huntinglon, kwa hivyo, uliona yale makutano na umati wa watu zaidi ya watu 35000, hata ilipita kwa televijieni na ilikuwa mshangazo kweli, ilikuwa kivumbi na jasho na kweli haijafanyika hata fasi ingine duniani. 

Jibu niliyowapa ni kwamba: Yatupasa tu kuamini yale Biblia inayotuambia. 

Tuwe waamini katika makanisa inayokuwa na msingi wa kusadiki kwao ndani ya Maandiko Matakatifu. 

Kweli Wainjilisti Mamboleo wanatuletea mambo kazaa na kazaa bali hiyo siyo wajibu wa Kanisa. 

Tunahitaji kuwa na walimu wengi wanaofundisha Biblia. 

Sisi watu tuliookolewa yatupasa kusimama imara na kuweka msingi safi wa Imani yetu ndani ya Maandiko Matakatifu, Neno la Mungu. 

Jambo ni kwamba, ni muhimu sisi kupeleka Injili mahali pote na kuwa wainjilisti, lakini siyo mpaka kiwango cha kwenda inje na mbali ya Maagizo ya Maandiko Matakatifu na kwenda inje ya Mafundisho ya Biblia. 

Yoane 5: 45 

“Musizanie ya kama nitawashitaki ninyi kwa Baba; yuko mmoja ambaye anawashitaki ninyi, hata Musa, taraja lenu.” 

Wayuda kwa kweli walikuwa wanaweka imani yao yote ndani ya Musa. 

Walifahamu hakika kwamba Musa alikuwa mutu wa Mungu. Bali, sikiliza Maandiko ya fwatayo: 

Yoane 5: 46  

“Kwa sababu kama mungaliamini MUSA, mungaliniamini mimi; kwa sababu yeye aliandika habari zangu.” 

Ni nini Bwana Yesu anapenda kuwaambia? 

Bwana Yesu anawaambia wayuda ya kwamba: 

Kama ninyi Wayuda mungeliamini Musa munayetumainia katika mambo yote na kuwekea matumaini yenu yote, hivyo ninyi mungeliniamini mimi vilevile. 

Hapo munavumbuwa kwamba ni raisi sana kusema eti unaamini Biblia, lakini waamini kweli Biblia? 

Wengi wetu watasema : 

“Ninaamini kwamba Biblia ni Neno la Mungu”, lakini hawafahamu hata andiko moja. 

Yawezekanaje wewe uamini kitu chenye haufahamu hata kidogo? 

Hiyo ni kuamini tu ya rejareja. 

Wajitetea kwamba wewe waamini Biblia ni Neno la Mungu, bali, haujuwe hata nugta moja ya Maandiko Matakatifu. 

Hilo ni jambo la kushangaza. 

Ni haya ambayo Bwana Mungu anayowaambia wayuda. 

“Ninyi munajiita kwamba muko watu wa Musa, na Musa kweli ni mtu wa mafaa, lakini kama kwa kweli munaamini Musa, mungeliniamini mimi vilevile.” 

Twende sasa kwa aya ya 47, hapo tutapata neno moja la msingi. 

Yoane 5: 47 

“Lakini kama hamuamini maandiko yake, mutaamini maneno yangu namna gani?” 

Tuchunguze neno “Lakini” 

Ni nani anayeandika? 

Ni Musa. 

Vitabu gani Musa alivyoandika? 

Eti ni Matayo, Marko,Luka? Hapana. 

Maandiko ya Musa ni: 

Mwanzo, Kutoka, Walawi, Hesabu na Kumbukumbu la Torati. 

Hivi ndivyo Vitabu tano vya Musa. 

Vinaitwa kwa jina gani? 

Vinaitwa Torati ama  Vitabu vya Sheria. 

Ebu tuchunguze Maandiko yaliyo katika aya hii

Lakini kama hamuamini maandiko yake(Torati , Maandiko ya Musa, Vitabu vya sheria), mutaamini maneno yangu namna gani? 

Jameni, munifwate na kunisikiliza kwa makini. 

Wale wote wanaotupia kando kitabu cha Mwanzo sura 1 na 2, wakisema kwamba eti mambo yaliyomo hayakufanyika, ni hadisi tu fulani fulani zilizotungwa, na kwamba maana yake si namna inavyoandikwa, watu wale hawawezi kamwe kuokolewa.   

