Friday, January 31, 2020

MWILI WA UREMBO / THE BODY BEAUTIFUL

Photo taken from B Smith's kitchen Window







     MWILI WA UREMBO 
     THE BODY BEAUTIFUL 
     Pastor Henry F. Kulp
     January 10, 1960 







Waefeso 2: 17 - 22 
“Akakuja na kuhubiri salama kwenu muliokuwa mbali, na salama kwao waliokuwa karibu. 
Kwa maana kwa yeye sisi sote tumepata njia ya kukaribia Baba katika Roho mmoja. 
Basi tangu sasa ninyi si wageni na wasafiri tena, lakini wenyeji pamoja na watakatifu, na watu wa nyumba ya Mungu. 

Mumejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kubwa la pembeni. 

Katika yeye jengo zima linaunganishwa vizuri na kukua hata lipate kuwa hekalu takatifu katika Bwana. 

Katika yeye ninyi vilevile munajengwa pamoja kuwa kao la Mungu katika Roho.” 

Katika siku zilizo pita, tulikuwa tukiwaonesha tofauti iliyokuweko zamani katikati ya Muyuda na mutu wa Mataifa. 

Wakati Mungu alikuwa bado angali anashimamisha kiambaza cha uadui, maagizo na ma shurti. 

Kulikuweko taifa lenye lilikuwa likifugwa kwa upendelevu kama vile mfuga nyama anaweza kufuga nyama. Kulikuweko Taifa pendelevu. 

Taifa hiyo ilikuwa ikipendelewa sana na kuwa na faida mbalimbali za upekee na lilo Taifa lilikuwa Taifa la Israeli. 

Mataifa mengine ama wapagani hawakuwa na faida lolote, hawakuwa na maagizo, ma shurti, ama sheria, wao hawakukuwa na agizo la kuja kwa Mwokozi, hawakuwa hata na kitu chochote, walikuwa wakitiwa mbali sana wakati Israeli ilikuwa karibu na Mungu. 

1/ Mungu alibomoa  kiambaza ile ya uadui kwa njia ya Yesu Kristo, na kwa sasa hakuna tena Muyuda wala mutu wa Mataifa na faida kubwa tunalolipata ni kwamba, wakati tunaamini Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo tunakuwa kiungo cha ule Mutu Mupya hiyo maagizo yote ya zamani na shurti zote za zamani  zikitupwa inje na kuvunjwa na shurti moja inayokuwa kwetu kwa leo inapatikana katika haya ya kumi na nane 18 inayosema: Muyuda na Mutu wa Mataifa, kwa njia ya Yesu Kristo, sisi sote tumepata njia ya kukaribia Baba katika Roho mmoja. 

Kweli hii ni kitu kipya, tunaona kwamba katika siku za kale haikuwezekana kukaribia Mungu Baba kwa mara moja, hata Wayuda, hata vile walivyokuwa na faida nyingi na walikuwa wapendelewa lakini hawakuweza kukaribia Baba Mungu kwa mara moja, kwa urahisi. 

2/ Hapo tunaona ya kwamba kiongozi ni Roho Mutakatifu. 
Ni Yeye njo mwenye anatufikisha katika uwepo wa Baba Mungu. 
Neno kupewa njiya ni neno la kigeni inatokea katika neno pros-ag-o. 
Pros inamaanisha uso kwa uso, 

Ago inamaanisha kuonesha mwelekeo. Yeye anatuelekeza tuwe uso kwa uso na misemwa hii inatumikishwa kwa ku maanisha kwenda mbele ya mukubwa mwenye mamlaka na uwezo, kuelekezwa mbele ya Yule Mwenye Uwezo kwa njia ya Yesu Kristo. 
Mbele ya kubomolewa kwa hiyo kiambaza cha uadui, neno hili halikujulikana. 

3/ Haya ya kumi na kenda 19  
Hapa tunafika kwa Ukweli huu wa kushangaza. 
Haya hii inaanza na neno Basi sasa. 

