Tuesday, September 24, 2019

INJILI YA PASAKA / THE GOSPEL OF EASTER




Photo taken from B Smith's Kitchen Window




     52 The Gospel of Easter / INJILI YA PASAKA 
     April 2, 1961
     Pastor Henry F. Kulp


Wagalatia 1:1-12 
Paulo, Mutume, (si mutume wa wanadamu, wala kutumwa na mwanadamu, bali na Yesu Kristo, na Mungu Baba aliemufufua kutoka kwa wafu),
Na ndugu wote walio pamoja nami, kwa makanisa ya Galatia;
Neema na iwe kwenu, na Amani, zitokazo kwa Mungu Baba, na kwa Bwana wetu Yesu Kristo;
Ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili ya zambi zetu, ili atuokoe na dunia hii mbovu iliyopo sasa, kama alivyopenda Mungu, Baba yetu.
Utukufu una Yeye milele na milele, Amina.
Nastaajabu kwa kuwa mnamwacha upesi hivi Yeye aliye waita katika Neema ya Kristo, na kugeukia injili ya namna ingine.
Wala si ingine; lakini wako watu wawataabishao na kutaka kuigeuza Injili ya Kristo.
Lakini ijapokuwa sisi ao malaika wa mbinguni atawahubiri ingine injili yoyote isipo kuwa hiyo tuliyo wahubiri, na alaaniwe.
Kama tulivyo tangulia kusema na sasa, nasema tena, mutu awayeyote akiwahubiri ingine injili isipokuwa hiyo mulio ipokea, na alaaniwe.
Maana, sasa je!
Ni wanadamu ninaowashawishi, au Mungu?
Au nataka kuwapendeza wanadamu?
Kama ningekuwa ata sasa nawapendeza wanadamu, singekuwa mutumwa wa Kristo.
Kwa maana, ndugu zangu, injili iyo niliyo wahubiri, nawajulisha ya kuwa siyo ya namna ya kibinadamu.
Kwa kuwa sikuipokea kwa mwanadamu wala sikufundishwa na mwanadamu, bali kwa ufunuo wa Yesu Kristo”.
Sawa vile tulivyo jifunza katika kitabu ya Wagalatia, tuliona ya kuwa walimu wengi wa uongo walijiingiza ndani ya muji ya Galatia na katika makanisa mingi na walikuwa wanawaalika na kuwafundisha watu waheshimu mafundisho ya utamaduni pahali ya Neema ya Mungu.
Na kwa kweli, kwa kufanya hivyo, walikuwa wanapenda kuzorotesha mutume Paulo na Injili yenye aliyowafundisha.
Ya kwanza, walikuwa wanakana wakisema kama Paulo haiko mutume wa Mungu, na Paulo aliwaonesha  kwa kutumia hakikisho mbalimbali inao onesha kama kwa kweli yeye ni Mutume wa Mungu.
Yeye alikuwa mutume wa Mungu na alikuwa akitumwa na Mwenyezi Mungu na anasamani ya kuonesha kama yeye ni wa Mungu.
Kiisha Mutume Paulo aliendelea kuonesha kwa kweli kama Injili aliyokuwa akifundisha ni hiyo pekee inayo faa kufundishwa na inayo kuwa kamilifu na yenye kuenea. 

1/ Munaona kwamba Mutume Paulo alihukumu kwa kulaani na kulahini yeyote yule hataitika hii injili ama mutu yeyote mwenye atahubiri ingine injili tafauti na hii. 
Tuaangalie sana,
Hapa mutume Paulo anasema:  Alaaniwe,
kweli ni maneno magumu, bali ni hiyo  njo neno yenye Mungu anapenda tujuwe.
Tuone hapo kama ni kulaaniwa mara mbili sababu anarudilia kusema alaaniwe.
Ni lazima kwetu tujuwe kama haiko kuhukumu ao kukufuru yenye inatoka kwa masemi ya watu, lakini hiyo njo kutaka kwa Mungu.
Ni kulaaniwa yenye Mungu anapenda iwe juu ya ule mutu.
Basi, inakuwa muhimu sana na yenye mafaa sana kufikiri na kuwa na uhakika wa kila neno mbele ya kuitamka wakati tunapokuwa tukihubiri habari njema. Angalisho na kuwaambia mali ya Bwana: “Hii ni Neno linalotoka kwa Mungu!”
Tunapashwa kufanya angalisho na kuwa na ujuzi na uhakikisho ya maneno tunayo yatamka.