Mwenyezi Mungu anatufahamisha wazi wazi na kukujulisha wewe unayezania kwamba uumbaji ulifanyika kwa njia nyingine, wewe usiye sadiki kwamba Adamu ndiye mtu wa kwanza  aliyeumbwa na Mungu,  na kwamba yeye ndiye baba wa kizazi nzima, ni yeye ndiye baba aliye zaa watu wote ulimwenguni. 

Kwa hiyo, Bwana Yesu anasema ya kwamba: 

Lakini kama hamuamini Maandiko yake Musa, yale yanayopatikana katika Mwanzo sura 1 na 2, hamuwezi kamwe kuamini.    

Munatambua sasa kwamba wote wale wenye wanawaambia ya kwamba wao hawaamini historia inayokuwa katika Maandiko ya Mwanzo sura 1 hadi 5 kuhusu uumbaji, Garika, hiyo inamaanisha ya kwamba watu wale hawajaokoka. 

Hawaamini Bwana Yesu Kristo na hii ni wazi kweli. 

Acheni niwasomee tena maandiko yale ili mashaka yafukuzwe: 

“Lakini kama hamuamini maandiko yake, mutaamini maneno yangu namna gani?” 

Muniruhusu kwa dakika chache niende inje kidogo ya majifunzo yetu ya leo, ili niwape kumbukumbu ya mambo moja moja ya msingi iliyo ya maana: 

Kuna vijana wengi wanaokuja kuniona kwa nia ya kuniuliza maswali mengi inayo elekea Sayansi ya nadharia ya mabadiliko. 

Mutambue vijana wangu kwamba sayansi ya nadharia ya mabadiliko ndiyo kweli sayansi ya upumbafu ndani ya dunia hii. 

Sina mashaka wala woga ya kupinga na kuleta changamoto ya kuthubutu kwa kila mwalimu wa chuo kikuu anayefundisha kuhusu sayansi ya nadharia ya mabadiliko. 

Nasema hivi kwa sababu: 

Kuna mambo matatu yenye inayowapa uvuguvugu na hata hawana tafsiri yoyote ile, wakishindwa kuleta maelezo kwa kuyafafanua na hiyo inaonesha wazi kwamba sayansi ya nadharia ya mabadiliko ni upumbafu mtupu. 

Kwanza: 

Kuna mpito gani ya badiriko toka hali ya kutokuwako kitu chochote, hali ya utupu hadi kugeuka kwa hali ya maumbile? 

Hakuna hata nadharia moja ya mabadiriko yenye inayo fasiriya mpito huu wa kutoka kwa utupu na kufikia kuwa na maumbile.   



Uvuguvugu wa pili. 

Mpito wa badiriko toka mbegu la msingi hadi kufikia kwa kitu kinachoishi. 

Namna gani kubadirika toka kitu bila uzima, wala uwezo wa kutikisika na kufikia kwenye kitu kinacho tikisika. 

Namna gani kubadirika toka hali ya jiwe na kugeuka kuwa mnyama? 

Uvuguvugu wa tatu. 

Ya wezekana je kubadirika toka kwemye mnyama na kugeuka kuwa mtu? 

Sayansi ya Nadharia ya mabadiliko inashindwa kuleta hata mwangaza ndogo ama jibu moja kwa maswali hizo tatu. 

Kwa kweli sisi hatuna hata kitu chochote dhidi ya maswali hizo na pia kila mtu mzima mwenye akili timamu anafahamu ya kwamba hapo kale ulimwengu huu haukukuweko. 

Kila mtaalam wa sayansi anapendelea kujua mwanzo wa vitu vyote katika dunia, ulimwengu uko tangu nyakati gani?

Wanadamu wanatumia karboni 14 kwa kujaribu kujua tangu nyakati gani ulimwengu uliumbwa. 

Na wanasema kwamba ni tangu ma milioni elfu kumi ya miaka. 

Sasa ulizo ni hili, jibu lile bado haijajibu swali lolote, sababu ni nini ilikuweko mbele ya tangu ma milioni elfu kumi ya miaka? 

Mwanzo wa vyote ulikuwa namna gani? 

Uvuguvugu inawajaa kichwani, wanazunguka zunguka tu katika kutafuta kuunda jibu lenye hawana. 

Watu wale wa Sayansi wenye wanaamini Sayansi ya Nadharia ya mabadiliko wanasema kwamba kwa mwanzo kulikuweko mlipuko. 