Sasa inakuwa ya muhimu kabisa na inaonesha kwamba ni katika wakati huu. Nikusema sisi tunapata kitu chenye hakuna mutu mwengine mwenye alikipata mbele. 
Na neno Basi sasa inamaanisha kitu kinacho pata sasa nafasi. 

Sababu kwa sasa Muyuda na mutu wa Mataifa wote kwa njia ya Bwana Yesu Kristo, wanakuwa na njia wazi kwa Baba Mungu, Roho Mutakatifu anawaongoza na kuwaelekeza mbele ya Mungu. 

Hatuko tena wageni na wasafiri, lakini wenyeji pamoja na watakatifu, hiyo inamaanisha nini? 

Kwa kweli, je, sisi si watakatifu? 
Kila yeye aliyeokolewa, yeye ni mutakatifu. 
Tafsiri ya Biblia King James haiko wazi hapa. 
Sisi tunakuwa wenyeji pamoja na watakatifu 

KUJISIKIA KWANGU MWENYEWE KWENYE ARZI na kweli hii inamaanisha nini? 
Hapo tusoma katika kitabu cha mutume Paulo kwa Waebrania 9: 8  

“Roho Mutakatifu akionyesha neno hili ya kuwa njia ya kuingia Pahali Patakatifu haijafunguka wazi bado, hema ya kwanza ilipokuwa ingali kusimama” 

Nafasi inaposemwa Pahali patakatifu pa patakatifu kama inavyosemwa na neno lilo moja la kigriki. 

Ni nafasi gani katika mbingu zote ilio nafasi patakatifu pa patakatifu? 
Nafasi hiyo haina kunjo, ama ukorofi, nafsi yenye haikumbwi na zambi, ni uwepo tu wa Baba Mungu, nafasi hiyo tutaishi milele na milele. 

Mambo mengine sawa vile mbingu mupya na dunia mupya yote itapita, bali ni nafasi hiyo tu njo itadumu milele ni kusema Mbinguni. 

Basi, sisi hatuko tena wageni lakini wenyeji pamoja na watakatifu katika mahali pa takatifu pa patakatifu huko juu Mbinguni.

4/ Watu wengine wanasema kama hawana uhakika wa kwenda mbinguni lakini sisi sharti tuwe na uhakika wa kwenda mbinguni sababu sisi ni wenyeji wa mbinguni, Makao yetu ni kule. 

HII NJO INAPASHWA KUWA KWA MWANZO WA KILA NENO LETU, NENO GANI LA RAHA NA MUSHANGAZO KWA SISI WENYE HAPO KALE TULIKUWA WAFU SABABU YA MAKOSA YETU NA ZAMBI, MBALI NA MUNGU, BILA MUNGU KATIKA DUNIA HII NA KWA LEO TUWE NA UWEZO WA KUANGALIA MUNGU ANA KWA ANA NA KUZUNGUMUZA NAYE KAMA BABA. PICHA HII YA KUSHANGAZA TUNAIPATA KATIKA KITABU CHA MUTUME PAULO KWA 

WAROMA 8:16  
“Kwa maana hamukupokea tena roho ya utumwa inayoleta woga, lakini mulipokea roho ya kufanywa wana, kwa sababu hii tunalia: Aba, Baba.”

Hapa inasemwa kwamba kama kwa maongozi ya Roho tunalia Aba Baba. 
Wataalamu wamoja wanatuambia kwamba Aba ni sawa vile mutoto anaita Baba, kama watoto wa kihebrania walivyokuwa wanaita wababa zao, sawa vile vile watoto wetu wachanga wanaita baba. Ni jina yenye inamaanisha undugu wa karibu sana, hiyo siyo lalamiko la namna ya kidini ama namna wayuda walikuwa wanaita Mungu. 

5/ Wakati tunaangalia mambo haya yote makubwa, tunaona kwa kweli kwamba wakati tunakaribia kweli uwepo wa Baba Mungu, hatupashwe kuchanganyikiwa ama kuwa na woga, hatupashwe kuwa wanyonge sababu sisi ni wana wa Mungu. 