2/ NI INJILI GANI?
Tunapata maelezo juu ya hii Injili katika moja Wakorinto 15: 1- 8,
Ni Yesu Kristo aliye sulubiwa musalabani juu yetu, alizikwa na akafufuka siku ya tatu.
1 Wakorinto 15: 1 - 8 
"Basi, ndugu zangu, nawaarifu ile Injili niliyo wahubiri; ambayo ndiyo mulioipokea, na katika hiyo munasimama, na kwa hiyo munaokolewa; ikiwa munayasikia sana maneno niliyo wahubiri isipo kuwa muliamini bure.
Kwa maana naliwatolea ninyi hapo mwanzo yale niliyo yapokea mimi mwenyewe, yakuwa Kristo alikufa kwa ajili ya zambi zetu, kama yanenavyo maandiko; na yakuwa alizikwa; na yakuwa alifufuka siku ya tatu, kama yanenavyo maandiko; na yakuwa alimutokea Kefa; tena na wale Kumi na wawili, baadaye aliwatokea ndugu Zaidi ya mia tano pamoja; katika hao wengi wanaishi ata sasa; ila baadhi yawo wamelala;
Baadaye akamtokea Yakobo; tena na mitume wote; na mwisho wa watu wote, alinitokea mimi, kama ni mutu aliyezaliwa si kwa wakati wake. “

3/ Wagalatia 1: 11-12 
“Kwa maana ndugu zangu, injili hiyo niliyo wahubiri, nawajulisha kuwa siyo ya namna ya kibinadamu.
Kwa kuwa sikuipokea kwa mwanadamu wala sikuifundishwa na mwanadamu, bali kwa ufunuo wa Yesu Kristo.”
         Tunaona hapa kama siyo injili iliyotoka kwa mutu, ao kupewa ama kufundishwa na mutu lakini ni Ufunuo toka Yesu Kristo.
Injili iliyotoka kwa Mungu, mutume Paulo aliipata toka mbinguni.

4/ INJILI HIYO ILITUTENDEA NINI?  
Ni Habari njema ya muhimu sana.
Lakini, kwa kweli, hiyo injili ilitutendea nini?
Twende basi tukayaona katika Ufunuo 1:18
Ufunuo 1:18 “Na aliye hai; nami nilikuwa nime kufa, na tazama ni hai hata milele na milele.
Nami ninazo funguo za mauti na za kuzimu.”
         Kama vile unavyoona sasa ni Yesu Kristo anayekuwa akisema, na Yesu Kristo anasema, ni Yeye msemaji na anasema Yeye ni Yule aliye hai na Yule aliyekufa,  na tazama Yeye ni hai milele kwa milele.
Ninazo funguo za mauti na za milango za hadeze.
Katika maisha yetu kama  wasafiri hapa chini duniani, sisi ni watenda zambi na tunaelekea kufa, na kiisha kufa ni pahali pa mapumuziko kiisha kufa.
Kufa ina nguvu, kama vile hadeze vilevile, na Bwana wetu Yesu alikufa, na Yeye alitoka toka kufa na Yeye yu hai na alisema nina funguo ya Hadeze, Jehenama haitaogopesha tena wale wanaomufwata Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, wao wanaoliamini Kufa kwake na kufufuka kwake,
Bwana Yesu alisema, mimi ninao funguo ya kifo. Kufa haina tena nguvu, nguvu ya Jehenama inakwisha.