Sasa ulizo, huo mlipuko ulisabatishwa na kitu gani?  

 Tukichunguza uvuguvugu huo wa pili. 

Namna gani kubadilika toka kwa kitu kisicho tikisika, kisicho na uzima na kufikia kitu kinachoishi, ama kitu kilicho na uzima. 

Watu hawa wa sayansi ya nadharia ya mabadiliko wanajitahidi juu na chini kwa kujibu swali hili wakishindwa mno. 

Acheni niwaoneshe jambo moja: 

Tusome pamoja katika kitabu cha Mwanzo 1: 24 

“Mungu akasema: Inchi iote kila kiumbe kilicho hai kwa namna yake; ngombe na matambazi na nyama ya inchi kwa namna yake; na ilikuwa hivi.” 

Tulete mwangaza kwa uvuguvugu wa pili kwa njia ya Aya hii tunalotoka kusoma. 

Mwanzo 1: 25  

“Mungu akafanya nyama ya inchi kwa namna yake, na ngombe kwa namna yake, na kila mtambazi juu ya udongo kwa namna yake; Mungu akaona ya kwamba ilikuwa vema.” 

Na Mungu akasema: 

Inchi itoe kila kiumbe kilicho hai. 

Sasa kama unakuwa na Biblia, tafsiri ya Scofied, pale pale utaona maana ya neno “kiumbe”. 

Ni nini? Nafsi, Nafsi. 

Wewe hautambuwi kwamba kila kiumbe kilicho hai kina nafsi? 

Watu wa zehebu inayojiita Mashahidi wa Yehova, wanapenda kupotosha watu kuhusu maana ya neno “nafsi”.  


Na wao wanauliza: 

Eti mwafahamu kwamba wanyama vile vile wana nafsi? 

Na wakati unaposikia maneno haya, waweka kikono yako juu ya kichwa ukishangaa sana. 

Ndiyo, wanyama vile vile, kweli wanakuwa na nafsi. 

Sasa, nafsi ni nini? 

Nafsi ni hali ya kujiongoza mwenyewe. 

Hiyo ndiyo inatofautisha vitu visivyo tikisika na wanyama. 

Ukiongoa mti na mizizi yake yote, ule mti utakufa. 

Tusome Matayo 8: 20   

“Yesu akamwambia: Mbweha wana pango, ndege za anga wana vioto, lakini Mwana wa watu hana pahali pa kulalisha kichwa chake.” 

Sasa chunguza tukio hili: 

Kama unaongoa mti ama furushi la majani, pale pale inakufa. 

Bali, unapomkimbiza mbweha toka pango lake, ama ndege toka kioto chake, atafanya nini? 

Atafanya yote yawezekanavyo ili arejee. 

Mwafahamu sasa? 

Wanyama wana uwezo wa kujiongoza wenyewe, wanatambua pango lao na wanatambua wenzao. 

Hii inatoonesha tofauti inayopatikana katika swali la uvuguvugu hule wa pili unaohusu kitu na nyama. 

Kitu ama vifaa haina nafsi, haina uwezo wa kujiongoza mwenyewe, bali mnyama ana huu uwezo. 

Sasa, tofauti gani iliyo kati ya mnyama na mtu? 

Sisi watu tunakuwa na nafsi, bali zaidi ya hiyo tuna nini ingine tofauti? 

 Sisi tuna ule ujuzi na ufahamu toka kwa Mungu. 

Tunakuwa na ufahamu wa kutambuwa mema na mabaya, tangu anguko letu. 

Mwatambua, ndugu zangu kwamba kuna shimo kubwa ya matengano yenye haiwezi kupata surulisho. 

Na kila mtu wa sayansi mwenye akili timamu atajihuzuru kupambana na maswali hizi, sababu kwa kweli, pahali pakuleta jibu, ni uvuguvugu mtupu ndiyo wanayoleta. 

Uvuguvugu na matengano kati ya utupu na vifaa. 

Uvuguvugu na matengano kati ya vifaa na vitu vilivyo hai 

Uvuguvugu na matengano kati ya wanyama wadogo wenye uhai na mtu. 

Maswali hayo hayawezi kamwe kupata jibu. 

Maandiko yetu yanasema: 

“Kwa njia ya mtu mmoja, zambi iliingia ulimwenguni,” 

Mara tena, tunapata tatizo hapa, sababu watu wanasema kwamba wao hawasadiki kama Adamu alitenda zambi, pia kwamba ni kwa ajili ya tendo hilo sisi sote tunakuwa wenye zambi. 