6/ Tuangalie kwanza hiyo namana ya kuitwa jina wenyeji wa, na jina Pahali Patakatifu pa patakatifu. 
Hiyo wazo haiko kigeni ndani ya Biblia, sababu katika kitabu cha mutume Paulo kwa 

Wafilipi 3: 20 
“Kwa maana sisi ni wenyeji wa mbinguni; kutoka pale tunangoja Mwokozi, Bwana Yesu Kristo”

Tunasoma hapo kama sisi ni wanainchi wa mbinguni ni kusema kwamba Mutume Paulo alikuwa anajuwa kwamba yeye ni mwanainchi wa mbinguni. 

Muji wa Filipi ulikuwa kikoloni ya wa Roma. 

Jina ukoloni kwa nyakati zile ilikuwa na maana na hali nyingine mbalimbali na sasa. 
Muji unaokuwa chini ya ukoloni wa waroma ni muji wenye ulikuwa na kujitoa na kufanya maneno ya ushujaa kwa faida ya utawala wa waroma na kwa namna ya malipo kwa  taifa na watu wa muji ule kwa kujitowa kwao na uaminifu wao, waroma walikuwa wanapatia muji ule jina ya ukoloni. 

Na ile kuitwa ukoloni wa waroma, ilikuwa unapatia palepale kila mukaaji wa muji ule anayekuwa huru, ilikuwa inamupatia kuwa mwanainchi wa Roma na yeye alipokea faida  na haki yote sawa sawa  na mwanaichi halali wa taifa la Roma. 

7/ Ilikuwa miaka michache mbele Mutume Paulo aandike waraka huu wa wafilipi njo taifa la wa Roma ilikuwa na ugonvi na taifa la ngambo ya Mashariki- Kaskazini.
Wakati vikosi vya askari wa roma walipofika Filipi, walikuta tayari wafilipi wamekwisha tayarisha vifaa na vikosi nyingi kwa niaba ya kuunga mukono na kusaidia askari waroma.  
Ma jemadari waroma walishangaa na kufurahi sana kwa tendo lile la ukarimu na kujitowa na walituma ripoti ya ajabu kwao Roma. 

Wabunge wakuu walikusanyika huko Roma na walipatia Filipi madaraka ya kuwa koloni ya Roma na kwa hiyo kila mukaaji wa Filipi angiweza kujiita kwamba yeye ni mukaaji wa Roma, yeye anakuwa sawa sawa na muroma na kuwa na haki yote yenye inajulikana kwa waroma. 

Kwa kweli wao walikuwa wakaaji wa Filipi na Filipi ilipatikana ndani ya Makedonia walikuwa basi na mapashwa yakutimiza juu ya serkali ya Makedonia, lakini Filipi ilikuwa chini ya uongozi wa gavernementi ya Roma na Wafilipi walikuwa na mujumbe wao ndani ya gavernementi ya Roma hii njo ilikuwa maana yake. 

Sisi vile vile tunaishi katika dunia hii ya zambi lakini sisi ni wenye zambi waliookolewa kwa Neema na sisi sote tunaungwa kwa Mwokozi wetu Yesu Kristo mwenyi enzi utukufu na mubarikiwa hata kama dunia inamukataa. 

Na Mungu anafurahia kujitowa kwetu kwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo katika nyakati hizi mbaya yenye watu hawamupendi Mwokozi Yesu Kristo. 

Na Mungu anapatia kila mutu anaye amini Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, kama Bwana na Mwokozi wake, huyu mutu Baba Mungu anamupa madaraka ya kuwa mukaaji na mwenyeji wa Mbinguni.

Watu hawa wanakuwa wenyeji wa mbinguni hata kama kwa sasa wao wangali wanaishi duniani.

Raha kubwa gani kuwa mukaaji wa Mbinguni. 
Mimi ninajuwa yakwamba nimeokoka. 
Mimi ninajuwa kwamba nimenunuliwa kwa bei ya damani. 
Mimi ninajuwa kwamba niko katika safari ya kwenda mbinguni sababu mimi ni mukaaji wa mbinguni. 