5/ TUNA MAADUI WAKUBWA WENYE NGUVU NA WANAO TUZUNGUUKA NA WENYE TUNAPASHWA KUSHINDA.    
Zambi, Kufa na Hadeze.
Ninakuambia wewe ndugu musikilizaji kwamba yapashwa upate Wokovu, ni Injili inayo kuokoa toka zambi, toka kufa na toka hadeze,
Kwa sababu hawo ndiyo maadui wako, na Biblia inatuonesha waziwazi namna gani Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo aliwasaga hawo maadui wako, na wakati alipotowa roho na kwenda Mbinguni, aliharibu nguvu ya kufa, nguvu ya zambi, nguvu ya Hadeze na sisi tunakuwa Huru.
 Ni hiyo njo Wokovu, hapana kitu kingine.  
Watu wanaweza kuunda madini mbalimbali, lakini dini haiwezi kuokowa.
Tufanye angalisho na dini,
Kitu cha maana kwetu sisi watenda zambi ni Ukombozi.

6/ NA UKOMBOZI NI KWETU
Ukombozi ni kwetu sasa, sawa vile kufa na hadeze vina tusonga, kwa sababu Yesu Kristo ana Funguo na Funguo ni alama ya Ukubwa na Mamlaka.
Hii inamaanisha kwamba Kristo ana Ukubwa usio kuwa na ubishi na Katika kufa kwa KRISTO, na ufufuko wake KRISTO ana Mamlaka juu ya kufa na hadeze, na kwa matafsiri ya musingi tunaona kama kufa njoo iko mbele ya maali pa mapumuziko ya wafu. Hivi njo mambo yafwatana.

7/ 1 WAKORINTO 15: 17 
“Na kama KRISTO hakufufuka, Imani yenu ni bure; mungalimo katika zambi zenu.”
Naomba musamaa juu ya hawo wahubiri wakarimu wa siku hizi wasiosadiki ufufuko wa Bwana Yesu Kristo, sababu, musingi wa maandiko hii inaonesha kama hata wahubiri wa namna hiyo wanaweza kuwa na imani ya namna gani, na kweli wanajizania wana Imani kubwa, ndugu musisahau hata siku moja, mujuwe kwamba Imani yao ni bure, haina musingi na wao wangali tu katika zambi zao.
Tena hapo tunaona kwamba kuamini katika kuamini za kidini ni hatari sana,
Inafaa tu kuamini Injili yenye Mutume Paulo anayo fundisha, kama sivyo, wewe unalaaniwa, na laana hii iko juu yako, Hii laana ya Mungu, sababu yatupasa kuamini UFUFUKO wa Bwana na Mwakozi wetu Yesu KRISTO.
WAROMA 10: 9 -10 
“Kwa Sababu Ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na Kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimufufua katika wafu, utaokoka.
Kwa maana kwa moyo mutu aamini hata kupata haki na kwa kinywa anakiri hata kupata wokovu.” Hakuna mutu awezaye kuokolewa kama hasipoamini waziwazi ufufuko wa KRISTO.

8/ SASA HIYO INJILI INAMAFAA GANI KWETU?  
Injili ya Kristo Yesu kusulubiwa na kufufuka toka wafu?
         Inatuokowa toka Kufa na Hadeze,
Lakini inakazi nyingi kuliko hiyo,
Tujuwe kwamba:
Katika Kitabu hiki kizuri tunayo jifunza, kitabu cha Wagalatia, tunapata mwangaza wa Ukweli wa samani kuu katika hii Habari njema,
Wagalatia 2:20 
“Nimesulubiwa pamoja na KRISTO; lakini ni hai; wala si mimi tena, bali Kristo yu hai ndani yangu; na uhai niliyo nao sasa katika mwili, ninao katika Imani ya Mwana wa Mungu, ambaye alinipenda, akajitowa nafsi yake kwa ajili yangu.”
         Ndiyo, ni hii ndiyo Mwamba, Maana kamilifu, Nguzo na Musingi wa KIKRISTO.
         Ukristo siyo mambo yenye wewe binafsi unaweza kutimiza ao kufanya, lakini ni Hiyo Bwana Yesu afanyalo akiishi ndani yako.
Hii njoo tofauti katikati ya Ukristo na Dini.  Sivyo?
Dini ni kitu chenye mutu anaumba na anafanya, ni kusema dini ni mutu afanyae kitu Fulani, lakini Ukristo ni Yesu afanyae vyote.