Mara nyingi, ninawaambia kwamba sisi ni wenye zambi, sababu tuliuriti toka Adamu. 

Wote wamefanya zambi katika Adamu. 

Wewe unafanya zambi sababu wewe ni mwenye zambi. 

Tuangalie dini inasema nini? 

Dini inatuambia : “Kwamba, mambo yale hayana maana yoyote. 

Siyo halali, sababu gani mimi ninaweza kugeuka kuwa mwenye zambi kwa sababu ya mtu mmoja tu aliyetenda zambi, miaka elfu sita, hapo zamani za kale? 

Sababu gani Mwenyezi Mungu anaweza kuweka mambo yale juu yangu, kuniweka mimi kuwajibika kwa zambi ile? Hii siyo halali.” 

Haya yote yanatokana na namna ya kuamini yale Mwenyezi Mungu anayotuambia. 

Eti, ndio ama hapana Adamu alikula tunda la muti wa kujua mema na mabaya? 

Kuna wale wanaoenda mbali sana wakisema ya kuwa zambi ya Adamu na Eva, ilikua zambi ya uzinzi. 

Hiyo ni upumbafu mtupu. 

Ni nini Mwenyezi Mungu aliyoambia Adamu katika Bustani la Edeni? 

“Alimuambia: Muongezeke na kuzidi na mujaze dunia.” 

Watajaza dunia namna gani? 

Kwa njia ya kujuana na kuzaa. 

Kuna wengine wanao zania kwamba zambi ya Adamu ni sababu alikula mvinyo iliyochacha na kwa hiyo zambi yake ilikuwa ya ulevi. 

Hiyo pia ni upumbafu mtupu. 

Kwa sababu watu hawakuwa na ujuzi huo wa kuchashisha mvinyo hadi vile anguko lao lilifika. 

Watu hawakuwa na ujuzi ule wa kuchashisha mvinyo hadi vile garika ilipopita. 

Baadaye, tuna wale wanaoamini ya kwamba Adamu alikula tunda.  


“Kwa njia ya mtu mmoja zambi iliingia duniani.” 

Hii inamaanisha nini? 

Huyo mtu mmoja Adamu ni yeye baba na kichwa cha kizazi cha watu wote ulimwenguni na wakati alipo anguka, akifanya zambi ya kula tunda la kujua mema na mabaya yeye aliingiza kizazi nzima cha wanadamu ndani ya zambi. 

Na, kwa njia gani nitafahamu kwamba hiyo ndiyo ukweli? 

Turudi kwa somo letu la Waroma 5. 

Namna gani nitajua na kufahamu mambo yale? 

Waroma 5: 12 

“Hivi kama kwa mtu mmoja zambi iliingia ulimwenguni, na kufa kwa njia ya zambi, na hivi kufa kulikuja juu ya watu wote, kwa sababu wote wamefanya zambi.” 

Eti ni kweli sharti siku moja kila mtu afe? 

Kweli, watu wengi sharti wanakufa. Watu wote wanakufa. 

Mushahara wa zambi ni mauti. Watu wote ulimwenguni pahali pote. 

Ni njia ya watu wote wenye uhai. 

Haijali nafasi gani unaweza kwenda, sharti utakutana na kifo. 

Sote tutakufa siku moja. 

Sasa wakati tunaposema: 

“Hivi kama kwa mtu mmoja zambi iliingia ulimwenguni, na kufa kwa njia ya zambi; na hivi kufa kulikuja juu ya watu wote, kwa sababu wote wamefanya zambi. Maana mbele ya sheria zambi ilikuwa ulimwenguni: lakini zambi haikuhesabiwa wakati sheria isipokuwa.” 

Namna gani sasa tutajifunza sehemu hii ya pili? 

“… Lakini zambi haihesabiwi wakati sheria isipokuwa…” 

Jameni, kuna swali lenye ningelipendelea mufahamu mbele ya kusonga mbele na majifunzo yetu. 

Katika BIBLIA TAKATIFU kuna Taasisi ine. 

Mambo mane ya hali ya kurasimisha, yenye tunapashwa kufahamu na itatusaidia kuongeza ufahamu dhidi ya majifunzo yetu ndani ya Maandiko haya. 