8/ Hapa tuna picha ya ajabu ya Roho Mutakatifu kama Mujengaji na tunakuwa na kweli ingine yenye ilikuwa hata wakati hiyo kiambaza cha uadui kilikuwa kingaliko. Na kweli hii tunaipata katika haya 21 na 22. 

“Katika yeye jengo zima linaunganishwa vizuri na kukua hata lipate kuwa hekalu takatifu katika Bwana. 
Katika yeye ninyi vilevile munajengwa pamoja kuwa kao la Mungu katika Roho” 

Kweli hiyo ni gani? 
Kweli hiyo ni kusema kwamba kwa siku za leo Mungu iko na Kao. 
Mungu ana kao lenye anaweza kuishi ndani yake. 
Kwa wakati huu wa Neema, kwa nyakati za sasa, kao lenye Mungu iko nalo ni Hai ama ni kao lililo hai. 

Hiyo kao la Mungu siyo kanisa kubwa yenye tunaona ya mawe, siyo hiyo kanisa nzuri ya kipresibiteriani lenye lilijengwa na ma milioni ya dolla, wala siyo hata moja ya makanisa ya gorofa kubwa lenye unafahamu, hakuna hata moja za hizo magorofa inayokuwa nyumba ya Mungu na watu wote wanafahamu hivyo. 

Mungu katika nyakati za Agano la kale alikuwa na nyumba lililo jengwa kwa vifaa mbalimali. 
Ndani ya nyumba hilo, hekalu kwa zamani, alikuwa akionesha utukufu wake mkubwa. 
Lakini kwa siku za leo, Mungu anaishi katika Kao lililo hai, hekalu lililo hai, siyo ya vitu ama vifaa mbalimbali. 

9/ Ni Kao la Mungu, Jengo la Mungu linalo undwa na mukusanyo wa watu, watu walio okolewa kwa kuamini Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 

1 Timoteo 3: 15 
“Lakini kama nikikawia, upate kujua sana namna inavyokupasa kutenda katika nyumba ya Mungu, iliyo kanisa la Mungu aliye hai, nguzo na msingi wa kweli.”

Inatuambia kwamba tunapashwa kuchunguza namna gani tunapaswa kutembea katika nyumba ya Mungu. 

Hii aimaanishe nyumba iliyojengwa kwa mikono ya watu lakini Nyumba yenye Mungu iko anajenga akitumikisha watu walio hai sawa viungo vya iyo jengo.  
Hii aisemi namna gani wewe kutembea katika kanisa lako la nafasi, (…) 
ama katika gorofa mulio jenga kama kanisa, lakini ukiwa sasa kiungo cha hiyo Kanisa lenye liko linajengwa unapashwa kujuwa namna gani inavyokupasa kutenda sababu tusilete magonvi katika Kao la Mungu. 

10/ Tuone musingi ya maneno haya katika haya ya 20. 
“Mumejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kubwa la pembeni.”

Tuona namna misemwa inapangwa mitume na manabii. 
Mutume Paulo hakusema mumejengwa juu ya msingi wa manabii na mitume. 
Anasema mitume na manabii. 

Niya muhimu sana kuangalia namna maneno haya mawili yanapangwa, sababu kwa siku za leo kuna wale wanaosema ya kwamba hakuna tofauti kati ya Kanisa na Ufalme wa Mungu. 
Na wanasema kwamba watakatifu wa Agano la Kale wako sawa na watakatifu wa siku za leo wanao okolewa katika utunzaji hii wa neema. Hiyo ni kutokujuwa kweli. 

Wanasema kwamba mitume wanaotajwa hapa ni wale mitume kumi na miwili wa Bwana Yesu na kwamba manabii wanao tajwa hapa ni wale manabii wa Agano la Kale. Si hivyo. 
Ingelikuwa ni hivyo, mutume Paulo angelisema Manabii na mitume, hiyo njo ingekuwa kupangwa iliyo halali. 

