Tuesday, June 30, 2020

NAMNA GANI KUJAZWA NA ROHO / HOW TO BE FILLED WITH THE SPIRIT

    Photo taken by B Smith from the patio



 

 

NAMNA GANI KUJAZWA NA ROHO

HOW TO BE FILLED WITH THE SPIRIT

September 25, 1960 

Pastor Henry. F. Kulp

 

 


 

Waefeso 5: 18 

“Wala musilewe kwa mvinyo, ndani yake ni makelele, lakini mujazwe Roho;” 

Kwa mahubiri yetu iliyopita, kwanza tuliwaambia sababu gani imewapasa kujazwa na Roho, sababu nyinyi  watu muna nafsi na roho  na yote inajaa ukorofi,  kwa sababu  ya hiyo  Mungu Baba aliwawezesha kuwa na mtu mupya, ili mupate kuwa  na mawasiliano katikati yenu na  Mungu. 

Pia, tuliwajulisha kwamba kuna umbalimbali kati ya mambo yanayoelekea Ujazi wa Roho, ama kujazwa na Roho mutakatifu katika nyakati hizi za Mwili wa Kristo, Kanisa leo, na katika Ufalme wa Mungu utakao kuwa duniani.  Katika hiyo nyakati ya Ufalme wa Mungu duniani, Roho Mutakatifu atatawala mutu, akimiliki umtu wake wote na kumuongoza kufanya tu mapenzi ya Mungu.  

Lakini, kwa nyakati hizi za Mwili wa Kristo, Roho Mutakatifu anakuja tu kufanya makao ndani yetu, na Yeye ni Msaidizi tu.

Kwa nyakati ya Ufalme wa Mungu, Roho Mutakatifu anaitwa: Kumwaga kwa Roho Mutakatifu. 

Umbalimbali kwa nyakati za sasa, tunapokea Roho Mutakatifu anayefanya makao na kuishi ndani yetu. 

Anaitwa tena : Ubatizo wa Roho Mutakatifu, wakati Bwana wetu Yesu Kristo atakapobatiza watu katika Roho Mutakatifu. Hiyo siyo kwa nyakati za leo, wala kwa siku za leo. 

Sasa, tuone kupitia Wagalatia 3: 26 – 27 

“maana ninyi wote ni wana wa Mungu, kwa Imani, katika Yesu Kristo. 

Maana ninyi wote muliobatizwa na kuingizwa katika Kristo, mumevaa Kristo.” 


1/ Tulibatizwa katika Kristo, na Waefeso 4: 5 

“Bwana mmoja, Imani mmoja, ubatizo mmoja.” 

Kwa siku za leo, hatuna ubatizo ndani ya Roho Mutakatifu, ubatizo tunao leo ni ubatizo katika Kristo Yesu. 


2/ Sasa, ulizo inayo tujia kichwani ni hili: 

Kujazwa na Roho Mutakatifu inamaanisha nini? 

Kila mutoto wa Mungu, kila aliye okolewa anakuwa na Roho Mutakatifu. Ni kwa hiyo njo Roho Mutakatifu anataka kufanya neno moja kwake. 

Haiko jambo linalotukia wakati mutu anajiangusha chini kwa udongo, wakati anapoomba. 

Bali ni kitu chenye Roho Mutakatifu mwenyewe anataka kufanya kwako. 


3/ Hatua ya kwanza ya kutimiza wakati mutu anataka kujazwa na Roho Mutakatifu, tunaipata katika Wakolosai 3: 16

“Neno la Kristo likae kwa wingi ndani yenu kwa hekima yote, mukifundishana na kuonyana kwa zaburi na nyimbo na tenzi za roho, mukiimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu." 

Tunaona hapo, jambo la Neno la Mungu kukaa kwa uwingi ndani ya nafsi zetu. Tu rudie tena katika Waefeso na tusome moja kwa moja maneno haya,  

Hatuvumbue kwamba aya hizi mbili zinaleta  matokeo sawasawa, wakati katika Wakolosayi, tunaombwa kwamba Neno la Mungu likae kwa wingi ndani yetu, na wakati katika Waefeso tunaombwa kujazwa na Roho Mutakatifu. 

Hii inamaanisha nini? 

Katika sayansi ya hesabu, kuna sheria moja ya zamani inayosema kwamba: Mambo inayokuwa sawasawa na nyingine, inakuwa sawasawa moja kwa moja. 