Taasisi hizo zilisimikwa na Mungu kwa ulinzi wa watu. 

Taasisi hizo ni kwa waamina na wasioamini vile vile. 

Ya kwanza ni: 

MAPENZI 

Mwenyezi Mungu alimupa kila mtu awe na Mapenzi, awe na mamlaka ya kuchaguwa, kwa hiyo mimi sifurahie wale wanaoamini kwamba wanadamu hawana uhuru wa kuchagua, wazo la kusema kwamba, nikitarajia kufanya jambo fulani kesho, hata mambo yabadirike je kiini tu mimi nitafanya jambo lile.

 Mwenyezi Mungu alimupa kila mmoja wetu uhuru wa kuchagua, mapenzi. 

Wakati alipomuweka Adamu katika Bustani la Edeni, alimwambia: 

“Usile kwa tunda la muti wa kujuwa mema na mabaya, sababu wakati utakula tunda la muti ule kweli utakufa.” 

Yeye alikuwa na namna ya kuchagua kitu gani ya kufanya, kuheshimu ama kugaili agizo. 

Na mimi na wewe ni wajibu wetu kila siku kufanya chaguo. 

Tangu kuzaliwa kwetu hadi kufa, wakati wote wa maisha yetu ni katika zoezi la kuchagua tu. 

Kwa hiyo, Mapenzi ni Taasisi ya kwanza na Biblia yote inajengwa juu ya Mapenzi. 

Ya pili ni: 

NDOA 

Ndoa ni ya muhimu sana. 

Wokovu ndiyo  kuamua mkuu,  kiisha hapo, kuamua ingine ya muhimu  yenye tunafanya maishani mwetu ni kuchagua mpenzi wetu . 

Ndoa ni kwa nini? 

Kwa siku za leo, kuna wale wanaosema: 

“Umbalimbali gani, ama kitu gani cha muhimu ndoa inacholeta?” 

“Ndoa ni kipande cha kartasi tu.” 

Kweli siyo hivyo. 

Ndoa siyo kipande cha kartasi. 

Ndoa ni kuamua, kukamata musimamo. 

Wa vijana wanasema: 

“Kwa sababu tunapendana, basi tuishi pamoja, kitu kigeni gani kilicho hapa?” 

Ndoa inakitu kipya kigeni inacholeta katika dunia hii. 

Tukumbuke kwamba ndoa ilikuwa mbele ya anguko la Adamu.

Kwa sababu gani ndoa? 

Ni kwa sababu Mwenyezi Mungu alisema: 

“Si vema mtu aishi peke yake.” 

Ni Mungu aliye amuru hivyo; na ni kwa njia hiyo tunajaza dunia na kuendelesha uzao wa wanadamu.  


Taasisi ya tatuni nini? 

JAMAA 

Jamaa ni kwa ajili ya ukingo. 

Sababu gani Mwenyezi Mungu aliumba Jamaa? 

Wakati mtoto mchanga anapozaliwa, yeye hawezi tenda kitu chochote peke yake; kwa mambo yote inabidi abebwe na kutegemea wengine. 

Yeye anahitaji kulishwa, kuoshwa, kulindwa katika usafi na mtu mwengine afwatiliye mambo yake yote. 

Mtoto anaendelea kuwa na lazima ya wazazi wake hata kufika kwa umri wa miaka 25 na zaidi; hata mimi vile vile, kwa umri wangu nina lazima ya wazazi wangu. 

Ninamushukuru Mwenyezi Mungu sababu mimi nilipata wazazi wenye walinijali sana na kunipenda sana hadi kufa kwao. 

Mimi nilikuwa na desturi ya kumuomba baba yangu mashauri wakati nilipofikia umri wa miaka 40 hadi 50 na mashauri ya baba yangu niliyakamata na samani kubwa. 

Jamaa ni ya muhimu sana. 

Taasisi ya ine ni nini? 

Hii ni neno lenye ningelitamani mulikamate kwa makini sana, sababu tutalijifunza kwa muda huu wote.  



UTAIFA   

Tutaijifunza na kuivumbua pamoja katika Kitabu cha Mwanzo sura 10

Hapa tunaona namna munara wa Babeli ulivyoanzwa.  

Mwanzo 10: 32 

“Hizi ni jamaa za wana wa Noa, kwa vizazi vyao, katika mataifa yao; na kwa hawa mataifa yamegawiwa duniani nyuma ya garika.”  