11/ Tukumbuke kwamba watakatifu wa Agano la Kale tunaowaita watu wa haki, wao hawako viungo vya hiyo Kanisa, hawako viungo vya iyo jengo hata kama kuwa wameokolewa. 

12/ Tusome kama tukitamani katika kitabu cha 2 Petro 3: 2  
“mupate kukumbuka maneno yaliyosemwa zamani na manabii watakatifu, na amri ya Bwana na Mwokozi iliyoletwa na mitume yenu.”

Nafasi hii Manabii wa Agano la kale wanatajwa na kapangwa mbele ya Mitume. 
Hii inaelekea habari ya kuja ama kurudi hapa duniani kwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo na inaonesha kwamba ni manabii wa Agano la kale njo walianza kwanza kutabiri juu ya neno hilo na kiisha hawa mitume kumi na miwili wa Bwana Yesu walisema tena kiisha juu ya jambo lilo. 

Manabii kiisha mitume ni hii mupango ulio kwa namna ya halali. 

13/ Lakini tukirudi katika Waefeso, tutaona kama pale haikupangwa namna hii. 
Katika Waefeso 4:11 tunasoma:

“Naye alitoa wengine kuwa mitume; na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wahubiri wa Habari Njema; na wengine kuwa wachungaji na walimu;”

Hapa inasemwa juu ya zawadi za kiroho yenye Bwana wetu Kristo Yesu aliipatia kanisa na hapo mutume Paulo anasema ya kwamba Kristo alitoa wengine kuwa mitume na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wahubiri wa Habari Njema; na wangine kuwa wachungaji na walimu. 

Tuchunguze namna misemwa inavyopangwa hapa, mitume kiisha manabii.
Hii aimaanishi wale kumi na wawili ama mitume wa Agano la kale. 

Mitume ni wanani? Kweli kwa siku zilizo pita tuliwakumbusha kwamba Mutume ni mutu aliyetumwa, Mutume Paulo alikuwa Mutume na alikuwa mutu aliye tumwa. Neno Mutume inamaanisha mutu aliye tumwa kwenda kuhubiri, naye ni mutume ndani ya Agano jipya. 
Alitumwa kuhubiri Maneno ya Mungu, siyo ya kutia uvuguvugu na hali ya kupana unabii wa mambo itakayo kuja. 

Yote ni zawadi ya Mungu kwa kanisa.

14/ Sasa, tukumbuke kwamba mitume na manabii wa Agano Jipya hawakuwa Msingi wa kanisa. 
Mutume Paulo hakusema yakwamba: mimi ni msingi, lakini alisema mimi ninatia msingi. 

1 Wakorinto 3: 11 
“Maana mtu hawezi kuweka msingi mwengine ila ule uliokwisha kuwekwa, yeye Yesu Kristo”

Walikuwa wakihubiri na kufundisha kwamba Yesu Kristo ndiye Msingi. Kanisa inajengwa juu ya Msingi ulio Imara hauwezi kutikisika. 

15/ Kiisha tuangalie neno “jengo linaunganishwa pamoja na kukua”, kugua inaonesha kukomaa, inamaanisha kuendelea mbele, kutimilika katika utimilivu. 

Kila mtu hagui kwa upekee, lakini jengo lote zima inakomaa ndani ya Hema takatifu ya Roho Mutakatifu katika Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 

Kweli hiyo ni raha kujuwa katika roho yako kwamba sisi ni mawe yaliyo hai katika jengo lile la utukufu. 

Nazani neno hili linasukuma nafsi yako kuona umuhimu wa kuishi maisha ya utakaso kwa kujuwa namna gani inatupasa kutembea katika nyumba ya Mungu, JENGO la Mungu, KANISA la Mungu, KAO la Mungu.” 

16/ Wakati wa Agano la Kale, wakati Hekalu la Solomono lilikuwa likijengwa, lilitiwa juu ya mulima wa moria, kwenye nafasi lililotengenezwa  
Kwenye chongo ya mulima. 
Mawe makuu yalikuwa yakichorewa na kutengenezwa na kupandishwa ili yatiwe kwa jengo la hekalu.  