9/ WAKOLOSAYI 1:27  
“Ambao Mungu alipenda kuwajulisha jinsi ulivyo utajiri wa utukufu wa siri hii katika mataifa, nao ni KRISTO ndani yenu, tumaini la utukufu.”
         Hii andiko inasema namna moja sawa hiyo ya wagalatia inayo sema KRISTO ndani yenu, tumaini la utukufu.
Kristo Yesu yu hai, Kristo ndani ya mwamini.
Hii Habari njema Nzuri inatuonesha namna gani Kristo anaishi ndani yetu.
Ni jambo la mastaajabu sana na ya kufurahisha!!!  

10/ HII UKWELI WA KRISTO AKIISHI NDANI YENU NI KITU KIPYA CHENYE KUELEKEA HIZI SIKU TUNAZOISHI.
         Watakatifu wa hapo kale hawakuishi hii ukweli,
Tukiangalia katika kitabu cha Yoane, tutakuta hii Ukweli ya Utukufu.
YOANE 14:17 
“Ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kupokea, kwakuwa haumwoni wala haumutambue; bali nyinyi munamutambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu.”
         Daudi, kama vile munavyo juwa, aliifikia kiwango cha juu sana.
Huyu muhimbaji wamanufaa wa Agano la kale.
Lakini, wewe na mimi tunapashwa kujuwa Zaidi ya Daudi.
Sisi tunapashwa kuwa wazuri na wakupendeza Mungu kushindia Daudi.
Sisi tungelipashwa kupanda milima mirefu Zaidi ya vile Daudi alifanya.
Sisi tungepashwa kuona mambo makuu kushinda hiyo Daudi aliyoona.
Sababu Daudi hakukuwa na KRISTO akiishi ndani yake.
Tutazame katika hii aye, inasema
KRISTO alihaidia kama siku inakuja nayo ni tayari hapo ROHO Mutakatifu ataishi ndani yao, lakini,  katika hizo siku za kale ROHO Mutakatifu alikuwa tu juu yao.
Lakini kwa leo, tunakuwa na KRISTO ndani yetu,
Taifa la Izraeli itakuwa na KRISTO ndani yao katika siku zijazo.

11/ KATIKA HII WAKATI YENYE TUNGALI NAFAFANUA HII WAZO, ACHA NIWAONESHE ANDIKO MOJA NZURI KATIKA
WAEFESO 3: 19
“Na kuujuwa Upendo wake Kristo, upitao ufahamu kwa jinsi ulivyo mwingi, mupate kutimilika kwa utimilifu wote wa Mungu.”
         Ukristu siyo aina ya utupu, ya bila mafaa yoyote
Ukristu siyo kitu isiyo ya faida, ya bure.                                              
Kama ukikutana na Ukristo usio vutia, usio na mafia, unao kuwa bure, fahamu ya kuwa unakutana na kitu kingine mbalimbali na Ukristu, sababu
Ukristu ni Uwingi, ni Kujaa.
Mungu anataka kuondoa kitu kimoja maishani mwako.
Wengi wetu wanasema, kweli mimi siwezi…
Kwa kweli, Hauwezi hata kuondowa kitu kimoja ndani mwako ili uokolewe.
Lakini kama unapenda kujuwa na kuishi ujazi wa Mungu, Mungu anapenda aondoshe ile isiyo stahili kuwa ndani yako.
Anapenda kuondosha kitu kimoja ndani mwako ili atiye nyingine ndani mwako.
Anaondosha yale mambo machafu ili ajifanyie nafasi ya kukaa na kukupatia ujazi wake.

12/ SOLOMONO KATIKA MAOMBI YAKE ALISEMA HIVI ”MBINGU NA DUNIA YOTE MUNGU HAWEZI AKAIENEE AMO”  
Lakini sasa, hapa tulipo sasa, tunaweza jazwa na Ujazi wake.
Ona sasa ndugu yangu namna gani Mungu ni Mwema!
Ni Hii Habari Njema ya Mastaajabu yenye hii Injili inafanya kwetu.
Hii habari Njema Inaweza kutujaza na Ujazi wa Kristo Yesu.