Sasa tusome 

Matendo ya Mitume 17: 26 

“Naye alifanya kila taifa la watu kuwa wa damu moja, wakae juu ya uso wa dunia yote, akaandika nyakati ambazo aliwa amuru tangu zamani, na mipaka na makao yao.” 

Mungu aliamuru tangu zamani nafasi na mipaka yenye kila inchi inapashwa kuishi ndani yake. 

Aliumba mataifa. 

Uweko wa Taifa la umoja duniani, hii siyo wazo la Mwenyezi Mungu. 

Dunia la umoja, Taifa la umoja ni miradi ya shetani. 

Umoja wa Mataifa siyo miradi ya Mwenyezi Mungu. Yeye haja jaribu kufanya hivyo. 

Sisi wenyewe, sawa mashahidi, twaona vinyume vya mipango mbalimbali ya Umoja wa Mataifa. 

Sababu gani Mwenyezi Mungu alipendelea Mataifa yawe? 

Nitawapa Maandiko mawili, na kweli ningeliwapa Maandiko mengi ya kuonesha sababu gani Mwenyezi Mungu alipendelea kuamuru Taasisi hili la ine inayoitwa UTAIFA. 

Yafaa kutambua kwamba UKOMINISTI siyo utaifa. 

Ujamaa inasema: 

Tuvunje Mataifa yote na tuunde tu Taifa moja inayokuwa na lugha moja. 

Kwa hiyo Mungu anasema: Hapana hata kidogo. 

Sasa, ni kwa sababu gani Mwenyezi Mungu alipenda Mataifa yawe? 

Ni ya muhimu kufahamu sababu gani Mwenyezi Mungu aliamuru Mataifa yawe. 

 “Alipanga kwamba Ujermani utakuwa hapa, Rusia sehemu hizi, Italia, sehemu zile, Ostralia hapo” Sababu gani? 

Tusome pamoja Waroma sura kumi na tatu. 

Hadi kufika kwa kiwango hiki tungali tu kwa “sehemu moja ya tatu” ya yale niliyohitaji kuwafahamisha leo. 

Waroma 13: 1 

“Kila mtu atii wakubwa wenye amri: Kwa maana hapana mamlaka ila kwa Mungu: Na mamlaka inayokuwa, imewekwa na Mungu.” 

Kila anayekuwa na mamlaka, aliinuliwa na kupewa na Mungu. 

Mafasirio zaidi tutaipata kwa neno inayofwata. 

“Hivyo yeye anayeshindana na mwenye mamlaka, anashindana na amri ya Mungu; nao wanaoshindana watajipatia hukumu.” 

(hukumu ama laana, kwa hiyo tusijaribu kushindana na Mamlaka iliyoshimikwa.) 

Tusome sasa Aya ya tatu.  

“Kwa maana watawala hawaleti watu woga kwa matendo mema, lakini kwa matendo mabaya. 

Basi unataka usiogope mwenye mamlaka? 

Fanya mema, na utapata sifa kwake.” 

“Kwa kuwa yeye ni mtumishi wa Mungu kwako kwa mema. Lakini wakati unapofanya mabaya ogopa; kwa sababu habebi upanga bure: maana ni mtumishi wa Mungu anayelipiza kisasi mwenye kufanya mabaya.” 

Sasa kufwatana na historia ya maisha ya watu, tunaona kwamba kulikuwa Viongozi na wakubwa wa serkali wa aina mbalimbali. 

Serkali maalum inayokuwa nzuri na yenye nguvu inaongozwa na Liwali mmoja, mwenye mamlaka makuu mmoja. 

Na mwazani serkali mbaya zaidi inayoishi sawa jehenamu yaweza kuwa serkali gani? 

Kidemokrasia ndiyo serkali mbaya katika yote. 

Serkali ya aina ya kijamuhuri inaongozwa na mtu mwongozi wa serkali. 

Wao wa Kidemokrasia wanatudanganya ya kwamba sisi sote tuko namna moja. Hii ni uwongo mtupu. Hii ni ndoto, sababu katika dunia hii, sisi sote hatuwezi kuwa sawasawa. 

Wewe waweza kuwa na kipaji fulani lenye mimi sina. 

Kuna wengine wanaokuwa na kipaji ya kumiliki na wengine hawana hiyo kipaji. 