Matokeo ya kujazwa na Neno la Mungu ni sawa na matokeo ya kujazwa na  Roho Mutakatifu … 

Hii jambo inapashwa kuwa wazi na ni ya muhimu sana kujua kwamba: 

Neno la Mungu lijaapo mukristo ni sawa na Roho Mutakatifu ajaapo mukristo. 


4/ Unaweza kusonga juu zaidi na kuona hakikisho ya neno hili katika kitabu cha Waefeso 5: 18 

“Wala musilewe kwa mvinyo, ndani yake ni makelele, lakini mujazwe Roho;” 


  Kujazwa na Roho. 

Tendo kujazwa hapa, linakuwa tendo la kufanywa na, na linafwatana moja kwa moja na neno linaloonesha ni nani anaye tenda tendo la kujaza. 

Kama ingelikuwa tendo la kufanywa na ingefwatwa na jambo la kuwa na, hapo ingelimaanisha milki. 

Na hiyo ingeoneshwa kwamba mpokeaji anajazwa na nini, nikusema anajazwa na Roho Mutakatifu. 

Siyo tatizo sisi tujazwe na Roho Mutakatifu, linalotupasa kujua ni kwamba ni Roho Mutakatifu ndiye anaye tenda tendo lile. 

Ni Yeye anaye jaza, ni Yeye mtendakazi ya kutujaza sisi. 

Anatujaza na nini? 

Anatujaza na Neno la Mungu. 

Ni kusema kwamba kujazwa na Roho siyo jambo la fumbo, la hisia, ama jambo la zoezi la kupoteza mafikili, lakini ni jambo la kujifunza Neno la Mungu, na hapo Roho Mutakatifu anatwaa Neno hili na anatujaza nalo. 

Sisi hatuwezi kufahamu maandiko kama Roho Mutakatifu hatuangazie. 

Na wakati tunapojifunza Maandiko matakatifu, tunaifahamu chini ya uongozi wa Roho Mutakatifu, kiisha anatujaza na Neno lile. 


5/ Watu wananiambia: 

Mimi ninajuwa kwamba Roho Mutakatifu aliniambia nifanye hiki ama kile, kwa kweli, mambo yale yanajaa machafuko mengi. 

Roho Mutakatifu hatumike namna hiyo. 

Roho Mutakatifu hatufundishe kitu inje ya Neno la Mungu. 

Wakati tunapopatikana katika shida fulani na hapo tunaamua kuketi chini na kufikili vema juu ya jambo linalotukumba, tunakumbuka kwamba Biblia inatuambia kwamba tujiepushe na mambo yote ya ibilisi,  ili tusiwe chanjo cha kuangusha ndugu yetu, na kwa hiyo tunageukia kwa yale Maandiko Matakatifu yanasema. Na ni hivi Neno la Mungu linavyo sema. 

Sisi tunapashwa kuwa watu wa aina hii: 

Jambo hili linatoka kwa muovu ama linaweza kuangusha ndugu? 

Eti, katika jambo hili, mapenzi ya Kristo inaonekana ama hapana? 

Kiisha nitafahamu kwamba niko katika makosa, na Roho Mutakatifu itanifunulia hayo kupitia Maandiko Matakatifu, Neno la Mungu. 

Hii ndilo hitimisho kamili la muhimu lenye ninapashwa kufikia.  

Twende tena kuchunguza katika Maandiko mengine ili tuhakikishe kawaida hii: 


6/ 1Wakorinto 2: 15   

“Lakini mwenye kufuata Roho anatambua maneno yote, lakini yeye mwenyewe hatambuliwi na mtu.” 

Mwenye kufuata Roho, ama mtu wa Kiroho. 

Kwa kuwa mtu wa Kiroho, yatupasa kujazwa na Roho Mutakatifu… 

Ninajuwa kwamba ninyi vilevile mumekubaliana nami. 

Mutu wa kiroho anahukumu, anatambua maneno yote. 

Ni kusema anafahamu maneno yote. 

Mutu wa kiroho anahukumu, anatambua na kufahamu maneno yote.

Namna gani anafikia kufanya hivyo? 

Kitabu cha 1Wakorinto sura mbili, kinasumulia tu juu ya Neno la Mungu.

Mtu fulani niwa Kiroho sababu anafahamu Neno la Mungu chini ya uongozi na msukumo wa Roho Mutakatifu. 