13/ LAKINI HABARI NJEMA HII YA SALAMA INATUOKOWA NA INAFANYA MAMBO MENGI MAKUBWA KWETU.
Ufufuko wa Bwana wetu Yesu Kristo njoo vilevile ufufuko wetu.
Waroma 8:19 
Kwa maana viumbe vyote pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa  kwa wana wa Mungu.”
Tunaona kwamba Roho wa Mungu aliye mufufua Bwana na Mwokozi wetu toka wafu, Roho ule anakaa ndani yako, Yeye aliye mfufua Kristo Yesu toka wafu, atabadirisha, kwa kufunga macho na kufungua, mwili wako uliokuwa wa kufa kwa nguvu ya Roho anayeishi ndani yako.
Mwili wa mukristo, mwili wa mwamini ni mali ya Roho Mutakatifu, ni mawazo ya Raha kweli. Kwa njia ya ufufuko wa Bwana Yesu, Roho yule aliye mufufua Bwana wetu Yesu Kristo toka kufa, anashurulikia mwili wetu huu wa udongo.
Kama Mwamini Mukristo anakufa, na mwili wake unazikwa kaburini, huyu mwili unachungwa na Roho Mutakatifu.
Kama wewe umekwisha kuamini, Mungu amekwisha kukupatia Roho Mutakatifu naye anaishi katika miili yenu na miili yenu ni Hekalu ya Roho Mutakatifu.
Na kwa hiyo, kama umehamishwa, na mwili wako umetiwa udongoni, mwili huo una baki katika ukingo wa Roho Mutakatifu, na huyo mwili utabadirishwa tena upya.

14/ KWA HIVYO WATU WENGI WANAMAULIZO MBALIMBALI JUU YA UFUFUKO WA WAFU, WAKIJIULIZA KAMA MWILI YA UFUFUKO ITAKUWA ILE ILE ILIYOINGIZWA KABURINI?  
         Roho Mutakatifu anahusika na hiyo miili na ni Yeye pekee njoo atarudisha kwa upya hiyo miili kwa uzima, sababu ni miili yake, Anaiishi ndani ya miili hiyo na hiyo miili ilikuwa hekalu lake, na kwa hiyo anahusika nazo naye ataziweka tena upya wa uzima.
Kuna mufano moja yenye nilisikia siku nyingi zilizopita, na ninawaza kama inaweza wasaidia kidogo kwa kusikia mambo haya.
Kamata bahasha ya kartasi yenye tunatumikisha kwa kubebeya ndani vyakula, kunjakunja hayo mukononi mwako, na kwa mwisho saa utapuliza hamo hewa, utaona kama bahasha hiyo itarudiliya sura yake iliyo kuwa nayo. Itakuwa hivo hivyo kwa miili yetu.
Katika hizo miili zenye zilizo kunjwa na kuharibishwa, miili yenye iko chini ya udongo, kwa siku ya ufufuko, Roho Mutakatifu atapulizia pumzi mu miili hizo na miili hizo zitakamata sura yake.
Na ni hizohizo miili njo zitafufuka katika utukufu wa milele.