Wengine kipaji yao inaonekana kwa kazi ya mikono, wanaunda vitu, wanafunuliwa na kupata mwangaza na ujuzi wa kuunda vitu vipya, lakini wengine hawana hiyo kipaji. 

Waweza kunikabizi msumeno, hama, na mimbari, kwa kweli, sitafurahi muone kitu nitakacho jenga. 

Mama yangu mzazi, hadi kufa kwake, alikuwa anachunga kiti ndogo kwa kinyesi chenye nilijenga hapo kale wakati ningali bado mu daraja la masomo ya kipusi. 

Ingelikuwa heri muione, ilikuwa ya kupengama pande ya mguu moja na upande ungine, ilikuwa ikiyumbayumba. 

Sifahamu kama mke wangu angali anaichunga ama hapana, kwa kweli mimi sikuwa museremala. 

Baba yangu alikuwa fundi wa kweli yeye alikuwa na ujuzi wa kujenga vitu vingi. 

Mwafahamu kweli kwamba tuna vipawa mbalimbali tofauti na vivyo hivyo siyo wote wanaokuwa na vipawa ya kumiliki na kuongoza. 

Jamuhuri nyingi za Kidemokrasia haziongozwe vizuri. 

Katika Uongozi wa aina ya Kijamuhuri, tunatambua ya kwamba kuna wale waliopewa ujuzi wa kumiliki wengine ama kuwa maliwali, kwa hiyo kuna serkali yenye inakuwa na yule anaye miliki. 

Sasa kitu gani inayotukia kwa leo katika vyombo vya habari? 

Tunaona uvuguvugu unaotokea kati ya wale wa Chama cha Kidemokrasia na wale wa Chama cha Kijamuhuri. 

Eti mumekwisha kusikia habari juu ya mtoto wa SAM hapo New York? 

Mumekwisha kusoma ma gazeti walioandika juu yake? 

Viongozi wa wale wasiotaka kuongozwa wakijiita wa kiliberali 

Liwali wa New York, anasema kwamba kwake hakutakuwa malipizi ya kifo, bali mwenyezi Mungu anapendelea utawala wa serkali. 

Sasa ingelikuwa heri mufahamu neno hili kwa sababu tutalijifunza juma kesho. 

Waroma 5: 13 

Serkali ni kwa usalama wako pia kwa usalama wangu

Ni kwa usalama wa Jamii na tena ni kwa kurahisisha kuleta usalama wa Taasisi ya kwanza tuliyoona. MAPENZI.  

Serkali iliamuriwa na Mwenyezi Mungu na ilishimikwa kwa kumlinda mtu, na Jamii yake na Ndowa yake. 

Ni nini inayotukia kama mtu anazidi kuwa mtenda zambi? 

Na hapo, mambo yote yanaharibika. 

Mungu akitaka, juma kesho tutajifunza Waroma 5: 13 

“maana mbele ya sheria zambi ilikuwa ulimwenguni; lakini zambi haihesabiwi wakati sheria isipokuwa.” 

Nilitaka kuwaonesha jambo moja ili mufikiri juu yake juma hili nzima. 

Maana mbele ya sheria zambi ilikuwa ulimwenguni; lakini zambi haihesabiwi wakati sheria isipokuwa. 

Sasa mwafahamu sababu gani neno “haikuhesabiwa “inatumikishwa hapa? Neno hili “kuhesabiwa” inatumikishwa mara moja tu katika Agano Jipya. 

Mwafahamu maana yake? 

Tusome Kitabu cha Filemono; ili mufahamu neno hili kwa makini sana, sababu kama ingelifaa kuwadanganya ni kwa njia ya  kutokuelewa neno hili. 

Filemono inakuwa na sura moja tu. 

Tusome Filemono: 18 

“Na kama amekukosea, au kuwa na deni, uandike hii juu yangu.” 

Hii ndiyo maana la tafsiri kwa Kigriki la neno: “kuhesabiliwa juu ya” 

Ni hapa tunapopata maana yake. 

“Maana mbele ya sheria zambi ilikuwa ulimwenguni, lakini zambi haikuandikwa juu ya huyo mtu wakati sheria isipokuwa.” 

Ni huo ndiwo utafsiri maalum katika tafsiri la Kigriki. 

Unapofanya utafiti utafahamu na kuvumbua kwamba ninasema ukweli. 


AMEN


N°Ref: 1976 / 003 - STUDIES IN LAW Part I / 02 /17 / 2021

No comments:

Post a Comment