Tujuwe kwamba 1Wakorinto 2: 9 inasema:

“Lakini kama ilivyoandikwa: 

Jicho halikuona, wala sikio halikusikia, wala hayakuingia katika moyo wa mutu, Maneno Mungu aliyotengenezea wenye kumupenda.” 

Hapa inaonekana kwamba siyo maneno ya duniani. 

Mwenyezi Mungu anahitaji nini kwangu? 

Mwenyezi Mungu anapenda mimi nifanye nini?

Namna gani mimi nitafahamu kuusu Mungu? 

Hatutaweza kufahamu maneno haya kwa kiasili, sawa vile inavyosemwa kwa aya ya kumi kwamba, Mwenyezi Mungu aliyafunua kwetu kwa kupitia Roho Yake.  

Namna gani alifanya hivyo? 

Kupitia Neno la Mungu. 

Ni kusema kwa kuwa mutu wa kiroho ama mutu anayejazwa na Roho Mutakatifu inafaa Roho mutakatifu akamate Neno la Mungu na atujaze na ile Neno la Mungu. 


7/ Jambo lingine ni kuhusu mtoto mchanga wa kiroho. 

Haiwezikane mukristo mupya, huyo anayemupokea Bwana Yesu punde kidogo tu, haiwezekani huyo kujazwa na Roho Mtakatifu. 

Ni kugumu Roho Mutakatifu kujaza mutu huyo, sababu bado hajajua Neno la Mungu. 

Ni kwa sababu hiyo inaombwa kwa mtoto wa Mungu aliyepokea Bwana Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wake, anaombwa kujifunza Neno la Mungu na kulificha moyoni mwake. 

Mukristo mchanga hawezi hesabiwa kuwa wa kiroho. 

Yeye si tayari kwa kiroho ama kwa kimwili.

Kama yeye ameonekana kuwa tayari kwa kiroho, itamupasa yeye kujifunza maandiko, akiruhusu Roho Mutakatifu kumujaza na Neno la Mungu. 

Imeombwa kwa mukristo muchanga kujifunza Neno la Mungu. 


8/ Twende sasa kuona umbalimbali gani uko kati ya: 

Kuwa uwanja wa kiroho, kuwa kimwili, kujajwa na kutokujajwa. 

Maneno haya yalikuwa yanaleta shida mwingi kwenye kanisa la Korinto.  

1Wakorinto 3: 1 – 2 

“Na mimi, ndugu zangu, sikuweza kusema na nyinyi kama na watu wa Roho, lakini kama na watu wa mwili; kama na watoto wadogo katika Kristo. 

Nimewakunywesha ninyi maziwa wala si chakula; kwa sababu mulikuwa hamujakiweza, hata sasa hamukiwezi;” 

Mpaka hapo, ninyi ni kama watoto wadogo katika Kristo. 

Nimewakunywesha ninyi maziwa wala si chakula, kwa sababu mulikuwa hamujakiweza, na hata sasa hamukiwezi. 

Hauwezi kamwe kujazwa na Roho Mutakatifu kama wewe bado kujazwa na Neno la Mungu.Hiyo ndiyo ukweli. 

Tuone kwamba 2Timoteo 3: 16 - 17  

“Kila andiko limepewa kwa maongozi ya Mungu, na linafaa kwa mafundisho, na kwa kuonya watu juu ya makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa mafundisho katika haki; 

Ili mutu wa Mungu awe mukamilifu, ametengenezwa kabisa kwa kila tendo njema.” 

Hii inatokana na Neno la Mungu, ni hii ni kweli wakati Neno inafundishwa katika kiroho. 


9/ Sasa yote inakuwa sambamba 

Namna gani Mutume Paulo alifikia kiwango hiki? 

Eti Mutume Paulo anatuambia tulifanye? 

Roho Mutakatifu tuliepewa, kama Mutenda kazi, anakamata Neno la Mungu na kuitia katika nia na mafikili yetu. 

Siyo jambo ya mazoezi ya hisia, mazoezi ya furaha ya kupita kipimo yenye hauwezi tena kuongoza, ama upendo wa kilokole, mambo yote inaenda sambamba. 