15/ UZURI NA RAHA GANI KUJUWA HIVYO!
Bwana Yesu Kristo atatubadirisha katika mwili wa utukufu unao fanana na mwili wake.
Ufufuko wake ni harabuni ya ufufuko wetu toka wafu.
KRISTO anaye ishi leo ndani ya mwamini, kwa njia ya kufa kwake na ufufuko wake.
Ni yakusikitisha sana kuona kama wengi hawafahamu Ukubwa wa Kazi ya Bwana wetu Kristo Yesu.
Siku moja nilikuwa nasoma maandiko ya Muganga Dr Tom Dooley, mwenye alikuwa muganga mukubwa naye alijulikana ulimwenguni pote na yeye alikuwa akipatikana katika Jungle ya LAOS.
Pa siku 02 Mwezi wa kumi na mbili wa mwaka wa elfu moja mia kenda makumi sita, nilipatikana nikiwa na uchungu na machozi nyingi rohoni mwangu wakati niliposoma maandiko yake ya mwisho wa maisha yake wakati ugonjwa wa kansa ulikuwa ukimusonga kweli, na yeye aliandikia Mwalimu moja mukubwa wa Yunivarsti akisema hivi:
“Wakati yoyote saa kansa yangu itanifikisha mwisho na kunibeba kwenye mauti, nilikuwa nawaza moyoni mwangu, nikiingia katika utu wangu wa ndani kwa muda pande,
Nikiona bila faida ao mafaa,  hospitali zangu kubwa zinazo patikana ulimwenguni pote,  na waganga wangu makumi kenda na ine wenye ujuzi wa juu sana kama mimi, na wenye kujulikana, na tena juu ya hiyo, nikajiuliza kama nilipima waza juu ya muganga moja toka mbinguni sababu ya vitu nyingi niliyotolea kwa makanisa, nilijiuliza kama haingiweza kutosha?
Ona hapa mufano wa mutu mwenye hakukuwa na tarajia maisha ya milele.
Huu ni mutu wa dini akiishi katika kujitoa kwa matoleo ya namna ya kibinadamu, akipana maisha yake kwa wengini.
Alikufa sababu alijitowa mwenyewe juu wengine wapate maisha mazuri hapa chini duniani.   
Lakini alikufa akiwa anahuzuni kubwa juu ya kifo yake mbaya na yenye uchungu yenye iko inamukaribia dakika kwa dakika.
 Yeye alikuwa mutu wa dini, mutu mwenye aliongeza matendo yake juu ya neema ya Mungu, hakuamini kama Kifo na Ufufuko wa Bwana na Mwokozi wetu Kristo Yesu tu njoo Yatosha juu ya wokovu wetu. Ni kwa njia hii njoo
ati Muganga Dr Dooley alifariki.
Yeye hakuandika juu ya Salama na Raha ndani ya Wokovu katika Kristo Yesu, lakini alikuwa akijiuliza kama matoleo yake nyingi na zaka zake nyingi hazikutoshelea?
Tunafahamu kwamba hata matoleo yetu yawe nyingi namna gani haiwezi hata kwa namna ya zamiri kukamilisha mwenye kuabudu, kutuokowa na kuponya roho yetu.
Ni Kazi tu Ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo njoo yatoshelea na kufaa kwa ukamilifu juu ya wokovu wetu.
Oh, sisi tuliokombolewa tunaweza fikia siku yetu ya kufa bila woga yoyote sababu tunajuwa kwamba Kristo anaishi ndani yetu, na ni kwa njia yake tutaishi milele.

16/ WAROMA 14: 9   
“Maana Kristo alikufa akawa hai tena kwa sababu hii, awamiliki walio kufa na walio hai pia.”
         Tuone kitu kingine hapa, inayoelekea kufa na kufufuka kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
Kwa siku hizi Kristo alikufa na alifufuka na kuhishi tena milele juu awe Bwana wa waliokufa na walio hai.
Hakuja onekana kabla mwana wa mwanadamu kwa miaka hii yote mwenye anaweza ongoza mambo ya dunia.
Magumu ya mwanadamu ni nini?
Magumu ya mwanadamu haiko tu vita, vita ni musiba katika historia ya mwanadamu.
Watu wanachukiana, watu wanatamani vyeo, kutawala na mamulaka juu ya wengini na hivyo njoo inawasukuma katika vita,  Na vita inakuwa musiba.
Nini inayo sumbuwa wanadamu? Wanasumbushwa na kifo.
Mutu hapande matungulu juu ioze udongoni na kupotea.
Mutu hapande mbegu ama milimo juu ibakie tu udongoni bila hata siku moja kupamba.
Mufurugano wa mwanadamu ni juu yeye anajuwa atakufa.
Atakufa katika zambi zake,  watu wanaonekana wakitembea duniani lakini wao kweli ni wafu katika zambi zao.
Hakuja patikana mwana wa mwanadamu hata mumoja, mwenye angeliweza kupiganisha kufa na kulipa zambi.
Hakuna hata mumoja mwenye angaliweza kufanya hivyo, ila MUNGU, asiye jua zambi, alijifanya kuwa zambi kwa ajili yetu akijifanya kuwa MUTU ili avunje Kufa na awe BWANA wa walio kufa na wenye walio hai.

AMEN
Ref:  04/02/1961 / njili ya Pasaka / 52 - The Gospel of Easter - 9/24/2019

No comments:

Post a Comment