Kiisha muda wa miaka saba, jengo lile lilikuwa kubwa sana na la mastaajabu na kupendeza kwa wakati ule katika daftari ya dunia zima. 

Na kulikuwa kitu kimoja cha upekee wakati hekalu lile lilikuwa likijengwa 
Majengo ya hekalu ilikuwa ikifanyika bila fujo yoyote, hata mulio wa hama haukuwa unasikilikana sababu mawe yote yalikuwa yakitengenezwa na kuchorewa huko chini  na kukatwa na kurandwa na kupewa umbo linalostahili, kiisha baadaye njo yanakwenda tiliwa katika jingo wakiunganisha jiwe moja pembeni ya jiwe lingine wakiyabananisha na simenti bila kutumikisha hama ya watumishi wajengaji. 
Ni kwa hiyo hapana mutu mwenye anastahili kusikia fujo ama mulio wowote katika Jengo la leo, kama kweli sisi ni Majiwe yaliyo na uhai, yanayo tiwa pamoja katika Hekalu ya Mungu, Kao la Mungu. 

Roho Mutakatifu njo mwenye kuchimba mawe yaliyo na uhai akayatosha  toka shimo la zambi, anayainua kwa Nguvu na Uwezo wake wa ajabu na kuyaingiza katika Jengo linalokuwa juu ya Msingi kubwa ndiye Mwokozi wetu Yesu Kristo. 

Kwa kweli, mawe haya yaliyo na uhai yanatokea katika bara la Afrika, yanatokea huko India, Chaina, katika visanga vyote vya ma bara, hii ni ukweli wa utukufu.

17/ Kama ungaliweza kuniuliza mawazo yangu kuhusu siku gani hayo majengo ya Hekalu lile yatamalizika na kutimizwa, nitakujibu kwamba inabaki tu kutiya Majiwe mamoja mamoja hapa na pale kwa ukuta wa juu na yote itatimilika. 
Nina uhakika kwamba tunakuwa ndani ya majira ya nyakati zenye majengo ya Hekalu tayari inaanza malizika. 

Inawezekana kwamba Jiwe la mwisho litatiwa leo hii na kazi yote itakwisha. 
Maombi yangu ni kwamba wewe vile vile uwe kiungo cha ile Hekalu la utukufu, Kao la Baba Mungu. 

Majengo ya Hekalu inaweza kwisha leo na itakuwa nyuma kwako hauta weza tena fanya kitu chochote kwa kuwa moja wa viungo vya lile jengo na itakuwa hasara sana. 

18/ Sasa twende ndani kabisa ya hii waraka. 
 Katika sura yake ya tatu Mutume Paulo anatuonesha namna gani alifikia kupewa Ufahamu wa Ukweli huu uliofunuliwa kwake. 

Anatuambia kwamba yeye aliupata kwa njia ya UFUNUO. 
Yeye hakupata ufunuo huu kwa Yakobo, ama kwa Yoane, ama kwa mumoja wa wale mitume kumi na miwili. 

Na sasa hii Ukweli yenye aliyo upata kwa ufunuo, inaita “SIRI KUU.” 

19/ Ni kwa sababu ya Ukweli huu njo alipatikana katika gereza wakati alikuwa akiandika Waraka kwa Waefeso.   

Mutume Paulo hakupatikana ndani ya gereza kwa makosa aliyo yafanya ama kwa sababu hakutii Baba Mungu, sivyo. 

Yeye alipatikana katika kifungo cha gereza sababu ya Ukweli huu wakusema kama hakuna tena Muyuda ama Mutu wa Mataifa, wote wanakuwa kwa daraja moja mbele ya Mungu Baba na wote watakuwa viungo vya Mwili Mumoja, hapana ufalme. 