Kuna jambo lingeni la muhimu lenye ningelipendelea kuongeza hapo na jambo hili tunalipata katika kitabu cha Waroma 8: 18, mahali Mutume Paulo anaposema: 

“Kwa maana ninahesabu…” 

Neno “kuhesabu”  inatoka kwa tendo la “kuhesabia”, ni hesabu kamilifu, ni matokeo ya majifunzo kamilifu kiisha kutazama na uakili wote. 

“Kwa maana ninahesabu mateso ya wakati huu wa sasa kuwa si kitu tukiyafananisha na utukufu ule utakaofunuliwa kwetu.” 

Mutume Paulo anasema: 

Nimetumikisha akili, nia na ujuzi wangu, na Roho Mutakatifu alinifunulia na ufunuo wake ulinituma nifikie kuhakikisha kwamba magumu na shida tunayo kumbwa nayo kwa sasa, si kitu tukiyafananisha na utukufu ule utakao funuliwa kwetu. Na hii ni kweli na ni sambamba. 


10/ Ni kwa sababu ya hiyo tuna mapashwa kazaa yenye tunapashwa kutimiza. 

2Timoteo 2: 15 

“Dumu kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mfanya kazi asiyeona haya, ukitafsiri vema neno la kweli.” 

Tunashurtishwa kujuwa Neno la kweli, na tunapashwa kulitafsiri vema. Hatupashwe kuwa sawa wafanyakazi walio jitaabisha bure. 

Sisi tunapashwa kujiwekea Neno la Mungu na kulichunga mioyoni mwetu na Roho Mutakatifu anaitafsiri kwetu. Na anaitafsiri ndani ya Mawazo na Ufahamu wetu. Hii inaonesha umuhimu wa Mawazo na ufahamu. 


11/ 2Wakorinto 10: 5  

“tukiangusha mawazo na kila kitu cha juu kinachonyanyuliwa juu ya elimu ya Mungu, tukitia kila wazo katika utumwa wa Kristo.” 

Tunaambiwa  kutia kila wazo katika utumwa wa Kristo, ili Neno la Mungu likae kwa wingi ndani yetu. 

Nikusema kwamba, kujazwa na Roho Mutakatifu, inamaanisha kujifunza Neno la Mungu, kuruhusu Roho Mutakatifu alitafsiri ndani yetu, na katika ufahamu wetu, turuhusu mawazo yetu ijae na Neno la Mungu.

 Maneno haya tumeyahakikishiwa tena katika kitabu cha

          Wakolosayi 3: 2. 

“Tieni mafikili yenu juu ya maneno ya juu, wala si juu ya maneno yaliyo duniani,” 

Mupende na mutiye mafikili yenu juu ya maneno ya juu. 

Itawezekana-je kufanya hivyo? 

Ni kupitia tu Neno la Mungu. 

Nikusema hivi: 

Muinue mafikili yenu juu ya vitu vya mbinguni kwa njia ya Neno la Mungu.

Tieni kilaa wazo katika utumwa, ni hapo mutatambua maana ya kujazwa na Roho Mutakatifu. 


12/ HII INGELIPASHWA KUWA KATIKA MUUNDO WA KISARUFI YA   WAEFESO 5: 18. 

MUFANO KUUSU ROHO. 

MFANO KIKOMBE AMA KIKOMBE CHA KIOO KINACHO JAA MAJI

NI KWELI KWETU SOTE KWAMBA NI BOMBA LA MAJI NDIO LIMETIA MAJI KATIKA HIYO KIKOMBE NA KUFANYA IJAE. 

HAINA LAZIMA BOMBA KUINGIA NDANI YA KIKOMBE ILI KIKOMBE IJAE MAJI. 

LAKINI NI BOMBA INAYOFANYA KAZI YA KUJAZA MAJI. 

NI HIVYO HIVYO ROHO MUTAKATIFU ANATUMIKA SAWA NA AYA HII YENYE IKO MBELE YETU. 

ROHO MUTAKATIFU NDIYE MUTENDA KAZI ANAYE TUJAZA, SIYO NA MAJI, BALI NA NENO LA MUNGU. 


13/ Namna gani mawazo hii inapingana na mawazo ya mutu kawaida wa kiroho. 

Mutu wa kawaida anazani kwamba kuomba, kuomba tena kuomba sana hiyo ndiyo kuwa mutu wa kiroho, na anafanya hivi bila hata kuchukuwa muda kidogo ili ajifunze Neno la Mungu. 

Hii tendo inaonesha wazi wazi namna gani watu hawa hawatambui maana ya kujazwa na Roho Mutakatifu. 

Ama namna gani kujazwa na Roho Mutakatifu. 

Kwa kweli maombi ni ya lazima na maana kabisa katika maisha ya mukristo.

Saa zote tunapashwa kuwa katika hali ya maombi. 

Lakini sasa tujiulize, ni nini ya muhimu  kati ya maneno sisi tunapenda kuambia Mwenyezi Mungu, ama Maneno Mwenyezi Mungu anataka kutuambia? 

Kwa kweli, kwa ulizo lile, jibu la kweli ni moja tu. 

Bila ubishi wowote, ni Maneno Mwenyezi Mungu anataka kutuambia ndiyo iko ya muhimu sana zaidi kupita neno sisi tulitaka ambia Mungu.  


14/ Hii ni hoja moja lenye linashikamana na hayo yote: 

2Timoteo 3: 16, 17 

“Kila andiko limepewa kwa maongozi ya Mungu, na linafaa kwa mafundisho, na kwa kuonya watu juu ya makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa mafundisho katika haki; 

Ili mutu wa Mungu awe mukamilifu, ametengenezwa kabisa kwa kila tendo njema.”  

Imesemwa hapa kwamba: 

Kila andiko limepewa kwa maongozi ya Mungu, chunguza vema hapa “Maongozi ya Mungu” 

Ili mutu wa Mungu awe mukamilifu, ametengenezwa kabisa kwa kila tendo njema.  


15/ Hali ya kujazwa na Roho ina matokeo Fulani, na kitabu ya Waefeso inatuonesha wazi namna gani tutakuwa wakati tunajazwa na Roho Mutakatifu, ama tunajazwa na Neno la Mungu.  

Tujifunze sasa matokeo ya kujazwa na Roho Mutakatifu. 

Waefeso 5: 19 – 20 

“mukisemezana ninyi kwa ninyi kwa zaburi na tenzi na nyimbo za roho, mukiimba na kushangilia Bwana mioyoni mwenu; 

Mukishukuru Mungu ndiye Baba siku zote kwa mambo yote, katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo;” 

Hii ingelitafsiriwa ifwatavyo: 

Mukisemezana ninyi kwa ninyi kwa zaburi na tenzi na nyimbo za roho, pahali pa kujizungumuzia binafsi. 

Inatupasa kusemezana moja na mwengine kwa nyimbo za roho. 

Katika maisha ya mwamini, tenzi na nyimbo za roho zinapashwa kuwa na nafasi kubwa tena ya heshima. 

Katika Kanisa Mwili wa Kristo, katika mazehebu yetu hapa duniani, ninashangazwa na kubabaishwa sana na mutu mwenye hajali kuimbia Mungu. Huyo mwenye nyimbo kwake haimwambie kitu. 

Yawezekanavyo hana kipaji cha uimbaji, lakini angelipenda kuimba. 


16/ Sasa tupime kusema kwa ufupi ndani ya dakika moja, kitu gani Mutume Paulo iko anazungumuzia hapo: 

Wasikilizaji walipo musikia Mutume Paulo akifundisha, walitambua palepale kwamba haifai mukristo kulewa sawa mutu mupagani mpaka kufika kiwango cha  ulevi wa mupagani, mwenye  kiisha kulewa na mvinyo  anaanza kuimbia  Bacchus mungu wa pombe, ama Venus(mungu wa mapendo). 


17/ Yakobo 5: 13 

“Mtu wa kwenu ameteswa? Aombe. Mtu amefurahiwa? Aimbe nyimbo.” 

Mtu kati yenu amefurahiwa? Aimbe nyimbo.

Nina uhakikisho kwamba katika maongozi ya ibada ya makanisa za mwanzo, nyimbo ilichukuwa nafasi kubwa tena ya heshima. Vile vile, Bwana wetu Yesu Kristo pamoja na mitume wake kiisha kugawa meza ya Bwana, waliimba tenzi la nyimbo 

Matayo 26: 30 

“Na wakati walipokwisha kuimba, wakatoka inje kwenda mlima wa Mizeituni.” 

Wakwisha kutambua kwamba ni muziki tu wa kikristo ndiyo inachezwa kupitiya ufungo wa msingi wa kinanda? 

   Twawezaje namna gani kuonesha furaha, raha, uzima, , nyimbo za kiroho zinatutia katika raha, pahali pakuwa wenye kuzoufika, wenye huzuni,waliokata tamaa. 