20/ Tuone namna inavyosemwa: 
Mimi Paulo, mufungwa wa Yesu Kristo kwa ajili yenu nyinyi Mataifa. 
Mutakumbuka ya kuwa ni wakati Mutume Paulo alikuwa akishuka toka mulango wa Hekalu ya Yerusalemu ndiyo wakati alio anza kutangaza hazarani kwamba yeye alitumwa na Bwana Yesu Kristo. Na kwamba Bwana Yesu Kristo alimutuma kwa Mataifa, ili aende kuhubiri Mataifa, wapagani na saa wayuda walisikia maneno haya walichanganyikiwa na kuwa na hasira kubwa sana zaidi na walilalamika na kupaza sauti wakisema “Ondocheni mutu wa namna hii katika dunia, sababu hastahili kuishi”  

Matendo ya Mitume 22: 22  
“Walimusikiliza mpaka neno hili, wakapaza sauti zao, wakisema: Mwondoshe huyu katika inchi kwa maana haifai aishi”

Ni kwa sababu ya hii, sisi Mataifa tunao kuwa wapagani kwa kuzaliwa kwetu, tuna  sababu kweli ya kuleta shukrani kubwa zaidi na  ya upekee na ya sifa kwa uhodari, ukamilifu na kustawi  na kustahimili kwa Mutume Paulo katika kutangaza na kuhubiri Mapenzi na Mupango wa Mungu katika Utunzaji wake huu mupya. 

Siyo miradi ya Ufalme lakini ni miradi ya Mwili wa Kristo.  
Ni kwa sababu ya Miradi hii ya Mwili wa Kristo njo maana mutume Paulo alishindana na kuvumilia haya na zarau na kupitisha siku nyingi katika mateso na uchungu kubwa, katika unyonge wa gereza na aliitika hayo yote pahali ya yeye kukosa kutangaza hata nugta moja ya Ukweli  na mwito na kujitoa yenye Baba Mungu aliutia ndani mwake. 

21/ Turuke haya zimoja za hii sura ya tatu ya Waefeso na twende kwa haya ya kenda: 
Waefeso 3: 9  
“na kuangazia watu wote wajue habari za madaraka ya siri iliyofichwa tangu zamani ndani ya Mungu aliyeumba vitu vyote;” katika Yesu Kristo.

Hii maneno ilikuwa inafichwa ndani ya MUNGU. 
Haisemwe tu kwamba hii siri ilikuwa tu inafichwa ndani ya Biblia, haiko kusema kwamba hii siri ilikuwa inapatikana katika Agano la Kale, na kwamba ilitupasa sisi kucheuwa na kuchimba na kuchunguza ili tuipate. Sivyo vile. 

Hii siri ilikuwa ikificha tangu zamani ndani ya Mungu na haikuwezekana hata mutu yeyote kuigundua kama haingelikuwa yeye Mwenyezi Mungu mwenyewe aifunulie mutu kwa ufunuo wa kimungu. 

Ni kwa ufunuo wa Mungu Mwenyewe njo siri hii ilifunuliwa kwa ufunuo kwa Mutume Paulo kwa njia ya Ufunuo toka Mungu yeye mwenyewe akimufunulia uso kwa uso. 

22/ Hata wamalaika wema sana na wabaya hakuna mwenye alikuwa na ufahamu wowote juu ya siri hii ya Mwili wa Kristo, mpaka ikamupendeza Mungu amufunulie kiumbe chake Paulo aliyekuwa akiishi ndani ya dunia, na kwa njia ya kutangaza kwa Mutume Paulo, wengine vile vile wapate kufunuliwa na wao vile vile wafunulie wengine, hii njo maana ya haya hiyo ya kumi. 

Waefeso 3: 10  
“ili sasa, kwa njia ya kanisa, hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi ijulishwe na falme na mamlaka katika pahali pa mbingu;”

Hii ni Ukweli mkubwa na ya manufaa yenye wengi wetu hawaelewe kwa siku za leo kwa sababu haiwezekane kuupapasa kwa namna ya kimutu, haiwezekane kuuona na mecho ya kibinadamu, na haiwezekane kuikadirisha na akili ya kimutu. 
 
AMEN

 
Ref: 01/10/1960 / 209 - THE BODY BEAUTIFUL / 1/31/2020

No comments:

Post a Comment