Lakini unaposikiliza nyimbo za kimataifa za siku hizi, sawa hiyo ya upumbafu rock “n” roll inayojaa na vifungo vya sauti kama vya rambirambi na kifo. 

Nilisikia kwamba huko Ungereza, kuna wimbo uliokatazwa sababu ulikuwa umekumba wavijana katika ulevi na furaha za ubatili wa kimwili. 

wimbo ule ulikuwa juu ya kumbukumbu ya jambazi moja alie fariki ndani ya ajali kubwa ya gari. 

Nyimbo zetu za kiroho zingepashwa kujaza mioyo yetu na nyimbo hizo zingelipashwa kujaa na Maneno ya Mungu.  


18/ Tufahamu kwamba tunapashwa imba pia kuchezea Mwokozi wetu muziki wa vinanda katika roho zetu. 

Yawezekana, sisi hatujuwi kucheza vyombo vya muziki, ili vilete sauti nyororo. 

Wengine wetu, kama wakilazimishwa kutowa sauti nyororo kupitia tu vyombo vya muziki, wao watakumbwa na shida, sababu hawataweza lolote. 

Lakini tizama ndugu yangu, kila roho ya mukristo ni kama kinanda na Roho mutakatifu anapulizia singa za kinanda na zinatowa sauti nyororo sana na inafikia sikio la Mungu Baba. 

Tujuwe kwamba tunapashwa imba zaburi, na tenzi na nyimbo za roho. 

Umbalimbali ni nini basi? 

Tenzi ni kwa niaba ya Mungu mwenyewe. 

Nyimbo sawa: “Yesu wangu ninakupenda”, ama, “Mungu wetu musaada wetu nyakati zote”, ama, “Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu Mungu Mwenye Uwezo”, ama “Mimi ni wako, O Mwokozi njia ni yako, Mwokozi wewe ni Mufinyazi, mimi ni udongo” 


Kiisha tuna zaburi:

Zaburi inasindikizwa na muziki wa nzenze, vinanda, na vyombo vyote vya muziki. 

Kiisha tuna nyimbo za roho: 

Nyimbo za sifa na Maabudu 

Mfano, wimbo wa ushuhuda, ninapenda shuhudia makuu Bwana aliyo nifanyia, “Mapendo ilinihimiza wakati sikuwa hata na musaada,…Mapendo ilinitowa kwenye shida,” ama “Mkombozi, nitakushuudia, nimeokolewa na Damu ya Mwana Kondoo.” 

Kiisha tena 

“Ole Damu ilitoka Mwokozi wangu, Mfalme wangu alikufa” 

Ama inaweza kuwa wimbo wa kufariji ama kupana angalisho.

“Amini na utii, sababu hakuna njia lingine” 

Kwa hiyo, mioyo yetu haingelipashwa kujazwa na nyimbo za kitamaduni, lakini ijazwe na nyimbo za roho. 

Ni Yeye anaye jazwa na Neno la Mungu, maana yake anayejazwa na Roho Mutakatifu ndiye anayekuwa akiimba nyimbo za sifa na maabudu kwa Mwokozi wetu Yesu Kristo. 


19/ Mwamini mwenye anajazwa na Roho, ni mwamini mwenye anakuwa mutu wa kushukuru. 

Akishukuru Mungu katika yote katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo. 

Nyakati zingine tunasema kwamba kuna mambo mengine ya shida zaidi inayo tukumba na tunashindwa kushukuru. 

Mambo mazito na magumu kweli. Mambo inayochoma roho zetu na kuvunja nafsi zetu. 

Sawa na mutu aliye pasuliwa mwili wake ili wanganga waondowe kitu kilichokuwa kikimuzoufisha, kumuuma na kumuregeza kwa hali isiyowezekanavyo. 

Mutu huyo atasikia kuumwa kwa visu vya waganga, lakini baadaye atakuwa na wajibu wa kusema asante sababu anakombolewa na hayo maumivu na mateso iliyo mukumba siku nyingi. 

Sasa inageuka kuwa Baraka, aksanti kwa Mungu kwa baraka hiyo. 


AMEN

 

N°Ref: 09/25/1960 / 22 - HOW TO BE FILLED WITH THE SPIRIT / 04/06/2020

No comments:

Post a Comment